wizara ya maliasili na utalii - tfs · 2016. 2. 10. · makala inaainisha dira, dhima, maadili...

70
MAKALA YA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA Julai, 2015 WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Upload: others

Post on 09-Feb-2021

6 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

  • MAKALA YA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA

    Julai, 2015

    WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

  • WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

    MAKALA YA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA

    Julai, 2015

    PICHA:Juu Kushoto: Hifadhi ya Mazingira Asilia–Uluguru

    Juu Kulia: Makao Makuu ya TFS Chini Kushoto: Ufugaji nyuki-Babati

    Chini Kulia: Shamba la miti ya Mikaratusi

  • ii

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Mr. Juma S. Mgoo (Mtendaji Mkuu)

    Makala ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania imeandaliwa mahsusi kwa ajili ya kutoa taarifa za mafanikio ya Wakala tangu kuanzishwa kwake. Makala hii imeandaliwa kwa mujibu wa maelekezo ya Ofi si ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma inayozitaka Wakala zote za Serikali kuandaa Makala za utendaji wake tangu kuanzishwa kwake. Lengo la Makala hii kwa mujibu wa hadidu za rejea ni pamoja na:

    Kuainisha kwa kina taarifa za kuanzishwa kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), ikiwa ni pamoja na lengo kuu la kuanzishwa kwake, Dira, Dhima, maadili makuu, Majukumu makuu; pamoja na taarifa/kumbukumbu mbalimbali za Wakala;

    Kuelezea changamoto mbalimbali pamoja na wazo, sababu za ndani au za nje zilizopelekea kuanzishwa kwa Wakala;

    Kuanisha Changamoto mbalimbali za ndani na nje ambazo Wakala umekabiliana au unakabiliana nazo tangu kuanzishwa kwake;

    Kufanya tathimini ya Wakala kwa kuelezea hali ya utendaji kabla na baada ya kuwa Wakala, kwa lengo la kuainisha na kuzielezea tofauti za kiutendaji zilizokuwepo;

    Kutoa taarifa za rasilimaliwatu, mapato na matumizi na mwenendo wake.

    Wakala wa Huduma za Misitu umekuwa na mafanikio makubwa katika kipindi cha miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake, aidha kumekuwepo na changamoto kadhaa ambazo Wakala umekabiliana nazo tangua utekelezaji wa Mpango Mkakati wake wa kwanza 2010/11-2013/14 (Kwasasa Wakala unatekeleza Mpango Mkakati wa pili 2014/15 -2018/19).

    Ninayo furaha kuwasilisha Makala hii inayoainisha mafanikio ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania katika kipindi cha miaka mitatu (2010/11-2013/14) tangu kuanzishwa kwake.

    Juma S. Mgoo

    DIBAJI

  • iii

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    MUHTSARI

    Makala hii inaelezea kuhusu Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ((Tanzania Forest Services (TFS) Agency)) ambao ulianzishwa kisheria kupitia Tangazo la Gazeti la Serikali (GN 269) la tarehe 30/7/2010 na kuzinduliwa rasmi tarehe 18/7/2011. Kuanzishwa kwa Wakala wa Huduma za Misitu ni kwa mujibu wa Sheria ya Wakala “the Executive Agencies Act Cap. 245 (Revised Edition 2009)”, pamoja na Sera ya Misitu ya mwaka 1998, Sera ya Ufugaji Nyuki ya mwaka 1998, Sheria za Misitu na Nyuki Sura 323 na Sura 224 za mwaka 2002.

    Makala inaainisha Dira, Dhima, Maadili makuu pamoja na Majukumu Makuu ya Wakala. Makala hii inaainisha kwa kina utendaji kazi wa Wakala tangu kuanzishwa kwake, mafanikio yaliyopatikana pamoja na changamoto mbalimbali ulizokabiliana nazo. Aidha, makala inafanya tathimini ya kina ya kuonesha utekelezaji wa majukumu kabla na baada ya kuanzishwa kwake. Pamoja na mambo mengine Makala hii inaainisha changamoto zilizokuwepo kabla ya kuanzishwa kwa Wakala (Idara ya Misitu na Nyuki), ikiwa ni Changamoto za ndani ya Idara ya Misitu na Nyuki na zile za nje ya Idara.

    Uwepo wa Wakala unazingatia agizo la kuanzishwa kwake kwa mujibu wa Hati ya mwaka 2010 ambayo imebainisha kwa kina kuhusu utawala, muundo na majukumu ya msingi katika utendaji wa shughuli za Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania. Aidha, hati imebainisha majukumu ya Bodi ya Ushauri ambayo ni mahsusi kwa ajili ya kumshauri Waziri wa Maliasili na

    Utalii (WMU) kuhusu utendaji na ufanisi wa Wakala. Hati pia imeainisha orodha ya misitu yote ya hifadhi inayopaswa kusimamiwa na Wakala.

    Katika Makala hii Muundo wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania umeelezewa. Muundo huo unajumuisha Mtendaji Mkuu, Wakurugenzi watatu, Meneja wawili wa Vitengo vya Sheria na ugavi, Mhasibu Mkuu na Mkaguzi Mkuu wa ndani. Wakala pia una Mameneja wa Kanda saba (7) na wa Mashamba ya miti 18. Vile vile Wakala umeboresha utendaji wake kupitia wilaya; ambapo Mameneja wa wilaya 118 wameteuliwa na kupatiwa nyenzo za kazi. Kanda hizo za Wakala ni; Mashariki, Kaskazini, Kati, Kusini, Nyanda za juu Kusini, Ziwa na Magharibi.

    Makala inaelezea kuhusu mifumo mbalimbali ya kimenejimenti iliyowekwa na Wakala kwa malengo ya kuongeza ufanisi wa kiutendaji, kuboresha utoaji huduma kwa wadau na kupunguza gharama za uendeshaji wa shughuli za Wakala. Mifumo hii ni pamoja na Mwongozo wa Utendaji Kazi, Hati ya Kuanzisha Wakala, Mpango Mkakati, Mpango wa Biashara wa kila mwaka, Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS), Uperembaji na Tathmini, Mkataba wa Huduma kwa Mteja pamoja na Mfumo wa Kushughulikia Malalamiko. Aidha, mifumo mingine iliyoelezewa katika makal hii ni Mfumo wa usimamizi na uhakiki wa fedha (Integrated Financial Management System (IFMS)), Human Capital Information Management System, Masjala na Uhasibu.

  • iv

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Makala inaelezea utendaji Kazi wa Wakala kwa kuzingatia Sheria ya Wakala za Serikali, Wakala “the Executive Agencies Act Cap. 245 (Revised Edition 2009)” Sheria ya Misitu Sur 323 ya mwaka 2002, Sheria ya Ufugaji Nyuki Sura 224 ya mwaka 2002 na Programu za Taifa za Misitu na Nyuki za mwaka 2001 ambazo ziliandaliwa kama vyombo vya kutekeleza Sera za Taifa ya Misitu na ya Nyuki. Makala pia inatoa maelezo ya kuhusu utekelezaji wa shuguli zake kwa kupitia: Mpango Mkakati (Strategic plan 2010/2014); Mipango ya Biashara ya kila mwaka (Business Plans); Mfumo wa wazi wa kupima utendaji kazi (OPRAS); Uperembaji na Tathmini (Monitoring and Evaluation) pamoja na huduma Mkataba wa Huduma kwa Mteja, Mfumo wa Malalamiko; na Mfumo wa Usimamizi na uhakiki wa fedha (IFMS). Makala imeainisha muhtasari wa masuala makuu yaliyofanikiwa chini ya Wakala katika kipindi cha miaka mitatu yakilinganishwa na yale yaliyotekelezwa na Idara ya Misitu na Nyuki katika kipindi cha miaka mitatu kabla ya kukabidhi majukumu kwa Wakala.

    Ufanisi wa Makusanyo ya maduhuli kwa miaka mitatu (2011/12-2013/14) chini ya Wakala umeongezeka, ambapo makusanyo halisi yalikuwa TAS 199,771,416,440 ambayo ni asilimia 101(101%) ya matarajio (maoteo) ya makusanyo ya TAS 197,467,522,456. Mwenendo wa ukusanyaji wa maduhuli unaonesha kuwa ukasanyaji ulikuwa unaongezeka mwaka hadi mwaka. Wakala unakusanya wastani wa TAS 66 bilioni kwa mwaka tangu kuanzishwa kwake ukilinganisha na kiwango cha juu cha makusanyo ya TASTAS billioni 28 kwa Mwaka kilichowahi kukusanywa na Idara kwa muda wote wa utendaji. Aidha, Mapato ya TRA yaliyokusanywa na Wakala kutokana na mauzo ya miti ya kupandwa kutoka kwa wateja wake yalifi kia jumla ya TAS 108,740,000,000. Kwa sasa ukusanyaji mapato wa Wakala ni zaidi ya asilimia 100 ya maoteo. Kwa mfano

    Mwaka 2014/15 Wakala umekusanya kiasi cha TZS 85,475,560,582 ambacho ni sawa na asilimia 105 ya maoteo ya shilingi 81,228,595,000 yaliyokadiriwa.

    Vilevile Wakala umewezesha sekta ndogo ya ufugaji nyuki katika uzalishaji wa mazao ya nyuki, ambapo tani 1,605 za nta zilizalishwa zikiwa na thamani ya TAS. 10,644,056,759, na tani 728 za asali zenye thamani ta Tsh. 2,753,284,771 zilizalishwa na kuwezesha sekta ndogo ya ufugaji nyuki iliweza kuchangia katika pato la taifa na kupunguza umaskini.

    Katika kuboresha usimamizi na uendelezaji misitu, Wakala umeweza kuongeza kasi ya upandaji miti katika mashamba ya miti kila mwaka ili kukidhi mahitaji ya mazao ya misitu ikiwa ni pamoja na kwa kushirikisha wadau mbalimbali kama wananchi/ jamii na taasisi kama shule katika kupanda miti na kuimarisha uhifadhi. Katika kipindi cha 2011/12 hadi 2013/14 jumla ya miti 21,000,000 ilipandwa na jamii, wananchi na taasisi mbalimbali. Uendelezaji wa mashamba ya miti ya Wakala umekuwa hekta 39,776 (2010/11 – 2014/15) ambapo upanuzi ni hekta 15,080.5 na upandaji wa kurudishia maeneo yaliyovunwa hekta 24,695.5. Upandaji huo ni sawa na wastani wa hekta 7,955 kwa mwaka.

  • v

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    DIBAJI ................................................................................................................................ iiMUHTSARI ...................................................................................................................... iiiORODHA YA JEDWALI .................................................................................................... vii 1. UTANGULIZI .......................................................................................................... 1 1.1 Lengo Kuu la Kuanzishwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania .......... 1 1.2 Dira ............................................................................................................ 1 1.3 Dhima ........................................................................................................ 1 1.4 Maadili makuu ........................................................................................... 1 1.5 Majukumu Makuu ..................................................................................... 2 1.6 Madhumuni ya Makala .............................................................................. 2

    2. CHANGAMOTO ZILIZOKUWEPO KABLA YA KUANZISHWA KWA WAKALA ..3 2.1 Changamoto za Ndani ya Idara .................................................................. 3 2.2 Changamoto za Nje ya Idara ..................................................................... 3

    3. TATHMINI YA UTENDAJI KAZI KABLA NA BAADA YA KUWA WAKALA .... 4 3.1 Hali ya Utendaji kabla ya kuanzishwa Wakala .......................................... 4 3.2 Hali ya Utendaji baada kuanzishwa kwa Wakala ...................................... 8 3.2.1 Makao Makuu ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) ..8 3.2.2 Kanda za Wakala na Mashamba ya miti .................................... 10 3.3 Mifumo ya Utendaji ya Wakala Baada ya Kuanzishwa ...................... 11 3.3.1 Mwongozo wa Utendaji Kazi (Framework document) .............. 11 3.3.2 Hati ya Kuanzisha Wakala (Establishment Order) ..................... 12 3.3.3 Mpango Mkakati (Strategic plan) .............................................. 12 3.3.4 Mpango wa Biashara wa mwaka (Business Plan) ..................... 12 3.3.5 Mfumo wa wazi wa kupima utendaji kazi (OPRAS) .................. 12 3.3.6 Uperembaji na Tathmini (Monitoring and Evaluation) ............... 12 3.3.7 Mkataba wa Huduma kwa Mteja .............................................. 12 3.3.8 Mfumo wa Malalamiko ............................................................. 13 3.3.9 Mfumo wa Usimamizi na uhakiki wa fedha (IFMS) ................... 13 3.3.10 Mfumo wa Uhasibu ................................................................. 13 3.3.11 Human Capital Information Management System ................... 13 3.3.12 Masjala ya Wazi na Siri ............................................................. 14 3.4 Sheria zingine ambazo Wakala unazitumia kufanikisha utendaji ............ 14 3.4.1 Sheria ya Mazingira ya 2004 ..................................................... 14 3.4.2 Sheria ya Manunuzi ya Umma 2011 ......................................... 14

    YALIYOMO

  • vi

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    3.4.3 Sheria ya Fedha 2001 ................................................................ 14 3.4.4 Sheria ya Ardhi 1999 na Sheria ya Ardhi ya Vijiji 1999 .............. 18 3.4.5 Matumizi ya TEHAMA .............................................................. 18 3.5 Tathmini ya kazi za Wakala baada ya kuanzishwa ....................... 18

    4. MAFANIKIO YALIYOPATIKANA TANGU KUANZISHWA WAKALA .. 19

    5. MUHTASARI WA MCHANGUNUO WA UTENDAJI KABLA NA BAADA YA KUANZISHWA WAKALA ................................................................ 34

    6. RASILIMALI FEDHA ............................................................................... 36

    6.1 Mapato kabla ya kuanzishwa Wakala .......................................... 36 6.2 Mapato baada ya kuanzishwa Wakala ......................................... 38

    7. RASILIMALI WATU ............................................................................. 39 8. MAPATO NA MATUMIZI YA WAKALA ............................................. 43 8.1 Vyanzo vya mapato ya Wakala kulingana na kasma /vifungu ...... 44 8.2 Mwenendo wa matumizi kabla ya Wakala .................................. 45 8.3 Mwenendo wa matumizi baada ya kuanzishwa Wakala ............. 46

    9. UTOAJI WA TAARIFA ZA FEDHA ...................................................... 48 10. MIPANGO YA WAKALA ...................................................................... 48 10.1 Mipango Mkakati ya Wakala ....................................................... 48 10.2 Mpango wa Kibiashara ................................................................ 49 10.3 Utekelezaji wa Mipango .............................................................. 50 10.4 Uwasilishaji wa Mipango na Taarifa ............................................ 50

    11. CHANGAMOTO ZILIZOJITOKEZA ..................................................... 51 11.1 Changamoto za utekelezaji majukumu ya Wakala ...................... 52 11.2 Changamoto zilizo nje ya Uwezo wa Wakala ............................. 52 11.2.1 Kucheleshwa kuhuishwa kwa Muundo wa Wakala wa Huduma za Misitu .................................................................................. 52 11.2.2 Kuchelewa kwa kuhuishwa kwa Sheria ya Misitu Na. 14 ya Mwaka 2002 ............................................................................ 52 11.2.3 Kuchelewa kukamilisha manunuzi .......................................... 52

    12. MIPANGO YA BAADAYE YA WAKALA .............................................. 52

    13. MIKAKATI ENDELEVU YA KUJITEGEMEA ........................................ 53

    14. MASUALA MAKUU YA BAADAYE NA YA KIPAUMBELE KWA WAKALA ................................................................................................. 60

  • vii

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    ORODHA YA JEDWALIJedwali Na.1: Mafanikio/Shughuli za Idara Kabla ya kuanzishwa Wakala ................................ 6

    Jedwali Na 2: Majengo na vitendea kazi vya FBD/TFS katika Makao Makuu na vituo vya nje..10

    Jedwali Na. 3: Mashamba ya miti chini ya usimamizi wa Wakala kwa hadi mwaka 2014 ... 22

    Jedwali Na. 4: Ujazo uliovunwa (cm) kutoka mashamba ya miti 2011/12-2013/14 .............. 22

    Jedwali Na. 5a: Upandaji miti kitaifa kwa kipindi cha miaka 2011/12 - 2013/14 ...................... 23

    Jedwali Na. 5b: Baadhi ya Mazao yatokanayo na misitu yaliyovunwa katika miaka mitatu ..... 25

    Jedwali Na. 6: Eneo na Hali ya hifadhi za nyuki zilizopendekezwa ......................................... 26

    Jedwali Na. 7: Idadi ya manzuki na mizinga inayosimamiwa na TFS ..................................... 27

    Jedwali Na.8: Misitu ya Hifadhi iliyokuwa na wavamizi ....................................................... 24

    Jedwali Na. 9: Makusanyo kutokana na Ukaguzi maalumu ................................................... 30

    Jedwali 10: Watumishi wa TFS waliohudhuria mafunzo (2011/12 -2013/14) ......................... 31

    Jedwali Na.11: Watumishi wapya kwa Kada walioajiriwa na Wakala ..................................... 31

    Jedwali Na.12: Idadi ya vituo vya Wakala vilivyotembelewa kwa ajili ya Uperembaji kwa ........ Kanda 7 kati ya 2012/13 na 2013/14 .............................................................. 33

    Jedwali Na. 13: Muhtasari wa Mchanganuo wa Utendaji wa Wakala .................................... 34

    Jedwali Na.14: Bajeti ya Matumizi ya kawaida inajumuisha Idara na taasisi zake kwa ........... miaka minne (2007/08 - 2010/11) .................................................................. 37

    Jedwali Na.15: Makadirio ya fedha za Miradi ya maendeleo kipindi cha 2007/08 - 2010/11 . 38

    Jedwali Na 16: Rasilimali watu walioazimwa kutoka Idara ya Misitu .................................... 40

    Jedwali Na.17: Mahitaji halisi ya Rasilimali ya Wakala .......................................................... 42

    Jedwali Na18: Mwenendo wa mapato na Maoteo 2011/2012 hadi 2013/2015 .................... 43

    Jedwali Na 19: Mgawanyo wa mapato ya Wakala (TFS) ........................................................ 44

    Jedwali Na.20: Vyanzo vya Mapato ya Wakala (2011/2012 hadi 2013/2014) ......................... 44

    Jedwali Na. 21: Takwimu za mazao ya nyuki (Asali na Nta) yanayosafi rishwa nje ya Nchi ...... 45

    Jedwali Na 22: Muhtasari wa matumizi ya Wakala kwa malengo kipindi cha 2011/2012 hadi

    2013/2014 ..................................................................................................... 46

    Jedwali Na 23: Fursa za kukuza utalii ikolojia katika hifadhi asilia ........................................... 56

  • viii

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    AIDS Acquired Immuno-Defi ciency SyndromeBP Business Plan

    BTC Belgium Technical Cooperation

    BTI Beekeeping Training Institute

    CAG Controller and Audit GeneralCM Cubic metre

    EAMCEFEastern Arc Mountains Conservation Endowment Fund

    FAO Food and Agricultural Organization

    FBD Forest and Beekeeping Division

    FITI Forest Industries Training InstituteFSU Forest Surveillance UnitFTI Forest Training Institute

    GEF Global Environmental Facility

    GN Government Notice NumberHa Hectare

    HIV Human Immuno-defi ciency Virus

    LMDA Logging and Miscellaneous Deposit Account

    MNRP Management of Natural Resources Programme

    NAFOBEDA National Forest and Beekeeping Database

    NAFORMA National Forest Resources Monitoring and Assessment

    NBRs National Bee Reserves

    NFP National Forest Programme

    NORAD Norwegian Agency for Development CooperationOC Operational Cost

    OPRAS Open Performance Review and appraisal System

    PFM Participatory Forest management

    PO-PSM President Offi ce Public Service ManagementPPP Public Private PartnershipRM Running metres

    SAP Strategic Analysis and PlanningSPI Strategic Plan ISPII Strategic Plan IITaFF Tanzania Forest Fund

    TAFORI Tanzania Forest Research Institute

    TFCMPTanzania Forest Conservation and Management Project

    TFS Tanzania Forest Services AgencyTP Transit Pass

    TRA Tanzania Revenue AuthorityTAS Tanzania Shillings

    UNDP United Nations Development ProgrammeUSD United States DollarVAT Value Added TaxVBRs Village Bee Reserves

    VLFRs Village Land Forest Reserves

    VNRCs Village Natural Resource Committees

    WMU Waziri wa Maliasili na Utalii

    VIFUPISHO (ACRONYMS AND ABBREVIATIONS)

  • 1

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    1. UTANGULIZI

    Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ((Tanzania Forest Services (TFS) Agency)) ulianzishwa kisheria kupitia Tangazo la Gazeti la Serikali (GN 269) la tarehe 30/7/2010 na kuzinduliwa rasmi tarehe 18/7/2011. Kuanzishwa kwa Wakala wa Huduma za Misitu ni kwa mujibu wa Sheria ya Wakala “the Executive Agencies Act Cap. 245 (Revised Edition 2009)”, pamoja na Sera ya Misitu ya mwaka 1998, Sera ya Ufugaji Nyuki ya mwaka 1998, Sheria za Misitu na Nyuki Sura 323 na Sura 224 za mwaka 2002.

    Aidha, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania uliundwa kwa kuzingatia Programu ya Serikali ya Maboresho katika Utumishi wa Umma ya mwaka 2000 (Public Service Reforms Programme (PSRP 2000)). Programu hii ililenga kuimarisha Idara na Wakala (Ministerial Departments & Agencies (MDAs)) katika kuhakikisha utoaji wa huduma bora na madhubuti katika utumishi wa umma, ambapo Wakala zinakuwa na uwezo, motisha na mbinu za mabadiliko yenye kuleta ufanisi na tija kiutendaji.

    1.1 Lengo Kuu la Kuanzishwa Wakala wa Huduma za Misitu TanzaniaKwa kuzingatia programu tajwa, Wakala wa Huduma za Misitu umeundwa kwa madhumuni ya kuhakikisha: Uwepo wa usimamizi madhubuti na wenye ufanisi na tija wa rasilimali za misitu na nyuki; kuongeza ubora na thamani ya kifedha katika kutoa huduma kwa umma; na kuendelea kukuza na kuboresha uwezo wa kutoa huduma kwa umma. Katika muktadha huu, masuala ya uendelezaji sera na sheria, pamoja na kanuni na taratibu zake yanashughuliwa na Idara ya Misitu na Nyuki katika Wizara ya Maliasili na Utalii. Hata hivyo majukumu ya Wakala yameongezeka licha ya kutoshughulikia sera na sheria. Wakala umepanua wigo kibiashara na kuongeza maeneo ya uzalishaji miti na mazao ya nyuki ili kukidhi mahitaji halisi, shughuli za uwekezaji, kuboresha njia mbadala za mapato na uboreshaji wa hifadhi za misitu na nyuki kwa ujumla.

    1.2 Dira “Kuwa kielelezo bora katika usimamizi endelevu wa rasilimali za misitu na nyuki.”

    1.3 Dhima “Kuwa na usimamizi endelevu wa rasilimali za kitaifa za misitu na nyuki ili kuchangia mahitaji ya kijamii, kiuchumi, ki-ikolojia na kiutamaduni kwa kizazi cha sasa na kijacho”.

    1.4 Maadili makuu Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania unaongozwa na maadili makuu kama yanavyoainishwa hapa chini:

    a. Uadilifu

    b. Usiri/Kutunza siri

    c. Kutoa huduma bora kwa wateja

    d. Ubunifu na kuleta mabadiliko

    e. Ufanisi na ufasaha

    f. Kuzingatia weledi

  • 2

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    g. Uwazi na uwajibikaji

    h. Kufanya kazi kwa ushirikiano

    1.5 Majukumu Makuu Majukumu makuu ya Wakala wa Huduma za Misitu ni pamoja na:

    a. Kuanzisha na kusimamia Misitu ya hifadhi na Hifadhi za Nyuki za Serikali kuu;

    b. Kuanzisha na kusimamia mashamba ya miti (Picha Na.1) na manzuki za Serikali kuu;

    c. Kusimamia rasilimali za misitu na nyuki katika ardhi ya jumla (General Land);

    d. Kusimamia utekelezaji wa Sheria za Misitu na Ufugaji Nyuki katika maeneo yaliyo chini ya Wakala;

    e. Kukusanya Maduhuli yatokanayo na mazao ya misitu;

    f. Kutoa huduma za ugani katika maeneo ya Wakala;

    g. Kufanya biashara ya mazao na huduma za Misitu na Ufugaji Nyuki;

    h. Uperembaji na tathimini kuhusu utekelezaji wa kazi za Wakala.

    1.6 Madhumuni ya MakalaMadhumuni ya makala hii ni kuainisha kwa kina utendaji kazi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania tangu kuanzishwa kwake, mafanikio yaliyopatikana pamoja na changamoto mbalimbali ulizokabiliana nazo. Aidha, makala inafanya tathimini ya kina ya kuonesha utekelezaji wa majukumu kabla na baada ya kuanzishwa kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania.

    Shughuli mbalimbali zinazofanywa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania

    Tathimini ya rasilimali za misitu; Kulia: Uandaaji miche ya miti kitaluni

    Picha Na.6:

  • 3

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    2. CHANGAMOTO ZILIZOKUWEPO KABLA YA KUANZISHWA KWA WAKALA

    Sehemu hii inaainisha changamoto mbalimabli zilizokuwepo kabla ya kuanzishwa kwa Wakala (Idara ya Misitu na Nyuki). Idara ilikabiliwa na changamoto nyingi ambazo ziliifanya ishindwe kutekeleza majukumu yake kikamilifu na kwa ufanisi. Changamoto hizo zilikuwa ni za ndani ya Idara yenyewe na za nje ya Idara, kama zinavyoainishwa hapa chini:

    2.1 Changamoto za Ndani ya Idara(a) Kasi kubwa ya ukataji miti katika misitu ya hifadhi na misitu katika ardhi ya

    jumla

    Mfumo wa usimamizi wa misitu ya hifadhi ulikuwa dhaifu na hivyo kushindwa kuthibiti uvunaji haramu kwa kutumia sheria. Hali hii ilitokana na: Uwezo mdogo wa idara katika upande wa watumishi na kifedha, taratibu ndefu na zenye urasimu za kukata leseni ambazo wakati mwingine zilipelekea kuwepo na mazingira ya rushwa.

    (b) Mfumo wa Kiutendaji wa Idara usio wa kibiashara

    Mfumo huu haukutoa nafasi ya kuwepo kwa mazingira ya ufanisi wa kibiashara, utekelezaji na utoaji wa huduma bora kwa mteja. Mfumo haukuzingatia huduma kwa mteja na ulikuwa na majukumu mengi yanayokinzana kwa hiyo haukuweza kuleta ufanisi. Aidha kulikuwa na uwezo mdogo wa kutoa motisha kwa watumishi kulikopelekea kupungua kwa morali ya kazi kwa watumishi.

    (c) Makusanyo madogo ya maduhuli

    Mapungufu katika utawala bora katika sekta ya misitu, hususani katika usimamizi wa ukusanyaji maduhuli, na kukosekana kwa uwajibikaji na usimamizi mahiri katika utendaji kazi kulikwamisha mafanikio katika ukusanyaji wa maduhuli. Mrahaba na ushuru wa leseni uliokusanywa na serikali ulitokana na bei zilizopangwa kiutawala na hivyo hazikuzingatia thamani yake kiuchumi wala nguvu ya soko.

    (d) Uhaba wa takwimu sahihi

    Idara ya Misitu na Nyuki haikuwa na mfumo madhubuti wa Usimamizi wa Takwimu ambao ungeweza kuleta ufanisi na ufasaha katika hatua za mipango na utoaji wa maamuzi muhimu.

    (e) Ushiriki mdogo wa jamii katika usimamizi wa rasilimali za misitu na nyuki

    Licha ya Sera za Taifa za Misitu na Nyuki kutamka wazi kuwa jukumu la kusimamia misitu ni la wananchi wote, dhana ya ushirikishwaji ilikuwa ngeni kwa wananchi na watumishi kwa ujumla.

    2.2 Changamoto za Nje ya Idara(a) Kutofautiana kwa mamlaka katika usimamizi wa misitu

    Mfumo wa usimamizi wa misitu katika ngazi ya mkoa na wilaya haukuendana na

  • 4

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    ule wa Idara ya Misitu na Nyuki (Serikali Kuu, Serikali za Mitaa/Halmashauri na Vijiji), hivyo kusababisha migongano ya kiutendaji na usimamizi hafi fu wa misitu kwa kushindwa kutekelezwa kwa sheria katika uhifadhi (Rejea Mchoro Na.1).

    (b) Matakwa ya Wahisani yaliyokinzana na Muundo wa utendaji wa Idara

    Miradi mingi iliyokuwa inapata fedha kutoka kwa wahisani ilikuwa imetengeneza mifumo yake ya usimamizi ambayo haikuendana na vipaumbele vya Idara ya Misitu na Nyuki. Miradi hiyo ilikuwa ikifanya kazi zake nje ya mifumo ya Idara ya Misitu na Nyuki. Hali hii ilikwamisha kuunganishwa kwa kazi katika miradi ya maendeleo iliyokuwa inafadhiliwa na wahisani katika mifumo ya serikali kuu na serikali za mitaa na hivyo kuifanya miradi hiyo isiweze kuwa endelevu.

    (c) Kushindwa kutekeleza Makubaliano ya Kimataifa ipasavyo

    Idara ilishindwa kutekeleza ipasavyo majukumu ya makubaliano ya kimataifa kutokana na ukosefu wa fedha za kutekeleza maazimio ya mikataba ambayo Tanzania imeridhia, kama vile mikataba ya mabadiliko ya tabianchi, uhifadhi wa bioanuwai, kukabiliana na jangwa na kadhalika.

    3. TATHMINI YA UTENDAJI KAZI KABLA NA BAADA YA KUWA WAKALA

    Sehemu hii inaainisha tofauti ambayo imepatikana baada ya kuanzishwa kwa Wakala katika utendaji, aidha inaelezea mabadiliko ya majukumu, upatikanaji wa rasilimali fedha, hali ya miundombinu na vitendea kazi kabla na baada ya kuanzishwa kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania.

    3.1 Hali ya Utendaji kabla ya kuanzishwa WakalaKabla ya kuanzishwa kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Idara ya Misitu na Nyuki (FBD) ilikuwa inatekeleza majukumu ya Programu ya Misitu ya Taifa. Hivyo majukumu ya idara kama yalivyoanishwa chini ya Programu ya Misitu ya Taifa yalikuwa kama ifuatayo: Kuendeleza na kusimamia Sera na Sheria za Misitu na Ufugaji Nyuki; Uperembaji na tathmini ya utekelezaji wa sera; Maendeleo ya rasilimali watu; Usimamizi wa vyuo vya misitu na ufugaji nyuki; Usimamizi wa misitu ya hifadhi yakiwemo mashamba ya miti; Uongoaji wa maeneo yaliyoharibika nje ya misitu ya hifadhi; Uratibu na utoaji wa huduma za ugani; Usimamizi wa rasilimali ya misitu na nyuki katika ardhi ya jumla; Utungaji na usimamizi wa Sera, Sheria na Kanuni; pamoja na Uratibu wa mafunzo na utafi ti. Aidha, Wizara ilikuwa inaandaa Mipango Mkakati (Strategic Plans) ambayo ilibainisha mikakati ya utekelezaji kwa ajili ya kutekelezwa na Idara zake. Vilevile, Mipango Kazi iliandaliwa kila mwaka ili kutekeleza mikakati iliyoainishwa. Katika kutekeleza majukumu yake, Idara iliongozwa na Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki (Director of Forestry and Beekeeping) akisaidiwa na Wakurugenzi Wasaidizi (Assistant Directors) wanne. Huduma za uhasibu, sheria na manunuzi zilikuwa zinafanywa chini ya Vitengo vya Wizara.

  • 5

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Mchoro Na.1: Mamlaka ya usimamizi wa Misitu kabla ya Wakala

  • 6

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Aidha, Idara ilikuwa na kanda saba za Uenezi na vikosi vya Doria za misitu (Forest Surveillance Unit - FSU) ambazo zilikuwa zinafanya kazi za misitu kwa kushirikiana na serikali za mitaa chini ya Mkurugenzi Msaidizi wa Misitu (Matumizi ya Misitu na Ughani). Vilevile, Idara ilikuwa inatekeleza Miradi iliyokuwa inapata fedha kutoka kwa wahisani mbalimbali. Kwa kupitia fedha za wahisani wa maendeleo Idara iliweza kutekeleza shughuli nyingi za maendeleo. Aidha, Idara ilikuwa inapewa fedha kidogo za retention na Wizara ya Maliasili na Utalii. Vilevile shughuli/miradi ilishindwa kuwa endelevu kwa kuwa ilikuwa tegemezi kwa asilimia 100%, hivyo kukoma mara baada ya ufadhili kufi kia kikomo. Jedwali Na.1 linaonesha mafanikio/shughuli za Idara kwa miaka mitatu (Julai 2007/08 – 2009/10) kabla ya Wakala.

    Jedwali Na.1: Mafanikio/Shughuli za Idara Kabla ya kuanzishwa Wakala

    SHUGHULI ZILIZOFANYIKA VYANZO VYA FEDHA/UFADHILI Hali ya misitu ya asili iliboreka kama vile uoto wa asili, kuongezeka maji na kupungua kwa uvunaji haramu na uvamizi (encroachment). Hali hii ilitokana na ushirikishwaji wa wananchi katika usimamizi shirikishi wa misitu (PFM). Takribani hekari milioni 4 za misitu ambazo ni asilimia 12.8 ya misitu yote iliwekwa chini ya Usimamizi Shirikishi (PFM); Aidha Maeneo ya misitu ya Mikoko nayo yaliongezeka

    Miradi ya Usimamizi Shirkishi (PFM) chini ya uhisani wa Denmark, Finland, World Bank/IDA Credit kupitia Mradi wa TFCMP, Serikali ya Norway (NORAD) kupitia Mradi wa Management of Natural Resources Programme (MNRP)

    Uendekezaji wa mashamba 16 ya miti ulikuwa hekta 6,376 (2005/06- 2009/10) ambapo ni wastani wa hekta 1275.2 kwa mwaka

    Idara ya Misitu na Nyuki - Fedha za Logging Miscellaneous Development Account (LMDA)

    Upimaji wa misitu ulifanyika katika wilaya 11 ambazo zina rasilimali kubwa ya misitu kama msingi wa kuandaa mipango ya usimamizi. Wilaya hizo ni Kilwa, Nachingwea, Liwale, Tunduru, Rufi ji, Mkuranga/Kisarawe, Kilombero, Mvomero/Morogoro, Ulanga, Handeni/Kilindi na Mpanda;

    SAP- Strategic Analysis and Planning - SIDA

    Mradi wa Uboreshaji Ufugaji Nyuki (Beekeeping Improvement Project) ulianzishwa katika wilaya 30. Chini ya Mradi huu vikundi vya wafugaji nyuki 135 vilianzishwa vikijumuisha watu 2,270 kutoka vijiji 75 katika wilaya 25.

    Serikali ya Ubelgiji kupitia Belgium Technical Cooperation (BTC)

    Kuongezeka kwa maduhuli na hivyo kuongezeka kwa fedha za retention scheme. Mwaka 2007/08 takribani TAS 23 bilioni za maduhuli zilikusanywa na mwaka 2008/2009 TAS15.5 bilioni maduhuli zilikusanywa.

    Retention scheme, World Bank/IDA Credit kupitia Mradi wa TFCMP

    Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF) ulianzishwa kama chanzo cha fedha kwa ajili ya shughuli za sekta.

    World Bank/IDA Credit kupitia Mradi wa TFCMP

    Vigezo vya ukusanyaji wa maduhuli na utaratibu wa kuimarisha uuzaji wa magogo na mfumo wa kuuza nje ya nchi mazao ya misitu ulitayarishwa. Mfumo wa usafi rishaji mkaa na kuni ulitayarishwa pia

    World Bank/IDA Credit kupitia Mradi wa TFCMP

  • 7

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    SHUGHULI ZILIZOFANYIKA VYANZO VYA FEDHA/UFADHILI Mfuko wa Hifadhi ya Milima ya Tao la Mashariki (Eastern Arc Mountains Conservation Endowment Fund (EAMCEF) ulianzishwa kama njia endelevu ya kupata fedha kwa ajili ya uhifadhi wa Misitu ya Milima ya Tao la Mashariki

    GEF/UNDP na World Bank kupitia Mradi wa TFCMP

    Kuanzishwa kwa Kikosi cha Doria (Forest Surveillance Unit (FSU) katika kanda nane kuhakikisha utii wa sheria (law compliance)

    World Bank/IDA Credit kupitia Mradi wa TFCMP

    Mwongozo wa Uvunaji Endelevu ulitayarishwa na Kamati za wilaya za kusimamia uvunaji zilianzishwa;

    World Bank/IDA Credit kupitia Mradi wa TFCMP

    Eneo la mikoko liliongezeka kwa kiasi cha asilimia 16 (16%) kutoka hekta 15,500 ha hadi hekta 133,480;

    Norway (NORAD) kupitia Mradi wa Management of Natural Resources Programme (MNRP)

    Mwongozo wa kupima ubora wa mazao ya nyuki uliandaliwa na sampuli 43 za asali zilikusanywa kwa ajili ya kupimwa kemikali

    Retention scheme chini ya FBD

    Mapitio ya Mitaala ya Chuo cha Ufugaji Nyuki na Chuo cha Misitu yalifanyika

    Mradi wa Finland - NFP- ISP

    Jumla ya watumishi 344 (19.1%) walihudhuria kozi za muda mrefu za misitu na ufugaji nyuki pamoja na kozi zingine. Kozi kama vile MSc -28, Diploma and Cheti - 314; na watumishi 45 walihudhuria kozi fupi

    Retention scheme FBD na World Bank/IDA Credit kupitia Mradi wa TFCMP

    Jengo la Makao Makuu ya TFS (Tanzania Forest Services - Mpingo House) lilikamilika na kuhamiwa na watumishi wa Wizara ya Maliasili na Utalii

    World Bank/IDA Credit kupitia Mradi wa TFCMP

    Majengo matatu ya Chuo cha FTI na BTI yalikarabatiwa . Vifaa vya ofi si vilinunuliwa na huduma ya mtandao iliwekwa katika vyuo vya FTI, BTI na FITI

    Finland kupitia mradi wa Vyuo NFP- ISP

    Mradi wa National Forest Resource Monitoring and Assessment (NAFORMA) ulianzishwa kwa ajili ya kupata taarifa za kitaifa katika rasilimali ya misitu ambazo zitatumika kama msingi wa kuandaa kanzidata za taifa;

    Retention scheme na Finland na FAO na World Bank Credit kupitia Mradi wa - TFCMP

    Hifadhi Asilia tatu zilianzishwa; Nilo, Kilombero na Uluguru kama sehemu ya kuboresha uhifadhi wa bionuwai ya misitu, Hifadhi za Asili 4 ziliingizwa kwenye mchakato wa kupandishwa hadhi (Magamba, Chome, Mkingu na Uzungwa scarp)

    GEF/ na Germany kupitia UNDP, Retention scheme na World Bank Credit kupitia Mradi wa - TFCMP

    Kanzidata ya Taifa ya Misitu na Nyuki (NAFOBEDA) ilienezwa katika wilaya 67 na iko katika Tovuti ya Wizara

    Miradi ya Danida, Finland na World Bank/ (IDACredit kupitia TFCMP

    Mafanikio ya shughuli za Idara ya Misitu na Nyuki kwa misaada ya wahisani wa maendeleo pamoja na mkopo kutoka World Bank kupitia TFCMP vimekuwa msingi bora wa mchakato wa kuanzishwa na kuingia kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania.

  • 8

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    3.2 Hali ya Utendaji baada kuanzishwa kwa WakalaMchakato wa kuanzisha Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania umewezeshwa na Mradi wa Usimamizi na Uhifadhi wa Misitu Tanzania (Tanzania Forest Conservation Management Project(TFCMP)) kupitia mkopo wa Benki ya Dunia (IDA Credit). Utekelezaji wa mradi ulikuwa chini ya uangalizi wa Kamati ya Uendeshaji ya Programu ya Taifa ya Misitu (NFP Steering Committee). Hata hivyo utekelezaji wa shughuli za mradi ulijumuishwa na shughuli za Idara ya Misitu na Nyuki. Mratibu wa TFCMP pamoja na Mkurugenzi wa Misitu na Nyuki na watumishi wa Idara ya Misitu na Nyuki waliwajibika katika utekelezaji wa Mradi. Mchakato wa kuanzisha Wakala huu ulichukua muda mrefu na ulitumia sehemu ya budget ya mradi wa TFCMP ya kiasi cha takribani dola za Kimarekani (USD) milioni 37.0.

    3.2.1 Makao Makuu ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)Makao Makuu ya Wakala yako katika Jiji la Dar es Salaam–katika Wizara ya Maliasili na Utalii, Wakala umepewa nafasi katika ghorofa ya Tatu ya jengo la Mpingo (Picha Na.2) lililopo 40 Barabara ya Nyerere, 15472 Dar es Salaam. Aidha, kuna majengo ambayo yanatumiwa na Mradi wa NAFORMA na Mfuko wa Misitu Tanzania (TaFF) katika eneo la Ivory Room.

    Picha Na.2: Jengo la Mpingo-Yalipo Makao Makuu ya TFS

    Kulingana na muundo wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (Mchoro Na.2) upo mgawanyiko katika maeneo makuu matatu: Makao Makuu, Kanda na Mashamba ya miti. Makao makuu inaundwa na menejimenti inayojumuisha Mtendaji Mkuu, Wakurugenzi watatu, Meneja wawili wa Vitengo vya Sheria na ugavi, Mhasibu Mkuu na Mkaguzi Mkuu wa ndani. Menejimenti ya Wakala na baadhi ya watumishi wengine wako katika jengo la Mpingo gorofa ya tatu. Wakala pia una Meneja wa Kanda saba (7) na Mashamba ya miti 18. Vile vile Wakala umeboresha utendaji wake kupitia wilaya; ambapo Meneja wa wilaya 118 wameteuliwa na kupatiwa nyenzo za kazi. Tofauti na Kanda saba za awali za Uenezi na vikosi vya Doria za misitu chini ya Idara; Muundo unaojumuisha Kanda saba za Wakala umeboresha tija katika utendaji kwa kuimarisha uhifadhi na usimamizi wa misitu, ukusanyaji wa mapato, uenezi, na ulinzi wa misitu.

  • 9

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Mchoro Na. 2: Muundo wa Wakala (TFS)

  • 10

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    3.2.2 Kanda za Wakala na Mashamba ya mitiWakala una Meneja wa Kanda saba (7). Kanda hizo ni Mashariki, Kaskazini, Kati, Kusini, Nyanda za juu Kusini, Ziwa na Magharibi. Vile vile Wakala umeimarisha utendaji katika ngazi ya Wilaya kwa kuteua na kusambaza Meneja wa Wilaya 118. Aidha katika ofi si 6 za kanda, Wakala unatumia majengo yaliyokuwa ya FBD ambayo yamefanyiwa ukarabati ili yaweze kutumika. Katika kanda ya Kusini, Wakala umekodi nyumba mjini Masasi. Aidha, wapo Meneja wa mashamba ya miti 18 ambayo ni: Buhindi, Kawetire, Kiwira, Korogwe, Longuza, Mbizi, Meru, Mtibwa, Kilimanjaro Kaskazini, Kilimanjaro Magharibi, Ruvu Kaskazini, Rondo, Rubare, Rubya, Sao Hill, Shume Ukaguru na Wini-Ifi nga. Meneja wa mashamba ya miti 15 wanatumia majengo yaliyokuwa chini ya FBD. Meneja wa Mashamba mapya wanatumia majengo yaliyopangishwa kwa Wakala au ofi si za zamani za idara ya misitu zilizotolewa na Halmashauri za Wilaya husika. Kila Meneja wa Kanda na wa shamba wana vitendea kazi kama magari, pikipiki, mitambo, kompyuta za vipakatalishi na mezani pamoja na vifaa vingine muhimu vya ofi si kwa ajili ya kufanyia kazi za Wakala.

    Pamoja na vitendea kazi kuwa vichakavu, kila Meneja ana bajeti ambayo iko kwenye mpango kazi wa kibiashara ukianisha shughuli za Wakala katika ngazi hiyo mfano, ukarabati wa majengo, barabara na ununuzi wa vitendea kazi; kama vile magari, pikipiki na matumizi mengine. Jedwali Na. 2 linaonesha majengo na vitendea kazi vya FBD na TFS katika Makao Makuu na vituo vya nje.

    Jedwali Na 2: Majengo na vitendea kazi vya FBD na TFS katika Makao Makuu na vituo vya nje.

    Vifaa Idadi vitendea kazi vilivyorithiwa kotoka FBD

    Idadi Vilivyonunuliwa na Wakala

    Jumla ya Vitendea Kazi vilivyopo

    Mitambo mikubwai) Bulldozer 5 5ii) Motor grader 4 1 5iii) Wheel loader 3 1 4iv) Stone crusher 1 1v) Tractors and Trailers 16 4 20

    Other working facilitiesvi) Generators 10 1 11vii) Water pumps 2 2i) Computers 42 105 147ii) Fax machines 3 3iii) Photocopier 11 11i) Telephones 16 (stations) 16ii) Radio communication Systems 3 (stations) 3iii) E-Mail/Internet systems 6 1 7Transport Equipmenti) Lorries 26 32 58

  • 11

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    ii) Light vehicles (4WD/SW) 109 30 139iii) Motor cycles 383 339 722iv) Bicycles 122 122 244v) Passanger Service Bus 1 3 4vi) Boat

    Buildings &Structuresi) Offi ce buildings 63 7 70ii) Residential buildings 580 580iii) Workshops & Garages 23 23iv) Dispensaries 09 09v) Social Hall/ Facilities 12 12vi) Stores 7 7

    Majengo na vitendea kazi yaliyokuwa ya FBD yote yamechukuliwa na Wakala (TFS) na kwa sasa ni mali ya TFS. Hali ya majengo yote yanayotumika ni nzuri kwa vile yanafanyiwa ukarabati mara kwa mara. Aidha, Wakala una mpango wa kujenga majengo ya vitega uchumi katika miji ya Mbeya, Kibaha na Dar es Salaam. Hii ni pamoja na kukaratiba majengo ambayo yalikuwa chini ya FBD ambayo kwa sasa hayatumiki ili kuweza kutumika kama vitega uchumi vya Wakala. Majengo hayo yapo miji ya Morogoro, Moshi, Tanga na Shinyanga.

    3.3 Mifumo ya Utendaji ya Wakala Baada ya KuanzishwaWakala wa Huduma za Misitu Tanzania umeweka mifumo mbalimbali ya kimenejimenti kwa malengo ya kuongeza ufanisi wa kiutendaji, kuboresha utoaji huduma kwa wananchi na kupunguza gharama za uendeshaji wa shughuli za Wakala. Kwa sehemu kubwa Mifumo hii inaratibiwa na Kurugenzi ya Huduma na Uendeshaji Shughuli katika Wakala. Mifumo hii ni pamoja na Mwongozo wa Utendaji Kazi, Hati ya Kuanzisha Wakala, Mpango Mkakati, Mpango wa Biashara wa Mwaka, Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS), Uperembaji na Tathmini, Mkataba wa Huduma kwa Mteja na Mfumo wa Kushughulikia Malalamiko. Aidha mifumo mingine inayotumiwa na Wakala kutekeleza majukumu yake ni Mfumo wa usimamizi na uhakiki wa fedha (Integrated Financial Management System (IFMS)), Human Capital Information Management System, Masjala na Uhasibu.

    3.3.1 Mwongozo wa Utendaji Kazi (Framework document)Mwongozo wa Utendaji Kazi unaelezea kwa kina namna ambavyo Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania unaendesha majukumu yake kwa kuzingatia Sheria ya Wakala za Serikali, Na. 30 ya mwaka 1997, Sheria ya Misitu Na. 14 ya mwaka 2002, Sheria ya Ufugaji Nyuki Na. 15 ya mwaka 2002 na Programu ya Taifa ya Misitu na Nyuki ya mwaka 2001 ambayo iliandaliwa kama chombo cha kutekeleza Sera ya Taifa ya Misitu na Nyuki.

  • 12

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    3.3.2 Hati ya Kuanzisha Wakala (Establishment Order)Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania umeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Wakala za Serikali, Na. 30 ya mwaka 1997 iliyorekebishwa mwaka 2009 (Cap. 245). Uwepo wa Wakala unazingatia agizo la kuanzishwa kwake kwa mujibu wa Hati ya mwaka 2010 ambayo imebainisha kwa kina kuhusu utawala, muundo na majukumu ya msingi katika utendaji wa shughuli za Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania. Aidha, hati imebainisha majukumu ya Bodi ya Ushauri ambayo ni mahsusi kwa ajili ya kumshauri Waziri wa Maliasili na Utalii (WMU) kuhusu utendaji na ufanisi wa Wakala. Hati pia imeainisha orodha ya misitu yote ya hifadhi inayopaswa kusimamiwa na Wakala.

    3.3.3 Mpango Mkakati (Strategic plan)Ili kufi kia malengo na kuleta mabadiliko chanya katika utendaji kazi, Wakala umeandaa na kutekeleza Mpango Mkakati wa awali wa Miaka mitatu (3) kati ya 2010/11–2013/14; na hatimaye Mpango Mkakati wa miaka mitano (5) kati ya 2014/15-2018/19 unaotekelezwa sasa. Mpango Mkakati wa miaka mitano utafanyiwa mapitio ya katikati ya kipindi cha mpango. Mpango Mkakati umeainisha dira, dhima, maadili makuu, malengo na matokeo yanayotarajiwa, mikakati ya utekelezaji malengo hayo kulingana na bajeti/matumizi.

    3.3.4 Mpango wa Biashara wa mwaka (Business Plan)Mpango wa Biashara (Picha Na. 18) huandaliwa kila mwaka kutokana na Mpango Mkakati husika. Mpango huo unaainisha kwa kina shughuli zitakazotekelezwa na Wakala katika mwaka wa fedha husika.

    3.3.5 Mfumo wa wazi wa kupima utendaji kazi (OPRAS)OPRAS ni mfumo wa kutekeleza malengo ya menejimenti katika Utumishi wa Umma na kujenga uhusiano mzuri wa utendaji kazi kati ya viongozi na wanaoongozwa. Wakala unazingatia matumizi ya OPRAS kwa mujibu wa Waraka wa Utumishi Na. 2 wa mwaka 2004 ikiwa ni hatua muhimu katika kuboresha utendaji kazi na utoaji huduma kwa Umma. Nia ya kupima utendaji kazi ni kuwezesha Wakala kufuatilia mwenendo wa utendaji kazi wa watumishi na kuwa na usimamizi mzuri wa Rasilimali watu.

    3.3.6 Uperembaji na Tathmini (Monitoring and Evaluation) Uperembaji na Tathmini ni mfumo wa kubaini tija na ufanisi katika utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Wakala kwa kupima matokeo kulingana na Mpango kazi na bajeti. Mfumo huu unaongozwa na mpango maalumu ulioundwa kwa kuzingatia Mpango Mkakati wa Wakala. Kupitia mfumo huu watumishi wameongeza ufanisi na tija katika utendaji.

    3.3.7 Mkataba wa Huduma kwa Mteja Ili kuboresha huduma kwa wananchi, Wakala wa Huduma za Misitu umeandaa Mkataba wa

  • 13

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Huduma kwa Mteja kwa malengo ya kupata ufanisi katika kazi zake. Matumizi ya Mkataba wa Huduma kwa Mteja yanaonesha kuwa Wakala umefanikiwa kwa kujenga utamaduni mzuri wa uwajibikaji hivyo kuongeza tija na kutumia rasilimali fedha kwa uangalifu mkubwa. Baada ya kutekeleza mfumo huu wateja wameridhika na huduma zinazotolewa na Wakala, hivyo kupunguza malalamiko yaliyokuwa yanajitokeza. Malalamiko yamekuwa machache kutokana na bidii katika kazi. Aidha wafanyakazi wamekuwa wepesi kukubali mfumo huu mpya.

    3.3.8 Mfumo wa Malalamiko Utaratibu wa kushughulikia Malalamiko katika Wakala ni moja ya juhudi za kuongeza uwajibikaji na kuimarisha taratibu za kuwasikiliza wateja. Mfumo huu unawezesha Wakala kushughulikia malalamiko ya wateja kwa ufanisi kwa kuwa unaharakisha ushughulikiwaji wa malalamiko, ni wa wazi, unasisitiza kutunza siri na ni rahisi kutumika.

    3.3.9 Mfumo wa Usimamizi na uhakiki wa fedha (IFMS)Mfumo huu (Integrated Financial Management System-IFMS) ulianzishwa rasmi na Wakala mwaka 2012/13 ili kuboresha utoaji wa huduma kwa watumishi na wadau wa Wakala wa ndani na nje. Kupitia mfumo huu ufanisi wa utendaji kazi umeboreshwa kwa: kutunza mahesabu ya Wakala kwa urahisi, utoaji wa taarifa za mapato na matumizi kwa wakati, kurahisisha malipo kwa wakati na kurahisisha usahihi wa vitabu vya hesabu na benki. Wakala unakusudia kuboresha mafunzo kwa watumishi wa kitengo cha uhasibu ili kuwa na tija katika uendeshaji wa mfumo huu. Vile vile Wakala unakusudia kusambaza mfumo huu katika vituo vyake vya Kanda na mashamba ya miti ili kuwepo na muunganiko wa mfumo kuanzia Makao Makuu ya Wakala hadi vituo vyake.

    3.3.10 Mfumo wa UhasibuUhasibu ni mojawapo ya mifumo muhimu iliyosimikwa na Wakala. Kupitia mfumo wa uhasibu huduma imetolewa kwa wadau wa ndani na nje kwa uwazi na uwajibikaji katika: kushughulikia malipo kwa wakati, kuandaa na kuwasilisha taarifa ya mapato na matumizi ya Wakala kwa njia ya ushirikishwaji na uwazi kwa Mtendaji Mkuu ambaye huwasilisha katika Bodi ya Ushauri ya Wizara na hatimaye kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali. Kupitia mfumo huu ofi si ya Makao Makuu ya Wakala na ofi si za Kanda na Mashamba ya miti zinaunganishwa katika uandaaji wa mahitaji ya fedha za kazi na matumizi, taarifa za mapato na uwekaji fedha kupitia benki. Mfumo huu umetenda kazi kwa ufanisi zaidi kupitia kuwepo kwa programu ya Uhasibu yaani Integrated Financial Management System.

    3.3.11 Human Capital Information Management System Huu ni mfumo unaoendeshwa kitaifa chini ya Ofi si ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma. Wakala umeingiza mfumo huu katika mifumo yake ya kawaida ili kuboresha utendaji kazi na kuongeza ufanisi. Kupitia mfumo huu Wakala umeweza kupanga na

  • 14

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    kusimamia orodha za watumishi za mishahara, kufanya marekebisho yanayohusiana na mishahara kwa wakati na kwa ufanisi, kuondoa kwa wakati watumishi waliofi kia ukomo wa ajira, kuingiza watumishi wapya katika orodha ya malipo na kurahisisha malipo ya mishahara ya watumishi kwa wakati ikiwa ni pamoja na taarifa za malimbikizo. Aidha kupitia mfumo huu Wakala ambaye ni mwajiri ameunganishwa vema na ofi si ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma kwenye masuala ya stahiki za watumishi.

    3.3.12 Masjala ya Wazi na SiriMfumo wa Masjala unahusika na utoaji wa huduma kwa watumishi na wadau wa ndani na nje. Kupitia mfumo huu Wakala umeweza kuboresha huduma kwa kupitia: utendaji kazi wa uwazi lakini wenye kuzingatia usiri wa taarifa za watumishi, uwajibikaji katika kuhakikisha kuwa kumbukumbu za watumishi wa Wakala zinatunzwa vizuri kuanzia wanapoajiriwa hadi kustaafu, kufuatilia majalada ya ndani na nje (PSPF, NSSF, Hazina nk). Mfumo huu umeboresha utoaji wa huduma kwa wakati na kuboresha ufanisi wa watumishi ambao hutumia muda mfupi kufuatilia masuala ya ajira zao na stahiki zao.

    3.4 Sheria zingine ambazo Wakala unazitumia kufanikisha utendajiKatika kutekeleza majukumu yake, Wakala (TFS) unatekeleza Sheria mbalimbali kama: Sheria ya Usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004, Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2011, Sheria ya Fedha Na. 14 ya mwaka 2001, Sheria ya Ardhi ya mwaka 1999, pamoja na Sheria ya Ardhi ya Vijiji ya mwaka 1999.

    3.4.1 Sheria ya Mazingira ya 2004Sheria hii inaweka misingi ya usimamizi endelevu wa mazingira kwa ajili ya kuhifadhi na kudhibiti uharibifu. Aidha, Sheria inaelekeza utekelezaji wa tathmini ya athari ya mazingira kabla ya kufanya uwekezaji katika misitu chini ya uratibu wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira.

    3.4.2 Sheria ya Manunuzi ya Umma 2011Katika kuhakikisha kuwepo kwa mfumo wenye ufanisi na uwazi katika manunuzi na usimamizi wa manunuzi, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania unatekeleza Sheria ya Manunuzi ya Umma ya mwaka 2011 (Public Procurement Act, 2011). Sheria hii inabainisha misingi bora na miongozo inayowezesha Wakala kupata huduma kama vifaa (magari, mitambo) na huduma za ujenzi wa miundombinu mbalimbali kulingana na thamani halisi ya fedha.

    3.4.3 Sheria ya Fedha 2001Sheria hii (Finance Act 2001) inaweka misingi ya kudhibiti Kodi na mapato ya Serikali kwa nia ya kuongeza makusanyo (mapato ya Serikali). Wakala wa Huduma za Misitu umekuwa mstari wa mbele katika makusanyo ya Serikali hususan Kodi ya ongezeko la

  • 15

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Wakala umehusika kutekeleza majukumu ya kiutendaji yaliyokuwa yanafanywa na Idara ya Misitu na Nyuki katika maeneo ya hifadhi kwa; Kubaini na kuimarisha mipaka; Kuondoa wavamizi; Kuandaa mipango ya uvunaji; Kuimarisha doria katika misitu ya hifadhi; Kushirikisha sekta binafsi na jamii katika uhifadhi na matumizi; Kuweka na kutekeleza mipango ya kudhibiti moto (Picha Na. 3); Kuimarisha vituo vya ukaguzi; pamoja na Kuimarisha ulinzi wa misitu kwa kuajiri kada ya walinzi wa misitu (forest guard) pamoja na kuimarisha usimamizi shirikishi wa misitu nchini.

    Katika Kuboresha usimamizi na uendelezaji mashamba ya miti ya kupandwa Wakala umehusika katika: Kuongeza kasi ya upandaji miti na kupanua mashamba ya miti (Picha Na. 4); Kuongeza ubora wa mazao ya misitu; Kuanzisha mpango wa uvunaji na ugawaji wa malighafi ; Kuhamasisha wadau katika matumizi ya teknolojia ya kisasa; Kuhakikisha mashamba ya miti yanapata cheti cha ubora; Kutumia mbegu bora na viini tete; pamoja na Kushirikisha wadau wengine katika kuongeza maeneo ya mashamba ya miti.

    Uzinduzi wa shamba jipya la miti-Mbizi, Sumbawanga

    b) Kuboresha usimamizi na uendelezaji mashamba

    Bango lenye ujumbe wa uhifadhi wa misitu ya asili;

    (a) Uhifadhi na udhibiti

    Kudhibiti moto katika hifadhi (shamba la miti Sao Hill)

    Upogoaji katika shamba la miti Meru;

    Picha Na.4:

    Picha Na.3:

  • 16

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    (c) Kuboresha ukusanyaji maduhuli

    Ili kuboresha ukusanyaji wa maduhuli Wakala umeweka Mifumo/Miundombinu imara ya ukusanyaji na matumizi ya fedha (Picha Na.5); Kupanga na kudhibiti tozo kulingana na nguvu ya soko; Kuwapatia motisha na vitendea kazi watumishi wanaokusanya maduhuli; Kuweka mfumo wa kugawanya gharama; pamoja na Kubainisha vyanzo vipya vya mapato.

    Picha Na.5:

    Juu:

    Kituo cha ukaguzi wa mazao ya misitu na nyuki Nangurukuru, Kilwa

    Chini:

    Kituo cha ukaguzi wa mazao ya misitu Nyangao, Lindi Vijijini

  • 17

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Wakala umeongeza huduma na uzalishaji wa mazao ya nyuki; Kuanzisha na kuendeleza mashamba (manzuki) na hifadhi za nyuki; Kuhamasisha matumizi ya teknolojia ya kisasa katika viwanda vilivyojikita katika masuala ya ufugaji nyuki; Kudumisha na kuendeleza ubora wa mazao ya nyuki; Kuhamasisha matumizi ya vifaa sahihi vya ufugaji nyuki (Picha Na. 6); Kuanzisha na kuendeleza mashamba ya uzalishaji wa mazao ya nyuki; Kuandaa na kutekeleza mpango wa udhibiti wa kemikali katika asali; Kuandaa na kutekeleza mfumo wa ufuatiliaji wa mazao ya nyuki; Kutoa mafunzo ya: uzalishaji wa malkia ili kuongeza makundi ya nyuki, uchakataji, ufungashaji na taarifa za masoko; pamoja na Kuwezesha utafi ti na upatikanaji wa taarifa ya shughuli za ufugaji nyuki.

    (d) Kuendeleza ufugaji nyuki

    Picha Na.6:

    Juu:

    Watumishi wakishiriki kuhamasisha matumizi ya vifaa bora vya nyuki;

    Katikati:

    Kituo cha ufugaji cha kikundi, Singida;

    Chini:

    Uwekaji mizinga kwa njia salama na rahisi

    (e) Kujenga uwezo wa Kitaasisi

    Wakala umewapatia watumishi mafunzo; Usimamizi wa fedha kwa mfumo wa kibiashara; Kuandaa mipango ya biashara kila mwaka; Kuimarisha na kuboresha miundo mbinu katika maeneo ya misitu; Kutumia mfumo wa OPRAS wa kupima utendaji kazi; Kuajiri watumishi kulingana na mahitaji; pamoja na Kuboresha maslahi ya watumishi.

    Kwa kuzingatia mikakati iliyowekwa hapo juu, Wakala umeimarisha usimamizi wa rasilimali za misitu na nyuki, umepanga watumishi wake wa kada mbalimbali ili kufi kia malengo yake katika Kanda na baadhi ya wilaya ambazo zina rasilimali kubwa za misitu na nyuki. Wakala unazingatia sifa, jinsi na uhitaji. Aidha, Wakala unatoa mafunzo kwa watumishi wake ili kuboresha utendaji wao na kutoa motisha kadri unavyowezekana.

  • 18

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    thamani (Value Added Tax - VAT).

    3.4.4 Sheria ya Ardhi 1999 na Sheria ya Ardhi ya Vijiji 1999Sheria hizi zinaweka misingi kwa Vijiji kumiliki na kusimamia rasilimali za misitu katika ardhi ya Kijiji na kuzitumia katika misingi endelevu kwa kutengeneza na kusimamia Sheria ndogo kupitia Kamati za Maliasili (Village Natural Resources Committees – VNRCs)) na mpango wa Usimamizi Shirikishi wa Misitu (Participatory Forest Management – PFM).

    3.4.5 Matumizi ya TEHAMA Matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) hususan kompyuta yanakua kwa kasi kubwa duniani. Shughuli nyingi za uendeshaji wa ofi si, kama vile kuchapa taarifa mbalimbali, mawasiliano na hata kuhifadhi nyaraka na taarifa zinafanywa kwa kutumia TEHAMA. Hali hii imefanya TEHAMA kuwa sehemu muhimu ya uendeshaji wa ofi si za Serikali. Mojawapo ya mikakati ya Serikali kupitia Ofi si ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma katika Awamu ya pili ya Programu ya Kuboresha Utumishi wa Umma, ni kuimarisha matumizi ya mtandao wa kompyuta unaojulikana kama Serikali-Mtandao kwa sekta zote za Serikali. Awamu hii ya pili, imelenga kuboresha utoaji huduma kwa wananchi kwa kuzingatia utendaji unaojali matokeo na uwajibikaji.

    Wakala wa Huduma za misitu Tanzania umesimika mifumo ya TEHAMA kama sehemu ya utekelezaji wa azma hiyo ya serikali ambayo inahimiza waajiri na watumishi wa umma kufuata maelekezo na utaratibu bora katika matumizi mbalimbali ya TEHAMA na vifaa vinavyohusiana na teknolojia hiyo ikiwemo matumizi ya barua pepe, vitunza kumbukumbu na huduma za mtandao.

    Baadhi ya Mifumo iliyosimikwa na kuanza kufanya kazi katika utekelezaji wa majukumu ya Wakala ni pamoja na Mfumo wa ufuatiliaji miti inayokatwa (Log track), Mfumo wa Kudhibiti moto msituni (Fire Monitoring system), Mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ya rasilimali misitu (NAFORMA). Aidha, Wakala unatumia Tovuti (www.tfs.tz) inayotoa taarifa mbalimbali za misitu na nyuki kwa jamii na Mitandao ya kijamii (Facebook) inayoruhusu mazungumzo na jamiii inayotaka kufahamu taarifa za misitu na nyuki.

    3.5 Tathmini ya kazi za Wakala baada ya kuanzishwaBaada ya kuanzishwa Wakala majukumu ya awali yaliyokuwa chini ya Idara ya Misitu na Nyuki na ambayo yalipaswa kutekelezwa na Wakala yaliongozeka kutokana na kuimarishwa kwa rasilimali fedha na vitendea kazi. Ili kutimiza majukumu yake Wakala uliandaa Mpango Mkakati (kwa kipindi cha miaka 5) na Mpango wa Kibiashara unaoandaliwa kila mwaka. Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, kwa sasa upo katika Mpango Mkakati wa Pili ((Strategic Plan II (SPII)). Mpango Mkakati wa Wakala huainisha mikakati mbalimbali ya kutekeleza majukumu yake. Katika kipindi cha Mpango Mkakati wa kwanza mikakati ya Wakala wa Huduma za Misitu ilikuwa;

  • 19

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Picha Na.7:

    Juu: Viongozi wa Timu ya NAFORMA wakiwa kazini

    Chini Kushoto: Makala ya NAFORMA

    Chini Kulia: Mtaalam wa NAFORMA akifanya tathmini ya miti

    4. MAFANIKIO YALIYOPATIKANA TANGU KUANZISHWA WAKALA

    Sehemu hii inaainisha mafanikio ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Wakala kwa mwaka 2011/12 - 2013/14. Aidha, mwaka 2010/11 kilikuwa kipindi cha mpito cha Wakala ambacho kilitumika kujipanga kuhusu namna ya kufanikisha majukumu yake.

    i) Jumla ya watumishi 2,031 kutoka TFS, mikoa na wilaya na wanavijiji 1,484 wamehamasishwa kuhusu kuchukua tahadhari na kupimwa HIV/AIDS kupitia warsha na semina. Matokeo ya uhamasishaji na uelimishwaji umewezesha watumishi zaidi kujua hali zao na idadi ya waliopima kwa hiari iliongezeka kutoka 53 hadi 277. Watumishi 31wanaoishi na UKIMWI walisaidiwa chakula.

    ii) Kufanya Tathmini na Uperembaji wa Rasilimali za Misitu (National Forest Resource Monitoring and Assessment (NAFORMA); (Picha Na. 7), ambayo ilianzishwa ili kupata taarifa sahihi na za uhakika kuhusu hali halisi, ukubwa, na matumizi ya rasilimali ya misitu ambayo ni muhimu kwa ajili ya kutoa maamuzi na kuandaa sera na programu za kutekeleza usimamizi endelevu wa misitu. Taarifa ya NAFORMA inapatikana katika tovuti ya Wakala (www.tfs.go.tz).

  • 20

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    iii) Wakala unasimamia mashamba ya miti 18 (Kati ya hayo mashamba 3 yameanzishwa na Wakala ndani ya kipindi cha miaka mitatu). Mashamba haya (18) yana jumla ya eneo la hekta 205,522. Aidha kati ya eneo hili ha 91,662 zimepandwa miti (Jedwali Na. 3). Uoteshaji wa miti umefanyika katika hekta 14,255 za maeneo ya mashamba ya miti (Picha Na. 8) na jumla ya hekta 7,947 zimepandwa katika maeneo mapya (extension) katika mashamba 15;

    iv) Miti iliyosimama (Standing wood stock) ina meta za ujazo wa 11,808,599 ikiwa ni sawa na ongezeko la meta 528,704 kwa mwaka. Uvunaji wa meta za ujazo 2,960,833 (Jedwali Na.4) umefanyika katika miaka mitatu ya Mpango Mkakati wa kwanza.

    Picha Na.8: Bustani ya miche shamba la miti West Kilimanjaro.

  • 21

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Picha Na.9:

    Upandaji miti kitaifa

    Kushoto : Makamu wa Rais Dr Gharib Bilal (Kisarawe).

    Kulia : Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda (Singida) Wakipanda miti siku ya maadhimisho ya upandaji miti kitaifa

    Picha Na.10: Kushoto: Uwekaji wa maboya ya mpaka -msitu wa hifadhi Geita; Kulia: Kibao cha alama ya msitu wa hifadhi Kitulang’alo

  • 22

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Jedwali Na. 3: Mashamba ya miti chini ya usimamizi wa Wakala kwa hadi mwaka 2014

    S/N JINA LA SHAMBA MAHALIENEO LA SHAMBA (Ha)

    ENEO LA UPANUZI (Ha)

    JUMLA YA ENEO (Ha)

    UJAZO WA MITI (m3)

    1 Sao Hill Mufi ndi 52,070 36,003 88,073 8,341,3712 Shume Lushoto 4,227 140 4,367 510,7923 Longuza Muheza 1,904 200 2,104 242,450

    4 West Kilimanjaro Hai 4,149 337 4,486 377,601

    5 North Kilimanjaro Rombo 6,177 200 6,377 563,941

    6 Ukaguru Kilosa 976 941 1,917 60,189

    7 Kiwira Rungwe 2,784 45 2,829 334,290

    8 Kawetire Mbeya 2,131 517 2,648 137,439

    9 Rondo Lindi 864 1,541 2,405 13,869

    10 Rubya Ukerewe 1,771 181 1,952 243,930

    11 Buhindi Sengerema 3,810 7,569 11,379 261,095

    12 Meru Arumeru 6,110 0 6,110 548,954

    13 Rubare Bukoba 1,227 1,920 3,147 23,275

    14 Mtibwa Mvomero 1,86 7 75 1,942 149,274

    15 Wino-Ifi nga1 Songea 1,380 10,000 11,380 130

    16 Mbizi2 Sumbawanga 158 11,442 11,600 0

    17 Korogwe2 Handeni 0 10,805 10,805 0

    18 North Ruvu2 Kibaha/Bagamoyo 56 32,000 0

      Total   91,662 81,916 205,522 11,808,600

    Chanzo: Taarifa ya utekelezaji ya Mashamba ya miti ya TFS kwa mwaka 2013/14

    1 Mashamba ya miti mapya

    2 Misitu ya hifadhi iliyobadilishwa kuwa mashamba ya miti

    Jedwali Na. 4: Ujazo uliovunwa (cm) kutoka mashamba ya miti 2011/12-2013/14

    JINA LA SHAMBA 2011/2012 2012/13 2013/14 Total

    Sao Hill 824,000 807,000 850,000 2,481,000

    Shume 22,236 21,453 22,211 65,900

    West Kilimanjaro 24,700 18,000 1,750 44,450North Kilimanjaro 20,000 20,000 20,000 60,000

    Buhindi 22,770 22,770 24,270 69,810

    Rubare 800 0 0 800Longuza 14,481 15,412 15,000 44,893Rubya 4,895 6,473 6,900 18,268Kiwira 5,000 144 2,000 7,144Kawetire 8,940 1,500 10,425 20,865Mtibwa 23,955 25,508 15,689 65,152Matogoro 2,421 1,000   3,421Rondo 0 13,630 10,500 24,130Meru 10,000 24,000 21,000 55,000Total 984,198 976,890 999,745 2,960,833

    Chanzo: Taarifa ya utekelezaji ya Mashamba ya miti ya TFS kwa mwaka 2011/12- 2013/14

  • 23

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    v) Uimarishaji wa mipaka umefanyika katika misitu ya asili ya hifadhi 102 iliyotengwa kwa ajili ya uzalishaji (production forests) kwa kufanya soroveya ya pili (resurvey) kwa mipaka yenye urefu wa kilomita 9,975; kuweka maboya 1,600 na kuweka vibao vya alama 3,300 (sign boards); kuchimba mashimo ya mwelekeo 162 (directional trenches) na kupanda miti kwenye mpaka wa urefu wa kilomita 110. Aidha, upandaji wa miche 253,600 (sawa na hekta 210) ya aina tofauti ya miti katika maeneo ya misitu yaliyoharibika (degraded forests) ulifanyika (Picha Na.9).

    vi) Katika kuboresha usimamizi na uendelezaji misitu Wakala umeongeza kasi ya upandaji miti katika maeneo mapya kila mwaka ili kukidhi mahitaji ya mazao ya miti kwa kushirikisha wadau mbalimbali kama wananchi/ jamii na taasisi kama shule katika kupanda miti na kuimarisha uhifadhi. Katika kipindi cha 2011/12 hadi 2013/14 jumla ya miti 21,000,000 ilipandwa. Jedwali Namba 5a linaonesha idadi ya miti iliyopandwa katika maeneo ya jamii na taasisi kupitia uwezeshaji wa Wakala katika kipindi cha miaka mitatu tangu kuanzishwa kwa Wakala

    Grafu Na. 1: Mazao makuu ya Misitu yaliyovunwa 2011/12-13/14

    Jedwali Na. 5a: Upandaji miti kitaifa kwa kipindi cha miaka 2011/12 - 2013/14

    Mwaka Idadi ya miti iliyopandwa

    2011/12 7,000,000

    2012/13 7,000,000

    2013/14 7,000,000

    Jumla 21,000,000

  • 24

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    viii) Urekebishaji wa ramani 23 za misitu ya hifadhi ya asili kwa ajili ya uzalishaji, pamoja na Mipango ya kina ya usimamizi kwa misitu 9 ilitayarishwa katika jumla ya hekta 273,274.

    ix) Wakala uliweza kusimamia Mipango ya uvunaji (sample harvesting plan) ya wilaya chini ya kanda zake 7, ambapo katika kipindi cha miaka mitatu mazao mbalimbali ya misitu yalivunwa (Jedwali Na. 5b na Grafu Na. 1). Aidha, mwaka 2011/12 kuni na nguzo vilivunwa kwa wingi; mwaka 2012/13 Mkaa na mbao; na mwaka 2013/14 mazao ya misitu ya Mkaa, nguzo na mbao yalivunwa kwa wingi. Mkaa na nguzo vikionyesha kuwa ni mazao ya misitu yanayotegemewa zaidi katika matumizi.

    Picha Na. 11: Mazao ya nyuki kutokana na mafunzo; Katikati: Mizinga ya TFS ya kugawanywa kwa wadau; Kulia: Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda akipata maelezo ya ufugaji nyuki

    Picha Na.12: Kushoto: Mafunzo ya utundikaji mizinga kwa kikundi cha ufugaji Haysali, Mbulu; Kulia: Mizinga iliyogawanywa na TFS kwa kikundi cha Nguvukazi, Biharamulo

    vii) Wakala uliweza kuimarisha mipaka katika misitu ya hifadhi ya asili (protection forests) kwa kufanya soroveya ya kuhakiki mipaka ya misitu ya hifadhi ya kilomita 3,262.78; Usimikaji wa maboya 227 na kuweka vibao vya alama 425 (Picha Na.10); kuchimba mashimo ya mwelekeo 511 na kupanda miti kwenye mipaka wa kilomita 17. Aidha, uzalishaji wa ramani 40 za misitu ya hifadhi na ramani 3 za hifadhi za nyuki zinazopendekezwa ulifanyika.

  • 25

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Jedwali Na. 5b: Baadhi ya Mazao yatokanayo na misitu yaliyovunwa katika miaka mitatu

    ZAO/MWAKA 2011/12 2012/13 2013/14 TOTAL

    Magogo (CBM) 14,140.0 29,100.3 21,378.0 64,618.3

    Kuni (CBM) 701,264.0 54,359.9 86,163.6 841,787.5

    Mkaa (Magunia) 265,966.0 641,703.2 1,000,837.1 1,908,506.3

    Nguzo (RM) pamoja na nguzo za mikoko 552,300.0 235,739.4 706,550.9 1,494,590.3

    Mbao (CBM) 97,834.2 409,866.6 485,015.2 992,716.0

    Chanzo: Taarifa za Kanda za TFS

    x) Wakala umeandaa Mpango Mkakati wa pili (SP II) ambao pamoja na mambo mengine unaainisha mikakati ya kuondokana na upungufu wa timbao ifi kapo mwaka 2030. Takribani hekta 185,000 zitapandwa kila mwaka kwa kushirikisha wadau wote. Utayarishaji wa Mipango ya Usimamizi katika mashamba ya miti umekamilika kwa asilimia 100. Mipango inaonesha ujazo unaelekea kuwa endelevu kwa Wakala; Jumla ya hekta 69,613 za hifadhi za nyuki zinazopendekezwa ambazo zitajumuisha za Taifa ((NBRs-(37,166ha)) na za Vijiji (VBRs)- 32,447 ha)) zipo katika hatua mbalimabli kama inavyooneshwa kwenye Jedwali Na.6.

    Picha Na. 13: Nyumba ya kulea malkia wa nyuki Kituo cha Kibaha, DSM

  • 26

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Jedwali Na. 6: Eneo na Hali ya hifadhi za nyuki zilizopendekezwa

    Mahali Eneo (ha) Hadhi

    Kanda ya Kati (Jongolo-1000ha, Wambura sendeko-1700ha, Wairo- 447ha and Mialo 500 ha Kondoa. 3,647 Eneo limepimwa na kukubaliwa na Serikali ya Kijiji.

    Msemembo and Aghondi -Manyoni) 1,700  Eneo limetambuliwa linasubiri maamuzi ya kijiji

    Kanda ya Magharibi: Buha - Kibondo 2,524 Eneo limetambuliwa na kupimwa

    Kanda ya ziwa: (Sengerema, Maswa, Bukombe, Misenyi, Bunda, Nyangwale, Biharamulo) 29,980 Eneo limetambuliwa

    Kanda ya Kusini: (Enje-Nachingwea and Lilindindo - Namtumbo) 4,000

    Eneo limetambuliwa , ramani imechorwa na mpango wa usimamizi umeandaliwa Usimamizi wa pamoja utafanyika kati ya Wakala na Kijiji

    Kanda ya Kaskazini: Kangata (1439ha), Kwenyunga Magiri (138 ha) - Handeni 1,578 Hifadhi ipo katika hatua za mwisho za kutangazwa

    Sambu Kilindi 567 Eneo limetambuliwa na kuidhinishwa na kijiji

    Kanda ya Kusini Nyanda za juu: Kipembwawe in Chunya and Ndarambo 23,150

    Eneo limepimwa, ramani imechorwa na hifadhi ipo katika hatua za mwisho za ktangazwa

    Shinji and Ndarambo - Momba District 2,000 Eneo limetambuliwa

    Kanda ya Mashariki: Lukenge – Kibaha; Leshata and lsitu - Kilosa)

    467 Eneo limetambuliwa na kufanyiwa soroveyaMsingisi, Lungo and Mlumbilo villages - Gairo and Mvomero

    Jumla Kuu ya Maeneo yote 69,613

    Chanzo: Taarifa ya utekelezaji za mwaka za TFS 2011/12-2013/14

    xi) Katika kipindi cha Mpango Mkakati (SPI), manzuki 21 zenye mizinga 3,870 zilisimamiwa, aidha Wakala ulitoa mafunzo kwa vikundi 921 (Washiriki 7,320) vya wafugaji nyuki, katika vijiji 242 kutoka wilaya 30.Vilevile Wakala uligawa bure mizinga 14,076 (Picha Na. 11 & 12).

    xii) Tangu kuanzishwa kwa TFS wilaya 29 na mashamba ya miti 7 zimeanzisha manzuki

    Picha Na 14: Kushoto: Mbao zilizokamatwa; Kulia: Uondoaji wa wavamizi -msitu wa hifadhi wa Nyahua Mbuga

  • 27

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    36 na kutundika mizinga 4,184 katika misitu ya hifadhi na mashamba ya miti kama inavyooneshwa kwenye Jedwali Na. 7.

    Jedwali Na. 7: Idadi ya manzuki na mizinga inayosimamiwa na TFS

    Mahali Idadi ya Manzuki Idadi ya mizinga

    Kanda ya Kaskazini 15 508

    Kanda ya Kusini 10 1,500

    Kanda ya Mashariki 1 42Kanda ya Nyanda za Juu Kusini 3 1,400

    Mashamba ya miti 7 724

    JUMLA 36 4,184

    Chanzo: Taarifa ya Utekelezaji ya miaka mitatu 2011/12-2013/14

    xiii) Wakala ulitoa mafunzo ya kulea malkia wa nyuki kwa watumishi 58, aidha Kituo cha kulelea malkia wa nyuki kimeanzishwa katika Kanda ya Mashariki (Picha Na 13). Katika Mpango Mkakati wa pili Wakala unakusudia kuwa na vituo vya kulea malkia katika kanda zote. Lengo likiwa ni kuhakikisha kuna upatikanaji mkubwa wa makundi ya nyuki. Mafunzo ya ubora wa asali, masoko na ufungashaji wa mazao ya nyuki na ujasiliamali, kanuni za ufugaji nyuki ziliendeshwa kwa wafugaji nyuki na wafanya biashara 241kutoka wilaya 25. Aidha, upimaji wa sampuli 172 za ubora wa asali ulifanyika na kugundua kuwa asali yetu inakidhi viwango vya masoko la kitaifa na kimataifa.

    xiv) Katika kipindi cha miaka 3 Wakala uliweza kufanya doria katika misitu ya hifadhi, hifadhi za nyuki, manzuki, misitu katika ardhi ya jumla na maeneo ya masoko. Jumla ya siku za doria 300,139 zilitumika. Kutokana na doria hizi uvunaji haramu wa mazao ya misitu umepungua kwa asilimia zaidi ya 50%. Baadhi ya mazao ya misitu yaliyokamatwa na kutaifi shwa ni mbao 295,508 (Picha Na.14-Kushto), magunia ya mkaa 97,451, milango 1,380, magogo 13,983 na nguzo 148,397. Vilevile TFS

    Picha Na. 15: Ukarabati wa nyumba za watumishi Chuo cha FTI, Olmotonyi- Arusha

  • 28

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    ilitoa mchango wa fedha na nguvu kazi katika operesheni maalum ya kupambana na ujangili, uvunaji haramu, na wavamizi wa misitu ya hifadhi. Kupitia operesheni hii jumla ya vipande vya mbao 15,143 magunia ya mkaa 678, magogo 135 na misumeno 60 ilikamatwa. Aidha, Kikosi kazi kilichokuwa kimeundwa na serikali na kuwezeshwa na TFS kushughulikia masuala ya uvunaji haramu na biashara katika mpaka kati ya Msumbiji na Tanzania kilifanikiwa kukamata mbao 32,085 na wahalifu 14 .

    xv) Wakala uliweza kuwaondoa wavamizi katika misitu ya hifadhi takribani 52 (Jedwali Na. 8) na (Picha Na. 14–Kulia) kwa kufanya siku za doria 99,335 wahalifu 1,328 walikamatwa, mali zao zilikamatwa pamoja na kulipishwa faini na kesi 60 ziko mahakamani.

    Jedwali Na.8: Misitu ya Hifadhi iliyokuwa na wavamizi

    S/N Msitu wa Hifadhi Mahali/Wilaya1 Nyahua Mbuga na Goweko Sikonge - Tabora2 Uyui-Kigwa – Rubuga na Urumwa Uyui - Tabora

    3 Igombe River, North Ugala and Mpandaline Kaliua/Urambo - Tabora

    4 Mkweni Kahama - Shinyanga5 Inyonga West and Mlele Hills Mlele - Katavi6 North-East Mpanda, Uruwa Mpanda - Katavi7 Ilombelo Nzega - Tabora8 Kising’alugalo Iringa - Iringa9 Mbeya Range Mbeya - Mbeya10 Kipembawe Chunya - Mbeya

    12 Mangalisa Mpwapwa - Dodoma

    13 Chenene Mpwapwa - Dodoma

    14 North Mamiwa-Kisara and South Mawiwa – Kisara, Palaulanga, Ukwiva, Mamboya na Milindo Kilosa - Morogoro

    15 Biharamulo and Nyantakala Biharamulo - Kagera17 Minziro NR Misenyi - Kagera18 Ruvu South & North Kibaha - Pwani19 Amani NR, Kwani, Tongwe, Muheza - Tanga20 Magamba NR Lushoto Tanga

    21 Mkingu NR Mvomero - Morogoro

    22 Chome NR Same - Kilimanjaro23 Bombo East and Bombo West, Nilo NR, Bubamavumbi Korogwe- Tanga

  • 29

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    24 Kilindi Kilindi - Tanga25 Korogwe Fuel wood, Kwasumba and Jungu Handeni - Tanga

    26 Mkuti, Makere North, Makere South and Mwalye Morogoro - Morogoro27 Geita Geita - Geita

    28 Sayanga Kondoa - Dodoma

    29 Nikonga Kahama - Shinyanga

    30 Rau Moshi - Kilimanjaro

    31 Hifadhi ya Mikoko ukanda wa kaskazini Tanga rural - Tanga32 Hifadhi ya Mikoko ukanda wa kati Rufi ji delta33 Kazimzumbwi Kisarawe34 Mselezi Ulanga35 Nandembo na Mhuwesi Tunduru36 Kipiki Namtumbo

    xvi) Katika kutoa elimu ya uhifadhi na kudhibiti moto jumla ya vijiji 1,772 vilivyo karibu na, misitu ya hifadhi vilihamasishwa. Vipindi vya redio 266, vipindi vya runinga 55, maonesho ya video 44, vipeperushi 99, nakala 400 za utendaji bora na nakala 22,886 ya vijitabu vya ugani zilitayarishwa na kusambazwa.

    xvii) Uongoaji wa hekta 10,951.5 za maeneo yaliyoharibika kwa kupanda miti 208,500 na kutoa misaada kwa jamii kama: viriba kilo 12,515 na mbegu za miti kilo 2,004 ili kupanda jumla ya miti 13,412,704 katika maeneo yaliyoharibika, vijishamba, mashamba binafsi, vijiji na kuzunguka shule.

    xviii) Hekta 52.42 za shamba la kamba Mafi a na hekta 562 za mashamba ya chumvi katika wilaya za Mkuranga, Rufi ji delta, Kilwa, Lindi na Mtwara zimetenga na kupimwa. Aidha, Kilomita 268.9 za njia za utalii (nature trails) zimejengwa; kilomita 69.3 za njia za gari (drive routes), kilomita 64 za njia ya utalii (nature trails), maeneo 10 ya kupumzika (resting points/picnic site) na maeneo 21 ya kuweka kambi (campsites); zimeimarishwa.Takribani hekta 135,000 zimetambuliwa na mchakato wa kuziweka katika usimamizi shirikishi unaendelea.

    xix) Miongozo ya usimamizi shirikishi imetayarishwa pamoja na Mwongozo wa mfumo wa kugawana faida na majukumu umetayarishwa na kukubaliwa na wadau. Mikataba 19 ya usimamizi wa pamoja wa misitu ya hifadhi ya taifa na sheria ndogo katika vijiji vinavyozunguka misitu ya hifadhi iliandaliwa, aidha mikataba 57 ya usimamizi wa msitu kwa ajili ya kurasimisha shughuli za usimamizi wa pamoja ilikubaliwa. Vilevile Vijiji 163 vimefundishwa na kuwezeshwa juu ya shughuli za kipato mbadala. Hadi kufi kia 2014 jumla ya hekta 7.7 zimewekwa katika usimamizi shirikishi na jamii, ikiwa ni ongezeko la hekta milioni 3.6 ya eneo chini ya usimamizi shirikishi ukilinganisha na eneo la awali la hekta 4.1 milioni za mwaka 2006.

  • 30

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    xx) Katika kutekeleza Mpango Kazi wa Nishati timbao jumla ya vituo 101 vya kukusanyia na kuuzia mkaa kandokando ya barabara za Dar es salaam – Morogoro – Segera pamoja na wilaya za Songea, Namtumbo, Mbinga, Handeni, Korogwe, Biharamulo, Kigoma, Shinyanga, Kilosa, Rufi ji, Gairo, Mvomero na Masasi vimeanzishwa. Aidha washiriki 30 kutoka kijiji cha Mbangamawe wilaya ya Songea walifundishwa njia za kuzalisha mkaa bora. Vilevile Wanawake 120 kutoka vijiji 6 vya wilaya za Mbozi, Chunya na Momba walifundishwa jinsi ya kutengeneza na kutumia jiko banifu. Wakala utaendelea kuongeza na kudhibiti vituo vya kuuzia mkaa.

    xxi) Ukaguzi maalumu wa maduhuli ulifanyika na jumla ya TAS 7.62 bilioni ziliokolewa kama inavyooneshwa katika Jedwali Na.9. Aidha kaguzi hizi zimeweza kuongeza utii wa sheria bila shuruti.

    Jedwali Na. 9: Makusanyo kutokana na Ukaguzi maalumu

    Mwaka Idadi ya Kaguzi Maduhuli yaliyookolewa (Billion TZS)2011/12 2 1.42012/13 6 3.952013/14 3 2.27Jumla 11 7.62

    Chanzo: Taarifa za utekelezaji za mwaka za TFS 2011/12-2013/14

    xxii) Jumla ya wilaya 85 kati ya wilaya lengwa 80 ziliwezeshwa kuandaa mipango ya uvunaji, kufanya mikutano ya kamati za uvunaji na kudhibiti uvunaji.

    xxiii) Jumla ya wakaguzi wa maduhuli 82 kati ya 200 wa Wizara ya Maliasili na Utalii na halmashauri za wilaya walishiriki kwenye warsha ya mafunzo ili kuboresha uwezo wa kukusanya maduhuli kwa kutumia vitabu vya kukusanyia maduhuli, utaratibu wa kupiga faini na matumizi ya kanuni za misitu; Vituo vya ukaguzi 35 viliwezeshwa kukagua, kuhakiki uhalali, kupitisha vibali vya kusafi risha (TP) mazao ya misitu na vituo vipya 25 vya ukaguzi vimeanzishwa ili kuimarisha utii wa sheria.

    xxiv) Mapitio ya mirahaba na ada za mazao ya misitu na huduma yalifanyika na kuidhinishwa na Waziri mwenye dhamana.

    xxv) Wakala umeweza kusaidia vyuo vya Misitu (FITI/FTI) na Nyuki (BTI) kununua vitabu, kukarabati nyumba za watumishi (Picha Na 15), madarasa uwanja wa michezo na mabweni ya wanafunzi;

    xxvi) Ili kuinua kiwango cha ufanisi wa kazi Wakala umetoa mafunzo kwa watumishi 57 kwa mafunzo ya muda mrefu na watumishi 132 - mafunzo ya muda mfupi (Jedwali 10). Aidha watumishi wengi wamepatiwa mafunzo mbalimbali ikilinganishwa na kipindi cha Idara.

  • 31

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Jedwali 10: Watumishi wa TFS waliohudhuria mafunzo (2011/12 -2013/14)

    Mwaka Watumishi wa waliohudhuria kozi ndefu

    Watumishi wa waliohudhuria kozi fupi

    Malengo Mafanikio Malengo Mafanikio2011/2012 47 39 151 112012/2013 67 76 120 252013/2014 61 57 100 68Jumla 371 132

    Chanzo: Taarifa za utekelezaji za mwaka za TFS 2011/12-2013/14xxvii) Mwaka 2013/14 Wakala umeajiri watumishi wapya 354 kama Jedwali Na. 11

    linavyoonyesha

    Jedwali Na.11: Watumishi wapya kwa Kada walioajiriwa na Wakala

    S/N Category 2013/14Afi sa Misitu 41

    Afi sa Nyuki 10Msaidizi Misitu 244Msaidizi Nyuki II 16Katibu Muhtasi III 12

    6 Afi sa Rasilimali watu 017 Msaidizi Masjala II 138 Dereva II 039 Mlinzi 02

    Picha Na. 16: Ofi si ya Hifadhi asilia Uluguru, Morogoro

  • 32

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    10 Msaidizi wa Ofi si 0611 Fundi Sanifu (Mechanical Technician) 0312 Mhudumu Kituo cha afya (Medical Attendant) 0213 Mgavi Msaidizi II 01

    Jumla 354

    Chanzo: Taarifa za utekelezaji za mwaka za TFS 2012/13-2013/14

    xxviii) Wakala umeweza kulipa watumishi wake stahiki zao, marupurupu na motisha, kununua huduma na kulipia huduma za ofi si kwa kanda 7, mashamba 18 na Makao makuu.

    xxix) Wakala umefanya maboresho ya makazi ya watumishi, ofi si (Picha Na. 16) pamoja na miundo mbinu kama: kuratibu ujenzi ofi si 1 na nyumba za wakuu wa safu 12, na kukarabati nyumba 5 kwa kutumia fedha za UNDP na Serikali ya Ujerumani. Vilevile Wakala umegharimia ujenzi wa majengo 7 katika mashamba ya miti Mtibwa (2), Rubare (1), Wino-Ifi nga (1), Ukaguru (2), Rondo (1). Ukarabati wa nyumba za watumishi 287 na majengo ya ofi si, pia nyumba 2 za nyuki zilijengwa katika Mradi wa Buha beekeeping project - Kibondo. Wakala umeweza kujenga barabara mpya za msituni zenye urefu wa kilomita 161, na kukarabati kilomita 7,672, Madaraja 53 na mnara 1 wa kufanyia doria za moto.

    xxx) Wakala umeweza kuandaa Mfumo wa uperembaji na tathmini na tayari unatumika. Aidha Wakala uliandaa Warsha ya mafunzo kwa watumishi 60 kuelimisha mpango wa uperembaji na tathmini. Jumla ya kanda 7 na mashamba 15 yalifanyiwa uperembaji. Jumla ya vituo 73 kati ya vituo 97 (75.2%) vilitembelewa na kufanyiwa ukaguzi (Jedwali Na.12). Vilevile ukaguzi wa ndani ulifanyika kama sehemu ya uperembaji kwenye mashamba 13 na kanda 5. Ukaguzi nje (external auditing) wa mahesabu kwa mwaka 2011/12 na 2012/13 ulifanyika na matokeo yalikuwa mazuri (“satisfactorily unqualifi ed audit report”).

    xxxi) Mkakati wa Kitaifa wa Kuzuia na Kupambana Rushwa ulitekelezwa ambapo warsha 7 za kuelimisha zilifanyika na kuhudhuriwa na watumishi 841 katika ngazi tofauti. Kwa sasa Mkakati wa kupambana na Rushwa wa Wakala (Picha Na.17) umeandaliwa na utekelezaji wake unatarajiwa kuleta mabadiliko yenye ufanisi kwa Wakala.

    xxxii) Huduma kwa Mteja inatekelezwa na inatarajiwa kuwa madhubuti ili kuimarisha uwazi na uwajibikaji na hivyo kuongeza ufanisi kazini. Wakala umeandaa andiko la Mkataba wa Huduma kwa Mteja (Picha Na.18) unaotarajiwa kuongeza tija katika utoaji wa huduma.

  • 33

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Picha Na.17: Mkakati wa Kupambana na Picha Na.18: Mkataba wa Huduma kwa Mteja

    Rushwa

    Jedwali Na.12: Idadi ya vituo vya Wakala vilivyotembelewa kwa ajili ya Uperembaji kwa Kanda 7 kati ya 2012/13 na 2013/14

    S/N Kanda Idadi ya Vituo Idadi ya maeneo yaliyotembelewa1 Kaskazini 18 112 Mashariki 15 93 Magharibi 9 74 Kati 18 165 Kusini 17 146 Ziwa 12 10

    7 Nyanda za Juu Kusini 8 6Jumla 97 73

    xxxiii) Wakala umeweza kuboresha maswala ya jinsi: asilimia 40 ya Wakuu wa Vitengo/ Meneja Waandamizi wa TFS Makao Makuu ni wanawake, asilimia 57 ya wasaidizi wa Meneja katika kanda za TFS ni wanawake, aidha wanawake 2 ni Meneja wa mashamba ya miti na mmoja ni Meneja wa Hifadhi Asilia.

  • 34

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    5. MUHTASARI WA MCHANGUNUO WA UTENDAJI KABLA NA BAADA YA KUANZISHWA WAKALA

    Mchanganuo ufuatao (Jedwali Na. 13) ni muhtasari wa masuala makuu yaliyofanikiwa chini ya Wakala katika kipindi cha miaka mitatu yakilinganishwa na yale yaliyotekelezwa na Idara ya Misitu na Nyuki katika kipindi cha miaka mitatu kabla ya kukabidhi majukumu kwa Wakala (TFS)

    Jedwali Na. 13: Muhtasari wa Mchanganuo wa Utendaji wa Wakala

    Na. Suala Kabla ya Wakala

    (Idara ya Misitu na Nyuki)

    Baada ya Uanzishwaji wa Wakala (TFS)

    1 Ukusanyaji wa Mapato/Maduhuli

    Mapato kwa miaka Mitatu (2007/8-2009/2010) yalikuwa ni jumla ya Takribani TAS Bilioni 87, ikiwa ni wastani wa billioni 29 kwa Mwaka.

    Mapato kwa miaka Mitatu (2011/12-2013/2014) yalikuwa ni jumla ya Takribani TAS Bilion 199.7, ikiwa ni wastani billion wa 67 kwa Mwaka.

    Mapato makubwa yalitokana na mrahaba, ambao ulichangia asilimia zaidi ya 92 ya mapato yote

    Mapato makubwa yalitokana na mrahaba ambao ulichangia asilimia zaidi ya 66 ya mapato yote

    2 Uhifadhi Mipango ya usimamizi wa misitu asili yenye eneo la hekta 1,338,800 ya uzalishaji na uhifadhi iliandaliwa, kati ya eneo hili misitu 8 ilikuwa ni misitu lindimaji yenye viumbe ndwele na bioanuwai ya hali ya juu ikiwemo misitu ya hifadhi ya Amani, Kilombero, Nilo, Uluguru, Magamba, Uzungwa, Mkingu na Chome

    Wakala ulisimamia ha 4,164,463 za misitu asili. Aidha, mipango ya kina ya usimamizi wa misitu ya asili yenye eneo la hekta 181,669 ya uzalishaji na uhifadhi iliandaliwa, Aidha Wakala uliendelea kutoa kipaumbele kwa misitu asilia 11 yenye bioanuwai nyingi na viumbe ndwele na adimu yaani: Amani, Kilombero, Nilo, Uluguru, Magamba, Uzungwa, Mkingu, Chome, Mt. Rungwe, Rondo na Minziro

    Mipango ya usimamizi wa Mashamba ya miti ya kupandwa yenye jumla ya eneo la hekta 150,000 ilitayarishwa kwa kipindi cha 2008/2009

    Mipango ya usimamizi wa Mashamba ya miti ya kupandwa yenye jumla ya eneo la ha 205,522 ilitayarishwa kwa kipindi cha 2012/2013 (likiwa ni ongezeko la ha. 55,522).

    Idara ilikuwa haina takwimu za rasilimali za misitu zinazotoa taarifa sahihi na za uhakika kuhusu hali halisi, ukubwa, na matumizi ya rasilimali za misitu ambazo zingesaidia katika kuandaa sera na programu za kutekeleza usimamizi endelevu wa misitu

    Uendelezaji wa mashamba ya miti ulikuwa hekta 6,376 (2005/06 – 2009/10)ambapo ni wastani wa hekta 1275.2 kwa mwaka

    Wakala umefanya Tathmini ya Rasilimali za Misitu (National Forest Resource Monitoring and Assessment (NAFORMA) inayotoa taarifa sahihi na za uhakika kuhusu hali halisi, ukubwa, na matumizi ya rasilimali ya misitu ambayo ni muhimu kwa ajili ya kutoa maamuzi na kuandaa sera na programu za kutekeleza usimamizi endelevu wa misitu.

    Uendelezaji wa mashamba ya miti umekuwa hekta 39,776 (2010/11 – 2014/15) ambapo upanuzi ni hekta 15,080.5 na upandaji wa kurudishia maeneo yaliyovunwa hekta 24,695.5. Upandaji huo ni sawa na wastani wa hekta 7,955 kwa mwaka.

  • 35

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Misitu mingi ya hifadhi haikufyekewa na kuhakikiwa mipaka hivyo ilivamiwa na kupoteza hadhi kutokana na migogoro ya uvamizi na kukosekana kwa mipaka

    Mipaka iliimarishwa na kupandishwa hadhi kwa asilimia 25 ya maeneo ya hifadhi. Takriban kilomita 9,975 za mipaka katika misitu ya asili ya hifadhi kwa ajili ya uzalishaji; Pamoja na urefu km 3,263 za mipaka ya misitu ya hifadhi asilia (Asilia/lindi maji) iliimarishwa.

    Idara ilikuwa na vituo 4 vyenye jumla ya manzuki 21

    Wakala umeendeleza vituo 4 na kuanzisha manzuki 57 na kutundika mizinga 8,054 katika misitu ya hifadhi na mashamba ya miti

    3 Vitendea Kazi/Mazingira ya Kazi

    Idara ilikuwa na vitendea kazi/majengo na miundo mbinu chakavu iliyohitaji ukarabati katika ngazi mbalimbali (ukarabati mkubwa/ukarabati mdogo)

    Wakala umefanya maboresho ya makazi ya watumishi pamoja na miundo mbinu; kama kujenga ofi si 1 na nyumba za wakuu wa safu 12, na kukarabati nyumba 5 kwa kutumia fedha za UNDP na Serikali ya Ujerumani. Vilevile Wakala umefanya Ujenzi wa majengo 7 katika mashamba ya miti Mtibwa (2), Rubare (1), Wino-Ifi nga (1), Ukaguru (2), Rondo (1). Ukarabati wa nyumba za watumishi 287 na majengo ya ofi si, pia Nyumba 2 za nyuki zilijengwa katika Mradi wa ufugaji nyuki-Kibondo. Wakala umeweza kujenga barabara mpya za msituni zenye urefu wa kilimita 161, na kukarabati kilomita 7,672 , Madaraja 53, mnara (1) wa kufanyia doria za moto.

    4 Wafanyakazi Idara ilikuwa na Wafanyakazi wachache, wengi wao wakiwa wanatimiza muda wa kustaafu; na mafunzo hayakujumuisha watumishi wengi.

    Wakala umeajiri na kupanga watumishi wa kada mbalimbali katika Kanda na baadhi ya wilaya ambazo zina rasilimali kubwa za misitu na nyuki. Wakala unazingatia sifa, jinsi na uhitaji. Aidha, Wakala umetoa mafunzo kwa idadi kubwa ya watumishi wake ili kuboresha utendaji wao na kutoa motisha kadri inavyowezekana.

    5 Mipango (SP/BP)

    Idara ilitekeleza Mipango Mkakati kama sehemu ya Mpango Mkakati wa Wizara. Aidha, Idara haikuwa na Mipango ya Kibiashara.

    Wakala umeanda Mipango Mkakati wa kwanza na wa pili, na unaandaa na kutekeleza Mipango ya Kibiashara ya kila mwaka

    6 Bajeti na Matumizi

    Idara ilikuwa na bajeti ya TAS bilioni 24.8. Bajeti ya matumizi ya kawaida (OC) pamoja na taasisi zake ilikuwa na wastani wa TAS 11.5 bilioni kwa kipindi cha mwaka 2007/8-2010/11 na bajeti ya matumizi ya maendeleo ilikuwa na wastani wa TAS 13.3 bilioni) kwa kipindi cha 2007/08-2010/11

    Bajeti ya Wakala ilikuwa ni wastani wa TAS 119.2 bilioni na matumizi ya TAS 100.3 bilioni kwa kipindi cha mwaka 2011/12 – 2013/14

  • 36

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    7 Uwekezaji endelevu

    Idara haikuwa na njozi/ndoto ya uwekezaji na mikakati thabiti ya uendelevu kulingana na mazingira ya kibiashara ambayo hayakuwepo wakati wa Idara

    Vitega uchumiWakala umeweka njozi ya kuendeleza ofi si zake zilizo katika miji mashuhuri na majiji ili kugeuza kuwa majengo ya kisasa ya uwekezaji. Ofi si hizo za Wakala ni zile zilizopo katika majiji ya Mbeya, Tanga na miji ya Morogoro na Moshi. Mkakati uliopo ni kujenga majengo ya kisasa yenye hadhi na kukodisha sehemu za majengo hayo kwa wawekezaji wa kibiashara. Sera ya Uwekezaji : Wakala upo katika mchakato wa kuandaa sera ya uwekezaji (investment policy) ili kuwa na uwekezaji wa aina mbalimbali

    Makao Makuu Mapya ya Wakala: Wakala upo katika mchakato wa kujenga ofi si mpya ya kisasa itakayokuwa na vitega uchumi. Vilevile Wakala upo katika mchakato wa kuomba kuwa Mamlaka (Authority)

    8 Utegemezi Idara ilikuwa inapata ruzuku Kutoka Serikalini kulipia matumizi ya Kawaida pamoja na mishahara. Aidha bajeti za maendeleo zilitolewa na Wahisani kwa takribani asilimia 100.

    Wakala unapata Malipo ya Mishahara ya Wafanyakazi wake kutoka Serikalini (Vote 69); Hata hivyo mishahara hiyo inatokana na fungu la mchango kutoka katika makusanyo ya Wakala kwenda Hazina. Hivyo Wakala unajitegemea kwa asilimia 100 ya matumizi yake ya kawaida

    9 Mchango wa Wakala kwa Serikali

    Serikali ilikuwa inatoa ruzuku kulipia matumizi ya Kawaida pamoja na mishahara

    Wakala ulichangia TAS 108.7 bilioni kwenda serikalini katika kipindi cha miaka mitatu (2011/12 - 2013/14) kwa mgawanyo ufuatao:

    Hazini (81.5 bilion); VAT (15.7 bilion), TaFF (9.2 bilion) & CESS (2.2 bilion).

    6. RASILIMALI FEDHA

    6.1 Mapato kabla ya kuanzishwa Wakala

    Idara ya Misitu na Nyuki ilikuwa inapata mapato kutokana na vyanzo vifuatavyo;

    a) Makusanyo ya maduhuli kutokana na rasilimali za misitu na nyuki (mashamba ya miti na misitu ya asili)

    b) Fedha kutoka serikalini kwa ajili ya kulipa mishahara

    c) Fedha za miradi kutoka kwa Washiriki katika maendeleo

    d) Mikopo na Misaada.

  • 37

    WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU WA TANZANIA

    Idara ya Misitu na Nyuki ilikuwa na madaraka kupitia sheria ya Misitu Na. 14 ya 2002 ya kukusanya ada na mrahaba wa mazao na huduma za misitu kutoka misitu ya hifadhi ya taifa na misitu iliyopo kwenye ardhi ya jumla (Kifungu II na Kifungu X cha sheria ya misitu ya 2002). Ingawaje, ada na mrahaba kutoka misitu ya hifadhi ya serikali za mitaa na misitu ya vijiji inakusanywa na serikali za mitaa na serikali za vijiji. Aidha, serikali za mitaa zina madaraka kupitia sheria ya fedha ya mwaka 1982 kukusanya ushuru wa asilimia 5 ya mapato (CESS) yanayotokana na mazao ya misitu yanayovunwa ndani ya wilaya husika.

    Ada na mrahaba hulipwa wakati mazao kama magogo, nguzo, fi to, kuni, mkaa, mbegu, miche nk. vinapovunwa kutoka katika misitu (iliyohifadhiwa na ya ardhi ya jumla) kwa leseni kwa mujibu wa (Kifungu VI cha sheria ya misitu 2002). Maduhuli yanayokusanywa kutoka misitu ya hifadhi ya taifa na misitu kwenye ardhi ya jumla yanapelekwa Wizara ya Maliasili na Utalii na hatimaye kupelekwa Wizara ya Fedha (Hazina) kwa ajili ya matumizi ya kitaifa. Wizara ya Maliasili na Utalii ilikuwa ni mojawapo ya Wizara zilizokuwa katika Retention Scheme na hivyo ilikuwa inarudishiwa asilimia 70% ya mapato yote kwa ajili ya matumizi ya Wizara.

    i) Tathmini kwa ujumla inaonesha kuwa maduhuli yaliyokusanywa na Idara ya Misitu na Nyuki yaliongezeka kutoka TAS 4.5 bilioni katika mwaka 2003/04 hadi TAS 21.8 bilioni katika mwaka 2007/08 (ikiwa ni kiwango cha juu kilichokusanywa).

    ii) Wastani wa makusanyo kwa mwaka ulikuwa ni takribani ya TAS 17.5 bilioni ambayo ni asilimia 43 ya makusanyo tarajiwa ambayo yangekusanywa. Makusanyo makubwa yalitokana na mr