programu ya uimrishaji miundombinu ya masoko, … · hadi mwezi disemba 2011 kazi ya mapitio ya...

25
1 RIPOTI YA KAMATI YA FEDHA, BIASHARA NA KILIMO YA BARAZA LA WAWAKILISHI - ZANZIBAR 2011/2012 SEHEMU YA KWANZA 1.0. UTANGULIZI Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo imeundwa kwa mujibu wa Kanuni ya 108 ya Baraza la Wawakilishi la Zanzibar toleo la mwaka 2011, ikiwa na majukumu yafuatayo:- a) Kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Kamati yaliyotolewa kwenye ripoti ya Kamati ya mwaka uliotangulia. b) Kufuatilia utekelezaji wa Sera na Mipango ya Wizara husika kadri Spika atakavyoelekeza kwa mujibu wa malengo yaliyowasilishwa Barazani wakati wa usomaji wa Bajeti na hotuba nyengine za Waziri alizotoa Barazani. c) Kuchambua mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya Wizara husika ya mapato na matumizi ya kila mwaka. d) Kufuatilia utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ya Kitaifa na Miradi ya Wananchi ya Wizara husika. e) Kuchunguza na kufuatilia mapato ya Serikali ya Wizara husika f) Kufikiria jambo lolote litakalopelekwa kwake na Spika. g) Kuchambua ahadi zote za Wizara zilizo chini ya Kamati kama zitavyokuwa zikitolewa katika Baraza na kufuatilia utekelezaji wa ahadi hizo. h) Kufikiria Miswada ya Sheria itakayopelekwa kwake na Spika Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo imepangiwa kufuatilia utekelezaji wa malengo hayo katika Wizara zifuatazo:- a) Wizara ya Nchi (OR) Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo. b) Wizara ya Biashara Viwanda na Masoko c) Wizara ya Kilimo na Maliasili. Kamati ilifanya kazi zake za kawaida ikiwa na Wajumbe wafuatao:- 1. Mhe. Salmini Awadh Salmini - Mwenyekiti 2. .Mhe. Abdalla Mohamed Abadalla - Makamo Mwenyekiti 3. Mhe Mahamoud Mohamed Mussa - Mjumbe 4. Mhe. Bikame Yussuf Hamad - Mjumbe 5. Mhe Rufai Said Rufai - Mjumbe 6. .Mhe. Raya Suleiman Hamad - Mjumbe 7. Mhe. Mlinde Mabrouk Juma Mjumbe 8. Ndg. Amour Mohamed Amour - Kati bu 9. Ndg. Shemsa Maabad Mohamed - Katibu Kamati imefanya kazi zake kwa muda wa Wiki nane (8) kama ilivyo utaratibu wake katika kufuatilia utekelezaji wa kazi zake katika Wizara, Idara na Mashirika mbali mbali ya Serikali. Kamati imefanya kazi hizo za kufuatilia utekelezaji wa malengo ya bajeti kama ilivyoainishwa katika vitabu vya bajeti za Wizara husika, kazi ya ufuatiliaji ilifanyika Unguja, Pemba na Tanzania Bara kwa Taasisi ambazo ni za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar au hata zile za Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa lengo la kupata kujifunza na kupata uzoefu.

Upload: others

Post on 04-Feb-2020

22 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

1

RIPOTI YA KAMATI YA FEDHA, BIASHARA NA KILIMO YA

BARAZA LA WAWAKILISHI - ZANZIBAR

2011/2012

SEHEMU YA KWANZA

1.0. UTANGULIZI

Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo imeundwa kwa mujibu wa Kanuni ya 108 ya Baraza la

Wawakilishi la Zanzibar toleo la mwaka 2011, ikiwa na majukumu yafuatayo:-

a) Kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Kamati yaliyotolewa kwenye ripoti ya Kamati ya

mwaka uliotangulia.

b) Kufuatilia utekelezaji wa Sera na Mipango ya Wizara husika kadri Spika atakavyoelekeza kwa

mujibu wa malengo yaliyowasilishwa Barazani wakati wa usomaji wa Bajeti na hotuba

nyengine za Waziri alizotoa Barazani.

c) Kuchambua mapendekezo ya Serikali kuhusu makadirio ya Wizara husika ya mapato na

matumizi ya kila mwaka.

d) Kufuatilia utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo ya Kitaifa na Miradi ya Wananchi ya Wizara

husika.

e) Kuchunguza na kufuatilia mapato ya Serikali ya Wizara husika

f) Kufikiria jambo lolote litakalopelekwa kwake na Spika.

g) Kuchambua ahadi zote za Wizara zilizo chini ya Kamati kama zitavyokuwa zikitolewa katika

Baraza na kufuatilia utekelezaji wa ahadi hizo.

h) Kufikiria Miswada ya Sheria itakayopelekwa kwake na Spika

Kamati ya Fedha, Biashara na Kilimo imepangiwa kufuatilia utekelezaji wa malengo hayo katika

Wizara zifuatazo:-

a) Wizara ya Nchi (OR) Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo.

b) Wizara ya Biashara Viwanda na Masoko

c) Wizara ya Kilimo na Maliasili.

Kamati ilifanya kazi zake za kawaida ikiwa na Wajumbe wafuatao:-

1. Mhe. Salmini Awadh Salmini - Mwenyekiti

2. .Mhe. Abdalla Mohamed Abadalla - Makamo Mwenyekiti

3. Mhe Mahamoud Mohamed Mussa - Mjumbe

4. Mhe. Bikame Yussuf Hamad - Mjumbe

5. Mhe Rufai Said Rufai - Mjumbe

6. .Mhe. Raya Suleiman Hamad - Mjumbe

7. Mhe. Mlinde Mabrouk Juma Mjumbe

8. Ndg. Amour Mohamed Amour - Kati bu

9. Ndg. Shemsa Maabad Mohamed - Katibu

Kamati imefanya kazi zake kwa muda wa Wiki nane (8) kama ilivyo utaratibu wake katika kufuatilia

utekelezaji wa kazi zake katika Wizara, Idara na Mashirika mbali mbali ya Serikali.

Kamati imefanya kazi hizo za kufuatilia utekelezaji wa malengo ya bajeti kama ilivyoainishwa

katika vitabu vya bajeti za Wizara husika, kazi ya ufuatiliaji ilifanyika Unguja, Pemba na Tanzania

Bara kwa Taasisi ambazo ni za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar au hata zile za Serikali ya

Jamhuri ya Muungano kwa lengo la kupata kujifunza na kupata uzoefu.

Page 2: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

2

SEHEMU YA PILI

2. 0. UTEKELEZAJI WA MALENGO YA WIZARA

2.1. WIZARA YA KILIMO NA MALIASILI

2.1.1. IDARA YA MIPANGO, SERA NA UTAFITI

MIRADI

Katika mwaka wa Fedha wa 2010/2011 Idara inasimamia na kuratibu utekelezaji wa programu na miradi

ya maendeleo ifuatayo:

i) Mradi wa Kuimarisha Huduma za Kilimo – ASSP

ii) Mradi wa Kuimarisha Huduma za Mifugo – ASDP-L

iii) Mradi wa Usarifu Mazao ya Kilimo.

iv) Mradi wa Miundombinu ya Masoko, Uongezaji thamani na huduma za Fedha vijijni (MIVARF)

MALENGO YA IDARA

a) Kufanya mapitio ya Sera ya Kilimo, Misitu, Mbegu na Hakimiliki za wavumbuzi.

b) Kusimamia na kuimarisha ukusanyaji wa Takwimu za uzalishaji wa mazao ya chakula, biashara

na maliasili.

c) Kusimamia utekelezaji wa mpango Mkuu wa Utafiti na Dira ya Elimu kwa wakulima.

d) Kukusanya mapato ya Tsh. 1,293,774,000/-

e) Kutayarisha na kutoa nakala 2,000 za Jarida la Mkulima.

f) Kuchapisha matokeo ya Tafiti mbalimbali za kilimo.

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza.

Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa kwa wadau.

Rasimu ya mwanzo ya Sheria ya Hakimiliki ya uvumbuzi wa mbegu mpya imekamilika na iko

kwenye ngazi ya Wizara.

Wizara imekusanya jumla ya Tsh. 234,849,615 hadi Novemba, 2011.

Nakala 1000 za Jarida la Mkulima zimechapishwa.

MRADI WA UIMARISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, UONGEZAJI THAMANI YA

MAZAO NA HUDUMA YA FEDHA VIJIJINI (MIVARF)

Mradi huu unatekelezwa katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar na umetengewa jumla ya

fedha USD 162 milioni sawa na Tanzania Shilingi 247.1 bilioni ikiwa ni fedha za mkopo kutoka Mfuko

wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo IFAD, AFDB na AGRA. Utekelezaji unafanyika kitaifa na

umeanza Julai 2011 na utadumu kwa miaka saba (2011/12 – 2017/18).

MALENGO YA MRADI

a) Ujenzi wa mfumo na miundombinu ya masoko mradi utasaidia katika maeneo yafuatayo:

(i) Ujenzi wa masoko Wilayani yatakayokuwa na huduma za uhifadhi wa bidhaa

zinazoharibika.

(ii) Ujenzi wa Viwanda viwili vya kuzalisha barafu kimoja Unguja na kimoja Pemba.

(iii) Ujenzi wa barabara za mashambani kuunganisha maeneo yote ya uzalishaji na barabara

kuu kwa lengo la kurahisisha kuyafikia masoko na utoaji wa huduma za kilimo.

b) Utoaji mafunzo na uwezeshaji katika usarifu wa bidhaa za kilimo. Mradi utasaidia.

(i) Kuimarisha vikundi vya wajasiriamali katika usindikaji na usarifu wa bidhaa za kilimo.

(ii) Kutoa mafunzo ya usarifu na usindikaji bidhaa za kilimo kwa wakulima, wajasiriamali

na watoaji huduma za usarifu na usindikaji bidhaa za kilimo.

c) Kuanzisha mfumo wa utoaji wa huduma za kifedha vijijini na Mradi utasaidia

(i) Kutayarisha sera ya upatikanaji wa huduma za fedha kwa wakulima na wajasiriamali

wadogo wadogo.

(ii) Kuanzisha na kuwezesha taasisi za kijamii za utoaji huduma za fedha vijijini.

Page 3: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

3

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Kwa kupitia fedha za wahisani ambazo ni TShs. 168, 209,860.00 kazi zifuatazo zimefanyika:

Uzinduzi na utambulisho wa Mradi.

Kuunda Timu ya Uratibu wa Mradi – Zanzibar

Kutambulisha Mradi kwa Kamati ya Kisekta ya Usimamizi.

Kutambulisha Mradi kwa Viongozi wa Wizara, Wakurugenzi na Wakuu wa Idara.

Kutambulisha Mradi kwa Kamati ya Ushauri na Utekelezaji wa Mradi za Mikoa na Wilaya.

Kununua samani na vitendea kazi.

Matumizi ya uendeshaji wa ofisi.

Kwa kupitia fedha za wahisani ambazo ni TShs. 48, 389,400.00 kazi zifuatazo zimefanyika

Kufanya matengenezo ya Ofisi za Mradi.

Utafiti wa mfumo wa masoko ya mazao ya kilimo, mifugo na uvuvi.

Ununuzi wa vipuri vya gari.

Ununuzi wa vitendea kazi

Matumizi ya Uendeshaji wa Ofisi.

2.1.2. IDARA YA UENDESHAJI NA UTUMISHI

MALENGO YA IDARA

a) Kutayarisha mpango wa mafunzo kwa wafanyakazi (Training Master Plan) utakaoonesha

maeneo ya vipaumbele katika fani za Wizara.

b) Kuimarisha utendaji katika uhifadhi wa kumbukumbu zikiwemo taarifa za wafanyakazi na

rasilimali za Wizara (data base).

c) Kutayarisha mpango mkakati (strategic plan) wa miaka mitatu wa Idara kwa lengo la

kuimarisha ufanisi wa kazi.

d) Kuhakikisha mali za Serikali zilizomo ndani ya Wizara zinatunzwa na kupatiwa hati miliki.

UTEKELEZAJI WA MALENGO

i) Utayarishaji wa mpango mkakati (strategic plan) wa miaka mitatu umekamilika, kwa

upande wa mpango wa mafunzo kwa wafanyakazi bado unaendelea. Hata hivyo baadhi ya

vipengele vya mpango mkuu wa mafunzo vimeanza kukamilika (Training Master Plan)

kama:

Kuunda Kamati ya mafunzo ya Wizara.

Kukusanya taarifa za elimu na fani walizonazo.

Kufanya uchambuzi wa taarifa zilizokusanywa, mpango huu unatarajiwa kukamilika

ifikapo Machi, 2012.

ii) Ukamilishaji hati miliki wa Rasilimali za Wizara umeanza kwa kukamilisha mambo

yafuatayo:-

Upimaji wa mashamba na vituo vya utafiti kama Kijichi, Kizimbani, Selem, Bambi na

maeneo ya chuo cha kilimo kizimbani umekamilika pamoja na kupatiwa michoro yake.

Aidha umefanyika upimaji wa maeneo yaliyozunguka nyumba zilizo chini ya Wizara

kama Mbweni, Mazizini, Saateni pamoja na Ofisi za ASSP/ASDPL Maruhubi.

Kwa upande wa vipando (vya usafiri) tayari vimekwisha orodheshwa na hivi sasa hatua

za kufanya usajili kwa ajili ya kupata nambari mpya unafanyika ili hatimae litayarishwe

daftari la kumbukumbu (Registration Book), mfano wa vyombo hivyo ni gari, pikipiki,

trekta, vespa

n.k.

Page 4: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

4

CHUO CHA KILIMO KIZIMBANI

MALENGO

i. Kutoa mafunzo ya cheti kwa wanafunzi 140 mwaka wa kwanza na wa pili

ii. Kujenga bweni la wanafunzi kupitia Miradi ya ASSP/ASDP-L.

iii. Kutoa mafunzo kwa wakulima 500 kwa mabonde matatu ya mpunga.

iv. Kukamilisha usajili wa Chuo kwa Baraza la Vyuo vya Ufundi Tanzania.

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Lengo limevukwa ambapo kwa sasa wanafunzi 156 wanaendele na masomo.

Ujenzi wa Bweni unaofadhiliwa na ASSP/ASD-L upo katika hatua za kupata mkandarasi

baada ya kufunguliwa zabuni

Mafunzo yametolewa kwa wakulima 337 wa mabonde ya Mtwango, Weni na Mangwena.

Chuo tayari kimeshasajiliwa na kupatiwa Hati Na. REG/ANE/027.

2.1.3. IDARA YA KILIMO

Idara hii ina jukumu kubwa la kusimamia maendeleo ya wakulima, kutoa pembejeo za kilimo na

upatikanaji wa mbegu na dawa.

MALENGO YA IDARA

i) Uongezaji tija wa kilimo cha mpunga wa juu.

ii. Kuimarisha soko la ndani la mchele.

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Wizara tayari imeshanunua tani 141 za mbegu kwa wakulima wa ndani na ziada ya tani 160

zitanunuliwa Tanzania Bara ili kufikia mahitaji ya wakulima kwa msimu huu ambayo ni Tani

355. Hatimae mbegu zitauzwa kwa wakulima kwa bei ya Sh. 200/- tu kwa kilo ikiwa ni bei ya

ruzuku kwa wakulima.

Jumla ya tani 490 za mbolea pamoja na lita 20000 za dawa zimeagizwa ili kuwahi msimu

lakini hadi mwezi Disemba, 2011 bidhaa hizo zilikuwa bado hazijawasili.

Jumla ya tani 3.4 za mbegu aina ya NERICA imezalishwa katika kituo cha kilimo Bambi na

zimesambazwa kwa wakulima

UDHIBITI WA INZI WA MATUNDA

MALENGO YA IDARA:

i) Kuwaelimisha wakulima 1,500 juu ya mbinu za kilimo bora.

ii) Kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa Mabibishamba/Mabwanashamba ili kuweza

kubadilishana utaalamu ikiwemo kuwapeleka katika maonesho ya nane nane Tanzania Bara.

iii) Kutayarisha makala 15 na vipeperushi 600 na kupatiwa wakulima.

vi) Kutayarisha vipindi 60 vya redio na 37 vya TV na kuvirusha hewani.

iv) Kununua gari tano kwa lengo la kufanikisha utoaji wa huduma za elimu kwa wakulima.

Page 5: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

5

v) Kuendeleza kazi za karantini na ukaguzi wa mazao.

vi) Kuzalisha na kusambaza tani 12 za mbegu za mahindi na mtama tani 5 na jamii ya kunde

tani 8.

vii) Kununua na kusambaza mbolea tani 1,090 (545 TSP na 545 Urea).

xi) Kutoa huduma za kilimo cha matrekta kwa kushirikiana na wenye matrekta binafsi pamoja

na kutengeneza matrekta mabovu 29 na zana zake.

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Hatua mbali mbali za udhibiti wa inzi wa matunda ikiwemo kusambaza mitego ya inzi. Tokeo kuanza

kazi ya udhibiti wa inzi wa matunda jumla ya mitego 65,000 imenunuliwa na kusambazwa katika sehemu

mbali mbali za mashamba na Mijini Unguja na Pemba.

Kazi ya kusambaza mitego ya inzi ilikuwa ikidhaminiwa na mradi wa MACEMP lakini kuanzia mwaka

2010/2011, Idara imeanza tena kutegemea Bajeti ya Serikali ambapo kwa mwaka wa fedha 2011/2012,

hadi Januari 2012, Idara imeshatumia jumla ya TShs. 75, 793,495/= kwa kazi za utekelezaji kama

ifuatavyo:-

1. Ununuzi wa dawa.

2. Usambazaji wa mitego 20,000 Wilaya Kaskazini “A” na “B” na Wilaya ya Micheweni

Pemba.

3. Ufuatiliaji na ubadilishaji wa dawa.

4. Maslahi ya wafanyakazi.

5. Gharama za Usafiri.

6. Kufanya tathmini juu ya kiwango cha uharibifu toka kuanza kuweka mitego. Tathmini

ya mwisho inaonesha kuwa kiwango cha uharibifu kimepungua kutoka asilimia 70

mwaka 2008, asilimia 43 mwaka 2010 hadi kufikia asilimia 30 mwaka 2012.

2.1.4. IDARA YA MISITU NA MALI ZISIZOREJESHEKA

Idara hii ina jukumu la kulinda na kuhifadhi misituya asili, kuratibu upatikanaji wa maliasili

zisizorejesheka na upatikanaji wa mbegu na miche bora ya miti ya mazao ya biashara, matunda, misitu na

mapambo.

MALENGO YA IDARA i. Kuzalisha miche 500,000 na ujenzi wa mabanda ya kuzalisha miche.

ii. Kutoa elimu ya upandaji na uendelezaji mikarafuu na kufanya sensa ya mikarafuu kwa Wilaya saba

(3 kwa Unguja na 4 kwa Pemba)

UTEKELEZAJI WA MALENGO

i. Idadi ya miche 240,000 imeoteshwa kwa Unguja na Pemba. Ujenzi wa mabanda mapya haukuanza.

Wakati elimu ya kuendeleza zao la karafuu imetolewa.

ii.Kuhusu sensa ya mikarafuu; kilichofanyika ni makisio tu ya kazi yenyewe ambayo ni Sh.303, 131,352

2.1.5. IDARA YA UMWAGILIAJI MAJI

Idara hii imeendelea kutekeleza majukumu yake kwa kuyaendeleza mabonde ya mpunga kwa kuimarisha

miundombinu yake kama vile uchimbaji wa visima, matengenezo ya njia na ujenzi wa misingi ya maji.

MALENGO YA IDARA

Kusimamia ujenzi wa miundombinu mipya ya umwagiliaji maji kwa ekari 237. Kazi hii

itafanyika kupitia Mradi wa TASAF na JICA.

Kujenga mtaro mkuu wa mita 500 na kujenga matuta katika ekari 25 bonde la Koani.

Page 6: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

6

Kutoa mafunzo ya muda mfupi kwa mabwana/mabibishamba 40 Unguja na Pemba.

Kusomesha wafanyakazi wawili Msc na wanane kiwango cha Diploma.

Kutoa mafunzo kwa wakulima 120 wa bonde la Kibokwa.

Kutayarisha vishamba 10 vya maonesho, kuongeza u taalamu kwa wakulima wa mpunga na

mboga mboga katika mabonde ya umwangiliaji maji.

Ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji maji katika maeneo mawili ya vituo vya uzalishaji

mbegu ekari 65 ambapo Kibonde Mzungu ekari 40 na Ole ekari 25.

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Serikali imetoa jumla ya Tsh.4, 165,000/- kwa ununuzi wa vifaa vya ujenzi wa msingi wenye

urefu wa mita 100 kwenye bonde la Kinyakuzi. Kwa upande wa bonde la Weni lenye ukubwa

wa hekta 16, jumla ya Shilingi 2, 100,000/- zilitolewa na zilitumika kwa ununuzi wa mawe kwa

ajili ya kukarabati banio (Spillways) kazi hiyo imekamilika kwa asilimia 90.

Kwa upande wa bonde la Makombeni ambalo kwa sasa kuna mradi unaofadhiliwa na Serikali ya

Japan wa JP 5 Bonde hilo linahitaji jumla ya Tsh. 238,280,000/- na Wafadhili wametoa jumla

ya Tsh.113,725,000/-, SMZ mchango wake ni Tsh. 12,500,000/- na sehemu iliyobaki ni nguvu

za wakulima ambayo ni karibu Tsh. 112,000,000/- ambazo zinaweza kuongezeka zaidi ya

hapo.Kazi ya uchimbaji wa kisima imekamilika lakini hata hivyo transforma na umeme bado

haujafika na pia matengenezo ya barabara ya kuingilia bondeni ambayo kwa wakati wa mvua

inakuwa ni vigumu kupitika hasa kwenye kilima bado haujafanyika. Mradi huo ambao ulikuwa

umalizike Januari, 2010.

Kisima cha Bumbwisudi kimechimbwa na majaribio ya wingi wa maji yamaefanyika. Jumla ya

Tshs 26, 000,000/- kutoka TASAF zimetumika.

Mitaro ya saruji mita 500 Bumbwisudi na mita 500 Uzini imejengwa na jumla ya Tsh

30,000,000/- kutoka TASAF zimetumika kwa kazi hiyo.

Ujenzi wa barabara kwa kiwango cha kifusi mita 100 umefanyika Bumbwisudi jumla ya Tshs

3,000,000/-kutoka TASAF zimetumika.

Vyanzo vya maji vya mto mawe Kikobweni na Kianga vimepandwa miti na kupigwa matuta ya

kuzuia mmong‟onyoko wa ardhi. Jumla ya Tsha 5, 000,000/-zimetumika kutoka TASAF.

.

Majaribio ya kumwaga na kupima wingi wa maji kisima cha Makombeni yamefanyika jumla ya

Tshs 700,000/- zimetumika kwa kazi hiyo.

Usafishaji wa kisima Tibirinzi umefanyika na jumla ya Tshs 700,000/- zimetumika.Kisima

kimepunguza kuzalisha maji na mpango wa Badea wa idara ni kuchimba kisima chengine.

Pampu mpya na transfoma zimewekwa katika bonde la Saninga Jumla ya Tshs 30,

000,000/zimetumika kwa kazi hiyo.

Banda la kupumzikia wakulima wa bonde la Saninga tayari limefikia kwenye linta ambapo

Serikali imetoa Tsh.4, 795,000/- kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya ujenzi na kazi nyengine ni

nguvu za wakulima wenyewe.

Ukarabati wa mtaro mita 60 Mtwango umefanyika jumla ya Tshs 1, 000,000/- za SMZ na jamii

zimetumika.

Pampu ya kisima cha umwagiliaji maji cha Uzini imetengenezwa na inafanya kazi , jumla ya

Tsh 6,000,000/- zimetumika kwa kazi hiyo.

Page 7: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

7

Ujenzi wa tuta unaendelea kwa ajili ya kuzuia uingiaji wa maji ya bahari katika bonde la

mpunga Mziwanda unaendelea na jumla ya Tshs 50, 000,000/- za SMZ zimetumika.

.

Vijishamba darasa 10 (kumi) vimetayarishwa vya maonesho Unguja na Pemba jumla ya

Tshs.,000,000/-zimetumika.

2.2. 0WIZARA YA BIASHARA VIWANDA NA MASOKO

2.2.1. IDARA YA BIASHARA NA UKUZAJI MASOKO

Idara ya Biashara, Viwanda na Masoko kwa mwaka wa fedha 2011/2012 imepangiwa kutekeleza

malengo yafuatayo:-

i) Kuendeleza, kuimarisha mazingira bora ya ukuzaji Biashara, kwa kuufanyia mapitio makubwa mfumo

wa utoaji leseni za biashara nchini.

ii) Kuwasilisha Serikalini kwa mazingatio rasimu za sheria mpya za ushindani, mizani na vipimo na

sheria ya biashara.

iii) Kuanza utekelezaji wa sheria ya viwango ya Zanzibar.

iv) Kuendelea kutafuta masoko ya ndani na nje ya bidhaa zinazozalishwa hapa Zanzibar.

v) Kukusanya mapato ya Tsh.30, 000,000.00, kutokana na kazi za ukaguzi wa vipimo.

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Kazi ya utekelezaji wa Sheria ya Viwango bado haijaanza .Hata hivyo Wizara imeshapatiwa

majengo mawili kwa ajili ya maabara na Ofisi.Serikali inaendelea na hatua za uteuzi wa

mtendaji mkuu.Aidha ununuzi wa vifaa, samani za ofisi na uajiri wa wataalamu wengine

utafanyika baada ya kuajiriwa mtendaji mkuu.

Mapitio ya mfumo wa leseni yamekamilika na utungaji wa rasimu ya sheria kwa ajili hiyo

unaendelea. Rasimu hiyo inakusudia kuifuta sheria ya leseni Nam.3 ya 1983 inayotumika hivi

sasa.

Mapitio ya Sheria zinazohusiana na ushindani na kumlinda mtumiaji, mizani na vipimo na sheria

ya biashara.

Wizara imesitisha kuendelea na taratibu hizi mpaka pale sheria mpya ya leseni itakapokuwa

tayari. Kwani sheria hiyo pamoja na mambo mengine itaelekeza mfumo wa utoaji vibali, usajili

na mambo mengine yanayohusiana na biashara.

Kusimamia uendeshwaji wa biashara halali kwa kuimarisha ufuatiliaji wa ubora wa vipimo na

mizani na kumlinda mtumiaji.

i) Kazi za Ukaguzi

Idara kwa kipindi cha Julai hadi Desemba, 2011 jumla ya mizani 919, Pampu za mafuta 15,

gari za kubebea mafuta 6, Underground tank na flow meter moja vilikaguliwa kwa Unguja na

Pemba. Kiasi cha Tsh. 10,920,500/- ambazo ni asilimia 33.64 ya lengo.

Maduka 1151, maghala 38 na viwanda 6 vimekaguliwa na bidhaa zenye thamani ya Tsh. 6, 677,

6000/- zimeharibiwa ambazo zilikutwa zikiwa tayari zimepitwa na wakati au kuharibika.

ii) Usimamizi wa bei za bidhaa muhimu za chakula.

Wizara imeanza utekelezaji wa kanuni za kusimamia bidhaa na huduma za biashara za mwaka

2011. Kanuni hizo pamoja na mambo mengine zimeweka utaratibu maalum wa uwekwaji wa

bei za bidhaa hizo muhimu.

Katika ufuatiliaji wa masoko ya ndani,Wizara imeratibu ushiriki wa wajasiriamali katika

maonesho ya kimataifa ya saba saba ambapo wajasiriamali 50 walishiriki,Maonesho ya nane

nane wajasiriamali 8, maonesho ya ujio wa Prince Charles wajasiriamali 8, maonesho katika

Mkutano wa Sita wa Baraza la Biashara (ZBC) Wajasiriamali 20 na maonesho ya Wasiria

ambapo wajasiriamali 10 walishiriki.

Page 8: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

8

Kwa upande wa masoko ya Nje Wizara imeratibu ushiriki wa maonesho ya Jua kati

yaliyofanyika Rwanda ambapo wajasiriamali sita walishirik.Aidha Wizara imewapatia mafunzo

juu ya mbinu za kisasa za utafutaji wa masoko ambapo Mjasiriamali mmoja alipelekwa nchini

Afirika ya Kusini chini ya udhamini wa Shirika la Biashara la Dunia (WTO) na Wajasiriamali

wawili nchini China kwa udhamini wa Serikali ya China.Aidha Wizara imetoa mafunzo ya

usarifu wa ngozi na utafutaji wa masoko kwa bidhaa zinazotokana na ngozi ambapo

wajasiriamiali 23 wanashiriki mafunzo hapa Zanzibar.

Uwanja wa Kimataifa wa Maonesho ya Biashara

Katika kuhakikisha kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendeleza ukuwaji wake wa

Uchumi kupitia Biashara; imeliandaa eneo la uwanja wa Maoneshao ya Kimataifa liliopo

Nyamanzi, Wilaya ya Magharibi nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Eneo hilo limewekwa alama yaani (becon) na kinachosubiriwa ni kutolewa Zabuni kwa ajili ya

kuliendeleza katika:-

i) Kutayarisha michoro ya matumizi ya ardhi (land use plan)

ii) Kutayarisha michoro ya kihandisi

iii) Kutayarisha gharama za mradi

Hata hivyo hadi mwishoni mwa mwezi wa Disemba zabuni hiyo haijatangazwa.

ZIARA YA KAMATI KATIKA SHIRIKA LA VIWANGO TANZANIA (TBS)

Katika kuhakikisha kuwa Serikali ya Mapinduzi inaweka taasisi ya kudhibiti ubora wa bidhaa

zinazotumiwa na Wananchi (ZBS). Kamati ilipata fursa ya kutembelea Shirika la Viwango Tanzania

(TBS) kwa lengo la kupata uzoefu ili kuweza kushauri Serikali juu ya suala hilo.

Shirika la Viwango Tanzania awali ililianzishwa kupitia Sheria ya Viwango Nam 3 ya mwaka 1975 na

kuanzishwa tena upya kwa sheria Nam 2 ya 2009, ambayo imeongeza nguvu na uwezo wa Shirika katika

kuchukua hatua mbalimbali kama vile kuondoa bidhaa hafifu zilizoko sokoni ,kufuta leseni,kuwepo kwa

utaratibu wa marejesho na/au faida,kuweka taratibu za kuharibu bidhaa duni au kuzirudisha zilikoagizwa

na kutozwa faini.

Miundombinu

Shririka la TBS limekuwa na majengo ya kisasa yenye kukidhi haja iliyopo yakiwemo majengo yenye

Maabara za upimaji bidhaa na yenye vifaa vya kisasa,majengo ya Afisi na wataalamu wenye sifa mbali

mbali katika taaluma ya sanyansi na kwa sasa lina jumla ya Wafanyakazi 195.

ZIARA YA KAMATI KATIKA DEPORT YA MTONI

Kamati imefanya ziara katika Deport za Mtoni kutokana na kuwepo ukosefu wa mafuta unaojitokeza

mara kwa mara.Katika ziara hiyo ambapo Kamati ilipata nafasi ya kuzungumza na uongozi wa Kampuni

zote tatu zinazojishughulisha na uagizaji wa mafuta Kampuni hizo ni GAPCO, United Petroleum (UP)

na Zanzibar Petroleum(ZP) na kupata changamoto zifuatazo ambazo ndizo zinazopelekea ukosefu huo

wa mafuta.:-

Urasimu mkubwa katika bandari ya Dar-es –Salam .Kutokana na kubadilika kwa sheria ya

EURA ambayo inaruhusu muagizaji mmoja tu wa mafuta kutoka nje ya Nchi na kuziuzia

Kampuni mbalimbali za mafuta kumesababisha kuwepo na foleni kubwa jambo ambalo

linapelekea meli ndogo hasa zinazotoka Zanzibar kuchelewa kuyapata mafuta hayo kwa wakati

,ambapo Kampuni ya GAPCO ndio wanaochukua Dar-es-Salaam.

.

Kupigwa marufuku uingizwaji wa mafuta kwa kutumia njia ya meli kwa meli ambapo njia hii

inapelekea kufanyika kwa magendo ya mafuta kwa wingi sana na kuikosesha Serikali mapato

yake.Utaratibu huo unafanywa na Kampuni ya United Petrolium na Zanzibar Petrolium (ZP)

Page 9: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

9

TARATIBU ZA KULIFUNGA SHIRIKA LA MAGARI

Hatua za kulifunga shirika zinaendelea kwa kutayarisha mafao ya wafanyakazi kwa kuzingatia

mabadiliko ya mishahara.,na kwa maana hiyo hati inatayarishwa ya kuzingatia deni na maslahi ya

Wafanyakazi .Hati hiyo inatarajiwa kuwasilishwa kwa Mheshimiwa Rais baada ya kukamilishwa kwa

kazi hizo.

SHIRIKA LA TAIFA LA BIASHARA (ZSTC)

Shirika la Taifa la Biashara limefanyiwa marekebisho katika muundo na uendeshaji wake.Katika kukidhi

haja hiyo sheria Nam 11 ya mwaka 2011 ilitungwa ikiainisha majukumu ya msingi ya

Shirika.Halikadhalika mpango kazi wa shirika umeandaliwa na ulitarajiwa kuwasilishwa Serikalini

mwezi Feburuari 2012.

Shirika la Taifa la Biashara Zanzibar ndilo lenye jukumu kubwa la ununuzi wa zao la karafuu kutoka

kwa wakulima wa Zanzibar. Zao ambalo ndio tegemeo kuu la kiuchumi kwa Taifa. Itakumbukwa

kwamba katika misimu ya mavuno ya karafuu iliyopita ununuzi wa karafuu ulikuwa ni mdogo sana kwa

Shirika pamoja na kuwa kulikuwa na mavuno ya kuridhisha lakini inaonekana wakulima wengi walikuwa

hawapeleki karafuu zao ZSTC kwa madai ya kwamba bei inayotolewa ni ndogo na hivyo wakulima

waliziuza kwa wafanyabiashara wa magendo.

Hali Halisi ya Ununuzi

Katika msimu ulioanzia mwezi Julai, 2011 Serikali kupitia ZSTC ilipandisha bei mara tatu kwa kipindi

cha kisichozidi miezi mitatu, ambapo bei iliyokuwapo ya Sh. 5,000/- kwa kilo ya karafuu ya daraja la

kwanza ilipanda hadi Sh.10, 000/- na baadae kuwa Sh. 12,000/- na kwa sasa [Septemba 2011] imefikia

Sh. 15,000/-.

Kwa kipindi cha miezi mitano Julai hadi Novemba, 2011 Shirika lilikadiria kununua tani za karafuu

2,165 kwa thamani ya Tshs 32.475bilioni kwa Unguja na Pemba,ambapo kwa kipindi hicho manunuzi

halisi yalikuwa ni jumla ya tani 2695.3335 zenye thamani ya Tshs 40,204,6,39500 ikiwa ni ziada ya

kuvukwa kwa lengo hilo kwa asilimia 24%. Kwa upande wa mauzo hadi kufikia tahere 30 Novemba

2011 Shirika limeweza kuuza jumla ya tani 2018.76 za karafuu zenye thamani ya USD 27.500,160

ambapo wastani wa bei ni kati USD 13.647.

Hali ya Magendo

Kwa ujumla suala la usafirishaji wa magendo ya karafuu Kisiwani Pemba limepungua kwa kiasi kikubwa

kwani idadi ya karafuu zinazopelekwa ZSTC inadhihirisha ukweli huo. Kipindi cha kuanzia mwezi Julai

hadi Septemba, 2011 jumla ya karafuu zenye uzito wa kilo 878 zilikamatwa.

Malalamiko Pamoja na kazi nzuri inayofanywa na wafanyakazi wa Shirika katika kutoa huduma kwenye vituo hivyo

Kamati ilipokea malalamiko yafuatayo:

Wakulima/wauza karafuu wanawalalamikia wachukuzi juu ya kuwatoza fedha nyingi kwa ama

kuwabebea mazao yao au kuwasafishia na kuwasindikia karafuu zao. Bei ya cheti cha kuchukulia

mazao inatofautiana kati ya Mkoa wa Kusini na Kaskazini (Mkoa wa Kusini ni Sh. 500/- wakati

Kaskazini ni Sh. 1,000/- kwa cheti kimoja)

Bado wakulima wana wasiwasi juu ya ubora wa mizani zinazotumiwa na Shirika kuwa ni za

kizamani lakini vile vile wakulima wenyewe baadhi yao wanashindwa kuzisoma wakati wa

kupimiwa karafuu zao.

Vipimo vya uzito wa gunia vilikuwa vinababaisha kati ya gunia lenye uzito wa kilo moja na lile

lenye uzito kilo moja na nusu. Halkadhalika uzito wa kipimo cha robo kilo ya karafuu nacho

kifanyiwe malipo. Utoaji wa vibali vya kusafirishia karafuu kutoka Wilaya moja kwenda nyengine

umekuwa na tatizo.

Majengo ya baadhi ya vituo vya kuuzia karafuu yako katika hali mbaya na hayana hata vyoo.

Page 10: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

10

2.3.0. WIZARA YA NCHI (OR) FEDHA NA MIPANGO YA MAENDELEO

2.3.1. IDARA YA MHASIBU MKUU WA SERIKALI

MAJUKUMU

Idara ya Mhasibu Mkuu wa Serikali ina majukumu makubwa ya kuitunza Hazina ya Serikali, kusimamia

mwenendo wa Deni la Taifa, kudhibiti mapato na vilevile kusimamia shughuli za kihasibu na Ukaguzi wa

Ndani kwa kuhakikisha kwamba taratibu na sheria zote zinazohusika zinafuatwa katika suala zima la

kudhibiti mapato na matumizi ya Serikali.

MALENGO YA IDARA

Katika kipindi cha mwaka 2011/2012 Idara ilipanga kutekeleza mambo yafuatayo:

(i) Kufanya jumuisho la Hesabu na kuliwasilisha kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za

Serikali.

(ii) Kuendelea kutoa kipaumbele kwa malipo ya mishahara, malipo ya Wastaafu na malipo mengineyo.

(iii) Kuendelea kutoa mafunzo (Muda mfupi na Muda mrefu)

(iv) Kusimamia Deni la Taifa.

UTEKELEZAJI WA MALENGO YA IDARA

Katika suala zima la jumuisho la Hesabu za Serikali ni kwamba Idara imekwisha kamilisha hesabu

kutoka kwenye Wizara zote na ipo katika hatua za mwisho na ilitarajiwa kuliwasilisha jumuisho hilo

kabla ya mwezi wa Disemba, 2011.

Kwa upande wa malipo ya mishahara, zoezi limeendelea kama kawaida na kwa wakati ikiwa ni pamoja

na mabadiliko ambayo yalianzia mwezi wa Oktoba, 2011. Mabadiliko hayo ambayo ni makubwa kiasi

yameleta changamoto kiasi lakini hata hivyo Serikali imeweza kukabiliana nazo. Aidha Serikali

inaendelea kuwalipa mafao Wastaafu ikiwa ni pamoja na viinua mgongo na pencheni zao kwa wakati

muwafaka, ambapo hadi kufikia mwezi wa Novemba, 2011 imeweza kuwalipa wastaafu wote waliostaafu

hadi mwezi wa Agosti, 2011. Na hivyo jumla ya Tsh.2.186 Billioni zimetumika kulipa viinua mgongo

vya wastaafu 351. Madai ya Wastaafu wa miezi ya Septemba, Oktoba na Novemba, 2011 yalikuwa ni

Tsh. 896 Milioni na yalitarajiwa kulipwa mwezi wa Disemba, 2011 na Januari, 2012.

Wakati huohuo suala la matumizi mengineyo (Other Charges) kwa kipindi cha miezi mitano (Julai –

Novemba) jumla ya Tsh. 2, 237, 597,000/- sawa na asilimia 41 zilitolewa kupitia Wizara na Taasisi

mbalimbali za Serikali. Deni la Taifa nalo limefikia Tsh. 186.25 Billioni hadi mwezi Novemba, 2011

hiyo ilikuwa ni sawa na asilimia 19.63 ya pato la Taifa. Kiwango hicho kwa Nchi zinazoendelea kama

yetu huwa hakitishi sana.

Wakati Deni la Ndani kwa mwezi huo wa Novemba lilikuwa limefikia Tsh.43.46 Billioni sawa na

asilimia 23 ya Deni lote, ikiwa ni ziada ya Tsh.7.12bil. Ikilinganishwa kama ilivyokuwa kwa mwezi wa

Juni,2011 ambapo kiwango kilikuwa ni Tsh.36.34 billioni. Deni la Nje nalo limeongezeka kwani hadi

kufikia mwezi wa Novemba, 2011 lilifikia Tsh. 142.79 bilioni sawa na asilimia 76.66 (USD 86.23mil)

ikiwa ni ziada ya Tsh.17.37 bilioni kwani mwezi wa Juni, 2011 Deni lilikuwa Tsh.125.42 bilioni (USD

79.39Mil).

Deni hili la Nje limeongezeka kutokana na sababu mbili kuu za msingi ambazo ni:-

a.) Kuingizwa kwa fedha katika Miradi

b.) Mabadiliko ya thamani ya Shilingi ya T anzania ikilinganishwa na zile za kigeni.

2.3.2. IDARA YA BAJETI

MALENGO YA IDARA

i) Kukamilisha maandalizi ya mfumo wa Program Based Budgeting na kuanza kutumia rasmi

mfumo huo wa bajeti katika mwaka wa fedha wa 2012/2013.

ii) Kusimamia utekelezaji wa Bajeti ya Serikali ya mwaka 2011/2012.

iii) Kutoa muongozo wa mafunzo maalum kwa Wizara na Taasisi mbali mbali za Serikali.

Page 11: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

11

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Katika kutekeleza suala la utayarishaji, utekelezaji na ufuatiliaji wa bajeti ya Serikali. Taasisi

zimepatiwa ruzuku kwa asilimia 100. Jumla ya fedha kwa ruzuku hizo ni Tshs 3,170,576,666/-

ambazo zilipewa Taasisi zifuatazo :-

i) Bodi ya Mapato Zanzibar

ii) Mfuko wa Barabara

iii) Chuo cha Utawala wa Fedha Chwaka

iv) Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali

v) Mamlaka ya Uwekezaji Vitega Uchumi Zanzibar

Muongozo wa kwanza umetayarishwa na umeshatolewa kwa Wizara sita pamoja na Mafunzo

kwa Wizara hizo, ambapo walengwa katika mafunzo hayo ni Makatibu

Wakuu,Wakurugenzi,Viongozi wa ndani wa Wizara ya Nchi (OR)Fedha ,Uchumi na Mipango

ya Maendeleo na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi. Fedha zilizotumika katika kufanikisha

kazi hiyo ni jumla ya Tshs 25,281,900/-.

2.3.3. IDARA YA UTUMISHI NA UENDESHAJI

MALENGO YA IDARA

i) Kuanza maandalizi ya Ofisi Pemba

ii) Kuendelea na utekelezaji wa mapendekezo ya Mshauri Mwelekezi ya kuwajengea uwezo

wafanyakazi wa Ofisi ya Rais Fedha Uchumi na Mipango ya Maendeleo.

iii) Kuwapatia wafanyakazi 83 wa Ofisi ya Rais Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo mafunzo

ya muda mrefu na mfupi ndani na nje ya nchi;

iv) Kuandaa mafunzo ya ndani (In house training) kwa wafanyakazi 60 kwa lengo la kuwaongezea

uwezo, ujuzi na uzoefu katika utendaji wa kazi zao.

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Maandalizi ya Ujenzi wa Ofisi ya Wizara Pemba yalianza lakini kwa bahati mbaya ujenzi huo

haukufikia hatua ya kukabidhiwa kutokana na makosa ya kiufundi yaliyotokea na kuathiri

kiwango kikubwa jengo hilo na kupelekea kusitishwa kwa kazi ya ujenzi.

Mpaka ujenzi unasitishwa gharama zilizotumika ni jumla ya Tshs 736,826,936/-.Wizara tayari

wameshapatiwa kiwanja chengine katika eneo la Gombani na iko katika hatua ya kuingia

mikataba na Idara ya Ujenzi Michenzani.

Wafanyakazi wamepatiwa mafunzo ya muda mrefu ni 13 na muda mfupi 34 fedha zilizotumika

katika kazi hiyo ni jumla ya Tshs 404,206,007/-.

2.3.4. IDARA YA URATIBU WA SHUGHULI ZA SMZ-DSM

MALENGO YA IDARA

Idara ina majukumu ya kuratibu shughuli mbalimbali za kiuchumi na maendeleo baina ya SMZ na

Wizara za SMT ikiwa ni pamoja na kuratibu ushirikiano wa kiuchumi baina ya SMZ na Ofisi za Kibalozi

pamoja na taasisi za Umoja wa Mataifa zenye Ofisi zake Dar es Salaam.

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Suala la kuratibu na kukuza ushirikiano.

Katika kipindi cha mwezi wa Novemba hadi Disemba 2011, Idara iliomba jumla ya Tsh. 14,589,000/-

kwa kazi ya kuratibu na kukuza ushirikiano na kuingiziwa TSH. 1,000,000/-.Kazi iliyofanyika ni

kushiriki kwenye vikao vya uteuzi wa waombaji wa masomo ya juu katika fani mbali mbali chini ya

ufadhili wa Nchi ya Serbia na kazi nyengine iliyofanyika ni kuhudhuria mkutano wa maandalizi ya

Mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Page 12: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

12

Suala la kuendeleza na kuimarisha uwezo wa Utawala wa rasilimali watu.

Hadi kufikia mwezi wa Disemba, 2011 Idara haikuweza kuingiziwa fedha ilizoomba (Tsh. 8,000,000/-)

na hivyo lengo hilo halikuweza kutekelezwa.

Suala la kuweka mazingira bora ya utendaji kazi ili kuleta ufanisi wa kazi.

Fedha zilizoingizwa kwa kazi hii ni jumla ya Tsh.21, 000,000/- kati ya 37,000,000/- zilizoombwa. Fedha

hizo zimewezesha kumpatia mafunzo mfanyakazi mmoja, kufanya matengenezo kwa gari moja na baadhi

ya huduma nyengine ndogondogo.

2.3.5. IDARA YA UHAKIKIMALI NA MITAJI YA UMMA

MALENGO YA IDARA

Idara imepanga kutekeleza majukumu yafuatayo:

i) Kukamilisha tathmini ya mali za kudumu na kukamilisha uandaaji wa Daftari la mali za

kudumu za Serikali.

ii) Kuendeleza uhakiki wa mali za Serikali katika Wizara na Taasisi za Serikali.

iii) Kusimamia na kuratibu ufunguji wa hesabu za mwaka katika mashirika ya Serikali

iv) Kusimamia ununuzi na uondoaji wa mali za Serikali kwa mujibu wa sheria.

v) Kuendelea kusimamia sheria ya manunuzi No 9 ya mwaka 2005 na sheria ya Mitaji ya

Umma No 4 ya mwaka 2002.

vi) Kuendelea kuwajengea uwezo watendaji katika masuala ya ununuzi Serikalini.

vii) Kufanya ukaguzi katika manunuzi yanayofanywa na taasisi za Serikali.

viii) Kuanzisha Daftari maalum la wakandarasi na watoa huduma nyengine wenye sifa za

kupewa kazi hizo Serikalini.

ix) Kufanyia tathmini mashirika ya umma na kuishauri Serikali juu ya marekebisho yake.

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Kuhusu lengo la kuendeleza uhakiki wa mali za Serikali na uanzishwaji wa Daftari la mali hizo

katika Wizara na Taasisi za Serikali.

Taratibu za kupata kampuni ya kufanyaka kazi ya kutathimini na uanzishwaji wa Daftari la

mali za Serikali zimekamilika na kazi hiyo imefanyika kwa asilimia 40.

Kazi ya kutengeneza nyaraka za manunuzi na miongozo yake inaendelea na imefanyika

kwa asilimia 50, fedha zilizotumika ni jumla ya Tshs 550,000/-

Idara imefanya semina nne Unguja na Pemba kwa wadau wote wa sheria ya manunuzi na

uondoshaji wa mali za Serikali,fedha zilizotumika ni Tshs 2,200,000/-

Kazi za ukusanyaji taarifa za manunuzi zinaendelea na zimeshafanyika kwa asilimia

75,fedha zilizotumika ni Tshs 750,000-/

Ripoti ya mwaka ya ukaguzi wa mali kazi na huduma za Serikali katika Wizara na Taasisi

za Serikali imetayarishwa kwa asilimi 60.

Idara imeweza kufanya uchanganuzi wa mahesabu kwa mashirika ya Bandari, Utalii na

Benki ya Watu wa Zanzibar, fedha zilizotumika ni Tshs 550,000/-na kazi hiyo imefanyika

kwa asilimia 75.

Kazi ya kuweka kumbukumbu za udhibiti wa mitaji na hisa za uwekezaji wa Serikali

inaendelea, jumla ya fedha zilizotumika Tshs 250,000 na kazi imefanyika kwa asilimia 50.

Miradi ya ujenzi wa Ofisi za Serikali inaendelea kwa kuanza matayarisho ya ujenzi kwa

Ofisi zifuatazo; Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu , Ofisi ya Mwanasheria

Mkuu, Jengo la E-Government, Katiba na Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora,

fedha zilizotumika Tshs 716,968,282/-.

Tathmini ya mali za Serikali.Kazi hiyo mshauri mwelekezi ameshapatikana na kazi

itaanza katika kipindi cha robo ya tatu.

MFUKO WA HIFADHI YA JAMII

MALENGO YA MFUKO

Mfuko umekusudia kufanyia mageuzi makubwa mfumo wa hifadhi ya jamii.Chini ya Mfuko huu

sheria ya ZSSF itafanyiwa marekebisho ili iweze kwenda sambamba na mageuzi hayo.

Page 13: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

13

UTEKELEZAJI WA MALENGO

Uwekezaji wa muda mfupi

Dhamana za hazina kupitia BoT zenye thamani ya Tshs 1,141,905,000/- zimenunuliwa na faida

iliyopatikana ni Tshs 43,628,179/-

Jumla ya Tshs 17,450,000,000/- zimewekezwa katika akiba za benki za muda maalum na faida

iliyopatikana ni Tshs 1,509,279,339/-

Fedha zilizowekezwa katika majengo na kodi iliyopatikana ni Tshs 1,552,907,518/-.

Uwekezaji wa muda mrefu:

Fedha zilizowekezwa kupitia TANRE zilikuwa 1,413,226,000/- hakuna gawio lililofanyika

hadi kufikia Disemba 2011.

Fedha nyengine zimewekezwa katika majengo na kodi ambazo ni Tshs 5,423,197,461/-. Na

faida iliyopatikana ni Tshs 112,706,000/-

Fedha zilizowekezwa katika dhamana za Serikali kupitia BoT ni Tshs 27,459,753,880/-

faida iliyopatikana ni Tshs 1,851,275,635/-

Thamani ya Vipande vya UTT ni Tshs 1,027,024,184/- na thamani ya vipande hivyo

iliongezeka kwa Tshs 25,620,315/- kwa kipindi cha miezi mitatu (Oktoba hadi Disemba,

2011).

Thamani ya hisa za TPCC ni Tshs 677,697,280/- thamani ya hisa hizo imeongezeka kwa

Tshs 6,516,320/- kwa kipindi cha (Oktoba hadi Desemba 2011).

Hisa za NMB ni Tsh 1,384,294,700/- hadi Disemba 2011 hakujakuwa na ongezeko la

thamani ya hisa hizo.

Hisa za CRDB ni 1,299,037,680/- hadi Disemba 2011 hakujakuwa na ongezekao la thamani

ya hisa hizo.

Jumla la Tshs 16,585,394,737/- zimekopeshwa kwa taasisi tofauti za Serikali na faida

iliyopatikana ni Tshs 198,795,223.33/- hadi kufikia Disemba 2011 .Fedha hizo

zimekopeshwa kwa Taasisi zifuatazo:-

ZRB, Tshs 3, 785, 394,737/-na faida iliyopatikana ni Tshs 136, 459,892/-

ZSTC, Tshs 12, 000, 000,000/- na faida iliyopatikana ni Tshs 62, 335,331/-

ZIPA, Tshs 800, 000,000/- hakuna faida iliyopatikana hadi Kamati inapatiwa maelezo

haya.

Jumla Tshs 7, 500, 000,000/- zimewekezwa kwenye dhamana za SMZ.

Thamani ya Vipande vya Jikimu Fund ni Tshs 1, 983, 524,181 hadi kufikia Disemba 2011

thamani ya vipande hivyo imepungua kwa Tshs 12, 434,542.02/- Gawio la Tshs 71,

725,894.80 limepatikana. Mfuko unatarajia faida ya Tshs 2, 221, 247,620/- katika uwekezaji

wake wa muda mrefu hadi Disemba 2011.

Ulipaji wa mafao.

Mfuko umekuwa ukiendelea kulipa mafao ya uzee, mafao ya urithi pamoja na mafao ya ulemavu. Jumla

ya Wanachama 114 wamelipwa mafao yao katika kipindi cha Oktoba 2011 hadi Disemba 2011 dhidi ya

lengo lililowekwa la Wanachama 201.Hii ni sawa na asilimia 54 ya lengo na Jumla ya fedha zilizotumika

ni Tshs 532, 951,022/-

Uwekaji wa Kumbukumbu

Mfuko unaendelea kutekeleza miradi ya kuboresha uwekaji wa kumbukumbu za Mfuko kwa kutumia

mifumo ya TEHAMA) ICT). Katika utekelezaji wa miradi hiyo mpango mkakati mkuu wa TEHAMA wa

miaka mitano uliandaliwa na kuanza utekelezaji wake mwaka 2009.Kati ya miradi saba ya ICT

iliyotarajiwa kutekelezwa mitano imeshaanza na imo katika hatua mbali mbali za utekelezaji.

Page 14: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

14

MAMLAKA YA KUSIMAMIA SHUGHULI ZA BIMA (TIRA)

Jukumu kubwa ni kusimamia shughuli za Bima ambazo zinatolewa na Kampuni mbalimbali za Bima

hapa nchini.

Kazi zake

Miongoni mwa kazi zake ni pamoja na Usajili wa Kampuni za Bima na Madalali, Usajili wa Mawakala

na Wakadiriaji Hasara, Ukaguzi wa Kampuni za Bima na Ushughulikiaji wa Malalamiko ya Wateja na

Wadau wengine wa Bima.

Utekelezaji.

Usajili wa Kampuni za Bima na Madalali kwa Upande wa Zanzibar.

Jumla ya kampuni nne za Bima zilizosajiliwa chini ya Sheria ya Bima hadi kufikia tarehe 31 Disemba,

2010 , ambazo ni Shirika la Bima la Zanzibar (ZIC), Jubilee Insurance Company (T) Ltd, National

Isurance Corporation (T) Ltd na African Life Assurance Company.

Jumla ya Madalali wa Bima waliosajiliwa hadi kufikia tarehe 31 Disemba, 2010 na wanafanya shughuli

zao Zanzibar ni kumi na nne (14).

TUME YA PAMOJA YA FEDHA.

Tume ya Pamoja ya Fedha ilianzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya

mwaka wa 1977, Ibara ya 134 na kuanzishwa kwa Sheria ya Tume hii ya mwaka 1996 (Sura ya 140).

MAJUKUMU YA TUME.

Miongoni mwa majukumu ya Tume ni :-

a) Kuchambua mapato na matumizi yanayotokana na, au yanayohusu utekelezaji wa Mambo ya

Muungano, na kutoa mapendekezo kwa Serikali zote mbili kuhusu mchango na mgao wa kila mojawapo

wa Serikali hizo;

b) Kuchunguza kwa wakati wote mfumo wa shughuli za fedha za Jamhuri ya Muungano na pia uhusiano

wa mambo ya kifedha kati ya Serikali mbili;

c) Kutekeleza majukumu mengine ambayo Rais ataipatia Tume au kama Rais atakavyoagiza, na kwa

mujibu wa Sheria iliyotungwa na Bunge.

UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU

Katika kutekeleza majukumu yake Tume imefanya stadi mbalimbali zikiwa kama ni ushauri wa

kitaalamu kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa

Tanzania (SMT) Miongoni mwa stadi hizo ni kuhusu:-

UHUSIANO WA KIFEDHA BAINA YA SMT NA SMZ.

Uchambuzi wa masuala ya fedha yanayohusu mambo ya Muungano.

Vyanzo vya Mapato ya Muungano.

Uimarishaji wa Sera za Bajeti na fedha baina ya SMZ na SMT.

Usimamizi wa Deni la Taifa baina ya SMT na SMZ.

MAPENDEKEZO. i) Vigezo vya kugawana Mapato na Kuchangia Gharama za Muungano.

ii) Marekebisho ya Sheria ya Tume ya Pamoja ya Fedha.

iii) Muongozo wa Uendeshaji wa Akaunti ya Fedha ya Pamoja.

iv) Kuimarisha mfumo wa Bajeti na Fedha baina ya SMT na SMZ.

v) Utaratibu wa kushughulikia ushauri unaotolewa na Tume kwa Serikali mbili.

vi) Marekebisho ya Sheria ya Ushuru wa Bidhaa.

Page 15: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

15

BENKI YA POSTA TANZANIA. Benki ya Posta Tanzania (TPB) imeanzishwa kisheria mwaka 1992 ikiwa ni Taasisi iliyopewa leseni na

Benki Kuu ya Tanzania ambayo inajiendesha kama taasisi ya Fedha (Non-bank Financial Insititution),

madhumuni makubwa yakiwa ni:-

Kukusanya amana za wateja.

Kuendesha shughuli zote zinazoendeshwa na mabenki ya biashara.

Kutoa huduma bora za kibenki kwa mujibu wa Sheria za Mabenki na Taasisi za Fedha nchini.

UTEKELEZAJI WA MALENGO.

Benki imepanga kutekeleza mambo yafuatayo:-

i) Kuongeza mtaji wa benki kutoka Tsh.6.7 Bilioni mwaka 2010 na kufikia Tsh. 11.6 mwaka 2011.

ii) Kuongeza amana za Wateja kutoka asilimia 20 hadi asilima 30 kwa kila mwaka, ambapo kw a

mwaka 2011 ilifikiwa.

iii) Kupunguza hasara zinazotokana na shughuli za kibenki ikilinganishwa na mapato, uwiano huo

usizidi asilimia 2 kwa mwezi.

iv) Kuongeza tija na ufanisi na uzalishaji wa faida kutoka Tsh. 3.5 milioni mwaka 2010 na kufikia

Tsh. 5.47 milioni kwa mwaka 2011.

Mgawanyo wa Hisa.

Mgawanyo wa hisa na umiliki wa benki hadi Novemba, 2011 ni kama ifuatavyo:-

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni asilimia 75.2

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ni asilimia 7.5

Shirika la Posta Tanzania lina asilimia 22.0 na

TP&TC SACCOs ni asilimia 6.5

Mikopo.

Benki ilianza kutoa mikopo mwaka 1998, Mikopo inayotolewa ni ya; Biashara, Watumishi wa Umma,

Mikopo midogo midogo na Mikopo ya Uwezeshaji.

Hadi kufikia mwezi wa Novemba, 2011 jumla ya Tsh .62, 972.7 milioni zimetolewa, kati ya hizo Tsh.

1,2037 milioni zimetolewa kwa Tawi la Zanzibar.

BENKI YA WATU WA ZANZIBAR LTD.

Tawi la Kariakoo – Dar es Salaam

Katika kuimarisha shughuli zake PBZ imeanza kutoa huduma Tanzania Bara kuanzia tarehe 29/4/2011

kwa ufunguzi wa Tawi lake liliopo Mtaa wa Kariakoo DSM , Tawi ambalo linatoa huduma zote za

kibenki zinazopatikana hata kwenye matawi mengine yote.

Maendeleo yake.

Tangu kuanzishwa kwake (Tarehe 29/4/2011) hadi Novemba, 2011 limeweza kuweka amana za Wateja

Tsh. 6,084,465,849/- na kutoa mikopo ya Tsh. 11,055,245,000/- kati ya hizo 1,700,000,000/- ni kwa ajili

ya mkopo wa Biashara.

Tawi la Huduma za Benki ya Kiislamu (Islamic Division).

Katika kutanua wigo wa Biashara, Benki pia imefungua tawi la huduma za Kiislamu ambalo

lilifunguliwa rasmi na kuanza huduma hizo Tarehe 10/12/2011.

Maendeleo yake.

Katika kipindi kisichozidi mwezi mmoja tangu kufunguliwa benki imeweza kuwa na wateja 190 na

kuweka amana za Tsh. 306 milioni.

Page 16: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

16

BENKI YA WATU WA ZANZIBAR TAWI LA CHAKE CHAKE-PEMBA.

Amana za Wateja.

Jumla ya Tsh 7,951.62 milioni zimewekwa kama amana za wateja hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2011

katika Tawi la Benki la Chakechake zikiwemo Tsh.4,540 milioni kama akiba (Saving), Tsh.3,137.56

milioni kama biashara (Current), Tsh. 274.06 milioni ni ya Muda maalum (Fixed). Wakati amana

nyenginezo zilikuwa na thamani ya Tsh.0.88 milioni.

Utoaji wa Mikopo.

Kwa upande wa Mikopo kwa wafanyakazi Tawi la Benki la Chakechake kwa kipindi cha kuanzia Julai,

2010 hadi Juni, 2011 limetoa mikopo kwa wafanyakazi 3,171 yenye thamani ya Tsh. 7,425 milioni.

Wakati kwa upande wa mikopo ya uwezeshaji wananchi kiuchumi (AK na JK) hadi kufikia Juni, 2011

wananchi waliofaidika na mikopo hiyo ni 201 kwa thamani ya Tsh.329.211 milioni. Ukilinganisha na

waliopata fursa hii katika kipindi kilichoishia Juni, 2010 idadi ya wananchi waliopata ni 188 kwa mkopo

wenye thamani ya Tsh.407.396 milioni.

Utoaji wa mikopo ya JK na AK imesitishwa kwa muda kutokana na kujitokeza kasoro ambazo

zimelifanya zoezi hili kuwa gumu hasa wakati wa marejesho ya mikopo hiyo. Hivyo Benki inasubiri

maelekezo kutoka kwa W izara ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kwa maelekezo na utaratibu mzuri

utakaowezesha mikopo hiyo kutolewa na kurejeshwa bila ya matatizo.

Faida ya Tawi.

Tawi la Benki la Chakechake linajiendesha wenyewe kwenye mapato na matumizi na kwa kipindi hadi

kufikia Tarehe 30 Juni, 2011 limeweza kupata faida ya Tsh. 125.63 milioni.

Aidha linaimarisha huduma zake kwa kutumia mtandao wa Benki (Banking Computer Software) ambao

unamruhusu mteja kuweza kupata huduma ya kutoa na kuweka fedha zake tawi lolote la Benki ya Watu

wa Zanzibar.

Katika kuendeleza huduma hizo na kupunguza msongamano kwa wateja Benki imeanzisha huduma

kwenye vituo vya Wete na Mkoani halikadhalika kumeanzishwa huduma za ATM kwa miji ya

Chakechake ATM tatu, Wete ATM moja, Mkoani ATM moja na Konde ATM moja.

Ujenzi wa Jengo Jipya.

Katika kufanikisha lengo la kutoa huduma bora kwa wateja Benki imejenga jengo jipya lenye uwezo

mkubwa wa kutoa huduma hizo kwa ufanisi. Jengo ambalo limekabidhiwa rasmi Tarehe 29 Septemba,

2011. Jengo lina sehemu mbili, moja inatoa hudumma za Benki za kawaida (Conventional) sehemu

nyengine ni kwa ajili ya huduma za kibenki za Kiislam.

Taratibu za benki hizi za Kiislamu na mawazo ya wengi ni kuwa labda benki ile ni ya watu maalum.

Utaratibu wa utoaji wa mikopo nao unahitaji mafunzo maalum ambayo pia yanaihusisha Benki Kuu ya

Tanzania ikiwa kama dhamana wa kusimamia benki kwa mujibu wa Sheria.

.

Benki Kuu ya Tanzania (BOT)

Benki Kuu ndio yenye jukumu la kusimamia benki zote zilizopo Tanzania, katika kufanya hivyo na

pamoja na mambo mengine inayozingatia ni suala zima la utoaji wa leseni ya biashara hiyo.

Benki kuu kupitia Tawi lake la Zanzibar imekuwa mshauri mzuri katika mambo yanayohusiana na

uchumi. Ushauri huo hutolewa kupitia tafiti mbalimbali zinazofanywa pamoja na kushiriki katika vikao

mbalimbali vya Kamati za kitaalamu kama vile Kamati ya kuweka Ukomo wa matumizi ya fedha (

ceiling committee) na Vikao vya matayarisho na maendeleo ya MKUZA.

Tafiti ambazo zinafanyika ni zile zinazohusiana na:

Sekta ya Viwanda.

Mfumko wa bei na Chakula.

Utafiti wa zao la Mpira.

Page 17: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

17

SHIRIKA LA BIMA LA ZANZIBAR.

Shirika la Bima la Zanzibar ni moja kati ya kampuni 29 zilizosajiliwa na Kamishna wa Tanzania kwa

lengo la kutoa huduma za Bima katika mfu mo wa biashara huria ulianzia mwaka 1998.

UTELEZAJI WA MALENGO.

Katika kipindi cha Januari hadi Disemba 2011 liliweka lengo la kukusanya jumla ya

Tshs..10,500,000,000/- fedha zilizokusanywa ni jumla ya Tshs 9,006,790,797/-sawa na asilimia 86 ya

lengo, mapato hayo yalitokana na aina za bima zifuatazo:-

i) Bima ya gari Tshs 8,106,111,717/-

ii) Bima ya moto Tshs 324,470,000/-

iii) Bima ya Meli Tshs 231,149,080/-

iv) Bima mchanganyiko Tshs 345,060,000/-

Uwekezaji wa fedha za Shirika.

Hadi kufikia Disemba 2011 Shirika limewekeza jumla ya Tshs 5,084,102,000 /- kama ifuatavyo:-

1) Makao makuu – uwekaji wa fixed deposit ni Tshs 1,619,102,000/- (FBME na

EXIM Bank)

2) Uwekaji wa dhamana za Serikali –Tshs 2,665,000,000/-.(BoT)

3) Kanda ya Pwani Tshs 800,000,000/-(BoA, Commerce, Africa Bank na DTB)

Katika mradi wa ujenzi, Shirika linatarajia kukamilisha mradi wake wa ujenzi wa ghorafa tano ujenzi huo

ulitarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi March 2012, ambapo uligharimu jumla ya Tshs 2.9

bilioni.Hatahivyo Shirika halijaweza kukamilisha azma yake ya kuanzisha huduma za bima zinazoendana

na maadili ya kiislamu (TAKAFUL).

(KANDA YA PWANI). Ofisi ya Shirika la Bima Zanzibar – Kanda ya Pwani inasimamia matawi yote yaliyoko Tanzania Bara,

ambayo ni Mwanza, Arusha, Mbeya na Dodoma.

UTEKELEZAJI WA MALENGO.

Katika kipindi cha Januari hadi Disemba, 2011 Ofisi ya Kanda ya Pwani ilipangiwa kukusanya jumla ya

Tsh.5, 684,950,000 na kutumia jumla ya Tsh.814, 157,597/- kwa uendeshaji wa Ofisi.

Hadi kufika mwezi Novemba, 2011 jumla ya Tsh.3, 988,551,556/- zilikusanywa. Mapato hayo ni sawa na

asilimia 70 ya lengo. Wakati matumizi yalikuwa Tsh.692, 033,957.79 sawa na asilimia 85 ya bajeti

iliyowekwa.

Katika suala la ulipaji wa madai ya wateja; jumla ya Tsh. I, 940,286,500/- zilitumika.

Mengineyo (Uwekezaji wa Fedha Taslim)

Hadi kufikia Novemba, 2011 Ofisi ya Kanda ya Pwani iliweza kuwekeza jumla ya Tsh.800, 000,000/-

ambapo kwenye Bank of Africa na Africa Bank Corporation kila moja wamewekeza Tsh.30, 000,000/-.

BODI YA MAPATO ZANZIBAR.

Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB) ilianzishwa chini ya sheria Namba 7 ya mwaka 1996 kama taasisi ya

ukusanyaji mapato ya Serikali yatokanayo na vyanzo vya ndani. Bodi ya Mapato ilianza kazi rasmi

mnamo mwezi Septemba, 1998.

UTEKELEZAJI WA MALENGO.

Katika kuyafikia malengo iliyowekewa; Bodi ya Mapato Zanzibar inasimamia Sheria zifuatazo:-

a) Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) nambari 4 ya mwaka 1998.

b) Sheria ya Kodi ya Mahoteli (Hotel Levy) nam. 1 ya mwaka 1995.

c) Sheria ya Kodi ya bidhaa za Mafuta ya Petroli nam. 7 ya mwaka 2001.

Page 18: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

18

d) Sheria ya Kodi ya Ushuru wa Stempu nam. 6 ya mwaka 1996.

e) Sheria ya Ada ya huduma ya Bandari na Viwanja vya Ndege nam. 2 ya mwaka 1999.

f) Sheria ya leseni za biashara ya mwaka 1983.

g) Sheria ya Kodi ya Majengo.

h) Sheria ya Usimamizi wa Kodi nam 7 ya mwaka 2009.

Mbali ya kusimamia sheria hizo, Bodi ya Mapato Zanzibar imepewa uwakala wa kusimamia ada na kodi

zilizokuwa zinasimamiwa na Taasisi nyengine hapa Zanzibar ambazo ni:-

• Leseni za Udereva

• Leseni za njia,

• Usajili wa vyombo vya moto na

• Kodi ya Ardhi

UTEKELEZAJI WA MALENGO YA UKUSANYAJI WA MAPATO.

Bodi ya Mapato Zanzibar ilikadiriwa kukusanya mapato yenye jumla ya Tshs. 71.2 bilioni kwa kipindi

cha Julai – Januari, 2011/2012 kutokana na vyanzo mbalimbali inavyovisimamia.

Makusanyo halisi kwa kipindi hiki cha miezi saba ni Tshs.71.3 bilioni, ambazo ni sawa na asilimia

100.08 ya makadirio kwa kipindi husika

MUHTASARI WA MAKADIRIO NA MAKUSANYO HALISI KWA MUJIBU WA VYANZO

KWA KIPINDI CHA MIEZI SABA JULAI - JANUARI, 2011/2012

KIANZIO

JULAI - JAN

2010/2011

JULAI - JAN

2011/2012

JULAI - JAN

2010/2011

JULAI - JAN

2011/2012

JULAI -

JAN

2010/20

11

JULAI - JAN

2011/2012

VAT&EXCISE DUTY 31.40 34.90 27.70 33.90 88.20 97.13

K/MAFUTA 13.70 16.00 13.50 14.80 98.50 92.50

K/NYENGINEZO 16.60 20.30 16.30 22.60 98.20 111.33

JUMLA 61.70 71.20 57.50 71.30 93.13 100.08

MAKUSANYO HALISI (BIL.

TZS) ASILIMIA YA

UTEKELEZAJI

MAKADIRIO YA

MAKUSANYO (BIL. TZS)

Kiutekelezaji kianzio cha VAT na Exercise Duty kwa pamoja vimeweza kukusanya jumla ya Tshs.33.9

bilioni ikilinganishwa na makisio ya Tshs.34.9 bilioni sawa na asilimia 97.13 na kianzio cha kodi za

mafuta kilichokadiriwa kukusanya jumla ya Tshs.16.0 bilioni na makusanyo halisi ni Tshs.14.8 bilioni

sawa na asilimia 92.50 na kianzio cha kodi nyenginezo kimekusanya Tshs.22.6 bilioni ukilinganisha na

makisio ya Tshs.20.3 bilioni sawa na asilimia 111.33.

Ikilinganishwa makadirio ya kipindi cha miezi Saba (Julai – Januari), katika mwaka 2011/12 ya Tshs.

71.2 bilioni na makusanyo halisi yaliyofikiwa ya Tshs. 71.3 bilioni kunajitokeza ongezeko la makusanyo

kwa kiasi cha Tshs. 0.1 bilioni sawa na asilimia 0.08 ya makadirio.

Page 19: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

19

Ikilinganishwa kiwango cha makusanyo ya Tshs. 57.5 bilioni kilichofikiwa katika kipindi cha Julai -

Januari, 2010/11 na kiwango cha Tshs. 71.3 bilioni kilichofikiwa katika kipindi cha Julai - Januari,

2011/12 kunajitokeza ongezeko la makusanyo ya Tshs. 13.8 bilioni.

MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA.

Kodi zinazosimamiwa na TRA Zanzibar:

Idara ya Kodi za Ndani ya TRA Zanzibar inasimamia ukusanyaji wa mapato chini ya sheria namba 11 ya

mwaka 2004 ya kodi ya mapato ambayo inahusisha kodi ya makampuni (Corporate tax) kodi za zuio

(Withholding Taxes), faida halisi kwa kuuza rasilimali (Capital gain), Kodi ya Mapato ya mtu binafsi na

kodi kwenye marupurupu ya ajira.

Aidha Idara hiyo inasimamia kodi ya kuendeleza ufundi stadi (Skill development levy) chini ya sheria

namba 8 ya mwaka 2006.

Idara ya Forodha inasimamia ukusanyaji wa mapato chini ya sheria ya Forodha ya Afrika Mashariki ya

mwaka 2004, ambayo inatoza kodi ya Forodha kwa Bidhaa zinazotumika moja kwa moja na mlaji. Pia

Idara inakusanya kodi ya ushuru wa bidhaa chini ya sheria ya kodi ya bidhaa.

Aidha, Idara inakusanya ushuru wa Bidhaa kwa mafuta ya kuendeshea vyombo vya moto na mitambo,

kwa sheria ya mafuta. Pia Idara ya Forodha inasimamia ukusanyaji wa kodi ya VAT kwa bidhaa

zinazoingia nchini kwa mujibu wa sheria namba 4 ya mwaka 1998.

MAKISIO YA MAPATO KWA MWAKA WA FEDHA 2011/2012.

Kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012 Mamlaka ya Mapato Tanzania ofisi ya Zanzibar ilipangiwa

kukusanya Shilingi 100,581 milioni ambazo ziliongezeka kwa asilimia 32 kuliko mapato halisi ya

Shilingi 76,335 milioni yaliyokusanywa katika mwaka wa fedha 2010/2011. Kati ya makisio hayo ya

shiling 100.581 milioni, Idara ya Forodha na Ushuru ilipangiwa kukusanya Shilingi 49,442.3milioni na

idara ya Kodi za Ndani ilipangiwa kukusanya shilingi 51,138.8 milioni.

Kwa kipindi cha miezi 7 cha kuanzia Julai – Januari Ofisi ya Mamlaka ya Mapato Zanzibar ilipangiwa

kukusanya shilingi 57,805.1 milioni ambapo Idara ya Kodi za Ndani ilikisiwa kukusanya Shilingi

28,879.6 milioni na Idara ya Forodha ilikisiwa kukusanya Shilingi 28,925.5 milioni.

MAPATO HALISI KATIKA KIPINDI CHA JULAI – JANUARI

Mapato halisi yaliyokusanywa na Mamlaka ya Mapato kwa kipindi cha Julai – Januari katika mwaka huu

wa fedha wa 2011/2012 ni Shilingi 49,780.5 milioni sawa na utekelezaji wa asilimia 86 ukilinganisha na

makisio ya kipindi hicho.

Mapato yaliyokusanywa kwa kipindi hichi cha mwaka huu wa fedha wa 2011/2012 yameongezeka kwa

asilimia 20 ukilinganisha na kipindi kama hicho cha mwaka wa fedha uliopita wa 2010/2011. Mwaka

uliopita kipindi kama hicho Mamlaka ya Mapato ilikusanya shilingi 41,355.1milioni.

Idara ya Forodha imevuka lengo la kipindi hicho cha miezi Saba kwa takriban asilimia 109 baada ya

kukusanya shilingi 31,485.9 milioni. Aidha, Idara ya Kodi za Ndani haikufikia lengo la kipindi hicho

baada ya kukusanya Shilingi 18,294.6 milioni dhidi ya lengo la Shilingi 28,879.6 milioni. Utendaji huu

ni wa asilimia 63.

Sababu kubwa ya kutofikia lengo kwa Idara ya Kodi za Ndani – Zanzibar kumechangiwa na

kutohaulishwa kwa Shilingi 10,500 milioni za PAYE kwa kipindi cha Julai – Januari 2012 zinazotokana

na watumishi wa Taasisi za Muungano zilizopo Zanzibar. Ilitegemewa kuwa PAYE ya Watumishi wa

Taasisi za Muungano waliopo Zanzibar ingelipwa kwa TRA Zanzibar kutoka Hazina Tanzania Bara

katika mwaka wa Fedha wa 2011/2012. Hata hivyo, matatizo ya kisheria yamekwamisha utekelezaji wa

azimio hilo.

Page 20: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

20

Jadueli namba 1: Ulinganisho wa utekelezaji kiidara katika mwaka wa fedha wa 2011/2012 na

2010/2011.

Idara

2010/2011

2011/2012

Makisio Hali Halisi Asilimia Makisio Hali Halisi Asilimia

Forodha 23,214.0 26,082.8 112 28,925.5 31,485.9 109

Kodi za

Ndani

15,638.0 15,272.5 98 28,879.6 18,294.6 63

Jumla Kwa

TRA

Zanzibar

38,852.0 41,355.3 106 57,805.1 49,780.5 86

MFUKO WA BARABARA.

MFUKO WA BARABARA – ZANZIBAR.

Makusanyo.

Kwa mwaka wa fedha 2011/2012 Mfuko ulikadiria kukusanya jumla ya Tsh. 6.432 bilioni na ambapo

kwa kipindi cha miezi minne (Julai hadi Oktoba, 2011) jumla ya Tsh. 1,797 bilioni ambazo ni sawa na

asilimia 28 ya makadirio. Mfuko umepokea Tsh. 1,424 bilioni.

UTEKELEZAJI WA MALENGO.

Jumla Tsh.1, 322 bilioni zililipwa kwa kazi za barabara pamoja na malipo ya ununuzi wa lami na Grader

Kalavati za Kiongele, pamoja na usafi wa Barabara.zikiwa ni asilimia 24 ya makadirio ya mwaka.

Barabara zilizotengenezwa kwa fedha hizo; kwa upande wa Unguja ni:-

Mwanakwerekwe – Nyumba Mbili, Soko la Mchina – Mbuyu Mnene, Kiboje -- Mabonde ya Mpunga,

Kiyashange – Kijijini.

Kwa upande wa Pemba ni uwekaji wa tabaka la lami barabara ya Weni – Wete, mambo mengine ni

uzibaji wa viraka na usafi wa barabara.

MRADI WA UJENZI WA AFISI.

Ujenzi wa Afisi ya Mfuko wa Barabara „White Villa‟ iliyopo Kikwajuni upo katika hatua za mwisho

kukamilika na ilitarajiwa kufunguliwa kwenye sherehe za Mapinduzi ya Januari, 2012.

Jengo hilo ambalo linajengwa na Mkandarasi „Rans Company Ltd‟ na kusimamiwa na Mshauri M/S

Yasser Consultant, na linajengwa kwa gharama ya Tsh. 696,575,000/- na Mjenzi huyo hadi mwezi

Disemba, 2011 ameshalipwa jumla ya Tsh.390,819,000/- kukiwa na bakaa ya Tsh.305,756,000/-.

Lengo la baadae la Mfuko ni kuweka mitambo ya kisasa ya ulinzi (CCTV Camera), ununuzi wa

Genereta la dharura na kwa kushirikiana na Baraza la Manispaa itajenga maegesho ya magari na bustani.

MAMLAKA YA UKUZAJI VITEGA UCHUMI.

TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA KAZI ZA AFISI YA ZIPA.

MAJUKUMU YA JUMLA.

Kwa ujumla kazi zinazotekelezwa zianatajwa katika Sheria ya uwekezaji No.11 ya Mwaka 2004, lakini

kazi hizo kwa ufupi ni kama ifuatavyo:-

Mamlaka ndicho chombo pekee cha Zanzibar cha kushughulikia ukuzaji vitega uchumi pamoja

na kazi zote zitazopelekea kufanikisha uwekezaji wa aina zote za vitega uchumi.

Page 21: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

21

Mamlaka ina wajibu wa kudumisha uhusiano wa Wawekezaji, Serikali na Mamlaka nyengine

zinazohusika na uwekezaji.

Mamlaka ni dhamana wa utawala, udhibiti na uendeshaji wa Bandari huru na Maeneo huru ya

Uchumi.

Mamlaka ina wajibu wa kutekeleza kazi nyengine zenye kufanikisha kufikia malengo ya

uwekezaji.

MALENGO YA MAMLAKA.

a. Kujenga maghala matatu katika eneo huru la Amani na matatu katika eno la Bandari

huru ya Maruhubi

b. Kufanya” Master plan “kwa eneo la Fumba.

c. Kukamilisha taratibu za mradi wa jengo la kitega uchumi la Mamlaka Pemba.

d. Kufanya ukarabati wa mfumo w a maji taka katika eneo la Amani.

e. Ujenzi wa uzio wa ukuta katika eneo la Bandari Huru Uwanja wa Ndege.

UTEKELEZAJI WA MALENGO.

Mamlaka inatekeleza kazi ya ujenzi wa Maghala kwa kushirikiana,ambapo Wawekezaji

wanajenga wenyewe maghala na kukatwa gharama hizo kwa mujibu wa makubaliano.

Mamlaka inafanya mawasilianao na mshauri elekezi kutoka kampuni ya Phills Internationa

kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango Mkuu (Master plan) wa uendelezaji wa maeneno ya

Fumba, Chaleni na Myamanzi.

Mamlaka imetafuta mshauri wa ujenzi na kazi ya tathmini inaendelea .Aidha kazi za

kujenga ofisi za muda za mamlaka zimeanza katika sehemu ya kiwanja cha Tibirinzi.

Ukarabati wa mfumo wa maji taka Amani hatua za awali za kufanyia marekebisho ya

michirizi imefanyika.

Taarifa ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2011/2012.

Katika kipindi cha miezi sita (Julai-Disemba) jumla ya Tshs 809,287,454.77 zilikusanywa kutoka vyanzo

tofauti vya mapto na Tshs 150,000,000.00/- ni ruzuku kutoka Serikalini, hivyo jumla ya makusanyo ni

Tshs 959,287,454.77/- ambazo ni sawa na asilimia 49.76 ya makadirio ya mwaka mzima.

Tathmini ya maombi ya miradi.

Jumla ya miradi kumi na sita(16) yenye thamani ya mtaji wa makisio ya USD 71, 421,300 iliidhinishwa

katika kipindi cha Julai –Disemba 2011. Kati ya miradi hiyo mitano ni ya hoteli, minne ni ya viwanda,

minne ya kilimo, miwili ya huduma na mmoja ni wa mawasilianao .Jumla ya Tshs 24, 718,000.00/-

zimetumika katika kazi hiyo.

Kuwajengea uwezo wa Wafanyakazi.

Jumla ya Wafanyakazi 9 wamepatiwa fursa ya kushiriki katika mafunzo ndani na nje ya nchi juu ya

mambo mbali mbali yanayohusu kazi zao kwa lengo la kuwaongezea taaluma na uwezo wao wa

kutekeleza majukumu yao ya kazi. Jumla ya Tshs 62, 977,070.00/- zimetumika.

Kutangaza fursa za uwekezaji.

Mamlaka ilitangaza fursa mbali mbali za uwekezaji kwa kufanya ziara za uenezi ,kushiriki katika

mikutano ya kikanda naya kimataifa ya uhamasishaji.Aidha makala mbali mbali katika magazeti kama

vile kwenye SACD directory,Tanzania Review,pamoja na uchapaji wa diary na kalenda ,ziara zimefaywa

katika Nchi zenye viwanda vya usindikaji samaki (Syscheles na Maldives) ili kujifunza na kushajihisha

wenye viwanda kuja Zanzibar,jumla ya Tshs 25,951,154.40 zimetumika kwa kazi hiyo.

Page 22: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

22

Kukuza teknolojia ya habari.

Tovuti ya www.zanzibarinvest.org imetafsiriwa kwa lugha ya kichina mwelekeo sasa ni kuwa na lugha

ya kirusi na kituruki, jumla ya Tshs 5, 700,000/- zimetumika.

Uimarishaji miundo mbinu (maji).

Mamlaka imesafisha kisima cha maji safi na kuweka pampu mpya ya kusukuma na kuvuta maji,

Tshs.7,000,000/- zimetumika.

Uimarishaji miundo mbinu (barabara).

Idara ya Ujenzi na Matengenezo ya Barabara imeshalipwa jumla ya Tshs 84,670,000/- kwa ajili ya ujenzi

wa barabara ya maeneo huru ya Amani na Maruhubi.

Ukarabati wa Maghala.

Mamlaka imefanya matengenezo ya maghala mawili hapo Amani Industrial Park (call center,) na

Maruhubi ghala linalotumiwa na kampuni ya Sham limited fedha zilizotumika ni jumla ya Tshs

115,566,910/-.

Kwa upande wa Pemba katika kipindi cha April-Juni, 2011 Afisi ilitumia Jumla ya Tshs 11,361,900 kwa

kazi za kawaida, taarifa imeelezwa kuwa hakuna mapato yoyote yaliyokusanywa katika kipindi hiki.

HALI YA UWEKEZAJI KWA KIPINDI CHA APRIL-JUNI (PEMBA).

Kwa kipindi cha April hadi Juni mradi mmoja ulisajiliwa.Wamiliki wa mradi huo ni Bwana Isaias Jose

Pena na Bwana Morin raia wa Uhispania na Bwana Rune.

Katika maeneo ya Micheweni hadi kamati ilipofika katika ofisi za ZIPA Pemba bado hakujawa na

mwekezaji yeyote aliyejitokeza.

Shughuli kuu iliyofanyika ni ukaguzi wa mara kwa mara kwa ajili ya kuangalia usalama wa maeneo.

Hata hivyo baada ya kuzungumza na wawekezaji ambao wamejenga maghala ya kuhifadhi mwani

kwenye maeneo hayo kukamilika, Afisi ya ZIPA Pemba imefanya utaratibu wa kuyapima na kuyawe

kea “Bicons”.

OFISI YA MTAKWIMU MKUU WA SERIKALI.

MALENGO YA IDARA

Miongoni mwa malengo yaliyopangwa na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu kwa kipindi cha mwaka wa fedha

wa 2011/2012 ni kama yafuatayo:-

(a) Kufanya tathmini juu ya hali ya ukuaji wa ukadiriaji wa Pato la Taifa kwa mwaka 2011

(b) Ukamilishaji wa matayarisho ya Sensa ya Watu na makaazi.

(c) Utekelezaji wa mpango mkuu wa Takwimu Tanzania.

(d) Kuendeleza kazi za mradi wa ZANSTAT na mchakato wake kwa awamu ya Pili.

UTEKELEZAJI WA MALENGO.

Takwim za Quarterly – GDP.

Idara imekamilisha ukadiriaji kwa mwaka wa kwanza na robo ya pili (April – Juni, 2011), robo ya tatu

inaendelea sambamba na kazi za ukusanyaji wa takwimu za Economic Survey.

Sensa ya Watu na Makaazi ya Mwaka 2012. Moja ya matayarisho ya Sensa hii ni utayarishaji wa ramani za Maeneo ya Kuhesabia Watu katika Mikoa

yote ya Tanzania na kutayarisha ramani hizo katika mfumo wa Geographical Information System kwa

kutumia Digitalization System. Kwa upande wa Zanzibar kazi ya kutenga maeneo kwa Mikoa yote

mitano imemalizika. Jumla ya maeneo 5,397 ya kuhesabia Watu yametengwa kwa ajili ya Sensa hiyo

ikilinganishwa na maeneo 2,062 ya mwaka 2002.

Matayarisho mengine yaliyofanyika ni kuandaa miongozo mbalimbali ikiwemo Muongozo wa Sensa

pamoja na kuunda kamati mbali mbali za kusimamia kazi za Sensa.

Page 23: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

23

Aidha kumefanyika Sensa ya majaribio ambapo maeneo 44 yalitengwa kwa madhumuni hayo, nayo ni

katika Mikoa ya Arusha, Kigoma, Dar es Salaam, Kilimanjaro, Manyara, Mara, Mtwara, Njombe na

Pwani kwa upande wa Tanzania Bara, na kwa upande wa Zanzibar jumla ya maeneo SITA yalihusishwa,

maeneo MANNE yalikuwa katika Shehia ya Chukwani, Unguja na maeneo MAWILI yalikuwa kwa

Shehia za Sizini na Maziwa Ng‟ombe , Pemba.

Aidha mradi wa Zanzibar Statiscal System Project umeanza kutekelezwa kwa lengo la kubadilisha

mfumo wa Takwimu Zanzibar na kuwezesha kutoa Tawimu zilizo bora na zinazokwenda na wakati.

SEHEMU YA TATU

3.0. HITIMISHO.

Baada ya Kamati kukamilisha kazi yake ya ufuatiliaji katika Wizara husika, ilitoa ushauri, maoni na

kuziagiza Idara na Taasisi zinazohusika kama ifuatavyo:-

3.0.1. WIZARA YA NCHI (OR) FEDHA, UCHUMI NA MIPANGO YA MAENDELEO.

MAONI/MAAGIZO YA KAMATI.

1. .Serikali zote mbili zisimamie utekelezaji wa utaratibu wa kuhakikisha kuwa kodi ya mapato

(income tax) kwa Wafanyakazi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wanaoishi

Zanzibar kodi yao ya Mapato (PAYE) iwe inakusanywa Zanzibar kupitia Bodi ya Mapato

Zanzibar kama wakala .

2. Utaratibu wa ukusanyaji kodi ya visa ubadilishwe kwani utaratibu unaotumika hivi sasa

hauoneshi uhalisia wa mapato halisi sambamba na idadi ya wageni wanaoingia Nchini.

3. .Suala la magendo ya mafuta linahitaji msukumo wa pamoja kati ya vyombo vyote vya ulinzi,

bandari na Wananchi kwa ujumla, wavuvi na wale wanaotumia bandari zisizo rasmi.

4. Elimu itolewe kwa Wafanyabiashara ikiwa na msisitizo wa kuhakikisha kuwa kila mfanya

biashara anatoa risiti bila ya hata kuombwa na mteja au kuweka masharti ya kupunguza bei

iwapo mteja hatapatiwa risiti.

5. Utaratibu uandaliwe wa kuanzisha mfumo wa utoaji risiti uliounganishwa na mtandao

(electronic receipt) ambao utamuwezesha kila mfanyabiashara kuwa na risiti.

6. Kuwe na udhibiti mzuri wa ukusanyaji wa kodi za mahotelini ili kuwe na uwiano ulio na idadi

sawa ya Wageni wanaoingia Zanzibar na kulala mahotelini na mapato halisi

yanayokusanywa.Aidha mapato yanayokusanywa yaendane na viwango vya mahoteli yenyewe.

7. TRA Zanzibar iangalie sana malipo ya ushuru unaotolewa ili kusiwe na malipo ya tofauti ya

ushuru huo iwapo bidhaa itasafirishwa kupelekwa Tanzania Bara.

8. Sheria Nam 6 ya mwaka 1996 ya “stamp duty” ifanyiwe marekebisho ili kuwe na uwezekano wa

kuweka kiwango maalum cha kodi ya mapato badala ya makisio.

9. Serikali iweke kipaumbele wa ujenzi kwenye miundo mbinu katika maeneno huru ya uchumi

ili iwe ni kivutio kwa Wawekezaji.

10. Mamlaka inayosimamia utoaji wa huduma za Bima (TIRA) iangalie vyema kanuni zake hasa ile

inayohusiana na umiliki wa mali zisizohamishika (Fixed Assets) ili kampuni zinazotoa huduma

za Bima ziweze kumiliki wenyewe majengo ya Afisi badala ya kukodi.

Page 24: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

24

11. Shirika la Bima la Zanzibar likamilishe taratibu zake za kuanzisha Bima inayoendana na maadili

ya Kiislam (TAKAFUL).

12. Serikali izitumie kikamilifu takwimu zinazotolewa na Mtakwimu Mkuu wa Serikali kwa ajili ya

kuweka vipaumbele, Miradi na Mipango mingine ya Maendeleo.

13. Bado wananchi wanashindwa kufahamu kwa undani madhumuni ya Takwimu na suala zima la

kuhesabiwa (Sensa) hivyo elimu zaidi inahitajika kutolewa kwa Wananchi ili waweze kutoa

taarifa kwa usahihi .

14. Kamati inaagiza kuwa Bodi ya Mapato Zanzibar ihakikishe kuwa inawatambua na kuwasajili

Wafanyabiashara wote wakubwa na wadogo.

15. Kamati inaagiza kuwa Wafanyabiashara wote kuwa wanafanya mauzo katika maeneo ya

biashara na wanatoa Ankara za kodi kwani hivi sasa walipa kodi wengi hawatoi risiti

wanapofanya mauzo.

3.0.2. WIZARA YA KILIMO NA MALIASILI.

MAONI / USHAURI /MAAGIZO YA KAMATI

1. Sheria na kanuni zinazohusiana na makosa ya uharibifu wa misitu na maliasili nyengine zipitiwe

upya kwani inaonekana adhabu zilizowekwa ni ndogo kiasi cha kutomtia khofu anayetenda

makosa..

2. Elimu zaidi iongezwe juu ya matumizi bora ya gesi na majiko mengine ambayo yanapunguza

matumizi ya kuni.

3. Upandaji wa mikarafuu mipya uwe ni mkakati wa makusudi kwa Wizara na isimamie kwa

karibu zoezi hili, hasa katika makuzi ya mikarafuu hiyo. Kila mwaka kuwe na takwimu halisi

inayoonesha idadi ya iliyopandwa, iliyokuwa vizuri, maeneo yaliyoonesha kiwango kizuri cha

ukuaji na yale ambayo hayakufanikiwa pamoja na sababu za kitaalamu zenye matokeo hayo.

4. Chuo cha Kilimo Kizimbani kizidi kuendelezwa ili kiwe miongoni mwa vyuo vya kilimo

vinavyotoa elimu hiyo kwa kiwango cha shahada (Degrees).

5. Wakulima wapatiwe mbegu bora za mpunga zinazozalishwa kwa wakati ili wawahi msimu wa

kilimo.

6. Wizara itayarishe maombi ya fedha Serikalini mapema ili fedha hizo zipatikane kwa wakati wa

msimu unaoendana wa kilimo.

7. Wakulima wapelekewe matrekta mapema kwa ajili ya kulima na kuburuga.

3.0.3. WIZARA YA BIASHARA VIWANDA NA MASOKO.

MAONI/USHAURI/MAAGIZO YA KAMATI.

1. Kuna haja ya kuwaelimisha wakulima umuhimu wa kuwepo kwa wachukuzi na

majukumu yao ili ipatikane njia muafaka itakayoondosha mgongano kati yao.

2. Kamati inazishauri Serikali za Wilaya kuwa na uwiano wa bei za vyeti vya mazao kati

ya Halmashauri moja na nyengine.

3. Kamati inalishauri Shirika kuangalia uwezekano wa kununua aina nyengine ya mizani

ya kisasa zaidi (Digital) ili kuondosha wasiwasi wa baadhi ya wakulima wanaouza

karafuu juu ya uwezo wa mizani zilizopo sasa.

Page 25: PROGRAMU YA UIMRISHAJI MIUNDOMBINU YA MASOKO, … · Hadi mwezi Disemba 2011 kazi ya mapitio ya awali ya Sera ya Kilimo hayajaanza. Rasimu ya mwanzo ya Sera ya Misitu imewasilishwa

25

4. Suala la kusafirisha karafuu kutoka Wilaya moja kwenda nyengine zikiwa mbichi au

kavu, Kamati inashauri bado Serikali iliangalie kwa makini na iandae utaratibu mzuri

wa kutoa vibali ili vibali hivyo visitoe fursa ya upelekwaji wa karafuu mahala pengine

pasipostahiki.

5. Kamati inashauri kufanyiwa matengenezo majengo ya vituo vya ununuzi wa karafuu

pamoja na ujengwaji wa vyoo.

6. Bado hakuna uwiano wa bei za bidhaa hasa za vyakula zinazouzwa katika sehemu

moja , hivyo Wizara haina budi kufanya ukaguzi wa mara kwa mara ili kuhakikisha

kwamba yale makubaliano ya bei kati yao na Wafanyabiashara yanatekelezwa kama

walivyokubaliana.

7. Juhudi za makusudi zifanyike ili kujua idadi sahihi ya maghala na maduka

yanayouzwa bidhaa kwa jumla na reja reja.

8. Zabuni kwa ajili ya matayarisho ya uwanja wa Kimataifa wa Maonesho ya Biashara

itangazwe mapema ili matumizi na gharama za eneo hilo zifahamike na walengwa.

9. Ukarabati wa Maghala ya kuhifadhia chakula cha akiba ya Nchi pamoja na

matayarisho mengine yanayohusiana na uhifadhi huo kwa mujibu wa sheria ufanyike

haraka ili angalau mwakani maghala hayo yaweze kutumika kwa kuhifadhia chakula

cha akiba.

10. Wizara isimamie suala la uhifadhi wa mafuta ya Nchi kwa ajili ya mafuta ya dharura.

11. Wizara iharakishe kufanya marekebisho ya sera ya viwanda ili iendane na wakati na

iwe na vivutio kwa wawekezaji katika Sekta ya Viwanda.

12. Kamati inaagiza Wizara kuwaajiri Wafanyakazi wa ukaguzi wa bidhaa wenye ujuzi wa

kutosha na kuwapatia vitendea kazi.

13. Elimu zaidi inahitajika kwa Wajasiriamali ili waweze kutengeneza bidhaa zitakazoweza

kukabiliana na ushindani katika masoko.