mpango kazi wa ushiriki wa mtoto tanzania - cdftz

59
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA 2014 - 2019 JANUARI, 2014

Upload: phamdang

Post on 02-Feb-2017

415 views

Category:

Documents


3 download

TRANSCRIPT

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA

WATOTO

MPANGO KAZI WA USHIRIKI WA MTOTO TANZANIA

2014 - 2019

JANUARI, 2014

ii

Dibaji

Kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Taifa ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012,

idadi ya watoto Tanzania Bara wenye umri chini ya miaka 18 ilikuwa ni 21,866,258,

ambao ni sawa na asilimia 50.1 ya idadi ya watu wote. Kati yao wasichana walikuwa

10,943,846 na wavulana walikuwa 10,922,412. Idadi ya watoto chini ya umri wa miaka

minane walikuwa 11,181,278 sawa na asilimia 51.1 ya watoto wote. Pamoja na kuwepo

kwa idadi hii kubwa ya watoto wa Tanzania ni kundi kubwa la jamii ambalo linakutana

na changamoto nyingi kimaisha. Pamoja na wingi wa kundi hili, haki zao nyingi

zinavunjwa na kwa muda mrefu walikuwa hawana chombo maalum cha kuwatetea na

sauti zao zilikuwa hazisikiki vya kutosha kwa kuwa walikuwa hawashiriki katika kufanya

maamuzi yanayohusu maisha yao licha ya uwepo wa sera na sheria mbalimbali za

kuwalinda. Athari kubwa wanayoipata watoto hao ni kukosa haki zao za msingi kama

zilivyoainishwa katika Sera ya Maendeleo ya Mtoto ya mwaka 2008, Sheria ya Mtoto ya

Mwaka 2009, Mikataba mbalimbali ya Kimataifa na ya Kikanda kuhusu haki za mtoto na

hivyo kuathiri ukuaji na ustawi wao na maisha yao kwa ujumla na hata maendeleo ya

nchi yetu.

Pamoja na juhudi za serikali kuandaa sera, sheria na mipango mbalimbali ya kumjali

mtoto, kumekuwepo na changamoto mbalimbali zinazokwamisha utekelezaji wa

programu za kumuendeleza na kumjenga mtoto na kulinda haki zake. Changamoto hizo

ni pamoja na ukosefu wa rasilimali fedha, ushiriki mdogo wa jamii katika kutatua tatizo

la uvunjaji wa haki za watoto, na uelewa mdogo wa jamii kuhusu haki za watoto. Kwa

hali hiyo, umuhimu wa suala la ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi yanayohusu

maisha yao umekuwa ni kitu cha kupewa kipaumbele ili sauti zao zisikike na mchango

wao uonekane katika kutetea haki zao.

Kwa hali ilivyo sasa, ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi ya masuala yanayohusu

maisha yao ni suala linalotiliwa mkazo sana nchini Tanzania hasa baada ya kuridhia

Mkataba wa Haki za Mtoto mwaka 1991. Baada ya hapo serikali iliona umuhimu wa

ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi mbalimbali kwa utaratibu rasmi na wenye

muendelezo mzuri hasa baada ya tukio la ushiriki wa watoto katika Kikao Maalum kwa

watoto kilichoandaliwa na Umoja wa Mataifa cha mwaka 2002 na hivyo kupendekeza

uwepo wa chombo mahsusi cha Kitaifa cha uwakilishi wa kudumu wa watoto yaani

Baraza la Taifa la Watoto chini ya usimamizi wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia

na Watoto.

Juhudi nyingine za kuwahusisha watoto katika ushiriki ni pamoja na mabaraza ya watoto

mashuleni, na vilabu cha watoto mashuleni na katika jamii au juhudi ambazo zinalenga

kwenye kuwahusisha watoto katika masuala mbalimbali yanayowahusu (kama vile

Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI wenyewe, malezi na matunzo

kisaikolojia na kijamii nk). Kati ya mwaka 2009 na mwaka 2010, Wizara ya Maendeleo

ya Jamii, Jinsia na Watoto ilitengeneza Kielekezi cha Taifa cha Ushiriki wa Mtoto

iii

ambacho kinaelekeza namna ya kufanikishaa ushiriki wa watoto na wanajamii katika

kujadili pamoja masuaala ya watoto. Hii ni nyenzo ya kuwawezesha watoto pamoja na

wanajamii kutambua na kujadili masuala muhimu yanayogusa maisha ya watoto katika

jamii na mazingira husika. Juhudi zote hizi za serikali pamoja na nyinginezo kama vile

kuridhia Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto mwaka 2003 na kupitishwa

kwa Sheria ya Mtoto ya Novemba 2009 pamoja na sera ya Mtoto ya mwaka 2008

zinaonyesha ari na utayari wa serikali wa kukuza haki ya ushiriki wa watoto. Wakati sera

ya Mtoto inazingatia uhuhimu wa ushiriki wa mtoto katika shughuli za maendeleo, na

maswala yanayohusu watoto wenyewe, sheria ya mtoto inawapa watoto haki ya watoto

kujieleza na kutoa maoni yao, kusikilizwa na kushiriki katika maamuzi yanayohusu

maisha yao.

Ili kuhakikisha sera na sheria tajwa zinatekelezwa ipasavyo, serikali chini ya uongozi wa

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto imeonelea ni vyema kuandaa Mpango

Kazi wa Ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi. Mpango kazi huu utatoa

maelekezo ya namna ya kufanikisha ushiriki wa watoto, uundwaji wa vyombo maalum

vitakavyowezesha watoto kushiriki na mwongozo wa jinsi ya kuingiza maoni ya watoto

na michango yao katika mipango, mikakati, programu na michakato mbalimbali na pale

inapowezekana hata katika kuingiza mchango wao katika taratibu za kutengeneza sheria

na taratibu za kimahakama.

Uandaaji wa Mpango Kazi huu unadhihirisha mabadiliko makubwa katika azma ya

ushiriki wa watoto ambao ni zaidi ya mchango wa maoni tu yanayotumika kama ushauri

na hivyo kuleta mafanikio endelevu katika ushiriki wa watoto kwenye michakato na

maswala ambayo yanahusu maisha yao. Mpango Kazi huu hata hivyo unahusu Tanzania

bara tu lakini kuna uwezekano wa kuupanua hadi Visiwani. Maandalizi ya Mpango huu

yalichukua sura shirikishi katika mchakato wake na maoni mbalimbali yaliyotolewa na

wadau wakati wote wa maandalizi yamezingatiwa na hivyo kuchukua sura shirikishi

ambayo itasaidia katika utekelezaji.

Mpango Kazi huu ambao unatarajiwa kuanza mwaka 2014 unalenga kuwafanya watoto

watambue kile ambacho jamii inatarajia kutoka kwao kwa maana ya majukumu hasa

wakati wanaposhiriki kikamilifu katika majadiliano, kupeana taarifa muhimu na

kutekeleza majukumu yanayowahusu kutokana na maamuzi waliyofanya katika ngazi ya

familia, jamii, kitaifa na kimataifa. Isitoshe, Mpango huu unalenga katika kuleta ufanisi

katika swala zima la ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi yanayohusu maisha yao

na ya jamii kwa ujumla na utekelezaji wake.

Mpango Kazi huu ni endelevu na katika hilo shughuli mbalimbali zitatekelezwa

zikiwemo kuelimisha jamii, watendaji wa serikali, wazazi/walezi wa watoto na watoto

wenyewe kuhusu athari zinazotokana na ukosefu wa ushiriki wa watoto kufanya

maamuzi kama wadau muhimu wa demokrasia, utawala bora na maendeleo endelevu ya

jamii. Mpango kazi huu pia utasaidia watoto kuibua vipaji vyao vya aina mbalimbali na

kuwapa fursa watoto kuchangia maoni na ushauri katika utungaji na utekelezaji wa sera

na sheria mbalimbali ili kuleta maendeleo yenye uwiano kijinsia na kijinsi.

iv

Mpango huu pia utatoa fursa kwa wazazi na walezi kujifunza njia bora za mawasiliano na

mahusiano mazuri kati yao na watoto wao na namna ya kuwashirikisha watoto katika

majadiliano na hata kunufaika na michango ya watoto kimawazo, ushauri na utekelezaji

wa maamuzi mbalimbali ya pamoja ya kutatua matatizo ya kipato duni, uvunjaji wa

sheria na taratibu mbalimbali na hata kubuni mikakati ya pamoja katika kutatua matatizo

hayo ya kijamii na mengineyo. Aidha watoto nao wote watafaidi haki yao ya msingi ya

kushiriki katika kufanya maamuzi yaani haki ya kusikika na kusikilizwa.

v

Shukrani

Katika kuandaa Mpango Kazi huu Shirikishi, wadau mbalimbali walishiriki kwa njia

moja au nyingine na hatuna budi kuwashukuru wote kwa dhati. Hawa ni pamoja na

watoto wa rika mbalimbali, wanajamii, wizara mbalimbali na idara za serikali, Asasi

Zisizo za Kiserikali, wadau wengine wa maendeleo, Mashirika ya Kidini,Wazee

wakimila na Wanataaluma.

Mchakato mzima kuandaa Mpango Huu ulikuwa chini ya usimamizi wa Wizara ya

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto. Mpango huu unawakilisha matokeo ya warsha za

majadiliano, mikutano, hojaji mbalimbali na mazungumzo na watoto, serikali, asasi

zisizo za kiserikali na wawakilishi wa wadau wengine wa maendeleo, wawakilishi wa

jamii mbalimbali ikiwa ni pamoja na wazee, na viongozi wa jamii na dini, kati ya mwezi

Mei na Julai 2010 kuhusu ushiriki wa Watoto katika maamuzi nchini Tanzania.

Shukrani za pekee zinapelekwa kwa Shirika la Kimataifa la Kushughulikia Watoto

Duniani (UNICEF) ambalo limechangia kwa hali na mali kuhakikisha kwamba kazi hii

inakamilika.

2014

vi

VIFUPISHO

AZAKI: Asasi Zisizo za Kiserikali

BEST: Basic Education Statistics, Tanzania “Takwimu za Elimu ya Msingi”

MKUKUTA: Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini Tanzania

NBS: National Bureau of Statistics “Idara ya Taifa ya Takwimu”

UKIMWI: Ukosefu wa Kinga ya Mwilini

WMJW: Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

OWMTMSM: Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

WAUJ: Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii

WSK: Wizara ya Sheria na Katiba

WMN: Wizara ya Mambo ya Ndani

vii

Yaliyomo Ukurasa

Dibaji ii

Shukrani v

Vifupisho vi

1.0 UTANGULIZI 2

1.1 Usuli na Muktadha wa Mpango Kazi huu 4

1.2 Changamoto katika kutimiza haki za watoto kushiriki 6

1.2.1 Tafsiri ya neno “Mtoto” 6

1.3. Umuhimu wa Mpango Kazi Huu na changamoto zake 9

1.3.1 Kwa nini ushiriki ni muhimu? 9

1.3.2 Changamoto za kufanikisha Ushiriki 10

2.0 HALI HALISI YA USHIRIKI WA WATOTO KWENYE

MAUDHUI YA KITANZANIA 13

2.1 Maudhui ya Kisheria 13

2.1.1 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 13

2.1.2 Sheria ya Mtoto (2009) 15

2.1.3 Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini (2004) 16

2.1.4 Sheria ya Virusi vya UKIMWI/ UKIMWI (Ulinzi na Kinga) (2008) 16

2.2 Maudhui ya Kisera 17

2.2.1 Sera ya Maendeleo ya Mtoto (2008) 17

2.2.2 Sera ya Elimu 17

2.2.3 Sera ya Maendeleo ya Vijana 18

2.2.4 Sera ya Taifa ya Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI/UKIMWI (2001) 18

2.2.5 Sera ya Utamaduni 18

2.2.6 Mchakato wa Maboresho ya Serikali za Mitaa 19

2.2. 7 Jumuisho la Sera 19

3.0 MATEGEMEO YA WATOTO KATIKA USHIRIKI 20

4.0 UCHAMBUI WA WADAU, WIZARA/TAASISI 23 4.1 Utangulizi 23

4.2 Serikali Kuu na Idara zake 24

viii

4.2.1 Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto 24

4.2.2 Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa 25

4.2.3 Wizara ya Fedha na Uchumi 26

4.2.4 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii 27

4.2.5 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi 28

4.2.6 Wizara ya Habari, Maendeleo ya Vijana na Michezo 30

4.2. 7 Wizara ya Sheria na Katiba 31

4.2.8 Wadau wa Maendeleo na Asasi Zisizo za Kiserikali 33

4.2.9 Familia 34

4.2.10 Baraza la Watoto la taifa 34

4.2.11 Maoni ya ziada kuhusu miundo na majukumu ya watendaji wakuu 34

5.0 MKAKATI 36 5.1 Mwelekeo 36

5.2 Lengo na Madhumuni 38

5.2.1 Lengo/Madhumuni ya jumla 38

5.3 Bango Kitita (Mpango wa Utekelezaji) 39

6.0 URATIBU, UFUATILIAJI NA TATHMINI YA UTEKELEZAJI 54

6.1 Utangulizi 54

6.2 Lengo la Ufuatiliaji na Tathmini 54

6.3 Malengo mahsusi 54

6.4 Uratibu 55

6.5 Mchakato wa Ufuatiliaji na tathmini ya Utekelezaji 56

6.5.1 Ufuatiliaji wa mchakato 56

6.5.2 Ratiba ya Utekelezaji na Matukio ya Ziada 57

7.0 REJEA 58

ix

1.0 UTANGULIZI

Mpango Kazi Shirikishi wa Ushiriki wa Watoto katika kufanya maauzi yanayohusu

maisha yao ni juhudi za serikali katika kutetea haki za watoto na kuimarisha demokrasia

nchini kulingana na sera za kitaifa na kimataifa, sheria mbalimbali zinazohusu watoto,

demokrasia na maridhiano ya kimataifa kuhusu haki za watoto na usawa wa jinsia.

Watoto wa Tanzania na kungineko wanakumbwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja

na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI wenyewe, kazi ngumu kwa watoto,

kiwango kikubwa cha kukatishwa masomo, kipato duni katika familia, na ukosefu wa

uhakika wa chakula. Matatizo mengine yanayowakumba watoto ni pamoja na elimu duni,

unyanyaswaji wa kijinsia, ukatili na kudhalilishwa. Watoto wanakutana na ukatili na

udhalilishwaji majumbani, mashuleni, ndani ya jamii zao na kungineko.

Matokeo ya awali ya utafiti uliofanyika kitaifa na mashauriano na watoto na vijana

kuhusu ukatili dhidi ya watoto yanaonyesha kuwa karibia asilimia 30 ya wasichana na

takriban asilimia 15 ya wavulana wamefanyiwa ukatili kabla ya kufikia umri wa miaka

18 na karibia asilimia 70 ya wasichana na 67 ya wavulana wamefanyiwa ukatili wa

shambulio la mwili. Wakati wa kuandaa Mpango kazi huu ilibainika kuwa kuna idadi

kubwa ya watoto wanaofanya makosa yanayo kinzana na sheria zilizopo au kuwa

mashahidi au waathirika wa uvunjaji wa sheria hizo. Idadi kubwa kidogo ya watoto wana

aina moja au zaidi ya ulemavu na wengi wao huishi mitaani1.

Kutokana na takwimu za Sensa ya Taifa ya idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2012,

milioni 21,866,258 ambao ni sawa na asilimia 50.1 ya idadi ya watu wote2 wana umri

chini ya miaka 18 kwa Tanzania Bara. Idadi ya watoto wa umri chini ya miaka minane

walikuwa 11,181,278. na takriban milioni moja wako chini ya umri wa miaka mitano,

takriban milioni nane ya watoto wanaishi kwenye umaskini uliokithiri na mmoja kati ya

wasichana wanne wenye umri chini ya miaka 18 tayari wameshaanza jukumu la kuzaa.

Aidha asilimia 58 ya watoto wenye umri kati ya miaka mitano hadi sita na asilimia 97.7

ya watoto wenye ulemavu hawapati elimu ya awali (BEST 2012). Takriban wasichana

8,000 wanaacha shule kila mwaka kutokana na mimba za utotoni. Mnamo 2001,

makadirio ya vijana wenye umri wa miaka 15-24 wanaoishi na virusi vya

ukimwi/UKIMWI walikuwa asilimia 4.3. Mkakati mmojawapo wa kuhudumia watoto

ambao wanaishi kwenye mazingira magumu na kuwalinda na kuwawezesha kupata haki

zao za elimu, afya na nyinginezo ni kuwawezesha kushiriki katika kufanya maamuzi ya

maswala yanayohusu maisha yao. Sababu hizi zinajenga hoja nzito ya uwepo wa Mpango

kazi huu ili kufanikisha utekelezaji.

Mchakato wa kukusanya maoni ya wadau katika uandaaji wa Mpango Kazi wa Ushiriki

wa Mtoto ulilenga kwenye kutathmini hali halisi ya sasa kuhusu ushiriki wa watoto

katika maswala yanayowahusu. Ilitambulika kuwa kwa kiasi fulani kuna uelewa

1 URT, NBS, National Population and Housing Sensus 2002 2 Sera ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto Tanzania, Oktoba 2013, uk.1

11

miongoni mwa watoto na hata watu wazima kuhusu ushiriki wa watoto , uelewa ambao

unaashiria kuwa mazingira yako mazuri na ni wakati muafaka kuhimiza ushiriki wa

watoto katika kufanya maamuzi ya masuala yanayowahusu. Licha ya hali kuwa hivyo,

kuna mitizamo hasi miongoni mwa wanajamii inayoashiria vikwazo /pingamizi katika

kuelewa kwamba watoto wana haki ya kushiriki katika kufanya maamuzi ya mambo

yanayohusu maisha yao na hivyo wanastahili kushiriki sawa na watu wazima katika

jukumu hilo la kijamii. Hali zote mbili zinatoa msisitizo wa uwepo wa Mpango Kazi

Shirikishi; kuimarisha uelewa uliopo kuhusu ushiriki wao na kujenga mitizamo chanya

katika swala hili na pia kutumika kama nyenzo ya kupambana na hisia hizo hasi

zinazopinga ushiriki wa watoto kwenye maamuzi muhimu yahusuyo maisha ya watu. Pia

kuna viashiria na vitendo vinavyochangia uwepo wa ushiriki wa watoto humu Tanzania,

yakiwemo mabaraza ya watoto katika jamii, na mashuleni, vilabu vya watoto, na kamati

mbalimbali pamoja na serikali inayojali ikishirikiana na Asasi Zisizo za Kiserikali.

Itambulike kuwa kutokana na mila na desturi za Mtanzania, utamaduni ulikuwa kwamba

mawasiliano na watoto yalijikita kwenye yale mambo yanayowahusu moja kwa moja

kwa kutumia mbinu mbalimbali kuendana na mazingira ya mila zao. Licha ya kwamba

mbinu hizi zilikuwa hazifuati kikamilifu taratibu za kidemokrasia za kuwahusisha watoto

kwa yale yote yanayohusu maisha yao, kwa kiwango kikubwa, bado hizi mila

zinatukumbusha kuwa umuhimu wa ushiriki wa watoto ulikuwa unatambulika na

unapaswa kuheshimiwa na kudumishwa ndani ya misingi ya haki za binadamu.

1.1 Usuli na muktadha wa Mpango Kazi Huu

Katika kuzingatia umuhimu wa ushiriki wa watoto katika kufanya maamuzi yanayohusu

maisha yao na ya jamii kwa ujumla, pamoja na umuhimu wa kuzingatia haki zao, serikali

ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa kipaumbele kikubwa kwa watoto. Hata

hivyo, Mpango Kazi huu unahusu Tanzania Bara tu ijapokuwa kuna uwezekano wa

kupanuka hadi Tanzania Visiwani.

Katika ngazi ya kitaifa, na katika kuhakikisha kuwa haki ya mtoto kushiriki katika

maamuzi yanayohusu maisha yake inazingatiwa, juhudi nyingi zimechukuliwa na serikali

kwa kuzingatia umuhimu wa kutimiza haki za watoto, hivyo serikali imetoa kipaumbele

kwa watoto kwenye nyanja mbalimbali kisera na kisheria:

a) Serikali ya Jamhuri ya Muungano imeridhia mikataba ya kimataifa na ya kikanda

inayohusu haki za watoto. Hii mikataba ni pamoja na:

i) Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watoto

ii) Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Watoto

b) Licha ya kuridhia mikataba hii ya kimataifa, serikali imechukua hatua madhubuti

kutunga sheria, sera, mikakati na mipango kazi ili kuhakikisha kwamba haki

zilizoainishwa katika mikataba hii inatekelezwa:

i) Mwaka 2002 Serikali ilisimamia uundwaji wa Baraza la Taifa la watoto na

mabaraza ya watoto katika ngazi ya jamii na mashuleni na klabu za watoto

pamoja na kamati za kushughulikia masuala ya watoto.

12

ii) Baada ya kuunda Sera ya Maendeleo ya Watoto mwaka 2008, mwaka

2009, Bunge la Muungano lilipitisha Sheria ya Mtoto inayobeba dhamira

ya serikali kuhakikisha kwamba watoto wote wanapata haki zao zote.

iii) 2011 Serikali ilitengeneza kielekezi cha ushiriki wa mtoto Tanzania

iv) 2011 Serikali ilitengeneza muongozo wa kuanzisha mabaraza ya vijiji,

kata, wilaya na mkoa.

v) Mwaka 2011 Serikali imesimamia na kuratibu utafiti wa kitaifa kuhusu

ukatili dhidi ya mtoto. Kutokana na matokeo ya utafiti huo, mwaka 2012,

Serikali iliandaa Mpango Kazi ulioshirikisha sekta mbalimbali katika

kuzuia na kukabiliana na ukatili huo.

vi) Mpango wa Kitaifa wa Kupunguza Umaskini, Mkukuta II (2010)

unatambua uwepo wa watoto wanaokabiliwa na hali hatarishi na kuweka

mikakati ya kuwalinda na kuhakikisha kwamba wanapata haki zao sawa

na watoto wengine.

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto (WMJJW) ndiyo yenye jukumu la

kusimamia na kuratibu utekelezaji wa mikataba, sera na sheria zinazolenga kutimiza haki

za watoto.

Mpango kazi huu unalenga katika kuhakikisha kuwa vikwazo vyote vinavyozuia ushiriki

wa watoto katika kufanya maamuzi ya masuala yanayohusu maisha yao vinakomeshwa

na sauti zao zinasikika na kuzingatiwa katika maamuzi ya kifamilia, kijamii na kitaifa na

kimataifa yanayohusu maisha ya watoto na haki zao. Inapendekezwa kuwa, wadau wote

ikiwa ni pamoja na serikali na asasi zisizo za kiserikali wapitie mpango kazi huu na

kuchagua malengo na shughuli zile zinazolingana na majukumu yao na hivyo kutekeleza

kikamilifu ili kupata mafanikio endelevu katika suala hili la ushiriki wa watoto.

1.2 Changamoto katika kutimiza haki za watoto kushiriki

1.2.1 Tafsiri ya neno “Mtoto”

Katika kufanikisha suala la ushiriki wa watoto, kuna haja ya kupata tafsiri halisi ya

maneno mawili muhimu; “mtoto” na “ushiriki wa mtoto” kulingana na sheria na sera za

Tanzania. Kisheria, kama ilivyoainishwa kwenye mkataba wa kimataifa wa haki za

mtoto, mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto na Sheria ya Mtoto, mtoto ni

mtu yeyote mwenye umri chini ya miaka 183. Kwa kuzingatia mazingira halisia ya

kisheria, na kulingana na aina ya majukumu anayopangiwa mtoto, umri unaweza kuwa

chini au juu ya miaka 18. Kwa mfano, katika Sheria ya Makosa ya Jinai, umri wa

kuwajibika kwa mhalifu ni miaka 10. Katika jamii nyingi, mtu yeyote ambaye bado ni

tegemezi kwa wazazi wake huwa anahesabika kuwa ni mtoto hata kama umri wake

3

13

unazidi miaka 18. Kwa upande mwingine, msichana ambaye amezaa au mtu yeyote

ambaye ametahiriwa au amepitia jando4 na unyago

5 anaweza asihesabike kuwa ni mtoto

hata kama umri wake ni chini ya miaka 18. Hata hivyo, kwa ujumla Mpango Kazi huu

unamtambua mtoto kuwa ni mtu mwenye umri chini ya miaka 18 kama ilivyotafsiriwa

katika Sheria ya Mtoto (Sehemu ya II, 11).

1.2.2 Tafsiri ya “ushiriki wa watoto na vijana wadogo” katika jamii

Zipo tafsiri kadhaa za dhana hii zikizingatia kifungu cha 12 cha Mkataba wa Kimataifa

wa Haki za Mtoto ambacho kinasema kwamba kila mtoto ambaye anaweza kuchangia

maoni ana uhuru na haki ya kutoa maoni hayo kuhusu masuala yanayomhusu bila woga

wowote na kwamba maoni yao yapewe uzito unaostahili kulingana na umri wao. Hii ni

mojawapo ya haki ambazo zimeainishwa kama haki ya msingi katika Mkataba wa Umoja

wa Mataifa wa Haki ya Mtoto. Haki hii pia inaainishwa katika kifungu cha 5 cha

Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto ambacho kinasema kuwa jukumu la kutoa

mwongozo katika kujali haki za watoto, wazazi na walezi wa watoto katika ushiriki wa

watoto kutoa maamuzi mbalimbali lilenge kwenye mwenendo wa ukuaji wa uwezo wa

watoto. Hii inamaanisha kwamba, watoto wanapata uzoefu na ujuzi katika nyanja hii ya

ushiriki jinsi wanavyokua na kupata fursa ya kushiriki na kupewa majukumu

yanayoendana na ushiriki wao na pia hukomaa wanavyopata utashi wa kuwajibika kwa

matendo yao yanayotokana na uchangiaji wao katika kufanya maamuzi yanayowahusu

wenyewe.

Mojawapo ya misingi mikuu iliyoainishwa kwenye Kamati ya Mkataba wa Kimataifa wa

Haki za Mtoto ni ule unaotokana na kifungu cha 3 ambacho kinatambua umuhimu wa

kuzingatia matakwa ya mtoto wakati wote wa kufanya maamuzi. Kamati hii inaainisha

kuwa kuna kuwajibika kwa pamoja katika kuamua kipi kina maslahi kwa watoto na hili

hutokana na majadiliano na makubaliano kati ya watoto na watu wazima ijapokuwa

uwajibikaji wa kufikia maamuzi hayo uko mikononi mwa watu wazima. Uwajibikaji huu

wa pamoja pia una mipaka yake na muelekeo unaotolewa na wazazi au walezi wa watoto

(na hata watu wengine wazima) unapaswa kuzingatia uwezo wa watoto kufanya

maamuzi.

Aina nyingine ya ushiriki ni ile inayoelezwa katika vifungu 13 hadi 17, ambavyo vinatoa

tafsiri ya mwelekeo mwingine wa ushiriki katika jamii ambao unajumuisha uhuru wa

kujieleza, uhuru wa dini, utashi, kujiunga kwenye kundi lolote, usiri na taarifa. Vifungu

hivi vinazingatia Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu (UN Universal Declaration of

Human Rights-UDHR), Kifungu cha 2, 12, 18, 19, 20 na 27. pamoja na mikataba ya

kimataifa ya haki za kiraia na kisiasa na mkataba wa kimataifa wa haki za kiuchumi,

14

kijamii na kitamaduni ambapo inatambulika na kutamkwa na kukubalika kuwa kila mtu

ana haki zote na uhuru zilizotamkwa kwenye matamko haya bila kujali tofauti za kitaifa,

rangi, jinsi, lugha, dini, vyama vya siasa au itikadi yoyote au kabila, mahali mtu

alipozaliwa au tofauti nyingine yoyote. Kuna misingi mingine ambayo inatukumbushia

pia kuwa haki za binadamu ni kwa binadamu wa mataifa yote na hazihodhiwi wala

kunyang‟anywa iwe ni haki za kiraia, kisiasa, kiuchumi, kijamii au kiutamaduni. Uwepo

wa haki mojawapo hufanikisha kuwepo kwa haki nyingine na hivyo hivyo uvunjaji wa

haki ya aina moja husababisha mlolongo wa uvunjaji wa haki nyingine. Ieleweke kuwa

haki hizi hazihamishiki na uvunjaji wake kwa makundi fulani lazima uwe na kibali cha

kisheria.

Vifungu vya Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto, hasa vile vinavyozungumzia

ushiriki inabidi vieleweke kwa kiwango kikubwa. Kwa wakati huu ndani ya jamii ya

Kimataifa, umuhimu umewekwa kwenye mlengo wa kuzingatia Haki za Binadamu ili

kufanikisha mkakati wa kuziona haki za binadamu kuwa hazihamishiki wala

kunyang‟anywa kutoka mtu mmoja kwenda mwingine. Mkataba wa Kimataifa wa Haki

za Mtoto, kama nyenzo ya kufanikisha kutokuvunjwa kwa haki za binadamu pia inatafsiri

haki za watoto katika jamii ambapo inajumuisha haki ya ushiriki katika maamuzi.

Isitoshe, katika maoni ya jumla ya Kamati ya Haki za watoto No. 12, kamati ilitambua

kifungu namba 12 kama kifungu muhimu katika kutambua msingi wa haki ya kushiriki

ambao unawahusu watoto wote wenye uwezo wa kuchangia maoni, bila kujali umri wao

mdogo, na kuwa haki hii inaainishwa katika nyanja zote za maisha, kuanzia katika ngazi

ya familia, nyumbani, katika jamii, mashuleni, sehemu zote zenye makundi ya watu na

huduma za jamii na popote pale ambapo sera na huduma za serikali zinahusika.

Kamati ilisisitiza umuhimu wa kuwapatia watoto taarifa muhimu katika kupata fursa na

muda wa kushiriki kikamilifu na kwa amani bila woga wala kubanwabanwa. Kwa hali

hiyo, tafsiri halisi ya ushiriki ni mchakato endelevu ambao watoto wanapata fursa /na

wanachangia kikamilifu katika kufanya maamuzi ya maswala yanayohusu maisha yao:

Huwapa watoto fursa ya kuchangia maoni kuhusu mwelekeo wa mchakato wa

utoaji maamuzi ya mambo muhimu ya maisha na yatokanayo na mchakato huo,

Huhitaji kupeana taarifa na kuendesha majadiliano kati ya watoto na watu

wazima ambayo yanalindwa na dhana ya kuheshimu mchango wa kila mmoja

wao, dhana ambayo inaimarisha kuelewana, kutoa maamuzi ya pamoja na

kushirikiana kwa nguvu moja katika kusimamia utekelezaji wa maamuzi hayo.

Kuheshimu nguvu ya watoto ya kuchangia katika maamuzi ambayo inakua kila

wanaposhiriki, ili kwamba uzoefu na mahitaji yao yanakubalika kama sehemu ya

ukuaji na aina ya ushiriki wao.

Humu Tanzania, Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, Sehemu ya 2 Kifungu cha 11,

kinaelezea namna ya kufanikisha kufikia malengo ya ushiriki wa mtoto kwa kuzingatia

kifungu 12 cha Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto:

“Mtoto ana haki ya kutoa maoni yake na kusiwe na mtu yeyote kumnyima haki ya

kushiriki mtoto ambaye ana uwezo wa kutoa maoni, kusikilizwa na kushiriki

katika kufanya maamuzi ambayo yanahusu maisha yake”.

15

1.3. Umuhimu wa Mpango Kazi Huu na changamoto zake

1.3.1 Kwa nini ushiriki ni muhimu?

Ushiriki kwa jinsi ilivyoonyeshwa hapo juu ni haki ya msingi, hivyo inatambulika kama

haki inayowezesha haki nyingine zote kuwepo. Watoto wote kama ilivyo kwa watu

wazima wana haki ya kushiriki na serikali zote duniani huwa zinategemewa kuheshimu

haki hii kwa watoto bila kujali tofauti za aina yoyote miongoni mwa watoto.

Ni muhimu kuelewa kuwa ushiriki wa watoto unachangia katika kufanikisha mchango wa

watoto katika jamii kama wananchi wengine. Kutokana na uzoefu wao katika ushiriki moja

kwa moja katika maswala yanayohusu maisha yao, watoto wanajijengea uwezo wa

kuchangia katika kudumisha amani na demokrasia katika nchi zao kama raia

wanaowajibika.Kitendo hiki kinachangia katika kuendeleza utamaduni wa kuheshimiana

ambao ni muhimu katika jukumu la kufanya maamuzi kwa kujadiliana badala ya

kugombana na kutumia udikteta. Watoto wanajifunza kuwa haki za binadamu ni kwa kila

mtu na hudumisha kuheshimiana na sio kushindana na kugombania. Ushiriki wa jamii

nzima katika kufanya maamuzi ambao unahusisha watoto unasaidia serikali kuboresha

huduma za jamii, na kuwapa wananchi nafasi ya kuwawajibisha watendaji wa serikali,

kuhakikisha kuwa mchakato wa utoaji haki na ufuatiliaji wa sheria una tija.

Watoto wanaposhiriki wanapata ujuzi, uelewa, na kujiamini, vitu ambavyo wanahitaji

katika maisha yao. Hili linachangia katika maendeleo ya watoto kwa kiasi kikubwa kwa

mfano huchangia katika kutimiza malengo ya elimu (Kifungu 29 cha Mkataba wa

Kimataifa wa Haki za Mtoto, maendeleo yao kikamilifu (kama ilivyoainisha katika

kifungu 6 cha Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto) na uwezo wao wa kufaidi haki

zao (Kifungu 5). Ushiriki wao pia unachangia katika kujali matakwa yao kama

ilivyoainisha katika kifungu 3.1 cha Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Mtoto na kile cha

4.1 cha Mkataba wa Kanda ya Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto. Watoto ambao

wanawezeshwa kijamii, kiuchumi na kisiasa wana uwezo pia wa kuwa wahamasishaji na

watetezi hodari wa haki zao.

Uwezeshaji huu una uwezo mkubwa wa kuchangia katika kujali haki za watoto. Watoto

mara nyingi huwa wakimya na wavumilivu tu hata pale wanapofanyiwa ukatili na

wanaponyanyaswa na watu wazima au watoto wenzao. Kuwapatia taarifa na

kuwahamasisha kuzungumzia matatizo yao, kuna waelimisha kuhusu njia za amani na

salama za kuhoji ukatili na unachangia kuwapa watoto ulinzi na kuishi kwa amani na

furaha.

Isitoshe, watoto wanaopata fursa ya kupata taarifa kuhusu afya na mambo ya afya ya uzazi

wana nafasi nzuri ya kujilinda dhidi ya mimba za utotoni, magonjwa ya zinaa, Maambukizi

ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Wafanyikazi vijana wanaojiunga kwenye vyama

vya kijamii na harakati za maendeleo wana nafasi kubwa ya kujilinda dhidi ya unyonyaji,

na udhalilishwaji katika sehemu zao za kazi, wana uwezo wa kudai malipo halali ya jasho

lao na mazingira mazuri ya kufanyia kazi. Kwa upande mwingine wana uwezo mkubwa

wa kupiga vita ajira za watoto makazini.

16

Zaidi ya hayo, ushiriki wa watoto unachangia kutoa na kusambaza taarifa na uelewa

ambao unasaidia kuboresha utungaji wa sheria, uandaaji wa sera na bajeti, na utoaji wa

huduma za jamii, kwa mfano, unachangia katika kufikia malengo ya Millennia (MDGs).

1.3.2 Changamoto za kufanikisha Ushiriki

Kuna changamoto nyingi katika kufanikisha ushiriki wa watoto. Kuna madaraja ya

kujenga kati ya azma ya ushiriki na uhalisia wake katika maisha ya watoto na katika

kufikia malengo mazuri ya sera zinazohusu watoto. Katika Kamati ya Haki za Watoto

yafuatayo yaliainishwa: katika kifungu cha 12:

Ili kufanikisha mashauriano, taarifa na michakato inatakiwa kuwafikia

walengwa. Lakini kujidanganya kuwa watoto wanasikilizwa ni changamoto

ndogo ila kukubali maoni yao na kuzipa uzito unaostahili hoja zao ni ishara

ya mabadiliko makubwa. Kusikiliza sauti za watoto isichukuliwe kuwa ndio

mwisho wa changamoto bali ieleweke kuwa njia tu kwa serikali kuwasiliana

na watoto na kujua matendo yao kwa niaba ya watoto ambao wana ari na

wamehamasika kulinda haki za watoto.

Kifungu cha 12 kinadai uwepo wa mipango endelevu ya ushiriki. Ushirikishi

na majadiliano na watoto huhitaji pia kuepuka kuonyesha kujali kwa kiasi

kidogo tu na kulenga kwenye kupata uwakilishi wa maoni ya walio wengi.

Msisitizo wa “masuala yanayowahusu”katika kifungu cha 12 (1) unaonyesha

kuwa upatikanaji wa waoni ya vikundi mbalimbali vya watoto walio wengi

kuhusu masuala yanayowahusu kwa mfano watoto ambao walishawahi

kukumbwa na uhalifu kushiriki kutoa maoni kuhusu namna ya kuboresha

sheria zinazolenga eneo hilo, au watoto walioasiliwa au wanaoishi katika

familia zinazoasili watotokutoa maoni yanayohusu sheria ya kuasili na sera.

Ni muhimu na jambo la busara kwa serikali kujenga mahusiano/mawasiliano

ya moja kwa moja na watoto, na sio tu mahusiano kupitia asasi zisizo za

kiserikali (AZAKI) au taasisi za kutetea haki za binadamu. Katika miaka ya

awali ya Makubaliano/Mapatano haya, AZAKI zilichangia kuanzisha

utaratibu wa kushirikisha watoto, lakini ni kwa faida ya serikali na watoto

kuwa na mahusiano na mawasiliano ya moja kwa moja.

Kamati ya Haki za Watoto pia ilisisitiza suala la sauti za watoto kusikilizwa katika ngazi

zote kuanzia kwenye familia na hili ni muhimu pia kwa Tanzania:

90. Familia ambazo zinawapa watoto uhuru wa kujieleza na kutoa maoni yao

ambayo yanathaminiwa kuanzia wakiwa kwenye umri mdogo zinakuwa za

mifano ya kuigwa na humuandaa mtoto kujizoesha katika kutafuta haki ya

kusikilizwa na jamii kubwa zaidi.

91. Makubaliano/Mapatano haya pia yanatambua haki na wajibu wa wazazi

au walezi wengine kuwapatia watoto wao muelekeo unaoeleweka na ushauri,

17

lakini pia inasisitiza kwamba yote haya yafanyike kwa lengo la kumwezesha

mtoto kufaidika na haki zake na kusisitiza kuwa muelekeo huo na ushauri

utolewe katika mazingira yanayojenga kumwezesha mtoto na sio vinginevyo.

92. Serikali zihimize kwa kupitia sheria na sera wazazi na walezi na wale

wanaohudumia watoto kuwasikiliza watoto na kuthamini maoni yao katika

masuala yanayowahusu watoto. Wazazi washauriwe pia kuwasaidia watoto

wao katika kutambua haki yao ya kujieleza na kuchangia maoni bila woga na

kuhakikisha maoni ya watoto yanathaminiwa wakati wote na katika ngazi zote

za jamii.

93. Ili kusaidia kuboresha mfumo wa makuzi ya watoto unaoheshimu haki ya

watoto ya kusikilizwa, Kamati inapendekeza kuwa serikali na vyombo vyake

iandae programu ya mafunzo kutoa elimu kwa kuanzia kuendeleza tabia na

mitizamo rafiki kwa watoto iliyopo na kutoa habari na taarifa kuhusu haki za

watoto na wazazi zilizoainishwa katika Makubaliano haya.

94. Programu hizo zinapaswa kushughulikia na kufanikisha yafuatayo:

Mahusiano yanayothamini mchango wa watoto na wazazi, Ushiriki wa watoto

katika kufanya maamuzi, Matokeo ya kuipa uzito unaostahili maoni na

michango ya mawazo ya kila mwanafamilia, Uelewa, uwezeshaji na

uendelezaji pamoja na uthamini wa ujuzi, uwezo na uzoefu unaokua wa

ushiriki wa watotona njia za kupambana na mitizamo na maoni hasi kuhusu

haki za watoto ndani ya familia

Mapendekezo ya misingi ya namna ya kupambana na mitizamo hii hasi na kujenga

mazingira yanayofaa na yenye tija ya majadiliano kati ya watoto na watu wazima ni kama

ifuatavyo:

1. Uwazi, ukweli na uwajibikaji

2. Mazingira rafiki kwa watoto

3. Usawa wa fursa

4. Ulinzi na usalama wa watoto

5. Ukereketwa wa kujali watoto na uwezo unaohitajika wa watu wazima

Hivyo basi, watu wazima wanaoamua kushiriki na watoto katika majadiliano wanapaswa

kufuata njia za uadilifu na kuyapa kipaumbele matakwa ya watoto. Watoto wanatakiwa

wajengewe mazingira rafiki ambayo ni salama, mazuri na yenye kuwapa motisha

kushiriki miongoni mwa watu wazima bila kuwa na woga wa kudharauliwa na kuzidiwa

nguvu. Makundi ambayo yamewekwa pembezoni na ambayo mara nyingi hayahusishwi

kwenye mambo mengi kama vile wasichana, au watoto wenye ulemavu ni muhimu

wahusishwe.

Watoto, kama ilivyo watu wazima ni kundi ambalo lina wahusika wanaotofautiana kwa

misingi ya kijinsia, kikabila, kiuwezo, kiuchumi na tofauti nyinginezo. Hatua za

makusudi zichukuliwe ili kuhakikisha kuwa makundi yote haya yanashiriki. Na uangalifu

uwepo ili wote wajisikie wana fursa sawa bila ubaguzi wala kunyanyasika kwa namna

18

yoyote ile au kuathirika aidha kisaikolojia au kimwili. Watu wazima nao wajaribu

kuhakikisha kuwa hawajifanyi wao wanajua zaidi na wawe wanawahamasisha watoto

kushiriki kikamilifu kama wana uelewa wa kutosha wa jambo wanalolijadili, tabia ya

usikivu na kuchangia maoni kwa faida ya wote. Hata hivyo, kwa wale wazee ambao

walizoea mfumo wa kidikteta au ukandamizaji na ukali, ambao watoto walikuwa

hawapati nafasi kukaa na wazee na kujadili pamoja, mabadiliko haya yatakuwa ni

changamoto kubwa kwao.

2.0 HALI HALISI YA USHIRIKI WA WATOTO KWENYE MAUDHUI YA

KITANZANIA

2.1 Maudhui ya Kisheria

2.1.1 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Kwa kuanzia, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inajali waTanzania wote bila

kujali umri (kifungu cha 8 (1). Kulingana na Katiba, serikali inapaswa kuwajibika kwa

watu, na watu kushiriki katika maswala yote ya serikali kulingana na misingi ya katiba.

Watu wanaotajwa kwenye katiba ni pamoja na watoto na demokrasia na uwajibikaji

vinazungumzia haki ya ushiriki hivyo watoto kama raia mwingine wa Tanzania

wanafaidika na haki za ushiriki zilizoainishwa katika kifungu cha 18 cha Katiba ambacho

kinatamka bayana uhuru wa kujieleza:

(1) Bila upendeleo kisheria, kila mtu ana haki ya uhuru kujieleza, na kutoa

maoni, kutafuta, kupokea na kusambaza taarifa na mawazo kupitia vyombo

vya habari, bila kujali uraia, na pia ana haki ya uhuru wa kutokubughudhiwa

kwenye mawasiliano hayo.

(2) Kila raia ana haki ya kupata habari/taarifa wakati wote kuhusu matukio

mbalimbali nchini na katika ulimwengu wote ambayo yana umuhimu katika

maisha ya watu na pia maswala muhimu yanayohusu jamii.

Kifungu 19 (1) kinaelezea haki ya uhuru wa mawazo, utashi, na imani:

Kila mtu ana haki ya uhuru wa mawazo, au utashi, imani au dini anayoipenda,

na uchaguzi katika maswala ya kidini, pamoja na uhuru wa kubadili dini au

imani za kidini

Kifungu 20 (1) kinahusu uhuru wa kujiunga na kikundi chochote:

Kila mtu ana uhuru wa kujumuika kwa amani, kushirikiana na watu wengine,

kutoa maoni yake kwa uwazi bila kificho, na kwa hakika zaidi kujiunga na

kundi lolote ambalo limeundwa kwa madhumuni ya kulinda na uendeleza

imani yake au matakwa yake au kwa jambo lingine lolote lile.

Kifungu 21(2) kinazungumzia ushiriki wa raia.

Kila raia ana haki pamoja na uhuru wa kushiriki kikamilifu katika mchakato

unaolenga kufanya maamuzi kuhusu maswala yenye athari kwake au

yanayomhusu maisha yake na yale ya taifa lake.

19

2.1.2 Sheria ya Mtoto (2009)

Sheria hii ambayo imeanza kutumika mwezi Aprili mwaka 2010 ndio sheria pekee

inayomlenga mtoto na ambayo imeweka misingi imara ya kulinda mtoto na kwa mara ya

kwanza kuingiza haki za watoto katika sheria ya nchi. Sheria hii inaweka bayana uhuru

wa watoto kujieleza na kutoa maoni yao, kusikilizwa na kushiriki katika kufanya

maamuzi kwa mambo yanayohusu maisha yao na ya jamii zao. Pia sheria hii inasisitiza

suala la kujali maslahi ya watoto kwanza katika maswala yote na kutokubagua watoto.

Katika sehemu ya 15, sheria hii inasisitiza msimamo wa Mkataba wa Kanda ya Afrika

wa Haki na Ustawi wa Mtoto, na kuhimiza kuwa watoto wana wajibu wa kuhudumia

jamii na taifa lao kwa kutumia uwezo wa nguvu zao na akili zao kulingana na umri na

uwezo.

Kwa kuzingatia zaidi uchambuzi kuhusu swala la ushiriki wa mtoto katika jamii ya

Kitanzania, Sheria hii ya Mtoto katika sehemu ya kwanza, Maelezo ya Awali imetamkwa

kuwa:

2. Sheria hii inahusu Tanzania Bara tu katika swala la kulinda, kuendeleza na

kusimamia maslahi na haki za mtoto

Sheria hii inaendelea kuelezea haki za watoto katika Sehemu ya Pili chini ya kichwa cha

habari cha Haki na Maslahi ya mtoto, kifungu kidogo cha (a) kuhusu Haki ya Mtoto

ambavyo Kifungu cha 4 hadi 14 kinaelezea lengo la sheria hii. Kifungu cha 11 kinasema

kuwa:

Kila Mtoto ana haki ya kutoa maoni yake na asitokee mtu kumnyima mtoto

mwenye uwezo wa kutoa maoni yake haki ya kujieleza, kusikilizwa na

kushiriki katika kufanya maamuzi yanayohusu maisha yake.

Kifungu hiki kinafafanua msimamo wa Sheria hii kama ilivyoelezwa katika kifungu cha

18 hadi 21 cha Katiba ya Nchi. Hili pia linaendana na Kifungu cha 12 cha Mkataba wa

Kimataifa wa Haki za Mtoto na Kifungu cha 7 cha Mkataba wa Afrika wa Haki na

Ustawi wa Mtoto ambacho kinasema:

Kila mtoto mwenye uwezo wa kujieleza atahakikishiwa haki yake ya kutoa

maoni yake kwa uhuru katika masuala yote na kusambaza maoni yake ili

mradi haendi kinyume na sheria zilizopo

Mpango Kazi huu ni njia mojawapo ya kuwawezesha watoto kutoa michango yao

inayotarajiwa katika jamii na taifa kama ilivyoelezwa katika sheria na mikataba

mbalimbali.

2.1.4 Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini (2004) Hii ni Sheria inayomlinda mtoto katika Sekta ya kazi. Sehemu ya 5 (1) ya sheria hii

inakataza ajira kwa watoto wenye umri chini ya miaka 14 ila wale wenye umri huo

na kuendelea wanaweza kuajiriwa kwenye kazi nyepesinyepesi ambazo hazina

madhara kwa ukuaji na afya yao na wala kuathiri maendeleo yao kielimu. Sheria

hii pia inakataza ajira kwa watoto wenye umri wa miaka 18 kwenye ajira/kazi

hatarishi. Ili kuwalinda watoto dhidi ya ajira za aina hizo, ni muhimu wao wenyewe

20

washiriki katika kuandaa taratibu za kuwalinda na Mpango Kazi huu utasaidia

katika kufanikisha hilo. Mwaka 1998 Tanzania imeridhia Mkataba wa ILO wa

Mwaka 1973 (Na. 138) kuhusu Umri wa Kuruhusu Mtoto Kuajiriwa and ule wa

Ajira Mbaya kwa Watoto wa 1999 (Na. 182) uliridhiwa mwaka 2001.

2.1.4 Sheria ya Virusi vya UKIMWI/ UKIMWI (Ulinzi na Kinga) (2008)

Serikali inatambua wajibu wake kutoa huduma ya tiba, matunzo na msaada kwa watu

wanaoishi na VVU na waliokatika hatari ya kuambukizwa VVU kwa kutumia raslimali

zilizopo. Sheria hii inatamka kuwa upimaji hiari unapatikana kwa watu wote kwa ridhaa

yao.Sehemu ya 15 (2) inalenga watoto kwa kutamka kuwa: “Mtoto au mtu yeyote

ambaye hana uwezo wa kutambua matokeo ya upimaji atapimwa kwa ridhaa ya

maandishi ya mzazi au mlezi anayetambulika”. Hata hivyo, tamko hili linasahau kuwa

siku hizi kuna mabadiliko kwa watoto kuwa wale wenye umri mkubwa kidogo wana

uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kuhusu upimaji wa Virusi vya Ukimwi na wanaweza

kuelewa majibu ya upimaji huo. Msimamo huu unakinzana na nia ya ushiriki wa watoto

na unaweza kukiuka haki za watoto katika suala la kupatiwa huduma zinazoendana na

Virusi vya UKIMWI/UKIMWI haswa kwa watoto wenye umri mkubwa kidogo ambao

wanaweza kuficha taarifa muhimu zakwao na za wenzao wa rika lao.

2.2 Maudhui ya Kisera

2.2.1 Sera ya Maendeleo ya Mtoto (2008)

Mazingira ya kisera ya kusimamia haki za watoto Tanzania ni mazuri kwa kiasi kikubwa.

Ziko sera kadhaa ambazo ni rafiki kwa watoto. Sera ya maendeleo ya Mtoto (2008) kwa

mfano hutoa miongozo kwa wadau wote katika kushiriki kwenye utekelezaji wa

programu zinazolenga haki za watoto na maisha yao. Sera hii inaandaa utaratibu kwa

wadau kuelewa majukumu yao ambayo yanapotekelezwa ipasavyo yanafanikisha

utekelezaji wa mipango kuhusu watoto na usimamizi wake. Katika lengo lake la nne kwa

mfano, sera hii inatamka wazi suala la ushiriki wa watoto unaolenga kutoa muelekeo

kuhusu kuishi, kulindwa, kushiriki, kutokubaguliwa na kuhusu maendeleo ya mtoto kwa

ujumla.

Mpango Kazi huu kwa hiyo, ni nyenzo mojawapo iliyoandaliwa kutoa muelekeo wa

namna ya kuwashirikisha watoto katika kutoa mchango wao na kushiriki katika masuala

yanayowahusu ambayo hatimaye yanamuwezesha mtoto kupata maisha yenye ulinzi wa

kutosha, usalama na maendeleo. Msimamizi wa sera hii ni Wizara ya Maendeleo ya

Jamii, Jinsia na Watoto, ambayo inawajibika kwa masuala ya familia. Wizara hii ina

jukumu la kuelimisha na kutoa ujuzi kwa familia na jamii kwa ujumla katika lengo la

kuwezesha watoto kuchangia na hivyo kuwa washiriki katika masuala yanayohusu

maisha yao, familia zao, jamii zao na ngazi nyingine za shuguli za kiraia. Wizara hii

katika Mpango Mkakati wake wa 2007/08 hadi 2009/10 imejidhatiti kujengea uwezo

familia na jamii katika swala la ushiriki katika kufanya maamuzi, kupanga mikakati

mizuri ya kutekeleza mipango ya maendeleo na kuimarisha uongozi wa kidemokrasia

katika ngazi ya serikali za mitaa na taasisi zake. Hatua hizi itachangia kiasi kikubwa

kufanikisha utekelezaji wa Mpango Kazi huu.

21

2.2.2 Sera ya Elimu

Sera ya Elimu inaweka bayana suala la elimu ya msingi kuwa lazima kwa watoto wote na

ushiriki wa watoto katika kamati za shule. Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Elimu

(2008-2017) inasisitiza malengo ya sera hii katika kulinda haki za binadamu ambazo ni

pamoja na haki ya kupata elimu na ushiriki wa watoto katika masuala yote

yanayowahusu. Kwa ujumla kila mtoto anapaswa kupitia mfumo wa elimu kabla ya

kuwa mtu mzima na hivyo elimu ni sehemu nzuri kwa watoto kuanza kushiriki kwa

kujijenga kwa maisha yao ya utoto na baadae ya utu uzima.

2.2.7 Sera ya Maendeleo ya Vijana

Sera ya Maendeleo ya Vijana inalenga katika kuhamasisha vijana kushiriki katika nyanja

zote za maendeleo kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni na kuhimiza sekta zote za

jamii kushiriki katika mipango inayolenga kwenye maeneo haya. Utekelezaji wa sera hii

una uwiano mzuri na Mpango Kazi huu wa ushiriki wa watoto ambao utahamasisha na

kuongoza vijana katika kuanza kutekeleza majukumu yao kuanzia umri wa chini. Katika

Sera hii tafsiri ya neno „vijana‟ ni watu wenye umri kuanzia miaka 15 hadi 35. Mpango

Kazi huu utahusishwa kwa karibu sana na Mkakati wa Kitaifa wa Ushiriki wa Vijana

ambao mipango yake ya utekelezaji inaandaliwa chini ya usimamizi wa Wizara ya

Uwezeshaji, na Maendeleo ya Vijana ambayo hivi karibuni jina lake limebadilishwa na

sasa inajulikana kama Wizara ya Habari, Maendelo ya Vijana na Michezo.

2.2.8 Sera ya Taifa ya Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI/UKIMWI (2001) Sera hii inatambua haki za vijana kuhusu usiri, na upimaji hiari na ushauri nasaha / kwa

ridhaa ya mlengwa baada ya kupata maelezo kamili. Sera hii pia inawezesha walenga

kupata taarifa sahihi kuhusu Virusi vya Ukimwi/UKIMWI, programu za elimu shirikishi

ya maswala ya kujamiiana, na taasisi zinazotoa elimu hiyo pamoja na mikakati maalum

kwa vijana walio nje ya shule. Mpango kazi huu utawawezesha kufanikisha ushiriki wa

watoto na mchango wao katika maswala yanayohusiana na Virusi vya

UKIMWI/UKIMWI katika maisha yao, maisha ya wana rika, familia na jamii zao kwa

ujumla.

2.2.9 Sera ya Utamaduni

Sera hii inatetea matumizi ya Kiswahili kama lugha ya taifa na kutoa motisha kwa

utumiaji wa lugha hii. Kiswahili ni lugha kuu ya mawasiliano katika ngazi zote na lugha

inayotumika katika mfumo wa elimu, hasa katika shule za msingi. Matumizi ya lugha

moja ya kitaifa yatasaidia sana kufanikisha utekelezaji wa Mpango Kazi huu. Lugha

moja ya kitaifa inatoa fursa kwa ushiriki wa watoto unaowawezesha mawasiliano rahisi

na yenye tija katika ngazi zote. Hata hivyo, Mpango Kazi huu unatoa nafasi kwa lugha

zote mbili, ya Kiswahili na Kiingereza kutumika katika utekelezaji.

2.2.10 Mchakato wa Maboresho ya Serikali za Mitaa

Maboresho ya serikali za mitaa yanayo lengo la kupeleka huduma za serikali karibu na

wananchi na kuhamasisha ushiriki mkubwa zaidi wa jamii katika uongozi, hii ikiwa ni

pamoja na ushiriki wa watoto. Ongezeko la ushiriki wa jamii katika uendeshaji na

uongozi wa kidemokrasia katika taasisi mbalimbali utasaidia kuleta uwiano na usawa

katika ugawaji wa raslimali katika serikali za mitaa, na mipango inayolenga maendeleo

22

ya watoto. Mpango kazi huu utasaidia kutoa mwongozo zaidi kwa serikali za mitaa na

taasisi zinazojali demokrasia katika kufanikisha kuingiza mchango wa watoto na ushiriki

wao katika kufanya maamuzi kwa yale yote yanayowahusu watoto na jamii zao.

2.2. 7 Jumuisho la Sera

Utekelezaji wa sera zote hizi unachangia katika kufanikisha utekelezaji wa MKUKUTA

II (Mpango wa Pili wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania) ambao

unatambua umuhimu wa utawala bora kama msingi wa kukua kwa uchumi, maisha bora

na katika kundi la III la maeneo muhimu ya MKUKUTA kwa mfano, MKUKUTA

unaelezea utaratibu wa kufanikisha utawala bora na ushiriki wa raia katika ngazi zote.

Mpango Kazi huu utasaidia katika utekelezaji wa lengo hili la MKUKUTA kwa kutoa

miongozo ya ushiriki wa watoto katika utawala. Ushiriki wa raia unaojumuisha ushiriki

wa watoto ni msingi wa demokrasia na utawala bora.

MKUKUTA II pia unasisitiza suala la kulinda haki za binadamu kwa watu wote, watoto

kwa watu wazima, wake kwa waume. Kuhusu haki za watoto, chini ya Lengo la 3

sehemu ya pili MKUKUTA unatambua umuhimu wa kuzilinda haki za watoto:

Kuheshimu haki za watoto kunachangia katika kuendeleza utamaduni

wakulinda haki za binadamu kwa vile watoto watakua wakiwa wanajua

haki zao, majukumu na wajibu wao kama watu wenye haki.

MKUKUTA pia unaelezea maudhui ya kuingiza ushiriki hasa wa vikundi vya watoto

wenye mahitaji maalum kwa lengo la kuboresha maisha yao kwa kuboresha huduma za

jamii kama vile elimu ulinzi na uhai wao, afya na lishe, maji safi na salama, usafi wa

mazingira, makazi yenye heshima, na mazingira endelevu.

Katika kufanikisha haya, aina na utawala unaothamini ushiriki wa raia wote

unatambulika kuwa ndio kiini cha mafanikio. Kwa hali hiyo, ushiriki wa watoto kama

inavyotambulika kikatiba, na nafasi yao kama ulivyoelezwa katika Sheria ya Watoto,

kuwa hakuna ubaguzi wala kutengwa kwa kikundi chochote, vyote hivi ni fursa kwa

watoto kushiriki katika majukumu ya kuleta maendeleo ya nchi kwa ushirikiano na watu

wazima. Ukweli ni kwamba, kwa kuwa watoto ni sehemu kubwa ya idadi ya waTanzania,

mchango wao ni muhimu katika kufanikisha malengo ya MKUKUTA. Kwa kupitia sauti

zao, matumaini ya kizazi ambacho hatimaye kitachukua dhamana ya hatma ya utawala na

uhai wa taifa yatafikiwa kwa manufaa ya raia wote na hivyo ushiriki wao ni muhimu

katika kufikia malengo ya MKUKUTA.

3.0 MATEGEMEO YA WATOTO KATIKA USHIRIKI

Mara nyingi ushiriki wa watoto umekuwa unatafsiriwa vibaya. Mfano halisi ni kuhusu

mchango wa watoto katika kazi za nyumbani, mahudhurio darasani, na mchango wa

majibu kwa maswali wanayouliza waalimu, pamoja na watoto wenyewe kuuliza maswali.

Shughuli hizi zinahusiana na dhana ya ushiriki wa watoto kama sehemu ya kuendeleza

ushiriki katika shughuli za jamii. Ni vigumu sana kwa watu wengi kuelewa ushiriki

katika jamii zaidi ya mifano iliyotajwa hapo juu, na tunapojaribu kuhusisha ushiriki

23

katika eneo la kufaidi haki za msingi za raia inawawia vigumu zaidi watu wengi. Kwa

mfano, kule tu kufikiria kwamba watoto waruhusiwe kutoa maoni yao katika kufanya

maamuzi mbalimbali inaweza kuonekana kwamba ni kitu cha kinadharia tu ambacho

hakiwezekani. Ukweli ni kwamba sio kitu kigumu hata kidogo. Kwa ufafanuzi rahisi

zaidi, kikundi cha mashirika mbalimbali ya ushiriki wa mtoto “Inter-Agency Working

Group on Children’s Participation”6 kimeelezea msingi mkuu katika suala hili kwamba:

Haki za kiraia zinaanzia pale mtoto anapozaliwa, wakati mtoto

anaandikishwa katika ofisi ya Uzazi na Vifo, ambapo tendo hili ni msingi

wa kufaidi haki nyingine ambazo ni stahili ya mtoto kama vile kupata

huduma za afya na elimu, ulinzi dhidi ya aina zote za unyonyaji kiuchumi,

na kijinsi, na kutendewa haki wakati mtoto anapotenda kosa au kuvunja

sheria

Mtoto anavyozidi kukua, mchango wake huongezeka na mazingira yanayomsaidia kutoa

mchango huo nayo hubadilika. Hili ni muhimu kueleweka katika Mpango Kazi huu,

ambao umejikita kwenye kusimamia „haki ya watoto kusikilizwa‟ na kupanua wigo wa

jinsi watoto wanaweza kuchangia katika kuandaa mipango na kufanya maamuzi muhimu

katika jamii ya kitanzania kwa ujumla. Kwa kuzingatia maudhui ya haki za binadamu,

ambapo ushiriki wa watoto ni kiini cha haki za binadamu, kuna haja ya kutambua hili

kuwa ni sehemu muhimu ya malezi na makuzi ya watoto, na kujitambua, ambavyo

vinaendana na kujenga uwezo wa kufanya maamuzi na maendeleo ya ari ya kujithamini

na kujiamini.

Kwa mtizamo wa Haki za Binadamu, ambapo ushiriki wa watoto ni miongoni mwa haki

hizo, inabidi itambulike kuwa haki hii ni sehemu ya makuzi na humfanya mtu kujitambua

na kujithamini na pale inapohusishwa na swala la kufanya maamuzi, huwa ni sehemu ya

ukuaji wa ari ya kujiendeleza kwa kujiamini. Kwa ujumla hakuna sababu ya

kutenganisha majukumu ya watu wazima na watoto kama ilivyokuwa siku za nyuma. Ili

kutambua hili, ni budi ifahamike kuwa haki za watoto sio tofauti na zile za watu wazima.

Hivyo basi, wote wanapaswa kufahamishwa haki zao hizo, na watoto wanapaswa

kuamini kuwa watapata haki zao ambazo ni pamoja na:

Kupata taarifa (kuhusu masuala yote yanayowahusu na mengineyo);

Kuweza kupata habari na pia kutafuta habari;

Kuwa na maoni yao na uwezo wa kusambaza maoni hayo yasikike (kwa watoto

wenzao na watu wazima);

Kuwa na uwezo wa kushiriki katika majukumu mbalimbali katika jamii

Kuheshimu maoni ya watu wengine na maoni yao kuheshimiwa/kuthaminiwa ;

Kushiriki kikamilifu katika majukumu na michakato mbalimbali katika jamii;

Kushirikishwa kutoa ushauri katika masuala ya kufanya maamuzi na kuwa

wadau wakuu katika kupitisha maamuzi hayo; na

24

Masuala yao muhimu kuzingatiwa na hivyo kuingizwa kwenye michakato ya

kufanya maamuzi, na wakiwa na taarifa kamili ya maamuzi hayo na matokeo au

athari ya maamuzi hayo.

Yote haya yafanyike kulingana na uwezo wa watoto kuchangia na kushiriki katika

michakato kwa njia ambazo maoni yao yatapewa uzito unaostahili kutokana na uwezo

(kifungu cha 5 cha Mkataba wa Kimataifa kuhusu Haki ya Mtoto, na hili lionekane kwa

mtizamo chanya na kuwa ni mchakato unaolenga kuleta maendeleo na makuzi,

kujitambua na kujieleza.

Mchango huu wa watoto uchukuliwe pia kuwa utazidi

kuongezeka kila wanapopata fursa ya kushiriki na kutoa nafasi kwa kila mtoto kuchangia

kwa uwezo wake. Ni vyema pia kutambua kuwa ukomavu wa watoto katika swala hili

unachangiwa kwa kiasi kikubwa na aina ya taarifa anayopata na kuitumia katika kila

fursa anayoipata na uzoefu anaoukusanya, mazingira, matarajio ya jamii kulingana na

tamaduni, na pia kiwango cha msaada anaoupata kutoka kwa watu wazima na jamii yake.

Utekelezaji na viwango vya ushiriki wa mtoto vinapendekeza; kuhakikisha yafuatayo:

Kwamba masuala yaliyo na manufaa kwa watoto kushiriki ni yale ambayo

watoto wananufaikanayo wakishiriki na yanayotokana na mchango wao,

kimaarifa, kiujuzi na kiuwezo;

Watoto wanahusishwa katika kuandaa vigezo vya kuchagua wawakilishi wao

katika ushiriki

Watoto wana muda wa kujiandaa kushiriki na michakato/mifumo inaandaliwa

kuhakikisha kuwa wanashiriki kikamilifu kutoa maoni yao na kupata ridhaa

kutoka kwa wenzao kwa yale watakayochangia.

Watoto wanashiriki kwa ridhaa yao wenyewe, bila shinikizo, na kwamba wana

uhuru wa kujitoa kwenye ushiriki wakati wowote watakavyoamua wao.

Watoto wanashiriki kwa namna, kiwango na kasi ambayo ni muafaka kulingana

na uwezo wao na matakwa yao.

Majukumu mengineyo ya watoto yanaheshimiwa na kuzingatiwa ili yasiathirike

(kwa mfano majukumu ya nyumbani, shuleni au kazi zao).

Utaratibu na mbinu zinazotumika zijumuishe mambo muhimu na kujengeka

kwenye misingi ya mifumo rafiki kwa watoto iliyopo, maarifa na uzoefu kwa

kuzingatia mazingira ya kijamii, kiutamaduni na mila na desturi.

Msaada kutoka kwa watu wazima katika kujenga maisha ya watoto, (kwa mfano

msaada wa wazazi/walezi na waalimu), unapatikana kuhakikisha kuwa

unahamasisha zaidi ushiriki na kuzingatia ushiriki wa wasichana na wavulana.

4.0 UCHAMBUI WA WADAU, WIZARA NA TAASISI

4.1 Utangulizi

Sehemu hii inazungumzia namna Mpango Kazi huu utakavyotekelezwa kwa kuhusisha

wadau mbalimbali. Kwa ujumla, ili sauti za watoto zisikike na kuthaminiwa kikamilifu,

majukumu mbalimbali yanahusika na watekelezaji ni pamoja na serikali, Asasi zisizo za

kiserikali, na wadau wengine wa maendeleo. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na

Watoto ambayo ndio msimamizi mkuu wa masuala ya watoto itashirikiana na serikali

kuu na idara zake, pamoja na Asasi zisizo za kiserikali kutekeleza mpango kazi huu.

25

4.2 Serikali Kuu na Idara zake

a) Kuandaa sera, ufuatiliaji na tathmini

i) Kuhakikisha kila wizara inaandaa sera husika ambazo zinalenga suala la

kulinda na kutetea haki ya mtoto ya kushiriki.

ii) Kuhakikisha mipango ya utekelezaji wa sera zilizotungwa inaandaliwa na

wizara husika na kutekelezwa ipasavyo.

iii) Kuhakikisha raslimali zinazohitajika zinapatikana kwa ajili ya utekelezaji wa

sera.

4.2.1 Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto

a) Kupanga na Kuratibu

i) Kuhakikisa kuwa Mpango huu wa Ushiriki wa Watoto unapitishwa kupitia

mchakato rasmi kwa muda mfupi iwezekanavyo

ii) Kupanga na kuandaa mkakati wa utekelezaji wa Mpango huu, uratibu,

ufuatiliaji na upimaji wa utekelezaji wake

iii) Kwa kupitia kamati inayojumuisha wizara zote, kukubaliana na wizara

nyingine kuingiza suala la ushiriki wa watoto katika sera, mipango, programu

na miongozo yao.

iv) Kuingia makubaliano na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali

za Mitaa kuwa itaratibu na kusimamia masuala ya ushiriki wa mtoto miongoni

mwa wizara mbalimbali katika ngazi za mikoa na serikali za mitaa. Hili

litahitaji uundwaji wa chombo cha kuratibu katika wizara mbalimbali.

v) Kuratibu ufuatiliaji na kuandaa taarifa za utekelezaji za Haki ya Mtoto ya

Ushiriki na haki nyinginezo zinazohusu ushiriki na utekelezaji wa Sera ya

Watoto, Mkataba wa Kimataifa kuhusu haki za Mtoto na Mkataba wa Afrika

kuhusu Ustawi wa Mtoto

vi) Kuunda mfumo wa kuratibu ushirika wa wadau wote katika utekelezaji na

kuratibu shughuli zote za Mpango Kazi huu.

b) Ushawishi

i) Kutoa mafunzo kwa maofisa wa Maendeleo ya Jamii watakao elimisha jamii

kuhusu Mpango huu wa Ushiriki wa Mtoto.

ii) Kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

na asasi zisizo za kiserikali pamoja na vyombo vya habari kutoa elimu ya

ufahamu kwa wadau wengine (wazazi, watoto, viongozi wa serikali za

vijiji/mitaa, vyombo vya habari na wadau wengine) kuhusu umuhimu wa

ushiriki wa watoto na mbinu za kufanikisha ushiriki huo kikamilifu katika

masuala yanayowahusu watoto wa Tanzania na jamii zao.

iii) Kuendeleza, kuhamasisha, na kuwezesha jamii kuwapatia watoto haki ya

ushiriki na haki nyinginezo

iv) Kupanga na kusimamia kampeni za ushawishi kwa jamii kuhusu Ushiriki wa

Watoto

c) Ufuatiliaji na Takwimu

i) Kufanya utafiti wa ongezeko la kiwango cha ushiriki wa watoto katika

mambo yanayowahusu na kukusanya na kusambaza takwimu

ii) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program zitakazoandaliwa

na wadau mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha ushiriki wa watoto

26

4.2.3 Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

a) Kupanga na Kuratibu

i) Tawala za Mikoa kuratibu mahusiano/mawasiliano kati ya mabaraza ya

watoto ya wilaya na Baraza la Taifa la Watoto na kuhakikisha kuwa mabaraza

haya yanafanya kazi ipasavyo na kuingiza mapendekezo kutoka kwenye

mabaraza haya katika maamuzi na mipango ya halmashauri.

ii) Halmashauri za Wilaya kuandaa taratibu za kuingiza masuala ya watoto katika

mchakato wa mipango ya maendeleo ya wilaya.

iii) Halmashauri za walaya na ngazi za chini za utendaji kuandaa taratibu ambazo

zitawezesha watoto kushiriki katika kufanya maamuzi katika ngazi hizo za

utawala.

iv) Kupanga na kuandaa mkakati wa wizara wa utekelezaji, uratibu, ufuatiliaji na

upimaji wa utekelezaji.

v) Kutoa miongozo ya uingizwaji wa masuala ya/hoja za watoto hasa kuhusu

Ushiriki wao, katika mipango ya maendeleo, utelekelezaji, usimamizi na

tathmini katika ngazi zote

vi) Kuandaa ripoti za utekelezaji za kupelekwa sehemu husika hasa Wizara ya

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto.

b) Ufuatiliaji na Takwimu

iii) Kufanya utafiti wa ongezeko la kiwango cha ushiriki wa watoto na kukusanya

na kusambaza takwimu kwa watekelezaji na wadau wengine

iv) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program zitakazoandaliwa

na wadau mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha ushiriki wa watoto

4.2.3 Wizara ya Fedha na Uchumi

a) Kupanga na Kuratibu

i) Kuandaa miongozo kuhusu namna ya kushiriki na watoto (kwa mfano

uwakilishi wa Baraza la Watoto kutumika) katika kuandaa bajeti na kutenga

fedha na rasilimali nyinginezo (kujadili kwa pamoja na kutoa maoni na

maamuzi) kwa ajili ya kufanikisha ushiriki wa watoto na kutimiziwa mahitaji

yao mengineyo katika ngazi zote.

ii) Kuhakikisha kuwa katika mwongozo wa bajeti ya mwaka kunakuwepo na

mwongozo kuhusu uingizwaji wa shughuli za ushiriki wa watoto na bajeti

kwa ajili ya kutekeleza Mpango Kazi huu inakuwepo na kutumika ipasavyo.

b) Ushawishi

i) Kutoa mafunzo kwa Maofisa Mipango watakaoelimisha wadau ndani ya

wizara na wengineo kwa kushirikiana na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya

Jamii, Jinsia na Watoto, kuhusu namna ya kuandaa bajeti shirikishi kwa

kuzingatia ushiriki wa watoto na kuzingatia hoja na mahitaji ya watoto katika

kufanikisha ushiriki wao katika kuandaa bajeti katika ngazi zote.

c) Ufuatiliaji na Takwimu

v) Kufanya utafiti wa ongezeko la kiwango cha ushiriki wa watoto na kukusanya

na kusambaza takwimu kwa watekelezaji na wadau wengine

27

vi) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program zitakazoandaliwa

na wadau mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha ushiriki wa watoto

4.2.4 Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii

a) Kupanga na Kuratibu

i) Kuandaa sheria na miongozo (kwa kushirikiana na Wizara ya maendeleo ya

Jamii, Jinsia na Watoto) kwa ajili ya wizara kuhusu utekelezaji wa sheria

mbalimbali ikiwepo sheria ya watoto ya mwaka 2009

ii) Kuandaa miongozo na taratibu kuhusu namna ya kufanikisha ushiriki wa

watoto wa makundi yote hasa ya wale wenye ulemavu katika ngazi zote ndani

na nje ya wizara hasa ngazi ya familia, mashuleni, katika jamii na katika

mifumo ya kisheria na utawala. Miongozo hii itasaidia kutafsiri ushiriki wa

watoto katika nyanja za sera na sheria mbalimbali zinazohusu watoto na

kuhakikisha huduma kwa watoto (haswa wale wenye ulemavu)

zinazowaandaa kuweza kushiriki zinaimarishwa

iii) Kusimamia, kufuatilia na kutathmini kiwango cha utekelezaji wa miongozo

mbalimbali ya ushiriki wa watoto wa makundi yote

b) Ushawishi

i) Kutoa mafunzo/semina kwa Maofisa wa Afya na Ustawi wa Jamii watakaoelimisha

wadau wengine kwa kushirikiana na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii,

Jinsia na Watoto, kuhusu namna ya kushirikisha watoto wenye ulemavu katika

mipango ya afya katika ngazi zote (familia, jamii, nk.) kwa kuzingatia haki yao ya

ushiriki.

c) Ufuatiliaji na Takwimu

i) Kufanya utafiti wa ongezeko la kiwango cha ushiriki wa watoto katika

mipango ya afya na ustawi wa jamii katika ngazi zote na kukusanya na

kusambaza takwimu kwa watekelezaji wa wizara na wadau wengine

ii) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program zitakazoandaliwa

na wadau mbalimbali wa afya na ustawi wa jamii kwa ajili ya kufanikisha

ushiriki wa watoto

4.2.5 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

a) Kupanga na Kuratibu

i) Kuandaa sera sheria, mipango na miongozo rafiki kwa watoto (kwa

kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto) kwa ajili ya

wizara na mikakati kuhusu ushiriki wa watoto hasa katika eneo la mitaala,

mbinu za ufundishaji na utawala.

ii) Kuandaa miongozo na taratibu kwa ajili ya Maafisa Elimu wa Wilaya na

viongozi wa shule kuhusu namna ya kuboresha mifumo ya utawala na

uendeshaij wa shule na kufanikisha ushiriki wa watoto wa makundi yote hasa

ya wale wenye ulemavu na namna ya kurasimisha uwepo wa mabaraza ya

watoto shuleni pamoja na mbinu za kuingiza masuala yaliyoibuliwa na watoto

katika mabaraza yao katika mamuzi ya shule kwa mfano kuhusu

miundombinu, ufundishaji na uongozi.

28

iii) Kusimamia, kufuatilia na kutathmini kiwango cha utekelezaji wa miongozo

mbalimbali ya sekta ya elimu na ufundi kuhusu ushiriki wa watoto wa

makundi yote hasa yale ya wale wenye ulemavu.

iv) Kwa kutumia uongozi na taasisi za elimu au shule, kusimamia uanzishwaji na

uendeshwaji wa mabaraza ya watoto ya shule na kuandaa utaratibu

utakaowezesha maoni ya watoto kutoka kwenye mabaraza hayo kuingizwa

kwenye mipango ya shule na menejimenti.

b) Ushawishi

i) Kutoa mafunzo/semina kwa Maofisa Elimu watakaoelimisha wadau wengine kwa

kushirikiana na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, kuhusu

namna ya kushirikisha watoto wa makundi yote hasa wale wenye ulemavu katika

mipango ya elimu katika ngazi zote (familia, jamii, nk.) kwa kuzingatia haki yao ya

ushiriki.

c) Ufuatiliaji na Takwimu

i) Kufanya utafiti wa ushiriki wa watoto katika mipango ya elimu katika ngazi

zote na kukusanya na kusambaza takwimu kwa watekelezaji wa wizara na

wadau wengine

ii) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program zitakazoandaliwa

na wadau mbalimbali kuboresha sekta ya elimu kwa ajili ya kuratibu kiwango

cha ushiriki wa watoto na ufanisi wa mabaraza ya shule na changamoto

zinazoyakabili

4.2.6 Wizara ya Habari, Maendeleo ya Vijana na Michezo

a) Kupanga na Kuratibu

i) Kuandaa miongozo kwa ajili ya vyombo vya habari kuhusu ushiriki wa

watoto na vijana kwenye masuala ya habari na mawasiliano na mikakati

kuhusu ushiriki wa watoto na vijana hasa katika eneo la vyanzo vya habari,

aina ya habari wanayohitaji watoto na vijana, usambazaji wa habari kwa

watoto na vijana unaokidhi mahitaji yao, mbinu za kusambaza habari kwa

watoto na vijana zinazozingatia mahitaji ya makundi mbalimbali ya watoto na

vijana hasa ya wale wenye ulemavu na uendeshaji wa programu mbalimbali

za vyombo vya habari.

ii) Kuandaa miongozo kwa waandaaji wa programu mbalimbali za vyombo vya

habari, waandishi wa vitabu na makala na vipindi vya watoto na vijana

kuhusu namna ya kuboresha na kufanikisha ushiriki wa watoto na vijana wa

makundi yote hasa ya wale wenye ulemavu

iii) Kusimamia, kufuatilia na kutathmini kiwango cha utekelezaji wa miongozo

mbalimbali ya sekta ya habari na utangazaji kuhusu ushiriki wa watoto na

vijana wa makundi yote hasa yale ya wale wenye ulemavu

b) Ushawishi

i) Kutoa mafunzo/semina kwa Maofisa Habari, Wahariri na Waandaaji wa

vipindi na programu mbalimbali watakaoelimisha wadau wengine kwa

kushirikiana na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,

29

kuhusu namna ya kushirikisha watoto wa makundi yote hasa wale wenye

ulemavu katika mipango ya ukusanyaji na usambazaji wa habari hasa ile ya

vyombo vya habari katika ngazi zote (familia, jamii, nk.) kwa kuzingatia haki

ya ushiriki kwa watoto na vijana.

ii) Kwa kuzingatia jukumu lake la mawasiliano, Wizara hii kwa kushirikiana na

Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na wadau wengine, kuandaa

mkakati utakaoboresha juhudi nyinginezo za utetezi wa haki za watoto na

vijana (kama zile zilizoainishwa kwenye „Ajenda ya Watoto‟).

c) Ufuatiliaji na Takwimu

i) Kufanya utafiti wa ushiriki wa watoto katika sekta ya habari katika

ngazi zote na kukusanya na kusambaza takwimu kwa watekelezaji wa

wizara na wadau wengine.

ii) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program

zitakazoandaliwa na wadau mbalimbali kuboresha sekta ya habari na

mawasiliano kwa ajili ya kuratibu kiwango cha ushiriki wa watoto.

4.2. 7 Wizara ya Sheria na Katiba

Utaratibu uliowekwa kwa ajili ya mahakama ya watoto unatoa fursa nzuri kwa watoto

kuweza kusikilizwa katika mahakama na inapaswa kuwa hivyo kwa masuala yote

yanayowahusu watoto.

a) Kupanga na Kuratibu

i) Kuandaa sera, sheria na miongozo kwa ajili ya wizara ambayo inatambua haki

za watoto pamoja na haki ya ushiriki na kuweka mazingira rafiki ya

kurahisisha ushiriki wa watoto katika utoaji huduma kwa watoto (kwa mfano

lugha rahisi inayoeleweka kwa watoto kuhusu mwenendo wa kesi zao

mahakamani na haki ya kusikilizwa) na kuhakikisha wizara nyingine na

wadau wengine wanarekebisha sheria zao ndogondogo na taratibu zao ili

kulinda haki za watoto pamoja na ile ya ushiriki.

ii) Kuandaa miongozo kwa vyombo na taasisi za wizara (kama vile mahakama,

polisi, n.k) na wadau wengine ambao wanashughulika na masuala ya watoto

kuhusu namna ya kuboresha na kufanikisha ushiriki wa watoto wa makundi

yote hasa ya wale wenye ulemavu kwenye kuandaa sera, sheria, mipango,

programu, taratibu na mikakati ya utekelezaji.

iii) Kwa kupitia Kamisheni ya Kurekebisha Sheria kutoa ushauri wa namna ya

kurekebisha sheria zinazohusu uhuru na haki ya watoto kusikilizwa na

kushiriki katika masuala yote yanayohusu maisha yao kama vile ndoa na

ushiriki katika ushauri na upimaji hiari wa UKIMWI na pia kutoa ushauri

kuhusu kuandaa taratibu na miongozo ya namna ya kusimamia Sheria ya

Watoto kwa ajili ya kulinda haki zao.

iv) Kwa kupitia Kamisheni ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, kuboresha

mifumo yake ya kupokea na kufuatilia malalamiko ya watoto, na kuhakikisha

kuwa haki za watoto zinazingatiwa na kupewa uzito unaostahili na watoto

wanafaidi haki yao ya kusikilizwa katika ngazi zote hasa katika kutoa taarifa

na malalamiko dhidi ya udhalilishwaji, unyonywaji na kufanyiwa ukatili.

30

v) Kusimamia, kufuatilia na kutathmini kiwango cha utekelezaji wa sheria, sera

na miongozo mbalimbali ya sekta ya sheria kuhusu haki za watoto na ushiriki

wa watoto wa makundi yote hasa ya wale wenye ulemavu

b) Ushawishi

i) Kutoa mafunzo/semina kwa maafisa, mahakimu (hasa wale wa mahakama ya

watoto), polisi, wataalamu wa kuandaa miswada ya sheria za watoto na

watumishi wengine wa wizara watakaoelimisha wadau wengine kwa

kushirikiana na maafisa wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto,

kuhusu namna ya kufanikisha na kuboresha ushiriki wa watoto wa makundi

yote hasa wale wenye ulemavu

ii) Kwa kuzingatia jukumu lake la kusimamia haki kutendeka, Wizara hii kwa

kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto na wadau

wengine, kuandaa mkakati utakaoboresha juhudi nyinginezo za utetezi wa

haki za watoto katika vyombo vya mahakama, ulinzi na usalama (kama zile

zilizoainishwa kwenye „Ajenda ya Watoto‟)

c) Ufuatiliaji na Takwimu

i) Kufanya utafiti wa ushiriki wa watoto katika sekta ya sheria katika

ngazi zote na kukusanya na kusambaza takwimu kwa watekelezaji wa

wizara na wadau wengine

ii) Kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa program

zitakazoandaliwa na wadau mbalimbali kuboresha sekta ya sheria kwa

ajili ya kuratibu kiwango cha ushiriki wa watoto

iii) Kufanya utafiti kuhusu malalamiko ya watoto kuhusu uvunjwaji wa

haki zao hasa ile ya kusikilizwa na utatuzi wa malalamiko hayo

pamoja na changamoto zinazojitokeza katika kufanikisha ushiriki wa

watoto katika sekta ya sheria

4.2.8 Wadau wa Maendeleo na Asasi Zisizo za Kiserikali

Wadau Wengine wa Maendeleo na Asasi Zisizo za Kiserikali watashiriki katika kujaza

mapengo kwa yale yanayofanywa na serikali katika ngazi zote. Hii ni pamoja na:

i) Kusaidia katika kutafuta rasilimali

ii) Kutoa mafunzo kwa vikundi mbalimbali, pamoja na watoto

iii) Kujenga ufahamu na uelewa kwa makundi mbalimbali kuhusu Haki ya

Watoto ya Ushihiriki na haki nyinginezo

iv) Kutetea haki za watoto pamoja na Haki ya Ushiriki

v) Kushiriki katika majadiliano na katika kufanya maamuzi mbalimbali

yanayohusu Ushiriki wa watoto katika sekta mbalimbali na katika tawala za

mikoa.

vi) Kushiriki katika eneo lingine lolote la Mpango Kazi huu kwa kutumia ujuzi

walionao na rasilimali zao ili kufanikisha kufikia malengo yote ya Mpango

Kazi kwa kufanya kazi kwa karibu sana na serikali

4.2.9 Familia Familia ndio taasisi ya kwanza ya malezi na makuzi ya watoto katika jamii za Tanzania.

Wazazi wana jukumu kubwa la kuhakikisha watoto wanaishi na kukua. Familia

31

itasaidiwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kupitia Idara ya Watoto

katika kutekeleza na kuendeleza ushiriki wa watoto.

4.2.10 Baraza la Watoto la taifa Baraza hili la watoto ndio chombo pekee rasmi ambacho kimeundwa kisheria kwa lengo

la kufanikisha ushiriki wa watoto humu Tanzania. Kitakapoandikishwa rasmi, na

kitakapopata ridhaa ya serikali za mitaa na Asasi Zisizo za Kiserikali, chombo hiki

kitakuwa cha uwakilishi wa watoto katika vyombo vya maamuzi na utekelezaji katika

jamii. Ngazi za chini za serikali za mitaa zinapaswa kuandaliwa kwa kuwezeshwa

kuandaa taratibu kwa watendaji/wadau wote ambao wana nia ya kufanya kazi na

mabaraza ya watoto au kwa niaba ya Mabaraza ya Watoto kwa kutumia Mwongozo wa

Kitaifa wa Mabaraza ya Watoto.

4.2.12 Maoni ya ziada kuhusu miundo na majukumu ya watendaji wakuu

Hapa Tanzania hakuna kamisheni au chombo kingine chochote maalum cha uchunguzi

wa malalamiko ya watoto. Ofisi au chombo cha aina hii kingesaidia kwa kiasi kikubwa

yafuatayo:

i) Kusuluhisha migongano kati ya watoto na watu wazima kuanzia katika ngazi

ya familia hadi ngazi ya mkuu wa nchi

ii) Kuboresha mawasiliano, kusimamia haki za watoto na kuratibu ushiriki

iii) Kushiriki katika utafiti and uundaji wa sera

iv) Kushughulikia malalamiko yanayotokana na mahusiano kati ya watoto na

watu wazima.

v) Kusaidia watu wazima pamoja na watoto na vijana wanaotaka au wenye ari ya

kutaka kuelewa zaidi kuhusu haki za watoto na vijana, na kusaidia serikali na

watu /taasisi rafiki kwa watoto/vijana kufahamu matakwa ya vijana.

vi) Kufanya utafiti ili kupata uelewa zaidi kuhusu mambo muhimu katika maisha

ya watoto na vijana.

vii) Kushauri serikali na wadau wengine kuhusu kufanya yale mambo mazuri tu

yanayofaa kufanyiwa watoto na vijana.

viii) Kama chombo huru cha kupokea malalamiko, kupokea, na pale

inapowezekana kutathmini/kuchambua malalamiko yanayowasilishwa na

vijana au watu wazima kwa niaba ya vijana na kuyapeleka kwa vyombo vya

utatuzi pale walalamikaji wanapotoa idhini yao.

ix) Kufuatilia kwa karibu na makini, kama chombo huru, utendaji wa mabaraza

ya watoto na mabaraza ya shule.

Kuna hisia kuwa ijapokuwa watoto katika nchi nyingine wamepewa fursa ya kuanzisha

mabunge au mabaraza yao ambayo ni nje ya mfumo wa vyombo vya serikali, kuna

mahusiano/mawasiliano kidogo sana kama yapo, kati ya mabaraza ya watu wazima na

mabaraza ya watoto. Vyombo vya aina hii ya uwakilishi wa matakwa ya watoto

vinapaswa pia kuwepo katika mfumo wa serikali katika ngazi zote za serikali na idara

zake. Katika kufanya kazi zake ndani ya serikali, hasa kwa kupitia Kamisheni maalum au

Chombo Maalum cha Kuchunguza Malalamiko ya Watoto, chombo kama hiki kina

uwezo mkubwa wa kufikisha maamuzi au ushauri au mapendekezo muhimu ya

32

maendeleo kutoka kwa wawakilishi wa watoto kwenda kwa watu wazima, mambo

ambayo wangeachiwa wenyewe watoto wasingeweza kuyafikisha kunakohusika.

Hata hivyo, jukumu la Kamisheni au Chombo Maalum cha Kuchunguza Malalamiko ya

Watoto linahitaji kuandaliwa mipango ya kina ili kuwapangia wawakilishi wa watoto

majukumu ambayo yanakidhi mahusiano kati ya viashiria vya sera, sheria, na utawala na

mahitaji muhimu. Kwa hali hiyo, katika Mpango Kazi huu, inapendekezwa kufanyika

utafiti mdogo kuhusu huduma za Kamisheni/ Vyombo Maalum vya Kuchunguza

malalamiko ya watoto vilivyopo duniani kwa ajili ya watoto hasa vile vya Afrika ya

Kusini na nchi ya Ethiopia. Ili kupata taarifa zaidi, kuna haja pia ya kujifunza kutoka

Taasisi ya Chombo Maalum cha Kuchunguza Malalamiko ya Watoto cha Kimataifa,

ambapo Kamisheni ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ya Tanzania ni mjumbe.

Katika taasisi hizi zilizoko ulimwenguni, kuna uwezekano mkubwa wa kupata msaada

utakaoiwezesha serikali yetu kuandaa ratiba ya kuandaa chombo hiki muhimu kwa

watoto. Vyombo vya uwakilishi wa watoto vilivyopo vitakuwa na jukumu kubwa la

kusambaza taarifa kuhusu chombo hiki kipya cha serikali, uundaji wake na hatua za

kuchukua kuelekea kwenye uchaguzi wa Kamishna au kuunda Chombo Maalum cha

Kuchunguza Malalamiko ya Watoto, kuandaa na kutafrisi majukumu ya ofisi hiyo, na

ratiba ya uteuzi wa Kamishna au uundaji wa chombo hicho maalum na muda wa kuanza

kazi.

Mabaraza ya Watoto nayo yana jukumu kubwa la kuiwezesha Wizara ya Maendeleo ya

Jamii, Jinsia na Watoto kutekeleza jukumu hili na mchakato mzima wa kuanzisha

Kamisheni ya pamoja na kusambaza taarifa za Mpango kazi huu ambao umeandaliwa

kwa ajili ya kulinda haki za watoto. Kwa vile lengo kuu la Mpango Kazi huu ni

kuhakikisha kwamba watoto wanashiriki kikamilifu katika mambo yote yanayohusu

maisha yao, ni dhahiri kwamba jukumu kubwa mojawapo kwa mabaraza ya watoto ni

kuanzisha jukwaa la kudumu litakalotumika kubadilishana uzoefu katika kusimamia

maendeleo na ufanisi katika utekelezaji wa Mpango kazi huu wa Kitaifa.

5.0 MKAKATI

5.1 Mwelekeo

Mpango Kazi huu unaangalia sehemu kuu nne:

1. Kuelimisha wadau wote pamoja na watendaji wa shughuli za serikali na

kijamii kuhusu sera, sheria, kanuni na taratibu mbalimbali pamoja na

makubaliano ya serikali yetu ya Kikanda na Kimataifa kuhusu haki ya

mtoto ya kusikilizwa na kushiriki katika mambo yote yanayomhusu.

2. Kuandaa/Kujenga mfumo wa kitaifa wa ushiriki wa watoto ambao

umejengeka kwenye misingi ya usawa, demokrasia na haki, misingi

ambayo inajali haki ya mtoto ya kusikilizwa na kushiriki.

3. Kuhakikisha taratibu na miongozo ya namna ya kutekeleza mfumo huo wa

Ushiriki wa Watoto pamoja na vyombo vya kufanikisha utendaji kwa

kufuata mfumo huo vinaandaliwa na kufahamika kwa wadau wote

4. Kuandaa utaratibu wa kuratibu utekelezaji wa Mpango kazi huu kwa

kugawa majukumu kwa wadau mbalimbali na kuelekeza namna ya

33

kuratibu na kutathmini utekelezaji kwa kuhusisha watoto na vyombo vyao

vya uwakilishi.

Kwa kiasi kikubwa Tanzania ina mazingira mazuri kisera na kisheria ya Ushiriki wa

watoto. Kwa kuzingatia uwepo wa mazingira haya, vyombo kadhaa vya ushiriki wa

watoto ikiwa ni pamoja na mabaraza ya watoto vimeshaundwa na tayari vinatumika japo

kwa kiasi kidogo bado. Kwa ujumla bado ushiriki wao haujaonekana vya kutosha

kwenye kuandaa mipango ya maendeleo ya sekta mbalimbali, hata zile ambazo watoto

wanahusika moja kwa moja. Maamuzi mengi kuhusu maisha yao na jamii kwa ujumla

yanafanywa bila kushirikisha watoto kwa visingizio mbalimbali pamoja kile cha

kutokujua namna ya kushirikisha watoto hasa wale wenye umri mdogo. Mila na desturi

nazo zinachangia kwa kiasi kikubwa kuwabagua watoto katika ngazi za maamuzi kuanzia

ngazi ya familia kwa visingizio kuwa watoto hawajui kitu wala hawajijui. Hali hii

imekuwa mbaya zaidi pale ambapo Tanzania imekuwa haina chombo maalum cha

kuchunguza malalamiko ya watoto ijapokuwa wako watetezi wengi wa haki za watoto.

Kwa ujumla serikali imeingia mikataba ya Kikanda na Kimataifa kuhusu suala hili la

kufanikisha ushiriki wa watoto na mikataba hii imasaidia kutoa miongozo mbalimbali

kuhusu utatuzi wa suala hili. Mpango kazi huu unatambua yote haya na ukamilifu wake

umezingatia sera, sheria, mikataba mbalimbali ambayo serikali yetu imeridhia pamoja na

hali halisi ya mazingira ya kitanzania kiuchumi, kijamii, kisiasa na kiutamaduni.

Ili kuhakikisha malengo na matarajio ya Mpango Kazi huu yanafikiwa, raslimali watu na

fedha zinahitajika na kwa hali hiyo ni jambo la busara kwa kila mdau kuandaa bajeti

inayotosheleza kwa majukumu yake katika kuwajibika ipasavyo. Kwa hali hiyo, sehemu

muhimu na ya awali ya maandalizi ya utekelezaji wa Mpango huu ni kuandaa raslimali za

kutosha kuweza kumudu shughuli zote za utendaji kuhusu mchakato mzima wa

kuhakikisha ushiriki wa mtoto unakuwa wa kiwango cha hali ya juu na wa kudumu kama

malengo na madhumuni ya Mpango Kazi huu yanavyofafanua.

5.3 Lengo na Madhumuni

5.3.1 Lengo/Madhumuni ya jumla

Lengo na Madhumuni ya Mpango Kazi huu ni kujenga mfumo wa kushirikiana pamoja

na watoto na kutoa mwongozo bayana kuhusu umuhimu wa ushiriki na michango ya

watoto katika mambo yote yanayowahusu na katika mazingira rafiki; pamoja na

kufafanua taratibu na kanuni za namna ya kushiriki pamoja na watoto katika ngazi

mbalimbali na katika maeneo yote ili kuhamasisha utetezi na usimamizi wa haki ya

watoto ya kusikilizwa miongoni mwa wale wenye madaraka na wadau mbalimbali.

5.3.2 Madhumuni Mahsusi

Ili kufikia lengo hili kuu, malengo mahsusi yafuatayo yanahusika:

i. Kutoa ufafanuzi kuhusu suala zima la matakwa na umuhimu wa mchango wa

watoto na ushiriki wao katika masuala yote yanayowahusu katika ngazi zote;

ii. Kutoa mwongozo na taratibu kuhusu jinsi ya kushiriki na watoto katika mazingira

ya aina zote;

34

iii. Kuhamasisha juhudi za kuandaa mazingira rafiki na fursa kwa watoto kushiriki

katika ngazi za familia, jamii na katika ngazi ya taasisi na mifumo mbalimbali;

iv. Kutoa fursa za kujenga mahusiano ya karibu na mshikamano kati ya watetezi wa

haki za watoto ndani ya serikali na idara zake, asasi zisizo za kiserikali, na

mashirika ya wadau wa maendeleo, na;

v. Kutoa mwongozo wa utaratibu wa ushiriki wa watoto humu Tanzania na kukuza

ushiriki huo kufikia kiwango cha juu hadi kufikia kuingizwa kwa haki zao za

kiraia, katika masuala yote yanayowahusu wao na katika kushiriki kufanya

maamuzi katika mambo yanayohusu maisha yao na ya jamii yao kwa kuzingatia

demokrasia halisi kwenye uongozi, utawala na utendaji ili kuboresha maisha yao.

5.3 Bango Kitita (Mpango wa Utekelezaji)

USHIRIKI WA MTOTO KITAIFA

LENGO VIASHIRIA VYA MATOKEO

Output Indicators SHUGHULI MUDA JUKUMU

Maendeleo

ya Mpango

wa Kitaifa

wa Ushiriki

wa Mtoto

Uwepo wa Mpango

wa Kitaifa wa

Ushiriki wa Mtoto

Mpango wa Kitaifa

wa Ushiriki wa

Mtoto uliochapishwa

katika Kiswahili na

Kiingereza

Rasimu ya Mpango wa

Kitaifa wa Ushiriki wa

Mtoto

Rasimu ya Mpango wa

Kitaifa wa Ushiriki wa

Mtoto uliothibitishwa na

Kamati ya pamoja ya

Baraza la Mawaziri ili

kuwasilishwa katika

Baraza la Mawaziri.

Rasimu ya Mpango wa

Kitaifa wa Ushiriki wa

Mtoto kuthibitishwa na

Baraza la Mawaziri.

Mpango wa Kitaifa wa

Ushiriki wa Mtoto wa

Kiswahili na Kiingereza

kuchapishwa.

Kuwasilisha Rasimu ya Mpango wa Kitaifa

wa Ushiriki wa Mtoto kwenye kamati ya

pamoja na Baraza la Mawaziri kwa ajili ya

kuthibitishwa.

Kutafsiri na kuchapisha matoleo ya Mpango

wa Kitaifa wa Ushiriki wa Mtoto.

Kuchapisha nakala za Kiingereza za Mpango

wa Kitaifa wa Ushiriki wa Mtoto ndani ya

miezi mitatu ya kuthibitishwa.

Kuchapisha nakala za Kiswahili za Mpango

wa Kitaifa wa Ushiriki wa Mtoto ndani ya

miezi mitatu baada ya kukamilika kwa

tafsiri.

Machi 2014

Mei 2014

Julai 2014

WMJJW

Maafisa wa

Serikali,

asasi za

Kiraia,

watoto na

Jamii

kuelewa na

kutekeleza

Maafisa wa Serikali,

asasi za Kiraia,

watoto na Jamii

wanatambua na

kuelewa pamoja na

kupendezewa na

Mpango wa Kitaifa

wa Ushiriki wa

Mpango wa Kitaifa wa

Ushiriki wa Mtoto

kusambazwa katika ngazi

zote

Shughuli za kukuza uelewa

kufanyika

Kusambaza Mpango wa Kitaifa wa Ushiriki

wa Mtoto katika ngazi zote

Kuinua uelewa juu ya yaliyomo kwenye

Mpango wa Kitaifa wa Kumshirikisha Mtoto

Kutengeneza ujumbe rahisi unaowasilisha

Novemba

2014

kuendelea

WMJJW

and

OWMTM

SM

pamoja na

wadau

36

Mpango wa

Kitaifa wa

Ushiriki wa

Mtoto.

Mtoto.

Maafisa wa Serikali,

asasi za Kiraia,

watoto na Jamii

kutumia Mpango wa

Kitaifa wa Ushiriki

wa Mtoto.

Mpango wa Kitaifa wa

Ushiriki wa Mtoto

kusambazwa katika

ujumbe uliorahisishwa

sehemu za Mpango wa Kitaifa wa Ushiriki

wa Mtoto kwa Kiswahili na Kiingereza kwa

kutumia vyombo vya habari na njia zingine

za mawasiliano.

Kushirikiana na watoto ili kuunda vipengele

rafiki vya mpango huo

Kanuni na

taratibu za

Sheria ya

Mtoto

zizingatie

haki ya

mtoto

kusikilizwa

na kushiriki

katika

masuala

yanayomuat

hiri katika

taasisi

mbalimbali.

Kuwapo kwa kanuni

na taratibu za sheria

ya mtoto

zinazoelekeza

utekelezaji wa

michango ya watoto

katika masuala ya

kisheria

yanayowahusu

watoto.

Michango iliyokusanywa

katika kutengeneza kanuni

na taratibu za sheria ya

mtoto.

Kanuni na taratibu za

sheria ya mtoto

zilizotengenezwa.

Usambazaji wa Kanuni na

taratibu za sheria ya mtoto.

Kuwa na mashauriano na kamati

za/mawaziri husika na Idara za serikali,

Mashirikia yasiyo ya kiserikali na wadau wa

maendeleo kujadili maeneo ya Sheria ya

Mtoto inayohitaji ufafanuzi wa mchango wa

mtoto na ushiriki wao katika masuala

yanayowahusu.

Kutengeneza kanuni na taratibu

zinazoongoza namna ya utekelezaji wa

ushiriki wa mtoto katika michakato

mbalimbali.

Kusambaza kanuni na taratibu za sheria ya

mtoto zinazoongoza namna ya utekelezaji wa

ushiriki wa mtoto katika michakato

mbalimbali.

Desemba

2014

WAUJ,

WSK

WMJJW,

OWTMS

M na

wadau

wengine.

Kushiriki katika Mipango ya Familia

Lengo Matokeo Output Shughuli Muda Jukumu

Kutangaza

na

kutambua

umuhimu

Watoto

wanashiriki

katika

maamuzi ya

Wazazi na walezi

kuhitaji mchango

na ushiriki wa

watoto katika

Kuinua uelewa wa haki za watoto wote kuchangia na

kushiriki katika maamuzi ya masuala yanayowahusu katika

ngazi ya familia kupitia programu za mafunzo ya jamii.

Julai 2014

na

kuendelea

WMJJW, Idara

yaUstawi wa

Jamii, Idara ya

Maendeleo ya

37

wa ushiriki

wa watoto

na

michango

yao katika

ngazi ya

familia.

kifamilia

katika masuala

yanayowahusu.

maisha ya familia.

Mafunzo ya mbinu

za stadi maisha

yanayohusisha

mawasiliano ya

mtoto, mzazi na

mlezi na uhusiano

kuboreshwa

Kuanza kwa

mitandao ya unasihi

wa Mzazi-mtoto

Utendaji mzuri wa

programu

zinazowapa wazazi

na walezi

kuwashirikisha

watoto katika

masuala muhimu ya

familia.

Kutumia programu za mafunzo ya jamii na vyombo vya

habari kuwahamasisha wazazi/walezi kushiriki katika

shughuli zingine ambazo watoto hushiriki mfano shuleni na

katika mabaraza ya watoto.

Watoto kutegemea watu wazima ili kuwaongoza,

kuwafunza na kuwalinda. Watoto Kufahamishwa kwamba

wanaweza kueleza hisia zao zilizo nzuri au mbaya katika

mazingira rafiki.

Kujumuisha mawazo ya watoto na uzoefu wao na

kuwashirikisha katika kuunda vitu vya kimalezi katika njia

chanya, uhusiano usio wa kihasama.

Kuwaandaa watoto kuwa washauri na wachangiaji katika

kampeni za kuuelewesha umma katika kutengeneza vifaa na

ujumbe mbalimbali kukuza uhusiano usio wa kihasama kati

ya watoto na wazazi na walezi.

Kuendesha mafunzo ya stadi za mawasiliano na mahusiano

ya mtoto na mzazi/ mlezi.

Kuanzisha mtandao wa unasihi wa mzazi-mtoto kwa

kushirikiana na Mashirika yasiyo ya Kiserikali yaliyo na

uzoefu katika eneo hili.

Kutumia programu za mafunzo ya umma na fursa za

vyombo vya habari kuzipa habari familia kuhusu mchango

unaopatikana kutokana na ushiriki wa watoto kwa kuonesha

faida zinazopatikana.

Jamii na asasi

za kiraia.

Ushiriki katika masuala ya Kijamii na Kidemokrasia

LENGO MATOKEO Output SHUGHULI MUDA JUKUMU

Kuunga Baraza la Baraza la Watoto la Kusajili Baraza la Watoto la Jamhuri ya Muungano wa Desemba WMJJW kwa

38

mkono

urasimishaji

wa Baraza la

Watoto la

Jamhuri ya

Muungano ya

Tanzania.

Watoto la

Jamhuri ya

Muungano

wa Tanzania

linafanya

kazi nchi

zima.

Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania kusajiliwa na

kutambuliwa kisheria.

Katiba ya Baraza la

Watoto la Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania

kufanyiwa marekebisho.

Kurekebishwa kwa

Mwongozo wa kitaifa wa

Baraza la Watoto la

Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania.

Watoto wote kushiriki

katika ufanyaji kazi wa

Baraza la Watoto la

Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania.

Tanzania na kutoa vyanzo madhubuti vya kufadhili mfumo

kifedha.

Kurekebisha upya, kuipitisha na kuhakikisha inafanya kazi

katiba ya Baraza la Watoto la Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania na kuingiza mambo mazuri na msingi kutoka

katika Mashirika yasiyo ya Kiserikali.

Kuboresha miongozo ya mwaka 2004, kuipitisha na

kutekeleza muongozo ulioboreshwa kwa kuzingatia mambo

mazuri kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali.

Kufanya chaguzi za kila mwaka za wawakilishi wa

mabaraza ya watoto katika ngazi zote.

Kuimarisha mabaraza yanayofanya kazi katika vijiji, miji,

wilaya na mikoani.

Kuwaelimisha watoto na jamii kuhusu Baraza la Watoto la

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na majukumu yake.

Kuandaa mfumo wa mgawanyo wa vyanzo vya fedha kwa

mabaraza ya wilaya kutokana na taratibu za matumizi za

serikali za mitaa

Kuwafunza watoto namna ya kushiriki katika masuala

yanayowahusu katika ngazi zote na hasa katika mabaraza ya

watoto (kufanyika sambamba na kuimarisha mifumo na

chaguzi)

Kutengeneza form ya kitaifa ya mzazi kukubali mtoto

kushiriki katika shughuli za Baraza la Watoto la Jamhuri ya

Muungano wa Tanzania.

2014 na

kuendelea

kushirikiana

na wadau wa

maendeleo na

mashirika

yasiyo ya

kiserikali.

39

Maamuzi

katika jamii

na utawala

yanazingatia

mawazo na

maoni ya

watoto

Mabaraza ya

watoto

kufanya kazi

katika vijiji,

ngazi za

mitaa, wilaya

na mikoa.

Mawazo ya

watoto

kuingizwa

katika

mipango wa

maendeleo

na yana

shawishi

ufanyaji

maamuzi.

Mabaraza ya watoto

kuimarishwa katika vijiji

vyote, ngazi za mtaa,

wilaya na mikoa.

Chaguzi za wawakilishi

wa Baraza la Watoto la

Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania kutoka vijiji

vyote, ngazi za mitaa,

wilaya, na mikoa

zinazofanyika mara kwa

mara.

Masuala yanayoibuliwa na

watoto kuingizwa katika

mipango ya serikali za

mitaa na michakato ya

mipango ya kitaifa ya

serikali.

Kuhusisha watoa mafunzo katika Nyanja ya ushiriki wa

watoto kutoa mafunzo kwa viongozi wa serikali za mitaa,

wafanyakazi wa maendeleo ya jamii, maofisa wa mashirika

ya kijamii na maofisa wa mashirika yasiyo ya kiserikali na

wadau.

Kuwapa mafunzo viongozi wa serikali za mitaa hasa

wafanyakazi wa maendeleo ya jamii, maofisa wa polisi,

maofisa wa mahakama na wengine watakaohusiana na

watoto, jinsi ya kushughulikia masuala yanayowahusu

watoto, namna ya kutumia mwongozo wa kitaifa wa

ushiriki wa watoto.

Kuwapa mafunzo wafanyakazi wa maendeleo ya jamii,

asasi za kiraia na wafanyakazi wa taasisi zisizo za kiserikali

kuhusu njia za kukuza ushiriki wa watoto katika masuala ya

kijamii na serikali za mitaa.

Kutetea masuala husika kwa kuyafanyia kazi kama sehemu

ya maswala ya kitaasisi.

Kutetea ushiriki wa watoto na vijana katika kuandaa na

kupita mipango ya bajeti na maendeleo ya serikali za mitaa

na manispaa pamoja na;

Mipango ya serikali za mitaa, sheria ndogondogo na

maamuzi mengine ya kisiasa na kiutawala yanayohusu

maisha ya watoto.

Kuishawishi Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za

Mitaa, kuwa na namna ya kuingiza mawazo ya watoto na

sauti zao katika utawala

Kuimarisha uratibu, usimamizi na utoaji taarifa na mrejesho

Desemba

2014 na

kuendelea

WMJJW,

Wizara ya

Serikali za

Mitaa na

OWMTMSM

ikisaidiwa na

mashirika

yasiyo ya

kiserikali na

wadau wa

maendeleo.

40

wa ushiriki wa watoto katika serikali za mitaa. Hii inaweza

kufanyika kwa kukubali mandalizi sambamba au maandalizi

ya baadaye ya maamuzi ya chini yanayotoa wigo mpana wa

ushiriki wa watoto kwa mfano katika toleo rafiki la

Vikwazo vya serikali na fursa za maendeleo. (i.e. watoto

wanashirikishwa katika mipango ya serikali za mitaa kupitia

fursa na changamoto za maendeleo).

Kuelekeza wafanyakazi wa maendeleo ya umma, taasisi za

kiraia, na maofisa wa mashirika yasiyo ya kiserikali kufuata

viwango vya kitaifa vya maadili katika kuwashirikisha

watoto.

Kutawanya na kuwapa mafunzo wadau kutumia kieleekezi

cha taifa ushiriki wa mtoto.

Maofisa wa

serikali za

mitaa

(maafisa

maendeleo ya

jamii na

ustawi wa

jamii, taasisi

za kirai na

wafanyakazi

wa mashirika

yasiyo ya

kiserikali

wanakuza

ushiriki wa

watoto katika

masuala ya

kijamii na

kiutawala

Maafisa

maendeleo

ya jamii,

ustawi wa

jamii na

taasisi za

kiraia,

maofisa wa

mashirika

yasiyo ya

kiserikali

wanashirikia

na na watoto

katika

masuala ya

kijamii na

kiutawala.

Maafisa maendeleo ya

jamii, ustawi wa jamii,

asasi za kiraia, na

watumishi wa mashirika

yasiyo ya kiserikali

kupewa mafunzo ya

kutetea na kukuza ushiriki

wa watoto katika jamii na

utawala.

Maafisa maendeleo ya

jamii, ustawi wa jamii,

asasi za kiraia na

wafanyakazi wa mashirika

yasiyo ya kiserikali

waliopewa semina elekezi

juu ya viwango vya kitaifa

vya ushirki wa mtoto na

maadili ya namna ya

Kutoa semina elekezi kwa wafanyakazi wa maendeleo ya

jamii, ustawi wa jamii, asasi za kiraia na wafanyakazi wa

mashirika yasiyo ya kiserikali juu ya viwango vya kitaifa

vya ushiriki wa mtoto na maadili ya namna ya kushiriki na

watoto katika jamii na masuala ya kiutawala. .

Desemba

2014

WMJJW,

WAUJ

ikishirikiana

na mashirika

yasiyo ya

kiserikali

wadau wa

maendeleo.

41

katika ngazi

mbalimbali.

kushughulika na watoto.

USHIRIKI MAZINGIRA YA SHULE:

Lengo Matokeo Output Shughuli Muda Jukumu

Kukuza

ushiriki wa

watoto na

haki ya

kusikilizwa

katika

mfumo wa

elimu na

utawala.

Watoto

wanachangia

katika

kuandaa na

kutekeleza

mipango ya

shughuli za

shule.

Mambo

yanayowahus

u watoto

kuingizwa

katika

maamuzi ya

uongozi wa

shule.

The National Costed

Tathmini ya

mchango wa watoto

na ushiriki wao

katika mambo ya

shule kufanyika.

Taratibu za uongozi

na utawala wa shule

kujumuisha

mawasilisho ya

watoto katika

utawala wa shule na

michakato ya

kufanya maamuzi.

Mabaraza ya shule

kuanzishwa kwenye

shule zote na vyuo

vya ufundi na wa

watoto

kuimarishwa.

Ushiriki, uratibu,

utoaji taarifa

kutengenezwa na

kuimarishwa

Walimu na

Kanuni na taratibu za Sheria ya Mtoto zielekeze michakato mbalimbali ya

ushirki wa mtoto izingatie mashauriano ya watoto waliopo shuleni kama

kundi na pia kuhakikisha kuwa kuna kumakinika katika mawazo ya mtoto

mmoja mmoja kuhusiana na maamuzi ya mtu mmoja juu ya elimu.

Michakato itatekelezwa kuhakikisha kwamba juhudi zipo katika kuangazia

masuala yanayoibuliwa na watoto kwa njia salama naya siri hasa katika

masuala ya vurugu na unyanyasaji shuleni.

Kutoa mamlaka kwa shirika la lisilo la kiserikali lenye uzoefu katika haki

za watoto na elimu kufanya tathmini ya ushiriki wa mtoto katika shule za

msingi na sekondari.

Kuwafunza wakaguzi wa shule jinsi ya kupitia tena taratibu za uongozi na

utawala wa shule ili zihusishe ushiriki wa watoto katika uongozi wa shule

na michakato ya maamuzi.

Kuandaa mtaalamu kuandaa kielekezi kinachoweza kutumika kuimarisha na

kurasimisha mabaraza ya shule katika shule zote na vyuo vya ufundi kitaifa.

Kuandaa miongozo ya utendaji wa mabaraza ya shule. Kuhakikisha kuwa

mabaraza ya elimu ya wilaya yanawajumuisha watoto katika ujumla wa

mipango ya shule-ikiungana na mpango ya maendeleo ya kijiji.

Kuongeza uungaji mkono kwa klabu za Tuseme, vyama mbalimbali

vilivyoko shuleni- kuhimiza klabu za vijana na kujihusisha na vikundi rika

vya kujitambua ili kuinua uelewa na kufanya eneo la shule kuwa mazingira

salama.

Kuhakikisha kwamba muunganiko kati ya watoto wasio mashuleni na

Machi

2015

OWMTMSM

na Wizara ya

Elimu na

Mafunzo ya

Ufundi

42

wafanyakazi

waliofunzwa njia za

kuwashirikisha

watoto.

vikundi vya watoto walio mashuleni na klabu umefanywa ili kuzaa matunda

mazuri.

Kuendeleza ushiriki tendwa wa mtoto, uratibu na utoaji taarifa baina ya

mabaraza ya watoto na uongozi wa shule.

Kuwafunza walimu na wafanyakazi wa shule katika njia na namna ya

kuwashirikisha watoto.

Ushriki katika mazingira ya Ulinzi wa Mtoto

Lengo Matokeo Output Shughuli Muda Jukumu

Mifumo yote

ya Ulinzi wa

Mtoto na

huduma za

Ulinzi wa

mtoto lazima

izingatie na

kutilia

maanani haki

ya mtoto ya

kusikilizwa na

kuheshimu

mawazo ya

mtoto.

Mpango

tendaji wa

kitaifa kwa

watoto walio

katika

mazingira

hatarishi

(2011-2015)

na kuibua

Mifumo ya ulinzi

mtoto kufanya kazi

katika ngazi zote.

Watoto, pamoja na

watoto walio katika

mazingira ya

hatarishi kuchangia

katika maamuzi ya

masuala

yanayohusu

usalama wao.

Serikali na maafisa wa

mashirika yasiyo ya kiserikali

kufunzwa kuunda timu za ulinzi

wa mtoto (kwa watoto

wanaoishi mitaani, watoto

wanaofanya kazi na watoto

walioambukizwa na wanaoishi

na virusi vya UKIMWI.

Shughuli mbalimbali za kujenga

uelewa zilizofanyika.

Mifumo ya kuripoti na kutoa

rufaa kwa watoto walio katika

hatari ya kunyanyaswa au

mazingira kufanyiwa ukatili au

waliofanyiwa ukatili.

Rasilimali za kutekeleza

mipango wa ulinzi wa mtoto

kutolewa.

Kanuni za Sheria ya mtoto iweke michakato ya

kuhakikisha kuwa sheria zote zinazomlinda

mtoto, mifumo ya ulinzi, huduma na programu za

ulinzi wa mtoto zinazingatia sauti za watoto na

maoni ya watoto katika kila jitihada za kumlinda

mtoto.

Maoni ya watoto lazima yazingatiwe na kutiliwa

maanani katika masuala yanayowahusu pamoja

na mapendekezo yao kwa ajili utatuzi madhubuti.

Maoni yao yasitumike tu kama taarifa za utafiti.

Kuhakikisha ushiriki wa mtoto ni suala la

kikanuni la kila mpango wa serikali kulinda na

kuchukua hatua kwa vitendo vya ukatili dhidi ya

watoto. Kuwapo kunamaanisha kuwa haki za

mtoto zinasikika na mapendekezo yao juu ya

utatuzi madhubuti yanaaksiwa katika viashiria

vinavyotumiwa na mpango kazi wa serikali.

Kuhakikisha kuwa haki za mtoto za kusikilizwa

zinakuwa miongoni mwa viwango vya chini vya

taratibu za programu za ulinzi wa mtoto.

Kutoa mamlaka na kufanya utafiti na watoto

Julai 2014

na kuendelea

WAUJ,

WMJJW

na wadau

43

programu za

kijamii za

kuwalinda

watoto

zinatunza haki

ya mtoto ya

kusikilizwa na

kukuza kwa

njia chanya

ushiriki wa

mtoto.

kuhusu njia wanazozipendekeza katika kuripoti

ukatili katika mazingira tofauti.

Kuhakikisha kuwa kuna taratibu kwa mtoto

kuripoti ukatili na unyanyasaji salama na kwa

ujasiri.

Kuwekeza katika kujenga mfumo wa siri wa

kutoa msaada, taarifa zinazojikita katika jamii na

misada ya kijamii. Kutoa njia za jinsi ya

kuwasiliana kwa hali ya juu kwenye mashule,

majengo ya kijamii na maizingira ya taasisi

mbalimbali.

Kuweka mfumo imara wa kuripoti katika mifumo

ya kitaasisi ili kwamba watoto wanaweza kutoa

taarifa kwa chombo kimoja wakati uonevu au

unyanyasaji unapojitokeza au pale mtoto

anapotishwa.

Kuhakikisha watoto wana uwezo wa kupata

utetezi huru na njia za kutoa malalamiko katika

miktadha mbalimbali.

Kufanya utafiti kubaini vizuizi vya watoto katika

kutafuta misaada kwa mfano ukosefu wa usiri au

kukosa mfumo mzuri wa kupata msaada kwa

makundi fulani ya watoto wakiwemo watoto

wenye ulemavu na waliokosa fursa (albino n.k)

Kutumia fedha iliyopo kusaidia kuunda na

kuimarisha uwezo wa vikundi rika vya vijana na

vikundi vinavyoongozwa na watoto na mashirikia

yanayojishughulisha na kukomesha vitendo vya

44

unyanyasaji kwa watoto ili viweze kufanya kazi

kufuatilia na kuripoti matendo mabaya katika

jamii yao.

Kufanya utafiti juu ya maoni ya watoto na uzoefu

wao katika matukio ya kikatili na mahusiano

chanya na mazingira na kuyahusisha katika

programu za mafunzo.

Kushirikisha watoto katika kuunda uhusiano

rafiki, usio wa kikatili wa vifaa vya kujifunza

kwa watumishi wanaojishughulisha na watoto.

Pale ambapo kuna timu za wilaya za kumlinda

mtoto, kuimarisha uratibu, usimamizi na kuwa na

namna ya kuwawezesha watoto kuripoti ili wawe

na taarifa na kujua ni wapi waende ili kupata

msaada katika jamii zao.

Kuhakikisha ushiriki wa mtoto katika kupanga,

kusimamia na kutathmini programu za ulinzi wa

kijamii kwa mtoto na kuhakikisha kuwa

muunganiko unakuwepo na vyombo vya kisheria

vyenye wajibu wa kuitika haraka katika masuala

ya watoto na ukiukwaji wa haki zao.

Kutambulisha mafunzo ya haki za mtoto yenye

moduli za ushiriki na ulinzi wa mtoto, katika

mafunzo ya kazi na kozi za vyuo vikuu kwa

wanafunzi wa ulinzi wa watoto, elimu iliyo wazi

na watu walio na wajibu wa kikazi karibu zaidi na

watoto (matibabu ya watoto, sheria etc).

Watoto na vijana watahusishwa katika kupanga,

45

kuunda, kutekeleza na kutathmini mipango

tendaji ya kitaifa inayohusiana na haki ya

kulindwa katika jamii. Lazima wawe wadau

wakuu katika utekelezaji wa mpango ili

utekelezaji uendane na watoto wenyewe.

Kukuza uelewa wa haki za watoto walio katika

mazingira magumu/hatarishi.

Kuanzisha na kuendeleza program endelevu za

kukuza na kuinua uelewa kwa wafanya maamuzi

juu ya faida na manufaa ya ushiriki watoto.

Kusisitiza ukweli kwamba masuala

yanayoawaathiri watoto ni mtambuka.

Maofisa wa serikali za mitaa (maofisa wa

maendeleo ya jamii na maafisa wa ustawi jamii),

maofisa wa vijiji, kata kufunzwa namna ya

kuinua ushiriki wa watoto katika kamati za

watoto wanaoishi katika mazingira magumu na

katika programu za ulinzi unaojikita katika jamii.

Kuboresha ushirkiano kati ya kamati za watoto

wanaoishi katika mazingira magumu na mifumo

ya serikali za mitaa na kuhakikisha kuna njia za

kuwashirikisha watoto.

Kuwafunza maofisa wa serikali na wa mashirika

yasiyo ya kiserikali kuanzisha klabu za ulinzi wa

mtoto na kamati (kwa ajili ya watoto wanaoishi

mitaani, wanaofanya kazi na wale

walioambukizwa na wanaosishi na virusi vyaa

UKIMWI).

46

Kuimarisha njia ya utoaji taarifa wa watoto

wanaokumbana na vitendo vya kikatili na hali za

unyanyasaji katika jamii zao.

Kutoa rasilimali za kutekeleza mfumo Awa ulinzi

kwa mtoto.

Watoto

waliokinzana

na sheria

kushiriki na

kuchangia

maamuzi juu

ya michakato

ya kisheria ya

mambo

yanayowahus

u.

Haki za

kisheria za

watoto

kusikilizwa na

kutiliwa

maanani

katika

masuala ya

kimahakama.

Utaratibu wa

kisheria kuhusu

watoto kushirikisha

watoto husika

katika michakato

yote.

Wanasheria

wanaotoa huduma

za kisheria kwa

watoto bure

wnatumia ujuzi na

maadili ya ushiriki

wa mtoto wakati

wakiwawakilisha

watoto.

Muongozo wa kushiriki watoto

waliokinzana na sheria

kutengenezwa.

Watoto kupata taarifa kuhusu

haki zao za kisheria na haki ya

kushirikishwa katika maamuzi

na katika michakato ya kisheria

inayowahusu.

Watoto waliokinzana na sheria

wapate huduma za kisheria

bure.

Kanuni za Sheria ya mtoto zihakikishe watoto

watoto wanaweza kushiriki katika michakato ya

kisheria ili waweze kuelezea maoni na mawazo

yao kwa uwazi kwenye mambo yanayowahusu

mfano kutengena kwa wazazi, kuasiliwa, na pale

ambapo mtoto ni shahidi katika masuala ya kesi

za jinai.

Kuwataka wote wanafanya kazi na watoto

waliokinzana na sheria wnato uzito unaostahiki

kwa mawazo ya watoto kwa kungalia umri na

uwezo wao wa kufikiri. .

Maboresho ya mfumo wa sheria za

zinazozungumzia watoto waliokinzana na sheria

yahakikishe mahitaji na matakwa ya watoto

yanazingatiwa na kuna mtazamo chanya wa

jamii.

Kutoa taarifa rahisi kwa watoto kuhusu haki zao

kisheria na haki yao ya kushiriki katika maamuzi

ya mambo ya kisheria yanayowahusu.

Kuhakikisha kuwa watoto wanapata fursa ya bure

ambayo ni huru kwenye ushauri wa kisheria na

juu ya uwakilishi katika zoezi la kulinda haki zao.

Kama sehemu ya wigo mpana wa mafunzo ya

ulinzi wa mtoto, kuwajengea uwezo wanasheria

Mei, 2015 WMN,

WKS,

WMJJW

na wadau

47

wanaowapa watoto huduma za kisheria bila

malipo wawe na ujuzi na maadili stahiki katika

kushirikisha watoto.

Kusambaza nakala viwango vya kitaifa vya

ushiriki na mwongozo wa maadili ya kitaifa

katika ushiriki wa mtoto kwa watekelezaji wa

sheria, maafisa wa mahakama, wanasheria na

maofisa wa ustawi wa jamii.

Kuandaa miongozo ya namna ya kuhusisha na

watoto waliokinzana na sheria katika maamuzi ya

michakato ya kisheria yanayowahusu katika ngazi

zote.

Kutoa taarifa nyepesi na rahisi kwa watoto juu ya

haki zao kisheria na haki ya kusihiriki katika

maamuzi ya kisheria ya mambo yanayowahusu.

Kutoa msada wa kisheria bure.

Watekelezaji

wa sheria

(Polisi,

Maofisa wa

mahakama, na

waendesha

mashtaka wa

umma) na

watumishi wa

umma kukuza

ushiriki wa

watoto katika

mfumo wa

sheria.

Watekelezaji wa

sheria (Polisi,

Maofisa wa

mahakama, na

waendesha

mashtaka wa

umma) na

watumishi wa

umma kuhusika

vyema katika

kuwashirikisha

watoto katika

mambo ya kisheria.

Watekelezaji wa sheria (Polisi,

Maofisa wa mahakama, na

waendesha mashtaka wa umma)

na watumishi wa umma

waliofunzwa njia za

kuwashirikisha watoto katika

mfumo wa sheria.

Wanasheria wanaotoa msaada

wa kisheria bure kwa watoto

waliopewa mafunzo, ujuzi na

maadili katika kuwashirikisha

watoto katika mambo ya

kisheria.

Kuwapa mafunzo watekelezaji wa sheria (Polisi,

Maofisa wa mahakama, na waendesha mashtaka

wa umma) na watumishi wa umma njia za

kuwashirikisha watoto katika masuala ya

kisheria.

Kuwawezesha wanasheria wanaotoa msaada wa

kisheria bure kwa watoto kupata weledi na

maadili ya mchango wa watoto na ushiriki wao

katika masuala ya kisheria.

Kutoa nakala za viwango vya kitaifa na maadili

ya kitendaji katika ushiriki wa mtoto

kwawatekelezaji wa sheria, maofisa wa

Oktoba,

2015 na

kuendelea

WSMK,

WMJJW

kwa

ushirikiano

kutoka

kwa

wadau

48

Wanasheria

wanaowapa watoto

huduma bure za

kisheria kutumia

weledi na maadili

wakati wa

kuwawakilisha

watoto.

Watekelezaji wa sheria, maofisa

wa mahakama na maofisa wa

watumishi wa umma

wanaojihusisha na watoto

kupewa nakala za viwango vya

kitaifa na maadili ya utendaji

katika kuwashirikisha watoto.

mahakama, wanasheria, na maofisa wa ustawi wa

jamii na maofisa huduma za umma wanajihusisha

na watoto katika utekelezaji wa masuala ya

kisheria.

Ushiriki wa Mtoto katika vyombo vya habari

Lengo Matokeo Output Shughuli Muda Jukumu

Watoto wana fursa

ya kutumia

vyombo vya habari

(redio, matangazo

na TV) kuchangia

na kushiriki katika

midahalo

mbalimbali.

Watoto

wanahusishwa

katika shughuli za

vyombo vya habari

zinazokuza ushiriki

wa watoto katika

masuala

yanayowahusu.

Maofisa wa vyombo

vya habari

wanafanya kazi kwa

kushirikiana na

watoto katika

vyombo vya habari.

Maofisa wa vyombo

vya habari

waliofunzwa juu ya

njia za kimaadili za

kuwashirikisha

watoto katika

vyombo vya habari.

Rasilimali fedha

zimetengwa katika

kuwashirikisha

watoto katika

vyombo vya habari.

Kujenga uwezo wa

mitandao ya vyombo

vya habari na

kuwashirikisha

watoto katika

vyombo vya habari.

Kushawishi Wizara ya Habari Michezo na Utamaduni

kuingiza masuala ya watoto katika vyombo vya habari

hasa katika masuala yanayowaathiri katika vyombo

vya habari.

Kuwapa mafunzo maofisa wa vyombo vya habari njia

za kimaadili za kuwashirikisha watoto katika vyombo

vya habari.

Kuweka rasilimali fedha katika ushiriki wa watoto

kwenye vyombo vya habari-kuinua misaada ya

vyombo vya habari katika mitandao ya kuripoti

masuala ya watoto.

Kupanua wigo wa kitaifa wa Gazeti la agenda ya

watoto.

Kufanya kazi na vyombo vya habari kutoa habari,

elimu na mawasiliano kwa umma juu ya masuala ya

watoto hasa masuala yanayohusiana na ukiukwaji

mkubwa wa haki za watoto (kama ukatili na

unyanyasaji).

Mei 2015

kuendelea

WMJJW na

WKMVM

kwa msaada

wa wadau

wenza wa

agenda ya

mtoto

49

Kutumia rasilimali fedha katika ushiriki wa mtoto

kwnye vyombo vya habari.

Kampeni za

vyombo vya habari

kuujulisha umma

juu ya umuhimu

wa michango ya

watoto na ushiriki

wao katika

masuala

yanayowahusu.

Jamii na wadau

wengine kujua

umuhimu wa

ushiriki wa mtoto na

nafasi ya mtoto

katika jamii.

Maofisa wa vyombo

vya habari

waliofunzwa juu ya

kutetea ushiriki wa

mtoto katika vyombo

vya habari katika

ngazi zote.

Kuwafunza maofisa wa vyombo vya habari juu ya

kutetea ushiriki wa mtoto katika vyombo vya habari

katika ngazi zote.

Mei,

2015

WMJJW na

WKMVM

kwa msaada

wa wadau

wenza wa

agenda ya

mtoto

6.0 URATIBU, UFUATILIAJI NA TATHMINI YA UTEKELEZAJI

6.1 Utangulizi

Mkakati wa ufuatiliaji na tathmini umetayarishwa ili kufanikisha utekelezaji wa Mpango

Kazi huu kufikia malengo yake. Ufuatiliaji na tathmini ni nyenzo muhimu katika kuweka

utaratibu au mfumo wa kujenga msingi wa kutambua ufanisi katika utekelezaji wa

masuala ya ushiriki wa watoto. Isitoshe, unalenga katika kupata taarifa ya utendaji na

ufanisi ambazo zitatumika katika kufanya maamuzi muhimu yatakayofanikisha malengo

yaliyokusudiwa.

6.2 Lengo la Ufuatiliaji na Tathmini

Umuhimu wa kuwa na mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ni kutoa mwongozo wa

utekelezaji wa Mpango kazi huu kuanzia hatua za awali ya utekelezaji wa Mpango huu ili

kutekeleza hatua mbalimbali kwa ufanisi.

6.3 Malengo mahsusi

i) Kuwa na vigezo vya viashiria vya upimaji wa utekelezaji wa Mpango Kazi

huu

ii) Kuweka shabaha na viwango vya utekelezaji wa Mpango Kazi

iii) Kutoa mwongozo kwa wadau katika kushiriki kwenye utekelezaji na

ufuatiliaji wa shughuli

iv) Kutoa mwongozo kwa mgawanyo wa raslimali katika kipindi cha utekelezaji

6.4 Uratibu

i) Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kupitia Idara ya

Maendeleo ya watoto itaratibu masuala yote yanayohusu Mpango kazi huu

katika ngazi ya taifa. Sekretarieti ya Mkoa itakuwa na jukumu la kuratibu

ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa Mpango Kazi huu katika ngazi ya

mkoa. Mamlaka ya serikali za Mitaa zitakuwa na jukumu la uratibu wa

ufuatiliaji na tathmini kuanzia ngazi ya kijiji hadi wilaya. Wadau wengine

watakuwa ni Washiriki wa Maendeleo, Asasi za Kiraia, Sekta binafsi, Taasisi

za Elimu, Taasisi za Sheria, Taasisi za Siasa, hawa watashiriki katika jukumu

la kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa Mpango Kazi huu katika maeneo

yao.

ii) Wizara inayohusika na Elimu na Mafunzo ya Ufundi itahakikisha kuwa

inatoa na kusimamia mitaala ya elimu itakayoendana na sera ya watoto hasa

katika suala la haki ya watoto ya ushiriki katika kufanya maamuzi muhimu,

utungaji wa sera na mikakati ya utekelezaji, mipango ya sekta hii, ukuzaji wa

mitaala rafiki, nk.

iii) Wizara inayohusiana na Sheria itahakikisha shughuli zote za marekebisho

ya kanuni na taratibu za kisheria zinazohusu watoto zinafanyiwa kazi ili

kuleta maboresho na kujenga mazingira rafiki ya kisheria kwa watoto.

iv) Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii itahakikisha kuwa wadau wote

wanafahamu maboresho ya kanuni na taratibu za kisheria na kutii mabadiliko

hayo ili kujenga mazingira rafiki na mahusiano mazuri na watoto katika ngazi

zote

51

6.5 Mchakato wa Ufuatiliaji na tathmini ya Utekelezaji

6.5.1 Ufuatiliaji wa mchakato

Utekelezaji wa Mpango Kazi huu utakuwa wa miaka mitano 2014-2019 na utaenda

sambamba na utekelezaji wa MKUKUTA II kati ya 2014 na 2015. Ukiwa ndio nyenzo ya

kwanza ya Kitaifa ya utekelezaji wa Ushiriki wa Watoto, Mpango huu utafanikisha

upimaji wa utekelezaji wa ushiriki huo pamoja na kuweka viashiria ya ufanisi pamoja na

ratiba ya utekelezaji ikiwa na malengo mahsusi na matarajio ya mchakato mzima wa

tathmini.

Nyenzo kadhaa za upimaji zinaweza kuandaliwa mapema na kuanza kutumika. Nyenzo

hizo inatakiwa kuwa rahisi na rafiki kwa wadau wote ili waweze kunufaika nazo (ona

mfano katika kiambatanisho Na. 11)

Maelezo ya

Mradi kwa

ufupi

Malengo Viashiria vya Awali Tahadhari na Matarajio

Kwa vile muda wa kufanya tathmini utakuwa baada ya miaka mitano tangu mpango huu

kuanza kutekelezwa, inapendekezwa kuwa kuwe na tathmini ya katikati ya muda wa

utekelezaji itakayoanza mwaka wa tatu wa utekelezaji. Tathmini hizo zitumie nyenzo

mbali mbali za kutathmini ambazo zinatumika kungineko kama vile kwa kuanza na zoezi

la uimara, mapungufu, fursa na vikwazo “SWOT” ili kurahisisha utoaji wa taarifa kwa

watendaji ambao wana wajibu wa mwisho wa kushughulikia matokeo ya tathmini.

Nyenzo nyingine saidizi ni ile ya Mti wa Matatizo (Problems Tree) kwa uchambuzi wa

matatizo na Mti wa Malengo (Objectives Tree) kwa kuonyesha maendeleo ya utekelezaji

na usimamizi. Matumizi ya nyenzo hizi pia yataambatana na ripoti ambayo itaonyesha

hali halisi na ushahidi kutoka maeneo ya utekelezaji na kwa wadau kwa msisitizo wa

kukusanya pia ushahidi wa watoto ambao ndio walengwa wa Mpango huu.

Katika kila tathmini inayofanyika, walengwa watakuwa ni wadau wote ikiwa ni pamoja

na watoto ambao watatakiwa kushiriki katika mchakato mzima. Watoto na vijana

wanatakiwa kuwa walengwa na pia kuwa washiriki wakuu katika kutathmini na

ufuatiliaji wa mchakato mzima kwa mfano kuwa watafiti katika tafiti zitakazofanywa

kama sehemu ya Mpango Kazi huu.

6.5.2 Ratiba ya Utekelezaji na Matukio ya Ziada

Ratiba hii inatoa maelezo ya kina kuhusu maandalizi ya utekelezaji na matukio katika

hatua yauandaaji na utekelezaji wa Mpango Kazi huu wa Ushiriki wa Watoto kwa

kuonyesha viwango vya Kitaifa na majukumu ya Kamishna wa Haki za Watoto/ Chombo

Maalum cha kuchunguza Malalamiko ya Watoto ambacho baadhi ya majukumu yake

yatakuwa kusimamia maendeleo ya hatua za utekelezaji za Mpango Kazi huu. Maelezo

zaidi kuhusu utekelezaji yanaonekana katika Mpango wa Utekelezaji, Jedwali Na. 1.

52

Utekelezaji na shughuli za kuandaa Mpango Kazi

wa Ushiriki wa Watoto

Viwango vya Kitaifa na mfumo wa kanuni

na taratibu

Kamishna wa Haki za watoto au

Chombo Maalum cha Kuchunguza

Malalamiko ya Watoto

Januari 2014

Kuwasilisha rasimu ya Mpango Kazi kwa Wizara ya

Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto (WMJW)

Warsha ya wadau kuhakiki na kukubali Mpango Kazi

huu itakayoandaliwa na WMJW

Mei 2014

Rasimu ya Mpango Kazi huu kupitishwa na Baraza

la Mawaziri

Mpango Kazi kukubalika kama Mpango wa Kitaifa

wa Ushiriki wa Watoto

Mei 2014

Kuunda chombo ambacho kitaandaa na

kusimamia Viwango vya kitaifa na mfumo wa

kanuni na taratibu ushiriki watoto

Kuagiza utafiti wa haraka kuangalia mifano ya

viwango vya kitaifa vilivyopo na mfumo wa

kanuni na taratibu

(kwa kushirikiana na Asasi Zisizo za

Kiserikali, UNICEF, nk)

Mei 2014

Kusambaza matokeo ya utafiti huo kwa wadau

wote

Kuanza kutengeneza Viwango vya Kitaifa

kuhusu Ushiriki wa Watoto

Juni 2014

Kukamilisha uandaaji wa Viwango vya Kitaifa

na kuanza kuandaa mfumo wa kanuni na

taratibu

Julai 2014

Kuanza zoezi la Ushiriki wa Watoto na uchangiaji

wao katika ngazi ya familia

Julai 2014

Kuagiza utafiti kuhusu namna ya kuanzisha

ofisi ya Kamishna wa Haki za Watoto/

Chombo Maalum cha Kuchunguza

Malalamiko ya watoto

Septembar 2014

Kukamilisha rasimu ya mfumo wa kanuni na

54

taratibu

Kuwasilisha rasimu kwa wanasheria wa serikali

kuhakikisha ufanisi/ukamilifu

Kutafsiri rasimu kwenye lugha ya Kiswahili

Kuanza kuandaa mabango na vipeperushi kwa

ajili ya shule, sehemu za huduma za watoto na

majengo ya serikali na jamii

Oktoba 2014

Kuanza kusambaza taarifa husika kwa viongozi na

watendaji wa serikali, vyama vya kiraia, watoto na

jamii ili kuelimisha kuhusu utekelezaji wa Mpango

Kazi huu wa Kitaifa wa Ushiriki wa Watoto

Oktoba 2014

Kuwa na machapisho ya Mpango Kazi huu kwa

lugha zote mbili za Kiswahili na Kiingereza

Kuweka tarehe ya Uzinduzi rasmi wa Viwango

vya kitaifa na mfumo wa kanuni na taratibu

Oktoba 2014

Kuunda Kamati au Jukwaa linalohusisha

watoto kwa ajili ya kuandaa ofisi ya

kamishna/Ombudsman (kuhusu maamuzi ya

jina la/wadhifa wa ofisi na majukumu yake

kulingana na matokeo ya utafiti yakinifu)

Desemba 2014

Majadiliano na wizara na idara za serikali , Asasi

Zisizo za Kiserikali na wadau wa maendeleo kujadili

sehemu za Sheria ya Mtoto na kushughulikia

maeneo ya kanuni na taratibu

Kurasmisha Baraza la watoto la Serikali ya Jamhuri

ya Muungano wa Tanzania

Maafisa wa Serikali za Mitaa na watendaji wa Asasi

Zisizo za Kiserikali kuanza rasmi utekelezaji wa

Ushiriki wa Watoto katika ngazi ya jamii na utawala

Kuanza rasmi Ushiriki wa watoto katika mfumo wa

elimu na utawala

Desemba 2014

Kutangaza nafasi za kazi kwa ajili ya ofisi

ya Kamishna wa Haki za Watoto/ Chombo

Maalum cha Kuchunguza Malalamiko ya

Watoto

Kuandaa/kutenga nafasi ya ofisi hii katika

jingo la serikali, kuunda kamati ya kuandaa

hadidu za rejea kwa wafanyikazi wa ofisi

hii na mahitaji yao kulingana na matokeo ya

utafiti wa awali.

Januari 2015

Uteuzi wa Kamishna/ Chombo Maalum cha

Kuchunguza Malalamiko ya watoto

Machi 2015

Kamishna/ Chombo Maalum cha

Kuchunguza Malalamiko ya Watoto

kuanza kazi

Mei 2015

Miongozo ya ushiriki wa Watoto katika maswala ya

55

sheria kuzinduliwa

Watoto kuanza kupata taarifa kuhusu haki zao za

kisheria, Haki ya kushiriki kwenye kufanya maamuzi

kuhusu taratibu za kisheria zinazohusu watoto na

haki ya kupata utetezi na huduma za kisheria

bure/bila gharama zozote

Kujenga/kuwepo kwa Uwezo wa watoto kutumia

vyombo vya habari na kampeni za wafanyakazi

kuhusu mchango na faida ya ushiriki wa watoto

katika vyombo vya habari

Oktoba 2015

Wasimamizi wa sheria na watendaji wa ustawi wa

jamii kuanza rasmi kuwajibishwa kusimamia swala

la Ushiriki wa Watoto katika ngazi zote pasipo

kuvunja sheria

7.0 REJEA

Alderson, Priscilla (1990) Choosing for Children: Parents’ Consent to Surgery, Oxford:

OxfordUniversity Press.

Alderson, Priscilla (1992) Consent to Health Treatment and Research: Differing

Perspectives (SSRU consent conference series), London: University of London Institute

of Education.

van Beers, Henk, Vo Phi Chau, Judith Ennew, Pham Quoc Khan, Tran Thap Long, Brian

Milne, TrieuThiAnhNguyet and Vu Thi Son (2006) Creating an enabling environment:

Capacity building in children’s participation, Viet Nam, 2000-2004, Bangkok: Save the

Children Sweden.

van Beers, Henk, AntonellaInvernizzi and Brian Milne (eds.) (2006) Beyond Article 12.

Essential Readings in Children’s Participation. Bangkok: Black on White Publications.

British Sociological Association (2006) Statement of Ethical Practice, Durham: British

Sociological Association.

Committee on the Rights of the Child (2000) Initial Reports of States Parties due in 1993

(Addendum), United Republic of Tanzania, CRC/C/8/Add.14/Rev.1, Geneva: UN.

Committee on the Rights of the Child (2001) Consideration of Reports of States Parties,

Initial report of the UnitedRepublic of Tanzania, CRC/C/SR.713. (Summary Record),

Geneva: UN.

Committee on the Rights of the Child (2001) Consideration of Reports of States Parties,

Initial report of the UnitedRepublic of Tanzania, CRC/C/SR.714. (Summary Record),

Geneva: UN.

Committee on the Rights of the Child (2001) Adoption of the Committee’s Report on its

Twenty-Seventh Session, CRC/C/SR.721. (Summary Record), Geneva: UN.

Committee on the Rights of the Child (2003), CRC General Comment No 5. General

measures of implementation of the Convention on the Rights of the Child,

CRC/GC/2003/5. Geneva: UN.

Committee on the Rights of the Child (2005) Second periodic reports of States parties

due in 2004,UnitedRepublic of Tanzania, CRC/C/70/Add.26, Geneva: UN.

Committee on the Rights of the Child (2005), General Comment No 7,Implementing

child rights in early childhood, CRC/C/GC/7/Rev.1, Geneva: UN.

Committee on the Rights of the Child (2006) Consideration of Reports Submitted by

States Parties under Article 44 of the Convention: Concluding observations: United

Republic of Tanzania, CRC/C/TZA/CO/2, Geneva: UN.

Committee on the Rights of the Child (2007) General Comment No 10, Children’s rights

in juvenile justice, CRC/C/GC/10, Geneva: UN.

57

Committee on the Rights of the Child (2009)General Comment No 12,The right of the

child to be heard, CRC/C/GC/12, 2009, Geneva: UN.

Ennew, Judith (1997) Monitoring Children’s Rights: Indicators for Children’s Rights

Project, Oslo: Childwatch International.

Gallagher, M. (2006) „Spaces of participation and inclusion?‟ in Tisdall, E.K.M.,Davis,

J.M., Hill, M. and Prout, A. (eds) Children, Young People and Social Inclusion, Bristol:

Policy Press.

Hart, R. A. (1992). Children’s Participation: from tokenism to citizenship, Florence:

UNICEF International Child Development Centre.

Inter-Agency Working Group on Children‟s Participation (IAWGCP) (2007) Minimum

Standards for Consulting with Children, Bangkok: IAWGCP.

Inter-Agency Working Group on Children‟s Participation (2008) Children as Active

Citizens: A Policy and Programme Guide, Bangkok: IAWGCP.

International Labour Organisation (ILO) (1973) Convention concerning Minimum Age

for Admission to Employment (Minimum Age Convention, No. 138), Geneva: ILO.

International Labour Organisation (ILO) (1999) Worst Forms of Child Labour

Convention, (No. 182), Geneva: ILO.

International Save the Children Alliance (ISCA) (2005) Practice Standards in Children’s

Participation, London: ISCA.

James, A and A. Prout (eds) (1997) Constructing and Reconstructing Childhood:

Contemporary Issues in the Sociological Study of Childhood, Cambridge: Polity Press.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA (BILA TAREHE) WIZARA YA

MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: MKAKATI WA UTEKELEZAJI

WA SERA YA MALEZI, MAKUZI NA MAENDELEO YA MTOTO KWA KIPINDI

CHA 2013-2018

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA: WIZARA YA MAENDELEO YA

JAMII, JINSIA NA WATOTO (2013): SERA YA MALEZI, MAKUZI NA

MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO TANZANIA

Lansdown, G. (2001) Children’s Participation in Democratic Decision-Making,

Florence: UNICEF.

Liebel, M. (2004) A Will of their Own: Cross-cultural Perspectives on Working Children,

London and New York: Zed Books.

Lovan, W.R., Murray, M., and Shaffer, R. (2004) „Participatory Governance in a

Changing World‟, in Lovan, W.R., Murray, M., Shaffer, R. (eds) Participatory

58

Governance: Planning, Conflict Mediation and Public Decision-Making in Civil Society,

Aldershot: Ashgate.

O‟Donnell, Daniel (2009), The right of children to be heard: Children’s right to have

their views taken into account and to participate in legal and administrative proceedings,

Innocenti Working PaperNo. 2009-04, Florence: UNICEF Innocenti Research Centre.

Organisation of African Unity (OAU) (1999) African Charter on the Rights and Welfare

of the Child, Addis Ababa: OAU.

Save the Children Norway (2008)Global Report on children’s participation in armed

conflict, post conflict and peace building, Oslo: Save the Children Norway.

Shier, Harry (2001) „Pathways to Participation: Opportunities and Obligations‟ in Young

People and Society, Vol. 15, Chichester:Wiley:107-17.

Snipstad, Mai Bente, Gro Therese Lie and DagfinnWinje (2010) ‚ „Child Rights or

Wrongs: Dilemmas in Implementing Support for Children in the Kilimanjaro Region,

Tanzania, in the Era of Globalized AIDS Approaches, in TatjanaThelen and

HaldisHaukanes (eds) Parenting After the Century of the Child: Travelling Ideals,

Institutional Negotiations and Individual Responses, Aldershot: Ashgate.

Treseder, Phil (1997) Empowering children and young people training manual:

promoting involvement in decision making, London: Save the Children.

UNICEF (2010) Violence against Children in Tanzania: Preliminary Findings from a

National Survey, Center for Disease Control and Prevention/ UNICEF.

UNICEF Evaluation Office (2002) Children Participating in Research, Monitoring And

Evaluation (M&E) - Ethics and Your Responsibilities as a Manager, Evaluation

Technical Notes No. 1, New York: UNICEF.

United Nations (UN) (1948) Universal Declaration of Human Rights, New York: UN.

United Nations (1989) Convention on the Rights of the Child, New York: UN.

United Nations Office on Drugs and Crime (2009) Justice in Matters involving Child

Victims and Witnesses of Crime: Model Law and Related Commentary, Vienna: United

Nations Office on Drugs and Crime.

United Republic of Tanzania (1998) Constitution of the United Republic of Tanzania, Dar

es Salaam: The United Republic of Tanzania.

United Republic of Tanzania (2005) The National Strategy for Growth and Reduction of

Poverty - NSGR), Dar es Salaam: Vice President‟s Office.

United Republic of Tanzania (2009) The Law of the Child Act, 2009, Dar es Salaam: The

United Republic of Tanzania.

59

United Republic of Tanzania (2010) National Strategy for Growth and Reduction of

Poverty II - NSGRP II, Dar es Salaam: Ministry of Finance and Economic Affairs.

Wessells, Mike (2009i) What Are We Learning About Protecting Children in the

Community? An inter-agency review of the evidence on community-based child

protection mechanisms in humanitarian and development settings, London: Save the

Children UK.

Wessells, Mike (2009ii) What Are We Learning About Protecting Children in the

Community? An inter-agency review of the evidence on community-based child

protection mechanisms (executive Summary), London: Save the Children UK.

Willow, Carolyne (2010) Children’s right to be heard and effective child protection. A

guide for Governments and children rights advocates on involving children and young

people in ending all forms of violence, Bangkok: Save the Children Sweden.

Wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto (2013): Mpango Kazi Shirikishi wa

Kudhibiti Tatizo la Watoto waishio/kufanya Kazi Mitaani