fataawa za shaykh muqbil kuhusu wanawake

47
1 Fataawa Kuhusu Wanawake ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy Imefasiriwa Na: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

Upload: wanachuoni

Post on 11-Nov-2014

519 views

Category:

Documents


34 download

DESCRIPTION

Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

TRANSCRIPT

Page 1: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

1

Fataawa Kuhusu

Wanawake

´Allaamah Muqbil bin Haadiy

al-Waadi´iy

Imefasiriwa Na:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

Page 2: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

2

Fataawa zilizomo:

1) ´Allaamah al-Waadi´iy Kuhusu Mwanamke Kuwa Mbele Anapowaongoza Wenzio

Katika Swalah

2) ´Allaamah Muqbil Kuhusu Mwanamke Kunyoa Nywele Za Mwilini Mwake

3) Alikuwa Hatoi Zakaah Ya Dhahabu Kwa Ujinga Na Sasa Dhadhabu Yote Imekwisha

4) Anamnyonyesha Mtoto Mbele Ya Dada Zake

5) Baada Ya Kutwahirika Akakutana Na Mumewe, Damu Imejitokeza Tena?

6) Baadhi Ya Vitabu Ambavyo Mwanafunzi Mwanamke Anapaswa Kuwa Navyo

7) Dalili Kuwa Mwanamke Mwenye Hedhi Anaruhusiwa Kugusa Msahafu Na Kusoma

8) Damu Inayomtoka Mwanamke Kabla Ya Kujifungua

9) Haijuzu Kuoa Mwanamke Ambaye Mwanaume Kanyonya Kwa Mama Yake

10) Kajifungua Baada Ya Kuingia Swalah Ya Dhuhr, Ni Wajibu Kuilipa?

11) Katwaharika Na Hedhi Lakini Daktari Kamkataza Kukoga

12) Kauli Yenye Nguvu Ni Kuwa Mwanamke Kuonesha Uso Wake Ni Haramu

13) Kumnyonyesha Mtoto Baada Ya Miaka Miwili

14) Kumpasua Mwanamke Ambaye Kafariki Na Tumboni Mwake Kuna Mtoto Hai

15) Kunyonyesha Mbele Ya Wanawake Waislamu

16) Kutumia Dawa Ya Kuzuia Mimba Kutokana Na Uzito Anaoupata Mwanamke

17) Maandamano Ya Wanawake

18) Mama Wa Mwanamke Niliyemtaliki Atabaki Kuwa Mahram Kwangu?

19) Mavazi Ambayo Anapaswa Kuvaa Mwanamke Aliyefiwa Na Mume Wake

20) Mke Hana Haki Yoyote Ya Kumpa Talaka Mwanaume

21) Mke Hataki Kukoga Janaba Na Anajua Ni Wajibu

22) Mke Kumfanyia Mume Wake Maakulati Aina Mbali Mbali

23) Mke Kuomba Talaka Kwa Mume Wake Bila Ya Sababu Yoyote

24) Mke Kuwapa Zakaah Dada Zake Na Mume Wake

25) Mke Wake Alipotea Na Baadae Akampata Kishakuwa Na Mume Mwingine

26) Msimamo Wa Shaykh Muqbil Kuhusu Mwanamke Kufunika Uso

27) Mume Hataki Hijaab, Nifanye Nini?

28) Mume Kamtaliki Mke Wake Mara Sita Kisha Anasema Kuwa Hakumbuki

29) Mume Na Mke Wanatofautiana Katika Masuala Ya Dini

30) Mume Wake Kamtupa Miaka Miwili Na Kwenda Kutafuta Elimu

31) Mwanamke Alikuwa Hajui Kuwa Anajibika Kutoa Zakaah Ya Dhahabu Zake Na Sasa

Amejua

32) Mwanamke Anasafiri Kila Siku Na Kwenda Kwenye Masomo Ya Mchanganyiko

33) Mwanamke Anatakiwa Kuolewa Pale Anapofikisha Miaka 13, 14 Au 15

34) Mwanamke Anaweza Kusafiri Na Mwanamke Mwenzake?

35) Mwanamke Kufanya Kazi Ili Awapatie Watoto Wake Riziki

36) Mwanamke Kufanya Kazi Katika Idara Na Hospitali Za Mchanganyiko

37) Mwanamke Kumkogesha Mama Mzee Na Mwendawazimu Wasiojiweza

38) Mwanamke Kunyoa Nywele Za Mguuni Mwake

39) Mwanamke Kuondosha Nywele Za Kwenye Kidevu, Miguuni Na Mwilini

40) Mwanamke Kusafiri Na Mahram Mtoto Awezae Kupambanua

41) Mwanamke Kuvaa Mavazi Meupe

Page 3: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

3

42) Mwanamke Kuvaa Suwali Mbele Ya Mume Wake Na Wanawake Wengine

43) Mwanamke Mwenye Hedhi Kuingia Msikitini Kutoa Darsa Kwa Wanawake Wenzio

44) Mwanamke Mwenye Hedhi Na Nifasi Kushika Msahafu Na Kuingia Msikitini

45) Mwanamke Wa Kiislamu Kutumia Vipodozi "Miquillaage"

46) Mwanaume Na Mwanamke Wote Ni Sunnah Kutahiriwa

47) Nasaha Za Shaykh Muqbil Kwa Mume Na Mke Ambao Ni Wanafunzi

48) Ni Wajibu Kwa Mwanamke Kuvaa Vifuniko Vya Mikoni (Gloves)

49) Ni Wajibu Kwangu Mke Kumhudumia Mama Wa Mume Wangu?

50) Ole Wako Mume Kumwacha Mke Wako Kwenda Kwa Wanawake Hizbiyaat

51) Shaykh Muqbil al-Waadi´iy Kuhusu Uke Wenza

52) Udugu Wa Kunyonya Wa Watoto Wa Mama Tofauti

53) Wamezini Katika Hali Ya Uchumba, Wanapigwa Mawe Au Wanauawa?

54) Yupi Bora Kati Ya Wanawake Hawa Wawili?

Page 4: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

4

1) ´Allaamah al-Waadi´iy Kuhusu Mwanamke Kuwa Mbele

Anapowaongoza Wenzio Katika Swalah

Swali:

Mwanamke akiwaongoza wanawake katika Swalah, je, asimame mbele ya

wanawake au asimame katikati yao kama alivyofanya ´Aaishah (Radhiya

Allaahu ´anha). Aliswalisha watu, akasimama katikati yao. Kasema hili

Imaam al-Bayhaqiy? Je, hili limethibiti kwake? Na kama limethibiti, je inafaa

kuitumia kama hoja?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ndio limethibiti. Na kuna upokezi mwingine unaofanana na wa ´Aaishah ya

kwamba Ummu Salamah alifanya hivyo. Ingawa kitendo cha ´Aaishah na

Ummu Salamah vimethibiti, lakini si hoja. Kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) anasema:

"Swalini kama mlivyoniona nikiswali."

Na Hadiyth hii inamgusa mwanaume na mwanamke. Kama ilivyo katika

Kauli Yake (Ta´ala):

كاة لة وآتوا الز وأقيموا الص

"Na simamisheni Swalaah, na toeni Zakaah." (02:110)

Hii inamgusa mwanaume namwanamke. Lililo la dhahiri ni kuwa, Sunnah ni

mwanamke atangulie mbele ya wanawake kama afanyavyo Imamu.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=778

Page 5: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

5

2) ´Allaamah Muqbil Kuhusu Mwanamke Kunyoa Nywele Za Mwilini

Mwake

Swali:

Je, mwanamke anaweza kuondosha nywele za usoni mwake na za mwili wake

wote isipokuwa tu za kichwani tu?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Tunachomnasihi asiziondoshe, isipokuwa tu ikiwa kama yuko na ndevu.

Hakuna ubaya akaziondosha. Kwa kuwa akiziondosha kwa mara ya kwanza,

zitaongezeka na kuwa nyingi zaidi. Isitoshe zitakuwangumu na mbaya ilihali

angeliziacha zingekuwa laini. Tunamnasihi asifanye hivyo, na lau atafanya

hivyo hakuna neno. Hakuna dalili inayoharamisha na hili - In Shaa Allaah -

haliingii katika kubadilisha maumbile ya Allaah.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1556

3) Alikuwa Hatoi Zakaah Ya Dhahabu Kwa Ujinga Na Sasa Dhadhabu Yote

Imekwisha

Swali:

Kuna mwanamke alikuwa na dhahabu na wala hatoi Zakaah kwa kutokujua.

Na kwa sasa hakubaki na kitu. Je, ni juu yake kutoa Zakaah sasa au afanye

nini?

Page 6: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

6

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ndio. Ni wajibu kwake kutoa Zakaah ikiwa yuko na uwezo wa kufanya

hivyo, la sivyo itabaki juu ya dhimmah yake. Kwa kuwa hii ni haki ya

mafukara. Huu ndio wajibu wake.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/default_ar.aspx?id=662

4) Anamnyonyesha Mtoto Mbele Ya Dada Zake

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke kumnyonyesha mtoto wake mbele ya dada zake?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Hakuna ubaya akamnyonyesha mtoto wake mbele ya dada zake.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=338

5) Baada Ya Kutwahirika Akakutana Na Mumewe, Damu Imejitokeza Tena?

Swali:

Mwanamke alikuwa na hedhi na baada ya masaa sita akatwahirika. Na baada

ya mume wake kumjamii, hedhi ikarudi. Afanye nini?

Page 7: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

7

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ikiwa siku zake za ada ni sita kwa mfano, na siku sita hizo zikapita, asijali kwa

hichi kilichodhiri. Isipokuwa tu ikiwa jambo hili litakariri, hapo kutatazamwa.

Au itatazamwa vile vile damu yake ni nyingi au ndogo, ikiwa ni damu ndogo

haidhuru. Na ikiwa ni damu nyingi, atachukulia damu ya siku zile kuwa ni

damu ya hedhi. Haruhusiwi kuswali wala kufunga. Na kwa kutumia fursa hii,

nimeambiwa kuwa baadhi ya wahubiri Hudaydah wametusemea uongo na

kusema kuwa mimi naamrisha mwanamke kulipa Swalah zake na asilipe

Swawm. Huu ni uongo. Mikanda ipo inayotolea ushahidi hilo. Anadai kuwa

kaambiwa na watu waaminifu. Ni watu gani waaminifu ambao

wamekwambia hivyo wewe masikini?

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?sec_id=15

6) Baadhi Ya Vitabu Ambavyo Mwanafunzi Mwanamke Anapaswa Kuwa

Navyo

Swali:

Ni vitabu vipi ambavyo unamnasihi mwanamke wa Kiislamu kuwa nayo?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Tunavyomnasihi navyo ni kwa mfano; "Riyaadh-us-Swaalihiyn", "Fath al-

Majiyd" ambacho ni Sharh Kitaab-ut-Tawhiyd, "al-Lu-ul wal-Marjaan" na

"Buluugh-ul-Maraam". Hivi ni kwa mwanamke ambaye anaweza kusoma na

kuandika. Ni vitabu ambavyo ni mukhtaswari. Hali kadhalika kitabu cha

ndugu yetu Muhammad "al-Qawl al-Mufiyd". Ama kwa mwanamke mwenye

uwezo wa kufanya utafiti na uhak-ikisho, inatakikana kwake kuwa na

Maktabah kubwa kadiri na atakavyoweza. Alhamdulillaah.

Page 8: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

8

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1596

7) Dalili Kuwa Mwanamke Mwenye Hedhi Anaruhusiwa Kugusa Msahafu

Na Kusoma

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke mwenye hedhi kugusa msahafu na kusoma ndani

yake?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Sijui kama kuna makatazo yoyote ya kufanya hivi.

Ama Kauli Yake (Ta´ala):

ه إل المطهرون ل يمس

"Hawaigusi isipokuwa waliotwahara." (56:79)

Makusudio ni Malaika, kama Alivyosema (Subhaanahu wa Ta´ala) katika

Aayah ya ash-Shu´araa:

ياطين وما ينبغي لهم وما يستطيعون لت به الش وما تنز

"Na (wala) hawakuteremka nayo (hii Qur-aan) mashaytwaan. Na (wala)

haipasi kwao (kuteremka na Qur-aan) na wala hawawezi." (26:210)

Na amesema Imaam Maalik katika "al-Mu´attwah": "Kauli Yake (Ta´ala):

Inafasiriwa na Aayah ya ´Abasaa:

ها رة تذكرة فمن شاء ذكره فيكل إن طه رفوعة م مة م كر بأيدي سفرة كرام بررة صحف م

"Sivyo katu! Hakika (hizi Aayah za Qur-aan) ni ukumbusho. Basi atakaye

akumbuke. (Zimeandikwa) Katika swahifa zilizokirimiwa (Al-Lawh Al-

Page 9: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

9

Mahfuwdh). Zimetukuzwa na zimetwaharishwa. (Zinazobebwa) Katika

mikono ya (Malaika) waandishi. Watukufu (na) watiifu." (80:11-16)

Yaani hawakuteremka nayo Mashaytwaan, isipokuwa imeteremka na

Malaika. "Katika mikono ya waandishi", nao ni Malaika. "Watukufu (na)

watiifu."

Na amepokea al-Bukhaariy katika Swahiyh yake:

"Ibn ´Abbaas alikuwa haonelei mwenye janaba tu kusoma Qur-aan."

Hakuna ubaya kwa hili In Shaa Allaah. Tumebakia na Hadiyth nyingine

inayosema:

"Haigusi Qur-aan isipokuwa aliye Twahara."

Hadiyth hii katika njia zake zote, kuna mtu dhaifu ndani yake naye ni Swaalih

bin Hujjiyah. Lakini hata hivyo, tunachukua kama alivyoif-asiri Imaam ash-

Shawkaaniy katika "an-Nayl al-Awtwaar":

Maana yake ni:

"Haigusi Qur-aan isipokuwa Muislamu."

Abu Hurayrah kapokea pia kuwa:

"Hakika ya Muislamu hajanasiki."

Hivyo, maana yake ni kuwa haigusi (Qur-aan) isipokuwa Muislamu tu. Kwa

dalili ya kwamba, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikataza

kusafiri na Qur-aan katika ardhi (miji) ya makafiri.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/default_ar.aspx?id=8107

8) Damu Inayomtoka Mwanamke Kabla Ya Kujifungua

Swali:

Page 10: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

10

Mwanamke kabla ya kujifungua anakuwa na alama na anatokwa na maji maji.

Na wakati mwingine hali inaendelea namna hii siku mbili mpaka zaidi. Ipi

hukumu ya Swalah wakati wa hali hiyo?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ikiwa ni kabla ya kujifungua, haidhuru In Shaa Allaah. Anatakiwa kuswali.

Na ikiwa ni damu, huzingatiwa kuwa ni damu katika damu ya uzazi (nifasi).

Hapo Swalah itasimama kwake.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=2594

9) Haijuzu Kuoa Mwanamke Ambaye Mwanaume Kanyonya Kwa Mama

Yake

Swali:

Je, inajuzu kwangu kuoa mwanamke ambaye nilinyonya kwa mama yake

lakini yeye hakunyonya kwa mama yangu?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Haijuzu kwa kuwa huyo huchukuliwa kuwa ni dada yake katika kunyonya.

Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

"Ni Haramu kwa kunyonya kama yalivyo Haramu yanayopatikana katika

nasabu."

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=533

Page 11: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

11

10) Kajifungua Baada Ya Kuingia Swalah Ya Dhuhr, Ni Wajibu Kuilipa?

Swali:

Kuna mwanamke ambaye kajifungua baada ya kuingia kwa wakati wa Dhuhr.

Na kabla ya kujiwa na alama za kujifungua, kazaa. Je, ni juu yake kulipa

Swalah ya Dhuhr?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Lililo la dhahiri ni kuwa hana juu yake kulipa, kwa kuwa kajifungua wakati

wa Dhuhr. Na Shari´ah haikumlazimu mtu kuswali pale mwanzo wa kuingia

kwa wakati.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=644

11) Katwaharika Na Hedhi Lakini Daktari Kamkataza Kukoga

Swali:

Kuna mwanamke mgonjwa aliyekuwa na hedhi sasa katwaharika. Afanye nini

baada ya kutwahirika naye amekatazwa kukoga?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Baada ya kukatika damu yake atatayamamu. Mgonjwa akikhofia maradhi

yake yasizidi au kudumu, Allaah Kajaalia kutayamamu badala ya kutia

Wudhuu (kwa maji).

Page 12: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

12

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=450

12) Kauli Yenye Nguvu Ni Kuwa Mwanamke Kuonesha Uso Wake Ni

Haramu

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Uzuri wa mwanamke uko usoni mwake. Kauli yenye nguvu ambayo

imeegemea katika dalili ni kuwa, ni Haramu kwake kutoka ikiwa bado angali

ni mjane. Ama kama ameshakuwa mzee, kapewa rukhusa ya hilo. Anasema

Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala):

جات بز والقواعد من الن تي ل يرجون نكاحا فليس عليهن جناح أن يضعن ثيابهن غير متبر ينة وأن ساء الل

يستعففن خير لهن

"Na Al-Qawaa’id (wanawake wazee wasiozaa tena au kutokwa hedhi)

miongoni mwa wanawake ambao hawataraji kuolewa, basi hakuna ubaya juu

yao kupunguza baadhi ya nguo zao bila ya kuonyesha mapambo yao (au

kujishaua). Na kama wakijisitiri (kwa kujifunika vyema) ni kheri kwao."

(24:60)

Ikiwa ni mama mwenye umri mkubwa na wala hakuogopwi kwake

kufitinisha watu, lau atatoka na uso wake kaufunua, hakuna neno kwa hilo.

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1203

13) Kumnyonyesha Mtoto Baada Ya Miaka Miwili

Swali:

Page 13: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

13

Je, inajuzu kwa mwanamke kuomnyonyesha mtoto wake baada ya miaka

miwili?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Sioni ubaya wowote wa hilo. Ama Kauli Yake (Ta´ala):

والوالدات يرضعن أولدهن حولين كاملين

"Na wazazi wa kike wanyonyeshe watoto wao miaka miwili kamili." (02:233)

Hii ndio aghlabu ya watoto wengi. Lakini lau mtoto atakataa, akamnyonyesha

mwezi mmoja, miwili, mitatu au minne, sioni ubaya wowote wa hili.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=756

14) Kumpasua Mwanamke Ambaye Kafariki Na Tumboni Mwake Kuna

Mtoto Hai

Swali:

Lau mwanamke anakufa na tumboni mwake ana kijusi (mtoto) ambaye yuko

hai. Je, inajuzu kwa tabibu kupasua tumbo lake?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Sioni kama kuna makatazo yoyote ya hili, hakuna ubaya In Shaa Allaah

kupasua tumbo lake na kumtoa mtoto nje.

Muulizaji:

Page 14: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

14

Baadhi yao (madaktari) wanawaua.

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Kuwaua haijuzu. Haijuzu kumuua mtoto.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=381

15) Kunyonyesha Mbele Ya Wanawake Waislamu

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke kumnyonyesha mtoto wake mbele ya ndugu zake

wanawake katika Uislamu?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Sioni ubaya wa kufanya hivyo.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=338

16) Kutumia Dawa Ya Kuzuia Mimba Kutokana Na Uzito Anaoupata

Mwanamke

Swali:

Page 15: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

15

Kuna mwanamke ana mtoto mdogo ambaye ana miezi kumi na kwa sasa ana

ujauzito mwingine. Anahisi uzito wa kutazama watoto wake na ubebaji wa

mimba. Je, baada ya mimba hii mpya naweza kutumia dawa ya kuzuia

mimba?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Tunachomnasihi, amkabidhi amri yake Allaah. Na akikhofia juu ya nafsi yake

maangamivu na akaambiwa na matabibu wenye fani hii huenda akafikwa na

maangamivu na akafa, hapo anaweza kutumia dawa hiyo. Tunachomnasihi ni

yeye amtegemee Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) na amkabidhi amri yake

Allaah (´Azza wa Jalla).

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=3068

17) Maandamano Ya Wanawake

Swali:

Ni ipi hukumu ya maandamano ya wanawake?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Maandamano yamezushwa, sawa ikiwa ya wanaume na wanawake.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=2151

18) Mama Wa Mwanamke Niliyemtaliki Atabaki Kuwa Mahram Kwangu?

Page 16: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

16

Swali:

Mama wa mke wangu ambaye nimemtaliki anabaki kuwa Mahram au

hapana?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ndio. Anabakiwa kuwa Mahram.

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1501

19) Mavazi Ambayo Anapaswa Kuvaa Mwanamke Aliyefiwa Na Mume

Wake

Swali:

Mwanamke ambaye amefiwa na mume wake, je avae mavazi meusi au haya

ni maneno tu ya watu? Na je, atie wanja?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Mwanamke ambaye amefiwa na mume wake, avae mavazi ambayo hayavutii

watu kwake, sawa mavazi hayo yakiwa ni meupe au meusi. Akae eda miezi

minne na siku kumi. Kama Alivyosema Allaah (Ta´ala):

والذين يتوفون منكم ويذرون أزواجا يتربصن بأنفسهن أربعة أشهر وعشرا

"Na wale wanaofishwa miongoni mwenu na wakaacha wake, (hao wake)

wangojee nafsi zao miezi minne na siku kumi (eda ya mfiwa)." (02:134)

Akae masiku haya naye yuko katika nyumba ya mume wake ambapo kafa

ndani yake.

Page 17: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

17

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=651

20) Mke Hana Haki Yoyote Ya Kumpa Talaka Mwanaume

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke kumtaliki mume wake akishikwa na

wendawazimu au akakosa kuwepo kwa muda mrefu?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Mwanamke hana haki ya Talaka. Lakini akidhurika kwa kukosa kuwepo

kwake, ataenda kwa kiongozi. Na ni wajibu wa kiongozi kukubali maombi

yake ya kutengana kisha awatenganishe. Inatakikana kuwa namna hii ikiwa

atadhurika, sawa kwa kukosa kuwepo mume au akiwa ni mwendawazimu.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=2730

21) Mke Hataki Kukoga Janaba Na Anajua Ni Wajibu

Swali:

Ipi hukumu ya mwanamke ambaye hakogi janaba naye anajua kuwa kukoga

ni wajibu?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Page 18: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

18

Atazingatiwa kuwa ni mfanya madhambi na anafanya Haramu. Allaah (´Azza

wa Jalla) Anasema:

هروا وإن كنتم جنبا فاط

"Na mkiwa na janaba basi jitwaharisheni." (05:06)

Wajibu kwa Muislamu ni yeye kukimbilia kujitwahirisha kunapokuja wakati

wa Swalah. Ama lau maingiliano yatakuwa mwanzoni mwa usiku, mume

wake anaweza kutangulia kukoga kisha akafuata mke au wakakoga wote

wawili. Wanaweza vile vile kuchelewesha mpaka kabla ya Fajr. Hakuna

ubaya kwa hili. Katika hali hii itabidi watawadhe. Hakuna ubaya kufanya

hivi. Na kunapokuja wakati wa Swalah, ni wajibu kwake mwanamke

ajitwahirishe na aswali. Na kunapokuja wakati wa Swalah asijitwahirishe

wala kuswali, huku kutokuswali kwake anazingatiwa kuwa ni kafiri.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=2431

22) Mke Kumfanyia Mume Wake Maakulati Aina Mbali Mbali

Swali:

Mwanamke akimtengenezea mume wake vyakula aina mbalimbali, je,

kufanya hivi ni katika pumbao la dunia jambo ambalo limekatazwa?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Hakuna ubaya kufanya hivi In Shaa Allaah. Na mume ni mtu bora. Anasema

Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala):

ه لكم موا طي بات ما أحل اللـ ها الذين آمنوا ل تحر يا أي

"Enyi mlioamini! Msiharamishe vizuri Aliyokuhalalishieni Allaah." (05:87)

ه ل يحب المسرفين يا بني آدم خذوا زينتكم عند كل مسجد وكلوا واشربوا ول تسرفوا إن

Page 19: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

19

"Enyi bani-Aadam! Chukueni mapambo yenu katika kila Masjid; na kuleni na

kunyweni; na wala msifanye israfu. Hakika Yeye (Allaah) Hapendi

wanaofanya israfu." (07:31)

Kunapobakia kitu katika chakula, asikimwage bali anatakiwa kukitoa awape

masikini na wanaohitaji. Jambo hili ni sahali. Ama mwenye kusema kuwa ni

Haramu au haijuzu, haitupasi kwetu kuwaharamishia watu kitu ambacho

Allaah Kawahalalishia. Allaah (Ta´ala) Anasema katika Kitabu Chake:

ه الكذب ول تقولوا ذا حرام ل تفتروا على اللـ ـ ذا حلل وه ـ لما تصف ألسنتكم الكذب ه

"Na wala msiseme yanayosifu ndimi zenu uongo; hii halaal na hii haraam ili

mumzulie Allaah uongo." (16:116)

بي لم تحر ها الن ه لك يا أي م ما أحل اللـ

"Ee Nabii! Kwa nini unaharamisha kile Alichokuhalalishia Allaah?" (66:01)

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=555

23) Mke Kuomba Talaka Kwa Mume Wake Bila Ya Sababu Yoyote

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke kuomba Talaka kwa mume wake na lini anaweza

kuomba?

´Allaamah Muqbil:

Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Mwanamke yeyoye atakayeomba Talaka kutoka kwa mume wake bila ya

sababu yoyote, ni kaharamishiwa harufu ya Pepo."

Tunachomnasihi ni yeye kuwa na subira, na subira kwa mume wake na jamaa

zake huzingatiwa ni katika aina bora ya ´amali anazojikurubisha nazo mja

Page 20: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

20

kwa Allaah. Kama jinsi Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

alivyomuamrisha mume kuwa naye na subira na akasema:

"Mwanaume asimchukie muumini mwanamke, akichukia tabia fulani kutoka

kwake atapenda nyingine alionayo."

Masuala haya ni lazima pande zote mbili kuwa na subira, la sivyo mwanamke

ambaye hana subira ataachika kila mwaka na kuolewa na mume mpya. Hali

kadhalika, mume ambaye hana subira hali itakuwa ni hii hii. Allaah (´Azza wa

Jalla) Anasema:

قوى ول تعاونوا على الثم والعدوان وتعاونوا على البر والت

"Shirikianeni katika wema na taqwa, na wala msishirikiane katika dhambi na

uadui." (05:02)

Allaah (´Azza wa Jalla) Anasema:

ه بعضهم على بعض وبما أنفقوا من أموالهم ل اللـ امون على الن ساء بما فض جال قو الر

"Wanaume ni wasimamizi juu ya wanawake kwa kuwa Allaah Amefadhilisha

baadhi yao kuliko wengine na kwa sababu ya (matumizi) wanayotoa katika

mali zao." (04:34)

تي تخافون نشوزهن ه والل الحات قانتات حافظات ل لغيب بما حفظ اللـ المضاجع فعظوهن واهجروهن فيفالص

واضربوهن فإن أطعنكم فل تبغوا عليهن سبيل

"Basi wanawake wema watiifu, wenye kuhifadhi (hata) wanapokuwa

hawapo (waume zao) kwa Aliyoyahifadhi Allaah. Na wale (wanawake)

ambao mnakhofu uasi wao, basi waonyeni na (wakiendelea uasi) wahameni

katika malazi (vitanda) na (mwishowe wakishikilia uasi) wapigeni.

Wakikutiini, basi msitafute dhidi yao njia (ya kuwaudhi bure)." (04:34)

Hali kadhalika, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

"Mwanamke ni mpungufu wa akili na Dini."

Na anasema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kama ilivyokuja

katika "Swahiyhayn", Hadiyth ya Abu Hurayrah:

"Ninawausia kuwatendea wanawake wema, hakika wao wameumbwa kwa

ubavu uliopinda... "

Page 21: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

21

Tunachotaka kusema, ni lazima kuwa na subira kwa pande zote mbili sawa

mume na mke. Na kuna ndugu zetu hapa ya kuwa kuna mwanaume

aliyetalika wanawake watano katika siku moja. Alimtaliki wa kwanza. Akaja

wa pili na kumuuliza: "Alikufanya nini?" Akamwambia: "Na wewe

nimekutaliki."

Akaja wa tatu na kumwambia: "Wewe ni mwanaume mwenye khasira, kwa

nini umemtaliki?" Akamwambia: "Na wewe nimekutaliki."

Akaja mke wa nne na kutaka kumpa nasaha. Akamwambia: "Na wewe

nimekutaliki."

Na jirani wa nyumbani akamwambia: "Una nini wewe, wamekufanya nini?"

Akamwambia: "Na wewe nimekutaliki mume wako akipitisha hilo." Mume

wake akasema: "Nimepitisha hilo."

Baada ya hilo ni lazima kuwa na subira kwa mwanaume na mwanamke. Sote

ni wenye kughadhibika na tuna mapungufu mbalimbali. Ni lazima

tuvumiliane na tumche Allaah.

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=757

24) Mke Kuwapa Zakaah Dada Zake Na Mume Wake

Swali:

Kuna mama anamiliki dhahabu na imefikisha Niswaab. Je, inajuzu kuwapa

Zakaah dada zake au mume wake ambaye ni mzee na hana mali zaidi ya

dhahabu hii anayomiliki?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ndio. Inajuzu kwake kuwapa Zakaah dada zake ikiwa ni mafukara. Na

mpaka wa ufukara ni kule kufikia daraja ya kuhitajia ikiwa hawana vya

Page 22: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

22

kuwatosheleza. Inajuzu vile vile kumpa mume wake ikiwa ni fakiri. Kama

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alivyomwambia Zaynab mke wa

´Abdullaah bin Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anha). Alipomuuliza:

"Je, ni Halali kwangu kumpa Swadaqah ya mali yangu?"

Akasema:

"Ndio."

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1645

25) Mke Wake Alipotea Na Baadae Akampata Kishakuwa Na Mume

Mwingine

Swali:

Kuna mwanaume kaoa mwanamke kisha akapotea na hakumpata.

Mwanamke huyo akaolewa na ndugu yake mwingine kisha akarejea mume

wa kwanza baada ya miaka kumi. Yule wa kwanza na huyu wa pili wote

wamezaa nae watoto. Ipi hukumu ya watoto?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ikiwa alimuacha na hakuwa ni mwenye kumpa matumizi au alikuwa ni

mwenye kumsubiri huku akitaraji atakuja, yule mwanamke akajivua katika

ndoa. Na baada ya kujivua, atakuwa sio Halali kwa yule wa kwanza na

atakiwa ni wa huyu wa pili. Ama ikiwa hakujivua, lakini mara nyingi

hupeleka mashtaka yake kwa hakimu na kujivua. Na Allaah (Ta´ala)

Anasema:

وهن ول تضار

"Na wala msiwadhuru." (65:06)

Page 23: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

23

Akijivua, yule wa kwanza atakuwa hana njia nyingine. Anaweza kujivua

ikiwa anadhurika kwa matumizi, maisha na anaogopa kutumbukia katika

machafu. Katika hali hii, anaweza kujivua na atakuwa sio Halali kwa yule wa

kwanza.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=3083

26) Msimamo Wa Shaykh Muqbil Kuhusu Mwanamke Kufunika Uso

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Nawaelekeza katika kitabu cha ndugu yetu Mustwafah bin al-´Adawiy

(Hafidhwahu Allaah) kwa kuwa muda hautoshi kuzungumzia hilo [hukumu

ya kufunua uso]. Hii ni Radd kwa Shaykh al-Albaaniy (Hafidhwahu Allaah)

na kumbainishia ya kwamba ni wajibu kwa mwanamke kufunika uso wake.

Hali kadhalika kitabu cha Shaykh al-Answaar, hata kama kuna upetukaji wa

mipaka kwa Shaykh Albaaniy. Yasichukulie hayo, lakini faida zilizomo ndani

yake zichukuliwe.

Chanzo: http://muqbel.info/fatwa.php?fatwa_id=149

27) Mume Hataki Hijaab, Nifanye Nini?

Swali:

Mwamamke akitaka kujisitiri kwa Hijaab na mume wake au mmoja katika

ndugu zake anamkataza, pamoja na kuwa anayefanya hivyo ni katika

wanaoswali. Je, unamnasihi nini?

Page 24: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

24

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Tunamchomnasihi mume huyu, anatakiwa kumshukuru Allaah (Subhaanahu

wa Ta´ala) ambaye Kamjaalia mke mwema ambaye anapenda Hijaab. Badala

yake, anatakiwa amshaji´ishe juu ya hili. Kuwaangalia wanawake ni fitina. Ni

fitina juu yao wanawake na vile vile ni fitina kwa yule mtazamaji. Na Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

"Wanawake ni wapungufu wa akili na Dini... "

"Sijaacha fitina iliokuwa kubwa baada yangu kwa wanaume kuliko (fitina ya)

wanawake.”

Na anasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

Na ni Haramu kwake mume kumkataza. Hakika Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) anasema:

"Mwanamke ni ´Awrah (uchi), Pindi anapotoka nje, matumaini ya Shaytwaan

huongezeka." (Kaipokea at-Tirmidhiy, Hadiyth ya ´Abdullaah bin Mas´uud

(Radhiya Allaahu ´ahu)

Haijuzu kwake kumkataza, kama tulivyotangulia kusema. Hali kadhalika,

mwanamke huyu haitakiwi kwake kumtii juu ya hili. Ajisitiri kwa Hijaab. Na

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

"Utiifu ni katika mema."

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1401

28) Mume Kamtaliki Mke Wake Mara Sita Kisha Anasema Kuwa

Hakumbuki

Swali:

Page 25: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

25

Kuna mwanamke kumuacha mume wake na kwenda katika nyumba ya dada

yake hali ya kuwa yuko na watoto na baba yake. Mume wa dada yake akataka

kuwasuluhisha. Alipotaka kufanya hivyo, akasema mke kuwa hatorudi kwake

kwa kuwa ameshamtaliki mara sita na mimi kwake ni kama ajinabi. Na pindi

ninapomkumbusha (mume juu ya Talaka hizo) anasema kuwa hakumbuki. Je,

kufuatwe kauli ya mke au mume?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ni juu ya mwenye kudai abainishe na mwenye kukanusha ale yamini. La

dhahiri ni kuwa mume ndio mwenye kudai, kwa kuwa yeye ndio kamtaliki.

Kutokana na hili, ni juu yake kuleta mashahidi ya kuwa kamtaliki. Na kama

hakufanya hivyo, hana jengine ila kula yamini. Hili ndio la dhahiri. Ama

yaliyo baina yake (mke) na Allaah, akijua kweli kuwa kamtaliki zaidi ya mara

tatu, haijuzu kwake kumpa kitu. Kwa kuwa akifanya hivyo atazingatiwa

anazini nae.

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1644

29) Mume Na Mke Wanatofautiana Katika Masuala Ya Dini

Swali:

Mke katofautiana na mume wake katika jambo la Shari´ah. Yeye mke

anaamini kuwa ni Haramu na mume anaamini kuwa inaruhusiwa. Mume

anamuamrisha kukifanya. Je, mke amtii?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ikiwa kafikia daraja ya Ijtihaad, atakuwa ni mwenye kufanya ´Ibaadah kwa

ufahamu wake na Ijtihaad yake. Ama ikiwa ni mwanamke anayefuata

matamanio yake, ni juu ya mume kumpiga. Kwa mfano kamwambia:

Page 26: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

26

"Usitoke, usijishauwe naye anajishaua na anasema kuwa kujishaua kunajuzu".

Hivyo, ikiwa ni ambaye kafikia Ijtihaad, hapana asimpige kwa kuwa atakuwa

ni mwenye kufanya ´Ibaadah kwa Ijtihaad yake na si juu yake mume

kumlazimisha. Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

Miongoni mwa kuwatendea wema

"Nawausia kuwatendea wema wanawake."

Ni yeye mume kumshaji´isha juu ya kufahamu Kitabu cha Allaah na Sunnah

za Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ama Kauli Yake

(Ta´ala):

ه بعضهم على بعض وبما أنفقوا من أموالهم ل اللـ امون على الن ساء بما فض جال قو االر تات لحات قان فالص

ه حافظات ل لغيب بما حفظ اللـ

"Wanaume ni wasimamizi juu ya wanawake kwa kuwa Allaah Amefadhilisha

baadhi yao kuliko wengine na kwa sababu ya (matumizi) wanayotoa katika

mali zao. Basi wanawake wema watiifu, wenye kuhifadhi (hata)

wanapokuwa hawapo (waume zao) kwa Aliyoyahifadhi Allaah." (04:34)

Aayah hii, makusudio yake ni katika jambo lisilokuwa hili ambalo ni masuala

ya Ijtihaad. Pengine akawa ni mtafutaji elimu, anajua kiarabu, Hadiyth za

Mtume wa Allaah, Kitabu cha Allaah na kwa mfano anaona kuwa kuweka

mkono wa kulia juu ya kifua baada ya Rukuu ni Sunnah, na yeye mume

anaona kuwa sio Sunnah, ni juu ya kila mmoja kufanya vile anavyoona na

yasiyokuwa hayo, hili linatumika hata ikiwa ni katika masuala ambayo mume

anaona kuwa ni Haramu na mke anaona kuwa inaruhusiwa kutokana na

Ijtihaad yake. Ikiwa mke ni mjinga, ni juu yake kumfunza na yeye mume

ataulizwa kwa alichokichunga.

"Kila mmoja wenu ni mchunga na ataulizwa kwa alichokichunga."

Muulizaji:

Ikiwa ni katika masuala ya kufunua uso. Mke anaona kufunua uso ni jambo

linajuzu. Je, mume amkataze?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Page 27: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

27

Asimkataze [ikiwa mwanamke kafikia daraja ya Ijtihaad]. Akiweza

kumsubiria ni jambo zuri, la sivyo aachana nae. Ikiwa hawezi kuvum-ilia, si

juu yake kumkataza. Ingawa na sisi tunaona kuwa ni wajibu kwake kufunika

uso wake, kutokana na Hadiyth zilizotangulia:

"Mwanamke ni ´Awrah (uchi)."

Na Kauli ya Allaah (´Azza wa Jalla):

زواجك وبناتك ونساء المؤمنين يدنين عليهن من جلبيبهن بي قل ل ها الن يا أي

"Ee Nabii! Waambie wake zako, na mabinti zako, na wanawake wa Waumini

wajiteremshie jalaabiyb zao." (33:59)

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=2595

30) Mume Wake Kamtupa Miaka Miwili Na Kwenda Kutafuta Elimu

Swali:

Afanye nini mwanamke ambaye mume wake kamtupilia zaidi ya miaka

miwili kwa hoja ya kwamba anatafuta elimu. Na mwanamke huyu kuna

khatari akatumbukia katika fitina kwa kumkosa mume wake. Ipi hukumu ya

hili?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Mwanamke huyu akiweza kusubiri na ameachiwa matumizi na akapenda

mwenyewe kusibiri, basi afanye hivyo. Ama akikhofia nafsi yake fitina,

anaweza kuomba waachane.

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=687

Page 28: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

28

31) Mwanamke Alikuwa Hajui Kuwa Anajibika Kutoa Zakaah Ya Dhahabu

Zake Na Sasa Amejua

Swali:

Kuna mwanamke anamiliki dhahabu ambazo zimefikisha Niswaab. Na tokea

amiliki dhahabu hizi zimeshafanya Hawl sita na hakutoa Zakaah kwa kuwa

alikuwa hajui kuwa anawajibika Zakaah. Baada ya kujua alitoa Zakaah ya

miaka miwili na kumebaki miaka miwili mingine. Ipi hukumu ya hilo na

anawajibika nini?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Miaka iliobaki iko juu ya dhimmah yake. Kwa kuwa ni haki ya mafukara.

Ataitoa pale ambapo Allaah Atamsahilishia. Katika dhimmah yake kumebaki

deni juu yake. Na pale ambapo Allaah Atamsahilishia ataitoa kuwapa

mafukara.

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1646

32) Mwanamke Anasafiri Kila Siku Na Kwenda Kwenye Masomo Ya

Mchanganyiko

Swali:

Baadhi ya wanawake wanasoma katika chuo kikuu cha mchanganyiko.

Wanapoambiwa wasifanye hivyo, wanasema kuwa wanajitengenezea

Mustaqbal wao. Isitoshe, mwanamke huyu anasafiri bila ya Mahram. Ni ipi

hukumu ya Kishari´ah kwa hilo?

Page 29: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

29

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Mwanamke anayesoma katika chuo kikuu ambacho ni mchanganyiko,

huzingatiwa kuwa ni mwenye kukosea na anapata madhambi. Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema, katika Hadiyth ambayo imepotea

Usaamah bin Zayd (Radhiya Allaahu ´anhu):

"Sijaacha fitina iliokuwa kubwa kwa wanaume kama wanawake."

Na anasema tena (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Wanawake ni wenye akili na Dini pungufu."

Mwanaume anaenda na kutaka kumchumbia kwa familia yake, hapo

kafikisha miaka 25. Anaambiwa karibu, ila haitowezekana isipokuwa mpaka

baada ya kumaliza masomo yake. Lini atamaliza masomo yake chuo kikuu?

Baada ya miaka 52. Anamaliza masomo huku kishakuwa mzee na havutii

tena. Ilihali lau angeliolewa katika usichana wake, angelikuwa amekwishazaa

watoto watano, sita, saba n.k., kwa kiasi ambacho Allaah (Subhanaahu wa

Ta´ala) Atakuwa Amempa. Tunamnasihi kuacha masomo haya. Na Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

"Yule mwenye kuacha kitu kwa ajili ya Allaah, Allaah Humpa kilicho bora

kuliko hicho alichoacha."

Muulizaji:

Kusafiri bila ya kuwa pamoja na Mahram?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

"Sio Halali kwa mwanamke ambaye anamwamini Allaah na siku ya Mwisho

kusafiri bila ya kuwa pamoja naye Mahram."

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=2303

Page 30: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

30

33) Mwanamke Anatakiwa Kuolewa Pale Anapofikisha Miaka 13, 14 Au 15

Swali:

Ipi hukumu ya mwanamke kufanya kazi ya udaktari, ualimu na zisizokuwa

hizo?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Haya ni mabalaa ambayo wamepewa majaribio kwayo Waislamu na kupotea

kwa sababu yake. Mwanamke anatakikana kuolewa naye ni msichana wa

miaka 13, 14 au 15. Namna hii ndivyo inavyotakikana. Lakini yeye anataka

kukamilisha masomo yake; Thanawiy, chuo kikuu, masta, Dr. kisha baada ya

hapo anatoka kama mwalimu na ikiwa ni mke wa mtu analeta mfanya kazi

nyumbani. Anashindwa kumpa mtoto malezi na maadili ya Kiislamu.

Muhimu ni kuwa, Waislamu hawahukumu kwa Shari´ah ya Allaah katika

jambo hili.

Na wajibu kwetu sote tuhukumu kwa Shari´ah ya Allaah. Mwanamke bora

kwake ni yeye kuwa nyumbani kwake. Na kutoka kwake, huzingatiwa ni

fitina kwake yeye au kwa wengine. Haitakikani kwa yeyote kutoa idhini ya

kufunza, isipokuwa tu ikiwa kama ni kufunzana Qur-aan na anajiwa na watu

nyumbani kwake au anatoka na wala hachanganyiki na wanaume. Ama

kufunza au kusoma katika masomo tulionayo na mchanganyiko kwenye chuo

kikuu, hili ni jambo lisilojuzu kwa hali yoyote ile, kwani huzingatiwa kuwa ni

fitina.

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1111

34) Mwanamke Anaweza Kusafiri Na Mwanamke Mwenzake?

Page 31: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

31

Swali:

Mwanamke anaposafiri hali ya kuwa pamoja naye yuko na mwanamke

mmoja tu. Katika hali hii, Mahram anakuwa si wajibu kwake?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Hapana. Uwajibu bado uko pale pale. Kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) anasema:

"Si Halali kwa mwanamke anayemwamini Allaah na siku ya Mwisho, kusafiri

isipokuwa awe pamoja naye Mahram."

Na makusudio ya Mahram, ni yule ambaye imeharamishwa kwake kumuoa.

Na makusudio hapa anaingia mume vile vile.

Chanzo: http://muqbel.info/fatwa.php?fatwa_id=639

35) Mwanamke Kufanya Kazi Ili Awapatie Watoto Wake Riziki

Swali:

Je, mwanamke kufanya kazi ni Haramu ilihali naye amelazimika ili awalishe

watoto zake na hakuna mwingine wa kuwalisha?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ikiwa hachanganyiki na wanaume, mudiri, tabibu au wasiokuwa hao, naye

isitoshe amelazimika, akafanya kazi naye anajiaminia nafsi yake, heshima

yake na Dini yake, In Shaa Allaah hakuna ubaya kwa hilo.

Page 32: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

32

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=729

36) Mwanamke Kufanya Kazi Katika Idara Na Hospitali Za Mchanganyiko

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke kufanya kazi katika idara za serikali kwa hoja

hana ambaye atampa matumizi?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Katika hali kama hii, haijuzu. Kwa kuwa atachanganyika na mudiri, raisi na

atachukua ujira kutoka kwake. Hili halijuzu. Mwanamke anazingatiwa kuwa

ni fitina. Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema: "Mwanamke

ni ´Awrah (uchi), Pindi anapotoka nje, matumaini ya Shaytwaan huongezeka."

وإذا سألتموهن متاعا فاسألوهن من وراء حجاب

"Na mnapowauliza (wake zake) haja, waulizeni nyuma ya pazia." (33:53)

Hata kama Aayah hii inawahusu wake za Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam). Hata hivyo, inawagusa wanawake wote, kama alivyosema Shaykh

ash-Shinqiytwiy (Rahimahu Allaah). Mimi ninawanasihi kina dada, bali

nasema kuwa haijuzu kufanya kazi katika idara kama hizi ambazo zina

mchanganyiko na fitina. Hali kadhalika Hospitali za mchanganyiko,

tunawanasihi kujiweka mbali na haya.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=3907

37) Mwanamke Kumkogesha Mama Mzee Na Mwendawazimu Wasiojiweza

Page 33: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

33

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke kumkogesha mwanamke ambaye ni

mwendawazimu ambaye yuko hai na mwanamke ambaye ni mzee ikiwa

hawawezi kujikogesha wenyewe?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Akijiaminia kutopatwa na fitina na anayemuosha akawa na nguo zake,

hakuna ubaya wa hili. Ama akikhofia nafsi yake kupatwa na fitina, hapana

haijuzu, sawa kwake yeye na wengine.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1827

38) Mwanamke Kunyoa Nywele Za Mguuni Mwake

Swali:

Kuna dada anauliza kama inajuzu kwake kunyoa nywele za mguuni kwa ajili

ya kujipamba?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Tunachomnasihi aache kufanya hivyo. Kwa kuwa akishanyoa mara ya

kwanza itakuwa akijishughulisha kila wakati wake kunyoa nywele za mguu

wake. Ama kuhusiana na kuwa ni Haramu, sio Haramu. Lakini tunamnasihi

asianze kufanya hivyo, kwa kuwa asimtaabishe kunyoa.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=3050

Page 34: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

34

39) Mwanamke Kuondosha Nywele Za Kwenye Kidevu, Miguuni Na

Mwilini

Swali:

Je, inajuzu kuondosha nywele zilizo kwenye mwili wa mwanamke au

miguuni mwake?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ama kama ni kujuzu, inajuzu. Ama kukipatikana dawa akaziondosha mara

moja, ni sawa. Ama nywele ambazo ziko miguuni mwa mwanamke sio

mbaya. Lakini nywele za kwenye kidevu, hakuna ubaya akaziondosha au

akatumia dawa ambayo itafanya zisijitokeze mara nyingine. Na kama

sikukosea nadhani ni an-Nawawiy ambaye amesema kuwa ni wajibu kwa

mwanamke kuondosha nywele za kwenye kidevu ili asijifananishe na

mwanaume. Ama nywele za kwenye miguu yake, hakuna ubaya

akaziondosha na si kama ndevu.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=3050

40) Mwanamke Kusafiri Na Mahram Mtoto Awezae Kupambanua

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke kutoka mji kwenda mwingine akiwa pamoja na

mtoto wa kiume wa dada yake kwa ajili ya matibabu naye (mtoto huyo)

hajafikisha umri wa kuota ?

Page 35: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

35

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ikiwa mtoto huyo anaweza kupambanua mambo, hakuna ubaya kwa hili. Na

aghlabu ambaye kishafikisha miaka 10, 11 au 13 anakuwa ni mwenye kuweza

kupambanua. Hakuna ubaya kusafiri pamoja naye ikiwa kutaaminika fitina.

Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

"Sio Halali kwa mwanamke ambaye anamwamini Allaah na siku ya Mwisho

kusafiri isipokuwa awe pamoja naye Mahram."

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1062

41) Mwanamke Kuvaa Mavazi Meupe

Swali:

Hadiyth ambayo imependekeza kuvaa mavazi meupe, je, ni kwa wanaume na

wanawake? Na je, ni jambo lililopendekezwa hata kwa wanaume?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Lilio la dhahiri ni kuwa ni kwa wanaume. Kwa dalili ya Hadiyth ya ´Aaishah,

ya kwamba aliona wanawake wa Answaar wametoka kwa ajili ya Swalah ya

Fajr na walikuwa wamevaa mavazi meusi. Pamoja na haya, sio Haramu kwa

mwanamke kuvaa mavazi meupe. Jambo lililo la Haramu kwake ni

kujifananisha na wanaume. Kama ilivyokuja katika Swahiyh:

"Allaah Anamlaani mwanaume anayejifananisha na mwanamke; na

mwanamke anayejifananisha na mwanaume."

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=650

Page 36: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

36

42) Mwanamke Kuvaa Suwali Mbele Ya Mume Wake Na Wanawake

Wengine

Swali:

Ipi hukumu ya mwanamke kuvaa suruwali nyumbani kwake na mume wake

au mbele ya wanawake wenzake?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ni kujifananisha na maadui wa Uislamu. Suruwali ni kujifananisha na maadui

wa Uislamu. Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

"Yule mwenye kujifananisha na watu, basi yeye ni katika wao."

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?id=6024

43) Mwanamke Mwenye Hedhi Kuingia Msikitini Kutoa Darsa Kwa

Wanawake Wenzio

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke mwenye hedhi kuingia Msikitini kutoa mihadhara

kwa wanawake wenzake?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Kumepokelewa Hadiyth kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

amesema:

"Mimi sikuhalalisha Msikiti kwa mwenye hedhi wala janaba."

Page 37: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

37

Lakini Hadiyth hii ni dhaifu.

Na imethibiti katika Swahiyh ya kwamba kuna mwanamke ambaye alikuwa

anafanya kazi Msikitini na analala Msikitini. Na mwanamke huyu ada yake na

tabia yake ilikuwa ni kama wanawake wengine (wanaopata hedhi). Alikuwa

anafanya kazi Msikitini na akiishi humo. Pamoja na hivyo hakuwahi (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) kumtoa wala kumkataza kutoingia humo.

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anamwambia vile vile ´Aaisha

(Radhiya Allaahu ´anha) hali ya kuwa alikuwa ni mwenye hedhi alipokuwa

katika Hajj:

"Fanya kama anayofanya mwenye kuhiji, lakini usitufu Ka´abah."

Anasema tena Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumwambia

´Aaishah pindi alipomwambia amsaidie kumpokeza kitu, akasema ´Aaishah:

"Mimi ni mwenye hedhi."

Akasema (´alayhis-Salaam):

"Hedhi yako haiko mikononi mwako."

Lililo la dhahiri ni kuwa, hakuna ubaya mwanamke mwenye hedhi kuingia

Msikitini kwa sharti asiuchafue Msikiti. Pengine akatokwa na kitu, ni lazima

ajisitiri na kitu vizuri ili asiuchafue Msikiti na awafanyie Darsa dada zake.

Chanzo: http://olamayemen.net/Default_ar.aspx?ID=3134

44) Mwanamke Mwenye Hedhi Na Nifasi Kushika Msahafu Na Kuingia

Msikitini

Swali:

Ipi hukumu ya mwanamke mwenye hedhi kugusa msahafu pasina kizuizi?

Na ni ipi hukumu ya mwanamke mwenye hedhi na nifasi kuingia Msikitini?

Page 38: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

38

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Kugusa msahafu pasina kizuizi ni kwamba inajuzu kwa kukosekana dalili

sahihi zinazopinga hilo. Ama Kauli Yake (Ta´ala):

ه إل المطهرون ل يمس

"Hawaigusi isipokuwa waliotwahara." (56:79)

Makusudio hapa ni Malaika. Kama Alivyosema hilo Allaah (Subhaanahu wa

Ta´ala) katika Kitabu Chake Kitukufu:

لت به ياطين وما ينبغي لهم وما يستطيعون وما تنز الش

"Na (wala) hawakuteremka nayo (hii Qur-aan) mashaytwaan. Na (wala)

haipasi kwao (kuteremka na Qur-aan) na wala hawawezi." (26:210)

"Iliyoifasiri Aayah hii vizuri, ni Kauli nyingine ya Allaah (Subhaanahu wa

Ta´ala):

ها تذكرة فمن شاء ذكره في رة بأيدي سفرة كرام بررة كل إن طه رفوعة م مة م كر صحف م

"Sivyo katu! Hakika (hizi Aayah za Qur-aan) ni ukumbusho. Basi atakaye

akumbuke. (Zimeandikwa) Katika swahifa zilizokirimiwa (Al-Lawh Al-

Mahfuwdh). Zimetukuzwa na zimetwaharishwa. (Zinazobebwa) Katika

mikono ya (Malaika) waandishi. Watukufu (na) watiifu." (80:11-16)

Na makusudio hapa katika Aayah hii ni Malaika. Hivyo Aayah hii ya al-

Waaqi´ah makusudio ni Malaika. Na Allaah (Ta´ala) ndiye Mwenye Kujua

zaidi.

Ama mwanamke mwenye hedhi na nifasi kuingia Msikitini, sijui kama kuna

dalili yoyote katika Kitabu na Sunnah inayokataza hilo. Ama kuhusu Hadiyth:

"Mimi sikuhalalisha Msikiti kwa aliye na hedhi na janaba."

Hadiyth hii ni dhaifu.

Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anamwambia ´Aaishah

(Radhiya Allaahu ´anha):

"Hedhi yako haiko mikononi mwako."

Page 39: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

39

Na alimwambia tena (´alayhis-Salaam):

"Hapana! Fanya anayopasa kufanya mwenye kuhiji, isipokuwa tu usitukufu

kwenye Ka´abah."

Na katika zama za Mtume kulikowepo mwanamke ambaye anafanya kazi

Msikitini na anaishi Msikitini. Na mwanamke huyu alikuwa kishakuwa

mama, anajiwa na yanayowajia wanawake wengine. Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) hakuwahi katu kumwambia:

"Unapojiwa na hedhi, toke nje (ya Msikiti)."

Hapa kuna dalili inaonesha kuwa, inajuzu kwa mwanamke kuingia Msikitini

naye yuko na hedhi au nifasi.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=284

45) Mwanamke Wa Kiislamu Kutumia Vipodozi "Miquillaage"

Swali:

Ipi hukumu ya vipodozi maquillage kwa mwanamke?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Imethibiti ya kwamba ina madhara kama nilivyoona mwenyewe katika

maandiko ya kwamba inamdhuru mwanamke. Na huenda ikazeekesha uso

wake mapema. Ni Haramu hata kama itakuwa haina madhara. Na ni

kijifananisha na maadui wa Uislamu. Kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) anasema:

"Yule mwenye kujifananisha na watu, basi yeye ni katika wao."

Page 40: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

40

Na mimi, bali hata nyie mnaamini kuwa mambo haya yalikuwa hayajulikani

mpaka yalipotujia kutoka kwa maadui wa Uislamu na tukajifananisha na

maadui wa Uislamu.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/Default_ar.aspx?id=6022

46) Mwanaume Na Mwanamke Wote Ni Sunnah Kutahiriwa

Swali:

Ipi hukumu ya mwanamke kutahiriwa katika Uislamu?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ni Sunnah ya kimaumbile. Na miongoni mwayo akatata kutahiriwa. Na hili ni

kwa wote wawili mwanaume na mwanamke.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1463

47) Nasaha Za Shaykh Muqbil Kwa Mume Na Mke Ambao Ni Wanafunzi

Swali:

Ni katika mpaka upi ambao ni wajibu kwa mwanamke kumtii mume wake?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Page 41: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

41

Ama masuala ya wajibu, anatakiwa kumtii katika yale mambo ambayo Allaah

Kamuwajibishia juu yake. Miongoni mwayo, ni pale ambapo atamwita

kitandani. Na ikiwa mume ni fakiri, inatakikana kwa mwanamke awe na

subira kwake kadiri na atakavyoweza.

Pamoja na hivyo, kuna jambo ambalo ni pana zaidi kuliko uwajibu huu. Na

jambo hilo sisi tunamnasihi amvumilie mume wake katika raha na shida,

asimkalifishe mume kwa asiyoyaweza na kununua mambo mapya. Akiona

gari na nguo mpya, anamuomba mume wake amnunulie mfano wa gari hii na

nguo hiyo. Inatakikana kwake awe na subira na mume wake, amtendee

wema, kuwalea watoto wake, amfulie nguo zake, amsaidie katika kheri na

amtengenezee chakula kizuri pale itapohitajika kufanya hivyo. Wawe ni

wenye kusaidizana na khaswa pale ambapo nyinyi nyote ni wanafunzi

wanaume na wanawake. Muda unaweza kuwa mfinyu kwa mwanamke na

hilo likasababisha akawa na mapungufu katika baadhi ya haki za mume wake.

Katika hali hii, inatakikana mume kuwa na subira kwa mke wake. Na muda

unaweza kuwa mfinyu kwa mume na akawa na mapungufu katika baadhi ya

haki za mke wake. Katika hali hii, inatakikana mke kuwa na subira kwa mume

wake.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1733

48) Ni Wajibu Kwa Mwanamke Kuvaa Vifuniko Vya Mikoni (Gloves)

Swali:

Ipi hukumu ya vifuniko vya mikono (gloves) pindi mwanamke anapotoka

nyumbani?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ndio, tumeshatangulia kusema ya kuwa ni wajibu kwake kuufunika mwili

wake wote. Na Mtume (Swalla Allaahu ´alayh wa sallam) anasema:

Page 42: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

42

"Mwanamke ni ´Awrah (uchi), Pindi anapotoka nje, matumaini ya Shaytwaan

huongezeka."

Huenda mwanaume akafitinishwa na mwanamke vile vile akafitinishwa,

kama livyosema mshairi ya kwamba chanzo cha yote ni mtazamo... Wajibu

kwa mwanamke ni yeye awe amejisitiri, na akiweza kubaki nyumbani ni bora

kwake. Uislamu umekuja kumhifadhia heshima yake, damu yake na mali

yake. Lakini Waislamu wengi leo, wao ndio ambao wamepuuza mafunzo

haya yenye baraka.

Chanzo: http://www.olamayemen.net/default_ar.aspx?id=2972

49) Ni Wajibu Kwangu Mke Kumhudumia Mama Wa Mume Wangu?

Swali:

Kuna dada ambaye analazimishwa na mume wake kumhudumia mama yake,

pamoja na kuwa mwanamke huyo - yaani mama wa mume wake -

husababisha matatizo baina ya wanandoa. Na sasa dada muulizaji hawezi

kustahamili zaidi ya hayo. Afanye nini?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Allaah Awajaze kheri kwa Da´wah na hima mnayoifanya juu ya Uislamu. Na

Allaah Awabariki kwa juhudi zenu na Allaah Aunufaishe Uislamu na

Waislamu kupitia kwenu. Ama kuhusiana kama ni wajibu, sio wajibu kwa

mwanamke huyu kumhudumia mama wa mume wake, khususan ikiwa

anaamiliana naye mu´amala mbaya. Ama nasaha zetu, tunamnasihi azidi

kusubiri zaidi na zaidi na zaidi ya alivyosubiri. Hakika ya Allaah (´Azza wa

Jalla) Anasema katika Kitabu Chake Kitukufu:

Hakika ya Allaah (´Azza wa Jalla) Anasema katika Kitabu Chake Kitukufu:

قوى ول تعاونوا على الثم والعدوان وتعاونوا على البر والت

Page 43: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

43

"Shirikianeni katika wema na taqwa, na wala msishirikiane katika dhambi na

uadui." (05:02)

Pengine hayo (ya kutomhudumia) yakapelekea katika mfarakano na matatizo

baina ya mume na mke. Tunamnasihi, kwa njia ya nasaha na si kwa njia ya

uwajibu, amvumilie na asaidiane nae na amhudumie kwa mipaka

atakayoweza. Ama kuhusiana kama ni wajibu, sio wajibu kwake. Ni juu ya

mwanamke asimame kwa kufanya yale atakayoweza katika kazi za

nyumbani. Kama ilivyo katika Swahiyh, hakika ya Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam), wakati Faatwimah alipoja na kumshtakia uzito anaoupata

kutokana na kazi za nyumbani. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

hakumwambia kuwa huu sio wajibu wako. Kinachotakikana na

tunachomnasihi awe na ustahamivu na asaidiane na mume wake.

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=242

50) Ole Wako Mume Kumwacha Mke Wako Kwenda Kwa Wanawake

Hizbiyaat

Swali:

Je, inajuzu kwa mwanamke ambaye ameolewa kwenda katika mihadhara na

Darsa bila ya idhini ya mume pamoja na kujua kuwa mume wake

anamkataza?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Haijuzu kwake kwenda. Lakini ikiwa ni mwanaume mwema na ashukuru

(afurahi) kwa hili. Tunamnasihi mwanaume huyu amchukue na kumpelekea

katika nyumba ambayo kunafanywa mihadhara na kwenda nae baada ya

kumalizika kwamuhadhara. Haijuzu kwake mume kumkataza ilihali naye

hamfunzi. Ole wako, ole wako kwenda na mke wako kwa wanawake

Page 44: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

44

Hizbiyaat! Utarudi ukute yeye yuko upande huu na wewe uko upande

mwingine.

Chanzo: http://www.muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=1524

51) Shaykh Muqbil al-Waadi´iy Kuhusu Uke Wenza

Swali:

Tunaoma kalima kwa wanaume na wanawake kuhusu ukewenza?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Hili ni jambo muhimu enyi ndugu zetu.

ن الن ساء مثنى وثلث ورباع فإن خفتم أل تعدلوا فواحدة فانكحوا ما طاب لكم م

"Basi oeni waliokupendezeni katika wanawake; wawili au watatu au wanne.

Mkikhofu kuwa hamtoweza kufanya uadilifu, basi (oeni) mmoja." (04:03)

Hapa ni pale ambapo mwanaume anaimania nafsi yake ya kuwa atafanya

uadilifu. Hili ni jambo la kwanza. Jambo lingine awe yuko na uwezo. Ama

hali yake ikiwa ni ile ya watoto wako ni wagonjwa na amekosa hata pesa za

matibabu, kisha baada ya hapo anataka kuoa mke wapili, watatu au wanne

naye isitoshe ni mwanafunzi, hili litamshughulisha enyi ndugu. Allaah

Akimfungulia milango ya riziki na akamrahisishia njia ya mali, hakuna ubaya

akafanya hivyo bali tunamnasihi kufanya hivyo. Hali kadhalika, awe ni

mwenye kujiaminia nafsi yake ya kutomili kwa mwanamke mmoja. Na wala

haijuzu kwa mwanaume wala mwanaume kuharamisha Aliyohalalisha Allaah

(Ta´ala).

Lakini inatakikana kama tulivyotangulia kusema, ajilazimishe kufanya

uadilifu na awe na uwezo wa kuongeza mke wapili, watatu au wanne. Na

tunamuomba Allaah (Ta´ala) Awawekee wepesi ndugu zetu ambao hawajaoa.

Page 45: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

45

Tunamuomba Allaah Awawekee wepesi. Na ni kweli ya kuwa, kuna

wanawake Sunniy Dammaaj na nje ya Dammaaj na wanatamani kuolewa na

watafutaji elimu katika Ahl-us-Sunnah. Lakini pengine mama yake akawa

amtenza ndugu na kumwambia:

"Mume wa msichana wangu hatokuwa na mke isipokuwa mmoja tu. Atakuwa

na gari, makumbusho (museum) n.k."

Pengine wazazi wa msichana huyu wakawa wanamshaji´isha katika hili na

wakamwambia mwanafunzi aliyekuja kuchumbia: "Tunasikitika! Tumempa

fulani kwa utajiri wake na wewe umekosa kwa ajili wewe ni mwanafunzi."

Masikini, huenda mwanafunzi huyu hana lolote zaidi ya kilemba chake,

kanzu yake na suruwali yake. Wapi atatoa pesa zote hizi? Tunachowanasihi

ndugu zetu wasaidizane na ndugu zao ili kutengeneza familia njema na yenye

Imani. Na ni juu yako mzazi kumchagulia msichana wako mwanaume

mwema, akimpenda atamkirimu na akifikia kumchukia hatomdhulumu.

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=2632

52) Udugu Wa Kunyonya Wa Watoto Wa Mama Tofauti

Swali:

Mwanamke ana watoto wanne ambao kila mmoja ana mama yake. Na yule

anayemnyonyesha ndio mtoto wake. Je, watoto hawa wawili huzingatiwa

kuwa ni ndugu wa kunyonya pamoja na kutofautiana kwa mama zao?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Ndio. Huzingatiwa kuwa ni ndugu wa kunyonya hata kama kila mmoja ana

mama yake.

Page 46: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

46

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=12

53) Wamezini Katika Hali Ya Uchumba, Wanapigwa Mawe Au Wanauawa?

Swali:

Kuna mwanaume alichumbia mwanamke na alikuwa hajazini nae na baadae

kukatokea Zinaa katika kipindi hichi (cha uchumba). Je, asimamishiwe

adhabu ya bikira au adhahabu ya ambaye kishaingia katika ndoa?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Lililo la dhahiri kwangu naona kuwa atasimamishiwa adhabu ya bikira. Kwa

kuwa alikuwa hajamuoa. Katika hali hii, wote wawili watasimamishiwa

adhabu ya bikira ikiwa ndo mara ya kwanza wanaingia katika ndoa.

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php

54) Yupi Bora Kati Ya Wanawake Hawa Wawili?

Swali:

Ikiwa mwanamke anapenda kubaki nyumbani kwake na anaona ni bora

kubaki humo na hatoki hata kwenda Msikitini. Na mwanamke mwingine

ambaye anatoka kwenda kutafuta elimu na kwenda Msikitini. Yupi bora kati

ya hawa wawili?

´Allaamah Muqbil al-Waadi´iy:

Page 47: Fataawa Za Shaykh Muqbil Kuhusu Wanawake

47

Mwanamke ambaye anapenda kubaki kwake na kusoma nyumbani kwake

ndio bora. Kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

"Msiwazuia waja wa Allaah kwenda kwenye Misikiti ya Allaah. Na nyumba

zao ni bora kwao."

Chanzo: http://muqbel.net/fatwa.php?fatwa_id=557

Swalah na salaam ziwe juu ya Mtume wetu Muhammad, ahli zake na

Maswahabaha zake wote.