mafanikio ya idara katika serikali ya awamu ya tano … · 2020. 3. 8. · mafanikio ya idara...

100
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII IDARA YA MAMBO YA KALE MAFANIKIO YA IDARA KATIKA SERIKALI YA AWAMU YA TANO 2015 - 2019 Aprili 2019 1 2 C C 3 4

Upload: others

Post on 27-Jan-2021

16 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

  • 1

    JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAWIZARA YA MALIASILI NA UTALII

    IDARA YA MAMBO YA KALE

    MAFANIKIO YA IDARA KATIKA SERIKALI YA AWAMU YA TANO 2015 - 2019

    Aprili 2019

    1 2

    C C

    3 4

  • 2

  • i

    Picha ya kwenye jalada inaonesha bonde la Olduvai (Olduvai Gorge) ni moja ya bonde ambalo ni maarufu Duniani kwa masalia mbalimbali ya Zamadamu yanayoonesha chimbuko la binadamu. Kutokana na tafiti zilizofanyika katika bonde hili zimegundua zamadamu walioishi miaka 1.75 hadi miaka milioni 2 iliyopita kama ifuatavyo (1 hadi 4 kwenye picha ya jalada): Australopithecus boisei(1) au Zinjanthropus boisie lililogunduliwa na Dkt. Mary Leakey na mumewe Dkt. Louis Leakey mwaka 1959; Homo habilis(2) aligunduliwa Mei 1960 Olduvai na Jonathan leakey mtoto wake leakey, ambaye inasadikika kuwa alitengeneza zana za Mawe Olduvai ziitwazo “Oldowan”; Homo erectus(3) aligunduliwa Olduvai Disemba 1960 na Dkt. Mary Leakey. Vilevile Dkt. Mary Leakey ndiye aliyegundua Homo sapiens (4) Olduvai. Aidha katika bonde hilo ziligunduliwa zana za mawe kama zinavyoonekana kwenye picha (c).

    Haki zote za kunakili zimehifadhiwa© 2019 Wizara ya Maliasili na Utalii

    ISBN 978-9976-93594-9Kimechapishwa na IPRINT LIMITED

  • ii

  • iii

    YALIYOMODIBAJI ................................................................................................................................. v

    MUHTASARI .................................................................................................................... vii

    SHUKRANI ......................................................................................................................viiiSURA YA KWANZA1.0 Uhifadhi wa Malikale Tanzania Bara .......................................................................... 11.1 Utangulizi .................................................................................................................... 11.2 Historia ya Idara Mambo ya Kale ............................................................................... 11.3 Sera, Sheria na Miongozo inayotumika kwenye Uhifadhi wa Malikale ..................... 21.4 Aina, Ubora na Umuhimu wa Malikale, Tanzania ...................................................... 3

    SURA YA PILI2.0 Majukumu, Muundo na Watumishi ............................................................................ 82.1 Utangulizi .................................................................................................................... 8 2.2 Majukumu ya Idara ...................................................................................................... 82.3 Muundo wa Idara ya Mambo ya Kale ......................................................................... 8 2.4 Watumishi wa Idara ya Mambo ya Kale na Viongozi ............................................... 11

    SURA YA TATU3.0 Ushiriki wa Serikali na Sekta Binafsi katika Uhifadhi wa Malikale ......................... 143.1 Utangulizi .................................................................................................................. 14 3.2 Umuhimu wa ushirikano wa Serikali na Binafsi katika Uhifadhi wa Malikale ........ 14 3.3 Ushiriki wa Taasisi za serikali. .................................................................................. 143.4 Ushiriki wa Taasisi binafsi ......................................................................................... 19

    SURA YA NNE4.0 Mafanikio ya Idara katika Serikali ya Awamu ya Tano ............................................. 214.1 Utangulizi .................................................................................................................. 21 4.2 Uhifadhi na Uendelezaji wa Malikale ....................................................................... 214.3 Makumbusho Mpya katika Kituo cha Bonde la Olduvai .......................................... 214.4 Uendelezaji wa Kituo cha Kimondo cha Mbozi, Mkoa wa Songwe ......................... 234.5 Mfumo wa Kukusanya Maduhuli .............................................................................. 294.6 Uendelezaji wa Vituo vya Mambo ya Kale Mkoa wa Iringa ..................................... 29

    4.7 Ukarabati wa BOMA la Iringa .................................................................................. 294.8 Uhifadhi na uendelezaji wa Makumbusho ya Chifu Mkwawa Kalenga ................... 334.9 Mapango ya Amboni .................................................................................................. 39

  • iv

    4.10 Uhifadhi wa Mji Mkongwe wa Mikindani Mtwara ................................................... 414.11 Uhifadhi wa Michoro ya Miambani, Tanzania .......................................................... 474.12 Mafanikio ya Idara kwa Upande wa Taasisi Binafsi .................................................49 SURA YA TANO5.0 Kuendeleza Vituo vya Mambo ya Kale na Makumbusho ........................................525.1 Utangulizi ..................................................................................................................525.2 Kuendeleza vituo vya Mambo ya Kale kwa kutumia Taasisi ....................................535.3 Taarifa ya Awamu ya Pili ya utekelezaji wa Maagizo ...............................................545.4 Kuendeleza Kituo cha kumbukizi ya Mwalim Nyerere Magomeni. .........................585.5 Idara ya Mambo ya Kale kuhamisha majukumu kwenda Makumbusho ya Taifa. ....61 SURA YA SITA6.0 Utangazaji na Uhamasishaji wa Vivutio vya Malikale ..............................................666.1 Utangulizi .................................................................................................................. 66 6.2 Historia ya Utangazaji na uhamasishaji .....................................................................666.3 Ushiriki wa Idara katika utangazaji na uhamasishaji ................................................666.4 Maboresho kwenye Makumbusho za vituo vya Mambo ya Kale na Makumbusho ..676.5 Maonyesho ambayo Idara ilishiriki 2018/2019. ........................................................686.6 Tamasha la Urithi ......................................................................................................696.7 Kilele cha Tamasha lilifanyika Arusha ......................................................................706.8 Maadhimisho ya Kumbukizi ya Vita vya Majimaji ..................................................71 SURA YA SABA7.0 Mikataba ya Kitaifa na Kimataifa na kutoa ushauri wa kitaalam ..............................797.1 Utangulizi .................................................................................................................. 79 7.2 Umuhimu wa Mikataba ya Kimataifa ........................................................................797.3 Kufanya tathmini ya Majengo ya kihistoria yenye asili ya Kijerumani ...................807.4 MradiwaKuhifadhiMagofuyaKisiwachaMafiaMkoawaPwani ........................80 7.5 Mkataba kati ya Idara ya Mambo ya Kale na NCAA ...............................................80 SURA YA NANE8.0 Maoni, Ushauri na Hitimisho .......................................................................................818.1 Maoni au ushauri kuhusu Malikale ............................................................................818.2 Hitimisho ..................................................................................................................82Kiambatisho Na. 1: Orodha ya Vituo vya Mambo ya Kale: .............................................83Kiambatisho Na. 2 Faharasa .............................................................................................86

  • v

    DIBAJI Malikale ni urithi wa matokeo ya maisha ya binadamu katika harakati za kukabiliana na mazingira anayoishi wakati wa kutekeleza shughuli za kila siku. Katika kumudu maisha ya kila siku binadamu au kiumbe chochote lazima awe mbunifu wa teknolojia mbalimbali zitakazomwezesha kutengeneza vitu au rasilimali zitakazomwezesha kuishi na wale wanaoshindwa hutoweka. Malikale hizi zinazotengenezwa na jamii husika baada ya kuonekana ni muhimu huzitunza na kuzihifadhi na hatimaye hurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine miaka hadi miaka. Urithishanaji huu wa malikale unakuwa ni sehemu ya utamaduni wao na huheshimiwa na jamii husika. Hivyo, Jamii huweka taratibu, kanuni na sheria za kuwezesha raslimali hizo kulindwa, kuhifadhiwa na hurithishwa kwa utaratibu maalum. Vilevile Malikale hujumuisha masalia ya binadamu, wanyama na mimea ambayo kutokananatafitimbalimbalizimeonyeshanakudhihirishahistoriayamabadilikoyaviumbehivi kimaumbile, kifikra, kiteknolojia na kisayansi. Malikale pia hujumuisha mazingiraaliyoishi au yaliyotumika na binadamu, wanyama na mimea.

    Malikale kwa ujumla ni urithi wa utamaduni unaonyesha binadamu alivyokuwa anaishi na hujumuishamahalinamazingiraaliyoishi,vitualivyotumia,sanaa, teknolojia,fikra,milana desturi kwa miaka kadhaa(ICOMOS 2002). Urithi huu huhifadhiwa kitaifa katika nchi mbalimbali na huweka utaratibu wa kuzihifadhi kiserikali au kwa kutumia sekta binafsi kwa ajili ya kumbukumbu ya kizazi kilichopo na kijacho. Pia, kwa baadhi ya nchi Malikale huendelezwa vizuri bila kuathiri uhalisia na kutumika kwa elimu na utalii ambao huchangia katika pato la Taifa. Malikale zenye sifa za kimataifa huhifadhiwa kama Urithi wa Dunia.

    Malikale katika Tanzania, kwa mujibu wa Sera ya Malikale ya mwaka 2008, hujumuisha rasilimali za urithi wa utamaduni zinazoshikika na zisizoshikika; zinazohamishika, na zisizohamishika, zilizo nchi kavu na majini ambazo zinadhihirisha mabadiliko ya kimaumbile, kifikra,zana,vyombonamazingiraaliyoishinakutumiabinadamunazenyeumriwamiakamiamoja(100).Malikalehizizinajumuishazanazamawenachuma,vyombovyausafiri,metali, miti na mifupa; visukuku vya binadamu, mimea na wanyama; michoro ya miambani; miji ya kihistoria, magofu ya majenzi. Rasilimali nyingine ni maeneo ya matambiko au ibada kama vile mapango, misitu, miti, mito, milima na mandhari iliyoteuliwa na jamii kwa madhumuni ya ibada; na kumbukumbu za matukio muhimu ya kihistoria, yakiwemo ya viongozi na mashujaa. Pia, Sheria ya Mambo ya Kale sura 333 ya mwaka 2002 sehemu ya pili kifungu cha tatu (3) Waziri mwenye dhamana ya Idara ya Mambo ya Kale anaruhusiwa kulitangaza eneo kuhifadhiwa chini ya Mambo ya Kale kutokana na sifa au umuhimu wake hatakamahaijafikishamiaka100.

    Tafitizamalikalezilizofanyikahapanchinizilianzamwaka1909hadileonazimechangiasehemu kubwa katika chimbuko la wanyama mbalimbali na binadamu kuanzia maisha au mazingira aliyokuwa anaishi, vyakula alivyokuwa anakula, majenzi au majengo aliyojenga, zananavyomboalivyokuwaakitumia.MatokeoyaTafitihizoyamewezeshaTanzaniakuwamiongoni mwa nchi ambazo zina utajiri mkubwa wa Malikale ambao baadhi kwa umaarufu wakeumewezakuitambulishanchiyetundaninanjeyanchi.Mfanoutafitiwamasaliayamijusi mikubwa (dinosaria) yalichimbuliwa kutoka Tendaguru Lindi kuanzia mwaka 1909 hadi1913yenyemiakamillioni150iliyopita.UtafitihuuulifanyikabaadayaMjerumani

  • vi

    mhandisi kugundua Masalia ya Mjusi Mkubwa mwaka 1906, huko Tendaguru Mkoani Lindi. Masalia hayo yalipelekea Makumbusho ya “Natural History” ya Ujermani kuja kufanyautafitizaidimwaka1909hadi1913(Heinrich,W.,etall;2011).

    Watafitiwengine kamaLouis Leakey naMary Leakeywataalamuwa akiolojiawalipataumaarufu kutokana na uvumbuzi wa masalia ya binadamu wa kale ambayo ni vielelezo vya Chimbuko la binadamu katika bonde la Olduvai yanayoonyesha kugunduliwa kwa zamadamu wanne: Australopithecus boisei au Zinjanthropus boisie lililogunduliwa na Dkt. Mary Leakey na mumewe Dkt. Louis Leakey mwaka 1959, Homo Habilis aligunduliwa Mei 1960 Olduvai na Jonathan leakey mtoto wake leakey, ambaye inasadikika kuwa alitengeneza zana za Mawe Olduvai ziitwazo “Oldwan”, Homo erectus aligunduliwa Olduvai Desemba 1960 na Dkt. Mary Leakey na Homo sapiens sapiens.Aidha,Utafiti uliofanyikaLaetolimwaka 1978 uligundua nyayo za zamadamu wengine wa spishi ya “Australopithecus afarensis”, pamoja na za wanyama na ndege mbalimbali walioishi miaka milioni 3.6 iliyopita, zilizogunduliwa na Dkt.Mary Leakey mwaka 1976 katika Bonde la Oldupai na Laetoli, Arusha.

    Aidha,Tanzaniakumefanyikatafitinyingizamichoroyamiambaniambazozimeonyeshauwezo wa binadamu kufikiri na kutunza kumbu kumbu kwa kutumiamichoro kabla yaugunduzi wa maandishi hadi sasa tunatumia Komputa. Michoro ya miambani Tanzania imegunduliwa Kondoa, Dodoma; Iramba, Singida; Iringa, Kagera, Arusha na Manyara. Hii ilikuwa njia ya kutunza kumbukumbu na mawasiliano. Wataalam wengine wa Mambo ya Kale wamefanyautafitikwenyezanazilizotumikazamanikuanziazanazaMawekamaOlduwanza Olduvai, Achelean huko Isimila na ufuaji na utengenezaji wa zana za Chuma uliofanyika katika mikoa mingi hapa Tanzania mfano Rukwa, Katavi, Kagera, Songwe na ukanda wa nyanda za juu kusini. Majengo ya kihistoria ni miongoni mwa maeneo yaliyofanyiwa utafitina ikagundulikakunamagofuyamajumbayakalenamakaburiyaliyojengwakwamatumbawe kuanzia karne ya nane na tisa hadi kumi na mbili katika sehemu kadhaa za pwani, kama vile Mkoa wa Tanga; Mkoa wa Pwani; Mkoa wa Dar es salaam; Mkoa wa Lindi na Mtwara. Maeneo mengine ni Kimondo, kilichopo kijiji cha Ndolezi, Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe; visukuku vya kilimo cha umwagiliaji cha miaka zaidi ya mia tatu iliyopita vilivyopo Engaruka, Wilaya ya Monduli, Mkoa wa Arusha, na mengineyo mengi.

    Tafiti hizi zaMalikale zilizofanyikakatikaNchi yaTanzania zimekuwanaumuhimuwakipekee duniani kutokana na mchango wake mkubwa katika sekta za kisayansi, kielimu, kiutamaduni na kiuchumi. Mchango wa malikale ni pamoja na: kutambulisha jamii; burudani; vituo vya elimu; vivutio vya utalii; vielelezo vya mabadiliko ya kihistoria, mazingira na chimbuko, maendeleo na uwezo wa binadamu hadi leo. Uhifadhi wa raslimali za malikale pia hujumuisha uhifadhi wa historia ya nchi yetu wakiwemo viongozi mbalimbali kuanzia machifu hadi Maraisi. Tanzania ni moja ya nchi za Afrika iliyokuwa na viongozi wenye sifa za kitaifa na kimataifa kwa umaahiri wao wa kupigania haki za binadamu kuanzia Machifu hadi Maraisi.

    Uhifadhi wa raslimali hizi za Malikale hauna budi kutekelezwa na kila mtu kwa sababu unamgusa kila mmoja kwa njia moja au nyingine na ni kumbukumbu kwa kizazi kijacho na Malikale hizi zikitumiwa ipasavyo zinaweza kuchangia pato la Taifa.

  • vii

    MUHTASARITaarifa hii inaelezea kazi zilizotekelezwa na Idara ya Mambo ya Kale kuanzia 2015 hadi 2019 katika serikali ya awamu ya Tano. Katika kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya Tano chakufikiauchumiwakati2025kumekuwanamabadilikomakubwayakuimarishaIdaraya Mambo ya Kale na Makumbusho ya Taifa katika mfumo wa muundo na utendaji. Lengo ni kuhahakikisha maeneo ya Mambo ya Kale yanaboreshwa na kutumika kama zao jipya la utalii ili kuongeza muda wa Watalii kukaa nchini, na kuchangia katika pato la Taifa na kuimarisha uhifadhi wa kumbukumbu hizi za Urithi wa Utamaduni. Katika mabadiliko hayo, Idara ya Mambo ya Kale imebaki na jukumu la kusimamia sera na sheria na kukabidhi baadhi ya majukumu ya kiutendaji au kiuendeshaji na uendelezaji Malikale kwa Shirika la Makumbusho. Vile vile Wizara iliangalia namna ya kuendeleza vituo vya Mambo ya Kale vilivyo chini ya Wizara bila kuathiri uhalisia na historia yake kwa kutumia Taasisi za Wizara kama Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii alivyoeleza katika kikao cha Bunge la Mei 2018 wakati anawasilisha hotuba ya bajeti ya Wizara ya mwaka 2018/2019.

    Sura ya Tano katika taarifa hii inaelezea hatua zote zilizochukuliwa kimaandishi za kukabidhi vituo vilivyo chini ya Wizara kwa Taasisi zilizo chini ya Wizara. Taasisi zilizokabidhiwa vituo hivyo tayari zimeshaanza kufanya tathimini ya namna ya kuvihifadhi mfano Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) waliunda kikundi kazi walitembelea vituo vya Kimondo cha Mbozi, Songwe; Engaruka, Michoro ya Miambani Mumba na Engarasero ambayo ipo Mkoa wa Arusha na Mapango ya Amboni Tanga. Shirika la Hifadhi ya Taifa Tanzania (TANAPA) ilitembelea kituo cha kumbukizi ya Mwalimu Nyerere Magomeni, Dar es Salaaam; kituo cha Caravan Serai, Bagamoyo na vituo vya Isimila na Kalenga Mkoani Iringa.

    Katika sura ya nne imeelezea mafanikio ya Idara katika kipindi hiki cha serikali awamu ya tano. Sura hii imeonyesha kazi zilizotekelezwa katika vituo vya Olduvai, Arusha; Kimondo cha Mbozi, Songwe; Mapango ya Amboni, Tanga; Makumbusho ya Nyumba ya Mwlimu Nyerere Magomeni, Dar es Salaam; Michoro ya Miambani Kolo, Kondoa; Makumbusho ya Mtwa Mkwawa Kalenga na Magofu ya Kunduchi, Dar es Salaam. Aidha, sura hii inalezea uanzishwaji wa Makumbusho Mpya ikiwemo Makumbusho ya Nyumba ya Rashidi Mfaume Kawawa.

    Taarifa hii pia imeonyesha historia ya Idara na majukumu yake, inafanya nini na imefanya nini. Katika sura ya kwanza hadi tatu imeonyesha Idara ilikoanzia, Sera, Sheria, Kanuni na miongozo iliyopo na inayotumika katika kusimamia, kutekeleza na kuongoza katika utendaji wakazi za kila siku zaUtafiti, uhifadhi na uendelezajiwaMalikale;Muundowa Idara;watumishi katika Idara ya Mambo ya Kale; aina za Malikale. Lengo ni kumwezesha mdau atakayesoma taarifa aelewe Idara ilikotoka, mahali ilipo, inakokwenda na majukumu yake.

    Mwisho taarifa hii inaonyesha Idara ilivyoshiriki katika utangazaji wa Malikale ndani na nje ya Nchi kwa kutumia machapisho, maonyesho au tamasha na vipindi vya television na ilivyoshirikisha jamii na wadau mbalimbali katika uhifadhi wa Malikale katika Serikali hii ya Awamu ya Tano kuanzia mwaka 2015 - 2019.

  • viii

    SHUKRANI Awali ya yote Idara inampongeza Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa uongozi maahiri wenye maamuzi mahususi yanayokusudia kuboresha uchumi wa Taifakufikiauchumiwakati2025katikaSerikaliyaawamuyaTano.Ameletamabadilikomakubwa katika Taifa hili yanayoonekana ukianzia kwenye miundo mbinu ya barabara, reli, viwanja vya ndege, maji na umeme. Amefufua Shirika la ndege la Tanzania kwa kununua ndege mpya na ameimarisha utendaji wa watumishi katika serikali na mengineyo mengi.

    Shukrani za pekee ziende kwa Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla (Mb) kwa kutoa kipaumbele katika uhifadhi na uendelezaji wa Malikale. Lengo ni kuhahakikisha maeneo ya Mambo ya Kale yanaboreshwa na kutumika kama zao jipya la utalii ili kuongeza muda wa Watalii kukaa nchini. Vilevile Shukrani za pekee ziende kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii 2017 hadi 2018 Mheshimiwa Japhet Hasunga (Mb) na Mheshimiwa Constantine Kanyasu (Mb) ambaye kwa sasa ndiye Naibu Waziri wa Maliasili kwa kazi nzuri ya walizofanya kwa Idara ya Mambo ya Kale.

    Shukrani za dhati ni kwa Katibu Mkuu Mstaafu “Major General” Gaudence Millanzi; Katibu Mkuu wa Sasa Prof. Adolf F. Mkenda, Naibu Katibu Mkuu Dkt. Aloice Nzuki na viongozi wengine wa Wizara kwa umaahiri wao katika kusimamia maagizo ya Mh. Waziri ya kuendeleza Mambo ya Kale na Makumbusho ya Taifa. Katibu Mkuu Mstaafu atakumbukwa kwa kutatua changamoto za kipindi kirefu kwa Idara ya Mambo ya Kale; Mfano, Kituo cha Chifu Mkwawa Kalenga mgogoro ulianza 2014 hadi 2018 mwezi wa Tano Wizara ikiongozwa na Katibu Mkuu Maj. Gen. Gaudence S. Milanzi na Mkoa ukiongozwa na Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Richard Kasesela na familia ya Mkwawa iliongozwa na Bw. Edmond Mkwawa. Maamuzi ya Kikao; Hiki ni kituo cha serikali na taratibu na sheria zizingatiwe.

    Nawapongeza Watumishi wa Idara ya Mambo ya Kale na Makumbusho ya Taifa kwa utendaji, ushirikiano na utulivu walionyesha katika Mabadiliko yaliyokuwa yanafanyika na uelewa mkubwa wa kukubali mabadiliko hayo. Tuendelee kufanya kazi kwa bidii ili mabadiliko haya yalete mchango chanya katika uhifadhi na uendelezaji wa Malikale ambayo yatatumika kwaelimu,kumbukumbu,utafitinakuchangiapatolaTaifakiutalii.

    Shukurani nyingi kwa Uongozi wa Idara Wakurugenzi Wasaidizi Dkt. Fabian Kigadye, Bwana Tibaijuka Anthony na Bwana Anacleth Mwijage; Wakuu wa Vituo Kwa niaba ya Watumishi wote vituoni, ambao ni Bw, John Paresso, Bi Reinfrida Kapela, Bi. Siyawezi Hungo, Bw. Paul Ndahani, Bw. Mbaruku Salehe, Bw. Paul Nyelo, Bw. Jumanne Maburi, Bw. Jordan Erick, Bi. Mariam Mgusi, Bw. Ally Mbarouk, Bi. Neema Mbwana, Bw. Zuberi Mabie, Bw. , Bi. Nengai Nairouwa, Bw. Kelvin Ngowi, Bi Mercy Mbogerah, Bw. M. Ngoma.MaafisawengineniDktBwasiriEmmanuel,Dkt.ChristowajaNtandu,Bw.WilliamMwita, Bw. Revacutus Bugumba, Bi Sikujua Ramadhani, Bw. Christognus Ngivingivi, Bi Frida Msongo, Bi Prisca Kirway, Bi Mwantum Haidari na Bi leila Mohamed. Asante kwa Bi Florida Munisi, Bi Zuena Mohamedi, Bi Labi Masalu kwa ushirikiano wanu wa karibu naShukranikwamadereva,maafisautumishi,masjala,Wahasibunawatumishiwotekwaushirikiano wenu kwa kipindi chote cha Uongozi wangu

    Digna Faustin Tillya Kaimu Mkurugenzi Mambo ya Kale

  • 1

    SURA YA KWANZAUHIFADHI WA MALIKALE TANZANIA BARA

    1.1 Utangulizi

    Sura hii inaelezea dhamana ya Idara ya Mambo ya Kale, historia ya Idara hii, Sera na Sheria zinazotumika katika kuteleza majukumu ya Idara ya Mambo ya Kale, Aina, Ubora na Umuhimu wa Malikale.

    1.2 Historia ya Idara ya Mambo ya Kale

    Idara yaMambo ya Kale ina dhamna ya kusimamia utafiti, uhifadhi na uendelezaji warasilimali za Malikale zilizopo nchini kwa manufaa ya kizazi kilichopo na kijacho. Malikale ni rasilimali za urithi wa utamaduni zilizotengenezwa, zilizojengwa, zilizoundwa au zenye kuhusiana au kutumiwa na binadamu wakati wa maisha yake. Rasilimali hizi historia, ujuzi, mila na desturi za mababu au kizazi kilichopita. Rasilimali nyingi hurithishwa kutoka kizazi kimoja kwenda kizazi kijacho. Kwa mujibu wa será ya Malikale ya mwaka 2008, Malikale hujumuisha rasilimali zinazoshikika, zinazohamishika na zisizohamishika na zinazopatikana juu na chini ya ardhi ambazo zinadhihirishamabadiliko ya kimaumbile, kifikra, zana namazingira aliyoishi na kutumia binadamu. Aidha, kuna Malikale ambazo kutokana na sifa au umuhimu wake kwa jamii husika na Taifa hata kama zina umri mdogo kuliko huo ulioainishwa na Sera na Sheria ya Mambo ya Kale, kulingana na sheria ya Malikale (Sura 333 ya Mwaka 2002) Waziri mwenye dhamana ana Mamlaka ya kuzitangaza kuwa Urithi wa Taifa (National Heritage).

    Uhifadhi wa Malikale ulianzia wakati wa Ukoloni mwaka 1937 ilipoanzishwa Sheria ya Uhifadhi wa Majengo ya Kihistoria (The Monument Preservation Ordinance, 1937). Wakati huoSerikali yaKikoloni kupitia ofisi zaWakuuwaWilaya ilijihusisha katika kutafutana kuorodhesha kumbukumbu za kihistkoria hasa zilizohusiana na ukoloni katika maeneo ya mwambao. Mwaka 1956 Mambo ya Kale ilianzishwa na kuanza kufanya kazi rasmi mwaka 1957. Kitengo cha Mambo ya Kale kilipandishwa hadhi kwa kuanzishwa kwa Idara ya Mambo ya Kale Mwaka 2009 baada ya kuhamishiwa Wizara ya Maliasili na utalii mwaka 1999 kutoka Wizara ya Elimu na Utamaduni.

    Mwaka 1964, ilitungwa Sheria ya Mambo ya Kale Na. 10 ambayo ilifanyiwa marekebisho kwa Sheria Na. 22 ya mwaka 1979. Sheria ya Mambo ya Kale Na. 10 ya mwaka 1964 imeendelea kuwa sheria mama ya uhifadhi wa urithi wa utamaduni mpaka sasa (mwaka 2019) ingawa imefanyiwa maboresho madogo mwaka 2002 Sura 333. Tangu kuanzishwa kwake, Kitengo cha Mambo ya Kale kimekuwa kikihamishwa kutoka wizara moja hadi nyingine. Kitengo hiki kimehamishwa kwa takribani mara kumi na moja (11) mpaka mwaka 1999 kilipohamishiwa Wizara ya Maliasili na Utalii. Katika Wizara nyingine Kitengo kilikaa kwa muda mfupi sana jambo ambalo limeathiri sana kasi ya maendeleo ya uhifadhi wa Malikale. Ifuatayo ni Orodha ya Wizara ambazo Idara imezipitia na vipindi husika:

    1957 – 1962 Wizara ya Elimu;

    1962 – 1964 Wizara ya Utamaduni na Vijana;

    1964–1967OfisiyaRais;

    1967 – 1968 Wizara ya Tawala za Mikoa na Maendeleo ya Vijiji;

    1968 – 1980 Wizara ya Elimu ya Taifa;

    1980 – 1984 Wizara ya Habari na Utamaduni;

  • 2

    1984–1985OfisiyaWaziriMkuu;

    1985 – 1988 Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Utamaduni, Vijana na Michezo;

    1988 – 1990 Wizara ya Utumishi wa Umma, Ustawi wa Jamii;

    1990 – 1999 Wizara ya Elimu na Utamaduni; na,

    1999 – 2019 Wizara ya Maliasili na Utalii

    Kwa kipindi chote cha kuhamahama Kitengo na baadaye Idara ya Mambo ya Kale majukumu yake yalitekelezwa kwa kuzingatia Sheria ya Mambo ya Kale Na. 10 ya mwaka 1964 ambayo ilifanyiwa marekebisho kwa Sheria Na. 22 ya mwaka 1979 na sura 333 ya mwaka 2002. Hivyo maeneo ya Malikale yalibakia na uhalisia wake bila ya kubadilishwa. Baada ya Kitengo hiki kuhamishiwa Wizara ya Maliasili na Utalii maeneo haya yalianza kuendelezwa kiutalii kwa kuzingatia Sera ya Malikale iliyoanzishwa mwaka 2008. Pia, Muundo wa Kitengo cha Mambo ya Kale ulibadilishwa na kuundwa Idara ya Mambo ya Kale mwaka 2009kwalengolakuimarishautekelezajiwamajukumuyautafiti,uhifadhinauendelezajiwa Maeneo ya Malikale bila kuathiri uhalisia.

    Lengo la Sera ya Malikale ya mwaka 2008 ni uhifadhi endelevu wa kuhifadhi na kuendeleza malikale kwa kuhusisha wadau mbalimbali. Sera hii inatoa fursa kwa kila Mtanzania kuwajibika katika suala zima la uhifadhi na uendelezaji wa Malikale. Hivyo, utekelezaji wa Sera ya malikale ya 2008 hauna budi kushirikisha Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali, Sekta Binafsi, Jamii, Jumuiya za Kikanda na Kimataifa na Mawakala wa Serikali na vyombo vingine vya dola.

    Katika kutekeleza uhifadhi wa Malikale, Maeneo yaliyohifadhiwa na Wizara chini ya Idara ya Mambo ya Kale ni 18 ambayo ni Olduvai Gorge na Nyayo za Zamadamu Laetoli Ngorongoro; Magofu ya Kaole, Mji Mkongwe wa Bagamoyo na Makumbusho ya Caravan Serai, Bagamoyo; Michoro ya Miambani Kolo, Kondoa; Makumbusho ya Mtwa Mkwawa Kalenga na Muhula wa Zama za Mawe Isimila, Iringa; Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara, Lindi; Kimondo cha Mbozi, Songwe; Mapango ya Amboni na Magofu ya Tongoni, Tanga; Makumbusho ya Kumbukizi ya Dkt Livingstone Ujiji, Kigoma; Tembe la Dkt. Livingstone Kwihara, Tabora; Makumbusho ya Nyumba ya Mwl. Nyerere Magomeni, Dar es Salaam na Magofu ya Kunduchi, Dar es Salaam; (Kiambatisho Na.1). Maeneo haya yana sifa za kipekee za kitaifa na kimataifa na yanatumika kiutalii na kielimu yana watumishi na huduma nyingine za kiutalii na kiuhifadhi. Maeneo ya Malikale Tanzania ni mengi na kutokananatafitizilizofanyikanizaidiya500,kilaMkoaunamaeneoyaMalikalenamengiyapo kwa watu binafsi au Taasisi binafsi.

    1.3 Sera, Sheria na Miongozo inayotumika kwenye Uhifadhi wa Malikale

    Idara ya Mambo ya Kale katika utendaji wa kila siku inafanya kazi kwa kuzingatia Sheria ya Mambo ya Kale Sura 333 ya mwaka 2002, Sheria ya Makumbusho Na.7 ya mwaka 1980 na Sheria ya Nyaraka za Taifa Na. 3 ya mwaka 2002. Sheria nyingine ni Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 (Kifungu namba 9 (c)), Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 na Sheria ya Ardhi ya Mwaka 1999. Aidha, Idara hutumia Dira ya Taifa ya Maendeleo (2025), Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (5) 2016/2017 – 2020/2021, Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2015-2020, Maelekezo ya Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hotuba yake ya uzinduzi wa Bunge la 11, Mpango Mkakati wa Wizara (2016/17 – 2020/21) katika kuteleza majukumu ya Wizara.

  • 3

    Madaraka makubwa ya kisheria amepewa Waziri mwenye dhamana ya Malikale akifuatiwa na Mkurugenzi wa Mambo ya Kale, Serikali za Mitaa na Halmashauri. Sheria ya Malikale kwa kiasi kikubwa imetokana na Sheria ya kikoloni ya mwaka 1937 “The Monuments Preservation Ordinance” ambapo kwa kipindi hicho kipaumbele kwenye Malikale ilikuwa niuhifadhinautafititu.

    Mwaka 2008 Sera ya Malikale ilianzishwa kwa ajili ya kuboresha uhifadhi uliokuwa sio endelevu kuwa uhifadhi endelevu wa malikale. Lengo la sera hii ni kuongeza uelewa kwa jamii na kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa Malikale na manufaa yake kiuhifadhi, kielimu, kiutalii ili wananchi waweze kutumia malikale hizo kujiongezea kipato. Sera hii hufafanua dhima na malengo ya malikale, kuainisha jinsi shughuli za malikale zitakavyoendeshwa na kusimamiwa,husisitizaumuhimuwakutafitinakuhifadhimalikalepamojanakufafanuajinsi wadau mbalimbali ikiwamo serikali na taasisi zake, sekta binafsi na umma kiujumla watakavyoshirikishwa katika shughuli za uhifadhi wa malikale. kuzitumia kujiamini na kujivunia utaifa wao

    1.4 Aina, Ubora na Umuhimu wa Malikale, Tanzania

    1.4.1 Raslimali za Malikale

    Idara ya Mambo ya Kale ndiyo yenye dhamana ya kutafiti, kuhifadhi na kuendelezaraslimali za malikale Tanzania Bara. Utekelezaji wa majukumu ya Idara ya Mambo ya Kale Tanzania ni kwa mujibu wa sheria ya Mambo ya Kale ya Mwaka 2002 Sura 333, ambapoMalikalebaadayakufanyiwautafitinakuonekanainavigezovyotevinavyostahilihuhifadhiwa kitaalam. Vigezo hivyo ni pamoja na uwepo wa malikale au vitu halisi vyenye historia au taarifa sahihi, vitu vyenye umri wa miaka mia au zaidi. Malikale zinazopatikana kwenyeutafitiniainambili;zinazohamishikanazisizohamishika.Malikalezisizohamishikahujumuisha Mazingira/maeneo aliyokuwa akiishi binadamu wa kale ambayo kupitia tafiti zaMambo yaKale kumepatikana viashiria aumasalia ya binadamuwa kale kamavile mifupa au zana alizokuwa akitumia kwa kuwinda, vitu au vyombo alivyotengeneza kwa ajili ya kupika chakula na kulia, vyakula alivyokuwa akitumia Mizizi, Miti, matunda na Wanyama na kadhalika. Malikale pia hujumuisha nyumba alizokuwa akijenga, nguo alizokuwaakitengeneza,Moton.k.MalikalehizibaadayakufanyikakwatafitizaMamboya Kale kwa kuzingatia sheria na kanuni za Mambo ya Kale huhifadhiwa aidha kwenye eneo lililovumbuliwa au lilikopatikana Malikale hizo au kuhamishiwa Makumbusho au kituo cha taarifakwazileambazozinahamishika.KutokananatafitihizoTanzaniainayohazinakubwayenye maeneo ya Malikale ambayo yapo katika makundi yafuatayo:-

    1) Maeneo yenye masalia ya Paleontolojia na akiolojia, hii inajumuisha masalia ya vitu mfu vya kale vya zaidi ya miaka mia, maelfu hadi milioni iliyopita. Baadhi ya maeneo hayo ni pamoja na Bonde la Olduvai na Laetoli (Arusha), Bonde la Ruhuhu (Ruvuma), Shingo Pana Songwe, Tendaguru (Lindi) na Isimila (Iringa);

    2) Magofu yenye hadhi ya kihistoria ambayo yamefikisha miaka iliyotajwa kwenyesheria na yenye sifa za kipekee. Baadhi ya magofu hayo ni kama yale ya Kaole na Bagamoyo (Pwani); Kilwa Kisiwani na Songo Mnara (Lindi); Magofu ya Tongoni na Pangani, (Tanga); na Magofu ya Kunduchi (Dar es Salaam);

    3) Miji ya kihistoria: Hii ni miji iliyokuwepo zamani inayodhihirisha maendeleo ya mtanzania kabla na baada ya ujio wa wakoloni hadi sasa, kwa mfano mji wa: Bagamoyo (Pwani), Kilwa Kisiwani, Songo Mnara, Sanje kati (Lindi), Pangani (Tanga) na Mikindani (Mtwara);

  • 4

    4) Makazi ya kijadi haya ni mengi yapo katika Mikoa yote na yangestahili kila Mkoa kupewa jukumu la kuweka Kutunza Mfano Kalenga (Iringa) na Bweranyange (Kagera), Ruvuma, Tabora, Mwanza, Kilimanjaro n.k.;

    5) Makazi, Nyumba na Makumbusho za Maasisi wetu Mfano Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere, Hayati Amri Abedi Amani Karume na Hayati Rashidi Mfaume Kawawa;

    6) Maeneo yenye kumbukumbu za harakati za ukombozi wa bara la Afrika kama vile Jengo lilikuwaOfisi yaKamati yaUkomboziwaBara laAfrikaMtaawaGhanaJijini Dar es Salaam; Makambi ya Wapigania uhuru kusini mwa Afrika, ambayo yapo katika Mikoa mingi hapa nchini Mfano Mazimbu na Dakawa Morogoro na Kongwa Dodoma, Iringa, Mbeya, Ruvuma;

    7) Majengo ya kihistoria ya muda mrefu na yenye hadhi ya kipekee yaliyojengwa nyakati mbalimbali. Haya ni majengo yaliyojengwa wakati wa ujio wa Wajerumani, Waingereza na Waarabu katika nchi yetu;

    8) Maeneo yenye matukio au kumbukumbu maalum za kihistoria yaliyoainishwa kisheria, kwa mfano makaburi ya wakoloni, makaburi au masalia ya vita mbalimbali ikiwemo vita ya Kwanza na ya Pili ya Dunia, Minara na kuta zenye kumbukumbu au matukio ya kihistoria kama vita ya Kagera-Songea, vita vya Majimaji mfano Makumbusho ya majimaji Songea, Azimio la Arusha;

    9) Maumbile asilia yenye historia au umaarufu kwa mfano Kimondo cha Mbozi (Mbeya), na Mapango ya Amboni (Tanga) ambayo yanatumika kwa shughuli za mila na desturi;

    10) Michoro ya Miambani yenye kuonyesha mazingira binadamu aliyoishi na wanyama waliokuwepo, Mfano maeneo ya Kolo na SwagaSwaga-Kondoa;

    11) Maeneo yaliyokuwa yanatumiwa na jamii kwa huduma mbalimbali mfano hospitali zenye historia, Shule alizosoma au kufundisha Baba wa Taifa na barabara, mitaa viwanja vyenye kumbukumbu ya kihistoria mfano Kiwanja cha Karimjee mahali paliposhushwa bendera ya Mwingereza na kupandishwa bendera ya Tanzania; na

    12) Makumbusho mbalimbali zinazojumisha Makumbusho za serikali mfano Makumbusho ya Taifa, Makumbusho za binafsi Mikindani Mtwara; Urithi, Tanga na Makumbusho za dini mfano Makumbusho ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani na Bujora Mwanza. Makumbusho hizi hutumika kwa ajili ya kutunza na kuhifadhi wa Malikale zinazohamishika kwa ajili ya utafiti kumbukumbu, maonyesho, machapisho, nakuelimisha umma kuhusu kuendeleza urithi wa utamaduni kwa manufaa ya kizazi kilichopo na kijacho.

    13) Makumbusho au nyumba za Waasisi wa Taifa mfano Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere Butiama (Mara) na Magomeni(Dar es Salaam), Hayati abedi Amani Karume, (Zanzibar) na Hayati Rashid Mfaume Kawawa.

    14) Maeneo au majengo ya kuabudia ya jamii mbalimbali kuanzia dini za mababu zetu hadi dini zilizoingia kutoka nje ya nchi za Kikristu na Kiislam.

  • 5

    1.4.2 Umuhimu/Thamani ya Raslimali za Malikale, Tanzania

    Tanzania na Duniani kote walikuwa wanaenzi na kuhifadhi vitu vya kale vilivyokuwa vimeipatia umuhimu au sifa fulani kutokana na mchango wake katika jamii husika na hurithishwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Malikale hizi zikitumika ipasavyo hutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya wananchi na serikali. Umuhimu na faida ya Malikale katika jamii ni;

    1.4.2.1 Kumbukumbu kwa kizazi kijacho

    Malikale nyingi zimetengenezwa na binadamu, na kwa maana hiyo kuna teknolojia iliyotumika au iliyobuniwa. Kwa hiyo zinapohifadhiwa husaidia kuthibitisha na kuonesha chimbuko la teknolojia na ustaarabu wa binadamu. Kizazi kinachokuja hupata historia ya kizazi kilichopita kwa kupitia Malikale zilizohifadhiwa vizuri na kujua maisha waliyokuwa wanaishi mababu na mababu. Uhifadhi wa kumbukumbu hizi ni muhimu na hurithishwa kwa kizazi kinachofuata na kwa wale wenye vipaji na ubunifu hutumia kumbukumbu hizi sambamba na zile za kisasa na hivyo kupanua wigo wa uwezo wetu wa kuyatawala na kuyatumia mazingira kwa njia endelevu.

    1.4.2.2 Malikale ni utambulisho wa Taifa

    Malikale ni kitambulisho cha ukoo, kabila na taifa husika. Tanzania inazo Malikale nyingi muhimu zenye sifa za kitaifa na kimataifa. Baadhi yake zimeitambulisha na kuitangaza nchi yetu nje ya mipaka yake. Mifano halisi ni Masalia ya Mjusi aliyepatikana Tendaguru Lindi miaka millioni 150 iliyopita, fuvu la zamadamu aliyeishi miaka milioni 1.75 iliyopita lililogunduliwa mwaka 1959 katika Bonde la Oldupai, na nyayo za zamadamu aliyeishi miaka milioni 3.6 zilizogundulika miaka katika eneo la Laetoli, ni nyayo ambazo zinaonyeha binadamu kipindi hicho alikuwa anatembea kwa miguu miwili. Mifano mingine ni Michoro ya miambani ambayo inapatikana katika maeneo mengi Tanzania mfano Kolo Kondoa.

    1.4.2.3 Elimu kwa vizazi vijavyo

    Malikale ni moja kati ya nyenzo muhimu katika kuwaelimisha watu au jamii juu ya historia na utamaduni wao. Huonyesha historia na mabadiliko ya binadamu kimaumbile kutoka kwenye miili mikubwa kama ya Dinosaria mpaka maumbile ya sasa hivi, huonyesha chimbuko na maendeleo ya Binadamu maisha aliyokuwa akiishi na zana alizokuwa akitumia mfano mapango kabla ya kujenga nyumba hadi leo ambapo kuna aina mbali za ujenzi wa nyumba, zana za mawe kabla ya ugunduzi wa chuma hadi silaha za Chuma, Utengenezaji au uundaji wa vyombo mbalimbali magari au baiskeli za miti hadi sasa kuna magari, ndege n.k. Malikale huonyeshauwezowabinadamukufikirina kutunzakumbukumbukablayaugunduziwamaandishi mfano Michoro ya miambani Kondoa hadi sasa tunatumia Komputa. Utunzaji wa hazina hii ni muhimu kuwawezesha vizazi vijavyo kuona vitu halisi vitokanavyo na urithi wa utamaduni. Zaidi ya hayo, malikale huwawezesha watu kutambua na kuthamini utu wao, historia yao na utamaduni wao. Kumbukumbu hizi zikitunzwa vizuri zitaelimisha umma kwa kuwaonyesha walikotoka na kuona umuhimu wa kuutunza, kuuendeleza na kurithishana urithi huu kwa manufaa ya elimu kwa kizazi kilichopo na kijacho.

    1.4.2.4 Malikale chanzo cha mapato

    Malikale ni kitegauchumi muhimu sana kinapotunzwa na kuendelezwa bila kuathiri uhalisia wake, ni kivutio kizuri cha watalii. Nchi nyingi duniani hupata mapato makubwa kutokana na utalii unaotegemea vivutio vya malikale. Utalii huchangia na kuongeza pato la serikali na la wananchi wanapofanya kazi katika sekta ya Malikale ama wanapouza bidhaa na kutoa huduma mbalimbali kwa watalii.

  • 6

    Wizara kupitia Idara ya Malikale na katika kutekeleza Sera ya Malikale 2008 na kwa mujibu wa sheria ya Mambo ya Kale sura 333 ya 2002 imeboresha na kuanza kukukusanya mapato kupitia vyanzo vifuatavyo:

    1) Viingilio

    Haya ni mapato yatokanayo na viingilio wanavyotozwa wageni watembeleao maeneo ya Mambo ya Kale pamoja na makumbusho.

    2) Adazautafiti

    HayanimapatoyatokanayonaadazinazotozwakwawatafitiwafanyaotafaitimbalimbalizaMamboyaKalenchini.Watafitihawawanawezakuwawandaninawanjeyanchi.Idarainatoza5%yaghramazautafitikamainavyoonekanakatiakasheriayaMamboyaKale

    3) Mrabaha

    Haya ni mapato yatokanayo na uwekezaji katika rasilimali za Malikale kama vile, majengo ya kihistorianamikusanyoinayotumiwanawatafitimbalimbalihususaniileiliyohifadhiwanjeya nchi. Kwa sasa Idara inapata mrahaba mmoja tu utokanao na Mkataba (MoU) iliyoingiwa na Idara ya Mambo ya Kale NCAA ambapo Mamlaka ya Hifadhi ya NCAA inakusanya mapato yote ya Oldupai nusu ya mapato yanayopatikana hupewa Idara na yanayobakia hutumika kuendeshea kituo cha Oldupai.

    4) Michango ya Wahisani wa Maendeleo (Grant)

    Idara hupata mapato yanayotokana misaada mbalimbali. Idara inatekeleza majukumu yake kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali wakiwemo Washirika wa Maendeleo kwa lengo la kuhakikisha kuwa raslimali Malikale zinahifadhiwa kwa lengo la kuziongezea muda wa uwepo wake. Hivyo Idara huandika miradi mbalimbali itakayosaidia katika uhifadhi na uendelezaji wa Malikale zilizo chini ya Wizara.

    5) Makusanyo ya mapato

    Mapato yote yanatokana na rasilimali za Malikale na kupitia vyanzo vilivyotajwa hapo juu yanakusanywa katika Mfuko wa Taifa wa Mambo ya Kale. Mfuko huu umeanzishwa kwa mujibu wa sheria ya Mambo ya Kale Na. 22 ya mwaka 1979, kifungu kidogo cha 19B (au Sura 333 kifungu 22). Kifungu hiki kimeainisha vyanzo vya mapato ya mfuko huu na kuwayanatumikakwaajiliyaUtafiti,uhifadhinauendelezajiwaRaslimalizaMalikale.Katika kusimamia makusanyo ya Mfuko wa Mambo ya Kale, kanuni huandaliwa kwa ajili ya ukusanyaji wa maduhuli kwenye vituo vya Mambo ya Kale ambazo huboreshwa mara kwa mara ili kuendana na wakati na mazingira. Kanuni inayotumika kwa sasa ni kanuni Na. 497 ya mwaka 2014 (the Antiquities user fees rules, 2014). Lifuatalo ni jedwali na 1 linaloonyesha Mapato na wageni 2006 / 2007 hadi 2017 / 2018.

    Jedewali Namba 1. Mapato na wageni 2006/2007 hadi 2017/2018

    Mwaka Wageni Mapato

    2006/2007 95,265 236,666,079

    2007/2008 120,919 266,241,803

    2008/2009 102,528 216,507,549

  • 7

    2009/2010 103,777 212,867,609

    2010/2011 161,666 231,825,095

    2011/2012 125,490 516,496,180

    2012/2013 214,214 1,321,340,797

    2013/2014 154,930 1,124,559,323

    2014/2015 107,334 1,023,860,957

    2015/2016 110,500 1,308,080,760

    2016/2017 118,566 1,824,538,604

    2017/2018 128,268 2,213,388,590

    Ongezeko la maduhuli kuanzia 2016 hadi 2018 limetokana na kuboreshwa kwa baadhi ya vituo kwa kuviendeleza na kuboresha miundombinu ikiwemo maji, umeme na ujenzi wa vituo vya taarifa na kumbukumbu katika vituo vifuatavyo; Makumbusho ya Kumbukizi ya Dkt. Livingstone, Ujiji mwaka 2006; Makumbusho ya muhula wa mawe, Isimila mwaka 2006; Michoro ya Miambani na kuiweka kwenye Orodha ya urithi wa Dunia mwaka 2006; Kukamilika kwa Ukarabati, Uboreshaji na kuzinduliwa kwa Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es Salaam kwa ufadhili wa Serikali ya Sweden; Ukarabati, Uimarishaji na Uendelezaji wa Tembe la Kwihara, Tabora mwaka 2014; Kukarabati majengo katika Makumbusho ya Kalenga mwaka 2014 na kuimarisha mipaka ya kituo hicho mwaka 2018; Kujenga Makumbusho mpya Olduvai iliyofunguliwa tarehe 03 Octoba 2017 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Arusha; KujengajengojipyalaofisinakutoataarifaMbozi,SongwenaMwishoWizarailiboreshamfumo wa ukusanyaji wa maduhuli ambao umesaidia mapato kupanda. Kwa ujumla haya ndio yaliyosababisha maduhuli kuongezeka kutoka 236,666,079 mwaka 2006/2007 hadi 2,213,388,590 mwaka 2017/2018.

    FedhazinakusanywahutumikakwaUtafiti,uhifadhi,uendelezajinakuendeshavituoikiwanipamojanaukarabatiwamajengonamajenziyakihistoriaulinzi,usafi,na utangazaji.Mwanzoni kabla ya Idara kuhamia Maliasili na Utalii vituo hivi kipaumbele ilikuwa kuhifadhi Malikale kwa kumbukumbu, Elimu na Utafiti na ukusanyaji wa maduhuli aumapato haukuwa kipaumbele. Makusanyo rasmi yameanza baada ya Idara kuhamia Wizara ya Maliasili na utalii na kuendelezwa kiutalii. Kwa miaka 12 iliyopita kuanzia 2006 hadi 2018 mapato yameongezeka kutoka 236,666,079 hadi 2,213,388,590. Hii inadhihirisha wazi kuwa vivutio vya Malikale vikitunzwa na kutangazwa vizuri vinaweza kutoa mchango mzuri katika Taifa kielimu na kiuchumi.

  • 8

    SURA YA PILI

    MAJUKUMU, MUUNDO NA WATUMISHI WA IDARA

    YA MAMBO YA KALE

    2.1 Utangulizi

    Sura hii inawasilisha majukumu ya Idara kuanzia kwa Mkurugenzi hadi kwa Wakurugenzi Wasaidizi na mabadiliko yaliyokuwa yakifanyika kimuundo kuanzia 2009 hadi 2019. Vilevile sura hii inaelezea watumishi wanaotakiwa kuajiriwa katika sekta hii ya Malikale, mafunzo, mfanyakazi bora na uteuzi wa watumishi wa Idara katika kushika vyeo vya Taifa na Wizara na Tanzania na imeonyesha vituo 18 ambavyo vinasimamiwa na Wizara yenye dhamana kupitia Idara ya Mambo ya Kale

    2.2 Majukumu ya Idara

    Jukumu kubwa la Idara ni utafiti, uhifadhi na kuendeleza urithi huo wa Malikale kwakuzingatia Sera na Sheria. Kwa ujumla katika kufanikisha utendaji Idara inatekeleza majukumu yafuatayo kwa mujibu wa muundo 2009 na maboresho ya 2018:

    2.2.1 Kuandaa na kurekebisha na kusimamia utekelezaji Sera, Sheria na kanuni za Malikale;

    2.2.2 Kusimamia na kuhakikisha kuwa uhifadhi na ulinzi stahili wa Malikale unafanyika;

    2.2.3 KusimamianakuratibutafitizaMalikaleTanzaniaBara;

    2.2.4 Kuhamasisha matumizi endelevu ya Malikale kama vivutio vya utalii na vituo vya mafunzo;

    2.2.5 Kuhuisha na kusimamia mikataba ya kimataifa ambayo serikali imerithia inayohusiana na Uhifadhi wa Malikale mfano UNESCO;

    2.2.6 Kushirikiana na jamii, watu binafsi, mashirika na taasisi za binafsi na serikali ikiwemo Makumbusho ya Taifa katika kulinda na kuendeleza rasilimalikale za Taifa na kutoa ushauri wa kitalaam kwa wadau mbalimbali wa Malikale.

    2.3 Muundo wa Idara ya Mambo ya Kale

    Kwa miaka Idara ya Mambo ya Kale ilikuwa kama kitengo chini ya Mkurugezi mmoja mpaka mwaka 2009 ambapo muundo wa Kitengo ulibadilishwa na kuwa Idara kamili ya Mambo ya Kale yenye Mkurugenzi na Wakurugenzi wasaidizi watatu.

    2.3.1 Muundo wa Idara kuanzia mwaka 2009

    Muundo wa Wizara uliopitishwa na serikali awamu ya nne mwaka 2009 ndio uliobadilisha Mambo ya Kale kutoka kwenye kitengo kwenda Idara kamili na kulikuwa na maboresho madogo mwaka 2013 wizara. Katika Muundo huo wa mwaka 2009 na 2013 idara iliongozwa na Mkurugenzi na iligawanyika katika sehemu kuu tatu zinazoongozwa na Wakurugenzi wasaidizi kama ifuatavyo:

  • 9

    2.3.1.1Sehemuyautafiti,MafunzonaTakwimu;

    2.3.1.2 Sehemu ya Uhifadhi na Ufundi na;

    2.3.1.3 Sehemu ya Undelezaji wa Urithi wa Utamaduni

    Kazi zilizotekelezwa na Sehemu za Idara 2009 hadi 2018

    Idara kwa Muundo wa mwaka 2009 hadi 2018 ilikuwa na sehemu tatu zenye Wakurugenzi Wasaidaizi kama zilivyoainishwa katika kifungu 2.3.1 na yafuatayo ni majukumu ya kila Sehemu:

    2.3.2 Sehemu ya Uhifadhi na Ufundi.

    2.3.2.1 Kusimamia na kuratibu Uhifadhi na Ufundi wa Urithi wa Utamaduni na majengo, Miji na maeneo ya akiolojia;

    2.3.2.2 Kuandaa miongozo na kusimamia Uhifadhi na usimamizi wa Urithi wa Utamaduni;

    2.3.2.3 Kuainisha na kuchambua miradi ya ukarabati na uendelezaji wa Majengo au Miji, Minara na maeneo ya kiakiolojia.

    2.3.2.4 Kutoa idhini ya ukarabati na uendelezaji wa maeneo ya kihistoria, maeneo ya hifadhi ya Kihistoria na kiakiolojia.

    2.3.2.5 Kutoa idhini ya ukarabati au uendelezaji wa maeneo ya kihistoria;

    2.3.2.6 Kuandaa, kuratibu na kusimamia utayarishaji wa mipango ya usimamizi ya maeneo ya Urithi wa utamaduni, na:

    2.3.2.7 Kusimamia na kuratibu utekelezaji wa mipango ya usimamizi ya maeneo/ vituo vya Mambo ya Kale.

    2.3.3 Sehemu ya Maendeleo ya Urithi wa Utamaduni na Mawasiliano.

    2.3.3.1 Kuhamasisha Utalii katika maeneo ya Urithi wa Utamaduni;

    2.3.3.2 Kuratibu, kuandaa kutathimini na kufanya maboresho kwenye Kanuni, miongozo na Viwango.

    2.3.3.3 Kuandaa, kutathimini na kufanya maboresho kwenye Kanuni, miongozo na viwango.

    2.3.3.4 Kuandaa mpango au mkakati wa kuhamasisha Utalii katika maeneo Urithi wa Utamaduni.

    2.3.3.5 Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa mifumo wa kutoa habari.

    2.3.3.6 Kuandaa na kusimamia mifumo bora ya ukusanyaji maduhuli na mipango ya matumizi ya Idara.

    2.3.3.7 Kuelimishajamii,wageni,shule,watoto,watafitikuhusuurithiwa utamaduni.

    2.3.3.8 Kuratibu Ushirikiano wa Kitaifa, kikanda na Kimataifa.

  • 10

    2.3.4 SehemuyaUtafiti,MafunzonaTakwimu

    2.3.4.1 KuainishamaeneoyaUtafiti,kupangavipaumbelenakuratibutafiti

    2.3.4.2 zinazofanywanaWatafiti,TaasisizautafitikatikaSektayamalikalekutoka hapa nchini na nje ya nchi;

    2.3.4.3 Kuandaa na Kuratibu Mpango wa Mapango Mafunzo wa Idara;

    2.3.4.4 Kufanya na kuratibu kazi za Upembuzi Yakinifu wa Athari za Urithi wa Utamaduni katika Miradi mikubwa ya Maendeleo;

    2.3.4.5 KutathinininakuchambuaMipangoyaUtafiti;

    2.3.4.6 KufanyatafitizaUrithinaUtamaduninakuwasilishamatokeoyatafitikwa

    2.3.4.7 jamii au taasisi husika;

    2.3.4.8 Kutoavibalivyautafiti,uchimbaji,upigajipichanakusafirishanjeyanchi mikusanyo ya Urithi wa utamaduni;

    2.3.4.9 Kuandaa na kusimamia “inventory” ya Urithi wa Utamaduni na maeneo ya Urithi wa Utamaduni hapa nchini;

    2.3.4.10Kuandaamiongozonakusaidiakufanyatafiti,mafunzoyauhifadhina kutoa.

    Pamoja na sehemu hizo, Idara ina jumla ya vituo kumi na nane (18). Kwa mujibu wa muundo wa Idara, vituo vinasimamiwa na Sehemu ya Uhifadhi na Ufundi. Vituo vya Mambo ya Kale vimeorodheshwa kwenye Kiambatisho Na. 1.

    2.4 Mabadiliko ya muundo 2018 hadi 2019

    Kwa mujibu wa Muundo Mpya wa Wizara, Julai 2018, Wizara nzima ikiwemo Idara ya Mambo ya Kale sehemu ya Utafiti,Mafunzo na Takwimu katika Idara zote zaWizarazilihamishiwa katika Kitengo kipya kilichoundwa na Wizara cha Takwimu na Mafunzo. Hivyo Idara ya Mambo ya Kale ilibaki na sehemu mbili ambazo ni;

    2.4..1 Sehemu ya Uhifadhi na Ufundi na;

    2.4..2 Sehemu ya Undelezaji wa Urithi wa Utamaduni na Mawasiliano.

    Vilevile, Wizara ya Maliasili na Utalii katika hotuba ya bajeti ya Mwaka 2018/2019 ilielezea Bunge kuwa imeandaa mkakati wa kundeleza vituo vya Malikale vilivyopo Wizarani ikiwa ni pamoja na kuhamisha baadhi majukumu ya Mambo ya Kale kwenda Makumbusho ya Taifa na Idara ya Mambo ya Kale kubakia na majukumu ya Sera na Sheria. Maelekezo haya yametekelezwa na majukumu yanayohamishiwa Makumbusho ya Taifa ni:

    (i) Kuhifadhi, kuendeleza na kulinda maeneo ya malikale;

    (ii) Kuandaa na kutekeleza Mipango ya Usimamizi na Uendelezaji wa maeneo ya malikale;

    (iii) Kuanzisha na kuendesha mifumo ya datakanzi za malikale;

    (iv) Kuhamasisha uhifadhi wa malikale kwa kushirikisha Jamii;

    (v) Kuhamasisha utalii wa utamaduni;

    (vi) KufanyautafitiwamalikaleTanzaniaBara;

  • 11

    (vii) Kuanzisha makumbusho na vituo vya kumbukumbu na taarifa;

    (viii) Kuhamasisha matumizi endelevu ya malikale kama kumbukumbu za Taifa; vituo vya elimu na mafunzo; na vivutio vya utalii; na,

    (ix) Kuendeleza vivutio vya utalii wa malikale kwa viwango vinavyokubalika Kitaifa na Kimataifa.

    2.5 Majukumu yanayobaki Idara ya Mambo ya Kale

    Baada ya kuhamisha majukumu ya usimamizi wa vituo vya mambo ya kale kwenda Makumbusho ya Taifa, majukumu yanayopendekezwa kubaki Idara ya Mambo ya Kale ni kama ifuatavyo:

    i. Kuandaa, kusimamia na kutathmini utekelezaji wa Sera, Sheria, Kanuni naMiongozoyaUhifadhi,UtafitinaUendelezajiwaMalikale;

    ii. Kuratibu na kurekebu uhifadhi, uendelezaji na ulinzi wa malikale;

    iii. Kuandaa Vigezo vya kutambua na kusimamia malikale katika ngazi mbali mbali;

    iv. Kuandaa Vigezo vya kuanzisha makumbusho na vituo vya kumbukumbu na taarifa;

    v. Kuandaa Orodha ya Maeneo ya Mambo ya kale;

    vi. Kuweka vigezo na kuratibu uhamasishaji utalii wa urithi wa utamaduni;

    vii. Kuanzisha, kusimamia, kuendeleza na kudumisha ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa unaohusu masuala ya malikale na makumbusho.

    Muundo huu bado unafanyiwa kazi na Wizara na baadaye utapelekwa utumishi kwa ajili ya kuthibitishwa. Vilevile Sheria za Idara ya Mambo ya Kale na Shirika la Makumbusho ya Taifa hazina budi kubadilishwa ili kuendana na mabadiliko yaliyofanyika ambapo Makumbusho waweza kutekeleza majukumu waliyoongezewa na Idara ya Mambo ya Kale, kubaki na majukumu ya kisheria na kisera.

    2.6 Watumishi wa Idara ya Mambo ya Kale na Viongozi2.6.1 Watumishi wa Idara

    Idara ina vituo kumi na nane (18- ikijumuisha Olduvai na Laetoli ambapo Idara imeingia mkataba na Mamlaka ya Ngorongoro- NCAA ) vyenye maeneo madogo na makubwa. Mfano Kilwa kuna visiwa viwili, Kilwa Kisiwani na Songo Mnara ambapo Kilwa Kisiwani ni Kilomita za Mraba 32 na Songo Mnara Kilomita za Mraba 50. Mapango ya Amboni Sq km 39.5, Michoro ya miambani maeneo yapo kwenye vijiji 13 na ukubwa ni Kilomita za Mraba 2230, (huu ni mfano wa vituo vikubwa ambapo kituo kimoja kinatakiwa kuwa na watumishi 8 hadi 10). Kwa vituo vidogo kituo kimoja kinahitaji watumishi wanne. Mmoja akiwa ni Mkuu wa Kituo, mmoja kupokea wageni na kukusanya maduhuli na mwingine kushughulikiauhifadhinauendelezajiwaKituonamwingineutangazajinautafiti.Maeneomakubwa kama Michoro ya Miambani Kondoa na magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara watumishi wanaohitajika ni kuanzia nane (8) hadi kumi. Hivyo jumla ya watumishi wanaotakiwa katika

    Idara ya Mambo ya Kale ni zaidi ya 200 kwa vituo vyote kumi na nane vilivyopo Wizara ya Maliasili na Utalii. Wakati huo huo kuna haja ya TAMISEMI na wadau mbalimbali kuhamasishwa kuajiri wataalam wa Mambo ya Kale watakaoshirikiana na Idara kuhifadhi na kuendeleza vivutio vya Malikale vilivyopo katika Tanzania nzima.

  • 12

    Idara mpaka Aprili 2019 watumishi 68 ambapo 50 vituoni na 18 Makao Makuu. Idadi hii ya Watumishi wamepungua ukilinganisha na mwaka 2015/2016 ambapo ilikuwa na watumishi 75, kwa sababu waliostaafu na kufariki hawakuajiriwa wengine. Kutokana na uhalisia wa maeneo ya Mambo ya Kale ikijumuisha kazi zilizopo na ukubwa wa maeneo watumishi waliopo ni wachache, wanaotakiwa ni zaidi ya 200. Idara ya Mambo ya Kale taaluma mbalimbalizauhifadhi,utafiti,Makumbushonakuongozawagenizinahitajika.

    2.5.2 Viongozi wa Idara ya Mambo ya Kale kuanzia Kitengo hadi Idara kamili

    Idara ya Mambo ya Kale baada ya uhuru ilitunga sheria na kuwa na uongozi ambao ulisimamia majukumuyautafitinauhifadhiwaMamboyaKale.IfuatayoniorodhayaWakurugenzinaWakurugenzi Wasaidizi waliongoza Idara kwa nyakati tofauti.

    2.6.2.1 Wakurugenzi

    1961-1968 - Neville Chittick1968-1981 - Amini Aza Mturi1981-1985 - S. Mongela1985-1997 - Simon S.A.C. Waane1997-2017 - Donatius K. Kamamba2018-2019 - Digna Faustin Tillya

    2.6.2.2 Wakurugenzi Wasadizi

    Idara baada ya kuwa Idara kamili mwaka 2009 Muundo uliopitishwa ulikuwa na Mkurugenzi na Wakurugenzi Wasaidizi watatu hadi 2017 mabadiliko ya muundo yalipofanyika katika Idara na kubakia na sehemu Mbili. Wakurugenzi Wasaidizi Walioteuliwa mwaka 2009 hadi sasa ni;

    1) 2009-2012 Bwana Felix Ndunguru, MkurugenziMsaidiziUtafitiTakwimunaMafunzo

    2) 2009-2017 Bwana John Kimaro, Mkurugenzi Msaidizi Ufundi na Uhifadhi

    3) 2009-2017 Bibi Digna Faustin. Tillya, Mkurugenzi Msaidizi Maendeleo ya Urithi Utamaduni

    4) 2015-2017 Bibi Eliwaa Maro, MkurugenziMsaidiziUtafitiTakwimunaMafunzo

    5) 2017-2019 Dkt Fabian Kigadye Mkurugenzi Msaidizi Ufundi na Uhifadhi

    6) 2017-2018 BwanaAnthonyTibaijuka,MkurugeziMsaidiziUtafiti Takwimu na Mafunzo(sehemu imehamishwa)

    7) 2017-2018 Bwana Anacleth Mwijage, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi

    Maendeleo ya Urithi wa Utamaduni

    2.6.3 Mafunzo au uendelezaji wa Watumishi wa Idara

    Idara ya Mambo ya Kale ni moja ya Idara ambazo ni mtambuka. Kutokana na majukumu ya kazi Idara huhitaji fani mbalimbali ili kuweza kutekeleza majukumu yake kikamilifu. Fani zinazotakiwa ni za ufundi wa Mambo ya Kale kama vile ujenzi au ukarabati, uchoraji, upimaji, sorovea kwa majengo ya kihistoria na maeneo ya kihistoria yanahitaji kuhifadhwa

  • 13

    bilakuharibuuhalisiawake.AidhaIdarahufanyautafitinamatokeohuwezeshakupatikanakwa historia, makazi, majengo, vifaa, nguo, zana za Mawe na Chuma, vyombo na vitu vilivyokuwa vikitumika kama silaha n.k. Vyote vinahitaji utaalamu wa kuvijali katika utunzajikwasababunivyasikunyingiutunzajisiowakawaida.Malikaleainayafloronafauna ni masalia yanayotokana na wanyama na mimea nayo kuna utunzaji wake ni wa hali ya juu. Kuna fani za Makumbusho ambazo zina utaalamu wake ni wa ajili ya maonyesho mbalimbali yanayowekwa katika Makumbusho zote mahali popote. Taaluma za mambo ya kale zinazohitajika ni Akiolojia; Jiolojia; Palentolojia; Anthropolojia; Sosholojia; Uhifadhi na Usanifu wa majengo ya kihistoria; Jiographia; Historia; Ethnolojia; Elimu ya viumbe; mipango miji; na Uhifadhi na Usimamizi wa Malikale.Aidha, Idara huandaa Mpango wa Mafunzo ya Muda mrefu na Mfupi kuwezesha watumishi kufanya kazi hizo kwa ufanisi.

    Kwa miaka 2016 hadi 2019 Idara iliwezesha watumishi mbalimbali kushiriki katika mafunzo yafuatayo; Katika kuhakikisha kuwa miji na majengo ya kihistoria nchini yanaendelea kuhifadhiwa kwa lengo la kutunza historia na kumbukumbu ya Taifa kwa mwaka 2016/2017 watumishi 2 wa Wizara walishiriki katika mafunzo yaliyoandaliwa na Mji wa Kihistoria wa Humburg, Ujerumani ambao una mashirikiano na Jiji la Dar es Salaam. Mafunzo hayo yalihusu uhifadhi na ukusanyaji wa kumbukumbu na taarifa za majengo na miji ya kihistoria. Baada ya kupata mafunzo hayo, Wizara imefanya tathmini ya hali ya uhifadhi wa majengo ya kihistoria 27 ndani ya Jiji Dar es Salaam. Aidha, watumishi wanne wamepata mafunzo ya muda mrefu; watatu wamepata Mafunzo ya Shahada ya uzamili (MA) kuanzia 2017 hadi 2018 na mmoja amemaliza masomo ya uzamivu (PHD) mwaka 2018 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Watumishi wanne wamepata mafunzo ya muda mfupi: mmoja alipata mafunzo ya dereva, mmoja alipata mafunzo ya kusimamia miradi, Katibu Muktasi alisomeshwa kwenye kozi za Katibu Muktasi.

    2.6.4 Mfanyakazi Bora wa Wizara, Katibu wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara na Mwenyekiti wa TUGHE 2018

    Katika kipindi hiki cha Serikali ya awamu tano watumishi wa Idara wamechaguliwa kushika nafasi mbalimbali za uongozi katika Wizara na pia kupata ufanyakazi bora. Kwa mwaka 2018 Aprili, Mfanyakazi bora wa Wizara alichaguliwa kutoka Idara ya Mambo ya Kale.mfanyakazi huyu Bwana Idiphonce Mlowoka alipatikana kwa kushindanishwa na watumishi wengine 12 wa Idara na vitengo vya Wizara ya Maliasili na Utalii. Mtumishi anaipenda kazi yake na anaifanya kwa kujituma na mazingira magumu. Taaluma yake ni Fundi mhifadhi wa Mambo ya Kale anatumika katika kuhifadhi majengo ya Kihistoria na magofu. Hii kazi ni ngumu na ni tete kwa sababu majenzi hayo yana zaidi ya miaka 50 na mengine mia, kinachotakiwa kuyarudishia kama yalivyo na mara nyingi usipokuwa makini huporomoka. Hivyo mwaka 2018 Wizara iliamua kumtunuku mtumishi huyu Idiphonce Mlowoka Mfanyakazi bora wa Wizara. Mwaka 2019 Aprili kwa mara ya pili Idara imepata mfanyakazi bora wa Wizara, Bi Neema Mbwana kutoka kituo cha Mwalim Nyerere Magomeni. Aidha kwa Mwaka 2018 Wizara ilimteua Bwana Anthony Tibaijuka kuwa Mwenyekiti wa TUGHE Tawi la Wizara na Bwana William Mwita alichaguliwa kuwa Katibu wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Maliasili na Utalii ambalo Mwenyekiti ni Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.

    2.6.5 Uteuzi Maalum

    Katika kipindi hiki cha Serikali ya awamu hii ya Tano watumishi wawili waliteuliwa na kupewa kazi nyingine. Mtumishi mmoja Mheshimiwa Simon Ezekiel Odunga aliteuliwa kutoka Idara ya Mambo ya Kale na Muheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kuwa Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Mkoa wa Dodoma Mwaka 2016. Mtumishi mwingine Dkt.EmmanuelBwasirialiteuliwakuwaKaimuMkurugenzikitengochautafitinamafunzocha Wizara ya Maliasili na Utalii mwaka 2019. Haya ni mafanikio makubwa kwa Idara katika kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya tano na haijawahi kutokea kwa miaka ya nyuma.

  • 14

    SURA YA TATU

    USHIRIKI WA SERIKALI NA SEKTA BINAFSI

    KATIKA UHIFADHI WA MALIKALE

    3.1 Utangulizi

    Sura hii inaeleza umuhimu wa uhifadhi wa Malikale na jinsi Taasisi za serikali kuanzia Makumbusho saba zinazosimamiwa na Wizara ambazo zipo Arusha, Dar es Salaam, Mara na Mkoa wa Ruvuma hadi Makumbusho ya Iringa inayosimamiwa na Mkoa wa Iringa. Lengo kuelimisha jamii kuhusu Makumbusho hizo. Taasisi za binafsi zilipo katika Mikoa ya Tanga, Mtwara, Pwani na Mwanza.

    3.2 Umuhimu wa ushirikano wa Serikali na Sekta Binafsi katika Uhifadhi wa Malikale

    Uhifadhi wa malikale ni muhimu ili kuhakikisha kwamba maeneo yenye malikale yanadumu na kuendelezwa kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo. Maeneo ya Malikale yametawanyika katika Tanzania nzima. Mfano mzuri ni ule wa Machifu. Karibu kila kabila lilikuwa na utawala wa machifu na waliweka utaratibu wa namna ya kuhifadhi na kurithishana urithi wao wa kichifu. Makazi haya ya jadi yapo mpaka leo, kwenye baadhi ya maeneo yameendelezwa na hutumika kama vivutio vizuri vya utalii na elimu. Hivyo, imefikawakatisasaSektabinafsinaTaasisimbalimbalikuhamasishwakuanzishashughuliza makumbusho katika sehemu mbalimbali nchini. Kwa vile malikale nyingi ziko mikononi mwa jamii yenyewe, jamii ina haki ya kuelimishwa na kushirikishwa katika uhifadhi na kutambua umuhimu wa malikale hizo kama utambulisho wa ukoo, kabila na taifa. Jukumu la uhifadhi wa malikale ni la umma mzima.

    3.3 Ushiriki wa Taasisi za Serikali.

    Shirika la Makumbusho ya Taifa ni Taasisi ya serikali kwenye Idara ya Mambo ya Kale ambayo ina jukumu kubwa la kuelimisha jamii umuhimu wa kuhifadhi Malikale. Shirika hili linaongozwa na Bodi ya Makumbusho ambaye mwenyekiti huteuliwa na Rais. Jukumu laMakumbusho yaTaifa ni kutafiti, kukusanya, kuhifadhi na kuelimishaUmma kupitiamaonyesho, machapisho na mihadhara kuhusu umuhimu wa kuhifadhi na kuendeleza urithi wa utamaduni, unaohamishika kwa manufaa ya kizazi kilichopo na kijacho. Shirika la Makumbusho linatekeleza majukumu yake kupitia makumbusho saba ambazo zipo moja kwa moja chini ya Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa kwa kuzingatia Sheria ya Makumbusho Na.7 ya mwaka 1980. Makumbusho hizo ni:

    3.3.1 Makumbusho na Nyumba ya Utamaduni Dar es salaam

    Makumbusho hii ilianza kama Makumbusho ya Taifa na ilianzishwa mwaka 1934 na kuanza kutumika mwaka 1940 na ilijulikana kama Makumbusho ya Mfalme George wa Tano (v). Mwaka 1963 baada ya uhuru Makumbusho ilipanuliwa na kuongeza majego ya maonyesho mbalimbali. Mwaka 2010 upanuzi ulifanyika kwa kuongeza jengo ambalo kwa sasa linajulikana kama Nyumba ya Utamaduni ambayo ina kumbi za maonyesho mbalimbali ikiwemosanaa,mgahawa,StudionaOfisi.

  • 15

    Picha za juu: Januari 19, 2019 Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla (Mb) akiangalia kwa makini Tai iliyovaliwa wakati wa sherehe ya Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961 na mifupa na fuvu la binadamu (Skeletoni), Makumbusho ya Taifa.

    Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Constantine Kanyasu (Mb) Katikati akiangalia wadudu waliokaushwa stoo ya Biolojia Mwezi Februari 2019 Dar es Salaam.

  • 16

    3.3.2 Kijiji cha Makumbusho Dar es Salaam

    Makumbusho inayoonyesha nyumba na vifaa vya tamaduni mbalimbali zinazopatikana katika nchi ya Tanzania. Eneo hilo lipo katika jiji la Dar es Salaam Wilaya ya Kinondoni. Kijiji cha Makumbusho kipo mkabala na barabara ya Ally Hassan Mwinyi nje kidogo ya mji. Kijiji hicho kilianzishwa mwaka 1966 kwa ajili ya kuonyesha na kutunza tamaduni ikiwemo tamaduni za asili, ngoma na tamaduni za makabila mbalimbali kama Wanyakyusa, Makonde, Masai, Chagga, Haya, Ngoni, Yao na mengine mengi.

    3.3.3 Makumbusho ya Azimio la Arusha

    Makumbusho haya yalianzishwa mwaka 1977 wakati wa kuadhimisha miaka 10 ya Azimio la Arusha. Ilianzishwa kwa ajili ya kutunza kumbukumbu za Azimio la Arusha kuhusu Siasa ya Ujamaa na kujitegemea. Jina la azimio la Arusha linatokana na mji wa Arusha lilikopitishwa tarehe 26-29 Januari 1967. Lengo la azimio hili ni kujikomboa dhidi ya umaskini wetu. (Chanzo - TANU, Dar es Salaam. (1967).

    3.3.4 Elimu ya Viumbe, Arusha

    Makumbusho ya Historia asilia Arusha ilifunguliwa mwaka 1987, na ni Makumbusho pekee nchini ya Historia asilia. Makumbusho hii ipo katika Mkoa wa Arusha na imejikita katika kutunza na kuhifadhi mikusanyo ya sampuli mbalimbali za Historia asilia, ikiwa ni pamoja na ukusanyaji wa kina wa masalia ya mifupa ya wanyama wenye uti wa mgongo pamoja na Historia ya mji wa Arusha - Boma. Makumbusho ya Historia asilia ipo katika Boma la zamani la kijeshi na ulinzi wa ukoloni wa wajerumani Arusha. Makumbusho hii inapakana naUkumbiwaKimataifawaMikutano(AICC)naManispaanaOfisiyaMkuuwaMkoaArusha. Mtindo wa awali uliboreshwa na wakazi wa mji wa Boma baada ya kipindi cha utawala wa Ujerumani. Maonyesho yaliyopo kwenye Makumbusho hiyo, yanaonyesha Chimbuko la Binadamu,Wanyama, Mimea na Mbuga Mbalimbali Mkoani Arusha. Kwa wanafunziwanapataelimuyaHistoria,Jiografia,Viumbehainamimea.

    Makumbusho hii ipo barabara ya Boma na inapakana na Ukumbi wa Arusha International Conference,OfisiyaMkuuwaMkoanaOfisiyaManispaayaArusha.

    Makumbusho ya Azimio la Arusha, Chanzo: Makumbusho ya Taifa

  • 17

    3.3.5 Makumbusho ya Baba wa Taifa Mwl. Nyerere

    Makumbusho hii ilianza mwaka 1999 mahali ambapo Baba wa Taifa Mw. Myerere alizaliwa na kuzikwa. Makumbusho hii inaonyesha Nyaraka binafsi za Mwalimu Nyerere pamoja na Maisha yake. Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alizaliwa mwaka 1922 katika kijiji cha mwitongo Wilaya ya Butiama mkoa wa Mara, alifariki Oktoba 14, 1999 nchini London, Uingereza. Hayati baba wa Taifa baada ya kufariki (14 Oktoba 1999), amezikwa kijiji cha mwitongo Wilaya ya Butiama mkoa wa Mara na makazi yake yamefanywa kuwa Makumbusho. Hivyo Makumbusho katika wilaya ya Butiama ziko mbili ambayo ipo chini ya Shirika la Makumbusho na makazi yake Baba wa Taifa yamekuwa nyumba ya makumbusho baada ya kufariki.

    Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Nyerere bado anakumbukwa na watanzania wengi kwa kupigania uhuru wa Tanganyika ambao ulipatikana 1961. Kwa bara la Afrika anakumbukwa kutokana na sera zake za kujali utu na ubinadamu, hasa kwa mchango wake mkubwa wakati wa harakati za kupigania uhuru katika nchi mbali mbali barani Afrika na alitoa vitu na maeneo mbalimbali katika Tanzania yakatumika katika kupigania uhuru wa nchi nyingine za Afrika mfano, Afrika ya Kusini, Msumbiji, Namibia, Angola n.k.

    3.3.6 Makumbusho ya Majimaji, Songea Mkoa wa Ruvuma

    Makumbusho haya yalifunguliwa rasmi tarehe 7/7/1980. Kuanzia hapo makumbusho haya yaliendelea kutoa huduma chini ya usimamizi wa Mkoa wa Ruvuma na wazee waliendelea kufanya maadhimisho ya siku ya Mashujaa katika eneo la Makumbusho haya kila mwaka mwezi Februari na ndio ambao wamekuwa wakitoa maelezo kwa wageni wanaotembelea makumbusho hayo. Tarehe 1 septemba 2005 makumbusho haya yalikabidhiwa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Songea na mwaka 2010 yalikabidhiwa Wizara ya Maliasili na Utalii na yanasimamiwa na Makumbusho ya Taifa.

    Makumbusho ya Elimu Viumbe. Chanzo Makumbusho ya Taifa

  • 18

    3.3.7 Nyumba ya Dkt. Rashid Mfaume Kawawa

    Tarehe 27 Februari, 2017 Familia ya Hayati Dkt. Rashid Mfaume Kawawa maarufu kama Simba wa Vita iliikabidhi Wizara ya Maliasili na Utalii nyumba iliyopo Bombambili Songea, nyaraka na vifaa mbalimbali alivyokuwa akivitumia Hayati Dkt. Rashid Mfaume Kawawa enzi za uhai wake ili itumike kama sehemu ya Makumbusho ya Taifa. Wizara imekarabati nyumba hiyo, kuwekewa uzio na ilizinduliwa mwaka 2017 na Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe tarehe 27/02/2017 kuwa miongoni mwa Makumbusho za Taifa.

    Picha mbili za Nyumba iliyokabidhiwa Serikali na Familia ya Hayati Dkt. Rashid Mfaume Kawawa. Picha ya kushoto, inaonyesha nyumba hiyo kwa

    nyuma na picha ya kulia inaonyesha nyumba hiyo kwa mbele

    Makumbusho ya Majimaji. Chanzo: Makumbusho ya Majimaji

  • 19

    3.4 Ushiriki wa Sekta binafsi na Taasisi zisizo za serikali

    Idara ya Mambo ya Kale katika kutekeleza majukumu ya uhifadhi wa Malikale hushirikiana na wadau mbalimbali wa serikali na sekta binafsi kuhakikisha urithi huu unalindwa na kutumika kiendelevu. Taasisi za binafsi zinazojihusisha na uhifadhi na uendelezaji wa malikale ni pamoja na Uzikwasa Pangani, Urithi Tanga mjini, Mkoa wa Tanga; Trade Aid, Mikindani, Mkoa wa Mtwara; Makumbusho ya Kanisa Bagamoyo Mkoa wa Pwani; Makumbusho ya Bujora na Mkoa wa Mwanza. Hizi ni baadhi ya taasisi ambazo zinashiriki katika kuhifadhi na kuendeleza Malikale. Taasisi hizo hutumia Malikale hizo kutoa mchango katika uchumi kama kivutio cha utalii na uwezekaji kwa kuzingatia misingi na kanuni za uhifadhi na zinajiendesha zenyewe.

    3.4.1 Taasisi ya Trade Aid.

    Trade Aid, Mikindani ni Shirika lisilo la Serikali ambalo Makao yake Makuu ni Uingereza. Shirika hili limeingia mkataba na Serikali kupitia Wizara ya Elimu tarehe 8 Agosti, 1997 kwa ajili ya kukarabati BOMA la Mikindani na kukamilika 1999. Baada ya ukarabati wa BOMA kukamilika jamii ya Mikindani ilishirikishwa kutoa maamuzi kuhusu jengo hilo litumikeje ili kulihifadhi na Jamii ya Mikindani kunufaika. Kazi zilizofanywa na Shirika hilo ni nyingi ikiwemo Elimu kwa vijana ya hotelia inayotolewa bure na mafunzo kwa vitendo wanafanyia hapohapo hotelini na kupata uzoefu zaidi wanapelekwa hoteli za nje ya Mikindani kama hoteli ya Serena ya Dar es Salaam, Pia Shirika hili limesaidia kutoa mafunzo ya Ujasiriamali kwa Wafanya biashara wadogo kama washonaji, wavuvi, kupanda miti na Ufugaji wa nyuki. Wananchi baada ya kupata mafunzo ya ufugaji nyuki wameanza kufuga nyuki na Mikindani wamepata ushindi mara mbili ya kitaifa ya ufugaji nyuki. Shirika hili la Trade Aid limewapatia wananchi wa kijiji cha Mitengo bomba la maji, limekarabati Kisima cha maji cha Yakkata na limetoa mchango mkubwa kwa ukarabati wa majengo ya kihistoria ya Mikindani likiwemo BOMA, jengo la Livingstone na Ghofu la Gereza.

    Kushoto BOMA Mikindani linatumika Trade Aid na Kulia BOMA, Tanga linatumiwa na Makumbusho Urithi Tanga, Majengo haya ya Kijermani yamebakia

    na uhalisia wake.

  • 20

    3.4.2 Taasisi ya Urithi Tanga

    URITHI Tanga ni makumbusho ya urithi wa Tanga, yalianzishwa mwaka 2007 na Taasisi au asasi isiyo ya kiserikali inayoitwa The Tanga Heritage Centre (URITHI). Makumbusho hayo yapokwenyejengolililokuwaBomalaTanga.Bomahilililijengwamwaka1890kamaofisina makazi ya mkuu wa wilaya. Jukumu kubwa ni kuhamasisha jamii kutambua umuhimu wa kuhifadhi na kurithisha mila, desturi na tamaduni zake kutoka kizazi kimoja hadi kingine. Ina Makumbusho kwenye BOMA la Tanga la Mkuu wa Wilaya ya Tanga

    3.4.3 Makumbusho ya Kanisa, Bagamoyo

    Makumbusho ya Bagamoyo yalianzishwa mwaka 1957 na ushahidi upo wa kanisa la kwanza katika mji huo la Wamisionari wa kwanza kuingia nchini kutoka Shirika la Roho Mtakatifu (HolyGhostFathers)ambaowalifikaBagamoyoAprili3,1868nandiomwanzowaharakatiza uinjilishaji na kuzaliwa kwa Kanisa Katoliki hapa nchini Bagamoyo.

    Pia kanisa la kwanza Bagamoyo lina historia ya David Livingstone (19 Machi 1813 – 4 Mei 1873)alikuwammisionarinampelelezikutokaUskotishinaalisafirikatikaNchizaAfrikaya kusini na kati. Livingstone aliaga dunia mnamo tarehe 30 Aprili 1873 katika kijiji cha Chitambo (Zambia). Watumishi wake chini ya uongozi wa Myao Susi walibeba mwili wake hadiBagamoyouliposafirishwakwamelihadiUingerezanakuzikwaLondonkatikakanisala Westminster Abbey tarehe 18 Aprili 1874.

    Kushoto Makumbusho ya Kanisa na Kulia Kanisa ambalo mwili wa Dkt.. Livingstone uliwekwa na baadaye kusarishwa hadi London kuzikwa katika kanisa la Westminster

    Kushoto, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo mwaka 2016 Mheshimiwa Anastazia Wambura alipotembelea Makumbusho hayo ya Urithi Tanga alipokuwa katika ziara yake ya kikazi mkoani hapo iliyolenga kujua uendeshwaji wa shughuli za kisekta. Mheshimiwa alipongeza Urithi Tanga kwa kuazisha Makumbusho hiyo ya kuweka kumbukumbu za Makabila ya Tanga pamoja na Mila na desturi.

  • 21

    SURA YA NNE

    MAFANIKIO YA IDARA KATIKA SERIKALI YA AWAMU YA TANO KWA MWAKA 2015 HADI 2019

    4.1 Sura hii inaelezea mafanikio katika kazi mbalimbali za uhifadhi na uendelezaji wa Malikale na hasa katika vituo vya Mambo ya Kale vya Olduvai Arusha; Kalenga, Mkoa wa Iringa; Mikindani, Mkoa wa Mtwara; Michoro ya Miambani Kondoa, Mkoa wa Dodoma; Kimondo cha Mbozi Mkoa wa Songwe, Mapango ya Amboni Mkoa wa Tanga na Makumbusho ya Mkoa wa Mtwara na mafanikio katika Taasisi binafsi

    4.2 Uhifadhi na Uendelezaji wa Malikale

    Katika kipindi hiki cha serikali awamu ya tano kuna mabadiliko makubwa yaliyofanywa kwenye Idara ya Mambo ya Kale. Lengo ni kuboresha maeneo ya Malikale na kuyaweka katikahalinzuriyakutumikakiutalii,kielimunakiutafitinakuingiziataifanawananchikipato kwa huduma mbalimbali za kitalii. Uhifadhi na Uendelezaji wa maeneo yenye malikale kiutalii ni suala changa sana katika nchi ya Tanzania na Idara ya Mambo ya Kale. Jitihada zimeanza siku za karibuni ambapo maeneo mbalimbali yameanza kuongezewa yale mahitaji muhimu ya kiutalii ili kukidhi viwango vya kitaifa na kimataifa. Tanzania ina maeneo ambayo yana sifa za kipekee mfano Olduvai, Michoro ya Miambani, Mapango, Kimondo cha Mbozi, Majengo ya kihistoria, Makazi ya Jadi, Mila na desturi zetu, vyakula, Ngoma,lugha, mavazi n.k. Imeonekana urithi huu wa Malikale ukitumiwa vizuri bila ya kuathiri uhalisia wake unaweza kuchangia pato la Taifa baada ya kuboreshwa kwa mujibu wa Sera na sheria ya Malikale. Katika kutekeleza azma hii kipindi hiki cha Serikali ya awamu ya Tano, mafanikio yafuatayo yamepatikana.

    4.3 Makumbusho Mpya katika Kituo cha Bonde la Olduvai

    Bonde la Olduvai ni maarufu duniani kutokana na kufahamika kwake kama chimbuko la binadamu wa Kale. Historia na umaarufu wa bonde hili unafuatia ugunduzi wa masalia ya zamadamuuliofanywanawatafitiDktLouisLeakeynamkeweMaryLeakey.

    Fuvu la binadamu wa Kale maarufu kama Zinjanthropus boisie liligunduliwa kwenye bonde hili mwaka 1959, ikifuatiwa na Homo habilis Desemba 1960, Homo erectus May 1960 na Homo sapiens mwaka 1972. Kituo hiki kipo ndani ya Hifadhi ya NCAA na kinapata wageni wengi wa ndani na Nje ya Nchi ukilinganisha na vituo vingine vya Malikale.

    Mwonekano wa Bonde la Olduvai Fuvu la Zinjathropus Boisei 1959 lilipatikana eneo hili (FLK)

  • 22

    Kituo cha Olduvai kinaingiza mapato mengi kutokana na wageni wanaotembelea eneo hili. Kituohikipiabadokinatumiwanawatafitiwengiwandaninanjeyanchi.Kutokananaumaarufu wa Kituo hiki cha Olduvai Wizara kwa ufadhili wa Jumuiya ya nchi za ulaya (EU), imejenga Makumbusho Mpya ambayo ilifunguliwa tarehe 03 Octoba 2017 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan. Pia, yamejengwa majengo yatakayotumiwa na jamii na lingine kwa Chakula.

    Makumbusho mpya ya Olduvai iliyofunguliwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan tarehe 03 Octoba 2017.

    Kushoto ni Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Maghembe (Mb) na Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mheshimiwa Mrisho Gambo.

    Kushoto (A) Makumbusho mpya Olduvai na kulia (B) Makumbusho ya Zamani

     

     

    A

    B

  • 23

    4.4 Uendelezaji wa Kituo cha Kimondo, Mbozi, Mkoa wa Songwe.

    4.4.1 Historia na Sifa ya Kimondo

    Kimondo cha Mbozi ni moja ya vituo vya Mambo ya Kale na kinahifadhiwa kwa mujibu wa sheria ya Mambo ya Kale Cap 333 ya mwaka 2002. Kimondo hiki kilianguka kutoka angani katika kilima cha Mlenje, Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe. Kimondo cha Mbozi kiliwekwa kwenye maandishi mwaka 1930 baada ya kutembelewa na Mjerumani kwa jina laW.H.Nottnakilifanyiwautafitiwakimaabaramwaka1931.UtafitihuoulibainiuzitowaKimondo cha Mbozi tani 12 na ni cha Pili Afrika kwa ukubwa na uzito na ni cha Nane katika Duniakatiyavimondo1036kwatakwimuzamwaka2002.UtafitihuopiaulibainiKimondocha Mbozi kina madini ya Chuma asilimia 90.45, Nikeli 8.69, Shaba 0.66, Phosphorous 0.11 na sulphur 0.01. Kimondo cha Mbozi kina mvutano wa sumaku na kikiguswa ni cha baridi muda wote. Kutokana na sifa hizo na historia hii katika Taifa letu la Tanzania ilionekana ni muhimu kuhifadhiwa na kutangazwa katika gazeti la serikali mwaka 1967. Kimondo hiki kinatembelewanaWatalii,wanafunzinawatafitiambaohuwawanashangaawanapoelezwanamna ya vimondo duniani vinavyoaguka na wanatamani kuona jinsi vinavyoanguka. Kimondo cha kwanza katika Afrika na Dunia ni Hoba, kipo Nchi ya Namibia, kiligundulika mwaka 1920 na kina uzito wa tani 60.

    Hizi ni baadhi ya picha zinazoonyesha aina ya wageni wanaotembelea Kimondo cha Mbozi kwa lengo la kujifunza na kujua historia ya Kimondo hicho na kilidondokaje kutoka angani. Wataalam wa Mambo ya Kale wanaelezea vizuri kuhusu kimondo

    hikikutokananatafitizilizofanyika.

  • 24

    4.4.2 Ziara ya Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa

    Kimondo cha Mbozi kimeiweka Tanzania katika ramani ya dunia katika masuala ya utalii ambapo kinaaminiwa kuwa ni kati ya vimondo nane vikubwa zaidi duniani kinachokadiriwa kuwa na uzito wa tani 12, urefu wa mita 3.3, upana wa mita 1.63 na kimo cha mita 1.22. Wageniwanaofika eneohilobado siowengi lakini kikitangazwazaidi namiundombinukuwekwa vizuri Tanzania itapata Watafiti na wanafunzi kwa wingi. Tafiti za kimondozinaendelea kufanyika Duniani.

    Waziri Mkuu wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa ( wa pili kulia) akiangalia nguvu ya mvutano kwenye Kimondo

    Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa tarehe 23 Julai 2017 alitembelea Kimondo cha Mbozi, Mkoa wa Songwe na alipata maelezo kwa mtaalam wa Mambo ya Kale katika Kituo cha Kimondo, Mbozi Mheshimiwa Waziri Mkuu aliagiza eneo hilo lihifadhiwe vizuri na liendelezwe kwa ajili ya utalii na matumizi ya elimu kwa wanafunzi wanaojifunza kuhusu anga.

    Jamii zinazoishi karibu na kimondo zinaomba na kufanya mambo ya kimila kama makongamano ya makundi ya sherehe za kimila, na harusi au ndoa kwenye Kimondo. Kimondo cha Mbozi ni kivutio cha Utalii na Elimu. Hutumika kama Nyenzo ya kufundishia masomo ya Sayansi na elimu ya Anga. Pia ni fursa ya ajira kwa jamii katika uhifadhi wa kimondo na upatikanaji wa fursa za kibiashara wakati eneo hili litakapoendelezwa kikamilifu. Matarajio ya baadaye ni kufanya eneo hili litumike kuadhimisha Tamasha la Vimondo duniani kila mwaka litakalojumuisha wageni wa ndani na nje ya nchi.

  • 25

    4.4.3 Uongozi wa Wizara kuangalia na kushauri kuendeleza Kimondo cha Mbozi Mkoa wa Songwe

    Picha ya juu, Mheshimiwa Japhet Hasunga ( wa kwanza kushoto) Mbunge wa Jimbo la Vwawa na Naibu Waziri Maliasili akiwa kwenye Kimondo mwaka 2018, akipata maelezo kutoka kwa mtumishi wa Idara ya Mambo ya Kale, kituo cha Kimondo Mbozi.

    Picha ya chini Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii “Major General” Gaudence Milanzi, ( wa kwanza kushoto) akipata maelezo kutoka kwa mtaalam wa Mambo ya

    Kale wakati alipotembelea kituo hicho mwezi February 13 2018.

  • 26

    4.4.4 Maboresho yaliyofanyika katika Kituo cha Kimondo Mbozi

    Kimondo cha Mbozi Songwe ni moja ya vivutio vya utalii vya Malikale chini ya Wizara ya Maliasili na utalii ambapo kinalindwa, kinahifadhiwa na kuendelezwa kwa kujengwa kwa Jengo la kituo cha taarifa na kumbukumbu. Ujenzi wa Jengo hilo ulianza Mei, 2017 na kukamilika mwezi mei, 2018, baadae ilibakia kazi za kumalizia na kuboresha eneo la nje (land scaping) ambapo ilikamilika Februari mwaka 2019. Jengo hili limekuwa chachu ya kukuza utalii Mkoa wa Songwe.

    PichayajuuofisiyaZamaniyaKituochaMbozinapichayachiniJengojipyakwaajiliyaofisinataarifaKituochaMbozi.

     

     

  • 27

    4.4.5 Tamasha la Vimondo Duniani katika Kimondo cha Mbozi, Songwe

    Kwa mara ya Kwanza Tanzania kitaifa iliadhimisha Tamasha la vimondo lililofanyika sambamba na maadhimisho ya siku ya Vimondo Duniani ambayo hufanyika Juni 30 kila mwaka kutokana na kikao cha Umoja wa Mataifa cha tarehe 6 Desemba, 2016 kilichopitisha maadhimisho hayo. Wizara kwa kushirikiana na Mkoa wa Songwe pamoja na wadau wengine wa uhifadhi na maendeleo ilifanya maadhimisho ya siku ya vimondo duniani katika kituo cha Kimondo cha Mbozi kijiji cha Ndolezi kata ya Mlangali, Wilayani Mbozi. Lengo la kuadhimisha siku ya Vimondo Duniani Kitaifa Mkoani Songwe ni kutangaza Kimondo cha Mbozi kilichopo hapa Tanzania kitaifa na kimataifa ili kuongeza idadi ya Watalii na kuvitangaza vivutio vingine vilivyopo hapa nchini hususan Ukanda wa Utalii wa Kusini. Tamasha hili lilifanyika kwa muda wa siku tatu kuanzia tarehe 27 hadi 30 Juni 2018 na mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Maji siku ya Ufunguzi na siku ya kufunga Mgeni Rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt.Hamisi Kigwangalla (Mb) Waziri wa Malisili na utalii tarehe 30 Juni 2018 chini ya Uongozi wa Mkuu wa Mkoa Luteni Mstaafu Chiku Gallawa. Maagizo aliyoyatoa ni Wizara kwa ujumla Idara na Taasisi zake kushirikiana na Mkoa wa Songwe kuendeleza vivutio vya utalii vilivyopo Mkoani Songwe.

    Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla, Waziri wa Wizara ya Maliasili na Utalii akipata maelezo kutoka kwa mtaalam wa Mambo ya Kale Bwana Filmerick Basange kuhusu Kimondo hicho cha Mbozi namna kilivyodondoka na sifa za Kimondo hicho.

    AfisahuyowaMamboyaKalealimwambiaMheshimiwaWaziri,ainazamadinizilizomokatika Kimondo hicho na uzito wake wa tani 12 ambao umefanya kimondo kuwa cha pili kwa ukubwa Afrika na cha nane duniani. Kimondo cha Mbozi ni baridi wakati wote na kina nguvu ya mvutano.

  • 28

    Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla (Mb) Waziri wa Malisili na Utalii alipotembelea Kimondo cha Mbozi tarehe 30 Juni 2018 wakati wa Maadhimisho ya siku ya Vimondo Duniani akifanya majaribio ya kuangalia nguvu ya mvutano katika Kimondo hicho

    Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla (Mb) Waziri wa Malisili na Utalii Wakati wa kufunga maadhimisho ya Vimondo Duniani alimtunuku Mkuu wa Mkoa wa Songwe Luteni Mstaafu Chiku Gallawa zawadi kwa kufanikisha Tamasha hilo na kuhamasisha Utalii ukanda wa Nyanda za Juu Kusini.

  • 29

    Katika ufungaji wa Tamasha hili Mgeni rasmi Mheshimiwa Dkt.Hamisi Kigwangalla Waziri wa Maliasili na Utalii alipata nafasi ya kutembelea mabanda mbalimbali likiwemo la Maliasili na mengine ya Wajasiriamali. Mabanda hayo yalikuwa yamejipanga kwa Wilaya, hivyo alitembelea Wilaya zote na kuona kuna nini wanaweza kuviendeleza kama vivutio vya Utalii. Pia Mkuu wa Mkoa alinunua eneo kubwa karibu na Kimondo cha Mbozi ambalo kila Wilaya itaweka vivutio vyake vya utalii ikiwa ni pamoja na utamaduni uliopo, uwekezaji, kilimo, viwanda machimbo ya madini yalipo Mkoani Songwe.

    4.5 Mfumo wa Kukusanya Maduhuli

    Idara ya Mambo ya Kale katika awamu hii ya serikali ya awamu ya Tano imekuwa mstari wa mbele katika kusimamia ukusanyaji wa Maduhuli. Imeshirikiana na Kitengo cha Wizara cha TEHAMA katika kuandaa mfumo wa kukusanya mapato kwenye vituo vya Mambo ya Kale. Watumishi wa vituoni walielemishwa kuhusu Mfumo huo na walishiriki katika kuainisha mahitaji ya mfumo wa kukusanya mapato kilichofanyika jijini Arusha kati ya tarehe 07-21/11/2017. Idara kwa kushirikiana na Kitengo cha TEHAMA imefanya tathmini yamiundombinu yaTEHEMAkwenye vituo vyaMambo vyaKale.Hadi kufikia tarehe10/06/2018 kazi hiyo imefanyika katika vituo vya Mikindani, Magofu ya Kilwa Kisiwani na Songo Mnara, Makumbusho ya Mwalimu Nyerere, Magomeni na Kunduchi, Dar es Salaam; Isimilia na Kalenga Iringa, Ngome Kongwe, Caravan Serai Magofu ya Kaole, Bagamoyo, Kwihara - Tabora na Ujiji – Kigoma. Kolo Kondoa na Amboni, Tanga. Kwa sasa vituo vyote 16 vimeshaingizwa katika Mfumo wa Wizara wa Kukusanya maduhuli (MNRT-PORTAL) na watumishi wa vituo 16 walipata Mafunzo ya kutumia POS kwaajili ya kukusanya maduhuli.

    4.6 Uendelezaji wa Vituo vya Mambo ya Kale Mkoa wa Iringa

    Mkoa wa Iringa ni moja ya mikoa iliyopo Nyanda za Juu Kusini na umetanda kati ya latitudo 7º05˝na12º32˝kusini,nalongitude33º47˝hadi36º32˝masharikimwaMeridian.Mkoahuu una maeneo yenye mwinuko kati ya mita 1200 hadi 2000 hupata mvua nyingi kiasi cha milimita 2000. Hali ya hewa ni kuanzia 15-25 ºC. Mkoa huu una mandhari na vivutio vizuri vya utalii kama vile Isimila, jiwe la Gangilonga, Makumbusho ya Chifu Mkwawa huko Kalenga, mbuga za Ruaha ambavyo kwa pamoja vikiendelezwa na kutangazwa vitaingiza mapato. Iringa ni mojawapo ya miji ya kihistoria nchini na ilianzishwa kama kambi la jeshi wakati wa vita ya Wajerumani dhidi ya Wahehe. Wahehe waliongozwa na Chifu Mkwawa ambaye makao yake makuu yalikuwa Kalenga. Asili ya jina la Iringa ni neno la Kihehe „liliga“ lenye maana ya boma. Mji umejengwa juu ya mlima ukitazama mto Ruaha bondeni. Mji huu ulijengwa baada ya kuharibu boma la mtemi Mkwawa huko Kalenga mwaka 1894.

    4.7 Ukarabati wa BOMA la Iringa

    Katika kipindi hiki cha serikali awamu ya Tano Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia (Idara ya Mambo ya Kale na Makumbusho) kwa kushirikiana na Mkoa wa Iringa na Chuo Kikuu cha Iringa kupitia mradi wa Fahari Yetu imekarabati Boma la Mjerumani na kulifanya kuwa Makumbusho ya Mkoa wa Iringa na Kituo cha Utamaduni. Ukarabati huu ulifadhiliwa na Jumuia ya Umoja wa Ulaya(EU). Ukarabati wa Boma hilo, umewezesha kuwepo kwa Makumbusho ya Mkoa, maduka ya zawadi, studio ya mziki wa asili, na mgahawa na umeleta manufaa ya kuongeza kivutio cha utalii na fursa za ajira kwa wananchi wa Iringa. Jengo hili lilijengwa kipindi cha utawala wa Wajermani mwaka 1896 na lilijengwa kwa mawe, matofali ya kuchoma ya udongo na plasta.

  • 30

    4.7.1 Hali Halisi kabla ya Ukarabati mwaka 2015

  • 31

    4.7.2 BOMA Wakati na baada ya ukarabati

    Picha ya juu ukarabati uliofanyika kwenye BOMA kipindi cha awamu ya Tano na picha ya chini Mwonekano wa BOMA la Iringa baada ya ukarabati mwaka 2015 - 2016

  • 32

    4.7.3 BOMA kwenye Ufunguzi baada ya ukarabati

    Makumbusho hii ilizinduliwa na Balozi Dkt. Augustine Philip Mahiga Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa tarehe 25/06/2016

    Muonekano wa Makumbusho ya Mkoa wa Iringa (BOMA) baada ya Ukarabati

  • 33

    4.7.4 Uongozi wa Wizara kutembelea BOMA

    Mheshimwa Naibu, Waziri Japhet Ngailonga Hasunga (Mb) katika ziara ya Nyanda za juu Kusini Octoba mwaka 2017 moja ya eneo alilotembelea ni Makumbusho ya Mkoa wa Iringa alikutana na Uongozi wa Makumbusho ya Mkoa wa Iringa akiwemo Mhadhiri wa Chuo Kikuu Iringa, Jimson Sanga na Mkuu wa Wilaya ya Iringa vijijini Mh. Richard Kasesela. Makumbusho hii inatoa fursa nyingi za utalii wa kiutamaduni kwa wenyeji, wakazi pamoja na watu kutoka kwa nje ya Iringa na Tanzania

    4.8 Uhifadhi na uendelezaji wa Makumbusho ya Chifu Mkwawa Kalenga

    4.8.1 Historia na Umaahiri wa Chifu Mkwawa

    Chifu Mkwawa au kwa jina refu Mkwavinyika Munyigumba Mwamuyinga alikuwa chifu wa kabila la Wahehe. Jina la Mkwawa ni kifupisho cha Mukwava ambalo tena ni kifupisho cha Mukwavinyika, lililokuwa jina lake la heshima likimaanisha “kiongozi aliyetwaa nchi nyingi”. Mkwawa alizaliwa mnamo mwaka 1855 mahali palipoitwa Luhota karibu na

    Picha hii inaonesha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (Mb) (kwanza kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela ( wa pili kuanzia kushoto) wakimsikiliza Mhadhiri wa Chuo Kikuu Iringa, Jimson Sanga ambaye pia ni Meneja Msaidizi wa Mradi wa Fahari Yetu unaojishughulisha Uendelezaji na Utangazaji wa utalii Nyanda za Juu Kusini Octoba 2017 ndani ya Makumbusho hiyo.

    Picha hii inaonesha ujumbe kutoka Mkoa wa Iringa, Wizara ya Maliasili na Utalii na Idara ya Mambo ya Kale ukipata maelezo kutoka Mhadhiri wa Chuo Kikuu Iringa, Jimson Sanga katika Makumbusho hiyo

  • 34

    Iringa mjini. Alikuwa mtoto wa chifu Munyigumba aliyeaga dunia mwaka 1879. Baba yake Munyingumba aliwahi kuunganisha temi ndogo za Wahehe na makabila ya majirani kuwa dola moja. Makumbusho ya Kalenga ni kaburi (Museleum) linalohifadhi fuvu la Chifu Mkwawa kuanzia mwaka 1954. Pamoja na makaburi mengine, kaburi hilo lipo katika eneo ambalo ni makazi au makao makuu rasmi ya Chifu Mkwawa ambaye alikuwa maarufu sana.

    Chifu Mkwawa alipata umaarufu huu kufuatia kuwaunganisha wananchi wake kupinga ukoloni wa Kijerumani kwa kupigana vita na majeshi yenye silaha za sasa ya Kijerumani. Katika awamu ya kwanza ya mapambano kati yake na jeshi la Wajerumani, Chifu Mkwawa alishinda vita kwa kuliangamiza jeshi la Kijerumani chini ya kamanda Von Zelewsky katika eneo la lugalo. Mwaka 1898 mnara ulijengwa ili kuweka kukumbuka ya Wajermani waliokufa katika vita ya Wajermani na Wahehe mwaka 1891. Mnara huu umetangazwa kwenye gazeti la Serikali mwaka 1953 kwa GN Na. 89. Mnara huu umejengwa katika kijiji cha Lugalo, Kata ya Lugalo, Tarafa ya Mazombe, Wilaya ya Kilolo, Mkoa wa Iringa upo umbali wa Km 25 kutoka Iringa mjini sambamba na barabara kuu kuelekea Morogoro hadi Dar es salaam (Alison Redmayne 1968, Erick Jordan 2018)

    Hata hivyo, baadaye majeshi ya Chifu Mkwawa yalishindwa na yeye mwenyewe kuamua kujiua kwa risasi ili kujiepusha na kukamatwa na majeshi ya Kijerumani. Makazi haya ya Kalenga inasadikika yalianza kujengwa mwaka 1887 na kumalizika mwaka 1891

    4.8.2 Uanzishwaji wa Makumbusho ya Chifu Mkwawa, Kalenga

    Katika eneo hili, lililokuwa makazi ya Chifu Mkwawa katika kijiji cha Kalenga, imejengwa Makumbusho ndogo mwaka 1953 inayohifadhi fuvu la Chifu Mkwawa. Baada ya Chifu Mkwawa kujiua wanajeshi wa Kijerumani walichukua kichwa chake wakakipeleka UjerumanikwasababuzakiutafitinakiuhifadhikatikaMakumbushoyaBerlin.Tarehe09Juni, 1954 (African Heritage - http//Afrolegends.com - 2018) ikiwa ni miaka 56 tokea kifo cha Chifu Mkwawa, Gavana wa mwisho wa koloni la Kiingereza nchini Tanganyika, Sir. Edward Twining alikabidhi fuvu hilo kwa Chifu Adam Sapi Mkwawa aliyekuwa mrithi

    Katika mwezi Julai 1891 Von Zelewski aliongoza kikosi cha maafisa Wajerumani13 na askari Waafrika hasa kutoka Sudan 320, pamoja na wapagazi 113. Walikuwa na bunduki za kisasa, bunduki za mtombo na mizinga midogo. Zelewski aliwadharau Wahehe waliokuwa na mikuki na pinde tu. Kwa hiyo hakuona haja ya kutuma wapelelezi wa awali. Tarehe 17 Agosti 1891 Von Zelewski na jeshi lake walipita kwenye manyasi marefu karibu na Lugalo. Mkwawa alikuwa alimsubiri na Wahehe 3,000 walionyamaza hadi Wajerumani waliotembea kwa umbo la safu ndefu walipokuwa karibu kabisa wakawashambulia. Wajerumani walikosa muda wa kuandaa silaha zao wakashtushwa kabisa. Sehemu kubwa ya askari waliuawa katika muda wa dakika chache pamoja na jemadari von Zelewski.(Alison Redmayne 1968)

  • 35

    wa kiti cha uchifu kwa wakati huo. Kurudishwa kwa fuvu hili kulifuatia utekelezaji wa Mkataba wa Kimataifa wa Versaille wa tarehe 28 Juni, 1919: Kifungu VIII sehemu ndogo ya246.KifunguhichokilihusumakubalianoyaliyofikiwakatiyaUingerezanaUjerumanikufuatia nchi ya Ujerumani kushindwa vita vya kwanza vya dunia na hivyo makoloni yake kukabidhiwa chini ya Umoja wa Mataifa. Uangalizi wa Tanganyika ikapewa nchi ya Uingereza.

    Makumb