halmashauri ya kijiji cha kasangantongwe · shughuli za kiuchumi za wakazi wa kijiji cha...
TRANSCRIPT
HALMASHAURI YA KIJIJI CHA
KASANGANTONGWE
MPANGO WA USIMAMIZI WA
MSITU WA HIFADHI WA KANKOSYA KIJIJI
CHA KASANGANTONGWE
HALMASHAURI YA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE S. L. P. 1 MPANDA.
i
SEHEMU YA KWANZA - UTANGULIZI ....................................................................... 1
MAELEZO YA JUMLA YA MPANGO ........................................................................... 1
MAELEZO...................................................................................................................... 2
Msitu wa Hifadhi ya Kijiji cha Kasangantongwe ........................................................... 2
MSITU WA HIFADHI WA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE; .................................... 3
MATUMIZI YA MSITU WA HIFADHI YA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE ............. 4
KIJIJI CHA KASANGANTONGWE ............................................................................... 6
Sehemu ya tatu: ............................................................................................................ 7
Madhumuni ya mpango wa usimamizi wa msitu wa kijiji cha Kasangantongwe........ 7
ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA MPAPA. .................................................................. 8
ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA KABHUKINDU. ..................................................... 10
ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA ZIWA TANGANYIKA ............................................ 11
SEHEMU YA PILI ........................................................................................................ 12
MPANGOWA UTEKELEZAJI ..................................................................................... 12
Meneja Mteule ............................................................................................................. 12
Uwezo na Majukumu ya Kamati ya Mazingira ........................................................... 13
Majukumu ya Mwenyekiti wa kamati ya Maliasili ya Kijiji ......................................... 15
Majukumu ya Katibu wa kamati ya mazingira: ........................................................... 15
Majukumu ya Mtunza hazina: .................................................................................... 17
Msimamizi wa Doria: ................................................................................................... 17
ii
Majukumu ya Wahusika Wengine .............................................................................. 18
Halmashauri ya Kijiji: ................................................................................................... 18
Wanakijiji...................................................................................................................... 18
Wataalamu wa Misitu katika ngazi mbalimbali ........................................................... 19
Viongozi wa Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa,............................................................... 19
UTENDAJI KAZI WA KAMATI YA MALIASILI YA KIJIJI. .......................................... 20
MAELEZO MENGINEYO ............................................................................................ 20
UTOAJI TAARIFA ....................................................................................................... 20
UWEKAJI WA KUMBUKUMBU .................................................................................. 21
MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA ZA KAMATI YA MAZINGIRA ......................... 21
MATARAJIO YA UFANISI WA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA USIMAMIZI WA
MSITU.......................................................................................................................... 22
UTUNZAJI KUMBUKUMBU ........................................................................................ 23
VITABU VYA KUMBUKUMBU .................................................................................... 23
KITABU CHA MAKOSA NA FAINI.............................................................................. 23
KITABU CHA STAKABADHI...................................................................................... 24
VITABU VYA VIBALI ................................................................................................... 24
KITABU CHA DORIA .................................................................................................. 24
KITABU CHA AKAUNTI .............................................................................................. 25
KITABU CHA MAPATO NA MATUMIZI ..................................................................... 26
USIMAMIZI WA FEDHA.............................................................................................. 26
iii
WAHUSIKA WAKUU; .................................................................................................. 26
AFISA MUWAJIBIKAJI WA MASUALA YA FEDHA ................................................. 26
MATUMIZI YANAYOIDHINISHWA; ............................................................................ 28
Mipaka ya Msitu wa hifadhi wa kijiji cha Kasangantongwe ........................................ 29
MAELEKEZO MAALUM .............................................................................................. 29
ULINZI NA UKAGUZI WA ENEO LA MSITU WA KIJIJI CHA
KASANGANTONGWE ................................................................................................ 29
Sifa za Walinzi wa Msitu. ............................................................................................ 30
Wajibu, Majukumu na Mafao ya Walinzi wa Msitu wa Hifadhi ya Kijiji ...................... 31
OPERESHENI ............................................................................................................. 31
ZAWADI YA PONGEZI KWA MWANA DORIA ........................................................ 32
Kanuni za Kutumia Msitu wa Hifadhi ya kijiji .............................................................. 32
Kanuni za matumizi ya msitu: ..................................................................................... 33
Matumizi ya Msitu yanayohusu Ukataji wa Miti .......................................................... 33
TARATIBU NA SHERIA NYINGINEZO ...................................................................... 34
Adhabu ........................................................................................................................ 34
MCHAKATO WA KUMSHUGHULIKIA MKOSAJI NA KOSA ................................... 34
FAINI NA ADHABU KWA KILA KOSA ....................................................................... 36
FAINI ZA KUTOWAJIBIKA ......................................................................................... 37
KUUENDELEZA MSITU ............................................................................................. 37
UTANGULIZI: .............................................................................................................. 38
iv
UVUNAJI WA MITI ...................................................................................................... 38
HATUA ZA HARAKA ................................................................................................... 39
UFUATILIAJI ............................................................................................................... 40
Vigezo vya Mafanikio: ................................................................................................. 40
Wafuatiliaji ................................................................................................................... 41
Taarifa ya Ufuatiliaji Itatolewa kwa: ............................................................................ 41
Muda wa Kufanya Ufuatiliaji ........................................................................................ 41
Wataalam wa Misitu & ngazi za Eneo, (W)/ (M): ........................................................ 42
RATIBA YA UTEKELEZAJI ........................................................................................ 42
Hatua za Awali za Utekelezaji: ................................................................................... 42
Hatua Zitakazofuata .................................................................................................... 43
MUDA WA MPANGO, MAREKEBISHO NA MAPITIO YAKE: .................................. 43
1
MPANGO WA USIMAMIZI SHIRIKISHI WA MSITU WA HIFADHI YA KIJIJI CHA
KASANGANTONGWE
SEHEMU YA KWANZA - UTANGULIZI
MAELEZO YA JUMLA YA MPANGO
Mpango huu wa usimamizi umeandaliwa na Timu ya Tathimini Shirikishi ya Rasilimali
za Msitu kwa kushiriana na wataalamu wa misitu wa halmashauri ya wilaya ya
Mpanda.
Maandalizi ya mpango huu wa usimamizi wa msitu wa kijiji cha Kasangantongwe
umefanyika kwa niaba ya wananchi wa Kijiji cha Kasangantongwe ambao ndio
wamiliki wa msitu huu.
Mpango huu umepitishwa na Halmashauri ya kijiji na Mkutano Mkuu wa kijiji cha
Kasangantongwe na kuidhinishwa na Halmashauri ya Wilaya Mpanda.
Uamuzi wa kutenga na kuuhifadhi msitu huu wa kijiji cha Kasangantongwe kuwa
msitu wa Hifadhi wa kijiji umetokana na wanakijiji wenyewe kuona umuhimu wa
uhifadhi. Pia kuweka taratibu za kisheria ili kuwezesha kijiji kupata manufaa
yatokanayo na mazao na huduma za msitu na kuepusha vizazi vijavyo kukosa kabisa
rasilimali za msitu huu.
Malengo makuu ya mpango huu wa usimamizi wa msitu wa kijiji cha
Kasangantongwe ni kuhifadhi, Kuuendeleza na Kutumia kwa namna endelevu kwa
manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho cha Tanzania na dunia kwa ujumla.
2
MAELEZO
Msitu wa Hifadhi ya Kijiji cha Kasangantongwe
Msitu wa Hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe unahifadhiwa na kumilikiwa na
halmashauri ya Kijiji cha Kasangantongwe. Madhumuni ya msingi ya kuhifadhi msitu
huu ni kutunza na kuhifadhi uoto wa asili uliopo kwa wingi kwenye msitu huu, kutoa
mazao ya msitu na huduma ya/za misitu kwa kuzingatia misingi ya matumizi endelevu
na kuhifadhi bioanuai muhimu zinazopatikana ndani yake kwa manufaa ya vizazi vya
sasa na vijavyo vya Tanzania na ulimwengu kwa jumla.
Msitu huu wa hifadhi ya kijiji ni matokeo ya zoezi la Mpango wa Matumizi Bora ya
Ardhi ya kijiji lililofanyika mwaka 2015 na kuridhiwa na wananchi wote wa
Kasangantongwe.
Msitu huu umeenea eneo la Milima Kankosya, mto Lwega hadi mlima Mbamba
kufuata mito Itoto, Kamkindo, Kamnyovu, Mkangasi kuvuka mto Kakese pembezoni
mwa ghuba za Bundola, Kakese, Mbamba Mkangasi hadi Ziwa Tanganyika.kwa
upande wa mashariki, unapakana na barabara ya zamani ya watafiti wa madini wa
kampuni ya Anglo. Ukubwa wa msitu huu una eneo la hekta 5859.
Msitu huu una uoto wa miti ambao kwa kadiri sehemu kubwa una umri mkubwa na
sehemu nyingi vilevile ambazo zina uoto mchanga. Kwa juu msitu umefunga kwa
viwango tofauti tofauti toka sehemu moja hadi nyingine. Kuna sehemu ambazo msitu
umefunga sana kwa juu hasa kando kando ya mito Mkangasi, Kamkindo na Itoto,
sehemu zilizofunga wastani, na sehemu zilizo wazi hasa kutokana na uvamizi wa
msitu kwa ajili ya kilimo, sehemu zenye uoto wa mianzi na miti mtawanyiko na zile
sehemu za mabonde ambayo ni vyanzo vya maji na mbuga. Ndani ya msitu huu kuna
njia za miguu zinazounganisha kijiji cha Kasangantongwe na baadhi ya vitongoji vyake
3
na pia vijiji jirani vya Lufubu.Pia kuna njia nyingi zisizo halali za miguu ambazo
hutumiwa na wavamizi wa msitu kwa ajili ya kilimo, wapasua mbao na wategaji wa
wanyamapori. Mipaka ya msitu huu imewekwa alama za kudumu za maboya ya zege
(bikoni) na kwa upande wa Kaskazini msitu huu unapakana na Mto Lwega.
MSITU WA HIFADHI WA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE;
Msitu huu upo kaskazini mwa Kijiji cha Kasangantongwe. Msitu huu una ukubwa wa
hekta 5859 wenye bioanuai nyingi muhimu kwa kijiji na taifa kwa ujumla. Msitu huu
umeathiriwa kwa kiasi na shughuli za kibinadamu kama vile uchungiaji wa mifugo,
uchomaji moto, uvunaji holela, Kilimo na makazi holela msituni.
Hali ya msitu huu sio nzuri sana kutokana na uharibifu mkubwa unaofanyika kutokana
na upasuaji mbao haramu wa miti ya Myovu. Wapasuaji mbao walio wengi wanatoka
nje ya kijiji cha Kasangantongwe. Pia uvamizi wa msitu kwa ajili ya kilimo, hasa kando
kando ya Mto Lwega, hufanyika. Wavamizi wengi wa msitu kwa ajili ya kilimo ni
wasukuma wanatoka nje ya kijiji na wachache toka vijiji jirani hasa kando kando na
ndani ya Mto Lwega wanatoka nje ya kijiji upande wa mkoa wa Kigoma.
(Wilaya ya Uvinza).
Moto ni tishio la msitu wote wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe. Vyanzo vya moto
ndani msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe ni wawindaji wa wanyamapori,
wawindaji wa asali, wavuvi, wasafiri na wavuta sigara. Madhara ya moto ndani ya
msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe ni kuwa umebadilisha ukuaji wa uoto
wa msitu huu.
4
Msitu huu pia una vivutio vingine vya utalii kama vile safu za Milima ya Kankosya,
Mbamba kandokando ya ziwa Tanganyika, maeneo mengi yanayopendelewa na
Sokwe kwa ajili ya malazi na chakula na maporomoko ya maji ya Mto Lwega
unapoingia ziwa Tanganyika,
Mmiliki mkuu wa msitu huu ni Halmashauri ya Kijiji Cha Kasangantongwe, ambacho
kutokana na utaratibu wa muundo wa serikali za mitaa, usimamizi wa msitu huu
utafanywa kupitia ‘kamati ya Maliasili ya Kijiji kwa niaba ya wana kijiji wote wa kijiji cha
Kasangantongwe kwa kuwa hii ndiyo kamati katika muundo wa utawala wa vijiji
ambayo inahusika na usimamizi wa masuala ya mazingira ya kijiji kwa ujumla.
MATUMIZI YA MSITU WA HIFADHI YA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE
Kabla, msitu huu hapo awali haukuwa na utaratibu wowote wa jinsi ya kutumia au
kuvuna rasilimali zake, bali kila mtu aliingia kwa wakati wake na kuvuna chochote
alichohitaji kwa manufaa yake na kutoka bila ya kuhojiwa na mtu. Hali kadhalika,
ndani ya msitu huu kuna wafugaji wa jamii ya Kisukuma toka Shinyanga na Bariadi
ambao huchangia miti midogo kupotea kabisa.
Ukataji wa miti usiofuata mpango wa Uvunaji kulingana na uwezo wa msitu hupelekea
kutoweka kwa miti muhimmu kama Mninga, Mkora na Msawala katika msitu huu. Hali
kadhalika uchomaji moto unaofanywa na wafugaji ili kupata nyasi mpya na wawindaji
ili kurahisisha kazi yao ya kuwinda Pia imani potofu kwa baadhi ya wanakijiji kuwa
ukianzisha moto na ukawaka muda mrefu maana yake ni utaishi miaka mingi. Vitendo
hivi huua kabisa makuzi ya machipukizi na hivyo msitu hubaki na kizazi cha miti
mikubwa tu ambayo ndiyo ilikuwa ikivunwa.
5
Kwa upande wa matumizi ya rasilimali za msitu huu; zipo rasilimali zipatikanazo katika
msitu huu ambazo zina manufaa kwa uchumi wa kila mwananchi na kijiji kwa ujumla,
hizi ni pamoja na; -
• Msitu huu ni makazi ya wanyamapori ambao ni faida kwa kijiji na taifa kwa
ujumla.
• Ipo miti yenye manufaa kiuchumi kwa wananchi mfano miti ya mbao kama
Milembela, Mitundu, Mininga, Mibanga, Mikurungu, Kasanda, Mfulu, Mpilipili,
ambayo ina umuhimu kiuchumi na kwamba itakinufaisha kijiji endapo utaratibu
wa uvunaji utasimamiwa ipasavyo na kwa uaminifu, ndani ya msitu huu kuna
makorongo ambyayo ni mito ya msimu hasa wakati wa masika ila hunyauka
wakati wa kiangazi mfano Mkangasi Kamkindo na Mto Kakese, pia pembezoni
mwa msitu huu kuna mto Lwega unaotiririsha maji mwaka mzima.
Kuni ni moja wapo ya matumizi muhimu kiuchumi toka katika msitu huu.
• Aidha, watumiaji wakuu wa rasilimali za msitu huu wa kijiji cha
Kasangantongwe, ni wanakijiji wenyewe wa Kasangantongwe, pili ni wananchi
toka vijiji jirani kama Ikola, Isengule na Lufubu kwa upande wa Mkoa wa
Kigoma. Watumiaji wengine ni wale wakutoka nje ya kijiji na kata hii ya Isengule
na wafanyabiashara wa mazao ya misitu toka Mpanda mjini. Pamoja na taratibu
za kulipia zatakazo wekwa lakini yapo mahitaji mengine ambayo wanakijiji wa
Kasangantongwe pekee wataruhusiwa kuingia na kuvuna bila malipo bali kwa
utaratibu maalum.
6
KIJIJI CHA KASANGANTONGWE
Kijiji cha Kasangantongwe ni miongoni mwa vijiji vinne vilivyomo katika kata ya
Isengule Tarafa ya Karema wilayani Mpanda. Vijiji vingine vilivyomo kwenye kata hii
ya Isengule ni pamoja na Isengule, Maana ya Neno Kasangantongwe imetokana na
lugha ya kitongwe maana yake "amekutwa Mtongwe" Kijiji hiki kina jumla ya wakazi
1319 wanaoishi katika jumla ya kaya 412.
Kihistoria Kasangantongwe kilikua kijiji kamili na kusajiliwa mwaka 1999 baada ya
kukidhi vigezo vya usajili wa kijiji. Kijiji hiki kina vitongoji vinne (4) ambavyo ni
Isimwa, Kapondogoro, Keselamuyaga, na Kasangantongwe. Kijiji cha
Kasangantongwe kinapakana na vijiji vifuatavyo, upande wa kaskazini kinapakana na
kijiji cha Lufubu, kusini ni kijiji cha Isengule na shukula. Kwa upande wa magharibi
kinapakana na ziwa Tanganyika.
Kijiji hiki kina mchanganyiko wa makabila kadhaa. Makabila yanayotawala katika kijiji
hiki ni Watongwe, Wabende, Wafipa Wasukuma, na waha.
Shughuli za kiuchumi za wakazi wa kijiji cha Kasangantongwe zinategemea sana
Uvuvi na kilimo. Kwa upande wa kilimo wananchi wa kijiji hiki hulima sana zao la
Mihogo, Ufuta, Mahindi, Maharage na Mtama. Mazao haya huuzwa hapa kijijini na na
mengine kwa wingi huuzwa kwa wafanyabiashara toka Ikola na kwingineko.
Aidha, shughuli ya ufugaji hufanywa na kabila la wasukuma, wanyamwezi na wafipa
kwa kiasi kikubwa japo makabila mengine hufuga mifugo midogo midogo kama mbuzi,
kondoo bata na kuku.
7
SEHEMU YA TATU:
Madhumuni ya mpango wa usimamizi wa msitu wa kijiji cha Kasangantongwe
Msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe ni msitu wa kijiji unaohifadhiwa kwa
lengo la kutunza vyanzo vya maji, udongo na upatikanaji wa mazao na huduma za
msitu kwa njia endelevu. Kutokana na uharibifu wa msitu unaoendelea kufanyika
madhumuni hayo ya msingi yameathirika sana. Hivyo dhumuni kuu la mpango huu ni
kuimarisha utumiaji, ulinzi na uendelezaji wa eneo hilo la msitu kwa kushirikisha
wananchi ili kurejesha hali nzuri ya msitu iliyokuwepo. Hii itafanikiwa kwa kufanya
yafuatayo:
• Kuweka taratibu / kanuni za kutumia, kulinda, na kuendeleza msitu na Ziwa
Tanganyika kwa njia endelevu.
• Kuboresha ushiriki wa wadau wote katika usimamizi msitu.
• Kuongeza ushirikiano kati ya wananchi, Halmashauri ya Kijiji, Halmashauri ya
Wilaya na wakala wa huduma za misitu Tanzania.
• Kuwaelimisha wanakijiji wa Kasangantongwe juu ya umuhimu wa msitu kwao,
Taifa na Ulimwengu na jukumu lao la kufuata taratibu za utunzaji na matumizi
zilizowekwa na kukubalika.
• Kuuweka msitu wetu katika udhibiti madhubuti unaokubalika na wanakijiji wote
ili kwamba kusiwe na uvunaji holela, uvamizi wa mifugo, na ujenzi wa makazi
holela au kupanua mashamba kuingia katika msitu huu. Kwa kufanya hivi,
tutasaidia msitu huu kuwa chini ya umiliki wa kijiji chote kwa manufaa yetu wote
bila kudhulumiana na kwamba rasilimali zilizopo zitumike katika misingi
endelevu kwa faida ya kizazi hiki na kijacho.
Msitu huu umegawanyika katika maeneo makuu Matatu ya usimamizi (3) yaitwayo
8
“maeneo madogo ya usimamizi” (EDU) kama ifuatavyo; -
1) ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA Mpapa (2113 ha)
2) ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA Kabhukindu (2611 ha)
3) ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA Ziwa Tanganyika (1135ha)
RAMANI YA MSITU WA HIFADHI WA KIJIJI CHA KASANGANTONGWE
ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA MPAPA.
Eneo hili dogo la usimamizi (EDU) la Mpapa lina ukubwa wa hekta 2113 ambalo liko
Mashariki mwa msitu wa kijiji cha Kasangantongwe. Lina anzia pembezoni mwa mto
Lwega Usawa wa bikoni namba 3 na 4 (VF3 na VF4) kuelekea kusini kuvuka mto Itoto
9
na Kamuyovu, lina ambaa na barabara ya Anglo kulekea kusini kuvuka mto Mkangasi
na kuishia kwenye bikoni namba 8 na 9 (VF8 na VF9). Kwa upande wa magharibi
inapakana na EDU ya Kabhukindu. Lengo kuu la uhifadhi wa EDU hii ni “MATUMIZI”.
Kutokana na hali halisi ya EDU hii na uwiano wa ukubwa wa miti, uvunaji unaweza
kufanyika baada ya miaka mitano toka sasa, ili kuipa nafasi ya ukuaji wa miti muhimu
ifikie kwenye kiwango cha kuweza kuvunwa. EDU hii ina jumla ya miti 1,019,522 kwa
ujumla wakati jumla ya miti 247 tu ni miti inayofaa kuvunwa kwa ajili ya mbao kwa
miaka mitano ijayo, ambayo ni sawa na miti 49 tu kwa mwaka. Miti hiyo ni; -
• Msawala
• Mpilipili
• Mlembela
• Mbanga
• Mninga
• Msindwi
• Kabamba
• Kasanda
• Mkurungu
Hivo basi kwa kuwa uvunaji hautokuwepo kwenye EDU hii kwa wakati huu, yapo
matumizi mengine yanayoruhusiwa nayo ni kama yafuatayo; -
• Urinaji wa asali
• Uchimbaji wa dawa za asili (miti shamba)
10
• Kusenya kuni kavu (si miti mibichi)
• Ukataji wa nyasi za kuezekea nyumba
• Uvunaji wa miti ya boriti (pau), fito na nguzo
ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA KABHUKINDU.
Eneo hili dogo la usimamizi la Kabhukindu lina ukubwa wa hekta 2611. Kaskazini
linaanzia mto Lwega pembezoni mwa jiwe namba 3 (VF3) kuelekea kusini kuvuka
mlima Kankosya, mto kamkindo, mlima Mbamba na kuishia mbele kidogo ya mto
Kakese. Kwa upande wa mashariki linapakana na EDU ya Mpapakaskazini kuna mto
Lwega unaotenganisha kijiji cha Kasangantongwe na Lufubu, na upande wa
Magharibi inapakana na EDU ya Uhifadhi ya Ziwa Tanganyika. Lengo kuu la uhifadhi
wa EDU hii ni “MATUMIZI”
Kwakuwa uvunaji unaruhusiwa (matumizi) kwa ujumla EDU hii ina jumla ya miti
2,347,861 kwa ujumla wakati jumla ya miti ni miti inayofaa kuvunwa kwaajili ya mbao,
ambayo ni sawa na miti 544 kwa mwaka. Miti hiyo haina tofauti na ile ya EDU ya
Mpapa kwa kuwa ni msitu mmoja na wenye uoto wa aina moja ya Miombo nayo ni; -
• Msawala
• Mpilipili
• Mlembela
• Mbanga
• Mninga
11
• Msindwi
• Msolankanga
• Kasanda
• Mkurungu
Matumizi mengine yatakayoruhusiwa katika EDU hii ni pamoja na:
• Urinaji wa asali
• Uchimbaji wa dawa za asili (miti shamba)
• Kusenya kuni zilizojikaukia
• Ukataji wa nyasi za kuezekea nyumba
• Uvunaji wa miti ya boriti (pau) na fito na nguzo
• Shughuli za Utalii
ENEO DOGO LA USIMAMIZI LA ZIWA TANGANYIKA
Eneo hili linapakana na ziwa Tanganyika kwa upande wa magharibi. linaazia kusini
kwenye ghuba ya Kakese kwenye jiwe namba VF1, kuelekea kaskazini kuvuka mto
mkangasi na matawi yake, milimba ya Mbamba na kuishia ukingoni mwa mto Lwega.
Ukubwa wa eneo hili ni hekta 1135. Kwa upande wa mashariki eneo hili linapakana
na eneo la Kabhukindu.
12
SEHEMU YA PILI
MPANGOWA UTEKELEZAJI
Meneja Mteule
Katika mpango huu wa usimamizi wa msitu wa hifadhi wa Kijiji cha Kasangantongwe,
meneja atakuwa ni KAMATI YA MALIASILI YA KIJIJI ambayo hufupishwa kama
VNRC (kwa kiingereza ni Village Natural Resources Committee). Kamati hii ni ile
inayoelekezwa katika muundo wa uongozi wa vijiji. Kamati hii itakuwa na wajumbe 14
kwa mchanganuo ufuatao;
• Wawakilisha toka kila kitongoji cha kijiji
• Skauti wa kijiji wasiopungua wawili kama hawapo basi hata askari mgambo
wanaweza kutumika badala ya Skauti wa kijiji
• Mtu/watu maarufu katika kijiji wanaoweza kuchangia katika suala zima la
uhifadhi. mfano wazee maarufu na wakongwe wa kijiji n.k.
• Wanawake (Theluthi moja au 30% ya wajumbe wote) maalumu kwa nafasi ya
upendeleo kwa wanawake.
Kamati hii itapatikana kwa kufuata utaratibu ufuatao; -
• Wajumbe hawa watachaguliwa na mkutano mkuu wa kijiji
• Baada ya majina hayo kupatikana Halmashauri kuu ya Kijiji huketi na
kuyathibitisha majina hayo.
• Kamati hii itakuwa madarakani kwa muda wa miaka mitatu (3) baada ya hapo
uchaguzi unafanyika tena. mjumbe anaweza kuchaguliwa tena kulingana na
imani ya wananchi kwake.
13
• Mwenyekiti, katibu na mweka hazina watachaguliwa miongoni mwa wajumbe
waliochaguliwa na mkutano mkuu na kuthibitishwa na Halmashauri ya kijiji.
• Kamati hii itapewa nguvu ya kisheria ya kusimamia sheria ya kijiji na itawajibika
kwa Halmashauri kuu ya Kijiji.
• Itaandika taarifa ya utekelezaji kwa Halmashauri ya kijiji mara moja kila mwezi,
yenye nakala kwa Afisa Misitu (W)
• Itafanya vikao vyake mara moja kila mwezi na vya dharura pale inapobidi.
• Itapokea, kujadili na kufuatilia taarifa za walinzi wa msitu (Kamati ya doria) na
vikundi vingine vitakazoundwa kuisaidia Kamati ya Mazingira katika kutekeleza
majukumu yake.
Uwezo na Majukumu ya Kamati ya Mazingira
• Kuhakikisha kuwa mipaka yote ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe
inaeleweka waziwazi kwa wanakijiji wote wa Kasangantongwe.
• Kusimamia utekelezaji wa mipango yote inayohusu utumiaji, ulinzi na uendelezaji
wa kijiji cha Kasangantongwe.
• Kutunza kumbukumbu zote zinazohusu shughuli za utumiaji, ulinzi, na uendelezaji
wa msitu wa hifadhi ya kijiji. Kumbukumbu hizo ni: -
▪ Mihtasari ya mikutano
▪ Doria
▪ Uhalifu na faini
▪ Vibali vilivyotolewa
▪ Mapato na matumizi ya fedha za msitu
14
▪ Uoteshaji na upandaji miti, pia shughuli zote za uhifadhi mazingira
ndani ya maeneo ya kijiji
• Kuhakikisha kuwa walinzi wa msitu (timu ya doria) wanatekeleza kazi yao
kikamilifu na kuchukua hatua zinazopasa kuondoa dosari zinazojitokeza katika
kazi ya ulinzi.
• Kufanya ukaguzi wa msitu wa hifadhi ya kijiji angalau mara mbili kwa mwezi.
• Kuhakikisha matumizi endelevu ya msitu yanazingatiwa kulingana na kanuni za
matumizi zilizowekwa na kukubaliwa.
• Kuwashughulikia wahalifu wa msitu kwa mujibu wa kanuni za adhabu zilizowekwa
na kukubalika kwa ushirikiano na Halmasahauri ya kijiji.
• Kwa ushirikiano na Halmashauri ya kijiji, kuwahamasisha wanakiiji kushiriki katika
suala zima la uhifadhi wa msitu na mazingira ya kijiji kwa ujumla.
• Kutumia na kutunza vitabu vya stakabadhi vilivyoidhinishwa na Halmashauri ya
Wilaya ya Mpanda.
• Kufungua Akaunti Benki ya Kamati ya Mazingira ya kijiji kwa ajili ya kuweka fedha
za mapato ya msitu (ushuru na faini).
• Kuhakikisha kuwa fedha za Akaunti ya Kamati ya Mazingira zinatumika kama
zilivyokusudiwa na kuidhinishwa na Halmashauri ya kijiji cha Kasangantongwe.
• Kuweka utaratibu wa utoaji wa vibali ili kuhakikisha kuwa vibali vinavyotolewa ni
vile vilivyoko katika mamlaka ya Kamati ya Mazingira na kwamba utoaji wa vibali
unakwenda sambamba na mahitaji yaliyopo na sio vinginevyo.
15
Majukumu ya Mwenyekiti wa kamati ya Maliasili ya Kijiji
• Kuhakikisha kuwa mikutano ya Kamati ya Mazingira inafanyika ipasavyo kwa
kufuata ratiba iliyopangwa. (angalau mara moja kila mwezi)
• Kuhakikisha kuwa Mhasibu na Katibu wa Kamati ya Mazingira wanafanya kazi
zao ipasavyo kwa kuweka kumbukumbu zote za vibali, doria, faini, idadi ya
wahalifu, fedha zilizopo, matumizi n.k.
• Kuhakikisha kuwa Kamati ya doria ya msitu wa hifadhi ya kijiji wanafanya kazi
yao ipasavyo na wanapewa haki zao kama zilizoainishwa kwenye Mpango huu.
• Atakuwa mmoja wa watia sahihi wa Akaunti ya Kamati ya Mazingira wakati wa
kutoa fedha Benki kwa matumizi yaliyoidhinishwa na Halmashauri ya kijiji kwa
ajili ya uendelezaji wa msituna shughuli zingine za maendeleo kijijini.
• Atawajibika kuhudhuria vikao vyote vya Halmashauri kuu ya kijiji na kutoa
taarifa ya utendaji kazi wa kamati.
Majukumu ya Katibu wa kamati ya mazingira:
• Atawajibika Kuweka na kutunza kumbukumbu zifuatazo: - Kumbukumbu za
mikutano yote (Kitabu cha kumbukumbu za mikutano)
o Doria zilizofanyika, uhalifu/uharibifu ulioonekana kwenye kitabu cha
Doria.
o Uhalifu ulioonekana, wahalifu waliohusika, faini zilizotozwa, tarehe ya
uhalifu na faini zilizolipwa kwenye kitabu cha “Uhalifu na faini”
o Vibali ilivyotolewa, kwa nani, kwa ajili gani, fedha zilizolipwa, tarehe,
namba ya risiti, n.k kwenye kitabu cha Vibali
16
o Fedha zilizotolewa, tarehe, kwa ajili gani, namba ya risiti kwenye kitabu
cha Risiti na fedha.
• Atahakikisha kuwa Akaunti ya Mazingira inafunguliwa na mara kwa mara baada
ya kupokea fedha na kuziingiza kwenye vitabu vinavyohusika zinapelekwa
Benki na Mweka Hazina.
• Atakuwa mmoja wa watia sahihi wa Akaunti ya Kamati ya Mazingira wakati wa
kutoa fedha Benki kwa matumizi yaliyoidhinishwa na Halmashauri ya kijiji kwa
ajili ya uendelezaji wa msitu na shughuli zingine za maendeleo kijijini.
• Atawajibika kusimamia utekelezaji wa maagizo ya Serikali ya Kijiji na
Halmashauri kuu ya kijiji
• Atawajibika kuandaa taarifa ya utendaji kazi wa kamati na maendeleo ya msitu
kila mwezi, robo mwaka, nusu mwaka na mwaka na kuwasilisha katika mkutano
mkuu wa kijiji wa robo mwaka baada ya kupitiwa na Halmashauri kuu ya kijiji.
• Ataidhinisha doria kufanyika kwa maandishi maalumu ambayo mwenyekiti wa
kijiji pia atapaswa kujulishwa kwa wakati utakaoonekana unafaa kulingana na
mazingira.
• Atapokea taarifa ya doria mara baada ya kumalizika na kukagua daftari la doria.
• Atatunza kumbukumbu za kesi zote za wavunaji haramu wa mazao ya msitu
wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe.
• Atawajibika kutunza orodha ya wavunaji wote wa rasilimali za msitu wa hifadhi
ya kijiji cha Kasangantongwe pamoja na kiasi walichovuna na kuwasilisha kwa
DFO/DED kila mwezi.
• Atawajibika kusimamia mapato na matumizi kwa umakini na kutoa taarifa kwa
Halmashauri ya kijiji kila inapoonekana inafaa
17
Majukumu ya Mtunza hazina:
• Atawajibika kutunza kumbukumbu zote za mapato yatokanayo na leseni za
uvunaji wa mazao ya misitu na vibali mbalimbali.
• Atawajibika kutunza kumbukumbu za matumizi yote ya fedha zitokanazo na
maduhuli ya mazao ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe kama
ilivyoidhinishwa na vikao husika vya kijiji cha Kasangantongwe na siyo
vinginevyo.
• Ataandaa taarifa ya Mapato na Matumizi ya fedha ya Kamati ya Mazingira na
kuiwasilisha kwenye vikao vya Kamati ya Mazingira.
• Atakuwa mmoja wa watia sahihi wa Akaunti ya Kamati ya Mazingira wakati wa
kutoa fedha Benki kwa matumizi yaliyoidhinishwa na Halmashauri ya kijiji kwa
ajili ya uendelezaji wa msitu na shughuli zingine za maendeleo kijijini.
Msimamizi wa Doria:
• Atatakiwa kusimamia doria zote na kuziongoza
• Atatunza daftari la kila mtu atakayekamatwa katika msitu wa kijiji akivuna
mazao ya misitu bila idhini (kibali) cha kijiji.
• Atawajibika kumuweka chini ya ulinzi mtu yeyote pamoja na maliasili
aliyokamatwa nayo (kama ipo) na kumkabidhisha kwa mtendaji wa Kijiji kwa
hatua zaidi za kisheria.
• Atawajibika kuhakikisha ulinzi wa mipaka ya msitu unadumu na kuwa imara ili
msitu usivamiwe kwa kilimo, makazi au kuchungia.
18
Majukumu ya Wahusika Wengine
Halmashauri ya Kijiji:
Itakuwa mhusika mkuu katika utekelezaji wa mpango huu kwa upande wa kijiji na
itakuwa na wajibu na majukumu yafuatayo: -
• Kusimamia utekelezaji wa mpango
• Kutunga na kusimamia Sheria ndogo
• Kuhakikisha kuwa Kamati ya Mazingira inafanya kazi yake ipasavyo.
• Kushirikiana na wataalamu wa Misitu wa ngazi zote katika kuandaa mikakati
mipya ya uhifadhi misitu na mazingira kwa jumla.
• Kufanya ufuatiliaji na tathimini ya utekelezaji wa mpango huu, kwa kuwa na
agenda ya kudumu katika vikao vyake vya kila mwezi pia kutembelea msitu wa
hifadhi angalau mara moja kila mwezi.
Wanakijiji
Watashiriki katika shughuli za utumiaji, ulinzi na uendelezaji wa msitu wa hifadhi kama
ifuatavyo: -
• Kuzuia na kuzima moto katika maeneo yao ya makazi, mashamba na misitu
inayowazunguka.
• Kusafisha mipaka ya nje ya msitu wa hifadhi ya kijiji na kuhakikisha kuwa iko
wazi wakati wote wa mwaka.
• Kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu.
• Kuotesha na kupanda miti kwa lengo la kupunguza utegemezi wa misitu ya asili
kwa kila zao au huduma ya msitu.
19
• Kushiriki katika mikutano na kuchangia katika kuandaa mikakati mipya ya
kutumia, kulinda na kuendeleza msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe.
• Kubuni na kutekeleza shughuli mbadala za kuongeza kipato ili kupunguza
umaskini kwa kutumia rasilimali zilizo ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji, zilizo
katika maeneo ya makazi. Baadhi ya mbinu hizo ni ufugaji wa nyuki kwa njia za
kisasa, usukaji wa mikeka kwa kutumia ukindu kwa ajili ya soko, Kuzingatia
matumizi ya majiko banifu, nishati mbadala na matumizi sahihi ya mazao ya
misitu.
Wataalamu wa Misitu katika ngazi mbalimbali
• Kutoa msaada wa kitaalam katika kubuni mikakati mipya ya kuhifadhi msitu wa
hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe
• Kusaidia shughuli za uoteshaji na upandaji miti.
• Kusimamia Sera ya Misitu na Sheria ya Misitu 14, 2002.
• Kufanya ufuatiliaji na tathimini ya utekelezaji wa mpango huu wa usimamizi.
• Kusaidia utekelezaji wa mpango.
Viongozi wa Kata, Tarafa, Wilaya na Mkoa,
• Kutoa msukumo katika utekelezaji wa mpango
• Kuhakikisha kuwa Polisi na Mahakama zinatekeleza wajibu wao ipasavyo
katika utekelezaji wa Sheria ya Misitu No. 14, 2002 na Sheria zinazosimamia
rasilimali za majini.
• Kushirikiana na Idara ya Misitu na Nyuki.
20
• Kutoa msukumo katika utekelezaji wa Sera, Sheria na Kanuni za kutunza na
kulinda misitu.
• Kusaidia utatuzi wa migogoro inapotokea.
UTENDAJI KAZI WA KAMATI YA MALIASILI YA KIJIJI.
• Itafanya kazi zile zile zilizoainishwa katika majukumu ya kamati ya maliasili ya
kijiji
• Itakutana mara moja kila mwezi
• Itatunza mihutasari ya mikutano yake
• Mkutano utafanyika iwapo tu idadi ya wajumbe imefika nusu ya wajumbe wote.
• Katika kila mkutano watapaswa kupokea taarifa ya doria na mwenendo wa
uvunaji wa mazao ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe kutoka kwa
kiongozi wa doria.
• Watatakiwa kujua idadi ya leseni zilizotolewa katika mwezi husika, kiasi cha
maliasili kilichovunwa na mapato yaliyopatikana
• Watapokea na kujadili maombi ya leseni za kuvuna mbao kwa kuwasilisha kwa
Serikali ya Kijiji.
• MAELEZO MENGINEYO
UTOAJI TAARIFA
• Kamati ya Mazingira ya kijiji itatoa taarifa ya utekelezaji kwa Halmashauri ya
kijiji mara moja kwa mwezi yenye nakala kwa Afisa Misitu wa Wilaya Mpanda.
21
• Afisa Mtendaji wa Kijiji (VEO) atatoa taarifa ya maendeleo ya shughuli za msitu
wa hifadhi ya kijiji na kwa Mkutano Mkuu mara nne (4) kwa mwaka yenye
nakala kwa Afisa Mtendaji Kata (WEO) na Afisa Misitu (W).
UWEKAJI WA KUMBUKUMBU
Kumbukumbu zifuatazo zitawekwa na kuhifadhiwa na Kamati ya Mazingira ya Kijiji:
• Mihutasari ya vikao vya kamati
• Uhalifu na faini zilizotozwa
• Doria zilizofanyika
• Stakabadhi ya fedha na Hati ya malipo.
• Vibali vilivyotolewa
• Akaunti ya Kamati ya Mazingira
• Mapato na matumizi ya fedha za msitu.
MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA ZA KAMATI YA MAZINGIRA
Mapato ya Kamati ya Mazingira yatatokana na:
• Faini zitakazotozwa wahalifu wa msitu wa hifadhi ya kijiji.
• Malipo ya mazao na huduma ya msitu yaliyoruhusiwa kwa kulipia katika
Mpango huu.
• Mauzo ya mazao ya msitu yaliyokamatwa na zana zilizokamatwa katika ulinzi.
• Wafadhili na wasamaria wema watakaotoa fedha/ msaada kwa ajili ya
22
Usimamizi wa msitu wa hifadhi ya kijiji.
Mapato yatokanayo na mazao na huduma za msitu wa kijiji cha Kasangantongwe
yatakua ni mali ya kijiji cha Kasangantongwe kwa asilimia 100% na hayatagawanywa
yatagawanywa kati ya Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda.
MATARAJIO YA UFANISI WA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA USIMAMIZI WA
MSITU
Katika matembezi ya kukatiza msitu vikwazo Matatizo yafuatavyo vilibainika msituni:
• Moto kichaa
• Uvunaji haramu wa mbao
• Uchungiaji wa mifugo
• Kilimo msituni
• Ukaaji wa miti
Mpango wa usimamizi ukitekelezwa vilivyo kwa msitu huu hifadhi wa kijiji cha
Kasangantongwe kwa kuzingatia vikwazo vilivyobainika katika matembezi ya kukatiza
msitu kama yalivyofupishwa hapo juu yafuatayo yanatarajiwa kuonekana;
• Kupungua au kutoweka kabisa kwa matukio ya moto
• Kuwepo kwa watuhumiwa wa kesi za uchomaji moto hovyo msituni kwa
utaratibu wa kukubalika/kwa kufuata taratibu za nchi
23
UTUNZAJI KUMBUKUMBU
Mpango huu wa usimamizi unaainisha bayana ni kumbukumbu zipi zitatunzwa,
zitatunzwa katika vitabu gani na vitabu hivyo vitatunzwa na nani kwa utaratibu gani.
Ufuatao ni ufafanuzi; -
VITABU VYA KUMBUKUMBU
Hiki ni kitabu kitakachohusika na kutunza kumbukumbu zifuatazo,
• Kumbukumbu za mihutasari ya vikao vya kamati
• Kumbukumbu za maamuzi mbalimbali ya kamati
• Tukio lolote linalofanywa na kamati au watu wachache waliotumwa na kamati
• Matokeo ya shughuli yoyote iliyofanywa na kamati au watu wachache
walioteuliwa na kamati
• Kumbukumbu za ukaguzi wowote uliofanywa na kamati au baadhi ya
wanakamati waliotumwa na kamati
KITABU CHA MAKOSA NA FAINI
Kumbukumbu za makosa yoyote yaliyofanywa na mhalifu dhidi ya sheria ndogo za
Kijiji cha Kasangantongwe ya Kuhifadhi Msitu wa Kijiji cha Kasangantongwe.
• Jina la mkosaji na kosa alilokosa Kiasi alichotozwa, tarehe aliyotozwa na
namba ya stakabadhi aliyopewa kwa faini aliyotozwa
• Ionyeshwe ni katika akaunti gani pesa hiyo imeingizwa
24
• kama idhini ya kutumika nimetolewa na mamlaka husika, onyesha hapa
imetumika kufanyia nini?
KITABU CHA STAKABADHI
Hivi ni vitabu ambavyo Mtunza hazina wa Halmashauri ya Wilaya atatoa kwa kijiji,
lakini ionyeshwe nani kapewa vitabu vingapi kuvitumia ndani ya kamati.
VITABU VYA VIBALI
Kazi ya kitabu hiki ni kutunza kumbukumbu za vibali vyote vilivyoidhinishwa na kamati
ya Maliasili ya Kijiji. Kitabu hiki kionyeshe mambo yafuatayo; -
• Kuainisha lengo la kibali, jina la aliyepewa kibali hicho,
• kiasi cha malipo aliyolipa,
• Namba ya stakabadhi iliyotolewa kwa mteja na
• tarehe ya kutolewa kibali na ya kuisha kutumika kibali hicho.
• Pia kitabu kionyeshe jina la mjumbe atakayekagua kibali hicho na la mjumbe
atakayesimamia matumizi ya kibali hicho.
Kimsingi, leseni na vibali vitasainiwa na katibu/ Mhasibu wa Kamati ya Maliasili ya Kijiji
kugongwa muhuri wa Kamati ya Maliasili ya Kijiji.
KITABU CHA DORIA
Hiki ni kitabu kitakachokuwa kinatunzwa na msimamizi wa doria. kinapaswa
kuandikwa mambo yafuatayo;
25
• Tarehe,
• Majiina ya wanaofanya doria siku hiyo,
• eneo ambalo watu hao watafanya doria,
• ni uharibifu gani umefanyika katika eneo hilo la msitu ambalo watu hao
wamepangiwa kufanya doria.
• Pia katika taarifa ya hao waliopangiwa kufanya doria katika eneo husika
wakiona kitu mfano, wanyamapori. wanapaswa kutoa taarifa kwa kamati ya
maliasili ya Kijiji.
KITABU CHA AKAUNTI
Baada ya muda kijiji kitakuwa na fedha nyingi kutokana na mapato ya msitu, hivyo
kutakuwa na kitabu cha benki kwa ajili ya kumbukumbu za kibenki. Katika kitabu hiki
kutakuwa na majina ya watia saini. watia saini watakuwa kama ifuatavyo;
• mtia saini kundi ‘A’ – toka Serikali ya Kijiji,
• Mtia saini kundi ‘A’ – toka Kamati ya Maliasili ya Kijiji,
• Mtia saini kundi ‘B’ – toka Serikali ya Kijiji
• Mtia saini kundi ‘B’ – toka Kamati ya Maliasili ya Kijiji.
N: B: Izingatiwe kuwa hakuna fedha itakayo chukuliwa benki bila ya kuwa na saini za
watia saini wawili toka makundi mawili tofauti pamoja na muhtasari wa kikao cha
mkutano mkuu wa kijiji ulioidhinisha matumizi ya fedha hizo.
26
KITABU CHA MAPATO NA MATUMIZI
Hiki ni kitabu kitakachukuwa kinatunza kumbukumbu za fedha zote zinazoingia kutoka
katika faini na ada za vibali au leseni mbalimbali. Pia kitakuwa na kumbukumbu za
matumizi yote ya fedha zinazotumika ikionyesha saini ya aliyechukuwa na
viambatanisho vya uthibitisho kuwa malipo hayo yameidhinishwa na mamlaka husika.
Mfano wa malipo ni pamoja na zawadi ya pongezi kwa wafanya doria kwa kazi nzuri
itakayokuwa imethibitishwa na kuidhinishwa kuwa wapewe kiasi kadhaa kwa
maandishi. Hapa ni lazima mpokeaji athibitishe kuwa amepokea pesa hiyo.
USIMAMIZI WA FEDHA
Katika kifungu hiki sisi wanakijiji cha Kasangantongwe tunaainisha mfumo
utakaotumika kusimamia fedha hususani katika matumizi yake.
WAHUSIKA WAKUU;
Mtu atakaye husika kushika vitabu vya risiti na kupokea fedha toka kwa mlipaji
atakuwa ni mtunza fedha. Fedha hizo zitahifadhiwa benki kwenye akaunti ambayo
itafunguliwa kwaajili ya fedha zitokanazo na msitu wa hifadhi ya kijiji cha
Kasangantongwe.
AFISA MUWAJIBIKAJI WA MASUALA YA FEDHA
Afisa muwajibikaji wa fedha za Msitu wa Kijiji atakuwa AFISA MTENDAJI WA KIJIJI
kwa kuwa huyu ndiye anayewajibika kwa masuala yote yahusuyo fedha hapa kijijini.
Anaweza kumhoji mtunza fedha na kukagua vitabu vya fedha wakati wowote
atakapoona inafaa. Hata hivyo mtunza hazina anapaswa kutoa taarifa ya mwenendo
wa makusanyo ya fedha kila wiki.
27
Hata hivyo, kwa kuzingatia misingi ya uhuru wa habari na taratibu za utawala bora
mwananchi yeyote anaweza kuomba kukagua kitabu cha makusanyo. pamoja na
taratibu hizi za pekee, Mamlaka inayowajibika ya juu kabisa katika kijiji ni Mkutano
mkuu, hivyo , taarifa ya mapato na matumizi yatasomwa kila baada ya miezi mitatu
katika mikutano mkutano mkuu wa kijiji kama ilivyo desturi ya mikutano hiyo hapa
kijijini.
Kwa upande wa ukiukwaji wa taratibu au tuhuma dhidi ya mtunza hazina taratibu
zifuatazo zitatumika;
Endapo mtunza hazina /fedha atahisiwa kuwa katumia fedha tofauti na utaratibu au
ridhaa ya wananchi hatua zifuatazo zitumike; -
• Mwenyekiti wa Kamati ya Maliasili ya Kijiji ataitisha kikao cha kamati yake na
kumhoji juu ya tuhuma husika
• Ikiwa ameshindwa kutoa maelezo ya kujitosheleza na kushindwa kuondoa
mashaka hayo, Taarifa hiyo itapelekwa kwa mwenyekiti wa kijiji ambaye
anapaswa kuitisha kikao cha Serikali ya Kijiji kumhoji juu ya tuhuma husika,
kama maelezo yake hayajajitosheleza kiasi cha kuuongezea uongozi wa kijiji
mashaka, Atapewa barua ya kujieleza ikiwa ni nafasi ya kujieleza kufuatia
tuhuma au mashaka dhidi ya matumizi mbaya ya fedha ya kijiji.
• Endapo maelezo yake katika barua hayataondoa utata, mwenyekiti ataitisha
Halmashauri ya kijiji iliyomchagua na kuwasilisha hoja ya kumsimamisha kazi
ili hatua za kisheria zichukue mkondo wake. Hoja ikipitishwa VEO ataandika
barua ya kumsimamisha kazi hadi hapo mahakama/baraza la kata itakapo
amua kuwa ana hatia ama la,
28
• Baada ya kusimamishwa kazi VEO atamfikisha mtuhumiwa
polisi/mahakamani/baraza la kata. moja ya vyombo hivyo ndicho kitakachotoa
tamko la mwisho.
• Akipatikana na hatia atafukuzwa kazi hiyo na kutekeleza adhabu zilizoamriwa,
na mara moja Mwenyekiti wa kijiji kufanya taratibu za kuziba pengo la mtunza
hazina aliyepita.
MATUMIZI YANAYOIDHINISHWA;
Kwanza ifahamike kuwa matumizi makuu ya fedha itokanayo na uhifadhi wa msitu
wetu yatagawanyika katika makundi makuu matatu kama ifuatavyo; -
• 50% itatumika katika shughuli za maendeleo ya kijiji kwaajili ya wananchi wote
• 30% pesa hii itatumika kwaajili ya kuboresha kamati ya maliasili ya Kijiji.
• 20% itatumika kwaajili ya kufanya shughuli za uhifadhi wa msitu wa kijiji cha
Kasangantongwe kuwa endelevu kama vile:
▪ Ununuzi wa vitabu vya kumbukumbu kama vilivyoainishwa katika
“Kugharamia marekebisho ya mipaka".
▪ Kugharamia tathimini ya Rasilimali na kuboresha Mpango huu wa
Usimamizi
▪ Kugharamia uendeshaji wa kesi.
▪ Kutoa motisha kwa kikosi cha doria na Kamati ya Maliasili ya Kijiji katika
kutekeleza majukumu yao.
29
▪ Kununua zana za doria mfano sare, mahema, tochi, makoti ya mvua n.k.
▪ Kugharamia mahitaji wakati wa doria kama chakula n.k.
Mipaka ya Msitu wa hifadhi wa kijiji cha Kasangantongwe
Msitu huu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe una jumla ya mawe (beacons}
saba (7) tu zinazozunguka mipaka ya nje ya msitu huu.
MAELEKEZO MAALUM
Katika maelekezo haya inasisitizwa kwamba maamuzi yote kuhusu usimamizi wa
msitu wetu turejee vipengele vilivyoelekezwa na kukubaliwa na sisi wenyewe katika
mpango huu. Hatutegemei tena wataalamu toka wilayani kuja kufanya maamuzi
kwaajili yetu bali kuwaomba ushauri katika kupambanua mkwamo fulani ili baadaye
sisi tufanye maamuzi.
ULINZI NA UKAGUZI WA ENEO LA MSITU WA KIJIJI CHA
KASANGANTONGWE
Kila mwanakijiji wa Kasangantongwe ana jukumu la kulinda na kutunza hifadhi ya ziwa
na msitu wa kijiji. Hili jukumu litafanyika kwa kutekeleza yafuatayo:
• Kutoa taarifa za uhalifu
• Kutambua na kutoa taarifa za wahalifu wa msitu wa hifadhi ya kijiji na zana za
uvunaji haramu ndani na hifadhi ya msitu wa kijiji.
• Kuzuia moto usitokee na kuzima unapotokea.
30
• Kushiriki katika shughuli za uoteshaji miche ya miti na upandaji wa miti katika
maeneo ya makazi na mashambani.
• Ni wajibu wa wakazi wote wa kijiji cha Kasangantongwe kushirikiana katika
ulinzi wa msitu wa hifadhi ya kijiji.
• Doria za ukaguzi katika msitu wa hifadhi ya kijiji zitafanywa na kamati ya doria
angalau mara mbili kwa mwezi.
• Walinzi wa msitu na hifadhi watachaguliwa na Halmashauri ya kijiji na
kuthibitishwa na Mkutano Mkuu wa kijiji kutoka katika vitongoji vyote vya kijiji
kwa uwakilishi wa Vitongoji vya Kaselamuyaga, Isimwa, Kasangantongwe na
Kapondogoro.
Sifa za Walinzi wa Msitu.
Zifuatazo ni miongni mwa sifa ambazo inabidi mlinzi wa msitu sharti awe nazo:
• Awe na tabia na mwenendo mzuri.
• Wenye kujituma na mwaminifu.
• Mkakamavu na mwenye afya nzuri.
• Asiwe mlevi
• Awe mkazi wa kijiji cha Kashagulu na raia wa Tanzania.
• Awe na umri wa miaka kumi na nane (18) na kuendelea.
• Ajue kusoma na kuandika.
31
Wajibu, Majukumu na Mafao ya Walinzi wa Msitu wa Hifadhi ya Kijiji
• Walinzi watachagua kiongizi wao (Kamanda) kutoka miongoni mwao ambaye
atawajibika kupanga utaratibu kwa kushirikiana na walinzi wenzake wa doria
na utoaji taarifa kwa Kamati ya Mazingira.
• Walinzi wa msitu hawatalipwa mishahara lakini watapata motisha kama
itakavyoamuliwa na Serikali ya kijiji. Aidha walinzi husika wanaweza kupewa
25% ya faini anayotozwa mhalifu.
• Walinzi wa msitu wanaweza kusamehewa kazi nyingine za maendeleo kijijini.
• Walinzi watakaokwenda kinyume na maadili yao ya kazi wataadhibiwa kwa
kuonywa, kutozwa faini na kufukuzwa au kushitakiwa Mahakamani kutokana
na ukubwa wa kosa lililotendeka.
• Walinzi watatoa taarifa yao ya doria kila wanapofanya doria kwa Kamanda wao
ambaye atapaswa kutoa taarifa kwa Kamati ya Mazingira haraka iwezekanavyo
(isizidi siku moja).
• Walinzi waliofanya kazi nzuri watazawadiwa kila mwisho wa mwaka na
Halmashaurii ya Kijiji. Walinzi hao watapendekezwa na Kamati ya Mazingira na
kuthibitishwa na Halmashauri ya kijiji. Zawadi/ motisha kwa walinzi waliofanya
vizuri itakuwa kama ilivyopendekezwa hapo juu.
OPERESHENI
Yapo mazingira ya pekee ambapo kikosi pekee hakitoweza kukabiliana na uhalifu
fulani wa mpito, hivyo operesheni maalumu itaandaliwa kwa idhini ya mwenyekiti wa
32
kijiji kupitia kamati yake ya serikali ya kijiji kwa ushauri wa kamati kuu mbili;- Kamati
ya Ulinzi ya Kijiji na
Kamati ya Maliasili ya Kijiji.
N:B. Maandalizi haya lazima yawe ya siri sana.
ZAWADI YA PONGEZI KWA MWANA DORIA
Kutakuwa na utaratibu wa kutoa zawadi ya pongezi au motisha kwa mwana kikosi cha
doria ambaye atafanya kazi kwa ujasiri, ushujaa na uadilifu mkubwa utakao thibitishwa
na wajumbe wa mkutano wa Halmashauri kuu ya Kijiji na Kuungwa mkono na Mkutano
Mkuu wa Kijiji. Kiasi cha pongezi au motisha kitapangwa na Halmashauri kuu ya kijiji.
zawadi hii itatolewa hadharani na kuwekwa katika kumbukumbu za vitabu husika.
Kanuni za Kutumia Msitu wa Hifadhi ya kijiji
• Mkazi yeyote wa kijiji cha Kasangantongwe, Afisa Misitu au mtu yeyote
aliyeruhusiwa wanaweza kuingia ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji kwa idhini
ya Kamati ya Mazingira.
• Afisa Misitu yeyote wa Idara ya Misitu na Nyuki wakati wowote anaweza kuingia
ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji aidha akiwa peke yake au kwa kushirikiana
na Kamati ya Mazingira ya kijiji kwa lengo la kufanya ukaguzi na kutoa ushauri
kwa Kamati ya Mazingira ambao unapaswa kupokelewa na kufanyiwa kazi kwa
lengo la kuboresha uendelezaji wa eneo hilo la msitu.
Kifungu Cha Kumi Taratibu
33
• Sio ruksa kwa mtu yeyote kuingia msitu wa hifadhi ya kijiji bila kibali kutoka kwa
Kamati ya Mazingira isipokuwa Walinzi wa msitu, Halmashauri ya kijiji, Kamati
ya Mazingira na Afisa Misitu wanaweza kufanya hivyo bila kibali.
• Wageni wote wenye vibali toka Wizarani, Wilayani au wafadhili ni sharti wapite
kijijini na kuonyesha vibali vyao kwa Kamati ya Mazingira ya kijiji kabla ya
kuanza kufanya kazi yoyote ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji.
Kanuni za matumizi ya msitu:
Mahitaji yaliyoruhusiwa yatapaswa kupatikana kutoka maeneo ya matumizi ndani ya
msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe. Maeneo yaliyohifadhiwa
hayataruhusiwa kupata mahitaji ya mbao, miti ya nguzo/miamba ya nyumba na
mengineyo yasiyoruhusiwa.
Matumizi ya Msitu yanayohusu Ukataji wa Miti
Mahitaji yote yanayohusu ukataji miti aina fulani kwa ajili ya mbao, nguzo na miamba
ya nyumba ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe yanaruhusiwa
katika EDU za Mpapa na Kabhukindu kwa kibali kitakachotolewa na Kamati ya
Mazingira na kuwekwa alama kwa kutumia nyundo maalum ya Idara ya Misitu ya
Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda. Miti husika itavunwa kwa kiwango ambacho
hakitaathiri lengo la msingi la kuhifadhi msitu ambalo ni kuhifadhi vyanzo vya maji na
upatikanaji endelevu wa rasilimali na huduma ya msitu kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
34
TARATIBU NA SHERIA NYINGINEZO
Adhabu
Uwezo na haki ya kupiga faini kwa Kamati ya Mazingira ya kijiji cha Kashagulu
umetolewa kwake na Halmashauri ya kijiji cha Kasangantongwe kufuatana na Sheria
za Serikali za Mitaa (Serikali za Vijiji) 1982 No. 7 zilizoundwa chini ya kifungu cha
120 (i) na 167.
Mtu yeyote atakayekiuka masharti ya matumizi ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha
Kasangantongwe yaliyowekwa na kukubaliwa atatozwa faini kwa mujibu wa Sheria
Ndogo ya kijiji cha Kasangantongwe ya kulinda na kutunza msitu wa hifadhi ya kijiji.
Kifungu Cha Kumi na Moja Adhabu
MCHAKATO WA KUMSHUGHULIKIA MKOSAJI NA KOSA
• Hairuhusiwi kwa mwanakijiji, mwanakamati, mlinzi au kiongozi yeyote kumtoza
faini mhalifu akiwa peke yake.
• Mazao ya misitu yaliyovunwa kinyume cha utaratibu pamoja na zana
zilizotumika katika uhalifu huo yakikamatwa ni lazima yafikishwe kwenye ofisi
ya kijiji ambapo hatua zaidi itachuliwa na Kamati ya Mazingira ya kijiji.
• Iwapo itabainika kuwa mtu au watu wamekiuka taratibu za matumizi ya msitu
wa hifadhi ya kijiji, mtu huyo au watu hao watafikishwa mbele ya Kamati ya
Mazingira ya kijiji na suala lao litashughulikiwa kwa utaratuibu ufuatao hapa
chini:
35
▪ Mhalifu/wahalifu watafikishwa katika ofisi ya kijiji ambapo Afisa Mtendaji
wa Kijiji atamuweka/atawaweka chini ya ulinzi. Afisa Mtendaji wa Kijiji
atawaarifu viongozi wa kamati/wajumbe wa Kamati ya Mazingira
angalau wawili ili kuwatoza faini wahalifu iwapo watakiri/atakiri kosa kwa
kuweka sahihi katika daftari la “makosa na faini”
▪ Iwapo mhalifu/mtuhumiwa atakataa kukiri kutenda kosa kwa kukataa
kuweka sahihi katika daftari, mtu huyo atatakiwa kupelekwa
mahakamani.
▪ Endapo mhalifu/wahalifu watakiri kutenda kosa, faini yote lazima iwe
imelipwa katika muda wa siku tatu (3) toka siku ya kukiri kutenda kosa
hilo. Hata hivyo mhalifu atalazimika kuwekewa dhamana na mtu
anayekubalika katika kijiji cha Kasangantongwe.
• Katibu atapokea malipo ya faini iliyolipwa kwa kuandika stakabadhi ambayo
atampatia mhalifu. Namba ya stakabadhi iliyotolewa itaandikwa kwenye daftari
la “Makosa na Faini” na kumkabidhi Mweka Hazina azipeleke kwenye akaunti
ya Kamati ya Mazingira ya kijiji.
• Iwapo mtu anayetuhumiwa kutenda kosa atakataa kukiri kosa mbele ya
Kamati ya Mazingira na mbele ya Mwenyekiti wa Kijiji au Afisa Mtendji wa Kijiji
basi itabidi vyombo hivyo vya utendaji vifikishe shauri hili mahakamani kwa
uamuzi zaidi.
• Iwapo mhalifu atashindwa kulipa faini katika kipindi kilichokubaliwa basi Kamati
ya Mazingira au Afisa Mtendaji wa Kijiji atafikisha suala hilo mahakamani.
36
FAINI NA ADHABU KWA KILA KOSA
Mtu yoyote atakayetiwa hatiani kwa kutenda kosa lolote lililoidhinishwa katika kifungu
cha 10 cha sheria ndogoza kulinda msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe
ataadhibiwa kama ifuatavyo:
• Kosa la kuingiza/kupitisha/kuchunga mifugo atatozwa Tshs 10,000/= kwa kila
mbwa, ng’ombe na Punda na Tsh 5000/= kwa mbuzi na kondoo.
Atakayeshindwa kulipa mifugo yake itaifishwe kulingana na gharama ya faini.
• Kosa la kuingia msituni bila kibali adhabu yake itakuwa ni faini isiyopungua Tsh
10,000/= na isiyozidi Tsh 20,000/=
• Kosa la Kuchoma mkaa faini shilingi Tsh 50,000/= na kutaifisha mkaa huo.
• Kosa la Kukata miti bila kibali adhabu itatolewa kulingana na thamani ya mti
uliokatwa na faini isiyopungua Tsh 10,000/= na isizidi Tsh 50,000/= pamoja na
kutaifisha miti hiyo.
• Kosa la Kufanya shughuli za kilimo faini shilingi elfu hamsini (50,000/=) kwa
hekari moja, kutaifisha mazao na kupelekwa mahakamani.
• Kosa la Kuchoma moto faini ya isiyopungua Tsh 5,000/= na isiyozidi Tsh
50,000/= na atashitakiwa kwa mujibu wa sheria ya kosa husika.
• Kosa la Kufanya shughuli nyingine yoyote isiyohusika katika msitu huo
atatozwa faini Tsh 5,000/=
• Kosa la kufanya shughuli za uvuvi itakuwa ni faini ya Tsh. 10,000 kwa kila
chombo cha mwanakijiji na Tsh. 50,000/=kwa kila mgeni.
37
FAINI ZA KUTOWAJIBIKA
Iwapo mjumbe yeyote katika Halmashauri ya Kijiji, Kamati ya Mazingira au walinzi wa
msitu atakiuka taratibu za kiutendaji kuhusiana na uhifadhi wa msitu wa hifadhi ya kijiji
cha Kasanagntongwe, atakuwa ametenda kosa kwa mujibu wa Sheria hii na atatozwa
faini itakayojulikana kama faini ya wenye dhamana/madaraka. Faini hiyo itakuwa mara
mbili ya faini zitakazotozwa kwa watu wasiokuwa na madaraka kijijini/ zilizoainishwa
hapo juu.
• Pamoja na faini hizo, makosa ya viongozi hao lazima yajadiliwe kwenye vikao
vya juu katika kijiji na kuwachukulia hatua kali kama vile barua za onyo la
maandishi, kusimamishwa na kuwaondoa kwenye nafasi zao baada ya
kuidhinishwa na Mkutano Mkuu wa Kijiji.
• Kwa wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji, Afisa Mtendaji Kata ataitisha Kikao
kujadili hatima ya kiongozi aliyefanya uhalifu huo.
Kifungu Cha Kumi na Mbili Kuboresha msitu na Ukarabati wake
KUUENDELEZA MSITU
Kwa bahati nzuri utengaji wa msitu ulizingatia maeneo ya kulima kuchungia mifugo,
makazi n.k. hivyo hakuna mvutano wa mgogoro wa hitaji la shughuli hizi katika eneo
la msitu huu. Shughuli kama hizi zitafanyika nje ya msitu kwa kujitosheleza. Hapa
Mpango huu wa Usimamizi wa Msitu unapiga marufuku kufanyika shughuli za aina
hii ndani ya msitu.
38
Aidha, ni marufuku mtu au kikundi cha watu kupanda mti wowote wa kigeni ndani ya
msitu huu.
Aina pekee za miti zinazoruhusiwa kuvunwa na kiasi chake zimeorodheshwa katika
majedwali ya viambat . Hairuhusiwi kutumia msumeno wa mnyororo katika msitu huu.
Kifungu Cha Kumi na Tatu Matumizi
UTANGULIZI:
Msitu huu ni msitu wa matumizi na Uhifadhi yaani uvunaji wa miti ya mbao
unaruhusiwa kwa kiwango kilicho ainishwa katika mpango huu, uvunaji wa rasilimali
nyinginezo za misitu unaruhusiwa katika EDU ya Mpapa na Kabhukindu. Lakini
jambo la kuzingatia ni kiasi, wakati na utaratibu wa uvunaji. EDU ya Uhifadhi ya Ziwa
Tanganyika haitaruhusiwa kufanyika shughuli zozote za uvunaji kwani ni kwa ajili ya
Uhifadhi tu kutokana na kuwa maeneo yanayopendelewa na sokwe pia makorongo
marefu, vyanzo vya maji na bioanuai mbalimbali muhimu na ni ukingoni mwa ziwa
Tanganyika. Hivyo basi, Mahitaji yaliyoruhusiwa yatapaswa kupatikana kutoka
maeneo ya matumizi ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe. Maeneo
yaliyozuiliwa / hifadhiwa hayataruhusiwa kupata mahitaji ya mbao, miti ya
nguzo/miamba ya nyumba na mengineyo yasiyoruhusiwa.
UVUNAJI WA MITI
Uvunaji wa miti unaoruhusiwa ni kwa miti ya aina zilizoorodheshwa katika Jedwali Na1
39
EDU hii ina jumla ya miti kama inavyoonyeshwa katika Jedwali Na 3 na 10 kwa EDU
zote mbili. Tazama katika viambata. Wakati aina ya miti ya kuvunwa imeainishwa
katika jedwali namba .. na .. ikiwa ni pamoja na matumizi mengineyo ya EDU hii
Kiasi kamili cha miti ya kuvunwa kwa kila aina ya mti vimeonyeshwa katika jedwali
namba 7 na 12 kwa EDU zote. Katika majedwali haya imeonyeshwa bayana kiasi gani
cha kuvunwa kwa kila mwaka na ni aina gani ya miti. Inapaswa kuzingatiwa bila
kuongeza hata kidogo.
Kifungu Cha Kumi na Nne Ratiba
HATUA ZA HARAKA
• KAMATI YA MALIASILI KIJIJI na Timu ya Doria zinapaswa kuchaguliwa
katika mkutano mkuu wa kijiji
• Kamati ya Maliasili ya Kijiji inapaswa kufanya mkutano wake wa kwanza
• Taratibu za ununuzi wa vitabu vya kumbukumbu zinatakiwa zifanyike mwanzoni
mwa mwezi December, 2016 ili Kamati ikutane na Mtunza Hazina wa WIlaya
kabla ya mwisho wa mwezi wa Novemba,2016. zoezi hili litakamilishwa na
Hafla au mkutano utakaohudhuriwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya kwa
uzinduzi rasmi.
• Mwezi January 2017 ni mwezi wa kuanza kazi rasmi kwa utekelezaji wa
Mpango wa Usimamizi wa Msitu huu wa hifadhi ya kijiji cha Kasangantongwe.
40
UFUATILIAJI
Vigezo vya Mafanikio:
Vifuatavyo ni Vigezo vya mafanikio vitatumika katika ufuatiliaji wa utekelezaji wa
Mpango huu wa Usimamizi wa msitu wa hifadhi ya kijiji:
• Wanakijiji kuunga mkono juhudi za uhifadhi kwa:
▪ Kutoa ushirikiano kwa Kamati ya Mazingira na walinzi wa msitu na
hifadhi.
▪ Kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu.
▪ Kuotesha na kupanda miti katika maeneo ya kaya na mashamba.
▪ Kuheshimu na kutekeleza taratibu za ulinzi na utunzaji Misitu.
• Kupungua kwa matukio ya upasuaji mbao, moto, uwindaji wa wanyama pori,
uvamizi wa msitu kwa ajili ya kilimo na ufugaji.
• Kupungua na kufunga kwa njia zisizoruhusiwa msituni.
• Kuongezeka kwa uoto wa asili na hivyo msitu kufunga hasa katika maeneo
yaliyoharibiwa.
• Kurejea au kuongezeka kwa wanyama pori, ndege na viumbe vingine hai katika
msitu wa kijiji.
• Kuongezeka kwa kiwango cha maji kwenye mito, chemchem au kufufuka kwa
chemechem zilizokufa kutokana na uharibifu.
• Kuongezeka kwa makundi ya nyuki ndani ya msitu wa hifadhi ya kijiji.
• Mipaka ya nje ya msitu wa hifadhi kuwa wazi, safi na kuonekana bila ugumu
wowote.
41
Wafuatiliaji
Wafuatao watahusika kufanya ufuatiliaji kwa kukusanya taarifa kuhusu vigezo vya
mafanikio:
• Wataalamu wa Misitu wa ngazi zote.
• Halmashauri ya kijiji
• Kamati ya Mazingira ya kijiji.
Taarifa ya Ufuatiliaji Itatolewa kwa:
• Afisa Misitu (W)/ Afisa Misitu (M) Mkutano Mkuu wa kijiji.
• Mkuu wa Wilaya/Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya.
• Halmashauri ya kijiji.
Muda wa Kufanya Ufuatiliaji
Kamati ya Mazingira: Itafanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa Mpango huu mara mbili
(2) kila mwezi na kuandaa taarifa kwa Halmashauri ya kijiji mara moja kwa mwezi
yenye nakala kwa Afisa Misitu (W).
Halmasahauri ya kijiji: Itafuatilia mpango huu mara moja (1) kila mwezi
• kwa kutembelea msitu wa hifadhi ya kijiji angalau mara moja kila mwezi
• kuwa na agenda ya kudumu katika vikao vyake Kwa kutumia taarifa ya
Kamati ya Mazingira.
42
Wataalam wa Misitu & ngazi za Eneo, (W)/ (M):
• Wataalam wa ngazi ya Eneo (Kata/Tarafa) watafanya ufuatiliaji wa mpango huu
mara moja kila mwezi.
• Wataalam wa ngazi ya Wilaya & Mkoa watafuatilia utekelezaji wa mpango huu
mara moja kila baada ya miezi mitatu (3) yaani robo mwaka
IKUMBUKWE: Taarifa ya matokeo ya ufuatailiaji itajadiliwa mara baada ya kazi ya
ufuatiliaji kukamilika.
Mpango huu unaweza kufanyiwa marekekebisho baada ya miaka mitano (5) ya
utekelezaji kwa kuzingatia taarifa za ufuatiliaji na uamuzi uliofikiwa wakati wa kujadili
taarifa hiyo.
RATIBA YA UTEKELEZAJI
Hatua za Awali za Utekelezaji:
• Kuchagua Kamati ya Mazingira na walinzi wa msitu (Kamati ya doria) itafanyika
mara baada ya mpango wa utekelezaji kupitishwa na Mkutano
Mkuu wa kijiji.
• Kikao cha kwanza cha Kamati ya Mazingira na walinzi kitafanyika siku moja
baada ya uchaguzi wao kufanyika.
• Kununua vitabu vya kumbukumbu itafanyika baada ya Kamati ya Mazingira
kufanya kikao chake cha kwanza.
43
Hatua Zitakazofuata
Kuweka mabango ya matangazo.
MUDA WA MPANGO, MAREKEBISHO NA MAPITIO YAKE:
Mpango huu wa utekelezaji utatumika kwa miaka mitano (5) kuanzia mwaka 2016 –
2021. Marekebisho ya mpango yatafanyika kwa kuzingatia mahitaji yatakayojitokeza
kwa lengo la kuuboresha 2021 na Kamati ya Mazingira ya kijiji itahusika kwa
ushirikiano na Afisa Misitu (W) Mpanda.
46
VIAMBATA
MPANGO WA UVUNAJI KWA AINA MBALIMBALI ZA MITI KATIKA EDU ZA
MPAPA NA KABHUKINDU
JEDWALI Na 1: ORODHA YA MITI YA INAYORUHUSIWA KUVUNWA - EDU YA
MPAPA.
MITI
MUHIMU
MITI
MINGINEYO
MATUMIZI MENGINEYO
Mkalya
Mbanga Mhongolo Urinaji wa asali
Kabhamba Mpandepande Uvunaji wa miti ya mbao
Muyovu Mhama Uchimbaji wa dawa za kienyeji
Mninga Mkundye Kukata nyasi
Mkurungu Munsa Kukusanya kuni
Msawala Mubha
Mbombo Ukatajiwa boriti, nguzo na fito
Maji
Matambiko
Kukusanya uyoga
Kuwinda wanyamapori
Ukataji wa milala
48
JEDWALI Na . 2 MAJUMUISHO YA TAKWIMU KUTOKA KATIKA PLOTI ZA SAMPULI
MSITU WA HIFADHI WA KANKOSYA EDU YA MPAPA UCHAMBUZI WA TAKWIMU ZA VIPIMO VYA MITI TOKA
KATIKA PLOTI ZA SAMPULI
Forest assessment form C
Village Kasangantongwe Forest Name Kankosya No. of sample plots (N) 30
FMU Name Mpapa FMU area (ha) (A) 2113 Plot area (ha) (P) 0.04
Diameter class <4 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+
Important spp
Mninga 0 - 0 0 1 1,761 1 1,761 0 0 0
0
Mkurungu 2 3,522 17 29,934 24 42,260 12 21,130 11 19,369 0
0
49
Mbanga 0 0 1 1,761 4 7,043 8 14,087 2 3,522 0
0
Kabamba 18 31,695 90 158,475 171 301,103 84 147,910 16 28,173 9
15,848
Mfuru 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
0
Msawala 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
0
Mkora 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
0
Mlembela 0 0 1 1,761 0 0 1 1,761 4 7,043 1
1,761
Mtundu 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
0
Myovu 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
0
FMU total 20 35,217 109 191,931 200 352,167 106 186,648 33 58,108 10
17,608
Average
17 91
167 88
28
8
Other spp
Msongati 5 8,804 62 109,172 84 147,910 27 47,543 0 0 0
0
Mkoma 3 5,283 1 1,761 5 8,804 0 0 0 0 0 0
50
mkole 2 3,522 5 8,804 11 19,369 3 5,283 0 0 0 0
Kolwe 0 0 5 8,804 19 33,456 6 10,565 0 0 0 0
Sifunfwe 51 89,803 96 169,040 91 160,236 27 47,543 3 5,283 0 0
Mhongolo 0 0 0 0 3 5,283 2 3,522 0 0 0 0
Mhunsa 5 8,804 14 24,652 23 40,499 9 15,848 0 0 0 0
Mtopetope 0 0 4 7,043 16 28,173 6 10,565 0 0 0 0
Mpapa 3 5,283 2 3,522 5 8,804 1 1,761 0 0 0 0
Mpogopogo 2 3,522 0 0 0 0 1 1,761 0 0 0 0
Kasemele 11 19,369 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kaselenge 0 0 1 1,761 2 3,522 0 0 0 0 0 0
Mkarakata 0 0 0 0 1 1,761 4 7,043 0 0 0 0
Tola 8 14,087 19 33,456 14 24,652 7 12,326 2 3,522 0 0
Msubhu 1 1,761 5 8,804 2 3,522 2 3,522 0 0 0 0
Mla Mbuzi 0 0 0 0 1 1,761 1 1,761 0 0 0 0
Ngawera 0 0 0 0 1 1,761 1 1,761 1 1,761 0 0
51
Mbeko 0 0 1 1,761 4 7,043 2 3,522 0 0 0 0
Mlama 0 0 1 1,761 3 5,283 1 1,761 0 0 0 0
Chinga 0 0 0 0 4 7,043 2 3,522 0 0 0 0
Mgoigoi 0 0 1 1,761 3 5,283 2 3,522 1 1,761 0 0
Bhuka 1 1,761 1 1,761 1 1,761 0 0 0 0 0 0
Mvundo 0 0 0 0 1 1,761 0 0 0 0 0 0
Mvinje 0 0 0 0 2 3,522 0 0 0 0 0 0
Msele 0 0 0 0 5 8,804 0 0 1 1,761 0 0
Kamshange 0 0 2 3,522 5 8,804 2 3,522 0 0 0 0
Mketya 0 0 0 0 2 3,522 0 0 0 0 0 0
Mbangalela 0 0 0 0 2 3,522 1 1,761 0 0 0 0
Msansamale 0 0 0 0 0 0 1 1,761 0 0 0 0
Mlabhuka 0 0 0 0 0 0 1 1,761 0 0 0 0
Kikarekare 0 0 0 0 2 3,522 0 0 0 0 0 0
Kacheko 0 0 2 3,522 6 10,565 2 3,522 0 0 1 1,761
52
Mpinipini 9 15,848 1 1,761 0 0 0 0 0 0 0 0
Mbarebare 1 1,761 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0
Kabumbu 0 0 0 0 0 0 1 1,761 2 3,522 0 0
Mpakakofi 0 0 4 7,043 0 0 0 0 0 0 0 0
Total in FMU Iother
spp 102 179,605 223 116,215 89 147,910 1 47,543 0 17,608 0 1,761
Average other spp 85 0 55 0 70 0 23 0 8 0 1
Important spp
20
35,217 109 191,931 229 352,167 106 186,648 33 58,108 10 1,761
Average important
spp 17 0 91 0 167 0 88 0 28 0 1
All spp combined 122 214,907 332.1055372 308,201 318.0421202 500,077 107.0004733 234,191 33 75,724 10
3,523
Average 102
146 0 237 111
36 2
JEDWALI Na 3 FOMU ‘C’ YA TATHIMINI
ASSESSMENT FORM C
Village Forest name No. of plots (N)
53
FMU Name FMU area (ha) (A) Plot area (ha) (P)
Diameter
classes
< 4 cm
4 – 7 cm
8 – 14 cm
15 – 29 cm
30 – 49 cm
50+
Important
Species
Measure
d total (T)
FMU total
(F)
Measure
d total
(T)
FMU total
(F)
Measure
d total
(T)
FMU
Total (F)
Measure
d total
(T)
FMU
Total (F)
Measure
d total (T)
FMU total
(F)
Measure
d total
(T)
FMU
Total (F)
Other
species
Total
For each dbh/size class, Total (F) = A/P * T/N Where A = FMU area (ha); N = No. of sample plots; T = No. of measured trees (in all sample plots
combined); P = Sample plot area (ha)
54
JEDWALI Na 4: MIHIMILI YA MSINGI KUONYESHA UWINGI WA MITI KATIKA EDU YA MPAPA.
Miti Muhimu - EDU YA MPAPA
Miti Mingineyo - EDU YA
MPAPA
Stems/ha
< 4 4-7 8-14 15-29 30-49 50+
DBH classes (cm)
85
55
70
23 8 1
0
20
40
60
80
100
< 4 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+ DBH classes
Stems/ha
17
91
167
88
28
8
0
20
40
60
80
100
120
140
160
180
55
MTI MUHIMU NA MINGINEYO
- EDU YA MPAPA
JEDWALI Na. 5 ; MIHIMILI YA IDADI YA KILA AINA YA MTI (MITI MUHIMU NA
102
146
237
111
36 9
0
50
100
150
200
250
4 < 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+ Diameter classes (Cm)
Stems/ha
56
Miti muhimu - EDU ya
Kabukindu 2611ha
MITI MUHIMU NA MINGINEYO-
EDU YA KABUKINDU, 2611ha
< 4 4-7 8-14 15-29 30-49 50+
DBH classes (cm)
MINGINEYO) - EDU YA KABUKINDU
Mingineyo - EDU ua Kabukindu
2611ha
20
136
226
102
37 18
0
50
100
150
200
250
< 4 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+ DBH classes
Stems/ha
42
234
413
163
42 19 0
100
200
300
400
500 stems/ha
58
JEDWALI Na 7. UFUPISHO WA MPANGO WA UVUNAJI KATIKA EDU YA Kabukindu KWA MWAKA 2016/2017 HADI
2020/2021
Na
JINA LA MTI
IDADI YA MITI
KATIKA EDU
IDADI YA MITI VUNWA KWA
MIAKA 5
2009/2010-2014/2015
IDADI YA MITI
VUNWA KILA
MWAKA
1 Msawala 172,616 227 44
2 Mkola 111,083 323 63
3 Mninga 104,548 454 91
4 Kabamba 16,764 421 84
5 Masaka 135,586 258 51
6 Myovu 157,366 669 134
7 Mkurungu 104,003 322 64
JUMLA KUU 1,301,966 2,674 531
JEDWALI Na 8: ORODHA YA MITI YA INAYORUHUSIWA KUVUNWA - EDU YA KABUKINDU
MITI MUHIMU MITI MINGINEYO MATUMIZI MENGINEYO
Msawala Mbarebare Uvuvi wa samaki
59
Kabamba Mhongolo Urinaji wa asali
Myovu Mvinje Uvunaji wa miti ya mbao
Mkola Mhama Uchimbaji wa dawa za kienyeji
Mninga Mkoma Kukata nyasi
Mkurungu Mhunsa Kukusanya kuni
Masaka Mubha Kamba za miti
Mbombo Ukatajiwa boliti,nguzo na fito
Matambiko
JEDWALI Na 9 MAJUMUISHO YA TAKWIMU TOKA KATIKA PLOTI ZA SAMPULI
UCHAMBUZI WA TAKWIMU TOKA KATIKA PLOTI ZA SAMPULI KATIKA EDU YA KABHUKINDU (2611ha)
Forest assessment form C
Village Kasangantongw
e
Forest Name
Kankosya No. of sample plots (N)
65
60
FMU Name Kabukindu FMU area (ha) (A) 2611 Plot area (ha)
(P)
0.04
Diameter class <4 4 - 7 8 - 14 15 - 29 30 - 49 50+
Important spp
Mninga 0 - 2 2,008 4 4,017 5 5,021 4 4,017 3 3013
Mkurungu 3 3,013 20 20,085 33 33,140 33 33,140 21 21,089 17 17,072
Mbanga 0 0 0 0 2 2,008 1 1,004 3 3,013 0 0
mpilipili 6 6,025 1 1,004 1 1,004 1 1,004 2 2,008 3 3,013
Msawala 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0 2 2,008
Kabamba 27 27,114 226 226,956 376 377,591 147 147,622 38 38,161 16 16,068
Mnyovu 0 0 0 0 0 0 0 0 0 0 7 7,030
Total important
spp 36 36,152 250 251,058 416 417,760 187 187,791 68 68,288 46 48,203
Stems/ha 14 0 96 0 160 0 72 0 26 0 18
61
Other spp
Mlama 0 0 3 3,013 7 7,030 1 1,004 0 0 0 0
Tola 1 1,004 5 5,021 2 2,008 2 2,008 1 1,004 0 0
Msongati 7 7,030 57 57,241 147 147,622 40 40,169 0 0 0 0
Kaselenge 0 0 1 1,004 5 5,021 8 8,034 1 1,004 0 0
Kalongolola 0 0 0 0 2 2,008 6 6,025 1 1,004 0 0
Msigisigi 1 1,004 7 7,030 11 11,047 1 1,004 0 0 0 0
Kamshange 0 0 10 10,042 12 12,051 0 0 0 0 0 0
Buka 1 1,004 7 7,030 15 15,063 0 0 0 0 0 0
Mbeko 0 0 6 6,025 9 9,038 9 9,038 0 0 0 0
Mvinje 2 2,008 2 2,008 3 3,013 1 1,004 0 0 0 0
Mgunga 1 1,004 0 0 0 0 4 4,017 1 1,004 0 0
Msubhu 1 1,004 4 4,017 0 0 1 1,004 0 0 0 0
Mbarebare 0 0 0 0 2 2,008 0 0 3 3,013 0 0
Mtopetope 3 3,013 4 4,017 2 2,008 1 1,004 0 0 0 0
62
Chinga 0 0 2 2,008 4 4,017 0 0 0 0 0 0
Mvundo 1 1,004 1 1,004 4 4,017 1 1,004 0 0 0 0
Mhunsa 2 2,008 0 0 4 4,017 0 0 0 0 0 0
Mfulofulo 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0
Kabumbu 4 4,017 15 15,063 21 21,089 4 4,017 2 2,008 1 1,004
Mhongolo 1 1,004 5 5,021 12 12,051 11 11,047 1 1,004 2 2,008
Kasemele 1 1,004 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0
Kolwe 0 0 0 0 16 16,068 2 2,008 0 0 0 0
Mfulu 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0 0 0
Mgagala 0 0 3 3,013 2 2,008 0 0 0 0 0 0
Kabolobolo 0 0 1 1,004 0 0 1 1,004 0 0 0 0
Mpogopogo 1 1,004 2 2,008 3 3,013 2 2,008 0 0 0 0
Mpogolo 0 0 7 7,030 4 4,017 0 0 0 0 0 0
Mkalakate 1 1,004 1 1,004 15 15,063 5 5,021 0 0 0 0
Simpogo 0 0 1 1,004 2 2,008 1 1,004 0 0 0 0
63
Mtungulu 0 0 1 1,004 0 0 2 2,008 0 0 0 0
Mbangubangu 0 0 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0
Nankungu 0 0 1 1,004 6 6,025 0 0 0 0 0 0
Mkolwa 0 0 4 4,017 8 8,034 3 3,013 0 0 0 0
Mtofu 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0
Tulu 0 0 0 0 3 3,013 0 0 0 0 0 0
Mzamba 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0
Mpapaipori 0 0 0 0 1 1,004 2 2,008 0 0 0 0
Mlyapombo 0 0 0 0 1 1,004 3 3,013 0 0 0 0
Mbuluu 1 1,004 1 1,004 0 0 0 0 0 0 0 0
Mbombo 0 0 0 0 1 1,004 0 0 1 1,004 0 0
Mfumbe 0 0 3 3,013 2 2,008 0 0 0 0 0 0
Kalyalya 0 0 0 0 2 2,008 0 0 0 0 0 0
Kankundu 0 0 2 2,008 0 0 1 1,004 0 0 0 0
Msakasaka 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0 0 0
Mketya 2 2,008 7 7,030 3 3,013 2 2,008 0 0 0 0
64
Mpangala 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0 0 0
Kalumilumi 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0
Mpapa 0 0 0 0 1 1,004 4 4,017 0 0 0 0
Mputuka 1 1,004 1 1,004 3 3,013 0 0 0 0 0 0
Tembwe 7 7,030 21 21,089 28 28,118 1 1,004 0 0 0 0
Mpakakofi 0 0 0 0 0 0 3 3,013 0 0 0 0
Mrabuka 0 0 0 0 1 1,004 1 1,004 0 0 0 0
Msogoro 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0
Mda 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0
Buketya 1 1,004 0 0 2 2,008 0 0 0 0 0 0
Mlyapombo 0 0 0 0 0 0 1 1,004 0 0 0 0
Kasanda 0 0 0 0 2 2,008 0 0 0 0 0 0
Bugogolo 0 0 1 1,004 0 0 0 0 0 0 0 0
Mlumbulu 0 0 0 0 0 0 2 2,008 1 1,004 0 0
Mlyansole 0 0 1 1,004 1 1,004 1 1,004 0 0 0 0
Nawowo 0 0 2 2,008 0 0 0 0 0 0 0 0
Kamshweke 0 0 2 2,008 2 2,008 0 0 0 0 0 0
sifunfwe 17 17,072 59 59,250 102 102,432 24 24,102 0 0 0 0
65
Mkoma 0 0 0 0 2 2,008 1 1,004 0 0 0 0
Mpapa 0 0 0 0 1 1,004 4 4,017 0 0 0 0
Mlangalanga 0 0 1 1,004 2 2,008 1 1,004 0 0 0 0
Simanzi 0 0 1 1,004 2 2,008 0 0 0
0
Total in FMU other spp 57 57,241 255 256,079 487 489,060 158 158,668 12 12,051 3 3,013
Average other spp 22
98 187
61 5
1
total in FMU important
spp 51,085
354,755 590,513
265,357 96,493
46,195
Average important spp
19.57
135.87
226.16
101.63
36.96
17.69
All spp combined 108,326
610,834 1,079,573
424,025 108,544
49,208
Average all spp
combined
41.49
233.95
413.47
162.40
41.57
18.85
Na
JINA LA MTI
IDADI YA MITI
KATIKA EDU
IDADI YA MITI VUNWA KWA
MIAKA 5
2016/2017-2020/2021
IDADI YA MITI
VUNWA KILA
MWAKA
1 Msawala 43,969 394 78
2 Mkola 39,466 58 12
3 Mninga 35,187 68 14