halmashauri ya wilaya ya kilosa - home | kilosa...

44
Graphic designer © Amandus Mtani -2016 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA

Upload: others

Post on 19-Feb-2020

13 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOSA

MADA

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

Mhe. Angellah J. Kairuki (Mb)

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

NINI MAANA YA UTAWALA BORA?

1:0 UTANGULIZI

Miaka ya hivi karibuni maneno " utawala" na

"utawala bora yamekuwa yakitumika sana

katika mazungumzo ya kila siku. Utawala

mbaya "Bad governance" ni neno ambalo pia

linatumika kama utawala mbaya na chanzo

cha uovu katika jamii. wahisani wakubwa na

taasisi za fedha za kimataifa hupendelea

kutoa misaada yao pale ambapo

kunaonekana kuwa kuna utawala bora.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

Utawala 'Governance' ni neno ambalo si jipya na

lilianza kutumika tangu ustaarabu wa kale kwa

kifupi likiwa na maana ya hatua au mchakato wa

kufanya maamuzi au uamuzi na kutekeleza

maamuzi yaliyofanywa au kutotekelezwa.

Neno utawala pekee linaweza kutumika katika fasihi

kadhaa, mfano utawala katika ngazi za taasisi

"corporate governance, utawala wa kimataifa '

international governance, utawala wa kitaifa

'national governance' lakini pia utawala wa mitaa '

local governance.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

Kwa kuwa utawala ni mchakato wa kufanya

maamuzi na kuyatekeleza, mchanganuo wa

utawala hulenga kote, watekelezaji rasmi na

wasio rasmi ( formal and informal actors) hawa

wote lazima wahusishwe katika maamuzi na

utekelezaji wake ambapo Serikali ni miongoni

mwa watekelezaji wa utawala.

Watekelezaji hawa ni pamoja na wafanyabiashara

wakubwa, vyama vya wakulima na wafanyakazi,

ushirika, NGOs, taasisi za utafiti, viongozi wa

dini, taasisi za fedha, vyama vya siasa, majeshi

n.k.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.0 UTAWALA BORA Utawala bora ni nini?

2.1.Utawala bora ni matumizi ya uwezo (mamlaka)

wa kiserikali katika jitihada za kuongeza na kutumia

rasilimali hizo ili kuboresha maisha ya wananchi

2.1.1 Utawala bora ni neno linalotumika na

maendeleo ya kimataifa kueleza namna taasisi za

umma zinavyofanya mambo yake kwa umma na

kusimamia rasilimali zao.

2.1.2 Kwa mujibu wa ripoti ya Utawala na

Maendeleo ya Mwaka 1992 iliyofanywa na Benki ya

Dunia, utawala bora ni matumizi sahihi katika

kusimamia uchumi wa nchi na rasilimali za

Jamii katika maendeleo.Graphic designer © Amandus Mtani -2016

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.1.3 Shirika la Maendeleo Duniani la Umoja wa

Mataifa ( The United Nations Development

Programme (UNDP) lilitoa maana ya neno utawala

bora Mwaka 1997 katika ripoti yake ya sera iliyoitwa

“Governance for Sustainable Human Development”

kuwa ni utekelezaji wa uchumi, siasa na mamlaka ya

utawala katika kusimamia mambo ya nchi katika

ngazi zote.

MISINGI YA UTAWALA BORA

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2 MISINGI YA UTAWALA BORA

Misingi ya Utawala bora inatambulika kwa tofauti ya

idadi, mingine hutambulika kuwa ni ni mitano,

wakati mwingi misingi sita hadi nane hutajwa lakini

hata hivyo, misingi 15 nimeibaini katika mada yetu

hii.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.1 Utawala wa kidemokrasia, uchaguzi huru na haki

Kuhakikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka unakuwa huru na wa

haki ili kuwawezesha wananchi kuitumia vyema haki yao ya

kidemokrasia kwa kuchagua viongozi wanaowataka.

Uchaguzi usiwe chanzo cha kuvurugika kwa amani ya nchi

hivyo ufanyike kwa amani na utulivu. Uwepo wa vipindi vya

uchaguzi wa viongozi na chaguzi zenye kuzingatia haki na

usawa

0

2.2.2 Ushirikishwaji wa umma

Kuhakikisha kuwa bila kujali jinsi, wanawake na

wanaume, wanashiriki katika ngazi zote za utawal

bora. Ushirikishwaji waweza kuwa wa moja kwa

moja au kwa njia ya uwakilishi kupitia taasisi

zinazotambuliwa. Ikumbukwe hata hivyo kwamba

ushirikishwaji si lazima uhusishe jamii isiyofikika

mfano, jamii inayokula mizizi na matunda lazima

ishiriki katika maamuzi. ushirikishwaji unahitaji

mtiririko wa taarifa na mipango, kwa maana nyingi

na hapa unazungumziwa uhuru wa kujieleza na

vyama vya kijamii 'civil society '.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.3 Utawala wa kisheriaUtawala wa sheria yaani 'Rule of law' lazima uwepo

kwenye utawala bora. Sheria ziwe zinaongoza nchi

na asiwepo mtu aliye juu ya sheria. Miongoni mwa

waasisi wa Utawala wa sheria ni mwanafilosofia

Aristotle, ambaye aliandika "Law should govern".

yaani 'Sheria ni lazima iongoze'. Hii ni kuhakikisha

kwamba-;A. Serikali na maofisa wake wanawajibika chini ya sheria

B. Sheria ziko wazi, zinaeleweka kwa umma, haziyumbi na

zinalinda misingi ya haki ikiwemo usalama wa watu

na mali zao.

C. Mchakato unaoruhusu sheria kutendeka kwa wakati,

kusimamiwa na upatikanaji wa haki

D. Kuwa na uwezo wa kupata haki inayotolewa na wanasheria

mahiri na wenye maadili, mawakili, majaji, wawakilishi,

wanasheria na kwamba rasilimali sheria zinapatikana.

NUKUU"Nchi yetu inaongozwakwa sheria...Hatuwezikuchagua kiongoziasiyeheshimu sheriaakawa anaongoza nchikwa kushauriwa namkewe, maana hamjuikesho akiamkaatamshauri nini?"

JKN

2.2.4 Matarajio ya wananchi

Msingi au nguzo nyingine muhimu ni kuhakikisha

kwamba, matarajio ya wananchi yanafikiwa katika

kiwango cha kuridhisha, hii inaondoa malalamiko

lakini pia itawatia nguvu wananchi katika

kuendeleza shughuli za maendeleo.

2.2. 5 Kuheshimu haki za msingi za binadamu

Kuheshimu haki zote za msingi za binadamu

huleta usawa kwa watu wote, huondoa dhana ya

ubaguzi katika ngazi zote. Kuheshimu haki za

binadamu huleta heshima katika tamaduni za

watu na tofauti zao (diversity), kama uhuru wa

kuabudu, uhuru wa kushiriki n.k

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.6 Uwazi katika kuendesha shughuli za maendeleo

Mipango na Mgawanyo wa Rasilimali: Ni kiasi gani cha

fedha kilichopo? Nini kimepangwa kufanyika? Watoa

huduma wamepanga kuzitumia vipi? Mgawo wa

fedha/rasilimali za umma hutolewa kulingana na

Mpango Mkakati ulioainisha shughuli zote kwa kina na

kuidhinishwa.

Uwazi una maana kwamba uamuzi unafanyika katika

misingi ya sheria na taratibu lakini pia ina maana

mawasiliano au taarifa zinapatikana wakati wote kwa

watu watakaohusika ma maamuzi

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.7 Uwajibikaji katika utendajiUwajibikaji ni msingi muhimu wa utawala bora na hii si tu

kwa taasisi za serikali lakini hata pia kwa taasisi binafsi.

Taasisi binafsi na za umma, mtu mmoja mmoja lazima

wawajibike. Rushwa za aina zote ni shurti zipigwe vita na

kusiwepo na mianya ya rushwa kwa muktadha huo. Je, watoa

huduma wanatekeleza wajibu wao kwa ufanisi? Watumishi wa

umma wanatoa huduma bora za jamii?

Kupokea kero na malalamiko na kuyatatua kwa wakati na

kuwajulisha wananchi hatua zilizochukuliwa. Kuweka

masanduku ya maoni ambayo yatamwezesha kila mwananchi

kuweza kutoa maoni yake kwa njia ya siri. Kuitisha Mikutano

ya maendeleo Mikutano Mikuu ya Kata, Vijiji na vitongoji ili

kuweza kujadili suala la Maendeleo kwa uwazi kwani kila

mmoja atakuwa na nafasi katika kutoa maoni katika Mkutano

huo wa Hadhara.

2.2.8 Uadilifu

Hii inashabihana na uwazi ambapo inahusiana sana

mgawanyo na utumiaji wa rasilimali za taifa kwa

minajili ambayo haibagui watu na haipendelei walio

katika madaraka. Katika kuzingatia uwepo wa uwazi,

uwajibikaji na uadilifu, mifumo tofauti

imetengenezwa na mashirika ya kijamii na serikali ili

iweze kutumika katika jamii zetu na kuhakikisha

ustawi wa jamii nzima.

Uwazi unaweza kuwepo katika nyanja mbalimbali

kama utendaji, fedha nk. mfano wa mifumo hiyo ni;

PETS (Public Expenditure Track System), PRA

(Participatory Rural Appraisal- Ushirikishaji wa jamii

ya vijijini katika tathmini).

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.9 Ufanisi na tija ( Effectiveness and efficiency)

Utawala bora una maana mchakato na taasisi

kuzalisha matokeo ambayo yanakidhi mahitaji ya

jamii kwa wakati kwa kutumia rasilimali zilizopo

katika maeneo yao.

Dhana ya 'efficiency' katika muktadha wa utawala

bora ina maana kutumia rasilimali ipasavyo na

kulinda mazingira na neno effectiveness ni

kukamilisha majukumu kwa wakati.

Ufanisi na tija ni hali ya utendaji inayozalisha

matokeo yanayokidhi malengo na matarajio ya watu

na kuhakikisha matumizi mazuri ya rasilimali.

Ufanisi na Tija unajumuisha mambo yafuatayo:

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.9 Ufanisi na tija ( Effectiveness and efficiency)

Utendaji wenye matokeo yanayokidhi malengo

na matarajio ya watu wote.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

Kutumia rasilimali kwa uangalifu na umakini

(Matumizi bora ya rasilimali).

Utumiaji endelevu wa rasilimali kwa ufanisi

Utunzaji wa mazingira.

Utoaji wa uhakika wa huduma za jamii na kwa

wakati

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.10 Ujuzi na Uwezo kuboreshwa

Watu wenye ujuzi na uwezo katika makundi yote

wanapaswa kuendelea kuboreshwa kwa ajili ya

maendele ya taifa na wananchi wenyewe. Nchi

inayojali utawala bora hapana shaka dhana hii

inatekelezwa ipasavyo.

2.2.11 Utayari wa kubadilika

Huu ni msingi mwingine ya utawala bora, nchi

ambayo ina utayari wa kubadilika. Mfano kupokea

madiliko yenye tija, kuwahimiza wananchi kuwa

wabunifu na kupokea ubunifu, ubunifu ni kigezo

muhimu katika maendeleo ya nchi.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.12 Maendeleo ya endelevu (Sustainable Development)

Hii ni kuhakikisha kwamba maendeleo ya nchi

hayayumbi kiuchumi, maendeleo yanaboreshwa na nchi

inasonga mbele, kuepuka suala la, leo uchumi

unaanguka kesho uinuka keshokutwa unaanguka tena.

Uchumi wa nchi lazima uwe na mwendeleo wa kiuchumi

lakini pia uchumi wa mtu mmoja mmoja lazima

uonekane2.2.13 Mwitikio

'Responsiveness' au mwitikio ni hali ya kutoa huduma

kwa jamii kwa wakati na kwa kiwango kinachokidhi

matarajio ya watu. Mwitikio unajumuisha mambo

yafuatayo:

Kujali na kusikiliza matatizo ya watu.

Kutoa huduma kwa haraka na kwa kiwango bora.

Kukidhi matarajio ya watu.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.14 Ugatuaji wa madaraka

Ugatuaji wa madaraka yaani 'decentralization' ni

msingi mwingine muhimu kwa wananchi na

maendeleo ya taifa lenye misingi ya demokrasia ya

kweli.

Serikali inafanya ugatuaji wa madaraka kutoka

serikali kuu na kupeleka serikali za mitaa kwa lengo

la kuleta maendeleo nchini kuanzia ngazi ya vijiji

hadi serikali kuu, mfano Wizara ya Afya

inavyowajengea uwezo wananchi kupitia Serikali za

Mitaa namna yakujiongoza wenyewe kwenye masuala

ya afya ili kupunguza vifo.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.15 Maridhiano

Utawala bora unahimiza kukutanishwa kwa mawazo

mbalimbali ili kupata suluhu au maamuzi ya pamoja

ambayo yanazingatia matakwa ya jamii nzima.

Kwa muktadha huo basi, misingi hii ikizingatiwa na

kufanyiwa utekelezaji lazima mabadiliko yataonekana.

Ili utawala bora uwe na sifa za kupendeza na kupendwa

na wananchi, lazima uzingatie misingi yake

iliyoainishwa.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.3 NGUZO ZA UTAWALA BORA

Dhana ya Utawala Bora ina nguzo kuu tano:

Katiba ya kidemokrasia

Ulinzi, ukuzaji na uzingatiaji wa haki za

binadamu;

Mgawanyo wa Madaraka

Uhuru wa Mahakama

Uhuru wa habari na uhuru wa vyombo vya

habari.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.3.1 Katiba ya Kidemokrasia

Katiba ni waraka wa kisiasa na kisheria wenye

muafaka wa kitaifa juu ya namna ya kuendesha

masuala ya nchi. Demokrasia ni mfumo wa kisiasa

wa kuchagua na kubadilisha serikali kwa njia ya

uchaguzi ulio huru na wa haki. Ni Ushirikishwaji wa

kweli wa wananchi katika maisha ya kiuchumi,

kisiasa na kijamii. Hivyo, Katiba ya Kidemokrasia ni

ile ambayo kuandikwa kwake kumetokana na ridhaa

na mwafaka wa wananchi.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.3.2 Ulinzi, Ukuzaji na Uzingatiaji wa Haki

za Binadamu

Utawala bora ni ule unaolenga kuboresha na

kujali maisha ya watu. Njia ya msingi ya kujali

maisha ya watu ni kulinda, kukuza na kuzingatia

haki za binadamu. Utawala bora unataka kuwe

na mfumo wa kisheria, kiutawala na utashi wa

kisiasa unaolinda, kukuza na kuzingatia haki za

binadamu.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.3.3 Mgawanyo wa Madaraka

Dhana ya mgawanyo wa madaraka inaeleza kuwa utawala

wa dola unapaswa kugawanywa katika vyombo vitatu

ambavyo ni Serikali, Bunge na Mahakama. Kila chombo kina

majukumu tofauti na chombo kingine. Kwa mujibu wa

dhana hii, mamlaka ya Serikali ni utendaji; mamlaka ya

Bunge ni kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa

shughuli za umma; na mamlaka ya Mahakama ni kutafsiri

sheria na kutoa haki.

Hapa nchini, dhana hii inatajwa kwenye Ibara ya 4 ya

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka

1977. Dhana hii inazuia chombo kimoja kutawala, kuingilia

na kufanya kazi za chombo kingine. Lengo la mgawanyo wa

madaraka ni kuongeza ufanisi na kuleta uwajibikaji wa

vyombo vya dola.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.3.4 Uhuru wa Mahakama

Uhuru wa Mahakama unamaanisha kuwa kila jaji au

hakimu yuko huru kuamua kesi iliyopo mbele yake

kwa mujibu wa sheria na ushahidi ulioletwa mbele

yake, na katika kutekeleza majukumu hayo,

hapaswi kuingiliwa, kushawishiwa, au kushinikizwa

na mtu au chombo chochote, ikiwemo Bunge na

Serikali kama inavyoelezwa katika Ibara ya 107B ya

Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya

mwaka 1977.

Hivyo, dhana ya uhuru wa mahakama inaitaka

mahakama kutekeleza majukumu yake bila woga

wala upendeleo. Uhuru wa mahakama unahifadhiwa

na kulindwa katika maeneo manne ambayo ni:

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

i) Kuzuia kuondolewa kwa Jaji au Hakimu katika ofisi

bila ya sababu za msingi na bila ya kufuata taratibu

zilizowekwa hata kama kuna sababu za kumuondoa,

ii) Kuweka kinga ya kutoshtakiwa kwa Jaji au Hakimu

kwa makosa yoyote, yawe ya jinai au madai kutokana na

maamuzi yake ya kimahakama aliyoyafanya,

iii) Kutopunguza au kuondoa mishahara na maslahi ya

Jaji au Hakimu, na

iv) Kutokuwa na vyeo kwenye vyombo vingine vya dola

au kushiriki katika shughuli za vyama vya siasa.

Hata hivyo, ni vema ikafahamika kwamba uhuru wa

mahakama sio kibali kwa jaji au hakimu kuamua kesi

kwa namna anavyojisikia yeye au kwa matakwa yake.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.3.5 Uhuru wa Habari na Uhuru wa Vyombo

vya Habari

Uhuru wa habari una maana ya watu kuweza

kuzungumza na kupashana habari na kuwa na haki ya

kupata habari kutoka katika vyombo vya umma na hata

binafsi ambavyo vinatekeleza wajibu wa umma.

Hili lazima liende sawia na kuwa na vyombo vya habari

vilivyo huru, kwa maana ya kuwa na uwezo wa kutafuta

na kuandika habari na kuzisambaza kwa watu ndani na

nje ya mipaka ya nchi bila ya kuingiliwa na bila ya

sababu maalum na Serikali.

Lengo ni kuwawezesha wananchi kufahamu namna

viongozi wanavyoendesha nchi na hatimaye kujadili na

kutoa maamuzi juu ya rasilimali za nchi yao.

MSISITIZO:

Dhana ya utawala bora ni pana sana ambayo

inahitaji umakini zaidi ili kuweza kuitekeleza hivyo

ni lazima watendaji tuwajibike ipasavyo katika

kuhakikisha wananchi wanapata huduma iliyobora

na yenye manufaa kwao, na hii si kufanya kazi kwa

nadharia bali kufanya kazi kwa vitendo.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.4 NINI KIFANYIKE KUBORESHA UTAWALA BORA?

Kuongeza ushirikishwaji wa wananchi katika utendaji

wa shughuli za umma

Kujenga uelewa kwa kutoa elimu ya uraia ili kujenga

jamii iliyohabarishwa

Kufanya ushawishi ili kuboresha hali ya demokrasia

nchini

Kuandaa mihadhara ili jamii iweze kujadili masuala

ya kiutawala na kisiasa yanayoendelea nchini.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.4 FAIDA YA UTAWALA BORAUtawala bora unasaidia kuwa na mambo yafuatayo:

Matumizi mazuri ya rasilimali za nchi,

Maendeleo endelevu,

Kupungua kwa umasikini, ujinga na maradhi,

Kutokomea kwa rushwa,

Huduma bora za jamii,

Amani na utulivu,

Kuheshimiwa kwa haki za binadamu,

Utatuzi wa migogoro kwa wa sheria na taratibu,

Kuleta ustawi wa wananchi.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

2.2.5 UMUHIMU WA WANANCHI KUSHIRIKI

KATIKA UTAWALA:

Kukosoa matumizi mabaya ya fedha na viongozi kwa

misingi ya demokrasia

Kushirikishwa kupanga kusimamia miradi ya

maendeleo katika maeneo yao

Kuunga mkono jitihada za serikali katika kuchochea

ustawi na maendeleo kwa jamii

Kuhoji utendaji wa serikali kuanzia ngazi ya mtaa,

kata, kijiji, wilaya kuhakikisha uwazi, uadilifu na

uwajibikaji.

2.6.0 MISINGI YA UTOAJI WA HAKI

Uzingatiaji wa utawala bora hauhusu tu mhimili wa

serikali, bali pia unahusu vyombo vya kutoa haki.

Vyombo hivyo ni mahakama, mabaraza yenye asili ya

mahakama, kamati za nidhamu na vyombo vingine

vinayofanya kazi zenye asili ya kimahakama.

Hivyo, ili kuzingatia utawala bora katika utoaji wa

haki, Ibara ya 107A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano

wa Tanzania ya mwaka 1977, pamoja na sheria

mbalimbali, imeweka misingi ambayo vyombo vya

kutoa haki vinatakiwa viifuate. Misingi hiyo ni kama

ifuatavyo:

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

Kuzingatia Katiba na sheria za nchi;

Kutenda haki kwa wote bila ya kujali hali ya

mtu kijamii au kiuchumi;

Kutochelewesha haki bila sababu ya msingi;

Kutoa fidia stahiki kwa watu wanaoathirika

kutokana na makosa ya watu wengine;

Kukuza na kuendeleza usuluhishi baina ya

wanaohusika katika migogoro;

Kutenda haki bila kufungwa kupita kiasi na

masharti ya kiufundi yanayoweza kukwamisha

haki kutendeka;

Kuzingatia kanuni za haki ya asili (natural

justice).

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

6.1 Kanuni za Haki ya AsiliKanuni za Haki ya Asili ni kanuni zinazoongoza

kufanya maamuzi ya utoaji wa haki yaliyo ya haki

na kwa kufuata utaratibu ulio wa haki. Wakati haki

na wajibu wa mtu yeyote vinahitaji kufanyiwa

uamuzi na mahakama au chombo kinginecho

kinachohusika, basi mtoa maamuzi ana wajibu wa

kufuata kanuni za haki ya asili. Kanuni hizo ni:

Haki ya Kusikilizwa

Wajibu wa kutopendelea

Wajibu wa kutoa sababu za uamuziVyanzo vya kanuni za haki ya asili ni Katiba, sheria

mbalimbali za nchi na maamuzi mbalimbali ya

mahakama. Ufafanuzi wa kanuni hizo ni kama

ifuatavyo:

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

6.1.1 Haki ya Kusikilizwa

Haki ya kusikilizwa ina maanisha fursa ya

kusikilizwa kwa ukamilifu na kwa haki. Haki hii

inajumuisha kupewa taarifa ya kutosha na

yavmapema ya kesi ili kupata muda wa kuandaa

majibu ya kesi dhidi yake, kupewa nafasi ya kutoa

ushahidi wake kwa ukamilifu (ikiwani pamoja na

kuita mashahidi), kupewa fursa ya kuwauliza

maswali washitaki wake na kupewa fursa ya

kuwakilishwa, kama ilivyoelezwa kwenye Ibara ya

13 (6) (a) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

6.1.2 Wajibu wa KutopendeleaKanuni hii inatamka kuwa, mtu hatakiwi kuwa

muamuzi katika kesi yake mwenyewe; na

inatokana na msingi kuwa mtoa maamuzi

hatakiwi kuwa na upendeleo na asihisiwe kuwa na

upendeleo. Upendeleo unaweza kusababishwa na

maslahi binafsi ya mtoa maamuzi, iwe moja kwa

moja au vinginevyo.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

6.1.3 Wajibu wa Kutoa Sababu za Uamuzi

Mtoa maamuzi ana wajibu wa kutoa sababu za

uamuzi wake. Hii ni kwa sababu kila upande

katika mgogoro una haki ya kujulishwa sababu za

uamuzi uliofikiwa na chombo cha kutoa haki.

Uamuzi wa chombo cha kutoa haki unatakiwa

uhalalishwe na sababu za kina na ushahidi. Sababu

za uamuzi zinausaidia kila upande kujua ni

kwanini umeshinda au umeshindwa. Sababu za

uamuzi zinaimarisha uwazi katika utoaji wa haki.

Graphic designer © Amandus Mtani -2016

7.0 HITIMISHO

Bila shaka umebaini kuwa utawala bora ni nyenzo

muhimu sana ya kufanikisha ajenda kuu za nchi

yetu na dunia ambazo ni amani, maendeleo

endelevu na ustawi wa mwanadamu na jamii kwa

ujumla.

Kwa kuwa sasa umejifunza kuhusu utawala bora,

inatarajiwa kuwa kwa nafasi yako utakuwa mdau

muhimu wa kujenga jamii ambayo misingi ya

utawala bora, demokrasia, haki za binadamu, utu

na ustawi wa mwanadamu inakuzwa, inalindwa,

inazingatiwa, inatekelezwa na kuhifadhiwa.