jamhuri ya muungano wa tanzania ofisi ya waziri...
TRANSCRIPT
i
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA WAZIRI MKUU
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA
MITAA
HALMASHAURI YA WILAYA
TANDAHIMBA
MKOA WA MTWARA
MPANGO MKAKATI 2014 – 2018 Umeandaliwa na: Mkurugenzi Mtendaji (W) S.L.P.03 Simu: 0232410030 Kinukulishi 0232410030
Julai, 2013
2
Dibaji Muhtasari .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. i Shukrani .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. ii Makisio ya gharama za utekelezaji wa mpango .. .. .. .. .. .. .. iii 1.0 Utangulizi .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 1 1.1 Taratibu za Kisheria na Kisera .. .. .. .. .. .. .. .. 1 1.2 Mchakato wa Uandaaji wa Mpango .. .. .. .. .. .. .. 1 1.3 Mpango wenyewe .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 2 1.4 Mpangilio wa Ripoti (Mpango) .. .. .. .. .. .. .. .. 2 2.0 Hali ya Wilaya .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 3 2.1 Hali ya hewa .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 3 2.2 Maeneo ya Kiutawala .. .. .. .. .. .. .. .. .. 3 2.3 Idadi ya Watu .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 3 2.4 Shughuli za Kiuchumi .. .. .. .. .. .. .. .. .. 3 3. Hali Halisi ya Utoaji Huduma katika Wilaya .. .. .. .. .. .. 4 3.1 Shughuli za Kiuchumi .. .. .. .. .. .. .. .. .. 4 3.1.1 Kilimo .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 4 3.1.2 Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi .. .. .. .. .. .. .. .. 4 3.2 Huduma Za Jamii .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 5 3.2.1 Elimu Awali na ya Msingi .. .. .. .. .. .. .. .. 5 3.2.2 Elimu ya Watu wazima .. .. .. .. .. .. .. .. 5 3.2.3 Elimu ya Sekondari .. .. .. .. .. .. .. .. .. 6 3.2.4 Elimu ya Ufundi .. .. .. .. .. .. .. .. .. 7 3.2.5. Huduma za Afya .. .. .. .. .. .. .. .. .. 7 3.2.6 Maji .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 8 3.2.7 Mtandao wa Barabara na Ujenzi .. .. .. .. .. .. .. 8 3. 3.Huduma Nyingine .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 9 3.3.1 Ushirika .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 9 3.3.2 Maendeleo ya Jamii .. .. .. .. .. .. .. .. .. 9 3.3.3 Fedha na Biashara .. .. .. .. .. .. .. .. .. 10 3.3.4 Utawala na Utumishi .. .. .. .. .. .. .. .. .. 11 3.3.5 Ardhi, Maliasili na Mazingira .. .. .. .. .. .. .. .. 11 3.3.6 Manunuzi .. .. .. .. .. .. .. .. ..13 3.3.7 Sheria .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. ..15 3.3.8 Ukaguzi wa ndani .. .. .. .. .. .. .. .. ..15 4.0 Dira na Dhima .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 17 4.1 Maeneo ya matokeo Muhimu, Malengo mahsusi na Viashiria .. .. .. 18 4.2 Mikakati na Muda wa Utekelezaji .. .. .. .. .. .. ..18 4.3 Makisio ya gharama za utekelezaji wa mpango .. .. .. .. .. ..18 5. Sababu muhimu zitakazo saidia katika utekelezaji wa Dira na Dima ya Halmashauri –Viwezeshi na vikwamishi .. .. .. .. .. .. .. .. .. .. 19 6.0 Viambatisho( Mpango wenyewe) .. .. .. .. .. .. .. .. 20
3
Muhtasari Mpango Mkakati wa Miaka Mitano (2014-2018) wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba
unatoa mwelekeo wa vipaumbele vya Wilaya katika kipindi cha miaka mitano ijayo. Mpango huu
umetengenezwa kwa kuzingatia, Dira ya Maendeleo Ya Taifa ya mwaka 2025, Ilani ya uchaguzi
ya CCM ya 2010, Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini(MKUKUTA II), Sera
mbalimbali za Kisekta na Malengo ya Milenia. Na pia uandaaje wake umezingatia sheria ya Bunge
Kifungu cha 6 ya mwaka 1999 na Katiba ya Nchi Ibara namba 145 na 146 na Sheria inayounda
serikali za mitaa namba 7, 8, 9 na 10 ya mwaka 1982.
Mtazamo wa Mpango huu ni kutoa bora kwa Wananchi. Kwa ujumla Mpango huu pia huangalia
maswala Mtambuka kama vile jinsia, mazingira, na mapambano juu ya ukimwi na virusi vya
ukimwi. Kwa muhtasari Mpango huu wa miaka mitano 2014-2018 umetengenezwa kwa kuzingatia
mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika kutekeleza Mpango Mkakati wa Kwanza wa
Halmshauri (2004-2008) ili kutoa msukumo na ari katika kutoa huduma bora kwa wananchi. Ni
matumaini ya yangu kwamba Serikali Kuu pamoja Wadau wa maendeleo katika wilaya wataunga
mkono kwa hali na mali katika kufanikisha utekelezaji wa malengo na vipaumbele vilivyoainishwa
katika Mpango huu.
Mheshimiwa Ally N. Ndingo
Mwenyekiti wa Halmashauri
Julai 2013 i
4
SHUKURANI Kwa niaba ya Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba pamoja na menejimenti ya Wilaya,
ninapenda kuwashukuru wale wote ambao kwa njia moja au nyingine wamefanikisha zoezi la
uandaaji wa Mpango Mkatati wa Halmashauri yetu kwa Kipindi cha Miaka Mitano (2014-2018)
ijayo. Mpango huu ni mwongozo muhimu kwa Halmashauri katika utelezaji wa majukumu yake ya
kutoa huduma bora na kuwatumikia wananchi. Shukrani nyingi zimwendee Mheshimiwa Waziri
wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mheshimiwa Hawa Ghasia(MP), Mwenyekiti wa
Halmashuri, Mheshimiwa Ali Ndingo, Wakuu wa Idara na Vitengo and wafanyakazi wote wa
Halmashauri ya Wilaya. Kujitoa kwao, ushauri na maoni yao ndiyo yamesaidia kufanikisha zoezi
zima la uandaaji wa Mpango Mkakati huu wa Halmashuri. Shukrani za dhati pia ziwaendeee wale
wote walioshiriki kwenye Warsha ya Wadau na Kikao cha Kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo.
Mwishoni kabisa ningependa pia kutoa shukrani zangu kwa Dk. Charles Tundui wa Chuo Kikuu
Mzumbe kwa kuwezesha zoezi la uandaaji wa Mpango Mkakati wa Halmashauri yetu. Kama
Halmashauri, tunategemea kuwa huu utakuwa ni mwanzo wa ushirikiano wa muda mrefu wa taasisi
zetu.
Abdallah H. Njovu
Mkurugenzi wa Wilaya Tandahimba
Julai 2013 ii
5
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI WA MPANGO
Bajeti ya jumla inayohitaji kutekeleza Mpango Mkakati (2014-2018) ni shilingi 178,376,938,436. Mahitaji ya kila idara yameonyeshwa kwenye jedwali lifuatalo hapo chini
ENEO LA HUDUMA Gharama za Utekelezaji % ya Bajeti yote
Afya 19,250,246,436 10.8
Elimu 8,286,100,000 4.6
Elimu ya Sekondari 5,917,430,000 24.8 Ardhi 1,952,400,000 1.1
Kilimo, Umwagiliaji na ushirika 71,529,280,000 40.1
Mifugo 1,695,200,000 1.0
Maji 15,238,200,000 9.5
Ujezi na Barabara 10,402,260,000 5.8
Fedha 627,700,000 0.4
Biashara 618,600,000 0.3
Uumishi na Utawala 149,700,000 0.1
Mipango 685,500,000 0.4
Misitu na Mazingira 235,200,000 0.1
Kitengo cha Nyuki 134,500,000 0.1
Wanyapori 107,000,000 0.1
Kitengo cha Kitengo cha sheria 379,250,000 0.2
Kitengo cha Ugavi na Manunuzi 296,000,000 0.2
Kitengo cha Ukaguzi wa ndani 182,700,000 0.1
Maendeleo ya Jamii 688,100,000 0.4
Jumla Kuu 178,376,938,512
100.0
iii
1
HALMASHAURI YA WILAYA TANDAHIMBA
MPANGO MKAKATI
1.0 Utangulizi
Huu ni Mpango Mkakati wa Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba. Mpango huu ni wa pili (2)
tangu Halmashuri ilipoingia katika mchakato wa maboresho ya serikali za mitaa hapo mwaka 2003.
Lengo kuu la Mpango wa Maboresho ya Serikali za Mitaa Tanzania lilikuwa kuziwezesha serikali
za mitaa nchini kutoa huduma bora kwa wananchi zikishirikiana na wadau mbalimbali waliopo
katika Halmashauri hizo. Kwa hiyo ili kuleta ufanisi katika kutoa huduma bora kwa wananchi,
Serikali za Mitaa nchini zinahitajika kuwa na Mpango Mkakati wa Maendeleo. Kufuata utaratibu
huu kumetokana na ukweli kwamba Mpango Mkakati hutoa nafasi kwa Halmashauri kujitambua
kwamba yenyewe ni nini, inafanya nini na iko kwa ajili ya nani. Kwa kufuata Mpango Mkakati pia
kunaiwezesha Halmashauri kuwa na nafasi nzuri zaidi ya kuelewa kule inakoelekea kwa muda wa
miaka mitani ijayo, na ni kwa jinsi gani itafika huko. Mpango Mkakati pia huipa Halmashauri
nafasi ya kujitahmini ili kujua kwamba imefika huko iendako au la. Kwa upande mwingine kufuata
Mpango Mkakati katika utoaji wa huduma kunaiwezesha Halmashauri kuwa tayari kukabaliana na
mabadiliko ya taratibu pamoja na sera hasa katika ulimwengu wa Utandawazi. Kwa kufuata
utaratibu wa Mpango Mkakati, Halmashauri inaweza kujiwekea vipaumbele, kufanya maamuzi
kwa kuangalia na kuzingatia matokeo ya baadaye ya maamuzi ifanyayo sasa, na kujiweka katika
hali ya utayari wa kukabiliana na mabadiliko ya ndani au ya nje. Kwa hiyo uandaaji wa Mpango
huu umezingatia mambo hayo muhimu hapo juu kwa kuangalia maeneo ya utoaji huduma katika
Halmashauri.
1.1 Taratibu za Kisheria na Kisera
Mpango Mkakati wa Halmashauri ya Wilaya Tandahimba kwa mwaka 2014-2018 umeandaliwa
kwa kuzingatia taratibu za nchi za kisheria na kisera. Kwa hiyo uandaaji wake umezingatia:
� Dira ya Maendeleo Ya Taifa ya mwaka 2025
� Ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2010,
� Mpango wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini(MKUKUTA II)
� Sera mbalimbali za Kisekta na
� Malengo ya Milenia.
Na pia uandaaje wake umezingatia sheria ya Bunge Kifungu cha 6 ya mwaka 1999 na Katiba ya
Nchi Ibara namba 145 na 146 na Sheria inayounda serikali za mitaa namba 7, 8, 9 na 10 ya mwaka
1982.
2
1.2. Mchakato wa Uandaaji wa Mpango
Ili kufikia hatua ya mwisho ya uandaaji wa Mpango huu, hatua mbili muhimu zimepitiwa. Katika
hatua ya kwanza, Wakuu wa idara/vitengo walifanya tathmini na uchambuzi wa utekekelzaji wa
Mpango Mkakati wa kwanza wa Halmshauri (2004-2009) pamoja na hali ya utoaji huduma katika
Halmashauri, kwa lengo la kubaini mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji
wake. Matokeo ya tathmini na uchambuzi huo yaliwasilishwa kwenye kikao cha Wadau wa
Halmashauri kilichofanyikwa kwa siku mbili wilayani Tandahimba kati ya tarehe 14 na 15 ya
Mwezi Juni 2013. Katika warsha hiyo, wadua kwa pamoja walipata fursa na kujadili chamngamoto
hizo. Katika warsha hiyo pia wadau walipata nafasi ya kubuni malengo, kubaini vipaumbele na
kuweka mikakati kwa ajili ya Mpango Mkakati wa Pili wa Halmashauri (2014-2018) ili kuteleza
dira na kufikia dhima ya Halmashauri.
1.3. Mpango wenyewe
Uandaaji wa Mpango huu hasa ulizingatia matokeo na maamuzi ya warsha ya Wadau. Kwa
kuzingatia hilo Wakuu wa Idara pamoja na Vitengo kwa pamoja waliangalia na kuhakiki malengo,
vipaumbele, mikakati na viashiria kama vilivyoainishwa na wadau. Pia walifanya uhakiki wa
utekezaji wa mikakati hiyo kwa kuangalia vyanzo mbalimbali vya mapato vya Halmashuri.
Mchakato wa uandaaji wa Mpango huu ulifanyika kuanzia tarehe 17 -22 Juni 2013.
1.4. Mpangilio wa Ripoti (Mpango)
Mpango huu una sehemu sita (6). Sekemu ya kwanza ni utangulizi na utaratibu uliotumika katika
uandaaji wa mpango. Sehemu ya pili ni muhtasari wa hali ya Halmashauri(Council profile), na
sehemu ya tatu inatoa hali halisi ya utoaji huduma katika katika Halmashauri. Sehemu ya nne
inaelezea Dira na Dhima ya Halmashauri kama ilivyohusihwa kwenye Kikao cha Wakuu wa
idara/vitengo. Sehemu hiyo pia inatoa malengo mkakati, viashiria, mikakati, pamoja muda wa
utekelezaji wa mikakati hiyo kwa kila sekta au eneo la huduma na vyanzo vya fedha kwa kwa
utekelezaji wa mikakati mbalimbali.
Sehemu ya tano inatoa mambo yale ambayo kwa namna moja au nyingine yanaweza kuathiri
utekelezaji wa mpango huu kwa ujumla wake. Na sehemu ya mwisho kuna viambatisho.
3
2.0 Hali ya Wilaya
Wilaya ya Tandahimba ni mojawapo ya wilaya tano za mkoa wa Mtwara. Wilaya inapakana na
Wilaya ya Newala kwa upande wa magharibi, Wilaya ya Mtwara Vijini kwa upande wa mashariki,
Mkoa wa Lindi upande wa kaskazini na Mkoa wa Ruvuma kwa upande wa kusini. Wilaya ina
jumla ya eneo la mraba la kilomita 167,331. Kati ya hizi hekta 166,535 zinafaa kwa kilimo. Hata
hivyo in hekta129,507 ambazo zinalimwa.
2.1 Hali ya hewa Wilaya ipo mita 900 juu ya usawa wa bahari na pia ina eneo kubwa lenye uwanda wa Savanna wa
Makonde pamoja na aina mbalimbali za nyasi na vichaka. Wilaya inapata mvua za wastani kati ya
800mm – 900 mm kwa mwaka. Wilaya pia ina msimu mmoja tu wa mvua ndefu zinazonyesh
kipindi cha Novemba - Mei. Kipindi cha ukavu huanza katikati ya mwezi Mei mpaka Oktoba.
Kiwango cha nyuzi joto ni kati ya nyuzi 21 katika mwezi wa Juni na nyuzi 28 katika mwezi wa
Oktoba.
2.2 Maeneo ya Kiutawala
Kiutawala wilaya imegawanyika katika tarafa 3 , kata 30, vijiji 157 na jimbo moja la uchanguzi
2.3 Idadi ya Watu
Kulingana za hesabu ya watu ya mwaka 2012, wilaya ina jumla ya watu 227,514. Kati ya hawa
wanaume ni 105,322 na wanawake ni 122,192. Wilaya ina kaya 56,878 zenye wastani ya watu 3.7
kwa kila kaya.
2.4 Shughuli za Kiuchumi
Shughuli kuu za kiuchumi katika wilaya ni kilimo ambacho kinachangia asilimia 75 ya pato la
wilaya. Mazao yanayolimwa ni pamoja na mihogo, mahindi, mtama na mpunga. Mazoa ya
biashara ni korosho, karanga, ufuta. Kulingana na takwimu, pato la mwananchi katika wilaya (per
capita income) kwa mwaka 2012, linakisiwa kuwa ya kati ya 230,000 na 350,000. Sababu zinazo
changia umaskini katika wilaya ni pamoja na zana duni la uzalishaji, miundo mbinu hafifu na mila
na desturi zinazopinga maendeleo.
4
3. Hali Halisi ya Utoaji Huduma katika Wilaya
Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba kama zilivyo halmashauri nyingine nchini inakabiliwa na
changamoto nyingi katika pamoja na raslimali katika kuwaletea wananchi wake maendeleo. Kwa
hiyo ina lazimika kutegemea serikali kuu kwa ajili ya ruzuku ili kuendesha shughuli zake za
maendeleo. Hali hii imesababisha utoaji wa huduma usiokidhi mahitaji. Hata hivyo wilaya inazo
fursa nyingi ambazo inaweza kuzitumia kuwaletea wananchi wake maendeleo. Muhtasari ufuatao
unatoa hali halisi ya utoaji huduma katika wilaya:
3.1 Shughuli za Kiuchumi
3.1.1 Kilimo
Kam ilivyokwisha kuanishwa hapo juu, wilaya ina jumla ya eneo la mraba la kilomita 167,331.
Kati ya hizi eneo linalofaa kwa kilimo ni hekta 166,535. Hata hivyo hekta129,507 tu ambazo ziko
chini ya shughuli za kilimo. Mazao yanayolimwa ni pamoja korosho, muhogo, mtama, mpunga,
ufuta, nazi na mengineyo.
Baadhi ya mafanikio ni pamoja na kuongeza uzalishaji wa mazao ya biashara kama vile
uzalishajiwa korosho kutoka tani 15,282 mwaka 2005 hadi kufikia tani 47,682 mwaka 2011/2012
na inakadiliwa kufikia tani 80,000 ifikapo mwaka 2018/2019, kuongeza uzalishaji wa karanga
kutoka kutoka tani 1271 mwaka 2004/2005 hadi tani 3,129 mwaka 2011/2012. Wilaya pia
imefanikiwa kuanzisha jumla ya vituo 3 vya kutolea elimu (resource centres) na kuimarisha
udhibiti wa visumbufu vya mazao na mimea. Wilaya pia inatekeleza miradi mitatu (3) ya
umwagiliaji katika maeneo ya ya Litehu, Lipalwe na Ng’apa. Miradi hii imeshaunda umoja wa
umwagiliaji na kusajiliwa kisheria. Jumla ya wanachama katika miradi yote mitatu ni 201. Miradi
inakamati za usimamizi na zina akaunti Benki.
3.1.2 Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Wilaya ina jumla ya ngombe 319 wa maziwa, mbuzi 289,975, kondoo 53,436 na wanyama
wengineo. Lengo ni kuwa na miundombinu muhimu kwa ajili ya kuendeleza tasnia ya mifugo. Ili
kutekeleza sheria ya nyama No. 10 ya mwaka 2006 ya kuhakikisha kuwa nyama inayoliwa ni
salama. Halmashauri kupitia idara ya Mifugo na Uvuvi imejenga machinjio 2, malambo 3 kwa ajili
ya kunyweshea maji mifugo yamejengwa na kujenga kliniki mojakwa ajili kutambua kimaabara
magonjwa ya mifugo.
Kwa upande wa uvuvi, idara imefanikiwa kutoa elimu juu ya ufugaji bora wa samaki kwa wafugaji
binafsi nakushauri wafugaji kuchimba mabwa wa kwa ajili ya kufuga samaki.
5
Baadhi ya changamoto zinazoikabili wilaya katika mifugo ni pamoja na upungufu wa maafisa
ugani ambao idadi yao haitoshi kusimamia shughuli za kilimo na mifugo na uvuvi katika wilaya,
ufinyu wa bajeti ili kununua chanjo na mafuta ili kuwafikia wafugaji wengi zaidi pamoja na bei
kubwa ya chanjo.
Kwa hiyo Wilaya inakusudia kuimarisha huduma za ugani kwa wafugaji. Hii ni pamoja na
kuongezeka kwa uzito wa ng’ombe kutoka kilo 250 hadi 350, kuongeza uzalishaji wa maziwa kwa
ng’ombe kwa mwaka kutoka lita 400 hadi 2000, na kuongezeka kwa mbuzi walioboreshwa
kutoka 217 – 3800 ifikapo 2018ifikapo mwaka 2018. Wilaya pia inalenga kuongeza idadi ya vijiji
vilivyotenga maeneo ya malisho na kuanzishwa kwa vikundi vya wafugaji vitano (5) vinavyotumia
nishati ya gesi (Bio-gas) ya kupikia ifikapo 2018.
3.2 Huduma Za Jamii
3.2.1. Elimu Awali na ya Msingi
Kwa upande wa elimu ya msingi, wilaya ina jumla ya shule 118. Shule hizi zina jumla ya
wanafunzi 37232 . Kati ya hawa wavulana ni 20,030 na wasichana ni 17,199. Aidha, kuna shule za
Awali 108 na vituo vya walimu 5. Kwa sasa kuna jumla ya walimu 998, kati yao 957 ni walimu
walio vituoni wanafundisha, 30 ni waratibu wa kata na 11 wapo ofisini.
Uandikishaji katika shule za msingi uko kwenye asilimia 82%, wakati utoro uko asilimia 44%.
Kwa upande mwingine kiwango cha kufaulu darasa la saba mwaka 2012 kilikuwa ni asiliamia
46.6%. Kati ya hawa ni asilimia 49% tu ambao walichaguliwa kujiunga na shule ya sekondari.
Viashiria vya utoaji wa huduma katika elimu ya msingi ni kama inavyoonekana hapo chini.
Jedwali 1: Majengo na samani
Aina ya samani Mahitaji Hali halisi Upungufu Asilim ia Madawati 22,638 18,264 4,374 19.3 Meza 2647 963 1684 63.6 Viti 2958 116 2842 96.0 Makabati 1628 173 1455 89.3 Aina ya majengo Nyumba za Walimu 1320 228 1092 82.7 Vyumba vya madarasa
1182 771 411 34.7
Vyoo wavulana 872 371 501 57 Vyoo wasichana 1079 380 699 64.7
6
3.2.2 Elimu ya Watu wazima
Wilaya imekuwa na mipango madhubuti ya kumpatia mtu mzima elimu kupitia programu
mbalimbali za Elimu ya watu Wazima kama ifuatavyo:
Mpango wa elimu kwa walioikosa(MENKWA), Kisomo chenye manufaa (Kumekuwa na madarasa
kwenye vijiji vya Pemba, Majengo, Namdowola, Mitondi A na Mitondi B), Mpango wa uwiano
kati ya elimu ya watu wazima na jamii(MUKEJA) na kisomo cha kujiendeleza (KCK).
Changamoto zinazoikabili wilaya katika utoaji wa elimu ni pamoja na mwamko mdogo wa
kieliemu katika jamii, ukosefu wa madarasa ya elimu ya watu wazima, walimu wenye sifa,
upungufu wa nyumba za walimu, ofisi na vifaa vya kufundishia na utoro.
Baadhi ya malengo katika kipindi hiki cha mpango ni pamoja na kuongeza idadi hiyo ya madarasa
katika kila shule ya msingi, kuongeza idadi ya watoto wanaosajiliwa wenye umri wa kwenda
shule kutoka 83% hadi 94% ya wanaoandikishwa, kupunguza utoro shuleni, kuongezwa idadi ya
madarasa yanayojengwa, nyumba za walimu, ukarabati wa majengo na ujenzi wa matundu ya vyoo.
3.2.3 Elimu ya Sekondari
Kuna jumla ya shule za sekondari 26 zinazomilikiwa na Halmashauri ya wilaya ya Tandandahimba.
Shule hizi ni za kutwa na zina mikondo ya kidato cha kwanza hadi cha Nne. Wilaya pia ina shule
moja yenye mikondo ya kidato cha tano na sita. Hata hivyo kwa mwaka 2012 shule hiyo
haijapangiwa wanafunzi wa vidato hivyo kutokana na ufaulu mdogo wa wanafunzi wa kidato cha
nne nchini. Ufaulu kwa kidato cha nne kwa mwaka 2012 ulikuwa asilimia 12 tu ya watahiniwa
wote, na kidato cha pili ulikuwa asilimia 36% tu . Takwimu za wanafunzi kwa mwaka 2013
zinaonesha kuwa shule za sekondari zina jumla ya wanafunzi 9,896. Kati ya hawa wavulana ni
5,277 na wasichana ni 4,619. Katika mwaka 2012 kiasi cha wanafunzi 2323 walichaguliwa
kujiunga na kidato cha kwanza. Na ni wanafunzi 1552 (66.8%) tu ambao walijiunga na masomo ya
sekondari.
Kwa upande wa walimu Wilaya ya Tandahimba ina jumla ya walimu 259. Kati ya hawa wanaume
ni 199 na wanawake ni 60. Hata hivyo wengi wa walimu waliopo ni wa masomo ya sanaa.
Changamoto nyingine zinazoikabili wilaya ni pamoja na utoro wa wanafunzi, ulipaji wa kusuasua
wa karo za wanafunzi na ushirikiano mdogo kwa baadhi ya wazazi,walimu au uongozi wa shule
katika masuala ya elimu. Wilaya pia inakabiliwa na wimbi la walimu kuomba kuhama kutokana na
mazingira magumu wanayokabiliana nayo katika shule hasa ukosefu wa nyumba za kuishi hasa
kwa maeneo ya vijijini ambako hakuna nyumba za kupanga walimu.
7
Halmashauri kwa kutambua changamoto wanazo kumbana nazo wanafunzi wa kike kwa
kushirikiana na wananchi imeweza kujenga majengo ya Hostel katika baadhi ya shule za sekondari
kama vile Mkonjowano, Dinduma,Kitama, Luagala,Mahuta na Ngunja kwa lengo la kuwasaidia
wanafunzi wa kike ili waweze kuishi shuleni. Hata hivyo hosteli hizi hazitumiki kikamilifu kwa
maana ya wazazi/walezi hawapendi kuwaruhusu watoto wao kuishi shuleni. Hali ya miundo mbinu
ni kama ifuatavyo:
Jedwali 2: Miundombinu-Elimu ya Sekondari
MAHITAJI MAHITAJI Hali halisi UPUNGUFU % (VILIVYOPO )
Nyumba 259 74 185 16.81
Madarasa 256 203 53 71.47
Matundu-vyoo 334 247 87 26.04
Maabara 78 06 72 7.69
Hostel 52 06 46 11.53
Majengo ya utawala 26 12 14 46.15
Katika kipindi hiki cha mpango pamojana mambo mengine wilaya inalenga kuongeza kiwango
ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha pili na cha nne, kuongeza idadi ya wanafunzi wanaosajiliwa
kujiunga na kidato cha kwanza kwa wanafunzi wanaokuwa na sifa za kujiunga kidato cha kwanza,
kuongeza idadi ya walimu walioajiriwa na madarasa na nyumba za walimu.
3.2.4. Elimu ya Ufundi
Wilaya ina vyuo viwili vya elimu ya ufundi. Vijana wanaomaliza darasa la VII hujiunga na vituo
vya ufundi stadi vilivyopo Matogoro na Luagala Mission na kupata mafunzo ya ufundi seremala,
uashi na sayansi kimu.
3.2.5. Huduma za Afya
Wilaya ya Tanndahimba ina jumla ya vituo 34 vya kutolea huduma za afya. Hii ni pamoja na Hospitali moja inayomilikiwa na serikali, vituo vya afya 3 kimoja kati ya vituo hivyo kinamilikiwa na shirika la Kanisa la Katoliki na vituo vingine 2 vinamilikiwa na serikali.Pia kuna zahanati 30, zahanati 29 kati ya hizo zinamilikiwa na serikali na moja inamilikiwa na mtu binafsi. Pia kuna maduka ya dawa baridi 27.
Jedwali 3: Huduma za Afya katika Wilaya ya Tandahimba
Huduma Serikali Za kidini Binafs1 Jumla
Hospitali 1 - - 1
Vituo vya Afya 2 1 3
Zahanati 29 1 30
Total 32 1 1 34
8
Viashiria vingine vya utoaji huduma ya afya ni kama inavyoonekana kwenye majedwali
tafuatayto.
Hali halisi Lengo
Vivyo vya akina mama
Wakati wa kujifungu :140 / 100,000 100/100,000
Vifo vya watoto chini ya miaka mitano : 400/1000 200/1000
Huduma ya uzazi wa mpango : 65% 75%
Maambukizi ya virusi vya ukimwi : 3% 1%
Vifo vinvyosababishwa na Malaria : 51 30
Kaya zenye vyoo bora : 30% 65%
Baadhi ya matatizo yanaikabili wilaya katika utoaji wa huduma ya afya ni pamoja na upungufu wa
fedha, wataalamu wa kutosha na sifa, upungufu wa madawa na vitendea kazi. Kwa hiyo Wilaya
inakusudia kuimarisha utaoji wa huduma kwa kujiri wataalamu zaidi nakuongeza idadi ya vitendea
kazi.
3.2.6 Maji
Takwimu za mahitaji ya maji katika Wilaya bado hazijulikani.Hata hivyo uzalishaji wa smaji
hautoshelezi matumizi ya wakazi katika wilaya. Tatizo kubwa ni kwamba Wilaya haina chanzo
chake chenyewe cha maji.
Kuzingatia hali hapo juu, halmshauri inakusudia kuaongeza huduma ya maji kwa wananchi kwa
kuileta huduma hiyo karibu na walipo. Hii ni pamoja na kuimarisha kamati na mifuko ya maji.
Wilaya pia inakusudia kuanzisha Mamlaka na bodi ya maji ya wilaya. Katika kipindi hiki cha
mpango, Wilaya inakusudia kuanzisha miradi mipya ya maji kwenye vijiji 50, kuwaelimisha
wananchi juu ya teknolojia rahisi na sahihi ya uvunaji maji katika vijiji 30 na Kuunda Mamlaka ya
Maji na Jumuiya 30 za watumia maji .
3.2.7 Mtandao wa Barabara na Ujenzi
Wilaya ya Tandahimba ina jumla ya km 1276 za mtandao wa barabara na kati ya hizo km 70 ni za
Kitaifa, km 225 ni za Kimkoa na km 981 ndizo zinahudumiwa na Halmashauri,ambapo kati ya hizo
km 98.06 ni za kiwango cha kifusi na km 882.94 ni za kiwango cha udongo. Kila mwaka
matengenezo yanayofanyika ni wastani wa km 370 tu . Aidha barabara zinazopitika kwa kipindi
chote cha mwaka ni asilimia sabini na tano (75%). Wilaya pia ina jumla ya makalvati 89
yaliyojengwa, na kati ya hayo makalvati 16 yanahitaji kufanyiwa ukarabati na mengine kujengwa
upya. Hata hivyo kutokana na uhaba wa fedha barabara hizo hazifanyiwi matengenezo ya mara
9
kwa mara. Kwa upande mwingine, Wilaya haina usafiri wa kuaminika kwa ajili ya usimamizi
kutokana na uchakavu wa gari lilipo na uhaba wa vifaa.
Kwa upande wa ujenzi, Idara ya ujenzi kupitia kitengo cha majengo kinashughulika na usimamizi
na ukaguzi wa majengo ya serikali na ya watu binafsi ili yaweze kujengwa katika viwango na
ubora unaotakiwa. Pamoja na kazi hizo za kitengo cha majengo, idara inashughulika pia na
kukagua na kupitisha michoro ya majengo ya serikali na ya watu binafsi ili yajengwe katika ubora.
Hata hivyo zoezi hilo limekosa ushirikiano kutoka kwa baadhi ya wananchi pale wanaposhauriwa
juu ya ujenzi wa nyumba zenye viwango na ubora unaotakiwa.
Katika kipindi hiki cha Mpango, Wilaya inakusudia kuongeza matengenzo ya barabara ikiwa ni
pamoja na ujenzi wa barabara mpya, ujenzi wa mifereji ya maji ya mvua na uwekaji wa alama za
usalama barabarani.
3. 3.Huduma Nyingine
3.3.1 Ushirika
Wilaya na jumla ya vyama vitano (5) vya kuweka na kukopa (SACCOS) vilivyoandikishwa na
kusajiliwa. Jumla ya wanachama wa vyma hivi ni 220.
Matatizo makubwa yanayoikabili idara ni pamoja na ukosefu wa wataalamu wa kutosha,
kukosekana kwa huduma za ukaguzi na mafunzo kwa wataalamu. Kwa hiyo lengo kubwa ni
pamoja na kuongeza idadi ya wataalamu wa ushirika, kutoa mafunzo kwa wanachama, kuimarisha
shughuli za ukaguzi wa vyama na kufanya uchaguzi kwa kufuata sheria.
3.3.2 Maendeleo ya Jamii
Idara ya maendeleo ya jamii inahusika zaidi katika kuwahamasisha wananchi katika kujiletea
maendeleo yao wenyewe kwa kutumia rasilimali walizo nazo. Hii ni pamoja na uanzishaji wa
vikundi mbalimbali vya uzalishaji. Katika kutekeleza majukumu yake Idara imeweza kusajili
vikundi 900 vya uzalishaji mali vya vijana, vijana 175 wameunganishwa na SACCOS za ufugaji
nyuki za Tandahimba na Chingungwe. Elimu ya ujasilimali imetolewa kwa vijana 2000 kwa
kushirikiana na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali.
Kwa upande wa akina mama Wilaya imefanikiwa kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa vikundi 67
yenye thamani Tsh 100,000,000/= toka mwaka 2008 hadi mwaka 2012, vikundi 1200 vya
wajasiliamali wanawake vimesajiliwa ngazi ya wilaya na VICOBA 300 vya wanawake
vimeanzishwa kuwawezesha wanawake kuweka na kukopa kwa riba nafuu.
10
Katika juhudi za kupambana na maambukizi ya virusi vya ukimwi, wilaya kupitia idara hii
imeweza kutoa elimu kwa wamama pamoja na vijana juu namna ya kujikinga na UKIMWI.
Wilaya pia imetoa mafunzo kwa makungwi na mangariba ili kuzuia mila potofu zinazochangia
maambukizi. Pamoja na mambo mengine, Wilaya pia imefanikiwa kuendesha makongamano ya
kupinga ukatili wa kijinsia.
Pamoja na mafanikio hayo, wilaya imeshindwa kutekeleza majukumu yake kama inavyostahili
kutokana na uhaba wa watumishi. Kwa mfano idara ina watumishi 16 tu. Huu ni upungufu wa
watumishi 23 wanaohitajika kulingana na sera ya maendeleo ya jamii inayotaka kila kata kupata
afisa maendeleo ya jamii. Idara pia inakabiliwa na ujereshaji hafifu wa mikopo ya wamama na
vijana. Na pia kwa upande wa vijana vikundi vingi vilivyosajiliwa haviko hai kutokana na vijana
wengi kukimbilia mijini na ufinyu wa bajeti ya mikopo kwa vijana. Wilaya pia imeshindwa kupata
mikopo yenye riba nafuu ya wanawake kutoka wizarani kutokana na kusitishwa kwake. Hii ni
pamoja na wilaya kushindwa kutenga asimilia 15 ya mapato yake ili kutoa mikopo kwa akina
mama.
Katika kipindi hiki cha mpango, Halmashauri inakusudia kuongeza urejeshaji wa mikopo ya vijana
na akina mama kwa wakati. Ili kutimiza lengo hilo mikopo ya wanawake na vijana itakuwa
inatolewa kupitia benki ya wananchi TACOBA. Wilaya pia inalenga kuongeza idadi ya vikundi
vya ujasiliamali vya wanawake na vijana vinavyopewa mkopo. Hii ni pamoja na kuwapa mafunzo
ya jinsi ya kuendesha biashara, kuongeza idadi ya watumishi wa idara, kuanzisha baraza la wazee
nk.
3.3.3 Fedha na Biashara
Kulingana na utaratibu na usimammizi wa fedha kama ilivyoainishwa kwenye Waraka wa pesa za
serikali za mitaa (Local Authorities Financial Memorandum made under the local Govt. Finance
Act No. 9 of 1982) majukumu makubwa ya idara ni:-
� Kuishauri Halmashauri katika masula yote yanayohusu pesa
� Kusimamia na kuhahakikisha sheria na kanuni za fedha zinafuatwa
� Kusimamia na kukusanyaji wa mapato ya Halmashauri
� Kusimamia na kuhakikisha matumizi yote ya pesa za Halmashauri yanafanyikga kulingana na
bajeti pamoja na mipango ya utekelezaji iliyopitishwa.
� Kuandaa mihutasari ya mapato na matumuizi ya pesa za Halmashauri kila mwaka na kuikabidhi
kwa Mkagiuzi Mkuu wa Serikali
11
Tatizo kubwa linaloikabili idara ni pamoja na ukosefu wa fedha za shughuli za idara pamoja na
usafiri. Kulingana na majukumu hayo hapo juu, idara inakusudia kuongeza ukusanyaji wa mapato
ya Halmshauri, kutoa huduma bora kwa wananchi na kuhakikisha kanuni na taratibu za fedha
zinafuatwa.
Biashara
Kitengo cha Biashara kina simamia taratibu na sheria za Biashara pia kusimamia
Wafanyabiashara katika Wilaya. Aidha kitengo kinasimamia maswala ya ulipaji kodi kwa hiari
pamoja na kukata leseni za biashara. Kitengo cha Biashara kinafanya shughuli za kukagua bei za
bidhaa mbalimbali na kufuatilia ushuru wa Halmashauri kutoka kwa wafanyabiashara mbalimbali.
Wilaya ya Tandahimba ina jumla ya wafanya biashara wa maduka 868, Nyumba za kulala wageni
14, Mashine za kukoboa na kusaga nafaka 94,Vituo vya mafuta 3, Biashara za Bar na Grocery 5 na
wafanyanyabiashara ndogondogo 609 ambao wanatambulika na kulipa ushuru na kodi mbalimbali.
Vyanzo vya Mapato vya Halmshauri
Zaidi ya 80% wananchi wa Wilaya ya Tandahimba wanategemea kilimo. Kwa hiyo mapato ya
wilaya kwa sehemu kubwa pia yanategemea shughuli hii(75% ya mapato yote). Asilimia inayobaki
inatokana na vyanzo vingine kama biashara. Vyanzo hivi ni pamoja na mapato kutoka kwenye
maduka, migahawa, vioski , mashine za kusaga nafaka, gereji, nyumba za kulala wageni na
maduka ya dawa baridi. Hata hivyo vyanzo hivi vimekuwa havitoshelezi mahitaji ya Wilaya. Kwa
hiyo wilaya kwa sehemu kubwa imekuwa ikitegemea ruzuku toka serikalini pamoja na wafadhili
wengine kwa jili ya shughuli zake za maendeleo.
3.3.4 Utawala na Utumishi
Idara hii inatoa huduma zifuatazo kwa watumishi wa Halmashauri:
Kutafsiri sheria, kanuni na taratibu za kiutumishi kwa watumishi wa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, kutekeleza huduma ya utawala bora kwa wananchi na watumizhi wa
Halmashauri ya wilaya Tandahimba.
Idara pia inahusika kutoa huduma ya Afya kwa watumishi wanaoletwa na Serikali ya Ajira pamoja
na Wizara mbalimba za Tanzania na kutekeleza maagizof yote yanayotolewa na Mkurugenzi
Mtendaji (W).
Kwa upande wa watumishi Halmashauri ina jumla ya watumishi 1673. Hawa ndiyo watumishi
wanaotarajiwa kutekeleza malengo yalioaninishwa katika Mpango Mkakati. Hata hivyo idadi yao
12
ni ndogo uikilinganisha na mahitaji halisi kama ikama ya Halmashauri inavyoonesha hapo chini.
Kuna upungufu katika baadhi ya idara, kiasi cha kuasiri utoaji huduma katika idara husika. Idara
ambazo zina upungufu mkubwa ni pamoja na Usafi na Mazingira, Maji na Ustawi wa Jamii na
Vijana. Kwa mantiki hiyo, ili kutekeleza malengo yaliyoainishwa kwenye Mpango Mkakati huu
Halmashauri inawajibika kuajiri watumishi zaidi. Jedwali lifuatalo linaonyesha ikama ya
Halmashauri ya andahimba.
Jedwali 4: Ikama ya Halmashauri
Idara Wanaohitajika Waliopo Upungufu % ya
upungufu
1 Utawala na Utumishi 98 56 42 42.9
2 Mipango, Takwimu na ufuatiliaji 4 2 2 50.0
3 Elimu ya Msingi 1498 968 530 35.4
4 Elimu ya Sekondari 440 260 180 40.9
5 Afya 400 244 156 39.0
6 Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa
Jamii na Vijana
38 14 24 63.2
7 Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika 98 56 42 42.9
8 Mifugo na Uvuvi 24 14 10 41.7
9 Ardhi na Maliasili 22 15 7 31.8
10 Usafi na Mazingira 35 7 28 80.0
11 Maji 15 6 9 60.0
12 Fedha na Biashara 15 15 0 0.0
13 Ujenzi 17 10 7 41.2
14 Kitengo cha Ufugaji na Nyuki 3 0 3 100.0
15 Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani 3 2 1 33.3
16 Kitengo cha Sheria 2 0 2 100.0
17 Kitengo cha Ugavi na manunuzi 5 4 1 20.0
18 Kitengo cha Uchaguzi wa ndani 1 0 1 100.0
19 Kitengo cha Teknolojia, habari,
mawasiliano na uhusiano
1 0 1
100.0
Jumla 2719 1673 1046 38.5
13
3.3.5 Ardhi, Maliasili na Mazingira
Jukumu kubwa la idara ya ardhi, maliasili na mazingira ni kuwawezesha wananchi kuitumia ardhi
kama rasilimali katika kuwaletea wananchi maendeleo katika hali endelevu. Kwa sasa wilaya
inavyo viwanja 6325 vilivyochorwa na 3015 vilivyopimwa na kugawiwa kwa waombaji. Na pia
halmshauri imefanikiwa kuandaa na kutoa jumla hati 500 kwa wamiliki wa ardhi mjini. Kwa
upande wa umilikishaji ardhi vijini, Halmashuri imefanikiwa kupima jumla ya vijiji 140, na jumla
ya vijiji 8 vimeshaandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi. Kwa upande wa upimaji Upimaji wa
mashamba ya Wananchi, Jujla ya mashamba 267 yamepimwa na hati 194 kuandaliwa. Pamoja na
mafanikio hayo Halmashauri imekuwa na changamoto zifuatzo: uchache wa wataalamu (upimaji na
utoaji miliki ardhi) na ulipaji wa fidia hasa fidia ya ardhi na mazao ni kubwa.
3.3.5.1 Sekta ya Maliasili
Sera ya Taifa ya Misitu ya mwaka 1998 ilalenga kuhakikisha jamii inatambua na kushiriki
kikamilifu katika uhifadhi na utumiaji wa rasilimali za misitu kwa maendeleo endelevu kwa vizazi
vilivyopo na vijavyo. Wilaya ya Tandahimba ina aina mbalimbali ya maliasili pamoja na vivutio
vya kitalii hii ni pamoja na mazao ya misitu, wanyama pori, samaki na nyuki na aina mbalimbali za
madini. Hata hivyo bado vivuito mbalimbali vya kitalii havijaendelezwa. Wilaya ya ina hifadhi ya
misitu ya ukubwa wa heka 149,320.8 Mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na jumla ya vijiji 10
kushiriki katika mpango wa uhifadhi wa misitu ya jamii yenye jumla ya ukubwa wa eneo hekta
149,310.8. Wilaya pia imekuwa ilipanda miti 500,000 kwa mwaka.
Kwa upande wa uzalishaji wa mazao ya nyuki, mazao hayo yanazalishwa kwa kiwango kidogo
katika wilaya. Hata hivyo wilaya imefanikiwa luongeza vikundi vya ufugaji nyuki na kufikia 20.
Wilaya pia imekuwa ikifanya doria dhidi ya wanyama wakali na waharibifu wa mazao. Hata hivyo
wilaya inakabiliwa na uchache wa wataalam na ushirikiano mdogo toka kwa jamii kuhusu uhifadhi
wa misitu.
Katika kipindi hiki cha mpango Halmashauri pamoja na mambo mengine inatarajia kuongeza idadi
ya viwanja vilivyopimwa pamoja kutoa hati miliki kwa wamiliki wa viwanja hivyo na kuongeza
makusanyo ya kodi ya ardhi. Wilaya pia inalenga kutambua mitaa 300 kwa majina na kuongeza
ajira za watumishi.
3.3.6 KITENGO CHA MANUNUZI (PMU)
Halmshauri za wilaya kwa kuzingati Sheria ya fedha Na 9 ya mwaka 1982 ya serikali za mitaa
zina mamlaka kamili ya kupanga matumizi yanayotokana na mapato mbalimbali ya fedha.
Halmashauri katika kutoa hudua kwa jamii matumizi makubwa yanahusu manunuzi ya namna
14
moja au nyingine. Ili kazi za manunuzi ziweze kufanyika kwa ufanisi Kitengo Cha Manunuzi
kimeanzishwa Lengo ni kuona kwamba taratibu na sheria za manunuzi zinazingatiwa wakati wa
utoaji huduma kwa jamii.
Kitengo cha Manunuzi ( Procurement Management Unit – PMU) katika Halmashauri kina jukumu
kubwa la kutoa huduma zinazo husu manunuzi ya aina zote. Pia kitengo hiki kinatoa ushauri
kwa Mkurugenzi Mtendaji juu kuzingatia sheria na taratibu za manunuzi ili kuepuka matatizo
ambayo yanaweza kutokea endapo taratibu na sheria zitakuwa zimekiukwa.
Aidha Kitengo cha Manunuzi kinawajibika na uandaaji taratibu za manunuzi kwa kuhakikisha
kwamba nyaraka zote muhimu kwa kabala ya kufanya manunuzi zinadaliwa . Mara nyingi ni
lazima kushindanisha wafanyabishara au makampuni,wakandarasi kwa kufuata taratibu baada ya
hapo mapendekezo hutolewa na watakao shinda basi manunuzi hufanyika kutoka kwao.
Ili kuona kwamba manunuzi yanafanyika kwa uwazi matangazo ya zabuni yanatolewa kwa
uwazi kwa kubandikwa kwenye mbao za matangazo na hata kwenye magazeti ili kupata ushindani
wa kutosha. Na pia ipo Bodi ya Zabuni ambapo Kataibu wake ni Mkuu wa Kitengo cha
Manunuzi. Bodi ya Zabuni moja ya majukumu yake ni kupitia na kuona kwamba taratibu za
manunuzi zinazingatiwa katika Halmashauri ya wilaya. Aidha kitengo cha Manunuzi
kinawajibika kuandaa taarifa ya mwenendo wa manunuzi kila robo mwaka.
Katika kipindi hiki cha Mpango, Kitengo kinalengo kufanya mambo yafuatayo:
• Kutangaza zabuni mara moja kila mwaka, kwa kuzingatia Mpango wa manunuzi na kwa
kufuata tender documents zinazopendekezwa na PPRA na kuweka uwazi katika shughuli za
manunuzi kwa kutangaza fursa za zabuni katika vyombo vya habari ( magazeti na mbao za
matangazo) kila mwaka.
• Pia Kitengo kinatarajia kupata thamani ya fedha kwa huduma zitolewazo na wazabuni na kutoa
mafunzo kwa wajumbe wa bodi ya zabuni juu ya sheria ya manunuzi ya 2011 na kanuni zake.
Kitengo pia kitaandaa mpango wa bajeti ya kitengo cha manunuzi ili kiweze kutekeleza
malengo yake kwa ufanisi mkubwa ifikapo mwezi Februari kila mwaka nk.
3.3.7 KITENGO CHA SHERIA
kitengo hiki kinajishughulisha na mambo au majukumu mtambuka ambayo ni:- Kuishauri
Halmashauri ya Wilaya juu ya mambo yote ya kisheria. Kitengo pia kinahusika kuandaa rasimu za
Sheria Ndogo mbalimbali na kuziwasilisha kwenye vikao vya Halmashauri na baadaye
kuziwasilisha OWM-TAMISEMI kwa ajili ya kuidhinishwa na Waziri mwenye dhamana.
15
Kitengo pia kina wajibu wa kusimamia utendaji wa kila siku wa Mabaraza ya Kata na Mabaraza ya
Ardhi ya vijiji. Lengo jingine ni kuandaa mikataba ya Halmashauri na kuishauri Halmashauri juu
ya mikataba mbalimbali. Na pia Kitengo kinahusika kuendesha mashauri mepesi Mahakamani au
katika mabaraza na kufanya tafiti juu ya mambo ya sheria na kuishauri Halmashauri. Katika kipindi
hiki cha mpango kitengo kinatarajia kuufanya pamoja na mambo mengine haya yafuatayo:
Kufanya uchambuzi wa sheria ndogo kutoka vijijini na kupitisha kwenye vikao vya Kamati
husika, kufanya vikao vya pamoja na serikali za vijiji ili kuahinisha sheria ndogo na kutoa
mafunzo kwa wajumbe wa h/za vijiji kuhusu namna ya kuandasheria ndogo.
Kitengo pia kitaandaa sheria ndogo za H/wilya na kuziwasilisha kwa waziri mwenye dhamana ya
serikali za mitaa ( TAMISEMI).
3.3.8 KITENGO CHA UKAGUZI WA NDANI
Madhumuni ya kuwa na Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani katika Halmashauri ni kuhakikisha
uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na Taratibu zilizowekwa juu ya rasilimali za Halmashauri
zinazingatiwa. Lengo kuu likiwa ni kumshauri Mkurugenzi Mtendaji Wilaya juu ya uzingatiaji
sheria, kanuni na taratibu zilizokubalika katika usimamizi na matumizi ya rasilimali za
Halmashauri.
Baadhi ya Majukumu ya kitengo cha ukaguzi wa ndani ni kama ifuatavyo:
• Kuandaa mpangokazi wa mwaka wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani kwa kushirikiana na
Mkurugenzi Mtendaji Wilaya na kisha kupelekwa nakala kwa Mdhibiti na sMkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali (CAG), Waziri mwenye dhamana na Serikali za Mitaa na kwa Mkuu wa
Mkoa kabla ya tarehe 15 Julai kila mwaka.
• Kuandaa mpangokazi wa kitengo cha ukaguzi wa ndani utakaozingatia vihatarishi katika zoezi
la ukaguzi (Annual Risk Based Internal Audit Plan) na kuuwakilisha katika kamati ya ukaguzi
na nakala kupewa Mkurugenzi Mtendaji Wilaya kwa ajili ya kuidhinisha.
• Kujiridhisha uzingatiaji wa sheria, kanuni na taratibu katika uandaaji wa hesabu na usimamizi
wa fedha za Halmashauri kwa kufanya yafuatayo;-
• Kuhakiki na kuripoti juu ya ufanisi na uhalisia wa taarifa za fedha na rasilimali zinazotumika
katika kuandaa taarifa za hesabu na ripoti za utekelezaji.
Pamoja na mafanikio katika utekelezaji wa majukumu yake, Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
kinakabiliwa na changamoto mbalimbali, baadhi ya changamoto hizo ni kama ifuatavyo:
16
� Muda wa kutoa na kutuma taarifa za ukaguzi; Memoranda ya Fedha za Serikali za Msitaa ya
mwaka 2010 inamtaka Mkaguzi wa Ndani kutoa taarifa ndani ya siku kumi na tano (15) baada
ya robo mwaka kuisha na pia inamtaka Mkurugenzi Mtendaji (W) kutuma taarifa ndani ya siku
za kazi kumi na tano (15) (working days) kwenda kwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali
(CAG), Katibu Mkuu TAMISEMI na Katibu Tawala Mkoa (RAS). Muda uliowekwa hautoi
fursa;-
� Muda uliowekwa hautoi fursa kwa Menejimenti kutoa majibu ya hoja za ukaguzi kwenda kwa
Mkaguzi wa Ndani vilevile hautoi furssa kwa Mkaguzi wa ndani kuyahakiki majibu ya
Menejimenti na kutoa ripoti ya mwisho (final report).
� Muda uliowekwa hautoi fursa ya taarifa kuingizwa katika vikao vya kamati ya ukaguzi, timu ya
wakuu wa idara (CMT) na kamati ya fedha, mipango na uchumi (FUM).
� Idadi ndogo ya watumishi; Kitengo kwa sasa kina wakaguzi wa ndani wawili (2) tu wakati
ikama inataka kuwe na wakaguzi watatu (3). Hivyo kuna upungufu wa Mkaguzi mmoja (1).
� Kitengo kukosa gari kwa ajili ya shughuli za ukaguzi na kulazimika kuomba magari kutoka
idara mbalimbali za Halmashauri. Hali hii imesababisha wakati mwingine Kitengo kushindwa
kutekeleza majukumu yake kwa wakati hasa pale inapotokea magari yote ya idara yanatumiwa
na idara husika na
� Wakaguzi wa Ndani kukosa mafunzo juu ya utumiaji wa taarifa za fedha zilizo katika mfumo
wa kielekroniki (EPICOR System) na kusababisha ukaguzi wa taarifa zilizo ndani ya mfumo
wa kielekroniki kutofanyika.
Katika kipindi hiki cha mpango, kitengo kinalenga kutelelza yafuatayo:
• Kufanya ukaguzi wa hesabu na kutoa ripoti ya ukaguzi pamoja na kufanya ukaguzi wa miradi
ya maendeleo na kutoa ripoti ya ukaguzi kila robo mwaka.
• Kitengo pia kinalenga kufanya ukaguzi wa rasilimali za Halmshauri na kutoa ripoti ya ukaguzi
kila robo mwaka, kuboresha mazingira ya kufanyia kazi na kuendeleza mapambano dhidi ya
Ukimwi.
• Pia kitengo kinatarjia kuongeza idadi ya wakaguzi wa ndani na kufikia watatu (3) ifikapo
mwaka wa fedha 2015/2016 na kuwajengea uwezo watumishi wawili (2) kwa kiwango cha
taaluma katika kiwango cha CPA.
17
4.0 Dira na Dhima
Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imeundwa na Sheria ya Mbunge ya Serikali za Mitaa
namba .7 ya mwaka 1982 na kama ilivyofanyiwa marekebisho namba 6 ya mwaka 1999. Sheria hii
ndiyo inayoipa Halmshauri Madaraka na mamlaka ya utendaji na kuwepo kwake. Kwa hiyo
utengenezaji wa Dira na Dhima umezingatia madaraka hayo muhimu kama yanavyoainisha katika
sheria.
Kwa kuzingatia, uwezo, changamoto, fursa na vikwazo katika utoaji huduma, Wakuu wa idara na
vitengo walifanya mapitio ya Dira na Dhima Halmshauri ya Wilaya ya Tandahimba (2004-2009)
na kubuni Dira na Dhima mpya kama ifuatavyo: -
Dira: –“ Ifikapo 2018 Halmashauri Ya Wilaya Ya Tandahimba, Kwa Kutumia Rasilimali
Zilizopo, Utalaamu Na Ushirikishwaji Wa Jamii, Iwe Imetoa Huduma Bora Na
Kujenga Uchumi Endelevu Utakaowezesha Maisha Bora Ya Wananchi’’
Dhima: Kutumia Rasilimali Na Fursa Zilizopo Ili Kuimarisha Huduma Za Kijamii, Kiuchumi,
Na Kuboresha Maisha Na Utawala Bora Kupitia Ushirikishwaji Wa Jamii
4.1 Maeneo ya matokeo Muhimu, Malengo mahsusi na Viashiria
Maeneo ya matokeo Muhimu, ni yake ambayo wadau katika Halmashauri wana haki ya kutarajia
matokeo kutoka Halmashauri ya Serikali yao ya Wilaya. Na haya ni maeneo ambayo Halmashauri
inatakiwa kuyapa kipaumbele kuyatekeleza. Maeneo ya matokeo muhimu, Malengo mahsusi na
Viashiria ni kama yalivyoainisha katika warsha ya Wadau. Maeneo ya matokeo muhimu, Malengo
mahsusi na Viashiria vimeonyeshwa kwenye viambatisho.
18
4.2 Mikakati na Muda wa Utekelezaji
Muda wa Mpango huu Mkakati ni miaka mitano kuanzia mwaka 2014 mpaka 2018. Mikakati
iliyoainishwa kwenye Mpango huu inalenga kila idara husika katika Halmashauri.Wakati wa
kubuni mikakati hii, lika lengo mahsusi, wakuu wa Idara wamehakikisha kwamba, mikakati hii
inafanyisha utelelezaji wa malengo yote mahsusi katika kila idara au sekta. Kwa hiyo kila lengo
mahsusi limevunjwavujwa kwenye mikakati midogomidogo kwa kurahisisha utekelezaji wake.
Mikakati ya kila Idara/sekta imeonyeshwa kwenye Viambatisho.
4.3 Makisio ya Gharama za Utekelezaji wa Mpango
Bajeti ya Jumla inayohitaji kutekeleza Mpango Mkakati ni shilingi 178,376,938,436. Mahitaji ya
kila idara yameonyeshwa kwenye jedwali lifuatalo hapo chini. Hata hivyo ni muhimu kuelewa
kuwa bajet hii ya makisio itapitiwa tena katika vikao vingine vya Halmashauri ili kubainishi
mahitaji halisi ya kila mwaka.
Jedwali 5: Masikio ya Mpango Mkakati (2014-2018)
ENEO LA HUDUMA
2014 2015 2016 2017 2018 Jumla % ya Jumla
Afya 3,923,224,936 3,964,500,500 4,839,870,600 5,826,000,300 696,650,100 19,250,246,436 10.8
Elimu 1,171,000,000 2,473,700,000 2,313,200,000 2,328,200,000 8,286,100,000 4.6
Elimu ya Sekondari
5,917,430,000 5,131,330,000 5,496,230,000 5,536,330,000 22,081,320,000 5,917,430,000 24.8
Ardhi 423,000,000 395,600,000 375,600,000 375,600,000 375,100,000 1,952,400,000 1.1
Kilimo, Umwagiliaji na ushirika
14,305,856,000 14,305,856,000 14,305,856,000 14,305,856,000 14,305,856,000 71,529,280,000 40.1
Mifugo 135,050,000 487,650,000 689,550,000 318,200,000 100,950,000 1,695,200,000 1.0
Maji 4,506,676,767 4,507,908,892 3,288,079,917 2,368,418,250 2,359,968,250 15,238,200,000 9.5
Ujezi na Barabara
1,020,720,000 2,074,500,000 2,211,300,000 2,400,250,000 2,575,700,000 10,402,260,000 5.8
Fedha 69,200,000 232,500,000 112,000,000 109,000,000 105,000,000 627,700,000 0.4
Biashara 123,720,000 123,720,000 123,720,000 123,720,000 123,720,000 618,600,000 0.3
Uumishi na Utawala
27,000,000 30,100,000 30,100,000 31,100,000 32,100,000 149,700,000 0.1
Mipango 59,000,000 48,500,000 208,000,000 186,000,000 184,000,000 685,500,000 0.4
Misitu na Mazingira
40,200,000 52,000,000 62,000,000 58,200,000 42,000,000 235,200,000 0.1
Kitengo cha Nyuki
24,500,000 29,000,000 29,000,000 34,000,000 24,000,000 134,500,000 0.1
Wanyapori 28,000,000 31,000,000 25,000,000 25,000,000 25,000,000 107,000,000 0.1
Kitengo cha Kitengo cha sheria
75,860,000 95,310,000 79,560,000 56,560,000 80,160,000 379,250,000 0.2
Kitengo cha Ugavi na Manunuzi
11,000,000 130,000,000 60,000,000 30,000,000 65,000,000 296,000,000 0.2
Kitengo cha Ukaguzi wa
24,900,000 30,600,000 37,900,000 42,500,000 46,800,000 182,700,000 0.1
19
ndani Maendeleo ya Jamii
127,500,000 215,000,000 119,500,000 110,300,000 109,300,000 688,100,000 0.4
Jumla Kuu 30,731,077,703 32,800,165,392 34,389,506,517 34,121,174,550 102,692,288,350 178,376,938,436
100.0%
Makisio ya bajeti kwa kila eneo la huduma yanaonyesha kuwa pesa nyingi zitahitaji ili kutekeleza
malengo na mikakati iliyoainishwa katika mpango huu. Kwa mantini hiyo, Mpango huu utaweza
tu kutekeleza kama Wilaya itaimarisha ukusaji wa mapato ya ndani. Hii ni pamoja na Halmashuari
kubuni vyanzo vingine vya mapato. Kwa upande mwingine Mpango huu utafanikiwa kama Serikali
Kuu pamoja na Wafadhili wataendelea kusaidia na kutoa fedha kwa ajili ya shughuli za
Halmashauri. Kulingana na mchanganuo hapo juu sehemu kubwa ya bajeti ya Mpango huu
itatumika kwa shughuli za kilimo, umwagiliaji na ushirika (40.1%), elimu (Msingi na
Sekondari)(29.4%), afya (10.8%) na maji(9.5%). Makisio ya bajeti kwa kila idara, ni kama
imeonyeshwa kwenye kiambatisho/jedwali namba moja(1). Utaratibu wa kisekta umetumika ili
kumpa msomaji urahisi wa kuelewa malengo, mikakati ya utekelezaji naa makisio ya bajeti ya kila
idara.
5. Sababu muhimu zitakazo saidia katika utekelezaji wa Dira na Dima ya Halmashauri –
Viwezeshi na vikwamishi
Utekelezaji wa mpango huu unategemea baadhi ya sababu muhimu. Sababu hizi kwa upande
mmmoja zinaweza zikawa voiwezeshe au vikwamishi. Hata hivyo nyingi ya sababu hizo ni za
kiuccumi, kijamii, , za kisera, za kifedha na nyinginezo.
5.1. Sababu za Kifedha
Imeonekana kwamba uwezo wa Halmashauri kutekeleza mpango huu kutoka vyanzo vyake
yenyewe ni modgo. Kwa mantiki hiyo basi Halmashauri haina budi kubuni vyanzo vingine vya
mapato, na wakati huohuo serikali kuongeza ruzuku. Hii ina maana pia kwamba ni muhimu kwa
wananchi kutekeleza baadhi ya majukumu kutokana na fursa walizo nazo na kwa upande mwingine
jumuiya ya wafadhili kusaidia juhudi za wananchi katika kujiletea maendeleo.
5.2. Rasilimali Watu
Kitu kingine muhimu kinachohitajika katika ufanishaji wa mpango huu ni upatikanaji wa rasilimali
watu. Kwa mantini hiyo, ufanisi katika utekelezaji wa mpango utafikiwa tu kama rasilimali watu
iliyopo inaujuzi wa kutosha, uzoezu na moyo wa kujituma. Hata hivyo ikama ya Halmashauri
imeonyesha kuwa kuna upungufu mkubwa kwa baadhi ya idara. Kwa hiyo wilaya haina budi
20
kuajiri wafanyakazi wengi zaidi pamoja na kubuni mpango wa kufanya wanaoajiriwa wasiondoke
kwa mfano kuwapa posho ya mazingira magumu.
5.3. Utawala bora
Utawala bora ni muhimu kwa mafanikio ya mpango huu pia. Hii inajumuisha mambo yote
yaliyohusu uwazi, demokrasia pamoja na utawala wa sheria katika uendeshaji wa shule za kila siku
za Halmashauri. Kama mambo hayo hayatakuwepo ushiriki wa wananchi katika shughuli za
kujiletea maendeleo utakuwa mgumu. Kwa maana hiyo basi ni muhimu kuwa kila kipengele cha
utawala bora kinatekelezwa ili halmshauri iweze kufanikiwa kutekeleza malengo na mikakati
iliyoaninshwa katika mpango huu. Ni muhimu pia kuzingatia pia kwamba vikao vyote vya kisheria
vya Halmashauri vinafanyika kama inavyotakiwa ili kuwapa wananchi nafasi ya kuchangia
maamuzi ya utekelezaji.
5.4. Ushirikishwaji wananchi
Maudhui ya mpango wa mkakati katika serikali za mitaa nchini ni kuzifanya Halmashauri kutoa
huduma bora kwa wananchi. Hii ni pamoja na kuwapa wananchi pamoja na wadau wengine nafasi
ya kushiriki katika kupanga na kutekeleza mipango ya maendeleo katika serikali yao. Kufikia lengo
hilo ni muhimu basi kuhakikisha wananchi wanapata nafasi ya kushirika maamuzi katika hatua
mbalimbali za mchakato wa kupanga shughuli mbalimbali za maendeleo yao. Ushirikishaji wa
wananchi utawapa nafasi ya kutoa mawazo yao na kumiliki mchakato mzima wa mpango wa
kujiendeleza. Lakini pia utasaidia katika kuleta hali ya maelewano kati ya Halmshauri na wananchi.
Katika hili pia ni muhimu kuhakikisha mambo yote muhimu yaliyoibuliwa na wadau yanaingizwa
na kupewa nafasi inayostahili katika mpango huu mkakati.
5.5. Mambo ya Jinsia
Kwa upande mwingine, mafanikio ya mpango huu pia yanategemea ni kwa jinsi gani na kwa
kiwango gani mambo yanayohusu jinsia katika jamii yanapata nafasi katika mpango huu. Kwa hiyo
ni muhimu kuhakikisha wakati wote kuwa jinsia zote zinapata nafasi katika kupanga, kutekeleza
na kutathimini miradi na programu zote za maendeleo.Hayo yanaeweza kufikiwa kwa kuzingatia
baadhi ya mambo yafuatayo.:
• Kubuni miradi itakayopunguzia wanawake mzigo katika jamii.
• Kubuni na kutumia teknologia zinazopunguza muda wa kazi, kwa mfano uvunaji wa maji
ya mvua, zana rahisi za usafiri na kubebea mizigo na kadhalika.
• Kuwapa wanawake nafasi ya kumiliki rasilimali, kutoa taarifa zinahohusu haki ya
wanawake pamoja na kuwafundisha juu ya haki ya mama na mtoto.
21
• Kutengeneza mazingira yatakayotoa nafasi kwa wanawake kushiriki katika mambo ya
uongozi na siasa.
22
6. VIAMBATISHO/ MPANGO WENYEWE LENGO MAHSUSI, VIASHIRIA, CHANZO CHA UHAKIKI NA DHA NA
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA MAJI
LENGO KUU: Kuboresha huduma ya maji vijijini kwa kujenga miundo mbinu mipya, kukarabati ile ya zamani na kujenga uwezo wa jamii kusimamia na kuendesha miradi ya maji kwa kutumia vyombo vyao vya kisheria.
NA ENEO LA MATOKEO
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA CHANJO CHA UHAKIKI DHANA
1 Jumuiya za watumia maji
Kuongeza jumuiya za watumia maji kutoka 12 hadi 62 ifikapo 2018
Jumuiya za watumia maji zilizoundwa
Kuzitembelea Jumuiya 50 Taarifa za utekelezaji
Kuwepo kwa fedha Jamii kutohiyari Kubadilika kwa sera ya nchi
Kujenga uwezo wa jumuiya za watumia maji juu ya umiliki na usimamizi wa miradi ya maji kutoka 5 hadi 50 ifikapo 2018
Jumuiya za watumia maji zilizojengewa uwezo
Taarifa ya utekelezaji Kuwepo kwa fedha Kubadilika sera
2 Miundombinu ya Maji
Kukarabati miradi ya maji11 ifikapo 2018
Miradi ya maji itakayokarabatiwa.
Taarifa ya utekelezaji
Kupatikana fedha na utayari wa jamii kupokea mradi
Kupanua njia ya bomba kwenda vijiji 2 ifikapo 2018
Miradi iliyopanuliwa Taarifa ya utekelezaji Kutembelea mradi
Kupatikana fedha Utayari wa jamii kupokea mradi
Kukarabati visima ndoo vinavyofanya kazi kutoka 12 hadi 27 ifikapo 2018
Visima ndoo Vilivyokarabatiwa
Taarifa ya utekelezaji Kutembelea mradi
Kupatikana fedha Utayari wa jamii kupokea mradi Kutafuta vyanzo vya maji
katika vijiji 25 ambavyo havina kabisa huduma ya maji ifikapo 2018
Idadi ya vyanzo vya maji vilivyopatikana
Taarifa ya utekelezaji Kutembelea mradi
Kupatikana fedha Kupata wazabuni wenye uzoefu Uendelevu wa Kujenga miradi mipya 22 ya Idadi ya miradi mipya Taarifa ya utekelezaji Kupatikana fedha
23
NA ENEO LA MATOKEO
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA CHANJO CHA UHAKIKI DHANA
3 Miradi na vyanzo vya maji
maji. ifikapo 2018 ya maji iliyojengwa Kutembelea mradi
Utayari wa jamii jamii kupokea mradi
Kutunza vyanzo na miradi ya maji katika vijiji 55 ifikapo 2018
Idadi ya miradi iliyotunzwa na inayofanya kazi
Taarifa ya utekelezaji Kutembelea mradi
Kupatikana fedha Utayari wa jamii kupokea mradi
4 Mazingira ya vyanzo vya maji
Kuanzisha sheria ndogo ya vijiji ya kuhifadhi na kutunza mazingira ya vyanzo vya maji katika vijiji 50 ifikapo 2018
Vyanzo vya maji vilivyohifadhiwa na kutunzwa
Taarifa ya utekelezaji Kutembelea mradi
Kupatikana fedha Utayari wa jamii kupokea mradi
5 Usafi na Usalama wa
Kuimarisha Usalama na Usafi wa maji
Upatikanaji wa maji salama na safi
Taarifa ya Utekelezaji
Upatikanaji wa fedha
6 Kujenga uwezo Kuajiri watumishi 8 wapya na kutoa mafunzo kwa watumishi 9 ifikapo 2018
Idadi ya watumishi watakaoajiriwa
Taarifa ya uttumishi Upatikanaji wa fedha Utayari wa watumishi kuajiriwa Tandahimba
7 Mazingira ya kazi
Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi, kujenga ofisi, karakana na kununua vifaa vya ofisi na vitendea kazi ifikapi 2018.
Ofisi iliyokamilika kujengwa Idadi ya vifaa na vitendea kazi vitakavyonunuliwa
Taarifa mbalimbali Kutembelea karakana na ofisi
Kuwepo na fedha
8 Mamlaka ya Maji
Kuanzisha Mamlaka ya maji ifikapo 2018
Kuwepo Mamlaka ya maji
Taarifa za utekelezaji Upatikanaji wa fedha na utayari wa jamii kuanzisha mfuko
9 VVU/Ukimwi
Kuendeleza mapambano ya ukimwi na virusi dhidi ya maambukizi mapya
Jumuiya za watumia maji zilizopewa mafunzo ya VVU/UKIMWI
Taarifa ya Uhamasishaji na mafunzo
Upatikanaji wa fedha Kutokubadilika kwa sera ya taifa ya maji na usafi wa mazingira
10 Utawala Bora Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa
Kupungua kwa malalamiko kwa wateja
Taarifa ya Dawati la malalamiko Uwepo wa fedha Uihiari wa watumishi
24
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: MAJI
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
LENGO 1 Kuongeza jumuiya za watumia maji kutoka 12 hadi 62 ifikapo 2018
Kuunda jumuiya za watumia maji 50 DWE/ DWST/DED
LENGO 2 Kujenga uwezo wa jumuiya za watumia maji juu ya umiliki na usimamizi wa miradi ya maji 50 ifikapo 2018
Kutoa mafunzo ya uendeshaji wa jumuiya za watumia maji 50
DWE/ DWST
LENGO 3 Kukarabati miradi ya maji 11 ifikapo 2018
Kutafuta fedha za kukarabati miradi DWE/ DWST/DED
Kutangaza na kupata wakandarasi wa kukarabati miradi
DWE/ DWST/PO/DE
D
Kujenga miradi na kukabidhi kwa jumuiya DWE/DWST WAKANDARA
SI
LENGO 4 Kutafuta vyanzo vya maji kwa ajili ya vijiji vyote ambavyo havijapata maji ifikapo 2018
Kutangaza na kupata wakandarasi wa kujenga vyanzo
DWE/ DWST / DED
25
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kutoa elimu kwa jamii za vijiji 50 vitakavyojengewa
DWE/ DWST / DED
Kujenga na kukamilisha vyanzo vya maji DWE/DWST
LENGO 5 Kupanua njia ya bomba kwenda vijiji 2 ifikapo 2018
Kutangaza na kupata mzabuni wa kupanua mradi
DWE/ DED/DWST/P
O
Kujenga na kukabidhi mradi DWE/DED/DWST
LENGO 6 Kukarabati visima ndoo vinavyofanya kazi kutoka 12 hadi 27 ifikapo 2018
Kutangaza kupata wakandarasi na kujenga miradi ya maji
DED/DWE/ WAKANDARA
SI
LENGO 7 Kujenga miradi mipya 22 ya maji ifikapo 2018
Kufanya usanifu, kutangaza na kupata wazabuni wa kujenga mradi
DWE/DWST/ PO
MSHAURI
Kujenga mradi na kukabidhi kwa jamii DWE/DED/DWST/
LENGO 8 Kutunza vyanzo na miradi ya maji katika vijiji 55 ifikapo 2018
Kuunda na kutoa mafunzo ya uendeshaji kwa kamati za watumia maji
DWE/DED/DWST
26
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kuanzisha mfuko wa maji wa wilaya DWE/DED/DWST/MOW/
LENGO 9 Kuanzisha sheria ndogo ya vijiji ya kuhifadhi na kutunza mazingira ya vyanzo vya maji katika vijiji 50 ifikapo 2018
Kutafuta fedha za kutunga sheria DWE/DED/DWST
Kutunga sheria za kuhifadhi na kutunza mazingira ya vyamzo vya maji
DWE/DED/DWST
LENGO 10 Kuimarisha Usalama na Usafi wa maji ifikapo 2018
Kuchukua sampuli za maji 3720 kwa ajili ya kutafiti hali ya maji ya Kifizikia, Kikemikali na Kibaolojia
DWE/DED/DWST
/BWO
LENGO 11 Kuajiri watumishi 8 wapya na kutoa mafunzo kwa watumishi 9 ifikapo 2018 Kutafuta fedha za kutoa mafunzo DWE/DED/DH
RO
Kutoa mafunzo ya ajira mpya kwa watumishi 9
DWE/DED/DHRO/
LENGO 12 Kuanzisha Mamlaka ya maji ya wilaya ifikapo 2018
Kutafuta fedha za kuanzisha Mamlaka ya Maji Tandahimba
DWE/DED/DHRO
Kuanzisha Mamlaka ya maji Tandahimba DWE/DED/DWST
LENGO 13 Kukamilisha ujenzi wa ofisi ya maji, ujenzi wa karakana, ununuzi wa vifaa vya ofisi na vitendea kazi ifikapi 2018.
27
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kutafuta fedha za kukamilisha ofisi, kujenga karakana na kununua vifaa vya ofisi na vitendea kazi
DWE/DED/PO/ WAZABUNI
LENGO 14 Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa ifikapo 2018
Kutoa elimu kuhusu athari za rushwa kijamii na kiuchumi
DWE/DED/DHRO/PCCB
LENGO 15 Kuendeleza mapambano ya ukimwi na virusi dhidi ya maambukizi mapya
Kutoa elimu na mafunzo jinsi ya kupambana na maambukizi mapya ya VVU/UKIMWI
DWE/DED/DMO/
DHO/DHRO
28
LENGO MAHSUSI, VIASHIRIA, CHANZO CHA UHAKIKI NA DHA NA
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA MAJI
LENGO KUU: Kuboresha huduma ya maji vijijini kwa kujenga miundo mbinu mipya, kukarabati ile ya zamani na kujenga uwezo wa jamii kusimamia na kuendesha miradi ya maji kwa kutumia vyombo vyao vya kisheria.
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA X 1,000,000 TSHS 2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO
CHA PESA LENGO 1 Kuongeza jumuiya za watumia maji kutoka 12 hadi 62 ifikapo 2018
Kuunda jumuiya za watumia maji 50
3,465,000 3,465,000 3,465,000 3,465,000 3,465,000 17,325,000 TDC, DP, MOW
LENGO 2 Kujenga uwezo wa jumuiya za watumia maji juu ya umiliki na usimamizi wa miradi ya maji 50 ifikapo 2018
Kutoa mafunzo ya uendeshaji wa jumuiya za watumia maji 50
4,331,250 4,331,250 4,331,250 4,331,250 17,325,000 TDC, DP, MOW
LENGO 3 Kukarabati miradi ya maji 11 ifikapo 2018
Kukarabati miradi 11 na kukabidhi kwa Jamii
916,666,667 916,666,667 916,666,667 2,750,000,000 TDC, DP, MOW
LENGO 4 Kutafuta vyanzo vya maji kwa ajili ya vijiji vyote ambavyo havijapata maji ifikapo 2018
Kutangaza na kupata wakandarasi
6,000,000 6,000,000 6,000,000 6,000,000 6,000,000 30,000,000 TDC, DP, MOW
Kutoa elimu kwa jamii za vijiji 50 vitakavyojengewa miradi ya maji
5,400,000 5,400,000 5,400,000 5,400,000 5,400,000 27,000,000 TDC, DP, MOW
Kujenga na kukamilisha vyanzo vya maji
390,000,000 390,000,000 390,000,000 390,000,000 390,000,000 1,950,000,000 TDC, DP, MOW
29
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA X 1,000,000 TSHS 2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO
CHA PESA LENGO 5 Kupanua njia ya bomba kwenda vijiji 2 ifikapo 2018
Kutangaza kupata mzabuni, kujenga mradi na kukabidhi
300,000,000 300,000,000 600.000,000 TDC, DP, MOW
LENGO 6 Kuongeza idadi ya visima ndoo vinavyofanya kazi kutoka 12 hadi 27 ifikapo 2018
Kutangaza kupata wakandarasi, Kujenga na kukabidhi miradi ya maji
5,000,000 5,000,000 5,000,000 15,000,000 TDC, DP, MOW
LENGO 7 Kujenga miradi mipya 22 ya maji ifikapo 2018
Kufanya tathmini na usanifu (Mshauri) Kutangaza na kupata wazabuni wa kujenga na kujenga miradi
1,860,000,000 1,860,000,000 1,860,000,000 1,860,000,000 1,860,000,000 9,300,000,000 TDC, DP, MOW
LENGO 8 Kutunza vyanzo na miradi ya maji katika vijiji 5 5 ifikapo 2018
Kufuatilia utendaji wao kamati za maji na kufanya 1tathmini
1,440,000 1,440,000 1,440,000 1,440,000 1,440,000 7,200,000 TDC, DP, MOW
Kuanzisha mfuko wa maji wlaya
3,450,000 3,450,000 6.900,000 TDC, DP, MOW
LENGO 9 Kuanzisha sheria ndogo ya vijiji ya kuhifadhi na kutunza mazingira ya vyanzo vya maji katika vijiji 50 ifikapo 2018
Kutunga sheria za kulinda na kutunza vyanzo vya maji
2,990,000 2,990,000 5,990,000 TDC, DP, MOW
LENGO 10 Kuimarisha Usalama na Usafi wa maji ifikapo 2018
Kuchukua sampuli za 16,400,000 16,400,000 16,400,000 16,400,000 16,400,000 82,000,000 TDC, DP,
30
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA X 1,000,000 TSHS 2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO
CHA PESA maji 3720 kwa ajili ya kutafiti hali ya maji ya Kifizikia, Kikemikali, na Kibaolojia
MOW
LENGO 11 Kuajiri watumishi 8 wapya na kutoa mafunzo kwa watumishi 9 ifikapo 2018
Kuwaendeleza kitaaluma watumishi
1,440,000 1,440,000 1,440,000 1,440,000 1,440,000 72,000,000 TDC, DP, MOW
LENGO 12 Kukamilisha ujenzi wa ofisi ya maji, ujenzi wa karakana, ununuzi wa vifaa vya ofisi na vitendea kazi ifikapi 2018.
Kununua vifaa/vitendea kazi vya ofisi
41,536,000 41,536,000 41,536,000 41,536,000 41,536,000 207,680,000
TDC, DP, MOW
LENGO 13 Kuanzisha Mamlaka ya maji ya wilaya ifikapo 2018
Kuanzisha mamlaka ya maji Tandahimba
29,956,000 29,956,000 29,956,000 29,956,000 29,956,000 149,780,000
TDC, DP, MOW
JUMLA
4,506,676,767 4,507,908,892 3,288,079,917 2,368,418,250 2,359,968,250 15,238,200,000
31
LENGO MAHSUSI, VIASHIRIA, CHANZO CHA UHAKIKI NA DHA NA IDARA YA KILIMO, UMWAGILIAJI NA USHIRIKA ENEO LA HUDUMA: KILIMO LENGO KUU: Kuhakikisha upatikanaji wa chakula kuanzia ngazi ya kaya na kuboresha kiwango cha lishe na maisha ya jamii nzima ya Tandahimba NA ENEO LA
MATOKEO LENGO MAHSUSI VIASHIRIA CHANJO CHA UHAKIKI DHANA
1 Huduma za ugani
Kuongezeka kwa idadi ya wakulima wanaopata mafunzo ya kilimo bora kutoka wakulima 106,000 mwaka 2013
Idadi ya wakulima waliopata mafunzo kupitia mashamba darasa
Taarifa za mwezi, robo na mwaka kutoka ngazi ya vijiji na kata Taarifa ya Halmsahauri
Mahudhurio hafifu ya wakulima katika maeneo ya mafunzo Upatikani wa fedha
Kusogeza elimu ya maarifa kwa wakulima kutoka 3 hadi 7 ifikapo mwaka 2018
Idadi ya vituo vya maarifa
Kutembelea vituo Taarifa za utekelezaji na kuptia LGMD2
Serikali kukosa pesa za kujengea vituo vya maarifa ya jamii 2 Kuongeza
thamani ya mazao
Kuongezeka kwa thamani ya mazao kwa 25% ifikapo 2018
Idadi ya vikundi vya usindikaji mazao korosho, muhogo na mbegu za mafuta
Taarifa za mwezi, robo na mwaka kutoka ngazi ya vijiji na kata
Kukosa fedha za kununulia vitendea kazi
3
Uhifadhi wa mazao /mavuno
Kupunguza uharibifu mazao baada ya kuvunwa kutoka 40% hadi 10% ifikapo mwaka 2018
Idadi ya maghala ya kuhifadhia nafaka
Taarifa za mwezi, robo na mwaka kutoka ngazi ya vijiji na kata Taarifa za za wilaya kupitia LGMD2
Kukosa pesa za kuendeshea mafunzo
4 Utunzaji maji na udongo ( Soil and water conservation)
Kuboresha uhifadhi wa maji na udongo katika vijiji 50 ifikapo mwaka 2018
Kuongezeka kwa maeneo/vijiji yaliyohifadhiwa kwa maji na udongo
Idadi ya vijiji vinavyotekeleza miradi
Utayari wa wanchi
5 Zana bora za kilimo
Kuongeza matumizi ya zana bora za kilimo kutoka 5% hadi 30% ifikapo mwaka 2018
Kiasi cha ongezeko Taarifa za utekelezaji Uwezo kwa wakulima, Upatikanaji wa mikopo
32
NA ENEO LA MATOKEO
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA CHANJO CHA UHAKIKI DHANA
6 Mbegu bora Kuongeza matumizi ya mbegu bora kutoka 10% hadi 50% mwaka 2018
Kiasi cha ongezeko Taarifa za Halmashauri kupita LGMD2
Utayari wa wakulima kuzalisha mbegu
7 Hali ya lishe Kuongeza matumizi ya lishe bora kutoka 20% hadi 40% ifikapo 2018
Kiasi cha ongezeko Kuwepo kwa afisa kilimo lishe Serikali kukosa pesa ya kuajiri
Afisa kilimo lishe kuajiriwa
Taarifa za hali ya lishe Serikali kukosa pesa za kuendesha mafunzo
8 Maendeleo ya Umwagiliaji
Kuongeza eneo la umwagiliji toka ekari 506 hadi 2500 ifikapo 2018
Ongezeko luzalishaji wa mpunga katika mabonde ya Litehu, Lipalwe na Ng’apa.
Taarifa za uzalishaji kupitia LGMD2
Utayari wa wakulima katika kuchangia miradi, uongozi wa kamati za miradi kuwa imara 9 Mazao ya
biashara Kuongezeka kwa uzalishaji wa zao la ufuta kutoka tani 256 hadi tani 457 mwaka 2018
Kuongezeka kwa eneo linalolimwa zao la ufuta
Taarifa za mwezi, robo, mwaka kuptia LGMD2
Utayari wa wakulima kulima zaom la ufuta
Kuongezeka kwa uzalishaji wa zao la korosho kutoka tani 34,000 hadi tani 55,000 mwaka 2018
Kiasi cha tani zilizozalishwa
Taarifa ya mwaka Mabadiliko ya hali ya hewa kutokana na mabadiliko ya tabia nchi
Kuongeza mazao ya mbeguza mafuta - Alizeti Ifikapo 2018
Uwepo wa mazao mapya ya biashara
Taarifa za uzalisahaji kuptia LGMD2
utayari wa wakulia
10 Mazao ya chakula
Kuongezeka kwa uzalishaji wa muhogo kutoka tani 105 hadi 160,000 ifikapo 2018
Kiasi cha tani zilizozalishwa
Taarifa za mwaka kupitia LGMD2
kuongezeka kwa magonjwa ya mihogo
Kuongezeka kwa Uzalishaji wa karanga kutoka tani 3,129 hadi tani 6500 ifikapo 2018
Eneo linalolimwa, Uzalishaji wa karanga,
Taarifa za mwezi, robo, mwaka kuptia LGMD2
Utayari wa wakulima
33
NA ENEO LA MATOKEO
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA CHANJO CHA UHAKIKI DHANA
11 Mazingira ya kazi
Kuboresha na kuimarisha mazingira ya kufanyia kazi
Idadi ya nyumba za maafisa ugani katika ngazi ya kata
Taarifa za mwezi, robo, mwaka kuptia LGMD2
Uwezo wa serikali kujenga nyumba za watumishi
34
LENGO MAHSUSI, VIASHIRIA, CHANZO CHA UHAKIKI NA DHA NA
B: ENEO LA HUDUMA : MAENDELEO YA USHIRIKA
1.0 LENGO KUU : Kuhakikisha kwamba makundi ya watu maskini katika jamii yanakuwa na chombo cha kuaminika cha kuwawezesha kufikia malengo yao ya kiuchumi na kijamii.
1
Vyama vya kuweka na kukopa (SACCOS)
Kuongezeka kwa SACCOS kutoka 5 mwaka 2013 hadi 20 mwaka 2018
Idadi ya SACCOS Rejista ya SACCOS Utayari wa wanachama
Kuimarisha vyama vya kuweka na kukopa
Kuongezesha kwa wanachama
Rejista ya wanachama Kukosekana kwa fedha za kutolea elimu ya ushirika
Kujenga uwezo Kuimarisha vyama vya ushirika Idadi ya wanachama waliopata mafunzo
Taarifa za ushirika Kukosekana kwa fedha za kutolea elimu ya ukimwi
35
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: KILIMO
Lengo Kuu: : Kuhakikisha upatikanaji wa chakula kuanzia ngazi ya kaya na kuboresha kiwango cha lishe na maisha ya jamii nzima ya Tandahimba
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 1 Kuongezeka kwa idadi ya wakulima wanaopata huduma za ugani kutoka wakulima 106,000 mwaka hadi 176,000 ifikapo mwaka 2018
Mkakati: 1 kufufua na kuanzisha mashamba darasa.
DED/DAICO/DIDF/AGHA KHAN FOUNDATION
Mkakati: 2kuajiri watumishi 10 kila mwaka TAMISEMI/DED/DHRO/DAICO
Lengo 2 Kusogeza elimu ya maarifa kwa wakulima kutoka 3 hadi 8 ifikapo mwaka 2018
Mkakati: 1 kujenga kituo 1 cha maarifa kwa wakulima kila mwaka
DED/DAICO/DE
Lengo 3 Kupunguza uharibifu mazao baada ya kuvunwa kutoka 40% hadi 10% ifikapo mwaka 2018
Mkakati 1: kutoa elimu ya uhifadhi wa mazao baada ya mavuno.
DAICO/NARI
Mkakati: 2 kuhamasisha sekta binasi kufungua maduka ya pembejeo
DAICO/DTO
Mkakati 3: Kutolewa kwa elimu juu ya ujenzi maghala rahisi ya kutunzia nafaka.
36
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 4 Kuongeza thamani ya mazao kwa 25% ifikapo 2018
Mkakati :1 kufundisha vikudi 30 namna ya usindikaji wa zao la muhogo
DED/DAICO/OWECO
Mkakati:2 .Kujengea uwezo wa namna ya usindikaji wa korosho vikundi 30
DED/DAICO/ OWECO
Mkakati:3 . Kujenga viwanda 3 vya kubangua korosho vya kati (medium scale factories) ifikapo mwaka 2017
AMCOSS/Benki (TIB)
Mkakati:4 .Kuwajengea uwezo vikundi 5 vya usindikaji wa zao la ufuta ili kutengeneza mafuta.
DED/DAICO/ MIVARF
Mkakati:5 .Kuvijengea vikundi 2 vya Lipalwe na Mchichira/Ng’apa uwezo wa usindikaji wa zao la mpunga
DED/DAICO/SIDO
Mkakati : 6. Kujengea uwezo vikundi 5 katika usindikaji wa alizeti ili kutengeneza mafuta
DED/DAICO/SIDO
Mkakati :7 kuongezausindikaji wa mazao kupitia vikundi kutoka vikundi 12 vya sasa hadi vikundi 37 vikundi 5 kila mwaka
Lengo:7. Kuboresha uhifadhi wa maji na udongo katika vijiji 50 ifikapo mwaka 2018
Mkakati:1 . Kutoa elimu juu ya uhifadhi wa vyanzo vya maji
DED/DWE/DEMO/NGOs
(MEPPO/TANGONET)
37
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
MKAKATI: 2 Kutoa elimu sehemu hatarishi za uharibifu wa udongo vjiji vya kando ya gema la Makonde ( makonde Escarpment)
DED/DWE/DAICO,DNREO,/NGOs/MEPPO/TANGONET
Lengo 8 DED/DAICO/TAMISEMI Kuongeza matumizi ya zana bora za kilimo kutoka 5% hadi 30% ifikapo mwaka 2018
Mkakati : kudhamini mikopo ya matrekta makubwa kwa wakulima 20
DED/DAICO/SUMA JKT, WAKULIMA
Lengo: 9 Kuongezeka kwa matumizi ya mbegu bora kutoka 10% hadi 50% ifikapo mwaka 2018
Mkakati 1 .Kununua mbegu za msingi za mahindi,karanga na mpunga kwa kuzalishia mbegu za daraja la kuazimia. (QDS)
DED/DAICO
Lengo :10 DED/DNO/DHO/DPLO Kuongeza uelewa wa lishe katika kaya500 ifikapo 2018
Mkakati 1.Kuajiri afisa kilimo lishe ili kuboresha afya za watumiaji wa vyakula.
DED/DAICO/DHRO/BWANA AFYA
Mkakati: 2 Kufanya vikao vya tathmini ya hali ya lishe wilayani
Lengo 11 Kuongeza eneo la Umwagiliji toka ekari 506 hadi 2500 ifikapo 2018
Mkakati 1. Kuibua miradi ya umwagiliaji vijiji vya kata za Michenjele,Mkorea, Maundo,Mchichira na Litehu.
DED/DAICO/DWE
38
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Mkakati 2. Kuelimisha jamii na kamati za miradi juu ya kuchangia na utunzaji wa miradi ya umwagiliaji
DED/DAICO/DWE
Mkakati 3 kufundisha jamii katika maeneo ya miradi ya Ng’apa, Lipalwe na Litehu juu ya kilimo cha majaruba
DED/DAICO/AGHA KHAN FOUNDATION
Mkakati 4 Kuendeleza ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika vjiji 10 mwaka 2018.
DED/DWE/ZITSU/DIDF/DAICO
Lengo 12 Kuongezeka kwa uzalishaji wa zao la ufuta kutoka tani 256 hadi tani 457 ifikapo mwaka 2018
Mkakati 1. Kufanya kampeni kabambe juu ya ulimaji wa zao la ufuta kwa wakulima.
DED/DAICO
Lengo 13. Kuongezeka kwa uzalishaji wa zao la korosho kutoka tani 34,000 hadi tani 80,000 ifkapo mwaka 2018
Mkakati 2. Kufanya kampeni kabambe juu ya uzalishaji wa zao la korosho kwa wakulima
DED/DAICO
Mkakati 3. Uboreshaji wa mashamba ya mikorosho kwa kupanda mbegu bora.
DED/DAICO/Wakulima
Mkakati: 4. Mafunzo juu matumizi ya madawa ya korosho kwa maafisa ugani/wakulima
DED/DAICO /NARI/WAEOs/VAEOs
Mkakati 5: kuwezesha mchakato wa usambazaji pembejeo kwa kutumia mawakala
DC/DED/DAICO/WAKFU
39
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Mkakati: 6 kujenga uwezo wa vikundi vya kuzalisha miche bora ya mikorosho /kutoa vitwendea kazi
VIKUNDI VYA KUZALISHA MICHE/ DAICO/MEPPO
Lengo 14 Kuongezeka kwa uzalishaji wa muhogo kutoka tani 105 hadi 160,000 ifikapo ifikapo 2018
Mkakati : Kusambaza mbegu mbora za mihogo toka kituo cha utafiti Naliendele
NARI/DAICO
Lengo 15 Kuongezeka kwa uzalishaji wa karanga kutoka tani 3,129 mwaka 2013 hadi tani 6500 ifikapo 2018 Mkakati: kuzalisha mbegu bora za karanga
kutuia daraja la kuazimiwa (QDS) kutumia vikundi
DED/DAICO/Vikundi/
Lengo 16 Kuongezeka kwa uzalishaji wa zao la alizeti
Mkakati 1 Kujenga uwezo kwa vikundi vya kuzalisha alizeti
DED/DAICO
Lengo 17 Kuboresha na kuimarisha mazingira ya kazi
Mkakati: 1 kujenga nyumba za maafisa ugani DED/DE/DAICO
Mkakati:2 Kumalizia /kukarabati ofisi ya DAICO
Mkakati: 3 Kujenga shedi ya kutunzia zana za kilimo
Mkakati 4 Kununua vinakilishi, printer, photocoy
40
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Mkakati 5 : kuchimba kisima cha kutunzia maji eneo la ofisi ya DAICO
Mkakati 6: kununua pikipiki 47 ifikapo 2018
Mkakati kuweka mazingira kwa maafisa ugani kujiendeleza
DED/DHRO/DAICO
Lengo 18 Kuongezeka kwa SACCOS kutoka 5 mwaka 2013 hadi 20 mwaka 2018 Mkakati 1 kujenga uelewa juu ya umuhimu wa SACCOS
DED/OWECO/DCO
Mkakati 2 Kuongeza idadi ya wanachama 240 hadi 12000 mwaka 2018
DED/OWECO/DCO
Mkakati Kufundisha wanachama na wasiowanachama faida za ushirika.
Lengo 19 Kuimarisha vyama vya ushirika
Mkakati1: kufanya ukaguzi wa vyama vya kuweka na kukopa
DED/DAICO/DEMO/NGOs
Mkakati2: Kuelimisha wanachama juu ya sheria za ushirika
DED/DEMO/NGOs
Mkakati3: kufanya uchaguzi kwa kufuata sheria DED/DCO
Mkakati 4: Kuajiri afisa ushirika 2 ifikapo 2018
DED/DHRO
41
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: KILIMO
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA 2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO
CHA PESA
Lengo 1 Kuongezeka kwa idadi ya wakulima wanaopata huduma za ugani kutoka wakulima 106,000 mwaka hadi 176,000 ifikapo mwaka 2018
Mkakati 1: kufufua na kuanzisha mashamba darasa.
6,000,000.00 8,000,000.00 8,000,000.00 8,000,000.00 8,000,000.00 TDC, CG,WAKFU
Mkakati 2: kuajiri watumishi wa ugani 10 kila mwaka kwa miaka 5
� � �
� DED/DHRO/DAICO
Mkakakti 3: kujenga kituo 1 cha maarifa kwa wakulima kila mwaka
35,000,000 35,000,000 35,000,000 35,000,000 35,000,000 TDC,
Lengo 2 Kupunguza uharibifu mazao baada ya kuvunwa kutoka 40% hadi 10% ifikapo mwaka 2018 Mkakati 1: Kutoa elimu ya uhifadhi wa mazao baada ya mavuno
2,000,000 2,000,000 2,000,000 6,000,000.00 DED/DAICO
Mkakati2 Kuhamasisha sekta binasi kufungua maduka ya pembejeo
500,000.00 500,000.00 500,000.00 500,000.00 20,000,000.00 DED/DAICO
Mkakati 3 Kutolewa kwa elimu juu ya ujenzi maghala rahisi ya kutunzia nafaka.
500,000.00 500,000.00 500,000.00 500,000.00 20,000,000.00 DED/DAICO
Lengo 3 Kuongeza thamani ya mazao kwa 25% ifikapo 2018 Mkakati 1 kufundisha vikudi 30 namna ya usindikaji wa zao la muhogo
1,200,000 1,200,000 1,200,000 1,200,000 4,800,000.00 DED/DAICO/MIVARF
Mkakati 2 : Kujengea uwezo wa namna ya usindikaji wa korosho vikundi 30
800,000.00 800,000.00 800,000.00 800,000.00 3200,000.00 DED/DAICO/MIVARF
Mkakati 3: Kujenga viwanda 3 vya kubangua korosho vya kati (medium scale factories) ifikapo mwaka 2017
1,500,000,000.00
1,500,000,000.00
DED/MIVARF/
42
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA 2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO
CHA PESA
Mkakati 4: Kuwajengea uwezo vikundi 5 vya usindikaji wa zao la ufuta ili kutengeneza mafuta
5,000,000,00.00 5,000,000,00.00 5,000,000,00.00
5,000,000,00.00 20,000,000.00 DED/NARI/DAICO/SID
O
Mkakati 5: Kuvijengea vikundi 2 vya Lipalwe na Mchichira/Ng’apa uwezo wa usindikaji wa zao la mpunga
5,000,000,00.00 5,000,000,00.00 5,000,000,00.00
15,000,000.00 DED/DAICIO/AGHA/C
AN FOUNDATI
ON/ Mkakati 6: Kujengea uwezo vikundi 5 katika usindikaji wa alizeti ili kutengeneza mafuta
500,000.00 500,000.00 500,000.00 500,000.00 2,000,000.00 DED/DAICO
Mkakati 7: kuongezausindikaji wa mazao kupitia vikundi kutoka vikundi 12 vya sasa hadi vikundi 37 vikundi 5 kila mwaka
1,200,000.00 1,200,000.00 1200,000.00 1200,000.00 4,800,000.00 DED/DAICO
Lengo 4 Kuboresha uhifadhi wa maji na udongo katika vijiji 50 ifikapo mwaka 2018 Mkakati 1 1 Kutoa elimu juu ya uhifadhi wa vyanzo vya maji
600,000.00 600,000.00 600,000.00 1800,000.00 DED/DAICO
Mkakakti 2 : Kutoa elimu sehemu hatarishi za uharibifu wa udongo vjiji vya kando ya gema la Makonde ( makonde Escarpment
500,000.00 500,000.00 500,000.00 1,500,000.00 DED/DAICO
Mkakati 3: Kuongeza matumizi ya zana bora za kilimo kutoka 5% hadi 30% ifikapo ifikapo mwaka 2018
1 kudhamini mikopo ya matrekta makubwa kwa wakulima 20
Lengo 5 Kuongezeka kwa matumizi ya mbegu bora kutoka 10% hadi 50% ifikapo mwaka 2018
43
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA 2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO
CHA PESA
Mkakati 1 1Kununua mbegu za msingi za mahindi,karanga na mpunga kwa kuzalishia mbegu za daraja la kuazimia. (QDS)
5,000,000.00 5,000,000.00 10,000,000.00 DED/DAICO
Lengo 6 Kuongeza uelewa wa lishe katika kaya500 ifikapo 2018
Mkakati 1 :.Kuajiri afisa kilimo lishe ili kuboresha afya za watumiaji wa vyakula.
� � � � DED/DHRO/DAICO
Mkakati :2 Kufanya vikao vya tathmini ya hali ya lishe wilayani
1,200,000.00 1,200,000.00 1,200,000.00 3,600,000.00 DED/DAICO
Lengo 7 Kuongeza eneo la Umwagiliji toka ekari 506 hadi 2500 ifikapo 2018
Mkakati 1: kufundisha jamii katika maeneo ya miradi ya Ng’apa, Lipalwe na Litehu juu ya kilimo cha majaruba
2,500,000.00 2,500,000.00 2,500,000.00 2,500,000.00 10,000,000.00 DED/DIDF/ZITSU
Mkakati 2: Kuendeleza ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika vjiji 10 mwaka 2018
1,200.000.000.00
1,200.000.000.00
2,400,000,000.00
DED/DIDF
Lengo 8 Kuongezeka kwa uzalishaji wa zao la ufuta kutoka tani 256 hadi tani 457 ifikapo mwaka 2018
Mkakati 1 Kufanya kampeni kabambe juu ya ulimaji wa zao la ufuta kwa wakulima.
5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 20,000,000.00 DED/DAICO
Mkakati 2 : Kuwezesha wakulima kupata mbegu za ufuta
5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 20,000,000.00 DED/DAICO
Lengo 9 Ongezeko la zao la korosho kutoka tani 34,000 hadi 55,000 ifikapo 2018
44
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA 2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO
CHA PESA
Mkakati 1 Kufanya kampeni kabambe juu ya uzalishaji wa zao la korosho kwa wakulima
25,000,000.00 25,000,000.00 25,000,000.00
25,000,000.00 100,000,000.00 DED/DAICO
Mkakati 2: Uboreshaji wa mashamba ya mikorosho kwa kupanda mbegu bora.
2,000,000.00 2,000,000.00 2,000,000.00 2,000,000.00 8,000,000.00 DED/DAICO
M kakati 3: Mafunzo juu matumizi ya madawa ya korosho kwa maafisa ugani/wakulima
5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 20,000,000.00 DED/DAICO
Mkakati 4: kuwezesha mchakato wa usambazaji pembejeo kwa kutumia mawakala
5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 20,000,000.00 DED/DAICO
Mkakati 5: Kujenga uwezo wa vikundi vya kuzalisha miche bora ya mikorosho /kutoa vitendea kazi
10,000,000.00 10,000,000.00 10,000,000.00
10,000,000.00 40,000,000.00 DED/DAICO
Lengo 10 Kuongezeka kwa uzalishaji wa muhogo kutoka tani 105 hadi 160,000 ifikapo ifikapo 2018
Mkakati 1: Kusambaza mbegu mbora za mihogo toka kituo cha utafiti Naliendele
2,000,000.00 2,000,000.00 2,000,000.00 2,000,000.00 8,000,000.00 /DED/WAKFU/DAICO
Mkakati 2 kuzalisha mbegu bora za karanga kutuia daraja la kuazimiwa (QDS) kutumia vikundi
2,000,000.00 2,000,000.00 2,000,000.00 2,000,000.00 8,000,000.00 DED/DAICO
Lengo 11
Kuongezeka kwa uzalishaji wa zao la alizeti
Mkakati 1 Kuwezesha wakulima kulima alizeti
0 5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 15,000,000.00 DED/DAICO
Lengo 12
Kuboresha na kuimarisha mazingira ya kazi
Mkakati 1: kujenga nyumba za maafisa ugani
30,000,000.00 30,000,000.00
30,000,000.00 90,000,000.00 DED/DAICO
45
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA 2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO
CHA PESA
Mkakati 2 : Kumalizia /kukarabati ofisi ya DAICO
20,000,000.00 20,000,000.00 DED/DAICO
Mkakati 3: Kujenga shedi ya kutunzia zana za kilimo ofisi ya DAICO
25,000,000.00 25,000,000.00 DED/DAICO
Mkakati 4: Kununua vinakilishi, printer, photocoy
10,000,000.00 10,000,000.00 DED/DAICO
Mkakati 5: kuchimba kisima cha kutunzia maji eneo la ofisi ya DAICO
15,000,000.00 15,000,000.00 DED/DAICO
LENGO 13 Kuongezeka kwa SACCOS kutoka 5 mwaka 2013 hadi 20 mwaka 2018 Mkakati 1 Kuongeza idadi ya wanachama 240 hadi 12000 mwaka 2018
2,000,000.00 2,000,000.00 2,000,000.00 2,000,000.00 8,000,000.00 DED/DCO
MKAKATI 2 Kutoa elimu ya ushirika ili kuongeza idadi ya wanachama 240 hadi 12000 mwaka 2018
800,000.00 800,000.00 800,000.00 800,000.00 3,200,000.00 DED
Lengo 14 Kuimarisha vyama vya ushirika DED/
Mkakati:1 kufanya ukaguzi wa vyama vya kuweka na kukopa
2,500,000.00 2,500,000.00 3,000,000.00 3,000,000.00 10,000,000.00 DED
Mkakati2: Kuelimisha wanachama juu ya sheria za ushirika
3,000,000.00 3,000,000.00 4,000,000.00 4,000,000.00 14,000,000.00 DED
Mkakati 3: kufanya uchaguzi kwa kufuata sheria
3,000,000.00 3,000,000.00 4,000,000.00 4,000,000.00 14,000,000.00 DED
JUMLA 14,305,856,000 14,305,856,000 14,305,856,000
14,305,856,000 71,529,280,000
46
ENEO LA HUDUMA: MIFUGO
Lengo Kuu: Kuwa na ufugaji wa kisasa wenye mifugo bora yenye uzalishaji mzuri, inayofugwa kibiashara na yenye kuboresha lishe na
kuinua kipato cha mfugaji/jamii ifikapo 2018
Na Eneo la Matokeo
Lengo Mahususi Viashiria vya Utekelezaji Chanzo cha Uhakiki Dhana
1 Uzalishaji wa mifugo
Kuongezeka kwa uzito wa ng’ombe kutoka kilo 250 hadi 350 ifikapo mwaka 2016
Idadi ya kilo za nyama
Taarifa ya utekelezaji � Upatikanaji wa fedha � Utayari wa jamii � Milipuko ya magonjwa
Kuongezeka kwa uzalishaji wa maziwa kwa ng’ombe kwa mwaka kutoka lita 400 hadi 2000 ifikapo mwaka 2018
Idadi ya lita za maziwa yalio zllishwa
� Taarifa ya utekelezaji Kufuatilia kwa wafugaji
� Utayari wa jamii � Upatikanaji wa fedha � Milipuko ya magonjwa
Kuongezeka kwa uzalishaji wa mayai ya kuku kutoka 60 hadi 300 kwa mwaka ifikapo 2016
Idadi ya mayai, yaliyozalishwashwa
� Taarifa ya utekelezaji kupitia LGMD2
� Kufuatilia kwa wafugaji
� Utayari wa jamii � Upatikanaji wa fedha � Milipuko ya magonjwa
Kuongezeka kwa mbuzi walioboreshwa kutoka 217 – 3800 ifikapo 2018
Idadi ya mbuzi bora
� Taarifa kupitia LGMDG2
� Kuvitembelea vikundi
� Upatikanaji wa fedha � Milipuko ya magonjwa
Kuongezeka kwa ng’ombe wa maziwa kutoka 319 – 3600 ifikapo 2018
Idadi ya ng’ombe wa maziwa
� Taarifa za wataalam � Kufuatilia kwa
wafugaji � Taarifa kupitia
LGMD2
� Utayari wa jamii kufuga
� Ukame � Milipuko ya magonjwa � Uwepo wa fedha
2 Nyama safi
na salama Kuongeza upatikanaji wa nyama safi na salama kutoka 20% hadi 70% ifikapo 2017
Idadi ya machinjio bora Idadi ya mabucha bora
� Taarifa za wataalam wa mifugo
� Taarifa ya utekelezaji kupitia LGMD2
� Upatikanaji wa fedha (Wafadhili)
� Utayari wa jamii
3 Kujenga Uwezo
Kuongezeka kwa idadi ya wataalam wa mifugo kutoka 14 hadi 36 ifikapo 2015
Idadi ya wataalam wa Mifugo walioajiriwa
� Taarifa ya wataalam � Taarifa kupitia
LGMD2
� Utayari wa wizara � Upatikanaji wa fedha
47
Na Eneo la Matokeo
Lengo Mahususi
Viashiria vya Utekelezaji Chanzo cha Uhakiki Dhana
Kuwapatia wataalam 36 wa mifugo mafunzo rejea ifikapo 2017
Idadi ya wataalam waliopata mafunzo
� Vyeti vya kufuzu mafunzo
� Taarifa za watumishi
� Upatikanaji wa fedha
Kuongezeka kwa wataalam wa mifugo wenye Diploma ya Mifugo kutoka 9 hadi 14 ifikapo 2017
Idadi ya wataalam wa mifugo wenye shahada
� Taarifa ya idara � vyeti vya taaluma
� Upatikanaji wa fedha � Uwezo wa wizara
Kuongezeka kwa wataalam wa mifugo waliopata mafunzo ya uhamilishaji kutoka 2 hadi 14 ifikapo 2016
Idadi ya wataalam waliopata mafunzo
� Taarifa ya Mifugo � Vyeti vya kufuzu
mafunzo
� Upatikanaji wa fedha
Kuanzisha na kuimarisha vikundi 20 vya wafugaji vilivyopata mafunzo ya uhamilishaji na utambuzi wa ng’ombe walio kwenye joto na muda wa kuwapandisha ifikapo 2016
Idadi ya vikundi vilivyopata mafunzo
� Kuvitembelea vikundi
� Taarifa ya utekelezaji kupitia LGMDG2
� Upatikanaji wa fedha � Utayari wa wafugaji
4 Huduma za ugani
Kupunguza vifo vya mifugo kutokana na magonjwa kutoka 54% hadi 15% ifikapo 2018
Idadi ya mifugo iliyopata kinga/tiba
� Taarifa za wataalam wa mifugo
� Taarifa kupitia LGMD2
� Upatikanaji wa fedha � Utayari wa jamii
5 Mazingira ya kazi
Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa wataalam 37 wa Mifugo na Uvuvi ifikapo 2018
Ofisi ya Mifugo na uvuvi Idadi ya nyumba za wataalam wa kata wa Mifugo
� Taarifa ya DLFDO � Kuitembelea Ofisi
� Upatikanaji wa fedha
6 Vitendea kazi
Kuongeza ufanisi wa kazi kwa wataalam 37 wa Idara ya Mifugo na Uvuvi ifikapo 2017
Vifaa vya kufanyia kazi vilivyonunuliwa
� Taarifa ya DLFDO
� Upatikanaji wa fedha
7 Miundo Mbinu
Kukamilisha ujenzi wa kituo 1 (Kliniki) cha afya cha mifugo ifikapo 2014
Idadi ya vituo vya afya ya mifugo vilivyojengwa
� Kutembelea kituo kilichojengwa
� Taarifa kupitia LGMD2
� Upatikanaji wa fedha
Kuongezeka kwa malambo ya maji kutoka 3 hadi 5 ifikapo 2018
Idadi ya malambo ya maji � Kutembelea malambo ya maji
� Taarifa ya utekelezaji
� Upatikanaji wa fedha
48
Na Eneo la Matokeo
Lengo Mahususi
Viashiria vya Utekelezaji Chanzo cha Uhakiki Dhana
Kuongezeka kwa machijio kutoka 2 hadi 7 ifikapo 2015
Idadi ya machinjio � Taarifa za wataalam � LGMD2
� Upatikanaji wa fedha
8 HIV/ UKIMWI
Kuendeleza mapanbano dhidi ya maambukizo mapya ya virus vya UKIMWI na UKIMWI kwenye makundi maalum 10 ifikapo 2018
Idadi ya vikundi Kupungua kwa maambukiza ya HIV/UKIMWI
� Taarifa za vikundi � Taarifa kupitia
LGMD2 � Kutembelea vikundi
� Upatikanaji wa fedha
Kuboresha maisha kijamii na kiuchumi kwa makundi maalum 10 ifikapo 2017
Idadi ya vikundi vilivyoboreshwa
� Taarifa za utekelezaji kupitia mfumo wa LGMDG
� Upatikanaji wa fedha
9 Hifadhi ya Mazingira
Kuongezeka kwa vijiji vilivyotenga maeneo ya malisho kutoka 2 hadi 7 ifikapo 2018
Idadi ya vijiji vilivyotenga maeneo ya malisho
Taarifa za watendaji wa vijiji � Taarifa ya wataalam
wa ardhi � Kutembelea maeneo
� Upatikanaji wa fedha � Utayari wa jamii katika
kutenga maeneo
Kuanzishwa kwa vikundi vya wafugaji vitano (5) vinavyotumia nishati ya gesi (Bio-gas) kupikia ifikapo 2018
Idadi ya vikundi vilivyoanzishwa Idadi ya vikundi vyenye nishati
� Taarifa za wataalam � Kuvitembelea
vikundi � Taarifa ya utekelezaji
kupitia LGMD2
� Upatikanaji wa fedha � Mwitikio wa jamii
10 Utawala bora
Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa kwa watumishi 14 ndani ya idara ifikapo 2015
Kupungua kwa malalamiko ya wateja
� Taarifa ya dawati la malalamiko
� Upatikanaji wa fedha � Uhiari wa watumishi
49
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: MIFUGO
Lengo Kuu: Kuwa na ufugaji wa kisasa wenye mifugo bora yenye uzalishaji mzuri, inayofugwa kibiashara na yenye kuboresha lishe na
Kuinua kipato cha mfugaji/jamii.ifikapo 2018
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 1 Kuongezeka kwa uzito wa ng’ombe kutoka kilo 250 hadi 350 ifikapo mwaka 2016
Kuanzisha vikundi vya unenepeshaji wa ng’ombe wa asili
DED, DLFDO, DPLO
Kutoa mafunzo kwa wanavikundi 20 juu unenepeshaji na utunzaji wa ng’ombe
DED, DLFDO, DSMSs
Livestock, LFOs
Kuanzisha na kutoa mafunzo kwa vyama vya wafugaji na wafanya biashara ya Mifugo (Ng’ombe )
DED, DLFDO, DTO, DCO
Lengo 2 Kuongezeka kwa uzalishaji wa maziwa kwa ng’ombe kwa mwaka kutoka lita 400 hadi 2000 ifikapo mwaka 2018
Kuboresha kosaafu kwenye ng’ombe wa maziwa kwa njia ya uhamilishaji
DLFDO, DSMSs Livestock
Kutoa mafunzo kwa vikundi vya ufugaji ng’ombe wa maziwa juu ya ufugaji bora na wa kibiashara
DED, DLFDO, DSMS Livestock
50
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 3 Kuongezeka kwa uzalishaji wa mayai ya kuku kutoka 60 hadi 300 kwa mwaka ifikapo 2016
Kufufua/kuunda vikundi 45 vya ufugaji kuku wa asili na kukarabati mabanda 45 bora ya kuku
DLFDO, DSMSs Livestock
Kuboresha kosaafu kwenye kuku wa asili kwa kununua majogoo 200 ya kisasa
DED, DLFDO, DSMSs Livestock
Kuendesha mafunzo kwa wanavikundi juu ya teknolojia za ufugaji bora wa kuku
DLFDO, DSMS Livestock, LFOs
Lengo 4 Kuongezeka kwa mbuzi walioboreshwa kutoka 217 – 3800 ifikapo 2018
Kuendeleza vituo vya uboreshaji mbuzi wa asili kwa kununua mbuzi (madume/majike) bora
DED, DLFDO, DSMS Livestock
Kutoa mafunzo juu ya uboreshaji mbuzi wa asili na ufugaji bora kwenye vikundi
DLFDO, DSMS Livestock, LFOs
Lengo 5 Kuongezeka kwa ng’ombe wa maziwa kutoka 319 – 3600 ifikapo 2018
Kuendeleza mfumo wa kopa ng’ombe lipa ng’ombe kwa kuchangia kununua ng’ombe 105 wa maziwa na kusambaza kwenye vikundi
DED, DLFDO
51
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kutoa mafunzo kwenye vikundi cha ufugaji ng’ombe wa maziwa juu ya utunzaji na kanuni /masharti ya ufugaji ng’ombe wa maziwa
DLFDO, DSMS Livestock
Lengo 6 Kuongeza upatikanaji wa nyama safi na salama kutoka 20% hadi 70% ifikapo 2017
Kujenga machinjio ndogo 10 (slaughter slabs) katika vijiji vinavyochinja mifugo (ng’ombe, mbuzi, kondoo) kwa wingi
DED, DLFDO, DPLO
Kujenga mabucha 30 katika vijiji vinavyochinja mifugo ili kuwa na sehemu salama za kuuzia nyama
DED, DLFDO, DPLO
Kuhamasisha uundwaji wa vikundi vya tasnia ya nyama na kuvipatia mafunzo juu ya sheria ya nyama Na. 10 ya mwaka 2006, sheria ya magonjwa ya mifugo Na. 17 ya mwaka 2003 na sheria ya chakula na dawa (TFDA) Na. 1 ya mwaka 2003
DLFDO, DCDO
Lengo 7 Kuongezeka kwa idadi ya wataalam wa mifugo kutoka 14 hadi 36 ifikapo 2015
Kuajiri wataalam 22 wa taaluma ya Mifugo wenye ngazi mbalimbali
DED, DHRO, DLFDO
52
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 8 Kuwapatia wataalam 36 wa mifugo mafunzo rejea ifikapo 2017
Kuwawezesha wataalam 36 wa mifugo kwenda kozi fupi za mifugo ili kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia katika fani ya Mifugo
DED, DLFDO
Lengo 9 Kuongezeka kwa wataalam wa mifugo wenye Diploma ya Mifugo kutoka 9 hadi 14 ifikapo 2017
Kuwawezesha wataalam 6 walio na cheti kwenda vyuo vya mifugo kusoma masomo ya Diploma ya Mifugo
DED, DHNRO, DLFDO
Lengo 10 Kuongezeka kwa wataalam wa mifugo waliopata mafunzo ya uhamilishaji kutoka 2 hadi 14 ifikapo 2016
Kuwawezesha wataalam 12 kupata mafunzo ya uzalishaji wa ng’ombe kwa njia ya chupa NAIC – ARUSHA
DED, DLFDO
Kununua mbegu bora (semen) na vifaa vya kupandishia
Lengo 11 Kuanzisha na kuimarisha vikundi 20 vya wafugaji vilivyopata mafunzo ya uhamilishaji na utambuzi wa ng’ombe walio kwenye joto na muda wa kuwapandisha ifikapo 2016
53
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kutoa mafunzo ya upandishaji ng’ombe kwa njia ya chupa, kutambua dalili za ng’ombe aliye katika joto na muda wa kupandishwa katika vikundi 20 vinavyofuga ng’ombe wa maziwa
DLFDO, DSMS Livestock, LFOs
(outsource)
Lengo 12 Kupunguza vifo vya mifugo kutokana na magonjwa kutoka 54% hadi 15% ifikapo 2018
Kudhibiti na kutokomeza magonjwa ya mlipuko (homa ya mapafu ya ng’ombe (CBPP), homa ya mapafu ya mbuzi (CCPP), mdondo wa kuku (NCD), sotoka ya mbuzi (PPR), kichaa cha mbwa (Rabies))
DLFDO, DVO, DSMS Livestock
Ujenzi wa vituo (Kliniki) 2 vya uchunguzi magonjwa ya mifugo kimaabara
DED, DLFDO, DE
Kuanzisha vituo 4 vya ukaguzi wa mifugo na mazao yake
DED, DLFDO
Kujenga vituo 2 vya kukusanyia mifugo (Holding Grounds) inayoingia wilayani ili kuchunguza kama inamagonjwa kabla ya kusambaa ndani ya wilaya
DED, DLFDO, DVO, DPLO
54
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kutoa mafunzo kwa viongozi wa vijiji, wafugaji juu ya udhibiti wa magonjwa na sheria za magonjwa ya mifugo Na. 17 ya mwaka 2003
DLFDO, DVO
Lengo 13 Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa wataalam 37 wa Mifugo na Uvuvi ifikapo 2018
Ujenzi wa Ofisi ya Idara ya Mifugo na Uvuvi (W),
DED, DE, DLFDO, PO
Ujenzi wa nyumba 5 za wataalam wa mifugo wa kata
DED, DE, DLFDO, PO
Lengo 14 Kuongeza ufanisi wa kazi kwa wataalam 37 wa Idara ya Mifugo na Uvuvi ifikapo 2017
Ununuzi wa gari ya Idara ya Mifugo na Uvuvi
DED, DLFDO, PO
Kuwawezesha wataalam kufanya kazi kwa ufanisi kwa kuwapa vyombo vya usafiri (pikipiki 15)
DED, DLFDO, PO
Ununuzi wa samani za ofisi, Kompyuta (laptops 5), printa 1, photocopy machine 1, Scaner 1, power point 1
DED, DLFDO, PO
Lengo 15 Kukamilisha ujenzi wa kituo 1 (Kliniki) cha afya cha mifugo ifikapo 2014
Ukamilishaji wa ujenzi wa Kliniki ya mifugo
DED, DE, DLFDO, PO
55
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Ununuzi wa samani za kliniki ya Mifugo
DED, DLFDO, PO
Lengo 16 Kuongezeka kwa malambo ya maji kutoka 3 hadi 5 ifikapo 2018
Kuhakikisha kuwa maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo yanapatikana kwa kuchimba malambo 2
DED, DWE, DLFDO
Lengo 17 Kuongezeka kwa machijio kutoka 2 hadi 7 ifikapo 2015
Kuhakikisha kuwa ukaguzi wa nyama unafanyika kwa kuzingatia sheria kwa kujenga machinjio ndogo (Slaughter slabs) 5
Lengo 18 Kuendeleza mapanbano dhidi ya maambukizo mapya ya virus vya UKIMWI na UKIMWI kwenye makundi m aalum 10 ifikapo 2018
Kutoa mafunzo ya kujikinga na maambukizi ya HIV/UKIMWI kwenye makundi maalum 10
DSWO, DCO, DLFDO, DMO,
CHAC
Lengo 19 Kuboresha maisha kijamii na kiuchumi kwa makundi maalum 10 ifikapo 2017
Kuwaboresha kijamii na kiuchumi vikundi 2 vya watu wanaoishi na HIV/UKIMWI kwa kuwachangia ng’ombe wa maziwa
DED, DLFDO
56
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kuboresha maisha ya vikundi 3 vya walemavu wa ngozi kwa kuchangia ng’ombe wa maziwa
DED, DLFDO
Kuboresha maisha ya vikundi 5 vya walemavu wa viungo kwa kuwachangia kuku
DED, DLFDO
Kuwajengea uwezo vikundi 10 vya makundi maalum juu ya ufugaji wa kibiashara
DLFDO, DSWO
Lengo 20 Kuongezeka kwa vijiji vilivyotenga maeneo ya malisho kutoka 2 hadi 7 ifikapo 2018
Kupanga matumizi bora ya ardhi katika vijiji 5 vinavyofuga ng’ombe
DLNREO, DLFDO, DCDO
Lengo 21 Kuanzishwa kwa vikundi vya wafugaji vitano (5) vinavyotumia nishati ya gesi (Bio-gas) kupikia ifikapo 2018
Kuwawezesha wanavikundi katika vikundi 5 vya ufugaji wa ndani wa ng’ombe wa maziwa kutumia nishati ya Bio-gas
DED, DLFDO, DSMS Livestock
Kuwajengea uwezo wanavikundi vya ufugaji wa ng’ombe wa maziwa juu ya matumizi ya Bio-gas
DLFDO, DSMS Livestock
Lengo 22 Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa kwa watumishi 14 ndani ya idara ifikapo 2015
57
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kutoa elimu kuhusu athari za rushwa kijamii na kiuchumi
DED, PCCB, DLFDO
58
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: MIFUGO
Lengo Kuu: Kuwa na ufugaji wa kisasa wenye mifugo bora yenye uzalishaji mzuri, inayofugwa kibiashara na yenye kuboresha lishe na
Kuinua kipato cha mfugaji/jamii ifikapo 2018
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO CHA PESA
Lengo 1 Kuongezeka kwa uzito wa ng’ombe kutoka kilo 250 hadi 350 ifikapo mwaka 2016
Kuanzisha vikundi vya unenepeshaji wa ng’ombe wa asili
15,800,000 15,800,000 31,600,000 TDC, MLFD, Wafadhili
Kutoa mafunzo kwa wanavikundi 20 juu unenepeshaji na utunzaji wa ng’ombe
5,500,000 4,900,000 10,400,000 TDC, NGOs,Wafadhili
Kuanzisha na kutoa mafunzo kwa vyama vya wafugaji na wafanya biashara ya Mifugo (Ng’ombe )
4,600,000 2,000,000 6,600,000 TDC, Act!on Aid, Wafadhili
Lengo 2 Kuongezeka kwa uzalishaji wa maziwa kwa ng’ombe kwa mwaka kutoka lita 400 hadi 2000 ifikapo mwaka 2018
Kuboresha kosaafu kwenye ng’ombe wa maziwa kwa njia ya uhamilishaji
6,600,000 6,000,000 7,000,000 8,000,000 10,000,000 37,600,000 TDC, Wafadhili
Kutoa mafunzo kwa vikundi vya ufugaji ng’ombe wa maziwa juu ya ufugaji bora na wa kibiashara
3,000,000 2,000,000 3,900,000 8,900,000 TDC, Wafadhili, NGOs,
Development
59
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO CHA PESA
Partners (DP)
Lengo 3 Kuongezeka kwa uzalishaji wa mayai ya kuku kutoka 60 hadi 300 kwa mwaka ifikapo 2016
Kufufua/kuunda vikundi 45 vya ufugaji kuku wa asili na kukarabati mabanda 45 bora ya kuku
10,500,000 8,500,000 19,000,000 TDC, NGOs, CG, Wafadhili.
Kuboresha kosaafu kwenye kuku wa asili kwa kununua majogoo 200 ya kisasa
8,500,000 8,500,000 TDC, Wafadhili, DP, NGOs
Kuendesha mafunzo kwa wanavikundi juu ya teknolojia za ufugaji bora wa kuku
3,000,000 3,000,000 6,000,000 TDC, Wafadhili
Lengo 4 Kuongezeka kwa mbuzi walioboreshwa kutoka 217 – 3800 ifikapo 2018
Kuendeleza vituo vya uboreshaji mbuzi wa asili kwa kununua mbuzi (madume/majike) bora
3,900,000 6,800,000 6,000,000 6,000,000 22,700,000 TDC, Wafadhili
Kutoa mafunzo juu ya uboreshaji mbuzi wa asili na ufugaji bora kwenye vikundi
2,400,000 3,600,000 6,000,000 TDC, Wafadhili, NGOs
Lengo 5 Kuongezeka kwa ng’ombe wa maziwa kutoka 319 – 3600 ifikapo 2018
Kuendeleza mfumo wa kopa ng’ombe lipa ng’ombe kwa kuchangia kununua ng’ombe 105 wa maziwa na kusambaza kwenye vikundi
17,850,000 17,850,000 17,850,000 17,850,000 17,850,000 89,250,000 TDC, Wafadhili
60
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO CHA PESA
Kutoa mafunzo kwenye vikundi cha ufugaji ng’ombe wa maziwa juu ya utunzaji na kanuni /masharti ya ufugaji ng’ombe wa maziwa
2,500,000 3,500,000 3,500,000 4,500,000 5,500,000 19,500,000 TDC, Wafadhili
Lengo 6 Kuongeza upatikanaji wa nyama safi na salama kutoka 20% hadi 70% ifikapo 2017
Kujenga machinjio ndogo 10 (slaughter slabs) katika vijiji vinavyochinja mifugo (ng’ombe, mbuzi, kondoo) kwa wingi
25,000,000 15,000,000 10,000,000 50,000,000 TDC, Wafadhili
Kujenga mabucha 30 katika vijiji vinavyochinja mifugo ili kuwa na sehemu salama za kuuzia nyama
30,000,000 30,000,000 30,000,000 90,000,000 CG/Jamii, NGOs
Kuhamasisha uundwaji wa vikundi vya tasnia ya nyama na kuvipatia mafunzo juu ya sheria ya nyama Na. 10 ya mwaka 2006, sheria ya magonjwa ya mifugo Na. 17 ya mwaka 2003 na sheria ya chakula na dawa (TFDA) Na. 1 ya mwaka 2003
5,600,000 5,600,000 11,200,000 TDC, NGOs
Lengo 7 Kuongezeka kwa idadi ya wataalam wa mifugo kutoka 14 hadi 36 ifikapo 2015
Kuajiri wataalam 22 wa taaluma ya Mifugo wenye ngazi mbalimbali
28,200,000 29,200,000 30,200,000 35,200,000 40,200,000 163,000,000 TDC, Hazina
Lengo 8 Kuwapatia wataalam 36 wa mifugo mafunzo rejea ifikapo 2017
Kuwawezesha wataalam 36 wa 5,000,000 7,000,000 8,000,000 20,000,000 TDC, Wafadhili
61
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO CHA PESA
mifugo kwenda kozi fupi za mifugo ili kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia katika fani ya Mifugo
Lengo 9 Kuongezeka kwa wataalam wa mifugo wenye Diploma ya Mifugo kutoka 9 hadi 14 ifikapo 2017
Kuwawezesha wataalam 6 walio na cheti kwenda vyuo vya mifugo kusoma masomo ya Diploma ya Mifugo
5,500,000 6,500,000 7,500,000 19,500,000 TDC, MLFD
Lengo 10 Kuongezeka kwa wataalam wa mifugo waliopata mafunzo ya uhamilishaji kutoka 2 hadi 14 ifikapo 2016
Kuwawezesha wataalam 12 kupata mafunzo ya uzalishaji wa ng’ombe kwa njia ya chupa NAIC – ARUSHA
3,000,000 5,000,000 8,000,000 TDC, Wafadhili
Kununua mbegu bora (semen) na vifaa vya kupandishia
4,500,000 6,500,000 11,000,000 TDC, Wafadhili
Lengo 11 Kuanzisha na kuimarisha vikundi 20 vya wafugaji vilivyopata mafunzo ya uhamilishaji na utambuzi wa ng’ombe walio kwenye joto na muda wa kuwapandisha ifikapo 2016
Kutoa mafunzo ya upandishaji ng’ombe kwa njia ya chupa, kutambua dalili za ng’ombe aliye katika joto na muda wa kupandishwa katika vikundi 20 vinavyofuga ng’ombe wa maziwa.
6,800,000 6,800,000 TDC, Wafadhili, NGOs
62
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO CHA PESA
Lengo 12 Kupunguza vifo vya mifugo kutokana na magonjwa kutoka 54% hadi 15% ifikapo 2018
Kudhibiti na kutokomeza magonjwa ya mlipuko (homa ya mapafu ya ng’ombe (CBPP), homa ya mapafu ya mbuzi (CCPP), mdondo wa kuku (NCD), sotoka ya mbuzi (PPR), kichaa cha mbwa (Rabies))
15,000,000 10,000,000 12,000,000 14,000,000 16,000,000 67,000,000 TDC, MLFD, Wafadhili
Ujenzi wa vituo (Kliniki) 2 vya uchunguzi magonjwa ya mifugo kimaabara
45,000,000 50,000,000 95,000,000 TDC, Wafadhili
Kuanzisha vituo 4 vya ukaguzi wa mifugo na mazao yake
4,0000,000 6,500,000 10,500,000 TDC
Kujenga vituo 2 vya kukusanyia mifugo (Holding Grounds) inayoingia wilayani ili kuchunguza kama inamagonjwa kabla ya kusambaa ndani ya wilaya
15,000,000 15,000,000 TDC, Wafadhili
Kutoa mafunzo kwa viongozi wa vijiji, wafugaji juu ya udhibiti wa magonjwa na sheria za magonjwa ya mifugo Na. 17 ya mwaka 2003
3,400,000 2,300,000 5,600,000 TDC, NGOs
Lengo 13 Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa wataalam 37 wa Mifugo na Uvuvi ifikapo 2018
Ujenzi wa Ofisi ya Idara ya Mifugo na Uvuvi (W), na ununizi wa
85,000,000 85,000,000 TDC, Wafadhili
63
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO CHA PESA
samani
Ujenzi wa nyumba 5 za wataalam wa mifugo wa kata
60,000,000 70,000,000 70,000,000 200,000,000 TDC, Wafadhili
Lengo 14 Kuongeza ufanisi wa kazi kwa wataalam 37 wa Idara ya Mifugo na Uvuvi ifikapo 2017
Ununuzi wa Gari ya Idara ya Mifugo na Uvuvi
250,000,000 250,000,000 Wafadhili, TDC
Kuwawezesha wataalam kufanya kazi kwa ufanisi kwa kuwapa vyombo vya usafiri (pikipiki 15)
18,750,000 18,750,000 37,500,000 TDC, Wafadhili
Ununuzi wa samani za ofisi, Kompyuta (laptops 5), printa 1, photocopy machine 1, Scaner 1, power point 1
15,000,000 15,000,000 TDC, Wafadhili
Lengo 15 Kukamilisha ujenzi wa kituo 1 (Kliniki) cha afya cha mifugo ifikapo 2014
Ukamilishaji wa ujenzi wa Kliniki ya mifugo
47,000,000 47,000,000 TDC, Wafadhili
Ununuzi wa samani za kliniki ya Mifugo
11,000,000 11,000,000 TDC. Wafadhili
Lengo 16 Kuongezeka kwa malambo ya maji kutoka 3 hadi 5 ifikapo 2018
Kuhakikisha kuwa maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo yanapatikana kwa kuchimba malambo 2
45,000,000 45,000,000 90,000,000 TDC, Wafadhili
64
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO CHA PESA
Lengo 17 Kuongezeka kwa machijio kutoka 2 hadi 7 ifikapo 2015
Kuhakikisha kuwa ukaguzi wa nyama unafanyika kwa kuzingatia sheria kwa kujenga machinjio ndogo (Slaughter slabs) 5
30,000,000 30,000,000 TDC, Wafadhili
Lengo 18 Kuendeleza mapanbano dhidi ya maambukizo mapya ya virus vya UKIMWI na UKIMWI kwenye makundi maalum 10 ifikapo 2018
Kutoa mafunzo ya kujikinga na maambukizi ya HIV/UKIMWI kwenye makundi maalum 10
4,500,000 4,500,000 TDC, Wafadhili
Lengo 19 Kuboresha maisha kijamii na kiuchumi kwa makundi maalum 10 ifikapo 2017
Kuwaboresha kijamii na kiuchumi vikundi 2 vya watu wanaoishi na HIV/UKIMWI kwa kuwachangia ng’ombe wa maziwa
11,350,000 11,350,000 22,700,000 TDC, Wafadhili
Kuboresha maisha ya vikundi 3 vya walemavu wa ngozi kwa kuchangia ng’ombe wa maziwa
6,950,000 6,950,000 TDC, Wafadhili
Kuboresha maisha ya vikundi 5 vya walemavu wa viungo kwa kuwachangia kuku
8,000,000 9,000,000 17,000,000 TDC, wafadhili, NGOs
Kuwajengea uwezo vikundi 10 vya makundi maalum juu ya ufugaji wa kibiashara
5,500,000 5,500,000 TDC, Wafadhili, NGOs
65
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO CHA PESA
Lengo 20 Kuongezeka kwa vijiji vilivyotenga maeneo ya malisho kutoka 2 hadi 7 ifikapo 2018
Kupanga matumizi bora ya ardhi katika vijiji 5 vinavyofuga ng’ombe
4,500,000 6,900,000 11,300,000 TDC, Wafadhili
Lengo 21 Kuanzishwa kwa vikundi vya wafugaji vitano (5) vinavyotumia nishati ya gesi (Bio-gas) kupikia ifikapo 2018
Kuwawezesha wanavikundi katika vikundi 5 vya ufugaji wa ndani wa ng’ombe wa maziwa kutumia nishati ya Bio-gas
17,200,000 17,200,000 TDC, Wafadhili, Jamii
Kuwajengea uwezo wanavikundi vya ufugaji wa ng’ombe wa maziwa juu ya matumizi ya Bio-gas
3,400,000 3,400,000 TDC, Wafadhili, NGOs
Lengo 22 Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa kwa watumishi 14 ndani ya idara ifikapo 2015
Kutoa elimu kuhusu athari za rushwa kijamii na kiuchumi
2,500,000 2,500,000 TDC
JUMLA KUU 135,050,000 487,650,000 689,550,000 318,200,000 100,950,000 1,695,200,000
66
ENEO LA HUDUMA: UVUVI
Lengo Kuu: Hifadhi, uendelezaji na matumizi endelevu ya raslimali za bahari kwa manufaa ya vizazi vijavyo ifikapo 2018
Na Eneo la Matokeo
Lengo Mahususi
Viashiria vya Utekelezaji Chanzo cha Uhakiki Dhana
1 Uzalishaji wa samaki
Kuanzisha uzalishaji wa samaki kufikia tani 20 ifikapo 2016
Idadi ya tani za samaki � Taarifa za wataalam � Taarifa kupitia LGMD2
� Mwitikio wa wavuvi/jamii
� Uwepo wa fedha 2 HIV/
UKIMWI Kuendeleza mapambano ya maambukizi ya virus
vya UKIMWI na UKIMWI kwa vijiji 10 vilivyo kandokando ya mto Ruvuma ifikapo 2018
Idadi ya vijiji vilivyofikiwa � Taarifa ya mafunzo � Kuvitembelea vijiji
� Mwitikio wa jamii � Upatikanaji wa
fedha
67
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: UVUVI
Lengo Kuu: Hifadhi, uendelezaji na matumizi endelevu ya raslimali za bahari kwa manufaa ya vizazi vijavyo ifikapo 2018
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 1 Kuanzisha uzalishaji wa samaki kufikia tani 20 ifikapo 2016
Kuhamasisha wananchi katika vijiji 15 kuchimba mabwawa ya kufugia samaki
DLFDO, DFO, DSMS fisheries
Kuanzishwa kwa vikundi 5 vyenye nia thabiti ya kuanzisha ufugaji wa samaki
DLFDO, DFO, DSMS fisheries
Kununua vifaranga vya samaki na kuvisambaza kwenye vikundi
DED, DLFDO, DFO
Kutoa mafunzo kwa wanavikundi juu ya ufugaji bora wa samaki na sheria za uvuvi
DLFDO, DFO, DSMS fisheries
Lengo 2 Kuendeleza mapambano ya maambukizi ya virus vya UKIMWI na UKIMWI kwa vijiji 10 vilivyo k andokando ya mto Ruvuma ifikapo 2018
68
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kutoa mafunzo ya kujikinga na maambukizi ya HIV/UKIMWI kwenye vijiji10
69
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: UVUVI
Lengo Kuu: Hifadhi, uendelezaji na matumizi endelevu ya raslimali za bahari kwa manufaa ya vizazi vijavyo ifikapo 2018
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO CHA PESA
Lengo 1 Kuanzisha uzalishaji wa samaki kufikia tani 20 ifikapo 2016
Kuhamasisha wananchi katika vijiji 15 kuchimba mabwawa ya kufugia samaki
4,360,000 4,200,000 8,560,000 TDC, CG, Jamii
Kuanzishwa kwa vikundi 5 vyenye nia thabiti ya kuanzisha ufugaji wa samaki
3,700,000 2,450,000 5,150,000 TDC, DADPs, Wafadhili
Kununua vifaranga vya samaki na kuvisambaza kwenye vikundi
5,000,000 5,900,000 10,900,000 TDC, MLFD, Wafadhili
Kutoa mafunzo kwa wanavikundi juu ya ufugaji bora wa samaki na sheria za uvuvi
6,000,000 6,000,000 TDC, NGOs
Lengo 2 Kuendeleza mapambano ya maambukizi ya virus vya UKIMWI na UKIMWI kwa vijiji 10 vilivyo kandokando ya mto Ruvuma ifikapo 2018
Kutoa mafunzo ya kujikinga na maambukizi ya HIV/UKIMWI kwenye vijiji10
4,600,000 6,900,000 4,200,000 15,700,000 TDC, Wafadhili, NGOs
70
EENEO LA HUDUMA: ELIMU YA MSINGI
LENGO KUU: Ifikapo mwaka 2018, mazingira ya kufundishia na kujifunzia yawe yameboreshwa ili kutoa fursa ya kutoa elimu bora itakayoinua maisha ya jamii ili kuondoa umaskini.
SN ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
1. Uandikishaji wa wanafunzi
Kuongeza watoto wanaosajiliwa wenye umri wa kwenda shule kutoka 83% hadi 94% ya wanaoandikishwa ifikapo 2018
Usajili ufikie 94% ya uandikishaji - Madodoso ya TSM - Taarifa za mwezi, robo,
nusu na mwaka - Ufuatiliaji
Utayari wa jamii kushiriki kusimamia maendeleo ya elimu ya watoto wao
Kuongeza watoto wanaosajiliwa kutoka shule za awali kuingia darasa la I wenye umri wa kwenda shule kutoka 72% hadi 85% wanaandikishwa ifikapo 2018
Usajili ufikie 85% ya uandikishaji - Madodoso ya TSA - Taarifa za mwezi, robo,
nusu na mwaka - Ufuatiliaji
Utayari wa jamii kushiriki kusimamia maendeleo ya elimu ya watoto wao
Watoto wanaosajiliwa kuanza madarasa ya awali wanaongezeka kutoka 58% hadi 65% 1fikapo 2018
Usajili ufikie 65% ya uandikishaji - Madodoso ya TSA - Taarifa za mwezi, robo,
nusu na mwaka - Ufuatiliaji
Utayari wa jamii kushiriki kusimamia maendeleo ya elimu ya watoto wao
Kuongeza asilimia ya usajili kwenye shule za ufundi ukue kutoka 42% hadi 50% ifikapo 2018
Usajili ufikie 50% ya uandikishaji - Taarifa za mwezi, robo,
nusu na mwaka - Ufuatiliaji
Utayari wa jamii kushiriki kusimamia maendeleo ya elimu ya watoto wao
2
Mahudhurio na kudumu shuleni
Kupunguza au kuacha utoro shuleni � Kwenye shule za Awali kutoka 21%
hadi 6% na � Kwenye shule za msingi kutoka 18%
hadi 12% ifikapo 2018
� Utoro upungue hadi 6% kwa shule za awali na 12% kwa shule za msingi
- Madodoso ya TSM & TSA - Taarifa za mwezi, robo,
nusu na mwaka - Ufuatiliaji
Utayari wa jamii kushiriki kusimamia maendeleo ya elimu ya watoto wao
Kuongeza asilimia ya watoto wanaoanza darasa la I waendelee na masomo na kufanya mitihani � Darasa la IV kutoka 89% hadi 92% � Darasa la VII kutoka 68% hadi 75%
ifikapo 2018
� Ongezeko la wanaoendelea na masomo na kufanya mitihani ifikie 92% kwa darasa la IV na 75% kwa darasa la VII
- Madodoso ya TSM - Taarifa za mwezi, robo,
nusu na mwaka Ufuatiliaji
Utayari wa jamii kushiriki kusimamia maendeleo ya elimu ya watoto wao
3. Miundombinu (Infrastructure)
Kuongezwa kwa idadi ya majengo yanayojengwa shuleni ifikapo 2018
Kuongezeka majengo mapya yaliyojengwa
- Madodoso ya TSM & TSA - Taarifa za mwezi, robo,
� Jamii itashiriki kikamilifu kusimamia
71
SN ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
(a) Majengo � Madarasa ya awali kutoka 4 hadi 25 � Madarasa ya shule za msingi kutoka 771
hadi 820 � Nyumba za walimu kutoka 228 hadi240 Ukarabati wa majengo ufanywe ifikapo 2018 � Ukarabati wa nyumba 70 za walimu � Ukarabati wa madarasa 150 � Ujenzi wa matundu ya vyoo kwa ajili ya
wasichana ufikie matundu 1079 kutoka 380 na wavulana ufikie matundu 872 kutoka 371
� Kujenga/kukarabati matanki ya maji chini ya ardhi 50.
� Madarasa ya awali 25 � Madarasa ya msingi 820 � Nyumba za walimu 240 Kufanyika kwa ukarabati wa � Nyuma 70 � Madarasa 150 � vyoo kwa ajili ya wasichana
ufikie matundu 1079 na wavulana kufikia matundu 872.
� Idadi ya matanki yaliyojengwa/karabatiwa
nusu na mwaka - Ufuatiliaji
maendeleo ya elimu ya watoto wao
� Utayari wa jamii kuanzisha shirika la kusimamia ubora wa elimu kupitia makato ya mapato ya zao la korosho
(b) Samani Kuongezwa kwa idadi ya samani shuleni ifikapo 2018 � Madawati kwenye shule za awali kutoka
221 hadi 400 � Madawati kwenye shule za msingi
kutoka 18,264 hadi 22,000. � Meza za walimu 963 hadi 1200 kwa
shule za Msingi � Meza za walimu 18 hadi 100 kwa shule
za awali � Viti vya walimu 116 hadi 250 kwa shule
za Msingi � Viti vya walimu 22 hadi 100 kwa shule
za awali
Kuongezwa kwa samani mpya zilizotengenezwa � Madawati 400 ya shule za
awali � Madawati 3800 ya shule za
msingi � Meza 1300 � Viti 350
- Madodoso ya TSM & TSA - Taarifa za mwezi, robo,
nusu na mwaka - Ufuatiliaji
Utayari wa jamii kushiriki kusimamia maendeleo ya elimu ya watoto wao Utayari wa jamii kuanzisha shirika la kusimamia ubora wa elimu kupitia makato ya mapato ya zao la korosho
(c) Vifaa Vya kujifunzia na kufundishia
� Kuhakikisha uwiano wa vitabu vya kujifunzia unakuwa 1:1(UKM) ifikapo mwaka 2018
� Kuhakikisha vifaa vya kufundishia vinaongezeka kwa kila somo kwa uwiano wa shule kwa vifaa kufikia 1:13 kutoka 1:9
Kuongezeka kwa vitabu vya kujifunzia (kiada) UKM 1:1 na vifaa vya kufundishia kufikia 1:13
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
Utayari wa jamii kuanzisha shirika la kusimamia ubora wa elimu kupitia makato ya mapato ya zao la korosho
4. Ustawi wa Walimu Ifikapo mwaka 2018 � Kuongeza walimu sambamba na
kupungua kwa kustaafu na mengineyo
� Ongezeko la uwiano wa mwalimu kwa mwanafunzi lipungue hadi 1:45
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
Utayari wa jamii kuanzisha shirika la kusimamia ubora wa elimu
72
SN ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
ifikapo mwaka 2018 ifikie 1: 45 badala ya 1:65 ya sasa.
� Kuhakikisha walimu viongozi wapya wanapata mafunzo ya uongozi kozi 1 kwa mwaka.
� Kuhakikisha walimu wanapata mafunzo ya mada ngumu/tata, masomo 2 kwa mwaka
� Walimu 60 wapate fursa ya kulipiwa masomo ya kujiendeleza
� Kusomesha walimu 100 wa english, sayansi na hisabati kwa mkataba maalum
� Kusomesha walimu 75 ujuzi wa kutumia kompyuta.
� Idadi ya mafunzo ya uongozi na utawala wa Elimu kwa viongozi wa kata na shule kwa mwaka
� Idadi ya masomo ya mada ngumu yatakayofanyika kwa mwaka
� Idadi ya walimu watakaolipiwa masomo
� Idadi ya walimu watakaosomeshwa kwa mkataba
� Idadi ya walimu watakaosomeshwa ujuzi wa kompyuta.
- Ufuatiliaji kupitia makato ya mapato ya zao la korosho Utayari wa Serikali na Halmashauri kutenga bajeti ya kuendesha mafunzo ya uongozi, masomo tata.
5. Utamaduni na Michezo
Kuimarisha utamaduni na michezo ifikapo 2018 (a) Michezo � Kuongezeka usajili wa vilabu vya
mpira wa miguu kutoka 37 hadi 60 � Kuwapo kwa timu 1 ya wilaya ya
mpira wa miguu ya wanawake � Kuongeza kiwanja cha michezo chenye
uzio wa tofali kutoka 1 kilichopo hadi 2 chenye uwezo wa kuchukua michezo mingi
� Kuongeza idadi ya michezo mfano mpira wa kikapu, wavu, pete, mikono, riadha nk ikiwemo ya jadi (bao, kulenga shabaha nk) itakayoshindanishwa katika ngazi mbalimbali.
� Kuendesha ligi ya kombe la wilaya kwa vilabu 37 na timu za Tarafa kwa michezo mbalimbali.
� Kuendesha mafunzo kwa walimu wa michezo walao kila mchezo mara 1
� Idadi ya vilabu vilivyosajiliwa ifikie 60
� Kuanzishwa kwa timu 1 ya wilaya ya mpira wa miguu ya wasichana
� Kiwanja 1 cha michezo chenye uzio kitakachojengwa
� Idadi ya michezo ya kisasa na jadi iliyoongezeka
� Idadi ya timu zitakazoshiriki kwenye mashindano ya wilaya kwa ngazi vilabu na tarafa.
� Idadi ya walimu na aina ya michezo itakayotolewa mafunzo.
� Idadi na aina ya vifaa vitakavyosambazwa kwenye shule.
� Idadi ya vilabu vya michezo isiyopewa kipaumbele iliyoanzishwa
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
� Utayari wa wadau kuchangia maendeleo ya michezo wilayani
� Utayari wa wadau hasa shule za msingi na sekondari kujifunza michezo mbalimbali ikiwemo ya jadi
� Utayri wa Wadau kuanzisha vilabu vya michezo mbalimbali.
73
SN ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
kwa mwaka. � Kuhakikisha usambazaji wa vifaa vya
michezo hadi kufikia aina 3 (mirusho) kutoka aina 1 (mipira)
� Kuhamasisha uanzishaji wa vilabu 10 vya michezo isiyopewa kipaumbele
(b) Sanaa � Kuvitambua na kuvisajili vikundi vya
sanaa kutoka 9 vya sasa hadi 25 � Kusimamia na kuendesha maonesho ya
kazi mbalimbali za sanaa mara 1 kwa mwaka.
� Kusimamia na kuendesha matamasha ya kazi mbalimbali za sanaa mara 1 kwa mwaka.
� Kuwa na kituo 1 cha utamaduni, mila na desturi.
� Idadi ya vikundi vya sanaa vilivyotambuliwa na kusajiliwa
� Idadi ya sanaa za maonesho yaliyofanyika kwa mwaka.
� Idadi ya matamasha ya sanaa yaliyofanyika kwa mwaka
� Idadi ya kituo 1 cha utamaduni, mila na desturi.
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
� Utayri wa wadau kujenga kumbi za kisasa za burdani
� Utayari wa Jamii kushiriki
(c) Vivutio vya Asili � Kuimarisha maeneo yenye vivutio vya
asili.
Idadi ya maeneo yaliyopendekezwa kuwa na vivutio vya asili.
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
� Ushiriki wa jamii katika kubaini maeneo mapya yenye vivutio vya asili
6. Maswala Mtambuka
(a) UKIMWI � Kuendeleza mapambano dhidi ya
maambukizi mapya ya UKIMWI na virusi vya UKIMWI kwenye shule zote 117 na watumishi ofisi za kata na wilaya.
� Idadi ya vilabu vilivyoanzishwa kwenye ngazi ya shule
� Kuanzishwa kwa kilabu ngazi ya wilaya
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
(b) Rushwa � Kuimarishwa vita dhidi ya rushwa
kwenye shule zote 117 na watumishi ofisi za kata na wilaya.
� Idadi ya vilabu vilivyoanzishwa kwenye ngazi ya shule
� Kuanzishwa kwa kilabu ngazi ya wilaya
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
� Ushiriki wa Jamii katika uzuiaji na kuchukia rushwa.
(c) Mazingira � Shule zote 117 zitashindanishwa kila
mwaka katika uhifadhi wa mazingira.
Idadi ya shule zilizoshindanishwa - Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
� Utayari wa shule kuanzisha na kuimarisha vilabu vya utunzaji wa mazingira ya shule
74
SN ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
(d) Jinsia � Wanafunzi kutoka shule 30
watahamasishwa juu ya uwezo na nafasi sawa katika masomo na utendaji mwingine
Idadi ya shule na wanafunzi wanaoshiriki kwenye makongamano ya jinsia
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
(e) Walemavu � Kuimarisha shule 1 ya walemavu wa
akili iliyopo. � Kutoa mahitaji yanayowakwaza
walemavu 10 waliopo kwenye shule za msingi.
� Idadi ya mipango ya kuendeleza shule ya walemavu wa akili.
� Idadi ya walemavu waliosaidiwa kutatua vikwazo vya kujifunza
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
� Utayri wa Wadau kushiriki katika kuendeleza elimu ya walemavu wa akili na waliopo kwenye shule za kawaida.
7 Usimamizi wa mipango ya kitaasisi
Ifikapo 2018: � Kuhakikisha uhusiano wa kiutawala
unaimarishwa na taasisi nyingine zenye udau na elimu.
� Kuimarisha Kamati za shule wenye shule zote 118.
� Kuimarisha ukaguzi kwenye shule zote 118
� Kuimarisha mifumo ya utoaji taarifa ndani na nje ya wilaya
� Idadi ya wadau walioshiriki � Idadi ya Kamati za shule
zilizopata mafunzo. � Utoaji wa taarifa kwa wakati
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
� Kuongezeka kwa ushirikiano na viongozi wa kata, vijiji, shule, vyama vya ushirika, mashirika ya dini, NGO’s
8. Mazingira bora ya kufanyia kazi
Ifikapo 2018: � Kuimarisha mfumo wa mawasiliano
kwa kuanzisha tovuti ya idara ya Elimu. � Kuimarisha uwezo wa kusafiri ndani ya
idara kwa kununua gari na pikipiki. � Kuimarisha utaratibu wa kutunza
nyaraka na mali nyeti. � Kuongeza ufanisi wa kazi kwa kuongeza
samani na vifaa vya kazi vya kielektroniki.
� Kufanya ukarabati wa jengo la idara
� Kuanzishwa kwa tovuti ya idara ya elimu.
� Idadi ya magari na pikipiki zitakazonunuliwa
� Idadi ya sehemu za hifadhi zilizojengwa
� Idadi ya vifaa vilivyonunuliwa
� Ukarabati wa jengo unaofanywa kwa mwaka
- Taarifa za mwezi, robo, nusu na mwaka
- Ufuatiliaji
� Utayari wa Jamii kuanzisha shirika la kusimamia ubora wa elimu kupitia makato ya mapato ya zao la korosho
� Kuimarika kwa mfumo wa kufanya kazi na utoaji taarifa
75
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: ELIMU YA MSINGI
LENGO KUU: Ifikapo mwaka 2018, mazingira ya kufundishia na kujifunzia yawe yameboreshwa ili kutoa fursa ya kutoa elimu bora itakayoinua maisha ya jamii ili kuondoa umaskini.
SN LENGO MKAKATI MHUSIKA
MUDA WA UTEKELEZAJI 2015 2016 2017 2018 2018/19
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1. Uandikishaji wa
wanafunzi � Kufanya sensa ya kuwatambua
wanafunzi wote wenye umri wa kwenda shule na ambao hawahudhurii shule.
DEO, MEK, Walimu Wakuu
2. Mahudhurio na kudumu shuleni
� Kuhamasisha wazazi na jamii kupitia opersheni za viongozi mbalimbali kusimamia elimu ya watoto.
DEO, Wadau, Madiwani
� Kuweka mazingira ya kuvutia shuleni mfano miti ya vivuli, mipango ya chakula cha mchana, bendi , michezo nk
MEK, Walimu Wakuu
� Kuhimiza matumizi ya sheria ya mahudhurio ya lazima kutekelezwa na vijiji
DEO, WEO, VEO
3. Miundombinu � Kuhakikisha jamii inashirikishwa kikamilifu kwenye miradi ya ujenzi na kutengeneza samani
DED, DEO, Wadau
� Halmashauri (W) itumie sehemu ya mapato yake ya ndani kusaidia nguvu za wananchi
DED
� Kushirikisha wadau mbalimbali wa elimu kuchangia mipango ya kuinua elimu kupitia uwepo wa miundombinu
DED, DEO, Wadau
� Kuanzisha mfuko maalum utakaotumika kuinua elimu
DC, DED, Wadau
76
SN LENGO MKAKATI MHUSIKA
MUDA WA UTEKELEZAJI 2015 2016 2017 2018 2018/19
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 4. Ustawi wa Walimu � Kuhakikisha walimu wakuu na
waratibu wote wanapatiwa mafunzo ya uongozi
DED, DEO
� Kuhakikisha walimu wanalipwa kwa wakati stahili zao mfano nauli za likizo, marupurupu ya uhamisho, kuugua nk
DED, DEO
� Kuhakikisha walimu wanapatiwa mafunzo ya masomo tata mfano english, hisabati, KKK na sayansi
DED, DEO
5. Utamaduni na michezo
� Uimarishaji wa michezo kwenye ngazi za shule
DED, DEO, DCSO
� Kuwa na vilabu vya michezo mbalimbali ya kisasa na ya jadi
DCSO
� Kuwa na mashindano ya michezo mbalimbali ngazi ya vilabu na maeneo ya kiutawala mfano ya tarafa ili kuwa na timu madhubuti za wilaya
DED, DCSO
� Kuanzisha, kusajili na kuimarisha sanaa za mikono na maonesho na kuandaa matamasha na maonesho
DCSO
� Ushirikishaji wa watu mashuhuri katika kuhifadhi historia na maeneo yenye vivutio vya asili
DED, DCSO, Watu mashuhuri
6. Maswala mtambuka
� Kuanzisha vilabu mbalimbali vihusuvyo UKIMWI, mazingira, rushwa, michezo, jinsia na walemavu ili kupata mbinu za
DED, DEO, TAKUKURU, Ustawi wa Jamii,
77
SN LENGO MKAKATI MHUSIKA
MUDA WA UTEKELEZAJI 2015 2016 2017 2018 2018/19
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 kuelimishana, kuondoa unyanyapaa na hata kujiongezea kipato
Madiwani,Mganga Mkuu (W)
7. Usimamizi wa mipango ya Kitaasisi
� Kuweka mazingira ya kuhamasisha utendaji kazi na kutoa motisha kwa watenda kazi bora kitaaluma, kuwa na vivutio shuleni, kutunza wanafunzi (retention) shule kuwa na mipaka inayoeleweka na kutoa hati bora na zawadi kwa shule bora.
DED, DEO
� Kushirikisha wadau katika kuajiri walimu maalum watakaosomeshwa masomo maalum kufundisha kwa mkataba.
DC, DED, DEO, Wadau
� Kuhakikisha shule zina mipaka inayoeleweka
DED, DEO, MEK, Walimu Wakuu
� Shule zote 118 ziwe na Kamati za shule hai zenye mafunzo
DEO, Walimu Wakuu
� Ukaguzi wa shule ufanyike kwenye shule zote
DED, DEO, DCSI
� Kuhakikisha idara inapata samani za kutosha
DEO
� Kuimarisha mfumo wa kupokea na kutuma taarifa ndani nje ya wilaya.
DEO
8. Mazingira bora ya kufanyia kazi
� Uchaguzi wa kamati za shule DED, DEO
� Kuunganishwa na mawasiliano ya Internet
DED, DE, DEO
� Kuimarisha uwezo wa idara wa kusafiri kwa kununua gari na pikipiki
DED, DEO
� Ujenzi wa strong room ya idara na makasiki kwenye shule
DEO
78
SN LENGO MKAKATI MHUSIKA
MUDA WA UTEKELEZAJI 2015 2016 2017 2018 2018/19
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 � Kununua samani na mashine ya
fotokopi, laptop na kompyuta DEO
� Kufanya ukarabati wa jengo la idara ya elimu
DEO, DE
� Kuandaa Mpango wa Maendeleo ya Elimu (W)
DED,DEO
79
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI WA MPANGO MKAKATI 2015 - 2018
ENEO LA HUDUMA: ELIMU YA MSINGI
SN LENGO MKAKATI MAKISIO YA GHARAMA
JUMLA MHUSIKA 2015 2016 2017 2018
Uandikishaji wa wanafunzi
� Kufanya sensa ya kuwatambua wanafunzi wote wenye umri wa kwenda shule na ambao hawahudhurii shule. 200,000 200,000 200,000 200,000 800,000
DEO
Mahudhurio na kudumu shuleni
� Kuhamasisha wazazi, jamii na watoto wao wanatambua umuhimu wa elimu kupitia opersheni za wadau mbalimbali. 4,000,000 4,000,000 4,000,000 4,000,000 16,000,000
DED, DEO Madiwani, wadau
� Kuweka mazingira ya kuvutia shuleni mfano miti ya vivuli, mipango ya chakula cha mchana, bendi , michezo nk 1,000,000 1,000,000 1,000,000 1,000,000 4,000,000
DEO
� Kuhimiza matumizi ya sheria ya mahudhurio ya lazima kutekelezwa na vijiji 500,000 500,000 500,000 500,000 2,000,000
DEO, WEO, VEO,
Miundombinu � Kuhakikisha jamii inashirikishwa kikamilifu kwenye miradi ya ujenzi na kutengeneza samani 400,000,000 400,000,000 400,000,000 400,000,000 1,600,000,000
Jamii, wadau
80
SN LENGO MKAKATI MAKISIO YA GHARAMA
JUMLA MHUSIKA 2015 2016 2017 2018
� Halmashauri (W) itumie sehemu ya mapato yake ya ndani kusaidia nguvu za wananchi 175,000,000 175,000,000 175,000,000 175,000,000 700,000,000
DED, DEO
Kushirikisha wadau mbalimbali wa elimu kuanzisha mfuko wa kuchangia mipango ya kuinua elimu kupitia uwepo wa miundombinu - 1,400,000,000 1,400,000,000 1,400,000,000 4,200,000,000
Jamii, wadau
Ustawi wa Walimu
Kuhakikisha walimu wakuu na waratibu wote wanapatiwa mafunzo ya uongozi 5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000 20,000,000
DED, DEO, Jamii
Kuhakikisha walimu wanalipwa kwa wakati stahili zao mfano nauli za likizo, marupurupu ya uhamisho, kuugua nk 120,000,000 120,000,000 120,000,000 120,000,000 480,000,000
DED. DEO
Kuhakikisha walimu wanapatiwa mafunzo ya masomo tata mfano english, hisabati, KKK na sayansi 10,000,000 10,000,000 10,000,000 10,000,000 40,000,000
DED, DEO, Jamii
Utamaduni na michezo
Uimarishaji wa michezo kwenye ngazi za shule 500,000 500,000 500,000 500,000 2,000,000
DEO, A/UTAMADUNI
Kuwa na vilabu vya michezo mbalimbali
5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000 20,000,000 A/UTAMA
81
SN LENGO MKAKATI MAKISIO YA GHARAMA
JUMLA MHUSIKA 2015 2016 2017 2018
ya kisasa na ya jadi
Kuwa na mashindano ya michezo mbalimbali ngazi ya vilabu na maeneo ya kiutawala mfano ya tarafa ili kuwa na timu madhubuti za wilaya 7,500,000 7,500,000 5,000,000 5,000,000 25,000,000
DED, A/UTAMDUNI
Kuanzisha, kusajili na kuimarisha sanaa za mikono na maonesho na kuandaa matamasha na maonesho 1,000,000 1,000,000 1,000,000 1,000,000 4,000,000 A/UTAMADUNI Ushirikishaji wa watu mashuhuri katika kuhifadhi historia na vivutio vya asili 500,000 - 500,000 - 1,000,000
DEO, A/UTAMADUNI
Maswala mtambuka
Kuanzisha vilabu mbalimbali vihusuvyo UKIMWI, mazingira, rushwa, michezo, jinsia na walemavu ili kupata mbinu za kuelimishana, kuondoa unyanyapaa na hata kujiongezea kipato 500,000 - - - 500,000
DEO
82
SN LENGO MKAKATI MAKISIO YA GHARAMA
JUMLA MHUSIKA 2015 2016 2017 2018
Usimamizi wa mipango ya Kitaasisi
Kuweka mazingira ya kuhamasisha utendaji kazi na kutoa motisha kwa watenda kazi bora kitaaluma, kuwa na vivutio shuleni, kutunza wanafunzi (retention) shule kuwa na mipaka inayoeleweka na kutoa hati bora na zawadi kwa shule 3,000,000 3,000,000 3,000,000 3,000,000 12,000,000 DED, DEO Kushirikisha wadau katika kuajiri walimu maalum watakaosomeshwa masomo maalum kufundisha kwa mkataba. 15,000,000 15,000,000 30,000,000
DED,DEO, Wadau
Kuhakikisha shule zina mipaka inayoeleweka 300,000 - - - 300,000 DEO Shule zote 118 ziwe na Kamati za shule hai zenye mafunzo
- 180,000,000 - - 180,000,000 DED, DEO Ukaguzi wa shule ufanyike kwenye shule zote 30,000,000 30,000,000 30,000,000 30,000,000 120,000,000 DED, DEO, DCSI Kuhakikisha idara inapata samani za kutosha - - 25,000,000 25,000,000 50,000,000 DED,DEO, Wadau
83
SN LENGO MKAKATI MAKISIO YA GHARAMA
JUMLA MHUSIKA 2015 2016 2017 2018
Kuimarisha mfumo wa kupokea na kutuma taarifa ndani nje ya wilaya. 12,000,000 12,000,000 12,000,000 12,000,000 48,000,000 DED, DEO
Mazingira ya kufanyia kazi
Uchaguzi wa kamati za shule 2,000,000 - - 2,000,000 4,000,000 DED, DEO Kuunganishwa na mawasiliano ya Internet 8,000,000 2,000,000 - - 10,000,000 DEO Kuimarisha uwezo wa idara wa kusafiri kwa kununua gari na pikipiki 250,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,000 256,000,000 DED, DEO Ujenzi wa strong room ya idara na makasiki kwenye shule 100,000,000 100,000,000 100,000,000 100,000,000 400,000,000 DEO Kununua samani na mashine ya fotokopi, laptop na kompyuta 5,000,000 - 1,500,000 - 6,500,000 DEO Kufanya ukarabati wa jengo la idara ya elimu - - 12,000,000 12,000,000 24,000,000 DED, DEO Kuandaa Mpango wa Maendeleo ya Elimu (W) 30,000,000 - - - 30,000,000 DEO
JUMLA KUU 1,171,000,000 2,473,700,000 2,313,200,000 2,328,200,000 8,286,100,000
84
ENEO LA HUDUMA: ELIMU SEKONDARI
LENGO KUU : Kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia ili kutoa elimu bora itakayoinua hali ya maisha ya jamii ili kuondoa umaskini ifikapo mwaka 2018.
NA ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
1 USAJILI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA
Kuongeza idadi ya wanafunzi wanaosajiliwa kujiunga na kidato cha kwanza kutoka 78% ya sasa mpaka 100% ya wanafunzi wanaokuwa na sifa za kujiunga kidato cha I wanasajiliwa ifikapo mwaka 2018.
Idadi ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Elimu ya Sekondari kusajiliwa. Idadi ya vyumba vya madarasa vilivyopo.
• Ukaguzi. • Taarifa/ufuatiliaji.
Jamii kushiriki kikamilifu katika kusimamia maendeleo ya elimu ya watoto wao.
2 MAHUDHURIO Ifikapo mwaka 2018 kuimarisha mahudhurio ya lazima kwa wanafunzi wa vidato vyote kwa kuzingatia kanuni, sheria na miongozo ya Wizara.
Idadi ya wanafunzi wanaonza/ andikishwa kidato cha kwanza na kuhitimu kidato cha nne
• Taarifa/ufuatiliaji • ukaguzi
Jamii kushiriki kikamilifu katika kusimamia maendeleo ya elimu ya watoto wao.
3 UFAULU Kiwango cha taaluma ya wanafunzi wanaofaulu elimu ya sekondari kiwe kimepanda kutoka 13.69% mwaka 2012 kufikia 58% ifikapo mwaka 2018.
Idadi ya wanafunzi waliofulu
• Ukaguzi. • Taarifa/ufuatiliaji.
Kuwepo kwa fedha za uwezeshaji na uendeshaji.
4 KUJENGA UWEZO Ifikapo mwaka 2018, • Kuongeza idadi ya walimu walioajiriwa
kutoka 265 wa sasa hadi kufikia walimu 440.
• Kuimarisha upatikanaji wa vitendea kazi vyote muhimu vya ofisi.
• kuwezesha walimu 141 wenye stashahada kwa sasa kusomea shahada ya Elimu.
• Kusomesha watumishi wawili walio ofisini kusomea Shahada ya juu ya Utawala katika Elimu.
Idadi ya walimu watakaoajiriwa. Idadi ya vitendea kazi.
Taarifa za robo, nusu, robotatu na mwaka.
Kupatikana kwa kibali cha ajira.
85
NA ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
5 MIUNDO MBINU Kufikia mwaka 2018 a) Idadi ya mikondo ifikie minne kwa
kila shule b) Shule 2 za sekondari zinazojengwa
ziwe zimekamilika na kufanya jumla ya shule 28 toka 26 zilizopo sasa.
c) Kuongeza idadi ya nyumba za walimu toka 74 hadi 194.
d) Kuongeza ya matundu ya vyoo vya wanafunzi kutoka 334 ya sasa hadi 574(was 130, wav 110)
e) Kuongeza ya matundu ya vyoo vya walimu kutoka 14 ya sasa hadi 112(ke 56, me 56)
f) Kuongeza idadi ya shule zenye maabara kutoka shule 3 hadi 28.
g) Hosteli 16 ziwe zimejengwa kutoka 8 zilizopo sasa.
h) Visima 184 viwe vimechimbwa toka 22 vilivyopo sasa.
i) Majengo ya utawala 28 yawe yamejengwa kutoka majengo 11.
j) Majengo 4 ya utawala ambayo hayajakamilia kwa sasa yawe yamekamilika.
k) Kujenga mabwalo ya chakula 16 kutoka 2 yaliyopo sasa.
l) Kujenga majiko 28 kutoka 1 lililopo sasa.
• Idadi ya majengo yatakayojengwa na kukamilika.
• Ujenzi wa shule mbili kukamilika, kusajiliwa na kuanzishwa.
• Kufuatilia • Kukagua • Kuwepo kwa taarifa za
robo, nusu na mwaka.
Kuwepo kwa fedha Uchangiaji wa nguvu kazi kutoka kwa jamii. Michango ya wahisani Serikali kuu kuchangia.
6. SAMANI Ifikapo mwaka 2018: a) Viti na meza za walimu kununuliwa
kutoka 54 vya sasa hadi kufikia 440. b) Viti na meza za wanafunzi kununuliwa
kutoka 8523 vya sasa hadi kufikia 19875.
Idadi ya samani zitakazoo nunuliwa.
• Ukaguzi • Taarifa/ ufuatiliaji
Kuwepo kwa fedha.
86
NA ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
7. VIFAA VYA KUFUNDISHIA NA KUJIFUNZIA
Uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi ufikie 1:3 kutoka uwiano wa sasa wa 1:8 ifikapo mwaka 2018.
Vitabu vya masomo mbalimbali 9800 viwe vimenunuliwa ifikapo mwaka 2018.
• Ukaguzi. • Taarifa/ufuatiliaji
Kuwepo kwa fedha. Kupatikana kwa wahisani.
8. KUMBUKUMBU NA NYARAKA
Ifikapo mwaka 2018 utunzaji wa kumbukumbu uwe umeboreshwa.
Idadi ya watumishi watakaopata mafunzo ya utunzaji kumbukumbu.
• Ukaguzi. • Taarifa/ufuatiliaji
Kuwepo kwa fedha.
9. MAWASILIANO Kuboresha mawasiliano katika Ofisi ya Elimu (W) ifikapo mwaka 2018
Kuunganishwa mitambo ya mawasiliano ya mkongo wa taifa.
Taarifa na ufuatiliaji. Kuwepo kwa fedha.
10 MICHEZO Kuimarisha michezo katika shuleni ifikapo mwaka 2018.
Uwepo wa vikundi vya michezo. Ufuatiliaji na uhamasishaji. Kupatikana kwa fedha.
11 VVU/UKIMWI Kuendeleza mapambana dhidi ya maambukizi mapya ifikapo mwaka 2018
Idadi ya vilabu vitakazoanzishwa na kuwa hai.
Taarifa na ufuatiliaji Maambukizi kupungua miongoni mwa watumishi na wanafunzi.
12 MAKUNDI MAALUMU
Ifikapo mwaka 2018 kuimarisha huduma za wanafunzi 200 waliokatika makundi maalumu.
Idadi ya wanafunzi watakaopatiwa huduma.
Taarifa na ufuatiliaji Kupatikana kwa fedha. Wahisani kuchangia
13 RUSHWA Kuendeleza mapambana dhidi ya rushwa ifikapo mwaka 2018.
Idadi ya vilabu vitakavyoundwa na kuwa imara
Kupatikana kwa fedha.
14 MAZINGIRA Kuboresha mazingira katika shule za sekondari 28 zitakazokuwepo ifikapo mwaka 2018.
Idadi ya miti ya matunda, vimvuli na na maua yatakayopandwa.
Ukaguzi na ufuatiliaji Kupatikana kwa fedha.
15 MIPAKA YA SHULE
Kuweka mipaka ya shule katika shule 28 ifikapo mwaka 2018.
Idadi ya shule zitakazopimwa. Ukaguzi na ufuatiliaji Kupatikana kwa fedha. Wanajamii kuhamasika kutoa maeneo yao bila fidia au fidia nafuu.
87
ENEO LA HUDUMA: ELIMU SEKONDARI
LENGO KUU: Kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia ili kutoa elimu bora itakayoinua hali ya maisha ya jamii ili kuondoa umaskini ifikapo mwaka 2018.
LENGO MKAKATI MHUSIKA MUDA WA UTEKELEZAJI
2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
1. Kuongeza idadi ya wanafunzi wanaosajiliwa kujiunga na kidato cha kwanza kutoka 78% ya sasa mpaka 100% ya wanafunzi wanaokuwa na sifa za kujiunga kidato cha I wanasajiliwa ifikapo mwaka 2018.
• Kujenga uwezo kwa bodi za shule kusimamia usajili na mahudhurio ya lazima kwa wanafunzi wote.
• Kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto wao kwa kuandaa na kuendesha kampeni maalumu ya elimu.
DC, DED, DSEO, MADIWANI, JAMII
2. Ifikapo mwaka 2018 kuwe na mahudurio ya lazima kwa wanafunzi wa vidato vyote kwa kuzingatia kanuni, sheria na miongozo ya Wizara.
• Kuchukua hatua za kisheria kwa wote wanaosababisha wanafunzi kuacha shule.
• Kuboresha mazingira ya shule kuyafanya yawe kivutio kwa wanafunzi.
• Kuhimimiza upatikanaji wa chakula cha mchana shuleni
DC, DED, DSEO, MADIWANI, JAMII, VEO, WEO
3.Kuinua kiwango cha taaluma ya wanafunzi wanaofaulu elimu ya sekondari kutoka 13.69% mwaka 2012 kufikia 58%ifikapo mwaka 2018.
• Kuhamasisha walimu kujiendeleza • Kutoa mafunzo kazini na kozi fupi • Kusomesha wanafunzi waliohitimu
kidato cha sita kwa mkataba hasa wa masomo ya Sayansi na Hisabati
• Kutafuta vyanzo vya fedha. • Kuimarisha ukaguzi wa shule kwa
kuwatumia wakaguzi wa shule. • Kulipa stahiki za watumishi kwa
wakati ili kuondoa mlundikano wa madeni hasa ya likizo na uhamisho.
DED, DHRO, DSEO, JAMII, WAKAGUZI
88
LENGO MKAKATI MHUSIKA MUDA WA UTEKELEZAJI
2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
4.Ifikapo mwaka 2018, • Kuongeza idadi ya walimu
walioajiriwa kutoka 265 wa sasa hadi kufikia walimu 440.
• Kuimarisha upatikanaji wa vitendea kazi vyote muhimu vya ofisi.
• Kuwezesha walimu 141 wenye stashahada kwa sasa kusomea shahada ya Elimu.
• Kusomesha watumishi wawili walio ofisini kusomea Shahada ya juu ya Utawala katika Elimu.
• Kuomba kibali cha ajira kitakachowesha kuajiri walimu 50 kila mwaka.
• Kuwa na mpango wa manunuzi ulio mahususi na wa wazi.
• Gari 1 la idara liwe limenunuliwa • Kukopesha pikipiki 28 kwa wakuu. • Kuweka umeme katika majengo ya
shule.
DED, DHRO, DSEO
5.Kufikia mwaka 2018, • Idadi ya mikondo ifikie minne kwa
kila shule • Shule 2 za sekondari zinazojengwa
ziwe zimekamilika na kufanya jumla ya shule 28 toka 26 zilizopo sasa.
• Kuongeza idadi ya nyumba za walimu toka 74 hadi 194.
• Kuongeza ya matundu ya vyoo vya wanafunzi kutoka 334 ya sasa hadi 574(was 130, wav 110
• Kuongeza ya matundu ya vyoo vya walimu kutoka 14 ya sasa hadi 112(ke 56, me 56)
• Kuongeza idadi ya shule zenye maabara kutoka shule 3 hadi 28.
• Hosteli 16 ziwe zimejengwa kutoka 8 zilizopo sasa.
• Visima 184 viwe vimechimbwa toka 22 vilivyopo sasa.
• Majengo ya utawala 28 yawe yamejengwa kutoka majengo 11.
• Majengo 4 ya utawala ambayo hayajakamilia kwa sasa yawe
• Kujenga vyumba 70 kila mwaka. • Kujenga majengo yote muhimu katika
shule 2. • Kujenga nyumba za walimu 30 za
walimu kila mwaka. • Kujenga matundu 60 ya vyoo vya
wanafunzi kila mwaka. • Kujenga maabara katika shule 6 kila
mwaka. • Kujenga matundu 24 ya vyoo vya
walimu kila mwaka. • Kujenga hostel za wasichana katika
shule 4 kila mwaka. • Kuchimba visima 40 kila mwaka. • Kujenga majengo ya utawala katika
shule 4 kila mwaka. • Kukamilisha majengo 4 ya utawala
ifikapo mwaka 2018. • Kujenga mabwalo 3 ya chakula kila
mwaka. Kujenga majiko katika shule 6 kila mwaka.
DC, DED, DSEO, MADIWANI, WANAJAMII, WADAU
89
LENGO MKAKATI MHUSIKA MUDA WA UTEKELEZAJI
2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
yamekamilika. • Kujenga mabwalo ya chakula 16
kutoka 2 yaliyopo sasa. • Kujenga majiko 28 kutoka 1 lililopo
sasa. 6. ifikapo mwaka 2018:
• Kuongeza idaid ya viti na meza za walimu kutoa 53 hadi kufikia 440
• Kuongeza Viti na meza za wanafunzi kutoka 8523 hadi kufikia 19875.
Kununua au kuchongesha meza na viti 80 vya walimu na 80 vya wanafunzi kwa kila shule kila mwaka.
DED, DSEO, WAHISANI
7. Uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi ufikie 1:3 kutoka uwiano wa sasa wa 1:8 ifikapo mwaka 2018.
• Kununua vitabu 3360 kwa kila somo kwa mwaka.
• Kujenga maktaba za kutosha katika shule zetu ili kuwa na uhifadhi/utunzaji mzuri wa vitabu vilivyopo na vitakavyonunuliwa.
DED, DSEO, WAHISANI
8. Ifikapo mwaka 2018 utunzaji wa kumbukumbu uwe umeboreshwa.
Kununua: • Mashine za kisasa (kamera ya video na
picha, “scanner 1”, “power pointi 1”) na kompyuta.
• Kujenga Chumba maalumu (strong room) cha kuhifadhia nyaraka(mf. Mitihani) katika shule zote 28 na ofisini.
DED, DSEO,
9. Kuboresha mawasiliano katika Ofisi ya Elimu (W) ifikapo mwaka 2018
• Kuendesha mafunzo kwa watumishi. • Mtambo wa mawasiliano ya mkongo wa
Taifa uliopo katika eneo la Halmashauri,kuunganishwa katika ofisi ya Elimu ifikapo mwaka oktoba 2014 • Kuanzisha tovuti ya Idara.
DED, DSEO, DE
10 Kuimarisha michezo katika shuleni ifikapo mwaka 2018.
• Kuongeza idadi ya wanafunzi walioteuliwa kujiunga kambi za taifa za michezo na kupata ufadhili
DED, DSEO, WAHISANI
11. Kuendeleza mapambana dhidi ya maambukizi mapya ifikapo mwaka 2018
• Kutoa elimu na kuhamasisha upimaji wa hiari.
• Wanafunzi na walimu kujengewa uelewa
DED, DSEO, DCDO, DMO, ASASI
90
LENGO MKAKATI MHUSIKA MUDA WA UTEKELEZAJI
2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
wa mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI kwa kuanzisha na kuimarisha vilabu kwa kila shule.
• Kuwatambua watumishi na wanafunzi walioathirika na VVU/UKIMWI
12 Ifikapo mwaka 2018 kuimarisha huduma za wanafunzi 200 waliokatika makundi maalumu
Kubaini makundi haya na kuwawezesha kupata mahitaji husika.
DED, DSEO, DCDO, WAHISANI
13. Kuendeleza mapambana dhidi ya rushwa ifikapo mwaka 2018
• Kuunda klabu za kupambana na kuzuia rushwa katika shule zote za sekondari kutoka 5 za sasa.
• Kuzuia mianya ya rushwa sehemu za kazi kwa kuboresha utoaji wa huduma.
DC, DED, DSEO, TAKUKURU, WATUMISHI, MADIWANI, WANAJIAMII
14. Kuboresha mazingira katika shule za sekondari 28 zitakazokuwepo ifikapo mwaka 2018.
Upandaji wa miti, maua na mbogamboga pamoja na uchimbaji wa mashimo ya takataka,
DED, DSEO, HMs, DAICO, WANAJAMII
15 Kuweka mipaka ya shule katika shule 28 ifikapo mwaka 2018.
• Kushirikiana na viongozi wa vyama vya msingi kuzisaidia shule kulipa fidia za mazao yaliyokatika maeneo ya shule.
• Kupima shule zote na kuzipatia hati miliki.
DED, DSEO, DLNREO, VYAMA VYA MSINGI, WANAJAMII
91
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: ELIMU SEKONDARI
LENGO MKAKATI
MAKISIO YA GHARAMA CHANZO
CHA FEDHA 2015 2016 2017 2018 JUMLA 1. Kuongeza idadi ya wanafunzi wanaosajiliwa kujiunga na kidato cha kwanza kutoka 78% ya sasa mpaka 100% ifikapo mwaka 2018.
Kujenga uwezo kwa bodi za shule kusimamia usajili na mahudhurio ya lazima kwa wanafunzi wote. 22,880,000 22,880,000 22,880,000 22,880,000 91,520,000
ADA, WAHISANI
Kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa elimu kwa watoto wao kwa kuandaa na kuendesha kampeni maalumu ya elimu.
4,000,000 4,000,000 4,000,000 4,000,000 16,000,000
2. Ifikapo mwaka 2018 kuwe na mahudurio ya lazima kwa wanafunzi wa vidato vyote kwa kuzingatia kanuni, sheria na miongozo ya Wizara.
Kuboresha mazingira ya shule kuyafanya yawe kivutio kwa wanafunzi kwa kuhimiza upatikanaji wa chakula shuleni.
186,200,000 196,000,000 215,600,000 225,600,000 823,400,000
WAHISANI, MICHANGO YA WAZAZI
3.Kuinua kiwango cha taaluma ya wanafunzi wanaofaulu elimu ya sekondari kutoka 13.69% mwaka 2012 kufikia 58%ifikapo mwaka 2018.
Kuhamasisha walimu kujiendeleza kwa ngazi mbalimbali za elimu. 5,000,000 6,000,000 7,000,000 8,000,000 26,000,000
BG, HALSHAURI
Kutoa mafunzo kazini na kozi fupi kwa walimu hasa kwa mada ngumu. 3,000,000 4,000,000 5,000,000 6,000,000 18,000,000 Kusomesha wanafunzi waliohitimu kidato cha sita kwa mkataba hasa wa masomo ya Sayansi na Hisabati 10,000,000 10,000,000 10,000,000 10,000,000 40,000,000
92
LENGO MKAKATI
MAKISIO YA GHARAMA CHANZO
CHA FEDHA 2015 2016 2017 2018 JUMLA 4.Ifikapo mwaka 2018, Kuimarisha ukaguzi wa shule
kwa kuwatumia wakaguzi wa shule. 20,000,000 20,000,000 20,000,000 20,000,000 80,000,000
� Kuongeza idadi ya walimu walioajiriwa kutoka 265 wa sasa hadi kufikia walimu 440.
Kulipa stahiki za watumishi kwa wakati ili kuondoa mlundikano wa madeni hasa ya likizo na uhamisho
55,000,000 55,000,000 55,000,000 55,000,000 220,000,000
� Kuwezesha walimu 141 wenye stashahada kwa sasa kusomea shahada ya Elimu.
Kuomba kibali cha ajira kitakachowezesha kuajiri walimu 50 kila mwaka.
27,250,000 29,250,000 31,250,000 33,250,000 121,000,000
� Kusomesha watumishi wawili walio ofisini kusomea Shahada ya juu ya Utawala katika Elimu.
Kuwa na mpango wa manunuzi ulio mahususi na wa wazi.
400,000 400,000 400,000 400,000 1,600,000
Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi
Gari 1 la idara liwe limenunuliwa
250,000,000 - - - 250,000,000
Halmshauri WAHISANI, BG
Kukopesha pikipiki 28 kwa wakuu. 98,000,000 - - - 98,000,000
Kuweka umeme katika majengo ya shule. 259,200,000 259,200,000 259,200,000 259,200,000 1,036,800,000
Kuandaa mpango wa masomo. 9,000,000 9,000,000 9,000,000 9,000,000 36,000,000
5.Kufikia mwaka 2018,
Kujenga vyumba 70 vya madarasa kila mwaka.
24,500,000 24,500,000 24,500,000 24,500,000 98,000,000
CDG, Halmashauri, WAHISANI � Idadi ya mikondo
ifikie minne kwa kila shule
93
LENGO MKAKATI
MAKISIO YA GHARAMA CHANZO
CHA FEDHA 2015 2016 2017 2018 JUMLA � Shule 2 za sekondari zinazojengwa ziwe zimekamilika na kufanya jumla ya shule 28 toka 26 zilizopo sasa.
Kujenga na kukamilisha majengo yote muhimu katika shule 2.
625,000,000 200,000,000 - - 825,000,000 � Kuongeza idadi ya nyumba za walimu toka 74 hadi 194.
Kujenga nyumba 30 za walimu kila mwaka.
1,050,000,000 1,050,000,000 1,050,000,000 1,050,000,000 4,200,000,000 � Kuongeza ya matundu ya vyoo vya wanafunzi kutoka 334 ya sasa hadi 574.(wav110, was 130)
Kujenga matundu 60 ya vyoo vya wanafunzi kila mwaka.
100,000,000 100,000,000 100,000,000 100,000,000 400,000,000
� Kuongeza ya matundu ya vyoo vya walimu kutoka 14 ya sasa hadi 112.(me 56, ke 56)
Kujenga matundu 24 ya vyoo vya wanafunzi kila mwaka.
30,000,000 30,000,000 30,000,000 30,000,000 120,000,000
� Kuongeza idadi ya shule zenye maabara kutoka shule 3 hadi 28.
kujenga maabara katika shule 6 kila mwaka
220,000,000 220,000,000 220,000,000 220,000,000 880,000,000 � Hosteli 16 ziwe zimejengwa kutoka 8 zilizopo sasa.
kujenga hostel nne za wasichana kila mwaka
150,000,000 150,000,000 150,000,000 150,000,000 600,000,000
� Visima 184 viwe vimechimbwa toka 22 vilivyopo sasa.
Kuchimba visima 40 kila mwaka
16,000,000 17,000,000 18,000,000 19,000,000 70,000,000
94
LENGO MKAKATI
MAKISIO YA GHARAMA CHANZO
CHA FEDHA 2015 2016 2017 2018 JUMLA � Majengo ya utawala 17 yawe yamejengwa kutoka majengo 11.
Kujenga majengo ya utawala katika shule 4 kila mwaka.
90,000,000 100,000,000 110,000,000 120,000,000 420,000,000
� Majengo 4 ya utawala ambayo hayajakamilia kwa sasa yawe yamekamilika.
kukamilisha majengo 4 ya utawala
48,000,000 - - - 48,000,000
� Kujenga mabwalo ya chakula 16 kutoka 2 yaliyopo sasa.
Kujenga mabwalo 3 ya chakula kila mwaka.
210,000,000 210,000,000 210,000,000 210,000,000 840,000,000 � Kujenga majiko 27 kutoka 1 lililopo sasa.
kujenga majiko katika shule 6 kila mwaka
60,000,000 72,000,000 78,000,000 84,000,000 294,000,000 Halshauri
6. ifikapo mwaka 2018:
Kutafuta vyanzo vya fedha kutoka sehemu mbalimbali na kuhamasisha jamii kuchangia ili kuwezesha:
-
CDG, WAFADHILI, Halmashauri, JAMII
� Viti na meza za walimu kununuliwa kutoka 53 vya sasa hadi kufikia 440
Kuchongesha viti na meza 80 za walimu kwa kila mwaka
9,600,000 9,600,000 10,400,000 10,400,000 40,000,000
� Viti na meza za wanafunzi kununuliwa kutoka 8523 vya sasa hadi kufikia 19875
Kuchongesha viti na meza 80 za wanafunzi kwa kila shule kwa kila mwaka
268,800,000 268,800,000 291,200,000 291,200,000 1,120,000,000
7. Uwiano wa kitabu kwa mwanafunzi
Kutafuta vyanzo vya fedha kutoka sehemu mbalimbali. 45,000,000 45,000,000 45,000,000 45,000,000 180,000,000
CDG, WAHISANI
95
LENGO MKAKATI
MAKISIO YA GHARAMA CHANZO
CHA FEDHA 2015 2016 2017 2018 JUMLA ufikie 1:3 kutoka uwiano wa sasa wa 1:8 ifikapo mwaka 2018.
Kujenga maktaba za kutosha katika shule zetu ili kuwa na uhifadhi/utunzaji mzuri wa vitabu vilivyopo na vitakavyonunuliwa.
8. Ifikapo mwaka 2018 utunzaji wa kumbukumbu uwe umeboreshwa.
Kutafuta vyanzo vya fedha vitakavywezesha kununua:
-
BG, HALSHAURI, CGG
Mashine za kisasa (kamera ya video na picha, “scanner 1”, “power pointi 1”) na kompyuta. 10,000,000 8,000,000 - - 18,000,000 Kujenga Chumba maalumu (strong room) cha kuhifadhia nyaraka (mf. Mitihani) katika shule zote 28 na ofisini.(7 kila mwaka) 70,000,000 70,000,000 70,000,000 70,000,000 280,000,000
9. Kuboresha mawasiliano katika Ofisi ya Elimu (W) ifikapo mwaka 2018
Kutafuta vyanzo vya fedha.
CDG,CB, HALSHAURI Kuendesha mafunzo kwa
watumishi. 9,000,000 10,000,000 11,000,000 12,000,000 42,000,000 Mtambo wa mawasiliano ya mkongo wa Taifa uliopo katika eneo la Halmashauri,kuunganishwa katika ofisi ya Elimu ifikapo mwaka oktoba 2014 10,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,000 16,000,000
Kuanzisha tovuti ya Idara. 1,000,000 - - - 1,000,000
10 Kuimarisha michezo katika shuleni ifikapo mwaka 2018.
Timu za UMISSETA kuweza kuzalisha wanamichezo watakaotoa hamasa kwa wanafunzi na wazazi kushiriki michezo shuleni. 45,000,000 48,000,000 51,000,000 54,000,000 198,000,000
ADA, BG, WAHISANI
96
LENGO MKAKATI
MAKISIO YA GHARAMA CHANZO
CHA FEDHA 2015 2016 2017 2018 JUMLA Kuongeza idadi ya wanafunzi walioteuliwa kujiunga kambi za taifa za michezo na kupata ufadhili 10,000,000 11,000,000 12,000,000 13,000,000 46,000,000
11. Kuendeleza mapambana dhidi ya maambukizi mapya ifikapo mwaka 2018
Kushirikiana na asasi mbalimbali zinazojihusisha na masuala ya mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI kutoa elimu na kuhamasisha upimaji wa hiari. 500,000 500,000 500,000 500,000 2,000,000
Wanafunzi na walimu kujengewa uelewa wa mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI kwa kuanzisha na kuimarisha vilabu kwa kila shule. 500,000 500,000 500,000 500,000 2,000,000
Kuwatambua watumishi na wanafunzi walioathirika na VVU/UKIMWI ili kuweza kuwapatia stahiki zao.
4,800,000 4,800,000 4,800,000 4,800,000 19,200,000
12 Ifikapo mwaka 2018 kuimarisha huduma za wanafunzi 200 waliokatika makundi maalumu
Kushirikiana na maafisa maendeleo na ustawi wa jamii kuyabaini makundi haya na kuwawezesha kupata mahitaji husika.
20,000,000 20,000,000 20,000,000 20,000,000 80,000,000
13. Kuendeleza mapambana dhidi ya rushwa ifikapo mwaka 2018
Kujenga uelewa dhidi ya rushwa kwa kuunda klabu za kupambana na kuzuia rushwa katika shule zote za sekondari kutoka 5 za sasa. 500,000 500,000 500,000 500,000 2,000,000
Kuzuia mianya ya rushwa sehemu za kazi kwa 48,000,000 48,000,000 48,000,000 48,000,000 192,000,000
97
LENGO MKAKATI
MAKISIO YA GHARAMA CHANZO
CHA FEDHA 2015 2016 2017 2018 JUMLA kuboresha utoaji wa huduma.
14. Kuboresha mazingira katika shule za sekondari 28 zitakazokuwepo ifikapo mwaka 2018.
Upandaji wa miti, maua na mbogamboga pamoja na uchimbaji wa mashimo ya takataka,
800,000 800,000 800,000 800,000 3,200,000
BG, ADA
15 Kuweka mipaka ya shule katika shule 28 ifikapo mwaka 2018.
Kushirikiana na viongozi wa vyama vya msingi kuzisaidia shule kulipa fidia za mazao yaliyokatika maeneo ya shule.
40,000,000 44,000,000 48,000,000 52,000,000 184,000,000
WAHISANI, MICHANGO YA JAMII, ADA
Kupima shule zote na kuzipatia hati miliki. 500,000 600,000 700,000 800,000 2,600,000
JUMLA KUU 5,917,430,000 5,131,330,000 5,496,230,000 5,536,330,000 22,081,320,000
98
ENEO LA HUDUMA : SEKTA YA ARDHI
Lengo Kuu: Kuwa na makazi bora na kumiliki ardhi kisheria mijini na vijijini
NA ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
1 Matumizi bora ya ardhi na umiliki wa Ardhi Mijini na Vijijini
Kuongeza Mpango Mkakati 1 undelezaji wa mji na ifikapo 2018
Mpango 1 uliondaliwa
Taarifa za utekelezaji Mchoro na ramani kutembelea maeneo
Kubadilika kwa sera ya Makazi, Uwepo wa fedha
Kuongeza upimaji wa viwanja toka 3015 hadi 6515 ifikapo 2018
Idadi ya viwanja vilivyopimwa
Taarifa za utekelezaji na utembeleaji wa
Uwepo wa fedha
Kuongeza hati miliki za kawaida mijini toka 500 hadi 5000 ifikapo 2018
Idadi ya hati zilizondaliwa
Taarifa za utekelezaji
Uwepo wa fedha
Kuongeza hati miliki za kimila toka 220 hadi 45,000 ifikapo 2018
Idadi ya hati zilizondaliwa
Taarifa za utekelezaji na utembeleaji wa maeneo
Kubadilika kwa sera ya Makazi Uwepo wa fedha
Kuongeza makusanyo ya Kodi ya ardhi toka Tsh. 12 milioni kwa mwaka hadi 40 milioni ifikapo 2018
Asilimia ya ongezeko la makusanyo ya mapato
Taarifa za utekelezaji na utembeleaji wa maeneo
Kubadilika kwa sera ya Makazi Uwepo wa fedha
2 Maeneo ya wazi Kuboresha maeneo ya 20 ifikapo 2018 Idadi ya maeneo yaliyoboreshwa
Taarifa za utekelezaji na utembeleaji wa maeneo
Uwepo wa fedha
3 Majina ya mitaa Kutambua mitaa 300 kwa majina ifikapo 2018
Idadi ya vibao vyenye majina
Taarifa ya Utekelezaji
Uwepo wa fedha
4 Kujenga uwezo Kuongeza ajira za watumishi toka 4 hadi 8 ifikapo 2018
Idadi ya watumishi walioajiriwa
Taarifa za hali ya watumishi
Uwepo wa fedha Kibali cha ajira
99
NA ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
Kuongeza vitendea kazi, Jumla station 1, plotter 1, plan cabinet 1, photocopy 2, printing machine 1 na pikipiki 4, compyuta 4 ifikapo 2018
Idadi ya vifaa vilivyonunuliwa
Taarifa ya utekelezaji
Uwepo wa fedha
Kuongeza watumishi waliopata mafunzo ngazi ya shahada toka 1 hadi 3 ifikapo 2018
Idadi ya watumishi waliopata mafunzo
Taarifa ya utekelezaji
Kuhakiki wa vyeti
Uwepo wa fedha
4 Ukimwi, jinsia Kuongeza uelewa kuhusu kujikinga Ukimwi na maswala ya jinsia ifikapo 2018
Idadi ya vikao vilivyofanyika
Taarifa ya utekelezaji
Uwepo wa fedha
5 Kupambana na rushwa
Kuongeza ulewa wa watumishi jinsi ya kuziba mianya ya rushwa ifikapo 2018
Idadi ya vikao vilivyofanyika
Taarifa ya utekelezaji
Uwepo wa fedha
100
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA ARDHI
Lengo Kuu: Kuwa na makazi bora na kumiliki ardhi kisheria mijini na vijijini
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 1 Kuongeza mpango Mkakati 1 wa undelezaji wa mji ifikapo 2018
Mkakati : Kutoa elimu kwa jamii kuhusu mipango ya uendelezaji miji
DED,DLNREO,TPLO
Mkakati: Kulipa fidia ya mashamba eneo la mjini
DED, DLNREO
Mkakati: Kuchora michoro ya mipango miji
DED,DLNREO
Lengo 2 Kuongeza hati miliki za kawaida mjini toka 500 hadi 5000 ifikapo 2018
Mkakati: Kununua vifaa vya upimaji wa kisasa GPS yenye Real Time Kinematic Mode (RTK) na Jumla Station
DED,DLNREO,DLS
101
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Mkakati: Kupima viwanja vya matumizi mbalimbali
DED, DLNREO
Mkakati: Kuandaa hati miliki za kawaida
Lengo 3 Kuongeza makusanyo ya Kodi ya ardhi toka Tsh. 12 milioni kwa mwaka hadi 40 milioni ifikapo 2018
Mkakati: Kutoa matangazo na vipeperushi ya ujumbe wa kulipa kodi ya ardhi
DED,DLNREO,DLO
Mkakati: Kuandaa orodha ya walipa kodi
DED,DLNREO
Lengo 4 Kuongeza hati miliki za kimila toka 220 hadi 45,000 ifikapo 2018
Mkakati: Kupima mipaka ya vijiji vilivyogawanyika
DED,DLNREO,DLS
Mkakati: Kupanga matumizi bora ya ardhi
DED,DLNREO
Mkakati: Kuandaa hati miliki za kimila
102
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 5 Kuboresha maeneo ya wazi 20 ifikapo 2018
Mkakati: Kusafisha na kuweka miondo mbinu
DED,DLNREO,DE,DWE
Lengo 6 Kutambua mitaa 300 kwa majina ifikapo 2018
Mkakati: Kuweka vibao vya mitaa
DED,DLNREO,DE
Lengo 7 Kuongeza ajira za watumishi toka 4 hadi 8 ifikapo 2018
Mkakati: Kuajiri ajira mpya
DED
Lengo 8 Kuongeza vitendea kazi, photocopy 2, printing machine 1 na pikipiki 4 ifikapo 2018
Mkakati: Kununua vitendea kazi na vifaa vya ofisi
DED
Lengo 9 Kuongeza watumishi waliopata mafunzo ngazi ya shahada toka 1 hadi 3 ifikapo 2018
Mkakati: Watumishi kuhudhuria mafunzo
DED
Lengo 10 Kuongeza uelewa wa watumishi kuhusu kujikinga Ukimwi na maswala ya jinsia ifikapo2018
103
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Mkakati: Kuwapa watumishi elimu ya kujikinga na maambukizi ya VVU na maswala ya jinsia
DLNREO
Kuongeza ulewa wa watumishi jinsi ya kuziba mianya ya rushwa ifikapo 2018
Mkakati: Kuotoa elimu ya kupambana na rushwa mahali pa kazi
DLNREO
104
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA ARDHI
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA CHANZO CHA PESA
Lengo 1 Kuongeza Mpango Mkakati 1 undelezaji wa mji na ifikapo 2018
Mkakati : Kutoa elimu kwa jamii kuhusu mipango ya uendelezaji miji
1,500,000.00 1,500,000.00 3,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kuandaa mpango mkakati
10,000,000.00 10,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kulipa fidia ya mashamba eneo la mjini
100,000,000.00
300,000,000.00 300,000,000.00 300,000,000.00 250,000,000.00 1,250,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kuchora michoro ya mipango miji
5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 25,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 2 Kuongeza hati miliki za kawaida mjini toka 500 hadi 5000 ifikapo 2018
Mkakati: Kununua vifaa vya upimaji wa kisasa GPS yenye Real Time Kinematic Mode (RTK) na Jumla Station
60,000,000.00 60,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kupima viwanja vya matumizi mbalimbali
20,000,000.00 20,000,000.00 20,000,000.00 20,000,000.00 20,000,000.00 100,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kuandaa hati 2,500,000.00 2,500,000.00 2,500,000.00 2,500,000.00 2,500,000.00 12,500,000.00 TDC, CDG,BG
105
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA CHANZO CHA PESA
miliki za kawaida Wafadhili
Lengo 3 Kuongeza makusanyo ya Kodi ya ardhi toka Tsh. 12 milioni kwa mwaka hadi 40 milioni ifikapo 2018
Mkakati: Kutoa matangazo na vipeperushi vya ujumbe wa kulipa kodi ya ardhi
500,000.00 500,000.00 500,000.00 500,000.00 500,000.00 2,500,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kuandaa orodha ya walipa kodi
500,000.00 500,000.00 500,000.00 1,500,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 4 Kuongeza hati miliki za kimila toka 220 hadi 45,000 ifikapo 2018
Mkakati: Kupima mipaka ya vijiji vilivyogawanyika
15,000,000.00 15,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 45,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kupanga matumizi bora ya ardhi
321,000,000.00 321,000,000.00 321,000,000.00 321,000,000.00 321,000,000.00 1,608,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kuandaa hati za kimila
5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 25,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 5 Kuboresha maeneo ya wazi 20 ifikapo 2018
Mkakati: Kusafisha na kuweka miondo mbinu
40,000,000.00 40,000,000.00 40,000,000.00 40,000,000.00 40,000,000.00 200,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 6 Kutambua mitaa 300 kwa majina ifikapo 2018
Mkakati: Kutengenezesha na
10,000,000.00 10,000,000.00 20,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
106
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA CHANZO CHA PESA
kuweka vibao vya mitaa
Lengo 7 Kuongeza ajira za watumishi toka 4 hadi 8 ifikapo 2018
Mkakati: Kuajiri ajira mpya
5,400,000.00 5,400,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 8 Kuongeza vitendea kazi, photocopy 2, printing machine 1 na pikipiki 4 ifikapo 2018
Mkakati: Kununua vitendea kazi na vifaa vya ofisi
22,000,000.00 500,000.00 27,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 9 Kuongeza watumishi waliopata mafunzo ngazi ya shahada toka 1 hadi 3 ifikapo 2018
Mkakati: Watumishi kuhudhuria mafunzo
3,500,000.00 3,500,000.00 3,500,000.00 3,500,000.00 3,500,000.00 17,500,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 10 Kuongeza uelewa wa watumishi kuhusu kujikinga Ukimwi na maswala ya jinsia ifikapo2018
Mkakati: Kuwapa watumishi elimu ya kujikinga na maambukizi ya VVU na maswala ya jinsia
100,000.00 100,000.00 100,000.00 100,000.00 100,000.00 500,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 11 Kuongeza ulewa wa watumishi jinsi ya kuziba mianya ya rushwa ifikapo 2018
Mkakati: Mkakati: Kuotoa elimu ya kupambana na rushwa mahali pa kazi
100,000.00 100,000.00 100,000.00 100,000.00 100,000.00 500,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
107
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA CHANZO CHA PESA
JUMLA 423,000,000 395,600,000 375,600,000 375,600,000 375,100,000 1,952,400,000
108
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA MISITU NA MAZINGIRA
Lengo kuu: Kutumia Rasilimali za Misitu kwa Maendeleo endelevu
NA ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
1 Hifadhi ya Misitu Kuboresha usimamizi shirikishi wa misitu ya hifadhi ya Halmashauri kwenye vijiji 5 ifikapo 2018.
Idadi ya vijiji vitakavyoshiriki
Taarifa za utekelezaji Kutobadilika kwa sera ya Makazi, Uwepo wa fedha
Kuongeza hifadhi ya misitu ya Ardhi ya vijijii toka 6 hadi 20 ifikapo 2018.
Idadi ya vijiji vyenye hifadhi ya misitu ya jamii
Taarifa za utekelezaji Kutobadilika kwa Sera ya Misitu Ushiriki wa jamii Uwepo wa fedha
2 Hifadhi ya vyanzo vya maji
Kuboresha hifadhi ya vyanzo vya maji vyanzo 8 vilivyopo ifikapo 2018
Idadi ya miti itakayopandwa na vyanzo vya maji vitakavyo hifadhiwa
Taarifa za utekelezaji Kutobadilika kwa Sera ya Misitu Ushiriki wa jamii Uwepo wa fedha
3 Mabadiliko ya tabianchi
Kukuza uelewa juu mabadiriko ya tabianchi katika vijiji 75 ifikapo 2018
Idadi ya vijiji vitakavyopata elimu ya mabadiliko ya tabia ya nchi na kuhifadhi mazingira
Taarifa za utekelezaji Kutobadilika kwa Sera ya Misitu Uwepo wa fedha
4 Kujenga uwezo Kuongeza ajira za watumishi toka 4 hadi 8 ifikapo 2018
Idadi ya watumishi walioajiriwa
Taarifa za utekelezaji Uwepo wa fedha
Kuongeza watumishi waliopata mafunzo ngazi ya shahada toka 1 hadi 2 ifikapo 2018
Idadi ya watumishi waliopata mafunzo
Taarifa za utekelezaji Uwepo wa fedha
Kuwa na vifaa na vitendea kazi muhimu Photokopi 1, kompyuta 3 na pikipiki 5 ifikapo
Idadi ya vitendea kazi vitakavyo
110
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA MISITU NA MAZINGIRA
Lengo Kuu: Kutumia Rasilimali za Misitu kwa Maendeleo endelevu
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 1
Kuboresha usimamizi shirikishi wa misitu ya hifadhi kwenye vijiji 5 ifikapo 2018.
Mkakati: Kutoa mafunzo ya jinsi ya kushiriki usimamzi wa pamoja wa misitu
DED,DLNREO,DFO
Mkakati: Kuandaa mipango ya uvunaji
DED,DLNREO,DFO
Lengo 2 Kuongeza hifadhi ya misitu ya Ardhi ya vijijii toka 6 hadi 20 ifikapo 2018.
Mkakati: Kuhamasisha vijiji vitenge misitu ya hifadhi
DED,DLNREO,DFO
Mkakati: Kupima misitu ilyotengwa na vijiji
DED,DLNREO,DFO
Mkakati: Kuandaa mipango ya uvunaji na usimamizi endelevu wa misitu
DED,DLNREO,DFO
Lengo 3 Kutoa elimu ya mabadiriko ya tabianchi na uapandaji miti kufikia asilimia 75 ya vijiji vyote ifikapo 2018
111
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Mkakati: Kuandaa na kutoa mafunzo kuhusu mabadiliko ya tabianchi
DED,DLNREO,DFO
Mkakati: Kupanda miti kwa wingi kila mwaka
DED,DLNREO,DFO
Lengo 4 Kuongeza ajira za watumishi toka 4 hadi 8 ifikapo 2018
Mkakati: Kuajiri watumishi wapya
DED,DLNREO,DFO
Lengo 5 Kuongeza watumishi waliopata mafunzo ngazi ya shahada toka 1 hadi 2 ifikapo 2018
Mkakati: Kuwapeleka watumishi kuhudhuria mafunzo vyuoni
DED,DLNREO,DFO
Lengo 6 Kuwa na vifaa na vitendea kazi muhimu Photokopi 1, kompyuta 3,scanner na pikipiki 4 ifikapo 2018
Mkakati Kununua vitendea kazi
DED,DLNREO
112
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA MISITU NA MAZINGIRA
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA CHANZO CHA PESA
Lengo 1 Kuboresha usimamizi shirikishi wa misitu ya hifadhi kwenye vijiji 5 ifikapo 2018
Mkakati: Kutoa mafunzo ya jinsi ya kushiriki usimamzi wa pamoja wa misitu
10,000,000.00 10,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kuandaa mipango ya uvunaji
25,000,000.00 25,000,000.00 25,000,000.00 25,000,000.00 100,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 2 Kuongeza hifadhi ya misitu ya Ardhi ya vijijii toka 6 hadi 20 ifikapo 2018.
Mkakati: Kuhamasisha vijiji vitenge misitu ya hifadhi
2,000,000.00 2,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kupima misitu ilyotengwa na vijiji
3,500,000.00 3,500,000.00 3,500,000.00 3,500,000.00 3,500,000.00 10,500,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kuandaa mipango ya uvunaji na usimamizi endelevu wa misitu
15,000,000.00 15,000,000.00 30,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 3 Kutoa elimu ya mabadiriko ya tabianchi na uapandaji miti kufikia asilimia 75 ya vijiji vyote ifikapo 2018
113
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA CHANZO CHA PESA
Mkakati: Kuandaa na kutoa mafunzo kuhusu mabadiliko ya tabianchi
6,000,000 6,000,000 6,000,000 6,000,000 6,000,000 30,000,000 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kupanda miti kwa wingi kila mwaka
4,000,000.00 4,000,000 4,000,000 4,000,000 4,000,000 20,000,000 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 4 Kuongeza ajira za watumishi toka 4 hadi 8 ifikapo 2018
Mkakati: Kuajiri watumishi wapya
7,200,000. TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 5 Kuongeza watumishi waliopata mafunzo ngazi ya shahada toka 1 hadi 2 ifikapo 2018
Mkakati: Kuwapeleka watumishi kuhudhuria mafunzo vyuoni
3,500,000 3,500,000 3,500,000 3,500,000 3,500,000 17,500,000 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 6 Kuwa na vifaa na vitendea kazi muhimu Photokopi 1, kompyuta 3,scanner na pikipiki 4 ifikapo 2018
Mkakati : Kununua vitendea kazi
4000,000 8,000,000 5,000,000 1,200,000 17,200,000 TDC, CDG,BG Wafadhili
JUMLA 40,200,000 52,000,000 62,000,000 58,200,000 42,000,000 235,200,000
114
ENEO LA HUDUMA : SEKTA YA NYUKI
Lengo kuu: Kupunguza umasikini kwenye jamii kwa kutumia mazao ya nyuki
NA ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
1 Manzuki (mashamba ya Nyuki)
Kuongeza uzalishaji wa asali toka lita 100,000 hadi 150,000 ifikapo 2018
Idadi ya vikundi vilivyoongezeka na vilivyowezeshwa vifaa vya kisasa na kiasi cha mazao ya nyuki yaliyouzwa sokoni
Taarifa ya utekelezaji Kutembelea vikundi
Uwepo wa fedha Ushiriki wa jamii
2 Kujenga uwezo wa watumishi na ufanisi kazini
Kuongeza watumishi 2 waliopata mafunzo ngazi ya diploma kuhusu ufugaji nyuki ifikapo 2018
Idadi ya watumishi waliopata mafunzo
Taarifa ya utekelezaji
Uwepo wa fedha
Kuwa na vitendea kazi, Kompyuta 2, photokopi 1 na pikipiki 2 ifikapo 2018
Idadi ya kompyuta na pikipiki zilizo nunuliwa
Taarifa ya utekelezaji
Uwepo wa fedha
115
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA NYUKI
Lengo Kuu: Kupunguza umasikini kwenye jamii kwa kutumia mazao ya nyuki
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 1 Kuongeza uzalishaji wa asali toka lita 100,000 hadi 150,000 ifikapo 2018
Mkakati: Kutoa mafunzo ya ufugaji bora wa nyuki kwenye vikundi vya ufugaji nyuki
DLNREO,DBO
Mkakati: Kutoa vifaa vyakisasa kwenye vikundi vya ufugaji
DED,DLNREO,DBO
Mkakati: Kufuatilia masoko ya mazao ya nyuki
DLNREO, DBO
Mkakati: Kutafiti maeneo yenye mimea inayofaa kwa ufagaji nyuki
DLNREO,DBO
116
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Mkakati: Kutafiti magonjwa na maadui wa nyuki ili kuzia madhara yake kwa nyuki
DED,DLNREO,DBO
Lengo 2 Kuongeza watumishi 2 waliopata mafunzo ngazi ya diploma kuhusu ufugaji nyuki ifikapo 2018
Mkakati: Kuwezesha watunishi kwenda kuhudhuria mafunzo ya
DED,DLNREO
Lengo 3 Kuwa na vitendea kazi, Kompyuta 2, photokopi 1 na pikipiki 2 ifikapo 2018
Mkakati: Kununua kompyuta photokopi na pikipiki
DED,DLNREO
117
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA NYUKI
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA CHANZO CHA PESA
Lengo 1 Kuongeza uzalishaji wa asali toka lita 100,000 hadi 150,000 ifikapo 2018
Mkakati: Kutoa mafunzo ya ufugaji bora wa nyuki kwenye vikundi vya ufugaji nyuki
4,000,000 4,000,000 4,000,000 4,000,000 4,000,000 20,000,000 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kutoa vifaa vyakisasa kwenye vikundi vya ufugaji
3,500,000 3,500,000 3,500,000 3,500,000 3,500,000 17,500,000 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kufuatilia masoko ya mazao ya nyuki
6,000,000 6,000,000 6,000,000 6,000,000 6,000,000 24,000,000 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kutafiti maeneo yenye mimea inayofaa kwa ufagaji nyuki ili kupanua maeneo ya ufugaji nyuki
3,000,000.00 3,000,000 3,000,000 3,000,000 3,000,000 15,000,000 TDC, CDG,BG Wafadhili
Mkakati: Kutafiti magonjwa na maadui wa nyuki ili kuzia madhara yake kwa nyuki
3,000,000 3,000,000 3,000,000 3,000,000 3,000,000 15,000,000 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 2 Kuongeza watumishi 2 waliopata mafunzo ngazi ya diploma kuhusu ufugaji nyuki ifikapo 2018
118
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA CHANZO CHA PESA
Kuwezesha watunishi kwenda kuhudhuria mafunzo ya ufugaji nyuki
4,500,000.00 4,500,000.00 4,500,000.00 4,500,000.00 18,000,000.00 TDC, CG, Wafadhili
Lengo 3 Kuwa na vitendea kazi, Kompyuta 2, Tv set, internet, photokopi 1 na pikipiki 2 ifikapo 2018
Mkakati: Kununua kompyuta, TV set, Internet na photokopi na pikipiki
5,000,000.00 5,000,000.00 5,000,000.00 10,000,000.00 25,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
JUMLA 24,500,000 29,000,000 29,000,000 34,000,000 24,000,000 134,500,000
119
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA WANYAMAPORI
Lengo kuu: Kusimamia na Kuhifadhi Rasilimali za Wanyamapori
NA ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
1 Wanyama waharibifu Kupunguza madhara ya wanyama waharibifu yanayofanywa kwenye vijiji 20 ifikapo 2018
Idadi ya vijiji na vikundi vilvyopatiwa mafunzo
Taarifa za utekelezaji
Uwepo wa fedha Ushiriki wa jamii
Kuongeza eneo la kufanya doria ya wanyama waharibifu toka vijiji 12 hadi 20 ifikapo 2018
Idadi ya vijiji ambavyo doria imefanyika
Taarifa za utekelezaji Uwepo wa fedha
2 Rasilimali za Wanyama Pori
Kutambua 20% vinasaba vya wanyama pori na mahali wanaopatikana ifikapo 2018
Idadi ya wanyama pori waliofanyiwa tathmini
Taarifa za utekelezaji Uwepo wa fedha
3 Kujenga uwezo wa watumishi na ufanisi kazini
Ununuzi wa pikipiki 2, mahema 4 na risasi 1000 ifikapo 2018
Idadi ya pikipiki, mahema, na risasizilizonunuliwa
Taarifa za utekelezaji Uwepo wa fedha
120
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA WANYAMAPORI
Lengo Kuu: Kusimamia na Kuhifadhi Rasilimali za Wanyamapori
Lengo/Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezji
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Lengo 1 Kupunguza madhara ya wanyama waharibifu kwenye vijiji 20 ifikapo 2018
Mkakati: Kutoa elimu ya kujikinga na wanyama hatari na waharibifu
DED,DLNREO,DGO
Mkakati: Kufanya doria dhidi ya wanyama waharibifu na hatarishi
DED,DLNREO,DGO
Lengo 2 Kutambua 20% ya aina ya wanyama pori na mahali wanapopatikana ifikapo 2018
Kufanya sensa ya wanyamapori
DED,DLNREO,DGO
Lengo 3 Kuwa na vitendea kazi, pikipiki 2, mahema 4 na risasi 1000 ifikapo 2018
Mkakati Kununua vitendea kazi
DED,DLNREO,DGO
121
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: SEKTA YA WANYAMAPORI
Lengo/Mkakati MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 20171/18 JUMLA CHANZO CHA PESA
Lengo 1 Kupunguza madhara ya wanyama waharibifu kwenye vijiji 20 ifikapo 2018
Kutoa elimu ya kujikinga na wanyama hatari na waharibifu
3,000,000.00 3,000,000.00 3,000,000.00 3,000,000.00 12,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Kufanya doria dhidi ya wanyama waharibifu na hatarishi
6,000,000.00 6,000,000.00 6,000,000.00 6,000,000.00 6,000,000.00 18,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 2 Kutambua 20% ya aina ya wanyama pori na mahali wanapopatikana ifikapo 2018
Kufanya sensa ya wanyamapori
15,000,000.00 15,000,000.00 15,000,000.00 15,000,000.00 15,000,000.00 60,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
Lengo 3 Kuwa na vitendea kazi, pikipiki 2, mahema 4 na risasi 1000 ifikapo 2018
Mkakati Kununua vitendea kazi
7,000,000.00 10,000,000.00 4,000,000.00 4,000,000.00 4,000,000.00 29,000,000.00 TDC, CDG,BG Wafadhili
JUMLA 28,000,000 31,000,000 25,000,000 25,000,000 25,000,000 107,000,000
122
ENEO LA HUDUMA: UJENZI
LENGO KUU: Kuboresha huduma ya mawasiliano kwa matengenezo ya Barabara zenye urefu wa km 981 na kalavati 89 ifikapo 2018.
ENEO LA MATOKEO
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
UJENZI/UKARABATI WA BARABARA
Ukarabati wa barabara za udongo kutoka km 371 hadi 790 ifikapo 2018
Km 419 zilizokarabatiwa na kupitika.
Kutembelea eneo la mradi. -Taarifa za utekelezaji
Upatikanaji wa fedha. -Uwepo wa usafiri wa uhakika.
Matengenezo ya barabara za changarawe kutoka km 98 hadi km 198.
Km 100 changarawe zilizo jengwa na kupitika
kutembelea eneo la mradi. -taarifa za maendeleo ya mradi kila robo/mwaka
-Upatikanaji wa fedha. -Uwepo wa usafiri wa uhakika.
-Ujenzi wa Box kalavati 90 ifikapo 2018.
Kalavati 90 zilizojengwa.
-kutembelea eneo la mradi. -taarifa za utekelezaji kwa robo/mwaka.
-upatikanaji wa fedha. -uhakika wa usafiri.
-Ujenzi mpya wa barabara km 5 za lami ifikapo 2018.
Km 5 za lami zilizojengwa.
-kutembelea eneo husika-taarifa za utekelezaji za robo/mwaka.
-upatikanaji wa fedha. -Uhakika wa usafiri.
-Ujenzi wa mifereji ya maji ya mvua km10 ifikapo 2018.
Km 10 za mifereji zilizojengwa.
-kutembelea eneo la mradi. -taarifa za utekelezaji za robo/mwaka
-uhakika wa usafiri. -upatikanaji wa fedha
-Uwekaji wa alama 180 za usalama barabarani ifikapo 201
Alama 180 za barabarani zilizowekwa.
- Kutembelea eneo la mradi. -taarifa za utekelezaji
-uhakika wa usafiri. -upatikanaji wa fedha
Kujenga uwezo -kuajiri mafundi sanifu 3 ifikapo 2018. -Kutoa mafundi kwa mafundi sanifu 4 ifikapo 2018.
Watumishi 3 wawe wameajiriwa. Mafunzo yawe yametolewa kwa watumishi 4.
-taarifa za ajira. -Vyeti vya taaluma -Vyeti vya taaluma. Taarifa za mafunzo.
-uwepo wa kibali cha ajira. -upatikanaji wa fedha. -upatikanaji wa fedha.
Mambo ya Jinsia/Ukimwi
Kuendeleza mapambano juu yakupunguza maambukizi ya
Kupungua kwa maambukizi ya ukimwi.
Taarifa za utekelezaji -taarifa za vikao.
-Upatikanaji wa fedha.
123
ENEO LA MATOKEO
LENGO MAHSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
Ukimwi kwa Watumishi ifikapo 2018. -Kuwahamasisha makampuni ya ujenzi ya wanawake kushiriki kwenye miradi ya barabara ifikapo 2018.
-Kampuni za wanawake kuongezeka.
-Vyeti vya usajili wa makampuni.
-Upatikanaji wa kampuni. -Ushiriki wa jamii.
Ufuatiliaji na Usimamizi.
Kuimarisha ufuatiliaji na usimamizi wa miradi ya barabara ifikapo 2018.
-Safari za ufuatiliaji na usimamizi kuongezeka.
-Taarifa za ufuatiliaji na usimamizi kwa robo/mwaka.
-Uhakika wa usafiri. -Upatikanaji wa fedha.
Utawala Bora Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa kwa kutoa elimu kwa watumishi/jamii.
Idadi ya vikao vilivyofanyika.
Kutokuwepo mashitaka ya rushwa. -Taarifa za vikao vilivyofanyika
Utayari wa watumishi/jamii
124
LENGO, MKAKATI NA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: UJENZI ( BARABARA )
Lengo Kuu: Kuboresha huduma ya mawasiliano kwa kutengeneza barabara KM 981, culverts 89 ifikapo 2018
Lengo/Mkakati MKAKATI MHUSIKA 2014 2015 2016 2017 2018 Ukarabati wa barabara za Udongo kutoka km 271 hadi km 490
Kutangaza Zabuni. DED &DE&PO
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
DE &DED
Matengenezo ya barabara za Changarawe kutoka Km 98 hadi Km 198.
Kutangaza Zabuni DE & PO
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
DE &DED
Ujenzi wa Box culvert mpya 90 ifikapo 2018
Kutangaza Zabuni DED &DE
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
DE &PO
Ujenzi mpya wa Barabara za lami Km 5 ifikapo 2018
Kutangaza Zabuni DED &DE
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
DE &PO
Kutoa mafunzo kwa mafundi sanifu 4 ifikapo 2018.
Kutoa mafunzo kwa fundi sanifu mmoja kwa kila mwaka
DED &DE
Ujenzi wa mifereji ya maji ya mvua
Kutangaza Zabuni DED,DE &POI
125
Lengo/Mkakati MKAKATI MHUSIKA 2014 2015 2016 2017 2018 Km 10 Ifikapo 2018
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
DED &DE
Uwekaji wa alama 180 za Usalama barabarani ifikapo 2018
Kutangaza Zabuni DE &PO
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
DE &PO
Kuajiri Mafundi sanifu 3 ifikapo 2016
Kuajiri fundi sanifu mmoja kwa kila mwaka
DED &DE
Kuwahamasisha Kampuni za Ujenzi za Wanawake kushiriki miradi ya barabara ifikapo 2018.
Kutoa Elimu katika jamii.
CDO &DE
Kuimarisha Ufuatiliaji na Usimamizi wa miradi ya barabara na majengo ifikapo 2018.
Kununua gari la usimamizi
DED &DE
Kufanya ukaguzi na usimamizi wa kila mara
DED,DED &MADIWANI
Kuendeleza
mapambano juu yakupunguza maambukizi ya Ukimwi kwa Watumishi ifikapo 2018.
Kutoa Elimu kwa watumishi kwa kila robo mwaka kwa pamoja na jamii husika ktk mradi
CDO &DE
Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa kwa kutoa elimu kwa
Kutoa elimu ya mara kwa mara kwa watumishi kwa kufanya vikao.
DE &TAKUKURU
127
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: UJENZI (BARABARA)
LENGO MIKAKATI
CHANZO CHA
FEDHA
MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA Ukarabati wa barabara za Udongo kutoka km 271 hadi km 490
Kutangaza Zabuni. TDC,ROADFUND 502,000,000 550,000,000
600,000,000
650,000,000
700,000,000 3,002,000,000
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
TDC,ROADFUND 25,100,000 27,500,000 30,000,000 32,500,000 35,000,000 150,010,000
Kutangaza Zabuni TDC,ROADFUND 380,000,000 400,000,000
450,000,000
480,000,000
500,000,000 2,210,000,000
Matengenezo ya barabara za Changarawe kutoka Km 98 hadi Km 198.
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
TDC,ROADFUND
19,000,000 20,000,000 22,500,000 24,000,000 25,000,000 110,500,000 Ujenzi wa Box culvert mpya 90 ifikapo 2018
Kutangaza Zabuni TDC,ROADFUND 72,000,000 90,000,000
120,000,000
150,000,000
180,000,000 612,000,000
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
TDC,ROADFUND 3,600,000 4,500,000 6,000,000 7,500,000 9,000,000 30,600,000
Ujenzi mpya wa Barabara za lami Km 5 ifikapo 2018
Kutangaza Zabuni TDC,ROADFUND
- 625,000,000 650,000,000
680,000,000
700,000,000 2,655,000,000
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
TDC,ROADFUND - 31,250,000 32,500,000 34,000,000 35,000,000 132,750,000
Kutoa mafunzo kwa mafundi sanifu 4 ifikapo 2018.
Kutoa mafunzo kwa fundi sanifu mmoja kwa kila mwaka
TDC
2,000,000 2,500,000 3,000,000 4,000,000 - 11,500,000 Kuajiri Mafundi sanifu 3 ifikapo 2016
Kuajiri fundi sanifu mmoja kwa kila mwaka
TDC - 3,600,000 4,000,000 4,500.000 5,000,000 17,100,000
Ujenzi wa mifereji ya maji ya mvua Km 10 Ifikapo 2018
Kutangaza Zabuni TDC,ROADFUND
120,000,000 150,000,000 200,000,000
220,000,000
250,000,000 940,000,000
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
TDC,ROADFUND 6,000,000 7,500,000 10,000,000 11,000,000 12,500,000 47,000,000
Uwekaji wa alama 180 za Usalama barabarani ifikapo 2018
Kutangaza Zabuni TDC,ROAD 45,000,000 60,000,000 75,000,000 90,000,000 270,000,000
128
LENGO MIKAKATI
CHANZO CHA
FEDHA
MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA FUND
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara
TDC,ROADFUND 2.250,000 3,000,000 3,750,000 4,500,000 13,500,000
Kuwahamasisha Kampuni za Ujenzi za Wanawake kushiriki miradi ya barabara ifikapo 2018.
Kutoa Elimu katika jamii. TDC
1,000,000 1,500,000 1,800,000 2,000,000 6,300,000 Kuimarisha Ufuatiliaji na Usimamizi wa miradi ya barabara na majengo ifikapo 2018.
Kununua gari la usimamizi TDC,ROADFUND
- 100,000,000 - - - 100,000,000 Kufanya ukaguzi na usimamizi wa kila mara
TDC 10,000,000 13,000,000
17,000,000
20,000,000
25,000,000 85,000,000
Kuendeleza mapambano juu yakupunguza maambukizi ya Ukimwi kwa Watumishi ifikapo 2018
Kutoa Elimu kwa watumishi kwa kila robo mwaka kwa pamoja na jamii husika ktk mradi
TDC, ROADFUND
500,000 800,000 1,000,000 1,200,000 1,500,000 5,000,000 Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa kwa kutoa elimu kwa watumishi/jamii.
Kutoa elimu ya mara kwa mara kwa watumishi kwa kufanya vikao.
TDC
400,000 600,000 800,000 1,000,000 1,200,000 4,000,000
JUMLA 1,020,720,000
2,074,500,000
2,211,300,000
2,400,250,000
2,575,700,000
10,402,260,000
129
ENEO LA HUDUMA: MIPANGO
LENGO KUU : Kuratibu na kusimamia utekelezaji wa Mpango wa maendeleo wa wilaya 2015- 2018.
NA ENEO LA MATOKEO
LENGO MAHUSUSI/MKAKATI
VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
1 Mpan go wa maendeleo wa wilaya
Kuandaa mpango kazi wa mwaka wa wilaya kila mwezi Februari kila mwaka
Mijadala ya kupanga vipaumbele vya maendeleo.
Taarifa za utekelezaji Kutoshiriki kwa baadhi ya makundi katika mijadala
2 Utekekelezaji wa miradi maendeleo
Kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wakati i kila mwaka.
Miradi iliyokamilika na inaoendelea kutekelezwa.
Taarifa za hali ya utekelezaji miradi za kila robo na mwaka.
Kuchelewa kwa fedha tofauti na mpango kazi.
4 Kuuhisha mpango makakati wa wilaya
Kuanda Mpango Mkakati mwingine wa miaka mitano ( 2019- 2024).
Taarifa za utekelezaji Kuwepo kwa Mpango Mkakati wa Wilaya.
Ufinyu wa bajeti.
5 Kujenga uwezo. Kuwapatia mafunzo watumishi 4 waliopo ifikapo mwaka 2015.
Ushiriki wa watumishi katika mafunzo mbalimbali.
Watumishi wanaohitimu mafunzo. Bajeti finyu
6 Mawasiliano Kuimallisha mawaliano kwa njia ya elektoroniki ifikapo.
Kumlika kwa mawasiliano.
Taarifa ya utekelezaji Bajeti finyu
7 Takwimu Kukusanya takwimu sahihi kutoka kwenye idara ifikapo 2018
Kuwepo kwa takwimu mbalimbali
Taarifa ya uteke lezaji Bajeti finyu
130
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI.
ENEO LA HUDUMA: MIPANNGO
LENGO KUU: Kuratibu na kusimamia utekelezaji wa Mpango wa maendelei wa wilaya 2014 - 2018.
Lengo/ Mkakati Mhusika Muda wa utekelezaji. 2014 2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kuandaa Mpango wa Maendeleo wa Wilaya ifikapo mwezi Februari kila mwaka. Mikakati 1.Kuuhisha miradi ya kata 30 kutokana na vipaumbele vya O&OD kila mwaka.
A/Mipango
2. Kupitisha vipaumbele vya miradi ya maendeleo katika Kamati za Kudumu na Baraza kila mwaka
A/Mipango
3. Kuandaa na kuwasilisha hazina makala ya Mpango wa mwaka wa wilaya.
A/Mipango
Kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wakati kila mwaka. Mikakati . 1.Kufanya tathimini na ufuatiliaji utekelezaji wa miradi ya maendeleo kila robo mwaka.
A/Mipango
2.Kutangazo zabuni za kutekeleza kwa wakati kila mwaka.
A/Mipango
3. Kuandika taarifa za hali ya utekelezaji miradi ya maendeleo kwa kujaza fomu mbalimbali ( CDR,IFMS nk) kila robo mwaka.
A/Mipango
Kuanda Mpango Mkakati mwingine wa miaka mitano ( 2019- 2024). Mikakati.
131
Lengo/ Mkakati Mhusika Muda wa utekelezaji. 2014 2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
1.Kufanya Mkutano na Wakuu wa Idara /vitengo kwa siku 10 mwaka 2018
A/Mipango
2. Kuandaa makala ya Mpango kwa kushirikiana na Muwezeshaji Mshauri mwaka 2018.
A/Mipango
Kuwapatia mafunzo watumishi 4 waliopo ifikapo mwaka 2015. Mikakati 1. Kuwapatia mafunzo watumishi 4 kuhusu PlanRep 3 pamoja na Epicor ifikapo Juni 2015.
A/Mipango
Kuimallisha mawaliano kwa njia ya elektoroniki ifik apo2018. Mikakati. 1. Kuunganisha mtandao wa internet katika ofisi zote 12 za halmashauri ya wilaya ifikapo Juni 2017
A/Mipango
Kukusanya takwimu sahihi kutoka kwenye idara ifikapo 2018 Mikakati . 1. Kukusanya takwimu muhimu kutoka kwenye kata kwa kutumia fomu za LGMD kila mwaka.
A/Mipango
2. Kununua vitendea kazi kwa ajilia ya kitengo cha takwimu ifikapo 2015.
A/Mipango
132
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: MIPANGO
Lengo Mikakati MAKISIO YA GHARAMA Chanzo cha fedha 2014 2015 2016 2017 2018 Jumla
1.Kuandaa mpango wa maendeleo wa wilaya ifikapo mwezi Februari kila mwaka.
Kuuhisha miradi ya kata 30 kutokana na vipaumbele vya O&OD kila mwaka. Kupitisha vipaumbele vya miradi ya maendeleo katika Kamati za Kudumu na Baraza kila mwaka. Kuandaa na kuwasilisha hazina makala ya Mpango wa mwaka wa wilaya.
12,000,000 25,000,000 20,000,000
14,000,000
14,000,000 14,000,000 14,000,000 69,000,000 25,000,000 20,000,000
Kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wakati kila mwaka.
Kufanya tathimini na ufuatiliaji utekelezaji wa miradi ya maendeleo kila robo mwaka. Kutangazo zabuni mbalimbali za miradi. Kuandika taarifa za hali ya utekelezaji miradi ya maendeleo kwa kujaza fomu mbalimbali ( CDR,IFMS nk) kila robo mwaka.
85,000,000 5,000,000 12,000,000
90,000,000 6,000,000 12,500,000
90,000,000 15,000,000
90,000,000 7.000,000 15,000,000
90,000,000 15,000,000
445,000,000 18,000,000 15,000,000
Kuanda Mpango Mkakati mwingine wa miaka mitano ( 2019-
Kukusanya takwimu na kufanya Mkutano wa Wadau ifikapo mwezi Juni
0
0
0
5,000,000
5,000,000
133
Lengo Mikakati MAKISIO YA GHARAMA Chanzo cha 2024). 2018
Kuahinisha malengo ,mikaati na gharama za kila lengo iikapo juni 2018
Kuwapatoa mafunzo watumishi 4 waliopo ifikapo mwaka 2015.
Kufanya mafunzo kuhusu IFMS kwa watumishi 4 ifikapo Juni 2015.
15,000,000 14,000,000 29,000,000
Kuimallisha mawaliano kwa njia ya elektoroniki ifikapo2018.
Kuunganisha mtandao wa internet katika ofisi zote 12 za halmashauri ya wilaya ifikapo Juni 2017
25,000,000
15,000,000 40,000,000
Kukusanya takwimu sahihi kutoka kwenye idara ifikapo 2018
Kukusanya takwimu muhimu kutoka kwenye kata kwa kutumia fomu za LGMD kila mwaka. Kununua vitendea kazi kwa ajilia ya kitengo cha takwimu ikapo 2015.
12,000,000 15,000,000
15,000,000 15,000,000
15,000,000 57,000,000 15,000,000
JUMLA 9,000,000 48,500,000 208,000,000 186,000,000 184,000,000 685,500,000
134
ENEO LA HUDUMA : FEDHA LENGO KUU: Kusimamia mapato na matumizi ya fedha kwa kuzingatia kanuni na taratibu za fedha. NO. ENEO LA
MATOKEO LENGO MAHSUSI/MKAKATI VIASHIRIA VYA
UTEKELEZAJI CHANZO CHA
UHAKIKI DHANA
1 Ukusanyaji wa mapato Kuongeza ukusanyaji wa mapato kutoka asilimia 90 hadi 100. - kutumia mawakala - kuainisha vyanzo vingine vya mapato.
Kiasi cha mapato kilichokusanywa
Taarifa za utekelezaji
Mawakala makini, kuwepo kwa fedha
2 Kanuni na taratibu za fedha
Kuimarisha utekelezaji wa kanuni na taratibu za fedha - Kuweka fedha benki kila siku punde tu zinapokusanywa - Ufungaji wa hesabu kwa wakati - Kuwa na chumba maalumu (strong room) cha kuhifadhia nyaraka za fedha. - Kusimamia matumizi ya fedha kwa kuzingatia taratibu na kanuni za fedha
Stakabadhi na benki pay in slip Vitabu vya mahesabu uwepo wa kasiki Nyaraka za fedha.
Taarifa za fedha kutoka kwa muhasibu, Taarifa za kibenki (bank statement) taarifa ya mkaguzi, hati safi
kufanya kazi kulingana na mpango kazi, kuwepo kwa watumishi wenye sifa. Kuwepo kwa miongozo ya fedha.
3 Mazingira bora ya kufanyia kazi
Kuimarisha mazingira bora ya kufanyia kazi -Kununua vitendea kazi, kompyuta, photocopy, printa, scanner -Ununzi wa pikipiki 3 -ununuzi wa samani
Kompyuta na photocopy vimenunuliwa Pikipiki zimenunuliwa
Uwepo kompyuta photocopy, printa Uwepo wa pikipiki 3
Uwepo wa fedha
4 Kujenga uwezo Wahasibu 6 wanapata mafunzo hadi kufikia mwaka 2018
Idadi ya watumishi watakaopata mafunzo
vyeti Uwepo wa fedha
5 Taarifa za mkaguzi wa nje
Kuondoa hoja za ukaguzi, kujibu hoja kwa wakati.
Kutokuwepo na hati chafu Hati safi Watumishi wenye sifa
6 Huduma kwa wateja Kutoa huduma kwa wakati Kupungua kwa malalamiko
Taarifa za utekelezaji
Utayari wa watoa huduma
136
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI ENEO LA HUDUMA : FEDHA LENGO KUU: Kusimamia mapato na matumizi ya fedha kwa kuzingatia kanuni na taratibu za fedha. Eneo la Matokeo Muhimu
Mkakati Mhusika Muda wa utekelezaji
2014 2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Ukusanyaji wa mapato
Kuongeza ukusanyaji wa mapato kutoka asilimia 90 hadi 100. - kutumia mawakala - kuainisha vyanzo vingine vya mapato.
DT, Afisa biashara
Kanuni na taratibu za fedha
- Ufungaji wa hesabu kwa wakati
DT na Wahasibu wote
- Kuwa na chumba maalumu (strong room) cha kuhifadhia nyaraka za fedha.
DED
Mazingira bora ya kufanyia kazi
Kununua vitendea kazi, kompyuta, photocopy, printa, scanner
Afisa manunuzi
Ununzi wa pikipiki 3 na samani
Afisa manunuzi
Kujenga uwezo Wahasibu 6 wanapata mafunzo hadi kufikia mwaka 2018
Wahasibu
Taarifa ya mkaguzi wa nje
Kutokuwepo na hati chafu Wahasibu, DT, wakuu wa idara na DED
137
Eneo la Matokeo Muhimu
Mkakati Mhusika Muda wa utekelezaji
2014 2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Huduma kwa wateja
Kutoa huduma kwa wakati
Watumishi wote wa idara ya fedha
138
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI ENEO LA HUDUMA: FEDHA Lengo Mkakati Makisio ya gharama
2014 2015 20116 20/17 20/18 JUMLA CHANZO CHA FEDHA
Ukusanyaji wa mapato kutumia mawakala kuainisha vyanzo vingine vya mapato.
15,000,000 18,000,000 20,000,000 21,000,000 25,000,000 99,000,000 Halmashauri
Kanuni na taratibu za fedha
Ufungaji wa hesabu kwa wakati
20,000,000 23,000,000 25,000,000 26,000,000 28,000,000 122,000,000 Halmashauri
Kuwa na chumba maalumu (strong room) cha kuhifadhia nyaraka za fedha.
150,000,000 150,000,000 Halmashauri
Mazingira bora ya kufanyia kazi
Kununua vitendea kazi, kompyuta, photocopy, printa, scanner
7,000,000 10,000,000 11,000,000 28,000,000 Halmashauri
Ununzi wa pikipiki 3 na samani
2,200,000 12,500,000 23,000,000 25,000,000 62,700,000 Halmashauri
Kujenga uwezo Wahasibu 6 wanapata mafunzo hadi kufikia mwaka 2018
10,000,000 12,000,000 14,000,000 15,000,000 16,000,000 67,000,000 Halmashauri
Taarifa ya mkaguzi wa nje
Kufanyia kazi taarifa za mkaguzi wa ndani ili kusiwepo na hati chafu
15,000,000 17,000,000 20,000,000 22,000,000 25,000,000 99,000,000 Halmashauri
Huduma kwa wateja Kutoa huduma kwa wakati
JUMLA 69,200,000 232,500,000 112,000,000 109,000,000 105,000,000 627,700,000
139
MPANGO MKAKATI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TANDAHIM BA 2014-2018 ENEO LA HUDUMA : BIASHARA LENGO KUU: Kuchochea Maendeleo na kasi ya ukuaji wa biasshara ,kuinua uwezo wa ushindani ili kuongeza kasi ya maendeleo ya kijamii ,kiuchumi na kuondoa umasikini kufikia 2018 NO. ENEO LA
MATOKEO LENGO MAHSUSI VIASHIRIA VYA
UTEKELEZAJI CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
1 Leseni za Biashara wafanyabiashara 600 wanatambuliwa na kupewa leseni - Usajili wa wafanyabiashara - mafunzo kwa wafanyabiashara
idadi ya wafanyabiashara
Taarifa za utekelezaji
uwepo wa fedha
2 Ushuru wa masoko Kupandisha kiwango cha ukusanyaji wa ushuru kutoka 80% hadi 100% -Kuanzusha maeneo mapya ya kufanyia biashara -Kurejea viwango vya kukusanyia ushuru - Ujenzi wa stendi kuu ya mabasi
idadi ya Mikataba iliyorejewa
Taarifa za utekelezaji
uwepo wa fedha na wafanyabiashara
140
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: BIASHARA Lengo Mkakati Mhusika Muda wa utekelezaji
2014 2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Leseni za Biashara Usajili wa wafanyabiashara
Afisa biashara
Mafunzo kwa wafanyabiashara
Ushuru wa masoko Kurejea viwango vya kukusanyia ushuru
DED
Ujenzi wa stendi kuu ya mabasi
DED
141
ENEO LA HUDUMA IDARA YA MAENDELEO YA JAMII, USTAWI WA JAMII NA VIJANA
LENGO KUU: Kuweka usawa wa kijinsia katika ukuaji wa kiuchumi, uwajibikaji, na kupunguza umasikini ili kuboresha maisha jamii kwa kutumia rasilimali zilizopo ifikapo 2018
ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI/ MKAKATI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
1 Vikundi vya wanawake na vijana
Kuongeza uhakiki vikundi vya kiuchumi vya wanawake na vijana kutoka 77 hadi 120 ifikapo 2018
Idadi ya vikundi vya wanawake vilivyo hakikiwa
Taarifa kutoka dawati la wanawake
Upatikanaji wa rasilimali fedha na mahitaji ya kikundi
Kuongeza kipato cha kiuchumi kwa vikundi vya ujasiliamali vya wanawake na vijana vinavyopewa mkopo wa kutoka 16 hadi 32 ifikapo 2018
Idadi ya vikundi vya wanawake na vijana vilivyopewa mkopo
Taarifa kutoka dawati la wanawake na vijana
Upatikanaji wa rasilimali fedha
Kuongeza idadi ya vikundi vya ujasiliamali kushiriki maonyesho ya biashara kutoka 4 hadi 14 ifikapo 2018
Idadi ya vikundi vitakavyo shiriki
Taarifa dawati la jinsia Upatikanaji wa mapato
2 Kujenga uwezo
Kuongeza idadi ya watumishi wa idara kutoka 16 waliopo hadi 39 ifikapo 2018
Idadi ya watumishi watakao ajiriwa
Taarifa kutoka idara ya utumishi
Upatikanaji wa kibali cha ajira
3 makundi maalum
Kuongeza vituo vya kulelea watoto wadogo umri(3-5),kutoka kituo 1cha sasa hadi vituo 4 ifikapo 2018
Kuwepo kwa vituo Taarifa ya vituo Upatikanaji wa fedha
Utayari wa jamii
Kuzijengea uwezo kamati za kuhudumia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi 75 kati ya 157 zilizopo ifikapo 2018
Idadi ya kamati zitakazojengewa uwezo
Taarifa ya utekelezaji Uwepo wa fedha na utayari wa jamii
142
ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI/ MKAKATI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
Kuanzisha mfuko wa kuhudumia makundi maalum ifikapo 2018
Kuwepo kwa mfuko Taarifa ya mfuko Utayari wa jamii katika kuchangia na upatikanaji wa fedha
Kuanzisha baraza la wazee ifikapo 2018 Kuwepo kwa baraza Taarifa ya utekelezaji Utayari wa jamii katika kuchangia na upatikanaji wa fedha
Takwimu Kuhuisha takwimu za makundi maalum ifikapo 2018
Kuwepo kwa takwimu mpya za makundi maalum
Kuwepo kwa takwimu Upatikanaji rasilimali fedha
Mfuko wa afya ya jamii
Kuwezesha makundi maalum 4 kujiunga na mfuko wa afya ya jamii(CHF) ifikapo 2018
Idadi ya makundi yatayojiunga na mfuko wa afya kwa jamii(CHF
Kuwepo kwa mfuko Uamasikaji wa jamii pamoja na kuwepo kwa fedha
Kutambua na kuwatoa wafungwa wanaostahili kutumikia kifungo cha nje kutoka 10 wa sasa hadi 100 ifikapo 2018
Idadi ya wafungwa watakao tambuliwa na kutolewa
Taarifa kutoka magereza,mahakamani na ofisi kitengo cha ustawi
Kuwepo kwa fedha na ushirikiano na jamii
Ndoa na familia
Kuimarisha ndoa na familia katika vijiji 121 kati ya vijiji 157 vilivyopo ifikapo 2018
Idadi ya vijiji vitavyopatiwa elimu.
Taarifa ya mafunzo kutoka kitengo cha ustawi
Kuwepo kwa fedha na ushirikiano na jamii
4 Virus vya UKIMWI UKIMWI
Kuendeleza mapambano dhidi ya maambukizo mapya ya vvu na UKIMWI katika vijiji 157 na kata 30 ifikapo 2018
Idadi ya maeneo yatakayo tembelewa
Taarifa ya utekelezaji Upatikanaji wa fedha
143
ENEO LA HUDUMA: IDARA YA MAENDELEO YA JAMII, USTAWI WA JAMII NA VIJANA
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
Lengo Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezaji 2014 2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
Kuongeza uhakiki wa vikundi vya kiuchumi vya wanawake na vijana kutoka 77 hadi 120 ifikapo 2018
Kutoa elimu sahihi ya ujasiliamali kwa wanawake na vijana kutoka 20 vya sasa hadi 120 ifikapo 2018
DCDO/WID �
Kuongeza kiasi cha fedha ya mikopo kwa vikundi kutoka 30milioni hadi 100milioni ifikapo 2018
DCDO/TACOBA
Kuongeza idadi ya vikundi vya ujasiliamalia kushiriki maonyesho ya biashara kutoka 4 hadi 14 ifikapo 2018
DCDO/WID
Kuajiri watumishi wa idara wenye sifa 23 ifikapo 2018
DHRO
Kuwepo kwa mpango wa idara unaonyesha bajeti y a watumishi 2 kwa kila mwaka hadi ifikapo 2018
DCDO/DPLO
Kuhakikisha idara inaweka kwenye bajeti watumishi 10 watakaojiendeleza ifikapo 2018
DCDO
Kuboresha huduma za idara ifikapo 2018
Kuongeza idadi ya watumishi wanaojiendeleza kitaaluma kutoka 3 wa sasa hadi 6 ifikapo 2018
DCDO/DPO
Kununua vitendea kazi na DCDO/DPLO
144
Lengo Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezaji 2014 2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
vitendea kazi kwa kununua vifaa vya ofisi,printer,photocopy machinery,laptop,thamani za ofisi ifikapo 2018 Ununuzi gari moja la idara ifikapo 2015
DED
Kuboresha huduma katika kuhudumia makundi 4 maalum yaliyopo ifikapo 2018
Kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu kwa kuhudumia makundi maalum katika tarafa tatu zilizopo ifikapo 2018
DSWO/DCDO
Kutoa elimu kwa jamii namna ya kuchangia mfuko wa makundi maalum katika vijiji 157 vilivyopo ifikapo 2018
SWO/DCDO
Kuzijengea uwezo kamati za kuhudumia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi 75 kati ya 157 zilizopo ifikapo 2018
SWO/DCDO
Kuanzisha baraza la wazee 1 ifikapo 2018
DSWO
Kuwezesha makundi maalum 4 kujiunga na mfuko wa afya ya jamii(CHF) ifikapo 2018
MRATIBUCHF/SWO
Kuhuisha takwimu za makundi maalum ifikapo 2018
DSWO
Kutambua na kuwatoa wafungwa kutumikia kifungo cha nje kutoka 10 wa sasa hadi
DSWO
145
Lengo Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezaji 2014 2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
100 ifikapo 2018 Kutoa elimu juu ya ndoa na familia katika vijiji 121 kati ya vijiji 157 vilivyopo ifikapo 2018
DSWO
Kuendeleza mapambano dhidi ya maambukizo mapya ya vvu na UKIMWI katika vijiji 157 na kata 30 ifikapo 2018
Kutoa mafunzo kwa kamati za UKIMWI za kata 15 kati 30 zilizopo ifikapo 2016
CHAC/DAC/DCDO
Kuendelea kuwezesha vikao 4 vya mwaka vya kamati ya kupambana na virus vya ukimwi na UKIMWI ya wilaya
CHAC
Kutoa elimu ya kujikinga maambukizo ya virus vya ukimwi na UKIMWI kwa vijana kutoka 450 waliopata elimu hadi 900 ifikapo 2017
CHAC/DAC
Kuhamasisha upimaji wa vvu kwa hiari katika kata 8 kati ya 30 ifikapo 2015
CHAC/DAC
Kutoa mafunzo kwa nghariba 60 wa sasa hadi 120 ifikapo 2015
CHAC/DAC
Kuhamasisha watu waishio na virus vya UKIMWI kujiunga katika vikundi 20 vilivyopo kwa sasa ifikapo 2018
CHAC/DCDO
Kuongeza idadi ya vikundi vya watu wanaoishi na vvu vinavyopewa fedha za miradi
CHAC/DSWO
146
Lengo Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezaji 2014 2015 2016 2017 2018 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
18 vya sasa hadi 36 ifikapo 2018 Kuongeza idadi ya watoto yatima wanaosaidiwa sare na vifaa vya shule kutoka 50 hadi 100 ifikapo 2018
CHAC/DSWO
Kuhuisha takwimu za watoto wanaoishi na vvu kutoka 32 waliopo ifikapo2018
CHAC
Kuzijengea uwezo kamati za kupambana na vvu na UKIMWI ngazi ya vijiji 157 zilizopo ifikapo 2018
CHAC
Kuongeza idadi ya makundi yanayohitaji msaada wa chakula kutoka 30 ya sasa ifikapo 2018
CHAC/DAC
Kuwajengea uwezo wahudumu wa wagonjwa wa UKIMWI wa majumbani 52 waliopo kwa sasa ifikapo 2018
CHAC/DAC
Kuimarisha mashirika yasiyoyaserikali 22 yaliyopo kwa sasa ifikapo 2015
Kutoa elimu ya usimamizi wa Asasi za kiraia kwa viongozi wa Asasi 22 zilizopo ifikapo 2015
DCDO
Kuhamasisha vikundi vya ujasiliamali 1200 kujiunga katika mtandao wa Asasi wa wilaya(TANGONET) ifikapo juni 2014
DCDO
148
MAKISIKIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI WA IDARA YA MAE NDELEO YA JAMII, USTAWI YA JAMII NA VIJANA MWAKA 2014/ 2018
LENGO MKAKATI MAKISIO YA GHARAMA 2014 2015 2016 2017 2018 Jumla CHANZO
CHA PESA Kuongeza uhakiki wa vikundi vya kiuchumi vya wanawake na vijana kutoka 77 hadi 120 ifikapo 2018
Kutoa elimu sahihi ya ujasiliamali kwa vikundi vya wanawake na vijana kutoka 20 vya sasa hadi 120 ifikapo 2018
2,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,00 10,000,000 DED, Wizara ya maendelao ya jamii.
Kuongeza kiasi cha fedha ya mikopo kwa vikundi kutoka 30milioni hadi 100milioni ifikapo 2018
20,000,000 20,000,000 20,000,000 20,000,000 20,000,000 100,000,000 DED,Wizara ya maendelao ya jamii
Kuongeza idadi ya vikundi vya ujasiliamalia kushiriki maonyesho ya biashara kutoka 4 hadi 14 ifikapo 2018
2,500,000 2,5000,000 2,500,000 2,500,000 2,500,000 12,500,000 DED,Wizara ya maendelao ya jamii
Kuajiri watumishi wa idara wenye sifa 23 ifikapo 2018
5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000, 5,000,000 25,000,000 DED
Kuwepo kwa mpango wa idara unaonyesha bajeti y a watumishi 2 kwa kila mwaka hadi ifikapo 2018
12,000,000 12,000,000 12,000,000 12,000,000 12,000,000 60,000,000 DED
Kuhakikisha idara inaweka kwenye bajeti watumishi 10 watakaojiendeleza ifikapo 2018
500,000 500,000 500,000 500,000 500,000 2,500,000 DED
Kuboresha huduma za idara ifikapo 2018
Kuongeza idadi ya watumishi wanaojiendeleza kitaaluma kutoka 3 wa sasa hadi 6 ifikapo 2018
6,000,000 6,000,000 6,000,000 6,000,000 6,000,000 30,000,000 DED
Kununua vitendea kazi vya 14,000,000 - - - - 14,000,000 DED
149
LENGO MKAKATI MAKISIO YA GHARAMA 2014 2015 2016 2017 2018 Jumla CHANZO
CHA PESA ofisi, printer,photocopy machinery, laptop, saamani za ofisi ifikapo 2018 Ununuzi wa gari moja la idara ifikapo 2015
- 75,000,000 - - - 75,000,000 DED
Kuboresha huduma katika kuhudumia makundi 4 maalum yaliyopo ifikapo 2018
Kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa kuhudumia makundi maalum katika tarafa tatu zilizopo ifikapo 2018
500000 500000 500000 500000 500000 2,500,000 DED
Kutoa elimu kwa jamii namna ya kuchangia mfuko wa makundi maalum katika vijiji 157 vilivyopo ifikapo 2018
800,000 800,000 800,000 800,000 800,000 40,000,000 DED
Kuzijengea uwezo kamati za kuhudumia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi 75 kati ya 157 zilizopo ifikapo 2018
1,500,000 1,500,000 1,500,000 1,500,000 1,500,000 7,500,000 DED
Kuanzisha baraza la wazee 1 ifikapo 2016
- - 10,000,000 - - 10,000,000 DED
Kuwezesha makundi maalum 4 kujiunga na mfuko wa afya ya jamii(CHF) ifikapo 2018
5,000,000 10,000,000 10,000,000 20,000,000 20,000,000 65,000,000 DED
Kuhuisha takwimu za makundi maalum ifikapo 2018
5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000 25,000,000 DED
Kutambua na kuwatoa wafungwa kutumikia kifungo cha nje kutoka 10 wa
2,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,000 10,000,000 DED
150
LENGO MKAKATI MAKISIO YA GHARAMA 2014 2015 2016 2017 2018 Jumla CHANZO
CHA PESA sasa hadi 100 ifikapo 2018 Kutoa elimu juu ya ndoa na familia katika vijiji 121 kati ya vijiji 157 vilivyopo ifikapo 2018
1,000,000 1,000,000 1,000,000 1,000,000 1,000,000 5,000,000 DED
Kuendeleza mapambano dhidi ya maambukizo mapya ya vvu na UKIMWI katika vijiji 157 na kata 30 ifikapo 2018
Kutoa mafunzo kwa kamati za UKIMWI za kata 15 kati 30 zilizopo ifikapo 2016
4,200,000 4,200,000 4,200,000 - - 12,600,000 DED/ TACAIDS
Kuendelea kuwezesha vikao 4 vya mwaka vya kamati ya kupambana na virus vya ukimwi na UKIMWI ya wilaya
5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000 25,000,000 DED TACAIDS
Kutoa elimu ya kujikinga maambukizo ya virus vya ukimwi na UKIMWI kwa vijana kutoka 450 waliopata elimu hadi 900 ifikapo 2017
4,000,000 4,000,000 4,000,000 4,000,000 16,000,000 DED/ TACAIDS
Kuhamasisha upimaji wa vvu kwa hiari katika kata 8 zilizobaki kati ya 30 ifikapo 2015
3,000,000 3,000,000 - - - 6,000,000 DED/ TACAIDS
Kutoa mafunzo kwa nghariba 60 wa sasa hadi 120 ifikapo 2015
5,000,000 5,000,000 - - - 10,000,000 DED/TACAIDS
Kuhamasisha watu waishio na virus vya UKIMWI kujiunga katika vikundi 20 vilivyopo kwa sasa ifikapo 2018
3,000,000 3,000,000 3,000,000 3,000,000 3,000,000 15,000,000 DED/ TACAIDS
Kuongeza idadi ya vikundi 5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000 25,000,000 DED/
151
LENGO MKAKATI MAKISIO YA GHARAMA 2014 2015 2016 2017 2018 Jumla CHANZO
CHA PESA vya watu wanaoishi na vvu vinavyopewa fedha za miradi 18 vya sasa hadi 36 ifikapo 2018
TACAIDS
Kuongeza idadi ya watoto yatima wanaosaidiwa sare na vifaa vya shule kutoka 50 hadi 100 ifikapo 2018
7,000,000 7,000,000 7,000,000 7,000,000 7,000,000 35,000,000 DED/ TACAIDS.
Kuhuisha takwimu za watoto wanaoishi na vvu kutoka 32 waliopo ifikapo2018
4,000,000 4,000,000 4,000,000 4,000,000 4,000,000 20,000,000 DED/ TACAIDS
Kuzijengea uwezo kamati za kupambana na vvu na UKIMWI ngazi ya vijiji 157 zilizopo ifikapo 2018
5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000 5,000,000 25,000,000 DED/ TACAIDS,
Kuongeza idadi ya makundi yanayohitaji msaada wa chakula kutoka 30 ya sasa ifikapo 2018
2,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,000 10,000,000 DED/ TACAIDS
Kuwajengea uwezo wahudumu wa wagonjwa wa UKIMWI wa majumbani 52 waliopo kwa sasa ifikapo 2018
1,000,000 1,000,000 1,000,000 1,000,000 1,000,000 5,000,000 DED/ TACAIDS
Kuimarisha mashirika yasiyoyaserikali 22 yaliyopo kwa sasa ifikapo 2015
Kutoa elimu ya usimamizi wa Asasi za kiraia kwa viongozi wa Asasi 22 zilizopo ifikapo 2015
500,000 500,000 500,000 500,000 500,000 2,500,000 DED/ WAHISANI.
Kuhamasisha vikundi vya ujasiliamali 1200 kujiunga katika mtandao wa Asasi wa
1,000,000 - - - 1,000,000 DED/ WAHISANI .
152
LENGO MKAKATI MAKISIO YA GHARAMA 2014 2015 2016 2017 2018 Jumla CHANZO
CHA PESA wilaya(TANGONET) ifikapo juni 2014
JUMLA 127,500,000 215,000,000 119,500,000 110,300,000 109,300,000 688,100,000
153
ENEO LA HUDUMA: AFYA
Lengo Kuu: Kutoa huduma bora za afya kwa Wananchi
ENEO LA MATOKEO LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
Huduma za mama na watoto Huduma muundo mbinu
Kupunguza Vifo vya mama wajawazito kutoka14 hadi 10 ifikapo juni 2018
Idadi ya wajawazito walio fariki
Taarifa za wajawazito walio jifungua kwenye vituo vya kutolea huduma na kwenye jamii
Upatikanaji wa fedha
Kuongeza kiwango cha chanjo kwa wajawazito na watoto chini ya miaka 5 kutoka 80% hadi 100% ifikapo juni 2018
Idadi ya watoto chini ya miaka 5 waliopata chanjo SURUA, PEPOPUNDA KIFUA KIKUU
Taarifa ya idadi ya watoto waliopata chanjo
Upatikanaji wa fedha Dawa za chanjo watumishi
Kupunguza vifo vya watoto wachanga kutoka 40 hadi 20 iflkapo juni 2018
Idadi ya watoto wachanga walio fariki
Taarifa ya watoto wa changa walio fariki kutoka kwenye jamii na vituo vya kutolea huduma
Upatikanaji wa fedha Dawa za chanjo watumishi
Kuongeza matumizi ya dawa za uzazi wa mpano toka asilimia 65 hadi 75 ifikapo juni 2018
Idadi ya akina mama waliojiunga uzazi wa mpango
Taarifa ya wateja walio jiunga na uzazi wa mpango
Upatikanaji wa fedha Dawa za chanjo watumishi
Kupunguza idadi yakina mama wanao jtfungulia nyumbani toka asilimia 48 hadi 40 ifikapo juni 2018
Idadi ya akina mama waliojifungulia nyumbani
Taarifa ya akina mama walio jifungulia kwenye vituo vya kutolea huduma na nyumbani
Upatikanaji wa fedha watumishi
Kuongeza asilimia ya watoto wanaopata Vit A toka 89 hadi 95 ifikapo juni 2018
Idadi ya watotp waliopata Vit A
Taarifa ya watoto walio pata Vit A
Upatikanaji wa fedha Dawa za chanjo watumishi
kuongeza idadi ya Zahanati kutoka 30 hadi 40 ifikapo juni 2018
zahanati zilizojengwa Taarifa za ujenzi wa zahanati
Upatikanaji wa fedha
154
ENEO LA MATOKEO LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
Kufanya ukarabati wa zahanati 14 ifikapo juni 2018
Ukarabati wa zahanati 14 Taarifa ya ukarabati wa zahanati
Upatikanaji wa fedha
Mpango wa utunzaji wa majengo uwe umeandaliwa ifikapo juni 2018
Idadi ya majengo ya lio kwenye mpango
Taarifa ya majengo yalio kwenye mpango
Upatikana wa fedha
Upatikanaji wa Dawa na vifaa Tiba ifikapo juni 2018
Uwepo wa dawa na vifaa tiba kwenye vituo vya kutolea huduma
Taarifa za Dawa kwenye Zahanati na vituo vya Afya
Upatikanaji wa fedha Watumishi
MAGONJWA YA KUAMBUKIZA
Kupunguza maambukizo ya UKIMWI toka asilmia 3 hadi 1 lfikapo juni 2018
Idadi ya watwalio pimwa virusi vya ukimwi
Taarifa ya waliopimwa na kugunduliwa kuwa wana virusi vya ukimwi
Upatikanaji wa fedha
Kuongeza vituo vya kutolea huduma ya kupatika kwa dawa za ARV toka 12 hadi 20 ifikapo juni 2018
Idadi ya vituo vilivyo ongezeka
Taarifa ya vituo vinavyo toa huduma
Upatikanaji wa fedha Watumishi
Kupunguza vifo vinavyo sababishwa na Malaria toka 51 hadi 30 ifikapo juni 2018
Idadi ya watu waliougua ugojwa wa malaria
Taarifa kutoka vituo vya kutolea huduma
Upatikanaji wa fedha Watumishi
MAGONJWA YA SIO PEWA KIPAUMBELE
Kuongeza idadi ya watu
wanaomeza dawa za kuzuia
maambukizo toka 80% hadi
90%yatmagonjwa VIKOPE
KICHOCHO
Idadi ya wananchi waliopata dawa za KICHOCHO VIKOPE
Idadi ya waliopata dawa KICHOCHO VIKOPE
Upatikanaji wa fedha Watumishi
Kupunguza maambukizo ya ugonjwa wa kukoma kutoka 24 hadi 8 ifikapo juni 2018
Idadi ya walio ugua ugonjwa wa ukoma
Taarifa za waliougua ugonjwa wa ukoma kutoka kwenye vituo vya kutolea huduma
Upatikanaji wa fedha Watumishi
Huduma za mkundi Kuongeza idadi watoto Idada ya watoto watakao Taarifa toka ofisi ustawi Upatikanaji wa fedha
155
ENEO LA MATOKEO LENGO MAHUSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
maalumu katika Jamii waopatia lishe bora watoto 32 hadi 50 wanaoishi na VVU Ifikapo juni 2018
hudumiwa wa jamii
Kuwapatia kadi za CHF wazee 500 Ifikapo juni 2018
Idadi ya wazee waliopata kadi za CHF
Taarifa toka ofisi ya ustawi wa jamii
Upatikanaji wa fedha
KUJENGA UWEZO Kuwajengea uwezo wafanyakazi 20 hadi 100 ifikapo juni 2018
Idadi ya wafanyakazi walio pata nafasi za masomo ya kujiendeleza
Taarifa za wafanya kazi waliorudi masomoni
Upatikanaji wa fedha
Kuhakisha watumishi wanalipwa stahili zao ifikapo juni 2018
Idadi ya watumishi wolio lipwa stahili zao
Taarifa za idadi ya watumishi waliolipwa stahili zao
Upatikanaji wa fedha
Idadi ya watumishi walio ajiriwa kwa kada
Utawala ufafanisi na upatikanaji wa vitendea kazi na dawa
Bodi ya Afya ya wilaya ,kamati za CHF Ziwe zimezina fanya kazi ifikapo juni 2018
Idadi ya kamati za CHF Zinazofanyakazi
Taarifa za CHF Toka kwenye vituo vya kutolea huduma
Upatikanaji wa fedha
Vitendea kazi na Dawa ziwe ziwezinapatikana ifikapo june 2018
Idadi ya vituo vilivyo pata na vitedea kazi
Taarifa ya vituo vilivyo pata dawa na vitendea kazi
Upatikanaji wa fedha Watumishi
156
ENEO LA HUDUMA: AFYA
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
Lengo Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezaji 2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 Kupunguza Vifo vya mama wajawazito kutoka14 hadi 10 ifikapo juni 2018
Kufanya ufutiliaji kwenye kata 30 kuanzisha mfuko wa matibabu ya dharura
DMO
Kufanya mikutano ya kujadili vifo vya mama wajawazito na watoto
DMO
Maadhimisho ya siku ya unyonyeshaji Duniani
DMO
Kufanya kampeni ya utowaji wa dawa za minyoo na Vit A
DMO
Kufanya huduma za Mkoba kwenye maeneo ambayo ni vigumu kufikika
DMO
Kuanzimisha siku ya chanjo Duniani
DMO
Kuanzisha kamati za ufuatilia wa vifo kwenye tarafa 3
DMO
Kufanya uhamasishaji wa jamii dhidi umuhimu wa uzazi wa mpango
DMO
Kuongeza idadi ya zahanati toka 30 hadi 40 ifikapo juni 2018
Ujenzi wa zahanati 2`
Kufanya ukarabati wa Ukarabati wa zahanati DMO
157
Lengo Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezaji 2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 zahanati 14 ifikapo juni 2019 Upatikanaji wa Dawa na vifaa Tiba
Uwepo wa dawa na vifaa tiba kwenye vituo vya kutolea huduma
DMO
Kupunguza maambukizo ya UKIMWI toka asilmia 3 hadi 1 lfikapo juni 2019
Kuwepo na mafunzo ya uzazi salama kwa watoa huduma
DMO
Mafunzo rejea ya kuzuia maambukizo VVU toka kwa mama kwenda kwa mtoto
DMO
Kufanya mikutano kila robo na watenda kujadili mambo ya liofanyka kwenye vituo vya kutolea huduma
DMO
Kusafirisha sampuli za damu kutoka kwenye vituo vya kutolea huduma
DMO
Ununuzi wa vitendanishi na kuvisabaza kwenye vituo vya kutolea huduma
DMO
Kuhamasisha jamii umuhi wa kupima VVU kwa wajawazito na weziwao
DMO
Kufanya usimamizi shirikishi kila robo mwaka
DMO
Kuadhimisha siku ya UKIMWI duniani
DMO
158
Lengo Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezaji 2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 Kuongeza vituo vya kutolea huduma ya kupatika kwa dawa za ARV toka 12 hadi 20 ifikapo juni 2019
Kutoa ya Mafunzo ya matumizi ya ARV Kwa watumishi
DMO
Kuhakikisha upatikanaji wa dawa za ARV Katika vituo vya kutolea huduma
DMO
Kuongeza idadi ya watu wanaomeza dawa za kuzuia maambukizo toka 80% hadi 90% ifikapo juni 2018
Kufanya kampeni kila mwaka kwenye jamii kuhimiza umuhimu kumeza dawa
DMO
Kuongeza idadi watoto waopatia lishe bora watoto 32 hadi 50 wanaoishi na VVU Ifikapo juni 2018
DMO
Kuwajengea uwezo wafanyakazi 20 hadi 100 ifikapo juni 2018
DMO
Kuhakisha watumishi wanalipwa stahili zao ifikapo juni 2018
DMO
Bodi ya Afya ya wilaya ,kamati za CHF Ziwe zinfanya kazi ifikapo juni 2018
DMO
Vitendea kazi na Dawa ziwe ziwezinapatikana
DMO
159
Lengo Mkakati Mhusika Muda wa Utekelezaji 2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 ifikapo june 2018
160
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: AFYA
Lengo MAKISIO YA GHARAMA Chanzo cha fedha
2014 2015 2016 2017 2018 Jumla
1. Huduma za mama na watoto 131,281,500 140,300,500 145,440,600 150,300,000 155,400,000 722,722,600
2.Huduma muundo mbinu 178,000,000 200,000,000 250,330,000 300,100,000 350,450,100 1,278,880,100 3. Magonjwa ya kuambukiza 74,444,952 80,500,000 94,500,000 120,000,000 130,000,000 499,444,952 4. Magonjwa ya sio pewa kipaumbele 36,300,100 40,200,000 45,500,000 50,200,000 55,300,000 227,500,100 5. Kuboresha huduma za mkundi maalumu katika Jami
2,733,000 3,500,000 4,000,000 4,500,300 5,500,000 20,233,300
7.Lengokuwajengea uwezo wafanyakazi
3,091,793,976 3,500,000,000 4,300,100,000 5,200,900,000 16,092,793,976
8.LengoUtawala ufanisi na upatikanaji wa vitendea kazi na Dawa
408,671,408 408,671,408
JUMLA 3,923,224,936 3,964,500,500 4,839,870,600 5,826,000,300 696,650,100 19,250,246,436
161
ENEO LA HUDUMA: IDARA YA UTAWALA NA UTUMISHI
Lengo Kuu: Kuboresha huduma za kiutumishi kwa watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Tandahimba ifikapo mwaka 2018.
ENEO LA MATOKEO
LENGO KUU
VIASHIRIA
VYANZO VYA UHAKIKI
DHANA
Mafunzo kwa watumishi
Kutoa mafunzo kwa watumishi wa kada mbalimbali katika idara za Halmashauri 13 na vitengo 6 ifikapo 2018
Idadi ya watumishi waliopata mafunzo:
Watumishi 15 idara ya Elimu Msingi wamepata shahada ya Elimu Ualimu na watumishi wote waliomba mafunzo wamepata mafunzo hayo.
Upatikanaji wa fedha za malipo ya Ada na fedha nyingine katika kugharamia mafunzo hayo.
Mazingira bora ya kufanyia kazi
Kuongeza idadi ya Vyombo vya usafiri kwa watendaji wa Kata, maafisa Maendeleo ya Jamii katika Kata, waratibu elimu Kata na Watumishi wengine wanaofanya kazi za kutoa huduma mbalimbali katika Halmashauri kwa kusafiri, watapata pikipiki ifukapo mwaka 2018
Idadi ya vyombo vilivyonunuliwa Kupatikana pikipiki 20 na Baiskeli 5.
Upatikanaji wa fedha kununulia vyombo vya usafiri.
Utunzaji wa kumbukumbu za kiutumishi
Masjala ya wazi na masjala ya siri katika ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji (W) zinakuwa na taarifa sahihi za watumishi muda wote ifikapo mwaka 2018
Register ya mzunguko wa majarada ya watumishi na majarada mengine katika masijara zote
Kuwepo reister mbalimbali katika masjara zote Watumishi wa masjara (Register Assistants) kupata mafuzo ya utunza kumbukumbu
Upatikanaji wa fedha za mafunzo na ununuzi wa Regislirs pamoja na majalada.
Kujenga Uwezo Kuendeleza mapambano juu ya kupunguza maambukizi ya UKIMWI kwa watumishi wa Halmashauri ya wilaya Tandahimba ifikapo mwaka 2018
Idadi ya watumishi waliopata mafunzo Kuwepo kwa mafunzo mbalimbali kwa watumishi juu ya Ukimwi na jinsi ya kujikinga na Ukimwi
Upatikana wa fedha za mafunzo Kutoa huduma ya chai kula kwa watumishi walio na maambukizi ya UKIMWI.
163
MPANGO KAZI WA UTEKELEZAJI WA MKAKATI.
LENGO : Kuboresha huduma za kiutumishi kwa watumishi 1,862 wa halmashauri ya wilaya ya tandahimba ifikapo mwaka 2018.
LENGO MKAKATI MHUSIKA
2014 2015 2016 2017 2018
Kutoa mafunzo kwa watumishi wa Halmashauri ifikapo mwaka 2018
Kuwaelimisha watumishi juu ya kujiendeleza kielimu na kuomba kujifunza
DED, DHRO
Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi ifikapo mwak 2018
Kununua vyombo vya kusafiria (Pikipiki) kwa Maafisa Watendaji Kata 12 na Waratibu wa Elimu Kata 8 na baiskeli 5 kwa Wahudumu wa ofisi na Ofisi bora za kufanyia kazi
DED, DHRO, DEO (P)
Kuwa na taarifa sahihi za watumishi katika Masijara ya wazi na masijara ya siri ya Mkurugenzi Mtendaji (W) ifikapo mwaka 2018
Kuboresha utunzaji wa kumbukumbuku sahihi za kila mtumishi
DHRO na OS
Kuendeleza mapambano dhidi ya Ukimwi kwa watumishi wa Halmashuri ya Wilaya ya Tandahimba
Kutoa mafunzo ya mara kwa mara kwa watumishi wa Halmshauri dhidi ya Ukimwi na Maambukizi ya Ukimwi
DED, DHRO, CHAC
164
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: HUDUMA ZA KIUTUMISHI
LENGO MKAKATI CHANZO CHA FEDHA
MAKISIO YA GHARAMA JUMLA
2014 2015 2016 2017 2018
Kuwapa mafunzo watumishi mbalimbali katika Idara 13 za Halmashauri na Vitengo 6 pamoja na kuwa na mpango wa matumizi ya fedha za kujenga uwezo (CBG)
Kuwawesha Watumishi walioomba kwenda mafunzoni kulingana na mpango wa mafunzo ya Idara na Vitengo ifikapo mwaka 2018
Vyanzo vya ndani Fedha za kujenga uwezo (CBG)
12,600,000
15,700,000 15,700,000 16,700,000 17,700,000 77,700,000
Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi ifikapo 2018
Kununua Pikipiki 20 na baiskeli 5 kwa ajli ya watumishi katika ngazi ya Kata na Halmashauri.
Vyanzo vya ndani
8,400,000 8,400,000 8,400,000
8,400,000 8,400,000 42,000,000
Kuimarisha utunzaji wa kumbukumbu za watumishi
Taarifa zote za watumishi zitunzwe ipasavyo katika majalada yao binafsi pamoja na majalada ya siri ifikapo 2018
Vyanzo vya ndani Fedha za kujenga uwezo (CBG)
1,500,000 1,500,000 1,500,000 1,500,000 1,500,000 7,500,000
Mapambano dhidi ya Ukimwi na Maambukizi ya Ukimwi
Watumishi wote wapewe Elimu juu ya Ukimwi na maambukizi ya Ukimwi Ifikapo mwaka 2018
Vyanzo vya ndani
4,500,000 4,500,000 4,500,000 4,500,000 4,500,000 22,500,000
JUMLA 27,000,000 30,100,000 30,100,000 31,100,000 32,100,000 149,700,000
165
ENEO LA HUDMA: BIASHARA
Lengo Kuu: Kuchochea Maendeleo na kasi ya ukuaji wa biashara, kuinua uwezo wa ushindani ili kuongeza kasi ya maendeleo ya kijamii ,kiuchumi na kuondoa umaskini kufikia 2018 Madhumuni ya Mkakati Mkakati Lengo la kutolea huduma Viashiria Njia ya kupima Dhana/Udhaifu
Kutambua wafanya biashara 600 ifikapo 2018
Usajili wa wafanyabiashara wilayani
Utoaji wa Leseni za biashara toka 220 hadi 600 ifikapo 2018 Ongezeko la biashara
Ukaguzi wa maeneo ya biashara
Usafiri/fFedha
kuongeza mapato kupitia biashara ndogondogo ifikapo 2018
Usajiri wa biashara ndogo ndogo
Utambuziwa wafanyabiashara ndogondogo 320 katika Wilaya ifikapo 2018
Ongezeko la maombi ya biashara ndogondogo
Uandikishaji wa wafanyabiashara Shajala/Fedha
Kurasimisha eneo la soko la Wilaya ifikapo 2018
Kupangisha vibanda vya soko
Upangishaji wa vibanda 289 vya soko ifikapo 2018
Ongezeko la maombi ya mahitaji ya wapangaji wa vibanda
Uandikishaji wa wafanyabiashara
Shajala/Fedha
166
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
LENGO LA KUTOLEA HUDUMA MIKAKATI 2014 2015 2016 201 7 2018 Utoaji wa Leseni za biashara toka 220 hadi 600 ifikapo 2018 Usajili wa wafanyabiashara Utambuzi wa wafanyabiashara ndogondogo 320 katika Wilaya ifikapo 2018
Uhamasishaji wa utambuzi wa wafanyabiashara
Upangishaji wa vibanda 289 vya soko ifikapo 2018
mafunzo kwa wafanyabiashara
Utozaji wa ushuru wa mabasi 100 hadi kufikia 2018
Kusajiri mabasi yanayotoka na kuingia
167
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKEZAJI
ENEO LA HUDUMA: BIASHARA
LENGO LA KUTOLEA HUDUMA
MIKAKATI 2014 2015 2016 2017 2018 JUMLA
Utoaji wa Leseni za biashara toka 220 hadi 600 ifikapo 2018
Usajili wa wafanyabiashara
30,000,000 30,000,000 30,000,000 30,000,000 30,000,000 150,000,000
Utambuzi wa wafanyabiashara ndogondogo 320 katika Wilaya ifikapo 2018
Uhamasishaji wa utambuzi wa wafanyabiashara
23,040,000 23,040,000 23,040,000 23,040,000 23,040,000 115,200,000
Upangishaji wa vibanda 289 vya soko ifikapo 2018
mafunzo kwa wafanyabiashara
34,680,000 34,680,000 34,680,000 34,680,000 34,680,000 173,400,000
Utozaji wa ushuru wa mabasi 100 hadi kufikia 2018
Kusajiri mabasi yanayotoka na kuingia
36,000,000 36,000,000 36,000,000 36,000,000 36,000,000 180,000,000
Jumla 123,720,000
123,720,000
123,720,000
123,720,000
123,720,000
618,600,000
168
ENEO LA HUDUMA: KITENGO CHA UGAVI NA MANUNUZI
ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI/ MKAKATI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
1 Usimamzi wa shughuli za manunuzi
Kuwa na mpango wa manunuzi wa mwaka wa Halmashauri kila ifikapo mwezi Februari kila mwaka
Kupokelewa kwa mahitaji ya manunuzi toka kila idara na kwa kupanga vipao mbele vya manunuzi
Taarifa za utekelezaji wa mchakato wa manunuzi.
Upatikanaji wa rasilimali fedha na watu.
Kutangaza zabuni mara moja kila mwaka, kwa kuzingatia Mpango wa manunuzi na kwa kufuata tender documents zinazopendekezwa na PPRA
Kuwepo kwa mpango wa manunuzi ulioidhinishwa na Halmashauri. Matumizi ya tender documents zilizoandaliwa na PPRA.
Taarifa za utekelezaji wa manunuzi kwa kila robo mwaka kuwasilishwa katika vikao vya CMT na Finance Commitee
Upatikanaji wa rasilimali fedha, watu na vitendea kazi (komputa, printer,photokopi)
Utawala bora Kuweka uwazi katika shughuli za manunuzi kwa kutangaza fursa za zabuni katika vyombo vya habari ( magazeti na mbao za matangazo) kila mwaka.
Kuwa na vikao vya kitengo cha manunuzi kila mwezi
Idadi ya matangazo ya zabuni yanayohusiana na mchakato wa manunuzi yaliyotolewa magazetini.
Mihtasari ya vikao vya kitengo vya kila mwezi
Taarifa za utekelezaji wa ukaguzi wa vifaa, Miradi na Huduma zilizonunuliwa kabla ya malipo kufanyika.
Taarifa ya utekelezaji wa vikao
Upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya kulipia matangazo katika magazeti
Rasilimali watu,
Shajala na fedha
Kupata thamani ya fedha kwa huduma zitolewazo na wazabuni
Viainisho sahihi vya mahitaji toka kwa wakuu wa Idara
Taarifa za utekelezaji wa ukaguzi wa vifaa, Miradi na Huduma zilizonunuliwa kabla ya malipo kufanyika.
Upatikanaji wa rasilimali fedha, watu na vitendea kazi.
2 Kujenga uwezo Kutoa mafunzo kwa wajumbe wa bodi ya zabuni juu ya sheria ya manunuzi ya 2011 na kanuni zake ifikapo 2018
Uwepo wa bajeti ya mafunzo kwa wajumbe wa bodi juu ya sheria mpya ya manunuzi ya mwaka 2011
Taarifa ya utekelezaji wa mafunzo.
Upatikanaji wa Rasilimali fedha, na rasilimali watu
169
ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI/ MKAKATI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
Kuandaa mpango wa bajeti ya kitengo cha manunuzi ili kiweze kutekeleza malengo yake kwa ufanisi mkubwa ifikapo mwezi Februari kila mwaka.
Vikao vya kupanga vipaumbale vya bajeti na mahitaji halisi ya kitengo cha ugavi
Taarifa ya uandaaji wa bajeti toka kitengo cha manunuzi
Upatikanaji wa rsilimali fedha, watu
Kuongeza kiwango cha ufanisi na weledi katika kazi kwa kuhudhuria mafunzo warsha na semina zinazotolewa na mamlaka za manunuzi (PPRA, PSPTB) kwa watumishi wanne (4) waliopo katika kada ya manunuzi ifikapo 2018
Idadi ya watumishi waliojiendeleza kila mwaka
Taarifa za kiutumishi na uwepo wa vyeti
Upatikanaji wa rasilimali fedha na watu
3 Mambo ya jinsia na Ukimwi
Kutoa mafunzo juu ya ugonjwa wa ukimwi kwa kupitia machapisho mbalimbali ya nyaraka za zabuni na katika mabango ya miradi ya ujenzi wa majengo na barabara ifikapo 2018
Nyaraka za zabuni na mabango ya miradi ya ujenzi
Taarifa ya utekelezaji wa kitengo cha manunuzi
Upatikanaji wa fedha
4 Ufuatiliaji na usimamizi
Kuwa na chombo cha usafiri kwa ajili ya shughuli za manunuzi
Kuwepo katika bajeti mahitaji ya chombo cha usafiri kwa ajili ya kitengo cha manunuzi
Taarifa ya utekelezaji Upatikanaji wa fedha
Kuwa na taarifa za uhakiki mali kila mwaka ifikapo mwezi Juni
Uwepo wa bajeti ya kufanya uhakiki mali
(stock taking)
Taarifa utekelezaji ya uhakiki mali
Rasilimali fedha, watu, shajara na usafiri.
Kuwa na ukaguzi wa vifaa vilivyopokelewa kabla ya kufanya malipo
Kuundwa kwa kamati za ukaguzi wa vifaa vilivyopokelewa
Taarifa ya ukaguzi wa vifaa vilivyopokelewa
Rasilimali watu na fedha
Kuboresha mfumo wa utunzaji kumbukumbu za manunuzi.
Uwepo wa mafaili ya wazabuni na mikataba yao pamoja na rejista za malipo mkataba, uwepo wa rejista ya
Uwepo wa rejista za mikataba (contractors registers) na utekelezaji
Rasilimali fedha,na watu
170
ENEO LA MATOKEO MUHIMU
LENGO MAHUSUSI/ MKAKATI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
mikataba wa mikataba.
171
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA:MANUNUZI
LENGO MIKAKATI
CHANZO CHA
FEDHA
MAKISIO YA GHARAMA
2014 2015 2016 2017 2018 Jumla Ujenzi wa ghala kudumu ifikapo 2018 Kutangaza Zabuni.
TDC/OWN SOURCE -
10,000,000 10,000,000 10,000,000
5,000,000 35,000,000
Mafunzo kwa wadau wa manunuzi/wajumbe bodi ya manunuzi na madiwani juu ya sheria mpya ya Manunuzi
Kumpata mshauri/consultant
Halmashauri
- 6,000,000 6,000,000 6,000,000 6,000,000 24,000,000 Kuwa na mpango wa manunuzi wa Halmashauri ifikapo 2018
Posho ya kujikimu kwa ajili ya wakuu wa idara
TDC / Halmashauri
11,000,000 11,000,000 11,000,000 11,000,000
11,000,000 55,000,000
Kutangaza zabuni na taarifa mbalimbali za manunuzi katika vyombo vya habari
Kuwa na bajeti ya matangazo ya zabuni.
Halmashauri
- 5,500,000 5,500,000 5,500,000 5,500,000 22,000,000
Kuimarisha utoaji wa taarifa za manunuzi kwa wakati
Shajara TDC - 2,500,000 2,500,000 2,500,000
2,500,000 10,000,000
Kuratibisha vikao vya bodi ya zabuni kwa kila mwezi
Posho kwa ajili ya wajumbe
TDC,ROAD FUND -
18,000,000 18,000,000 18,000,000
18,000,000 72,000,000
Kuhudhuria warsha,semina na mafunzo yanayohusiana na manunuzi kwa wajumbe wa bodi (PPRA/PSPTB,ROAD FUND)
Posho za kujikimu TDC,ROADFUND - 2,500,000 2,500,000 2,500,000
2,500,000 10,000,000
Kuhakiki mali za halmashauri kila mwaka ifikapo 2018
Posho kwa watumishi
TDC,BUSKET FUND - 2,000,000 2,000,000 2,000,000
2,000,000 8,000,000
Kuwa na chombo cha usafiri Kuwa na bajeti ya kununua gari
TDC -
70,000,000 - - - 70,000,000
172
ENEO LA HUDUMA: KITENGO CHA SHERIA
LENGO KUU: Kuwa na mfumo wa uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na taratibu katika shughuli mbalimbali za maendeleo ifikapo 2018.
ENEO LA MATOKEO LENGO MAHSUSI VIASHIRIA CHANZO CHA UHAKIKI
DHANA
MABARAZA YA KATA
Kuimalisha Mabaraza ya Kata 30 lfikapo mwaka 2018
Kuwepo kwa mabaraza hai katika kata zote 30.
Kutembelea mabaraza ya Kata. -Taarifa za utendaji kutoka katika Mabaraza hayo
Upatikanaji wa fedha. -Uwepo wa usafiri wa uhakika.
KUJENGA UWEZO
-Kuajiri Afisa Sheria mmoja (1) ifikapo mwaka 2015 .-Kumwendeleza kitaaluma Afisa Sheria mmoja ifikapo 2015 Kuimarisha kitengo cha sheria ifikapo mwaka 2018
Watumishi mawili (2) wawe wameajiriwa. -Afisa Sheria aliyeedeelezwa kitaaluma 2015. Kitengo kuwa na mwanasheria.
-Taarifa za ajira. -Vyeti vya taaluma Taarifa ya Utumishi
-Uwepo wa kibali cha ajira. -Upatikanaji wa fedha.
MAMBO YA JINSIA NA UKIMWI
Kuendeleza mapambano dhidi maambukizi mapya ya Ukimwi kwa Watumishi ifikapo 2018.
Kupungua kwa maambukizi mapya ya UKIMWI.
-Taarifa za utekelezaji -Taarifa za vikao.
-Upatikanaji wa fedha. -Ushiriki wa jamii.
UTAWALA BORA Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa kwa watumishi kila mwaka.
Idadi ya vikao vilivyofanyika. Kutokuwepo mashitaka ya rushwa na taarifa za vikao vilivyofanyika
Utayari wa watumishi/jamii
SHERIA NDOGO
-Kuwa na sheria ndogo mbalimbali katika vijiji na Halmashauri ifikapo 2018
- Sheria Ndogo katika H/wilaya zinatumika
-taarifa kuhusu sheria ndogo zilizoidhinishwa na -kuwepo kwa nyaraka malimbali za sheria ndogo.
-Utayari wa wananchi na wadau mbalimbali Upatikanaji wa fedha
KESI NA MADAI MBALIMBALI YA HALMASHAURI
-Kusimamia kesi na madai mbalimbali ya h/wilaya kila mwka ifikapo 2018.
Kuwepo kwa kesi na madai mbalimbali zinazoendelea .
Taarifa kuhusu kesi na madai Kuwepo fedha
173
MPANGO WA UTEKELEZAJI
ENEO LAHUDUMA: KITENGO CHA SHERIA
Lengo/Mkakati
Mhusika
Muda wa utekelezaji 2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 Kufanya uchqguzi na kuwapata wajumbe katika kata zote 30 ifikapo 2015
LO & WDC
Kutoa mfunzo kwa wajumbe 300 wa mabaraza ya kata ifikapo Juni 2015
LO
Kufanya ufuatailiaji ili kukutana na wajumbe wa Mabaraza ya Kata kila robo mwaka ifikapo Juni 2018
DED & LO
Mwanasheria 1 kupatiwa mafunzo ya kuimalisha taaluma yake ifikapo mwaka 2015.
DHRO
Kuajiri mwanasheria 1 ifikapo Juni 2015
DHRO
Kununua samani za ofisi na vitedea kazi ifikapo Juni 2015.
LO
Kununua pikipiki/gari kwa ajili ya usafri wa kitengo ifikapo mwka 2015
DED
Kuendeleza mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya UKIMWI
CDO
Kuwahamasisha wanajamii kuhudhuria makongamano ya Elimu ya Afya ya Uzazi ifikapo 2018
CDO
Kuimarisha ufuatiliaji na usimamizi wa mambo mtambuka ya kitengo
LO
Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa
LO & PCCB
174
Lengo/Mkakati
Mhusika
Muda wa utekelezaji 2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 Kufanya uchambuzi wa sheria ndogo kutoka vijijini na kupitisha kwenye vikao vya Kamati husika ifikapo mwaka 2015
LO, WAKUU WA IDARA NA MADIWANI
Kufanya vikao vya pamoja na serikali za vijiji ili kuahinisha sheria ndogo ifikapo mwaka 2018
LO & MADIWANI
Kutoa mafunzo kwa wajumbe wa h/za vijiji kuhusu namna ya kuandasheria ndogo ifikapo mwaka 2018.
LO & HALMASHAURI ZA VIJIJI
Kuhudhuria mahakamani na mabaraza ya ardhi wakati wa mashauri na kesi kila mwezi ifikapo mwaka 2018
LO
Kuandaa kesi na madai mbalimbali ya h/wilaya kila mwezi ifikapo ikapo juni 2018
175
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: KITENGO CHA SHERIA
Malengo Makisio ya Gharama Chanzo
cha fedha 2014 2015 2016 2017 2018 Jumla Kufanya uchaguzi na kuwapata wajumbe katika kata zote 30 ifikapo 2015
4,000,000 6000000 6000000 6000000 6000000 28,000,000 TDC
Kutoa mfunzo kwa wajumbe 300 wa mabaraza ya kata ifikapo Juni 2015
0 15,000,000 0 0 15,000,000 30,000,000 TDC
Kufanya ufuatailiaji ili kukutana na wajumbe wa Mabaraza ya Kata kila robo mwaka ifikapo Juni 2018
2,000,000 15,000,000 15,000,000 2,000,000 2,000,000 36,000,000 TDC
Mwanasheria 1 kupatiwa mafunzo ya kuimalisha taaluma yake ifikapo mwaka 2015.
0 10,000,000 12,000,000.0 8,000,000 14,000,000 44,000,000
Kuajiri mwanasheria 1 ifikapo Juni 2015
3,000,000 3,000,000 3,000,000 3,000,000 3,000,000 15,000,000 TDC
Kununua samani za ofisi na vitedea kazi ifikapo Juni 2015.
7,000,000 7,000,000 7,000,000 7,000,000 7,000,000 35,000,000 TDC
Kununua pikipiki/gari kwa ajili ya usafri wa kitengo ifikapo mwka 2015
6,000,000 6,000,000/= 6,000,000 6,000,000 6,000,000 30,000,000 TDC
Kuendeleza mapambano dhidi ya maambukizi mapya ya
0 5,000,000 5,000,00 5,000,000/= 5,000,000/= 25,000,000 TDC
176
Malengo Makisio ya Gharama Chanzo
cha fedha 2014 2015 2016 2017 2018 Jumla UKIMWI
Kuwahamasisha wanajamii kuhudhuria makongamano ya Elimu ya Afya ya Uzazi ifikapo 2018
0 4,900,000.0 4,900,000.0 4,900,000 4,900,000 19,600,000
Kuimarisha ufuatiliaji na usimamizi wa mambo mtambuka ya kitengo
8,760,000 8,760,000 8,760,000 8,760,000 8,760,000 43,800,000 TDC
Kuendeleza mapambano dhidi ya rushwa
3,600,000 3,600,000 3,600,000 3,600,000 3,600,000 18,000,000 TDC
Kufanya uchambuzi wa sheria ndogo kutoka vijijini na kupitisha kwenye vikao vya Kamati husika ifikapo mwaka 2015
0 5,000,000 0 0 2,600,000 7,600,000 TDC
Kufanya vikao vya pamoja na serikali za vijiji ili kuahinisha sheria ndogo ifikapo mwaka 2018
0 4,750,000 6,000,000 0 0 10,750,000 TDC
Kutoa mafunzo kwa wajumbe wa h/za vijiji kuhusu namna ya kuandasheria ndogo ifikapo mwaka 2018.
2,500,000 2,500,000 2,500,000 2,500,000 2,500,000 12,500,000
TDC
177
Malengo Makisio ya Gharama Chanzo
cha fedha 2014 2015 2016 2017 2018 Jumla Kuhudhuria mahakamani na mabaraza ya ardhi wakati wa mashauri na kesi kila mwezi ifikapo mwaka 2018
38,000,000 3,800,000 3,800,000 3,800,000 3,800,000 19,000,000
TDC
Kuandaa kesi na madai mbalimbali ya h/wilaya kila mwezi ifikapo ikapo juni 2018
1,000,000 1,000,000 1,000,000 1,000,000 1,000,000 5,000,000
TDC
Jumla 75,860,000 95,310,000 79,560,000 56,560,000 80,160,000 379,250,000
178
ENEO LA HUDUMA:UKAGUZI WA NDANI
LENGO KUU :Kuboresha usimamizi wa mapato, matumizi ya fedha na usimamizi wa rasilimali nyingine za halmashauri
NA ENEO LA MATOKEO
LENGO MAHUSUSI/ MKAKATI VIASHIRIA VYA UTEKELEZAJI
CHANZO CHA UHAKIKI DHANA
1. Ukaguzi wa hesabu. Kufanya ukaguzi wa hesabu na kutoa ripoti ya ukaguzi kila robo mwaka.
Taarifa za ukaguzi
Uwepo wa hesabu zilizokaguliwa.
Taarifa za utekelezaji. Uwepo wa bajeti inayokidhi mahitaji.
2. Ukaguzi wa Miradi ya maendeleo.
Kufanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo na kutoa ripoti ya ukaguzi kila robo mwaka.
Taarifa za Ukaguzi. Taarifa za utekelezaji. Uwepo wa bajeti inayokidhi mahitaji na upatikaji wa usafiri wa uhakika.
3. Ukaguzi wa Rasilimali za Halmashauri.
Kufanya ukaguzi wa rasilimali za Halmshauri na kutoa ripoti ya ukaguzi kila robo mwaka.
Taarifa za Ukaguzi . Taarifa za utekelezaji. Upatikaji wa usafiri wa uhakika.
4. Mazingira ya kufanya kazi
Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi ifikapo mwaka 2015.
Samani zinanunuliwa. Taarifa za utekelezaji. Uwepo wa bajeti inayokidhi mahitaji.
5. Mambo ya jinsia/ukimwi
Kuendeleza mapambano dhidi ya Ukimwi. Kupungua kwa maambukizi mapya ya Ukimwi.
Taarifa za utekelezaji. Uwepo wa bajeti inayokidhi mahitaji na utayari wa jamii.
6. Kujenga uwezo Kuwa na wakaguzi wa ndani watatu (3) ifikapo mwaka wa fedha 2016.
Idadi ya wakaguzi waliajiriwa Taarifa za utekelezaji. Uwepo wa kibari cha ajira na kuripoti kwa watumishi wapya.
Ifikapo mwaka 2016 watumishi wawili (2) wawe wameongeza kiwango cha taaluma katika kiwango cha CPA.
Idadi ya watumishi waliohudhuria mafunzo na kuhitimu
Taarifa za utekelezaji. Uwepo wa bajeti inayokidhi mahitaji.
179
LENGO, MKAKATI NA MUDA WA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: UKAGUZI WA NDANI
LENGO KUU: Kutoa ushauri juu ya uzingatiaji wa sheria, kanuni na taratibu katika utekelezaji wa shughuli za Halmashauri.
NA LENGO MKAKATI MHUSIKA MHUSIKA
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
1. Kufanya ukaguzi wa hesabu na kutoa ripoti ya ukaguzi kila robo mwaka.
• Kuwa na mpangokazi wa ukaguzi wa ndani wa taarifa za hesabu.
Mkaguzi wa ndani.
• Kufanya ukaguzi kila robo mwaka kwa kuzingatia mpangokazi uliopo.
Mkaguzi wa ndani.
• Kutoa taarifa ya ukaguzi wa ndani mara baada ya robo mwaka kuisha.
Mkaguzi wa ndani.
• Kuhakiki majibu ya hoja za ukaguzi na kutoa maoni.
Mkaguzi wa ndani.
2 Kufanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo na kutoa ripoti ya ukaguzi kila robo mwaka
• Kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelazwa na kuona hatua miradi ilipofika.
Mkaguzi wa ndani.
• Kuzipitia taarifa za utekelezaji wa miradi husika.
Mkaguzi wa ndani.
• Kutoa maoni/ushauri juu ya utekelezaji wa miradi pamoja na ripoti ya ukaguzi.
Mkaguzi wa ndani.
3 Kufanya ukaguzi wa rasilimali za Halmshauri na kutoa ripoti
• Kuzihakiki rasilimali za Halmashauri kwa kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo/waraka itolewayo juu ya
Mkaguzi wa ndani.
180
NA LENGO MKAKATI MHUSIKA MHUSIKA
2014 2015 2016 2017 2018
1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4 1 2 3 4
ya ukaguzi kila robo mwaka matumizi na usimamizi wa rasilimali za Halmashauri.
4 Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi ifikapo mwaka 2015.
• Kununua samani za ofisi kulingana na bajeti iliyopitishwa.
Mkaguzi wa ndani.
5 Kuendeleza mapambano dhidi ya Ukimwi.
Kutoa mafunzo na Elimu ya mapambano zidi ya Ukimwi
Mkaguzi wa ndani.
6 Kuwa na wakaguzi wa ndani watatu (3) ifikapo mwaka wa fedha 2016.
• Kuajiri wakaguzi wa kitengo cha ukaguzi wa ndani.
Afisa Utumishi
7 Ifikapo mwaka 2016 watumishi wawili (2) wawe wameongeza kiwango cha taaluma katika kiwango cha CPA.
• Kuhudhuria mafunzo mbalimbali yatakayokuwa yanatolewa kwa lengo la kujenga uwezo kwa watumishi.
Mkaguzi wa ndani.
181
MAKISIO YA GHARAMA ZA UTEKELEZAJI
ENEO LA HUDUMA: UKAGUZI WA NDANI
NA LENGO MIKAKATI MAKISIO YA GHARAMA CHANZO CHA
FEDHA 2014 2015 2016 2017 2018
1. Kufanya ukaguzi wa hesabu na kutoa ripoti ya ukaguzi kila robo mwaka.
• Kuandaa mpangokazi wa kitengo cha ukaguzi wa ndani.
1,200,000 3,000,000 3,500,000 4,000,000 4,300,000 TDC/ Wizara ya Fedha
• Kufanya ukaguzi kila robo mwaka kwa kuzingatia mpangokazi uliopo.
1,000,000 1,700,000 2,000,000 2,500,000 3,000,000 TDC/ Wizara ya Fedha
• Kutoa taarifa ya ukaguzi wa ndani mara baada ya robo mwaka kuisha.
2,000,000 2,500,000 3,000,000 3,500,000 4,000,000 TDC/ Wizara ya Fedha
• Kuhakiki majibu ya hoja za ukaguzi na kutoa maoni.
500,000 1,000,000 1,500,000 2,000,000 2,500,000 TDC/ Wizara ya Fedha
2. Kufanya ukaguzi wa miradi ya maendeleo na kutoa ripoti ya ukaguzi kila robo mwaka.
• Kutembelea miradi ya maendeleo iliyotekelazwa na kuona hatua miradi ilipofika.
5,000,000 5,000,000 8,000,000 8,000,000 8,000,000 TDC/ Wizara ya Fedha
• Kuzipitia taarifa za utekelezaji wa miradi husika.
1,400,000 1,400,000 1,700,000 2,100,000 2,400,000 TDC/Wizara ya Fedha
• Kutoa maoni/ushauri juu ya utekelezaji wa miradi pamoja na ripoti ya ukaguzi.
500,000 700,000 900,000 1,100,000 1,300,000 TDC/Wizara ya Fedha
3. Kufanya ukaguzi wa rasilimali za Halmshauri na
• Kuzihakiki rasilimali za Halmashauri kwa kuzingatia sheria, kanuni,
2,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,000 2,000,000 TDC/ Wizara ya
182
NA LENGO MIKAKATI MAKISIO YA GHARAMA CHANZO CHA
kutoa ripoti ya ukaguzi kila robo mwaka.
taratibu na miongozo/waraka itolewayo juu ya matumizi na usimamizi wa rasilimali za Halmashauri.
Fedha
4. Kuboresha mazingira ya kufanyia kazi ifikapo mwaka 2015.
• Kuhakikisha samani za ofisi zinanunuliwa kulingana na bajeti iliyopitishwa.
2,500,000 2,500,000 2,500,000 2,500,000 2,500,000 TDC/ Wizara ya Fedha
5 Kuendeleza mapambano dhidi ya Ukimwi.
• Kujifunza na kutoa Elimu ya mapambano zidi ya Ukimwi
1,000,000 1,000,000 1,000,000 1,000,000 1,000,000 TDC/ Wizara ya Fedha
6. Kuwa na wakaguzi wa ndani watatu (3) ifikapo mwaka wa fedha 2016.
• Kuhakikisha kitengo cha ukaguzi wa ndani kinaongezewa Mkaguzi mmoja ili ikifika mwaka 2015 ikama ya watumishi watatu iwe imetimia.
4,800,000 4,800,000 4,800,000 4,800,000 4,800,000 TDC/ Wizara ya Fedha
7. Ifikapo mwaka 2016 watumishi wawili (2) wawe wameongeza kiwango cha taaluma katika kiwango cha CPA.
• Kuhudhuria mafunzo mbalimbali yatakayokuwa yanatolewa kwa lengo la kujenga uwezo kwa watumishi.
3,000,000
5,000,000
7,000,000
9,000,000
11,000,000
TDC/ Wizara ya Fedha
JUMLA 24,900,000 30,600,000 37,900,000 42,500,000 46,800,000