july,2013 - ihi.kazi.proihi.kazi.pro/wordpress/wp-content/uploads/2017/08/... · 1.uchambuzi wa...

24
TAASISI YA UTAFITI NA UTETEZI WA HAKI ZA ARDHI UCHAMBUZI WA RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JULY,2013

Upload: others

Post on 04-Feb-2020

31 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

TAASISI YA UTAFITI NA UTETEZI WA HAKI ZA ARDHI

UCHAMBUZI WA RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

JULY,2013

1.UCHAMBUZI WA RASIMU YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

1.1 SEHEMU YA UTANGULIZI KATIKA RASIMU

Aya ya kwanza:-Inavyosomeka katika Rasimu

KWA KUWA, Sisi, Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii

inayoheshimu na kuzingatia misingi ya utu, uhuru, haki, usawa, udugu, amani, umoja na mshikamano katika nyanja zote za maisha yetu;

Aya ya kwanza:-Maoni yanayopendekezwa

KWA KUWA , Sisi, Watu wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar tumeamua kuingia katika shirikisho au

muungano(moja wapo kati ya hayo)rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu usawa, udugu, amani, umoja na mshikamano katika Nyanja

zote za maisha yetu

Pia neno Tanzania Bara inapendekezwa lisitumike na badala yake pale inapojitokeza isomeke Jamhuri ya Tanganyika katika Rasimu nzima

ya Katiba

Aya ya mwisho:- Inavyosomeka Katika rasimu

HIVYO BASI, KATIBA HII YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ILIYOPENDEKEZWA NA BUNGE MAALUM LA

KATIBA imetungwa na SISI WANANCHI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kupitia KURA YA MAONI kwa madhumuni

ya kujenga jamii kama hiyo, na kuhakikisha kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya

demokrasia na utawala wa sheria, kujitegemea na isiyokuwa na dini.

Aya ya mwisho:- Inavyopendekezwa

HIVYO BASI, KATIBA HII YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ILIYOPENDEKEZWA NA BUNGE MAALUM LA

KATIBA imetungwa na SISI WATU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA kupitia KURA YA MAONI kwa madhumuni ya

kujenga jamii kama hiyo, na kuhakikisha kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya

demokrasia na utawala wa sheria, kujitegemea na isiyokuwa na dini.

SURA YA KWANZA-JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Sehemu ya kwanza-Mipaka,Alama,Lugha,Utamaduni na Tunu za Taifa

Ibara

Ibara inavyosomeka Ibara inavyopendekezwa Sababu za mabadiliko

1(1)(2)

1.-(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni

Shirikisho lenye

mamlaka kamili ambayo imetokana na Muungano wa

nchi mbili za

Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa

Zanzibar ambazo kabla

ya Hati za Makubaliano ya Muungano ya mwaka 1964

zilikuwa nchi

huru.

(2) Jamhuri ya Muungano ni Shirikisho la

kidemokrasia

linalofuata mfumo wa vyama vingi vya siasa, usawa

wa binadamu,

kujitegemea, utawala wa sheria na kuheshimu haki za

binadamu.

Katiba iainishe ni neno gani kati

ya shirikisho au muungano

litumike na sio yote kwa pamoja

Maneno “Shirikisho” na

“Muungano” haviwezi kutumika

pamoja kwani mifumo yake

kiutawala ni tofauti

2

Eneo la Jamhuri ya Muungano ni eneo lote la Tanzania

Bara ikijumuisha sehemu yake ya bahari na eneo lote

la Zanzibar ikijumuisha sehemu yake ya bahari.

-mipaka halisi ya nchi za

muungano yaani Jamuhuri ya

Tanganyika na Jamuhuri ya watu

wa Zanzibar ianishwe kwenye

katiba

- Pia neno Tanzania Bara

inapendekezwa lisitumike na

badala yake pale inapojitokeza

isomeke Jamuhuri ya

Tanganyika

Muungano wa 1964 ulihusisha

Jamuhuri ya Tanganyika na

Jamuhuri ya watu wa Zanzibar

4(3)

Serikali itaweka mazingira yatakayowezesha kuwepo

kwa mawasiliano ya lugha mbadala zikiwemo lugha za

alama,na nukta nundu kwenye sehemu muhimu za

umma na katika vyombo vya habari vinavyotangaza

habari zake kitaifa kwa ajili ya watu wenye mahitaji

maalum.

Serikali itaweka mazingira

yatakayowezesha kuwepo kwa

mawasiliano ya lugha mbadala

zikiwemo lugha za alama,

maandishi yaliyokuzwa na

nukta nundu kwenye sehemu

muhimu za umma na katika

vyombo vya habari

vinavyotangaza habari zake

kitaifa kwa ajili ya watu wenye

mahitaji maalum.

-kukidhi mahitaji ya

mawasiliano kwa watu wenye

mahitaji maalumu

5(h)

5. Jamhuri ya Muungano itaenzi na kuzingatia Tunu za

Taifa

zifuatazo:

(a)utu;

(b) uzalendo;

(c)uadilifu;

(d)umoja;

(e)uwazi;

(f)uwajibikaji; na

(g)lugha ya Taifa.

Nyongeza katika ibara hii:-

(h)Utamaduni, Mila na Desturi

zinazokubalika kwa mujibu wa

sheria

Tanzania ni nchi inayoamini

misingi ya watu kuishi kindugu

bila kujali dini, rangi, kabila,

mila, desturi na utamaduni

5(i) (i)Udugu

5(j)

(j)Muungano Ni tunu ya Jamuhuri ya nchi

mbili zilizoungana kwa muda

mrefu licha ya misukosuko ya

hapa na pale ukaendelea kudumu

Sehemu ya pili-Mamlaka ya Wananchi,Utii na Hifadhi ya taifa

6

Jamhuri ya Muungano ni nchi inayofuata misingi ya

demokrasia inayozingatia haki ya kijamii, na kwa

hiyo:

Jamhuri ya Muungano ni nchi

inayofuata misingi ya

demokrasia inayozingatia haki

na usawa wa jamii, na kwa

hiyo:

Usawa ni dhana muhimu sana

katika maisha ndani ya jamii

6(a)

(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka za nchi, na

Serikali itapata madaraka na mamlaka yake kutoka

kwa wananchi ambao kwa umoja na ujumla wao

wanaimiliki na kuipatia Katiba hii uhalali;

(a) wananchi ndio msingi wa

mamlaka za nchi, na Serikali

itapata madaraka na mamlaka

yake kutoka kwa wananchi

Uandishi sahihi wa neno la

Kiswahili

ambao kwa umoja na ujumla wao

wanaimiliki na kuipa Katiba hii

uhalali;

6(b)

(b) lengo kuu la Serikali litakuwa ni maendeleo na

ustawi wa wananchi

(b) lengo kuu la Serikali litakuwa

ni maendeleo na ustawi wa

wananchi wote bila ubaguzi

Kuweka Msisitizo

7(2)(c )(j)

7(2)(c)Serikali itahakikisha kuwa shughuli

zinazofanywa zinatekelezwa kwa njia ambazo

zitahakikisha kwamba utajiri wa Taifa unaendelezwa,

unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya

wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia mtu

kumnyonya mtu mwingine;

7(2)(j)utajiri wa rasilimali na maliasili za Taifa

unaelekezwa katika kuleta maendeleo, kuondoa

umaskini, ujinga na

maradhi; na

-7(2)(c)Serikali itahakikisha

kuwa shughuli zinazofanywa

zinatekelezwa kwa njia ambazo

zitahakikisha kwamba

utajiri wa Taifa unaendelezwa,

unahifadhiwa na unatumiwa kwa

manufaa ya wananchi wote kwa

jumla bila ya unyonyaji wa aina

yoyote ile;

-utajiri wa rasilimali na

maliasili za Taifa

- utajiri wa taifa na utajiri wa

rasilimali na maliasili

vifafanuliwe katika kipengele

cha ufafanuzi katika rasimu

7(2)(d )

ardhi ikiwa rasilimali kuu na msingi wa Taifa,

inalindwa, inatunzwa na kutumiwa na wananchi wa

Tanzania kwa manufaa, maslahi na ustawi wa kizazi

cha sasa na vizazi

vijavyo;

ardhi ikiwa rasilimali kuu,

kielelezo cha uhai, utamuduni na msingi wa Taifa, inalindwa,

inatunzwa na kutumiwa na

wananchi wa Tanzania kwa

manufaa, maslahi na ustawi wa

kizazi cha sasa na vizazi

Kwa maisha ya mtanzania ardhi

ni uhai ,utamaduni na kielelezo

cha uchumi na maisha endelevu

7(2)(g )

utu, heshima na haki nyingine zote za binadamu

zinahifadhiwa na kudumishwa kwa kuzingatia mila na

utu, heshima na haki nyingine

zote za binadamu zinahifadhiwa

Kuepusha mila na desturi

kandamizi na hatarishi kwa

desturi za kitanzania na kwa kufuata mikataba

mbalimbali iliyoridhiwa na Jamhuri ya Muungano;

na kudumishwa kwa kuzingatia

mila na desturi za kitanzania

zinazokubalika kisheria na kwa

kufuata mikataba mbalimbali

iliyoridhiwa na Jamhuri ya

Muungano

baadhi ya makundi ya kijamii

8(1)

Bila ya kuathiri masharti ya Katiba za Washirika wa

Muungano kwa mambo yasiyo ya Muungano, Katiba

hii itakuwa sheria kuu katika Jamhuri ya Muungano.

Maneno bila kuathiri masharti ya

katiba za washirika wa

muungano kwa mambo yasiyo

ya muungano yaondolewe na

kusomeka tu „Katiba hii itakuwa

sheria kuu katika Jamuhuri ya

Muungano‟

-Hii inaipa katiba hii ya

Muungano kuwa katiba

kuu(Katiba mama ya muungano)

-Pia, itawezesha uandaaji wa

Katiba za nchi washirika kutii

katiba ya muungano

9(3)

(3) Kwa madhumuni ya kuhifadhi masharti ya Ibara

ndogo ya (1) na (2), Serikali itaweka utaratibu wa

kuisambaza Katiba hii kwa

wananchi na kuiweka katika mitaala ya elimu ili

kuwezesha wananchi kuifahamu, kuilinda na kuitii.

(3) Kwa madhumuni ya

kuhifadhi masharti ya Ibara

ndogo ya (1) na (2), Serikali

itaweka utaratibu wa kuisambaza

Katiba hii kwa

wananchi, kwa kuzingatia

mahitaji ya watu wenye

ulemavu na kuiweka katika

mitaala ya elimu ili kuwezesha

wananchi kuifahamu, kuilinda na

kuitii.

Kuna uwepo wa mahitaji ya

kipekee ya walemavu

SURA YA PILI-MALENGO MUHIMU,MISINGI YA MWELEKEO WA SHUGHULI ZA SERIKALI NA SERA ZA KITAIFA

11(3)(b )(i)

(i) kuhakikisha kwamba heshima ya binadamu

inahifadhiwa na kudumishwa kwa kufuata mila,

desturi na Kanuni za Tangazo la Dunia kuhusu

Haki za Binadamu na mikataba mingine ya

kimataifa iliyoridhiwa na Tanzania;

(i) kuhakikisha kwamba heshima

ya binadamu

inahifadhiwa na kudumishwa

kwa kufuata mila na desturi

zinazokubalika kisheria na

Kanuni za Tangazo la Dunia

Kuepusha mila na desturi

kandamizi kwa baadhi ya

makundi ya kijamii

kuhusu haki za Binadamu na

mikataba mingine ya

kimataifa iliyoridhiwa na

Tanzania;

11(3)(b)(ii)

(ii) kuhakikisha kwamba Serikali na vyombo vyake

vyote vya umma vinatoa nafasi na fursa zilizo sawa

kwa raia wote, bila ya kujali rangi, kabila, dini, nasaba,

hali ya mtu au mahali alipo;

(ii) kuhakikisha kwamba Serikali

na vyombo vyake

vyote vya umma vinatoa nafasi

na fursa zilizo sawa kwa raia

wote, bila ya kujali rangi, kabila,

dini, nasaba,jinsia hali ya mtu au

mahali alipo;

Jinsia ni neno linalobeba

jinsi,rika,mgawanyo wa

majukumu, mazingira, nk tofauti

na jinsi ambalo humaanisha

mwanamke au mwanaume

11(3)(c) (xii)

Nyongeza katika ibara 11(3)(c) Kuweka mazingira ya uhakika

wa chakula bora na maji salama

kwa wananchi

-Ni mahitaji muhimu kwa

wananchi kwa ustawi wa jamii

na ni jukumu la serikali

kuhakikisha upatikanaji wake

11(3)(c )(iii)

kuweka mazingira bora kwa ajili ya kuanzisha na

kuendeleza vyombo vya uwakilishi wa wakulima,

wafugaji na wavuvi;

kuweka mazingira bora kwa ajili

ya kuanzisha na kuendeleza

vyombo vya uwakilishi wa

wakulima,

wafugaji, wavuvi;na jamii

zingine za wazalishaji

Kuepusha kutaja aina mbalimbali

za wazalishaaji wa msingi nchini

kwani makundi ni mengi zaidi ya

wakulima, wavuvi na wafugaji

11(1)

11.-(1) Lengo Kuu la Katiba hii ni kulinda, kuimarisha

na kudumisha udugu, amani, umoja na utengamano

wa wananchi wa Jamhuri ya Muungano kwa

kuzingatia ustawi wa wananchi na kujenga Taifa huru

lenye demokrasia, utawala bora na kujitegemea.

11

utengamano wa watu litumike

badala ya wananchi

-neno watu linatumika sana kwa

uzoefu wa katiba za nchi

nyingine na pia sheria za

kimataifa zinatambua

watu(peoples)

SURA YA TATU-MAADILI NA MIIKO YA UONGOZI WA UMMA

Sehemu ya kwanza- Maadili ya viongozi wa umma&Sehemu ya pili-Miiko ya uongozi wa umma

15

15.-(1) Zawadi au kitu chochote kitakachotolewa kwa

mtumishi wa umma katika shughuli za kiserikali ni

15.-(1) neno tuzo liongezwe

Kupanua wigo wa uwajibikaji

zawadi kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na

itawasilishwa kwa Katibu

Mkuu Kiongozi kupitia kwa Katibu Mkuu wa Wizara

au taasisi ya Serikali inayohusika, akiainisha:

Sura hii inatakiwa Kutungiwa sheria ya maadili na miiko ya uongozi wa umma kwa nchi washirika katika

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania

Hakuna sheria ya muungano

kuhusiana na maadili na miiko ya

uongozi wa umma wala Katiba

ya Muungano haijaainisha

uwajibikaji huo kisheria

16(2)(c)

watoto wake walio chini ya umri wa miaka kumi na

nane, mara moja kila mwaka, au kadri

itakavyoamuliwa na sheria

watoto wake walio chini ya

uangalizi wake , mara moja kila

mwaka, au kadri

itakavyoamuliwa na sheria

Uzoefu unaonyesha kuwa watoto

huendelea kuwa chini ya

uangalizi wa wazazi hata wakiwa

zaidi ya miaka 18 na pia sheria

mbalimbali za nchi nyingi zina

ukomo wa miaka tofauti tofauti

kuhusiana na tafsiri ya umri wa

motto kutegemeana na

madhumuni ya sheria husika

14(3)

Wadhifa “Kiongozi wa Umma” kama ulivyotumika

katika Sehemu hii utajumuisha viongozi wa

kuchaguliwa na kuteuliwa kama watakavyoainishwa

kwenye sheria itakayotungwa na Bunge

Wadhifa “Kiongozi wa Umma”

kama ulivyotumika katika

Sehemu hii utajumuisha viongozi

wa kuteuliwa na kuainishwa

majukumu yake ikiwemo

kutangazwa hadharani kwa

umma kwa lengo la kutolewa

maoni na kuidhinishwa kama

watakavyoainishwa kwenye

sheria itakayotungwa na Bunge

-Kuepusha mgongano wa

kimaslahi

21(1) 21.-(1) Mtumishi wa umma aliye katika ajira ya

kudumu hataruhusiwa kuingia katika ajira nyingine

yoyote yenye malipo ya

mshahara.

Mtumishi wa umma aliye katika

ajira ya kudumu hataruhusiwa

kuingia katika ajira nyingine

yoyote yenye malipo ya

-kukuza uwajibikaji kwenye

utumishi wa umma na kuepusha

mgongano wa kimaslahi

mshahara, wala kujihusisha na

na shughuli za kibiashara

zinazoingiliana au kuleta

mgongano wa maslahi katika

uendeshaji wa shughuli zake

za umma,

SURA YA NNE-HAKI ZA BINADAMU,WAJIBU WA RAIA NA MAMLAKA ZA NCHI

Sehemu ya kwanza-Haki za Binadamu

23(2) Nyongeza katika Ibara ya 23 -haki ya kuishi inajumuisha

watoto ambao hawajazaliwa

Rasimu ipo kimya kuhusiana na

watoto ambao hawajazaliwa na

hivyo kutoa mwanya wa utoaji

wa mimba 23(3) -Kutoa mimba ni ukiukwaji wa

haki ya kuishi isipokuwa pale tu

itakapothibitishwa na mtaalamu

wa afya.

23 Kila mtu anayo haki ya kuishi na kupata hifadhi ya

maisha yake kutoka katika Serikali na jamii kwa

mujibu wa sheria.

Kila mtu anayo haki ya kuishi na

kupata hifadhi ya maisha yake

kutoka katika Serikali na jamii

Haki za binadamu ni haki asilia

japo zinapaswa kulindwa na

sheria

24(6) Neno “kubagua” lilivyotumiwa katika Ibara ndogo ya

(2), halitafafanuliwa kwa namna ambayo itaizuia

mamlaka ya nchi kuchukua hatua za makusudi zenye

lengo la kurekebisha matatizo mahsusi katika

jamii.

Suala la matatizo mahsusi

yafafanuliwe

-Kuepusha matumizi mabaya ya

ibara hii

24(7)(g) Nyongeza katika ibara hii 24(7) Haki ya kupata msaada wa

kisheria bure kwa mujibu wa

sheria itakayotungwa na Bunge

Watanzania wengi wanahitaji

huduma hii japo inakosekana

mahali pengi

28(2)(b)(iii) Kulinda manufaa ya umma kwa jumla au kuhifadhi

maslahi fulani mahsusi au maslahi ya sehemu fulani ya

umma,

-Ufafanuzi wa maneno manufaa

ya umma na maslahi fulani

mahsusi

-Kuepusha matumizi mabaya ya

ibara hii maneno hayo

yafafanuliwe katika kipengele

cha ufafanuzi

29(1)(b) Kila mtu anayo haki ya kupewa taarifa wakati wowote

kuhusu:

Kila mtu anayo haki ya kupewa

taarifa na serikali kutoa taarifa

Ni wajibu wa serikali kutoa

taarifa kwa umma pale

zinapohitajika

hizo wakati wowote kuhusu:

38(2) Mamlaka za nchi zitaweka utaratibu wa sheria

utakaowezesha:

(a) mtuhumiwa kupata nakala ya mashtaka

yanayomkabili na kumbukumbu ya mwenendo wa

mashtaka;

(b) mtuhumiwa au mfungwa kupata nakala ya

mwenendo wa mashtaka baada ya shauri kukamilika

mahakamani;

(c) Mtuhumiwa au mfungwa kufikishwa mahakamani

ili kuthibitisha uwepo wake.

Nyongeza :

Mamlaka za nchi zitaweka

utaratibu wa sheria

utakaowezesha:

(b) mtuhumiwa au mfungwa

kupata nakala ya hukumu na

nakala ya mwenendo wa

mashtaka baada ya shauri

kukamilika mahakamani;

.

(d)Mtuhumiwa au mfungwa

mweye ulemavu kupatiwa

nyenzo za kujimudu kutokana

na mahitaji yake

Hukumu zinachelewa sn na

wakati mwingine hazitolewi

kabisa na ni haki ya lazima

katika miendendo ya mahakama

-Kumwezesha mtu mwenye

ulemavu kumudu hali wakati

anapokuwa kizuizini

42(1)a 42.-(1) Kila mtoto ana haki ya-

(a) kupewa jina na uraia;

kila mtoto ana haki ya kupewa

jina stahiki na uraia

Kuepusha watoto kupewa majina

yanayotweza utu wao bila ridhaa

yao

44(1) b kupata elimu kwa kutumia vifaa maalum na kushiriki

katika shughuli za kijamii;

kupata elimu na kujifunza kwa

kutumia vifaa maalum na

kushiriki

katika shughuli za kijamii;

Ili kumwezesha mwenye

ulemavu kujifunza kwa nyenzo

badala ya kutegemea

kufundishwa kupata elimu tu

44(1)(g) Nyongeza

kiepengele (g) katika ibara hii

-kulindwa na kupata msaada wa

kisheria

Itaepusha watu wenye ulemavu

kusaidiwa kisheria pale

wanapohitaji msaada huu

kulingana na aina ya ulemavu

45 Mamlaka ya nchi itaweka utaratibu wa sheria

utakaowezesha makundi madogo katika jamii:

Neno makundi madogo

litafsiriwe kumaanisha kikundi

katika jamii kilichokosa au

Makundi madogo linaleta

mkanganyiko wa nani anahusika

kuwa katika kundi dogo na

kunyimwa fursa sawa na

makundi mengine (marginalized

or vulnerable)

vigezo vyake kama ni idadi ya

watu au uwezo wa kiuchumi au

nafasi katika jamii

46(g) kupata huduma ya juu ya afya inayopatikana. kupata huduma bora ya afya

inayopatikana.

Kiswahili sahihi

47 Mamlaka ya nchi itaweka utaratibu utakaowezesha

wazee kupata fursa ya:

Ukomo wa umri uwekwe

kwenye katiba au sheria itoe

tafsiri kuwa ni watu wenye umri

wa kuanzia miaka 60

kuepusha mgongano

unaojitokeza katika matumizi ya

neno uzee

Sehemu ya Pili-Wajibu wa Raia na Mamlaka za Nchi

52(1) Katika kutafsiri masharti ya Sura hii ya Haki za

Binadamu, Mahakama, Baraza au chombo kingine

chochote cha kufanya uamuzi kitazingatia mambo

yafuatayo:

(a) haki ya usawa, utu na uhuru wa mtu binafsi;

(b) sheria za kimataifa na haki za binadamu; na

(c) haki za jamii na maslahi ya jamii kwa ujumla

Nyongeza ibara hii (d)

(d)Misingi ya haki asilia

Haki za msingi kwa binadamu

wote

MAONI NA MAPENDEKEZO YA MASUALA YASIYOJITOKEZA KATIKA SURA YA NNE

HAKI YA KUMILIKI ARDHI:-

Ardhi yote ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ni mali ya watu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania

1. Kila raia ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ana haki ya kupata, kutumia, kugawa, kuuza, kununua, kumiliki na kudhibiti ardhi katika

jamhuri

2. Ni marufuku kwa mtu asiye raia wa jamhuri ya muungano kumiliki ardhi katika jamhuri ya muungano isipokuwa wageni watapewa fursa ya

kupangisha ardhi kwa kiwango na ukomo maalumu kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maenedelo ya jamhuri

3. Serikali itakuwa na jukumu la kuhakikisha kuwa ardhi na rasilimali zitatumiwa kwa misingi ifuatayo

(a) matumizi endelevu ya ardhi kwa kuzingatia vizazi vijavyo

(b) usawa wa jinsia katika upatikanaji na matumizi ya ardhi

(c ) Mfumo shirikishi wa usimamizi wa ardhi unaowapa wananchi fursa ya kufanya maamuzi kwa njia za kidemokrasia

(d) ulipwaji wa fidia kamili, ya haki na kwa wakati endapo umiliki utasitishwa kwa sababu yoyote ile kwa manufaa ya watu wa Jamhuri ya muungano

ya Tanzania yatakayokuwa yamebainishwa katika sheria itakayotungwa na Bunge

(e) Mfumo shirikishi, fanisi na rahisi na wa haraka katika wa utatuzi wa migogoro ya ardhi

4. Misingi ya umiliki, matumizi na usimamizi wa ardhi iliyowekwa na katiba hii itazingatiwa na na kulindwa washirika wa jamhuri ya muungano kwa

sheria zitakazotungwa na mabunge ya washirika wa Muungano

SURA YA TANO-URAIA KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO

Ibara za Sura hii

zimetumia maneno:-

Tanzania bara na

Zanzibar

Ibara takribani zote zina maneno-Tanzania bara na

Zanzibar

Kila palipotumiwa neno

Tanzania Bara pasomeke -

Jamhuri ya Tanganyika na

palipotumiwa neno Zanzibar

pasomeke Jamhuri ya watu wa

zanzibar

1964 muungano ulihusisha

Jamuhuri ya Tanganyika na

Jamuhuri ya watu wa Zanzibar

Hoja ya Uraia wa nchi mbili:-

54(2) (2) Uraia wa Jamhuri ya Muungano ni wa aina mbili

na utapatikana kwa njia ya kuzaliwa au kujiandikisha.

Uraia wa Tanzania ni wa aina

moja na unapatikana kwa njia ya

kuzaliwa au kujiandikisha

Raia wa Tanzania haruhusiwi

kuwa na uraia wa nchi nyingine

hadi pale atakapoukana uraia wa

Tanzania. Raia wa kuzaliwa na

kujiandikisha wana hadhi sawa

za uraia hivyo hakuna uraia wa

aina mbili

54 54.-(1) Mtu ambaye,kabla ya Katiba hii kuanza

kutumika, ni raia wa Jamhuri

ya Muungano ataendelea kuwa raia wa Tanzania.

(2) Uraia wa Jamhuri ya Muungano ni wa aina mbili

na utapatikana kwa njia

ya kuzaliwa au kujiandikisha.

Nyongeza katika ibara hii

54(3)Raia wa Tanzania atapoteza

uraia wake kwa kuwa raia wa

nchi nyingine

54(4) Raia wa nchi nyingine

atapata uraia wa jamuhuri wa

muungano wa Tanzania kwa

kujiandikisha kulingana na

masharti ya sheria itakayotungwa

Kulinda uzalendo na asili ya

watu wa jamhuri ya muungano

na Bunge

55(4) Mtoto mwenye umri chini ya miaka saba akikutwa

ndani ya mipaka ya Jamhuri ya Muungano katika

mazingira ambayo wazazi wake hawajulikani,

atahesabika kuwa ni raia wa Jamhuri ya Muungano wa

kuzaliwa.

Mtoto mwenye umri chini ya

miaka saba akikutwa ndani ya

mipaka ya Jamhuri ya Muungano

katika mazingira ambayo wazazi

wake hawajulikani, atadhaniwa

(presumed) kuwa ni raia wa

Jamhuri ya Muungano wa

kuzaliwa. Endapo itathibitika

kwamba wazazi wake si raia

wa Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania haki hii itafutika na

ataruhusiwa kuomba uraia

kwa kujiandikisha

-hii itasaidia kudhibiti uingiaji

holela wa wageni hasa kwenye

nchi zenye matatizo ya kivita na

pia kuzingatia haki na maslahi ya

mtoto

56(3) Endapo ndoa iliyorejewa katika Ibara ndogo ya (2)

itavunjika, kama mtu huyo hakuukana uraia wake,

ataendelea kuwa raia wa Jamhuri ya Muungano.

Endapo ndoa iliyorejewa katika

Ibara ndogo ya (2) itavunjika,

kama mtu huyo hakuukana uraia

huo, ataendelea kuwa raia wa

Jamhuri ya Muungano

-Kuondoa utata wa tafsiri wa

uraia upi unaozungumziwa

56(4) Mtoto aliyezaliwa katika ndoa iliyorejewa katika Ibara

ndogo ya (2), ataendelea kuwa raia wa Jamhuri ya

Muungano isipokuwa kama ataukana uraia huo

au ataomba na kupata uraia wa nchi nyingine

.

Maneno

…au ataomba na kupata uraia

wa nchi nyingine…yafutwe

Rasimu hii ina dhana ya

kutambua uraia wa nchi mbili

bila kuwa bayana hivyo ili

kuweka msimamo wa kuwa na

uraia wa nchi moja tu inabidi

isomeke hivyo

SURA YA SITA- MUUNDO WA JAMUHURI YA MUUNGANO

Ibara za Sura hii

zilizoainishia

maneno:-

Shirikisho,Serikali ya

Tanzania bara,

Katiba itamke kuwa Tanzania ni jamhuri ya shirikisho la nchi mbili za Jamhuri ya

Tanganyika na jamhuri ya watu wa Zanzibar yenye muundo wa serikali tatu ambazo ni

Serikali ya jamhuri ya shirikisho la Tanzania, serikali ya Jamhuri ya Tanganyika na

serikali ya jamhuri ya watu wa Zanzibar

ufafanuzi huu unaondoa utata

wa kuyatumia maneno

muungano na shirikisho kwa

pamoja kana kwamba yana

maana moja

SURA YA SABA-SERIKALI YA JAMHURI YA MUUNGANO

Sehemu ya Kwanza-Serikali,Rais na Makamu wa Rais

69(1)(j)(k) (k) kuidhinisha utekelezaji wa

adhabu ya kifo iliyotolewa kwa

mujibu wa sheria za nchi.

Kifungu hiki kifutwe Inakinzana na haki ya mtu kuishi

75(c) angalau mmoja kati ya wazazi

wake ni raia wa kuzaliwa wa

Jamhuri ya Muungano;

wazazi wake ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya

Muungano;

Uzalendo

75(d) wakati wa kugombea, ana umri

usiopungua miaka arobaini;

Wakati wa kugombea, ana umri usiopungua miaka

thelathini na tano(35) na usiozidi miaka Sitini (60

Umri muafaka wa kugombea na

pia ukomo wa juu ni umri wa

kustaafu utumishi wa kawaida

wa umma ukiacha wa

kuchaguliwa au kuteuiwa

75(a-l) Nyongeza ibara ya 75(m) Atakuwa ameshiriki mdahalo wa wazi utakaoratibiwa

na Tume ya uchaguzi

Kutoa fursa kwa wananchi wote

kutambua uwezo wa kiongozi

atakayewaongoza

83(3) (3) Isipokuwa kama ataacha

kushika madaraka ya Rais

kutokana

na kura ya kutokuwa na imani

na Rais, haitakuwa halali kwa

mtu

kumshtaki au kufungua

mahakamani shauri lolote la

jinai au la madai

dhidi ya mtu aliyekuwa

anashika madaraka ya Rais

baada ya kuacha

madaraka hayo kutokana na

jambo alilofanya wakati

alipokuwa bado

anashika madaraka ya Rais.

(3) Isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais

kutokana na kura ya kutokuwa na imani na Rais,

itakuwa halali kwa mtu kumshtaki au kufungua

mahakamani shauri lolote la jinai au la madai dhidi ya

mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais kabla na

baada ya kuacha madaraka hayo kutokana na jambo

alilofanya wakati alipokuwa bado anashika madaraka

ya Rais

Hakuna mtu aliye juu ya sheria

84(6) Endapo hoja ya kuunda Kamati Endapo hoja ya kuunda Kamati ya Uchunguzi itaungwa Asilimia 75 zilizopendekezwa

ya Uchunguzi itaungwa

mkono na Wabunge

wasiopungua asilimia sabini

na tano ya Wabunge

wote, Spika atatangaza majina

ya wajumbe wa Kamati ya

Uchunguzi

mkono na Wabunge wasiopungua wasiopungua 2/3 ya

wabunge wote, Spika atatangaza majina ya wajumbe

wa Kamati ya Uchunguzi

hapo awali ni nyingi na inaweza

isiwe rahisi kufikiwa

84(7) Kamati ya Uchunguzi, kwa

madhumuni ya Ibara hii,

itakuwa na

wajumbe wafuatao:

(a) Jaji Mkuu wa Jamhuri ya

Muungano, ambaye atakuwa

Mwenyekiti wa Kamati;

(b) Jaji Mkuu wa Tanzania

Bara;

(c) Jaji Mkuu wa Zanzibar; na

(d) wajumbe wengine sita

watakaoteuliwa na Spika.

jukumu la kuchagua wajumbe kwenye kamati ya

uchunguzi litakuwa la kamati inayohusika na Sheria na

Katiba au Kamati inayofanana na hiyo

Kuleta heshima kwenye

mchakato mzima wa utekelezaji

wa majukumu ya Kamati ya

Uchunguzi. Vilevile kulinda

heshima ya chombo cha

mahakama katika utendaji

84(12) Baada ya taarifa ya Kamati ya

Uchunguzi kuwasilishwa,

Bunge litaijadili taarifa hiyo na

kutoa fursa kwa Rais kujieleza,

na kisha, kwa kura za Wabunge

wasiopungua asilimia sabini na

tano ya Wabunge wote, Bunge

litapitisha azimio kuwa

mashtaka dhidi ya Rais ama

yamethibitika au

hayakuthibitika.

Baada ya taarifa ya Kamati ya Uchunguzi

kuwasilishwa, Bunge litaijadili taarifa hiyo na kutoa

fursa kwa Rais kujieleza, na kisha, kwa kura za

Wabunge wasiopungua 2/3 ya Wabunge wote, Bunge

litapitisha azimio kuwa mashtaka dhidi ya Rais ama

yamethibitika au hayakuthibitika.

Asilimia 75 zilizopendekezwa

hapo awali ni nyingi na inaweza

isiwe rahisi kufikiwa

85(2) Mshahara na malipo mengineyo

yote ya Rais hayatapunguzwa

mishahara ya Rais na malipo mengine yoyote yanaweza

kuongezwa au kupunguzwa kulingana na hali ya

Kuleta usawa na kukamilisha

dhana ya utumishi kwa umma

wakati Rais atakapokuwa bado

ameshika madaraka yake kwa

mujibu wa Katiba hii.

uchumi wa taifa na hali halisi ya watumishi wengine wa

umma

85(3) 85.-(1) Rais atalipwa mshahara

na malipo mengineyo kama

yatakavyoainishwa na Tume ya

Utumishi wa Umma na

atakapostaafu

atapokea malipo ya uzeeni na

stahili nyingine kutoka Mfuko

Mkuu wa

Hazina ya Serikali ya Jamhuri

ya Muungano.

(2) Mshahara na malipo

mengineyo yote ya Rais

hayatapunguzwa wakati Rais

atakapokuwa bado ameshika

madaraka

yake kwa mujibu wa Katiba hii.

Nyongeza katika kipengele hiki

(3)Mshahara wa Rais hautakuwa wa kifahari na

utakatwa kodi kama ilivyo kwa mishahara ya watumishi

wengine wa umma

Awali kipengele hiki

hakikuwepo hali inayo ondoa

usawa katika utumishi wa umma

92(2) (2) Mwanasheria Mkuu wa

Serikali atahudhuria vikao vya

Baraza la Mawaziri lakini

hatakuwa na haki ya kupiga

kura.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali atahudhuria vikao vya

Baraza la Mawaziri lakini atakuwa na haki ya kupiga

kura

Baraza la Mawaziri ni la

kitaaluma na Mwanasheria Mkuu

naye ni mwanataaluma kwahiyo

ana haki ya kupiga kura

92(5) Nyongeza Wizara ya Mambo ya Nje, Wizara ya Ulinzi na

Usalama, Wizara ya Fedha na Wizara ya Katiba

zitatambulika kama wizara andamizi

Kuweka madaraja na hadhi

katika utendaji katika shughuli za

serikali

93(2) Kwa madhumuni ya Ibara

ndogo ya (1), idadi ya Mawaziri

wa Serikali ya Jamhuri ya

Muungano haitozidi kumi na

tano.

…Idadi ya Wizara na Mawaziri itazingatia idadi ya

masuala ya Muungano yaliyoorodheshwa kwenye

nyongeza ya rasimu hii

Kupunguza mrundikano wa

wizara na kuipunguzia serikali

gharama

94(1)(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri

ya Muungano kwa mujibu wa

Sheria za nchi;na

Ni raia wa Jamhuri ya Muungano wa kuzaliwa au

wa kuandikishwa ambaye amedumu na huo uraia

wa kuandikishwa kwa miaka 15

Kutoa fursa kwa raia wengine

kupata fursa ya kutumikia umma

97(1) Kutakuwa na Mwanasheria

Mkuu wa Serikali ya

Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania ambaye katika Katiba

hii atatajwa tu kwa kifupi kama

"Mwanasheria Mkuu" ambaye

atateuliwa na Rais na

kuthibitishwa na Bunge.

Kutakuwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye katika

Katiba hii atatajwa tu kwa kifupi kama "Mwanasheria

Mkuu" ambaye atateuliwa na Rais kutoka miongoni

mwa majina yatakayowasilishwa kwake na tume ya

utumishi wa mahakama na hatashika wadhifa wake hadi

atakapohojiwa, kujadiliwa na kuthibitishwa na Bunge.

Kuongeza umakini katika kupata

raia makini kwenye nafasi hii

97(2)(d) awe ni mtumishi mwandamizi

katika utumishi wa umma

au taasisi zake;

au Mwanasheria mwenye sifa ya kuwa jaji wa

mahakama kuu kutoka katika vyama vya kitaaluma vya

wanasheria au miongoni mwa wanachama waliotumikia

vyama hivyo kwa muda usiopungua miaka kumi na

tano.

ili kupanua wigo wa watu wenye

sifa kuteuliwa kwa nafasi hiyo

hata kama hawamo katika

utumishi wa umma

98(1) 98.-(1) Kutakuwa na Katibu

Mkuu Kiongozi atakayeteuliwa

na Rais kutoka miongoni mwa

watumishi waandamizi na

kuthibitishwa na

Bunge.

98.-(1) Kutakuwa na Katibu Mkuu Kiongozi

atakayeteuliwa na Rais kutoka miongoni mwa

watumishi waandamizi wa umma ambaye kabla ya

kushika wadhifa wake atahojiwa, kujadiliwa na

kuthibitishwana Bunge

kutanua wigo wa uwazi na

uwajibikaji katika uteuzi wa

viongozi wenye dhamana ya

utumishi wa umma

SURA YA TISA-BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO

Sehemu ya kwanza-Kuundwa kwa Bunge la Jamhuri ya muungano

105(2)(b) Wabunge watano

watakaoteuliwa na Rais kutoka

miongoni

mwa watu wenye sifa za

kuchaguliwa kuwa wabunge

kuwakilisha watu wenye

ulemavu kwa kuzingatia uwiano

wa Washirika wa Muungano.

Wabunge watano watakaoteuliwa na Rais baada ya

mashauriano na vyama vya walemavu

vilivyosajiliwa kisheria kutoka miongoni mwa watu

wenye sifa za kuchaguliwa kuwa wabunge kuwakilisha

watu wenye ulemavu kwa kuzingatia uwiano wa

Washirika wa Muungano.

Kutoa fursa ya ushirikishwaji wa

makundi yenye ulemavu

yanayowakilishwa na wabunge

na pia kuwezesha dhana ya

uwajibikaji wa wabunge katika

makundi hayo

SURA YA KUMI-MAHAKAMA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Sehemu ya Kwanza-Misingi ya utoaji Haki na Uhuru waMahakama

-Maoni kuhusiana na muundo wa Mahakama ya juu na mahakama ya rufani-

-Rufaa zote ziishie mahakama ya Rufani pekee

-Mahakama ya juuIsikilize masuala muhimu matatu yafuatayo

(i) kusikiliza na kuamua mara ya kwanza na mwisho mashauri yanayohusu uchaguzi wa Rais na wabunge wa Jamhuri ya muungano;

–(ii) kusikiliza na kuamua mashauri kuhusu tafsiri ya Katiba ya Shirikisho yanayoletwa na serikali yoyote kati ya tatu zilizopo;

–(iii) kusikiliza na kuamua migogoro baina ya serikali hizo inayoletwa na mmoja wao.

146(2) (2)Mahakama Kuu ya Tanzania

Bara na Mahakama Kuu ya

Zanzibar zitakuwa na mamlaka

sawa ya kusikiliza katika ngazi

ya awali,

mashauri ya madai na jinai

kuhusu Mambo ya Muungano

katika maeneo

ya utawala ya Washirika wa

Muungano.

Ibara hii ifutwe Mahakama ya juu ndo yenye

jukumu la kusikiliza kwanza na

mwisho mambo ya muungano

147(1)(a)(b) 147.-(1)Kutakuwa na

Mahakama ya Juu ya Jamhuri

ya

Muungano au kwa kifupi

itaitwa “Mahakama ya Juu”

ambayo itakuwa

na:

(a) Jaji Mkuu ambaye atakuwa

Rais wa Mahakama ya Juu;

147.-(1)Kutakuwa na Mahakama ya Juu ya Jamhuri ya

Muungano au kwa kifupi itaitwa “Mahakama ya Juu”

ambayo itakuwa

na:

(a) Jaji Mkuu ambaye atakuwa mkuu wa mhimili wa

Mahakama ya Juu;

(b) Naibu Jaji Mkuu ambaye atakuwa Makamu mkuu

wa

Mhimili wa Mahakama ya Juu; na

-Neno Rais limetumika kuonesha

“ukuu” wa wadhifa katika

mhimili wa kimahakama

(b) Naibu Jaji Mkuu ambaye

atakuwa Makamu wa Rais wa

Mahakama ya Juu; na

147(1)(c) (c) Majaji wengine wa

Mahakama ya Juu wasiopungua

saba.

(c) Majaji wengine wa Mahakama ya Juu wasiopungua

watatu ( 3)

Idadi hii itapungua pale tu

majukumu matatu pekee ndo

yatakayoshughulikiwa na

mahakama ya juu. Pia itaepusha

serikali kuingia gharama kubwa

ya idadi ya majaji kama

inavyosomeka katika Rasimu

149(1)(a) Mahakama ya Juu itakuwa ni

ngazi ya mwisho ya rufani

katika Jamhuri ya Muungano na

itakuwa na madaraka ya:

(a) pekee na ya awali ya

kusikiliza na kuamua mashauri

yanayohusu matokeo ya

uchaguzi wa Rais wa Jamhuri

ya Muungano;

Mahakama ya Juu itakuwa ni ngazi ya mwisho ya rufani

katika Jamhuri ya Muungano na itakuwa na madaraka

ya:

(a) pekee na ya awali ya kusikiliza na kuamua mashauri

yanayohusu matokeo ya uchaguzi wa Rais na wabunge

wa Jamhuri ya Muungano;

Wabunge wa muungano

umeongezwa kutokana na

mhimili huu wa juu na mwisho

149(1)(d) kusikiliza na kuamua rufani

kutoka Mahakama ya Rufani;

Inafutwa -Hii ni kutokana na pendekezo la

kuifanya mahakama ya Rufani

kuwa mahakama ya mwisho kwa

ajili ya Rufaa

153(3) (3) Kwa kuzingatia masharti ya

Ibara ndogo ya (2), iwapo Rais

ataridhika kwamba japokuwa:

(a) mtu mwenye sifa mojawapo

ya hizo sifa zilizoainishwa

katika Ibara ndogo ya (2)

hakuwa nayo sifa hiyo kwa

muda

‐ 60 ‐unaopungua miaka kumi;

Inafutwa Ibara hii inatoa mwanya kwa

watu wasio na sifa kuteuliwa na

Rais

na

(b) mtu huyo ana uwezo, ujuzi

na kwa kila hali anafaa

kukabidhiwa madaraka ya Jaji

wa Mahakama ya Juu;

(c) kuna sababu za kumfanya

mtu huyo kustahili kukabidhiwa

nafasi ya madaraka hayo,

basi Rais anaweza kutengua

sharti la kuwa na sifa kwa muda

usiopungua

miaka kumi, na baada ya

kushauriana na Tume ya

Utumishi wa

Mahakama, kumteua mtu huyo

kuwa Jaji wa Mahakama ya Juu.

155(3) Bila ya kuathiri masharti ya

Ibara ndogo ya (1) na (2), Jaji

Mkuu, Naibu Jaji Mkuu na Jaji

wa Mahakama ya

Juualiyetimiza umri wa kustaafu

atalazimika kuendelea kufanya

kazi baada ya kutimiza umri

huo mpaka amalize kutayarisha

na kutoa hukumu au mpaka

akamilishe

shughuli nyingine yoyote

inayohusika na mashauri

ambayo alikwishaanza

kuyasikiliza kabla hajatimiza

umri wa kustaafu.

Bila ya kuathiri masharti ya Ibara ndogo ya (1) na (2),

Jaji Mkuu, Naibu Jaji Mkuu na Jaji wa Mahakama ya

Juu aliyetimiza umri wa kustaafu atalazimika kuendelea

kufanya kazi baada ya kutimiza umri huo kwa kipindi

cha miaka mitatu mpaka amalize kutayarisha na kutoa

hukumu au mpaka akamilishe shughuli nyingine yoyote

inayohusika na mashauri ambayo alikwishaanza

kuyasikiliza kabla hajatimiza umri wa kustaafu.

Kudhibiti utendaji wa majaji

kuendelea kufanya kazi katika

kipindi kirefu baada ya kutimiza

umri wa kustaafu

162(3) Mtu anaweza kuteuliwa kuwa Mtu anaweza kuteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Kuwezesha utendaji wa kazi

Mwenyekiti wa Mahakama ya

Rufani endapo atakuwa

amefikisha umri wa miaka

arobaini na tano au zaidi na

mwenye sifa ya uadilifu, tabia

njema na uaminifu na:

Mahakama ya Rufani endapo atakuwa amefikisha umri

wa miaka arobaini na tano na usiozidi miaka sitini (60)

na mwenye sifa ya uadilifu, tabia njema na uaminifu na:

katika kipindi ambacho mtu ana

uwezo wa kutenda kazi

kulingana na umri wake

Ilivyoandikwa-SURA YA KUMI NA MOJA-UTUMISHI WA JAMHURI YA MUUNGANO

Inavyopendekezwa-UTUMISHI KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO

177- Bila ya kuathiri masharti ya

Katiba hii, utumishi wa umma

na uongozi katika Jamhuri ya

Muungano utazingatia misingi

kwamba utoaji wa ajira na

uteuzi wa viongozi utakuwa

kwa uwiano baina ya Washirika

wa Muungano, kwa kuzingatia

weledi na taaluma katika eneo

au nyanja husika.

Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, utumishi wa

umma na uongozi katika Jamhuri ya Muungano

utazingatia misingi kwamba utoaji wa ajira na uteuzi wa

viongozi utakuwa kwa uwiano utakaoainishwa kwa

mujibu wa sheria itakayotungwa na Bunge

- -Kuepusha migororo ya

kutokubaliana kuhusu idadi ya

uwiano wa watumishi kutoka

nchi za shirikisho

SURA YA KUMI NA MBILI-UCHAGUZI KATIKA VYOMBO VYA UWAKILISHI NA VYAMA VYA SIASA

Sehemu ya Kwanza-Uwakilishi wa wananchi

181(6)(c) (c) mtu ambaye anashika nafasi

ya madaraka katika asasi zisizo

za kiserikali au aliyewahi

kushika nafasi ya madaraka

katika

asasi zisizo za kiserikali ndani

ya muda usiozidi miaka mitano

kabla ya uteuzi kufanyika.

MANENO “au aliyewahi kushika nafasi ya madaraka

katika asasi zisizokuwa za kiserikali ndani ya muda

usiozidi miaka mitano kabla ya uteuzi kufanyika”

yafutwe

Hakuna sababu ya kuwabana

waliowahi kushika madaraka

katika asasi za kiraia wakati

waliowahi kuwa watumishi

katika utumishi wa umma

hawajazuiwa. Ili kutoa fursa

sawa kwa watu wote, maneno

hayo yafutwe au maneno kama

hayo yaongezwe kwenye ibara ya

181(6) (b)

184(1)(e) Kutayarisha na kuchapisha

ripoti za kila mwaka kuhusu

ripoti za ukaguzi wa fedha wa

kila chama cha kisiasa; na

kutayarisha na kuchapisha ripoti za kila mwaka kuhusu

ripoti za ukaguzi wa fedha wa kila chama cha kisiasa;

na wagombea huru

Rasimu hii imetambua uwepo wa

wabombea huru ambao ibara hii

haikuwaainisha

184(8) (8) Kwa madhumuni ya Ibara

ndogo ya (8), watu wanaohusika

na uchaguzi ni-

(8) Kwa madhumuni ya Ibara ndogo ya (7), watu

wanaohusika na uchaguzi ni-

Makosa ya kiuchapaji Ilipaswa

kuwa ibara ndogo ya 7

SURA YA KUMI NA TATU-TAASISI ZA UWAJIBIKAJI

Mapendekezo ya Jumla katika sura hii-Sifa na upatikanaji wa wajumbe wa Tume ya maadili na tume ya haki za binadamu hazijaainishwa. Pia

upatikanaji uende sambamba na kuanza kwa utekelezaji wa kazi pamoja na Mwenyekiti na Makamu mwenyekiti wa Tume hiziPia sheria

itakayotungwa na Bunge izingatie mapendekezo haya ikiwa ni pamoja na sifa zifuatazo

Sifa za wajumbe wa Tume ya Maadili ya uongozi

-Awe raia wa kuzaliwa nchini na wazazi wake ni raia wa kuzaliwa wa Tanzania

-Awe amefuzu mafunzo ya sheria,uhasibu na utumishi wa umma;

-ana uzoefu usiyopungua miaka kumi na tano katika utumishi

wa umma;

-ana uzoefu usiyopungua miaka kumi na tano katika masuala

yanayohusu maadili ya uongozi wa umma; na

-ni mtu mwenye heshima, weledi, uaminifu, uadilifu na asiye

na upendeleo unaotiliwa shaka na jamii.

Sifa za wajumbe wa Tume ya haki za Binadamu

-Awe raia wa kuzaliwa nchini na wazazi wake ni raia wa kuzaliwa Tanzania

-awe amefuzu mafunzo ya juu ya Sheria,haki za binadamu na utawala bora

- ana uzoefu usiyopungua miaka kumi na tano katika utumishi

wa umma;

-ana uzoefu usiyopungua miaka kumi na tano katika masuala

yanayohusu haki za binadamu na utawla bora na

-ni mtu mwenye heshima, weledi, uaminifu, uadilifu na asiye

na upendeleo unaotiliwa shaka na jamii.

Mapendekezo ya namna ya upatikanaji wa wajumbe wa Tume

-Watateuliwa na Rais baada ya kupendekezwa na Tume ya Utumishi wa Umma

Sehemu ya Kwanza-Tume ya Maadili ya Uongozi na Uwajibikaji

194(c) (c)mtu mwenye uzoefu wa

utumishi wa umma kwa kipindi

kisichopungua miaka kumi

(c)mtu mwenye uzoefu wa masuala ya haki za

binadamu na masuala ya kijamii kwa kipindi

kisichopungua miaka kumi

-Kuepusha kuzuia watu ambao

hawajapata fursa za ajira katika

utumishi wa umma lakini

wanauzoefu.

202(1)(d) (d)kutayarisha ripoti ya mwaka

na kuiwasilisha Bungeni kwa

ajili ya kujadiliwa na kutolewa

mapendekezo.

(d)kutayarisha ripoti ya mwaka na kuiwasilisha kwa

tume ya maadili na kisha Bungeni kwa ajili ya

kujadiliwa na kutolewa mapendekezo.

Kuwezesha tume ya maadili

kutekeleza majukumu yake kama

yaliyoainishwa

SURA YA KUMI NA TANO –ULINZI NA USALAMA KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO

232,235 Zinapedekezwa kufutwa Kuepusha mgongano wa

majukumu ya majeshi hayo dhidi

ya majeshi ya nchi za muungano

SURA YA KUMI NA SITA-Mengineyo

238 Nyongeza katika ibara hii Masuuli,maduhuli,watu,wananchi,utajiri wa rasilimali

na maliasili,unyonyaji, wakala, kila mtu, raia,maslahi ya

umma,wabunge

Kurahisisha tafsiri ya matumizi

ya maneno katika Katiba hii na

kuepusha matumizi ya maneno

kutafsriwa kwa Nyanja pana na

kupelekea kuibuka kwa

mgongano wa tafsiri za ibara ya

Katiba

SEHEMU YA

NYONGEZA

KATIKA KATIBA

Mambo ya muungano Mahakama ya muungano Ni eneo muhimu la muungano