mpango kazi wa ushiriki wa mtoto tanzania - cdftz
TRANSCRIPT
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA
WATOTO
MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA
2014 - 2019
JANUARI, 2014
ii
Dibaji
Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012,
idadi ya watoto Tanzania Bara wenye umri chini ya miaka 18 ilikuwa ni 21,866,258,
ambao ni sawa na asilimia 50.1 ya idadi ya watu wote. Kati yao wasichana walikuwa
10,943,846 na wavulana walikuwa 10,922,412. Idadi ya watoto chini ya umri wa miaka
minane walikuwa 11,181,278 sawa na asilimia 51.1 ya watoto wote. Pamoja na kuwepo
kwa idadi hii kubwa ya watoto wa Tanzania ni kundi kubwa la jamii ambalo linakutana
na changamoto nyingi kimaisha. Pamoja na wingi wa kundi hili, haki zao nyingi
zinavunjwa na kwa muda mrefu walikuwa hawana chombo maalum cha kuwatetea na
sauti zao zilikuwa hazisikiki vya kutosha kwa kuwa walikuwa hawashiriki katika kufanya
maamuzi yanayohusu maisha yao licha ya uwepo wa sera na sheria mbalimbali za
kuwalinda. Athari kubwa wanayoipata watoto hao ni kukosa haki zao za msingi kama
zilivyoainishwa katika Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008, Sheria ya Mtoto ya
Mwaka 2009, Mikataba mbalimbali ya Kimataifa na ya Kikanda kuhusu haki za mtoto na
hivyo kuathiri ukuaji na ustawi wao na maisha yao kwa ujumla na hata maendeleo ya
nchi yetu.
Pamoja na juhudi za serikali kuandaa sera, sheria na mipango mbalimbali ya kumjali
mtoto, kumekuwepo na changamoto mbalimbali zinazokwamisha utekelezaji wa
programu za kumuendeleza na kumjenga mtoto na kulinda haki zake. Changamoto hizo
ni pamoja na ukosefu wa rasilimali fedha, ushiriki mdogo wa jamii katika kutatua tatizo
la uvunjaji wa haki za watoto, na uelewa mdogo wa jamii kuhusu haki za watoto. Kwa
hali hiyo, umuhimu wa suala la ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi yanayohusu
maisha yao umekuwa ni kitu cha kupewa kipaumbele ili sauti zao zisikike na mchango
wao uonekane katika kutetea haki zao.
Kwa hali ilivyo sasa, ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi ya masuala yanayohusu
maisha yao ni suala linalotiliwa mkazo sana nchini Tanzania hasa baada ya kuridhia
Mkataba wa Haki za Mtoto mwaka 1991. Baada ya hapo serikali iliona umuhimu wa
ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi mbalimbali kwa utaratibu rasmi na wenye
muendelezo mzuri hasa baada ya tukio la ushiriki wa watoto katika Kikao Maalum kwa
watoto kilichoandaliwa na Umoja wa Mataifa cha mwaka 2002 na hivyo kupendekeza
uwepo wa chombo mahsusi cha Kitaifa cha uwakilishi wa kudumu wa watoto yaani
Baraza la Taifa la Watoto chini ya usimamizi wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia
na Watoto.
Juhudi nyingine za kuwahusisha watoto katika ushiriki ni pamoja na mabaraza ya watoto
mashuleni, na vilabu cha watoto mashuleni na katika jamii au juhudi ambazo zinalenga
kwenye kuwahusisha watoto katika masuala mbalimbali yanayowahusu (kama vile
Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI wenyewe, malezi na matunzo
kisaikolojia na kijamii nk). Kati ya mwaka 2009 na mwaka 2010, Wizara ya Maendeleo
ya Jamii, Jinsia na Watoto ilitengeneza Kielekezi cha Taifa cha Ushiriki wa Mtoto
iii
ambacho kinaelekeza namna ya kufanikishaa ushiriki wa watoto na wanajamii katika
kujadili pamoja masuaala ya watoto. Hii ni nyenzo ya kuwawezesha watoto pamoja na
wanajamii kutambua na kujadili masuala muhimu yanayogusa maisha ya watoto katika
jamii na mazingira husika. Juhudi zote hizi za serikali pamoja na nyinginezo kama vile
kuridhia Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto mwaka 2003 na kupitishwa
kwa Sheria ya Mtoto ya Novemba 2009 pamoja na sera ya Mtoto ya mwaka 2008
zinaonyesha ari na utayari wa serikali wa kukuza haki ya ushiriki wa watoto. Wakati sera
ya Mtoto inazingatia uhuhimu wa ushiriki wa mtoto katika shughuli za maendeleo, na
maswala yanayohusu watoto wenyewe, sheria ya mtoto inawapa watoto haki ya watoto
kujieleza na kutoa maoni yao, kusikilizwa na kushiriki katika maamuzi yanayohusu
maisha yao.
Ili kuhakikisha sera na sheria tajwa zinatekelezwa ipasavyo, serikali chini ya uongozi wa
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto imeonelea ni vyema kuandaa Mpango
Kazi wa Ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi. Mpango kazi huu utatoa
maelekezo ya namna ya kufanikisha ushiriki wa watoto, uundwaji wa vyombo maalum
vitakavyowezesha watoto kushiriki na mwongozo wa jinsi ya kuingiza maoni ya watoto
na michango yao katika mipango, mikakati, programu na michakato mbalimbali na pale
inapowezekana hata katika kuingiza mchango wao katika taratibu za kutengeneza sheria
na taratibu za kimahakama.
Uandaaji wa Mpango Kazi huu unadhihirisha mabadiliko makubwa katika azma ya
ushiriki wa watoto ambao ni zaidi ya mchango wa maoni tu yanayotumika kama ushauri
na hivyo kuleta mafanikio endelevu katika ushiriki wa watoto kwenye michakato na
maswala ambayo yanahusu maisha yao. Mpango Kazi huu hata hivyo unahusu Tanzania
bara tu lakini kuna uwezekano wa kuupanua hadi Visiwani. Maandalizi ya Mpango huu
yalichukua sura shirikishi katika mchakato wake na maoni mbalimbali yaliyotolewa na
wadau wakati wote wa maandalizi yamezingatiwa na hivyo kuchukua sura shirikishi
ambayo itasaidia katika utekelezaji.
Mpango Kazi huu ambao unatarajiwa kuanza mwaka 2014 unalenga kuwafanya watoto
watambue kile ambacho jamii inatarajia kutoka kwao kwa maana ya majukumu hasa
wakati wanaposhiriki kikamilifu katika majadiliano, kupeana taarifa muhimu na
kutekeleza majukumu yanayowahusu kutokana na maamuzi waliyofanya katika ngazi ya
familia, jamii, kitaifa na kimataifa. Isitoshe, Mpango huu unalenga katika kuleta ufanisi
katika swala zima la ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi yanayohusu maisha yao
na ya jamii kwa ujumla na utekelezaji wake.
Mpango Kazi huu ni endelevu na katika hilo shughuli mbalimbali zitatekelezwa
zikiwemo kuelimisha jamii, watendaji wa serikali, wazazi/walezi wa watoto na watoto
wenyewe kuhusu athari zinazotokana na ukosefu wa ushiriki wa watoto kufanya
maamuzi kama wadau muhimu wa demokrasia, utawala bora na maendeleo endelevu ya
jamii. Mpango kazi huu pia utasaidia watoto kuibua vipaji vyao vya aina mbalimbali na
kuwapa fursa watoto kuchangia maoni na ushauri katika utungaji na utekelezaji wa sera
na sheria mbalimbali ili kuleta maendeleo yenye uwiano kijinsia na kijinsi.
iv
Mpango huu pia utatoa fursa kwa wazazi na walezi kujifunza njia bora za mawasiliano na
mahusiano mazuri kati yao na watoto wao na namna ya kuwashirikisha watoto katika
majadiliano na hata kunufaika na michango ya watoto kimawazo, ushauri na utekelezaji
wa maamuzi mbalimbali ya pamoja ya kutatua matatizo ya kipato duni, uvunjaji wa
sheria na taratibu mbalimbali na hata kubuni mikakati ya pamoja katika kutatua matatizo
hayo ya kijamii na mengineyo. Aidha watoto nao wote watafaidi haki yao ya msingi ya
kushiriki katika kufanya maamuzi yaani haki ya kusikika na kusikilizwa.
v
Shukrani
Katika kuandaa Mpango Kazi huu Shirikishi, wadau mbalimbali walishiriki kwa njia
moja au nyingine na hatuna budi kuwashukuru wote kwa dhati. Hawa ni pamoja na
watoto wa rika mbalimbali, wanajamii, wizara mbalimbali na idara za serikali, Asasi
Zisizo za Kiserikali, wadau wengine wa maendeleo, Mashirika ya Kidini,Wazee
wakimila na Wanataaluma.
Mchakato mzima kuandaa Mpango Huu ulikuwa chini ya usimamizi wa Wizara ya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Mpango huu unawakilisha matokeo ya warsha za
majadiliano, mikutano, hojaji mbalimbali na mazungumzo na watoto, serikali, asasi
zisizo za kiserikali na wawakilishi wa wadau wengine wa maendeleo, wawakilishi wa
jamii mbalimbali ikiwa ni pamoja na wazee, na viongozi wa jamii na dini, kati ya mwezi
Mei na Julai 2010 kuhusu ushiriki wa Watoto katika maamuzi nchini Tanzania.
Shukrani za pekee zinapelekwa kwa Shirika la Kimataifa la Kushughulikia Watoto
Duniani (UNICEF) ambalo limechangia kwa hali na mali kuhakikisha kwamba kazi hii
inakamilika.
2014
vi
VIFUPISHO
AZAKI: Asasi Zisizo za Kiserikali
BEST: Basic Education Statistics, Tanzania “Takwimu za Elimu ya Msingi”
MKUKUTA: Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania
NBS: National Bureau of Statistics “Idara ya Taifa ya Takwimu”
UKIMWI: Ukosefu wa Kinga ya Mwilini
WMJW: Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
OWMTMSM: Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
WAUJ: Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
WSK: Wizara ya Sheria na Katiba
WMN: Wizara ya Mambo ya Ndani
vii
Yaliyomo Ukurasa
Dibaji ii
Shukrani v
Vifupisho vi
1.0 UTANGULIZI 2
1.1 Usuli na Muktadha wa Mpango Kazi huu 4
1.2 Changamoto katika kutimiza haki za watoto kushiriki 6
1.2.1 Tafsiri ya neno “Mtoto” 6
1.3. Umuhimu wa Mpango Kazi Huu na changamoto zake 9
1.3.1 Kwa nini ushiriki ni muhimu? 9
1.3.2 Changamoto za kufanikisha Ushiriki 10
2.0 HALI HALISI YA USHIRIKI WA WATOTO KWENYE
MAUDHUI YA KITANZANIA 13
2.1 Maudhui ya Kisheria 13
2.1.1 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 13
2.1.2 Sheria ya Mtoto (2009) 15
2.1.3 Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini (2004) 16
2.1.4 Sheria ya Virusi vya UKIMWI/ UKIMWI (Ulinzi na Kinga) (2008) 16
2.2 Maudhui ya Kisera 17
2.2.1 Sera ya Maendeleo ya Mtoto (2008) 17
2.2.2 Sera ya Elimu 17
2.2.3 Sera ya Maendeleo ya Vijana 18
2.2.4 Sera ya Taifa ya Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI/UKIMWI (2001) 18
2.2.5 Sera ya Utamaduni 18
2.2.6 Mchakato wa Maboresho ya Serikali za Mitaa 19
2.2. 7 Jumuisho la Sera 19
3.0 MATEGEMEO YA WATOTO KATIKA USHIRIKI 20
4.0 UCHAMBUI WA WADAU, WIZARA/TAASISI 23 4.1 Utangulizi 23
4.2 Serikali Kuu na Idara zake 24
viii
4.2.1 Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto 24
4.2.2 Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa 25
4.2.3 Wizara ya Fedha na Uchumi 26
4.2.4 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii 27
4.2.5 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi 28
4.2.6 Wizara ya Habari, Maendeleo ya Vijana na Michezo 30
4.2. 7 Wizara ya Sheria na Katiba 31
4.2.8 Wadau wa Maendeleo na Asasi Zisizo za Kiserikali 33
4.2.9 Familia 34
4.2.10 Baraza la Watoto la taifa 34
4.2.11 Maoni ya ziada kuhusu miundo na majukumu ya watendaji wakuu 34
5.0 MKAKATI 36 5.1 Mwelekeo 36
5.2 Lengo na Madhumuni 38
5.2.1 Lengo/Madhumuni ya jumla 38
5.3 Bango Kitita (Mpango wa Utekelezaji) 39
6.0 URATIBU, UFUATILIAJI NA TATHMINI YA UTEKELEZAJI 54
6.1 Utangulizi 54
6.2 Lengo la Ufuatiliaji na Tathmini 54
6.3 Malengo mahsusi 54
6.4 Uratibu 55
6.5 Mchakato wa Ufuatiliaji na tathmini ya Utekelezaji 56
6.5.1 Ufuatiliaji wa mchakato 56
6.5.2 Ratiba ya Utekelezaji na Matukio ya Ziada 57
7.0 REJEA 58
1.0 UTANGULIZI
Mpango Kazi Shirikishi wa Ushiriki wa Watoto katika kufanya maauzi yanayohusu
maisha yao ni juhudi za serikali katika kutetea haki za watoto na kuimarisha demokrasia
nchini kulingana na sera za kitaifa na kimataifa, sheria mbalimbali zinazohusu watoto,
demokrasia na maridhiano ya kimataifa kuhusu haki za watoto na usawa wa jinsia.
Watoto wa Tanzania na kungineko wanakumbwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja
na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI wenyewe, kazi ngumu kwa watoto,
kiwango kikubwa cha kukatishwa masomo, kipato duni katika familia, na ukosefu wa
uhakika wa chakula. Matatizo mengine yanayowakumba watoto ni pamoja na elimu duni,
unyanyaswaji wa kijinsia, ukatili na kudhalilishwa. Watoto wanakutana na ukatili na
udhalilishwaji majumbani, mashuleni, ndani ya jamii zao na kungineko.
Matokeo ya awali ya utafiti uliofanyika kitaifa na mashauriano na watoto na vijana
kuhusu ukatili dhidi ya watoto yanaonyesha kuwa karibia asilimia 30 ya wasichana na
takriban asilimia 15 ya wavulana wamefanyiwa ukatili kabla ya kufikia umri wa miaka
18 na karibia asilimia 70 ya wasichana na 67 ya wavulana wamefanyiwa ukatili wa
shambulio la mwili. Wakati wa kuandaa Mpango kazi huu ilibainika kuwa kuna idadi
kubwa ya watoto wanaofanya makosa yanayo kinzana na sheria zilizopo au kuwa
mashahidi au waathirika wa uvunjaji wa sheria hizo. Idadi kubwa kidogo ya watoto wana
aina moja au zaidi ya ulemavu na wengi wao huishi mitaani1.
Kutokana na takwimu za Sensa ya Taifa ya idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012,
milioni 21,866,258 ambao ni sawa na asilimia 50.1 ya idadi ya watu wote2 wana umri
chini ya miaka 18 kwa Tanzania Bara. Idadi ya watoto wa umri chini ya miaka minane
walikuwa 11,181,278. na takriban milioni moja wako chini ya umri wa miaka mitano,
takriban milioni nane ya watoto wanaishi kwenye umaskini uliokithiri na mmoja kati ya
wasichana wanne wenye umri chini ya miaka 18 tayari wameshaanza jukumu la kuzaa.
Aidha asilimia 58 ya watoto wenye umri kati ya miaka mitano hadi sita na asilimia 97.7
ya watoto wenye ulemavu hawapati elimu ya awali (BEST 2012). Takriban wasichana
8,000 wanaacha shule kila mwaka kutokana na mimba za utotoni. Mnamo 2001,
makadirio ya vijana wenye umri wa miaka 15-24 wanaoishi na virusi vya
ukimwi/UKIMWI walikuwa asilimia 4.3. Mkakati mmojawapo wa kuhudumia watoto
ambao wanaishi kwenye mazingira magumu na kuwalinda na kuwawezesha kupata haki
zao za elimu, afya na nyinginezo ni kuwawezesha kushiriki katika kufanya maamuzi ya
maswala yanayohusu maisha yao. Sababu hizi zinajenga hoja nzito ya uwepo wa Mpango
kazi huu ili kufanikisha utekelezaji.
Mchakato wa kukusanya maoni ya wadau katika uandaaji wa Mpango Kazi wa Ushiriki
wa Mtoto ulilenga kwenye kutathmini hali halisi ya sasa kuhusu ushiriki wa watoto
katika maswala yanayowahusu. Ilitambulika kuwa kwa kiasi fulani kuna uelewa
1 URT, NBS, National Population and Housing Sensus 2002 2 Sera ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto Tanzania, Oktoba 2013, uk.1
11
miongoni mwa watoto na hata watu wazima kuhusu ushiriki wa watoto , uelewa ambao
unaashiria kuwa mazingira yako mazuri na ni wakati muafaka kuhimiza ushiriki wa
watoto katika kufanya maamuzi ya masuala yanayowahusu. Licha ya hali kuwa hivyo,
kuna mitizamo hasi miongoni mwa wanajamii inayoashiria vikwazo /pingamizi katika
kuelewa kwamba watoto wana haki ya kushiriki katika kufanya maamuzi ya mambo
yanayohusu maisha yao na hivyo wanastahili kushiriki sawa na watu wazima katika
jukumu hilo la kijamii. Hali zote mbili zinatoa msisitizo wa uwepo wa Mpango Kazi
Shirikishi; kuimarisha uelewa uliopo kuhusu ushiriki wao na kujenga mitizamo chanya
katika swala hili na pia kutumika kama nyenzo ya kupambana na hisia hizo hasi
zinazopinga ushiriki wa watoto kwenye maamuzi muhimu yahusuyo maisha ya watu. Pia
kuna viashiria na vitendo vinavyochangia uwepo wa ushiriki wa watoto humu Tanzania,
yakiwemo mabaraza ya watoto katika jamii, na mashuleni, vilabu vya watoto, na kamati
mbalimbali pamoja na serikali inayojali ikishirikiana na Asasi Zisizo za Kiserikali.
Itambulike kuwa kutokana na mila na desturi za Mtanzania, utamaduni ulikuwa kwamba
mawasiliano na watoto yalijikita kwenye yale mambo yanayowahusu moja kwa moja
kwa kutumia mbinu mbalimbali kuendana na mazingira ya mila zao. Licha ya kwamba
mbinu hizi zilikuwa hazifuati kikamilifu taratibu za kidemokrasia za kuwahusisha watoto
kwa yale yote yanayohusu maisha yao, kwa kiwango kikubwa, bado hizi mila
zinatukumbusha kuwa umuhimu wa ushiriki wa watoto ulikuwa unatambulika na
unapaswa kuheshimiwa na kudumishwa ndani ya misingi ya haki za binadamu.
1.1 Usuli na muktadha wa Mpango Kazi Huu
Katika kuzingatia umuhimu wa ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi yanayohusu
maisha yao na ya jamii kwa ujumla, pamoja na umuhimu wa kuzingatia haki zao, serikali
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa kipaumbele kikubwa kwa watoto. Hata
hivyo, Mpango Kazi huu unahusu Tanzania Bara tu ijapokuwa kuna uwezekano wa
kupanuka hadi Tanzania Visiwani.
Katika ngazi ya kitaifa, na katika kuhakikisha kuwa haki ya mtoto kushiriki katika
maamuzi yanayohusu maisha yake inazingatiwa, juhudi nyingi zimechukuliwa na serikali
kwa kuzingatia umuhimu wa kutimiza haki za watoto, hivyo serikali imetoa kipaumbele
kwa watoto kwenye nyanja mbalimbali kisera na kisheria:
a) Serikali ya Jamhuri ya Muungano imeridhia mikataba ya kimataifa na ya kikanda
inayohusu haki za watoto. Hii mikataba ni pamoja na:
i) Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watoto
ii) Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Watoto
b) Licha ya kuridhia mikataba hii ya kimataifa, serikali imechukua hatua madhubuti
kutunga sheria, sera, mikakati na mipango kazi ili kuhakikisha kwamba haki
zilizoainishwa katika mikataba hii inatekelezwa:
i) Mwaka 2002 Serikali ilisimamia uundwaji wa Baraza la Taifa la watoto na
mabaraza ya watoto katika ngazi ya jamii na mashuleni na klabu za watoto
pamoja na kamati za kushughulikia masuala ya watoto.
12
ii) Baada ya kuunda Sera ya Maendeleo ya Watoto mwaka 2008, mwaka
2009, Bunge la Muungano lilipitisha Sheria ya Mtoto inayobeba dhamira
ya serikali kuhakikisha kwamba watoto wote wanapata haki zao zote.
iii) 2011 Serikali ilitengeneza kielekezi cha ushiriki wa mtoto Tanzania
iv) 2011 Serikali ilitengeneza muongozo wa kuanzisha mabaraza ya vijiji,
kata, wilaya na mkoa.
v) Mwaka 2011 Serikali imesimamia na kuratibu utafiti wa kitaifa kuhusu
ukatili dhidi ya mtoto. Kutokana na matokeo ya utafiti huo, mwaka 2012,
Serikali iliandaa Mpango Kazi ulioshirikisha sekta mbalimbali katika
kuzuia na kukabiliana na ukatili huo.
vi) Mpango wa Kitaifa wa Kupunguza Umaskini, Mkukuta II (2010)
unatambua uwepo wa watoto wanaokabiliwa na hali hatarishi na kuweka
mikakati ya kuwalinda na kuhakikisha kwamba wanapata haki zao sawa
na watoto wengine.
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto (WMJJW) ndiyo yenye jukumu la
kusimamia na kuratibu utekelezaji wa mikataba, sera na sheria zinazolenga kutimiza haki
za watoto.
Mpango kazi huu unalenga katika kuhakikisha kuwa vikwazo vyote vinavyozuia ushiriki
wa watoto katika kufanya maamuzi ya masuala yanayohusu maisha yao vinakomeshwa
na sauti zao zinasikika na kuzingatiwa katika maamuzi ya kifamilia, kijamii na kitaifa na
kimataifa yanayohusu maisha ya watoto na haki zao. Inapendekezwa kuwa, wadau wote
ikiwa ni pamoja na serikali na asasi zisizo za kiserikali wapitie mpango kazi huu na
kuchagua malengo na shughuli zile zinazolingana na majukumu yao na hivyo kutekeleza
kikamilifu ili kupata mafanikio endelevu katika suala hili la ushiriki wa watoto.
1.2 Changamoto katika kutimiza haki za watoto kushiriki
1.2.1 Tafsiri ya neno “Mtoto”
Katika kufanikisha suala la ushiriki wa watoto, kuna haja ya kupata tafsiri halisi ya
maneno mawili muhimu; “mtoto” na “ushiriki wa mtoto” kulingana na sheria na sera za
Tanzania. Kisheria, kama ilivyoainishwa kwenye mkataba wa kimataifa wa haki za
mtoto, mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto na Sheria ya Mtoto, mtoto ni
mtu yeyote mwenye umri chini ya miaka 183. Kwa kuzingatia mazingira halisia ya
kisheria, na kulingana na aina ya majukumu anayopangiwa mtoto, umri unaweza kuwa
chini au juu ya miaka 18. Kwa mfano, katika Sheria ya Makosa ya Jinai, umri wa
kuwajibika kwa mhalifu ni miaka 10. Katika jamii nyingi, mtu yeyote ambaye bado ni
tegemezi kwa wazazi wake huwa anahesabika kuwa ni mtoto hata kama umri wake
3
13
unazidi miaka 18. Kwa upande mwingine, msichana ambaye amezaa au mtu yeyote
ambaye ametahiriwa au amepitia jando4 na unyago
5 anaweza asihesabike kuwa ni mtoto
hata kama umri wake ni chini ya miaka 18. Hata hivyo, kwa ujumla Mpango Kazi huu
unamtambua mtoto kuwa ni mtu mwenye umri chini ya miaka 18 kama ilivyotafsiriwa
katika Sheria ya Mtoto (Sehemu ya II, 11).
1.2.2 Tafsiri ya “ushiriki wa watoto na vijana wadogo” katika jamii
Zipo tafsiri kadhaa za dhana hii zikizingatia kifungu cha 12 cha Mkataba wa Kimataifa
wa Haki za Mtoto ambacho kinasema kwamba kila mtoto ambaye anaweza kuchangia
maoni ana uhuru na haki ya kutoa maoni hayo kuhusu masuala yanayomhusu bila woga
wowote na kwamba maoni yao yapewe uzito unaostahili kulingana na umri wao. Hii ni
mojawapo ya haki ambazo zimeainishwa kama haki ya msingi katika Mkataba wa Umoja
wa Mataifa wa Haki ya Mtoto. Haki hii pia inaainishwa katika kifungu cha 5 cha
Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto ambacho kinasema kuwa jukumu la kutoa
mwongozo katika kujali haki za watoto, wazazi na walezi wa watoto katika ushiriki wa
watoto kutoa maamuzi mbalimbali lilenge kwenye mwenendo wa ukuaji wa uwezo wa
watoto. Hii inamaanisha kwamba, watoto wanapata uzoefu na ujuzi katika nyanja hii ya
ushiriki jinsi wanavyokua na kupata fursa ya kushiriki na kupewa majukumu
yanayoendana na ushiriki wao na pia hukomaa wanavyopata utashi wa kuwajibika kwa
matendo yao yanayotokana na uchangiaji wao katika kufanya maamuzi yanayowahusu
wenyewe.
Mojawapo ya misingi mikuu iliyoainishwa kwenye Kamati ya Mkataba wa Kimataifa wa
Haki za Mtoto ni ule unaotokana na kifungu cha 3 ambacho kinatambua umuhimu wa
kuzingatia matakwa ya mtoto wakati wote wa kufanya maamuzi. Kamati hii inaainisha
kuwa kuna kuwajibika kwa pamoja katika kuamua kipi kina maslahi kwa watoto na hili
hutokana na majadiliano na makubaliano kati ya watoto na watu wazima ijapokuwa
uwajibikaji wa kufikia maamuzi hayo uko mikononi mwa watu wazima. Uwajibikaji huu
wa pamoja pia una mipaka yake na muelekeo unaotolewa na wazazi au walezi wa watoto
(na hata watu wengine wazima) unapaswa kuzingatia uwezo wa watoto kufanya
maamuzi.
Aina nyingine ya ushiriki ni ile inayoelezwa katika vifungu 13 hadi 17, ambavyo vinatoa
tafsiri ya mwelekeo mwingine wa ushiriki katika jamii ambao unajumuisha uhuru wa
kujieleza, uhuru wa dini, utashi, kujiunga kwenye kundi lolote, usiri na taarifa. Vifungu
hivi vinazingatia Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu (UN Universal Declaration of
Human Rights-UDHR), Kifungu cha 2, 12, 18, 19, 20 na 27. pamoja na mikataba ya
kimataifa ya haki za kiraia na kisiasa na mkataba wa kimataifa wa haki za kiuchumi,
14
kijamii na kitamaduni ambapo inatambulika na kutamkwa na kukubalika kuwa kila mtu
ana haki zote na uhuru zilizotamkwa kwenye matamko haya bila kujali tofauti za kitaifa,
rangi, jinsi, lugha, dini, vyama vya siasa au itikadi yoyote au kabila, mahali mtu
alipozaliwa au tofauti nyingine yoyote. Kuna misingi mingine ambayo inatukumbushia
pia kuwa haki za binadamu ni kwa binadamu wa mataifa yote na hazihodhiwi wala
kunyang‟anywa iwe ni haki za kiraia, kisiasa, kiuchumi, kijamii au kiutamaduni. Uwepo
wa haki mojawapo hufanikisha kuwepo kwa haki nyingine na hivyo hivyo uvunjaji wa
haki ya aina moja husababisha mlolongo wa uvunjaji wa haki nyingine. Ieleweke kuwa
haki hizi hazihamishiki na uvunjaji wake kwa makundi fulani lazima uwe na kibali cha
kisheria.
Vifungu vya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto, hasa vile vinavyozungumzia
ushiriki inabidi vieleweke kwa kiwango kikubwa. Kwa wakati huu ndani ya jamii ya
Kimataifa, umuhimu umewekwa kwenye mlengo wa kuzingatia Haki za Binadamu ili
kufanikisha mkakati wa kuziona haki za binadamu kuwa hazihamishiki wala
kunyang‟anywa kutoka mtu mmoja kwenda mwingine. Mkataba wa Kimataifa wa Haki
za Mtoto, kama nyenzo ya kufanikisha kutokuvunjwa kwa haki za binadamu pia inatafsiri
haki za watoto katika jamii ambapo inajumuisha haki ya ushiriki katika maamuzi.
Isitoshe, katika maoni ya jumla ya Kamati ya Haki za watoto No. 12, kamati ilitambua
kifungu namba 12 kama kifungu muhimu katika kutambua msingi wa haki ya kushiriki
ambao unawahusu watoto wote wenye uwezo wa kuchangia maoni, bila kujali umri wao
mdogo, na kuwa haki hii inaainishwa katika nyanja zote za maisha, kuanzia katika ngazi
ya familia, nyumbani, katika jamii, mashuleni, sehemu zote zenye makundi ya watu na
huduma za jamii na popote pale ambapo sera na huduma za serikali zinahusika.
Kamati ilisisitiza umuhimu wa kuwapatia watoto taarifa muhimu katika kupata fursa na
muda wa kushiriki kikamilifu na kwa amani bila woga wala kubanwabanwa. Kwa hali
hiyo, tafsiri halisi ya ushiriki ni mchakato endelevu ambao watoto wanapata fursa /na
wanachangia kikamilifu katika kufanya maamuzi ya maswala yanayohusu maisha yao:
Huwapa watoto fursa ya kuchangia maoni kuhusu mwelekeo wa mchakato wa
utoaji maamuzi ya mambo muhimu ya maisha na yatokanayo na mchakato huo,
Huhitaji kupeana taarifa na kuendesha majadiliano kati ya watoto na watu
wazima ambayo yanalindwa na dhana ya kuheshimu mchango wa kila mmoja
wao, dhana ambayo inaimarisha kuelewana, kutoa maamuzi ya pamoja na
kushirikiana kwa nguvu moja katika kusimamia utekelezaji wa maamuzi hayo.
Kuheshimu nguvu ya watoto ya kuchangia katika maamuzi ambayo inakua kila
wanaposhiriki, ili kwamba uzoefu na mahitaji yao yanakubalika kama sehemu ya
ukuaji na aina ya ushiriki wao.
Humu Tanzania, Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, Sehemu ya 2 Kifungu cha 11,
kinaelezea namna ya kufanikisha kufikia malengo ya ushiriki wa mtoto kwa kuzingatia
kifungu 12 cha Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto:
“Mtoto ana haki ya kutoa maoni yake na kusiwe na mtu yeyote kumnyima haki ya
kushiriki mtoto ambaye ana uwezo wa kutoa maoni, kusikilizwa na kushiriki
katika kufanya maamuzi ambayo yanahusu maisha yake”.
15
1.3. Umuhimu wa Mpango Kazi Huu na changamoto zake
1.3.1 Kwa nini ushiriki ni muhimu?
Ushiriki kwa jinsi ilivyoonyeshwa hapo juu ni haki ya msingi, hivyo inatambulika kama
haki inayowezesha haki nyingine zote kuwepo. Watoto wote kama ilivyo kwa watu
wazima wana haki ya kushiriki na serikali zote duniani huwa zinategemewa kuheshimu
haki hii kwa watoto bila kujali tofauti za aina yoyote miongoni mwa watoto.
Ni muhimu kuelewa kuwa ushiriki wa watoto unachangia katika kufanikisha mchango wa
watoto katika jamii kama wananchi wengine. Kutokana na uzoefu wao katika ushiriki moja
kwa moja katika maswala yanayohusu maisha yao, watoto wanajijengea uwezo wa
kuchangia katika kudumisha amani na demokrasia katika nchi zao kama raia
wanaowajibika.Kitendo hiki kinachangia katika kuendeleza utamaduni wa kuheshimiana
ambao ni muhimu katika jukumu la kufanya maamuzi kwa kujadiliana badala ya
kugombana na kutumia udikteta. Watoto wanajifunza kuwa haki za binadamu ni kwa kila
mtu na hudumisha kuheshimiana na sio kushindana na kugombania. Ushiriki wa jamii
nzima katika kufanya maamuzi ambao unahusisha watoto unasaidia serikali kuboresha
huduma za jamii, na kuwapa wananchi nafasi ya kuwawajibisha watendaji wa serikali,
kuhakikisha kuwa mchakato wa utoaji haki na ufuatiliaji wa sheria una tija.
Watoto wanaposhiriki wanapata ujuzi, uelewa, na kujiamini, vitu ambavyo wanahitaji
katika maisha yao. Hili linachangia katika maendeleo ya watoto kwa kiasi kikubwa kwa
mfano huchangia katika kutimiza malengo ya elimu (Kifungu 29 cha Mkataba wa
Kimataifa wa Haki za Mtoto, maendeleo yao kikamilifu (kama ilivyoainisha katika
kifungu 6 cha Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto) na uwezo wao wa kufaidi haki
zao (Kifungu 5). Ushiriki wao pia unachangia katika kujali matakwa yao kama
ilivyoainisha katika kifungu 3.1 cha Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto na kile cha
4.1 cha Mkataba wa Kanda ya Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto. Watoto ambao
wanawezeshwa kijamii, kiuchumi na kisiasa wana uwezo pia wa kuwa wahamasishaji na
watetezi hodari wa haki zao.
Uwezeshaji huu una uwezo mkubwa wa kuchangia katika kujali haki za watoto. Watoto
mara nyingi huwa wakimya na wavumilivu tu hata pale wanapofanyiwa ukatili na
wanaponyanyaswa na watu wazima au watoto wenzao. Kuwapatia taarifa na
kuwahamasisha kuzungumzia matatizo yao, kuna waelimisha kuhusu njia za amani na
salama za kuhoji ukatili na unachangia kuwapa watoto ulinzi na kuishi kwa amani na
furaha.
Isitoshe, watoto wanaopata fursa ya kupata taarifa kuhusu afya na mambo ya afya ya uzazi
wana nafasi nzuri ya kujilinda dhidi ya mimba za utotoni, magonjwa ya zinaa, Maambukizi
ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Wafanyikazi vijana wanaojiunga kwenye vyama
vya kijamii na harakati za maendeleo wana nafasi kubwa ya kujilinda dhidi ya unyonyaji,
na udhalilishwaji katika sehemu zao za kazi, wana uwezo wa kudai malipo halali ya jasho
lao na mazingira mazuri ya kufanyia kazi. Kwa upande mwingine wana uwezo mkubwa
wa kupiga vita ajira za watoto makazini.
16
Zaidi ya hayo, ushiriki wa watoto unachangia kutoa na kusambaza taarifa na uelewa
ambao unasaidia kuboresha utungaji wa sheria, uandaaji wa sera na bajeti, na utoaji wa
huduma za jamii, kwa mfano, unachangia katika kufikia malengo ya Millennia (MDGs).
1.3.2 Changamoto za kufanikisha Ushiriki
Kuna changamoto nyingi katika kufanikisha ushiriki wa watoto. Kuna madaraja ya
kujenga kati ya azma ya ushiriki na uhalisia wake katika maisha ya watoto na katika
kufikia malengo mazuri ya sera zinazohusu watoto. Katika Kamati ya Haki za Watoto
yafuatayo yaliainishwa: katika kifungu cha 12:
Ili kufanikisha mashauriano, taarifa na michakato inatakiwa kuwafikia
walengwa. Lakini kujidanganya kuwa watoto wanasikilizwa ni changamoto
ndogo ila kukubali maoni yao na kuzipa uzito unaostahili hoja zao ni ishara
ya mabadiliko makubwa. Kusikiliza sauti za watoto isichukuliwe kuwa ndio
mwisho wa changamoto bali ieleweke kuwa njia tu kwa serikali kuwasiliana
na watoto na kujua matendo yao kwa niaba ya watoto ambao wana ari na
wamehamasika kulinda haki za watoto.
Kifungu cha 12 kinadai uwepo wa mipango endelevu ya ushiriki. Ushirikishi
na majadiliano na watoto huhitaji pia kuepuka kuonyesha kujali kwa kiasi
kidogo tu na kulenga kwenye kupata uwakilishi wa maoni ya walio wengi.
Msisitizo wa “masuala yanayowahusu”katika kifungu cha 12 (1) unaonyesha
kuwa upatikanaji wa waoni ya vikundi mbalimbali vya watoto walio wengi
kuhusu masuala yanayowahusu kwa mfano watoto ambao walishawahi
kukumbwa na uhalifu kushiriki kutoa maoni kuhusu namna ya kuboresha
sheria zinazolenga eneo hilo, au watoto walioasiliwa au wanaoishi katika
familia zinazoasili watotokutoa maoni yanayohusu sheria ya kuasili na sera.
Ni muhimu na jambo la busara kwa serikali kujenga mahusiano/mawasiliano
ya moja kwa moja na watoto, na sio tu mahusiano kupitia asasi zisizo za
kiserikali (AZAKI) au taasisi za kutetea haki za binadamu. Katika miaka ya
awali ya Makubaliano/Mapatano haya, AZAKI zilichangia kuanzisha
utaratibu wa kushirikisha watoto, lakini ni kwa faida ya serikali na watoto
kuwa na mahusiano na mawasiliano ya moja kwa moja.
Kamati ya Haki za Watoto pia ilisisitiza suala la sauti za watoto kusikilizwa katika ngazi
zote kuanzia kwenye familia na hili ni muhimu pia kwa Tanzania:
90. Familia ambazo zinawapa watoto uhuru wa kujieleza na kutoa maoni yao
ambayo yanathaminiwa kuanzia wakiwa kwenye umri mdogo zinakuwa za
mifano ya kuigwa na humuandaa mtoto kujizoesha katika kutafuta haki ya
kusikilizwa na jamii kubwa zaidi.
91. Makubaliano/Mapatano haya pia yanatambua haki na wajibu wa wazazi
au walezi wengine kuwapatia watoto wao muelekeo unaoeleweka na ushauri,
17
lakini pia inasisitiza kwamba yote haya yafanyike kwa lengo la kumwezesha
mtoto kufaidika na haki zake na kusisitiza kuwa muelekeo huo na ushauri
utolewe katika mazingira yanayojenga kumwezesha mtoto na sio vinginevyo.
92. Serikali zihimize kwa kupitia sheria na sera wazazi na walezi na wale
wanaohudumia watoto kuwasikiliza watoto na kuthamini maoni yao katika
masuala yanayowahusu watoto. Wazazi washauriwe pia kuwasaidia watoto
wao katika kutambua haki yao ya kujieleza na kuchangia maoni bila woga na
kuhakikisha maoni ya watoto yanathaminiwa wakati wote na katika ngazi zote
za jamii.
93. Ili kusaidia kuboresha mfumo wa makuzi ya watoto unaoheshimu haki ya
watoto ya kusikilizwa, Kamati inapendekeza kuwa serikali na vyombo vyake
iandae programu ya mafunzo kutoa elimu kwa kuanzia kuendeleza tabia na
mitizamo rafiki kwa watoto iliyopo na kutoa habari na taarifa kuhusu haki za
watoto na wazazi zilizoainishwa katika Makubaliano haya.
94. Programu hizo zinapaswa kushughulikia na kufanikisha yafuatayo:
Mahusiano yanayothamini mchango wa watoto na wazazi, Ushiriki wa watoto
katika kufanya maamuzi, Matokeo ya kuipa uzito unaostahili maoni na
michango ya mawazo ya kila mwanafamilia, Uelewa, uwezeshaji na
uendelezaji pamoja na uthamini wa ujuzi, uwezo na uzoefu unaokua wa
ushiriki wa watotona njia za kupambana na mitizamo na maoni hasi kuhusu
haki za watoto ndani ya familia
Mapendekezo ya misingi ya namna ya kupambana na mitizamo hii hasi na kujenga
mazingira yanayofaa na yenye tija ya majadiliano kati ya watoto na watu wazima ni kama
ifuatavyo:
1. Uwazi, ukweli na uwajibikaji
2. Mazingira rafiki kwa watoto
3. Usawa wa fursa
4. Ulinzi na usalama wa watoto
5. Ukereketwa wa kujali watoto na uwezo unaohitajika wa watu wazima
Hivyo basi, watu wazima wanaoamua kushiriki na watoto katika majadiliano wanapaswa
kufuata njia za uadilifu na kuyapa kipaumbele matakwa ya watoto. Watoto wanatakiwa
wajengewe mazingira rafiki ambayo ni salama, mazuri na yenye kuwapa motisha
kushiriki miongoni mwa watu wazima bila kuwa na woga wa kudharauliwa na kuzidiwa
nguvu. Makundi ambayo yamewekwa pembezoni na ambayo mara nyingi hayahusishwi
kwenye mambo mengi kama vile wasichana, au watoto wenye ulemavu ni muhimu
wahusishwe.
Watoto, kama ilivyo watu wazima ni kundi ambalo lina wahusika wanaotofautiana kwa
misingi ya kijinsia, kikabila, kiuwezo, kiuchumi na tofauti nyinginezo. Hatua za
makusudi zichukuliwe ili kuhakikisha kuwa makundi yote haya yanashiriki. Na uangalifu
uwepo ili wote wajisikie wana fursa sawa bila ubaguzi wala kunyanyasika kwa namna
18
yoyote ile au kuathirika aidha kisaikolojia au kimwili. Watu wazima nao wajaribu
kuhakikisha kuwa hawajifanyi wao wanajua zaidi na wawe wanawahamasisha watoto
kushiriki kikamilifu kama wana uelewa wa kutosha wa jambo wanalolijadili, tabia ya
usikivu na kuchangia maoni kwa faida ya wote. Hata hivyo, kwa wale wazee ambao
walizoea mfumo wa kidikteta au ukandamizaji na ukali, ambao watoto walikuwa
hawapati nafasi kukaa na wazee na kujadili pamoja, mabadiliko haya yatakuwa ni
changamoto kubwa kwao.
2.0 HALI HALISI YA USHIRIKI WA WATOTO KWENYE MAUDHUI YA
KITANZANIA
2.1 Maudhui ya Kisheria
2.1.1 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Kwa kuanzia, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inajali waTanzania wote bila
kujali umri (kifungu cha 8 (1). Kulingana na Katiba, serikali inapaswa kuwajibika kwa
watu, na watu kushiriki katika maswala yote ya serikali kulingana na misingi ya katiba.
Watu wanaotajwa kwenye katiba ni pamoja na watoto na demokrasia na uwajibikaji
vinazungumzia haki ya ushiriki hivyo watoto kama raia mwingine wa Tanzania
wanafaidika na haki za ushiriki zilizoainishwa katika kifungu cha 18 cha Katiba ambacho
kinatamka bayana uhuru wa kujieleza:
(1) Bila upendeleo kisheria, kila mtu ana haki ya uhuru kujieleza, na kutoa
maoni, kutafuta, kupokea na kusambaza taarifa na mawazo kupitia vyombo
vya habari, bila kujali uraia, na pia ana haki ya uhuru wa kutokubughudhiwa
kwenye mawasiliano hayo.
(2) Kila raia ana haki ya kupata habari/taarifa wakati wote kuhusu matukio
mbalimbali nchini na katika ulimwengu wote ambayo yana umuhimu katika
maisha ya watu na pia maswala muhimu yanayohusu jamii.
Kifungu 19 (1) kinaelezea haki ya uhuru wa mawazo, utashi, na imani:
Kila mtu ana haki ya uhuru wa mawazo, au utashi, imani au dini anayoipenda,
na uchaguzi katika maswala ya kidini, pamoja na uhuru wa kubadili dini au
imani za kidini
Kifungu 20 (1) kinahusu uhuru wa kujiunga na kikundi chochote:
Kila mtu ana uhuru wa kujumuika kwa amani, kushirikiana na watu wengine,
kutoa maoni yake kwa uwazi bila kificho, na kwa hakika zaidi kujiunga na
kundi lolote ambalo limeundwa kwa madhumuni ya kulinda na uendeleza
imani yake au matakwa yake au kwa jambo lingine lolote lile.
Kifungu 21(2) kinazungumzia ushiriki wa raia.
Kila raia ana haki pamoja na uhuru wa kushiriki kikamilifu katika mchakato
unaolenga kufanya maamuzi kuhusu maswala yenye athari kwake au
yanayomhusu maisha yake na yale ya taifa lake.
19
2.1.2 Sheria ya Mtoto (2009)
Sheria hii ambayo imeanza kutumika mwezi Aprili mwaka 2010 ndio sheria pekee
inayomlenga mtoto na ambayo imeweka misingi imara ya kulinda mtoto na kwa mara ya
kwanza kuingiza haki za watoto katika sheria ya nchi. Sheria hii inaweka bayana uhuru
wa watoto kujieleza na kutoa maoni yao, kusikilizwa na kushiriki katika kufanya
maamuzi kwa mambo yanayohusu maisha yao na ya jamii zao. Pia sheria hii inasisitiza
suala la kujali maslahi ya watoto kwanza katika maswala yote na kutokubagua watoto.
Katika sehemu ya 15, sheria hii inasisitiza msimamo wa Mkataba wa Kanda ya Afrika
wa Haki na Ustawi wa Mtoto, na kuhimiza kuwa watoto wana wajibu wa kuhudumia
jamii na taifa lao kwa kutumia uwezo wa nguvu zao na akili zao kulingana na umri na
uwezo.
Kwa kuzingatia zaidi uchambuzi kuhusu swala la ushiriki wa mtoto katika jamii ya
Kitanzania, Sheria hii ya Mtoto katika sehemu ya kwanza, Maelezo ya Awali imetamkwa
kuwa:
2. Sheria hii inahusu Tanzania Bara tu katika swala la kulinda, kuendeleza na
kusimamia maslahi na haki za mtoto
Sheria hii inaendelea kuelezea haki za watoto katika Sehemu ya Pili chini ya kichwa cha
habari cha Haki na Maslahi ya mtoto, kifungu kidogo cha (a) kuhusu Haki ya Mtoto
ambavyo Kifungu cha 4 hadi 14 kinaelezea lengo la sheria hii. Kifungu cha 11 kinasema
kuwa:
Kila Mtoto ana haki ya kutoa maoni yake na asitokee mtu kumnyima mtoto
mwenye uwezo wa kutoa maoni yake haki ya kujieleza, kusikilizwa na
kushiriki katika kufanya maamuzi yanayohusu maisha yake.
Kifungu hiki kinafafanua msimamo wa Sheria hii kama ilivyoelezwa katika kifungu cha
18 hadi 21 cha Katiba ya Nchi. Hili pia linaendana na Kifungu cha 12 cha Mkataba wa
Kimataifa wa Haki za Mtoto na Kifungu cha 7 cha Mkataba wa Afrika wa Haki na
Ustawi wa Mtoto ambacho kinasema:
Kila mtoto mwenye uwezo wa kujieleza atahakikishiwa haki yake ya kutoa
maoni yake kwa uhuru katika masuala yote na kusambaza maoni yake ili
mradi haendi kinyume na sheria zilizopo
Mpango Kazi huu ni njia mojawapo ya kuwawezesha watoto kutoa michango yao
inayotarajiwa katika jamii na taifa kama ilivyoelezwa katika sheria na mikataba
mbalimbali.
2.1.4 Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini (2004) Hii ni Sheria inayomlinda mtoto katika Sekta ya kazi. Sehemu ya 5 (1) ya sheria hii
inakataza ajira kwa watoto wenye umri chini ya miaka 14 ila wale wenye umri huo
na kuendelea wanaweza kuajiriwa kwenye kazi nyepesinyepesi ambazo hazina
madhara kwa ukuaji na afya yao na wala kuathiri maendeleo yao kielimu. Sheria
hii pia inakataza ajira kwa watoto wenye umri wa miaka 18 kwenye ajira/kazi
hatarishi. Ili kuwalinda watoto dhidi ya ajira za aina hizo, ni muhimu wao wenyewe
20
washiriki katika kuandaa taratibu za kuwalinda na Mpango Kazi huu utasaidia
katika kufanikisha hilo. Mwaka 1998 Tanzania imeridhia Mkataba wa ILO wa
Mwaka 1973 (Na. 138) kuhusu Umri wa Kuruhusu Mtoto Kuajiriwa and ule wa
Ajira Mbaya kwa Watoto wa 1999 (Na. 182) uliridhiwa mwaka 2001.
2.1.4 Sheria ya Virusi vya UKIMWI/ UKIMWI (Ulinzi na Kinga) (2008)
Serikali inatambua wajibu wake kutoa huduma ya tiba, matunzo na msaada kwa watu
wanaoishi na VVU na waliokatika hatari ya kuambukizwa VVU kwa kutumia raslimali
zilizopo. Sheria hii inatamka kuwa upimaji hiari unapatikana kwa watu wote kwa ridhaa
yao.Sehemu ya 15 (2) inalenga watoto kwa kutamka kuwa: “Mtoto au mtu yeyote
ambaye hana uwezo wa kutambua matokeo ya upimaji atapimwa kwa ridhaa ya
maandishi ya mzazi au mlezi anayetambulika”. Hata hivyo, tamko hili linasahau kuwa
siku hizi kuna mabadiliko kwa watoto kuwa wale wenye umri mkubwa kidogo wana
uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kuhusu upimaji wa Virusi vya Ukimwi na wanaweza
kuelewa majibu ya upimaji huo. Msimamo huu unakinzana na nia ya ushiriki wa watoto
na unaweza kukiuka haki za watoto katika suala la kupatiwa huduma zinazoendana na
Virusi vya UKIMWI/UKIMWI haswa kwa watoto wenye umri mkubwa kidogo ambao
wanaweza kuficha taarifa muhimu zakwao na za wenzao wa rika lao.
2.2 Maudhui ya Kisera
2.2.1 Sera ya Maendeleo ya Mtoto (2008)
Mazingira ya kisera ya kusimamia haki za watoto Tanzania ni mazuri kwa kiasi kikubwa.
Ziko sera kadhaa ambazo ni rafiki kwa watoto. Sera ya maendeleo ya Mtoto (2008) kwa
mfano hutoa miongozo kwa wadau wote katika kushiriki kwenye utekelezaji wa
programu zinazolenga haki za watoto na maisha yao. Sera hii inaandaa utaratibu kwa
wadau kuelewa majukumu yao ambayo yanapotekelezwa ipasavyo yanafanikisha
utekelezaji wa mipango kuhusu watoto na usimamizi wake. Katika lengo lake la nne kwa
mfano, sera hii inatamka wazi suala la ushiriki wa watoto unaolenga kutoa muelekeo
kuhusu kuishi, kulindwa, kushiriki, kutokubaguliwa na kuhusu maendeleo ya mtoto kwa
ujumla.
Mpango Kazi huu kwa hiyo, ni nyenzo mojawapo iliyoandaliwa kutoa muelekeo wa
namna ya kuwashirikisha watoto katika kutoa mchango wao na kushiriki katika masuala
yanayowahusu ambayo hatimaye yanamuwezesha mtoto kupata maisha yenye ulinzi wa
kutosha, usalama na maendeleo. Msimamizi wa sera hii ni Wizara ya Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na Watoto, ambayo inawajibika kwa masuala ya familia. Wizara hii ina
jukumu la kuelimisha na kutoa ujuzi kwa familia na jamii kwa ujumla katika lengo la
kuwezesha watoto kuchangia na hivyo kuwa washiriki katika masuala yanayohusu
maisha yao, familia zao, jamii zao na ngazi nyingine za shuguli za kiraia. Wizara hii
katika Mpango Mkakati wake wa 2007/08 hadi 2009/10 imejidhatiti kujengea uwezo
familia na jamii katika swala la ushiriki katika kufanya maamuzi, kupanga mikakati
mizuri ya kutekeleza mipango ya maendeleo na kuimarisha uongozi wa kidemokrasia
katika ngazi ya serikali za mitaa na taasisi zake. Hatua hizi itachangia kiasi kikubwa
kufanikisha utekelezaji wa Mpango Kazi huu.
21
2.2.2 Sera ya Elimu
Sera ya Elimu inaweka bayana suala la elimu ya msingi kuwa lazima kwa watoto wote na
ushiriki wa watoto katika kamati za shule. Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Elimu
(2008-2017) inasisitiza malengo ya sera hii katika kulinda haki za binadamu ambazo ni
pamoja na haki ya kupata elimu na ushiriki wa watoto katika masuala yote
yanayowahusu. Kwa ujumla kila mtoto anapaswa kupitia mfumo wa elimu kabla ya
kuwa mtu mzima na hivyo elimu ni sehemu nzuri kwa watoto kuanza kushiriki kwa
kujijenga kwa maisha yao ya utoto na baadae ya utu uzima.
2.2.7 Sera ya Maendeleo ya Vijana
Sera ya Maendeleo ya Vijana inalenga katika kuhamasisha vijana kushiriki katika nyanja
zote za maendeleo kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni na kuhimiza sekta zote za
jamii kushiriki katika mipango inayolenga kwenye maeneo haya. Utekelezaji wa sera hii
una uwiano mzuri na Mpango Kazi huu wa ushiriki wa watoto ambao utahamasisha na
kuongoza vijana katika kuanza kutekeleza majukumu yao kuanzia umri wa chini. Katika
Sera hii tafsiri ya neno „vijana‟ ni watu wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 35. Mpango
Kazi huu utahusishwa kwa karibu sana na Mkakati wa Kitaifa wa Ushiriki wa Vijana
ambao mipango yake ya utekelezaji inaandaliwa chini ya usimamizi wa Wizara ya
Uwezeshaji, na Maendeleo ya Vijana ambayo hivi karibuni jina lake limebadilishwa na
sasa inajulikana kama Wizara ya Habari, Maendelo ya Vijana na Michezo.
2.2.8 Sera ya Taifa ya Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI/UKIMWI (2001) Sera hii inatambua haki za vijana kuhusu usiri, na upimaji hiari na ushauri nasaha / kwa
ridhaa ya mlengwa baada ya kupata maelezo kamili. Sera hii pia inawezesha walenga
kupata taarifa sahihi kuhusu Virusi vya Ukimwi/UKIMWI, programu za elimu shirikishi
ya maswala ya kujamiiana, na taasisi zinazotoa elimu hiyo pamoja na mikakati maalum
kwa vijana walio nje ya shule. Mpango kazi huu utawawezesha kufanikisha ushiriki wa
watoto na mchango wao katika maswala yanayohusiana na Virusi vya
UKIMWI/UKIMWI katika maisha yao, maisha ya wana rika, familia na jamii zao kwa
ujumla.
2.2.9 Sera ya Utamaduni
Sera hii inatetea matumizi ya Kiswahili kama lugha ya taifa na kutoa motisha kwa
utumiaji wa lugha hii. Kiswahili ni lugha kuu ya mawasiliano katika ngazi zote na lugha
inayotumika katika mfumo wa elimu, hasa katika shule za msingi. Matumizi ya lugha
moja ya kitaifa yatasaidia sana kufanikisha utekelezaji wa Mpango Kazi huu. Lugha
moja ya kitaifa inatoa fursa kwa ushiriki wa watoto unaowawezesha mawasiliano rahisi
na yenye tija katika ngazi zote. Hata hivyo, Mpango Kazi huu unatoa nafasi kwa lugha
zote mbili, ya Kiswahili na Kiingereza kutumika katika utekelezaji.
2.2.10 Mchakato wa Maboresho ya Serikali za Mitaa
Maboresho ya serikali za mitaa yanayo lengo la kupeleka huduma za serikali karibu na
wananchi na kuhamasisha ushiriki mkubwa zaidi wa jamii katika uongozi, hii ikiwa ni
pamoja na ushiriki wa watoto. Ongezeko la ushiriki wa jamii katika uendeshaji na
uongozi wa kidemokrasia katika taasisi mbalimbali utasaidia kuleta uwiano na usawa
katika ugawaji wa raslimali katika serikali za mitaa, na mipango inayolenga maendeleo
22
ya watoto. Mpango kazi huu utasaidia kutoa mwongozo zaidi kwa serikali za mitaa na
taasisi zinazojali demokrasia katika kufanikisha kuingiza mchango wa watoto na ushiriki
wao katika kufanya maamuzi kwa yale yote yanayowahusu watoto na jamii zao.
2.2. 7 Jumuisho la Sera
Utekelezaji wa sera zote hizi unachangia katika kufanikisha utekelezaji wa MKUKUTA
II (Mpango wa Pili wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania) ambao
unatambua umuhimu wa utawala bora kama msingi wa kukua kwa uchumi, maisha bora
na katika kundi la III la maeneo muhimu ya MKUKUTA kwa mfano, MKUKUTA
unaelezea utaratibu wa kufanikisha utawala bora na ushiriki wa raia katika ngazi zote.
Mpango Kazi huu utasaidia katika utekelezaji wa lengo hili la MKUKUTA kwa kutoa
miongozo ya ushiriki wa watoto katika utawala. Ushiriki wa raia unaojumuisha ushiriki
wa watoto ni msingi wa demokrasia na utawala bora.
MKUKUTA II pia unasisitiza suala la kulinda haki za binadamu kwa watu wote, watoto
kwa watu wazima, wake kwa waume. Kuhusu haki za watoto, chini ya Lengo la 3
sehemu ya pili MKUKUTA unatambua umuhimu wa kuzilinda haki za watoto:
Kuheshimu haki za watoto kunachangia katika kuendeleza utamaduni
wakulinda haki za binadamu kwa vile watoto watakua wakiwa wanajua
haki zao, majukumu na wajibu wao kama watu wenye haki.
MKUKUTA pia unaelezea maudhui ya kuingiza ushiriki hasa wa vikundi vya watoto
wenye mahitaji maalum kwa lengo la kuboresha maisha yao kwa kuboresha huduma za
jamii kama vile elimu ulinzi na uhai wao, afya na lishe, maji safi na salama, usafi wa
mazingira, makazi yenye heshima, na mazingira endelevu.
Katika kufanikisha haya, aina na utawala unaothamini ushiriki wa raia wote
unatambulika kuwa ndio kiini cha mafanikio. Kwa hali hiyo, ushiriki wa watoto kama
inavyotambulika kikatiba, na nafasi yao kama ulivyoelezwa katika Sheria ya Watoto,
kuwa hakuna ubaguzi wala kutengwa kwa kikundi chochote, vyote hivi ni fursa kwa
watoto kushiriki katika majukumu ya kuleta maendeleo ya nchi kwa ushirikiano na watu
wazima. Ukweli ni kwamba, kwa kuwa watoto ni sehemu kubwa ya idadi ya waTanzania,
mchango wao ni muhimu katika kufanikisha malengo ya MKUKUTA. Kwa kupitia sauti
zao, matumaini ya kizazi ambacho hatimaye kitachukua dhamana ya hatma ya utawala na
uhai wa taifa yatafikiwa kwa manufaa ya raia wote na hivyo ushiriki wao ni muhimu
katika kufikia malengo ya MKUKUTA.
3.0 MATEGEMEO YA WATOTO KATIKA USHIRIKI
Mara nyingi ushiriki wa watoto umekuwa unatafsiriwa vibaya. Mfano halisi ni kuhusu
mchango wa watoto katika kazi za nyumbani, mahudhurio darasani, na mchango wa
majibu kwa maswali wanayouliza waalimu, pamoja na watoto wenyewe kuuliza maswali.
Shughuli hizi zinahusiana na dhana ya ushiriki wa watoto kama sehemu ya kuendeleza
ushiriki katika shughuli za jamii. Ni vigumu sana kwa watu wengi kuelewa ushiriki
katika jamii zaidi ya mifano iliyotajwa hapo juu, na tunapojaribu kuhusisha ushiriki
23
katika eneo la kufaidi haki za msingi za raia inawawia vigumu zaidi watu wengi. Kwa
mfano, kule tu kufikiria kwamba watoto waruhusiwe kutoa maoni yao katika kufanya
maamuzi mbalimbali inaweza kuonekana kwamba ni kitu cha kinadharia tu ambacho
hakiwezekani. Ukweli ni kwamba sio kitu kigumu hata kidogo. Kwa ufafanuzi rahisi
zaidi, kikundi cha mashirika mbalimbali ya ushiriki wa mtoto “Inter-Agency Working
Group on Children’s Participation”6 kimeelezea msingi mkuu katika suala hili kwamba:
Haki za kiraia zinaanzia pale mtoto anapozaliwa, wakati mtoto
anaandikishwa katika ofisi ya Uzazi na Vifo, ambapo tendo hili ni msingi
wa kufaidi haki nyingine ambazo ni stahili ya mtoto kama vile kupata
huduma za afya na elimu, ulinzi dhidi ya aina zote za unyonyaji kiuchumi,
na kijinsi, na kutendewa haki wakati mtoto anapotenda kosa au kuvunja
sheria
Mtoto anavyozidi kukua, mchango wake huongezeka na mazingira yanayomsaidia kutoa
mchango huo nayo hubadilika. Hili ni muhimu kueleweka katika Mpango Kazi huu,
ambao umejikita kwenye kusimamia „haki ya watoto kusikilizwa‟ na kupanua wigo wa
jinsi watoto wanaweza kuchangia katika kuandaa mipango na kufanya maamuzi muhimu
katika jamii ya kitanzania kwa ujumla. Kwa kuzingatia maudhui ya haki za binadamu,
ambapo ushiriki wa watoto ni kiini cha haki za binadamu, kuna haja ya kutambua hili
kuwa ni sehemu muhimu ya malezi na makuzi ya watoto, na kujitambua, ambavyo
vinaendana na kujenga uwezo wa kufanya maamuzi na maendeleo ya ari ya kujithamini
na kujiamini.
Kwa mtizamo wa Haki za Binadamu, ambapo ushiriki wa watoto ni miongoni mwa haki
hizo, inabidi itambulike kuwa haki hii ni sehemu ya makuzi na humfanya mtu kujitambua
na kujithamini na pale inapohusishwa na swala la kufanya maamuzi, huwa ni sehemu ya
ukuaji wa ari ya kujiendeleza kwa kujiamini. Kwa ujumla hakuna sababu ya
kutenganisha majukumu ya watu wazima na watoto kama ilivyokuwa siku za nyuma. Ili
kutambua hili, ni budi ifahamike kuwa haki za watoto sio tofauti na zile za watu wazima.
Hivyo basi, wote wanapaswa kufahamishwa haki zao hizo, na watoto wanapaswa
kuamini kuwa watapata haki zao ambazo ni pamoja na:
Kupata taarifa (kuhusu masuala yote yanayowahusu na mengineyo);
Kuweza kupata habari na pia kutafuta habari;
Kuwa na maoni yao na uwezo wa kusambaza maoni hayo yasikike (kwa watoto
wenzao na watu wazima);
Kuwa na uwezo wa kushiriki katika majukumu mbalimbali katika jamii
Kuheshimu maoni ya watu wengine na maoni yao kuheshimiwa/kuthaminiwa ;
Kushiriki kikamilifu katika majukumu na michakato mbalimbali katika jamii;
Kushirikishwa kutoa ushauri katika masuala ya kufanya maamuzi na kuwa
wadau wakuu katika kupitisha maamuzi hayo; na
24
Masuala yao muhimu kuzingatiwa na hivyo kuingizwa kwenye michakato ya
kufanya maamuzi, na wakiwa na taarifa kamili ya maamuzi hayo na matokeo au
athari ya maamuzi hayo.
Yote haya yafanyike kulingana na uwezo wa watoto kuchangia na kushiriki katika
michakato kwa njia ambazo maoni yao yatapewa uzito unaostahili kutokana na uwezo
(kifungu cha 5 cha Mkataba wa Kimataifa kuhusu Haki ya Mtoto, na hili lionekane kwa
mtizamo chanya na kuwa ni mchakato unaolenga kuleta maendeleo na makuzi,
kujitambua na kujieleza.
Mchango huu wa watoto uchukuliwe pia kuwa utazidi
kuongezeka kila wanapopata fursa ya kushiriki na kutoa nafasi kwa kila mtoto kuchangia
kwa uwezo wake. Ni vyema pia kutambua kuwa ukomavu wa watoto katika swala hili
unachangiwa kwa kiasi kikubwa na aina ya taarifa anayopata na kuitumia katika kila
fursa anayoipata na uzoefu anaoukusanya, mazingira, matarajio ya jamii kulingana na
tamaduni, na pia kiwango cha msaada anaoupata kutoka kwa watu wazima na jamii yake.
Utekelezaji na viwango vya ushiriki wa mtoto vinapendekeza; kuhakikisha yafuatayo:
Kwamba masuala yaliyo na manufaa kwa watoto kushiriki ni yale ambayo
watoto wananufaikanayo wakishiriki na yanayotokana na mchango wao,
kimaarifa, kiujuzi na kiuwezo;
Watoto wanahusishwa katika kuandaa vigezo vya kuchagua wawakilishi wao
katika ushiriki
Watoto wana muda wa kujiandaa kushiriki na michakato/mifumo inaandaliwa
kuhakikisha kuwa wanashiriki kikamilifu kutoa maoni yao na kupata ridhaa
kutoka kwa wenzao kwa yale watakayochangia.
Watoto wanashiriki kwa ridhaa yao wenyewe, bila shinikizo, na kwamba wana
uhuru wa kujitoa kwenye ushiriki wakati wowote watakavyoamua wao.
Watoto wanashiriki kwa namna, kiwango na kasi ambayo ni muafaka kulingana
na uwezo wao na matakwa yao.
Majukumu mengineyo ya watoto yanaheshimiwa na kuzingatiwa ili yasiathirike
(kwa mfano majukumu ya nyumbani, shuleni au kazi zao).
Utaratibu na mbinu zinazotumika zijumuishe mambo muhimu na kujengeka
kwenye misingi ya mifumo rafiki kwa watoto iliyopo, maarifa na uzoefu kwa
kuzingatia mazingira ya kijamii, kiutamaduni na mila na desturi.
Msaada kutoka kwa watu wazima katika kujenga maisha ya watoto, (kwa mfano
msaada wa wazazi/walezi na waalimu), unapatikana kuhakikisha kuwa
unahamasisha zaidi ushiriki na kuzingatia ushiriki wa wasichana na wavulana.
4.0 UCHAMBUI WA WADAU, WIZARA NA TAASISI
4.1 Utangulizi
Sehemu hii inazungumzia namna Mpango Kazi huu utakavyotekelezwa kwa kuhusisha
wadau mbalimbali. Kwa ujumla, ili sauti za watoto zisikike na kuthaminiwa kikamilifu,
majukumu mbalimbali yanahusika na watekelezaji ni pamoja na serikali, Asasi zisizo za
kiserikali, na wadau wengine wa maendeleo. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na
Watoto ambayo ndio msimamizi mkuu wa masuala ya watoto itashirikiana na serikali
kuu na idara zake, pamoja na Asasi zisizo za kiserikali kutekeleza mpango kazi huu.
25
4.2 Serikali Kuu na Idara zake
a) Kuandaa sera, ufuatiliaji na tathmini
i) Kuhakikisha kila wizara inaandaa sera husika ambazo zinalenga suala la
kulinda na kutetea haki ya mtoto ya kushiriki.
ii) Kuhakikisha mipango ya utekelezaji wa sera zilizotungwa inaandaliwa na
wizara husika na kutekelezwa ipasavyo.
iii) Kuhakikisha raslimali zinazohitajika zinapatikana kwa ajili ya utekelezaji wa
sera.
4.2.1 Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
a) Kupanga na Kuratibu
i) Kuhakikisa kuwa Mpango huu wa Ushiriki wa Watoto unapitishwa kupitia
mchakato rasmi kwa muda mfupi iwezekanavyo
ii) Kupanga na kuandaa mkakati wa utekelezaji wa Mpango huu, uratibu,
ufuatiliaji na upimaji wa utekelezaji wake
iii) Kwa kupitia kamati inayojumuisha wizara zote, kukubaliana na wizara
nyingine kuingiza suala la ushiriki wa watoto katika sera, mipango, programu
na miongozo yao.
iv) Kuingia makubaliano na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali
za Mitaa kuwa itaratibu na kusimamia masuala ya ushiriki wa mtoto miongoni
mwa wizara mbalimbali katika ngazi za mikoa na serikali za mitaa. Hili
litahitaji uundwaji wa chombo cha kuratibu katika wizara mbalimbali.
v) Kuratibu ufuatiliaji na kuandaa taarifa za utekelezaji za Haki ya Mtoto ya
Ushiriki na haki nyinginezo zinazohusu ushiriki na utekelezaji wa Sera ya
Watoto, Mkataba wa Kimataifa kuhusu haki za Mtoto na Mkataba wa Afrika
kuhusu Ustawi wa Mtoto
vi) Kuunda mfumo wa kuratibu ushirika wa wadau wote katika utekelezaji na
kuratibu shughuli zote za Mpango Kazi huu.
b) Ushawishi
i) Kutoa mafunzo kwa maofisa wa Maendeleo ya Jamii watakao elimisha jamii
kuhusu Mpango huu wa Ushiriki wa Mtoto.
ii) Kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
na asasi zisizo za kiserikali pamoja na vyombo vya habari kutoa elimu ya
ufahamu kwa wadau wengine (wazazi, watoto, viongozi wa serikali za
vijiji/mitaa, vyombo vya habari na wadau wengine) kuhusu umuhimu wa
ushiriki wa watoto na mbinu za kufanikisha ushiriki huo kikamilifu katika
masuala yanayowahusu watoto wa Tanzania na jamii zao.
iii) Kuendeleza, kuhamasisha, na kuwezesha jamii kuwapatia watoto haki ya
ushiriki na haki nyinginezo
iv) Kupanga na kusimamia kampeni za ushawishi kwa jamii kuhusu Ushiriki wa
Watoto
c) Ufuatiliaji na Takwimu
i) Kufanya utafiti wa ongezeko la kiwango cha ushiriki wa watoto katika
mambo yanayowahusu na kukusanya na kusambaza takwimu
ii) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program zitakazoandaliwa
na wadau mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha ushiriki wa watoto
26
4.2.3 Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
a) Kupanga na Kuratibu
i) Tawala za Mikoa kuratibu mahusiano/mawasiliano kati ya mabaraza ya
watoto ya wilaya na Baraza la Taifa la Watoto na kuhakikisha kuwa mabaraza
haya yanafanya kazi ipasavyo na kuingiza mapendekezo kutoka kwenye
mabaraza haya katika maamuzi na mipango ya halmashauri.
ii) Halmashauri za Wilaya kuandaa taratibu za kuingiza masuala ya watoto katika
mchakato wa mipango ya maendeleo ya wilaya.
iii) Halmashauri za walaya na ngazi za chini za utendaji kuandaa taratibu ambazo
zitawezesha watoto kushiriki katika kufanya maamuzi katika ngazi hizo za
utawala.
iv) Kupanga na kuandaa mkakati wa wizara wa utekelezaji, uratibu, ufuatiliaji na
upimaji wa utekelezaji.
v) Kutoa miongozo ya uingizwaji wa masuala ya/hoja za watoto hasa kuhusu
Ushiriki wao, katika mipango ya maendeleo, utelekelezaji, usimamizi na
tathmini katika ngazi zote
vi) Kuandaa ripoti za utekelezaji za kupelekwa sehemu husika hasa Wizara ya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.
b) Ufuatiliaji na Takwimu
iii) Kufanya utafiti wa ongezeko la kiwango cha ushiriki wa watoto na kukusanya
na kusambaza takwimu kwa watekelezaji na wadau wengine
iv) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program zitakazoandaliwa
na wadau mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha ushiriki wa watoto
4.2.3 Wizara ya Fedha na Uchumi
a) Kupanga na Kuratibu
i) Kuandaa miongozo kuhusu namna ya kushiriki na watoto (kwa mfano
uwakilishi wa Baraza la Watoto kutumika) katika kuandaa bajeti na kutenga
fedha na rasilimali nyinginezo (kujadili kwa pamoja na kutoa maoni na
maamuzi) kwa ajili ya kufanikisha ushiriki wa watoto na kutimiziwa mahitaji
yao mengineyo katika ngazi zote.
ii) Kuhakikisha kuwa katika mwongozo wa bajeti ya mwaka kunakuwepo na
mwongozo kuhusu uingizwaji wa shughuli za ushiriki wa watoto na bajeti
kwa ajili ya kutekeleza Mpango Kazi huu inakuwepo na kutumika ipasavyo.
b) Ushawishi
i) Kutoa mafunzo kwa Maofisa Mipango watakaoelimisha wadau ndani ya
wizara na wengineo kwa kushirikiana na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na Watoto, kuhusu namna ya kuandaa bajeti shirikishi kwa
kuzingatia ushiriki wa watoto na kuzingatia hoja na mahitaji ya watoto katika
kufanikisha ushiriki wao katika kuandaa bajeti katika ngazi zote.
c) Ufuatiliaji na Takwimu
v) Kufanya utafiti wa ongezeko la kiwango cha ushiriki wa watoto na kukusanya
na kusambaza takwimu kwa watekelezaji na wadau wengine
27
vi) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program zitakazoandaliwa
na wadau mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha ushiriki wa watoto
4.2.4 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii
a) Kupanga na Kuratibu
i) Kuandaa sheria na miongozo (kwa kushirikiana na Wizara ya maendeleo ya
Jamii, Jinsia na Watoto) kwa ajili ya wizara kuhusu utekelezaji wa sheria
mbalimbali ikiwepo sheria ya watoto ya mwaka 2009
ii) Kuandaa miongozo na taratibu kuhusu namna ya kufanikisha ushiriki wa
watoto wa makundi yote hasa ya wale wenye ulemavu katika ngazi zote ndani
na nje ya wizara hasa ngazi ya familia, mashuleni, katika jamii na katika
mifumo ya kisheria na utawala. Miongozo hii itasaidia kutafsiri ushiriki wa
watoto katika nyanja za sera na sheria mbalimbali zinazohusu watoto na
kuhakikisha huduma kwa watoto (haswa wale wenye ulemavu)
zinazowaandaa kuweza kushiriki zinaimarishwa
iii) Kusimamia, kufuatilia na kutathmini kiwango cha utekelezaji wa miongozo
mbalimbali ya ushiriki wa watoto wa makundi yote
b) Ushawishi
i) Kutoa mafunzo/semina kwa Maofisa wa Afya na Ustawi wa Jamii watakaoelimisha
wadau wengine kwa kushirikiana na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii,
Jinsia na Watoto, kuhusu namna ya kushirikisha watoto wenye ulemavu katika
mipango ya afya katika ngazi zote (familia, jamii, nk.) kwa kuzingatia haki yao ya
ushiriki.
c) Ufuatiliaji na Takwimu
i) Kufanya utafiti wa ongezeko la kiwango cha ushiriki wa watoto katika
mipango ya afya na ustawi wa jamii katika ngazi zote na kukusanya na
kusambaza takwimu kwa watekelezaji wa wizara na wadau wengine
ii) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program zitakazoandaliwa
na wadau mbalimbali wa afya na ustawi wa jamii kwa ajili ya kufanikisha
ushiriki wa watoto
4.2.5 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
a) Kupanga na Kuratibu
i) Kuandaa sera sheria, mipango na miongozo rafiki kwa watoto (kwa
kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto) kwa ajili ya
wizara na mikakati kuhusu ushiriki wa watoto hasa katika eneo la mitaala,
mbinu za ufundishaji na utawala.
ii) Kuandaa miongozo na taratibu kwa ajili ya Maafisa Elimu wa Wilaya na
viongozi wa shule kuhusu namna ya kuboresha mifumo ya utawala na
uendeshaij wa shule na kufanikisha ushiriki wa watoto wa makundi yote hasa
ya wale wenye ulemavu na namna ya kurasimisha uwepo wa mabaraza ya
watoto shuleni pamoja na mbinu za kuingiza masuala yaliyoibuliwa na watoto
katika mabaraza yao katika mamuzi ya shule kwa mfano kuhusu
miundombinu, ufundishaji na uongozi.
28
iii) Kusimamia, kufuatilia na kutathmini kiwango cha utekelezaji wa miongozo
mbalimbali ya sekta ya elimu na ufundi kuhusu ushiriki wa watoto wa
makundi yote hasa yale ya wale wenye ulemavu.
iv) Kwa kutumia uongozi na taasisi za elimu au shule, kusimamia uanzishwaji na
uendeshwaji wa mabaraza ya watoto ya shule na kuandaa utaratibu
utakaowezesha maoni ya watoto kutoka kwenye mabaraza hayo kuingizwa
kwenye mipango ya shule na menejimenti.
b) Ushawishi
i) Kutoa mafunzo/semina kwa Maofisa Elimu watakaoelimisha wadau wengine kwa
kushirikiana na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, kuhusu
namna ya kushirikisha watoto wa makundi yote hasa wale wenye ulemavu katika
mipango ya elimu katika ngazi zote (familia, jamii, nk.) kwa kuzingatia haki yao ya
ushiriki.
c) Ufuatiliaji na Takwimu
i) Kufanya utafiti wa ushiriki wa watoto katika mipango ya elimu katika ngazi
zote na kukusanya na kusambaza takwimu kwa watekelezaji wa wizara na
wadau wengine
ii) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program zitakazoandaliwa
na wadau mbalimbali kuboresha sekta ya elimu kwa ajili ya kuratibu kiwango
cha ushiriki wa watoto na ufanisi wa mabaraza ya shule na changamoto
zinazoyakabili
4.2.6 Wizara ya Habari, Maendeleo ya Vijana na Michezo
a) Kupanga na Kuratibu
i) Kuandaa miongozo kwa ajili ya vyombo vya habari kuhusu ushiriki wa
watoto na vijana kwenye masuala ya habari na mawasiliano na mikakati
kuhusu ushiriki wa watoto na vijana hasa katika eneo la vyanzo vya habari,
aina ya habari wanayohitaji watoto na vijana, usambazaji wa habari kwa
watoto na vijana unaokidhi mahitaji yao, mbinu za kusambaza habari kwa
watoto na vijana zinazozingatia mahitaji ya makundi mbalimbali ya watoto na
vijana hasa ya wale wenye ulemavu na uendeshaji wa programu mbalimbali
za vyombo vya habari.
ii) Kuandaa miongozo kwa waandaaji wa programu mbalimbali za vyombo vya
habari, waandishi wa vitabu na makala na vipindi vya watoto na vijana
kuhusu namna ya kuboresha na kufanikisha ushiriki wa watoto na vijana wa
makundi yote hasa ya wale wenye ulemavu
iii) Kusimamia, kufuatilia na kutathmini kiwango cha utekelezaji wa miongozo
mbalimbali ya sekta ya habari na utangazaji kuhusu ushiriki wa watoto na
vijana wa makundi yote hasa yale ya wale wenye ulemavu
b) Ushawishi
i) Kutoa mafunzo/semina kwa Maofisa Habari, Wahariri na Waandaaji wa
vipindi na programu mbalimbali watakaoelimisha wadau wengine kwa
kushirikiana na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,
29
kuhusu namna ya kushirikisha watoto wa makundi yote hasa wale wenye
ulemavu katika mipango ya ukusanyaji na usambazaji wa habari hasa ile ya
vyombo vya habari katika ngazi zote (familia, jamii, nk.) kwa kuzingatia haki
ya ushiriki kwa watoto na vijana.
ii) Kwa kuzingatia jukumu lake la mawasiliano, Wizara hii kwa kushirikiana na
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na wadau wengine, kuandaa
mkakati utakaoboresha juhudi nyinginezo za utetezi wa haki za watoto na
vijana (kama zile zilizoainishwa kwenye „Ajenda ya Watoto‟).
c) Ufuatiliaji na Takwimu
i) Kufanya utafiti wa ushiriki wa watoto katika sekta ya habari katika
ngazi zote na kukusanya na kusambaza takwimu kwa watekelezaji wa
wizara na wadau wengine.
ii) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program
zitakazoandaliwa na wadau mbalimbali kuboresha sekta ya habari na
mawasiliano kwa ajili ya kuratibu kiwango cha ushiriki wa watoto.
4.2. 7 Wizara ya Sheria na Katiba
Utaratibu uliowekwa kwa ajili ya mahakama ya watoto unatoa fursa nzuri kwa watoto
kuweza kusikilizwa katika mahakama na inapaswa kuwa hivyo kwa masuala yote
yanayowahusu watoto.
a) Kupanga na Kuratibu
i) Kuandaa sera, sheria na miongozo kwa ajili ya wizara ambayo inatambua haki
za watoto pamoja na haki ya ushiriki na kuweka mazingira rafiki ya
kurahisisha ushiriki wa watoto katika utoaji huduma kwa watoto (kwa mfano
lugha rahisi inayoeleweka kwa watoto kuhusu mwenendo wa kesi zao
mahakamani na haki ya kusikilizwa) na kuhakikisha wizara nyingine na
wadau wengine wanarekebisha sheria zao ndogondogo na taratibu zao ili
kulinda haki za watoto pamoja na ile ya ushiriki.
ii) Kuandaa miongozo kwa vyombo na taasisi za wizara (kama vile mahakama,
polisi, n.k) na wadau wengine ambao wanashughulika na masuala ya watoto
kuhusu namna ya kuboresha na kufanikisha ushiriki wa watoto wa makundi
yote hasa ya wale wenye ulemavu kwenye kuandaa sera, sheria, mipango,
programu, taratibu na mikakati ya utekelezaji.
iii) Kwa kupitia Kamisheni ya Kurekebisha Sheria kutoa ushauri wa namna ya
kurekebisha sheria zinazohusu uhuru na haki ya watoto kusikilizwa na
kushiriki katika masuala yote yanayohusu maisha yao kama vile ndoa na
ushiriki katika ushauri na upimaji hiari wa UKIMWI na pia kutoa ushauri
kuhusu kuandaa taratibu na miongozo ya namna ya kusimamia Sheria ya
Watoto kwa ajili ya kulinda haki zao.
iv) Kwa kupitia Kamisheni ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, kuboresha
mifumo yake ya kupokea na kufuatilia malalamiko ya watoto, na kuhakikisha
kuwa haki za watoto zinazingatiwa na kupewa uzito unaostahili na watoto
wanafaidi haki yao ya kusikilizwa katika ngazi zote hasa katika kutoa taarifa
na malalamiko dhidi ya udhalilishwaji, unyonywaji na kufanyiwa ukatili.
30
v) Kusimamia, kufuatilia na kutathmini kiwango cha utekelezaji wa sheria, sera
na miongozo mbalimbali ya sekta ya sheria kuhusu haki za watoto na ushiriki
wa watoto wa makundi yote hasa ya wale wenye ulemavu
b) Ushawishi
i) Kutoa mafunzo/semina kwa maafisa, mahakimu (hasa wale wa mahakama ya
watoto), polisi, wataalamu wa kuandaa miswada ya sheria za watoto na
watumishi wengine wa wizara watakaoelimisha wadau wengine kwa
kushirikiana na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,
kuhusu namna ya kufanikisha na kuboresha ushiriki wa watoto wa makundi
yote hasa wale wenye ulemavu
ii) Kwa kuzingatia jukumu lake la kusimamia haki kutendeka, Wizara hii kwa
kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na wadau
wengine, kuandaa mkakati utakaoboresha juhudi nyinginezo za utetezi wa
haki za watoto katika vyombo vya mahakama, ulinzi na usalama (kama zile
zilizoainishwa kwenye „Ajenda ya Watoto‟)
c) Ufuatiliaji na Takwimu
i) Kufanya utafiti wa ushiriki wa watoto katika sekta ya sheria katika
ngazi zote na kukusanya na kusambaza takwimu kwa watekelezaji wa
wizara na wadau wengine
ii) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program
zitakazoandaliwa na wadau mbalimbali kuboresha sekta ya sheria kwa
ajili ya kuratibu kiwango cha ushiriki wa watoto
iii) Kufanya utafiti kuhusu malalamiko ya watoto kuhusu uvunjwaji wa
haki zao hasa ile ya kusikilizwa na utatuzi wa malalamiko hayo
pamoja na changamoto zinazojitokeza katika kufanikisha ushiriki wa
watoto katika sekta ya sheria
4.2.8 Wadau wa Maendeleo na Asasi Zisizo za Kiserikali
Wadau Wengine wa Maendeleo na Asasi Zisizo za Kiserikali watashiriki katika kujaza
mapengo kwa yale yanayofanywa na serikali katika ngazi zote. Hii ni pamoja na:
i) Kusaidia katika kutafuta rasilimali
ii) Kutoa mafunzo kwa vikundi mbalimbali, pamoja na watoto
iii) Kujenga ufahamu na uelewa kwa makundi mbalimbali kuhusu Haki ya
Watoto ya Ushihiriki na haki nyinginezo
iv) Kutetea haki za watoto pamoja na Haki ya Ushiriki
v) Kushiriki katika majadiliano na katika kufanya maamuzi mbalimbali
yanayohusu Ushiriki wa watoto katika sekta mbalimbali na katika tawala za
mikoa.
vi) Kushiriki katika eneo lingine lolote la Mpango Kazi huu kwa kutumia ujuzi
walionao na rasilimali zao ili kufanikisha kufikia malengo yote ya Mpango
Kazi kwa kufanya kazi kwa karibu sana na serikali
4.2.9 Familia Familia ndio taasisi ya kwanza ya malezi na makuzi ya watoto katika jamii za Tanzania.
Wazazi wana jukumu kubwa la kuhakikisha watoto wanaishi na kukua. Familia
31
itasaidiwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kupitia Idara ya Watoto
katika kutekeleza na kuendeleza ushiriki wa watoto.
4.2.10 Baraza la Watoto la taifa Baraza hili la watoto ndio chombo pekee rasmi ambacho kimeundwa kisheria kwa lengo
la kufanikisha ushiriki wa watoto humu Tanzania. Kitakapoandikishwa rasmi, na
kitakapopata ridhaa ya serikali za mitaa na Asasi Zisizo za Kiserikali, chombo hiki
kitakuwa cha uwakilishi wa watoto katika vyombo vya maamuzi na utekelezaji katika
jamii. Ngazi za chini za serikali za mitaa zinapaswa kuandaliwa kwa kuwezeshwa
kuandaa taratibu kwa watendaji/wadau wote ambao wana nia ya kufanya kazi na
mabaraza ya watoto au kwa niaba ya Mabaraza ya Watoto kwa kutumia Mwongozo wa
Kitaifa wa Mabaraza ya Watoto.
4.2.12 Maoni ya ziada kuhusu miundo na majukumu ya watendaji wakuu
Hapa Tanzania hakuna kamisheni au chombo kingine chochote maalum cha uchunguzi
wa malalamiko ya watoto. Ofisi au chombo cha aina hii kingesaidia kwa kiasi kikubwa
yafuatayo:
i) Kusuluhisha migongano kati ya watoto na watu wazima kuanzia katika ngazi
ya familia hadi ngazi ya mkuu wa nchi
ii) Kuboresha mawasiliano, kusimamia haki za watoto na kuratibu ushiriki
iii) Kushiriki katika utafiti and uundaji wa sera
iv) Kushughulikia malalamiko yanayotokana na mahusiano kati ya watoto na
watu wazima.
v) Kusaidia watu wazima pamoja na watoto na vijana wanaotaka au wenye ari ya
kutaka kuelewa zaidi kuhusu haki za watoto na vijana, na kusaidia serikali na
watu /taasisi rafiki kwa watoto/vijana kufahamu matakwa ya vijana.
vi) Kufanya utafiti ili kupata uelewa zaidi kuhusu mambo muhimu katika maisha
ya watoto na vijana.
vii) Kushauri serikali na wadau wengine kuhusu kufanya yale mambo mazuri tu
yanayofaa kufanyiwa watoto na vijana.
viii) Kama chombo huru cha kupokea malalamiko, kupokea, na pale
inapowezekana kutathmini/kuchambua malalamiko yanayowasilishwa na
vijana au watu wazima kwa niaba ya vijana na kuyapeleka kwa vyombo vya
utatuzi pale walalamikaji wanapotoa idhini yao.
ix) Kufuatilia kwa karibu na makini, kama chombo huru, utendaji wa mabaraza
ya watoto na mabaraza ya shule.
Kuna hisia kuwa ijapokuwa watoto katika nchi nyingine wamepewa fursa ya kuanzisha
mabunge au mabaraza yao ambayo ni nje ya mfumo wa vyombo vya serikali, kuna
mahusiano/mawasiliano kidogo sana kama yapo, kati ya mabaraza ya watu wazima na
mabaraza ya watoto. Vyombo vya aina hii ya uwakilishi wa matakwa ya watoto
vinapaswa pia kuwepo katika mfumo wa serikali katika ngazi zote za serikali na idara
zake. Katika kufanya kazi zake ndani ya serikali, hasa kwa kupitia Kamisheni maalum au
Chombo Maalum cha Kuchunguza Malalamiko ya Watoto, chombo kama hiki kina
uwezo mkubwa wa kufikisha maamuzi au ushauri au mapendekezo muhimu ya
32
maendeleo kutoka kwa wawakilishi wa watoto kwenda kwa watu wazima, mambo
ambayo wangeachiwa wenyewe watoto wasingeweza kuyafikisha kunakohusika.
Hata hivyo, jukumu la Kamisheni au Chombo Maalum cha Kuchunguza Malalamiko ya
Watoto linahitaji kuandaliwa mipango ya kina ili kuwapangia wawakilishi wa watoto
majukumu ambayo yanakidhi mahusiano kati ya viashiria vya sera, sheria, na utawala na
mahitaji muhimu. Kwa hali hiyo, katika Mpango Kazi huu, inapendekezwa kufanyika
utafiti mdogo kuhusu huduma za Kamisheni/ Vyombo Maalum vya Kuchunguza
malalamiko ya watoto vilivyopo duniani kwa ajili ya watoto hasa vile vya Afrika ya
Kusini na nchi ya Ethiopia. Ili kupata taarifa zaidi, kuna haja pia ya kujifunza kutoka
Taasisi ya Chombo Maalum cha Kuchunguza Malalamiko ya Watoto cha Kimataifa,
ambapo Kamisheni ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ya Tanzania ni mjumbe.
Katika taasisi hizi zilizoko ulimwenguni, kuna uwezekano mkubwa wa kupata msaada
utakaoiwezesha serikali yetu kuandaa ratiba ya kuandaa chombo hiki muhimu kwa
watoto. Vyombo vya uwakilishi wa watoto vilivyopo vitakuwa na jukumu kubwa la
kusambaza taarifa kuhusu chombo hiki kipya cha serikali, uundaji wake na hatua za
kuchukua kuelekea kwenye uchaguzi wa Kamishna au kuunda Chombo Maalum cha
Kuchunguza Malalamiko ya Watoto, kuandaa na kutafrisi majukumu ya ofisi hiyo, na
ratiba ya uteuzi wa Kamishna au uundaji wa chombo hicho maalum na muda wa kuanza
kazi.
Mabaraza ya Watoto nayo yana jukumu kubwa la kuiwezesha Wizara ya Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na Watoto kutekeleza jukumu hili na mchakato mzima wa kuanzisha
Kamisheni ya pamoja na kusambaza taarifa za Mpango kazi huu ambao umeandaliwa
kwa ajili ya kulinda haki za watoto. Kwa vile lengo kuu la Mpango Kazi huu ni
kuhakikisha kwamba watoto wanashiriki kikamilifu katika mambo yote yanayohusu
maisha yao, ni dhahiri kwamba jukumu kubwa mojawapo kwa mabaraza ya watoto ni
kuanzisha jukwaa la kudumu litakalotumika kubadilishana uzoefu katika kusimamia
maendeleo na ufanisi katika utekelezaji wa Mpango kazi huu wa Kitaifa.
5.0 MKAKATI
5.1 Mwelekeo
Mpango Kazi huu unaangalia sehemu kuu nne:
1. Kuelimisha wadau wote pamoja na watendaji wa shughuli za serikali na
kijamii kuhusu sera, sheria, kanuni na taratibu mbalimbali pamoja na
makubaliano ya serikali yetu ya Kikanda na Kimataifa kuhusu haki ya
mtoto ya kusikilizwa na kushiriki katika mambo yote yanayomhusu.
2. Kuandaa/Kujenga mfumo wa kitaifa wa ushiriki wa watoto ambao
umejengeka kwenye misingi ya usawa, demokrasia na haki, misingi
ambayo inajali haki ya mtoto ya kusikilizwa na kushiriki.
3. Kuhakikisha taratibu na miongozo ya namna ya kutekeleza mfumo huo wa
Ushiriki wa Watoto pamoja na vyombo vya kufanikisha utendaji kwa
kufuata mfumo huo vinaandaliwa na kufahamika kwa wadau wote
4. Kuandaa utaratibu wa kuratibu utekelezaji wa Mpango kazi huu kwa
kugawa majukumu kwa wadau mbalimbali na kuelekeza namna ya
33
kuratibu na kutathmini utekelezaji kwa kuhusisha watoto na vyombo vyao
vya uwakilishi.
Kwa kiasi kikubwa Tanzania ina mazingira mazuri kisera na kisheria ya Ushiriki wa
watoto. Kwa kuzingatia uwepo wa mazingira haya, vyombo kadhaa vya ushiriki wa
watoto ikiwa ni pamoja na mabaraza ya watoto vimeshaundwa na tayari vinatumika japo
kwa kiasi kidogo bado. Kwa ujumla bado ushiriki wao haujaonekana vya kutosha
kwenye kuandaa mipango ya maendeleo ya sekta mbalimbali, hata zile ambazo watoto
wanahusika moja kwa moja. Maamuzi mengi kuhusu maisha yao na jamii kwa ujumla
yanafanywa bila kushirikisha watoto kwa visingizio mbalimbali pamoja kile cha
kutokujua namna ya kushirikisha watoto hasa wale wenye umri mdogo. Mila na desturi
nazo zinachangia kwa kiasi kikubwa kuwabagua watoto katika ngazi za maamuzi kuanzia
ngazi ya familia kwa visingizio kuwa watoto hawajui kitu wala hawajijui. Hali hii
imekuwa mbaya zaidi pale ambapo Tanzania imekuwa haina chombo maalum cha
kuchunguza malalamiko ya watoto ijapokuwa wako watetezi wengi wa haki za watoto.
Kwa ujumla serikali imeingia mikataba ya Kikanda na Kimataifa kuhusu suala hili la
kufanikisha ushiriki wa watoto na mikataba hii imasaidia kutoa miongozo mbalimbali
kuhusu utatuzi wa suala hili. Mpango kazi huu unatambua yote haya na ukamilifu wake
umezingatia sera, sheria, mikataba mbalimbali ambayo serikali yetu imeridhia pamoja na
hali halisi ya mazingira ya kitanzania kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni.
Ili kuhakikisha malengo na matarajio ya Mpango Kazi huu yanafikiwa, raslimali watu na
fedha zinahitajika na kwa hali hiyo ni jambo la busara kwa kila mdau kuandaa bajeti
inayotosheleza kwa majukumu yake katika kuwajibika ipasavyo. Kwa hali hiyo, sehemu
muhimu na ya awali ya maandalizi ya utekelezaji wa Mpango huu ni kuandaa raslimali za
kutosha kuweza kumudu shughuli zote za utendaji kuhusu mchakato mzima wa
kuhakikisha ushiriki wa mtoto unakuwa wa kiwango cha hali ya juu na wa kudumu kama
malengo na madhumuni ya Mpango Kazi huu yanavyofafanua.
5.3 Lengo na Madhumuni
5.3.1 Lengo/Madhumuni ya jumla
Lengo na Madhumuni ya Mpango Kazi huu ni kujenga mfumo wa kushirikiana pamoja
na watoto na kutoa mwongozo bayana kuhusu umuhimu wa ushiriki na michango ya
watoto katika mambo yote yanayowahusu na katika mazingira rafiki; pamoja na
kufafanua taratibu na kanuni za namna ya kushiriki pamoja na watoto katika ngazi
mbalimbali na katika maeneo yote ili kuhamasisha utetezi na usimamizi wa haki ya
watoto ya kusikilizwa miongoni mwa wale wenye madaraka na wadau mbalimbali.
5.3.2 Madhumuni Mahsusi
Ili kufikia lengo hili kuu, malengo mahsusi yafuatayo yanahusika:
i. Kutoa ufafanuzi kuhusu suala zima la matakwa na umuhimu wa mchango wa
watoto na ushiriki wao katika masuala yote yanayowahusu katika ngazi zote;
ii. Kutoa mwongozo na taratibu kuhusu jinsi ya kushiriki na watoto katika mazingira
ya aina zote;
34
iii. Kuhamasisha juhudi za kuandaa mazingira rafiki na fursa kwa watoto kushiriki
katika ngazi za familia, jamii na katika ngazi ya taasisi na mifumo mbalimbali;
iv. Kutoa fursa za kujenga mahusiano ya karibu na mshikamano kati ya watetezi wa
haki za watoto ndani ya serikali na idara zake, asasi zisizo za kiserikali, na
mashirika ya wadau wa maendeleo, na;
v. Kutoa mwongozo wa utaratibu wa ushiriki wa watoto humu Tanzania na kukuza
ushiriki huo kufikia kiwango cha juu hadi kufikia kuingizwa kwa haki zao za
kiraia, katika masuala yote yanayowahusu wao na katika kushiriki kufanya
maamuzi katika mambo yanayohusu maisha yao na ya jamii yao kwa kuzingatia
demokrasia halisi kwenye uongozi, utawala na utendaji ili kuboresha maisha yao.
5.3 Bango Kitita (Mpango wa Utekelezaji)
USHIRIKI WA MTOTO KITAIFA
LENGO VIASHIRIA VYA MATOKEO
Output Indicators SHUGHULI MUDA JUKUMU
Maendeleo
ya Mpango
wa Kitaifa
wa Ushiriki
wa Mtoto
Uwepo wa Mpango
wa Kitaifa wa
Ushiriki wa Mtoto
Mpango wa Kitaifa
wa Ushiriki wa
Mtoto uliochapishwa
katika Kiswahili na
Kiingereza
Rasimu ya Mpango wa
Kitaifa wa Ushiriki wa
Mtoto
Rasimu ya Mpango wa
Kitaifa wa Ushiriki wa
Mtoto uliothibitishwa na
Kamati ya pamoja ya
Baraza la Mawaziri ili
kuwasilishwa katika
Baraza la Mawaziri.
Rasimu ya Mpango wa
Kitaifa wa Ushiriki wa
Mtoto kuthibitishwa na
Baraza la Mawaziri.
Mpango wa Kitaifa wa
Ushiriki wa Mtoto wa
Kiswahili na Kiingereza
kuchapishwa.
Kuwasilisha Rasimu ya Mpango wa Kitaifa
wa Ushiriki wa Mtoto kwenye kamati ya
pamoja na Baraza la Mawaziri kwa ajili ya
kuthibitishwa.
Kutafsiri na kuchapisha matoleo ya Mpango
wa Kitaifa wa Ushiriki wa Mtoto.
Kuchapisha nakala za Kiingereza za Mpango
wa Kitaifa wa Ushiriki wa Mtoto ndani ya
miezi mitatu ya kuthibitishwa.
Kuchapisha nakala za Kiswahili za Mpango
wa Kitaifa wa Ushiriki wa Mtoto ndani ya
miezi mitatu baada ya kukamilika kwa
tafsiri.
Machi 2014
Mei 2014
Julai 2014
WMJJW
Maafisa wa
Serikali,
asasi za
Kiraia,
watoto na
Jamii
kuelewa na
kutekeleza
Maafisa wa Serikali,
asasi za Kiraia,
watoto na Jamii
wanatambua na
kuelewa pamoja na
kupendezewa na
Mpango wa Kitaifa
wa Ushiriki wa
Mpango wa Kitaifa wa
Ushiriki wa Mtoto
kusambazwa katika ngazi
zote
Shughuli za kukuza uelewa
kufanyika
Kusambaza Mpango wa Kitaifa wa Ushiriki
wa Mtoto katika ngazi zote
Kuinua uelewa juu ya yaliyomo kwenye
Mpango wa Kitaifa wa Kumshirikisha Mtoto
Kutengeneza ujumbe rahisi unaowasilisha
Novemba
2014
kuendelea
WMJJW
and
OWMTM
SM
pamoja na
wadau
36
Mpango wa
Kitaifa wa
Ushiriki wa
Mtoto.
Mtoto.
Maafisa wa Serikali,
asasi za Kiraia,
watoto na Jamii
kutumia Mpango wa
Kitaifa wa Ushiriki
wa Mtoto.
Mpango wa Kitaifa wa
Ushiriki wa Mtoto
kusambazwa katika
ujumbe uliorahisishwa
sehemu za Mpango wa Kitaifa wa Ushiriki
wa Mtoto kwa Kiswahili na Kiingereza kwa
kutumia vyombo vya habari na njia zingine
za mawasiliano.
Kushirikiana na watoto ili kuunda vipengele
rafiki vya mpango huo
Kanuni na
taratibu za
Sheria ya
Mtoto
zizingatie
haki ya
mtoto
kusikilizwa
na kushiriki
katika
masuala
yanayomuat
hiri katika
taasisi
mbalimbali.
Kuwapo kwa kanuni
na taratibu za sheria
ya mtoto
zinazoelekeza
utekelezaji wa
michango ya watoto
katika masuala ya
kisheria
yanayowahusu
watoto.
Michango iliyokusanywa
katika kutengeneza kanuni
na taratibu za sheria ya
mtoto.
Kanuni na taratibu za
sheria ya mtoto
zilizotengenezwa.
Usambazaji wa Kanuni na
taratibu za sheria ya mtoto.
Kuwa na mashauriano na kamati
za/mawaziri husika na Idara za serikali,
Mashirikia yasiyo ya kiserikali na wadau wa
maendeleo kujadili maeneo ya Sheria ya
Mtoto inayohitaji ufafanuzi wa mchango wa
mtoto na ushiriki wao katika masuala
yanayowahusu.
Kutengeneza kanuni na taratibu
zinazoongoza namna ya utekelezaji wa
ushiriki wa mtoto katika michakato
mbalimbali.
Kusambaza kanuni na taratibu za sheria ya
mtoto zinazoongoza namna ya utekelezaji wa
ushiriki wa mtoto katika michakato
mbalimbali.
Desemba
2014
WAUJ,
WSK
WMJJW,
OWTMS
M na
wadau
wengine.
Kushiriki katika Mipango ya Familia
Lengo Matokeo Output Shughuli Muda Jukumu
Kutangaza
na
kutambua
umuhimu
Watoto
wanashiriki
katika
maamuzi ya
Wazazi na walezi
kuhitaji mchango
na ushiriki wa
watoto katika
Kuinua uelewa wa haki za watoto wote kuchangia na
kushiriki katika maamuzi ya masuala yanayowahusu katika
ngazi ya familia kupitia programu za mafunzo ya jamii.
Julai 2014
na
kuendelea
WMJJW, Idara
yaUstawi wa
Jamii, Idara ya
Maendeleo ya
37
wa ushiriki
wa watoto
na
michango
yao katika
ngazi ya
familia.
kifamilia
katika masuala
yanayowahusu.
maisha ya familia.
Mafunzo ya mbinu
za stadi maisha
yanayohusisha
mawasiliano ya
mtoto, mzazi na
mlezi na uhusiano
kuboreshwa
Kuanza kwa
mitandao ya unasihi
wa Mzazi-mtoto
Utendaji mzuri wa
programu
zinazowapa wazazi
na walezi
kuwashirikisha
watoto katika
masuala muhimu ya
familia.
Kutumia programu za mafunzo ya jamii na vyombo vya
habari kuwahamasisha wazazi/walezi kushiriki katika
shughuli zingine ambazo watoto hushiriki mfano shuleni na
katika mabaraza ya watoto.
Watoto kutegemea watu wazima ili kuwaongoza,
kuwafunza na kuwalinda. Watoto Kufahamishwa kwamba
wanaweza kueleza hisia zao zilizo nzuri au mbaya katika
mazingira rafiki.
Kujumuisha mawazo ya watoto na uzoefu wao na
kuwashirikisha katika kuunda vitu vya kimalezi katika njia
chanya, uhusiano usio wa kihasama.
Kuwaandaa watoto kuwa washauri na wachangiaji katika
kampeni za kuuelewesha umma katika kutengeneza vifaa na
ujumbe mbalimbali kukuza uhusiano usio wa kihasama kati
ya watoto na wazazi na walezi.
Kuendesha mafunzo ya stadi za mawasiliano na mahusiano
ya mtoto na mzazi/ mlezi.
Kuanzisha mtandao wa unasihi wa mzazi-mtoto kwa
kushirikiana na Mashirika yasiyo ya Kiserikali yaliyo na
uzoefu katika eneo hili.
Kutumia programu za mafunzo ya umma na fursa za
vyombo vya habari kuzipa habari familia kuhusu mchango
unaopatikana kutokana na ushiriki wa watoto kwa kuonesha
faida zinazopatikana.
Jamii na asasi
za kiraia.
Ushiriki katika masuala ya Kijamii na Kidemokrasia
LENGO MATOKEO Output SHUGHULI MUDA JUKUMU
Kuunga Baraza la Baraza la Watoto la Kusajili Baraza la Watoto la Jamhuri ya Muungano wa Desemba WMJJW kwa
38
mkono
urasimishaji
wa Baraza la
Watoto la
Jamhuri ya
Muungano ya
Tanzania.
Watoto la
Jamhuri ya
Muungano
wa Tanzania
linafanya
kazi nchi
zima.
Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kusajiliwa na
kutambuliwa kisheria.
Katiba ya Baraza la
Watoto la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania
kufanyiwa marekebisho.
Kurekebishwa kwa
Mwongozo wa kitaifa wa
Baraza la Watoto la
Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Watoto wote kushiriki
katika ufanyaji kazi wa
Baraza la Watoto la
Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Tanzania na kutoa vyanzo madhubuti vya kufadhili mfumo
kifedha.
Kurekebisha upya, kuipitisha na kuhakikisha inafanya kazi
katiba ya Baraza la Watoto la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na kuingiza mambo mazuri na msingi kutoka
katika Mashirika yasiyo ya Kiserikali.
Kuboresha miongozo ya mwaka 2004, kuipitisha na
kutekeleza muongozo ulioboreshwa kwa kuzingatia mambo
mazuri kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali.
Kufanya chaguzi za kila mwaka za wawakilishi wa
mabaraza ya watoto katika ngazi zote.
Kuimarisha mabaraza yanayofanya kazi katika vijiji, miji,
wilaya na mikoani.
Kuwaelimisha watoto na jamii kuhusu Baraza la Watoto la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na majukumu yake.
Kuandaa mfumo wa mgawanyo wa vyanzo vya fedha kwa
mabaraza ya wilaya kutokana na taratibu za matumizi za
serikali za mitaa
Kuwafunza watoto namna ya kushiriki katika masuala
yanayowahusu katika ngazi zote na hasa katika mabaraza ya
watoto (kufanyika sambamba na kuimarisha mifumo na
chaguzi)
Kutengeneza form ya kitaifa ya mzazi kukubali mtoto
kushiriki katika shughuli za Baraza la Watoto la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
2014 na
kuendelea
kushirikiana
na wadau wa
maendeleo na
mashirika
yasiyo ya
kiserikali.
39
Maamuzi
katika jamii
na utawala
yanazingatia
mawazo na
maoni ya
watoto
Mabaraza ya
watoto
kufanya kazi
katika vijiji,
ngazi za
mitaa, wilaya
na mikoa.
Mawazo ya
watoto
kuingizwa
katika
mipango wa
maendeleo
na yana
shawishi
ufanyaji
maamuzi.
Mabaraza ya watoto
kuimarishwa katika vijiji
vyote, ngazi za mtaa,
wilaya na mikoa.
Chaguzi za wawakilishi
wa Baraza la Watoto la
Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kutoka vijiji
vyote, ngazi za mitaa,
wilaya, na mikoa
zinazofanyika mara kwa
mara.
Masuala yanayoibuliwa na
watoto kuingizwa katika
mipango ya serikali za
mitaa na michakato ya
mipango ya kitaifa ya
serikali.
Kuhusisha watoa mafunzo katika Nyanja ya ushiriki wa
watoto kutoa mafunzo kwa viongozi wa serikali za mitaa,
wafanyakazi wa maendeleo ya jamii, maofisa wa mashirika
ya kijamii na maofisa wa mashirika yasiyo ya kiserikali na
wadau.
Kuwapa mafunzo viongozi wa serikali za mitaa hasa
wafanyakazi wa maendeleo ya jamii, maofisa wa polisi,
maofisa wa mahakama na wengine watakaohusiana na
watoto, jinsi ya kushughulikia masuala yanayowahusu
watoto, namna ya kutumia mwongozo wa kitaifa wa
ushiriki wa watoto.
Kuwapa mafunzo wafanyakazi wa maendeleo ya jamii,
asasi za kiraia na wafanyakazi wa taasisi zisizo za kiserikali
kuhusu njia za kukuza ushiriki wa watoto katika masuala ya
kijamii na serikali za mitaa.
Kutetea masuala husika kwa kuyafanyia kazi kama sehemu
ya maswala ya kitaasisi.
Kutetea ushiriki wa watoto na vijana katika kuandaa na
kupita mipango ya bajeti na maendeleo ya serikali za mitaa
na manispaa pamoja na;
Mipango ya serikali za mitaa, sheria ndogondogo na
maamuzi mengine ya kisiasa na kiutawala yanayohusu
maisha ya watoto.
Kuishawishi Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa, kuwa na namna ya kuingiza mawazo ya watoto na
sauti zao katika utawala
Kuimarisha uratibu, usimamizi na utoaji taarifa na mrejesho
Desemba
2014 na
kuendelea
WMJJW,
Wizara ya
Serikali za
Mitaa na
OWMTMSM
ikisaidiwa na
mashirika
yasiyo ya
kiserikali na
wadau wa
maendeleo.
40
wa ushiriki wa watoto katika serikali za mitaa. Hii inaweza
kufanyika kwa kukubali mandalizi sambamba au maandalizi
ya baadaye ya maamuzi ya chini yanayotoa wigo mpana wa
ushiriki wa watoto kwa mfano katika toleo rafiki la
Vikwazo vya serikali na fursa za maendeleo. (i.e. watoto
wanashirikishwa katika mipango ya serikali za mitaa kupitia
fursa na changamoto za maendeleo).
Kuelekeza wafanyakazi wa maendeleo ya umma, taasisi za
kiraia, na maofisa wa mashirika yasiyo ya kiserikali kufuata
viwango vya kitaifa vya maadili katika kuwashirikisha
watoto.
Kutawanya na kuwapa mafunzo wadau kutumia kieleekezi
cha taifa ushiriki wa mtoto.
Maofisa wa
serikali za
mitaa
(maafisa
maendeleo ya
jamii na
ustawi wa
jamii, taasisi
za kirai na
wafanyakazi
wa mashirika
yasiyo ya
kiserikali
wanakuza
ushiriki wa
watoto katika
masuala ya
kijamii na
kiutawala
Maafisa
maendeleo
ya jamii,
ustawi wa
jamii na
taasisi za
kiraia,
maofisa wa
mashirika
yasiyo ya
kiserikali
wanashirikia
na na watoto
katika
masuala ya
kijamii na
kiutawala.
Maafisa maendeleo ya
jamii, ustawi wa jamii,
asasi za kiraia, na
watumishi wa mashirika
yasiyo ya kiserikali
kupewa mafunzo ya
kutetea na kukuza ushiriki
wa watoto katika jamii na
utawala.
Maafisa maendeleo ya
jamii, ustawi wa jamii,
asasi za kiraia na
wafanyakazi wa mashirika
yasiyo ya kiserikali
waliopewa semina elekezi
juu ya viwango vya kitaifa
vya ushirki wa mtoto na
maadili ya namna ya
Kutoa semina elekezi kwa wafanyakazi wa maendeleo ya
jamii, ustawi wa jamii, asasi za kiraia na wafanyakazi wa
mashirika yasiyo ya kiserikali juu ya viwango vya kitaifa
vya ushiriki wa mtoto na maadili ya namna ya kushiriki na
watoto katika jamii na masuala ya kiutawala. .
Desemba
2014
WMJJW,
WAUJ
ikishirikiana
na mashirika
yasiyo ya
kiserikali
wadau wa
maendeleo.
41
katika ngazi
mbalimbali.
kushughulika na watoto.
USHIRIKI MAZINGIRA YA SHULE:
Lengo Matokeo Output Shughuli Muda Jukumu
Kukuza
ushiriki wa
watoto na
haki ya
kusikilizwa
katika
mfumo wa
elimu na
utawala.
Watoto
wanachangia
katika
kuandaa na
kutekeleza
mipango ya
shughuli za
shule.
Mambo
yanayowahus
u watoto
kuingizwa
katika
maamuzi ya
uongozi wa
shule.
The National Costed
Tathmini ya
mchango wa watoto
na ushiriki wao
katika mambo ya
shule kufanyika.
Taratibu za uongozi
na utawala wa shule
kujumuisha
mawasilisho ya
watoto katika
utawala wa shule na
michakato ya
kufanya maamuzi.
Mabaraza ya shule
kuanzishwa kwenye
shule zote na vyuo
vya ufundi na wa
watoto
kuimarishwa.
Ushiriki, uratibu,
utoaji taarifa
kutengenezwa na
kuimarishwa
Walimu na
Kanuni na taratibu za Sheria ya Mtoto zielekeze michakato mbalimbali ya
ushirki wa mtoto izingatie mashauriano ya watoto waliopo shuleni kama
kundi na pia kuhakikisha kuwa kuna kumakinika katika mawazo ya mtoto
mmoja mmoja kuhusiana na maamuzi ya mtu mmoja juu ya elimu.
Michakato itatekelezwa kuhakikisha kwamba juhudi zipo katika kuangazia
masuala yanayoibuliwa na watoto kwa njia salama naya siri hasa katika
masuala ya vurugu na unyanyasaji shuleni.
Kutoa mamlaka kwa shirika la lisilo la kiserikali lenye uzoefu katika haki
za watoto na elimu kufanya tathmini ya ushiriki wa mtoto katika shule za
msingi na sekondari.
Kuwafunza wakaguzi wa shule jinsi ya kupitia tena taratibu za uongozi na
utawala wa shule ili zihusishe ushiriki wa watoto katika uongozi wa shule
na michakato ya maamuzi.
Kuandaa mtaalamu kuandaa kielekezi kinachoweza kutumika kuimarisha na
kurasimisha mabaraza ya shule katika shule zote na vyuo vya ufundi kitaifa.
Kuandaa miongozo ya utendaji wa mabaraza ya shule. Kuhakikisha kuwa
mabaraza ya elimu ya wilaya yanawajumuisha watoto katika ujumla wa
mipango ya shule-ikiungana na mpango ya maendeleo ya kijiji.
Kuongeza uungaji mkono kwa klabu za Tuseme, vyama mbalimbali
vilivyoko shuleni- kuhimiza klabu za vijana na kujihusisha na vikundi rika
vya kujitambua ili kuinua uelewa na kufanya eneo la shule kuwa mazingira
salama.
Kuhakikisha kwamba muunganiko kati ya watoto wasio mashuleni na
Machi
2015
OWMTMSM
na Wizara ya
Elimu na
Mafunzo ya
Ufundi
42
wafanyakazi
waliofunzwa njia za
kuwashirikisha
watoto.
vikundi vya watoto walio mashuleni na klabu umefanywa ili kuzaa matunda
mazuri.
Kuendeleza ushiriki tendwa wa mtoto, uratibu na utoaji taarifa baina ya
mabaraza ya watoto na uongozi wa shule.
Kuwafunza walimu na wafanyakazi wa shule katika njia na namna ya
kuwashirikisha watoto.
Ushriki katika mazingira ya Ulinzi wa Mtoto
Lengo Matokeo Output Shughuli Muda Jukumu
Mifumo yote
ya Ulinzi wa
Mtoto na
huduma za
Ulinzi wa
mtoto lazima
izingatie na
kutilia
maanani haki
ya mtoto ya
kusikilizwa na
kuheshimu
mawazo ya
mtoto.
Mpango
tendaji wa
kitaifa kwa
watoto walio
katika
mazingira
hatarishi
(2011-2015)
na kuibua
Mifumo ya ulinzi
mtoto kufanya kazi
katika ngazi zote.
Watoto, pamoja na
watoto walio katika
mazingira ya
hatarishi kuchangia
katika maamuzi ya
masuala
yanayohusu
usalama wao.
Serikali na maafisa wa
mashirika yasiyo ya kiserikali
kufunzwa kuunda timu za ulinzi
wa mtoto (kwa watoto
wanaoishi mitaani, watoto
wanaofanya kazi na watoto
walioambukizwa na wanaoishi
na virusi vya UKIMWI.
Shughuli mbalimbali za kujenga
uelewa zilizofanyika.
Mifumo ya kuripoti na kutoa
rufaa kwa watoto walio katika
hatari ya kunyanyaswa au
mazingira kufanyiwa ukatili au
waliofanyiwa ukatili.
Rasilimali za kutekeleza
mipango wa ulinzi wa mtoto
kutolewa.
Kanuni za Sheria ya mtoto iweke michakato ya
kuhakikisha kuwa sheria zote zinazomlinda
mtoto, mifumo ya ulinzi, huduma na programu za
ulinzi wa mtoto zinazingatia sauti za watoto na
maoni ya watoto katika kila jitihada za kumlinda
mtoto.
Maoni ya watoto lazima yazingatiwe na kutiliwa
maanani katika masuala yanayowahusu pamoja
na mapendekezo yao kwa ajili utatuzi madhubuti.
Maoni yao yasitumike tu kama taarifa za utafiti.
Kuhakikisha ushiriki wa mtoto ni suala la
kikanuni la kila mpango wa serikali kulinda na
kuchukua hatua kwa vitendo vya ukatili dhidi ya
watoto. Kuwapo kunamaanisha kuwa haki za
mtoto zinasikika na mapendekezo yao juu ya
utatuzi madhubuti yanaaksiwa katika viashiria
vinavyotumiwa na mpango kazi wa serikali.
Kuhakikisha kuwa haki za mtoto za kusikilizwa
zinakuwa miongoni mwa viwango vya chini vya
taratibu za programu za ulinzi wa mtoto.
Kutoa mamlaka na kufanya utafiti na watoto
Julai 2014
na kuendelea
WAUJ,
WMJJW
na wadau
43
programu za
kijamii za
kuwalinda
watoto
zinatunza haki
ya mtoto ya
kusikilizwa na
kukuza kwa
njia chanya
ushiriki wa
mtoto.
kuhusu njia wanazozipendekeza katika kuripoti
ukatili katika mazingira tofauti.
Kuhakikisha kuwa kuna taratibu kwa mtoto
kuripoti ukatili na unyanyasaji salama na kwa
ujasiri.
Kuwekeza katika kujenga mfumo wa siri wa
kutoa msaada, taarifa zinazojikita katika jamii na
misada ya kijamii. Kutoa njia za jinsi ya
kuwasiliana kwa hali ya juu kwenye mashule,
majengo ya kijamii na maizingira ya taasisi
mbalimbali.
Kuweka mfumo imara wa kuripoti katika mifumo
ya kitaasisi ili kwamba watoto wanaweza kutoa
taarifa kwa chombo kimoja wakati uonevu au
unyanyasaji unapojitokeza au pale mtoto
anapotishwa.
Kuhakikisha watoto wana uwezo wa kupata
utetezi huru na njia za kutoa malalamiko katika
miktadha mbalimbali.
Kufanya utafiti kubaini vizuizi vya watoto katika
kutafuta misaada kwa mfano ukosefu wa usiri au
kukosa mfumo mzuri wa kupata msaada kwa
makundi fulani ya watoto wakiwemo watoto
wenye ulemavu na waliokosa fursa (albino n.k)
Kutumia fedha iliyopo kusaidia kuunda na
kuimarisha uwezo wa vikundi rika vya vijana na
vikundi vinavyoongozwa na watoto na mashirikia
yanayojishughulisha na kukomesha vitendo vya
44
unyanyasaji kwa watoto ili viweze kufanya kazi
kufuatilia na kuripoti matendo mabaya katika
jamii yao.
Kufanya utafiti juu ya maoni ya watoto na uzoefu
wao katika matukio ya kikatili na mahusiano
chanya na mazingira na kuyahusisha katika
programu za mafunzo.
Kushirikisha watoto katika kuunda uhusiano
rafiki, usio wa kikatili wa vifaa vya kujifunza
kwa watumishi wanaojishughulisha na watoto.
Pale ambapo kuna timu za wilaya za kumlinda
mtoto, kuimarisha uratibu, usimamizi na kuwa na
namna ya kuwawezesha watoto kuripoti ili wawe
na taarifa na kujua ni wapi waende ili kupata
msaada katika jamii zao.
Kuhakikisha ushiriki wa mtoto katika kupanga,
kusimamia na kutathmini programu za ulinzi wa
kijamii kwa mtoto na kuhakikisha kuwa
muunganiko unakuwepo na vyombo vya kisheria
vyenye wajibu wa kuitika haraka katika masuala
ya watoto na ukiukwaji wa haki zao.
Kutambulisha mafunzo ya haki za mtoto yenye
moduli za ushiriki na ulinzi wa mtoto, katika
mafunzo ya kazi na kozi za vyuo vikuu kwa
wanafunzi wa ulinzi wa watoto, elimu iliyo wazi
na watu walio na wajibu wa kikazi karibu zaidi na
watoto (matibabu ya watoto, sheria etc).
Watoto na vijana watahusishwa katika kupanga,
45
kuunda, kutekeleza na kutathmini mipango
tendaji ya kitaifa inayohusiana na haki ya
kulindwa katika jamii. Lazima wawe wadau
wakuu katika utekelezaji wa mpango ili
utekelezaji uendane na watoto wenyewe.
Kukuza uelewa wa haki za watoto walio katika
mazingira magumu/hatarishi.
Kuanzisha na kuendeleza program endelevu za
kukuza na kuinua uelewa kwa wafanya maamuzi
juu ya faida na manufaa ya ushiriki watoto.
Kusisitiza ukweli kwamba masuala
yanayoawaathiri watoto ni mtambuka.
Maofisa wa serikali za mitaa (maofisa wa
maendeleo ya jamii na maafisa wa ustawi jamii),
maofisa wa vijiji, kata kufunzwa namna ya
kuinua ushiriki wa watoto katika kamati za
watoto wanaoishi katika mazingira magumu na
katika programu za ulinzi unaojikita katika jamii.
Kuboresha ushirkiano kati ya kamati za watoto
wanaoishi katika mazingira magumu na mifumo
ya serikali za mitaa na kuhakikisha kuna njia za
kuwashirikisha watoto.
Kuwafunza maofisa wa serikali na wa mashirika
yasiyo ya kiserikali kuanzisha klabu za ulinzi wa
mtoto na kamati (kwa ajili ya watoto wanaoishi
mitaani, wanaofanya kazi na wale
walioambukizwa na wanaosishi na virusi vyaa
UKIMWI).
46
Kuimarisha njia ya utoaji taarifa wa watoto
wanaokumbana na vitendo vya kikatili na hali za
unyanyasaji katika jamii zao.
Kutoa rasilimali za kutekeleza mfumo Awa ulinzi
kwa mtoto.
Watoto
waliokinzana
na sheria
kushiriki na
kuchangia
maamuzi juu
ya michakato
ya kisheria ya
mambo
yanayowahus
u.
Haki za
kisheria za
watoto
kusikilizwa na
kutiliwa
maanani
katika
masuala ya
kimahakama.
Utaratibu wa
kisheria kuhusu
watoto kushirikisha
watoto husika
katika michakato
yote.
Wanasheria
wanaotoa huduma
za kisheria kwa
watoto bure
wnatumia ujuzi na
maadili ya ushiriki
wa mtoto wakati
wakiwawakilisha
watoto.
Muongozo wa kushiriki watoto
waliokinzana na sheria
kutengenezwa.
Watoto kupata taarifa kuhusu
haki zao za kisheria na haki ya
kushirikishwa katika maamuzi
na katika michakato ya kisheria
inayowahusu.
Watoto waliokinzana na sheria
wapate huduma za kisheria
bure.
Kanuni za Sheria ya mtoto zihakikishe watoto
watoto wanaweza kushiriki katika michakato ya
kisheria ili waweze kuelezea maoni na mawazo
yao kwa uwazi kwenye mambo yanayowahusu
mfano kutengena kwa wazazi, kuasiliwa, na pale
ambapo mtoto ni shahidi katika masuala ya kesi
za jinai.
Kuwataka wote wanafanya kazi na watoto
waliokinzana na sheria wnato uzito unaostahiki
kwa mawazo ya watoto kwa kungalia umri na
uwezo wao wa kufikiri. .
Maboresho ya mfumo wa sheria za
zinazozungumzia watoto waliokinzana na sheria
yahakikishe mahitaji na matakwa ya watoto
yanazingatiwa na kuna mtazamo chanya wa
jamii.
Kutoa taarifa rahisi kwa watoto kuhusu haki zao
kisheria na haki yao ya kushiriki katika maamuzi
ya mambo ya kisheria yanayowahusu.
Kuhakikisha kuwa watoto wanapata fursa ya bure
ambayo ni huru kwenye ushauri wa kisheria na
juu ya uwakilishi katika zoezi la kulinda haki zao.
Kama sehemu ya wigo mpana wa mafunzo ya
ulinzi wa mtoto, kuwajengea uwezo wanasheria
Mei, 2015 WMN,
WKS,
WMJJW
na wadau
47
wanaowapa watoto huduma za kisheria bila
malipo wawe na ujuzi na maadili stahiki katika
kushirikisha watoto.
Kusambaza nakala viwango vya kitaifa vya
ushiriki na mwongozo wa maadili ya kitaifa
katika ushiriki wa mtoto kwa watekelezaji wa
sheria, maafisa wa mahakama, wanasheria na
maofisa wa ustawi wa jamii.
Kuandaa miongozo ya namna ya kuhusisha na
watoto waliokinzana na sheria katika maamuzi ya
michakato ya kisheria yanayowahusu katika ngazi
zote.
Kutoa taarifa nyepesi na rahisi kwa watoto juu ya
haki zao kisheria na haki ya kusihiriki katika
maamuzi ya kisheria ya mambo yanayowahusu.
Kutoa msada wa kisheria bure.
Watekelezaji
wa sheria
(Polisi,
Maofisa wa
mahakama, na
waendesha
mashtaka wa
umma) na
watumishi wa
umma kukuza
ushiriki wa
watoto katika
mfumo wa
sheria.
Watekelezaji wa
sheria (Polisi,
Maofisa wa
mahakama, na
waendesha
mashtaka wa
umma) na
watumishi wa
umma kuhusika
vyema katika
kuwashirikisha
watoto katika
mambo ya kisheria.
Watekelezaji wa sheria (Polisi,
Maofisa wa mahakama, na
waendesha mashtaka wa umma)
na watumishi wa umma
waliofunzwa njia za
kuwashirikisha watoto katika
mfumo wa sheria.
Wanasheria wanaotoa msaada
wa kisheria bure kwa watoto
waliopewa mafunzo, ujuzi na
maadili katika kuwashirikisha
watoto katika mambo ya
kisheria.
Kuwapa mafunzo watekelezaji wa sheria (Polisi,
Maofisa wa mahakama, na waendesha mashtaka
wa umma) na watumishi wa umma njia za
kuwashirikisha watoto katika masuala ya
kisheria.
Kuwawezesha wanasheria wanaotoa msaada wa
kisheria bure kwa watoto kupata weledi na
maadili ya mchango wa watoto na ushiriki wao
katika masuala ya kisheria.
Kutoa nakala za viwango vya kitaifa na maadili
ya kitendaji katika ushiriki wa mtoto
kwawatekelezaji wa sheria, maofisa wa
Oktoba,
2015 na
kuendelea
WSMK,
WMJJW
kwa
ushirikiano
kutoka
kwa
wadau
48
Wanasheria
wanaowapa watoto
huduma bure za
kisheria kutumia
weledi na maadili
wakati wa
kuwawakilisha
watoto.
Watekelezaji wa sheria, maofisa
wa mahakama na maofisa wa
watumishi wa umma
wanaojihusisha na watoto
kupewa nakala za viwango vya
kitaifa na maadili ya utendaji
katika kuwashirikisha watoto.
mahakama, wanasheria, na maofisa wa ustawi wa
jamii na maofisa huduma za umma wanajihusisha
na watoto katika utekelezaji wa masuala ya
kisheria.
Ushiriki wa Mtoto katika vyombo vya habari
Lengo Matokeo Output Shughuli Muda Jukumu
Watoto wana fursa
ya kutumia
vyombo vya habari
(redio, matangazo
na TV) kuchangia
na kushiriki katika
midahalo
mbalimbali.
Watoto
wanahusishwa
katika shughuli za
vyombo vya habari
zinazokuza ushiriki
wa watoto katika
masuala
yanayowahusu.
Maofisa wa vyombo
vya habari
wanafanya kazi kwa
kushirikiana na
watoto katika
vyombo vya habari.
Maofisa wa vyombo
vya habari
waliofunzwa juu ya
njia za kimaadili za
kuwashirikisha
watoto katika
vyombo vya habari.
Rasilimali fedha
zimetengwa katika
kuwashirikisha
watoto katika
vyombo vya habari.
Kujenga uwezo wa
mitandao ya vyombo
vya habari na
kuwashirikisha
watoto katika
vyombo vya habari.
Kushawishi Wizara ya Habari Michezo na Utamaduni
kuingiza masuala ya watoto katika vyombo vya habari
hasa katika masuala yanayowaathiri katika vyombo
vya habari.
Kuwapa mafunzo maofisa wa vyombo vya habari njia
za kimaadili za kuwashirikisha watoto katika vyombo
vya habari.
Kuweka rasilimali fedha katika ushiriki wa watoto
kwenye vyombo vya habari-kuinua misaada ya
vyombo vya habari katika mitandao ya kuripoti
masuala ya watoto.
Kupanua wigo wa kitaifa wa Gazeti la agenda ya
watoto.
Kufanya kazi na vyombo vya habari kutoa habari,
elimu na mawasiliano kwa umma juu ya masuala ya
watoto hasa masuala yanayohusiana na ukiukwaji
mkubwa wa haki za watoto (kama ukatili na
unyanyasaji).
Mei 2015
kuendelea
WMJJW na
WKMVM
kwa msaada
wa wadau
wenza wa
agenda ya
mtoto
49
Kutumia rasilimali fedha katika ushiriki wa mtoto
kwnye vyombo vya habari.
Kampeni za
vyombo vya habari
kuujulisha umma
juu ya umuhimu
wa michango ya
watoto na ushiriki
wao katika
masuala
yanayowahusu.
Jamii na wadau
wengine kujua
umuhimu wa
ushiriki wa mtoto na
nafasi ya mtoto
katika jamii.
Maofisa wa vyombo
vya habari
waliofunzwa juu ya
kutetea ushiriki wa
mtoto katika vyombo
vya habari katika
ngazi zote.
Kuwafunza maofisa wa vyombo vya habari juu ya
kutetea ushiriki wa mtoto katika vyombo vya habari
katika ngazi zote.
Mei,
2015
WMJJW na
WKMVM
kwa msaada
wa wadau
wenza wa
agenda ya
mtoto
6.0 URATIBU, UFUATILIAJI NA TATHMINI YA UTEKELEZAJI
6.1 Utangulizi
Mkakati wa ufuatiliaji na tathmini umetayarishwa ili kufanikisha utekelezaji wa Mpango
Kazi huu kufikia malengo yake. Ufuatiliaji na tathmini ni nyenzo muhimu katika kuweka
utaratibu au mfumo wa kujenga msingi wa kutambua ufanisi katika utekelezaji wa
masuala ya ushiriki wa watoto. Isitoshe, unalenga katika kupata taarifa ya utendaji na
ufanisi ambazo zitatumika katika kufanya maamuzi muhimu yatakayofanikisha malengo
yaliyokusudiwa.
6.2 Lengo la Ufuatiliaji na Tathmini
Umuhimu wa kuwa na mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ni kutoa mwongozo wa
utekelezaji wa Mpango kazi huu kuanzia hatua za awali ya utekelezaji wa Mpango huu ili
kutekeleza hatua mbalimbali kwa ufanisi.
6.3 Malengo mahsusi
i) Kuwa na vigezo vya viashiria vya upimaji wa utekelezaji wa Mpango Kazi
huu
ii) Kuweka shabaha na viwango vya utekelezaji wa Mpango Kazi
iii) Kutoa mwongozo kwa wadau katika kushiriki kwenye utekelezaji na
ufuatiliaji wa shughuli
iv) Kutoa mwongozo kwa mgawanyo wa raslimali katika kipindi cha utekelezaji
6.4 Uratibu
i) Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kupitia Idara ya
Maendeleo ya watoto itaratibu masuala yote yanayohusu Mpango kazi huu
katika ngazi ya taifa. Sekretarieti ya Mkoa itakuwa na jukumu la kuratibu
ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Mpango Kazi huu katika ngazi ya
mkoa. Mamlaka ya serikali za Mitaa zitakuwa na jukumu la uratibu wa
ufuatiliaji na tathmini kuanzia ngazi ya kijiji hadi wilaya. Wadau wengine
watakuwa ni Washiriki wa Maendeleo, Asasi za Kiraia, Sekta binafsi, Taasisi
za Elimu, Taasisi za Sheria, Taasisi za Siasa, hawa watashiriki katika jukumu
la kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Mpango Kazi huu katika maeneo
yao.
ii) Wizara inayohusika na Elimu na Mafunzo ya Ufundi itahakikisha kuwa
inatoa na kusimamia mitaala ya elimu itakayoendana na sera ya watoto hasa
katika suala la haki ya watoto ya ushiriki katika kufanya maamuzi muhimu,
utungaji wa sera na mikakati ya utekelezaji, mipango ya sekta hii, ukuzaji wa
mitaala rafiki, nk.
iii) Wizara inayohusiana na Sheria itahakikisha shughuli zote za marekebisho
ya kanuni na taratibu za kisheria zinazohusu watoto zinafanyiwa kazi ili
kuleta maboresho na kujenga mazingira rafiki ya kisheria kwa watoto.
iv) Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii itahakikisha kuwa wadau wote
wanafahamu maboresho ya kanuni na taratibu za kisheria na kutii mabadiliko
hayo ili kujenga mazingira rafiki na mahusiano mazuri na watoto katika ngazi
zote
51
6.5 Mchakato wa Ufuatiliaji na tathmini ya Utekelezaji
6.5.1 Ufuatiliaji wa mchakato
Utekelezaji wa Mpango Kazi huu utakuwa wa miaka mitano 2014-2019 na utaenda
sambamba na utekelezaji wa MKUKUTA II kati ya 2014 na 2015. Ukiwa ndio nyenzo ya
kwanza ya Kitaifa ya utekelezaji wa Ushiriki wa Watoto, Mpango huu utafanikisha
upimaji wa utekelezaji wa ushiriki huo pamoja na kuweka viashiria ya ufanisi pamoja na
ratiba ya utekelezaji ikiwa na malengo mahsusi na matarajio ya mchakato mzima wa
tathmini.
Nyenzo kadhaa za upimaji zinaweza kuandaliwa mapema na kuanza kutumika. Nyenzo
hizo inatakiwa kuwa rahisi na rafiki kwa wadau wote ili waweze kunufaika nazo (ona
mfano katika kiambatanisho Na. 11)
Maelezo ya
Mradi kwa
ufupi
Malengo Viashiria vya Awali Tahadhari na Matarajio
Kwa vile muda wa kufanya tathmini utakuwa baada ya miaka mitano tangu mpango huu
kuanza kutekelezwa, inapendekezwa kuwa kuwe na tathmini ya katikati ya muda wa
utekelezaji itakayoanza mwaka wa tatu wa utekelezaji. Tathmini hizo zitumie nyenzo
mbali mbali za kutathmini ambazo zinatumika kungineko kama vile kwa kuanza na zoezi
la uimara, mapungufu, fursa na vikwazo “SWOT” ili kurahisisha utoaji wa taarifa kwa
watendaji ambao wana wajibu wa mwisho wa kushughulikia matokeo ya tathmini.
Nyenzo nyingine saidizi ni ile ya Mti wa Matatizo (Problems Tree) kwa uchambuzi wa
matatizo na Mti wa Malengo (Objectives Tree) kwa kuonyesha maendeleo ya utekelezaji
na usimamizi. Matumizi ya nyenzo hizi pia yataambatana na ripoti ambayo itaonyesha
hali halisi na ushahidi kutoka maeneo ya utekelezaji na kwa wadau kwa msisitizo wa
kukusanya pia ushahidi wa watoto ambao ndio walengwa wa Mpango huu.
Katika kila tathmini inayofanyika, walengwa watakuwa ni wadau wote ikiwa ni pamoja
na watoto ambao watatakiwa kushiriki katika mchakato mzima. Watoto na vijana
wanatakiwa kuwa walengwa na pia kuwa washiriki wakuu katika kutathmini na
ufuatiliaji wa mchakato mzima kwa mfano kuwa watafiti katika tafiti zitakazofanywa
kama sehemu ya Mpango Kazi huu.
6.5.2 Ratiba ya Utekelezaji na Matukio ya Ziada
Ratiba hii inatoa maelezo ya kina kuhusu maandalizi ya utekelezaji na matukio katika
hatua yauandaaji na utekelezaji wa Mpango Kazi huu wa Ushiriki wa Watoto kwa
kuonyesha viwango vya Kitaifa na majukumu ya Kamishna wa Haki za Watoto/ Chombo
Maalum cha kuchunguza Malalamiko ya Watoto ambacho baadhi ya majukumu yake
yatakuwa kusimamia maendeleo ya hatua za utekelezaji za Mpango Kazi huu. Maelezo
zaidi kuhusu utekelezaji yanaonekana katika Mpango wa Utekelezaji, Jedwali Na. 1.
Utekelezaji na shughuli za kuandaa Mpango Kazi
wa Ushiriki wa Watoto
Viwango vya Kitaifa na mfumo wa kanuni
na taratibu
Kamishna wa Haki za watoto au
Chombo Maalum cha Kuchunguza
Malalamiko ya Watoto
Januari 2014
Kuwasilisha rasimu ya Mpango Kazi kwa Wizara ya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto (WMJW)
Warsha ya wadau kuhakiki na kukubali Mpango Kazi
huu itakayoandaliwa na WMJW
Mei 2014
Rasimu ya Mpango Kazi huu kupitishwa na Baraza
la Mawaziri
Mpango Kazi kukubalika kama Mpango wa Kitaifa
wa Ushiriki wa Watoto
Mei 2014
Kuunda chombo ambacho kitaandaa na
kusimamia Viwango vya kitaifa na mfumo wa
kanuni na taratibu ushiriki watoto
Kuagiza utafiti wa haraka kuangalia mifano ya
viwango vya kitaifa vilivyopo na mfumo wa
kanuni na taratibu
(kwa kushirikiana na Asasi Zisizo za
Kiserikali, UNICEF, nk)
Mei 2014
Kusambaza matokeo ya utafiti huo kwa wadau
wote
Kuanza kutengeneza Viwango vya Kitaifa
kuhusu Ushiriki wa Watoto
Juni 2014
Kukamilisha uandaaji wa Viwango vya Kitaifa
na kuanza kuandaa mfumo wa kanuni na
taratibu
Julai 2014
Kuanza zoezi la Ushiriki wa Watoto na uchangiaji
wao katika ngazi ya familia
Julai 2014
Kuagiza utafiti kuhusu namna ya kuanzisha
ofisi ya Kamishna wa Haki za Watoto/
Chombo Maalum cha Kuchunguza
Malalamiko ya watoto
Septembar 2014
Kukamilisha rasimu ya mfumo wa kanuni na
54
taratibu
Kuwasilisha rasimu kwa wanasheria wa serikali
kuhakikisha ufanisi/ukamilifu
Kutafsiri rasimu kwenye lugha ya Kiswahili
Kuanza kuandaa mabango na vipeperushi kwa
ajili ya shule, sehemu za huduma za watoto na
majengo ya serikali na jamii
Oktoba 2014
Kuanza kusambaza taarifa husika kwa viongozi na
watendaji wa serikali, vyama vya kiraia, watoto na
jamii ili kuelimisha kuhusu utekelezaji wa Mpango
Kazi huu wa Kitaifa wa Ushiriki wa Watoto
Oktoba 2014
Kuwa na machapisho ya Mpango Kazi huu kwa
lugha zote mbili za Kiswahili na Kiingereza
Kuweka tarehe ya Uzinduzi rasmi wa Viwango
vya kitaifa na mfumo wa kanuni na taratibu
Oktoba 2014
Kuunda Kamati au Jukwaa linalohusisha
watoto kwa ajili ya kuandaa ofisi ya
kamishna/Ombudsman (kuhusu maamuzi ya
jina la/wadhifa wa ofisi na majukumu yake
kulingana na matokeo ya utafiti yakinifu)
Desemba 2014
Majadiliano na wizara na idara za serikali , Asasi
Zisizo za Kiserikali na wadau wa maendeleo kujadili
sehemu za Sheria ya Mtoto na kushughulikia
maeneo ya kanuni na taratibu
Kurasmisha Baraza la watoto la Serikali ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania
Maafisa wa Serikali za Mitaa na watendaji wa Asasi
Zisizo za Kiserikali kuanza rasmi utekelezaji wa
Ushiriki wa Watoto katika ngazi ya jamii na utawala
Kuanza rasmi Ushiriki wa watoto katika mfumo wa
elimu na utawala
Desemba 2014
Kutangaza nafasi za kazi kwa ajili ya ofisi
ya Kamishna wa Haki za Watoto/ Chombo
Maalum cha Kuchunguza Malalamiko ya
Watoto
Kuandaa/kutenga nafasi ya ofisi hii katika
jingo la serikali, kuunda kamati ya kuandaa
hadidu za rejea kwa wafanyikazi wa ofisi
hii na mahitaji yao kulingana na matokeo ya
utafiti wa awali.
Januari 2015
Uteuzi wa Kamishna/ Chombo Maalum cha
Kuchunguza Malalamiko ya watoto
Machi 2015
Kamishna/ Chombo Maalum cha
Kuchunguza Malalamiko ya Watoto
kuanza kazi
Mei 2015
Miongozo ya ushiriki wa Watoto katika maswala ya
55
sheria kuzinduliwa
Watoto kuanza kupata taarifa kuhusu haki zao za
kisheria, Haki ya kushiriki kwenye kufanya maamuzi
kuhusu taratibu za kisheria zinazohusu watoto na
haki ya kupata utetezi na huduma za kisheria
bure/bila gharama zozote
Kujenga/kuwepo kwa Uwezo wa watoto kutumia
vyombo vya habari na kampeni za wafanyakazi
kuhusu mchango na faida ya ushiriki wa watoto
katika vyombo vya habari
Oktoba 2015
Wasimamizi wa sheria na watendaji wa ustawi wa
jamii kuanza rasmi kuwajibishwa kusimamia swala
la Ushiriki wa Watoto katika ngazi zote pasipo
kuvunja sheria
7.0 REJEA
Alderson, Priscilla (1990) Choosing for Children: Parents’ Consent to Surgery, Oxford:
OxfordUniversity Press.
Alderson, Priscilla (1992) Consent to Health Treatment and Research: Differing
Perspectives (SSRU consent conference series), London: University of London Institute
of Education.
van Beers, Henk, Vo Phi Chau, Judith Ennew, Pham Quoc Khan, Tran Thap Long, Brian
Milne, TrieuThiAnhNguyet and Vu Thi Son (2006) Creating an enabling environment:
Capacity building in children’s participation, Viet Nam, 2000-2004, Bangkok: Save the
Children Sweden.
van Beers, Henk, AntonellaInvernizzi and Brian Milne (eds.) (2006) Beyond Article 12.
Essential Readings in Children’s Participation. Bangkok: Black on White Publications.
British Sociological Association (2006) Statement of Ethical Practice, Durham: British
Sociological Association.
Committee on the Rights of the Child (2000) Initial Reports of States Parties due in 1993
(Addendum), United Republic of Tanzania, CRC/C/8/Add.14/Rev.1, Geneva: UN.
Committee on the Rights of the Child (2001) Consideration of Reports of States Parties,
Initial report of the UnitedRepublic of Tanzania, CRC/C/SR.713. (Summary Record),
Geneva: UN.
Committee on the Rights of the Child (2001) Consideration of Reports of States Parties,
Initial report of the UnitedRepublic of Tanzania, CRC/C/SR.714. (Summary Record),
Geneva: UN.
Committee on the Rights of the Child (2001) Adoption of the Committee’s Report on its
Twenty-Seventh Session, CRC/C/SR.721. (Summary Record), Geneva: UN.
Committee on the Rights of the Child (2003), CRC General Comment No 5. General
measures of implementation of the Convention on the Rights of the Child,
CRC/GC/2003/5. Geneva: UN.
Committee on the Rights of the Child (2005) Second periodic reports of States parties
due in 2004,UnitedRepublic of Tanzania, CRC/C/70/Add.26, Geneva: UN.
Committee on the Rights of the Child (2005), General Comment No 7,Implementing
child rights in early childhood, CRC/C/GC/7/Rev.1, Geneva: UN.
Committee on the Rights of the Child (2006) Consideration of Reports Submitted by
States Parties under Article 44 of the Convention: Concluding observations: United
Republic of Tanzania, CRC/C/TZA/CO/2, Geneva: UN.
Committee on the Rights of the Child (2007) General Comment No 10, Children’s rights
in juvenile justice, CRC/C/GC/10, Geneva: UN.
57
Committee on the Rights of the Child (2009)General Comment No 12,The right of the
child to be heard, CRC/C/GC/12, 2009, Geneva: UN.
Ennew, Judith (1997) Monitoring Children’s Rights: Indicators for Children’s Rights
Project, Oslo: Childwatch International.
Gallagher, M. (2006) „Spaces of participation and inclusion?‟ in Tisdall, E.K.M.,Davis,
J.M., Hill, M. and Prout, A. (eds) Children, Young People and Social Inclusion, Bristol:
Policy Press.
Hart, R. A. (1992). Children’s Participation: from tokenism to citizenship, Florence:
UNICEF International Child Development Centre.
Inter-Agency Working Group on Children‟s Participation (IAWGCP) (2007) Minimum
Standards for Consulting with Children, Bangkok: IAWGCP.
Inter-Agency Working Group on Children‟s Participation (2008) Children as Active
Citizens: A Policy and Programme Guide, Bangkok: IAWGCP.
International Labour Organisation (ILO) (1973) Convention concerning Minimum Age
for Admission to Employment (Minimum Age Convention, No. 138), Geneva: ILO.
International Labour Organisation (ILO) (1999) Worst Forms of Child Labour
Convention, (No. 182), Geneva: ILO.
International Save the Children Alliance (ISCA) (2005) Practice Standards in Children’s
Participation, London: ISCA.
James, A and A. Prout (eds) (1997) Constructing and Reconstructing Childhood:
Contemporary Issues in the Sociological Study of Childhood, Cambridge: Polity Press.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA (BILA TAREHE) WIZARA YA
MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: MKAKATI WA UTEKELEZAJI
WA SERA YA MALEZI, MAKUZI NA MAENDELEO YA MTOTO KWA KIPINDI
CHA 2013-2018
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA: WIZARA YA MAENDELEO YA
JAMII, JINSIA NA WATOTO (2013): SERA YA MALEZI, MAKUZI NA
MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO TANZANIA
Lansdown, G. (2001) Children’s Participation in Democratic Decision-Making,
Florence: UNICEF.
Liebel, M. (2004) A Will of their Own: Cross-cultural Perspectives on Working Children,
London and New York: Zed Books.
Lovan, W.R., Murray, M., and Shaffer, R. (2004) „Participatory Governance in a
Changing World‟, in Lovan, W.R., Murray, M., Shaffer, R. (eds) Participatory
58
Governance: Planning, Conflict Mediation and Public Decision-Making in Civil Society,
Aldershot: Ashgate.
O‟Donnell, Daniel (2009), The right of children to be heard: Children’s right to have
their views taken into account and to participate in legal and administrative proceedings,
Innocenti Working PaperNo. 2009-04, Florence: UNICEF Innocenti Research Centre.
Organisation of African Unity (OAU) (1999) African Charter on the Rights and Welfare
of the Child, Addis Ababa: OAU.
Save the Children Norway (2008)Global Report on children’s participation in armed
conflict, post conflict and peace building, Oslo: Save the Children Norway.
Shier, Harry (2001) „Pathways to Participation: Opportunities and Obligations‟ in Young
People and Society, Vol. 15, Chichester:Wiley:107-17.
Snipstad, Mai Bente, Gro Therese Lie and DagfinnWinje (2010) ‚ „Child Rights or
Wrongs: Dilemmas in Implementing Support for Children in the Kilimanjaro Region,
Tanzania, in the Era of Globalized AIDS Approaches, in TatjanaThelen and
HaldisHaukanes (eds) Parenting After the Century of the Child: Travelling Ideals,
Institutional Negotiations and Individual Responses, Aldershot: Ashgate.
Treseder, Phil (1997) Empowering children and young people training manual:
promoting involvement in decision making, London: Save the Children.
UNICEF (2010) Violence against Children in Tanzania: Preliminary Findings from a
National Survey, Center for Disease Control and Prevention/ UNICEF.
UNICEF Evaluation Office (2002) Children Participating in Research, Monitoring And
Evaluation (M&E) - Ethics and Your Responsibilities as a Manager, Evaluation
Technical Notes No. 1, New York: UNICEF.
United Nations (UN) (1948) Universal Declaration of Human Rights, New York: UN.
United Nations (1989) Convention on the Rights of the Child, New York: UN.
United Nations Office on Drugs and Crime (2009) Justice in Matters involving Child
Victims and Witnesses of Crime: Model Law and Related Commentary, Vienna: United
Nations Office on Drugs and Crime.
United Republic of Tanzania (1998) Constitution of the United Republic of Tanzania, Dar
es Salaam: The United Republic of Tanzania.
United Republic of Tanzania (2005) The National Strategy for Growth and Reduction of
Poverty - NSGR), Dar es Salaam: Vice President‟s Office.
United Republic of Tanzania (2009) The Law of the Child Act, 2009, Dar es Salaam: The
United Republic of Tanzania.
59
United Republic of Tanzania (2010) National Strategy for Growth and Reduction of
Poverty II - NSGRP II, Dar es Salaam: Ministry of Finance and Economic Affairs.
Wessells, Mike (2009i) What Are We Learning About Protecting Children in the
Community? An inter-agency review of the evidence on community-based child
protection mechanisms in humanitarian and development settings, London: Save the
Children UK.
Wessells, Mike (2009ii) What Are We Learning About Protecting Children in the
Community? An inter-agency review of the evidence on community-based child
protection mechanisms (executive Summary), London: Save the Children UK.
Willow, Carolyne (2010) Children’s right to be heard and effective child protection. A
guide for Governments and children rights advocates on involving children and young
people in ending all forms of violence, Bangkok: Save the Children Sweden.
Wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto (2013): Mpango Kazi Shirikishi wa
Kudhibiti Tatizo la Watoto waishio/kufanya Kazi Mitaani