mwongozo wa kufundisha afya katika shule na jamii kupitia ...shn.cloudapp.net/shared...

20
Mwongozo wa kufundisha afya katika shule na jamii kupitia wafanyakazi wa afya

Upload: others

Post on 25-Jan-2021

19 views

Category:

Documents


0 download

TRANSCRIPT

  • Mwongozo wa kufundisha afyakatika shule na jamii kupitia

    wafanyakazi wa afya

  • Hati zifuatazo zimeandikwa kwa ushirikiano kati ya Partnership for child

    Development (PCD) yani Ushirikiano wa Maendeleo ya Mtoto, na Serikali ya

    Kenya, Taasisi ya Utafiti ya Kenya ya magonjwa (KEMRI) na International Rescue

    Committee, Umoja wa Mataifa wa Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) na Shirika la

    Chakula Duniani (WFP).

    Maudhui imeanzishwa kushughulikia changamoto za afya na maarifa, mitazamo na

    mazoea ya jamii la Turkana na kambi la Kakuma zinazohusiana na; tabia ya Kula,

    viini vya ungojwa na maambukizi, Trachoma, Usafi wa Maji na Mazingira. Taarifa

    zilikusanywa kupitia utafiti wa shule za msingi nafasihi ya mapitio ya data sekondari ili

    kuhakikisha ujumbe pia kuti maanani umuhimu wa mazingiramaalum na utamaduni.

    Picha ni hati miliki ya Ushirikiano wa Maendeleo ya Watoto(PCD), Imperial College London.

    Maelezo [email protected]

  • 3

    Mathumuni ya kijitabu hiki ni kupatia wafanyakazi wa afya wa kambi ya wakimbizi kakuma na

    habari kuwasaidia kufundisha na kuwasiliana kuhusu madhara ya kutokula chakula bora

    magonjwa yanayo wadhuru siku hizi kambini na maeneo jirani. Kijitabu hiki ni mojawapo ya

    maelekezo ya kuchangia kuhusu afya ya jamii pamoja na mazingira bora ya afya, maelezo ya

    lishe bora kwa madhumuni ya kuboresha afya ya jamii kambini na maeneo jirani. Kulingana na

    habari zilizopatikana baada ya kukadiria mahitaji, kijitabu hiki kinapeana habari muhimu

    ambayo wenyeji wanaweza kutumia kujikinga pamoja na familia zao magonjwa pamoja na

    vyakula wanavyo tumia kwa lishe bora.

    Kitabu hiki kita patiana elimu na hoja pia habari kuhusu uzuiaji wa magonjwa, ulaji wa lishe

    bora na wakati wa kutafuta matibabu ya magonjwa yanayo wakabili. Lishe bora ina umuhimu

    mkubwa kwa afya ya mama na watoto, inachangia pakubwa ukuaji wa mtoto, ukomavu wa

    akili na pia kuzuia uambukizi wa magonjwa. Jumbe za usafi na mazingira bora ina faidi watu

    kwa maarifa ambayo yata badilisha tabia na kuzuia uambukizaji wa magonjwa tofauti tofauti.

    Mwisho, itachangia kwa habari kuhusu magonjwa na uzuiaji na pia wakati wa kuhitaji

    matibabu ambayo itasaidia jamii kushughulikia afya na kuwapa nafasi nzuri kuishi kwenye

    mazingira ya afya na maisha mazuri.

    Kitangulizi

  • 4

    Kitabu hiki kina ujumbe kwa mambo manne

    ambayo yanaweza kusaidia wafanya kazi wa

    afya kupeana ujumbe wa afya na lishe bora

    kwa wananchi wa kakuma. Kila sehemu

    inaelekeza kiini cha habari, ikieleza hali ya

    afya na magonjwa na njia mwafaka za

    kujizuia pamoja na jamii na familia wasipate

    Marathi na pia kusambaza magonjwa.

    Sehemu ya mwisho inazungumzia mamboa

    yote yanayoweza kusaidia uzuiaji wa

    magonjwa katha na Marathi mengineyo.

    Kiini cha habari zifuatazo hapa chini zinaweza

    kusaidia kujumuisha jamii na kusaidia

    uelewaji wa hatari za magonjwa na pia

    wanacho takiwa kufanya kujizuia na lishe

    isiyo faa.

    Ishara na Muundo

    Elimu ya lishe – Umuhimu wa lishe bora una zungumziwa kwa ufasaha,

    ambapo kula chakula chenye madini yote na vyenye aina tofauti za

    vyakula pamoja na kuzidisha madini bora ya afya ya watu Kaunti ya

    Turkana.

    Kuepuka ugonjwa wa macho – Sehemu hii inzungumzia zaidi ugonjwa

    wa macho unaosababishwa na viini ambavyo vinapatikana sana ndani ya

    kambi ya Kakuma. Mbinu zinaelezwa jinsi ya kuzuia ugonjwa wa macho

    kutumia tahathari – SAFE (upasuaji, madawa, kuosha uso, kuboresha

    mazingira).

    Malaria – Ni ugonjwa mbaya ambao unsambazwa na mbu. Sehemu hii

    inatujuza kuhusu vimelea (vidudu) na kueleza vile vinavyo smbazwa kwa

    wanadamu, dalili na jinsi ya kutibu na pia njiwa za kujikinga kuambikizwa

    na ugonjwa wa malaria.

    Zuia Minyoo! – Sehemu hii inahusika na minyoo ya tumbo, vile

    wafanyavyo mwilini, vile zina sambazwa jinsi ya kujizuia kupata minyoo na

    la kufanya ukiwa umeambukizwa.

    Maji, mazingira na usafio (WASH) – Sehemu hii inazungumzia

    umuhimu wa kuosha mikono mara kwa mara na pia uso kuzuia magonjwa

    kwa jamii. Inatufunza kitakacho tokes kukiwa hakuna maji, mazingira bora

    ama usafi na pia la kufanya kutahathari na la kufanya ukiwa mgonjwa. Ina

    sisitiza sana umuhimu wa kutumia choo na kuosha mikono baada ya

    kutoka chooni na pia wakati wa kupika chakula.

    Ishara:

    1.

    2.

    3.

    4.

    5.

  • Lishe hafifu inatokea wakayi watu hawapati

    chakula chenye nguvu, protein, mafuta,

    vitamin na madini muhimu kutoka kwa

    chakula wanacho kula. Haya madini

    yanahitajika kwenye mwili ili kufanikisha,

    hasa lishe duni inasababishi motto kutokuwa

    inavyo hitajika na huweza pia kusababisha

    unyonge na umbilikimo, pia iki tatiza uwezo

    wa mtoto kusoma vizuri. Baathi ya lishe duni

    zinapotokea (chini ya miaka mitano) ni

    vigumu sana kurekebika. Ndio maana kuna

    umuhimu wa kutengneza chakula kizuri kwa

    jamii na watoto wadogo na pia kuhakikisha

    watoto wanakula chakula cha kutosho.

    Pamoja na hivyo, hata kama chakula ni kizuri,

    kama mtu ana njaa siku yeyote ile ni vigumu

    kuzingatia na kufanya mambo magumu, ni

    vizuri kila familia kula chakula bora na chenye

    madini muhimu.

    Vyakula viwe na vitu muhimu kama vile GO,

    GROW and GLOW – ‘ G Tatu. Hizi aina tatu

    za vyakula vinaelezwa hapa.

    Kuendelesha jamii elimu juu ya vyakula

    vinavyo faa kula ina changia sana kubadilisha

    tabia zao za kubadili tabia zao wale vyakula

    vya kujenga miili yao

    1. Ni nini lishe bora? Kwanini ni muhimu?

    Lishe bora ni chakula chenye anina tatu

    za vyakula; chakula cha kujenga mwili,

    vyakula vya kupatia mwili nguvu,

    vyakula vya kuzuia magonja.

    Hizi aina tatu za vyakula vinakumbukwa kama

    GO, GROW and GLOW vyakula – ‘ Gs’Tatu.

    • Vyakula vya GO vyakula vyenye

    kupatiana nguvu (carbohydrates kama

    vile nafaka na vyakula kama mihogo, viazi

    5

    1: Elimu ya lishe

    Baraza la kufundisha 1: Vyakula vyenye Afya

    Umuhimu wa kula vyakula

    vyenye afya: ‘GLOW GROW na

    GO’ Ujumbe na aina tofaiti za

    vyakula

    Tunawezaje kuongeza uzuri

    wa chakula chetu?

    Uduni wa madini muhimu

    Micronutrient deficiencies

    Vyakula vilivyo jaza madini

    muhimu wa kuvijua.

    Ishara:

    1.

    2.

    3.

    4.

  • 6

    tamu, karoti na mafuta). Vinatupa nguvu

    ya kuendelea na kazi ngumu na kwa mda

    mrefu, Tusipokula vyakula vya kuongeza

    nguvu mara nyingi tutakuwa na uchovu

    na huwezi kufanya shughuli za kila siku.

    • Vyakula vya kukua – GROW ni vya

    kujenga mwili (kama nyama,

    maharagwe and maziwa), Vinatu fanya

    kukuwa, omekana na nguvu na wenye

    afya. Usipokula vyakula vya kujenga

    mwili, watoto wanaweza kuwa na mwili

    mdogo sana dhidi ya umri wao.

    • Vyakula vya GLOW ni vyakula vya

    kukinga mwilivikiwa vime jaa vitamin

    na nadini (matunda na mboga za

    majani). (Vina saidia kukuza akili

    (ubongo) na kufanya mwili kuwa na

    nguvu na kukuwa vizuri. Vinatusaidia

    kukinga magonjwa na pia husaidia baada

    ya kupona ugonjwa. Tusipokula vyakula

    vyakuzuia kwa wingi tunaweza kuugua

    nmara kwa marana tuta pona pole pole

    sana.

    2. Tunaweza je kuboresha vyakula vyetu

    na vitu tunavyo kula?

    Ili kuwa na afya bora na pia kusaidia familia

    kuwa na afya jamii wanahimizwa kutengeneza

    vyakula vya nyumbani hivi:

    • Tengeneza aina tofauti za vyakula kutoka

    kwa vikundi vya GO, GROW and GLOW

    • Ongeza ukulaji wa vitamin na madini kwa

    kula matunda safi, mboga za majani. ma.

    Machungwa, matunda ya njano na

    mboga za majani mabichi zina lishe bora.

    • Lima shamba dogo la mboga pamoja na

    matunda ili yaliwe yangali mazuri.

    • Himiza mama kunyonyesha watoto wao

    hadi miezi sita’ Maziwa ya mama yana

    lishe zote mototo ana hitaji ili kukua na

    mguvu na pia kuzuia maambukizi ya

    magonjwa. Kusitisha unyonyeshaji wa

    motto yaweza kusababisha kukua kwa

    shida na kusababisha motto apate

    magonjwa katha.

    • Kula vyakula kama nyama za ngombe,

    mbuzi, samaki na kuku ambavyo vina

    madini muhimu yanayoweza kuzuia

    ukosefu wa damu. Ukiwa huna damu ya

    kutosha, kuna kuwa na ukosefu wa hewa

    mwilini. Hii husababisha uchovu,

    usumbufu, kukosa hewa na huweza

    kuzimia.

    • Usipike mboga zaidi, hii ina sababisha

    madini muhimu kupotea ndanin ya maji

    hivyo kuharibu. Pika kidogo tuu ndio

    upate madini ya sawa.

    3. Kuongeza madini, kwa chakula

    Madini ya aina Fulani yana hitajika kwa mwili

    kwa asili mia kidogo kidogo. Ukosefu wa hayo

    madini husababisha mwili kukosa vitu vya

    muhimu na huwa sana kwa watoto. Kwenye

    sehemu hii madini muhimu ya afya ya jamii

    yana zungumziwa hapa, yanapopatikana, na

    muhimu wake kwa mwili, ukosefu na jinsi ya

    kuzungumzia kupitia kuongeza madini

    kwenye vyakula.

    4. Kutambua madini, kazi zinazofanya,

    na shida zinazoletwa kwa upungufu

    wake.

    Madini ndani ya vyakula yana hitajika

    mwilini na vitu vilivyo hai kwa maisha

    yao yote. Madini hutumika kwa mambo

    mengi kwa maish ya wanadamu. Madini

    huchangia sehemu nyingi za maisha. Madini

    inayo maslahi katika wizara ya afya ni

    Vitamin A, Iodine, Zinki na iron. Ukosefu wa

    haya madini kwa maisha ya kila siku yana

    julikana kama Ukosefu. Ukosefu wa haya

    madini husababishwa na:

    • Mchanga mahali Fulani una kosa madini

    Fulani.

    • Vyakula vya jamii Fulani havina madini

    muhimu.

    • Magonjwa ya aina Fulani yana sababisha

    ukosefu wa madini Fulani.

  • 7

    Vitamini A

    Madini yaIodini

    Madini yachuma

    Madini yaZinc

    Maziwa, mayai,

    maini, mboga za majani

    kama vile spinachi,

    sukuma wiki na

    machungwa, matunda,

    karoti, malenge, viazi

    tamuna papayu

    Chumvi iliyo na iodini,

    maziwa ya ngombe na

    mayai

    Nyama, samaki,

    maini, spinachi,

    mayai, mboga za

    majani

    Nyama, kuku, samaki,

    maziwa, nafaka na

    njugu

    • Ni muhimu kwa afya ya macho na kuona

    vizuri. Pia inafanya ngozi kuwa nadhifu na

    yenye afya. Ina zuia kuhara, ukambe,

    utapiamulo.

    • Ukosefu a vitamini A husababisha kuto

    ona vizuri na pia upofu wa usiku.

    • Inasadia mwili katika kupumua na kukua kwa

    misuli. Ni muhimu sana kwa kukua na

    kuongeza nguvu ya ubongo na neva.

    • Iodini hupatikana kwenye vyakula vinavyo

    pandwa mchngani wenye hayo madini kwa

    wingi. Mchanga usio namadini ya iodine

    unapatikana sehemu za milimani.

    • Ukosefu wa iodini leads husababisha ugonjwa

    wa goita (uvimbe kwenye shingo).

    • Inweza kuwa hali mbaya sana hasa kwa

    mama wajawazito kusababisha kuzaa

    watoto wenye uzani mdogo, uavia mimba na

    watoto walemavu.

    • Husaidia damu kuwa na afya nzuri. Kama

    huli vya kutosha inasababisha ukosefu wa

    damu, uchovu, uvuvu, kizunguzungu na

    kuumwa na kichwa.

    • Husaidi kufanya mwili kuwa na afya na

    kuendeleza ukuaji wa mototo na baru baru.

    • Ukosefu wa madini ya zinc ina sababisha

    kutokua na magonjwa kama vile kuhara.

    Baathi ya mathara yanaelezwa hapa:

    Ukosefu wa madini yeyote ni vigumu san kutambua. Kuzuia ni kujaribu kula vyakula vyenye

    hayo madini na chakula cha muhimu.

    Aina ya madini yanapotoka Kazi yake mwilini

  • 8

    5. Mazungumzo juu ya kuongeza madini

    kwa chakula

    Ili kuzuia ukosefu wa madini kwa jamii,

    vyakula Fulani vya weza kuongezewa madini

    ambapo vitaminni, na madini vinachanganywa

    kuongeza lishe za muhimu.

    Waulize jamii kama wanajua hivi vyakula

    ambavyo vimeongezwa madini.

    6. Kuhakikisha umekula vyakula vilivyo

    ongezwa madini muhimu

    Serikali ya Kenya imesema kuna aina Fulani

    ya vyakula vya vinavyo weza kuongezewa

    madini:

    • Unga wa ngano – umeongezwa Zinc and

    chuma

    • Unga wa mahindi – umeongezwa Zinc

    and chuma

    • Chumvi – imeongezwa Iodini

    • Mafuta ya kupikia – yameongezwa

    vitamini A

    Kanuni: Zungumzia kuhusu ana nyingi

    za vyakula ambavyo wako navyo hapo

    nyumbani na uliza kama kuna vyakula

    vilivyo ongezewa madini ama vyaweza

    kuongezewa madini.

    Eleza kwamba ni vizuri kununua vyakula ambavyo vimeongezwa madini na vitamin kila wakati

    iwezekanavyo ili kuwa na afya nzuri. Pia tuangalie vile vyakula vinavyo fungwa, kama vile

    chumvi, sukari, ma futa ili kuwa na afya bora nyumbani.

    Eleza vyakula vyote vilivyo ongezwa

    madini Kenya vina alama ya kuthihirisha.

    Onyesha hiyo alama. Uliza kama

    nyumbani wana chakula chenye hiyo alama

  • 9

    Taswira

    Trachoma ni ungonjwa unaosabishwa na

    vimelea na hatimaye kusababisha upofu na

    huambukizwa na mikono michafu, nguo na nzi

    ambao hubeba vimelea hivyo. Mapema kabla

    ya maambukizi, trachoma huwa haina dalili,

    lakinimaambukizi husababisha muwasho,

    macho mekundu na kutoa usaa. Dalili zingine

    ni kuwashwa kwa macho na kuathiriwa na

    mwangaza mkali kwa macho. Vimelea

    husambazwa sana na kati ya watoto wadogo

    na hatimaye kusababisha upofu wa macho.

    Trachomahuathiri jamii maskini, na wanaoshi

    katika misongamano na pia wanaoishi bila

    maji safi. Jamii zinazoishi maeneo kame na

    kavu pia huathirika pakubwa. Uzuiaji wa

    maambukizi huhusishwa sana na uoshaji wa

    uso (ambao hupunguza uvujaji wa macho

    ambayo husababisha maambukizi na pia nzi),

    mazingira safi na uwepo wa maji safi

    piahupunguza maambukizi.

    Upofu wa macho unaweza kuzuiwa, wakati

    haswa ubora wa mazingira safi umetiliwa

    maanani na jamii zote. Pia unaweza kuzuiwa

    kwa kutumia maji safi, kunawa nyuso na

    sabuni na pia mikono. Utafiti unaonyesha

    kuwa, kupunguza kunya mahali ambapo

    hakuna vyoo ni muhimu katika kupunguza

    maambukizi haya ya trachoma na

    kipindupindu. Mikakati ya WHO ni kuangamiza

    ugonjwa wa trachoma hapo mwaka wa 2020

    wakitumia mikakati inayofahamika kama

    SAFE (Surgery, Antibiotics, Facial cleanliness

    and Envirnmental improvement).

    Ni muhimu kwa jamii zinazokabiliwa na

    maambukizi kufahamu jinsi ya kujikinga

    kutokana na maambukizi haya sas na pia kwa

    siku zijazo na lipi la kufanya iwapo

    wataambukizwa. Ni muhimu pia kuzitia moyo

    jamii zilizoathirika kutafuta huduma za

    matibabu kwa nja ya madawa ama upasuaji

    kabla ya kupofuka macho.

    Maudhui

    Maelezo yafuatayo yananuiwa kusaidia jamii

    na elimu ya kuikinga dhidi ya trachoma.

    Sehemu ifuatayo imepeana vipengele muhimu

    vya afya kuhusu tabia zitakazosaidia kuzuia

    maambukizi hayo.

    1. Trachoma ni nini?

    Trachoma ni ugonjwa wa maambukizi

    ya macho unaosababishwa na uchafu

    (vimelea). Hatimaye, husababisha upofu wa

    macho kwani husababishakubambuka kwa

    kope za macho – kwanza ugonjwa huu ndio

    kiini kikuu kinachosababisha upofu ambao

    hatimaye unaweza kuzuiwa.

    2: SAFE from Trachoma

    Trachoma ni nini?

    Husambazwaje?

    Tutawezaje kusitisha

    ugonjwa huu?

    Hutibiwa vipi ugonjwa huu?

    Vipengele:

    1.

    2.

    3.

    4.

  • 10

    2. Trachoma husambazwaje?

    Trachoma husababishwa na uchafu na

    vimelea, pia trachoma inaeza ambukizwa

    kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine kupitia

    uhusiano wa karibu hususani kwa vitu

    vilivyoathirika kutokana na ugonjwa huo.

    Trachoma huambukizwa haswa wakati kitu

    kimegusa jicho lililoathirika na baadaye

    kugusa jicho ambalo halija athirika, kwa

    mfano:

    • Taweli, vitambaa vya mkono na

    karatasi ya chooni

    • Vidole

    • Nzi

    3. Tutawezaje sitisha/komesha

    trachoma?

    Usambazaji wa Trachoma unaweza

    komeshwa kupitia aina tofauti za

    utendakazi.Tunafahamu SAFE.

    S is for Surgery: Baadhi ya watuwalioambukizwa trachoma kwa muda mrefu

    wanaweza fanyiwa upasuaji ili kurekebisha

    macho yao.

    A is for Antibiotics: Baadhi ya watuwalioambukizwa na vimelea hivyo wapate

    madawa ili kuuwa viini hivyo.

    F is for Facial cleanliness: Kuweka usokuwa msafi ili kuzuia nzi kubeba viini hivyo

    kwa macho.

    E is for Environmental improvement:Kwa kuimarisha usafi wa shule na nyumba,

    na matumizi ya vyoo, unaeweza punguza

    nzi karibu na wewe na hatimaye kupunguza

    uwezekano wa kupata viini

    vinavyosababisha trachoma.

    Upasuaji na madawa yanahitajika kwa visa muhimu, lakini tunaweza kuhusika kwa sasa ili

    kuzuia ogonjwa wa trachoma. Kuweka uso na pia uimarishaji wa usafi wa shuleni na nymbani

    utaweza kupunguza nafasi za uambukizaji wa trachoma.

    Shughuli: Katika kiwango cha boma na pia kila mhusika ama wahusika wa boma, angalia

    vitu ama shughuli ambazo zinaweza changia sana katika maambukizi ya trachoma na pia

    vitu vinavyoweza kuzuia usambazaji huo.

    Baadhi ya vitu hivyo ni: Nyumba safi, jiko. Matumizi ya choo ama ufukiaji wa kinyesi.

    Uoshaji wa uso na usaidizi wa watoto wa changa kunawa mikono.

    Unapotembea katika kila boma, angalia vitu vizuri na vibaya kwa wanajamii. Elezea athari

    zilizoko,(kwa mfano uwepo wa nzi kwa nyuso za watoto) na jinsi ya kuzizuia (mfano kwa

    kunawa uso na kuweka mazingara safi).

  • 11

    3: Malaria

    Utangulizi

    Malaria ni ugonjwa unaosababishwa na mbu.

    Huathiri mamilioni ya watu ulimwenguni

    mzima na pia husababisha ugonjwa kwa

    watoto na wamama waja wazito. Viini

    vyenyewe hutambulikana kama Plasmodium

    ambavyo huishi kwa damu. Mbu zilizoathirika

    na viini hivyo husababisha ugonjwa huo

    kupitia kuuma wakati inapofyonza damu.

    Walioambukizwa malaria huwa wagonjwa

    sana, wakiwa na homa kali, kuhara, kutapika,

    kuumwa na kichwa au kuhisi baridi mwilini.

    Huhisi kuchoka kwa sababu ya upungufu wa

    damu mwilini kwani viini hivyo vya

    plasmodium huzaana na kuongezeka mwilini.

    Kwa watoto, na pia wamama waja wazito,

    malaria yaweza kuwaathiri zaidi. Tiba ya

    haraka ni kumeza tembe za malaria ili

    kupunguza ueneaji wa viini hivyo. Watu pia

    wanaweza kujikinga kwa kulala ndani ya

    vyandarua kwani mbu zinazosababisha

    malaria huuma usiku. Matumizi ya vyandarua

    ama unyunyiziaji wa dawa kwa manyumba pia

    husaidia kuuwa mbu kabla ikuume na

    kusababisha madhara.

    Maudhui

    Agenda zifuatazo zinanuiwa kuhamasisha

    jamii kuhusu athari za malaria, utoaji wa

    mafunzo ya kujizuia wao na familia zao

    kutokana na malaria na kugundua dalili za

    malaria ili kutoa matibabu mapema.

    1. Malaria ni nini?

    Malaria ni ugonjwa unaosababisha kifo.

    Hufanya watu kuwa wanyonge na kushindwa

    na kufanya kazi ama pia kusoma vizuri, na

    husababishwa na mbu. Unaposhikwa na

    malaria, mtu huhisi uchovu, homa, kuumwa

    na kichwa ama pia kuendesha is a killer

    disease. Viini vya malaria hujulikana kama

    Plasmodium na vidogo sana zaidi ya mbu.

    Vinapokuwa ndani ya mwili, huongezeka na

    mwishowe kumaliza chembechembe za damu

    hivyo kusababisha ukosefu wa damu mwilini.

    2. Huambukizwaje?

    Malaria huambukizwa kupitia mbu.

    Mbu aina ya Anopheles ndo huhusika sana.

    Huishi katika kila nchi ote ulimwenguni

    ambapo viwango vya joto ni shwari.

    Wakati mwengine inaweza maanisha malaria

    ni ugonjwa wa msimu. Huwa wakati wa mvua

    pekee. Mbu ya kike huitaji maji kulea mayai.

    Ni muhimu basi kupunguza maji

    yaliyosimama karibu na nyumba na kufunika

    vyombo vya maji karibu na maeneo yenu ili

    kupunguza hali hii. Mbu ambayo haijaathirkia

    huathirika inapouma mtu aliyeathirika.

    3. Nani yuko hatarini?

    Kila mtu aliyeumwa na mbu aliyeathirika

    yumo hatarni, lakini watoto wachanga na

    wamama waliowjswszito wamo hatarini zaidi

    na wanaweza kuaga kfuatia ugonjwa huo. Ni

    muhimu basi endapo mtu wa jamii yuko na

    malaria umsaidie apate matibabu.

    Wengine huibuwa kinga sababu ya kukaa na

    viini hivyo kwa muda mrefu, hii ndio sababu

    watoto na waliokuja karibuni wamo katika

    hatari ya kuuguwa na malaria.

    4. Hutibiwaje?

    Iwapo unashuku ama unajua mtu

    aliyeathirika na ugonjwa huu, ni muhimu

    kupata usaidizi wa kimatibabu katika kituo

    cha afya. Tiba ni kupeana dawa za malaria.

    Ikiwa hali hii itasalia kama haijatibiwa,

    huenda ikasababisha kifo.

    Malaria ni nini?

    Huambukizwaje?

    Nani yuko hatarini?

    Hutibiwaje?

    Uzuizi wa dawa za malaria

    dhidi ya kinga ni nini?

    Tunawezaje kuzuia maambukizi

    ya malaria?

    Vipengele:

    1.

    2.

    3.

    4.

    5.

    6.

  • 12

    5. Uzuizi wa dawa za malaria dhidi ya

    kinga ni nini?

    Huu ni ule wakati viini vya malaria, kwa muda

    hushindwa kuhisi makali ya dawa na hivyo

    kuwa sugu katika kukabiliana na viini hivyo.

    Mgonjwa hushindwa kupata afueni hata baada

    ya kumeza tembe hizo. Hii ni hatari kwa

    sababu matibabu watakayopokea

    hayatawasaidia. Tukio hili linatendeka sana

    ulimwenguni na sana ni kwa sababu ya dawa

    duni ama kutomaliza dawa zote unapopewa

    kwa matibabu. Ni muhimu kuhakikisha dawa

    ni za kiwango kizuri. Ni muhimu pia

    kuhakikisha na anameza kiwango sawa cha

    dawa hizo alizopewa mpaka apate nafuu.

    Ni muhimu pia kuhakikisha dawa zinazofanya

    kazi zafanya!

    6. Unaweza kujizuiaje na wengine kupata

    malaria?

    Kulala chini ya chandarua huzuia mbu kuuma

    kwani mbu za malaria huuma usiku. Hii ni

    muhimu kwa watoto wachanga katika jamii

    na vile vile wamama wajawazito. Ni muhimu

    pia kulala chini ya chandarua ikiwa

    umeambukizwa malaria kwani huzuia mbu

    kutoathirika. Vyandarua vinafaa kufunika

    mwenye amelala na kuchomekezwa chini ya

    godoro Mashimo ama alama zilizobuniwa kwa

    chandarua hicho zafaa kurekebishwa haraka

    ili kuzuia mbu. Kuvaa nguo zinazofunika

    mkono na miguuwakati wa usiku pia husaidia.

    Ni muhimu kuzuia watoto wachanga kwa

    kutumia njia hii.

    Dawa ya kufukiza ni kemikali inayoweza

    kuuwa mbu au kupunguza maisha ya mbu a

    hivyo kuuma watu wachache. Vyandarua na

    kunyunyuzia vyumba na dawa hizi mwishowe

    husaidia kuzuia mbu kutouma. Dawa hizi za

    kemikalli zinafaa kunyunyiziwa kila baada ya

    miezi 6 hadi mwaka mmoja.

    Ikiwa una chandarua cha kudumu. kinafaa

    kubadilishwa bssds ys miaka 3.

    Mbu aina ya Anopheles hupenda kuishi kwa

    maji, ziwa, kidimbwi, na pia mosquitoes like

    to breed in water, lakes, ponds and even little

    pools of water made in potholes and ditches.

    Ikiwezekana hakikisha ya kuwa hakuna maji

    yaliyotulia karibu na nyumba.

    Shughuli : Uliza mwenye nyumba kama wana vyandarua vya mbu?Uliza

    kuonyeshwa. Elezea tofautikati ya LLIN na chandarua kinachostahili kutibiwa kila

    baada ya mwaka.

    Ikiwa kuna mashimo kwa chandarua elezea sababu ya mashimo hayo na jinsi

    yanaweza kurekebishwa.

    Onyesha njia nzuri na mwafaka ya kulala kwa chandarua hicho. (completely covered

    and with the edges of the net tucked into the mattress).

    Uliza mwenye nyumba walichokuwa wakifanya kwa kitanda usiku uliopita? Elezea

    umuhimu wa kujifunika usiku, kuwa kwa nyumba na kuzuia kuumwa na mbu wakati

    wa msimu.

  • Taswira

    Soil-transmitted helminths (STH) ni minyoo

    ambazo huishi kwa tumbo na husambazwa

    kupitia mchanga, mikono, na wakati

    mwenginekupitia kwa chakula ambacho

    hakijapikwa vizuri ama kusafishwa vizuri na

    huwa na mayai ya Minyoo. Maambukizi

    husababisha uchovu, kuumwa na tumbo na

    kufura kitambi. Baada ya muda Minyoo hizo

    huchangia kutohudhuria shule na matokeo

    duni na pia kiwango cha chini cha lishe kwa

    ukuaji na maendeleo. Kwa watu wazima, kuna

    shida ukuaji na uwezo wa kufanya kazi na

    kubidika katika utendaji majukumu ya siku

    kwa siku kwani Minyoo huishi kwa tumbo na

    hula chakula kilichonuiwa hivyo basi kudorora

    kiafya na kutokuwa vyema.

    Maudhui

    Zifuatazo ni ajenda za mafunzo kwa lengo la

    kuwafahamisha wanachama wa jumuiya

    hatari ya maambukizi ya vimelea minyoo, na

    njia ambazo wanaweza kujilinda na kulinda

    familia kupitia tabia ya usafi na jinsi ya

    kuvunja mzunguko wa kuambukizwa. Lengo

    la ujumbe wa afya ni muhimu kusaidia

    kuzingatia kuwa natabia ya usafi.

    1. Minyoo ni nini?

    Elezea wanajamii kwamaba Minyoo huishi

    kwa tumbo na kuzuia chakula na madini

    kufika katika sehemu zinazostahili za miili

    ya watot. Maambukizi na Minyoo

    huwafanya kuchoka, kuumwa na tumbo na

    kuwafanya kuhisi wanyonge. Kwa watoto.

    maambukizi huzuia ukuaji na pia

    huzuia kutohudhuria shule na hatimaye

    kupata matokeo duni. Kwa watu wazima,

    na pia watoto, mambukizi husababisha

    ugumu wa kufanya kazi vyema za siku

    baada ya siku. Kuna aina tatu ya

    maambukizi ya STH: hookworm,

    roundworm, and whipworm.

    13

    4: ZUIA minyoo!

    Minyoo ni nini?

    Huambukizwaje?

    Tunawezaje kusitisha tatizo

    hili la minyoo?

    Maana ya Echinococcus jinnsi

    ya kuizuia

    Vipengele:

    1.

    2.

    3.

    4.

  • 14

    2. Huambukizwaje?

    Elezea kwamba Minyoo hutaga mayai

    ambayo hutoka kwa tumbo kupitia kinnyesi

    na kuambukiza watu wengine kupitia ngozi,

    chakula na mikono ambayo haikusafishwa

    vizuri baada ya kugusa mayai yaliyo kwa

    kinyesi.

    Mayai ya Hookworm huanguliwa kwa kinyesi

    na kutmbea mahali mtu alitupa kinyesi kupitia

    kwa miguu.

    Mayai ya Roundworm na whipworm huganda

    kwa mikono na chakula kutoka nje. Kula

    kutumia mikono chafu ama kuweka mikono

    michafu husababisha maambukizi.

    3. Tunawezaje kusitisha tatizo hili la

    minyoo?

    Minyoo zinaweza kuzuiwa kwa njia tofauti:

    1. Kutumia choo kila mara

    2. Kunawa mikono baada ya kutumia

    choo, kuosha motto na baada ya kula.

    3. Kuvaa viatu.

    4. Kupokea matibabu ya Minyoo mara

    moja kila mwaka.

    Elezea kuwa utumizi wa choo huzuia watu

    wengine kukanyaga kinyes na hatimaye

    kuambukizwa hookworm, na pia hueka

    kinyesi mbali na watu wengine na mikono.

    Mayai ya wadudu wengine hukaa kwa muda

    mrefu katika mazingira, hii inamaanisha

    yanaweza kuchukuliwa kwa urahisi bila

    ufahamu wa kujua umegusa kinyesi

    Eleza umuhimu wa kunawa mikono:kunawa

    mikono na sabuni baada ya kuenda choo

    huangua mayai ya wadudu hawa endapo

    yataganda kwa mikono na hivyo kuifanya

    mikono kuwa salama kucheza na marafiki

    ama kula. Minyoo yengine huishi kwa

    mchanga, kwa hivyo ni vizuri kunawa mikono

    baada ya kucheza na mchanga ama kutoka

    shambani.

    Kuvaa viatu pia huzuia maambukizi ya

    hookworm ambazo huishi kwa mchangana

    karibu na nyumba pia. Zinaweza kuganda

    kwa ngozi na kutambaa ndani, kabla ziingie

    kwa tumbo.

    Kupokea matibabu mara moja kila mwaka

    huangamiza minyookatika mwili na hatimaye

    kupunguza idadi ya Minyoo. Madawa haya ni

    salama na unahitaji tu tembe moja! Tembelea

    kituo chako cha afya upate matibabu.

    4. Echinococcus na jinsi ya kuizuia

    Echinococcus ni aina nyingine ya Minyoo

    ambayo kwa kawaida haishi kwa binadamu,

    bali huishi kwa mbwa na ng’ombe, kondoo na

    mbuzi pia huwa na Minyoo hizi. Kwa kawaida,

    njia ya maambukizi huwa ni kati ya mbwa na

    wanyama wanaofugwa, wakiambukiza kupitia

    nyama ya ng’ombe ama mbuzi (kupitia kwa

    mbwa) na kutokakwa kinyesi cha mbwa

    ikirudi kwa ng’ombe. Wakati mwengine, watu

    huambukizwa kwa kula kinyesi cha mbwa ka

    bahati mbaya na hatimaye kusababisha

    ugonjwa wa hydatid. Hii hutokea kutokana na

    uchafu, mikono michafu ama kunywa maji

    kutoka kwa kidimbwi kilichowachwa wazi.

    Ugonjwa huu ni vigumu kupata matibabu kwa

    hiyo ni vyema mtu kujikinga kwa mara ya

    kwanza. Njia za kuzuia maambukizi haya ni

    kama ifuatavyo:

    • Kunawa mikono kabla ya kugusa chakula

    kila mara

    • Kutibu maji yaliyochotwa kutokakwa

    kidimbwi kilichowachwa wazi kabla ya

    kunywa.

  • Taswira

    Uhaba wa maji na usafi duni wa kiafya yote

    haya yamesababisha maambukizi kupitia

    uchafu kama vile kinyesi. WASH yaani Water,

    Sanitation and Hygiene ni muhimu katika

    kuzuia magonjwa kwa hali kama vile

    kuharisha trachoma na maambukizi ya

    wadudu. Kwa muktasari, maji safi huzuia

    usambazaji wa magonjwa yanayohusiana na

    maji kama vile kuharisha na kipindupindu.

    Kuharisha ni baadhi ya magonjwa matatu

    ambayo husababisha vifo kwa watoto.

    Vile vile, usafi wa maji huzuia usambazaji wa

    magonjwa kama vile trachoma na magonjwa

    mengine yanayosababishwa na wadudu.

    Maambukizi ya

    magonjwa haya

    yanaweza kutokea

    kupitia hali duni za

    kiafya kwa sababu ya

    uhaba wa maji safi ya

    kuosha.

    Mbinu za usafi, kama vile kuongeza

    matumizi ya vyoo inaweza kusaidia kuweka

    kinyesi na vitu vingine vinavyosababisha

    maambukizi mbali na watu na hivyo kuzuia

    nzi kuzaa. Kinyesi kwa mara nyingi huweka

    mayai ya wadudu na pia uchafu. Hookworm

    kwa mfano hupatikana kwa kinyesi na

    inaweza kusambazwa kupitia kutembea kwa

    kinyesi na kutonawa mikono kabla ya kula na

    kutayarisha chakula.

    Mabadiliko kuhusu

    huduma za WASH ni

    lazima ziambatane na

    mabadiliko ya

    mapendekezo kuhusu

    afya, ambayo ndo

    maana elimu ya afya na

    habari ni muhimu.

    Unawaji wa kawaida wa mikono baada ya

    kutumia choo na kabla ya kutayarisha chakula

    unaweza kupuguza mizigo mingi ya

    magonjwa na athari zake.

    Maudhui

    Agenda za mafunzo zifuatazo zimelenga

    kuhamasisha wahusika wa jamii kuhus njia

    ambazo wanaweza kujikinga wao pamoja na

    jamii zao kutokana na vimelea na viini

    vinavyosababisha maambukizi. Kiini kikuu cha

    ujumbe wa afya ni vipi maambukizi ya

    vimelea na viini vinaweza kuafikiwa kupitia

    uoshaji wa mikono, matumizi ya vyoo safi na

    uvaaji wa viatu.

    1. Kwa nini uwekaji wa mikono na nyuso

    ni muhimu?

    Magonjwa mengi husababishwa na uchafu

    ama viini ambavyo husambaa kupitia kwa

    mikono michafu na mazingira machafu.

    Magonjwa haya ni Minyoo, trachoma na

    kipindupindu.

    Elezea jamii na wenye nyumbas: Viini vingi

    huwa kwa kinyesi na inaweza kukupea

    ugonjwa iwapo utakula ama kunywa kwa

    bahati mbaya. Huwa ni vidogo mno, kwa hiyo

    hatuwezi kuviona na ni muhimu mtu kuwa

    muangalifu.

    Kwa nini uwekaji safi wa

    mikono na nyuso ni muhimu?

    Kuharisha ni nini na ni vipi

    inaweza kutibiwa?

    Ni vipi tunaweza kudumisha

    usafi wa mikono nyuso?

    Wakati muhimu wa

    kutekeleza uoashaji a mikono

    Jua lini na vile utaweza

    kutibu maji kabla ya kunywa.

    Vipengele:

    1.

    2.

    3.

    4.

    5.

    15

    5: Maji na Usafi wa Mazingira and wa mwili

  • 16

    Viini i vinaweza kukusababisha ukawa

    mgonjwa na kufanya tumbo kuwa na shida na

    hatimaye kuharisha. Viini hivi ni vimelea na

    Minyoo ambavyo ni vidogo mno. Huanza

    kidogokwa kimo na hatimaye kukuwa kwa

    urefu wa zaidi 35cm

    E lezea jamii kwa vile viini viko kwa mchanga

    ni muhimu kuepuka yafuatayo:

    • Matumizi ya choo kumaanisha watu

    hawatagusa kinyesi

    • Kunawa mikono kumaanisha hutashika

    viini au hata kula na mikono chafu.

    • Kuweka choo kuwa kisafi kumaanisha

    hutabeba uchafu unapoenda choo

    • Kutoenda choo ama kunya karibu na maji

    husambaza viini kupitia kwa maji.

    • Kuvaa viatu.

    Hatua hizi pia ni muhimu kwa kuzuia

    trachoma: kujiweka msafi na nyumba yako

    na shule itaondoa nzi ambazo husababisha

    kuenea kwa trachoma.

    2. Kuharisha ni nini na ni vipi kunaweza

    kutibiwa?

    Uliza mwenye jamii jinsi anavyoeza kuelezea

    ya kwamba kuna kuharisha ?

    Eleza kwamba: DKuharisha hutokana na

    kula chakula ama maji machafuyaliyo na viini

    hivyo. Kunaweza sababishwa na kutumia

    mikono chafu.

    Dalili za kuendesha ni kama kunya damu,

    ama kutoa choo laini kwa siku kwa muda wa

    siku tatu.

    Husababisha kuishiwa na maji mwilini. Watoto

    wachanga wanaweza poteza uhai sababu ya

    kuishiwa na maji mwilini.

    Lipi la kufanya ikiwa kuna mtu katika jamii

    ambaye anaharisha?

    Eleza kwamba: Ni muhimu kuhakikisha

    kwamba mgonjwa anakunywa maji mengi na

    kula chakula kilicho na madini ili kustiri

    upotevu wa maji mwilini. Kwa

    kawaidakikombe kimoja (250ml) cha maji

    kwa kila kipindi.

    Oral Rehydration Therapy pia husaidia na

    endapo atakuwa mgonjwa sana, ORS pia

    husaidi mwili.

    Eleza njia ya kutengeza ORS nyumbani

    ukitumia yafuatayo:

    • Vijiko 6 vya sukari.

    • Kijiko ½ teaspoon chumvi.

    • Litre moja ya maji masafi yaliyotibiwa.

    Elezea pia ni muhimu kuhakikisha ya kwamba

    vipimo ni kamili.

  • 17

    3. Jinsi ya kuweka uso na mikono yako

    kuwa safi

    Eleza jinsi ya kunawa mikonos:

    1. Loa mikono yako na maji safi

    2. Weka sabuni kwa mikono yote

    3. Sunza mikono ukitumia maji safi

    Ikiwa sabuni haipo, tumia jivu Kunawa uso

    fanya hivyo pia.

    4. Ni wakati gani unafaa kunawa mikono

    na uso?

    • Wahusika wote wa jamii wanapaswa

    kunawa nyuso zao kila siku kupunguza

    athari za kupta trachoma.

    • Unafaa kunawa mikono na sabuni ama

    jivu baada ya kuenda chooni ili kupunguza

    viini.

    • Unafaa kunawa mikono kabala ya kula

    chakula ama kutayarisha chakula kuzuia

    maambukizi.

    • Mikono inafaa kusafishwa baada ya

    kubadiliisha mtoto.

    • Mikono inafaa kusafishwa kabla ya

    kunyonyesha.

    5. Kunywa maji masafi

    Maji yaliyochotwa kutoka kwa mto ama

    kidimbwi kilichowazi yanafaa kutibiwa kabla

    ya matumizi ili kupunguza viini na uchafu na

    hatimaye kuifanya kuwa salama. Kwa mfano:

    • Kuchemsha maji: maji yanafaa kuwa

    yakichemka kwa muda wa dakika 10.

    • Kutibu na aquatabs, PUR.

    • Kutumia chlorine: 1/8 yakijiko kidogo

    cha unga huo kwa lita 10 za maji. Unga

    huo unafaa kuwa mkavu na kuhifadhiwa

    kwa mkebe uliofunikwa. Maji na Chlorine

    yanafaa yatulie kwa muda wa dakika 30.

    • Kuua vini vya ungojwa vilivyomo

    ndani ya maji kwa kutumia nguvu za

    miali ya jua: Jua hua na miyale ambayo

    pia huaribu viini vinavyosababisha

    maradhi. Acha maji yatulie kwa chupa

    kwa muda masaa matano.

  • 18

    Maelezo

  • Maelezo

    19

  • Partnership for Child Development

    Imperial College London

    School of Public Health

    Norfolk Place

    London

    W2 1PG

    www.schoolsandhealth.org

    @schoolshealth