jamhuri ya muungano wa tanzania wizara …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae...

15
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA MUONGOZO WA UTUMIAJI MFUMO WA USAJILI WATOA HUDUMA YA MSAADA WA KISHERIA Imeandaliwa na Alfred Chunga-0785998384 Aprili 10, 2019

Upload: others

Post on 14-Jul-2020

4 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

MUONGOZO WA UTUMIAJI MFUMO WA USAJILI

WATOA HUDUMA YA MSAADA WA KISHERIA

Imeandaliwa na Alfred Chunga-0785998384 Aprili 10, 2019

Page 2: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

UTANGULIZI

Mfumo wa Usajili na tathmini kwa watoa huduma ya msaada wa kisheria kwa

umma ni mfumo unaoratibu shughuli nzima ya usajili wa watoa huduma ya

msaada wa kisheria katika maeneo yao nchini kwa njia ya mtandao. Watoa

huduma wana wajibu wa kujisajili kupitia mfumo huu kwa kuambatisha

nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili.

Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini. Sehemu ya

kwanza usajili iko tayari na sehemu ya pili tathmini inaboreshwa.

Mfumo huu unapatikana kupitia https://legalaid.sheria.go.tz au kupitia tovuti

rasmi ya Wizara ya Katiba na Sheria www.sheria.go.tz katika sehemu ya

huduma za TEHAMA, Chagua Msaada wa Kisheria, bonyeza fungua hapa.

Page 3: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

1. USAJILI WA TAASISI YA HUDUMA YA MSAADA WA

KISHERIA (LEGAL AID PROVIDER)

VIAMBATISHO MUHIMU;

a) Cheti cha usajili cha taasisi mfano NGO,CBO,FBO au kampuni

b) Taasisi inayotaka kuhudumia wilaya pekee inatakiwa kupata Barua

kutoka ofisi ya mkuu wa wilaya husika, Kwa Mkoa inatakiwa kupata

Barua kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kwa nchi nzima inatakiwa

kupata Barua kutoka Ofisi ya Rais Tamisemi.

c) Orodha ya Mawakili/Wanasheria kama inavyotakiwa kwenye sheria

ya msaada wa Kisheria ambao wapo katika taasisi ikiambatana na

Vyeti vya taaluma (“Bachelor” kwa mwanasheria, “Practising

Certificate” kwa wakili). Kama taasisi ina paralegals pekee inatakiwa

kuambatisha “affiliation certificate/letter/declaration” kwa taasisi

iliyosajiliwa na yenye wakili.

d) Nakala halisi ya malipo ya ada ya usajili.

e) Fomu ya Maombi ya Taasisi ya inayotoa huduma ya Msaada wa

Kisheria “Application Form” kutoka kwenye kanuni.

f) Barua kutoka Mamlaka ya usajili wa Taasisi “Clearance Letter from

Registering Authority”.

g) Katiba au nyaraka ya kuanzisha taasisi (Mfano Katiba, MEMATS)

NB. Tafadhali hakikisha una viambatisho vyote na vimehifadhiwa katika pdf

ili mfumo uweze kukuruhusu kujisajili.

Page 4: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

Kusajili taasisi katika mfumo huu bonyeza sehemu iliyoandika “REGISTRATION”

kisha chagua “REGISTER LEGAL AID PROVIDER”.

Katika sehemu hii utajaza taarifa za mtu aliyeteuliwa na taasisi kuwasilisha

nyaraka na taarifa zake katika mfumo. Jaza sehemu zote muhimu kama jina la

Page 5: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

kwanza, jina la mwisho, barua pepe, neno siri na baada ya kujaza sehemu zote

bonyeza “REGISTER LAP”. Sehemu ya kuingia katika mfumo itafunguka na

utatakiwa kujaza barua pepe(e-mail) uliyoisajili na neno la siri ili kuingia katika

mfumo ambapo utatakiwa kuhakiki barua pepe yako kwa kutumiwa “Link”

kwenye barua pepe yako, Ukishabonyeza link hiyo mfumo utakupeleka

kuendelea na usajili.

Page 6: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

Usajili wa taasisi umegawanyika katika sehemu kuu tano ambazo ni taarifa za

taasisi, huduma na eneo la kufanyia kazi,wafanyakazi,malipo na sehemu ya

kuwasilisha nyaraka muhimu.

i) Taarifa za taasisi- Tafadhali jaza na kuambatisha taarifa zote muhimu za

taasisi yako kama jina la taasisi, anwani,namba ya mlipakodi kama

ipo, chagua idadi ya chini kabisa ya wafanyakazi kama inavyotakikana

na sheria ya msaada wa kisheria. Iwapo utachagua Paralegals watatu

au Mwanasheria mmoja na Paralegals wawili inakupasa kuonyesha

“Affiliation” katika taasisi inayotoa msaada wa kisheria yenye Wakili

na kuambatisha Ushahidi wa “Affiliation” hiyo. Chagua Aina ya taasisi

yako kama ni NGO,FBO,CBO au Biashara na ambatisha nyaraka ya

usajili, bonyeza “NEXT” kuendelea na hatua inayofata.

ii) Chagua huduma utakazozitoa katika jedwali la kushoto kwa kubonyeza

“ADD” ambapo zitaonekana katika jedwali la kulia, kisha chagua eneo

utakalohudumia kama ni Wilaya,Mkoa au Taifa(Ikiwa utachagua

Wilaya ambatisha barua toka ofisi ya mkuu wa wilaya, ikiwa

utachagua mkoa ambatisha barua toka ofisi ya mkuu wa mkoa na

ikiwa utachagua Nchi nzima ambatisha barua toka Ofisi ya Rais

TAMISEMI). chagua sehemu uliyopo katika “Jurisdiction”. Jaza kata

na mitaa utakayofanyia kazi. Jaza taarifa zingine katika “Other

information” kama zipo. Bonyeza “NEXT” kuendelea na hatua

inayofuata.

Page 7: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

iii) Katika sehemu ya tatu jaza kulingana na uchaguzi ulioufanya katika

hatua ya kwanza sehemu ya wafanyakazi. Kama ulichagua

“Paralegals” watatu basi inakupasa uwajaze kwa kubonyeza “Add

Paralegals” na kisha jaza taarifa zote zinazohitajika na kuambatisha

Ushahidi wa malipo na baada ya hapo bonyeza “Register Paralegal”

Fanya hivyo kwa idadi inayotakiwa. Hivyo hivyo kama ulichagua

mawakili wawili itakupasa kubonyeza “Add Lawyer/Advocate” na jaza

taarifa zote zinazotakiwa.

Page 8: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

iv) Sehemu hii ni sehemu ya malipo hivyo utatakiwa kujaza taarifa za malipo

yako ya ada ya usajili. Unatakiwa kujaza jina la benki, tawi, umelipa

lini na kuambatisha nakala halisi ya malipo ya benki(Paying slip)

bonyeza kitufe cha “Save Details” kuhifadhi taarifa zako . Baada ya

kuhifadhi bonyeza kitufe cha “NEXT STEP” kuendelea na hatua

inayofuata.

Page 9: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

v) Sehemu hii ni ya viambatisho muhimu. Angalia orodha ya viambatisho

vinavyohitajika katika jedwali la kushoto “Required Attachment” na

chagua kiambatisho kimoja kimoja katika orodha ya chini ya jedwali

la kushoto “Select Attachment File”. Bonyeza kitufe cha “Attach”

kuchagua kiambatisho katika kompyuta yako na bonyeza kitufe cha

“UPLOAD” kuhifadhi nyaraka hiyo. Rudia hatua hizi kwa nyaraka zote

zinazohitajika. Bonyeza kitufe cha “Finish & Submit your Application”

kuwasilisha maombi yako ya usajili baada ya kuhifadhi nyaraka zote

zinazohitajika.

Page 10: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini
Page 11: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

2. USAJILI WA MTOA HUDUMA YA MSAADA WA

KISHERIA(PARALEGAL)

VIAMBATISHO MUHIMU;

a) Nakala Halisi ya cheti cha taaluma kilichothibitishwa na kamishna wa

viapo.

b) Nakala ya cheti cha mafunzo ya “Paralegal”

c) Barua kutoka katika taasisi yako kukuthibitisha “Letter from Institution

Supervisor”

d) Fomu ya Maombi ya mtoa huduma ya msaada wa Kisheria“Application

Form” kutoka kwenye kanuni.

e) Barua au cheti kutoka kwa Shahidi aliyehudumiwa na mtoa huduma ya

msaada wa kisheria “Witness Introduction Letter”.

f) Barua au cheti cha utambulisho kutoka eneo analoishi mtoa huduma ya

msaada wa kisheria “Hamlet leader Introduction Letter”.

g) Nakala halisi ya malipo ya ada ya usajili.

NB. Tafadhali hakikisha una viambatisho vyote na vimehifadhiwa katika pdf

ili mfumo uweze kukuruhusu kujisajili.

Mtoa huduma ya msaada wa kisheria anaweza kusajiliwa kwenye mfumo kwa

njia tatu ambazo ni;

i) Sehemu ya nje ya mfumo bonyeza “REGISTRATION” kisha “REGISTER

PARALEGAL”. Ambapo fomu ya usajili itaonekana. Utatakiwa

kuchagua Taasisi yako katika orodha “CHOOSE YOUR LEGAL AID

PROVIDER” na jaza taarifa zote muhimu ikiwemo majina yako,barua

pepe,neno siri n.k. kisha bonyeza “Register” kujisajili, Baada ya hapo

mfumo utakuhitaji kuingia kwa kujaza barua pepe na neno la siri ili

kuendelea, utahitajika kuhakiki barua pepe yako na baada ya

kubonyea kitufe cha uhakiki kwenye barua pepe yako mfumo

utaendelea sehemu ya na usajili.

NB. Taasisi lazima iwe imeshasajiliwa kwenye mfumo kabla ya

kumsajili mtoa huduma.

Page 12: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini
Page 13: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini
Page 14: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini
Page 15: JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA …...nyaraka zote muhimu kwa ajili ya uhakiki na baadae kupatiwa vyeti vya usajili. Mfumo huu una sehemu mbili ambazo ni usajili na tathmini

ii) sehemu ya ndani ya mfumo baada ya mtoa huduma kuingia kwenye

mfumo, bonyeza sehemu ya “Registration” iliyoko upande wa

kushoto kisha bonyeza “Register Paralegal”. Fomu ya usajili itatokea

na utatakiwa kujaza taarifa zote muhimu pamoja na kuambatisha

nyaraka muhimu.

3. Pia

unaweza kumsajili mtoa huduma “Paralegal” katika hatua ya tatu ya

usajili wa taasisi kwa kubonyeza kitufe kilichoandikwa “ADD

PARALEGAL”.