bonde la pangani · 2013. 9. 12. · d.2 usimamizi wa serikali, sheria na sera ... jedwali la 3:...

98
Coast Development Authority Bonde la Pangani: Uchambuzi wa Hali Halisi (Toleo la pili)

Upload: others

Post on 25-Oct-2020

0 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

Page 1: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Coast Development Authority

Bonde la Pangani:Uchambuzi wa Hali Halisi (Toleo la pili)

Page 2: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Bonde la Pangani:Uchambuzi wa Hali Halisi (Toleo la pili)

Programu ya IUCN Afrika Mashariki na Kusini

2009

i

Page 3: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Mchapishaji:

Hatimiliki: © 2009 Shirika la Kimataifa la Uhifadhi ya Uasili na Maliasili.

Kitabu hiki kinaweza kutolewa chote au sehemu yake kwa njia yoyote kwa matumizi ya maendeleo ya elimu au matumizi mengine yasiyo ya biashara bila ya kuomba kibali kutoka kwa mmiliki, ilimradi rejeo litajwe. IUCN ingependelea kupata nakala ya makala yoyote ambayo itatumia kitabu hiki kama rejea.

Hairuhusiwi kuuza kitabu hiki, au kukitumia kwa madhumuni mengine ya kibiashara bila ya idhini ya maandishi ya IUCN.

Jina kamili: Programu ya IUCN Afrika ya Mashariki, 2009. Uchambuzi wa Hali Halisi Bonde la Mto Pangani. Toleo la pili, xii + uk.83.

ISBN: 978-2-8317-1191-1

Usanifu na Mpangilio: Gordon O. Arara

Mpiga chapa: Kulgraphics Ltd.

Picha ya 1: Kilele cha Mlima Kilimanjaro; Picha ya 2: Sehemu ya msitu wa Shiri Njoro; Picha ya 3: Banio la kudhibiti maji yanayoingia katika mfereji wa umwagiliaji; Picha ya 4: Watoto wakiogelea kwenye hodhi ya maji ya umwagiliaji; Picha ya 5: Shamba la mkonge; Picha ya 6: Mradi wa umwagiliaji wa mpunga ; Picha ya 7: Kituo cha kupimia usawa wa maji- Chemchemi ya Chemka; Picha ya 8: Banio la mfereji wa umwagiliaji lililoharibiwa; Picha ya 9: Ukuta wa Bwawa la Nyumba ya Mungu (mabadiliko ya rangi yanaonesha upunguaji wa kina cha maji); Picha ya 10: Mchuuzi akiuza maji kutoka kwenye kisima.

Picha namba 1, 3, 5, 6, 8, 9 hatimiliki ya 2003 ya Kelly West; Picha namba 2 na 7 hatimiliki ya 2002 ya Kim Geheb; Picha namba 4 na 10 hatimiliki ya 2003 ya Ger Bergkamp.

Kitabu hiki kinapatikana: Kitengo cha Huduma za Uchapishaji cha IUCN-ESARO, S.L.P. 68200–00200, Nairobi, Kenya; Simu ++254 20 890605-12 Faksi ++254 20 890615; Barua pepe; [email protected]

Uteuzi wa Maumbo ya kijiografia na nyenzo zilizotumika kuwasilisha ujumbe katika kitabu hiki, hayawakilishi kwa namna yoyote ile maoni ya asasi zinazoshiriki kuhusiana na sheria ya nchi yoyote, au eneo lake, au mamlaka zake, au kuhusu makazi na uwekaji wa mipaka yake.

Maoni yaliyotolewa na waandishi katika kitabu hiki sio lazima kwamba yanawakilisha maoni ya PBWO, CDA, WANI au IUCN.

1

2 3 4

5

6

7 89 10

ii

Page 4: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Yaliyomo

Tafsiri ya vifupisho ............................................................................................................................vDibaji ................................................................................................................................................viiMuhtasari .......................................................................................................................................viii

A Utangulizi wa Uchambuzi wa Hali Halisi wa Bonde la Mto Pangani ...................................1 A.1 Maelezo ya jumla ya Bonde la Mto Pangani ...................................................................1A.2 Usimamizi wa Pamoja wa Mabonde ya Mito (wa) ............................................................5 A.3 Programu ya Hifadhi ya Maji na Uasili (WANI) .................................................................6 A.4 Uchambuzi wa Hali Halisi: madhumuni na matokeo ........................................................7 A.5 Vyanzo vya data ..............................................................................................................7 A.6 Muundo wa Uchambuzi wa Hali Halisi .............................................................................8

B Rasilimali za asili zilizopo katika Bonde la Mto Pangani .....................................................9B.1 Utangulizi .............................................................................................................................9B.2 Misitu iliyopo katika Bonde ..................................................................................................9B.3 Maji na ardhioevu ..............................................................................................................15B.4 Maeneo yaliyohifadhiwa ....................................................................................................19B.5 Bayoanuwai na Hifadhi ......................................................................................................20B.6 Uvuvi .................................................................................................................................22B.7 Udongo ..............................................................................................................................23B.8 Majumuisho ya hoja...........................................................................................................23

C Uchumi wa kijamii katika Bonde la Mto Pangani ................................................................25C.1 Maelezo ya jumla ..............................................................................................................25C.2 Shughuli za Viwanda .........................................................................................................27C.3 Shughuli za Kilimo .............................................................................................................27C.4 Shughuli za Wafugaji .........................................................................................................31C.5 Shughuli za Mijini ..............................................................................................................32C.6 Shughuli za Asasi Zisizo za Kiserikali na Mashirika ya Kimataifa ....................................32C.7 Migogoro ...........................................................................................................................40C.8 Majumuisho ya hoja .........................................................................................................46

D Usimamizi wa Maliasili katika Bonde la Mto Pangani .......................................................47D.1 Utangulizi ........................................................................................................................47D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera............................................................................ 47D.3 Usimamizi katika ngazi ya jamii ........................................................................................52D.4 Usimamizi wa bonde kimataifa .........................................................................................55D.5 Ukusanyaji na ufuatiliaji wa data ......................................................................................55D.6 Majumuisho ya hoja..........................................................................................................57

E Matatizo na masuala mbalimbali katika Bonde la Mto Pangani......................................58E.1 Utangulizi ..........................................................................................................................58E.2 Masuala na matatizo ya Bonde la Mto Pangani ................................................................58E.3 Maeneo ya kipaumbele kwa Utendaji ...............................................................................62

F Hitimisho ................................................................................................................................64F.1 Majumuisho ya Matokeo ...................................................................................................64

G Rejea ....................................................................................................................................68

H Kiambatanisho cha 1: Mabonde madogo yaliyojumuishwa kiutawala katika Bonde la Pangani ..................................................................................................... 75H.1 Utangulizi .........................................................................................................................75

iii

Page 5: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

H.2 Bonde la Mto Umba .........................................................................................................75H.3 Bonde la Mto Msangazi....................................................................................................77H.4 Bonde la Mto Zigi .............................................................................................................78H.5 Bonde la Mto Mkulumuzi ..................................................................................................82

Orodha ya MajedwaliJedwali la 1: Aina, matumizi na hadhi ya kisheria ya misitu ya Tanzania ...........................................9Jedwali la 2: Upotevu wa utando wa msitu wa Milima ya Tao la Mashariki katika

Bonde la Mto Pangani .................................................................................................13Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya

mahitaji ya maji mwaka 2015 ......................................................................................18Jedwali la 4: Misingi ya Uchumi wa kijamii wa Tanzania na Kenya mwaka 2001 ............................26Jedwali la 5 Idadi ya Mifugo katika baadhi ya maeneo ya Bonde la Mto Pangani (2002) ............ 31Jedwali la 6: Hati za kutumia maji katika Bonde la Mto Pangani (Tanzania), Mei, 2003 ..................50Jedwali la 7: Eneo la misitu chini ya Usimamizi wa Misitu wa Pamoja kwa mikoa ..........................54

Orodha ya Michoro Mchoro Na.1: Bonde la mto Pangani lilivyoenea Tanzania na Kenya .................................................2 Mchoro Na 2: Bonde la Mto Pangani ..................................................................................................3Mchoro Na 3: Utawala wa Misitu Tanzania .......................................................................................51Mchoro Na 4: Ramani ya Bonde la Pangani- Utawala .....................................................................83

Orodha ya PichaPicha ya 1: Ramani ya Bonde la Mto Pangani .................................................................................33Picha ya 2: Ramani ya Bonde la Pangani kiutawala ........................................................................34Picha ya 3: Kilele maarufu chenye barafu cha Mlima Kilimanjaro mwaka 1993 na 2000 ................................................................................................................35Picha ya 4: Mto Karanga - Moshi ......................................................................................................36Picha ya 5: Mlima Kilimanjaro ..........................................................................................................36Picha ya 6: Mfereji wa umwagiliaji Wilayani Moshi ...........................................................................37Picha ya 7: Chemchemi iliyofunikwa ya Shiri-Njoro ..........................................................................38Picha ya 8: Miteremko kwenye misitu ya Mlima Meru ......................................................................38

Orodha ya VisandukuKisanduku cha 1: Usimamizi wa Mahitaji ya maji ................................................................................6Kisanduku cha 2: Taarifa za msingi za misitu ya Bonde la Mto Pangani ...........................................10Kisanduku cha 3: Milima ya Taita ......................................................................................................11Kisanduku cha 4: Tishio kwa misitu ya Bonde la Mto Pangani..........................................................14Kisanduku cha 5: Taarifa za msingi za maji na ardhioevu katika Bonde la Mto Pangani .............15Kisanduku cha 6: Tishio kwa rasilimali za maji na ardhioevu ya Bonde la Mto Pangani ..................16Kisanduku cha 7: Tishio kwa maeneo yaliyohifadhiwa ya Bonde la Mto Pangani ............................20Kisanduku cha 8: Maeneo muhimu sana kwa bayoanuwai ..............................................................21Kisanduku cha 9: Kundi la kwanza la spishi ya ndege wa Milima ya Usambara

walio hatarini ........................................................................................................22Kisanduku cha 10: Kasoro za usanifu wa miundombinu ya mifereji ya asili .....................................28Kisanduku cha 11: Magadi na chumvichumvi ....................................................................................30Kisanduku cha 12: Utawala wa Maji nchini Kenya ............................................................................51Kisanduku cha 13: Uanzishwaji wa usimamizi wa kijamii katika msitu wa Duru-Haitemba,

Mkoani Manyara ............................................................................................53Kisanduku cha 14: Mfano wa Chama Cha Watumia Maji .................................................................56

iv

Page 6: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Tafsiri ya VifupishoANR ...................... Hifadhi ya Asili ya AmaniASL ....................... Juu ya Usawa wa BahariAUWSA................. Mamlaka ya Maji safi na na Maji taka ArushaBWB ..................... Bodi ya Maji ya BondeBWO ..................... Afisa wa Maji wa BondeCBNRM ................ Usimamizi wa Maliasili KijamiiCCM ..................... Chama Cha MapinduziCDA ...................... Mamlaka ya Maendeleo Pwani (Kenya)CFR ...................... Hifadhi ya Misitu ya JamiiCFP ...................... Mradi wa Misitu Eneo la Chanzo cha MtoCPRs .................... Rasilimali za JamiiDFO ...................... Afisa Misitu wa WilayaDGIS ..................... Wizara ya Mambo ya Nje ya UholanziEACBP ................. Mradi wa Bayoanuwai za kimataifa za Afrika MasharikiEU......................... Umoja wa Nchi za UlayaEU-ACP ................ Umoja wa Ulaya – Afrika, Caribbean na PasifikiFAO ...................... Shirika la Kilimo na Chakula la Umoja wa MataifaFBD ...................... Idara ya Misitu na NyukiGEF ...................... Mfuko wa huduma ya Mazingira DunianiGIS ....................... Mifumo ya Habari wa KijiografiaGOK...................... Serikali ya KenyaHa ......................... HektaIRBM ..................... Usimamizi wa Pamoja wa Mabonde ya MitoIDA ........................ Chama cha Maendeleo cha KimataifaIUCN ..................... Shirika la Kimataifa la Hifadhi ya Uasili JFM ....................... Usimamizi wa Pamoja wa MisituKWH ..................... Kilowati kwa saaLGA....................... Serikali za MitaaLMIS ..................... Skimu ya Umwagiliaji ya “Lower Moshi”MAFS .................... Wizara ya Kilimo na ChakulaMCM ..................... Mita za ujazo Milioni MGR ..................... Hifadhi ya Wanyamapori ya MkomaziMMP ..................... Mradi wa Usimamizi wa MikokoMoU ...................... Mkataba wa MakubalianoMoWLD ................. Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo MTESM ................. Mkakati wa Taifa Kuendeleza Sekta ya MajiMW ....................... MegawatiNAWAPO .............. Sera ya maji ya Taifan.d......................... Hakuna TareheNEMC ................... Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira

v

Page 7: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

NGO ..................... Shirika Lisilo la KiserikaliNPF ...................... Mradi Mpya wa Maporomoko ya Mto PanganiNORAD ................. Shirika la Kimataifa la Misaada la NorwayNRM ..................... Usimamizi wa MaliasiliNWP ..................... Sera ya MajiNyM ...................... Bwawa la Nyumba ya MunguPA ......................... Maeneo Yaliyohifadhiwa PBWB ................... Bodi ya Maji ya Bonde la PanganiPBWO ................... Ofisi ya Maji ya Bonde la PanganiPRB ...................... Bonde la Mto PanganiPRBMP ................. Mradi wa Usimamizi wa Bonde la Mto PanganiRBM ...................... Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya MajiRBMSIIP ............... Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Maji na Uboreshaji wa Kilimo cha

Umwagiliaji cha Wakulima Wadogo wadogoRCE ...................... Kituo cha Kanda cha viumbe vipatikanavyo kipekeeRHO ...................... Afisa Haidrolojia wa MkoaRNRO ................... Afisa Maliasili wa MkoaSA ......................... Uchambuzi wa Hali Halisi SNV ...................... Shirika la Maendeleo la UholanziTANAPA ................ Mamlaka ya Hifadhi za TaifaTANESCO ............ Shirika la Ugavi wa Umeme TanzaniaTCMP ................... Ubia wa Usimamizi wa Pwani TanzaniaICZCDP ................ Programu ya Hifadhi na Maendeleo ya Ukanda wa Pwani TangaTFAP ..................... Mpango wa Utekelezaji wa Misitu TanzaniaTFCG .................... Kikundi cha Hifadhi ya Misitu TanzaniaTIP ........................ Shirika la Umwagiliaji Kiasili na Maendeleo ya MazingiraTPC ...................... Kampuni ya Kiwanda cha Sukari Moshi (Tanzania)UNICEF ................ Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Dharura kwa WatotoUNDP ................... Shirika la Maendeleo la Umoja wa MataifaUSAID................... Wakala wa Marekani kwa Maendeleo ya KimataifaVNRC ................... Kamati ya Maliasili za KijijiVWN ..................... Dira ya Maji na UasiliWANI .................... Programu ya Hifadhi ya Maji na Uasili ya IUCNWDM ..................... Usimamizi wa Mahitaji ya MajiWHO ..................... Shirika la Afya la Umoja wa MataifaWRMA .................. Mamlaka ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji (Kenya)WRM Act ............... Sheria ya Usimamizi wa Rasilimalui za Maji ya mwaka 2009WUA ..................... Chama Cha Watumiaji Maji

vi

Page 8: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Dibaji

Madhumuni ya toleo la kwanza la Uchambuzi ya Hali ya Bonde la Mto Pangani yalikuwa kuainisha rasilimali za asili zilizomo katika Bonde hilo, matukio yanayoziathiri na kutambua maeneo ya kufanyia kazi. Madhumuni mengine yalikuwa kutambua mashirika, asasi na wadau wengine ambao IUCN ingeweza kushirikiana nao.

Lengo la WANI ni kuhakikisha kwamba suala zima la ikolojia linazingatiwa katika sera, mipango, na usimamizi wa mabonde ya mito. Katika maeneo ya mabonde ya kufanyia maonyesho yaliyoteuliwa duniani, WANI imepania: kuonyesha namna ya kusimamia mfumo ikolojia, kuwawezesha wananchi kushiriki katika usimamizi endelevu wa rasilimali za maji, kuendeleza usimamizi bora wa vyanzo vya maji na ardhioevu, kuanzisha na kutumia nyenzo za kiuchumi na vivutio, kuongeza maarifa ya kusaidia kufikia maamuzi na kutoa mafunzo yatakayoleta mwamko wa matumizi bora ya maji.

Kufuatia mashauriano na wadau katika Bonde na kwa kuzingatia maazimio ya warsha iliyoendeshwa na Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani (PBWO) kwa ushirikiano na IUCN - Shirika la Kimataifa la Kuhifadhi Uasili iliyofanyika Moshi, Tanzania, kuanzia tarehe 8 hadi 10 Mei, 2002, Bonde la Mto Pangani nchini Tanzania na Kenya lilichaguliwa kuwa eneo la maonyesho la WANI.

Ikiwa ni sehemu ya shughuli zake za mradi wa maendeleo katika Bonde la Mto Pangani, IUCN ilimwajiri Mshauri Mtaalamu Dk. Kim Geheb, kufanya Uchambuzi wa Hali halisi ya bonde hili. Kazi za ugani kwa ajili ya uchambuzi wa hali halisi zilifanyika mwezi Novemba, mwaka 2002, na ilihusisha mahojiano na wadau mbalimbali katika bonde. Vyanzo vya ziada vya taarifa vilikuwa ni marejeo ya machapisho pamoja na mjadala wa warsha iliyotajwa hapo juu, iliyojulikana kwa jina la “Bonde la Mto Pangani: Usimamizi Shirikishi”

Madhumuni ya Uchambuzi wa Hali halisi ni kama yafuatayo:-• Kuainisha rasilimali mbalimbali zilizomo katika Bonde la Mto Pangani , na kufahamu michakato na

matukio yanayoziathiri.• Kutambua kwa mapana maeneo ya kiutendaji ambayo yanaweza kushughulikiwa kwa manufaa ya

kimaendeleo.• Kutambua taasisi na asasi mbalimbali zilizopo, na zenye nia ya kujishughulisha na rasilimali za

maji, ambazo IUCN inaweza kuingia nazo ubia kwa lengo la kuendeleza juhudi za WANI katika Bonde la Mto Pangani.

Kitabu hiki “Uchambuzi wa Hali Halisi ya Bonde la Mto Pangani“ awali kilitafsiriwa na Ofisi ya Maji Bonde la Pangani. Bw. Ipyana E. Mwakalinga alikamilisha kwa kuboresha baadhi ya sehemu na kuhariri toleo hili la pili kwa lugha ya Kiswahili.

Rasimu ya kwanza ya Uchambuzi wa Hali Halisi katika Bonde la Mto Pangani ilikamilika mwishoni mwa mwaka 2002 na kusambazwa kwa wadau kwa ajili ya mapitio na maoni. Katika warsha iliyoandaliwa na PBWO na IUCN mjini Moshi mwezi Machi 2003, wadau walitoa maoni na kupendekeza marekebisho kadhaa. Maoni na mapendekezo ya ziada yalipokelewa kutoka PBWO na Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani (CDA - Kenya) kwenye mkutano wa IUCN, PBWO na CDA uliofanyika Nairobi mwezi Mei, mwaka 2003. Mwaka 2009 uchapishaji upya wa Uchambuzi ya Hali ya Bonde ulihitajika na ikaamuliwa kutumia nafasi hii kufanyia mapitio ya taarifa chache ikizingatiwa kuwa sheria mpya ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji iliyopitishwa July 2009 na inafanya kazi. Ieleweke kuwa taaarifa zilizofanyiwa mapitio ni zile tu zinazohusu miuondo ya utawala, mifumo ya kitaasisi, sheria na sera za maji, vilevile taarifa mpya kuhusu mafanikio ya utekelezaji wa Mradi wa Usimamizi wa Bonde la Pangani zimeongezewa, lakini maeneo mengine yote ya uchambuzi yameachwa kama yalivyo. Kazi hii yakufanyia mapitio Uchambuzi ya Hali ya Bonde la Pangani imegharamiwa na Global Water initiative (mpango wa maji wa dunia) unaofadhiliwa na mfuko wa Howard G. Buffett (Howard G. Buffett Foundation).

Felix Peter, Helen Lema, Fatuma Omar na Renalda Mukaja kutoka Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Rasilimali za Maji uliopo chini ya Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo ya Tanzania walijitolea kutayarisha na kufanya makadirio ya maeneo katika ramani zilizopo katika kitabu hiki.

vii

Page 9: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Muhtasari

Bonde la Mto Pangani lina eneo la takriban kilomita za mraba 43,650, sehemu kubwa ikiwa nchini Tanzania na karibu asilimia 5 iko katika Jamhuri ya Kenya. Nchini Tanzania, bonde hili limeenea katika mikoa minne: Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Tanga. Katika Jamhuri ya Kenya eneo la bonde liko katika Wilaya ya Taita-Taveta. Mto Pangani unaundwa na matawi makubwa mawili , Mto Kikuletwa na Ruvu ambayo huunganika katika bwawa la Nyumba ya Mungu lenye eneo la kilomita za mraba 140. Mto unapotoka katika bwawa hili unajulikana kwa jina la Mto Pangani, ambao hutiririka kwa umbali wa kilomita 432 kabla ya kuingia Bahari ya Hindi.

Bonde hili lina rasilimali nyingi. Bila shaka maji na ardhi inayofaa kwa kilimo ndizo rasilimali muhimu zaidi kwa wakazi wapatao milioni 3.7 wa bonde hili waishio upande wa Tanzania. Nyanda za juu za bonde hupata mvua nyingi zaidi ukilinganisha na uwanda wa chini. Hata hivyo kutokana na msongamano na ushindani wa kupata ardhi ulioko katika nyanda za juu, wakulima wamelazimika kuanza kumwagilia maji mashamba yao ili kuinua uzalishaji. Wale walioshindwa kupata ardhi katika nyanda za juu wamelazimika kutafuta maeneo katika uwanda wa chini wenye mvua haba, ambako kilimo cha umwagiliaji ni wa muhimu sana. Ugumu wa hali unazidishwa zaidi na mwenendo wa upungufu wa mvua katika bonde.

Ushindani wa kupata ardhi umesababisha rasilimali nyingine katika bonde kama vile misitu, kuingia katika ushindani wa moja kwa moja na kilimo. Sehemu ya misitu inalindwa kutokana na hadhi yake ya hifadhi, kama vile Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA) ambayo ipo chini ya Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA). Misitu mingine inalindwa na idara za misitu za Kenya na Tanzania. Kutokana na sababu mbalimbali, zikiwemo uhaba wa wafanyakazi na ukosefu wa fedha, misitu hii haifaidi viwango sawa vya hifadhi ikilinganishwa na ile iliyopo chini ya TANAPA. Kuwepo shinikizo kwenye misitu ya pwani na Milima ya Tao la Mashariki katika bonde la mto Pangani kunatia wasiwasi mkubwa sana, hasa ikizingatiwa kuwa maeneo hayo yana kiwango cha juu cha mimea na viumbe adimu ndani yake.

Rasilimali nyingine katika bonde ni madini, ambayo ni pamoja na tanzanite, bati na vito. Nyingine ni uvuvi, maeneo ardhioevu na vivutio vingi vya utalii.

Rasilimali hizi hutumika kwa namna mbali mbali. Uchambuzi huu wa hali halisi unaweka matumizi hayo katika makundi yafuatayo:

• Shughuli za viwanda, ambazo ni pamoja na mchango mkubwa wa nishati ya umeme wa nguvu ya maji katika gridi ya taifa, uchimbaji wa madini na viwanda vya kilimo kama vile kiwanda cha sukari na vya usindikaji wa katani.

• Shughuli za kilimo: Kwa sehemu kubwa kilimo katika bonde hili ni cha asili na hutegemea umwagiliaji. Mifereji ya umwagiliaji ina ufanisi mdogo sana, inaweza kupoteza kiasi cha asilimia 85 ya maji kati ya mahali yanapochukuliwa hadi yanapopelekwa. Kadhalika kuna kilimo cha umwagiliaji cha viwango vikubwa katika bonde, yakiwemo mashamba ya miwa, mkonge na maua. Kadiri ya hekta kati ya 29,000 na 40,000 humwagiliwa katika bonde la Pangani upande wa Tanzania. Kiasi cha maji kinachotumiwa kinakadiriwa kuwa kati ya mita za ujazo milioni 400 na 480 kwa mwaka.

• Shughuli za ufugaji: Idadi kamili ya mifugo iliyopo katika bonde kwa sasa haifahamiki. Inadhaniwa kuwa, ifikapo mwaka 2015, ufugaji utatumia mita za ujazo 36,400 za maji kwa siku.

• Shughuli za mijini: Bonde lina miji miwili mikubwa, yaani Arusha na Moshi. Kadri miji hii inavyokua, mahitaji ya maji yameongezeka katika nyanja mbili: kwa matumizi ya viwandani na nyumbani, na kama njia ya kuondolea maji taka. Inatarajiwa kuwa, ifikapo mwaka 2015, mahitaji ya maji mijini katika bonde yatafikia mita za ujazo 163,600 kwa siku.

viii

Page 10: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Kutokana na hali hiyo kuna asasi na mashirika mbalimbali katika bonde, ambayo yanaweza kutumia madaraka ya viwango tofauti katika kumiliki rasilimali zilizoko katika bonde. Tofauti hii ya viwango vya madaraka ni msingi wa migogoro mingi ya matumizi ya rasilimali hizo. Uchambuzi huu wa hali halisi unainisha migogoro hiyo kama ifuatavyo:

• Migogoro itokanayo na viwango: Uhusiano kati ya watumiaji wa maji wa ukubwa na uwezo tofauti katika bonde la Mto Pangani mara nyingi huelezewa katika hali mbili kinzani. Hivyo mashamba makubwa yatumiayo mamia ya lita za maji kwa sekunde na kutumia mifumo ya umwagiliaji maji yenye ufanisi wa hali ya juu, hutofautiana sana na watumiaji wadogo ambao hutumia maji kidogo na mifumo duni ya umwagiliaji yenye ufanisi mdogo. Tofauti hizi kubwa za matumizi ndiyo vyanzo halisi vya migogoro. Uchambuzi huu wa hali halisi unatoa mifano ya migogoro ya aina hii kuwa ni maslahi kati ya watumiaji wa mijini na vijijini; na kati ya wachimbaji madini wa viwango vikubwa na vidogo.

• Migogoro itokanayo na umiliki: Kitabu hiki kinafafanua umiliki kama haki ya kusimamia rasilimali. Nchini Tanzania, Usimamizi wa Maliasili Kijamii (CBNRM) umeonekana kama njia ya kuvutia ya kuongeza ufanisi wa Usimamizi wa Maliasili za Taifa (NRM). Mwenendo huu haufuatwi sana nchini Kenya. Ukinzani katika mifumo hii unahusiana na matumizi na usanifu wake. Hapa, jamii zinaweza zisishirikishwe katika kubuni mkakati wa usimamizi, utekelezaji wake au hata mifumo yake ya kisheria. Hali hii inaweza kudhihirisha kuwa taasisi hizi hazitimizi wajibu wa usimamizi ulioundwa ili ziufanyie kazi. Mifano ni migogoro ya usimamizi wa misitu kati ya ngazi ya jamii na serikali; baina ya watumiaji rasilimali wa aina mbalimbali; na migogoro kuhusu nyanja mbali mbali za usimamizi.

• Migogoro itokanayo na mahali: Watumiaji walioko maeneo ya juu ya mito wana nafasi nzuri ya kutumia maji kuliko walioko sehemu za chini. Kwa kiwango kikubwa matatizo haya yanaweza kuonekana kwenye mifereji ya umwagiliaji ambako watumiaji walio karibu na chanzo cha maji wanaweza kuotesha mazao yanayohitaji kiasi kikubwa cha maji (kama vile mpunga) na wale walioko mwishoni mwa mifereji wakilazimika kupanda mazao yanayohitaji maji kidogo. Matatizo makubwa yanayoikabili mitambo ya umeme wa maji iliyoko upande wa chini wa mito ni mfano mwingine. Mifano ya migogoro ya aina hii ni ile iliyopo kati ya watumiaji wa maji wa maeneo ya juu ya mto na wa maeneo ya chini ya mto, na migogoro kati ya wazalishaji wa umeme wa maji na wamwagiliaji wadogo wadogo.

Migogoro juu ya rasilimali ni moja ya ushahidi wa ushindani mkubwa uliopo baina ya watumiaji wa rasilimali zilizoko katika bonde. Athari ya ongezeko la watu, tofauti ya mgawanyo wa rasilimali na hali ya kuwa na ukomo husababisha mbinu za matumizi yake mara nyingi kuwa mbaya. Mifano ya uharibifu wa rasilimali ni kama ifuatayo:

• Misitu iliyopo katika bonde inakabiliwa na hatari ya ukataji hovyo wa miti, kuingiliwa ndani ya mipaka yake kwa mahitaji ya matumizi ya ardhi, uchomaji wa mkaa na ukusanyaji kuni. Inakisiwa kuwa karibu asilimia 77 ya misitu ya Milima ya Tao la Mashariki imepotea katika kipindi cha miaka 2,000 iliyopita kutokana na shughuli za binadamu, wakati kilomita za mraba 41 za misitu asilia ya Kilimanjaro zimetoweka kati ya mwaka 1952 na 1982.

• Ugawaji wa maji katika bonde unakabiliwa na tatizo la mahitaji makubwaambapo imedhihirika kuwa mahitaji ya rasilimali hiyo yanazidi upatikanaji wake. Sababu kuu ya ongezeko la mahitaji ni mifumo duni ya umwagiliaji kwa njia ya mifereji yenye ufanisi mdogo. Maeneo ya ardhioevu katika bonde yapo hatarini kutoweka kutokana na ujenzi wa mabwawa.

• Maeneo yaliyohifadhiwa ya bonde yanakabiliwa na ujangili, na matatizo mengine kama yale yanayoikabili rasilimali ya misitu.

• Sehemu kubwa ya viumbehai katika bonde inatokana na mazingira ya kipekee ya misitu iliyopo. Tishio la maisha ya viumbehai hutokea kutokana na hatari inayokabili mazingira.

ix

Page 11: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

• Uvuvi katika bonde la Mto Pangani unakabiliwa na shinikizo la uvuvi uliokithiri, na ukuaji wa magugumaji unaosababishwa na shehena kubwa ya virutubisho. Takriban tani 24 za udongo kwa hekta kutoka eneo la vyanzo vya mito huingia katika bwawa la Nyumba ya Mungu kila mwaka. Mwaka 1970, tani 28,509 za samaki zilivuliwa kutoka bwawa la Nyumba ya Mungu. Upatikanaji wa samaki umekuwa ukipungua kwa kiasi kikubwa tokea hapo, na katika mwaka 1983, tani 2,430 za samaki zilipatikana.

Kuna idadi kubwa ya mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali katika bonde hili yanayotaka kudhibiti uharibifu uliotajwa na kujaribu kuboresha maisha ya watumiaji wa rasilimali. Katika miaka ya karibuni, shughuli muhimu za kiwango kikubwa ni zile zilizogharamiwa na Benki ya Dunia kupitia Mradi wa Usimamizi wa Matumizi ya Rasilimali za Maji na Uboreshaji wa Kilimo cha Wamwagiliaji Wadogo Wadogo (RBMSIIP), na Mradi wa UNDP-GEF wa Viumbe anuwai wa Afrika Mashariki. Mradi wa kwanza ulikuwa maalum katika kuimarisha Ofisi ya Maji ya bBonde la Pangani (PBWO) na vilevile kuimarisha uwezo wa usimamizi wa matumizi ya maji katika bonde.

Juhudi za mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) katika bonde hili ni pamoja na kujihusisha na Usimamizi Shirikishi wa ukanda wa pwani ya Tanzania na misitu yake ya mikoko, na Kaskazini mwa bonde ni uboreshaji wa umwagiliaji wa kiasili, na uwezeshaji wa njia za mawasiliano baina ya watumiaji wa ngazi ya chini wa rasilimali na uongozi wa bonde. Juhudi za ziada zinatilia mkazo hifadhi ya rasilimali za misitu na wanyamapori katika bonde.

Mfumo wa Utawala wa bonde ni changamano. Nchini Tanzania, ni kawaida kutokea vyombo viwili kutawala rasilimali moja: Utawala unaotokana na serikali kuu na ule wa serikali za mitaa. Wakati huo huo, Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani (BMBP) imeanzishwa katika bonde kwa lengo la kusimamia rasilimali ya maji katika bonde zima. Hii maana yake ni kuwa, mara nyingi, mipaka ya mamlaka baina ya watawala wa rasilimali na wasimamizi inaweza kuwa haieleweki na/ au yenye utata. Aina hii ya utata inajirudia katika ngazi za chini. Kama ilivyoelezwa awali, Tanzania imegeukia kwa kiasi kikubwa kwenye Usimamizi wa Maliasili Kijamii (CBNRM) kama njia ya kuboresha usimamizi wa rasilimali zake za asili. Hata hivyo, hali hii inamanisha kuwa kamati au mashirika mengine ya ngazi ya jamiii yameundwa kushughulikia rasilimali maalum, na sio maliasili kwa ujumla. Hivyo, kuna Kamati za Maliasili za Vijiji (VNRCs), Vyama vya Watumiaji Maji (WUAs), Serikali za Vijiji n.k, hali inayozidisha utata katika usimamizi na kuongeza gharama za uendeshaji kwa kiasi kikubwa.

Nchini Kenya, hivi karibuni rasilimali za maji zimewekwa chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji (WRMA) inayotumia mabonde ya mito kama maeneo ya msingi ya usimamizi, na ambayo imekabidhiwa jukumu la kuratibu usimamizi shirikishi wa mabonde hayo na kuhusisha vikundi vya wadau katika muundo wa usimamizi. Huu ni utaratibu mpya kiasi, unaoweza kukabiliana na vikwazo kuhusiana na uhusishaji wa wadau katika muundo wa usimamizi, na ugumu wa kushirikisha sekta mbali mbali za utawala wa mabonde.

Njia hii ya usimamizi kisekta ipo pande zote za mpaka na inajionesha katika hali ambapo idara zinahusika na usimamizi wa misitu, maji, umwagiliaji, wanyamapori na rasilimali nyingine. Hali hii inaweza kusababisha malengo ya usimamizi na njia za kuyafikia kwenda sambamba, na hivyo kuleta utata katika uwezekano wa kuweka usimamizi shirikishi wa bonde. Hata hivyo PBWO imeamua kuhakikisha angalau idara mbalimbali zinakuwa na mawasiliano baina yao kwa kutuma wawakilishi katika Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani (PBWB). Hata hivyo Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani ina wawakilishi kutoka idara mbalimbali za serikali ili kuhakikisha kuwa angalau idara hizi zinawasiliana. Kwa mujibu wa sheria mpya ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji, bodi ina mamlaka ya kuandaa mipango ya usimamizi wa rasilimali za maji katika bonde, kwa kuwahamasisha na kuwahusisha wahusika wote, wakiwemo wasimamizi na watumia rasilimali za bonde.

Uchambuzi huu wa Hali Halisi unaeleza kwa ufupi ugumu wa hali na matatizo yaliyotajwa juu kwa kuainisha masuala mbalimbali ambayo yanahitaji umakini mkubwa katika usimamizi wake. Kimsingi, matatizo ya mazingira ni matatizo ya kijamii. Kwa urahisi na kwa ajili ya kuonesha hali ya mazingira ya bonde la Mto Pangani, matatizo haya yanagawanywa kati ya masuala ya mazingira na ya kijamii kama ifuatavyo:

x

Page 12: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Masuala ya mazingira:• Ukataji miti - husababisha matatizo katika uviaji wa maji ardhini, ongezeko la kasi ya mitiririko

ya maji na hivyo kusababisha mmomonyoko wa udongo, mafuriko na ongezeko la usafirishaji wa mchangatope.

• Mahitaji ya Ardhi – misitu mingi iko kwenye maeneo muhimu ya kilimo ambayo hupata kiasi kikubwa cha mvua. Jambo hili ni tishio kubwa kwa hifadhi ya misitu ya bonde hili.

• Shughuli za kilimo: mbinu mbalimbali za kilimo katika bonde hili zilianzishwa wakati idadi ya watu ilikuwa ndogo sana, na upatikanaji wa rasilimali ulikuwa ni wa kutosha. Kwa kuwa idadi ya watu imeongezeka mbinu hizo sasa zinaweza kutishia uhai wa mazingira ya bonde hili. Mifumo iliyopo haina ufanisi wa matumizi ya maji na umwagiliaji wa mfululizo unaweza kusababisha hali ya chumvi chumvi na/au magadi ardhini.

• Ongezeko la mifugo: suala hili halijulikani sana lakini linadhaniwa kuwa ni tatizo kubwa. Kutokana na kuongezeka kwa kilimo katika maeneo tambarare ya bonde, ardhi kwa ajili ya ufugaji imechukuliwa na wakulima, na hivyo kukuza zaidi ukubwa wa tatizo la wingi wa mifugo.

• Maendeleo: maendeleo yasiyosimamiwa katika bonde hili ni chanzo cha uchafuzi wa mazingira kutokana na njia zisizotosheleza za uondoaji taka.

• Ubora wa maji: ubora wa maji unaathiriwa na uchafuzi, lakini pia maji yanachafuliwa kutokana na hali ya kijiolojia inayosababisha ongezeko la madini ya floraidi majini.

• Uvuvi unaokithiri: shughuli za uvuvi katika bwawa la Nyumba ya Mungu zinaonekana kukithiri. Uvuvi pia unatishiwa na ukuaji wa magugumaji kwenye mito na maziwa unaosababishwa na ongezeko la virutubisho katika bonde.

• Uchimbaji madini: shughuli za uchimbaji madini zisizodhibitiwa katika bonde ni tishio kwa mandhari yake na manufaa ya ardhi katika siku zijazo. Aidha, hali hiyo ni tishio la uchafuzi wa mazingira. Uchimbaji wa mchanga mitoni hudhoofisha kingo za mito hiyo.

• Ukosefu wa mwamko wa mazingira baina ya wakazi wa bonde.

.

Masuala ya kijamii, kiuchumi na kisiasa• Umasikini: Kutokuwepo kwa shughuli za ngazi ya pili na ya tatu katika bonde ambazo ni ajira

katika sekta za biashara na viwanda, wakazi wake wengi hujitafutia maisha katika shughuli za msingi kama vile kilimo, uvunaji wa mazao ya misitu, uvuvi n.k.

• Migogoro: kwa vile watu wengi hujihusisha na shughuli za msingi, hali ya migogoro huibuka baina ya watumiaji wadogo, na kati ya watumiaji wadogo na wakubwa.

• Manufaa ya kisiasa: wanasiasa wenye shauku ya kupata kura kutoka kwenye majimbo yao ya uchaguzi, wakati mwingine huchochea matumizi yasiyo endelevu ya rasilimali.

Masuala ya usimamizi na utawala• Sera zisizotosheleza: sera zinazoonekana kuwa sahihi na zilizotungwa vizuri zinaweza zisifae

kwa sababu utekelezaji wake hauwezi kufuatiliwa, na wahalifu hawaadhibiwi.• Matatizo ya kifedha: Haya hujitokeza karibu katika kila sehemu ya utawala wa bonde, kuanzia

kwenye ugumu wa kutoa malipo ya kutosha hadi kwenye ununuzi wa teknolojia itakayosaidia ufuatiliaji katika bonde.

xi

Page 13: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

• Ukosefu wa Usimamizi Shirikishi: mgawanyo wa kiutawala kati ya ngazi ya mkoa na ya taifa ukiunganishwa na njia za usimamizi za kisekta unadhihirisha kuwa sehemu kubwa ya usimamizi wa rasilimali za asili (NRM) katika bonde siyo shirikishi, kwa kuwa sekta au ngazi moja ya utawala hutumia mbinu ya usimamizi iliyo tofauti na ngazi au sekta nyingine katika bonde. Tatizo hili vile vile linajitokeza katika ngazi ya kimataifa: hakuna utaratibu uliowekwa kati ya Kenya na Tanzania wa kuratibu usimamizi wao katika Bonde la Mto Pangani.

• Matatizo na utawala wa jamii: hii huhusiana, kwanza na mchango hafifu unaotolewa na jamii katika ubunifu, utekelezaji na utiliaji mkazo wa mfumo wa usimamizi wa rasilimali za asili (NRM) ambao unawaelemea. Pili, nyingi ya njia hizi zinazoshinikizwa kutoka nje ya jamii, zinataka kuanzishwa kwa kamati za NRM za aina mbali mbali, hali ambayo matokeo yake ni mkanganyiko mwingi kupita kiasi katika ngazi ya jamii na hivyo kuchochea matatizo ya kisekta yaliyoelezwa hapo juu, migogoro ya mamlaka na mafanikio duni ya usimamizi.

Kwa kuzingatia masuala yaliyoelezwa hapo juu, Uchambuzi wa Hali Halisi unabainisha maeneo mbalimbali ya kipaumbele katika utekelezaji kama ifuatavyo:

Kuwepo kwa mikakati ya usimamizi inayounganisha sekta husika kwa ajili ya bonde la Mto Pangani ikishirikisha majukwaa mbalimbali. Hapana shaka hata kidogo kuwa bonde la Mto Pangani linahitaji haraka mikakati hiyo ambayo inaweza kukidhi upana na ugumu wa maswaala hayo. Mapendekezo yanayoweza kufikiriwa ni pamoja na kutengeneza mikakati ya kutambua mahitaji ya maji, kutathmini mahitaji ya maji ukanda wa chini wa mto kwa ajili ya watu na mazingira, kupanua wigo wa usimamizi wa maji na kuiongezea jamii wajibu wa kubuni na kutekeleza masuala ya usimamizi shirikishi wa rasilimali za asili (NRM).

Kuwepo kwa mikakati madhubuti ya kuwezesha mazungumzo miongoni na kati ya watumiaji rasilimali na wasimamizi wa aina mbalimbali na waliohusishwa katika sekta mbalimbali kwa lengo la kuongeza uelewa katika ngazi zote za usimamizi. Taratibu zinahitajika ili kuhakikisha kuwa fursa za maongezi kati na miongoni mwa wadau na wasimamizi zinaongezeka kwa kiasi kikubwa, ili kuhakikisha kuwa ubadilishanaji wa habari kwa pande zote unakuwepo, usambazaji unaboreshwa na elimu ya jinsi wadau wote watakavyoshiriki katika ustawi wa bonde inatolewa. Ni muhimu uhamasishaji ufanyike kuhusu vipengele vyote na hali ya usimamizi wa bonde na wadau wake katika ngazi zote za usimamizi na uratibu wake. Sehemu ya ziada ya eneo hili la kipaumbele ni uanzishaji wa mabaraza yenye uwezo wa kuifanya kazi hii, na kutumika kama vyombo vya kutatua migogoro, na viungo kati ya ngazi mbalimbali za utawala.

Kuainisha na kuanzisha mfumo sahihi wa ukusanyaji na ufuatiliaji wa data. Eneo hili la utendaji haliishii katika mifumo ya uendelezaji na ukusanyaji wa data za kihaidrolojia. Tathmini ya Setilaiti na GIS ya matumizi ya ardhi, viwango vya matumizi na mabadiliko ya kijiografia ni mahitaji ya msingi katika kupanga mipango na ufuatiliaji wa matumizi ya ardhi. Uundaji wa mbinu za kutathmini na kupima sababu za msingi za kijamii na za kiuchumi zinazosababisha uharibifu wa mazingira na utumiaji wa rasilimali uliokithiri pia zinahitaji kutambuliwa. Mifumo kama hii inabidi pia iwe na uwezo wa kutambua mahitaji ya maji katika Bonde. Mifumo ya data na ufuatiliaji iliyopendekezwa lazima iendane na uwezo wa ndani wa kifedha na matengenezo.

xii

Page 14: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

A Utangulizi wa Uchambuzi wa Hali Halisi Bonde la Mto Pangani

A.1 Maelezo ya jumla ya Bonde la Mto Pangani

Bonde la Pangani ni moja kati ya mabonde 9 yaliyoanzishwa na kuchapishwa katika gazeti la serikali kwa mujibu wa Sheria ya Maji ya 1074 (Usimamizi na Udhibiti) Na. 42 na marekebisho yake Na. 10 ya 1981 (sheria hii ilifutwa na sheria mpya ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji ya mwaka 2009) kwa madhumuni ya kuhamisha madaraka ya usimamizi wa maji kutoka ngazi ya Taifa na kupeleka ngazi ya mabonde. Bonde la Pangani lina eneo kadiri ya kilomita za mraba 58,8001 kiutawala na linajumuisha Bonde la Mto Pangani na mabonde ya mito midogo ya Umba, Msangazi, Zigi2 na mito midogo ya pwani, ukiwemo Mkulumuzi. Uchambuzi huu wa hali halisi unahusu zaidi Bonde la Mto Pangani. Maelezo ya mabonde ya mito midogo yanayosimamiwa kiutawala na Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani yanatolewa katika Kiambatanisho Na.1.

Bonde la Mto Pangani lina eneo la kilomita za mraba 43,6501, kati ya hizo, kilomita za mraba 3,9141 ziko Kenya (Mchoro wa 1). Nchini Tanzania, bonde hili lipo katika mikoa ya Kilimanjaro, Manyara, Arusha na Tanga. Sehemu ya bonde iliyopo Kenya karibu yote ipo katika wilaya ya Taita- Taveta.

Mto Pangani unaundwa na matawi makubwa mawili, ambayo yanatokea katika sehemu ya Kaskazini ya bonde. Tawi la kwanza ni Mto Kikuletwa unaonzia katika miteremko ya Mlima Meru na miteremko ya Kusini ya Mlima Kilimanjaro, na la pili ni Mto Ruvu, unaoanzia katika miteremko ya Mashariki ya Mlima Kilimanjaro na Ziwa Jipe. Mito hii inaungana katika bwawa la Nyumba ya Mungu, lenye eneo la kilomita za mraba 140 (Rohr na Killingtveit, 2002). Mto Pangani3 hutoka katika bwawa hili, ukitiririka kwa umbali wa kilomita 432 kabla ya kuingia katika Bahari ya Hindi..

Kwa ujumla, bonde hili lina mwinuko mdogo unaoteremka kuelekea upande wa Kusini na Kusini Mashariki hadi Bahari ya Hindi. Kwa wastani, sura hii ya nchi ijulikanayo kama Nyika za Masai ziko kwenye usawa wa mwinuko wa mita 800, na sehemu yake kubwa hupata mvua inayozidi kidogo milimita 500 kwa mwaka. Mkabala nayo ni safu ya milima inayoinuka kutoka uwanda huu ambayo mwinuko wake unafidia kwa kiwango kikubwa matatizo ya hali ngumu ya uwanda wa nyika. Katika sehemu hii ya juu, kiasi cha mvua kwa mwaka kinafikia milimita 2,000. Jinsi ilivyo, milima hii ni kama visiwa, wakati ambapo nyanda zinazoizunguka zinaonesha bayoanuwai duni, na hali ngumu ya kujitafutia riziki, milima hii ni visiwa vya bayoanuwai ya kuvutia na viumbe hai wengi. Binadamu hawakushindwa kuona ubora wa milima hii, na hata kabla ya ujio wa utawala wa kikoloni nchini Tanzania, milima iliyopo katika Bonde la Mto Pangani ilikuwa eneo linalokaliwa na idadi kubwa zaidi ya watu katika bonde hili.

1

1Tafiti nyingi za awali zinalielezea eneo la chanzo cha mto lililoko kwenye utawala wa Bonde la Pangani nchini Tanzania kuwa ni kilomita za mraba 56,300, na eneo la Bonde la Mto Pangani katika Tanzania na Kenya kuwa ni kilomita za mraba 42,000 kulingana na makisio ya planimita yaliyofanywa na S. Kamugisha (1992). Hatimaye taasisi mbili tofauti (TANRIC ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Rasilimali ya Maji katika Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo) zimekadiria maeneo haya kwa kutumia GIS. Makadirio haya ya hivi karibuni ni makubwa zaidi kuliko yale ya awali ya makisio ya planimita. Tofauti hizi huenda ni matokeo ya tafsiri mbalimbali za mipaka ya bonde, hasa upande wa magharibi na tofauti kati ya njia za planimeta na zile za GIS (Kamugisha na Mwakalinga pers. Wahojiwa, 2003).2Baadhi ya Waandishi hutumia tahajia za “Sigi”, “Zigi” ndiyo tahajia inayopendelewa na wakazi wa eneo la chanzo cha mto huu (Wahojiwa, 2003).3Baadhi ya tafiti na ramani zinataja Mto utokao katika Bwawa la Nyumba ya Mungu kuwa ni Ruvu mpaka unapoungana na Mto Mkomazi, mahali ambapo unakuwa Mto Pangani. Utafiti huu unataja Mto huu kutoka unapotoka Nyumba ya Mungu hadi unapoingia baharini kuwa ni Mto Pangani.

Page 15: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Jinsi Mto Pangani unavyoambaa kuelekea Mashariki, na kushukia uwanda wa pwani ya Tanzania, ndivyo unavyozidi kukabiliana na hali ya hewa na mazingira ya kutatanisha. Kinyume na hali ya hewa ya Kaskazini, ambayo imebadilika kwa kiasi kikubwa katika kipindi cha miaka elfu moja kutoka kipindi kimoja cha barafu hadi kingine, hali ya hewa inayotokana na Bahari ya Hindi imebakia bila mabadiliko makubwa. Mwambao wote wa pwani ya Afrika Mashariki unaonesha viunga vya misitu ya kale, na hali yake ya hewa imewezesha misitu hii kuhifadhiwa kutokana na uthabiti wake.

Mabadiliko ya tabianchi katika maeneo mengine barani Afrika yamebadili kabisa hali ya mazingira, na kusababisha kwa kiwango kikubwa kutoweka kwa viumbe hai na kuanza upya mchakato wa hatua za mabadiliko, kiasi cha kufanya misitu ya mwambao mwa Tanzania ifanane kidogo na misitu ya sehemu nyingine barani. Katika milima iliyopo bonde la Mto Pangani, mistiu hii inaonesha kutetereka kwa bayoanuwai na upatikanaji wake katika maeneo haya.

Leo hii idadi ya watu wanaokadiriwa kufikia milioni 3.7 huishi katika sehemu ya bonde iliyoko Tanzania, wakati ambapo nchini Kenya idadi ya watu wa Taita -Taveta inakaribia 40,900. Mtindo wa makazi katika bonde ni taswira ya kutowiana kwa hali ya mazingira ya bonde hili. Nchini Tanzania asilimia 90 ya watu wanaoishi katika bonde hili huishi katika nyanda za juu, asilimia 80 ya hao kwa njia moja au nyingine hutegemea kilimo kwa ajili ya mahitaji yao (Mwamfupe, 2002). Mkusanyiko huu wa makazi huleta msongamano wa watu unaofikia hadi watu 300 kwa kilometa ya mraba. Mwaka 1988, mikoa ya pwani ya Tanzania ilikuwa na idadi ya watu 28.4 kwa kilometa ya mraba (ukiacha Dar es Salaam), ongezeko la kutoka watu 18 tu kwa kilometa ya mraba mwaka 1967. Katika Milima ya Usambara Magharibi, idadi ya watu imekua kwa mara 23 tangu mwaka 1900, wakati katika maeneo ya nyanda za juu za Mlima Kilimanjaro, msongamano wa watu ni mkubwa kiasi cha watu 900 kwa kilomita ya mraba (Gillingham, 1999). Kinyume chake, maeneo ya nyanda za chini yameonesha kuwa na msongamano mdogo wa kiasi cha watu 65 kwa kilomita ya mraba.

Kihistoria, wakazi wa bonde hili wamekuwa na shughuli za kiuchumi ambazo ni kielelezo cha hali zilizotofauti za mazingira katika bonde. Nyanda za chini zilikimu wafugaji, wakati nyanda za juu zilikimu wakulima. Kutokana na ujio wa wakoloni kutoka Ulaya, maeneo makubwa ya ardhi ya kilimo yalitengwa kwa kilimo cha mashamba makubwa. Katika wilaya ya Taita – Taveta ya Kenya, karibu ardhi yote ilitengwa kwa ajili ya kilimo cha mkonge. Hali hii ilisababisha kukua kwa kiwango cha kilimo. Johnston (1946) anasema kuwa, mwaka 1943, umilikaji ardhi katika nyanda za juu za Kilimanjaro kwa wastani ulikuwa hekta 1.2 kwa mtu mmoja. Katika mwaka 1946, ulikuwa mita za mraba 2.5 tu.

Wastani wa kiwango cha umilikaji wa ardhi katika nyanda za juu za Kilimanjaro umeongezeka tokea hapo, na Lein (2002) anasema kiwango cha umilikaji ardhi kuwa ni wastani wa hekta 0.6 kwa kaya. Kaya za nyanda za chini hulima mashamba ya wastani wa eneo la hekta 10.4.

Wastani huo unaelekea kupungua. Kadiri ukubwa wa mashamba katika nyanda za juu unavyokuwa mdogo zaidi na zaidi, uwezo wake wa kukidhi mahitaji ya maisha ya watu unapungua, na udongo umechoshwa kutokana na kupanda mazao mfululizo pamoja na umwagiliaji uliokithiri, watu wamelazimika kutafuta ardhi katika maeneo ya nyanda za chini. Kwa sababu hiyo, idadi ya watu imekuwa kubwa kando ya mito ya bonde la mto Pangani na umwagiliaji umeenea kwa kiasi kikubwa sana. Matokeo yake, maeneo ya bayoanuwai yaliyopo hapa na pale katika uwanda wa bonde yako katika shinikizo la kutoweka.

2

Mchoro wa 1: Bonde la Mto Pangani lilivyoenea Tanzania na Kenya (Rejea:Mradi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Rasilimali za Maji)

Page 16: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

3

Mch

oro

wa

2: B

onde

la M

to P

anga

ni

Ang

alia

pia

Pic

ha y

a 1,

uku

rasa

wa

33

(Rej

ea: M

radi

wa

Usi

mam

izi w

a M

atum

izi

Bor

a ya

Ras

ilim

ali z

a M

aji)

Page 17: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Kwa hiyo, kiini cha matatizo ya Bonde la Mto Pangani kinahusiana na msogamano wa watu na mahitaji yao mawili makuu na muhimu kwa kilimo na ufugaji: ardhi na maji. Mwingiliano wa mambo haya, na mahitaji waliyo nayo watu katika rasilimali za bonde, yamesababisha migogoro ya aina mbalimbali:

Migogoro itokanayo na viwangoUhusiano baina ya watumiaji maji wa ukubwa tofauti katika Bonde la Mto Pangani mara nyingi unajieleza katika namma mbili, yaani mashamba makubwa yanayotumia mamia ya lita za maji kwa sekunde na kutumia mifumo ya umwagiliaji yenye ufanisi mkubwa, tofauti kabisa na watumiaji wadogo wanaotumia maji kidogo na mifumo duni ya umwagiliaji. Tofauti hizi za viwango vya matumizi haziishii kwenye teknolojia pekee, bali hata ardhi. Watumiaji wakubwa karibu wakati wote hutumia ardhi kubwa zaidi kuliko watumiaji wadogo. Jambo jingine tofauti na la pekee ni kuwepo kwa mitambo ya uzalishaji umeme katika bonde. Ardhi inayokaliwa na mitambo hii siyo kubwa sana, lakini mahitaji yake ya maji ni makubwa sana. Ni dhahiri maji haya hurudishwa mtoni, hii ikiwa na maana uzalishaji umeme huyaacha maji katika hali na kiasi kile kile kilichochukuliwa. Pamoja na hayo matumizi hayo ni kwa maslahi ya taifa. Bonde la Mto Pangani huzalisha kiasi kinachofikia asilimia 17 ya umeme wa Tanzania, na vinu vyake vingi vimesanifiwa maalum kwa kutilia maanani mtiririko wa maji. Iwapo matumizi ya maji kati ya vyanzo vya maji na mitambo ya umeme yatazidi, inabidi mitambo izalishe kwa kiwango chini ya uwezo wake. Mgogoro uliopo hapa ni kulinda maslahi ya kitaifa dhidi ya watumiaji wadogo.

Migogoro itokanayo na umilikiKitabu hiki kinatumia neno umiliki kama haki ya kusimamia rasilimali. Kama ilivyo kwenye sehemu nyingi ulimwenguni, dhana ya usimamizi kwa misingi ya kijamii katika Tanzania na Kenya ni mpya. Katika nchi ambazo mifumo ya usimamizi inayotegemea serikali, imedumu kwa zaidi ya nusu karne, bila mafanikio mazuri na kusababisha ongezeko la matatizo ya mazingira, usimamizi wa maliasili kwa misingi ya kijamii (CBNRM) unaonekana kuwa chaguo la kuvutia. Kwa hali hiyo nchini Tanzania kuna asasi nyingi mno za usimamizi wa kijamii. Dhana ya usimamizi wa maliasili kijamii inabakia kuwa mpya sana nchini Kenya. Ukinzani wa mifumo hii unahusiana na mwenendo wa matumizi na miundo yao. Hapa, jamii zinaweza zisihusishwe katika uundaji wa mfumo wa usimamizi, utekelezaji wake au hata mifumo yake ya kisheria.

Migogoro itokanayo na mahaliMaeneo ya watumiaji maji yaliyoko juu hutoa nafasi nzuri zaidi ya matumizi ya rasilimali kuliko ilivyo kwa watumiaji wa maeneo ya chini. Kimsingi, matatizo haya yanaweza kuonekana katika mifereji ya umwagiliaji ambapo watumiaji walio karibu na chanzo cha maji wanaweza kuotesha mazao yanayohitaji maji mengi sana (kama vile mpunga) na wale wanaoishi mwishoni mwa mfereji hulazimika kupanda mazao yenye mahitaji madogo ya maji. Matatizo makubwa yanayoikabili mitambo ya umeme wa maji iliyopo upande wa chini ni mfano mwingine.

Taasisi kuu mbili zinatawala rasilimali ya maji ya Bonde la Mto Pangani. Nchini Tanzania ni Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani (PBWO), wakati katika Kenya ni Mamlaka ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji (WRMA). Chini ya sheria ya hivi karibuni ya Tanzania, mabonde yote yamewekwa (au yatawekwa) chini ya ofisi kama hizo. Hata hivyo, mabonde mengine ni madogo mno kustahili kuanzishiwa ofisi zitakazojitegemea kiusimamizi. Bonde la Pangani limezungukwa na mabonde manne ya aina hiyo (mito ya Umba, Zigi, Msangazi, na mabonde madogo ya mito ya pwani). Haya kiutawala yanawekwa chini ya PBWO, na hayakujumuishwa katika uchambuzi wa hali halisi katika kitabu hiki. Hata hivyo, muhtasari wa taarifa kuhusu mabonde hayo unaambatanishwa(Kiambatanisho Na 1).

Bonde la Mto Pangani linakabiliana na matatizo kadhaa makubwa ya kiusimamizi. Kwa kuzingatia tofauti kubwa za aina za maliasili za bonde, pamoja na mahitaji na matarajio mbalimbali ya matumizi, haja ya kuwa na usimamizi shirikishi haiwezi kupuuzwa. Hapo nyuma, njia ile ile ya usimamizi wa ‘kisekta’ kwa bonde hili ilimaanisha kuwa rasilimali ya wanyamapori ilisimamiwa kipekee tofauti na shughuli za misitu, bila kujua, kwa upande mwingine kipaumbele cha usimamizi wa maji. Tatizo pia linajitokeza katika utoaji kipaumbele, sekta ya maji ikidai kuwa maji ni kiungo kinachounganisha rasilimali zote za bonde, lakini watu wa misitu wakilalamika kuwa sehemu kubwa ya maji ya bonde yanatoka katika misitu iliyo kwenye mamlaka yao kisheria.

4

Page 18: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

5

A.2 Usimamizi wa Pamoja wa Mabonde ya Mito (IRBM)Kwa vyovyote vile, mfumo wa usimamizi wa maliasili kimabonde ndio unaofaa. Mabonde ya mito yanahusisha vyanzo na michakato yote ambayo hatimaye itahakikisha kuwa maji yanafika hadi mwisho wa mto. Hivyo, bonde la mto linahusisha vijito vya awali vya mto, mito midogo na mabonde yake. Pia ni pamoja na delta iliyohusiana na mto, na maji ya ardhini, ardhioevu na mabwawa yoyote yaliyomo.

Mchanganyiko wa michakato inayohakikisha kuwa maji yanasafiri kutoka kwenye chanzo cha mto hadi mwisho wake ni mgumu na una mambo mengi. Rasilimali za ziada, kama vile misitu na ardhioevu, zinachangia mchakato huu. Kiasi cha maji ambacho hatimaye hufika mwishoni mwa mto pia kitategemea kiasi cha maji yanayochukuliwa kwa matumizi yanapopita katika mkondo wake pamoja na kiwango cha uvukizaji katika maeneo ardhioevu na mimea ya majini na ya kandokando ya mto. Mwisho, ubora wa maji yatakayofika mwishoni mwa mto pia utaonesha michakato iliyopo katika bonde kama vile mbinu za kilimo ambazo huongeza au kupunguza mmomonyoko, maendeleo ya miji au viwanda n.k.

Usimamizi wa Mabonde ya Mito (RBM) unatambua kuwa usimamiaji wa mto hauwezi kutekelezwa kwa kutenganisha michakato na hali nyingi mbalimbali zinazoathiri mtiririko wa mto na ubora wa maji yake. RBM hulichukulia bonde la mto kama kitengo cha usimamizi kinachohusisha matumizi na uhifadhi wa (a) mifumo midogo ya ikolojia (mabonde madogo ya mito, misitu, ardhioevu, maeneo ya milima, ardhi kame, n.k); na (b) mifumo ya matumizi ya binadamu iliyomo ndani ya eneo la maji (kilimo, umwagiliaji, uvuvi, usafirishaji, uchimbaji madini, viwanda, n.k). RBM kwa kawaida hufuata kanuni ya kuwa maji huunganisha mifumo ikolojia iliyomo ndani ya bonde la mto (Howard, 2002).

Usimamizi wa Pamoja wa Bonde wa Mto hujaribu kuleta uwiano wa masilahi ya watumiaji wote waliopo katika bonde, na wakati huo huo kukuza ufanisi wa matumizi ya rasilimali na kuhakikisha kunaendelea kuwepo maji ambayo kwayo mifumo hii inategemea (Howard, 2002). IRBM inaweza kufafanuliwa kama ifuatavyo:

”… ni mchakato unaokuza uratibu wa maendeleo na usimamizi wa maji, ardhi na rasilimali zinazohusiana nazo ili kuzidisha ustawi wa kiuchumi na kijamii kwa njia ya usawa bila ya kuathiri uendelevu wa mifumo muhimu ya ikolojia (GWP, 2002:1).

IRBM hushughulika na rasilimali kwa mapana zaidi iwezekanavyo. Inabidi kuziangalia rasilimali za maji kwa mtazamo mzima wa mifumo ya kijamii, kiuchumi na kiikolojia ya mkoa au nchi. Kiutendaji, hii ina maana ya kuwa sera na programu katika maeneo mengine ya rasilimali hazina budi kuchambuliwa kwa makini ili kuona jinsi zinavyoathiri mahitaji yanayoshughulikiwa na sekta ya maji (GWP, 2002) IRBM inayapa mazingira umuhimu sawa na watu katika mahitaji ya rasilimali za maji. IRBM lazima ifanye kazi kulingana na malengo yaliyokubaliwa na wadau wa bonde walio wengi na kufuata kanuni za usimamizi wa rasilimali za maji, usimamizi wa mfumo ikolojia, uhifadhi wa bayoanuwai, usimamizi endelevu wa maliasili na ufufuaji wa mfumo ikolojia. (Howard, 2002).

Sehemu muhimu ya Usimamizi wa Pamoja wa Bonde wa Mto ni mpango wa matumizi ya ardhi. Kwa kuwa mambo mengi sana yanayotokea kuhusu maji yanahusu maendeleo ya ardhi, ni muhimu matumizi ya ardhi yasimamiwe kwa njia ambayo itahakikisha upatikanaji wa maji na kwamba michakato ya kihaidrolojia haiingiliwi. Kwa mfano, ukuaji wa miji mara nyingi umekuwa na athari kubwa kwa rasilimali ya maji kutokana na ongezeko kubwa la majitaka. Kwa njia hiyo hiyo, misitu na kilimo vinaweza kuwa na athari kwa wingi na ubora wa maji.

Mifano ya mapendekezo ya usimamizi wa matumizi ya ardhi ni pamoja na (a) kugawa kanda-hapa maeneo maalum hubainishwa ambamo aina fulani za matumizi ya ardhi hukatazwa. Kwa mfano kanda za maji ya kunywa, au maeneo ambayo ujenzi hupigwa marufuku kutokana na hofu ya mafuriko. (b) hatua za kulinda udongo na kudhibiti mmomonyoko, kama vile kilimo cha kontua, au ushauri wa upandaji wa miti (c) kanuni za uondoaji taka, kama vile kuweka maeneo ya kutupa taka (GWP,2002).

Page 19: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

A.3 Programu ya Maji na Uasili (WANI)IUCN (shirika la kimataifa la kuhifadhi uasili) inasaidia kupata utatuzi wa busara wa changamoto zinazotukabili duniani katika maendeleo ya jamii na utunzaji wa mazingia. IUCN inafadhili tafiti za kisayansi, na inasimamia miradi na huunganisha serikali za kimataifa, asasi zisizo za kiserikali, mashirika ya Umoja wa Mataifa, makampuni na jamii katika kutunga na kutekeleza sera, sheria na utendaji bora.

IUCN ni mtandao wa masuala ya mazingira ulio mkubwa kuliko yote duniani. Ni umoja wa kidemokrasia wenye wanachama 1,000 kutoka serikali na asasi zisizo za kiserikali, mashirika na wanasayansi 10,000 wa kujitolea katika nchi zaidi ya 160. Ina waajiriwa wataalamu 1,100 katika ofisi zake 62 na mamia ya washiriki kutoka jamii, asasi na sekta isiyo rasmi ulimwenguni kote. Makao makuu yake yapo Gland, karibu na Geneva, Uswisi.

IUCN ilizindua mpango wa maji na uasili (Water and Nature Initiative (WANI)) mwaka wa 2001. WANI ni mpango wa utendaji unaofanya kazi na washiriki 80 katika nchi 30 katika kuhusisha kwa kiasi kikubwa mambo ya mazingira na jamii wakati wa utayarishaji wa mipangao ya usimamizi wa rasilimali za maji. Mpango wa WANI hutumia menejimenti ya mfumo wa ikologia kama mkakati wa usimamizi uwiano na wa pamoja wa ardhi maji, bayoanuai na jamii. WANI husaidia katika utatuzi wa kuchagua katika mtanziko wa maendeleo ya jamii na hifadhi ya rasilimali zilizo majini kwa kutanzua migogoro ya matumizi ya maji, na kufufua mito na kuchochea maendeleo ya jamii.

WANI huandaa na kuonyesha njia sahihi ya utendaji katika kutekeleza usimamizi wa rasilimali za maji wa uwiano. Husaidia katika kufanyia mageuzo ya kudumu na kujenga uwezo wa jamii unaohitajika katika kutekeleza mageuzi hayo. Katika awamu ya kwanza, kuanzia mwaka wa 2001 hadi mwaka wa 2008 WANI ilifanya kazi katika mabonde ya maji 12 katika nchi zaidi ya 30 ulimwenguni kote, kazi iliyogharimu dola za Marekani 40m. Sehemu kubwa ya fedha hizi zilitolewa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Uholanzi. Miradi ya majaribio ya WANI ilionyesha nama hali ya watu na mifumo ya ikolojia inavyoweza kunufaika kwa kutumia usimamizi endelevu wa mabonde ya maji. Miradi ya WANI ni washiriki wa jumuia, wanachama wa IUCN, jamii za kiraia na serikali.

6

Kisanduku cha 1: Usimamizi wa Mahitaji ya Maji

Usimamizi wa Mahitaji ya Maji (WDM) umetokana na kutambua kuwa (a) mahitaji ya maji yana-ongezeka bila ya kuambatana na ongezeko la upatikanaji wa maji; (b) matokeo yake, gharama ya kuongeza usambazaji wa maji hupanda kwa sababu uchukuaji maji kutoka katika vyanzo vipya unakuwa mgumu zaidi. Gharama zinazoambatana na uanzishaji wa teknolojia au mbinu mpya ya uchukuaji maji inawezekana zisikubalike. WDM, basi, inajaribu kuokoa maji yachukuliwayo kutoka vyanzo vilivyopo vya maji, yalete manufaa kwa vyote viwili, uchumi na mazingira. WDM inaweza kufafanuliwa kama mkakati wa kuboresha matumizi fanisi na endelevu ya rasilimali za maji kwa kuzingatia masuala ya kiuchumi, kijamii na kimazingira (Wegelin-Schuringa, 1998). Lengo kuu la WDM ni kuchangia katika utoaji huduma za maji na uondoaji majitaka kwa ufanisi na usawa. IUCN inaamini kuwa hili linaweza kufikiwa kupitia utumiaji wa vivutio mbalimbali vya kiuchumi, kukuza ufanisi na usawa wa matumizi ya maji na vile vile hatua kadhaa za kuhifadhi maji zitakazolenga katika kukuza uelewa juu ya uhaba na tabia ya asili ya kumalizika kwa rasilimali hii. WDM huchu-kua hatua mbalimbali zinazolenga kuleta usimamizi endelevu. Nazo ni pamoja na:

• kulinda ubora wa maji• kupunguza upotevu wa maji• kuboresha ugawaji wa maji baina ya watumiaji • kuweka mfumo sahihi wa upangaji bei• hatua za kuhifadhi maji

Page 20: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

WANI inasaidia kufanya mabadiliko kwa kuunganisha vipaumbele vya maendeleo, huduma zitolewazo na mifumo ya ikolojia, utawala bora wa rasilimali za maji, ushiriki wa wadau, mapato endelevu ya fedha, kujifunza na uongozi.katika utendaji.

Toleo la kwanza la Uchambuzi ya Hali ya Bonde llikuwa tokeo la kazi ya awali katika bonde la Pangani na liliweka msingi wa miradi iliyofuata awamu ya kwanza ya WANI ilianza kufanya kazi katika bonde lote la Pangani na kufuatana na matokeo ya kazi hii Ofisi ya Maji Bonde la Pangani iliweza kupata ufadhili wa nyongeza kutoka Kamisheni ya Ulaya kupia msaada wa mfuko wa maji wa Umoja wa Ulaya, Mfuko wa Mazingira wa Ulimwengu (Global Environment Facility) kupitia Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).

A.4 Uchambuzi wa Hali halisi: madhumuni na matokeoUchambuzi wa Hali halisi ni hatua muhimu ya mradi wa IUCN. Ni uchambuzi wa hadhi, hali, mienendo na masuala muhimu yanayoathiri mifumo ikolojia, watu na taasisi katika hali ya kijiografia ya ngazi yoyote (jamii, taifa, kanda, kimataifa)’ (IUCN, 1999:1). Madhumuni ya Uchambuzi wa Hali halisi ni kutoa tathmini inayotosheleza dhamira ya kipaumbele au maeneo ya utendaji yatakayoendelezwa.

Kwa mantiki hii madhumuni ya Uchambuzi huu ni kama yafuatayo:

• Kutambua rasilimali zilizomo katika Bonde la Mto Pangani na michakato na matukio yanayoziathiri. Uchambuzi utayaonesha maeneo hayo maalum ambayo yanahitaji kushughulikiwa ili kuyanusuru, kwa kuzingatia ushahidi unaoonesha kuwa uwiano kati ya upatikanaji wa riziki ya kutosha kwa wakazi wa Bonde hili na uendelevu wa rasilimali za Bonde umeharibiwa.

• Kutambua maeneo ya utendaji kwa mapana ambamo hatua zinaweza kuchukuliwa kwa manufaa. Uchambuzi unatambua kuwa nyingi ya hatua hizo zinaweza zisiwe ndani ya utaalam wa IUCN. Hivyo utataka kuainisha mashirika, vikundi au taasisi nyingine ambazo IUCN inaweza kuingia nazo ubia kadri inavyotaka kuendeleza juhudi za WANI katika Bonde la Mto Pangani.

A.5. Vyanzo vya data Uchambuzi huu wa Hali halisi umefanyika kwa kutumia data zilizopatikana kutokana na vyanzo vikuu viwili:

• Taarifa iliyochapishwa. Umuhimu wa kipekee upo katika matokeo ya tafiti juu ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji zilizofanyika katika Bonde la Mto Pangani, ambazo ni juhudi za pamoja kati ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Teknolojia na Sayansi cha Norway. Kwa nyongeza, Uchambuzi wa Hali halisi pia umetumia taarifa ya warsha iliyoitwa “Bonde la Mto Pangani: Mapendekezo ya Usimamizi Shirikishi”, iliyofanyika hoteli ya “Kilimanjaro Crane” , Moshi, Tanzania, tarehe 8 –10 Mei, 2002.

• Mahojiano yasiyoandaliwa kikamilifu baina ya mwandishi na wadau wa Bonde la Mto Pangani. Waliohusika ni pamoja na watawala wa maji, watu wa misitu, jamii za wakulima, wahifadhi wa wanyamapori na watumiaji binafsi wa maji. Mahojiano yalifanyika Arusha, Moshi, Hale, Tanga na Dar es Salaam kati ya Novemba 12 na 22, 2002. Mahojiano, wahojiwa na ushirikishwaji wa taasisi zao vimetolewa kama sehemu ya rejea za waraka huu.

Uchambuzi huu wa hali halisi umefanyiwa mapitio na idadi kubwa ya wadau wa Bonde la Mto Pangani. Wakati wa warsha iliyofanyika Moshi-Tanzania, kati ya tarehe 10 na 12 Machi, 2003, Uchambuzi wa Hali halisi uliwasilishwa kwa wadau kwa ajili ya mapitio na maoni. Mwezi Mei, 2003, maoni ya nyongeza yalipokelewa kutoka Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani na Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani (CDA Kenya). Marekebisho yaliyopendekezwa hatimaye yalizingatiwa na yamejumuishwa.

7

Page 21: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

A.6 Muundo wa Uchambuzi wa Hali halisiUchambuzi huu wa hali halisi unaanza kwa maoni ya jumla ya rasilimali za bonde hili na matatizo yanayozikabili. Kisha unaangalia shughuli za rasilimali watu katika bonde, uchumi wao, matatizo na vikwazo vya upatikanaji wa rasilimali. Kisha uchambuzi unaendelea kuangalia matatizo na masuala ambayo wadau mbalimbali wanaona kuwa yapo katika bonde kama msingi wa kujadili muundo wa Usimamizi wa Maliasili za bonde. Katika sura nyingi, uchambuzi umefupisha dondoo muhimu ambazo msomaji anatakiwa kuzifahamu na kuzizingatia kadiri anavyoendelea na sehemu za uchambuzi zinazofuata. Mihutasari hii imewekwa pamoja katika hitimisho la kitabu hiki, ambapo majadiliano yatarudi kwenye madhumuni yake, na kuangalia jinsi matatizo yaliyotambuliwa, juhudi za usimamizi ambazo zimechukuliwa na mapendekezo ambayo yamefikiriwa kwenye kitabu hiki kwa pamoja yanaweza kuwa kichocheo na msingi wa uchukuaji wa hatua muafaka na ushirikiano wa WANI.

8

Page 22: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

B Maliasili za Bonde la Mto Pangani

B.1 UtanguliziUtangulizi wa Uchambuzi huu wa Hali halisi umetoa mwanga kuhusu rasilimali anuwai zilizomo katika Bonde la Mto Pangani. Katika sura hii, tunaanza kwa kuangalia misitu iliyopo katika bonde, mchango wake na tishio la hifadhi ambalo linatoa changamoto kwa misitu hiyo. Mfumo kama huo huo utatumika kuangalia rasilimali za ziada katika bonde, zikiwemo maji na maeneo ardhioevu, maeneo yaliyohifadhiwa na bayoanuwai. Sura hii itahitimishwa kwa muhtasari wa dondoo muhimu. Sura hii kimsingi inahusika na rasilimali za maji na viumbe hai. Mashapo ya madini yaliyopo katika bonde hayakuzingatiwa sana kutokana na ukosefu wa data.

B.2 Misitu ya BondeMgawanyo wa misitu, aina na hadhi yake kisheria nchini Tanzania iko kama ifuatavyo:

Jedwali la 1: Aina, matumizi na hadhi ya kisheria ya misitu nchini Tanzania.

Hekta 1,000 %

Aina ya Msitu

Misitu (mingine mbali ya misitu ya mikoko) 1,141 3.4

Misitu ya Mikoko 115 0.3

Misitu ya Mbao 32,299 96.3

Jumla 33,555 100.0

Matumizi ya Ardhi ya Misitu

Eneo la misitu ya uzalishaji 23,810 71.0

Eneo la misitu inayohifadhiwa (hasa maeneo ya vyanzo vya mito) 9,745 29.0

Jumla 33,555 100.0

Hadhi ya Kisheria

Hifadhi ya Misitu 12,517 37.3

Misitu/misitu ya mbao katika mbuga za taifa, n.k. 2,000 6.0

Ardhi ya misitu isiyohifadhiwa 19,038 56.7

Jumla 33,555 100.0(Rejea: Lambrechts et al., 2002).

Misitu ya Bonde la Mto Pangani huwakilishwa na aina kuu tano: (a) Misitu ya milima ya Afrika (b) Misitu ya Mikoko (c) Misitu ya Mwambao (d) Misitu ya Miombo (e) Misitu ya kandokando ya mito. Misitu hii inaweza kuwa ya hifadhi, uzalishaji au misitu isiyokuwa na hadhi maalum. Misitu ya Pwani na ya milima ya Afrika, kutokana na upekee wake wa bayoanuwai, hupata nafasi ya kufikiriwa zaidi. Shughuli za kimataifa za bayoanuwai katika misitu hii pia zinasaidia upatikanaji zaidi wa data kuliko ilivyo kwenye aina nyingine za misitu. Hili linajionesha katika kitabu hiki.

Sehemu kubwa ya uwezo wa Bonde la Mto Pangani katika upatikanaji wa maji inachangiwa na misitu yake. Kwa mfano kwenye Mlima Kilimanjaro, kiasi cha asilimia 96 ya maji yanayotiririka kutoka mlimani chanzo chake ni kwenye ukanda wa msitu pekee (Lambrechts et al., 1992), na Mlima Kilimanjaro unakadiriwa kutoa asilimia 60 ya maji yanayoingia Bwawa la Nyumba ya Mungu, na asilimia 55 ya maji yatiririkayo juu ya ardhi katika bonde (Rohr na Killingtveit, 2002).

9

Page 23: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Misitu ya vyanzo vya maji inafanya kazi tatu muhimu (Akitanda, 2002):

• Misitu huchangia kwenye hifadhi ya maji kwa kurekebisha kasi ya maji, kuzuia mmomonyoko wa udongo, kuweka akiba ya maji na kuboresha ubora wa maji.

• Huhifadhi mkusanyiko wa jeni: Misitu kama ile ya unyevunyevu ya kitropiki huonesha viwango vya juu sana vya bayoanuwai, na huchangia udumishaji wa mkusanyiko wa jeni wa dunia.

• Misitu hutoa mazao kwa ajili ya matumizi ya jamii, kama vile mbao na mimea ya madawa.

Misitu ya MikokoMisitu ya mikoko hutoa mchango mkubwa katika kuhifadhi ukanda wa pwani. Huhifadhi mashapo laini yaliyoko kando ya bahari kutokana na mmomonyoko, huzuia masimbi na kutumika kama virutubisho. Miti yenyewe na matope kuzunguka mizizi yake ni makazi muhimu kwa viumbe mbalimbali wa majini na wale wajifichao. Wakati wa mawimbi makubwa, mamia ya aina za samaki huhamia katika misitu ya mikoko ili kujipatia chakula au mazalio. Samaki wengi na kamba hutegemea mikoko kama sehemu za kulelea vifaranga vyao. Miti ya mikoko ni migumu sana na hivyo inastahimili mchwa na kuvu. Inatumika kwa shughuli mbalimbali. Matawi ya Rhizophora, Ceriops na Bruguiera ni marefu na yamenyooka, kwa hiyo hutumika maalum kama miti ya kujengea ingawa hutumika pia kama nguzo, na katika utengenezaji wa mitego ya samaki na samani. Katika miaka ya karibuni, mikoko pia imetumika kutengeneza mkaa na pia

10

Kisanduku cha 2: Taarifa za Msingi za Misitu iliyomo katika Bonde la Mto Pangani

Misitu ya Bonde la Mto Pangani ni muhimu kwa haidrolojia yake kwa sababu:• hurekebisha kasi ya maji, huzuia mmomonyoko wa udongo, huhifadhi maji na kuboresha

ubora wa maji;• huchangia katika matengenezo na hifadhi ya mkusanyiko wa jeni;• hutoa mbao na madawa kwa matumizi ya jamii .

Kuna aina kuu tano za misitu katika Bonde:• Misitu ya mikoko: Hutoa mchango mkubwa katika kuhifadhi ukanda wa pwani. Huhifadhi

mashapo laini yaliyoko kando ya bahari kutokana na mmomonyoko, huzuia masimbi na hutumika kama virutubisho. Miti yenyewe na matope kuzunguka mizizi yake ni makazi muhimu kwa viumbe mbalimbali vya majini na maficho yao.

• Misitu ya pwani ya Afrika Mashariki: Hii ni misitu ya kipekee iliyoko Afrika Mashariki na ina bayoanuwai na viumbe wengi. Iko katika uwanda wa pwani kati ya misitu ya mikoko na Milima ya Tao la Mashariki.

• Misitu ya milima ya Afrika (Afromontane): Misitu ya Milima ya Tao la Mashariki ina kiwango cha juu cha bayoanuwai na viumbe wengi kama ilivyo katika misitu ya pwani. Katika Milima ya Kilimanjaro na Meru, misitu hii haionyeshi anuwai inayofanana, lakini inatoa mchango muhimu kihaidrolojia.

• Misitu ya kandokando ya mito: hii huimarisha kingo za mito, na mto Pangani unapotiririka kupitia nyanda za chini zilizo kavu na kame, huwa maeneo ya kipekee ya miti na vichemchemi kwa matumizi ya binadamu na wanyama pori.

• Msitu wa miombo: hii inajumuisha kundi kubwa la miti ya jamii ya mnondondo (Brachystegia, Isoberlinia na Julbernadia). Tofauti na misitu ya mvua, misitu ya miombo haisongamani sana kiasi cha kuzuia mwanga usifike ardhini. Matokeo yake ni kuwa, nyasi hufunika eneo kubwa la ardhi chini ya msitu, na wakati wa msimu wa mvua, nyasi hukua hadi kufikia kimo cha mita moja.

Page 24: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

hukusanywa kama kuni. Misitu ya mikoko iliyoko karibu na miji hutumika kwa wingi kwa madhumuni haya. Mikoko inaweza kupunguzwa matawi ili kuongeza ukuaji wake na upandikizaji upya pia ni rahisi. Hata hivyo hakuna shughuli yoyote kati ya hizi inayofanyika katika mwambao wa Tanzania (Richmond, 1997).

Karibu mwambao wote wa pwani ya Tanzania umepambwa na misitu ya mikoko. Katika eneo la Bonde la Mto Pangani, inapatikana katika mkoa wa Tanga pekee, ambako karibu asilimia 11 ya mikoko ya Tanzania hupatikana. (Bwathondi na Mwamsojo, 1993) Hii ni pamoja na hekta 753 za misitu ya mikoko iliyosongamana kuzunguka mdomo wa mto Pangani (Kijazi, 2002).

Misitu ya Pwani ya Afrika MasharikiMisitu ya pwani ya Afrika Mashariki iko katika uwanda wa pwani, kati ya Milima ya Tao la Mashariki na mikoko ya pwani. Misitu hii imetawanyika sana, na viunga vya misitu vimetenganishwa na maeneo ya mifumo ikolojia nusu kame. Imeenea kati ya mwinuko wa mita 500 na 1,000 juu ya usawa wa bahari. Tabia muhimu ya misitu ya pwani (ambayo ipo pia katika misitu ya Milima ya Tao la Mashariki) ni ile ya kuitegemea hali ya hewa ya Bahari ya Hindi na uthabiti wa kihistoria iliyoipatia. Kwa kuwa pekee katika uwanda wa pwani ya Afrika Mashariki, kujitenga kwa misitu hii kutoka mifumo mingine ya misitu ya Afrika kumesababisha viwango vya juu vya upatikanaji wa spishi (tazama hapa chini) (Burgess et al.,1996). Inasadikiwa kuwa kuna misitu 76 ya pwani nchini Tanzania (Burgess et al.,1996). Mingi ipo katika uwanda wa nyasi wa pwani kati ya mdomo wa mto Pangani hadi chini ya milima ya Usambara (tazama Baker na Baker, 2001).

Misitu ya milima ya Afrika (Afromontane)Milima ya Tao la Mashariki inaambaa kutoka mpaka wa Tanzania na Zambia hadi milima ya Taita nchini Kenya. Inahusisha milima ya kale ya fuwele iliyopo Mashariki ya Tanzania na Kusini Mashariki ya Kenya ambako inakabiliana moja kwa moja ya hali ya hewa ya Bahari ya Hindi. Katika Bonde la Mto Pangani inahusisha milima ya Pare ya Kaskazini na Kusini, milima ya Usambara ya Mashariki na Magharibi na Milima ya Taita. Milima hii ni ya zamani sana, na kipindi cha karibuni zaidi cha uharibifu wa miamba iliyoiathiri kilitokea miaka milioni 7 iliyopita. Kwa kulinganisha, lava ya zamani zaidi katika Mlima Kilimanjaro ina umri wa miaka milioni 1 tu. (Burgess et al., 1996).

Ukaribu wa milima hii na bahari pia umefanya hali yake ya hewa kubaki kuwa thabiti kabisa. Wakati wa zama za mwisho za barafu, hali ya joto la uso wa bahari ya Hindi haikubadilika. Hivyo, ingawa zama za barafu zinaweza kuwa zimebadili hali ya hewa katika sehemu nyingine za Afrika, haikufanya hivyo kwa milima ya Tao la Mashariki. Kwa hiyo milima hii imefaidi kipindi kirefu sana cha uthabiti wa mazingira, na pia imetengwa na misitu mingine na kwa hakika, kati ya msitu mmoja na mwingine (Burgess et al.,1996).

Matokeo ya mabadiliko haya ni kuwa tabia za viumbe hai vya milima hii ni za namna mbalimbali na zinaainishwa na viwango vya juu vya upatikanaji kwa wingi au unaokaribia kuwa kwa wingi (tazama chini). Inawezekana kuwa kwa kiasi fulani kiwango cha chini cha spishi anuwai na upatikanaji wake katika Mlima Kilimanjaro ni matokeo ya uchanga wake.

11

Kisanduku cha 3: Milima ya Taita

Milima ya Taita ni Milima pekee ya Tao la Mashariki katika Kenya. Milima hii na misitu yake inachukua spishi zaidi ya 2,000 za mimea yote (flora) na wanyama wote (fauna), ambapo aina 13 kati ya hizo zinapatikana kwa wingi. Mimea 67 ya asili inayojulikana, ikiwemo kahawa mwitu (Coffee fademi), husitawi milimani. Milima ya Taita ni Eneo Muhimu la Ndege (IBA), na ina spishi tatu zinazopatikana kwa wingi: Taita Apalis, Taita Thrush na Taita White – eye. Misitu ya milima hii pia ina utajiri wa amfibia (wanyama waishio majini na nchi kavu), wadudu na viumbe vingine. Ni kilomita za mraba 6 tu ndizo zinazobaki katika Milima ya Taita, zikiwa zimegawanyika katika viunga 13 vya misitu. Newmark (1998) anakadiria kuwa mabaki haya ya milima huwakilisha asilimia 2 tu ya mtandao wa misitu hii miaka 2,000 iliyopita. Milima ya Taita imepoteza misitu zaidi kuliko mlima wowote wa Tao la Mashariki.

Page 25: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Msitu wa Mlima Kilimanjaro umegawanyika katika aina mbalimbali za uoto: kanda ya savana, eneo la kilimo na misitu lililo na watu wengi, ukanda wa misitu, ukanda wa mimea (alpine) mirefu kiasi na mirefu. Kwa mifumo ikolojia na bayoanuwai, ukanda wa misitu ni muhimu zaidi katika mlima huu, na una karibu nusu ya spishi zote za mimea ya milima huu (Lambrechts et al., 2002).

Misitu ya kandokando ya mito (Riverine)Misitu ya kandokando ya mto kuzunguka sehemu ya Kinamasi ya Kirua inaweza kugawanywa katika makundi saba kama ifuatavyo (IVO-NORPLAN, 1997):

• Uoto wa kando ya mto: huu ni pamoja na uoto unaokwenda hadi mita 50 kila upande wa kingo za mto. Kwa upande wa mashariki, spishi kuu ni Cyperaceae (mf. Cyperus alticulatus C. laevigatus) Gramineae (mf. Phragmites mauritianus, Echnochloa Colonum) na Typhaceae (eg. Typha domingensis). Pale ambapo kina cha ukingo wa mto ni kirefu Ficus Sur na Acacia Zanzibarica ndizo maarufu. Ukingo wa magharibi umetawaliwa na Ficus sur, Trichilia emetica, Elaeis guineense, jamii ya Mchenje/Msesewe (Albizia graberrima, Antidesma Venosum na A. Zanzibarica). Tabaka la vichaka vya kando ya mto linatawaliwa na spishi kama vile Sesbania Sesbans na Phyllanthus muellerianus.

• Ardhi ya kinamasi cha Cyperus na Sesbania: katika maeneo ambayo maji hutuwama wakati wote, spishi kama Cyperus axaltatus na Typha domingensis ndizo zinazotawala. Katika maeneo yale ambayo hupata mafuriko kwa vipindi, Sesbania sesbands, Cyperus Laevigatus na Mkongoe (Acacia Xanthophloea) ndio aina za pekee za miti zinazohusishwa na aina hii ya uoto. Hii ni aina ya uoto iliyo maarufu sana kwenye eneo la kinamasi la Kirua, ingawa ni maarufu zaidi katika ukingo wa mashariki wa mto kuliko ukingo wa magharibi. Kwa upande wa mashariki, inaweza kutanda hadi kilomita 3 kutoka mtoni, wakati ambapo umbali mrefu zaidi ni kiasi cha mita 700 tu kutoka mtoni kwa upande wa magharibi wa mto.

• Nyanda za nyasi za Sporobolus pyramidalis na Cynodon dactylon: Jamii ya Poaceae ndio inayotawala hapa, ikiambatana na miti michache iliyotawanyika na vichaka. Katika eneo la Kinamasi la Kirua, aina hii ya uoto inaenea katika eneo kubwa zaidi. Inaweza kutokea kama viunga au maeneo makubwa ya nyasi.

• Misitu ya mbao ya Mkongoe (Acacia Xanthophloea): Aina hii ya uoto hutawaliwa na spishi ya Acacia, ambayo hufikia urefu wa hadi mita 18, na ikiwa na utando ulioziba eneo la kiasi cha asilimia 20 ya eneo la ardhi. Aina hii ya uoto ina thamani kubwa kijamii na kiuchumi kwa wakazi wa eneo hili oevu.

• Jangwa lenye vifungu vya Suaeda monoica: Aina ya uoto inayojieleza, ambayo kwa kawaida hupatikana mbali kidogo na mto baada ya sehemu za uoto wa nyasi.

• Eneo la vichaka vya mpoma wa Afrika (Commiphora africana): Mwendelezo wa ukanda wa eneo la vichaka linalotawaliwa na C. Africana ambao hupatikana chini ya Mwinuko wa Martin. Kwa kawaida, kila kichaka kina urefu pungufu ya mita 6, na utando wake unaziba zaidi ya asilimia 20 ya eneo la ardhi.

• Ardhi ya kilimo: Mnamo mwaka 1997, kilimo katika eneo la Kinamasi cha Kirua kilikomea kuwa cha maeneo madogo, na kutawaliwa na mazao yanayohitaji maji mengi kama migomba na miwa, pamoja na mahindi.

Misitu ya miomboMisitu ya Miombo imeenea katika eneo la asilimia 50 ya Tanzania na ni uoto wa aina moja ulio mkubwa zaidi katika Afrika ya Mashariki. Misitu ya miombo ya Afrika Mashariki ni mfumo uliodhoofishwa wa spishi ya miombo iliyoenea sana katika Afrika ya Kati (Rogers, 1997).Inaweza kuelezewa kama ifuatavyo; ‘miti inayopukutisha majani isiyokuwa na miiba (yenye spishi chache zenye miiba) inayojitokeza katika maeneo ya mvua za msimu mmoja katika ardhi chakavu kijiolojia, yenye asidi, na ya mchanga. Inajulikana kwa miti ya jamii ndogo ya Caesalpinoideae, hususan spishi za jamii ya myombo (Brachystegia na Julbernadia).

12

Page 26: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

13

Tabaka la vichaka linatofautiana kwa unene, asilimia ya ueneaji na spishi zilizomo. Mara nyingi hutawaliwa na Mgoto/Mtobwe (Diplorhynchus na Combretum spp). Utando wa ardhi hutofautiana kutoka kwenye nyasi nyingi hadi kwenye vichaka haba na nyasi ndogo ndogo. Muundo na spishi zilizomo kwa kiwango kikubwa unadumishwa na mioto ya vipindi vya msimu (Rogers, 1996:301). Kiasi cha kilomita za mraba millioni 3 za Afrika zimefunikwa na misitu ya miombo. Katika Bonde la Mto Pangani imeenea zaidi katika maeneo ya mwambao, pande zote mbili za Kaskazini na Kusini mwa mdomo wa Mto Pangani.

Tishio na Hadhi ya HifadhiKwenye Mlima Kilimanjaro, misitu inaendelea kutishiwa kuingiliwa zaidi na zaidi kutokana na uvamizi wa kilimo, ambacho kinatokana na ongezeko la idadi ya watu. Vitisho vingine vya ziada ni ukataji wa miti kwa ajili ya mbao, uanzishwaji wa mashamba ya miti ya mbao laini, moto, uvunaji haramu uliokithiri wa miti ya mbao, ujangili na urinaji haramu wa asali (Yanda na Shishira, 2001). Katika sehemu zote isipokuwa katika mitelemko ya Kaskazini, ukataji haramu wa magogo hufanyika kwa wingi katika maeneo ya msitu yaliyo chini ya mita 2,500, ilikoenea zaidi miti ya kafuri, seda na miti mingine ya asili (Lambrechts et al., 2002). Tishio la ziada ni pamoja na uanzishaji wa ‘vijiji vya misituni’ (ambako viko 18 kwenye eneo la hekta 215) ndani ya hifadhi ya msitu. Mashamba pia yanazidi kuwa ya kawaida katika hifadhi. Mwezi Agosti, mwaka 2001, kulikuwa na matanuru 125 ya mkaa yaliyoonekana katika mitelemko ya Kusini Mashariki ya mlima (Lambrechts et al., 2002). Uchungaji wa mifugo hufanyika kufikia kilomita 8 ndani ya msitu, na katika mwezi Agosti, mwaka 2001 wanyama wafugwao 814 walihesabiwa, wengi wao wakiwa kwenye mitelemko ya Kaskazini ya mlima (Lambrechts et al., 2002).

Kati ya mwaka 1952 na 1982, eneo la misitu ya asili ya Kilimanjaro ilipungua kwa kilomita za mraba 41. Maeneo ambapo awali misitu ya asili ilikuwepo sasa nafasi yake imechukuliwa na kilimo au uoto ulioharibiwa. Kingo za misitu ya hifadhi ndizo zilizoharibiwa vibaya zaidi, (Yanda na Shishira, 2001) hususan kwenye sehemu zijulikanazo kama ‘ukanda wa nusu maili’. Mnamo mwaka 1941, serikali ya kikoloni ilitenga eneo la hifadhi ya msitu wa Kilimanjaro kama eneo la msitu wa kilimo. Ukanda huu umeenea kati ya Mito Kikuletwa na Sanya, na mwendo wa nusu maili kwenda juu ya mlima kutoka kwenye ukingo wa hifadhi. Huu ‘ukanda wa nusu maili’ ulikusudiwa kupandwa miti ikuayo haraka kwa ajili ya matumizi ya jamii za Wachaga waishio chini ya hifadhi, ambako uhaba wa ardhi ulizuia upandaji wa miti (Baldwin, 1946). Leo, kadiri ya asilimia 66 ya maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya mashamba ya misitu yamekuwa ya kilimo au yamesafishwa, (Lambrechts et al., 2002).

Jedwali la 2: Upotevu wa utando wa msitu wa Milima ya Tao la Mashariki katika Bonde la Mto Pangani

Msitu Msitu wa asili Idadi ya Viunga Msitu Upotevu wa tando (km2) vya misitu uliofungwa wa asili wa (km2) msitu (%)

Pare ya Kaskasini 151 2 28 50

Pare ya Kusini 333 5 120 73

Usambara Magharibi 328 17 245 84

Usambara Mashariki 413 8 221 57

Taita 6 13 4 98

Rejea: Newmark, 1998:4) Katika Bonde la Mto Pangani, Milima ya Tao la Mashariki ipo kwenye maeneo yenye msongamano mkubwa wa watu. Katika Milima ya Usambara Magharibi kwa mfano, idadi ya watu imeongezeka kwa mara 23 tangu 1900 (Newmark, 1998). Katika mazingira ya kijamii yenye sifa ya umaskini, umuhimu wa ardhi ya kilimo hauwiani kwa kiasi kikubwa. Shinikizo linalowakilishwa na tatizo hili kwenye hifadhi zilizobaki za misitu katika bonde linatisha. Ikidhaniwa kuwa Milima ya Tao la Mashariki, kihistoria ilikuwa karibu muda wote imejaa misitu, asilimia yake 77 itakuwa imepotea kutokana na shughuli za binadamu na/au moto katika miaka 2,000 iliyopita (Newmark, 1998). Tatizo la ziada ni kuwa mingi ya michakato hii imesababisha kutokea kwa viunga vya misitu, na spishi za wanyama

Page 27: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

mara nyingi haziko tayari kuvuka nafasi wazi kati ya viunga vya misitu. Hii ina maana kuwa katika viunga kimoja kimoja, mkusanyiko wa jeni hupungua na uhai wa spishi huhatarishwa kutokana na kuzaliana wenyewe kwa wenyewe. Katika Bonde la Mto Pangani upotevu huu ni kama inavyoonyeshwa katika jedwali la 2.

Hadhi ya msitu kuwa “msitu wa hifadhi” inaonekana kushindwa kupunguza viwango vya ukataji miti. Katika Hifadhi ya Msitu ya Nilo (hekta 5872.1), katika Milima ya Usambara, kuna hekta 33.8 za ‘kilimo chini ya msitu’, hekta 372.3 za kilimo cha ‘wakulima wadogo wadogo’, hekta 37.2 za ardhi tupu na hekta 1.9 za makazi ya binadamu (Cordeiro, 1998). Misitu ya Pwani ya Tongwe-Muheza ilikuwa na eneo la hekta 1,202, lakini ni hekta 300 tu za msitu zilizobaki, wakati ambapo Hifadhi ya Msitu wa Gombero imefyekwa kabisa kwa ajili ya kilimo (Baker na Baker, 2002).

Kwenye Mlima Meru, matatizo yanayoikabili misitu yanafanana na yale yanayoutishia Mlima Kilimanjaro, nayo ni kama yafuatavyo (Bwoyo, mhojiwa):

• Ukataji haramu wa miti – Misitu ya milimani huvunwa miti inayovutia kibiashara ya mireteni (Juniper) na Mshio (Olea Capensis).

• Malisho – Wakati wa msimu wa kiangazi, jamii za jirani hulisha mifugo yao ndani ya msitu.

• Uhaba wa ardhi – upande wa Mashariki wa mlima, uvamizi wa ardhi ni tatizo kubwa linaloongezeka.

• Kutokuungwa mkono - katika baadhi ya vijiji, mradi wa msitu wa maeneo ya vyanzo vya maji (CFP – utakaoelezwa chini) huungwa mkono kwa kiwango kidogo na viongozi wa vijiji, ambao baadhi yao wanahusika binafsi na uvunaji wa msitu.

• Moto – hili lilikuwa tatizo kubwa kati ya miaka ya 1998 na 1999.

14

Kisanduku cha 4: Tishio kwa Misitu ya Bonde la Mto Pangani

• Mahitaji ya ardhi: kadri msongamano wa watu unavyoongezeka na uchumi unavyobaki kuwa duni, mahitaji ya ardhi ya kilimo huongezeka, na hivyo, misitu hukatwa kutoa nafasi ya kilimo.

• Mahitaji ya mbao: misitu mingi iliyobaki katika PRB ina spishi za mbao zenye thamani ya kiuchumi, ambayo, jinsi inavyoadimika, ndivyo inavyopata bei kubwa. Miti pia hukatwa kwa ajili ya kuni na utengenezaji wa mkaa.

• Mahitaji ya malisho: idadi ya mifugo katika bonde inaonekana kuongezeka. Jinsi ardhi ya kilimo inavyoongezeka, ardhi ya malisho hupungua, na wafugaji hupanda milima kutafuta malisho.

• Makazi ya msituni: kadri watu wanavyojitahidi kutafuta kuongeza ardhi ya kilimo na malisho, hivyo pia hufanya makazi ndani ya mipaka ya misitu.

• Udhaifu wa Sheria: licha ya hadhi ya uhifadhi wa misitu mingi ya bonde, mamlaka haziwezi kutekeleza sheria zinazotakikana kwa sababu ya uchache wa wafanyakazi, mishahara duni na rushwa. Kwa nyongeza, Idara ya Misitu na Nyuki na Mradi wa Misitu ya vyanzo vya maji inapatiwa fedha karibu zote na wahisani pekee, hali inayoibua maswali kuhusu uendelevu wake. Mwisho, ushirikishwaji wa jamii katika usimamizi wa misitu ya bonde ni dhana ngeni na kwa sasa haijawa na ufanisi mkubwa.

• Uendelezaji wa misitu: uendelezaji wa misitu ya mashamba badala ya misitu ya asili huongeza matatizo ya uhifadhi.

• Kugawanyika kwa misitu: Jinsi shinikizo linavyozidi kwenye misitu ya bonde mara nyingi hugawanyika vipande vipande. Spishi nyingi za msituni haziwezi kuvuka nafasi wazi kati ya msitu, na hivyo kusababisha matatizo ya uhifadhi wa bayoanuwai.

• Moto: Kwa kawaida huanzishwa na binadamu ama makusudi (ili kuharibu misitu inayodhaniwa kuhifadhiwa isivyostahili na iliyozuiliwa) au kwa kawaida zaidi, ajali (kwa mfano, kutokana na ajali wakati wa kuchoma mkaa au kurina asali kutoka kwenye mizinga).

Page 28: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

• Fedha – CFP haipati fedha zozote kwa ajili ya kuendeshea shughuli zake kutoka serikalini. Bwoyo (mhojiwa) anadai kuwa kwa sababu ya mchango muhimu wa misitu katika Bonde la Mto Pangani, kiasi cha fedha lazima kitengwe kwa ajili ya CFP kutoka kwa makampuni yazalishayo umeme wa maji au Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani (angalia pia Evans, 1997).

B.3 Maji na ardhioevuMto Pangani unaundwa na matawi ya mito mikubwa miwili: Mto Ruvu, ambao hutokea kwenye miteremko ya Mashariki ya Mlima Kilimanjaro; na Kikuletwa, ambao hutokea kwenye Mlima Meru na mitelemko ya Kusini ya Mlima Kilimanjaro. Mito ya Ruvu na Kikuletwa huungana katika Bwawa la Nyumba ya Mungu, lenye eneo la kadiri ya kilomita za mraba 140 (Rohr na Killingtveit, 2002). Maji yanayoingia katika bwawa yanakaribia kuwa mita za ujazo 43.37 kwa sekunde (TANESCO, 1994). Mto unapotoka kwenye bwawa, huitwa Mto Pangani, na hutiririka kwa kilomita 432 kabla ya kuingia katika Bahari ya Hindi, ambako humwaga maji ya kiasi cha kilomita za ujazo 0.85 kwa mwaka (Vanden Bossche na Beracsek, 1990).

Ndani ya Bonde la Mto Pangani, Mlima Kilimanjaro ndio sehemu yenye umuhimu wa pekee kihaidrolojia(Lambrechts et al., 2002). Kama ilivyoelezwa awali, mvua kwenye mlima huu zinakadiriwa kutoa asilimia 60 ya maji yanayoingia katika Bwawa la Nyumba ya Mungu, na asilimia 55 ya maji ya juu ya ardhi katika Bonde (Rohr na Killingtveit, 2002). Pia, cha muhimu – ingawa kiasi hakijulikani, ni maji yatokanayo na kuyeyuka kwa barafu kutoka milimani. Barafu inayoyeyuka kutoka mlimani huipa nguvu chemchemi kuu katika hifadhi maarufu ya Taifa ya Amboseli nchini Kenya. Myeyuko pia huzipa nguvu chemchemi ambazo mradi wa Ugavi wa Maji wa Nol Turesh ya Kenya hutegemea, unasambaza maji kwenye miji kadhaa mashuhuri ya Kenya, ikiwa ni pamoja na Machakos na Kajiado.

Maji katika Bonde la Mto Pangani kwa kiasi kikubwa hutokana na mvua, ambayo mgawanyo wake hauko sawa ndani ya bonde. Kwa wastani, bonde hili hupata mita za ujazo 34, 773.4 kwa mwaka na kiasi cha wastani cha upoteaji maji kwa uchavushaji ni milimita 1,410 kwa mwaka. Kwa kuzingatia tofauti za mvua, bonde hili, linaweza kugawanywa katika mifumo miwili ya kihaidrolojia.

Maeneo ya nyanda za juu yanachukuliwa kuwa ni yale yaliyoko mita 900 juu ya usawa wa bahari, kama vile mitelemko ya Milima Meru na Kilimanjaro, pamoja na maeneo ya Milima ya Usambara na Pare, ambayo hupata mvua kati ya milimita 1,200 na 2,000 kwa mwaka. Misimu ya mvua huwa miwili katika maeneo haya, nyingi ikiwa kati ya miezi ya Machi na Mei na kidogo kati ya miezi ya Oktoba na Novemba. Mvua katika kipindi cha kwanza inaweza kuzidi milimita 600 kwa mwezi, na milimita 300 katika kipindi kinachofuata.

15

Kisanduku 5: Taarifa za Msingi za Maji na Ardhioevu katika Bonde la Mto Pangani

• Maeneo ya nyanda za juu ya Bonde la Mto Pangani hupata mvua nyingi kuliko nyanda za chini. Hivyo kilimo kinafanyika zaidi kwenye nyanda za juu wakati nyanda za chini zinafaa kwa ufugaji.

• Sehemu kubwa ya maji ya Mto Pangani hutokana na mvua na myeyuko wa barafu.

• Kiasi kikubwa cha maji yanayoingia kwenye Bwawa la Nyumba ya Mungu yanatoka Mlima Kilimanjaro. Yaliyobaki yote yanatoka Mlima Meru na Milima ya Pare Kaskazini.

• Matumizi makuu ya maji katika Bonde hili ni umwagiliaji mashamba. Uzalishaji umeme na uvuvi ni matumizi ya muhimu ya ziada, kama yalivyo mahitaji ya mijini na viwandani.

• Bonde la mto Pangani lina rasilimali kubwa ya maeneo ardhioevu, ikiwa ni pamoja na ziwa Jipe na Chala, na Bwawa la Nyumba ya Mungu. Yote haya husaidia uvuvi. Bonde hili lina rasilimali nyingi za kinamasi, ingawa mchango wake kihaidrolojia na bayoanuwai haujulikani sana.

Page 29: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Juu ya bwawa la Nyumba ya Mungu, kwa ujumla mvua imepungua tangu uwekaji wa kumbukumbu ulipoanza mwanzoni mwa miaka ya 1930. Mfumo wa sasa wa mvua kwa kawaida hutofautiana kwa asilimia 10 kutoka wastani. (Mkhandi na Ngana, 2001).

Maeneo yaliyo chini ya mita 900 hupata mvua kidogo zaidi katika Bonde hili, ikipungua kufikia milimita 500 kwa mwaka (Mkhandi na Ngana, 2001). Kwa hakika asilimia 50 ya Bonde la Mto Pangani inachukuliwa kuwa kame au nusu kame (Rohr na Killingtveit, 2002).

Vyanzo vya ziada vya maji katika bonde hili ni chemchemi. Baadhi ya chemchemi zilizo kubwa katika bonde hili huchangia kadri ya mita za ujazo 20 kwa sekunde za maji yaingiayo bwawa la Nyumba ya Mungu, kiasi ambacho kinakuwa muhimu sana wakati wa kiangazi ambapo mchango wa mvua hupungua (Rohr et al., 2002). Sehemu kubwa ya chemchemi zinazozalisha maji katika Bonde imejikusanya zaidi katika maeneo matatu ya mkoa wa Kilimanjaro: Kambi ya Choka, Rundugai na Chemka (Rohr et al., 2002). Chanzo cha maji ya chemchemi iliyotajwa mwisho haijulikani na kiwango cha maji kitokacho hubaki kuwa sawa kwa mwaka mzima. Mfumo wa mvua kwenye Mlima Kilimanjaro, ambao uko upande wa Kaskazini wa chemchemi, unaonekana kutokuwa na athari yoyote kwenye utoaji wa maji wa chemchemi hiyo (Rohr et al. 2002). Nchini Kenya, Mto Lumi hukusanya maji kutoka mitelemko ya Kusini ya Mlima Kilimanjaro na ndio chanzo kikuu cha maji ya Ziwa Jipe. Karibu maji yote ya mto yanayoingia kwenye ziwa hili yanatoka kwenye chemchemi (Musyoki, 2003).

Kiasi cha asilimia 5 ya maji yote yanayotumika katika Bonde la Mto Pangani yanatoka katika vyanzo vya chini ya ardhi. Visima virefu vitoavyo zaidi ya mita za ujazo 100 kwa saa vimechimbwa kwenye ukanda wa Kahe wakati visima vinavyotoa kati ya mita za ujazo10–50 kwa saa vimechimbwa katika ukanda wa Sanya na Miamba ya Karoo ya Tanga. Uongezekaji wa maji ya chini ya ardhi kwa kiasi kikubwa unatokana na mvua na mito (Makule n.d.).

Mto Pangani unapotoka kwenye Bwawa la Nyumba ya Mungu, hukabiliwa na mahitaji yafuatayo (Mujwahuzi 2001):

Kiasi cha chini kwa kuzalisha umeme ................................mita za ujazo 24 kwa sekunde (Firm Power Production)

Umwagiliaji .........................................................................mita za ujazo 7 kwa sekunde

Matumizi ya nyumbani .......................................................mita za ujazo 1-2 kwa sekunde

Jumla ..................................................................................mita za ujazo 32-33 kwa sekunde

16

Kisanduku 6: Tishio kwa rasilimali za maji na ardhioevu ya Bonde la Mto Pangani

• Ifikapo mwaka 2015, mahitaji ya maji katika Bonde hili yanatarajiwa kuwa mara mbili, wakati huo huo kuna ushahidi uhaba wa maji umekuwepo tangu miaka ya 1940.

• Maeneo muhimu ya matatizo ni ongezeko la mahitaji ya umwagiliaji na mijini. Katika umwagiliaji, upotevu wa maji unaweza kufikia kiasi cha asilimia 85.

• Kadri idadi ya watumiaji maji inavyoongezeka, pamoja na ushindani baina yao, kuna uwezekano wa migogoro baina ya watumiaji maji kuongezeka.

• Uvuvi katika Bwawa la Nyumba ya Mungu unasemekana kuwa katika matatizo makubwa kutokana na uvuvi uliokithiri.

• Sehemu kubwa ya eneo ardhioevu kubwa zaidi katika Bonde hili - Kinamasi cha Kirua – imekauka kutokana na utaratibu wa mtiririko wa maji yanayotoka kwenye Bwawa la Nyumba ya Mungu kudhibitiwa.

• Kiasi kikubwa cha virutubisho vinavyoingia kwenye Ziwa Jipe vimestawisha kwa wingi mafunjo na Typha ambazo zinatishia kulifunika ziwa.

Page 30: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Hata hivyo, Sarmett (Mhojiwa) anaeleza kuwa, ni mara chache sana Nyumba ya Mungu huwa na uwezo wa kutoa mita za ujazo 22 kwa sekunde.

Bwawa la Nyumba ya Mungu ndiyo hifadhi kubwa zaidi ya maji katika bonde hili. Nyingine tatu zilizopo ni: ziwa Ambusseli, na maziwa Chala na Jipe yaliyoko mpakani mwa Tanzania na Kenya. Maziwa haya huonekana mara nyingi kwenye mipango ya umwagiliaji na ya kihaidrolojia ya wilaya ya Taita -Taveta ya Kenya. Usawa wa maji ya Ziwa Jipe na eneo lake hubadilika kwa kiwango kikubwa kutokana na kiasi cha mvua. Hivyo, eneo lake hutofautiana kutoka kilomita za mraba 28 (1947) hadi kilomita za mraba 18 (1954), wakati kiasi cha maji yaliyomo hutofautiana kutoka mita za ujazo milioni 20 hadi 60, (Musyoki na Mwandotto, 1999). Ndani ya Kenya sehemu ambayo ni chanzo cha maji ya Ziwa Jipe kuna sehemu ya Mbuga ya Taifa ya Tsavo Magharibi, kilomita za mraba 48.5 za kinamasi, kilomita za mraba 435 za mashamba ya mkonge na kilomita za mraba 196.5 za kile kinachoelezwa kuwa ni ‘ardhi ya umma’ iliyotengwa kwa ajili ya Mpango wa Makazi wa Ziwa Jipe (Musyoki na Mwandotto 1999). Kiasi cha mchangatope unaokadiriwa kufikia tani 300,000 huingia kwenye ziwa kwa mwaka (Musyoki, 2003).

Ziwa Chala liko kwenye kreta ndogo ya volkano ya miteremko ya kusini ya Mlima Kilimanjaro. Lina kina cha kati ya mita 85 na 90 na lina eneo la kiasi cha kilomita za mraba 3.15. Lina kiasi cha maji ya kati ya mita za ujazo milioni 300-350 (Musyoki na Mwandotto 1999). Kwa ubora, maji yake ni mzuri sana, na kwa sababu hii yanaonekana kuwa ndiyo chanzo cha ukuaji wa maeneo ya miji ya pwani ya Kenya. Viwango vya matumizi ya maji kwa siku zijazo vinatazamiwa kufikia mita za ujazo 7 kwa mwaka (Musyoki, 2003). Hali yake ya mwinuko inamaanisha kuwa maji yanaweza kusafirishwa kwa nguvu ya mteremko hadi yanakotakiwa.

Bonde la Mto Pangani linadhaniwa kuwa na hekta 90,000 za kinamasi, sehemu yake kubwa ikiwa ni Kinamasi ya Kirua iliyopo Kusini mwa Bwawa la Nyumba ya Mungu. Vinamasi hivi tayari vimekwisha athirika kwa kiasi kikubwa kutokana na udhibiti wa mtiririko wa maji ya mto kutoka bwawani, na maeneo makubwa ya kinamasi yamekauka. Hata hivyo, bado yanadhaniwa kuhifadhi kiasi kikubwa cha maji ya Mto Pangani. Laiti kama Mto ungeelekezwa njia na mfereji kuchimbwa kupitia kwenye kinamasi, ongezeko la mita za ujazo milioni 42.4 zingeyafikia mabwawa yaliyoko upande wa chini ya mto kwa mwaka (IVO - NORPLAN,1997). Uoto wa ardhi hizi za kinamasi umeelezewa juu kuwa ni mifano ya misitu ya kandokando ya mito.

Ardhi nyingine ya Kinamasi ni Ruvu (karibu kilomita za mraba 35) ambayo iko mahali Mto Ruvu unapotoka kwenye Ziwa Jipe, na kinamasi iliyopo mahali mito ya Ruvu na Kikuletwa inapokutana na kuingia Nyumba ya Mungu. Eneo la kinamasi lililotajwa mwisho linasemekana kuwa na kilomita za mraba 40 (Baker na Baker 2001).

Tishio na hadhi ya HifadhiKatika sehemu ya Bonde iliyoko Tanzania, makisio na matarajio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na 2015 yanaonyeshwa kwenye Jedwali la 3.

Katika Wilaya ya Taita – Taveta iliyoko katika sehemu ya bonde upande wa Kenya, mahitaji ya maji yanakadiriwa kufikia mita za ujazo 5,625 kwa siku. Hadi kufikia mwaka 2005 mahitaji yanatazamiwa kuongezeka kufikia mita za ujazo 8,844 kwa siku, na kufikia mita za ujazo 12,521 kwa siku ifikapo mwaka 2015 (Mpango wa Maji wa Wilaya ya Taita – Taveta wa mwaka 1995, kama inavyonekana katika Musyoki, 2003). Kutokana na mahitaji ya maji kukadiriwa kuwa mara mbili itakapofika mwaka 2015, shinikizo kwa rasilimali za maji katika bonde linafikiriwa kuwa kubwa mno. Tayari bonde linachukuliwa kuwa lina matumizi makubwa ya maji, na kwa kukosekana msisitizo wowote mkubwa wa udhibiti hadi sasa, inaonekana hakuna uwezekano wa tishio hili kupungua.

17

Page 31: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji mwaka 1995 na matarajio ya mahitaji ya maji mwaka 2015

Mahitaji ya maji m3/siku

Matumizi 1995 2015

Mijini 71,200 163,600

Vijijini 52,000 83,500

Mifugo 30,500 36,400

Mkonge 1,300 1,300

Jumla 155,000 284700

(Rejea: IVO- NORPLAN, 1997)

Upo ushahidi wa kutosha wa matatizo ya maji. Mujwahuzi (2001) anabainisha kuwa katika kituo 1DC1 cha Mto Ruvu, wastani wa mtiririko wa maji kwa mwezi umepungua kutoka mita za ujazo 14.2 kwa sekunde kati ya mwaka 1958 – 65 hadi mita za ujazo 11.45 kwa sekunde kati ya mwaka 1987-97. Vijito vingi katika nyanda za juu za bonde havitiririshi maji wakati wa msimu wa kiangazi (mwezi Septemba hadi Februari) kwa sababu ya wingi wa shughuli za umwagiliaji. Baada ya maji kuchukuliwa kwa ajili ya umwagiliaji, Mto Rau hukauka kabisa (Mujwahuzi 2001). Mahitaji ya maji kutoka kwenye mito ya Kikafu na Weruweru huwa ni kati ya asilimia 90 –125, ambayo ni makubwa zaidi ya kiasi cha maji kinachopatikana kwa uhakika mtoni cha asilimia 80. (Mwamfupe, 2002). Maji yanayotoka katika Bwawa la Nyumba ya Mungu, huchepushwa kwa matumizi mbalimbali kabla ya kufika kwenye maporomoko ya Pangani. Mara nyingi na hususan wakati wa kiangazi, maji yanayofika hayatoshelezi kuendesha mitambo ya kituo cha umeme wa maji iliyopo hapo (Lugeiyamu, Mhojiwa). Ushahidi wenye nguvu sana wa tatizo la maji unaweza kuwa ni ongezeko la idadi ya migogoro inayohusiana na maji katika bonde hili. Migogoro hii inaangaliwa kikamilifu hapa chini.

Kati ya mwaka 1992 na 1989, eneo la kilele cha barafu cha Mlima Kilimanjaro lilipungua kwa asilimia 75 kutoka kilomita za mraba 12.5 hadi kilomita za mraba 2.6. Kati ya mwaka 1989 hadi 2000 karibu robo ya barafu iliyosalia ilitoweka. Kuhusu sababu ya badiliko hili la ghafla na haraka, lawama zinaelekezwa katika shughuli za binadamu, ingawa hili kwa vyovyote haliko dhahiri (Hastenrath na Greischar, 1997). Kama upunguaji huu utaendelea Bonde la Mto Pangani hivi karibuni litakoma kupata maji yatokanayo na kuyeyuka kwa barafu.

Ukuaji wa magugu aina ya Typha kwenye Ziwa Jipe unasemekana kutodhibitiwa vya kutosha kiasi kwamba magugu haya yamekaribia kufunika ziwa. Mwelekeo huu ni dhahiri umetokana na virutubisho na mchangatope unaochukuliwa na maji kutoka kwenye Mlima Kilimanjaro na Milima ya Pare Kaskazini. Mchangatope umepunguza kina cha Ziwa na kusababisha kupanda kidogo kwa usawa wa maji. Uingiaji wa virutubisho kwenye ziwa unadhaniwa kusababisha ongezeko la alikali na/au magadi na kusababisha mayungiyungi kutoweka. Uingiaji wa mchangatope pia huathiri bwawa la Nyumba ya Mungu, lakini hili si tatizo kwa sasa kutokana na bwawa kuwa na eneo kubwa la kuhifadhi maji.

Kama ilivyojadiliwa awali, udhibiti wa Mto Pangani umepunguza mafuriko katika kinamasi ya Kirua, na hivyo maeneo makubwa ya kinamasi kukauka. Kwa kiasi cha utoaji wa maji cha mita za ujazo 25 kwa sekunde kutoka NYM, kinamasi kinafurika, lakini wakulima waliovamia ardhi hii hulalamika vikali (Ngula, Mhojiwa). Bwawa la Nyumba ya Mungu husaidia uvuvi ambao hufanyika kwa kiwango kikubwa, kama itakavyojadiliwa zaidi chini.

18

Page 32: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

B.4 Maeneo YaliyohifadhiwaKatika Tanzania, Bonde la Mto Pangani lina hifadhi moja ya akiba ya wanyamapori (Mkomazi – kilomita za mraba 3,276), wakati sehemu za Hifadhi za Taifa za Kilimanjaro (kilomita za mraba 756) na Arusha (kilomita za mraba 137) pia zipo katika bonde hili. Sehemu ya Mbuga ya Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Magharibi nchini Kenya (kilomita za mraba 9,065) pia inaangukia katika bonde hili, na inapakana na hifadhi ya akiba ya Wanyamapori ya Mkomazi. Sehemu ya Hifadhi ya Taifa ya Sadani iko katika bonde hili, lakini haitajadiliwa hapa. Kihoja, hifadhi za misitu pia ni maeneo yaliyohifadhiwa, lakini haya hayajadiliwi hapa (angalia juu). Zote hizi zina mchango wenye thamani kwa uchumi wa Tanzania kwa kuvutia watalii. Kilimanjaro pekee hupokea wageni wapatao 67,000 kwa mwaka (WCMC, 1987).

Mlima Kilimanjaro ni mlima mrefu zaidi uliosimama wenyewe duniani na mrefu zaidi kuliko yote katika Afrika. Una mwinuko wa mita 5,000 juu ya uwanda wazi wenye milima na mabonde wa wastani wa mita 800 juu ya usawa wa bahari (Lambrechts et al., 2002). Mbuga hii ni eneo lililohifadhiwa zamani zaidi katika Afrika, likiwa limepata hadhi hii mwanzoni mwa karne ya 20. Mnamo mwaka 1921 mbuga hii ilitangazwa kuwa hifadhi ya msitu, na kisha, katika mwaka 1973, eneo lililo juu ya mita 2,700 za kontua, lilipewa hadhi ya Hifadhi ya Taifa. Kwa sasa, mbuga hii ina eneo la hekta 75,353 na imezungukwa na hekta 107,828 za hifadhi ya misitu (Lambrechts et al,2002). Mnamo mwaka 1987 Mbuga ya Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro iliwekwa katika orodha ya maeneo ya Urithi wa Dunia, ikiwa eneo la saba la Tanzania la Urithi wa Dunia (Lambrechts et al.,2002).

Hifadhi ya akiba ya Wanyamapori ya Mkomazi ni mwendelezo wa Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Magharibi ya Kenya. Kama zilivyo Hifadhi za Taifa za Tsavo na Arusha, Mkomazi ipo katika mpango wa kituo cha uendelezaji wa wanyama cha ukanda wa Somali – Masai (Somali – Maasai Regional Centre of Endemism, RCE). Inatanda toka mpakani mwa Tanzania na Kenya hadi chini ya milima ya Pare na Usambara Magharibi. Hifadhi hii ina tabia ya misitu ya savana, na mpaka mwaka 1988, wafugaji kutoka makabila mbalimbali waliruhusiwa kunufaika na malisho yake. Homewood na Brockington (1999) wanaeleza kuwa ingawa hifadhi hii ina manufaa makubwa kwa Tanzania kwa kuwa na hazina kubwa ya bayoanuwai umuhimu wake umefunikwa kwa kiasi kikubwa na kanda nyingine zenye hazina kubwa zaidi za bayoanuwai, bila kusahau Milima ya Pare na Usambara. Keith Eltringham et al., (1999) alibainisha kuwepo kwa spishi 102 za wanyama wanaonyonyesha (mamalia) ndani ya Mkomazi, wakiwemo Faru weusi walioletwa tena hivi karibuni.

Mbuga ya Taifa ya Arusha iko kwenye kingo za Mlima Meru (mita 4,565) na ilianzishwa mwaka 1967. Mbuga ina mazingira ya aina nyingi mbalimbali, mifano mizuri ni pamoja na misitu ya milimani kwenye Mlima Meru, Maziwa ya Kreta ya Momela na nyanda za chini za nyika za savana na misitu ya miombo. Orodha ya ndege waliopo katika mbuga hii ina spishi 400, na ni moja ya mbuga chache za Tanzania ambazo mbega weusi na weupe huonekana kwa kawaida. Mbuga hii inapakana na Hifadhi ya akiba ya Wanyama ya Mlima Meru yenye eneo la kilometa za mraba 300. Mbuga ya Hifadhi ya Taifa ya Arusha inaaminika kuwa na msongamano mkubwa zaidi wa twiga duniani.

Barabara kuu ya Nairobi-Mombasa hutenganisha Mbuga za Hifadhi za Tsavo Magharibi na Tsavo Mashariki. Hifadhi hizi zilizoanzishwa mwaka 1948, kwa pamoja zinaunda mbuga ya hifadhi ya Taifa kubwa kuliko zote nchini Kenya, na moja ya maeneo makubwa zaidi yaliyohifadhiwa duniani. Mnamo mwaka 1983, mipaka ya Kaskazini Magharibi ya hifadhi ya Tsavo Magharibi ilipanuliwa na kuchukua vilima vya Chyulu ambavyo ndivyo chanzo kikuu cha chemchemi za Mzima ambazo ni maarufu katika mbuga hii. Lita milioni 225 za maji hububujika kutoka kwenye chemchemi hizi kila siku, ambayo huipatia maji Mombasa, jiji la pili kwa ukubwa nchini Kenya. Zaidi ya watu 150,000 hutembelea Tsavo Magharibi kila mwaka. Sura ya makunyanzi ya hifadhi hii ilisababishwa na milipuko ya zamani ya volkano, iliyoacha mikondo ya mtiririko wa lava yake, maeneo ya vipande vya lava na pia koni ndogo ndogo za volkano. Mbuga hii ina idadi kubwa zaidi ya tembo walioko Kenya. Eneo la mbuga la Ngulia limekuwa moja ya maeneo muhimu sana nchini Kenya ya hifadhi ya faru. Milima ya miamba iliyoko Ngulia ndiyo kituo muhimu cha mapumziko kwa ndege wahamaji wanaotoka katika Kizio cha Kaskazini, ambao wengi wao ni adimu sana.

19

Page 33: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Tishio na hadhi ya HifadhiMwishoni mwa miaka ya 1980, Idara ya Wanyamapori nchini Tanzania iliona Mkomazi kuwa ni eneo lililoishiwa na mimea na wanyama. Miongoni mwa matatizo yaliyoikabili mbuga ilikuwa kutoweka kwa faru. Katikati ya miaka ya 1960 kulikuwa na takriban faru 150 katika hifadhi hii, lakini spishi hii ilimalizwa, hasa kutokana ujangili. Mnamo mwaka 1997 faru waliletwa tena kwenye hifadhi hii (Keith Eltringham et al., 1999) pamoja na mbwa mwitu. Hali ya mbuga hii kuwepo jirani na mpaka wa Kenya inaleta tishio la ujangili.

Kilimanjaro haionekani kukabiliwa na tishio la aina hii la ujangili. Hapa, tishio lipo hasa kwenye mipaka ya hifadhi ya misitu, ambako ukataji miti, kilimo, ukusanyaji wa kuni na uchomaji wa mkaa umeshamiri. Tatizo la ziada kwenye mbuga hii ya hifadhi ya taifa ni idadi kubwa ya wageni wanaoitembelea, ambao huacha takataka nyingi , ambazo haziwezi kuoza katika hewa nyepesi na baridi sana ya mlimani.

Maeneo yanayozunguka Mbuga ya Taifa ya Arusha yana idadi kubwa ya watu na inasemekana mbuga inakabiliwa na tishio la kuingiliwa na shughuli za binadamu na kiwango kikubwa cha ujangili (WCMC, 1985).

Mbuga ya Taifa ya Tsavo Magharibi inakabiliwa na matatizo makubwa ya ujangili. Uuaji wa tembo katika mbuga siku zilizopita mara nyingi ulikuwa ukielezewa mfululizo katika vyombo vya habari. Zaidi ya hayo, mbuga hii iko katika ukanda wa ukame na hali ya hewa inayobadilika badilika, hali inayoifanya mbuga hii kuwa katika hatari ya moto. Mioto pia ni tatizo katika Mlima Kilimanjaro, kama ilivyojadiliwa hapo juu.

Rasilimali nyingine za wanyamapori pia hupatikana katika bonde zima, wakiwemo wengi wa wanyamapori wanaopatikana katika misitu ya milima ya Tao la Mashariki na ile ya Pwani. Tishio kwa msitu huu uliotajwa mwisho ni kubwa sana (angalia chini). Katika nyika za Masai za uwanda wa chini wa bonde, wanyama wenye kwato hupatikana, wakati mto na maeneo ardhioevu mengine yana hazina ya wanyama pori pia.

B.5 Bayoanuwai na hifadhiKenya na Tanzania zina utajiri mkubwa wa rasilimali za bayoanuwai. Kulingana na idadi ya spishi kwa eneo, Kenya ina kiwango cha juu cha tatu kwa mamalia anuwai katika Afrika, cha pili kwa ndege anuwai na cha tatu kwa reptilia anuwai.

Tanzania ina kiwango cha juu cha pili kwa reptilia, amfibia na mimea anuwai katika bara la Afrika (Rodgers et al., 2001). Misitu ya Tao la Mashariki na ile ya Pwani ni moja kati ya ‘sehemu 25 zenye umuhimu mkubwa kwa bayoanuwai’ duniani. Bayoanuwai na upatikanaji wa spishi adimu zinazohusiana nazo katika milima hii hazina mfano wake duniani. Kadri ya asilimia 30 ya spishi za mimea kama 2000 hivi na zaidi ya asilimia 80 ya makundi ya buibui na majongoo hupatikana katika milima hii pekee. Mimea maarufu ya urujuani (Saintpaulia) inatipakana kiasili katika misitu ya Milima ya Tao la Mashariki na Pwani pekee.

Walau spishi nne za mamalia, tano za ndege, nne za amfibia, ishirini na saba za watambazi (reptilia), arobaini za vipepeo, ishirini za majongoo, mia nne za mimea na idadi isiyojulikana ya nzi, aina za mende na wanyama wengine wasio na uti wa mgongo hupatikana katika misitu ya pwani ya Afrika Mashariki pekee (Burgess et al., 1996). Kiwango hiki cha uadimu kimetokea kwa sababu ya kujitenga kwa misitu hii na misitu mingine ya Afrika, kuwepo kwake kwa miaka mingi na ukweli kwamba hali ya hewa ya Bahari ya Hindi imebaki thabiti bila mabadiliko kwa muda mrefu sana.

20

Kisanduku cha 7: Tishio kwa Maeneo yaliyohifadhiwa ya Bonde la Mto Pangani

• Sehemu kubwa ya mbuga katika Bonde la Mto Pangani ziko katika tishio la ujangili.

• Hatari zinazoikabili Mbuga ya Taifa ya Kilimanjaro zinahusiana zaidi na kuingiliwa katika hifadhi yake ya misitu na uvuniaji wa mbao.

• Idadi kubwa ya watalii katika Mlima Kilimanjaro husababisha matatizo makubwa ya utupaji hovyo na kiasi kikubwa cha taka, kwani takataka huganda na haziozi

Page 34: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Matokeo yake, vitishio ambavyo vinakabili nyingi ya spishi hizi vinahusiana na uhifadhi wa mazingira yao. Kwa kuwa sehemu kubwa ya misitu ya Tao la Mashariki na ile ya Pwani iko hatarini, spishi zake nyingi za wanyama ziko hatarini (angalia kisanduku hapo chini).

Katika Mlima Kilimanjaro spishi za mimea 2,500 zimetambuliwa, zikiwemo spishi 130 za miti kutoka jenasi (spishi zenye sifa zinazofanana) 100 na jamii 50. Spishi 170 za vichaka zimetambuliwa kutoka misitu ya milima huu, na hii iko kwenye zaidi ya jenasi 100 na jamii 40 (Lambrechts, et al., 2002). Spishi 140 za mamalia zimetambuliwa kuwepo mlimani, ikiwemo kundi kubwa zaidi linalojulikana duniani la mindi (Abbot’s duiker), spishi iliyo hatarini sana ulimwenguni (Lambrechts et al., 2002). Mbuga hii ina panya wadogo wapatikanao katika eneo hili pekee, spishi nne na spishi ndogo za vipepeo zipatikanazo kipekee, mimea ya aina 6 ya kipekee, kuvumwani kumi na mbili wanaopatikana eneo hili pekee na mmea aina ya liverworts (Baker na Baker, 2001).

Papa dume (Carcharrhinus leucas) walio adimu na hatarini mara chache huogelea kuelekea juu katika Mto Pangani kutoka kwenye delta zake, na wameonekena katika mkondo wake kuelekea juu hadi Jambe (TANESCO, 1994). Hata hivyo, mbali na papa, hakuna spishi zozote kati ya 41 za samaki wa mto huu, zinazofikiriwa kuwa hatarini. Kuna spishi kadhaa zilizoko kwa wingi kukiwa na samaki wa aina mbili za “cyprinids” (Barbus paegnstecheri na Labeo coubie), aina moja ya “characin” (Rhabdalestes leleupi) na aina tatu za “cichlids” (Ctenochromis pectoralis, Oreochromis korogwe na O. pangani) (TANESCO, 1994).

Jenasi ya perege, Oreochromis, imepata jina lake kutoka lugha ya kilatini la Mlima ‘Chromis’ ambalo Gunther aliipa mwaka 1889 baada ya kugundua Orechromis hunterti katika Ziwa Chala, lililopo kwenye miteremko ya Mlima Kilimanjaro (Dadzie et al, 1988). Kwenye Ziwa Jipe aina mbili za ziada za perege walio adimu zinapatikana: Perege jipe na perege girigan. Orechromis esculentus wanaopatikana katika Ziwa Victoria pekee4, wamepandikizwa katika Bonde, na wamekuwa ni sehemu kubwa ya samaki wanaovuliwa kutoka Bwawa la Nyumba ya Mungu. Perege wa ziada wa kigeni, T. rendalii, wamevuliwa kutoka Ziwa Chala.

Tishio na hadhi ya HifadhiTishio kuu linalokabili bayoanuwai ya Bonde la Mto Pangani linahusiana na uharibifu wa makazi. Kiwango cha juu sana cha wingi wa bayoanuwai huendana na viwango vya juu vya upekee na anuwai za makazi katika bonde, hususan misitu yake ya milima ya Afrika na ya pwani. Kwa mfano, karibu spishi zote za ndege zinazopatikana katika bonde hili pekee, pia huchukuliwa kuwa spishi za eneo hili tu, na hivyo kuwa hatarini zaidi kudhuriwa kutokana na uharibifu na kugawanyika kwa makazi.

21

Kisanduku cha 8: Sehemu zenye umuhimu mkubwa wa bayoanuwai

Sehemu zenye umuhimu mkubwa wa bayoanuwai huteuliwa na Shirika la Hifadhi la Amerika, Conservation International. Ni maeneo ambayo yana aina mbali mbali za spishi duniani, lakini ambayo wakati huo huo, yameathiriwa na kubadilishwa sana na shughuli za binadamu. Mimea anuwai ndiyo kigezo cha uteuzi wa maeneo hayo, kwa kuwa mimea ni msingi wa anuwai katika kuainisha kisayansi makundi mengine. Ili kustahili hadhi hii, lazima eneo liwe na walau spishi 1,500 za mimea inayopatikana katika eneo hilo pekee, kwa ukamilifu asilimia 0.5 ya jumla ya mimea inayojulikana ulimwenguni. Kwa nyongeza, asilimia 70 au zaidi ya makazi ya asili ya eneo hilo lazima yawe yameharibiwa au kubadilishwa.

Kati ya hizo, sehemu 25 zenye umuhimu mkubwa zaidi wa bayoanuwai duniani zinachukua asilimia 1.4 tu ya eneo la dunia, lakini zina asilimia 44 ya mimea inayojulikana duniani, na asilimia 35 ya wanyama wote wenye uti wa mgongo wanaojulikana duniani.

Sehemu hizo muhimu mara nyingi ni ‘visiwa’ vya bayoanuwai vilivyozungukwa na maeneo ya bayoanuwai duni kiasi. Kama ilivyo kwa Milima ya Tao la Mashariki, maeneo haya kiasili yamepata bayoanuwai yake kama matokeo ya hali za mazingira ambazo hazikubadilika kwa kipindi kirefu.

Mbali na sehemu za umuhimu mkubwa wa bayoanuwai za Misitu ya Tao la Mashariki na ile ya Pwani, kuna sehemu nyingine nne za namna hiyo katika Afrika. Madagascar na visiwa vya Bahari ya Hindi, Misitu ya Guinea ya Afrika ya Magharibi, Jimbo la Cape maarufu kwa maua na Karoo zenye utomvu katika pwani ya kusini magharibi ya Afrika.

4Katika hali ya mabadiliko ya kushangaza, spishi hii sasa imetoweka kabisa katika Ziwa Viktoria

Page 35: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Hofu ya uharibifu wa makazi haya ya msitu yenye thamani imefanya misitu ya pwani ya Tanzania na Milima ya Tao la Mashariki ipate uangalizi wa Kimataifa. Hakika yote ina hadhi ya Eneo Muhimu la Ndege (IBA) (Baker na Baker, 2001), inayowezesha kulenga uangalizi wa Hifadhi ya Kimataifa kwenye hii mifumo ikolojia ya kupendeza na nyepesi kudhuriwa. Hata hivyo, ni misitu michache sana ya Tao la Mashariki au ya Pwani katika bonde ambayo siyo hifadhi ya misitu.

B. 6 UvuviSamaki mara nyingi ni chanzo muhimu cha protini ya wanyama kwa jamii za vijijini za Afrika. Mwaka 1970, uvuvi katika bwawa la Nyumba ya Mungu ulikimu wavuvi 3,161, ambao walivua tani 28,509 za samaki kwa ujumla wao. Kufikia mwaka 1983, kulikuwa na wavuvi 1,342, ambao waliweza kupata tani 2,430 za samaki (Vanden Bossche na Bernacsek, 1999).

22

Kisanduku cha 9: Kundi la 1 la spishi za ndege wa Milima ya Usambara lililo hatarini

Walio hatarini sana

• Mbayuwayu mwenye mdomo mrefu (Orthotomus moreaui): hawakujulikana mpaka mwaka 1931 na bado ni spishi inayojulikana kidogo

Wasio salama (wenye kuweza kudhuriwa)• Bundi wa Sokoke (Octus ireneae): waligunduliwa mnamo mwaka 1965 katika msitu wa Arabuko-

Sokoke ya pwani ya Kenya, ambapo ilichukuliwa kama spishi inayopatikana hapo pekee mpaka kundi lingine lilipogunduliwa katika milima ya Usambara mnamo mwaka 1995.

• Bundi Tai wa Usambara (Bubo vosseleri): Waligunduliwa kati ya misitu ya uwanda wa chini wa Usambara katika mwaka 1992, baada ya kufikiriwa kama ndege wa msongamano mdogo wa mwinuko wa juu hapo awali.

• Zuwanende bakajeupe/kirumbizi (Swynnertonia Swynnertoni): aligunduliwa katika Usambara pekee mnamo mwaka 1990.

• Zuwanende wa pwani ya Mashariki (Shepperdia gunningi): aligunduliwa katika milima ya Usambara mnamo mwaka 1992.

• Zuwanende mabaka meusi wa milimani (Modulatrix orostruthus): uadimu wake katika milima ya Usambara ya Mashariki huenda ni matokeo ya kugawanyika vipande vipande kwa mistiu.

• Chozi wa Amani (Hedydipna pallidigaster): alielezwa kwanza na Sclater na mtaalamu maarufu wa elimu ndege, Moreau, katika mwaka 1935, ndege huyu mdogo sana anafahamika kutoka sehemu tatu tu za Afrika Mashariki. Katika milima ya Usambara, ni eneo la kilomita za mraba 320 tu la makazi yanayofaa ndiyo limebaki (Cheke et al., 2001).

• Chozi mwenye mistari (Anthreptes rubritorgues): anajulikana kutoka sehemu nne tu katika Tanzania. Makazi yake makubwa zaidi ni milima ya Udzungwa.

• Kwera wa Usambara (Ploceus nicolli): kwera hupatikana katika milima ya Usambara pekee ambako, Zimmerman et al., (1996) anakadiria wamebaki chini ya 100.

Walio hatarini kidogo:• Tai-miraba kusi (Circaetus fasciolatus): Awali alidhaniwa kuwa mkazi wa kawaida katika misitu

ya pwani inayotanda kutoka Kaskazini Mashariki ya Kenya hadi Kaskazini Mashariki ya Afrika ya Kusini. Sasa anafikiriwa kutishiwa na msongamano wa binadamu na matumizi yaliyokithiri ya misitu ambayo ni makazi yake makuu. Makadirio ya jozi moja kwa kilomita za mraba 100 yanabaki katika kiwango hicho (Ferguson-Lees na Christie, 2001).

• Kulukulu (Tauraco fischeri); kwa kawaida hupatikana msituni pote. Anatishiwa na biashara ya Kimataifa ya ndege mwitu.

Page 36: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Typha na mafunjo hutanda karibu katika nusu ya uso wa Ziwa Jipe, na karibu yakwamishe shughuli za uvuvi upande wa Tanzania wa ziwa (Sarmett na Kamugisha, 2002). Kwa upande wa Kenya wa Ziwa Jipe, wanavijiji 200 katika vijiji vitatu wanasemekana kutegemea uvuvi wa ziwani. Mbali na matatizo yanayohusiana na magugu maji, ziwa kujaa mchangatope pia ni tishio kwa uvuvi (Musyoki, 2003).

Wanavijiji wanaoishi kuzunguka Kinamasi ya Kirua chini ya bwawa la Nyumba ya Mungu wanalalamikia upungufu wa samaki kutokana na taratibu za kudhibitiwa mtiririko wa maji kutoka bwawani (Sarmett na Kamugisha, 2002).

B.7 UdongoSehemu kubwa ya Bonde la Mto Pangani ina safu ya jiolojia ya fuwele na mawe ya chokaa, pamoja na viunga vya mashapo kutoka ziwani. Karibu zaidi na pwani, jiolojia ni ya mashapo ya katika mlango wa mto. Maeneo karibu na Mlima Meru na Mlima Kilimanjaro kwa asili ni Volkano za alikali zenye rutuba nyingi (Geological Survey, 1960). Mchanganyiko huu wa udongo wenye asili ya ziwa na ile ya volkano, na vilevile maeneo yenye wastani wa juu wa mvua kwa mwaka umezifanya sehemu za Bonde la Mto Pangani kuonekana kama eneo zuri la uzalishaji chakula nchini Tanzania.

Matatizo makuu kuhusiana na udongo wa Bonde la Mto Pangani ni kupungua kwa rutuba ya ardhi, na upotevu wa udongo kutokana na mmomonyoko. Stoorvogel na Smaling (1990) walikadiria kuwa ardhi inayofaa kwa kilimo katika Tanzania hupoteza kilogramu 27 za Naitrojeni, kilogramu 9 za Fosfeti na kilogramu 21 za Potasiamu kwa hekta kwa mwaka kwa mwaka 1983. Walikadiria kwamba ikifikia mwaka 2000, viwango hivi vya upotevu vitaongezeka na kufikia kilogramu 32 za Nitrogen, kilogramu 12 za Fosfeti na kilogramu 25 za Potasiam ikiwa upotevu wa virutubisho ulioonekana mwaka 1983 haukubadilika. Kwa naitrojeni na fosforasi, viwango hivi vya upotevu ni sawa na tani 251,448 na tani 115,1122 kwa mwaka. Stoorvogel na Smaling walieleza kuwa upotevu huu ulitokana na mambo matatu: kwanza uvunaji wa kawaida wa mazao ambapo virutubisho vingi hupotea. Pili, uondoaji wa mabaki ya mazao. Kwa mfano, maharage yanapovunwa katika wilaya ya Arumeru mkoani Arusha, mmea mzima unang’olewa toka ardhini. Tatu, kutokana na mmomonyoko, hususan kutokana na kilimo katika mitelemko mikali (Kaihura et al. 2001). Ifahamike kwamba si kilimo chote katika Bonde la Mto Pangani ni cha kiharibifu (Kaihura et al. 2001).

B.8 Majumuisho ya hojaRasilimali za Bonde la Mto Pangani zinatumika kwa kiwango kikubwa sana. Katika sehemu hii, kwanza tunatoa muhtasari wa mchango muhimu unaotolewa na rasilimali hizi katika bonde na katika sehemu ya pili, tunatoa muhtasari wa hatari zinazozikabili.

Rasilimali za Bonde la Mto Pangani• Misitu ina mchango muhimu sana katika haidrojia ya bonde, inarekebisha kasi ya maji, kupunguza

mmomonyoko, kuhifadhi na kusafisha maji. Misitu iliyopo Bonde la Mto Pangani inatoa mchango muhimu kwa bayoanuwai ya ulimwengu. Katika misitu ya bonde hili baadhi ya spishi za kiwango cha juu cha upatikanaji kwa wingi ulimwenguni na bayoanuwai hupatikana.

• Maji katika Bonde la Pangani ni ya muhimu kwa uchumi wa kilimo wa bonde, uzalishaji wa umeme, maendeleo ya miji, mahitaji ya viwandani na majumbani, na kwa ajili ya mifugo. Vinamasi pia katika bonde huchangia sana katika hifadhi na urekebishaji mwenendo wa maji.

• Bonde hili lina maeneo manne yaliyohifadhiwa. Kilimanjaro, kipekee ina mchango muhimu katika uchumi wa taifa kutokana na utalii, na pia huhifadhi spishi nyingi ya mimea na wanyama.

• Bayoanuwai ya bonde hili kwa kiasi fulani haina mfano ulimwenguni, na ni eneo la shughuli nyingi za Kimataifa za masuala ya hifadhi.

23

Page 37: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

• Uvuvi katika Bonde la Pangani unatoa mchango muhimu wa chakula na kiuchumi kwa jamii za vijijini katika bonde.

• Ardhi ndiyo msingi mkuu wa uchumi wa kilimo wa bonde hili. Historia ya mlipuko wa volkano ya eneo hili na viunga vya mashapo ya mto yenye rutuba, huchangia katika umaarufu wa Bonde la Mto Pangani kuwa eneo la kutegemewa kwa uzalishaji chakula nchini Tanzania.

Tishio kwa rasilimali za Bonde la Mto Pangani• Misitu iliyopo katika bonde inahatarishwa na ukataji miti, uingiliwaji eneo lake la pembezoni,

mahitaji ya ardhi, utengenezaji wa mkaa na ukusanyaji wa kuni.

• Upatikanaji wa maji katika Bonde unahatarishwa na mahitaji makubwa mno ambayo yamedhihirisha kuwa rasilimali za maji zinaonekana kuelemewa. Chanzo kikuu cha mahitaji hayo ni mifumo duni ya mifereji ya umwagiliaji. Vinamasi vya bonde hili vinahatarishwa na utaratibu wa udhibiti wa maji kwa kutumia mabwawa.

• Maeneo yaliyohifadhiwa katika bonde yanahatarishwa, kwa upande mmoja na ujangili, na kwa upande mwingine, vitisho sawa na vile vinavyokabiliwa na rasilimali za misitu.

• Sehemu kubwa ya bayoanuwai ya bonde imepatikana kutokana na safu za aina ya kipekee za makazi katika misitu yake. Matokeo yake, hatari ya kutoweka kwa bayoanuwai zinatokea kwa sababu ya tishio kwa makazi.

• Uvuvi katika bonde unatishiwa na shinikizo la uvuvi lililokithiri, na ukuaji wa magugu unaosababishwa na kiasi kikubwa cha virutubisho.

• Viwango vya chini vya kurudishia rutuba na matumizi ya pembejeo, na vile vile viwango vya juu vya mmomonyoko, vinahatarisha udongo katika bonde.

24

Page 38: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

C Uchumi wa Jamii katika Bonde la Mto Pangani

C.1 Maelezo ya jumlaInakadiriwa kuwa kuna watu wapatao milioni 3.7 katika Bonde la Mto Pangani, asilimia 80 wakitegemea ama moja kwa moja au kwa njia moja au nyingine, kilimo kwa maisha yao. Asilimia 90 ya idadi ya wakazi wa bonde hili huishi katika sehemu za ukanda wa juu. Msongamano huo wa makazi hufikia watu 300 kwa kilomita moja ya mraba. Katika maeneo ya nyanda za juu za Kilimanjaro kuna watu 900 kwa kilomita moja ya mraba yenye wastani wa vishamba vya hekta 0.2 tu kwa kaya. Wakati huo huo, katika maeneo ya nyanda za chini kulikuwa na watu 65 tu kwa kilometa ya mraba, na kila kaya ililima wastani wa eneo la hekta 10.4 (Lein, 2002).

Shughuli za kiuchumi katika Miji na viwanda ndani ya bonde si kubwa kiasi cha kutosha kuchukua nguvu kazi hii. Matokeo yake, idadi ya watu ambayo inazidi kukua, hupata riziki yake kutokana na kilimo, ambacho kwa sehemu kubwa ni cha umwagiliaji. Kadiri matumizi ya maji yanavyoongezeka, ndivyo migogoro inavyoongezeka. Mahitaji ya maji ni ishara ya mahitaji makubwa zaidi ya kufikia aina zote za rasilimali, ikiwemo ardhi, mazao ya misitu, malisho, madini na hatimaye kujipatia riziki. Kujipatia riziki kunaweza kuelezwa kama ifuatavyo:

“….. njia ya kujihakikishia maisha …Ndani yake kukiwa na rasilimali kwa ujumla wake, shughuli na mazao yanayowezesha kuishi. Inategemea umiliki wa, au upatikanaji wa mazao au shughuli za uzalishaji. Upatikanaji wa riziki hupimwa kwa kutumia vipimo vyote viwili vya mali -yaani hifadhi na vyombo- na upatikanaji wa chakula na fedha “(Conway na Barbier, 1990: 117).

Dhana ya kufikia rasilimali ni kigezo cha muhimu sana katika kuamua kuwa utafutaji wa riziki ni wa mafanikio au la (cf. Ellis, 2000). Hivyo ina maana kuwa pale ambapo rasilimali inayotegemewa na jamii inakuwa haba, basi upatikanaji wake unapungua. Kadiri rasilimali zinavyokuwa haba zaidi, basi hatua watakazochukua watu ili kujaribu kujipatia rasilimali zinaweza kuwa mbaya zaidi, na kuwa vigumu zaidi kwa rasilimali husika kudumu. Mtindo huu hatimaye unaweza kufikia mahali ambapo utafutaji riziki ukapuuza uwezo wa rasilimali kujizalisha upya.

Jambo linalokuza matatizo yanayohusiana na mahitaji ya riziki ni kama rasilimali zinazohusika ni Rasilimali za Pamoja za Jamii (CPRs). Hizi ni rasilimali ambazo zina tabia mbili za msingi zinazofanana; (a) ‘zinapunguzika’. Upunguzaji wa kiasi cha maji sehemu ya juu ya mto husababisha upungufu wa kiasi cha maji sehemu ya chini ya mto. Vivyo hivyo, mvuvi anayevua kilogramu 100 za samaki anafanya kuwe na kilogramu 100 pungufu za samaki kwa ajili ya wavuvi wengine. (b) Ni vigumu au haiwezekani ‘kuzikinga’ rasilimali za pamoja za jamii. “Kulinda” kisitiari inamaanisha matatizo makubwa ya kuzisimamia. Kutokana na asili zao, rasilimali za pamoja za jamii (kama vile bahari, angahewa au mikondo ya mto) haziwezi kujengewa uzio, na pia ni vigumu sana kuzifuatilia na kuzisimamia. Rasilimali za pamoja za jamii kwa hiyo, husimamiwa vizuri zaidi kwa pamoja, kukiwa na mchango wa watumiaji wote. Ikiwa mtindo huo wa usimamizi wa pamoja haupo, zitakuwa hatarini sana kuwa wazi kuingiliwa’, ambapo muundo wa utumiaji ni wa ‘huru-kwa-wote’, watumiaji wa rasilimali wakichukua zaidi ya wanachohitaji leo kwa kuhofia kuwa wanaweza wasipate kitu kesho. Mitindo ya utumiaji kama hiyo ina viwango vya juu sana vya ushindani baina ya watumiaji, na thamani halisi zinazohusiana na hifadhi ya rasilimali hazijaliwi kabisa. Wakati rasilimali zinapotumika katika mtindo kama huu, ‘mwisho wa wanyonge’, unasemekana kuwa umewadia na kutoweka kwa rasilimali kunakuwa ni jambo la wazi.

Kwa viwango mbalimbali, na kutegemeana na aina ya rasilimali, rasilimali nyingi za Bonde la Mto Pangani zina tabia ya kuwa wazi kuingiliwa na matatizo makubwa sana kutokana na utafutaji wa riziki. Mahusiano yanayoainisha utumiaji wa rasilimali za bonde mara nyingi yanaelezwa kama yenye kuhitilafiana. Ili

25

Page 39: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

kurahisisha na kufafanua matatizo haya, sura hii inazingatia matakwa ya shughuli mbali mbali za kiuchumi, ikianzia na shughuli za viwanda ambazo ni pamoja na uzalishaji wa umeme, na kisha kuendelea kuangalia sehemu kubwa ya uchumi wa bonde, ambayo ni kilimo. Shughuli nyingine pia zinazingatiwa, na sura hii inamalizia na tathmini ya migogoro ya kawaida katika uendelezaji wa bonde hili.

Jedwali la 4:Taarifa ya msingi ya uchumi wa kijamii wa Tanzania na Kenya mwaka 2001 isipokuwa ikionyeshwa vinginevyo

Kenya Tanzania

Idadi ya watu Milioni 29 Milioni 32

Kwango cha ongezeko la idadi ya watu kwa mwaka, mwaka 2000 2.6 2.8

Kiwango cha vifo vya watoto wachanga kwa 1000 waliozaliwa hai 75.0 91.0

Kiwango cha vifo vya watoto wenye umri chini ya miaka 5 kwa 117.0 142.0 1000 waliozaliwa hai

Uwezekano wa kufa, wanaume < miaka 5, (katika kila 1000) 100.0 157.0

Uwezekano wa kufa, wanawake < miaka 5, (katika kila 1000) 99.0 148.0

Matarajio ya umri wa kuishi wakati wa kuzaliwa (wanaume) 47.3 44.4

Matarajio ya umri wa kuishi wakati wa kuzaliwa (wanawake) 48.1 45.6

Asilimia ya upatikanaji wa maji salama ya kunywa 44.0 66.0

Asilimia ya upatikanaji wa usafi wa kutosha 85.0 86.0

Asilimia ya watoto waliozaliwa na uzito mdogo1 16.0 14.0

Asilimia ya watoto waliodumaa (wastani na kiasi kikubwa)2 33.0 42.0

Asilimia ya watoto waliodhoofika )3 6.0 6.0

Wastani wa kula kalori kwa mtu kwa siku (1999)4 1,886.0 1,940.0

GNP (Dola za Kimarekani) kwa mtu 340.0 210.0

Dondoo

1 kuzaliwa na uzito mdogo mara nyingi kunaashiria shinikizo la uzazi wakati kijusi kiko tumboni, kama vile kuugua (ikiwemo utapiamlo).

2 Kudumaa ni aina ya kudumu ya utapiamlo unaotokana na kutopata lishe ya kutosha, iliyo bora, kwa kipindi kirefu

3 Kudhoofika ni aina hatari na kali, ya utapiamlo iletwayo na kutopata lishe ya kutosha, iliyo bora, kwa kipindi kifupi.

4 FAO imeweka mahitaji ya nguvu ya chini kabisa kwa binadamu kuwa kilo kalori (kcal) 2,600 kwa siku

Rejea: UNICEF; 2001; FAO, 2001; WHO, 2001

26

Page 40: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

C.2 Shughuli za viwanda Kuna uwezekano kuwa shughuli iliyo kubwa zaidi ya viwanda katika Bonde la Mto Pangani ni uzalishaji wa umeme. Mzalishaji mkuu wa umeme ni Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO), linalomilikiwa na serikali, ambalo linamiliki mitambo minne ya uzalishaji umeme wa maji katika Mto Pangani. Nayo ni Nyumba ya Mungu (yenye uwezo wa MW 8), Hale (MW 21) na Mitambo mipya ya Maporomoko ya Mto Pangani (MW 68). Mitambo hii ya umeme imeunganishwa na gridi ya taifa na huchangia kadiri ya asilimia 17 ya jumla ya nishati ya umeme wa maji unaozalishwa nchini (Ngula, 2002). Mahitaji ya kiasi cha maji kwa uzalishaji wa uhakika (Firm power) kwa mitambo ya umeme ni kadiri ya mita za ujazo 24 kwa sekunde, ambapo mahitaji ya juu kabisa ni mita za ujazo 45 kwa sekunde. Mitambo ya “Old Pangani” hufanya kazi mara chache kutokana na ukosefu wa maji ya kutosha (Lugeiyamu, Mhojiwa).

Wakati wa msimu wa kiangazi, upungufu wa maji unaweza kusababisha uzalishaji wa umeme katika bonde kupungua hadi MW 32 (Sarmett na Kamugisha, 2002).

Kuna shughuli nyingi za uchimbaji wa madini katika Bonde la Mto Pangani. Hizi ni pamoja na machimbo ya bati eneo la Korogwe, machimbo ya tanzanaiti na fosfati katika mkoa wa Arusha, na machimbo ya mawe ya chokaa katika mkoa wa Tanga (Mkuula, 1993). Vito johari pia vinapatikana kwa kiasi cha kutosha, na asilimia 80 ya hifadhi za tanzanaiti ijulikanayo duniani inapatikana Mererani, kilomita 50 Kaskazini Mashariki ya Arusha. Uchimbaji wa mchanga kwa shughuli za ujenzi hufanyika zaidi katika kingo za mito, na katika sehemu za bonde kwa upande wa Kenya, uchimbaji wa rubi hufanyika.

Viwanda vingine katika bonde ni vile vinavyohusiana na kilimo, kama vile vya uzalishaji wa sukari na vya mchakato wa usafishaji wa katani. Katika wilaya ya Taita-Taveta nchini Kenya, uzalishaji wa katani ndio shughuli kuu ya kilimo.

C. 3 Shughuli za Kilimo Watu wa jamii ya Wachaga wameishi katika miteremko ya Mlima Kilimanjaro kwa miaka kati ya 300 hadi 450. Umilikaji wao wa ardhi kwa ajili ya kilimo umegawanywa katika namna mbili. Kwanza ni “shamba”, ambapo yametengwa maeneo maalum katika ukanda wa chini ya mlima ambapo mvua si ya uhakika, na umwagiliaji wa kadiri unahitajika sana. Matumizi ya ardhi ya shamba yalikuwa yakisimamiwa na machifu wa Kichaga, ambao waliwapangia wakulima sehemu za ardhi kwa msimu. Ingawa mkulima aliweza kutumia ardhi kwa kipindi kirefu, haikuwa mali yake hata kidogo (Johnston, 1946). Aina ya pili ya umilikaji ardhi ya uchaga ni ‘kihamba’, ambacho kilitengwa kwa matumizi binafsi ya wakazi wa uchagani. Kihamba kilikuwa, na bado kinalimwa kwa kiwango kikubwa. Hata katika miaka ya 1940, wakati wa maandishi ya Johnston (1942), kulikuwa na ardhi ndogo sana ya kihamba iliyobaki ambayo ingeweza kutumika kama malisho, hivyo mifugo mingi ilifungiwa na kulishwa mazizini. Katika maeneo yale ambapo mkazo wa kilimo ulikuwa juu, na hakikupatikana kihamba kingine, machifu wa Kichaga walipaswa kubadilisha ardhi ya shamba kuwa kihamba, matokeo yake, kitendo hiki kilichangia kuhamisha kilimo kilichokuwa kimezidi katika miteremko ya juu, kwenda katika miteremko ya chini ya milima. Wachaga hawakuweza kujitanua mpaka mlimani kwa vile eneo hili lilikwishatengwa kama hifadhi ya msitu, na hawakuweza kujitanua kwenye maeneo ya mteremko wa kati kwa kuwa hii ilikuwa ardhi iliyotengwa kwa ajili ya walowezi wa kizungu (Lein, 2002).

Kutokana na hali hii ya msongamano mkubwa wa kilimo, Wachaga walibuni mifumo ya mifereji ya maji kutoka kwenye vyanzo vya asili hadi kwenye mimea yao. Mfumo huu unasemekana kuwa mmojawapo wa mifumo ya zamani sana (inafikiriwa kuwa ulianza katika karne ya 18, Gillingham, 1999) na mifumo mikubwa zaidi ya mifereji ya umwagiliaji katika Afrika (Rohr et al., n.d.). Ili kupata maji hayo ya mfereji, ilibidi mtu awe mwanachama wa bodi ya mfereji, ambayo iliongozwa na wazee wa mifereji ambao maagizo yao yalibidi wakulima wayafuate kwa kuhofia adhabu ya faini au kuzuiliwa kutumia maji ya mfereji (Johnston, 1946). Wajumbe wa bodi ya mfereji pia walitegemewa kushughulikia utunzaji wa mifereji. Watumiaji wa maji ambao waliyachukua kutoka katika mifereji inayomilikiwa na watu binafsi ilibidi walipe ada ya kufanya hivyo.

27

Page 41: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Licha ya ukubwa wa kilimo na shinikizo la idadi ya watu kwenye ardhi ya kihamba, taratibu za kijadi za utawala na uzuiaji migogoro zinaonekana kuwa na ufanisi. Johnston (1942) alisema “…….ni jambo la kuvutia kuwa, pamoja na kuwa na mfumo wa mifereji yenye utata , lakini mambo yanaendeshwa vizuri sana na wazee wa mifereji, kiasi kwamba idadi ya mashauri yatokanayo na migogoro ya haki ya kutumia maji imekuwa ndogo sana” (uk. 4).

Kwa upande wa kusini, msongamano wa shughuli za kilimo katika milima ya Usambara, pia ulianza kuwa wa matatizo machoni mwa wakoloni. “Ulazima wa wenyeji kulima mfululizo kwenye kingo za mlima hufanya mmonyoko wa udongo kuwa tatizo kubwa sana, na maeneo makubwa ya ardhi ….huchukuliwa na maji (Dobson 1940:3). Wasambaa walikabiliwa na matatizo yaliyofanana na yale ya Wachaga. Maeneo ya miteremko ya kati ya milima yalikuwa na hali ya hewa iliyowapendeza wakulima wa Kijerumani, ambao walitenga maeneo makubwa ya ardhi kwa ajili ya kilimo cha mkonge.

Maji katika jamii ya Wasambaa yalichukuliwa kuwa ni mali ya jamii, na mtu ambaye alikuwa na chanzo cha asili cha maji katika ardhi yake hakuweza kuzuia watu kutoka nje kuyatumia. Wamiliki wa ardhi waliweza kuwatoza faini wafugaji iwapo mifugo yao iliharibu mazao yao, au kama maji yalichafuliwa.

Maji kutoka kwenye mfereji, ambayo yalitumiwa sana katika miaka ya awali ya 1940, yalikuwa ni mali ya wale waliochimba mfereji huo (Dobson 1940).“Mfereji ulipokuwa unachimbwa, wenye mashamba waliamua baina yao wenyewe kuhusu nani apate maji na kwa siku zipi”(uk. 22). Aidha, licha ya ukubwa wa kilimo na msongamano wa watu, migogoro ya haki ya kutumia maji ilikuwa michache. “Kulionekana kuwa na migogoro michache kiasi cha kushangaza” aliandika Dobson (1940) ….” lakini kwa suala la mifereji mirefu sana, wazee kwa ujumla walimweka mtu anayeaminika kusimamia na kuhakikisha kuwa kila mmoja anapata mgao wake wa maji kwa usawa na hakuna maji yanayopotea bure …” (uk. 22).

Tofauti na Wachaga, Wasambaa hawakutaka kabisa kuteremka chini ya milima kutafuta vyanzo mbadala vya ardhi ya kilimo. Kutokuwepo kwa migogoro ya haki ya kutumia maji na ukweli kuwa kuhamia kwenye nyanda za chini lilikuwa ni jambo la hiari, inaonesha kuwa msongamano wa kilimo haukuwa mkubwa katika miaka ya 1940, kama ilivyo leo.

Bonde la Mto Pangani wakati wa kipindi cha ukoloni, lilikuwa eneo muhimu la maendeleo, lililokuwa na mashamba makubwa ya kahawa, mkonge, ngano na shughuli za uzalishaji sukari zilizoanzishwa ndani ya bonde hili. Hivyo, mahitaji ya wafanyakazi yaliongezeka, na hivyo kuwavutia wahamiaji kutoka sehemu yote ya nchi na hata kutoka nje ya nchi kama vile Rwanda, Burundi na Msumbiji (Mbonile, 2002)

Haijafahamika wazi ni eneo kiasi gani la Bonde la Mto Pangani linamwagiliwa kwa sasa. Kwa eneo la bonde ambalo liko upande wa Tanzania, Mujwahuzi (2001) anakadiria kuwa hekta 40,000 zinamwagiliwa, Rohr et al. (n.d.) anasema kuwa hekta 29,000 zinamwagiliwa kwa ufanisi, wakati ambapo Ngula (2002) anakadiria kuwa hekta 31,075 katika Bonde la Mto Pangani zinamwagiliwa.

Kisanduku cha 10: Kasoro za usanifu wa mifereji ya asili

Kwa mujibu wa Mwamfupe (2001), matatizo ya usanifu wa mifereji ya asili katika Bonde la Mto Pangani ni kama yafuatayo:

• Maji mengi hupotea pale yanapochukuliwa kwa sababu ya nyenzo duni (mashina ya migomba) zinazotumiwa kuchepusha maji yaingie katika mifereji ya kumwagilia;

• Muundo wa vishamba ni duni –hayakusawazishwa, jambo linalosababisha maji kutuwama, yakisababisha chumvi chumvi na mazao haba.

• Mifereji haikujengwa imara na ina kingo dhaifu, jambo linalosababisha maji kuzivunja.

Matatizo mengine ni kuwa mara nyingi wakulima huhusisha kiasi cha maji cha kuchukua na ukubwa wa ardhi ambayo wanahitaji kuimwagilia, na si kwa maji yanayopatikana. Maji yanayochukuliwa hayarudishwi mtoni, na mara nyingi hutuama. Si kawaida kwa wakulima kujenga mitaro ya kurudisha maji kwenye vyanzo vya maji. “Mifumo ya ya umwagiliaji ya Tanzania ni upotezaji tu wa maji” ( Nasari, Mhojiwa)

28

Page 42: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Katika sehemu ya bonde iliyoko Kenya, mahitaji pekee makubwa ya maji ya Ziwa Jipe ni umwagiliaji. Eneo linalotegemea Ziwa hili upande wa Kenya lina miradi 10 ya umwagiliaji yenye ujumla wa hekta 1,717. Eneo hili linatarajiwa kuongezeka. Mpango wa Umwagiliaji maji wa Ziwa Jipe utakuwa kwenye mwambao wa Ziwa Jipe na utachukua eneo la hekta 77.2 na utahitaji mita za ujazo 308 za maji kwa saa (Musyoki na Mwandotto 1999). Kwa sasa, kiasi kikubwa cha maji kinachukuliwa kutoka sehemu ambayo mto Lumi unatiririka kupitia Kenya, ambamo ndani yake kuna miradi 21 ya maji. Jumla ya kiasi kinachochukuliwa katika eneo la Kenya la Bonde la ziwa hili ni mita za ujazo 77,274 kwa siku. Mita za ujazo 54,681 za ziada huchukuliwa wakati wa kipindi cha mafuriko (Musyoki na Mwandotto, 1999).

Kwa mujibu wa Ngula (2002) mahitaji ya maji kwa sasa ndani ya sehemu ya bonde iliyoko Tanzania ni mita za ujazo milioni 807.99 kwa ufanisi wa umwagiliaji wa asilimia 20. Umwagiliaji katika bonde hili hutumia kati ya mita za ujazo milioni 400 na 480 za maji kwa mwaka (Mujwahuzi, 2001). Mgao wa matumizi haya unaonekana kutokuwa na usawa – nusu ya jumla ya matumizi yote ya maji katika bonde ikiwa imesongamana kuzunguka Mlima Kilimanjaro. Hapa, mifereji ya jadi 500 ya umwagiliaji yenye urefu wa jumla wa kilomita 1800, huchukua maji ya kadiri ya mita za ujazo milioni 200 kwa mwaka kutoka kwenye mito ya mlima huu (Gillingham, 1999). Rohr et al. (n.d.) anarejea kazi inayoonesha kuwa, kati ya mwaka 1997 na 2007, kwa kila ongezeko la asilimia 1.5 la idadi ya watu wa bonde hili, mtiririko wa mito katika msimu wa mvua haba hupungua kwa mita za ujazo 8 kwa sekunde. Katika mkoa wa Kilimanjaro asilimia 80 ya matumizi ya maji ni kwa umwagiliaji (Ngana 2001). Maeneo ya Wilaya za Hai na Moshi Vijijini (kuzunguka Mlima Kilimanjaro) yanaonesha msongamano mkubwa zaidi wa mifereji ya jadi barani Afrika (Tagseth, 2002). Matokeo yake, viwango vya mmomonyoko wa ardhi kutoka kwenye Mlima Kilimanjaro viko juu (Mtalo na Ndomba, 2002). Tani 24 za udongo kwa hekta kutoka eneo la vyanzo vya mito husafirishwa na kuingia katika bwawa la Nyumba ya Mungu kila mwaka (Mtalo na Ndomba, 2002).

Umwagiliaji wote huu unatumia mifereji 2000 ya jadi ya Bonde la Mto Pangani (Mujwahuzi, 2001), ambayo inawiana na asilimia 80 ya eneo la bonde linalomwagiliwa (Mwamfupe 2001). Hata hivyo huenda hii si ishara ya ukubwa wa kilimo. Tagseth (2002), kutokana na data za eneo lake la utafiti lenye sehemu tatu kusini mwa Wilaya ya Moshi Vijijini, anasema kwamba kiasi cha maji yanayotumika kwa kweli kimepungua kati ya mwaka 1940 na 1993, kama ilivyopungua idadi ya mifereji.

Sababu za umwagiliaji ziko za namna mbili. Katika maeneo ya uwanda wa juu, wastani wa ukubwa wa shamba ni kati ya hekta 0.1 na 0.2. Hapa msongamano wa watu uko kati ya watu 700 – 1000 kwa kilomita ya mraba (Mwamfupe, 2001). Ili kufidia udogo huo wa mashamba na kuhakikisha kuwa ardhi iliyopo inazalisha kadiri iwezekanavyo, umwagiliaji unafanyika. Eneo la chini la bonde, katika maeneo ya mashamba ya asili, mashamba ni makubwa zaidi (hekta 0.8 – 1.5) na msongamano wa kilimo ni mdogo (Mwamfupe, 2001). Hata hivyo, hapa mvua hazina kanuni maalum, na umwagiliaji unafanyika ili kupunguza athari mbaya za hali ya hewa.

Ni wazi kuwa kwa viwango hivi vya umwagiliaji, watumiaji wa maji wa maeneo ya juu ya mto wako mahali pazuri zaidi kuliko watumiaji walioko upande wa chini. Upungufu wa maji katika bonde hili ni jambo la kawaida sana. Utafiti wa Mwamfupe (2001) umefanyika katika sehemu mbili: Makuyuni, katika miteremko ya Kilimanjaro, na Kahe, chini zaidi ya mlima. Wahojiwa wake walisema kuwa hawapati maji ya kutosha kwa umwagiliaji. Sehemu kubwa ya wahojiwa - ambao wengi wao walitoka Kahe - walitupia lawama za upungufu huu kwa ukame wa muda mrefu; wakifuatiwa na wale - hasa kutoka Makuyuni – ambao walilaumu ongezeko la matumizi na mahitaji ya maji. Ni asilimia 7.3 tu waliolaumu matatizo ya maji kuwa yametokana na usanifu usiofaa wa mifereji.

Ni muhimu kutambua kuwa sehemu kubwa ya sababu za kutobadilika kwa mifumo hii ya umwagiliaji wa asili, licha ya ufanisi mdogo, ni kwa sababu ya gharama zinazohusika kuweza kupata mifumo mbadala ya umwagiliaji yenye ufanisi, inayohitaji matengenezo madogo na ya kudumu. Ni muhimu pia kutambua kuwa usanifu wa mfereji unaweza kuleta manufaa ya kijamii na kiuchumi ambayo ni makubwa kuliko hasara zinazotokana na usafirishaji maji wenye ufanisi mdogo.

29

Page 43: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Kiasi cha uoto katika bonde kimepungua, kikichangia katika kupungua kwa mtiririko wa maji wakati wa kiangazi, na kutishia upatikanaji wa riziki. Wakulima wamekabiliana na upungufu wa maji kwa njia kadhaa. Wamepunguza kiasi cha kahawa wanayolima, na kupendelea kulima nyanya, ambazo zinahitaji muda mfupi kustawi na zina soko zuri5. Mwamfupe (2001) pia anaeleza kuwa kahawa inatelekezwa kwa sababu ya kupanda na kushuka kwa bei. Kaya za wakulima pia zimepanua wigo wa kujipatia maisha kwa kujitafutia mapato yasiyotokana na kilimo. Kinachoshangaza ni kuwa aina ya shughuli mbadala zinatofautiana kulingana na eneo analotoka mkulima. Shughuli mbadala walizozipata kaya za nyanda za juu ilikuwa pamoja na ushonaji, utengenezaji wa redio na televisheni, utengenezaji wa saa na ushonaji wa viatu. Katika nyanda za chini, shughuli mbadala ilikuwa pamoja na uuzaji wa majani ya kulishia ngo’mbe, uvunjaji mawe, utengenezaji mkaa na kazi za vibarua. Mwamfupe (2002) anadokeza kuwa hii ni kwa sababu eneo la nyanda za juu limeendelea zaidi na lina maeneo ya miji zaidi kuliko maeneo ya nyanda za chini, hivyo fursa za kuingia katika sekta ya huduma ni kubwa zaidi.

Miongoni mwa matatizo yanayotokana na wingi wa shughuli za umwagiliaji ni magadi na chumvichumvi. Katika maeneo matatu ya utafiti (yote katika Wilaya ya Moshi Vijijini) wa Misana na Makoi (2001), maji ya umwagiliaji, hayakuwa sababu ya chumvichumvi, ingawa kumekuwa na kukwama kwa kiwango kidogo hadi kikubwa cha upenyaji wa maji katika tabaka la juu la udongo kwa maeneo yote ya utafiti. Katika maeneo mawili umwagiliaji ulichangia katika kusababisha magadi. Wanasema, maji yenye ‘ubora mzuri’ yanahitajika ili kushughulikia tatizo hili. Umwagiliaji haukuonekana kuathiri rutuba ya udongo isipokuwa katika eneo moja. Misana na Makoi (2001) walipendekeza matumizi ya viwango vya chini vya mbolea za aina mbalimbali kutatua tatizo hili la kutotosheleza kwa rutuba ya udongo. Wanatoa rai kuwa chumvichumvi zinaweza kuchujwa vizuri kwa umwagiliaji, lakini pale maji yanaposimama basi tatizo hili halitatuliki kwa vile inasababisha mabadiliko ya kimuundo kwa tabaka la udongo wa juu, ikiathiri upenyaji wa maji kutoka udongo wa juu kwenda kwenye sehemu ya mizizi ya mmea.

Mashamba makubwa zaidi katika Bonde ni shamba la miwa la Kampuni ya Sukari (TPC) (hekta 17,000), Skimu ya Umwagiliaji ya Moshi (Lower Moshi Irrigation Scheme) chini ya Programu ya Maendeleo ya Kilimo Kilimanjaro (KADP - hekta 6,320), na Shamba la Kahawa la Burka, Arusha.

TPC ipo kusini ya mji wa Moshi, na ilianzishwa kwa mara ya kwanza na wawekezaji wa Kiholanzi katika miaka ya mwanzo ya 1930. Ilitaifishwa mwaka 1980, na kubinafsishwa tena mwaka 2000 kwa wawekezaji

Kisanduku cha 11: Magadi na chumvichumvi

Magadi ni kuwepo kwa ziada ya ‘sodiamu inayobadilishika’ (chumvi chumvi za sodiamu zenye uwezo wa alikali ya ‘haidrolisis’) na kusababisha mpenyo na ucheu duni wa udongo. Chumvi chumvi ipo sana katika maeneo kame na nusu kame kwa kuwa hakuna maji ya kutosha kuondoa chumvichumvi zilizojikusanya katika sehemu ya mizizi ya mimea. Hali ya chumvichumvi inaweza kutokea pale uingiaji chumvi unapozidi uondoaji wake kwa kufurika au kuchujwa. Kati ya matatizo mengi yanayohusiana na chumvichumvi ardhini ni athari yake katika ufyonzaji wa udongo na uwekaji unyevu. Uvunjaji wa vitu asili katika udongo husababisha tabaka lake la juu kujigandamiza, na kusababisha upenyezaji wa maji kutoka tabaka la juu kwenda eneo la mizizi uzuiliwe. Katika Bonde la Mto Pangani, tatizo la chumvi limetolewa taarifa katika miradi kadhaa ya umwagiliaji, ikiwemo Musa Mwijanga, Kikafu Chini (yote wawili katika Wilaya ya Hai) na Mawala (Wilaya ya Moshi Vijijini) (Misana na Makoi, 2001), na vile vile katika baadhi ya miradi mikubwa ya binafsi ya umwagiliaji katika bonde (Sahib, 2002).

5Ni lazima itambulike kuwa kupanda na kushuka kwa bei katika soko la dunia la kahawa, na vile vile kwa bidhaa nyingine za kilimo na ubadilikaji wa mitindo ya uchumi wa kitalii, vyote huchangia katika kubadilisha uthabiti wa uchumi wa Bonde lenyewe na kuathiri uwezo wa wakazi wake kupata riziki ya kutosha.

30

Page 44: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

wa Mauritius (Deep River Bean Champ Sugar Estate, Mauritius) na wa Kifaransa (Group Quartier Francais Reunion Island). Shamba hili lina ukubwa wa hekta 17,000 ambapo hekta 5,750 kati ya hizo kwa sasa zina miwa. Inafikiriwa kuongeza eneo hili kufikia hekta 7,500 katika siku za karibuni (Sahib, 2002).

Eneo hili linapata milimita 450 tu za mvua, hivyo umwagiliaji ni lazima kwa kilimo cha miwa. Kiasi cha upungufu wa maji kwa mimea umekadiriwa kwa kiwango cha chini zaidi cha milimita 1,200 kwa mwaka hivyo kuhitaji matumizi ya umwagiliaji yanayotofautiana kati ya milimita 1,500 – 1,900 kwa mwaka kutegemeana na mfumo na mbinu za umwagiliaji. Takriban nusu ya shamba humwagiliwa kwa kutumia mabomba ya juu, wakati sehemu iliyobaki inamwagiliwa kwa mifereji ya juu ya ardhi. Mito iliyopo katika mpaka wa upande wa Magharibi wa shamba hutoa sehemu ya maji ya umwagiliaji, na yaliyobaki huchukuliwa kutoka hazina ya maji ya chini ardhi kupitia visima virefu vinavyotoa maji mengi (meta za ujazo 500 kwa saa) (Sahib, 2002).

Nchini Tanzania, maji yanaweza kuchukuliwa kisheria iwapo tu watumiaji wana hati ya haki ya kutumia maji, ambayo, kwa Bonde la Pangani, hutolewa na Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani (PBWB), na kupangiwa ada kutegemeana na aina ya matumizi ya maji. Bodi hii inakabiliana na matatizo makubwa katika kutekeleza mfumo wa vibali vya maji kwani watumiaji wengi wa viwango vidogo wanaamini kuwa maji ni ‘zawadi kutoka kwa Mungu’. Ingawa wanataka kutumia maji kisheria, kiasili hawaamini kuwa wanapaswa kulipa kwa kufanya hivyo. Hata hivyo watumiaji wengi wa viwango vikubwa hulipa ada ya matumizi ya maji (Sarmett, Mhojiwa).

C. 4 Shughuli za WafugajiKati ya mwaka 1994 na 1995, mifugo ilichangia asilimia 30 ya pato la taifa (GDP) la Tanzania. Nchi inakadiriwa kuwa na hekta milioni 60 za ardhi nzuri kwa ufugaji, na inaaminika kuwa inaweza kuhifadhi mifugo milioni 20. Nchi inakadiriwa kuwa na mifugo milioni 16 kwa sasa.

Kuna data chache kuhusu wafugaji katika Bonde la Mto Pangani. Mnamo mwaka 1995, mifugo katika Bonde ilikadiriwa kuhitaji mita za ujazo 30,500 za maji kwa siku, wakati inategemewa kuhitaji mita za ujazo 36,400 kwa siku ifikapo mwaka 2015 (IVO-NORPLAN, 1997). Idadi kamili ya mifugo katika Bonde kwa sasa haijulikani. Tarakimu za karibuni zaidi zilizopatikana kwa utafiti huu ni za mwaka 2002, na zimechukuliwa kutoka wilaya na manispaa mbalimbali katika Bonde zima (Jedwali la 4).

Jedwali la 5: Idadi ya mifugo katika baadhi ya maeneo ya Bonde la Mto Pangani (2002)

Mkoa Ng’ombe *Mbuko Punda

Wilaya ya Simanjiro, Mkoa wa Manyara 305,075 133,000 11,000

Manispaa ya Arusha na Wilaya ya Arumeru, 470,000 461,450 21,991 Mkoa wa Arusha

Mkoa wa Kilimanjaro 568,689 534,420 12,380

Mkoa wa Tanga 421,261 378,442 Hawakuhesabiwa

Wilaya ya Taita – Taveta (Kenya) 37,800 40,277 Hawakuhesabiwa

Jumla 1,765,025 902,972 Rejea: Marejeo mbalimbali. *‘mbuko’ ni mchanganyiko wa mbuzi na kondoo.

31

Page 45: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

C. 5 Shughuli za MijiniBonde la Mto Pangani lina maeneo makuu mawili ya miji. Upande wa Kaskazini, iko miji ya Moshi na Arusha ambayo iko karibu karibu sana. Mwaka 1995, matumizi ya maji mijini katika bonde yalikadiriwa kuwa mita za ujazo 71,200 kwa siku, na yanakadiriwa kufikia mita za ujazo 163,600 kwa siku ifikapo mwaka 2015 (IVO-NORPLAN, 1997). Ujazo wa maji yanayotumika kwa sasa, Sarmett na Kamugisha (2002) wanakadiria kuwa wa chini, na si zaidi ya mita za ujazo 1.1 kwa sekunde.

Manispaa ya Arusha ina idadi ya watu kati ya 250,000 na 350,000 (wanaoitegemea mamlaka). Ingawa maji mengi zaidi yanayotoka Mlima Meru yanatumika kwa umwagiliaji na matumizi ya nyumbani, mtumiaji mkubwa kuliko wote wa maji kibiashara ni Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Mjini Arusha (AUWSA). Ina visima 15 na wastani wa uwezo wa mita za ujazo milioni 7.4 kwa mwaka (Sechambo, 2002). Mamlaka pia inapata maji kutoka chemchemi mbili zenye wastani wa jumla wa karibu mita za ujazo milioni 6.4 kwa mwaka (Sechambo, 2002).

Mito pia hutumika kutupia takataka za mji. Manispaa ya Moshi, Ngana (2001) anasema inatupa majitaka moja kwa moja katika mito, wakati Mkuula (1993) anadai kuwa mito ya Themi (karibu na Arusha), Karanga, Njoro na Rau (karibu na Moshi) yote inachafuliwa na takataka za viwanda vya mijini.

C.6 Shughuli za NGO na mashirika ya kimataifa katika Bonde la Mto Pangani

Kuna mashirika mengi yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi katika Bonde la Mto Pangani, na mashirika machache ya kimataifa. Katika sehemu hii, inaeleweka kuwa mashirika haya kimsingi hayana mahitaji katika maliasili za bonde, bali shughuli zao mara nyingi zinalenga katika Usimamizi wa Maliasili (NRM), kuhifadhi, kuendeleza na kudumisha kazi za kujitafutia riziki. Kuna shughuli nyingi za mashirika yasiyo ya kiserikali na wahisani wa kimataifa kuliko vile inavyofikiriwa. Haya yatakayojadiliwa hapa chini yanaweza kuweka msingi kwa shughuli za usimamizi shirikishi katika bonde, kama itakavyoelezwa katika hitimisho.

Asasi Zisizo za Kiserikali (NGO’s)PAMOJA ni NGO ya Kitanzania inayoamini kuwa majadiliano ni muhimu katika hali ya migogoro. Inatoa hoja kuwa kama sauti za vikundi vya jamii visivyo rasmi na vya pembezoni zinasikiwa na kusikilizwa na watunga sera na watoaji wa maamuzi, watendaji wenyeji wanaweza kuchangia kwa ufanisi ulinzi na ukarabati wa vyanzo vya maji, na wakati huo huo wakiongeza ufanisi wa uzalishaji wa kiuchumi na matumizi ya maji (PAMOJA, 2002:3). Wanasema, makubaliano ya pande mbili, yanafanya kazi nzuri zaidi kuliko sheria. Hivi sasa, PAMOJA imeonekana kutambulika na Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani, kuwa ni njia itakayowezesha majadiliano na maelewano ya pande mbili baina yake na watumiaji maji wa bonde kuendelezwa.

Ukiwa umezinduliwa mwaka 1992, Mradi wa Mpango wa Kazi ya Misitu Tanzania (TFAP) katika Milima ya Pare ya Kaskazini ulijihusisha na matatizo kadhaa makubwa, yakiwemo msongamano mkubwa wa watu, mashamba madogo, uchakavu wa udongo na viwango vya kutisha vya kuvamiwa kwa misitu. Kwa kutumia njia ya kuandaa mipango ya usimamizi wa maeneo maalum, na kwa ushirikiano na jamii za eneo la mradi, mradi uliweza kuboresha rutuba ya udongo, kupunguza kasi ya mtiririko wa maji na kuimarisha kingo za mito. TFAP pia ilijaribu kutumia mifumo ya umwagiliaji iliyoanzishwa na kutumiwa na Wapare kwa karne nyingi. Hata hivyo, ukubwa wa mashamba, umebaki kuwa mdogo, na zao pekee la biashara lililolimwa katika eneo hili lilikuwa kahawa, linalofanya Mndeme (n.d.) atoe hoja kuwa uanzishaji wa fursa za kutafuta kipato kwa njia isiyo ya kilimo na ubadilishaji wa msingi wa zao la biashara itakuwa muhimu kwa mafanikio ya baadaye ya mradi huu (rejea: Mndeme, n.d.).

Shirika la Umwagiliaji wa Kiasili na Maendeleo ya Mazingira (TIP) lilisajiliwa Tanzania tangu mwaka 1999. Shirika hili lilirithi mali na shughuli za mradi wa awali wa miaka 13 uliokuwa ukifadhiliwa na wahisani ulioitwa

32

Page 46: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Pic

ha y

a 1:

Bon

de la

Mto

Pan

gani

(Rej

ea: M

radi

wa

Usi

mam

izi w

a M

atum

izi B

ora

ya M

aji)

33

Page 47: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

34

Pic

ha y

a 2:

Bon

de la

Pan

gani

- U

taw

ala

(Rej

ea: M

radi

wa

Usi

mam

izi w

a M

atum

izi B

ora

ya M

aji)

Page 48: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

35

Picha ya 3: Kilele maarufu cha theluji cha Mlima Kilimanjaro katika mwaka 1993 (juu) na mwaka 2000

(Rejea: Bergkamp et al. 2003)

Page 49: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

36

Picha ya 4: Mto Karanga - Moshi (Kim Geheb 2002)

Picha ya 5: Mlima Kilimanjaro (Kim Geheb, 2002)

Page 50: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

37

Picha ya 6: Mfereji wa umwagiliaji katika Wilaya ya Moshi Vijijini. Picha ya juu inauonesha karibu na chanzo chake, wakati ya chini inauonesha karibu na

mwisho wake. (Kim Geheb, 2002)

Page 51: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

38

Picha ya 7: Chemchemi iliyojengewa Shiri-Njoro. Ukuta unaogawanya maji katika sehemu ya mbele inaelekeza maji kuingia katika mifereji ya kijiji, wakati lango la udhibiti lililojengewa katika jengo imara

la zege kwa nyuma linayaelekeza maji kwenda Moshi.(Kim Geheb, 2002)

Picha ya 8: Miteremko yenye msitu katika Mlima Meru (Kim Geheb, 2002)

Page 52: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Programu ya Umwagiliaji wa Kiasili. Kama ilivyokuwa kwa Programu ya awali, lengo kubwa la TIP ni kusaidia kwenye uondoaji umaskini na kuendeleza upatikanaji wa chakula kwa jamii ya wakulima wadogo wadogo wa umwagiliaji wa kiasili kwenye maeneo teule ya Tanzania kwa kuboresha njia za kijadi za umwagiliaji. TIP inasisitiza mpango wa matumizi ya ardhi kuwa ni msingi wa usimamizi wa bonde, na inatoa hoja kuwa, kama hatua ya kuanzia, bonde hili lazima ligawanywe katika maeneo madogo madogo. Katika kila moja, lazima kuwe na bodi ya eneo dogo yenye wawakilishi kutoka katika kila kijiji kilichomo kwenye eneo hilo. Kila bodi ya eneo dogo itakuwa na wawakilishi kwenye Bodi ya Maji ya Bonde (Mjata, Mhojiwa).

TIP inafanya kazi kupitia Hati ya Muafaka (MOUs) baina yake na wilaya nne za Tanzania: Same na Mwanga katika mkoa wa Kilimanjaro, Lushoto mkoani Tanga na Arumeru katika mkoa wa Arusha. Huwafikia wateja na wahitaji wengine kwa njia ya mikataba na shughuli mbalimbali pale wanapohitajiwa (Mjata, 2002).

Programu ya Hifadhi na Maendeleo ya Kanda ya Mwambao wa Tanga (TCZCDP) ina ubia na Halmashauri ya Wilaya za Pangani na Muheza, Halmashauri ya Manispaa ya Tanga, Mamlaka ya Mkoa wa Tanga, Wahisani wa Irish Aid, na IUCN kwa ajili ya ushauri wa kiufundi na kiusimamizi. Madhumuni ya jumla ya TCZCDP ni matumizi endelevu ya rasilimali za pwani. Programu hii ina lengo la kuinua hali ya jamii za pwani mkoani kwa kuboresha afya ya mazingira ambayo wanayategemea na kuzipanua njia za matumizi ya mazingira ya pwani. TCZCDP ilianza kazi zake mwaka 1987 na shughuli zake zinaendelea (Mgongo 2002).

Ubia wa Usimamizi wa Mwambao wa Tanzania (TCMP) ni juhudi za pamoja kati ya Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Kituo cha Rasilimali za Pwani/Chuo Kikuu cha Kisiwa cha Rhode na USAID. Ubia huu ulianzishwa mwaka 1997 ili kuendeleza na kutumia mfumo wa kitaifa wa usimamizi wa mwambao. Mfumo huu uko kwenye msingi wa mikakati yenye lengo la kuendeleza mpango wa usimamizi shirikishi wa ukanda wa pwani wa Tanzania na kuanzisha shughuli endelevu za uchumi zenye kutunza mazingira katika eneo hili (Luhikula 2002).

Kikundi cha Hifadhi ya Misitu Tanzania (TFCG) kilianzishwa mwaka 1985, na kinakuza uhifadhi wa misitu yenye bayoanuwai nyingi katika Tanzania. Kati ya mafanikio ya kikundi hiki, ni ushawishi wa uundaji wa Mbuga ya Taifa ya Udzungwa, mbuga ya kwanza nchini Tanzania ya msitu wa mvua; ununuzi wa Msitu wa Mazumbai katika Milima ya Usambara Magharibi kwa madhumuni ya utafiti wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam; na kushawishi EU-IUCN/Wizara ya Mifugo na Kilimo kufadhili Mradi wa Hifadhi na Maendeleo ya Usambara Mashariki. Kati ya shughuli zake za sasa katika Bonde la Mto Pangani ni kuendeleza mfumo wa Usimamizi Shirikishi wa Misitu (JFM) kwa msitu wa Ambangulu (Milima ya Usambara Magharibi) kati ya jamii za wenyeji, serikali za mitaa na shamba la chai lililopo karibu. Kutokana na kufanya kazi kwa pamoja na jamii zilizo jirani na Msitu wa Kambai (Milima ya Usambara Magharibi), TFCG imeweza kupanda miti 600,000. Huko Ngulwi (Milima ya Usambara Magharibi), TFGG inajaribu kupanda miti katika miteremko iliyoachwa wazi bila miti na kuanzisha programu ya utalii wa ikolojia.

Shughuli za Kimataifa Katika BondeInasadikiwa kuwa programu ya usimamizi bora ya maji na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji cha wakulima wadogo wadogo (RBMSIIP) ndiyo mradi mkubwa zaidi ya yote uliotekelezwa katka Bonde la Mto Pangani. Huu ni mradi wenye sehemu kubwa mbili ulitekelezwa na Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo kupitia Idara yake ya Rasilimali za Maji, na Wizara ya Kilimo na Chakula kupitia Idara ya Umwagiliaji. RBMSIIP awali ilibuniwa kama mpango wa miaka sita (1996/97 – 2001/02) ukifadhiliwa na mfuko wa mkopo wa IDA pamoja na serikali. Kufuatia mapitio ya nusu kipindi katika mwaka 2001, tarehe mpya ya mradi kukamilika ilipelekwa mbele kwa mwaka mmoja kufikia mwezi Juni mwaka 2003 kukamilisha shughuli zilizopangwa.

Madhumuni makuu ya mradi huu ni kuimarisha uwezo wa serikali kusimamia rasilimali zake za maji kwa njia shirikishi na pana ambayo italeta usawa, ufanisi na maendeleo endelevu ya rasilimali na kushughulikia masuala ya mazingira yahusianayo na maji katika ngazi ya taifa na katika mabonde ya mito Rufiji na Pangani; na kuboresha ufanisi wa umwagiliaji wa miradi iliyoteuliwa ya umwagiliaji wa kiasili

39

Page 53: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

wa mashamba ya wakulima wadogo katika mabonde haya mawili yaliyokusudiwa. Mafanikio makuu ya mradi mpaka sasa ni mapitio ya sera ya maji ya taifa na kuandikwa rasimu ya sera mpya ya maji. Rasimu hii iliidhinishwa na Serikali ya Tanzania mnamo mwezi Julai 2002.

Mradi wa UNDP GEF wa Bayoanuwai ya kimataifa ya Afrika ya Mashariki (EACBP) ni mradi wa kikanda unaofadhiliwa na Huduma ya Mazingira Duniani (GEF) kupitia UNDP, na katika Tanzania, unatekelezwa na Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC). Mradi huu unafanya kazi kwa kutumia miundo ya utawala iliyopo katika kanda hii, na ushirikishaji mkubwa wa jamii kama nguzo yake. Lengo kuu la mradi ni kupunguza kiwango cha upotevu wa bayoanuwai katika maeneo ya mipakani yaliyochaguliwa katika Afrika ya Mashariki. Mradi una malengo mawili yanayohitaji utekelezaji wa haraka. La kwanza ni kuunda mazingira yanayowezesha ambayo mawakala wa serikali na jamii kwa pamoja wanaweza kurekebisha matumizi ya rasilimali; la pili ni kuweka uwiano wa upatikanaji na mahitaji, mambo ambayo huathiri hifadhi na matumizi bora ya bayoanuwai. Katika eneo la bonde, EACBP imekuwa ikifanya kazi katika Hifadhi ya Msitu ya Shegena, ambao ni msitu mkubwa zaidi katika Milima ya Pare ya Kaskazini, ambapo ilifanyika jitihada ya kuanzisha mfumo wa JFM na jamii za wenyeji.

PRBMP hutoa taarifa nyingi za kisayansi na huanzisha mabaraza ya ushirikishwaji kwa madhumuni ya kuimarisha usimamizi wa rasilimali za maji wa pamoja unaojumuisha mabadiliko ya hali ya hewa duniani, matumizi ya maji kwa usawa na utawala bora wa maji kwa ajili ya kujipatia riziki na kutunza mazingira kwa ajili ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo. Ofisi ya Maji Bonde la Pangani inatekeleza mradi huu kwa msaada wa kitaaluma kutoka IUCN (shirika la kimataifa la kuhifadhi uasili) Shirika la Maendeleo la Uholanzi (SNV) na asasi isiyo ya serikali inayoitwa PAMOJA. Mradi unafadhiliwa na mpango wa IUCN wa hifadhi ya maji na uasili, serikali ya Tanzania, Mfuko wa Maji wa Umoja wa Ulaya, Mfuko wa Mazingira wa Ulimwengu (Global Environment Facility) kupitia Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).

C.7 MigogoroKama ilivyoelezwa hapo juu, watumiaji wa maji wanapaswa kisheria kupata kibali cha kutumia maji kitolewacho na Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani. Gharama vibali vya kutumia maji zinategemea aina ya matumizi ya maji. Watumiaji wadogo mara nyingi hawapendi kuomba hati na kulipa ada ya maji, wakitoa hoja kuwa maji ni ‘zawadi kutoka kwa Mungu’. Kwa mujibu wa Mujwahuzi (2001) kuna hati za maji 1,028 katika bonde zenye uwezo wa kuchukua mita za ujazo 30.7 kwa sekunde. Hata hivyo, kuna matoleo ya ziada ya maji 2,094 yenye uwezo wa kuchukua mita za ujazo 40 kwa sekunde. “Migogoro iliyopo sasa na inayotazamiwa kuwepo hapo baadaye ya matumizi ya maji katika bonde, ni matokeo ya maendeleo ambayo hayakuratibiwa tangu zamani na yanayoongezeka sasa ya rasilimali za maji za bonde hususan juu ya Bwawa la Nyumba ya Mungu” (Mujwahuzi, 2001:131).

Migogoro katika Bonde la Mto Pangani, hata hivyo, haiishii kwa watumiaji maji peke yao. Katika mifano inayotolewa hapo chini, itaonekana wazi kuwa migogoro mingi inayoikabili sekta ya maji ipo pia kwa sekta nyingine zinazotumia rasilimali, na kati ya matumizi na mahitaji mbalimbali juu ya rasilimali. Aina za migogoro iliyobainishwa hapa inarahisisha kueleza utatanishi wa hali ya juu na asili ya ushindani unaoanzisha migogoro. Uchambuzi huu wa Hali halisi unaiweka migogoro hii katika makundi matatu makuu, yaliyobuniwa ili kutoa maoni ya jumla ya aina mbalimbali na viwango vya migogoro iliyopo katika bonde. Makundi haya hayatengani, ikichukuliwa kuwa ni kawaida kwa migogoro ya maliasili na mahitaji ya riziki kuwa matatizo yanayoathiri upatikanaji wa rasilimali yanaingiliana, na mara nyingi yanazidishana. Hivyo, migogoro ya viwango inaweza kuzidisha migogoro ya umiliki na kinyume chake. Makundi haya ni: migogoro ya viwango, migogoro ya umiliki na migogoro ya mahali.

Migogoro inayotokana na viwangoUhusiano kati ya watumiaji wa maji wa ukubwa na uwezo tofauti katika Bonde la Mto Pangani mara nyingi huelezwa katika namna mbili zinazokinzana. Hivyo, mashamba makubwa yanayotumia mamia ya lita za maji kwa sekunde na kutumia mifumo ya umwagiliaji yenye ufanisi mkubwa, yanatofautiana kabisa

40

Page 54: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

na watumiaji wadogo wanaotumia maji kidogo na mifumo ya umwagiliaji iliyo duni sana. Itambulike kuwa migogoro kama hiyo hiyo inaweza kutokea pia ndani ya jamii, kati ya taasisi zilizokabidhiwa madaraka (kama vile serikali za vijiji) na wanajamii wengine. Tofauti kubwa hizi ni sababu ya kutosha kwa migogoro kuzuka. Mifano ya aina hizi za migogoro ni kama ifuatayo:

Mamlaka ya Maji safi na Majitaka Moshi dhidi ya Kijiji cha Shiri-Njoro Shiri – Njoro ni kijiji kilichopo kando ya barabara ya Moshi – Arusha, karibu na mji wa Moshi. Moshi ni eneo la mji linalokua kwa haraka sana likisaidiwa kwa kiwango kikubwa na kilimo. Kadiri mji huu unavyokua, ndivyo mahitaji ya maji yanavyoongezeka pia. Mnamo mwaka 2000, wahandisi kutoka Mamlaka ya Maji safi na Maji taka ya Manispaa ya Moshi (MUWSA) walifika Shiri-Njoro na kujengea mfuniko chemchemi kuu ya jamii. Chemchemi hiyo hutoa lita 218 kwa sekunde, na MUWSA ilipata kibali cha kutumia maji ya lita 116 kwa sekunde. Kijiji kilikuwa na mifereji mitatu inayotoka katika chemchemi hiyo, kila mmoja ukiwa na kibali cha kuchukua lita 30 kwa sekunde. MUWSA , kwa hiyo, ilitakiwa kuacha kiasi cha maji cha kutosha mahitaji ya mifereji ya jamii.

Hata hivyo, MUWSA, huchukua maji kadiri ya lita 24 kwa sekunde zaidi ya ilivyoruhusiwa. Serikali ya Kijiji cha Shiri – Njoro inadai kuwa haiwezi kuendelea kutumia kikamilifu mifereji yake mitatu kutoka kwenye chemchemi, na kwamba jamii pamoja na uchumi wake wa kilimo vimeathirika vibaya. Ni nia yao kuipeleka MUWSA mahakamani na wanasema “tutauza mbuzi na mbwa wetu ili tupate fedha” za kufanya hivyo (Wahojiwa: Serikali ya Kijiji cha Shiri – Njoro).

Afgem na wachimbaji wadogo wa MereraniTanzanaiti ni madini ya mawe ya thamani yenye rangi ya zambarau ya kibuluu, yanayopatikana Tanzania pekee. Eneo la ardhi yenye tanzanaiti inasemekana lipo katika eneo la kilometa za mraba 20 tu huko Mererani. Eneo hili limegawanywa katika safu ya vitalu, A, B, C na D. Kitalu C chenye kilomita za mraba 8 kinasemekana kuwa na mashapo ya madini mengi zaidi, tani milioni 2.2 za tanzanaiti kwa makisio. Tanzanaiti iligunduliwa katika eneo hili mwaka 1967, na mji wa Mererani sasa una wakazi 75,000 (Majtenyi na Muindi, 2001). Ni makazi yenye ‘vurugu na uhalifu yanayoweza kufananishwa na mji wa machimbo ya dhahabu wa California (Lovgren, 2001:1).

Mnamo mwaka 1999, Kampuni ya Kimataifa ya Afrika ya Kusini, (Afgem Ltd.), ilitafuta na kupata miliki ya miaka 13 ya uchimbaji madini katika Kitalu C.Ilipofika mwaka 2001, Afgem ilishawekeza dola za kimarekani milioni 8 katika miliki hiyo, na dola nyingine milioni 12 zingefuata mara Kampuni itakapoanza uzalishaji kamili (Majtenyi na Muindi, 2001).

Hata hivyo, Afgem si wachimbaji madini pekee waliopo Mererani. Kwa kweli shughuli hii inatawaliwa na wachimbaji wadogo 10,000, ambao wanapinga shughuli za Afgem kwa sababu zifuatazo (Majtenyi na Muindi, 2001):

• Wanaishutumu Afgem kwa kujaribu kuhodhi uchimbaji wa tanzanaiti katika eneo hili, na kwa kujaribu kuwaondoa wachimbaji wadogo kutoka eneo hili. Afgem inajibu vikali hoja hiyo kuwa: asilimia 70 ya miliki yake inachimbwa kinyume cha sheria. Katika shimo la pili kati ya mawili ya mgodi wake, wafanyakazi waligundua njia ya chini kwa chini inayokwenda mpaka kwenye eneo la machimbo ya wachimbaji wadogo katika Kitalu B (Lovgren, 2001).

• Mara baada ya kupata miliki, Afgem ilianza kuzungushia uzio Kitalu C. Hata hivyo wachimbaji wenyeji wanadai kuwa, mipaka kati ya sehemu hizi nne haiko wazi na kwamba Afgem haina haki ya kulitenga eneo hilo.

• Inadaiwa kuwa Afgem ilijaribu hata kupiga chapa vito vyake kama alama ya ubora na uhalali. Wachimbaji wenyeji wanatoa rai kuwa hii kwa kweli, ni hila ya kuhakikisha kuwa vito vyao vinaonekana kuwa vya bandia, hali inayowalazimisha kuuza vito vyao kwa wakala wa Afgem tu.

Mwaka 2000, mara Afgem ilipotaka kuzungushia uzio eneo la miliki yake, wachimbaji wadogo waliwavamia. Askari wa ulinzi wa Afgem walifyatua risasi, wakawaua wachimbaji wadogo saba na kujeruhi wengine wengi. Mwezi Aprili, 2001, lilifanyika shambulio jingine na kijana mmoja aliuawa. Mwezi Mei uliofuata, wachimbaji wadogo makumi kadhaa walijeruhiwa wakati wachimbaji 400 walipovamia Kitalu C, wakitaka Afgem iondolewe kwenye eneo hilo (Majtenyi na Muindi, 2001).

41

Page 55: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Kutoka hapo wachimbaji wadogo wakaifungulia mashitaka Kampuni ya Afgem, wakidai kuwa askari wake wa usalama waliwatesa wachimbaji wadogo sita. Katika hati ya mashitaka mahakamani, walidai pia kuwa leseni ya uchimbaji ya Afgem ni batili, kwamba viongozi wa Kampuni huwapekua isivyo halali watembea kwa miguu na wamewazika wachimbaji wadogo 30 katika mgodi uliotelekezwa. Kutokana na kugubikwa na hali hii ya vurugu, Waziri wa Nishati na Madini akatangaza Mererani kuwa eneo lililodhibitiwa, na askari polisi hufanya doria katika kipande cha barabara kinachounganisha mji na barabara kuu eneo la uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro, umbali wa km. 14. Vilevile serikali imeunda kamati mbili kuchunguza mapigano hayo (Majtenyi na Muindi, 2001).

Afgem inaungwa mkono na Serikali ya Tanzania, ambayo inatoa rai kuwa kuifukuza kampuni hiyo itakuwa kinyume na sera inayotetea Sheria ya Madini ya Mwaka 1998. Zaidi ya hayo, Mkuu wa Mkoa, anatoa hoja kuwa kuifukuza Afgem itakuwa sawa na kukubali kushindwa na uhalifu (Majtenyi na Muindi, 2001).

Migogoro inayotokana na umilkiKitabu hiki kinafafanua umiliki kama haki ya kusimamia rasilimali. Nchini kote Tanzania (na kiasi fulani cha Kenya), Usimamizi wa Maliasili Kijamii, umeonekana kuwa ni njia bora ya kuongeza ufanisi wa Usimamizi wa Maliasili za Taifa. Hivyo Vitengo vya Usimamizi wa Fukwe katika uvuvi, Kamati za Maliasili za Vijiji katika misitu na Vyama vya Watumiaji Maji kwenye mikondo ya mito, vyote vimeundwa. Ukinzani katika mifumo hii unatokana na jinsi vinavyotumiwa na kuundwa. Hapa, jamii zinaweza zisihusishwe katika uundaji wa mifumo ya usimamizi, utekelezaji wake au hata mifumo yake ya sheria. Hali hii inaweza kufanya taasisi hizi zishindwe kutimiza kazi za usimamizi zilizokusudiwa kutekelezwa. Kwa kuongezea, mitindo ya aina hii ya utekelezaji inaweza kusababisha taasisi mpya za wenyeji zilizoundwa za usimamizi wa rasilimali kuingia kwenye mgogoro na taasisi za kijamii zilizokuwepo awali. Litakalokuwa dhahiri kutokana na mifano itakayotolewa hapa chini ni kuwa umiliki unahusiana na haki ya kuchagua matumizi ya rasilimali, na uwezo wa kuwazuia wengine wasiitumie kwa kazi tofauti. Hivyo, migogoro ya umiliki pia itahusisha migogoro baina ya aina tofauti za watumiaji wa rasilimali.

Mgogoro wa usimamizi wa Msitu wa Duru – HaitembaMsitu wa Duru – Haitemba ni msitu wa miombo wenye eneo la hekta 40,000. Katika kingo za msitu huu kuna vijiji vinane vilivyoanzishwa zamani, ambavyo wakazi wake walikuwa na udhibiti wa msitu – ingawaje haukuwa imara sana. Utengenezaji mkaa, ulimaji ndani ya msitu na makazi, na uchomaji moto wa misitu, vyote vilipigwa marufuku. Kutokana na mwongozo wa sera ya serikali, mnamo mwaka 1983 vijiji hivi vilianza hatua ya kuomba umiliki wa ardhi ya vijiji, ikiwa ni pamoja na miinuko ya misitu inayopakana navyo. Mnamo mwaka 1985 hata hivyo, Msitu wa Duru – Haitemba uliteuliwa kuwa hifadhi ili kuhakikisha kuendeleza uzalishaji wake wa siku zijazo, kuhakikisha uhifadhi wake, na likiwa ni jambo geni (wakati ule), kuufanya msitu ujigharamie wenyewe kwa usimamizi wake kwa kupitia kwa mfano, uwekaji wa vibali vya kuutumia, au faini. Udumishaji wa uhifadhi wa msitu ulikuwa ufanywe kupitia idadi kubwa ya walinzi wa msitu. Wawakilishi wa vijiji waliwaonesha waziwazi maofisa msitu wa serikali kuwa ingawaje wanaunga mkono uhifadhi wa msitu, hawakupenda kuukosa msitu wao kwa ajili ya kufanikisha jambo hili. Mara tu walinzi wa Msitu walipoanza kazi, shughuli zote za jumuia zilizofanana na hizi ziliachwa. Mashamba yalilimwa ndani ya msitu, uchomaji mkaa ulianza, ukataji miti ulianza na watu wa nje ya vijiji walipoona kuwa udhibiti wa serikali ulikuwa ni sawa na kuwa ‘huru-kwa-wote’, walianza kuleta ng’ombe wao msituni kuwalisha. “Kwa kuondoa hali ya umiliki kwa wenyeji, hata kama ni kwa udhaifu kiasi gani haki za wenyeji ziliungwa mkono na sheria au zilitekelezwa kwa vitendo, serikali pia iliondoa ulinzi wa kijadi, au utambuzi katika jamii kwa ujumla kuwa misitu haikuwa mali ya umma…” (Wiley, 1999:53-54). (Rejea: Wiley,1999).

Migogoro baina ya watumiaji rasilimali wa aina tofautiJinsi ardhi inavyozidi kuwa adimu katika maeneo ya juu ya Bonde la Mto Pangani, wakulima wanatafuta ardhi ya ziada na nafasi za umwagiliaji maji kwenye maeneo ya chini. Mapema mwaka 1946, Johnston alisema kuwa “…kadiri Wachaga wanavyopanua makazi (vihamba) yao kuelekea upande wa chini ya mitelemko ya Mlima Kilimanjaro, ndivyo watakavyoanza kuwachukia wageni ambao machifu hapo awali

42

Page 56: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

waliwaruhusu kufanya makazi” (uk.4). Mgogoro huu baina ya watu wa makabila mbalimbali huzidi pale ambapo mahitaji ya pande zote ni ardhi na maji. Mahitaji tofauti ya rasilimali hata hivyo, siyo lazima yaondoe msingi wa mgogoro. Sehemu kubwa ya ardhi katika maeneo ya nyanda za chini za bonde kiasili zilitumiwa na wafugaji wa Kimasai. Wamasai wanachukulia uhamiaji kuingia kwenye ardhi yao ya jadi kama uvamizi kwenye eneo lao, na ubadilishaji wa eneo zuri kwa malisho kwa matumizi mengine.

Wilaya ya Simanjiro iko upande wa Kusini wa mji wa Arusha na ndani yake kuna mji wa Machimbo wa Mererani. Mwaka 1995, asilimia 85 ya wakazi wake 65,000 walikuwa ni wafugaji wa Kimasai. Ufugaji mara nyingi huchukuliwa kuwa ni njia muafaka zaidi ya matumizi ya ardhi katika ardhi kame na nusu kame za Afrika. (cf Warren,1995). Mifumo hii, hata hivyo, huchukulia kiwango fulani cha rasilimali kuwa cha kudumu. Taasisi za usimamizi wa rasilimali za mifugo, mitindo ya maisha inayohusiana na miundo ya kijamii mara nyingi hujengwa katika msingi wa kuwa eneo lao halitabadilishwa matumizi yake. Hali haikuwa hivyo Simanjiro.Ardhi ya jadi ya malisho ya Wamasai wa Simanjiro imekuwa katika tishio kutoka pande tatu:

• Kilimo cha Biashara: hadi kufika mwaka 1994, hekta 50,000 za ardhi ya Simanjiro zilikuwa zimetengwa kwa matumizi ya kilimo cha mashamba makubwa ya kati ya hekta 90 na 13,000. Mashamba haya yalizalisha zaidi maharage kwa ajili ya kusafirishwa kwenda Uholanzi. Ili kuwakatisha tamaa na kuwazuia wafugaji kuchungia ng’ombe wao katika mashamba haya, mabaki yote ya mimea huchomwa mara tu baada ya mavuno (Ole Sikar, 1996:1)). Wenye ardhi pia waliwakamata ng’ombe, waliwatoza faini watu walioingia bila ruhusa, na ole Sikar anadai kuwa, waliwapiga risasi mifugo na wachungaji wao.

• Uchimbaji madini – wa viwango vidogo na vikubwa, umezuia maeneo makubwa ya ardhi ya Simanjiro ambayo ama yameharibiwa vibaya kiasi kwamba hayatoi malisho mazuri, au yamefungwa kabisa kwa kuchungia wanyama.

• Utalii: Kama ilivyokuwa kwa wafugaji ndani na kuzunguka Hifadhi ya Wanyamapori ya Mkomazi, ardhi ya Simanjiro imetengwa kwa madhumuni ya kuwalinda wanyamapori. Wamasai wa wilaya hii wanatoa hoja kuwa hii haina umuhimu, ikichukuliwa kwamba wameishi pamoja na wanyamapori kwa karne nyingi. ‘Kaya zimelazimishwa kuacha kuchunga wanyama wao katika maeneo haya. Wakati huo huo wanyamapori wameruhusiwa kula majani pamoja na wanyama wafugwao katika maeneo ya asili ya kuchungia kama vile nyanda tambarare za Simanjiro’ (ole Sikar, 1996:2). Kwa nyongeza, Wamasai wanalalamika, wanyamapori huambukiza mifugo yao maradhi. Wamasai wa Simanjiro hawakufidiwa kwa malisho yaliyopotea wala mifugo iliyokufa kwa magonjwa ya wanyamapori.

Mielekeo hii imetokea kinyume na misingi ya sera rasmi ya serikali inayotaka kuwepo,hususan, uwekezaji wa viwango vikubwa katika kilimo na viwanda unaokusudia kukidhi mahitaji ya nchi zaidi ya maslahi ya wafugaji wenyeji. Hivyo mikakati inayokusudiwa kufikia malengo ya taifa inaweza kusababisha ugumu wa kutatua matatizo ya usimamizi wa ndani, na matatizo ya kutumia rasilimali zenye ugumu kuzisimamia hivyo kusababisha matumizi yaliyokithiri na migogoro mahali hapo. Kwa maana hii, migogoro ya Simanjiro na maeneo mengine ya Wamasai pia ni migogoro ya viwango, na hutoa kielelezo cha mfano wa jinsi migogoro ya viwango inavyoweza pia kuwa migogoro ya umiliki wakati huo huo.

Wilaya ya Taita–Taveta nchini Kenya haina kinga ya migogoro hii.Theluthi mbili ya ardhi ya wilaya iko chini ya wamiliki wawili tu wa ardhi na halmashauri ya jimbo. Matokeo yake, idadi kubwa ya wenyeji wa Taita–Taveta wanakaa katika maeneo kinyume cha sheria. Vilevile kuna mgogoro mkubwa kati ya watu wasio na ardhi na wale wanaomiliki ardhi. Migogoro kama hii inaleta utata sana katika usimamizi wa maliasili za wilaya, tatizo ambalo linakwenda hadi kwenye sekta ya maji.Wakazi wasio rasmi wanaolima katika eneo hili nusu kame wanategemea zaidi umwagiliaji (Musyoki, pers.comm.). Hata hivyo, hawana vibali vya maji kama inavyotakiwa wawe, na maji mengi zaidi hata hivyo, yanatumiwa katika maeneo ya juu ya mto na makampuni makubwa ya katani wilayani. Kwa kiasi fulani katika juhudi za kushughulikia mgogoro wa eneo hili, serikali imenunua hekta 9,700 katika jitihada za kutafuta ardhi kwa ajili ya wakulima wadogo wadogo.

43

Page 57: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

44

Migogoro kati ya mitazamo inayotofautiana ya usimamizi wa maji: mfano kutoka Mlima Kilimanjaro Tagseth (2002) anaonelea kuwa kushindwa kwa mifumo ya utawala rasmi katika bonde kutambua haki za kimila za maji na utawala wake umekuwa chanzo cha mgogoro kati ya maslahi ya kimila na utawala rasmi wa Bonde la Mto Pangani. Moja ya njia iliyotumiwa na utawala rasmi katika bonde ni utumiaji wa milango (banio) ya kudhibiti maji. Inasemekana kuwa, kwa kuwa jamii za wamwagiliaji wa viwango vidogo hawakushirikishwa kwanza, walichukulia udhibiti huo kama ukiukaji mkubwa wa haki zao za kupata maji. Kwa sehemu kubwa, milango hiyo imehujumiwa au imeharibiwa kabisa (Mchoro wa 4).Katika maeneo mengine, wanavijiji wamechimba sehemu mpya za kuchukulia maji katika kingo za mto kuzunguka milango ya kudhibiti maji (Shishira, 2002).

PAMOJA (2002) inaeleza kuwa jamii zilizoko katika bonde zinachukulia kupata maji kama moja ya haki zao za msingi, na hawaridhiki na jitihada za serikali za kuweka ada na sheria kwa matumizi yake. Sehemu kubwa ya ukinzani wa jamii kwa utawala wa Bonde la Mto Pangani unatokana na mtazamo wao kuwa watumiaji wakubwa wa kibiashara wanapendelewa kuliko wao wenye matumizi madogo zaidi ya maji. PAMOJA inadai kuwa utara-tibu wa Serikali wa amri kutoka juu kwenda chini, ambao hauna majadiliano ya pande mbili, huleta ugumu wa kutatua migogoro. Wanafikiri kuwa njia za majadiliano, zina uwezo wa “kutoa mwelekeo kwenda mbele na kuyafikia mahitaji na dhamira za watunga sera, watunga sheria na jamii kadhalika” (PAMOJA 2002:2).

Katika Mlima Kilimanjaro, Mwenyekiti wa kamati ya mfereji alikuwa akisimamia kijadi mfereji wa umwagiliaji. Daima wenyeviti huwa wanaume, na wanapatikana kutokana na ukoo wa mtu ambaye ndiye aliyechimba mfereji huo. Mfereji hupitia kwenye ardhi ya watumiaji mbalimbali maarufu wa maji, wengi wao wakiwa wa-nahitaji kuyatumia kwa madhumuni ya umwagiliaji. Ili kuweza kupatiwa maji, watumiaji lazima wawachangie wafanyakazi wa ukarabati ambao mara kwa mara hufanya doria kwenye mfereji kukagua uharibifu. Sheria mbalimbali za ziada zinasimamia matumizi ya maji, kama vile nyakati ambazo maji yanaweza kuchukuliwa, zamu za matumizi ya maji baina ya watumiaji na kadhalika. Sheria hizi sio kuwa hazibadiliki. Hii ni muhimu kwa sababu baadhi ya watu walio kando kando ya mifereji wanaweza kuhitaji maji kidogo kuliko wengine, wakati wengine wanahitaji maji mengi zaidi. Gillingham (1999) anaelezea njia tano ambazo watu wanao-hitaji maji zaidi kuliko vibali vyao vinavyoruhusu wanaweza kupata maji ya ziada: ya kwanza ni ‘kuazima’ maji - mtu anayehitaji maji zaidi anaweza kuazima maji kutoka kwa mtu anayemfahamu kuwa anahitaji maji kidogo. Hii ndiyo njia inayotumika zaidi ya kupata maji ya ziada kwa mtu anayehitaji. Njia ya pili ni ya kupata maji ya ziada kutoka kwenye mfereji wa jirani. Njia ya tatu ni kununua maji – hapa, mtu aliyetumia maji kidogo kuliko anayohitaji anaamua kuuza yaliyobaki kwa mtu anayemjua kuwa anahitaji maji mengi kuliko mgao wake. Kwa vile maji yanachukuliwa kuwa ni ‘zawadi kutoka kwa Mungu’, hivyo si halali kuyanunua wazi wazi. Wauzaji hukwepa ukweli huu kwa kutoa kazi kwa mnunuzi, na hivyo wakiulizwa husema kuwa mnunuzi anaazima mabaki ya mgao wao wa maji. Njia ya nne ni kumwagilia usiku wakati ambapo hakuna mgao wa maji. Mwisho, njia ya tano ya kupata maji ya ziada ni kwa kuiba, kwa mfano kumwagilia wakati ni siku ya zamu ya mtu mwingine, ingawaje hii haitokei mara kwa mara (Gillingham, 1999).

Sheria kuweza kubadilika badilika, Gillingham (1999) anaeleza, ‘….ni muhimu kwa ufanisi wa mgao na uendelevu wa mfumo wa umwagiliaji …… kama watumiaji wote wa mifereji wangelazimika kutumia mgao wao rasmi tu, mfumo wa umwagiliaji wa kutumia mifereji ungetosheleza mahitaji ya umwagiliaji ya watumiaji mifereji wachache sana’. Gillingham anasema mfumo huu ni wa kutegemewa, kwa sababu wizi hauruhusiwi chini ya mfumo rasmi wa ugawaji wala chini ya kanuni za kazi – laiti kama mfumo huu ungekuwa si wa kutegemewa, watu wasingechangia ukarabati wa mifereji. Uhusiano mkamilifu baina ya sheria rasmi na za kazi unachukua muda mrefu kukua – mifereji ya kwanza kwenye Mlima Kilimanjaro ilichimbwa katika karne ya 18. Katika maeneo ya nyanda za chini, ambako makazi yameanza hivi karibuni, hali ya hewa imekuwa kavu zaidi, watu wametawanyika zaidi na tofauti za kijamii zimekuwa kubwa zaidi, hivyo uhusiano kati ya sheria rasmi na za kazi sio mkubwa sana.

Sheria hizi zinasisitiza usawa wa jamii na kupunguza migogoro. Hazikai vizuri na sheria mpya, zinazoshinikizwa kutoka nje ambazo zinataka matumizi bora ya maji. Kwa nyongeza, sheria hizi mpya zinataka kuanzisha Vyama vya Watumiaji Maji (WUAs), ambavyo si sawa na Kamati za Mifereji. Vyama vya watumiaji maji

Page 58: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

45

vinategemewa kukusanya ada kutoka kwa watumiaji maji ambazo zitachangia kulipia kibali cha kutumia maji, inayopatikana kutoka Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani. Katika utamaduni ambapo maji yanaonekana kuwa ni ‘zawadi kutoka kwa Mungu’, wazo kuwa ni lazima maji yalipiwe halina mantiki. Kwa nyongeza, Gillingham anahofia kuwa sheria zilizoamriwa kutoka nje hazielekei kufanikiwa kuliko zile zilizotokea ndani ya jamii, ambazo zimebadilishwa kulingana na sifa za utamaduni na mazingira ya jamii kwa muda wa kipindi kirefu. Gillingham anaamini kuwa kutooana kati ya mchakato wa usimamizi katika ngazi ya wenyeji na ile ya ngazi ya nje kunaweza kuhatarisha mafanikio ya juhudi za usimamizi zilizoanzia nje.

Migogoro inayotokana na mahaliWatumiaji maji waliopo katika maeneo ya juu ya mto wapo mahali pazuri zaidi pa kupatia maji kuliko watumiaji wa eneo la chini. Kama msingi wake mkubwa, matatizo haya yanaonekana katika mifereji ya umwagiliaji ambapo watumiaji walio karibu na chanzo cha maji wanaweza kulima mazao yanayohitaji maji mengi sana. Kwa mfano, mpunga wa kumwagiliwa unahitaji lita 3,000 za maji kutoa mavuno ya kilogramu moja. Watumiaji waliopo mwishoni mwa mfereji, wanalazimika kulima mazao yanayohitaji maji kidogo. Matatizo makubwa yanayoikabili mitambo ya umeme wa maji iliyoko katika maeneo ya chini ya mto ni mfano mwingine.

Skimu ya Umwagiliaji ya “Lower Moshi”Kabla ya kuanzishwa kwa Skimu ya Umwagiliaji ya “Lower Moshi” mnamo mwaka 1987, kulikuwa na kiwango kidogo sana cha kilimo cha mpunga wa umwagiliaji katika eneo hili, na wakulima walitegemea kuvuna kadiri ya tani 2 za mpunga kwa hekta. Kufuatia kukamilika kwa skimu hiyo, mavuno yaliongezeka kufikia tani 8 kwa hekta, hali iliyoshawishi wakulima wa nje ya mradi kujaribu kuiga mbinu za kilimo za skimu hiyo. Matokeo yake, mahitaji ya maji yaliongezeka sana, kiasi cha kusababisha tatizo la kudumu la upungufu wa maji katika maeneo ya upande wa chini ya skimu. Skimu yenyewe imekabiliwa na upungufu wa maji kwa sababu ya matumizi makubwa ya maji katika maeneo ya juu, na imelazimika kupunguza eneo la umwagiliaji kutoka hekta 2,300 hadi 647 mnamo mwaka 1994. Wakulima waliohusishwa katika Skimu hawakufurahia kabisa hali hiyo, walieleza kuwa mgao wao wa maji ulifuata programu iliyopangwa vizuri. Watumiaji wa maeneo ya upande wa juu hawakuwa na programu kama hii, hivyo walisababisha upungufu wa maji katika eneo la Skimu. Zaidi ya hayo, wakulima walidai kuwa watumiaji maji wa maeneo ya upande wa juu walikuwa na ushawishi katika serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM), (chama tawala cha Tanzania), hivyo wasingeweza kubughudhiwa (Mujwahuzi, 2001; 134 na 136).

Mgogoro baina ya wamwagiliaji wadogo na Shirika la Ugavi wa Umeme TanzaniaTANESCO inadai kuwa inahitaji angalau mita za ujazo 40 kwa sekunde kuendesha mitambo ya umeme wa maji ya Maporomoko ya Pangani . Baada ya maji kufunguliwa kutoka katika Bwawa la Nyumba ya Mungu na kuingia mto Pangani, maji ya nyongeza yanaungana na mto huo kupitia vijito vyake vichache. Hata hivyo hadi maji yafikapo kituo hicho, mara nyingi huwa hayatoshelezi kuendesha mitambo. “Wakati mwingine tunakuwa na maji kidogo mno kiasi kwamba inabidi tufunge kituo na kuacha maji kujikusanya kwa usiku mzima, ili tuweze kufungua tena asubuhi” (Lugeiyamu, Mhojiwa).

Kadiri ardhi inavyokuwa adimu zaidi na zaidi katika sehemu za juu za bwawa la Nyumba ya Mungu, kilimo katika eneo la upande wa chini wa bwawa pia kimeongezeka. Kwa kuwa hali hapa ni ya joto zaidi na mvua ni haba, haja ya kumwagilia ni kubwa zaidi. Kwa hiyo, Meneja wa kituo cha uzalishaji umeme cha maporomoko ya Pangani analalamikia uchukuaji wa maji usiodhibitiwa ambao unasababisha wao kupata kiasi cha maji kisichotosheleza mahitaji. Anafafanua kuwa wakati ambapo maji kwa ajili ya mitambo yake yamepungua, maeneo ya umwagiliaji hayapungukiwi. “Wamwagiliaji wadogo hawatumii umeme, hivyo hawayaelewi matatizo haya” (Lugeiyamu, Mhojiwa).

Wakati huo huo, udhibiti wa uchukuaji wa maji umepungua. Wakati mradi mpya wa Maporomoko ya Pangani ulipojengwa, kulikuwa na fedha za kujengea milango (banio) ya kudhibiti maji kwenye sehemu muhimu za kuchukulia maji kutoka mitoni na ufuatiliaji wake. Kwa vile utoaji wa fedha umepungua, ufuatiliaji umekuwa siyo wa mara kwa mara, milango ya kudhibiti uchukuaji maji imeharibiwa na /au vituo vipya vya kutolea maji vimeanzishwa kwenye kingo za mito.

Page 59: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

46

Matokeo ya hali hii ni kupungua kwa uzalishaji wa umeme. Katika mwezi Aprili mwaka 1999, kituo cha uzalishaji umeme cha maporomoko ya Pangani kilizalisha kWh milioni 45. Mwezi Aprili mwaka 2002 zilizalishwa kWh milioni 25. Ni dhahiri kuwa hili lina athari ya wazi kwenye uvutiaji wa uwekezaji kwenye mtambo. TANESCO, kwa sasa, inataka kubinafsishwa. “Kama mtambo wa kuzalisha umeme wa Nyumba ya Mungu una uwezo wa kuzalisha MW 8 na tunaweza kutoa 3 tu, ni nani atakayewekeza kwetu?” (Lugeiyamu, Mhojiwa).

C.8 Majumuisho ya hojaKwa undani wake, matatizo yanayokabili matumizi ya rasilimali katika Bonde la Mto Pangani yanahusiana na ongezeko la watu katika mazingira ya viwango vikubwa vya umasikini. Umasikini na uharibifu wa mazingira mara nyingi huonekana vinahusiana (cf. WCED, 1987). Matatizo ya kusimamia Rasilimali za Jamii (CPRs) mara nyingi yanafikiriwa kuongezeka kunapokuwa na idadi kubwa ya watu wanaohusika, hususan pale umoja wao wa kijadi unapokuwa dhaifu (cf. Ostrom, 1990). Muundo na kazi za utafutaji maisha vijijini unaweza kuhatarishwa endapo uwezo wa watu wa vijijini wa kutawala na kujihakikishia njia za kutosha za kujipatia riziki zitakuwa hatarini.

Sura hii imepitia matatizo haya kwanza kwa kuainisha ‘vivutio’ vikuu ndani ya bonde. Baada ya hapo ikaendelea kuangalia migogoro mbalimbali iliyomo baina yao. Dondoo muhimu zinazoweza kupatikana kutokana na majadiliano haya ni kama ifuatayo:

• Shughuli muhimu katika bonde ni pamoja na shughuli za viwanda (umeme, madini na kilimo), kilimo (mashamba makubwa na madogo, yote kwa kiasi kikubwa yanategemea umwagiliaji), shughuli za ufugaji (hususan katika nyanda za chini), na shughuli za mijini ambazo zinakua. Sura hii ililenga kimsingi kwenye matumizi ya maji ya shughuli hizi. Waliofanya kazi kati ya shughuli hizi mbalimbali na wingi wa maliasili ndani ya bonde hili ni pamoja na mashirika yasiyo ya kiserikali na wakala wa wahisani wa kimataifa. Mamlaka yao kimsingi ni kuhifadhi na/ au kuendeleza na kuwezesha upatikanaji wa riziki vijijini.

• Ni muhimu kutambua kuwa idadi ya watu katika bonde hili ni kubwa, na kwamba kwa wengi wao, riziki hupatikana kutokana na kilimo, na kwamba kuna mengi yanayoashiria kwamba wako hatarini kiuchumi. Kwa kuongezea, utofauti na utajiri wa rasilimali za bonde hili una maana kuwa wenye shughuli kubwa kubwa wanavutiwa na bonde hili, na uwekezaji wa kutosha umefanyika. Kati ya shughuli hizi za viwango vikubwa na shughuli za viwango vidogo vya kujipatia riziki, kuna mwanya mkubwa wa migogoro.

• Sura hii inaigawa migogoro katika makundi makuu matatu yanayohusiana. Kundi la kwanza linahusiana na migogoro ya viwango, ambapo imeelezwa kuwa watumiaji wadogo wadogo mara nyingi inabidi washindane dhidi ya watumiaji wakubwa kwa rasilimali hizo hizo. Kundi la pili linahusiana na migogoro ya umiliki. ‘Umiliki’ hapa una maana ya haki ya mtu kusimamia rasilimali zake, na mgogoro hutokea baina ya vyanzo tofauti vya usimamizi na kipaumbele. Daraja la tatu la mgogoro linahusiana na mahali. Hapa, jinsi mahali pa kundi la watumiaji wa rasilimali panavyoweza kuwaingiza kwenye mgogoro na watumiaji wa mahali pengine, ni jambo lililoangaliwa. Mfano mzuri wa mgogoro kama huo ni ule baina ya watumiaji wa maeneo ya juu na wale wa maeneo ya chini ya mto.

• Kwa hiyo, ni wazi kuwa tofauti ya rasilimali katika Bonde la Mto Pangani husababisha pia aina tofauti za migogoro. Changamoto ya Bonde la Mto Pangani ni kwa kiasi gani menejimenti inaweza kushughulikia migogoro ya viwango vyote na matatizo ya ugawaji wa maliasili yanayoambatana.

Page 60: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

47

D Usimamizi wa Maliasili katika Bonde la Mto Pangani

D.1 Utangulizi

Sura hii inaangalia Usimamizi wa Maliasili za Bonde la Mto Pangani. Katika sehemu ya kwanza, utawala ‘rasmi’ wa bonde unaangaliwa. Mikono mingi ya serikali inalitawala bonde hili. Hili pekee ni tatizo kwa sababu inaweza kumaanisha kuwa juhudi za tawi lolote zinaweza kudhoofisha shughuli za matawi mengine. Kwa mfano, juhudi za hifadhi ya maji zinaweza kudhoofishwa na shughuli za maendeleo ya umwagiliaji. Zaidi ya hayo, serikali kuu inaweza kutaka kutekeleza sera za taifa katika bonde bila kuzingatia hali ya mahali, mahitaji na matatizo ya rasilimali. Mwishowe, humaanisha pia kupatikana usimamizi ambao kwa kiwango kikubwa ni mwelekeo wa kisekta unaosababisha,idara za misitu kutokuwa na habari, kwa mfano, kuhusu juhudi za uendelezaji wa wanyamapori. Wakati juhudi za uendelezaji wa wanyamapori zinaweza zisihusike na misitu moja kwa moja, huwa zinahusika na usimamizi wa jumla wa bonde, ambao sekta hizi zote ni sehemu yake muhimu. Sehemu ya kwanza ya Sura hii inazingatia shughuli za sekta kuu mbili katika Bonde: maji na misitu, na kuzitathmini katika mtazamo wa utoaji huduma ya usimamizi.

Sehemu ya pili inazitathmini shughuli za usimamizi katika ngazi ya jamii, wakati ya tatu inazingatia usimamizi wa bonde kuvuka mipaka ya nchi. Sehemu ya nne inashughulikia matatizo ya ufuatiliaji na ukusanyaji data katika bonde. Sehemu ya mwisho itatoa muhtasari wa matokeo ya Sura hii.

D. 2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na seraUtawala wa maji: sheria na sera

Sheria mama ya kusimamia rasilimali za maji Tanzania ni Sheria ya Usimamizi wa Rasilimalui za Maji ya mwaka 2009 inayoweka misingi ya kutekeleza Sera ya Maji 2002. Sheria hii inafuta sheria ya zamani ya Udhibiti wa Matumizi ya Maji ya mwaka 1974. Sheria ya Udhibiti wa maji ilianzisha mfumo wa kusimamia rasilimali za maji kwa kufuata mipaka ya mabonde. Kwa mujibu wa sheria hiyo na marekebisho yake ya 1981 mabonde 9 yalianzishwa na kuchapishwa katika gazeti la serikali lakini ilichukua miaka 10 kwa mamlaka (ofisi za maji) za kudhiti matumizi ya maji kuanzishwa Ofisi ya Maji Bonde la Pangani ilikuwa ya kwanza kuanzishwa mwaka 1991 ikifuatiwa na Ofisi ya Maji Bonde la Rufiji mwaka 1993, kufikia 2004 ofisi za mabonde yote 9 zilikuwa zimeanzishwa. Kuanzishwa kwa ofisi ya Pangani ilitokana na shauku ya wafadhili wa mradi wa umeme kwenye maanguko ya Pangani kuwa maji yasingetosha kwa mradi huo kama kusingekuwa na udhibiti wa matumizi ya maji ya mto Pangani na wakati huohuo migogoro mingi ya matumizi ya maji inajitokeza na kuongezeka katika mabonde ya Pangani na Rufiji.

Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji inaweka mfumo wa kisheria na kitaasisi kwa usimamizi wa mabonde ya mito kama sera inavyoelekeza na imeweka ngazi tatu za usimamizi: Taifa, Bonde na Mabonde madogo. Serikali za mitaa na vyombo vya kijamii au jumuiya za watumia maji ni washirika wakuu katika baadhi ya taasisi hizi na Waziri anaweza kukasimu baadhi ya majukumu kwa vyombo hivi. Maji ni rasilimali ya umma na yamekasimiwa kwa Rais kwa faida ya raia; hivyo kitaifa Waziri mwenye dhamana ya maji ni msimamizi mkuu wa shughuli zote za rasilimali za maji na mwenye mamlaka ya rufaa. Waziri anao wajibu wa kutayarisha wa Sera ya Taifa na mkakati, kuteua Wajumbe wa Bodi ya Maji ya Taifa, Mkurugenzi wa Rasilimali za Maji na Maafisa wa Maji wa Bodi za Madonde. Waziri anaunda Bodi za Maji za Mabonde na kamati za mabonde madogo na kuwezesha uratibu na upangaji mipango wa kisekta. Waziri anasaidiwa na Mkurugezi wa Rasilimali za Maji, kushauriwa na Bodi ya Maji ya Taifa katika masuala ya uratibu wa sekta mbalimbali kuhusu mipango na usimamizi shirikishi wa rasilimali za

Page 61: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

48

maji. Mkurugenzi ni mshauri mkuu wa Serikali juu ya masuala yote ya rasilimali za maji, anasimamia na kuratibu shughuli za Bodi za Mabonde, kuandaa Mpango wa Kitaifa wa Rasilimali za Maji na kutayarisha mkakati wa utekelezaji wake, kuratibu utayarishaji wa mipango ya mabonde na kwa ujumla kuhakikisha uratibu wa maendeleo ya rasilimali za maji, usimamizi na udhibiti wake.

Bodi mpya za maji zina mamlaka katika mambo yote yanayohusu ugawaji usimamizi na kulinda rasilimali za maji katika bonde husika na uandaaji wa sera na mipango inayolenga katika usimamizi na uendelezaji wa rasilimali za maji na kuzuia uchafuzi wa maji. Bodi za maji zina uwezo wa kisheria na kiutendaji katika kuandaa mipango ya maji inayojumuisha mipango ya sekta zingine na mipango ya wilaya. Bodi huratibu shughuli za sekta mbalimbali katika mambo yanayohusu maji, zinaidhinisha utoaji wa vibali vya kutumia maji, hufuatilia, hutathmini na kuidhinisha ujenzi wa miundo mbinu ya maji na kwa ujumla hufuatilia hali ya mito, maji chini ya ardhi, mabwawa na maziwa, ardhioevu na hutekeleza sheria. Bodi za maji humshauri mkurugenzi wa maji na huratibu shughuli za kamati za mabonde madogo. Afisa wa Maji wa Bonde ni mtendaji mkuu wa bodi mwenye majukumu ya kusimamia shughuli zote za bodi na ni katibu wa bodi. Bodi ya maji ya Pangani inategemewa kufanya kazi kwa kufuata mfumo wa kitaasisi kama unavyoelekezwa na Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji ya mwaka 2009.

Ofisi ya Maji Bonde la Pangani hushawishi uundaji wa vyombo vya watumiaji maji na kwa kawaida wakulima wadogo wadogo wanaotumia chanzo kimoja cha maji na miundombinu moja ya kuchukua maji wanajiunga katika umoja wa watumiaji maji ambao huomba kibali cha kutumia maji kwa niaba ya wanaumoja wake. Ingawa vyombo vya watumiaji wa maji ni vya manufaa kwa washiriki mitazamo ya watu wengine ni kuwa vyombo vya watumiaji wa maji ni vya manufaa kwa ofisi ya bonde kwani hukusanya ada ya maji kutoka kwa mtumiaji maji mmoja mmoja. Umoja wa watumiaji wa maji hukusanya maduhuli kutoka kwa washiriki wake kwa ajili ya uendeshaji wa mradi na kiasi kidogo hutumika katika kulipia ada ya hutumia maji.

Ofisi ya Maji ya Bonde inahimiza uundaji wa Vyama vya Watumiaji Maji (WUAs), na kwa hakika, maji kwa ajili ya umwagiliaji yanaweza kuombwa na vyama hivyo pekee. Hili linasemekana kuwa linarahisisha shughuli za utawala, kwa sababu Ofisi ya Bonde itakuwa inashughulika na Vyama badala ya watu wengi binafsi. Vyama vya watumiaji maji vinatarajiwa kukusanya ada kutoka kwa watumiaji maji ambayo hatimaye itatumika kulipia hati zao za maji.

Mwanzoni mwa miaka ya 1990, wenye hati za maji katika Bonde la Mto Pangani walitumia jumla ya mita za ujazo 33.4 kwa sekunde, lakini ukaguzi uliofanywa na Ofisi ya Bonde mwaka 1992/93 ulionesha kuwa matumizi halisi yalifikia mita za ujazo 48 kwa sekunde (Mujwahuzi, 2002). Kuna hati za maji 567 za kudumu katika mikoa minne ya Tanzania ambayo imo katika Bonde la Mto Pangani, wakati ambapo hati za muda zilizotolewa ni 300. Hata hivyo, kuna karibu matumizi mara mbili zaidi yanayofanyika bila ya hati za maji (Jedwali la 6). Karibu asilimia 46 ya hati za kudumu na za muda zilizotolewa zinatoka mkoa wa Kilimanjaro. Karibu asilimia 66 ya matumizi ya maji yasiyo rasmi kisheria katika bonde hutokea katika mkoa huu.

Kwa hiyo ni wazi kuwa kuna matatizo makubwa katika kufuatilia matumizi ya maji na katika kutekeleza vifungu vya sheria ya maji ya Tanzania. Baadhi ya matatizo yanayoikabili Ofisi ya Maji ya Bonde ni haya yafuatayo:

• Ingawa kuna vituo vingi vya upimaji/ufuatiliaji katika eneo lote la bonde, uendeshaji wake siyo sahihi, na mara nyingi data zinapingana kwa sababu vituo vinakwama kufanya kazi. Ufuatiliaji kwa kutumia watu pia unafanyika lakini wakusanyaji data mara nyingi hawalipwi vizuri na hukosa motisha ya kukusanya data hizi. Matokeo yake, hati za maji hutolewa bila kujua kwa hakika kiasi cha maji kinachopaswa kugawanywa. Data muhimu za ziada, kama vile data za mtiririko wa maji kwa ajili ya mahitaji ya mazingira, hazipatikani, na Ofisi ya Bonde haifahamu ni kiasi gani cha maji ni lazima kibakizwe katika bonde kwa matumizi ya mifumo ikolojia (Sarmmet, Mhojiwa)

• Kwa vile matumizi mengi ya maji hayana hati za kisheria, si rahisi kwa Ofisi ya Maji Bonde la Pangani kujua kiasi halisi cha maji kinachukuliwa.

• Ofisi ya Maji ya Bonde la Mto Pangani na ofisi za mabonde mengine hazina uwezo wa kitaasisi na kifedha wa kusimamia kufuatilia na kudhibiti matumizi yote ya maji katika bonde. Ndiyo maana, milango mingi ya kudhiti maji iliyojengwa na ofisi ya bonde la Pangani katika makutano ya mifereji na mito mwaka wa 1994 ilibomolewa na wananchi ambao hawakutambua matumizi yake na

Page 62: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

ambao walikuwa hawataki kulipa ada za maji. Uharibufu huu ungeweza kuzuilika kama wahusika wangeelewa manufaa ya milango hiyo na kama serikali za mitaa zingehusishwa mapema katika kuandaa mpango wa ujenzi huo.

• Ofisi ya Maji Bonde la Pangani inapaswa ijitegemee kiutawala na kifedha. Hata hivyo, watumiaji wengi wa maji wanaamini kuwa maji ni ‘zawadi kutoka kwa Mungu’, na hukataa kulipia hati zao za maji, pamoja na viwango kuwa vya chini sana. Hivyo Ofisi ya Bonde inakabiliana na matatizo makubwa ya uhaba wa fedha. Sheria iko kimya kuhusu jinsi ya kuwashughulikia wadaiwa. Matokeo yake, karibu asilimia 60 ya madai ya ada ya matumizi ya maji kwa mwaka hayalipwi (Sarmett na Kamugisha, 2002).

• Sheria ya usimamizi wa rasilimali za maji hajaweka uhusiano wa moja kwa moja kati ya Bodi ya Maji Bonde la Pangani na Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs) au ngazi za chini za utawala kusaidia uwakilishi katika bodi ya bonde na kamati za mabonde madogo. Hata hivyo, Waziri anaweza kukasimu utekelezaji wa jukumu lolote kwa mamlaka ya serikali za mitaa kama ilivyoelekezwa katika sheria. Maafisa wa Maji si sehemu ya mamlaka za serikali za mitaa na hawana majukumu sawa katika bonde, lakini ni muhimu wakafanya kazi pamoja kwa misingi ya shabaha moja lakini yenye utekelezaji tofauti. Kufanya kazi na LGAs na mkusanyiko wa wadau wengine na mahitaji mbalimbali ya kisekta ni changamoto kwa Maafisa wa Maji ambao wanatakiwa kuwa weledi kwa mtazamo huu. Kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji, Bodi za Mabonde zinatakiwa kujumuisha mipango ya Wilaya ndani ya mipango ya usimamizi wa rasilimali za maji wa mabonde yao ambayo itakuwa na nguvu za kisheria kwa wahusika wote ndani ya bonde.

• Mipaka ya kisheria ya utawala wa Ofisi ya Bonde ni Bonde la Mto Pangani, ambalo halifuati mipaka rasmi ya kiutawala. Katika bonde hili, Ofisi ya Maji Bonde Pangani inatakiwa kufanya kazi na serikali za mitaa nyingi sana.

• Mabonde ya mito yana idadi kubwa ya rasilimali zinazohusiana na mabadiliko ya rasilimali moja yanaweza kuwa na athari kwa rasilimali nyingine. Katika Bonde la Mto Pangani, upangaji wa mipango ni wa mgawanyiko, kwa misingi ya kisekta, kimkoa au kiwilaya. Bodi za maji zina mamlaka na zinaagizwa na sheria ya maji kuandaa mipango jumuishi ya usimamizi wa rasilimali za maji katika mabonde yao ambayo itakuwa na nguvu za kisheria kwa uendelezaji, usimamizi na utunzaji wa maji wowote.

Utawala wa maji nchini Kenya unaongozwa na Sheria ya Maji ya Mwaka 2002 (RoK, 2002). Mpaka sasa, kadiri usimamizi wa mabonde kwa mapana unavyohusika (kipengele ambacho kimo katika Sheria ya Maji), Mkakati wa Usimamizi wa Rasilimali za Maji wa Taifa (RoK, 2003) unakuwa na umuhimu mkubwa.

Sheria ya Maji ilianzisha Mamlaka ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji (WRMA) yenye jukumu la usimamizi na utawala wa sehemu kubwa ya rasilimali za maji za Kenya. Kuna asasi kadhaa zilizopangwa chini ya WRMA, ambazo zinaelezwa katika Kisanduku kifuatacho. Hapa, ushirikishwaji wa wadau katika usimamizi na utawala wa Sheria unazingatiwa.

Kitengo cha usimamizi ambacho WRMA inategemewa kulenga ni eneo la chanzo cha mto, ambalo linatakiwa kuliaainisha. Kila eneo la chanzo cha mto linapaswa kuwa na Kamati ya Ushauri (CAAC) ya watu 15, walioteuliwa na WRMA, na kuwa na wawakilishi kutoka sekta mbalimbali za wadau binafsi na za umma. Chini ya Sheria ya Maji, CAAC ina wajibu wa ‘kuwashauri maafisa wa mamlaka hii (WRMA) katika ofisi stahiki ya mkoa kuhusu:

a) hifadhi, matumizi na mgao wa rasilimali ya maji;b) utoaji, urekebishaji, ufutaji au ubadilishaji wa kibali chochote [cha maji]; nac) masuala mengine yoyote yanayoambatana na usimamizi mzuri wa rasilimali ya maji (RoK, 2000: 953).

Mamlaka halisi ya usimamizi wa Sheria ya Maji (ikiwa ni pamoja na uwezo wa kumtia mtu nguvuni, kushtaki na kutoa vibali vya maji) yako mikononi mwa WRMA. Aidha imepewa wajibu wa kuendeleza mkakati wa maji wa taifa ambao ulichapishwa mwaka 2003 (Rok, 2003). Mkakati huo unaelezea uhusishwaji wa wadau katika usimamizi na utawala wa maji ya Kenya kama ifuatavyo: Sera ya Maji ya Taifa (NWP) inatambua hali ambapo mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) na jamii zitakuwa na majukumu makubwa katika sekta ya maji ikiwa ni pamoja na usimamizi wa rasilimali za maji. Kwa hali hii itahitajika watendaji wapya kupatiwa mafunzo ya kuwajengea uwezo …. (RoK 203:73).

49

Page 63: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Mkakati unasisitiza uhifadhi wa mazingira katika maeneo yote ya vyanzo vya mito, na unatoa mwongozo wa sera ufuatao:

‘Kuhakikisha maendeleo endelevu ya kimazingira, yanayolenga katika ushirikishaji na uimarishaji wa thamani ya mazingira na utiliaji maanani upangaji wa mipango ya rasilimali za maji, usimamizi na maendeleo na kuongeza ufahamu wa [sic] athari zake kwa afya ya binadamu, maendeleo na maliasili nyingine. Mkazo kimsingi utazidishwa kwenye kufafanua, kuboresha na kuweka wazi taasisi na michakato itakayohusika katika ushirikishwaji wa masuala ya mazingira katika usimamizi wa rasilimali za maji kwa ujumla (RoK, 2003:23).

Kwa nyongeza, Mkakati huu unasisitiza kuhifadhi vyanzo vya mito, hususan katika kuhifadhi misitu ya Kenya ambayo inapungua kwa kasi kubwa:

‘Maeneo ya vyanzo vya maji yanahitaji … kuainishwa na kuonyeshwa katika mchoro na programu za uhifadhi na ulinzi zianzishwe na wizara zinazohusika na misitu. Kwa nyongeza, kanda za hifadhi ya maji ya chini ya ardhi zitahitajika kuainishwa kuepuka umalizikaji wa rasilimali hii ili kukuza usimamizi shirikishi wa vyanzo vya mito. Wadau wote watahimizwa kutumia rasilimali zao katika kulinda vyanzo vya maji vya nchi yao (RoK, 2003:33).

Katika hali hii, Sera ya Maji ya Kenya inaeleza misingi ambayo usimamizi wa rasilimali za Bonde la Mto Pangani zinazovuka mipaka ya nchi unaweza kufanyika, ikitiliwa maanani kuwa ukataji miti kwenye mitelemko ya Mlima Kilimanjaro (nchini Tanzania) huathiri moja kwa moja kina na ubora wa maji ya Ziwa Jipe (nchini Kenya).

50

Jedwali la 6: Hati za kutumia maji katika Bonde la Mto Pangani (Tanzania), Mei 2003

Mkoa Hati za Hati za Maombi Bila Hati Jumla kudumu muda ya hati ya hati zisizotumika kwa muda

Arusha 184 135 57 141 144 661

Manyara 3 3 2 10 0 18

Kilimanjaro 264 138 118 1224 203 1947

Tanga 116 24 25 488 118 771

Jumla 567 300 202 1863 465 3397

Dondoo

Hati ya kudumu: Hati ya iliyotolewa kuwa ya kudumu na inayotumika.

Hati ya muda: Hati iliyotolewa kwa muda, ili mwombaji amalizie ujenzi wa mifumo ya kupitisha maji kama inavyotakiwa na PBWO. Kwa kawaida mtumiaji hupewa mwaka mmoja wa kufanya hivyo, baada ya muda huo lazima aombe kuongeza muda kama hajamaliza.

Maombi ya hati: Ombi linalotolewa kwa PBWO, ambayo inashughulikia maombi hayo kwa kufuata taratibu zilizopo kabla ya kufikisha katika kikao cha PBWB kwa ajili ya idhini na utoaji wa kibali.

Bila ya hati: hawa ni watumiaji wasio na hati ya kisheria (wanatumia bila hati). Nusu ya hawa wanakisiwa kila mmoja anachukua lita 10 kwa sekunde; makadirio haya yanahitaji kuthibitishwa.

Hati zisizotumika kwa muda: Hizi ni hati zilizotolewa, lakini wamiliki wake kwa sasa hawatumii maji. Kama hati haitumiki kwa miaka mitatu, hufutwa. Tathmini ya hati na matumizi ya maji inahitajika ili kubainisha idadi ya hati zilizolala katika bonde hili, na kupitisha uamuzi kama zifutwe au la.

Rejea: Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani.

Page 64: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Utawala wa misitu, sheria na sera Usimamizi wa misitu ya Tanzania umegawanywa kati ya mamlaka kuu mbili. Mlinzi mkuu wa misitu ya taifa ni Idara ya Misitu na Nyuki (FBD), ambayo iko chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Ofisi ya Rais pia ni mhusika katika usimamizi wa misitu ya Tanzania kwa kupitia kazi zinazofanywa na tawala za mikoa na serikali za mitaa. Chombo cha tatu cha usimamizi ni Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) ambazo husimamia misitu iliyopo katika mipaka ya mbuga za hifadhi za Taifa (Lambrechts et al., 2002). Kama ulivyo utawala wa maji wa sasa, utawala wa misitu pia una pande mbili. Katika ngazi ya mkoa, Afisa Maliasili wa Mkoa (RNRO) hukaa kwenye Sekretarieti ya Mkoa akiwakilisha misitu. Wanaowajibika kwa RNRO ni Maafisa Watendaji wa Wilaya, ambao chini yao kuna Maafisa Maliasili wa Wilaya.

Utawala wa mkoa hauna mamlaka ya kisheria kwenye Misitu ya Eneo la Chanzo cha Mto. Mradi wa Misitu ya maeneo ya vyanzo vya mito (CFP) ulizinduliwa mwaka 1976 na Idara ya Misitu na Nyuki. Katika mkoa wa Arusha, hekta 118,921 za misitu zimo kwenye mradi. Katika mkoa wa Kilimanjaro ni hekta 138,785 wakati ambapo Tanga ni hekta 107,499 (Kijazi 2002). Misitu ya maeneo la vyanzo vya mito huchukuliwa kuwa ‘maeneo muhimu yaliyohifadhiwa’ na yanatawaliwa kutoka kwenye ofisi ya CFP katika

51

Kisanduku 12: Utawala wa Maji Kenya

• Waziri wa Maji: Hudhibiti rasilimali zote za maji kulingana na Sheria ya Maji ya Mwaka 2002.

• Mkurugenzi wa Maji: humsaidia Waziri kutekeleza kazi zake.

• Mamlaka ya Usimamizi wa Rasilimali ya Maji (WRMA): inafanya kazi ya usimamizi wa rasilimali ya maji.

• Kamati ya Ushauri ya Eneo la chanzo cha mto (CAAC): huwashauri maafisa wa WRMA kwa masuala ya usimamizi wa maji yanayohusiana na eneo la chanzo cha mto lililoko chini ya mamlaka yake.

• Hifadhi ya Maji ya Taifa na Shirika la Mabomba (NWC & PC): kwa niaba ya Waziri, hushughulika na uendelezaji wa miradi ya taifa inayotoa huduma ya maji mengi ya matumizi kwa wenye leseni na watoaji wengine wa huduma za maji

• Bodi ya Rufaa ya Maji (WAB): husikiliza na kuamua kesi yoyote ya mtu mwenye kibali au mali ambayo inaathirika moja kwa moja na uamuzi wa kisheria wa Mamlaka.

• Vyama vya Watumiaji wa Rasilimali ya Maji: husaidia mamlaka katika ulinzi wa rasilimali za maji katika ngazi ya chini kabisa.

Serikali za Mitaa

Mkurugenzi Mtendaji (Wilaya)

DNRO

DFO

Misitu

Misitu ya Hifadhi ya asili

Serikali kuu

FBD

RNRO

FCFO

Misitu ya vyanzo vya maji wilayani

Misitu ya uzalishaji

Mchoro wa 3: Utawala wa misitu nchini Tanzania

Page 65: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

makao makuu ya Idara ya Misitu na Nyuki, ambayo huwajibika kwa serikali kuu. Wanaowajibika kwenye ofisi ya CFP ni Mameneja wa Misitu ya maeneo ya vyanzo vya mito wa mikoa- mmoja kwa kila mkoa. Mameneja wa wilaya wa misitu ya maeneo ya vyanzo vya mito huwajibika kwa Meneja wa Mkoa. Mameneja hawa hupata fedha moja kwa moja kutoka kwenye ofisi ya CFP, na lazima wawe na mpango wa usimamizi kwa kila msitu ulio chini ya mamlaka yao. Ngazi hizi mbili tofauti za utawala zinaonyeshwa kwenye Mchoro wa 2. Katika ngazi ya wilaya, Maafisa wa Misitu wa Wilaya (DFOs) hutekeleza shughuli za Idara ya Misitu na Nyuki, ikiwa ni pamoja na ukusanyaji wa mapato. Mara nyingi, misitu ya asili na ya uzalishaji huwa chini ya utawala wa wilaya, lakini misitu ya eneo la chanzo cha mto inaweza pia kuwa chini yao. Kwa vile Maafisa Misitu wa Wilaya hukusanya mapato kwa niaba ya Idara ya Misitu na Nyuki, hivyo wale wote wenye elimu ya diploma au zaidi hulipwa na Idara ya Misitu na Nyuki (Kijazi na Nashanda, Wahojiwa).

Sera ya Misitu ya mwaka 1998 inahimiza ushirikishwaji wa jamii katika usimamizi wa maliasili na hii ni pamoja na zile jamii zinazopakana na hifadhi ya misitu ya mikoko. Mkakati wa Usimamizi unataka juhudi zifanyike ili kujumuisha jamii za wenyeji katika shughuli mbalimbali kutoka kwenye upangaji hadi kwenye utekelezaji. Shughuli hizo ni pamoja na udhibiti wa uvunaji, upandaji mikoko katika maeneo yaliyo wazi, shughuli za ulinzi kama vile doria, na uhamasishaji (Kijazi, 2002).

Nchini Kenya, misitu kwa kiasi kikubwa haijasimamiwa kikamilifu, ukweli unaoonyeshwa na kiwango cha ukataji miti cha kutisha kiasi cha kusababisha asilimia 2 hadi 3 tu ya nchi kubaki na misitu. Hatua za haraka za urekebishaji zinazofanywa na serikali, ikiwa ni pamoja na marekebisho muhimu katika Idara ya Misitu na uanzishaji wa sheria mpya ya Misitu, hazijazaa matunda. Katika sehemu ya Bonde la Mto Pangani iliyoko Kenya kuna hifadhi za misitu chache zilizosalia, isipokuwa viunga vidogo vidogo vya misitu katika Milima ya Taita, kiwakilishi pekee cha Milima ya Tao la Mashariki nchini Kenya. Matatizo mengi yahusianayo na uharibifu wa misitu yanayotokea Kenya yanahusiana na ukataji miti kuvuka mpaka wa Tanzania, hali inayotoa mfano mzuri wa haja ya kuwa na mkakati wa kutosha katika usimamizi wa kimataifa wa bonde.

D.3 Utawala wa ngazi ya jamiiMawazo kuhusu usimamizi wa pamoja wa rasilimali, hivi karibuni, yamekuwa ndio chaguo linalopendelewa katika usimamizi wa maliasili. Mara nyingi (lakini sio mara zote) wadau wanaohusika katika mpango wa usimamizi ni serikali na jamii zinazotumia rasilimali. Katika hatua hii ya majadiliano ya kina, dhana ya usimamizi wa pamoja haieleweki vizuri, kwa upande mmoja, kwa sababu ya kuwepo kwa haja ya kuendeleza mifumo ya Usimamizi wa Maliasili ambayo inalenga moja kwa moja mahali na jamii.

Mara nyingi, katika hatua hizi za mwingiliano katika usimamizi, menejimenti hutumia taasisi kama sehemu ya utawala wake. Taasisi ni “…sheria za kuendesha mambo katika jamii au, kuwa rasmi zaidi … vikwazo vilivyobuniwa na binadamu ili kutengeneza mifumo ya maingiliano ya binadamu“ (North, 1993:3). Kwa hali hii, taasisi huweka vikomo ambavyo ndani yake maisha ya watu huendeshwa. Lazima tahadhari ichukuliwe ili kuelewa kuwa taasisi sio matokeo tuli, bali ni hatua pana ambazo hubadilika ili kukabiliana na misukumo kutoka nje, mabadiliko ya ndani, migogoro na shinikizo nyingine. Taasisi za jamii zinaweza kufanya kazi muhimu katika kujitafutia njia ya kuendeleza uchumi wake na hasa, jinsi inavyopokea uchumi kutoka nje. Taasisi sio mashirika, ambayo mafanikio na utendaji wake daima unategemea taasisi.

Katika maandishi mengi kuhusu usimamizi wa rasilimali za pamoja, ni taasisi za kijadi ndizo zinazopendekezwa kuwa msingi wa maendeleo ya usimamizi wa pamoja (angalia mifano katika Berkes, 1989 na Mackay na Acheson, 1983). Kila mara hawa wanachukuliwa kuwa ushahidi kwamba jamii zina uwezo wa kusimamia rasilimali zao. Hata hivyo taasisi zina kazi maalum na ni za muda, na zinaendelezwa kutegemeana na mahitaji maalum ya kijamii na kiuchumi katika wakati na mahali maalum (North, 1993; Ostrom, 1990 Crean na Gehib 2001). Hivyo taasisi za kijadi zilizoundwa kusimamia misitu huenda zilifanya kazi katika mazingira ambayo vibali vya utumiaji vilikuwepo, masoko yalikuwa haba, na watu walikuwa wachache. Kinyume cha hali hiyo, taasisi hizi inawezekana hazikuwa na thamani kubwa kiusimamizi. Hata hivyo zinabaki na mvuto kwani huenda zinaweza kuwa na mvuto kijamii na kiutamaduni, kuliko zilivyo taasisi ngeni, zilizotoka nje.

52

Page 66: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

53

Kundi la pili la taasisi za muhimu za usimamizi ni miundo na mashirika ya serikali ambayo yamekuwepo kwa muda mrefu wa kutosha kiasi kwamba jamii inayaona kuwa ya ‘kawaida’ katika mazingira ya maisha yao ya kila siku. Kwa maana hii, miundo kama hii imefanywa kuwa rasmi kwa jamii ya wenyeji.

Kama ilivyojadiliwa kabla, Tanzania imekuwa na bidii ya kuanzisha taasisi za Usimamizi wa Maliasili za Jamii (CBNRM) katika maeneo yake yote ya rasilimali. Katika Bonde la Mto Pangani, miongoni mwa taasisi muhimu zaidi ni Vyama vya Watumiaji Maji na Kamati za Maliasili za Vijiji (VNRCs). Zote hizi mbili zinazingatiwa katika sehemu hii.

Tagseth (2002) aliainisha aina mbili za uongozi wa mifereji katika ngazi ya kijiji. Wa kwanza kati ya hizi umelenga katika vikundi vya watumiaji visivyo na majina na visivyo rasmi vilivyoelezwa hapo juu, vikiongozwa na mwenyekiti ambaye hupanga watumiaji katika vikundi kazi ili kukarabati mifereji kwa malipo ya kugawiwa maji. Wenyeviti wamekuwa wakimiliki mifereji yao kwa vizazi vingi. Mfumo huu wa kihistroria wa uongozi wa mifereji na maji yake humaanisha kuwa uongozi unaona kuwa kutafuta kibali cha kutumia maji ya mfereji, kwa mfano kutoka Ofisi ya Maji Bonde la Pangani, kuwa jambo geni kabisa.

Aina ya pili ya uongozi wa mifereji ulioainishwa na Tagseth (2002) ni utaratibu rasmi zaidi. Kiongozi wake anachaguliwa au kuteuliwa. Kuna sheria nyingi zaidi zinazotawala, kwa mfano, michango kwa skimu hiyo na ugawaji wa maji. Ugawaji wa maji unapangwa kwa kutumia ada ya uanachama, faini zitokanazo na uvunjaji wa sheria na pengine rushwa.

Ni wazi kuwa aina ya kwanza kati ya taasisi hizi mbili si rasmi, ambayo inaweza isivutie mifumo ya utawala wa serikali yenye bidii ya kuunda miundo ya kirasimu na ya kueleweka. Hata hivyo, pia ina misingi ya itikadi za asili za jamii ambayo huenda inamaanisha kuwa (a) inaweza kuwa bora zaidi katika kushughulikia matatizo na migogoro ya wenyeji; na (b) inalingana zaidi na mitazamo na mawazo ya wenyeji. Kwa maana hii, taasisi ya kwanza, isiyo rasmi, inaweza zaidi kushughulikia viwango vya juu vya tofauti za kijamii, rasilimali na kiutamaduni zilizopo katika Bonde la Mto Pangani, wakati ile ya pili isingeweza kushughulikia mawazo kama haya, yasiyo na sababu.

Awali, mawazo yanayoshutumu uanzishaji na utekelezaji wa Vyama vya Watumiaji Maji yalijadiliwa. Ilidaiwa kuwa licha ya msisitizo wa jamii uliomo katika dhana hii, Vyama vya Watumiaji Maji bado viliweka vikwazo kwa jamii ambazo hazikuviheshimu sana (PAMOJA, 2002). Hata hivyo ni lazima isisitizwe kuwa taasisi kama hizi, mbali na kuingizwa kwa nguvu katika jamii, bado ‘zinaweza kufanywa kuwa za jamii’; kwa maana kwamba zinaweza kupindishwa kukidhi mahitaji ya jamii na ili zisihatarishe matakwa ya

Kisanduku cha 13: Uanzishwaji wa usimamizi wa kijamii katika msitu wa Duru-Haitemba, Mkoani Manyara

Hapo juu, mgogoro ulioibuka kati ya wanajamii wanaoishi kandokando ya msitu wa Duru-Haitemba na serikali ya Tanzania wakati msitu ulipogeuzwa kuwa hifadhi umeelezewa. Mara ilipodhihirika kuwa msitu huu haufaidiki na usimamizi wa serikali, na kwa vile serikali za mitaa zilibakiwa na rasilimali chache za kuweza kuwahudumia wafanyakazi wa msitu, iliamuliwa kuzipa jamii nafasi ya kuuendesha msitu wao wenyewe. Sharti pekee lililowekwa ni ufanisi: kwamba Duru-Haitemba inabaki bila kukaliwa na watu, kwamba hali yake iliyoharibiwa inarejeshwa ilivyokuwa na kwamba mazao yake yavunwe kwa uendelevu.

Hatua za awali zilizochukuliwa na jamii zilianza kwa kuugawa msitu katika kanda ambazo kila jamii inazozizunguka zingewajibika nazo. Kisha mpango rahisi sana wa usimamizi ulitolewa kwa kila kanda. Mipango hii ilieleza (a) ni nani alipaswa na hakupaswa kuutumia msitu, (b) matumizi ya msitu ambayo jamii zilijiruhusu kuyatumia, (c) ni matumizi gani yangeweza kufanyika kwa mgao unaosimamiwa na kijiji na mfumo wa vibali tu; na (d) ni matumizi gani ya msitu ambayo yalizuiwa kabisa. Wavamizi walifukuzwa mara moja, uchomaji mkaa, uwindaji na ukataji miti vilipigwa marufuku, na wakataji magogo wasiokuwa wenyeji ‘walihimizwa’ kuondoka. Maeneo yaliyoharibiwa yalifungwa yasitumiwe na jamii, wakati ambapo sheria nyingi mbalimbali zilisaidia kuhakikisha kuwa matumizi yoyote yaliyofanyika yalikuwa endelevu. Misimu mipya ya “kufungwa” na “kufunguliwa” ilianzishwa ikiruhusu aina fulani za matumizi zifanyike katika maeneo fulani na nyakati fulani za mwaka (kama vile ulishaji mifugo). Mwisho vijana wa kiume kutoka katika jamii walipelekwa kufanyia doria msitu, na kuzawadiwa sehemu ya faini walizofanikiwa kukusanya (Rejea: Willy, 1999)

Page 67: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

54

jamii ya kujitafutia riziki. Hata hivyo hii haina maana kuwa taasisi ndiyo itakuwa inafanya usimamizi uliotarajiwa. Ili hili litokee, malengo ya usimamizi kwa namna fulani pia lazima yazuie hofu za jamii, na kwa kiasi fulani kuhakikisha kuwa inachangia katika kukidhi matarajio yao. Ili hili litokee, jamii lazima ishiriki katika majukumu muhimu ya kupanga na kutekeleza mifumo ya usimamizi, hususan mifumo inayohusiana na utoaji wa adhabu.

Mradi wa misitu ya maeneo ya vyanzo vya mito (CFP) katika Tanzania unasimamia misitu kwa pamoja na jamii za wenyeji zinazopakana na misitu 23 ya aina hiyo kwa majaribio. Asilimia 36.5 ya misitu katika mikoa mitatu ya Tanzania inayochangia Bonde la Mto Pangani iko chini ya Usimamizi wa Misitu wa Pamoja (JFM: Jedwali la 6). Sehemu kuu ya jamii katika juhudi hizi ni Kamati za Maliasili za Vijiji (VNRC). Kila kamati ina wajumbe kati ya 8 na 15 ambao wamechaguliwa kidemokrasia. Angalau wajumbe wawili lazima wawe wanawake. Kadiri ya kamati 129 (asilimia 70) za Maliasili za Vijiji zinashiriki katika kupanga na kufanya maamuzi, vile vile kuhamasisha wanavijiji katika Usimamizi wa Misitu wa Pamoja. Rasimu ya mipango ya usimamizi kwa ajili ya Hifadhi ya Misitu ya Jamii (CFRs) tisa zilizopewa kipaumbele imetolewa, ikiwemo Mlima Kilimanjaro, Chome na Kindoroko katika mkoa wa Kilimanjaro na hifadhi ya Kwani/Tongwe na msitu wa kilima cha Mafi katika mkoa wa Tanga.

Idara ya Misitu na Nyuki pia imetekeleza Mradi wa Usimamizi wa Mikoko (MMP), ambao ulizinduliwa mnamo mwaka 1988. Hii ilianza na utayarishaji wa mpango wa usimamizi kwa mifumo ikolojia ya mikoko ya Tanzania bara. Mkakati wa usimamizi uliobuniwa ulihitaji juhudi zifanywe kuhusisha jamii za wenyeji katika shughuli mbalimbali, kuanzia upangaji hadi utekelezaji. Shughuli hizo ni pamoja na kudhibiti uvunaji, upandaji wa mikoko katika maeneo ilikopungua, shughuli za ulinzi kama vile doria, na uhamasishaji.

Mradi wa Usimamizi wa Mikoko umehusisha vijiji 100 kati ya 130 vilivyo karibu na misitu ya mikoko katika usimamizi wake. Zaidi ya hayo, mradi umekuwa ukiboresha msitu wa mikoko kwa kukata mitambaazi katika hekta 430, na kukuza shughuli mbadala za uzalishaji kwa jamii za wenyeji, kama vile shughuli za kilimo cha mimea ya baharini na ufugaji nyuki (Kijazi, 2002).

Mradi wa Usimamizi wa Mikoko umerudisha upya uhai wa misitu ya mikoko katika hekta 1,300 kati ya hekta 2,000 zilizokusudiwa, ambapo hekta 100 zilifanyiwa kazi kwa njia ya kujitolea na wanavijiji na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayojishughulisha na mazingira. Ufanisi wa misitu iliyopandwa upya unatofautiana kwa asilimia kutoka 80 hadi 40. Hali ni duni zaidi katika maeneo ambayo kilimo cha mpunga kinafanyika, kama vile Delta ya Mto Rufiji, kutokana na baadhi ya wamiliki wa mashamba kutokubali kuruhusu mikoko kukua upya.

Kamati za Maliasili za Vijiji zinashirikiana na menejimenti ya mradi kwa kuangalia taratibu za uvunaji. Chini ya usimamizi huu, mapato ya Serikali Kuu yameongezeka kutoka TSh. milioni 12 mwaka 1999/2000 hadi milioni 17 mwaka 2001 kutokana na uuzaji wa miti ya ujenzi na ada za usimamizi kutoka kwenye visima vya chumvi (Kijazi, 2002).

Mpaka sasa katika kubuni shughuli mbadala za uzalishaji, mradi wa usimamizi wa mikoko ulipeleka mizinga 830 ya asili na 28 ya kisasa ya nyuki katika misitu ya mikoko mnamo mwaka 2001. Zaidi ya hayo, kilimo cha mimea ya baharini kinafanyika katika mwambao wa pwani.

Jedwali la 7: Eneo la misitu chini ya Usimamizi wa Misitu wa Pamoja kwa mikoa

Mkoa Eneo (Hekta) Idadi ya vijiji vilivyohusishwa

Arusha* 7,0248 70

Kilimanjaro 122,996 63

Morogoro 58,579 33

Tanga 15,233 19

Jumla 267,056 185

(Rejea: Kijazi, 2002). * inajumuisha na Mkoa wa Manyara

Page 68: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

55

Katika mchakato wa uhamasishaji, programu ya kutoa elimu ya ikolojia ya mikoko ilifanyika katika shule za msingi 47 katika Kanda za Kaskazini na Kusini. Mikutano ya vijiji, programu za redio, na maonesho ya majadiliano ya video yalitumika pia.

D.4 Usimamizi wa Bonde kimataifa

Nyenzo za kusimamia rasilimali za Bonde la Mto Pangani, kati ya mataifa wafadhili ya Kenya na Tanzania hazitoshelezi. Jitihada za kurekebisha tatizo hili kwa kiasi kikubwa zinategemea juhudi za IUCN-EARO za kuhifadhi Ziwa Jipe. Nchini Kenya Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani (CDA) ina madaraka ya kuratibu na kupanga maendeleo ya sehemu ya bonde iliyoko Kenya. Mnamo mwaka 1993, iliamuliwa kuwa CDA ijitahidi kuandaa mpango kabambe wa usimamizi na maendeleo kwa ajili ya sehemu ya bonde iliyoko Kenya, pamoja na kutafuta njia za kushughulikia matatizo mahsusi ya Ziwa Jipe. CDA iliona kuwa ni lazima ishirikiane na mamlaka za aina yake za upande wa Tanzania (Howard, 1999).

Mnamo mwaka 1994, CDA na Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani (PBWO) walikutana Mombasa, Kenya ili kujadili masuala ya pamoja na njia zitakazowawezesha kufanya kazi pamoja ili kuendeleza mfumo wa usimamizi ulioratibiwa kwa ajili ya bonde, ardhioevu na maji ya Ziwa Jipe. Mwaka 1996, PBWO na CDA zilikamilisha tathmini ya mahitaji ya eneo la chanzo cha maji na ardhioevu ya Ziwa Jipe. Katika mwaka 1999, CDA, PBWB na wadau wengine walishiriki katika warsha ya kuanzisha mfumo wa kusimamia Ziwa Jipe (Howard, 1999).

PBWO hivi sasa imelifikisha shauri la magugu maji yaliyoko Ziwa Jipe katika Bunge la Jumuia ya Afrika Mashariki kwa kufanyiwa kazi. Kutoka hapo, kasi imepungua, na haja ya kuendeleza mfumo wa kuweza kuratibu usimamizi kati ya nchi mbili hizi unabaki kuwa muhimu kuliko wakati mwingine wowote. Hili ni dhahiri zaidi ikitiliwa maanani maendeleo ya hivi karibuni ya Kenya ambayo yameshuhudia uanzishwaji wa mamlaka za Usimamizi wa Rasilimali za Maji. Umuhimu wa uundwaji wake kwa Bonde la Mto Pangani na jinsi watakavyoshirikiana na wenzao wa Tanzania bado haifahamiki.

D.5 Ukusanyaji wa data na ufuatiliaji Wasiwasi unaoibuka mara kwa mara baina ya wataalam waliohojiwa kwa ajili ya Uchambuzi huu wa hali halisi na katika maandishi kuhusu Bonde la Mto Pangani unahusiana na ukosefu wa data za kutosha katika Bonde hili. Mara kwa mara, wasiwasi huo unalenga kwenye ukosefu wa data za kihaidrolojia, na wasiwasi ni kwamba mfumo wa sheria inayohusu utoaji wa hati za maji lazima uweze kujua wingi wa maji yaliyopo. Katika mito iliyopo Bonde la Mto Pangani, kuna vituo vingi vya kihaidrolojia. Kwa sababu mbalimbali – kama vile udhaifu wa utunzaji na kumalizika kwa betri – vituo vingi kati ya hivi havikuendeshwa kwa muda wa kutosha kitakwimu. Wakati mwingine, vituo hivi vimeacha kufanya kazi baada ya miaka miwili tu, na hakuna kilichofanyika kuvirejesha katika hali ya utoaji huduma.

Inawezekana kuchukua vipimo kwa kutumia watu, lakini motisha za kufanyia hivyo kwa fundi, kama wanavyodai watoa habari, lazima ziwianishwe na mafao yake ambayo hayatoshelezi. Mara nyingi wahojiwa wameonekana kupendelea uendelezaji wa mfumo wa haidrolojia unaojiendesha wenyewe ambao vipimo vinavyofanywa na watu vinaweza kulinganishwa navyo, na ambavyo vinaweza kuwa uti wa mgongo wa mfumo wa ufuatiliaji wa kutosha.

Kwa hakika, ufuatiliaji, sio ukusanyaji wa data pekee. Kuzitafsiri data hizo katika mfumo wa taratibu za matumizi kutakuwa na manufaa endapo kutakuwa na kanuni fulani inayounga mkono ili kuhakikisha kuwa data hizi zinatoa mchango muhimu katika kazi za usimamizi. Hivyo, kujua ni samaki kiasi gani wapo katika Bwawa la Nyumba ya Mungu haina maana kama taarifa hiyo haiwezi kutafsiriwa katika utendaji wa usimamizi. Katika hali inayofanana na hiyo, uendelezaji wa mfumo wa ukusanyaji data za haidrolojia wa kujiendesha wenyewe hauna maana kama utumiaji haramu wa maji hauwezi kuzuiliwa.

Page 69: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

56

Pia ni muhimu kusisitiza kuwa data za vipimo vya kiufundi vya mabadiliko ya rasilimali (kama vile upunguaji wa mtiririko wa maji, au mabadiliko ya eneo la msitu) hutoa tu taarifa kuhusu matokeo ya mienendo na michakato itokeayo kwingineko, mara nyingi katika uga wa kijamii na kiuchumi (ingawaje siyo mara zote k.m. mabadiliko ya hali ya hewa). Kama sababu za mabadiliko ya kimazingira na maliasili zina asili ya kijamii na kiuchumi, ni muhimu kuendeleza mifumo yenye nguvu ya ufuatiliaji wa tofauti za uchumi wa jamii, kinachosababisha hali hiyo na kuendeleza migogoro. Mifumo hii lazima pia iwe na uwezo wa kutambua mahitaji ya maji katika bonde.

Kisanduku cha 14: Mfano wa Chama cha Watumiaji Maji

Chama cha Watumiaji Maji cha Tegemeo, Kijiji cha Kawaya, Wilaya ya Hai

Chama cha Watumiaji Maji cha Tegemeo kilianzishwa mwaka 1999 na PBWO ili kutatua tatizo la ugawaji wa maji katika vijiji vitano wilayani Hai. Watu 5,000 hutumia maji ambayo Tegemeo huchukua, lakini ni watu 300 tu ambao wamesajiliwa nacho. WUA inasema watu wanahitaji kuelimishwa kuhusu manufaa ya uanachama. Manufaa hayo ni (a) kwamba watajifunza kuhusu sera na sheria za maji, (b) wanaweza kupata kibali cha kutumia maji kwa urahisi zaidi, (c) kwamba wanaweza kuvutia wahisani na shughuli za NGO (d) wanaweza kurekebisha miundombinu yao ya maji kwa urahisi zaidi wakiwa kama kikundi; na (e) wanaweza kutatua matatizo yao kama kikundi. Vyanzo vyao vikuu vya maji ni chemchemi kadhaa. Maji huingizwa kwenye mifereji ya kijadi, ambayo mara nyingi huwa imepewa majina ya watu ambao waliichimba hapo zamani. Baadhi huwa mirefu sana-ulio mrefu zaidi una kilomita 14. Tegemeo kwa sasa ina hati tatu za maji zenye jumla ya lita 720 kwa sekunde, na imeomba kuongezewa. Chama hukusanya ada kutoka kwa watumiaji wenye mashamba, na kila mtumiaji analazimika kulipa bila kujali kama ni mwanachama au la.

Watumiaji walioko mwanzoni mwa mfereji hufaidika zaidi ya wale walioko mwishoni. Chama kina sheria ndogondogo zinazowapangia kiasi cha maji ambacho watumiaji walioko kwenye chanzo cha mfereji wanaruhusiwa kutumia, lakini watu hudanganya. Tatizo lingine wanalokabiliana nalo ni kuwa eneo hilo ni tambarare sana. Kwa kutokuwepo na mteremko, maji daima hutuwama na hayatiririki. Matatizo ya ziada yanayowakabili ni pamoja na:

• Migogoro kati ya watumiaji wa maji wa sehemu ya juu na ya chini.

• Ulimaji katika maeneo ya chanzo cha maji na ukataji miti.

• Wakulima wa mpunga mara nyingi hawarudishi maji yasiyotumika kwenye mfereji.

• Chumvichumvi.

• Wafugaji huleta mifugo yao kunywa maji miferejini na kuharibu kingo zake.

• Eneo la huduma la WUA ni kubwa mno na mara nyingi huwa vigumu kwa wanachama kufika kwenye eneo la tatizo.

• Maji siyo safi. Wakati wa mvua kina cha maji ardhini hupanda na kufanya vyoo vifurike. Baadhi ya watu hawayachemshi maji wanayochota na hupata maradhi

• Umwagiliaji kwa vipindi virefu hupunguza rutuba ya ardhi.

Chanzo: Jumuiya ya Watumiaji Maji Tegemeo na Serikali ya Kjiji cha Kawaya

Page 70: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

57

D.6 Majumuisho ya hojaUtawala wa maliasili za Bonde la Mto Pangani ni wa kisekta. Shughuli za idara za misitu sio lazima ziwe zimeoanishwa kwa kiasi kikubwa na kukiuka mpango wa usimamizi wa Bonde la Mto Pangani, bali matokeo ya sera za misitu, kama ilivyo kwa shughuli za taasisi zinazohusika na usimamizi wa maji zinavyoshughulikia Sera ya Maji ya Taifa. Hali hii ya kisekta huenda chini hadi kwenye mikakati ya utawala ya ngazi za jamii. Hivyo Kamati za Maliasili za Vijiji zinazotumika katika Usimamizi wa Pamoja wa Misitu sio sawa na Vyama vya Watumiaji Maji. Jamii zilizo jirani na maeneo ya uvuvi na yaliyohifadhiwa, zinaweza pia zikalazimika kuunda Vitengo vya Usimamizi wa Fukwe na kamati za hifadhi ya wanyamapori kama ilivyo kwenye sera za Idara ya Wanyamapori na Idara ya Uvuvi. Wingi wa kupita kiasi wa taasisi za vijijini nchini Tanzania unazifunika zile zilizoundwa hapo awali kama vile Serikali za Vijiji. Mara nyingi, kazi ambazo kila kikundi kinafanya hazitofautiani na kazi zinazofanywa na vikundi vingine. Hatimaye, taasisi hizi zote hazina budi kushughulika mgao wa haki wa rasilimali katika jamii, matumizi endelevu na uhifadhi wake.

Kutokana na majadiliano ya hapo juu, dondoo zifuatazo zinatiliwa mkazo:

• Sheria ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji ya mwaka 2009 inaipa mamlaka ya kiutetendaji Bodi ya Maji ya Bonde la Pangani kuandaa mipango ya usimamizi wa bonde na ambayo itakuwa msingi wa ugawaji wa maji. Sheria hii mpya imeweka mfumo wa ngazi za utawala zenye ufanisi na mfumo wa kitaasisi ulio wazi ambao unaonyesha majukumu ya kila mmoja katika kutekeleza sera na sheria. Usimamizi wa maji Kenya umegawa katika mabonde 6 (kuna mabonde 5 lakini bonde la Ziwa Victoria limegawa katika maeneo mawiili, Kasikazini na Kusini) kama ifuatavyo: Ziwa Victoria kasikazini, Ziwa Victoria Kusini. Bonde la Ufa, Athi, Tana, na Iwaso Ng’iro. Sehemu ya bonde la Pangani upande wa Kenya huangukia katika bonde la Athi. Sheria ya maji 2002 ya Kenya imeweka mfumo mpya wa kitaasisi wa kusimamia na kutunza rasilimali za maji katika ngazi ya taifa, mabonde na mabonde madogo.

• Idara ya Misitu na Nyuki inaonekana kutokuwa na mipango yoyote ya aina hii ya kuundwa upya, na utawala wa misitu katika bonde unabaki kuwa wa pande mbili kati ya watawala wa ngazi ya taifa na ile ya mkoa, na kati ya nchi mbili ambamo Bonde la Mto Pangani limo.

• Sera zote, ya maji na ya misitu katika bonde hili zinazidi kutilia mkazo matumizi ya taasisi za kijamii katika utekelezaji wake. Wasiwasi umejitokeza kuhusu ni kiasi gani taasisi hizi zimeshinikizwa kuingia katika jamii. Kama jamii hazikushirikishwa katika uundaji na utekelezaji wa taasisi hizi, kunaweza kuwa na matokeo yasiyofaa katika usimamizi wake. Kulielewa tatizo hili kunaweza kutoa mafunzo kwa Kenya ambayo inataka kujumuisha watumiaji katika usimamizi wa rasilimali za taifa.

• Usimamizi wa kimataifa wa bonde ni muhimu. Zipo mamlaka, hata hivyo, zenye madaraka ya kulisimamia na kuliendeleza Bonde hili katika pande zote mbili za mpaka wa Tanzania na Kenya, na majadiliano yanayolenga katika kutambua ufumbuzi wa matatizo ya usimamizi wa bonde hili yameanza.

• Mfumo wa ukusanyaji na ufuatiliaji wa data katika bonde unaonekana kuwa dhaifu, bila ya kujali sekta ya rasilimali. Sura hii imetahadharisha kuwa kutilia mkazo ukusanyaji wa data kama jambo muhimu kwenye mfumo wa usimamizi hakutakuwa na maana iwapo data hizo haziwezi kusaidia ufuatiliaji kamili wa usimamizi. Pia inasisitiza haja ya kuanzisha njia za ufuatiliaji wa mabadiliko ya kijamii na kiuchumi, na kubainisha mahitaji ya maji katika bonde, kama nyongeza kwenye vipimo vya kiufundi vya mabadiliko ya rasilimali.

Sura inayofuata inatoa muhtasari wa ‘masuala’ yanayolikabili Bonde la Mto Pangani. Inaanzia na muhtasari wa masula yaliyopatikana kutoka katika kumbukumbu za warsha ya hivi karibuni ya Bonde la Mto Pangani, pamoja na yale yaliyojitokeza wakati wa mahojiano yaliyofanyika kwa ajili ya Uchambuzi huu wa Hali halisi. Sura hii inayatathmini masuala haya kama msingi wa uwekaji wa maeneo ya kipaumbele kwa ajili ya kuyafanyia kazi, na mapendekezo kuhusi-ana na hali hii yanatolewa katika sehemu yake ya mwisho.

Page 71: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

58

E Matatizo na masuala ya Bonde la Mto Pangani

E.1 Utangulizi

Sura hii msingi wake ni vyanzo viwili vya taarifa. Cha kwanza ni kumbukumbu za warsha kuhusu Bonde la Mto Pangani, iliyofanyika Mei, 2002 mjini Moshi. Cha pili ni mahojiano yaliyofanyika kwa ajili ya Uchambuzi huu wa hali halisi. Sura hii inajaribu kuunganisha maoni ya wadau mbalimbali katika Bonde la Mto Pangani kama msingi mkuu wa kuweza kutambua maeneo ya kipaumbele kwa ajili ya utendaji wa siku zijazo. Masuala ya Bonde la Mto Pangani yamegawanywa kati ya masuala ya mazingira, masuala ya uchumi wa jamii na siasa, masuala ya usimamizi na utawala, maeneo ya utafiti, na mwisho, mawazo ya wahojiwa kuhusu nini kipewe kipaumbele katika usimamizi wa bonde. Kwa misngi ya masuala haya, sehemu ya hitimisho inorodhesha maeneo kadhaa ya kipaumbele kwa ajili ya kuyafanyia kazi.

Takriban katika kila jambo, masuala yaliyoangaliwa hapa chini yanajitokeza katika mazingira ya ukuaji wa haraka na wa kiwango kikubwa cha idadi ya watu na ongezeko la msongamano wa watu. Hali ya rasilimali za bonde kuwa na kikomo inafanya ongezeko la watu na ukuaji wa polepole wa maendeleo katika bonde kusababisha uwezekano wa kuleta matatizo na masuala yaliyoangaliwa hapa, au pengine kuyazidisha.

E.2 Matatizo na masuala ya Bonde la Mto PanganiMasuala ya mazingiraKati ya matatizo ya bonde hili, kubwa zaidi ni ukataji miti, tatizo ambalo huathiri moja kwa moja uwezo wa kuhifadhi maji, huongeza kasi ya mtiririko wa maji na hivyo kusababisha mmomonyoko wa udongo katika bonde. Upande wa chini wa mto, mchakato huo huweza kusababisha mafuriko kutokea na hivyo wingi wa mchangatope kwenye mikondo ya maji katika bonde kuwa mkubwa.

Katika hatua nyingne, ukataji miti umesababishwa na mahitaji makubwa ya mazao ya misitu. Mingi ya misitu iliyobaki katika bonde ina mbao zenye thamani kubwa, ambazo kunapokosekana mfumo imara wa ufuatiliaji na utoaji adhabu, hukatwa kwa urahisi. Misitu pia hukatwa kwa ajili ya utengenezaji wa mkaa, pamoja na kuni kukidhi mahitaji ya nyumbani. Zaidi ya hayo, misitu ya bonde mara nyingi imo kwenye maeneo muhimu ya kilimo. Misitu ya Tao la Mashariki, kwa mfano, iko katika maeneo ya mwinuko ambayo mvua ni nzuri. Kadiri idadi ya watu kwenye bonde inavyoongezeka na idadi ya wakazi katika kingo za misitu huongezeka na kuzidisha hatari ya moto katika misitu. Moto pia hutumika kwa kusafisha ardhi kwa ajili ya kilimo.

Katika sehemu nyingi, kilimo kinachotumika kilianzishwa wakati ambapo rasilimali zilikuwa nyingi zaidi kuliko zilivyo hivi sasa, na huenda kisiweze kuendana na hali ya uhaba wa rasilimali uliopo. Hivyo, sehemu kubwa ya kilimo cha umwagiliaji wa kijadi kilichopo katika bonde hili hakina ufanisi kabisa na kilianzishwa katika mazingira ambapo kulikuwepo na maji ya kutosha kwa kila mtu. Kwa vile uchukuaji wa maji umeongezeka kutegemeana na msongamano wa watu, mifumo hii ya kilimo inaweza kuwa na athari kubwa kwa mazingira ya bonde. Mashinikizo haya yamesababisha kujitokeza kwa kilimo kwenye kingo za mto, ndani ya mabonde ya vijito na kwenye vyanzo vya chemchemi. Ongezeko la mchangatope lina madhara kwenye mkondo wa mto (inaweza kusababisha kubadili mkondo) pamoja na viwanda vilivyoko eneo la chini la mto, hususan mabwawa yatumikayo kuhifadhi maji kwa ajili ya nishati ya umeme.

Wingi wa shughuli za kilimo katika bonde hili umesababisha udongo kuendelea kuchoka kwa vile nafasi ya mfumo wa mzunguko wa mazao imechukuliwa na kilimo cha mwaka mzima. Kwa vile ardhi sasa ni nadra kuachwa bila mazao, inabidi imwagiliwe maji ili kuendelea kutoa mazao. Mifumo ya kijadi ya uchukuaji maji ina ufanisi mdogo sana na kiasi cha maji kinachoifikia mimea kinaweza kufikia asilimia 85 pungufu ya kiasi kilichochukuliwa kutoka kwenye chanzo. Umwagiliaji wa kurudiarudia huongeza uwezekano wa kuongeza chumvichumvi na/au magadi kwenye udongo. Zaidi ya hivyo, kiasi kikubwa sana cha maji yanayochukuliwa kutoka kwenye vyanzo katika bonde hili, kimepunguza mtiririko wa maji, inadhaniwa kuwa ni pamoja na kiasi cha maji yanayohitajika kwa ajili ya mazingira.

Page 72: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Katika maeneo ya nyanda za chini ya bonde hili inaonekana kuwa idadi ya mifugo imeongezeka kwa kiasi kikubwa, wakati ambapo kiasi cha malisho kimepungua kutokana na maendeleo ya kilimo. Hii imesababisha kujitokeza kwa tatizo la ufugaji wa kupita kiasi na matokeo yake ni uharibifu wa ardhi ya wafugaji.

Kadiri maendeleo yanavyoongezeka ndani ya bonde bila ya mifumo ya uondoaji taka inayoambatana nayo, pia ndivyo uwezekano wa uchafuzi katika ngazi ya jamii na ya bonde kwa ujumla unavyoongezeka. Matatizo ya ubora wa maji pia yanajitokeza kwa sura tofauti – hali ya viwango vya floraidi kuwa juu inaweza kuwa na matokeo mabaya kwa watu waishio kando kando ya mito.

Kama ilivyo katika sehemu nyingine za Tanzania, uvuvi uliokithiri katika bonde ni tatizo, uvuvi wa pwani na katika bwawa la Nyumba ya Mungu ukiwa ndiyo suala lenye uzito mkubwa. Katika Ziwa Jipe ukuaji wa magugumaji umekuwa mkubwa kiasi cha kukwamisha uvuvi. Magugu hayo yametokana na ongezeko la virutubisho vinavyoingia na maji yatokayo kwenye maeneo ya kilimo kwenye Mlima Kilimanjaro na Milima ya Pare Kaskazini. Kwingineko katika bonde, magugumaji aina ya “water hyacinth” ni tatizo.

Matatizo yanayokabili ardhi ya kinamasi ya bonde hili yanatofautiana. Kwa upande mmoja, ukaushaji wa maji kwenye vinamasi una matokeo mabaya kwa urekebishaji wa mtiririko wa mto, pamoja na bayoanuwai zinazotegemea ardhioevu. Kwa upande mwingine, uelekezaji wa mikondo ya maji (pamoja na ile inayopita kwenye ardhi ya kinamasi) unaweza kuongeza kiasi cha maji kitakachopatikana sehemu za chini za mto, hususan kwa ajili ya uzalishaji wa umeme. Siyo tu maji yanayobaki katika vinamasi hivyo hupunguza mtiririko wa mto, bali pia ongezeko la viwango vya mchavusho vinavyosababisha.

Uchimbaji madini usiodhibitiwa unaweza kuathiri sura ya nchi, na unaweza hata kusababisha uchafuzi kama uchimbaji huo unahitaji mchakato unaotumia kemikali. Uchimbaji wa mchanga kwenye mikondo ya mito unaweza kuharibu uimara wa kingo za mito.

Nyingi za tabia zilizotajwa hapo juu hutokana na uelewa mdogo kuhusu mazingira. Kwa upande mmoja, haya yanahusiana na ukosefu wa data kuhusu mtiririko wa maji kwenye bonde na kiasi cha maji yanayohitajika kutosheleza mahitaji ya mazingira. Kwa upande mwingine, wengi wa watu walioko katika bonde hili hawana uelewa wa athari za mazingira yatakayotokana na shughuli zao za kiuchumi.

Ukubwa wa matumizi ya rasilimali, maendeleo, uendeshaji na mabadiliko ndani ya bonde vina matokeo mabaya kwa bayoanuwai za bonde hili. Bonde lina baadhi ya rasilimali za bayoanuwai za pekee duniani zenye viwango vya juu vya spishi zinazopatikana katika sehemu hiyo na spishi nyingi zinazozuiliwa. Sehemu kubwa ya spishi hizi (lakini kwa vyovyote si zote) ziko kwenye misitu. Wakati rasilimali nyingi za kimsingi za bonde zikiwa kwenye tishio kutokana na njia zilizoelezwa juu, rasilimali hizi za bayoanuwai zinakabiliwa na hatari zilizo dhahiri na mbaya kabisa.

Masuala ya kiuchumi wa jamii na kisiasaKama ilivyo kwa watu wengine wa Tanzania, wakazi wengi wa Bonde la Mto Pangani sio matajiri. Ingawa bonde hili lina miji mingi, lakini siyo mikubwa kiasi cha kuweza kupokea ziada ya nguvukazi iliyoko vijijini. Wengi (kama si karibu wote) wa wakazi wa bonde hili hawana elimu ya kutosha na/au hawana stadi za kutosha. Kwa hali yoyote ile, hata kama stadi zingekuwepo, kuna shaka kama soko la ajira limeendelezwa vya kutosha kuweza kuwaajiri wote. Maendeleo katika bonde - kama ilivyo kwingineko nchini Tanzania - yameshindwa kuzalisha nafasi mbadala za kuingiza mapato zinazooana na viwango vya ufundi na stadi vya wakazi wa bonde.

Matokeo yake, njia pekee iliyopo ya kujipatia riziki kwa wengi walioko katika bonde ni ile ya msingi , yaani riziki kutokana na utumiaji wa moja kwa moja wa rasilimali za bonde iwe ni misitu, uvuvi, rasilimali za wanyama- pori au, la muhimu zaidi, kilimo. Kwa walio wengi, mafanikio ya shughuli hizi ndogo ndogo, yanahusiana moja kwa moja na upatikanaji wa ardhi na maji. Kadiri idadi ya watu inavyoongezeka, ndivyo pia migogoro inavyoongezeka baina ya watumiaji wa aina na viwango mbalimbali. Kwa matokeo hayo, Uchambuzi huu wa Hali halisi umewasilisha mifano ya migogoro ambayo hutokea kati ya watumiaji maji wa upande wa juu na wa chini wa mto, pamoja na ule wa kati ya watumiaji wa viwango vikubwa na wa viwango vidogo.

59

Page 73: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Ni dhahiri kuwa migogoro ni ishara moja ya ushindani kwa ajili ya rasilimali. Kadiri hali hii inavyozidi kuenea katika maeneo ya juu ya mto katika bonde, wakulima wanalazimika kuelekea upande wa chini wa mto ili kujaribu kilimo katika hali isiyotosheleza ya kilimo. Kama ilivyojadiliwa mapema, jambo hili huwanyang’anya ardhi wafugaji na hivyo kuwaingiza wakulima kwenye mgogoro na wafugaji.

Kama ilivyoelezwa hapo juu, matumizi makubwa ya ardhi katika bonde hili yanaweza kuwa na matokeo mabaya kwa mazingira. Kwa kweli, matokeo haya yanaweza moja kwa moja kuathiri uwezo wa ardhi kusaidia kwenye matumizi ya kiuchumi yatakayofanyika kwayo. Katika hali nyingine, msaada wa kisiasa wa kubadili au kuzuia mienendo hii haupo, au huwa ni kinyume, kwa wanasiasa kuwahimiza watu kutumia rasilimali kwa wingi ili wao waweze kujipatia kura.

Tatizo la mwisho la kisiasa lililotolewa na wahojiwa lilikuwa lile la Serikali Kuu ya Tanzania, katika juhudi zake za kutekeleza sera, inaweza kufanya maamuzi ya usimamizi yahusianayo na rasilimali bila ya kuwashirikisha watawala na wasimamizi wa rasilimali katika bonde. Kilichotia wasiwasi hasa ni miradi mikubwa ya maendeleo (kama vile miradi ya umwagiliaji na vibali vya uchimbaji madini) vilivyoonekana kusababisha migogoro ya ziada ya ndani au kuathiri vibaya hali ya rasilimali.

Masuala ya usimamizi na utawalaSheria na sera za usimamizi wa maliasili za bonde hili, mara nyingi zinajitosheleza, lakini zinafanya kazi pale tu zinapopata msaada wa usimamizi na ufuatiliaji wa kutosha wa utekelezaji wa kisheria. Ufuatiliaji sio tu uwezo wa kuangalia matumizi haramu ya rasilimali, bali pia uwezo wa kupima uzalishaji na mabadiliko ya rasilimali. Kwa mfano, kukosekana kwa mtandao wa kutosha wa ufuatiliaji wa mtiririko wa maji maana yake ni kuwa mamlaka zinazohusika na maji hazijui kiasi cha maji kinachopita katika bonde, kwa hiyo haziwezi kutoa vibali vya matumizi ya maji kwa msingi huo. Vivyo hivyo, hakuna njia yoyote ya kufuatilia na kupima sababu za kijamii na kiuchumi ambazo zinasababisha sehemu kubwa ya uharibifu wa mazingira na utumiaji wa kupita kiasi wa rasilimali.

Wafuatiliaji waliowekwa na taifa kuangalia mienendo ya matumizi ya rasilimali wanaweza wakashindwa kufuatilia rasilimali hizo kama hawalipwi vizuri. Ujira duni unaweza pia kuwa sababu ya kuwafanya maafisa wapokee rushwa hivyo kutoangalia matumizi haramu ya rasilimali. Viwango vya chini vya utaalamu, au kukosekana kwa teknolojia ya kutosha kunaweza pia kuzidisha matatizo ya ufuatiliaji.

Matatizo ya fedha yanaweza kuathiri sehemu nyingine za mfumo wa usimamizi. Kwa kukosekana kwa fedha za kutosha kwa mfano, inakuwa vigumu kuona jinsi mfumo wa kufaa wa ufuatiliaji unavyoweza kutekelezwa ndani ya bonde bila ya kujali rasilimali zinazohusika. Ukosefu wa fedha unaweza pia kusababisha hata data zinazoweza kukusanywa zisiweze kuchambuliwa au matokeo yasiweze kutafsiriwa kwa usahihi. Mwisho, matatizo ya fedha yanaweza pia kukwamisha maendeleo ya uwezo na ufanisi wa usimamizi.

Zaidi ya hayo, usimamizi unaweza kudhoofishwa kutokana na namna unavyopangwa. Katika Bonde la Mto Pangani, tatizo hili linaonekana kutokea katika ngazi mbili. Kwa upande mmoja, menejimenti siyo shirikishi, kiasi kwamba shughuli za usimamizi katika sekta moja, kama vile maendeleo ya umwagiliaji- zinaweza kuwa na athari kubwa katika sekta nyingine kama vile hifadhi ya maji. Kwa upande mwingine, mipaka ya mamlaka mara nyingi hutokea kuwa na utata, kwa kuingiliana kwa mamlaka za kiutawala au kwa hakika mamlaka za kisheria zisizotosheleza. Hivyo, mfumo wa Tanzania wa serikali kuu na serikali za mitaa husababisha kuwapo kwa watendaji wakuu wa kiutawala wawili wanaohusika katika usimamizi wa kila rasilimali moja. Nchini Kenya, madaraka ya kimaendeleo ya Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani yanaonekana kuingiliana na yale ya Mamlaka iliyoundwa hivi karibuni ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji.

Jamii za watumiaji rasilimali zinaweza kutatua mengi ya matatizo ya utata wa kiutawala na ufuatiliaji usiotosheleza kwa kupitia viwango mbalimbali vya ushirikishwaji. Katika Bonde la Mto Pangani, utekelezaji wa mchakato huu umekabiliwa na matatizo kadhaa. Kwanza, mifumo mingi ambayo imekusudiwa jamii zihusishwe katika usimamizi imefikishwa kwao, bila kuishirikisha jamii katika kubuni muundo wa utawala, katika utekelezaji wa mikakati ya usimamizi au kuadhibu wahalifu. Pili, kwa kuwa jamii inaweza isiwe na mchango mkubwa katika muundo na utekelezaji wa usimamizi, aina hizi za mifumo kwa kweli zinaweza kudhoofisha uwezo wa jamii kukidhi mahitaji ya maisha au

60

Page 74: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

uwezo wao wa kushindana vizuri na watumiaji wengine wa rasilimali. Tatu, aina nyingi za ‘kamati’ za rasilimali mbalimbali zimeundwa kote katika bonde, badala ya kuziongezea mamlaka serikali za vijiji zilizokuwepo kabla. Hivyo, utawala wa ngazi ya vijiji umefanywa kuwa mgumu na kamati nyingi za Usimamizi wa Maliasili zina majukumu yanayoingiliana au kukinzana. Mwisho, njia za mawasiliano kati ya mamlaka kuu za usimamizi wa maliasili na jamii zinaweza kuwa hazijaendelezwa kiasi cha kutosha. Matokeo yake, mahitaji na maoni ya jamii yanaweza yasizingatiwe au yasitambuliwe. Kwa namna hiyo hiyo, malengo ya usimamizi wa rasilimali au hifadhi ya mamlaka za usimamizi wa maliasili zilizowekwa chini ya makao makuu hazitaeleweka au hata kueleweka vibaya kwa ujumla na jamii.

Mchakato wa kiutawala na wenye urasimu unaweza kukwamisha au kudhoofisha shughuli za usimamizi zilizokusudiwa kwa nia njema. Kwa mfano, jamii za watumiaji wa rasilimali zimepewa madaraka ya kutunga sheria ndogo ndogo ambazo zinatambuliwa na serikali kuu, mamlaka za mkoa na wilaya. Hata hivyo, hatua ya kuziidhinisha itachukua muda mrefu kiasi kwamba juhudi za jamii na msukumo wa uongozi unadhoofishwa na mamlaka kuonekana kutoziunga mkono.

Bonde la Mto Pangani ni rasilimali inayovuka mipaka ya nchi. Utaratibu unaohitajika ili kuhakikisha kuwa usimamizi unalingana kwa pande zote Kenya na Tanzania haupo.

Maeneo ya UtafitiMatatizo yaliyotajwa hapo juu, mara nyingi yanazidishwa na ukosefu wa data sahihi na za kutosha juu ya mienendo na michakato inayoipa Bonde la Mto Pangani sura yake, na kuathiri usimamizi wake. Haieleweki wazi jinsi ongezeko la idadi ya watu katika bonde litakavyoathiri rasilimali zake hapo baadaye. Wala haieleweki vizuri ni aina gani za mbinu za usimamizi wa maliasili zitakazotumiwa, zinazoweza kufanya kazi katika misongamano kama hii ya watu.

Mengi ya mahitaji ya utafiti katika bonde hili yanahusu maji na haidrolojia. Hivyo, wakati idadi ya matoleo ya maji yenye hati yanajulikana, uchukuaji usio halali uliojilimbikiza haujulikani. Kwa nyongeza kiasi cha maji yanayohitajika ili kudumisha mifumo ya mazingira ya bonde pia hakijulikani. Athari za kuelekeza maji ya Mto Pangani katika eneo la Vinamasi vya Kirua zinahitaji utafiti wa ziada (angalia IVO-NORPLAN, 1997). Mchango wa theluji ya kilele cha Mlima Kilimanjaro kwenye mtiririko wa maji ya Bonde hili haujulikani, kama ilivyo kwa matokeo ya upunguaji wa theluji hiyo.

Mwisho, utafiti mdogo umefanywa ili kubainisha shughuli za usimamizi zinazofaa ambazo zitaweza kuendana na tabia na matatizo mahsusi ya bonde hili. Haieleweki jinsi maji yanavyoweza kusambazwa kwa kiasi cha kutosha na kwa usawa kati ya watumiaji wa maeneo ya juu ya mto na wale wa chini. Hakuna ufahamu wa jinsi mfumo wa usimamizi unavyoweza kufuatiliwa na kutekelezwa kwa ufanisi katika mazingira ya utoaji fedha usiotosheleza na usio wa kudumu, mchango mdogo wa kiufundi, viwango vya chini vya stadi na ushirikishwaji duni wa jamii. Muhimu zaidi, uendelezwaji wa mifumo ya usimamizi inayoweza kuendelea kuwepo chini ya vikwazo kama hivi hapo baadaye haujatokea. Mwisho, misingi ya kitaasisi yenye ufanisi ya usimamizi shirikishi wa rasilimali za Bonde bado haijaanzishwa.

Usimamizi wa Bonde la Mto PanganiMajadiliano yaliyofanyika wakati wa warsha ya mwezi Mei 2002 kuhusu Bonde la Mto Pangani, pamoja na mahojiano yaliyofanyika ili kusaidia Uchambuzi huu wa Hali halisi, yalipendekeza mambo kadhaa ambayo menejimenti ya bonde inaweza kuyafikiria. Kati ya hayo ilikuwa hoja kuwa wakazi wa bonde wanahitaji kufahamu kuhusu Bonde la Mto Pangani na majukumu yake. Kumeibuka malalamiko kwamba bonde hili la mto halitambuliwi vya kutosha kama kitengo cha utawala, na kuwa watawala na wenye urasimu waliokabidhiwa madaraka wanashindania kudumisha msisitizo wa utawala wa nchi kimkoa na kitaifa. Wahojiwa walisema fedha zinazotolewa zinatakiwa ziwe za kutosha na taratibu zinazohusika za utoaji wa fedha ziwe zenye ufanisi.

Menejimenti ya bonde itahitaji kuhakikisha kuwa idara za serikali zinashirikiana na taasisi nyingine za usimamizi. Data zenye ubora wa hali ya juu zinahitajika kukusanywa ili kuipa taarifa menejimenti, na menejimenti lazima iwe shirikishi. Mwisho, kati ya mapendekezo kadhaa ya mipango ya kitaifa iliyotolewa ni kuwa usimamizi wa Bonde la Mto Pangani uunganishwe na mikakati ya kudhibiti ongezeko la watu.

61

Page 75: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Kwa kuwa wengi wa washiriki wa Warsha na watu waliohojiwa kwa ajili ya Uchambuzi huu wa Hali halisi wametoka kwenye sekta ya maji, mapendekezo mengi ya usimamizi yaliyokusanywa yalihusiana moja kwa moja na matumizi ya maji na sheria zake. Hivyo, ilipendekezwa kuwa menejimenti itakuwa na haja ya kufuata mipango ya kazi iliyo wazi ambayo lazima iwe na hatua za kuchukuliwa kutokana na upotevu wa maji na matumizi ya maji yasiyo ya ufanisi. Menejimenti itatakiwa kuwa na uwezo wa kutoa mgao wa maji ya kutosha na kwa usawa, na matumizi haramu au yasiyofaa ya maji lazima yafuatiliwe na kuchukuliwa hatua za kisheria. Matoleo ya maji lazima yawe na hati ili uchukuaji uweze kufuatiliwa. Wahojiwa walidai kuwa, menejimenti ya bonde pia lazima iwe na uwezo wa kurekebisha uharibifu wa vyanzo vya maji, na Ofisi ya Bonde lazima iwe na muundo ulioboreshwa wa ukusanyaji ada.

Baadhi ya washiriki wa warsha walikuwa na maoni kuwa upungufu wa maji haukutambuliwa vya kutosha katika sera za Tanzania na kwamba hili lilihitaji kurekebishwa. Ili kuhakikisha kuwa maoni ya wadau yanawakilishwa inavyofaa kwenye menejimenti ya maji ya bonde, wito ulitolewa kuwe na uwakilishi mzuri zaidi wa wadau katika Bodi ya Maji ya Bonde. Mwisho, mkakati wa kutosha unahitajika ili kusimamia utekelezaji wa Sera mpya ya Maji ya Tanzania.

Baada ya Baraza la Mawaziri kuidhinisha sera mpya ya maji Julai 21, 2002 Mkakati wa Taifa Kuendeleza Sekta ya Maji (MTESM), uliandaliwa. Mkakati unaainisha namna sera ya maji itakavyotekelezwa na unaeleza mabadiliko ya ki-sheria na kitaasisi yanayohitajika ili kufikia malengo yaliyoainishwa katika mkakati huo. Kuhusu mifumo ya kitaasisi mkakati unasema: Maji ni rasilimali ya taifa na kimataifa ambayo upatikanaji wake haufuati mipaka ya vijiji, wilaya, mikoa, au nchi na zinaweza kusimamiwa vizuri katika mabonde na bodi za mabonde na kamati za mabonde madogo. Uwakilishi wa halmashauri za wilaya na serikali za mitaa katika bodi na kamati hizo unahakikisha kuwa kuna sauti ya waliochaguliwa kidemokrasia katika maamuzi yanayohusu uhifadhi, usimamizi, ugawaji, uendelezaji na utumiaji wa rasilimali za maji. Pia mkakati unahimiza uainishaji wa maeneo ya sera za sekta muhimu yanayohusu rasilimali za maji ili yawiane na Sera ya Maji na kuweka wazi wajibu wa kila mhusika katika mfumo unaoweka bayana majukumu na wajibu na kuepuka kufanya shughuli kwa kurudia au nyingine kusahaulika. Sheria ya maji ya 2009 ilitungwa ili kuweka mfumo wa kisheria wa usimamizi wa rasilimali za maji.

E. 3 Maeneo ya Kipaumbele ya Kufanyiwa kaziKwa msingi wa majadiliano hapo juu, maeneo matatu ya kipaumbele yameainishwa:

1. Uendelezaji wa mikakati ya usimamizi shirikishi ya Bonde la Mto Pangani pamoja na mabaraza yanayoambatana nayo. Bila shaka Bonde la Mto Pangani linahitaji kwa haraka mikakati ya usimamizi shirikishi ambayo inaweza kuendana na masuala mbalimbali na yenye utata ambayo yameelezwa katika Uchambuzi huu wa Hali halisi. Kwa hivyo, inapendekezwa kuwa eneo la kwanza la kipaumbele ambalo linahitaji kufikiriwa ni uendelezaji wa mikakati hiyo. Katika hatua hii, mkazo unaelekezwa kwenye sehemu zifuatazo za mkakati huo:

• Ushirikishaji ni muhimu katika mtazamo wa mazingira wa wapangaji mipango na watawala ili kuhakikisha kuwa menejimenti inafuata mikakati ya mipango ya jumla, na ya bonde lote yenye uwezo wa kushughulikia rasilimali mbalimbali na matatizo yanayolikabili bonde.

• Ni muhimu Bonde la mto lionekane kama kitengo cha utawala ambamo ndani yake ushirikishwaji wa usimamizi utatokea na migogoro ya rasilimali itatatuliwa. Pia ni muhimu kuwa matumizi ya bonde la mto kama kitengo cha utawala yasiwe kinyume cha ukamilifu wa utawala wa kitaifa na kimkoa na malengo ya sera.

• Chombo cha ziada cha utawala ambacho kinaweza kufikiriwa ni kufuata mfumo wa Usimamizi wa Mahitaji ya Maji (WDM) (angalia A.2 hapo juu). Kwa kuzingatia ushahidi uliopo, kuwa upatikanaji wa maji katika bonde umeelemewa, na kwamba mahitaji ya sasa yanazidi upatikanaji, utekelezaji wa mifumo ambayo itasaidia kuhifadhi maji na kuhimiza matumizi bora ingekuwa wa muhimu katika mazingira ya usimamizi shirikishi wa bonde.

62

Page 76: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

• Upo umuhimu wa kubuni mikakati ambayo katika hatua zake za awali, inaweza kutekelezwa kwa kuongezwa kadiri mipango na upatikanaji wa fedha unavyoruhusu. Kwa kukosekana msaada wa kutosha wa mipango na kifedha, mikakati pekee ambayo inaweza kufanya kazi kupitia matumizi ya haraka na yasiyo na uhakika inaweza kushindikana. Uwezekano mmoja ni kulenga mipango kwenye mabonde madogo (sub-basin).

• Wingi wa taasisi za kijamii zinazoshughulika na sekta zote zitumiazo maliasili unatatanisha na hauna ufanisi kiutawala. Hivyo, inafaa kutafuta njia ambazo taasisi za mahali husika zenye mwelekeo mpana zinaweza kuendelezwa kuwa na uwezo na madaraka ya kutatua matatizo yote ya usimamiazi wa maliasili katika eneo lake. Kila taasisi itahitaji msaada wa taifa, hususan katika kuweka sheria ndogondogo za jamii, na kusaidia juhudi za usimamizi za jamii.

• Mipango ya matumizi ya ardhi lazima ifikiriwe kuwa ni sehemu muhimu ya mkakati wa mpango shirikishi toka mwanzoni.

• Mikakati ya mipango ioane na uelewa wa uwezo na hali ya kifedha kwa baadaye. Haina maana sana kuanzisha mikakati ya mipango inayotegemea msaada wa fedha, data na mipango ambavyo ama vitatoweka mara fedha za wahisani zitakapokosekana, au ambayo haioani na msingi wa muundo wa kitaasisi wa bonde.

2. Uanzishaji wa mikakati inayofaa kuwezesha mazungumzo miongoni na kati ya watumiaji rasilimali na wasimamizi wa aina mbalimbali na kushirikishwa katika sekta mbalimbali kwa lengo la kuboresha uelewa katika ngazi zote za usimamizi. Zinahitajika taratibu za kuhakikisha kuwa fursa za mazungumzo kati na miongoni mwa wadau na wasimamizi zinakuzwa, ili kuhakikisha kuwa upashanaji habari wa pande mbili unakuwepo, usambazaji habari unaboreshwa na kujua jinsi wadau wote wanavyofanya kazi katika ustawi wa bonde zima. Ni muhimu uhamasishaji ufanyike kuhusu nyanja zote za hali na usimamizi wa bonde na wadau wake katika ngazi zote za usimamizi na uratibu wake. Inapendekezwa kuwa yaanzishwe mabaraza kwa madhumuni haya, ambayo yatakuwa na mamlaka hadi kwenye usuluhishi wa migogoro.

Kwa nyongeza, mabaraza hayo yangeweza kuwa na uwezo wa kiutawala na utendaji, ambao sekta zote za utawala katika bonde zinawakilishwa. Kipengele muhimu cha mchakato huu ni kuhakikisha kuwa njia za kutosha za mawasiliano na mazungumzo zinaanzishwa kati ya ngazi za juu za utawala na zile za chini kabisa, ngazi ya jamii.

Uwezekano wa kutumia redio na njia nyigine za habari lazima zifikiriwe kama njia zinazoweza kutumiwa katika uanzishaji wa mazungumzo na zinazofaa kwa usambazaji na ubadilishanaji wa taarifa. Tahadhari lazima ichukuliwe kuhakikisha kuwa wadau wote na wasimamizi wanafahamu maendeleo ya sera mpya na mabadiliko katika utawala na kanuni za rasilimali. Majukumu ya mabaraza yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya ushirikishi lazima yapanuliwe ili kuhusisha wajibu wa majadiliano na kupashana habari. Juhudi hizi zingeweza kusaidiwa na juhudi za ughani ambazo pia zingeweza kutumika kupata maoni na kero za jamii husika.

3. Kubainisha na kuendeleza mfumo wa kutosha wa ukusanyaji na ufuatiliaji wa data. Eneo hili la utendaji halikomei katika uendelezaji wa mifumo ya ukusanyaji data kwa ajili ya data za kihaidrolojia. Tathmini ya matumizi ya ardhi kwa kutumia Setilaiti na Mfumo wa Habari wa Kijiografia (GIS), viwango vya matumizi ya ardhi na mabadiliko ya kijiografia ni mahitaji ya msingi katika kuendeleza upangaji na ufuatiliaji wa matumizi ya ardhi. Kwa nyongeza, njia zitakazofaa kufuatilia na kupima mabadiliko ya kijamii na kiuchumi na kuongezeka kwa migogoro zinahitajika kuainishwa na kutekelezwa. Mifumo ya data na ufuatiliaji iliyopendekezwa lazima iendane na uwezo wa ndani wa kifedha na uendeshaji. Mwisho, matumizi ya mashirika ya kijamii ya usimamizi wa maliasili, kama njia ya ufuatiliaji wa matumizi ya rasilimali pia lazima yazingatiwe.

63

Page 77: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

F Hitimisho

F. 1 Majumuisho ya MatokeoItakumbukwa kuwa lengo la awali la Uchambuzi wa Hali halisi lilikuwa kubainisha rasilimali zilizopo katika Bonde la Mto Pangani na michakato na matukio yanayoziathiri.

Bonde la Mto Pangani lina aina nyingi sana za rasilimali. Baadhi ya rasilimali hizi, na kazi muhimu zinazofanya katika bonde ni kama zifuatazo:

• Misitu, inafanya kazi muhimu katika haidrolojia ya Bonde, ya kurekebisha kasi ya maji, kupunguza mmomonyoko, kuhifadhi na kutakasa maji. Aidha, inatoa mchango muhimu wa Bonde la Mto Pangani kwa bayoanuwai ya dunia.

• Maji katika bonde la mto Pangani ni muhimu kwa uchumi wa kilimo, uzalishaji wa umeme, mahitaji ya mijini, majumbani, viwandani na mifugo. Maji yanaendeleza maisha ya viumbe vyote katika bonde.

• Bonde hili lina maeneo manne yaliyohifadhiwa. Mlima Kilimanjaro, kipekee una mchango muhimu sana katika uchumi wa utalii wa taifa, na pia unahifadhi spishi nyingi za mimea na wanyama. Hifadhi ya wanyamapori ya Mkomazi na Mbuga ya Taifa ya Tsavo Magharibi ni mifano ya Kituo cha kanda ya Masai-Somali cha Spishi zipatikanazo eneo hilo pekee (Regional Centre of Endemism).

• Bayoanuwai ya bonde hili haina mfano wake ulimwenguni, na ni eneo lenye umuhimu mkubwa kimataifa katika masuala ya hifadhi.

• Uvuvi katika bonde la mto Pangani unatoa mchango muhimu wa lishe na uchumi kwa jamii za vijijini katika bonde.

• Udongo wenye rutuba wa volkano katika bonde la mto Pangani ndio msingi wa uchumi wake wa kilimo, na kulifanya kuwa ‘eneo muhimu la uzalishaji mazao nchini Tanzania’.

• Uchimbaji madini unatoa mchango muhimu katika uchumi wa taifa na katika kutoa ajira. Manufaa yake ni lazima yafikiriwe dhidi ya athari zake mbaya, ikiwa ni pamoja na uchafuzi wa mazingira na udhoofishaji wa kingo za mito.

Hatari zinazokabiliwa na rasilimali za bonde karibu zote zinahusiana na utumiaji uliokithiri. Kiini cha hatari hizi kinahusiana na ongezeko la idadi ya watu katika mazingira ya umaskini uliokithiri. Umaskini na uharibifu wa mazingira mara nyingi vinaonekana kwenda pamoja (cf. WCED, 1987). Matatizo ya Usimamizi wa Rasilimali za Jamii (CPRs) mara nyingi yanafikiriwa kuongezeka kunapokuwa na idadi kubwa ya watu waliohusishwa, hususan pale mshikamano wa tamaduni zao unapokuwa dhaifu (cf. Ostrom, 1990). Muundo na uwezo wa kufanya kazi za kujipatia riziki vijijini unanaweza kuhatarishwa wakati uwezo wa watu wa vijijini kumiliki na kutunza vyanzo vya kutosha vya kujipatia riziki unapotishiwa.

Hapo juu, wadau wa bonde na shughuli zao zilielezwa kama ifuatavyo:

• Shughuli kuu katika bonde ni za viwanda (umeme, uchimbaji madini na kilimo), kilimo (kilimo cha viwango vikubwa na viwango vidogo, vyote vikitegemea kwa sehemu kubwa umwagiliaji), shughuli za wafugaji (hususan katika maeneo ya nyanda za chini), na shughuli zinazokua za mijini. Mashirika yasiyo ya kiserikali na mawakala wa wahisani wa kimataifa wanafanya kazi kati ya shughuli hizi mbalimbali na maliasili nyingi zilizopo katika bonde hili. Wajibu wa mashirika haya kimsingi ni kuhifadhi na/au kuendeleza na kuongeza uwezo wa utafutaji riziki vijijini.

64

Page 78: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

• Ni muhimu kutambua kuwa, idadi ya watu katika bonde hili ni kubwa. Sehemu kubwa ya idadi hii ya watu riziki yao inatokana na kilimo, na kuna mengi yanayoonesha kuwa wako hatarini kiuchumi. Kwa nyongeza, aina mbalimbali na utajiri wa rasilimali uliopo katika bonde hili huwa kivutio cha shughuli za viwango vikubwa, na hivyo uwekezaji mkubwa umefanyika. Baina ya shughuli hizi kubwa za uwekezaji na zile zilizo ndogo ndogo za kujitafutia riziki, uwezekano wa kuwepo migogoro ni dhahiri.

• Uchambuzi huu wa Hali halisi umeigawa migogoro ya Bonde la Mto Pangani katika makundi makuu matatu. Kundi la kwanza linahusiana na migogoro ya viwango, ambayo ilitolewa hoja kuwa watumiaji wa viwango vidogo mara nyingi inabidi washindane dhidi ya mahitaji makubwa zaidi ya wenye nguvu katika kuwania rasilimali moja. Eneo la pili la migogoro lililobainishwa lilihusiana na migogoro ya umiliki. ‘Umiliki’ hapa unahusiana na haki ya mtu ya kusimamia rasilimali. Ilielezwa kuwa utaratibu wa kuzipangia jamii za watumiaji rasilimali aina tofauti za vyama na/ au kamati zitakazosimamia rasilimali hizo unazidi kupata umarufu nchini Tanzania. Matumaini ni kuwa uundaji wa taasisi kama hizi utatoa matokeo bora ya usimamizi. Hata hivyo, kulikuwa na hoja kuwa namna taasisi hizi mara nyingi zilivyolazimishwa kuiingizwa katika jamii, ambazo awali hazikuwa na mchango katika ubunifu, malengo au kanuni zake, zingeweza kudhoofisha ubora wa matokeo ya kazi zao. Kundi la tatu la migogoro linahusiana na mahali. Hapa, jinsi eneo la kikundi cha watumiaji rasilimali linavyoweza kuwaingiza katika mgogoro na watumiaji wa mahali pengine, ilizingatiwa. Mfano mzuri wa mgogoro wa aina hii wa ‘mahali’ unaotokea kati ya watumiaji wa sehemu ya juu ya mto na wale wa chini ya mto ulitolewa. Hapa, watumiaji wa upande wa chini ya mto huathiriwa na matumizi yaliyokithiri ya watumiaji wa upande wa juu.

Sura D ilieleza kuwa utawala wa maliasili za Bonde la Mto Pangani ni wa kisekta. Shughuli za Idara ya Misitu na Nyuki hazikulazimika kuoanishwa na baadhi ya seti ya mikakati mipana na mikuu ya usimamzi wa Bonde la Mto Pangani, bali inafuata sera ya misitu na nyuki kama shughuli za Ofisi ya Maji Bonde la Pangani zinavyofuata Sera ya Maji ya Taifa.

Utawala huu wa kisekta unapenya hadi kwenye mikakati ya utawala katika ngazi ya jamii. Hivyo, Kamati za Maliasili za Vijiji vya Tanzania zilizotumika katika Usimamizi wa Pamoja wa Misitu si sawa na Vyama vya Watumiaji Maji. Jamii zilizo karibu na maeneo ya uvuvi na yaliyohifadhiwa, pia zinaweza kulazimika kuunda Vitengo vya Usimamizi wa Fukwe na kamati za ulinzi wa wanyamapori kwa mujibu wa sera za Idara ya Wanyamapori na Idara ya Uvuvi. Wingi wa asasi za vijijini nchini Tanzania umezifunika zile zilizoundwa hapo awali kama Serikali za Vijiji. Mara nyingi, kazi ambazo kikundi kimoja kinatakiwa kifanye hazitofautiani na kazi ambazo vikundi vingine vinafanya. Hatimaye inabidi asasi zote hizi zijishughulishe na ugawaji wa haki wa rasilimali katika jamii, matumizi yake endelevu na kuzilinda kutokana uvamizi wa watu kutoka nje.

Nchini Kenya, kinyume chake, kuna vikundi vichache sana vya namna hiyo, ingawa sera mpya za maliasili zinazidi kutaka kuwashirikisha watumiaji katika miundo yake ya usimamizi.

Sura D ilitilia mkazo vipengele vifuatavyo:

• Sheria ya maji inaipa madaraka bodi ya maji kuandaa mipango ya usimamizi wa wa rasilimali za maji ambayo itakuwa msingi wa kugawa maji Sheria mpya imeweka mfumo wa ngazi za utawala zenye ufanisi na mfumo wa kitaasisi ulio wazi ambao unaonyesha majukumu ya kila mmoja katika kutekeleza sera na sheria. Sera mpya ya maji ya Kenya inaelekeza uundwaji wa mamlaka ya usimamizi wa rasilimali za maji unaohusisha wadau wote katika kusimamia rasilimali za mabonde.

• Idara ya Misitu na Nyuki inaonekana kutokuwa na mipango yoyote inayofanana na hii ya kujipanga upya, na utawala wa misitu katika bonde unabaki kati ya tawala mbili za ngazi ya taifa na mkoa. Nchini Kenya, uundaji upya wa Idara ya misitu bado haujatoa matunda. Hii inaweza kuwa na matokeo ya ustawi mdogo kwa sehemu ya Bonde iliyoko Kenya, ambayo inapata matatizo hasa yatokanayo na ukataji miti nchini Tanzania.

• Sera zote, ya maji na ya misitu katika bonde zinazidi kutilia mkazo matumizi ya mashirika ya kijamii katika utekelezaji wao. Kwa upande wa Tanzania, kuna hofu juu ya kiasi ambacho mashirika haya yamepandikizwa katika jamii. Ikiwa jamii hazikushirikishwa katika ubunifu na

65

Page 79: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

utekelezaji wake, matokeo ya usimamizi yanaweza yasiwe ya kuridhisha. Mafunzo wanayoyapata Watanzania kutokana na uzoefu huu yanaweza kuwa na manufaa katika ubunifu na utekelezaji wa mifumo ya namna hii huko Kenya.

• Mtandao wa ukusanyaji na ufuatiliaji wa data katika bonde unaonekana kuwa duni, bila kujali sekta ya rasilimali. Sura hii imetahadharisha kuwa kusisitiza ukusanyaji data kama jambo muhimu kwa mfumo wa usimamizi hakuna maana ikiwa data hazitawezesha ufuatiliaji wa kiusimamizi.

Dhumuni la pili la Uchambuzi wa Hali halisi lilikuwa kubainisha kwa mapana maeneo ya utendaji ambamo hatua zinaweza kuchukuliwa kwa manufaa.

Sura E ilitumia kumbukumbu za warsha kuhusu Bonde la Mto Pangani na mfululizo wa mahojiano na wadau wa bonde kuorodhesha matatizo na masuala ya bonde. Kwa msingi huo maeneo matatu ya kipaumbele cha utendaji yalibainishwa. Maeneo haya yalikuwa:

• Kuendeleza mikakati ya usimamizi shirikishi kwa ajili ya Bonde la Mto Pangani pamoja na mabaraza yanayoambatana nayo. Bila shaka Bonde la Mto Pangani linahitaji mikakati ya usimamizi shirikishi inayoweza kuendana na masuala mbalimbali na yenye utata yaliyoelezwa katika uchambuzi huu wa hali halisi.

• Uanzishaji wa mikakati inayofaa kuwezesha mazungumzo miongoni na kati ya watumiaji rasilimali na wasimamizi wa aina mbalimbali na kushirikishwa katika sekta mbalimbali kwa lengo la kuboresha uelewa katika ngazi zote za usimamizi. Inahitajika mifumo ya kuhakikisha kuwa nafasi za mazungumzo baina na kati ya wadau na wasimamizi zinaongezwa, ili kuhakikisha kuwa kunakuwepo na upashanaji taarifa wa pande mbili, usambazaji wa taarifa unaboreshwa na maarifa ya jinsi wadau wote wanavyotimiza wajibu wao katika ustawi wa bonde hili unafikiwa. Ni muhimu uelewa ujengwe kwenye vipengele vyote vya hali na usimamizi wa Bonde na wadau wake kwenye ngazi zote za usimamizi na uratibu wake. Vipengele vingine vya ziada katika eneo hili la kipaumbele ni uanzishaji wa mabaraza yenye uwezo wa kufanya kazi hii, pamoja na kufanya kazi kama nyenzo ya kuondoa migogoro, na kupunguza tofauti kati ya ngazi mbalimbali za utawala.

• Kuainisha na kuendeleza mfumo wa kutosha wa ukusanyaji na ufuatiliaji wa data. Eneo hili la utendaji halikomei katika uendelezaji wa mifumo ya ukusanyaji data kwa ajili ya data za kihaidrolojia. Tathmini za Setilaiti na GIS za matumizi ya ardhi, viwango vya matumizi na mabadiliko ya kijiografia ni mahitaji ya awali katika kupanga na ufuatiliaji wa matumizi ya ardhi. Kuendeleza mbinu za kutathmini na kupima sababu za kijamii na za kiuchumi za uharibifu wa mazingira na matumizi yaliyokithiri ya rasilimali pia zinahitajika kutambuliwa. Mifumo hiyo lazima pia iwe na uwezo wa kutambua mahitaji ya maji katika bonde. Mifumo ya data na ufuatiliaji inayopendekezwa lazima ioane na uwezo wa ndani kifedha na uendeshaji.

Lengo la tatu ya Uchambuzi wa Hali Halisi ilikuwa ni kutambua mashirika mengine, shughuli au asasi ambazo IUCN inaweza kuingia nazo ubia wakati inapojaribu kuanzisha juhudi za WANI katika Bonde la Mto Pangani.

Katika kifungu cha C6, ushiriki wa mashirika yasiyo ya kiserikali na mashirika ya kimataifa ulizingatiwa na kufanyiwa tathmini kufuatana na mchango wao muhimu katika kuendeleza na kutekeleza mikakati ya usimamizi shirikishi kwa ajili ya bonde hili. Hapa tunauendeleza zaidi ule uchambuzi na kupendekeza njia ambazo asasi hizi zinaweza kuchangia katika usimamizi shirikishi wa Bonde la Mto Pangani.

• Utaalamu wa PAMOJA uko kwenye eneo la kukuza majadiliano, hususan kati ya Serikali na shughuli za kijamii. Utaalamu huu unaweza kutoa mchango wa muhimu sana katika kuunganisha mipango na utawala wa serikali na ngazi ya chini ya jamii katika usimamizi wa rasilimali. Wakati huo huo, ni muhimu kuwa matatizo na mawazo ya jamii yazingatiwe vya kutosha katika utoaji maamuzi na utendaji wa serikali. PAMOJA ina uwezo wa kuhakikisha kuwa hili linafanyika.

66

Page 80: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

• Shirika la Umwagiliaji maji Kiasili na Uendelezaji wa Mazingira (TIP) lina uzoefu sawa na PAMOJA, na linaweza kuboresha matumizi yake. Hata hivyo, la kuvutia zaidi ni michango ya kiufundi ambayo TIP inaweza kutoa katika kusanifu na kuendeleza miundombinu itakayoboresha usafirishaji maji (mifereji ya umwagiliaji ) na utawala wake.

• Uzoefu wa Mpango wa Utendaji wa Misitu Tanzania (TFAP) wa kuendeleza ngazi ya jamii na kuishirikisha katika ufumbuzi wa matatizo ya rasilimali , unaonekana kuwa wa manufaa katika Bonde la Mto Pangani. Uendelezaji wa mifumo hii kwa jamii zinazoishi kando ya misitu ya bonde hili ungekuwa ni jambo la kufurahiwa kwa mpango wowote wa usimamizi katika bonde. Kama ingeunganishwa na shughuli za Kikundi cha Hifadhi ya Misitu Tanzania (TFCG), ueneaji wa juhudi hizi ungeongezeka zaidi, mashirika yote haya mawili yangefaidika kwa pamoja kutokana na kubadilishana uzoefu na maarifa na mkakati wenye ufanisi wa kushughulikia upotevu na uharibifu wa misitu ungeanzishwa.

• Programu ya Hifadhi na Maendeleo ya Kanda ya Pwani ya Tanga (TCZCDP) ina uzoefu muhimu kivitendo katika uundaji wa mkakati wa usimamizi shirikishi wa maliasili, ambao Bonde la Mto Pangani ungeweza kujifunza kutoka kwake na kuweza kujijenga kiuwezo, ikieneza mafunzo haya kuelekea juu na mbali zaidi kutoka eneo la mamlaka ya kisheria la TCZCDP. Eneo la mamlaka ya kisheria la Ubia wa Usimamizi wa Pwani ya Tanzania (TCMP) ni kubwa zaidi, na kwa sababu hiyo, shirika hili lingeweza kuwa na uzoefu wa hali ya juu wa usimamizi shirikishi wa maeneo makubwa yenye aina nyingi sana za maliasili.

• Mradi wa Usimamizi wa Usimamizi wa Matumizi Bora ya Maji na Uboreshaji wa Kilimo cha Umwagiliaji cha Wakulima Wadogo wadogo (RBMSIIP) ni mradi pekee uliojaribu kutumia mwelekeo wa kimabonde katika kutatua matatizo ya Bonde la Mto Pangani. Kwa nyongeza, pia umejaribu kushirikisha masuala ya hifadhi ya maji na juhudi za maendeleo ya maji. Maarifa yaliyomo kwenye Mradi huu katika maeneo haya ni muhimu sana katika kuendeleza mikakati ya usimamizi kwa ajili ya bonde. Zaidi ya hayo, uzoefu wa Mradi huu katika kuendeleza mtandao wa ukusanyaji data za kihaidrolojia kwa ajili ya bonde pia ni wa manufaa makubwa kwa Bonde la Mto Pangani.

• Uzoefu wa Mradi wa Bayoanuwai za kimataifa za Afrika Mashariki (EACBP) wa UNDP-GEF katika usimamizi wa rasilimali za kimataifa ni muhimu kwa Bonde la Mto Pangani. Kwa nyongeza, uzoefu wa EACBP wa uundaji na utekelezaji wa usimamizi wa pamoja wa misitu kijamii ungeweza kuwa wenye manufaa kwa usimamizi shirikishi wa bonde.

Ofisi ya Maji Bonde la Pangani inashirikiana na baadhi ya mashirika haya na kwa hiyo hii inaweza kuwa orodha ya manufaa kwa kumbukumbu ya baadaye.

67

Page 81: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

68

G Rejea

Published sources:Akitanda, P. 2002. South Kilimanjaro catchment forestry management strategies: perspectives and

constraints for integrated water resources management in Pangani Basin. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 152 – 160.

Baker, N. E. and Baker, L. M. 2001. Tanzania. In Fishpool, L. D. C. and Evans, M. I. (eds.) Important bird areas of Africa and its associated islands: priority areas for conservation. Newbury and Cambridge, UK, Pisces Publications and BirdLife International (BirdLife Conservation Series No. 11).

Baldwin, R. R. 1946. Native Authority afforestation on Mt. Kilimanjaro. Tanzania Notes and Records 21 (1946): 81 – 84.

Bergkamp, G., Orlando, B. and Burton, I. 2003. Change: Adaptation of water resources to climate change. IUCN/WANI. Gland, Switzerland and Cambridge, UK, World Conservation Union.

Berkes, F. (ed.) 1989. Common property resources: ecology and community based sustainable development. London, Belhaven Press.

Burgess, N., FitzGibbon, C. and Clarke, P. 1996. Coastal Forests. In: McClanahan, T. R. and Young, T. P. (eds.) East African ecosystems and their conservation. New York, Oxford University Press: 329 – 359.

Bwathondi, P. O. J. and Mwamsojo, G. U. J. 1993. The status of the fishery resource in the wetlands of Tanzania. G. L. and Crafter, S. A. (eds.) Wetlands of Tanzania: proceedings of a seminar on the wetlands of Tanzania, Morogoro, 27 – 29 November, 1991. IUCN, Gland, Switzerland: 49 – 60.

Cheke, R. A., Mann, C. F. and Allen, R. 2001. Sunbirds: A guide to the sunbirds, flowerpeckers, spiderhunters and sugarbirds of the world. Helm Identification Guides. London, Christopher Helm.

Conway, G. R. and Barbier, E. B. 1990. After the green revolution: sustainable agriculture for development. London, Earthscan Publications Ltd.

Cordeiro, N. J. 1998. A preliminary survey of the montane avifauna of Mt Nilo, East Usambaras, Tanzania. Scopus 20 (May 1998): 1 – 18.

Crean, K. and Geheb, K. 2001. Sustaining appearances: sustainable development and the fisheries of Lake Victoria. Natural Resources Forum 25 (2001): 215 – 224.

Dadzie, S., Haller, R. D. and Trewavas, E. 1988. A note on the fishes of Lake Jipe and Chale [sic.] on the Kenya – Tanzania Border. Journal of the East African Natural History Society and National Museum 78 (192): 46 –51.

Dobson, E. B. 1940. Land tenure of the Wasambaa. Tanzania Notes and Records 10 (1940): 1 – 27.

Ellis, F. 2000. Rural livelihoods and diversity in developing countries. Oxford, Oxford University Press.

Evans, T. D. 1997. Records of birds from the forests of the East Usambara lowlands, Tanzania, August 1994 – February 1995. Scopus 19 (1997): 92 – 108.

FAO (Food and Agricultural Organization), 2001. Food Balance Sheets. www.fao.org. Rome, Food and Agricultural Organization.

Page 82: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

69

Ferguson-Lees, J. and Christie, D. A. 2001. Raptors of the world. Boston, Houghton Mifflin Company.

Geological Survey, 1960. Summary of the geology of Tanganyika. Part II: Geological map. Dar es Salaam, Geological Survey, Ministry of Mines and Commerce.

Gillingham, M. E. 1999. Gaining access to water: formal and working rules of indigenous irrigation management on Mount Kilimanjaro, Tanzania. Natural Resources Journal 39 (3): 419 – 441.

GWP, 2002. Policy guidance and operational tools. ToolBox: Integrated Water Resources Management, Version 1. Global Water Partnership.

Hastenrath, S. and Greischar, L. 1997. Glacier recession on Kilimanjaro, East Africa. Journal of Glaciology 43 (145): 455 – 459.

Homewood, K. and Brockington, D. 1999. Biodiversity, conservation and development in Mkomazi Game Reserve, Tanzania. Global Ecology and Biodiversity 1999 (8): 301 – 313.

Howard, G. (ed.). 1999. Lake Jipe Cross-border Planning Workshop on a Proposal for the Development of Mechanisms for Trans-boundary Management of a Shared Ecosystem. 13th - 15th October, 1999, Moshi (Tanzania and Taveta (Kenya). IUCN - The World Conservation Union, Eastern Africa Regional Programme. Nairobi, December, 1999.

Howard, G. 2002. Integrated River Basin Management (IRBM). In: The Pangani River Basin: Options for Integrated Management. Report on a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8 – 10 May, 2002. Nairobi, IUCN – EARO: 92 - 95.

IUCN, 1999. Situation Analysis: an IUCN approach and method for strategic analysis and planning based on the experience of IUCN Regional and HQ programmes. Prepared by the M&E Initiative. Revised July 1999. Gland, The World Conservation Union (IUCN).

IVO – NORPLAN 1997. Pangani River Training Project Feasibility Study. PBWO – TANESCO, Pangani Falls Redevelopment. IVO International and NORPLAN A/S.

Johnston, P. H. 1946. Some notes on land tenure on Kilimanjaro and the kihamba of the Wachagga. Tanzania Notes and Records 21 (1946): 1 – 20.

Kaihura, F. B. S., Stocking, M. and Kahembe, E. 2001. Soil management and agrodiversity: a case study from Arumeru, Arusha, Tanzania. Paper presented to the symposium on Managing Biodiversity in Agricultural Systems, Montreal, Canada, November 8 - 12, 2001.

Keith Eltringham, S., Morley, R. J., Kingdon, J., Coe, M. J. and McWilliam, N. C. 1999. Checklist: Mammals of Mkomazi. In Coe, M. J., McWilliam, N. C., Stone, G. N. and Packer, M. J. (eds.). Mkomazi: the ecology, biodiversity and conservation of a Tanzanian Savanna. London, Royal Geographical Society (with the Institute of British Geographers): 505 – 510.

Keith Eltringham, S., Cooksey, I. A., Dixon, W. J. B., Raine, N. E., Sheldrick, C. J., McWilliam, N. C. and Packer, M. J. 1999. Large mammals of Mkomazi. In Coe, M. J., McWilliam, N. C., Stone, G. N. and Packer, M. J. (eds.). Mkomazi: the ecology, biodiversity and conservation of a Tanzanian Savanna. London, Royal Geographical Society (with the Institute of British Geographers): 485 – 504.

Kijazi, A. S. 2002. Catchment and mangrove management programmes: activities and environmental concerns in the Pangani Basin. In: The Pangani River Basin: options for management. Report of a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8-10 May 2002. December 2002. Nairobi, IUCN – EARO: 36 - 40.

Lambrechts, C., Woodley, B., Hemp, A., Hemp, C. and Nnyiti, P. 2002. Aerial survey of the threats to Mt. Kilimanjaro forests. Dar es Salaam, GEF Small Grants Programme, UNDP.

Page 83: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

70

Lein, H. 2002. Migration, irrigation and land-use changes in the lowlands of Kilimanjaro, Tanzania. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 28 – 38.

Lovgren, S. 2001. All That Glitters. With Rena Singer and David Enrich. U.S. News & World Report, 131 (6), 13/8/2001.

Luhikula, G. 2002. The Tanzania Coastal Management Partnership (TCMP): a partner in conservation. In: The Pangani River Basin: Options for Integrated Management. Report on a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8 – 10 May, 2002. Nairobi, IUCN – EARO: 86 – 90.

Majtenyi, C. and Muindi, M. 2001. Tanzania: big is beautiful at Merelani. New African, Oct. 2001, Issue 400.

Makule, D. E. n.d. The Pangani Basin Water Resources Management. http://srdis.ciesin.columbia. edu/cases/tanzania-019.html

Mbonile, M. J. 2002. Rural population mobility in the Pangani Basin, Tanzania. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 14 – 27.

McCay, B. J. and Acheson, J. M. (eds.) 1987. The question of the commons: the culture and ecology of communal resources. Tucson, University of Arizona Press.

McClanahan, T. R. and Young, T. P. (eds.) 1996. East African ecosystems and their conservation. New York, Oxford University Press.

Mgongo, E. N. E. 2002. Tanga Coastal Zone Conservation and Development Programme: activities and concerns in the Lower Pangani River Basin. In: The Pangani River Basin: Options for Integrated Management. Report on a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8 – 10 May, 2002. Nairobi, IUCN – EARO: 81 – 85.

Misana, S. and Makoi, J. 2001. The impact of irrigation on soil fertility and salinity/sodicity in the Pangani River Basin. In Ngana, J. O. (ed.). Water resources management in the Pangani River Basin: challenges and opportunities. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 83 – 103.

Mjata, P. J. 2002. The Traditional Irrigation and Environmental Development Organisation (TIP). In: The Pangani River Basin: Options for Integrated Management. Report on a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8 – 10 May, 2002. Nairobi, IUCN – EARO: 78 – 80.

Mkhandi, S. and J. O. Ngana 2001. Trend analysis and spatial variability of annual rainfall. In Ngana, J. O. (ed.). Water resources management in the Pangani River Basin: challenges and opportunities. Dar es Salaam University Press, Dar es Salaam. 150pp.: 11 - 20

Mkuula, S. 1993. Pollution of wetlands in Tanzania. In: Kamukala, G. L. and Crafter, S. A. (eds.) Wetlands of Tanzania: proceedings of a seminar on the wetlands of Tanzania, Morogoro, 27 – 29 November, 1991. IUCN, Gland, Switzerland: 85 – 93.

Mpemba, E. B. 1993. Wildlife resources and tourism in wetlands of Tanzania. In: Kamukala, G. L. and Crafter, S. A. (eds.) Wetlands of Tanzania: proceedings of a seminar on the wetlands of Tanzania, Morogoro, 27 – 29 November, 1991. IUCN, Gland, Switzerland: 61 – 66.

Mtalo, F. W. and Ndomba, P. M. Estimation of soil erosion in the Pangani Basin upstream of Nyumba ya Mungu Reservoir. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 196 – 210.

Mujwahuzi, M. R. 2001. Water use conflicts in the Pangani Basin. In Ngana, J. O. (ed.). Water resources management in the Pangani River Basin: challenges and opportunities. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 128 – 137.

Page 84: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

71

Musyoki, M. M. 2003. The situation analysis of the Kenyan part of the Pangani River Basin Catchment: the Lake Jipe Watershed and system. Mombasa, Kenya: The Coast Development Authority, April 2003.

Musyoki, M. M. and Mwandotto, B. A. J. 1999. Presentation of results/reports on the assessment of management needs for the watershed wetlands and waters of Lake Jipe. Paper presented at the Lake Jipe Cross-border Workshop, 13th - 15th October, 1999.

Mwamfupe, D. 2001. Shortage of water for irrigation and farmers’ response: a case study of Makuyuni and Kahe wards of Kilimanjaro Region, Tanzania. In Ngana, J. O. (ed.). Water resources management in the Pangani River Basin: challenges and opportunities. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 73 - 82.

Mwamfupe, D. G., 2002. The role of non-farm activities in household economies: a case study of Pangani Basin, Tanzania. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 39 – 47.

Newmark, W. D. 1998. Forest area, fragmentation, and loss in the Eastern Arc Mountains: implications for the conservation of biological diversity. Journal of East African Natural History 87 (1998): 1 – 8.

Ngana, J. O. 2001. Integrated water resources management: the case of the Pangani River Basin. In Ngana, J. O. (ed.). Water resources management in the Pangani River Basin: challenges and opportunities. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 1 - 8.

Ngula, D. E. P. 2002. Pangani River Basin: power generation and the environment. In: The Pangani River Basin: options for management. Report of a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8-10 May 2002. December 2002. Nairobi, IUCN – EARO: 67 – 71.

North, D. 1990. Institutions, institutional change and economic performance. Cambridge, Cambridge University Press.

Nshubemuki, L. 1993. Forestry resources in Tanzania’s wetlands: concepts and potentials. In: Kamukala, G. L. and Crafter, S. A. (eds.) Wetlands of Tanzania: proceedings of a seminar on the wetlands of Tanzania, Morogoro, 27 – 29 November, 1991. IUCN, Gland, Switzerland:

Ole Sikar, T. Conflicts over natural resources in Maasai district of Simanjiro, Tanzania. Forests, trees and people - Newsletter No. 30, March 1996.

Ostrom, E. 1990. Governing the commons: the evolution of institutions for collective action. Cambridge University Press, Cambridge.

PAMOJA, 2002. Dialogue on Water: A concept paper on water resource use and management of conflicts in the Pangani River Basin: the possible role of PAMOJA. Moshi, PAMOJA.

Richmond, M. D. (ed.) 1997. A guide to the seashores of Eastern Africa and the Western Indian Ocean Islands. SIDA/Department for Research Cooperation, SAREC.

Rodgers, A. Mugabe, J. and Muthenge, C. 2001. Beyond Boundaries: Regional Overview of Transboundary Natural Resource Management in Eastern Africa. In Biodiversity Support Program, Beyond Boundaries: Transboundary Natural Resource Management in Eastern Africa. Washington, D.C., U.S.A.: Biodiversity Support Program.

Rodgers, W. A. The Miombo Woodlands. In McClanahan, T. R. and Young, T. P. (eds.) East African ecosystems and their conservation. New York, Oxford University Press: 299 - 325.

RoK (Republic of Kenya) 2002. Kenya Gazette Supplement. Acts, 2002 (no. 9); The Water Act, 2002. Nairobi, October 24th, 2002. Nairobi, The Government Printer.

RoK (Republic of Kenya) 2003. The First National Water Resources Management Strategy. Nairobi, Ministry of Water Resources Management and Development, April 2003.

Page 85: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Røhr, P. C. and Killingtveit, Å. 2002. Study of two catchments on the hillside of Mt. Kilimanjaro. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 211 – 231.

Røhr, P. C. , Ngana, J. and Killingtveit, Å. 2002. Investigations of Chemka Spring, Kilimanjaro Region, Tanzania. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 265 - 272.

Røhr, P. C., Killingtveit, Å., Nderingo, G. M. and Kigadye, P. E. n.d. Water and environmental conflicts in the Pangani River Basin – hydropower or irrigation? Undated manuscript.

Røhr, P. C., Killingtveit, Å Rumambo, O. H. 2002. Brief report on the River Basin Management Project in Tanzania. In: The Pangani River Basin: options for management. Report of a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8-10 May 2002. December 2002. Nairobi, IUCN – EARO: 44 – 48.

Sahib, I. 2002. The Tanzania Planting Company. In: The Pangani River Basin: options for management. Report of a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8-10 May 2002. December 2002. Nairobi, IUCN – EARO: 72 – 73.

Sarmett, J. D. and Kamugisha, S. M. 2002 Control of water utilisation in the Pangani Basin: the role of PBWO and PBWB. In: The Pangani River Basin: options for management. Report of a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8-10 May 2002. December 2002. Nairobi, IUCN – EARO: 19 – 24.

Schechambo, F. 2002. Forest valuation and economic policies: learning from Mount Meru Forest Reserve. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 161 – 169.

Sishira, E. K. 2002. Land use change and sustainability of water resource utilisation in The Pangani River Basin downstream of the Nyumba ya Mungu. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 83 – 89.

Sjöholm, H. and Luono, S. 2002. The green forest pastures of Suledo - Maasai communities organise to save their forests and secure their livelihoods. Forests, trees and people - Newsletter No. 46, September, 2002.

Stoorvogel, J. J. and Smaling, E. M. A. 1990. Assessment of soil nutrient depletion in subsaharan Africa: 1983 - 2000. Vol. 1, Main Report. Wageningen, The Netherlands, Winand Staring Centre for Integrated Land, Soil and Water Research.

Tagseth, M. 2002. Local practises and changes in farmer-managed irrigation in the Himo Catchment, Kilimanjaro. In Ngana, J. O. (ed.) Water resources management: the case of Pangani River Basin. Issues and approaches. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 48 - 63.

TANESCO, 1994. Environmental Impact Assessment of the redevelopment of the hydroelectric power station at Pangani Falls: Baseline studies: mitigation of adverse impacts and monitoring the attainment of intended mitigation. IVO – NORPLAN Joint Venture.

URT (United Republic of Tanzania), 2002. National Water Policy. Dar es Salaam, Ministry of Water and Livestock Development.

Vanden Bossche, J.-P. and Bernacsek, G. M. 1990. Sourcebook for the inland fishery resources of Africa. Vol. 1. Cifa Technical Paper 18/1. Rome, Food and Agricultural Organization.

Warren, A. 1995. Changing understandings of the nature of environmental paradigms. Transactions of the Institute of British Geographers NS 20 (1995): 193 - 203.

72

Page 86: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

W.C.E.D. 1987. Our common future. Oxford, O.U.P for the World Commission on Environment and Development.

W.C.M.C. (World Conservation Monitoring Centre). 1985. Arusha National Park Factsheet. www.unep.wcmc. org

W.C.M.C. (World Conservation Monitoring Centre). 1987. Kilimanjaro National Park Factsheet. www.unep. wcmc.org

Wegelin-Schuringa, M. 1998. Water Demand Management and the Urban Poor. The Netherlands, IRC International Water and Sanitation Centre.

West, K. 2002. The Water and Nature Initiative Challenge. In: The Pangani River Basin: Options for Integrated Management. Report on a Workshop held at the Kilimanjaro Crane Hotel, Moshi, Tanzania, 8 – 10 May, 2002. Nairobi, IUCN – EARO: 95 – 96.

WHO (World Health Organization). 2001. National health statistics. www.who.org. Geneva, World Health Organization.

Wily, L. 1999. Moving forward in African community forestry: trading power, not use rights. Society and Natural Resources 12 (1999): 49 – 61.

Wilson, D. C., Medard, M. Harris, C. K. and Wiley, D. S. 1996. Potentials for comanagement of the Nile perch fishery – Lake Victoria, Tanzania. Paper presented at the ‘Voices from the Commons’ conference, International Association for the study of common property, Berkeley, CA, June 5-8, 1996.

UNICEF (United Nations International Children’s Emergency Fund). 2001. The State of the World’s Children 2000. www.unicef.org. New York, UNICEF.

Yanda, P. Z. and Shishira, E. K. 2001. Forestry conservation and resource utilisation on the southern slopes of Mount Kilimanjaro: trends, conflicts and resolutions. In Ngana, J. O. (ed.). Water resources management in the Pangani River Basin: challenges and opportunities. Dar es Salaam, Dar es Salaam University Press: 104 - 117.

Zimmerman, D., Turner, D. Pratt, D Willis, I. 1996. Birds of Kenya and Northern Tanzania. London, Christopher Helm.

.

73

Page 87: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

Wahojiwa Burra, R., Mshauri, PAMOJA, Arusha tarehe 13, Novemba, 2002

Bwoyo, D., Meneja Misitu wa Eneo la Chanzo cha Mto, Arusha, tarehe 22, Novemba, 2002

Fundi, H., Mtaalam wa Haidrolojia wa Mkoa, Mkoa wa Tanga, Tanga, tarehe 18, Novemba 2002.

Kijazi, A., na Nashanda, E. Idara ya Misitu na Nyuki, Dar es Salaam, tarehe 15, Novemba, 2002

Lugaiyamu, J., Meneja, Mfumo wa Mitambo ya Umeme wa maji Pangani TANESCO, Hale, tarehe 18, Novemba, 2002

Mihayo, J. M., Mkurugenzi, Rasilimali za Maji, Dar es Salaam, tarehe 15, Novemba, 2002

Mjata, P.J., Afisa Mipango wa Matumizi ya Ardhi, TIP, Moshi, tarehe 21, Novemba, 2002

Msuha, M. Afisa ndege, Chama cha Hifadhi ya Wanyama pori cha Tanzania, Dar es Salaam, tarehe 14, Novemba, 2002

Nasari, J., Mhaidrolojia wa Mkoa, Mkoa wa Arusha, Arusha, tarehe 13, Novemba, 2002

Ngana, J., Profesa Mwandamizi wa Utafiti, Taasisi ya Tathmini ya Rasilimali, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, tarehe 14, Novemba, 2002

Ngula, D., Meneja- Utafiti na Maendeleo, TANESCO, tarehe 14 Novemba, 2002

Rumambo, O., Mshauri wa Usimamizi wa Bonde, Mradi wa Usimamizi wa Mabonde ya Mito, Wizara ya Maji na Maendeleo ya Mifugo, Dar es Salaam, tarehe 15, Novemba, 2002

Salehe, J., Meneja Mradi wa Taifa, UNDP/GEF- Mradi wa Bayoanuwai za kimataifa za Afrika ya Mashariki, Arusha, Novemba, tarehe 22, Novemba, 2002

Sarmett, J., Afisa wa Maji, Ofisi ya Maji Bonde la Pangani, Dar es Salaam, tarehe 14, Novemba, 2002

Serikali ya Kijiji cha Shiri – Njoro, Moshi, tarehe 22, Novemba, 2002;

Tegemeo na Serikali ya kijiji cha Kawaya- Kawaya, tarehe 21, Novemba, 2002.

Waliohojiwa kwa ajili ya kiambatanisho cha 1

Aram, F. V. – Mamlaka ya Maji safi na Majitaka Mjini Tanga.

Denis, E. M. –Ofisi ya Mhandisi wa Maji Wilaya ya Handeni.

Fundi, H. – Afisa wa Haidrolojia wa Mkoa wa Tanga

Hamisi, H. – Mratibu, Hellen Keller International (APOC)

Kisheru, N. – Afisa Maliasili wa Mkoa, RAS Tanga

Lyimo, Z.C.- Afisa Mifugo wa Mkoa, RAS Tanga

Maggid, R.E. B. – Mratibu, Mradi wa CDTI Tanga.

Malange, J. P. –Mhandisi wa maji Mkoa wa Tanga, RAS Tanga

Materu, E.A. – Maabara ya Maji Tanga

Matiku, W. – Misitu ya Eneo la Vyanzo vya Mito Usambara Mashariki

Mwakibuzi, H. – Afisa Mipango wa Wilaya, Muheza

Mzee, R. S. – Hifadhi ya Asili Amani

Mtemi, A. - Hifadhi ya Asili Amani

Sesame, M. – Ofisi ya Mhandisi wa Maji Wilaya ya Handeni

Tungu, L.S. M. – Afisa Kilimo wa Mkoa, RAS Tanga

74

Page 88: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

75

H. Kiambatanisho cha 1: Mabonde madogo yaliyojumuishwa kiutawala katika

Bonde la Pangani6

H.1 UtanguliziBonde la Mto Pangani lina eneo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 43,650. Bonde hili limezungukwa na mabonde madogo yanayojitegemea, amabayo si sehemu hasa ya Bonde la Mto Pangani kihaidrolojia. Kiutawala yapo chini ya Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani (PBWO) kwa sababu ni madogo mno kustahili kuwa na ofisi za mabonde yao yenyewe. Eneo linalosimamiwa kiutawala na Ofisi ya Maji ya Bonde la Pangani ni pamoja na Bonde la Mto Pangani, mabonde madogo ya Umba, Zigi7, Msangazi, Mkulumuzi na mito midogo ya pwani, yote pamoja hufanya jumla ya kilomita za mraba 58,510. Katika kiambatanisho hiki, taarifa kuhusu mabonde haya ya nyongeza zimetolewa kwa muhtasari kama msingi ambapo shughuli za mradi katika Bonde la Mto Pangani zinaweza kupanuka baadaye ili kujumuisha mabonde haya ya ziada. Mabonde yanayohusika ni:

• Bonde la Mto Umba (kilomita za mraba 8,070)

• Bonde la Mto Msangazi (kilomita za mraba 5,030)

• Bonde la Mto Zigi (angalia mito ya Pwani)

• Bonde la Mito ya Pwani (kilomita za mraba 2,080 ikiwemo Zigi na Mkulumuzi): mbali na Mkulumuzi mito mingi ya Eneo la Chanzo cha Mito ya Pwani ni ya msimu.

Kila moja ya maeneo haya ya vyanzo vya mito linajadiliwa kipekee.

H.2 Bonde la Mto Umba Bonde la Mto Umba lina eneo lenye ukubwa wa kilomita za mraba 8,070 (kilomita za mraba 2,560 kati ya hizo ziko nchini Kenya), ambapo mdomo wa Mto Umba uko eneo la Vanga katika pwani ya Kenya. Mto huu una mtandao mkubwa wa vijito vingi vikitokea katika miteremko ya Kaskazini Magharibi ya Milima ya Usambara. Vijito hivi huingia katika mto Umba kutokea Kusini. Mto huu unapata vijito vichache sana kutoka Kaskazini. Eneo hili hupata mvua ya wastani wa milimita 600 kwa mwaka.

Hifadhi ya wanyamapori ya Umba, ambayo awali ilikuwa sehemu ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Mkomazi, ipo katika bonde hili. Uoto wa asili wa mbuga hii unachukua eneo kubwa la chanzo cha mto huu: vichaka vya aina ya Savana ya ukame iliyotawanyika na miti mifupi. Miteremko ya milima katika bonde inafunikwa na msitu wa milima ya Afrika. Bonde la Mto Umba lina watu wachache. Matumizi makubwa ya ardhi katika sehemu yake ya Kaskazini ni hifadhi ya wanyamapori, wakati ufugaji wa ngo’mbe ni matumizi makubwa ya ardhi upande wa Kusini.

6Kiambatanisho hiki kimetayarishwa na Ofisi ya Maji Bonde la Pangani

7Baadhi ya Waandishi hutumia tahajia ‘Sigi’, ‘Zigi’ ndio tahajia inayopendelewa na wakazi wa eneo la chanzo cha mto (pers. Comm., 2003).

Page 89: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

76

Kilimo na Umwagiliaji Kilimo kinachotegemea mvua kinafanyika zaidi kuliko kilimo cha umwagiliaji. Hata hivyo, mbali na mabonde ya Mkomazi na Luengera, ambayo yapo katika eneo la Bonde la Mto Pangani, miradi mingi midogo ya umwagiliaji iliyopo au iliyopendekezwa katika mkoa wa Tanga ipo katika bonde la mto Umba na vijito vyake. Miradi hii ni pamoja na Mnazi, Kitivo, kijiji cha Kivingo Mnazi na mradi wa umwagiliaji wa Mwakijembe. Zao linalomwagiliwa zaidi ni mpunga, likifuatiwa na mahindi. Katika sehemu za juu za bonde; mbogamboga na viazi mviringo pia vinalimwa kwa kumwagiliwa. Eneo lililo chini ya mpango wa umwagiliaji kwa ujumla linakadiriwa kuwa hekta 1475, likitumia kiasi cha maji kinachokadiriwa kuwa mita za ujazo 25.2 x 106 kwa mwaka.

MaliasiliMaeneo yaliyohifadhiwaHifadhi ya wanyamapori ya Umba ina eneo la kilomita za mraba 450 likipakana na mbuga ya Taifa ya Tsavo ya Kenya. Wanyamapori wanaopatikana katika hifadhi hii ni pamoja na nyati, tembo, simba na aina nyingi za swala. Tishio kubwa linaloikabili hifadhi hii ni ujangili unaofanywa na wenyeji na watu wanaoingia katika eneo hili kutoka Kenya.

MisituEneo la Chanzo cha Mto Umba hapo awali lilikuwa na utajiri wa misitu mingi ambamo zilikuwemo spishi za miti kama Mkarambati na Mkingu. Mkarambati unatumika zaidi kwa kutengeneza sanaa za uchongaji, miti ya kujengea na samani. Inavunwa kwa wingi na inadhaniwa kuwa spishi iliyo hatarini kutoweka. Uvunaji haramu wa misitu kwa ajili ya kutengeneza mkaa pia hufanyika.

Ili kushughulikia tazizo la uvunaji haramu wa misitu, njia za usimamizi wa misitu kijamii zimeanzishwa na wanavijiji kama vile vijiji vya Mwakijembe, Mwanyumba, Mavovo na Daluni.

MadiniBonde la Mto Umba lina utajiri wa mashapo ya madini, hususan kuzunguka maeneo ya Mghwashi na Kararani, johari ya bluu inapatikana, pamoja na ‘tomalini’ ya kijani na ganeti ya waridi. Uchimbaji madini kwa sasa unafanywa na wachimbaji wadogo ambao hawana masoko ya ndani, na hulazimika kuuza vito johari vyao kwa njia ya magendo nchini Kenya (Kisheru, Mhojiwa)

Mgogoro wa matumizi ya maji Kuna migogoro kati ya watumiaji maji kutokana na ugavi usiotosheleza, hasa katika maeneo ambako kilimo cha umwagiliaji kinafanyika.

Mtandao wa ukusanyaji data• Kituo cha Mto Umba kilichoko Mlalo (Namba IB 1): kituo kidogo, chenye safu ya geji 0-3 m: kituo

hiki kinafanya kazi, “rating curve” inahitaji kuboreshwa.

• Kituo cha Mto Umba kilichoko Mwakijembe (Namba IB 4A): kituo kikuu, chenye safu ya geji 0-4m; Kituo kina kiingiza data aina ‘orpheus’, kinafanya kazi japo kinahitaji marekebisho.

• Kituo cha Mto Mbalamo kilichoko Kivingo (Namba IB1A): kituo kidogo chenye safu ya geji 0-2m. Kinahitaji ukarabati.

• Kituo cha Mto Bombo kilichoko Kwamkole (Namba IB 5): kituo kidogo, kinachofanya kazi, kina safu ya geji 0-3m.

• Kituo cha mvua cha Mlalo (Namba 94.38068); kinafanya kazi na kiko katika hali nzuri.

• Kituo cha hali ya hewa cha Mnazi (Namba 94.38075): kinafanya kazi vizuri, kina vifaa vya upimaji vya kawaida na kinachojiendesha chenyewe.

Page 90: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

77

H. 3 Bonde la Mto MsangaziBonde la Mto Msangazi lina ukubwa wa kilomita za mraba 5,030 na linafikiriwa kujumuisha maeneo ya vyanzo vyembamba vya mito vilivyotanda kutoka Magharibi mpaka Mashariki, karibu upana mzima wa mkoa wa Tanga. Linapakana na Bonde la Mto Pangani kwa upande wa Kusini. Vijito vingi hutiririka wakati wa majira ya mvua nyingi kuliko kawaida katika maeneo yake ya juu. Hata hivyo katika sehemu za upande wa chini wa mji wa Handeni, mto Msangazi hutiririka kwa utaratibu wa kawaida wakati wa msimu wa masika.

Bonde lina sura ya nchi inayofanana, na linaweza kuainishwa kama vilima, ingawa sehemu za chini ambako kuna mashamba ya mkonge na minazi ni tambarare. Uoto uliopo ni vichaka na miti michache ya savana. Mbali na kilimo cha mtawanyiko, sehemu kubwa ya ardhi haijatumika kiuchumi. Wastani wa mvua kwa mwaka ni kadiri ya milimita 900.

Idadi ya watuBonde la Mto Msangazi limeenea wilaya tatu za mkoa waTanga: Kilindi, Handeni na Pangani. Idadi ya watu katika eneo lilopo katika wilaya ya Kilindi ilikuwa 31,177 mwaka 2002, na Handeni walikuwa 141,263. Idadi hii inawakilisha kadiri ya asilimia 44 ya idadi ya watu wa wilaya hizi mbili. Idadi ya watu katika bonde la mto Msangazi katika wilaya ya Pangani ni watu 10, 298.

Matumizi ya ardhi• Kilimo: kilimo ni cha kujikimu. Mazao yanayolimwa ni pamoja na mahindi, mihogo, maharage,

ndizi, miwa na aina mbalimbali za mboga. Zao jipya lililoanzishwa hivi karibuni, mirongeronge, inatumika kwa kutengeneza mafuta ya kupikia na usafishaji wa maji.

• Mifugo: idadi ndogo ya ng’ombe, mbuzi na kondoo hufugwa katika bonde.

MaliasiliMajiMji mkubwa katika bonde la mto Msangazi ni Handeni (watu 7,700). Kiasi kikubwa cha maji kwa matumizi ya mji huu huchukuliwa kutoka Mto Pangani. Kwa nyongeza, mji huu hupata maji kutoka kwenye visima virefu viwili: Nderema (mita za ujazo 9 kwa saa) na Mnazini (mita za ujazo 12 kwa saa). Visima hivi huhudumia asilimia 35 ya wakazi wa mji huu. Chanzo cha mwisho cha maji cha mji huu kinatoka katika moja ya vijito vya mto Msangazi, ambacho kimejengewa bwawa dogo. Bwawa hili lina uwezo wa kuhifadhi mita za ujazo 22,500, na kadiri ya mita za ujazo 12 huchukuliwa kwa saa.

MisituMisitu ya Bondo na Kwamsisi yote miwili ipo katika bonde hili. Spishi za miti zinazopatikana ni mtondoro, mpingu, mninga na mkomba.

WanyamaporiWanyamapori wavumilivu hupatikana sehemu za juu za maeneo ya chanzo cha mto, ikiwa ni pamoja na nguruwe mwitu, kima, nyani na palahala. Katika sehemu ya chini ya maeneo ya chanzo cha mto (katika Wilaya ya Pangani) kuna Mbuga ya Taifa ya Sadani, ambamo kuna tembo, twiga, na aina za paa/palahala

Madini Bonde la mto Msangazi halina madini muhimu yanayojulikana.

Page 91: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

78

Matatizo na migogoro Inayoweza kutokea• Kuingiliwa na kilimo kuzunguka vyanzo vya maji, zikiwemo kingo za mto.

• Mioto ya vichakani/misituni: Haya ni matatizo makubwa, moto huwashwa ili kusafisha vichaka kwa ajili ya kilimo.

• Uvunaji haramu wa miti: kwa ajili ya mbao, miti ya kujengea na mkaa. Miti ya mbao inayotakiwa sana ni mninga, mpingu, mtondoro na mkomba.

• Kuna mgogoro unaoibuka kati ya wafugaji na wakulima juu ya maeneo ya kunyweshea mifugo.

MagonjwaMagonjwa yanayotokea kwa wingi katika bonde la mto Msangazi ni malaria na homa ya matumbo. Kipindupindu na magonjwa mengine yanayosababisha kuharisha hutokea mara chache.

Mtandao wa ukusanyaji data

• Kituo cha Mto Msangazi kilichoko Kideleko (Namba IE 3): kituo kidogo, kinafanya kazi, kina geji 0-1m

• Kituo cha Mto Msangazi kilichoko Kwedilomba (Namba IE 1): kituo kinafanya kazi, safu ya geji 0-2m, kina kiingiza data aina ya ‘Thalamides’.

• Kituo cha hali ya hewa cha Handeni (Namba 95.38079): kinafanya kazi pamoja na kituo kinachojiendesha chenyewe.

• Kituo cha mvua kilichoko Kwedilomba: kinafanya kazi.

Mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi katika Bonde la mto Msangazi• World Vission (shirika lisilo la kiserikali)

• HADEA (Chama cha Maendeleo Handeni)

• HIAP – Mradi Shirikishi wa Kilimo mseto Handeni (lilimaliza shughuli zake mwaka 2002)

• Ded-GTZ-Msaada wa kiufundi na ushauri katika wilaya (maji)

H.4 Bonde la Mto ZigiMto wa kudumu wa Zigi huanzia katika miteremko ya mashariki ya Milima ya Usambara, na una vijito vikuu viwili vinavyotiririka kutoka Kaskazini na Kusini (Muzi na Kihuhwi). Baada ya kuungana, Mto Zigi hutiririka kuelekea Mashariki na kuingia katika Bahari ya Hindi kupitia Bwawa la Mabayani, chanzo kikuu cha maji kwa Jiji la Tanga.

Maeneo ya juu ya chanzo cha mto Zigi ni ya milima, ambayo kwa sehemu kubwa ina misitu minene iliyopakana na mashamba ya chai. Sehemu zake za chini ni za vilima vyenye vichaka vya aina ya savana kame na miti mifupi, pia mashamba ya mkonge. Katika ukanda wa pwani, minazi na michikichi iko kwa wingi. Kwa ujumla eneo zima la bonde hili lina uoto wa kutosha na hatari ya mmomonyoko ni ndogo.

Mvua katika Bonde la Mto Zigi ni za misimu miwili. Hata hivyo, mgawanyo wake hutofautiana kati milimita 1,000 mpaka 2,000. Wastani wa mvua kwa mwaka unakadiriwa kuwa milimita 1,200 hadi milimita 1,400.

Page 92: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

MaliasiliMisitu Kuna hekta 30,000 za msitu katika eneo la Chanzo cha Mto Zigi, ambao unajumuisha msitu wa eneo la vyanzo cha mito wa Usambara Mashariki (EUCF), ambao ni sehemu ya misitu ya Milima ya Tao la Mashariki. Umuhimu wa misitu ya eneo la chanzo cha mto ni pamoja na:

• Utoaji mbao na mimea ya dawa kwa jamii;

• Misitu hii ni chanzo cha Mto Zigi, ambao hutoa maji ya matumizi ya nyumbani kwa Jiji la Tanga;

• Kuhifadhi maji kwa kurekebisha kasi ya mtiririko wa maji, kuzuia mmomonyoko wa udongo, kuboresha upenyaji wa maji kwenye hazina ya maji ya ardhini na ubora wa maji;

• Ni makazi ya viwango vya juu sana vya bayoanuwai, na huchangia kudumisha makundi ya jeni kidunia;

• Misitu ya kwenye genge la Milima ya Usambara Mashariki huzuia mmomonyoko na mporomoko wa ardhi.

Bayoanuwai na maeneo yaliyohifadhiwaHifadhi ya Asili ya Amani (ANR) ilianzishwa mwaka 1997 na ina jumla ya eneo la hekta 8,380. Hifadhi hii iko kwenye misitu ya vyanzo vya mito ya Usambara Mashariki (EUCF). Milima ya Usambara Mashariki ni fungu la mlima lililo kubwa zaidi katika safu ya Milima ya Tao la Mashariki. Hifadhi ya Asili ya Amani ina misitu mirefu ya kuvutia ya milimani na misitu inayopukutisha majani ya nyanda za chini zenye wastani wa kikomo cha mwinuko cha mita 850.

Kibayolojia, Hifadhi ya Asili ya Amani ina utajiri mkubwa wa mchanganyiko wa spishi. Milima ya Usambara Mashariki inachukuliwa kama kituo cha kidunia cha mimea anuwai. Miongoni mwa jenasi na spishi za mimea inayopatikana katika hifadhi hii ya msitu pekee ni ‘Saintapaulia’ (spishi 9), Cynometra (spishi 4), ‘Streptokapus’ (spishi 2), Impatients katae, Vernonia amaniencis, Dolichometra leucantha na Cordia peter;

Kwa kuongezea, Milima ya Usambara Mashariki inatambuliwa kuwa ni ya pili kwa kuwa na aina mbalimbali za wanyama barani Afrika. Baadhi ya mamalia wa Hifadhi ya Asili ya Amani wamewekwa kwenye kundi la walio hatarini kutoweka duniani, kama vile Popo Matunda wa Afrika Mashariki (Myonyctaris relicta), Panya wadogo (wanaofanana na tembo) wekundu na weusi (Rhyncoyon petersi), Nguchiro wenye mikia yenye manyoya (Bdeo-grade crassicaud omnivore) na Palahala wa Abbot (Cephalophus spadix).

Halmashauri ya Kimataifa ya Kuhifadhi Ndege (ICBP) imeainisha misitu ya milimani na ya nyanda za chini ya Usambara ya Mashariki kama eneo maalum la ndege wanaopatikana kipekee (EBA). Spishi kumi na tatu za ndege walio hatarini kutoweka duniani, kama vile Bundi Tai wa Usambara (Bubo vosseleri) Kwera Usambara (Ploseus nicolli), Chozi Pwani (Anthreptes pallidigaster), na Kolokolo domorefu (Apalismoreaui moreaui), wanajulikana kuwa huishi katika Hifadhi ya Asili ya Amani.

Miongoni mwa spishi za amfibia za Hifadhi na Misitu hii, spishi za watambaazi, wanyama wasio na uti wa mgongo na bayoanuwai pia hupatikana kwa wingi kipekee katika sehemu hii kwa kiwango cha juu sana. Amfibia wengi huzaliana na kujipatia makazi ndani na kandokando ya Mto Zigi, ambao pia hufanya makazi kwa spishi nyingi za watambaazi na wadudu.

Maji na Udongo

Hifadhi ya Asili ya Amani ni mojawapo ya maeneo ya chanzo cha maji iliyo muhimu sana katika Milima ya Usambara Mashariki. Misitu ya mvua ya milimani ambayo huenea sehemu kubwa zaidi ya Hifadhi hii hutoa mchango muhimu katika haidrolojia ya Mkoa wa Tanga. Mto Zigi hutoa maji kwa matumizi ya nyumbani kwa Jiji la Tanga (lenye watu 300,000), viwanda vilivyopo, mashamba na jamii zinazopakana nayo.

Bwawa la Mabayani liko katika Mto Zigi, ambalo maji yake hukimu Jiji la Tanga. Hodhi yake ni takriban mita 3,500 kwa urefu na wastani wa upana wa mita 400. Hapo awali (mwaka 1978), hodhi hii ilikuwa na

79

Page 93: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

80

uwezo wa kuhifadhi mita za ujazo milioni 7.7, lakini kiasi hiki kimepungua polepole kutokana na kujaa kwa mchangatope kunakosababishwa na mmomonyoko na mporomoko wa ardhi. Mashapo ya ziada yanatokana na mimea iliyong’olewa na maji ya mafuriko, maji machafu yatokanayo na mchakato wa kuponoa katani na mata zizalishwazo katika bwawa lenyewe na jamii za mimea na wanyama wadogo wadogo wanaoishi katika maji, samaki na wanyama wengine wasio na uti wa mgongo.

Uozaji wa mata za viumbe hai unahitaji hewa ya oksijeni, hali inayosababisha uondoaji oksijeni kwenye maji yanayozizunguka. Kuwepo kwa virutubisho hivyo pia kunachochea uzalishaji wa mimea zaidi, na kusababisha uzalishaji zaidi wa mata za viumbe hai na hatimaye upunguaji wa oksijeni chini ya bwawa. Mchanganyiko wa michakato hii ya uingiaji wa virutubisho na hatimaye uondoaji wa oksijeni vinaweza kusababisha ongezeko la viwango vya virutubisho, ingawa hakujapatikana ushahidi wa jambo hii kutoka kwenye bwawa hilo. Hata hivyo, shaka ya kuwa hii inaweza kutokea ipo, na yafuatayo ni mapendekezo ya hatua zinazoweza kupunguza:

• Kufuatilia ulimbikizaji wa masimbi/mata za viumbe hai katika bwawa;

• Kuondoa mara kwa mara magugu ya majini (mfano hyacinth na makabichi ya Mto Nile) kutoka bwawani kwa mikono, kibayolojia au kwa mashine.

• Kudhibiti ubora na ujazo wa maji machafu kutoka viwanda vya katani vilivyopo eneo la juu la mto;

• Kutambua uwiano wa kiasi cha mimea ya majini ambayo huzolewa kupitia njia ya kupunguzia maji ya bwawa hili. Ikiwa kiasi ni kidogo, mbinu za kuongeza lazima zitafutwe.

UvuviUvuvi unafanyika zaidi katika pwani ya Bahari ya Hindi, ambako mdomo wa Mto Zigi ndipo ulipo. Uvuvi mdogo mdogo upo katika mkondo wake, ukilenga samaki kama kambare, perege, ningu, ngogogo, kuyu na wengineo. Uvuvi katika bwawa la Mabayani umepigwa marufuku kwa sababu maji yake yamekusudiwa kama chanzo cha maji ya matumizi ya nyumbani kwa Manispaa ya Tanga.

ArdhiMatumizi makuu ya ardhi katika bonde ni kilimo, kinachofanyika zaidi katika ngazi ya kiwango kidogo. Mazao kama mahindi, mihogo, ndizi na matunda yanalimwa, wakati mazao ya biashara ni mkonge, chai na misitu (kama mradi wa Shamba la Mitiki la Longuza).Kwa kiasi kidogo, ufugaji wa ng’ombe pia hufanyika.

Matatizo• Uharibifu wa misitu: hii hutokea hasa kama matokeo ya uvunaji haramu wa miti kwa ajili ya mbao,

kuni miti ya kujengea, usafishaji kwa ajili ya kilimo, nk., na husababisha kuongeza kasi ya mtiririko wa maji juu ya ardhi, wakati ikipunguza kiasi cha maji kinachopenya ardhini.

• Uondoaji wa maji machafu: Maji machafu yanayoondolewa kutoka viwanda vya katani bila kusafishwa au yasiyosafishwa kikamilifu husababisha uondoaji oksijeni katika maji ambayo uchafu huu huingia, na hufanya kazi kama virutubisho, hivyo kusaidia kukuza ongezeko la virutubisho.

• Matumizi ya kemikali za kilimo: ingawa hakujapatikana data juu ya athari ya kemikali za kilimo kwenye vyanzo vya maji katika bonde hili, upo uwezekano kuwa mabaki ya kemikali za kilimo hufikia vyanzo vya maji kupitia maji ya mvua. Kutegemeana na aina ya kemikali ya kilimo na kiwango cha kukolea, afya ya binadamu na viumbe vya majini inaweza kuathirika kwa mabaki hayo. Katika eneo la chanzo cha Mto Zigi, kemikali za kilimo, yakiwemo madawa ya kuulia wadudu, dawa za mimea na mbolea hutumika zaidi katika mashamba ya chai ya Amani na vitalu vya miti (Materu, Mhojiwa).

• Makazi ya binadamu karibu na vyanzo vya maji: hii husababisha uharibifu wa ardhi na ukusanyikaji wa mabaki kuongezeka katika maji, uchafuzi wa maji kwa upenyaji wa kinyesi kutoka vyooni au utupaji wa kinyesi moja kwa moja, na pia kiasili na kikemikali kwa utupaji wa taka ngumu katika maji.

Page 94: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

• Magugu ya majini: spishi kadhaa za magugu ya majini hupatikana katika Mto Zigi na Bwawa la Mabayani, kwa mfano magugumaji “water hycinth” (Eichhornia crassipes), makabichi ya Nile (Pistia stratiotes) na water ivy, (Lpomoea aquatica). Magugumaji yana uwezo wa kufunika uso wa maji kiasi cha kuathiri ubora wa maji. Hali hii pia inaweza kuathiri afya za binadamu kwa kuboresha hali zinazohitajika kuwezesha vijidudu vya maradhi kuzaliana, ambavyo ni muhimu katika mzunguko wa maisha ya pathojeni mbalimbali za binadamu, kama vile mbu (malaria), na konokono (kichocho).

• Mbinu duni za kilimo: matumizi ya moto kwa kusafisha mashamba, kilimo kwenye miteremko ya milima, ukataji miti na shughuli nyingine za binadamu katika maeneo ya vyanzo vya maji yanaweza kuchafua maji kwa kuongeza tope katika maji, rangi na shehena ya masimbi, hususan wakati wa msimu wa mvua. Sababu hizi zinafikiriwa kusababisha ongezeko la tope katika Bwawa la Mabayani mwezi Desemba, 1999 kutoka kipimo cha NTU 20-30 hadi NTU 1,400 (Materu, Mhojiwa).

• Magonjwa: Ugonjwa wa Usubi hutokea katika Wilaya ya Muheza, Bonde la Mto Zigi. Husababishwa na mnyoo (filaria) anayeitwa Onchocerca volvulus. Kimelea hiki huambukizwa kwa binadamu kwa kuumwa na nzi wadogo weusi. Mbali na upofu, ugonjwa huu pia unasababisha matatizo makubwa ya ngozi. Nzi hawa huzaliana katika maji yanayotiririka kwa kasi yaliyo na oksijeni nyingi. Magonjwa mengine katika Bonde la Mto Zigi yanayohusiana na maji ni kipindupindu, homa ya matumbo na malaria (Maggid, Mhojiwa)

Migogoro iliyopo na Inayoweza Kutokea• Mgogoro unatarajiwa kutokea kati ya watumiaji maji wa Manispaa ya Tanga na mji wa Muheza.

Upatikanaji wa maji kwa mji wa Muheza kwa sasa hautoshelezi mahitaji, na kuna pendekezo la kuchukua maji kutoka mto Zigi ambao ni tegemeo pekee la watu wa Jiji la Tanga kwa sasa.

• Mgogoro kati ya matumizi ya maji majumbani na mahitaji ya mazingira: kiasi cha chini kabisa cha mtiririko wa maji unaotakiwa kuhimili mfumo ikolojia chini ya bwawa la Mabayani hakijulikani.

• Mgogoro kati ya wachafuzi na wasimamizi wa maji: kwa mfano, mgogoro kati ya wasimamizi wa maji na wenye shughuli za kilimo, pale wasimamizi wa maji wanapojaribu kudhibiti uchafuzi wa maji, kwa mfano, uchafuzi utokanao na mchakato wa viwanda vya mashamba ya mkonge (Mjesani, Kibaranga, Lanconi na Bamba), na uchafuzi kutokana na madawa ya kilimo kutoka mashamba ya chai.

Mtandao wa ukusanyaji data

• Kituo cha mto Zigi kilichopo Lancon (Namba IC 1): kituo kikuu, kinafanya kazi, kina safu ya geji 0-10m; kituo kina kiingiza data cha aina ya ‘orpheus’.

• Kituo cha mto Zigi kilichopo Miembeni (Namba IC 2); kituo kidogo, kinafanya kazi na kina safu ya geji 0-4m; “rating curve” inahitaji kuboreshwa.

• Kituo cha mto Zigi kilichopo Kisiwani (IC 4); kituo kidogo chenye safu ya geji 0-3m. Kipo maalum kwa matumizi ya misitu ya Bonde la Mto Zigi. “rating curve” inahitaji kuboreshwa. Geji ya 0-1m imechukuliwa na mafuriko.

• Kituo cha mto Muzi kilichopo Msakazi (ICA 1): kinafanya kazi, lakini “rating curve” inahitaji kuboreshwa

.• Kutuo cha mvua cha Zigi-Lancon: kinafanya kazi.

• Vituo vya usawa wa maji na mvua vya Bwawa la Mabayani: vinafanya kazi.

• Vituo vya mvua vya ziada katika bonde vinavyoendeshwa na taasisi mbalimbali, kama vile Msitu wa Longuza, Msitu wa eneo la vyanzo vya mito, Usambara Mashariki (EUCF) n.k.

81

Page 95: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

H.5 Bonde la Mto Mkulumuzi (na mito ya Pwani )Mito ya pwani huanzia katika genge linaloenda sambamba na pwani kwa umbali wa kilomita 20-30. Wastani wa mvua katika eneo hili la chanzo cha mto ni milimita 1,100. Ikolojia inalingana kwa kiasi. Miteremko ya awali ni vilima kwa ujumla, na polepole inakuwa tambarare kadiri inavyoingia uwanda wa pwani. Minazi, michikichi na mikorosho inatawala uoto. Mkonge pia hustawishwa katika mashamba makubwa. Matatizo ya mmomonyoko wa udongo hayajaonekana katika maeneo haya..

Mito mingi ya pwani hutiririka kwa vipindi vifupi tu katika msimu wa mvua na huwa mikavu kwa kipindi kinachobaki cha mwaka. Mto pekee wa kudumu ni Mkulumuzi. Eneo la chanzo cha mto huu ni kilomita za mraba 337, ambalo lipo upande wa Kusini la eneo la chanzo cha Mto Zigi. Chanzo chake kipo katika Msitu wa Magoroto.

MaliasiliMajiMto Mkulumuzi ni chanzo cha maji cha mji wa Muheza, wenye idadi ya watu wapatao 25,700.

KilimoKilimo katika eneo hili kwa kiwango kikubwa ni cha kujikimu, isipokuwa mkonge, ambao hulimwa katika viwango vya kibiashara. Mazao ya kujikimu yalimwayo ni pamoja na mahindi, ndizi, mihogo, mpunga, na viazi vitamu. Matunda (hususan machungwa), nazi, korosho na viungo hulimwa kama mazao ya biashara.

Mifugo Ufugaji katika maeneo haya si mkubwa sana. Idadi ndogo ya ngo’mbe wa maziwa, mbuzi na nguruwe hufugwa.

UvuviIngawa uvuvi ni shughuli inayofanywa na watu wengi katika pwani, hakuna shughuli kubwa ya uvuvi inayofanyika katika maeneo ya vyanzo vya mito ya pwani.

Migogoro muhimu iliyopo• Makazi: Mahitaji makubwa ya ardhi ya makazi yametokea baada ya mashamba ya Mkonge kufa,

na wafanyakazi kufukuzwa.• Maji yasiyotosheleza kwa mji wa Muheza.

Mtandao wa ukusanyaji data• Kituo cha mto Mkulumuzi kilichoko Upare (hakijasajiliwa): kituo kipya cha upimaji maji mtoni,

kilicho na kiingiza data cha aina ya ‘Thalimedes’• Kituo cha mto Msimbazi kilichopo Lugongo: kituo kipya cha upimaji maji mtoni chenye safu

ya geji 0-2m.• Kituo cha hali ya hewa cha Mlingano (chini ya wizara ya Kilimo na Chakula): kinafanya kazi.

Mashirika yanayofadhili • Irish Aid: hufadhili programu shirikishi zilizopangwa katika eneo hili• TASAF-Mfuko wa hifadhi ya jamii• NORAD: hufadhili Programu ya Usafiri na Usafirishaji Vijijini (VTTP)• IUCN: inajishughulisha na Hifadhi ya Mazingira ya Pwani, kwa ushirikiano na Ireland Aid• AXIOS International: husaidia yatima na watoto walio katika mazingira magumu• GTZ: husaidia miundombinu ya afya, ufadhili wa ugawaji wa madawa ya msingi kwa vituo vya afya• APOC/CDTI: Udhibiti wa ugonjwa wa Usubi

82

Page 96: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

83

Mch

oro

Na

4: U

taw

ala

wa

Bon

de la

Pan

gani

Ang

alia

pia

pic

ha y

a 2,

uku

rasa

wa

34(R

ejea

; Mra

di w

a U

sim

amiz

i wa

Mat

umiz

i Bor

a ya

Maj

i)

Page 97: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia
Page 98: Bonde la Pangani · 2013. 9. 12. · D.2 Usimamizi wa Serikali, Sheria na Sera ... Jedwali la 3: Makadirio ya mahitaji ya maji kwa mwaka 1995 na matarajio ya ... kuanzisha na kutumia

IUCN Water and Nature Initiative Rue Mauverney 28CH-1196 GlandSwitzerlandTel + 41 22 999 0001Faxl + 41 22 999 0002E-mail: [email protected]

GWI Running Dry ProgramCARE International in EthiopiaP.O.Box 4710; Addis Ababa, EthiopiaPhone: +251-11-618 3294 Ext 160Fax: +251-11-618 3295Web: http://www.care.org.et

Pangani Basin Water Board P.O. Box 5978Hale Tanga TanzaniaTel ++ 255 27 2640836Fax ++ 255 27 2641031E-mail: [email protected]

IUCN Eastern and Southern Africa Regional OfficeP.O. Box 68200-00200Nairobi KenyaT: +254 20 890605-12; W:+254 20 249 3561/65/70M: +254 724 256 804 or + 254 734 768 770F:+254 20 890615 E-mail: [email protected]

Coastal Development Authority (CDA)P.O. Box 1322Mombasa KenyaTel + 254 41 22440E-mail: [email protected]

IUCN – Shirika la Kimataifa la Hifadhi ya UasiliLikiwa limeanzishwa mwaka 1948, Shirika la Kimataifa la Hifadhi ya Uasili linakutanisha pamoja nchi, mawakala wa nchi na mashirika mbalimbali yasiyo ya serikali katika ubia wa pekee duniani: zaidi ya wanachama wake 1000, wameenea katika nchi zaidi ya 160.

Kama shirika, IUCN inalenga kushawishi, kutia moyo na kusaidia jamii ulimwenguni kuhifadhi hadhi na anuwai ya uasili na kuhakikisha kwamba matumizi yoyote ya maliasili yanafanywa kwa stahili na yanakuwa endelevu kiikolojia.

Shirika la Kimataifa la Hifadhi ya Uasili linategemea nguvu ya wanachama wake, mitandao na ubia katika kuendeleza uwezo wao na kusaidia muungano wa kilimwengu wa kulinda maliasili katika ngazi ya kitaifa, kikanda na kiulimwengu.

Programu ya Maji na Uasili ya IUCN (WANI)Programu ya Maji na Uasili ya IUCN (WANI) ni mpango wa utekelezaji wa miaka 5 wa kuonesha kwamba usimamizi wenye misingi ya mifumo ya ikolojia na ushirikshwaji wa wadau utasaidia katika kukabiliana na changamoto zihusuzo maji kwa sasa – kuhuisha mito na kuidumisha rasilimali hii kwa manufaa ya wengi.

Ofisi ya Bonde la Pangani (PBWO)Marekebisho ya sheria ya matumizi ya maji (Na. 10 ya 1981) ya Tanzania yalianzisha utaratibu wa Usimamizi na Ugawaji wa maji kufuata mipaka ya kihaidrolojia. Kutokana na hiyo Ofisi ya Maji Bonde la Pangani ilianzishwa mwaka 1991. Majukumu yake makuu ni kudhibiti na kusimamia matumizi ya maji, kwa kuzingatia ubora na wingi wake katika Bonde la Pangani.

Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani (CDA)Mamlaka ya Maendeleo ya Pwani ni Mamlaka ya Maendeleo ya Kanda iliyoanzishwa kufanikisha mipango shirikishi ya maendeleo, uwezeshaji, uanzishwaji, uratibu na utekelezaji wa miradi na programu ndani ya eneo la mamlaka, ambalo ni Jimbo la Pwani lote na Wilaya ya Ijara na Ukanda Maalumu wa Uchumi wa Kenya (EEZ).

Mpango wa Maji wa Dunia (Global Water Initiative)Mpango wa Maji wa Dunia unaofadhiliwa na mfuko wa Howard G. Buffet ulianzishwa Septemba 2006 kwa lengo la kuhakikisha jamii zilizopo katika mazingira hatarishi duniani zinapata huduma ya maji safi na salama bila kuathiri hadhi, haki, utamaduni na mazingira yao ya asili. Malengo mkakati ya mpango huu ni kusaidia usimamizi wa pamoja wa rasilimali maji katika nchi zilizoainishwa, kuanzisha na kuendeleza umoja wa watumia maji katika maeneo yao, na pia kueneza ushawishi hata nje ya mipaka ya eneo la mpango huu ili kufikia wigo mpana zaidi. Mpango unalenga katika kuanzisha ubia baina ya asasi mahsusi katika kanda tatu za kijiografia duniani kama ifuatavyo: Afrika Mashariki (Ethiopia, Kenya, Tanzania na Uganda), Afrika Magharibi (Burkina Faso, Ghana, Mali, Niger na Senegal) na Amerika ya Kati (El Salvador, Guatemala, Honduras na Nicaragua). Asasi zinazohusika katika mpango huu kwa sasa ni “Action against Hunger (AAH), CARE, Catholic Relief Services (CRS), International Institute of Environment and Development (IIED), International Union of Conservation of Nature (IUCN), Oxfam America na SOS Sahel”

Katika kanda ya Afrika ya Mashariki, mpango huu unajulikana kama mkakati wa kukabiliana na ukame (GWI Running Dry) na unaratibiwa na ofisi ya kanda yenye makao yake Addis Ababa, Ethiopia (chini ya kivuli cha CARE International, Ethiopia).

Coast Development Authority