masharti ya chama - crdb saccos ya chama.pdf · 2014-01-09 · mpaka akidhi masharti yote ya kuwa...

30
Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited CRDB WORKERS’ SAVINGS AND CREDIT COOPERARIVE SOCIETY LIMITED MASHARTI YA CHAMA CRDB WORKERS SACCOS LTD

Upload: others

Post on 11-Feb-2020

5 views

Category:

Documents


7 download

TRANSCRIPT

Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

CRDB WORKERS’ SAVINGS AND CREDIT COOPERARIVE SOCIETY LIMITED

MASHARTI

YA

CHAMA

CRDB WORKERS SACCOS LTD

i Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

YALIYOMO

SEHEMU YA KWANZA

JINA, FUNGAMANO, ANWANI NA USAJILI ....................................................................................... 1

1. Jina, Fungamano na Anwani ............................................................................. 1

2. Usajili wa Chama ............................................................................................. 1

3. Ufafanuzi wa Maneno ....................................................................................... 1

SEHEMU YA PILI

MADHUMUNI, MAMLAKA NA WAJIBU WA CHAMA .......................................................................... 2

4. Madhumuni ya Chama hiki yatakuwa ................................................................. 2

5. Mamlaka ya Chama yatakuwa ........................................................................... 3

6. Wajibu wa Chama ............................................................................................ 3

SEHEMU YA TATU

SIFA, UTARATIBU, URITHI NA UKOMO WA KUWA MWANACHAMA ............................................ 4

7. Sifa za Kuwa Mwanachama ............................................................................... 4

8. Utaratibu wa kujiunga na Chama ....................................................................... 4

9. Ukomo wa Uanachama ..................................................................................... 4

10. Kuachishwa Uanachama ................................................................................... 5

11. Haki ya Mtu Aliyekoma Uanachama ................................................................... 6

12. Mrithi Wa Mwanachama ................................................................................... 6

SEHEMU YA NNE

WAJIBU NA HAKI ZA MWANACHAMA ................................................................................................ 6

13. Wajibu wa Mwanachama .................................................................................. 6

14. Haki za Mwanachama ....................................................................................... 7

15. Daftari la Wanachama ...................................................................................... 7

SEHEMU YA TANO

KIINGILIO, HISA, AMANA NA AKIBA ZA CHAMA ............................................................................. 8

16. Kiwango Cha Kiingilio, Hisa, Amana na Akiba ..................................................... 8

17. Kiingilio ........................................................................................................... 8

18. Hisa ................................................................................................................ 8

ii Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

19. Akiba .............................................................................................................. 9

20. Amana ............................................................................................................ 9

SEHEMU YA SITA

VYANZO NA UWEKEZAJI WA FEDHA ZA CHAMA ........................................................................... 10

21. Vyanzo vya Fedha ya Chama ni ........................................................................ 10

22. Uwekezaji wa Fedha za Chama ........................................................................ 10

SEHEMU YA SABA

MWAKA WA FEDHA, MAHESABU YA CHAMA NA MGAO WA ZIADA ........................................... 10

23. Mwaka wa Fedha ............................................................................................ 10

24. Mahesabu ya Chama ....................................................................................... 11

25. Mgao wa Ziada ............................................................................................... 11

SEHEMU YA NANE

FEDHA ZA CHAMA .............................................................................................................................. 12

26. Kuhifadhi Fedha za Chama............................................................................... 12

SEHEMU YA TISA

AKIBA NA AMANA ............................................................................................................................... 13

27. Taratibu za Uwekaji Akiba ................................................................................ 13

SEHEMU YA KUMI

MIKOPO ................................................................................................................................................ 14

28. Taratibu za Mikopo ......................................................................................... 14

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

MIKUTANO YA CHAMA ....................................................................................................................... 14

29. Aina ya Mikutano ndani ya Chama .................................................................... 14

30. Mkutano Mkuu wa Mwaka ................................................................................ 15

31. Mikutano Mikuu ya Kawaida ............................................................................. 15

32. Mkutano Mkuu Maalum ................................................................................... 16

33. Taarifa za Mikutano ......................................................................................... 16

34. Muda wa Matangazo ....................................................................................... 16

35. Mahudhurio kwenye Mikutano .......................................................................... 17

36. Uendeshaji wa Mikutano ya Chama .................................................................. 18

iii Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

SEHEMU YA KUMI NA MBILI

BODI NA KAMATI ZA CHAMA ........................................................................................................... 18

37. Bodi ya Chama ............................................................................................... 18

38. Kamati Ndogo ya Mikopo ................................................................................. 21

39. Kamati ya Usimamizi ....................................................................................... 22

SEHEMU YA KUMI NA TATU

USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA CHAMA ........................................................................................... 23

40. Usimamizi wa Shughuli za Chama ..................................................................... 23

41. Meneja ........................................................................................................... 23

42. Mhasibu ......................................................................................................... 23

43. Wawakilishi wa Chama .................................................................................... 23

SEHEMU YA KUMI NA NNE

KUFUTWA KWA CHAMA NA MENGINEYO ....................................................................................... 25

44. Kufutwa kwa Chama ....................................................................................... 25

45. Mengineyo ..................................................................................................... 25

1 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

SEHEMU YA KWANZA

JINA, FUNGAMANO, ANWANI NA USAJILI

1. Jina na Anwani:-

(a) Jina la chama litakuwa: CRDB WORKERS’ SAVINGS AND CREDIT

COOPERATIVE SOCIETY LIMITED, kwa

kifupi “CRDB Workers SACCOS Limited”;

(b) Fungamano: Wafanyakazi wa Benki ya CRDB na kampuni

zake tanzu (Benki) au Waajiriwa wa CRDB

Workers SACCOS Limited;

(c) Anwani ya Chama: S.L.P 268, DAR ES SALAAM;

(d) E-mail: [email protected]

(e) Eneo la shughuli za Chama: Mahali popote zilipo ofisi na Matawi

ya Benki

(f) Makao Makuu ya Ofisi za Chama: KATIKA OFISI ZA MAKAO MAKUU YA

CRDB BANK PLC

2. Usajili wa Chama:-

(a) Tarehe ya kuandikishwa: 11/01/2014

(b) Nambari ya kuandikishwa: 5410

(c) Idadi ya wanachama waliofanya maombi: 1,412

3. Ufafanuzi wa Maneno:

Maneno yafuatayo yanapotumika katika masharti haya yatakuwa na maana

kama inavyoelezwa hapa: -

(a) “Benki” itamaanisha “Benki ya CRDB” na kampuni zake tanzu;

(b) “Bodi ya wakurugenzi” (Board of Directors) yaani Kamati ya kuongoza

shughuli zote za kawaida zenye kuhusu chama hiki;

(c) “CRDB Workers SACCOS” AU “CRDB Workers SACCOS Limited”, AU

“Chama”, inamaanisha CRDB WORKERS SAVINGS AND CREDIT

COOPERATIVE LIMITED;

2 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

(d) “Kanuni za Uhasibu” inamaanisha kanuni za kiuhasibu kulingana na

“Bodi ya Uhasibu na Ukaguzi wa Hesabu (NBAA)”, “Sheria za Kimataifa

za Ukaguzi wa Mahesabu (IFRS)”; na Kanuni na Taratibu za kiuhasibu

kulingana na Sheria ya Ushirika;

(e) “Kiongozi” (Leader) yaani Wajumbe wote wa Bodi na Wajumbe wa

Kamati ya Usimamizi;

(f) “Mrajisi” (Registrar of Cooperative Societies) yaani Mrajisi wa Vyama

vya Ushirika Tanzania Bara;

(g) “Mtoto au Mtoto mdogo” mwenye umri chini ya miaka 18;

(h) “Mwajiri” ni CRDB Workers SACCOS Limited au Benki;

(i) “Savings and Credit Cooperative Society Limited” yaani Chama cha

Ushirika cha Akiba na Mikopo;

SEHEMU YA PILI

MADHUMUNI, MAMLAKA NA WAJIBU WA CHAMA

4. Madhumuni ya Chama hiki yatakuwa:-

(a) Dhumuni kubwa la Chama ni kustawisha na kuinua hali ya kiuchumi ya

Wanachama;

(b) Kuhamasisha na kupokea viingilio vya uanachama, Hisa, Akiba, Amana

na michango mbalimbali kutoka kwa Wanachama kwa mujibu wa

Sheria ya Ushirika;

(c) Kuweka viwango vya faida juu ya Hisa, na riba juu ya Amana na Akiba;

(d) Kutoa mikopo inavyohitajika na wanachama wake;

(e) Kukuza na kulinda fedha ya wanachama kwa:-

(i) Kuwahamasisha wafanyakazi wa Benki kujiunga kwa kununua

hisa, na kuweka akiba na amana katika Chama;

(ii) Kuwahamasisha Wanachama kuongeza hisa, amana na akiba

zao;

(iii) Kuweka kinga ya majanga (BIMA) dhidi ya fedha na rasilimali

nyingine za Chama;

3 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

(iv) Kuwekeza sehemu ya rasilimali ya chama katika maeneo

yanayoongeza tija na faida zaidi kwa wanachama;

(f) Kutoa elimu ya Ushirika na mambo mengine ya msingi kwa

Wanachama na wafanyakazi ili kukijenga Chama katika misingi ya

Ushirika;

(g) Kufanya shughuli nyingine halali kwa manufaa na ustawi wa Chama na

Wanachama;

5. Mamlaka ya Chama yatakuwa:-

(a) Kukopa fedha kutoka kwenye taasisi za fedha kwa ajili ya kuwekeza

katika maeneo yanayoleta tija;

(b) Kuanzisha na kuendeleza shughuli zozote za kiuchumi kwa manufaa ya

Wanachama kama itakavyokubaliwa na Mkutano Mkuu na kuidhinishwa

na Mrajisi wa Vyama vya Ushirika;

(c) Kufanya kazi kwa kusudi ya kufikia na kutimiza madhumuni yake kama

yalivyo ndani ya Masharti;

(d) Kutoza faini (adhabu) kwa Wanachama watakaoshindwa kurejesha

mikopo kulingana na taratibu zilizopo za Chama;

(e) Chama kitakopa baada ya kupata idhini ya Wanachama na Mrajisi wa

Vyama vya Ushirika kwa kuzingatia mambo yafuatayo:-

i. Chama hakiwezi kukopa Mkopo zaidi ya robo (1/4) – yaani

asilimia ishirini na tano (25%) ya jumla ya rasilimali zote za

Chama;

ii. Chama kitakopa kwa uamuzi wa angalau robo tatu (3/4) ya

Wanachama wake;

6. Wajibu wa Chama kwa Wanachama:-

(a) Kulinda maslahi ya Wanachama wakati wote;

(b) Kulinda Akiba, Hisa na Amana za Wanachama;

(c) Kuweka Masharti na Sera muafaka ili kulinda na kukuza rasilimali za

Chama;

4 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

SEHEMU YA TATU

SIFA, UTARATIBU, URITHI NA UKOMO WA KUWA MWANACHAMA

7. Sifa za Kuwa Mwanachama:-

(a) Awe ni mtu mwenye akili timamu na anayeaminika na wenzake;

(b) Awe ni mfanyakazi wa Benki; aliyeajiriwa kwa masharti ya kudumu au

kwa mkataba usiopungua mwaka mmoja (1), AU awe mwajiriwa wa

CRDB Workers SACCOS Limited;

(c) Awe tayari kufuata na kuheshimu masharti ya Chama na Sheria ya

Vyama vya Ushirika;

(d) Awe ametimiza umri usiopungua miaka 18;

(e) Kama ni Kikundi au Taasisi, lazima Bodi ijiridhishe Wanachama wake

wana sifa zilizotajwa hapo juu.

8. Utaratibu wa kujiunga na Chama:-

(a) Mtu anayetaka kuwa Mwanachama atajaza fomu ya maombi ya

kujiunga na chama na kuiwakilisha ofisi za CHAMA moja kwa moja au

kupitia kwa Wawakilishi wa Matawini;

(b) Bodi itajadili maombi hayo, na inaweza kukubali au kuyakataa;

(c) Mapendekezo ya Bodi yatajadiliwa na Wanachama katika Mkutano

Mkuu;

(d) Mwombaji akikubaliwa kujiunga na Chama, atalipa michango yote kwa

mujibu wa Sera na Taratibu za wakati husika;

9. Ukomo wa Uanachama:

(a) Mwanachama ataweza kukoma uanachama kwa sababu zifuatazo:-

i. Kwa mwanachama kujiuzulu mwenyewe kwa taarifa ya

maandishi;

ii. Kuachishwa uanachama kwa azimio litakaloungwa mkono na

Wanachama wasiopungua theluthi mbili (2/3) ya Wanachama

waliohudhuria katika Mkutano Mkuu huo;

iii. Mwanachama Kuchukua hisa zake zote;

5 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

iv. Kufariki kwa mwanachama;

v. Mwanachama kupoteza uwezo wake wa kiakili uliothibitishwa na

daktari;

vi. Mwanachama anapostaafu, kuachishwa au kufukuzwa kazi na

Mwajiri;

vii. Kwa sababu zozote zilizotajwa katika kifungu cha 25 cha kanuni

za Vyama vya Ushirika (Rules), 2004.

(b) Barua ya Mwanachama ya kuacha Uanachama itajadiliwa na

kuamuriwa na Bodi ndani ya kipindi cha miezi mitatu na taarifa

kupelekwa kwenye Mkutano Mkuu.

10. Kuachishwa Uanachama:

(a) Mwanachama anaweza kuachishwa uanachama kwa sababu zifuatazo:-

i. Kushindwa kutoa michango ya lazima ndani ya Chama kwa

kipindi cha miezi mitatu mfululizo bila sababu ya msingi

itakayokubalika na Bodi ya Chama; na taarifa kupelekwa kwa

kwa Mkutano Mkuu;

ii. Kutoa rushwa kwa kiongozi au mtumishi wa Chama hiki kwa nia

ya kufanyiwa upendeleo wowote ndani ya chama hiki, au

kupokea rushwa kutoka kwa kiongozi au mtumishi kwa sababu

yoyote ile;

iii. Kufanya kitendo chochote ambacho Bodi itajiridhisha kuwa ni

cha kutokuwa mwaminifu au ambacho ni kinyume na

madhumuni ya Vyama vya Ushirika vya Akiba na Mikopo;

iv. Kushindwa kulipa mkopo wake katika muda muafaka, bila ya

kuwa na sababu zinazokubalika na Bodi ya Chama;

(b) Kabla ya Mwanachama hajaachishwa uanachama wake, atapewa nafasi

ya kujitetea kwa maandishi kwa Bodi na mbele ya Mkutano Mkuu;

6 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

11. Haki ya Mtu Aliyekoma Uanachama:-

(a) Mwanachama ambaye uanachama wake umekoma:-

i. Atarudishiwa hisa na akiba zake ndani ya siku tisini (90) baada

ya kutolewa kwa maandishi ya kuacha Uanachama;

ii. Hatarejeshewa hisa zake mpaka madeni yake na ya wanachama

aliowadhamini yawe yamelipwa yote, au wadhaminiwa

kubadilisha wadhamini;

iii. Na yule ambaye kaachishwa/kaacha au kafukuzwa kazi na

Mwajiri atarudishiwa fedha zake zote mara moja baada ya

kuhakikisha hana deni na chama;

(b) Mtu aliyeacha au kufukuzwa uanachama anaweza kuomba kujiunga

tena kwa mujibu wa masharti ya Chama;

12. Mrithi Wa Mwanachama:-

(a) Kila Mwanachama atamteua mrithi wake ambaye atakuwa na haki ya

kulipwa akiba, hisa na faida zote ndani ya Chama;

(b) Mwanachama atakuwa na haki ya kubadilisha jina la mrithi pale

anapotaka;

(c) Mrithi wa Mwanachama hawezi kurithi kuendelea kuwa Mwanachama,

mpaka akidhi masharti yote ya kuwa Mwanachama katika kipengele

cha 7 cha Masharti ya haya.

SEHEMU YA NNE

WAJIBU NA HAKI ZA MWANACHAMA

13. Wajibu wa Mwanachama:-

(a) Kuwa mwaminifu na kushiriki kikamilifu katika shughuli zote za

maendeleo ya Chama;

(b) Kununua Hisa, kuweka Akiba na Amana mara kwa mara;

(c) Kukopa na Kurejesha kwa mujibu wa Masharti na Sera za Chama;

7 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

(d) Kuhudhuria Mikutano yote ya Wanachama kama ilivyoainishwa ndani

ya Masharti

14. Haki za Mwanachama:-

(a) Kuchagua au kuchaguliwa kwenye uongozi;

(b) Kupata taarifa zote za maendeleo ya Chama;

(c) Kutoa Maoni Binafsi kwa Maendeleo ya Chama;

(d) Kupata Mikopo kutoka kwenye Chama kulingana na Masharti;

(e) Kupata Stakabadhi za malipo yote anayolipa kwenye Chama;

(f) Kukishtaki Chama au Uongozi wa Chama pale anapoona kuna

ukiukwaji wa taratibu za Chama au kupotea kwa mali za Chama;

(g) Kupata riba itokanayo na Akiba na Amana zake ndani ya Chama;

(h) Kupata gawio kwenye Hisa zake zilizo ndani ya Chama

15. Daftari la Wanachama:-

(a) Chama kitakuwa na Daftari la Wanachama wote likiwa na taarifa

zifuatazo:

i. Majina ya Mwanachama

ii. Tarehe ya Kujiunga na Chama

iii. Nambari ya Uanachama

iv. Idadi na Nambari ya Stakabadhi ya Hisa na Thamani zake

v. Picha ya Mwanachama

vi. Nambari ya Shahada ya Mwanachama

(b) Taarifa hizi katika Daftarti la Wanachama zitakuwa zinaboreshwa mara

kwa mara

8 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

SEHEMU YA TANO

KIINGILIO, HISA, AMANA NA AKIBA ZA CHAMA

16. Kiwango Cha Kiingilio, Hisa, Amana na Akiba:-

(a) Viwango vya Kiingilio, Hisa na Akiba vitakuwa vikipangwa na Bodi ya

Chama na kuidhinishwa na Mkutano Mkuu;

(b) Kiwango cha Amana kitakuwa kulingana na uwezo wa Mwanachama

atakavyojiweza.

17. Kiingilio:-

(a) Mtu atakayekubaliwa kujiunga na Chama atawajibika kulipa ada ya

Kiingilio;

(b) Mwanachama hatarejeshewa Kiingilio chake endapo uanachama wake

utakoma;

(c) Kiwango cha Kiingilio kitakuwa TZS 10,000/= (Shilingi za Kitanzania

Elfu Kumi Tu);

18. Hisa:-

(a) Hakuna Mwanachama atakayeruhusiwa kumiliki hisa zaidi ya moja ya

tano (1/5) – yaani asilimia ishirini (20%) ya hisa zote za Chama;

(b) Kwa mujibu wa kifungu cha 9(a) na (b) cha masharti haya,

mwanachama anayetaka kuchukua hisa na akiba zake au sehemu,

anatakiwa kutoa taarifa ya siku 90 kwa maandishi;

(c) Mwanachama haruhusiwi kupunguza hisa zake hadi kufikia chini ya

hisa kumi;

(d) Mwanachama anaweza:-

i. Kurithisha hisa zake;

ii. Kuuza hisa zake kwa Mwanachama mwingine;

iii. Kuzihamisha kwenda kwa Mwanachama mwingine;

(e) Kila Mwanachama atakuwa na hati yake ya Hisa (Share Certificate) na

kuingizwa kwenye daftarti la Wanachama

9 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

19. Akiba:-

(a) Kila Mwanachama atatakiwa kuweka Akiba mara kwa mara ili itumike

kama kigezo cha kukopea mkopo;

(b) Mwanachama atapata faida inayotokana na Akiba zake mara moja kwa

Mwaka, kwa kadri itakavyopendekezwa na Mkutano Mkuu;

(c) Kiwango cha lazima cha Akiba cha kila Mwezi kitakatwa moja kwa moja

kutoka kwenye mshahara wa Mwanachama; ila Mwanachama anaweza

kuweka kiwango cha ziada moja kwa moja kwenye akaunti yake ndani

ya Chama;

(d) Mwanachama aliye na mkopo, hataruhusiwa kupunguza akiba zake

chini ya nusu (1/2) ya madeni yake ndani ya Chama.

(e) Kila mwanachama atatakiwa kuweka kiwango cha lazima cha Akiba;

ingawa anaruhusiwa kuweka kiwango chochote juu ya hapo kadri

awezavyo ili kuongeza Akiba zake;

(f) Mwanachama anaweza kuweka kiwango cha ziada moja kwa moja

kwenye Akaunti ya Chama iliyo Benki;

(g) Taratibu na viwango mbalimbali vya Akiba vitatajwa katika Sera na

Taratibu za Bidhaa na Huduma (Policy and Procedures for Products and

Services);

20. Amana:-

(a) Kila Mwanachama anahimizwa kufungua Akaunti na kuweka Amana

zake ndani ya Chama;

(b) Kutakuwa na aina mbalimbali za amana kulingana na mahitaji ya

wanachama;

(c) Kila Akaunti ya Amana itakuwa inalipwa faida kila mwisho wa kipindi au

mwisho wa mwaka, kulingana na Sera na Taratibu za Bidhaa na

Huduma;

(d) Viwango, gharama, utaratibu na aina mbalimbali za Amana zitakuwa

kwenye Sera na Taratibu za Bidhaa na Hududma.

10 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

SEHEMU YA SITA

VYANZO NA UWEKEZAJI WA FEDHA ZA CHAMA

21. Vyanzo vya Fedha ya Chama ni: -

(a) Akiba na Amana za wanachama;

(b) Hisa za Wanachama;

(c) Fedha zinazotokana na viingilio na michango maalum au ruzuku, na

misaada mbalimbali;

(d) Mikopo kutoka Mabenki au Taasisi nyingine za fedha;

(e) Adhabu zinazotolewa kwa wanachama;

(f) Ziada halisi ya Chama;

(g) Akiba ya lazima na malimbikizo mengine;

(h) Mapato kutokana na Vitega uchumi (investments);

(i) Mapato yatokanayo na mikopo mibaya;

(j) Mapato yatokanayo na gharama za mikopo.

22. Uwekezaji wa Fedha za Chama:-

(a) Kutoa Mikopo kwa Wanachama;

(b) Kuweka Amana kwenye Mabenki;

(c) Kuwekeza katika Hisa au vitega uchumi vingine ili kuongeza faida

katika Chama;

SEHEMU YA SABA

MWAKA WA FEDHA, MAHESABU YA CHAMA NA MGAO WA ZIADA

23. Mwaka wa Fedha:-

(a) Mwaka wa fedha wa Chama utakuwa kuanzia tarehe 01 Januari hadi

tarehe 31 Disemba ya kila mwaka;

(b) Mwaka wa fedha unaweza kubadilishwa na wanachama katika Mkutano

Mkuu

11 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

24. Mahesabu ya Chama:-

(a) Chama kitaandika vitabu na mahesabu kutunza kumbukumbu muhimu

kulingana na Sheria ya Ushirika na Kanuni za Kiuhasibu kulinga na Bodi

ya Uhasibu na Ukaguzi wa Hesabu;

(b) Wajumbe wa Bodi ya Chama watapitia mfumo wa hesabu na utunzaji

wa kumbukumbu za Chama kila mwaka kwa kushirikiana na Mkaguzi

wa Vyama au Mkuguzi mwingine atakayependekezwa na Bodi; na

kuidhinishwa na Mkutano Mkuu;

(c) Wajumbe wa Kamati ya Usimamizi watakagua vitabu na kumbukumbu

za Chama wakati wowote;

(d) Chama kitaanda taarifa za fedha kwa ajili ya ukaguzi kulingana na

Kanuni za Uhasibu;

(e) Gharama za Ukaguzi wa Chama zitalipwa na Chama;

(f) Chama kitakuwa na Sera na Mwongozo wa Kutunza Vitabu na

Kumbukumbu, na Utaratibu Maalum wa Fedha (Accounting and

Finance Manual);

(g) Chama kitafuata taratibu za uhasibu kama zinavyoainishwa na Bodi ya

Uhasibu na Ukaguzi (NBAA) katika kutunza vitabu vya hesabu na

kumbukumbu nyingine.

25. Mgao wa Ziada:-

(a) Kila mwaka Chama kitatenga kiasi kisichopungua asilimia thelathini

(30%) kutokana na faida halisi kwa ajili ya akiba ya lazima ambayo

itaweza kutumika kwa kufidia hasara zisizoweza kuepukika;

(b) Chama kitatenga asilimia kumi (10%) ya faida halisi kwa ajili ya mfuko

wa Elimu;

(c) Asilimia kumi na tano (15%) ya faida halisi itatengwa kwa ajili ya

kukombolea hisa;

(d) Asilimia kumi na tano (15%) ya faida halisi itatengwa kwa ajili ya

Madeni mabaya (bad and doubtful debts);

(e) Akiba ya lazima itabakia kuwa ni mali ya Chama hiki na haitaweza

kugawanywa isipokuwa kama Chama kimevunjwa;

12 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

(f) Bodi ya Chama inaweza kupendekeza kwa Mkutano Mkuu kuongeza

mifuko mingine iwapo Chama kina Mapato halisi ya kutosha;

(g) Baki itagawanywa kwa mgawo kwa kutumia kiwango cha hisa na

nyingine kwa ajili ya mipango ya maendeleo;

(h) Ziada iliyobaki, yaani asilimia thelathini (30%) itagawanywa kama

gawio la kwenye hisa (dividends) na shughuli mbalimbali za maendeleo

baada ya vitabu kufungwa na ukaguzi kufanywa. Hii ni pamoja na

kutoa faida kwa akiba za wanachama;

(i) Gawio sio lazima liwe kwa fedha taslimu; bali linaweza kulipwa kwa

kuongeza akiba au hisa za Mwanachama;

SEHEMU YA NANE

FEDHA ZA CHAMA

26. Kuhifadhi Fedha za Chama:-

(a) Wanachama, kupitia katika Mkutano Mkuu, wataidhinisha

mapendekezo ya Bodi juu ya Benki itakayotumika kuhifadhi Fedha za

Chama;

(b) Malipo yote ya Chama, yatafanyika kwa njia ya hundi, TISS, Internet

Banking, nk; hata hivyo Bodi inaweza kutenga kiasi chochote kidogo

(petty cash) ili kukidhi matumizi madogo ndani ya Chama;

(c) Fedha yote ya Chama isipokuwa ile inayohitajika kwa matumizi

madogomadogo itahifadhiwa kwenye Akaunti ya Chama ndani ya

Benki;

(d) Fedha ambayo haitumiki kwa mikopo kwa Wanachama yaweza

kuwekwa katika:

i) Benki.

ii) Kuwekeza katika rasilimali kama Bodi itakavyoona inafaa;

13 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

iii) Mikopo au hisa za Vyama vingine vya akiba na mikopo,

lakini visizidi asilimia ishirini na tano (25%) ya jumla ya

rasilimali ya Chama.

SEHEMU YA TISA

AKIBA NA AMANA

27. Taratibu za Uwekaji Akiba:-

(a) Kila Mwanachama atakayejiunga na Chama atapatiwa kitabu cha akiba

(pass book) ambacho kitaonyesha kiasi cha akiba na amana

alichoweka, kiasi cha mkopo alichokopa na baki ya hisa zake ndani ya

Chama;

(b) Vitabu vya akiba vitawekwa nambari zinazofuatana na mara moja

vitatolewa kwa Wanachama. Nambari ya vitabu hivi itaandikwa kwenye

daftari la Wanachama na kadi/leja yake ya akiba, amana na mikopo;

(c) Tarehe ya malipo ya hisa na kiingilio vilivyolipwa na Mwanachama

mpya viingizwe kwenye safu ya kitabu inayohusika na kuwekwa sahihi

na Meneja au mtu mwingine aliyeidhinishwa kupokea fedha; kisha

kitabu hicho apewe mwanachama kikiwa kama stakabadhi yake rasmi

na kumbukumbu ya shughuli zake zote za baadaye;

(d) Vitabu vya akiba na amana vitatunzwa na Wanachama wenyewe.

Kitabu kikipotea na upotevu huo ukathibitishwa na Bodi ya chama

kitabu kingine kitatolewa na Mwanachama atatakiwa kulipa ada ya

kiasi kitakachowekwa na Bodi ya chama;

(e) Kitabu cha akiba na amana ni budi kionyeshwe wakati wote wa kuweka

na kuchukua fedha ili watendaji waweze kuingiza kiasi kilichowekwa au

kuchukuliwa;

14 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

(f) Chama kitakuwa na Sera na Taratibu ya Bidhaa na Huduma za Akiba

na Amana itakayoelezea aina, faida na sifa za Bidhaa za Akiba na

Amana

SEHEMU YA KUMI

MIKOPO

28. Taratibu za Mikopo

(a) Mikopo itatolewa kwa Wanachama wa Chama tu;

(b) Mwanachama mpya hataweza kukopeshwa mpaka atakapokuwa na

muda wa miezi mitatu kwenye Chama kama mwanachama kamili, au

vinginevyo kwa idhini ya Bodi;

(c) Mkopo hautatolewa kwa Mwanachama yeyote zaidi ya mara tatu ya

akina zake alizonazo kwenye Chama, na hataweza kukopeshwa zaidi ya

asilimia tano (5%) ya mali yote ya chote;

(d) Chama kitakuwa na Sera na Taratibu za Bidhaa na Huduma za Mikopo

zitakazobainisha aina ya mikopo, sifa za mkopaji, utaratibu na

mchakato mzima wa kutoa mikopo kwa Wanachama.

SEHEMU YA KUMI NA MOJA

MIKUTANO YA CHAMA

29. Aina ya Mikutano ndani ya Chama:-

(a) Mkutano Mkuu wa Mwaka;

(b) Mkutano Mkuu wa Kawaida;

(c) Mkutano Mkuu Maalum

15 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

30. Mkutano Mkuu wa Mwaka:-

(a) Madaraka Makuu yanayohusu Chama yatakuwa mikononi mwa

Wanachama katika Mkutano Mkuu;

(b) Mkutano Mkuu wa mwaka wa Chama utafanyika mara baada ya

kufunga mwaka wa chama na ndani ya miezi tisa (9) baada ya mwisho

wa mwaka wa hesabu;

(c) Mambo yafuatayo lazima yajadiliwe katika Mkutano Mkuu wa mwaka:-

i. Kusoma na kuthibitisha mambo ya mkutano uliopita.

ii. Kupokea na kujadili taarifa ya mwaka ya mahesabu ya mkaguzi

(Auditor)

iii. Kupokea na Kujadili taarifa ya:

I. Bodi

II. Kamati mbalimbali

iv. Kujadili na kupitisha mgawo wa ziada kwa kuzingatia masharti

ya chama, kanuni na sheria ya Vyama vya Ushirika ya 2003;

v. Kuidhinisha ununuzi/au uuzaji wa mali ya Chama ambayo

hayakuwa kwenye yenye thamani inayozidi shilingi

10,000,000/= (Shilingi za Kitanzania Milioni Kumi Tu);

vi. Kuidhinisha makisio ya mapato na matumizi kwa mwaka

unaofuata;

vii. Kupanga posho mbalimbali kwa wasio waajiriwa wa chama;

viii. Kuzungumzia mambo mengine yanayohusu maendeleo ya

Chama kwa jumla na kutoa maelekezo ya utekelezaji kwa Bodi

ya Chama;

ix. Kuangalia na kupanga idadi ya wajumbe wa bodi ya chama.

31. Mikutano Mikuu ya Kawaida:-

(a) Kutakuwa na Mkutano Mkuu wa Kawaida angalau mara moja

utakaofanyika wakati wowote katika mwaka wa fedha wa Chama.

(b) Mambo yafuatayo yatajadiliwa katika Mkutano Mkuu wa kawaida:

i. Kuthibitisha muhtasari wa Mkutano uliopita.

ii. Kupokea na kujadili taarifa ya maendeleo ya utekelezaji kutoka

kwa Bodi ya Chama.

16 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

iii. Kuthibitisha kuingizwa na kufukuzwa kwa wanachama.

iv. Kuweka ukomo wa madeni chini ya sheria ya vyama vya

Ushirika ya 2003.

v. Kuchagua, kuwasimamisha au kuwafukuza wajumbe wa Bodi ya

chama.

vi. Kuchagua wajumbe wa kuwakilisha Chama katika Vyama na

Taasisi nyingine zinazohusika na maendeleo ya chama.

vii. Kuzungumzia mambo yote yanayohusu maendeleo ya chama.

32. Mkutano Mkuu Maalum:-

(a) Mrajisi au mtu Mwingine na aliyeidhinishwa na Mrajis anaweza kuitisha

na kusimamia Mkutano Mkuu au Mkutano Maalum;

(b) Kutakuwepo na Mkutano Mkuu Maalum wakati wowote iwapo

utaitishwa na Mrajisi kwa maombi ya maandishi ya wanachama

wasiopungua theluthi moja (1/3);

(c) Kwa Mkutano Mkuu Maalum ulioombwa na wanachama maombi lazima

yataje sababu za kutaka mkutano huo ufanyike na waombaji lazima

waweke sahihi zao na kupeleka kwa mwenyekiti wa chama na nakala

kwa Afisa Ushirika;

(d) Mkutano Mkuu Maalum hautazungumzia mambo zaidi ya yale

yaliyotakiwa kuzungumzia katika mkutano huo;

(e) Gharama zote za mkutano zitalipwa na chama.

33. Taarifa za Mikutano:-

(a) Matangazo ya Mkutano yatabandikwa katika ofisi ya Chama na

kutumwa kwenye matawi yote ya CRDB Bank LTD kwa kutumia

taratibu zinazokubalika katika sehemu hiyo. Tangazo hili litabidi

lionyeshe waziwazi tarehe ya Mkutano, saa, mahali pa mkutano na

mambo yatakayozungumziwa.

34. Muda wa Matangazo:-

(a) Muda wa matangazo ya mikutano utakuwa:

i. Kwa Mkutano Mkuu wa Mwaka si chini ya siku 21.

17 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

ii. Kwa Mkutano Mkuu ya Kawaida si chini ya siku 21.

iii. Kwa Mkutano Mkuu Maalum si chini ya siku 7.

(b) Wanachama watakumbushwa kwa njia ya simu na barua pepe kuhusu

siku ya mkutano pale itakapowezekana;

35. Mahudhurio kwenye Mikutano:-

(a) Mahudhurio katika mikutano ya chama yatabidi kuwa si chini ya nusu

ya Wanachama wote au wanachama 100, ukichukulia idadi yoyote iliyo

ndogo;

(b) Kwa mkutano maalum uliothibitishwa na Mrajisi wa Vyama vya Ushirika

idadi yoyote ya Wanachama waliohudhuria wataendesha mkutano na

yote yatakayozungumzwa ni halali;

(c) Kwa mikutano mikuu ya mwaka na kawaida, ikiwa mahudhurio

hayatoshi baada ya saa 1.30 ya saa zilizopangwa, mkutano

utaahirishwa kwa siku saba na mambo yatakayozungumzwa ni yale

yale ya mkutano ulioahirishwa. Iwapo mahudhurio hayatoshi tena

maazimio yanaweza kutolewa kwa idadi isiyopungua (2/3) ya

waliohudhuria; na maamuzi yatakayofanywa yatakuwa halali;

(d) Kwa Mkutano Mkuu maalum ulioitishwa na wanachama, Mkutano

utafutwa kabisa iwapo mahudhurio hayatoshi;

(e) Wanachama waliopo Makao Makuu ya CRDB Bank PLC na matawi

yaliyopo Dar es salaam watachukua dhamana ya kuendesha shughuli

zote za chama. Wanachama katika matawi nje ya Makao Makuu

wataendelea kuhudumiwa na Chama na mambo yafuatayo

yatazingatiwa: -

i. Viongozi wa Chama watatoka katika Makao Makuu ya Chama na

matawi yaliyopo Dar es salaam.

ii. Mikutano ya Wanachama itafanyika iwapo waliohudhuria mkutano

huo ni zaidi ya nusu ya wanachama waliopo Makao Makuu na

matawi ya Dar es salaam, au Wanachama 100, namba yeyote iliyo

chini;

18 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

iii. Kwa Mkutano Mkuu wa Mwaka, wanachama walioko kwenye

Matawi nje ya Dar es Salaam, ikiwa tawi lina Wanachama angalau

kumi (10), watamchagua mwakilishi mmoja kutoka tawi hilo ili

kuwawakilisha wenzake;

iv. Wawakilishi wa Wanachama walioko nje ya Mkoa wa Dar es

Salaam, watakuwa wanachaguliwa mara moja kwa Mwaka, na

muda wao utaisha pale tu Mkutano Mkuu wa Mwaka na Mkutano

Mkuu wa Kawaida inapomalizika

36. Uendeshaji wa Mikutano ya Chama:-

(a) Mwenyekiti wa Chama ataendesha mikutano yote isipokuwa ule

Mkutano Mkuu Maalum ulioitishwa na Mrajis, ambao utaendeshwa na

Mrajis mwenyewe au mtu atakayeteuliwa na Mrajis kuwa Mwenyekiti.

(b) Mwenyekiti akiwa hayupo, makamu wake ataongoza mkutano, na

iwapo wote wawili hawapo katika muda wa dakika 15 baada ya

mkutano kuanza mtu yeyote katika waliohudhuria atachaguliwa kuwa

mwenyekiti wa muda na ataongoza mkutano huo;

(c) Utaratibu utakaofanywa katika kuendesha mikutano mikuu ni kama

ilivyo katika kanuni ya 27 na 28 ya sheria ya Vyama vya Ushirika.

SEHEMU YA KUMI NA MBILI

BODI NA KAMATI ZA CHAMA

37. Bodi ya Chama:-

(a) Kutakuwa na Bodi ya Chama ambayo itachaguliwa na Mkutano Mkuu

wa Wanachama;

(b) Wajumbe wa Bodi hiyo watashika madaraka yao kwa muda wa miaka

tisa, theluthi moja ya Wajumbe wa Bodi watajiuzulu baada ya miaka

mitatu (3). Nusu ya Wajumbe waliobaki watajiuzulu baada ya miaka

sita [(Act Sec.63 2-3)].

19 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

(c) Utaratibu wa kujiuzulu kwa Bodi hiyo utakuwa kwa zamu na itapangwa

katika mkutano wa kwanza baada ya kuandikishwa chama. Wajumbe

wanaojiuzulu wanaruhusiwa kugombea tena nafasi ambazo zitakuwa

wazi;

(d) Hakuna mjumbe wa Bodi atakayekuwa na haki ya kudai malipo ya

mshahara au posho, isipokuwa kama ilivyoelezwa katika masharti

haya;

(e) Bodi ya chama itakuwa na wajumbe si chini ya watano na hawatazidi

tisa akiwemo mwenyekiti na makamu wake (S. 63);

(f) Bodi ya Chama itafanya mikutano yake ya kawaida mara moja kila

mwezi.

(g) Bodi inaweza kufanya mkutano usio wa kawaida wakati wowote.

Mahudhurio ya wajumbe wengi wa Bodi ya Chama yatahitajika kwa kila

mkutano;

(h) Mwenyekiti au Makamu wake wataongoza Mkutano wa Bodi. Kama

wote hawapo kikao kitamchagua mwenyekiti wa muda miongoni mwa

wajumbe waliopo;

(i) Mjumbe wa Bodi ataacha madaraka kama atafukuzwa na Mkutano

Mkuu, au sababu yoyote kama ilivyo katika kanuni ya 49 ya Kanuni za

Vyama vya Ushirika ya mwaka 2004;

(j) Mjumbe wa Bodi atakishindwa kuhudhuria vikao vitatu mfululizo bila ya

sababu inayokubaliwa na Bodi ya Utendaji, anaweza kuachishwa

uongozi na kuteuliwa Mwanachama mwingine badala yake hadi

Mkutano Mkuu unaofuata;

(k) Bodi inaweza kuchagua kamati ndogondogo kama itakavyoona inafaa,

kwa ajili ya utekelezaji bora zaidi wa kazi za Chama;

(l) Bodi ya Chama itakuwa na mamlaka ya kusimamia shughuli za kawaida

za chama, mali na kazi ambazo kwa jadi hufanyika na Bodi ya Chama

cha Ushirika;

(m) Bodi ya Chama itakuwa na wajibu wa kufanya mambo yafuatayo kwa

mujibu wa kanuni ya 44 Kanuni za Vyama vya Ushirika ya mwaka

2004:-

20 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

i) Kueneza elimu ya uwekezaji wa akiba na mikopo, kuwaelimisha

wanachama kuhusu matumizi bora ya mapato yao.

ii) Kupokea na kujadili maombi ya wanachama wapya na

kuyafikisha mbele ya Mkutano Mkuu ili kuidhinisha.

iii) Kuhakikisha kuwa wakopaji wanalipa madeni yao kama

walivyoahidi na kuwachukulia hatua za kisheria wakopaji wasio

waaminifu.

iv) Zitokeazapo nafasi katika Bodi ya Ushirika au Kamati ya Mikopo

au usimamizi kutakuwa na mtu wa kuteuliwa kwa wingi wa

kura za wajumbe walioko katika Bodi ya Utendaji ya wakati ule.

Wanakamati watakaoteuliwa vilevile watashika nafasi hizo

mpaka Mkutano mwingine mkuu wa mwaka ambako nafasi

zilizo wazi zitajazwa kwa kura na wanachama.

v) Kuweka taratibu za uendeshaji wa shughuli za akiba na mikopo

ila kwa masharti kwamba taratibu hizo zisikiuke sheria na

kanuni za vyama vya ushirika.

vi) Kuajiri kulingana na matakwa ya usimamizi wa Chama,

kusimamia na kufukuza watumishi pale inapohitajika;

vii) Kusimamia matumizi yote ya Chama isipokuwa kazi ya

kuidhinisha maombi ya mikopo kulingana na masharti ya utoaji

mikopo yaliyowekwa na Bodi hii na Mrajisi wa Vyama vya

Ushirika.

viii) Kufikisha mbele ya Mkutano Mkuu wa mwaka mapendekezo ya

makisio, na hesabu ya mapato na matumizi, mizania na taarifa

ya ukaguzi aliyothibitishwa na Mrajisi wa Vyama vya ushirika.

ix) Muhtasari wa majadiliano na maazimio yote ya Mikutano ya

Bodi ya Ushirika ni budi yaandikwe katika kitabu cha

kumbukumbu za mikutano na kutiwa sahihi na Mwenyekiti,

Katibu wa Wajumbe wote waliohudhuria.

x) Katika kuendesha shughuli za Chama, Bodi itatumia busara

kama wafanyabiashara wa kawaida, hasara yoyote itakayotijea

Chamani kutokana na Bodi kutojali wajibu wao na madaraka

waliyopewa na wanachama, itawalazimu kufidia hasara hiyo.

21 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

xi) Kusimamia kazi ya urejeshaji wa mikopo kutoka kwa

wanachama na kuidhinisha ufutaji wa mikopo ambayo

imeshindikana kabisa kulipwa.

xii) Kutoa mapendekezo ya kusimamisha uanachama wanachama

au mjumbe yeyote wa kamati ya mikopo na ya usimamizi

kutokana na tabia mbaya au kushindwa kutimiza wajibu wake

wa kazi na kupeleka mapendekezo kwa mkutano mkuu

unaofuata ili uamuzi wa mwisho utolewe.

xiii) Bodi ya Chama cha Ushirika itakuwa na madaraka kuongoza

shughuli za maendeleo ya chama hiki.

38. Kamati Ndogo ya Mikopo:-

(a) Itakuwa ni juu ya Kamati ndogo ya mikopo kuyapitia maombi yote ya

mikopo, kuhakikisha kwamba mkopo huo utakuwa na manufaa kwa

mkopaji na kuchunguza kama dhamana iliyotolewa kwa uamuzi wao

itatosha na mapatano yaliyofanywa kama ni sawa;

(b) Idadi ya Wajumbe wa Kamati ya Mikopo itakuwa ni watatu (3) ambayo

itachaguliwa na wajumbe wa Bodi kutoka miongoni mwao;

(c) Wajumbe wa kamati ndogo ya mikopo watachaguliwa kwa muda wa

miaka mitatu, ingawa wanaweza kuchaguliwa tena kwa kipindi kingine

kama ataendelea na ujumbe wa Bodi;

(d) Wajumbe wa kamati ndogo ya mikopo watachagua miongoni mwao

mwenyekiti. Katibu wa kamati hii atakuwa ni Afisa Mikopo ambaye

atatengeneza na kuweka kumbukumbu sahihi za mambo yote

yatakayofanywa na kamati ya mikopo;

(e) Shughuli za mwenyekiti na katibu zinaweza kufanywa na mtu mmoja.

(f) Kamati ya mikopo itafanya mikutano kama vile shughuli za Chama hiki

zitakavyohitaji lakini siyo chini ya mara moja kwa kila mwezi. Taarifa ya

mikutano hiyo itatolewa kwa wanachama jinsi itakavyoamuliwa na

kamati hiyo mara kwa mara.

(g) Idadi ya juu ya jumla ya wanakamati wote itatosha kuendesha

shughuli katika mikutano.

22 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

(h) Kwa wingi wa kura, Kamati ya Mikopo inaweza kumchagua Afisa au

Maofisa wa Mikopo kufanya kazi kama itakavyohitajika na Kamati na

kumpa uwezo wa kuidhinisha mikopo kwa kadri ya kiasi

kitakachowekwa na Kamati.

(i) Mchakato na undanii wa kazi za Kamati ya Mikopo utabainishwa katika

Sera na Taratibu za Bidhaa na Huduma ya Mikopo

39. Kamati ya Usimamizi:-

(a) Kamati ya usimamizi itachaguliwa na Wanachama na itakuwa na

Wajumbe wasiozidi watatu ambao ni Wanachama wa Chama;

(b) Mwanachama yeyote wa Kamati ya Mikopo au mtumishi yeyote wa

Chama hiki hatastahili kuchaguliwa katika Kamati hii;

(c) Wajumbe wa Kamati hii watashika madaraka yao kwa muda wa miaka

mitatu, na wanaweza kuchaguliwa tena;

(d) Theluthi moja ya wajumbe itajiuzulu kila mwaka na wanaweza

kuchaguliwa tena.

(e) Wajumbe wa Kamati ya usimamizi watatengeneza utaratibu wao wa

kutosheleza kazi za Kamati hiyo. Katibu atatengeneza, atahifadhi na

atazichunguza kumbukumbu zote pamoja na hatua zitakazochukuliwa

na Kamati hiyo. Kazi ya Mwenyekiti na Katibu inaweza kushikwa na

mtu mmoja.

(f) Kamati hii itakuwa na kazi zifuatazo:

i) Usimamizi na ukaguzi wa fedha na rasilimali zote za Chama kwa

niaba ya Wanachama;

ii) Itakuwa na uwezo wa kuamuru ufanyike uchunguzi pamoja na

ukaguzi wa vitabu wakati wote itakapoona inafaa;

iii) Kutayarisha taarifa ya maandishi juu hali ya fedha na huduma

zitolewazo kwa Wanachama kwa Kamati ya Utendaji na Mkutano

Mkuu na nakala kwa Afisa Ushirika wa Wilaya, Mrajis wa Mkoa,

mara mbili kwa mwaka.

23 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

SEHEMU YA KUMI NA TATU

USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA CHAMA

40. Usimamizi wa Shughuli za Chama:-

(a) Bodi itaajiri watu wenye uwezo ili wasimamie shughuli za kila siku za

Chama, akiwemo Meneja;

(b) Shughuli zote za Chama zitasimamiwa na Meneja;

(c) Bodi itaweza kuajiri wafanyakazi mbalimbali kulingana na mahitaji ili

kuendesha shughuli za Chama kwa ufanisi zaidi;

41. Meneja:-

(a) Chama kitamwajiri Meneja ili kusimamia kazi za kila siku za chama kwa

niaba ya Bodi ya Chama.

(b) Kazi za meneja zitakuwa ni kwa mujibu wa kanuni ya 50 ya Kanuni za

Vyama vya Ushirika ya mwaka 2004, na zitabainishwa katika Sera na

Taratibu za Ajira kwa Watumishi wa Chama;

42. Mhasibu:-

(a) Chama kitakuwa na Mhasibu mwenye sifa na ujuzi wa kutunza hesabu

na kumbukumbu za Chama;

(b) Kazi za Mhasibu zitabainishwa katika Sera na Taratibu za Ajira kwa

Watumishi wa Chama.

43. Wawakilishi wa Chama Mikoani:-

(a) Ili kusimamia kwa karibu shughuli za Chama, kutakuwa na Wawakilishi

wa Chama katika Matawi ya Benki yaliyo Mikoani;

(b) Tawi lililo Mikoani lenye wanachama angalau kumi (10) litakuwa na

Mwakilishi mmoja wa Chama atakayekuwa anachaguliwa na

wanachama wenzake tawini, kila mwanzo wa Mwaka wa fedha;

(c) Kwa matawi ambayo hayajafikisha wanachama kumi (10) au idadi ya

wafanyakazi ni ndogo, Mwakilishi wa Chama katika tawi la karibu

24 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

lililokidhi idadi ya wanachama, itampasa kuhudumia matawi haya,

mpaka pale yatakapokuwa na Mwakilishi wao;

(d) Wawakilishi wa Chama watakuwa ndo wawakilishi wa Wanachama

katika Mkutano Mkuu wa Mwaka;

(e) Wawakilishi wa Chama watalipwa posho kulingana na uwezo wa

Chama;

(f) Wasimamizi watapewa Hadidu za Rejea na malengo wanayotakiwa

kufikia kwa Mwaka;

(g) Wasimamizi wa Shughuli za Chama watakuwa na kazi zifuatazo:-

i. Kuhamasisha wafanyakazi wote walio kwenye tawi kuwa

wanachama katika Chama;

ii. Kuelimisha wanachama na wasio wanachama kuhusiana na

utaratibu, bidhaa, sera na masharti ya Chama ili kuongeza

muamuko katika kushiriki kwenye shughuli za Chama;

iii. Kutoa maelezo juu ya maswali mbalimbali wanayouliza

wanachama, au wafanyakazi wengine wa Benki, kuhusiana na

Chama na kuwasilisha maoni kwa Meneja wa Chama;

iv. Kuhamasisha wanachama kutumia bidhaa mbalimbali za Chama

– kuongeza Akiba, kuweka Amana, kukopa na kununua Hisa

zaidi;

v. Kutoa taarifa ya hali ya Ushindani dhidi ya bidhaa za Chama

katika Tawi au Taasisi nyingine zinazowahudumia wafanyakazi

wa Benki Tawini;

vi. Kuwawakilisha wanachama katika Mkutano Mkuu wa Mwaka;

vii. Kuandaa au kuratibu mafunzo ya kwa wanachama katika

matawi yao;

viii. Kuratibu mawazo mapya kutoka kwa wanachama na wasio

wanachama kwenye tawi juu ya uboreshaji wa shughuli na

bidhaa za Chama;

25 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

SEHEMU YA KUMI NA NNE

KUFUTWA KWA CHAMA NA MENGINEYO

44. Kufutwa kwa Chama:-

(a) Chama hiki kinaweza kufutwa katika daftari la vyama kwa amri ya

Mrajis chini ya kifungu cha 100 cha sheria ya Vyama vya Ushirika ya

2003.

45. Mengineyo:-

(a) Sera na Taratibu za Chama – Chama kitakuwa na Sera na Taratibu

mbalimbali katika kuhakikisha kinasimamia rasilimali na kuendesha

shughuli zake, kama ifuatavyo:-

i) Sera na Taratibu za Bidhaa na Huduma za Mikopo;

ii) Sera na Taratibu za Bidhaa na Huduma za Amana na Akiba;

iii) Sera na Taratibu za Fedha na Hesabu ya Chama;

iv) Sera na Taratibu za Ajira kwa Watumishi wa Chama;

v) Sera na Taratibu za Uendeshaji wa Chama;

(b) Siri juu taarifa za Chama – wajumbe wa Bodi, Kamati mbalimbali, na

watumishi wa Chama, watatunza siri kuhusu maisha binafsi ya

Wanachama, isipokuwa masuala ya utoaji na ukusanyaji wa mikopo

ambayo Bodi ya Chama inaweza kuchukua hatua zozote za lazima dhidi

ya wasiokuwa waaminifu;

(c) Bima ya Uaminifu – Chama kitakata bima ya Uaminifu (Fidelity

Insurance) kulinda rasilimali za Chama dhidi udanganyifu na wizi

utakaoweza kufanywa na Wajumbe wa Bodi, Kamati ya Usimamizi na

Watumishi wa Chama;

(d) Upatikanaji wa Taarifa za Chama – Vitabu vya hesabu na kumbukumbu

nyingine za Chama hiki zinaweza kuchunguzwa wakati wowote na

wajumbe wa Kamati mbalimbali za Chama. Mwanachama yeyote

atakuwa na haki ya kutazama masharti, mizania, muhtasari ya

mikutano mikuu na nyaraka za Mrajis.

26 Copyright ©2014. CRDB Workers SACCOS Limited

(e) Migogoro au Malalamiko – migogoro au malalamiko yoyote kuhusu

masharti au huduma za Chama hiki kwa wanachama wa sasa au wa

zamani na kati ya wanachama ipelekwe kwa Mrajisi wa Vyama vya

Ushirika ambaye uamuzi wake kuhusu shauri lolote utakuwa wa

mwisho.

(f) Uzembe katika Uendeshaji – Iwapo chama kitapata hasara kutokana na

uzembe, ubadhirifu au matumizi mabaya ya fedha, Wajumbe wa Bodi

watawajibika kufidia hasara yote iliyotokana na utendaji wao;

(g) Mapitio ya Masharti – Masharti haya, kama kuna marekebisho au

maboresho yoyote, yatapendekezwa na kupitishwa na wanachama

katika mikutano ya Wanachama. Mapitio ya Masharti haya yatakuwa ni

mara moja kwa mwaka.

(h) Mapendekezo ya masharti haya yameandaliwa na Wajumbe wa Bodi na

Kamati ya Usimamizi – kama walivyooredheshwa hapa chini, kwa ajili

ya kupitishwa na wanachama:-

Na. Jina la Mjumbe wa

Bodi Cheo Saini

1 JOHN FIDELIS KOMBA Makamu Mwenyekiti wa Bodi

2 OMARY KILIMA Mjumbe wa Bodi

3 LEONARD KOSIA Mjumbe wa Bodi

4 MAKAYE MAO Mjumbe wa Bodi

5 THEOPHIL AKARO Mjumbe wa Bodi

6 HAMISI MHINI Mjumbe wa Bodi

7 ANNA MSOFE Mjumbe wa Bodi

8 BENJAMINI KOMBA Mjumbe wa Bodi

9 GODWIN SEMUNYU Mjumbe wa Bodi

10 Leevan Maro Mjumbe Kamati ya Usimamizi

11 John Mtindo Mjumbe Kamati ya Usimamizi

12 Negwako Mvungi Mjumbe Kamati ya Usimamizi