ripoti ya kamati ya kuchunguza na kudhibiti · pdf fileubadhirifu wa fedha za serikali na...

Download RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI · PDF fileubadhirifu wa fedha za Serikali na ubadhirifu na ufujaji wa mali za Taasisi hizo, ... Miradi mingi ya TASAF inayohusiana na Ufugaji,

If you can't read please download the document

Upload: lamdat

Post on 07-Feb-2018

607 views

Category:

Documents


114 download

TRANSCRIPT

  • 1

    RIPOTI YA KAMATI YA KUCHUNGUZA NA KUDHIBITI HESABU ZA SERIKALI

    NA MASHIRIKA (P.A.C) YA BARAZA LA WAWAKILISHI, ZANZIBAR, 2012/2013.

    SEHEMU YA KWANZA:

    1.0 UTANGULIZI:

    Katika Historia ya Kamati za Baraza la Wawakilishi tokea kuanzishwa kwake mwaka 1980,

    Kamati ya Kuchunguza na Kudhibiti Hesabu za Serikali (P.A.C) imeanza kuwepo tokea mwaka

    huo (1980), na katika kufanya kazi zake, pamoja na kuwa na majukumu mengi, jukumu maarufu

    linalotarajiwa kuwanyiwa kazi kila mwaka ni kuchunguza na kutoa ripoti yake juu ya hesabu za

    mwaka na matumizi ya fedha za Serikali na Mashirika yake na hesabu nyengine zozote

    zitakazowasilishwa mbele ya Baraza kupitia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za

    Serikali.

    Kwa kawaida, ripoti hiyo ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu huwa ni moja kwa kila

    mwaka, na imetokezea mwaka 2009/2010, Kamati ilifanyia kazi Ripoti tatu za Mdhibiti na

    Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa wakati mmoja, lakini mwaka huu, Kamati imefanyia

    kazi Ripoti tano (Mbili za Ukaguzi wa Hesabu, na 3 za Thamani halisi ya fedha (value for

    money) kwa pamoja.

    Katika kuzifanyia kazi Ripoti hizo, Kamati imegundua namna Wizara na Taasisi mbali mbali za

    Serikali zinavyotekeleza majukumu yao kwa mnasaba wa hoja mbali mbali zilizoripotiwa na

    Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu. Aidha, kuna hoja mbali mbali zimepata majibu, na

    nyingi hazijapata majibu ya kuridhisha. Kibaya zaidi, Kamati imegundua kuwepo kwa

    ubadhirifu wa fedha za Serikali na ubadhirifu na ufujaji wa mali za Taasisi hizo, huku Sheria ya

    Fedha na Kanuni zake za mwaka 2005 pamoja na Sheria ya Manunuzi na Ugavi wa Mali za

    Serikali na Kanuni zake, zinaendelea kuvunjwa. Hali hii inaisikitisha sana Kamati, ambayo kwa

    muda mrefu sasa inaendelea kusisitiza haja ya kufuatwa kwa Sheria hizo ipasavyo.

    1.1 MAJUKUMU YA KAMATI:

    Kamati inatekeleza majukumu yake kwa mnasaba wa Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Sheria

    Namba 4 ya mwaka 2007, Sheria Namba 12 na Sheria Namba 9 za mwaka 2005 (pamoja na

    kanuni zao), na Kanuni za Baraza la Wawakilihi, Zanzibar. Kwa upande wa toleo la mwaka

    2012, Kamati inatekeleza majukumu yake zaidi kupitia kanuni ya 118(2) ya Kanuni za Baraza,

    ambayo hapa chini tunainukuu:

    (a) Kuchunguza na kutoa taarifa juu ya hesabu za mwaka za matumizi ya fedha za Serikali na Mashirika yake na hesabu nyengine zozote zitakazowasilishwa mbele ya

    Baraza kupitia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

    (b) Kuchambua na kutafakari ripoti yeyote ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu pale ambapo Rais aliagiza ukaguzi huo ufanywe.

  • 2

    (c) Kuchunguza kwa njia yeyote inayofaa mambo yote yanayohusu hesabu za Serikali na asasi zake.

    (d) Kutoa Ripoti yake baada ya kufanya uchunguzi kuhusiana na matumizi ya ziada ya fedha iliyotolewa kwa mwaka wa fedha unaohusika.

    (e) Kufuatilia utekelezaji wa maagizo ya Kamati yaliyotolewa kwenye Ripoti ya Kamati ya mwaka uliotangulia.

    (3) Katika kufanya kazi zake Kamati ya PAC itakuwa na wajibu wa kuchunguza kama:

    a. Fedha zilizooneshwa katika makadirio ya Matumizi ya Serikali na

    Mashirika yake zimetumika kama iliyvokubaliwa;

    b. Matumizi yalikuwa chini ya mamlaka iliyohusika; na

    c. Matumizi yaliyofanywa yalizingatia thamani halisi ya fedha.

    1.2 WAJUMBE WA KAMATI:

    Kamati ya Kuchunguza na Kudhibiti Hesabu za Serikali na Mashirika kwa mwaka 2012/2013,

    inaundwa na Wajumbe 8 na Makatibu 2. Wajumbe wa Kamati ni hawa wafuatao:

    1. Mhe. Omar Ali Shehe Mwenyekiti 2. Mhe. Fatma Mbarouk Said Makamo Mwenyekiti 3. Mhe. Abdalla Juma Abdalla Mjumbe 4. Mhe. Farida Amour Mohammed Mjumbe 5. Mhe. Mbarouk Wadi Mussa (Mtando) Mjumbe 6. Mhe. Mohammed Mbwana Hamad Mjumbe 7. Mhe. Shadya Mohd Suleiman Mjumbe 8. Mhe. Shamsi Vuai Nahodha Mjumbe.

    Aidha, kwa upande wa Makatibu (ambao ndio Sekretarieti ya Kamati), kazi zote za uratibu wa

    Kamati, zimeratibiwa na Watendaji wafuatao:

    1. Ndg. Amour Mohd Amour Katibu. 2. Ndg. Othman Ali Haji Katibu

    1.3 REJEA ZA KAZI:

    Katika kutekeleza jukumu lake lililoainishwa na Kanuni ya 118(2)(a) ya Kanuni za Baraza la

    Wawakilishi, toleo la 2012, Kamati imefuatilia Ripoti tano za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa

    Hesabu za Serikali. Ripoti hizo ni hizi zifuatazo:

    1) Ripoti ya Ukaguzi Yakinifu wa Miradi ya Maendeleo ya Wananchi na Miradi ya TASAF, kwa mwaka wa fedha 2009/2010.

  • 3

    2) Ripoti ya Ukaguzi Yakinifu wa Udhibiti na Uhifadhi wa Mali za Kudumu za Serikali, kwa mwaka wa fedha 2009/2010.

    3) Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu kwa Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali, kwa mwaka wa fedha 2009/2010.

    4) Ripoti ya Ukaguzi wa Hesabu kwa Mawizara, Mashirika na Taasisi za Serikali, kwa mwaka wa fedha 2010/2011.

    5) Ripoti ya Ukaguzi Yakinifu kwa Miradi ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa mwaka wa fedha 2010/2011.

    Mbali na Ufuatiliaji huo wa Ripoti hizo, Kamati kwa kutumia kanuni ya 118(2)(c) ya Kanuni za

    Baraza la Wawakilishi, Kamati pia ilifuatilia uchambuzi wa Mapato na Matumizi kwa Baadhi ya

    Taasisi na Mashirika ya Serikali kwa mwaka 2010/2011, ili kuangalia kwa namna gani Taasisi

    hizo zinakusanya na zinatumia fedha za umma kwa mujibu wa taratibu za Sheria zilizowekwa.

    1.4 UHUSIANO ULIOPO BAINA YA KAMATI YA PAC NA AFISI YA MDHIBITI

    NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZANZIBAR.

    Kwa kawaida, baada ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, kuwasilisha Ripoti

    yake ya ukaguzi katika Baraza la Wawakilishi, kazi inayofuata ni Ripoti hiyo kuwasilishwa na

    kukabidhiwa kwa Kamati ya Kuchunguza Hesabu za Serikali na Mashirika (P.A.C), kwa lengo la

    kuifanyia kazi, na baada ya kazi hiyo, Kamati nayo hutakiwa kuwasilisha ripoti yake Barazani.

    Hali hii kwa namna yoyote ile, inazifanya Taasisi hizi mbili kuwa na mashirikiano ya karibu

    mno kila wakati.

    Aidha, Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu inashirikiana na Kamati ya P.A.C katika

    ufuatiliaji na utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewea na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa

    Hesabu katika ripoti yake. Na takriban Afisi ya Mdhibiti na Kamati ya P.A.C zinasimamia kwa

    pamoja dhana nzima ya matumizi ya fedha za umma kwa mujibu wa Sheria na taratibu

    zilizowekwa. Kwa namna moja ama nyengine, Afisi hii ya Mdhibiti na Kamati hii ya P.A.C, ni

    vigumu kuzitenganisha. Katika hali kama hii, ni wazi kwamba, kazi ya kukagua, kuchunguza na

    kudhibiti fedha za Serikali ni ngumu mno na inahitaji moyo wa kizalendo. Lakini ni muhimu

    mno kwa Serikali, na Serikali inayojali maslahi na ustawi wa wananchi wake, kama ilivyo kwa

    Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, hufanya kila njia kuwepesisha utekelezaji wa majukumu ya

    Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, pamoja na Kamati ya Kuchunguza

    na Kudhibiti Hesabu za Serikali.

    Ili kuunganisha spirit ya uzalendo na kusimamia ipasavyo majukumu haya mazito, lazima

    changamoto zinazoikabili Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, ziondolewe mara

    moja, ili kuweka wepesi na kujenga ujasiri wa watumishi wa Afisi hii, wa kudhibiti hesabu za

    Serikali. Hili katika utekelezaji wake, litaanza kwa kupiga kelele juu ya maslahi madogo ya

  • 4

    watendaji wa Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu. Kamati imezoea kulipigia kelele

    suala hili zaidi ya miaka mitano iliyopita, na itaendelea kufanya hivyo, kwa kuamini kwamba,

    iwapo tutajenga imani na ukinaifu kwa wakaguzi wa fedha za Umma, tutakuwa tumeshajenga

    ngome ya kufichuliwa kwa wabadhirifu wa mali za umma.

    Aidha, katika kuzipa uwezo Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu pamoja na Kamati

    ya P.A.C, ni kuzipa wepesi katika kutekeleza Sheria zinazohusiana na utekelezaji mzima wa

    majukumu yao. Kwa mfano kwa kuwa kuna mapungufu mengi ya kiutendaji katika sheria yake

    namba 11 ya 2003 ya Uanzishwaji Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, na kwa

    kuwa Sheria Namba 12 ya mwaka 2005 na Namba 9 ya mwaka 2005 tayari zinahitaji

    kurekebishwa kutokana na ama kuwemo kwa baadhi ya vifungu vya sheria hizo vinavyopingana

    na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984; ama sheria za kimataifa za ukaguzi au hata kupitwa na

    wakati, basi ni wazi kwamba, kufanyiwa marekebisho ya haraka kwa Sheria hizo, ni kuzisaidia

    sana Afisi ya Mdhibiti na Kamati ya P.A.C, kuweza kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi

    mkubwa.

    La mwisho ambalo pia ni muhimu, ni uhusiano wa kitaaluma unaohitajika uwepo baina ya Afisi

    ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu na Kamati ya P.A.C. Hii ina maana, Ripoti yoyote ya

    ukaguzi inayotelewa na Afisi ya Mdhibiti ni ya kitaalamu. Na kwa bahati njema, Wajumbe wa

    Kamati sio wote wataalamu wa Ukaguzi, lakini wanalazimika kufanya kazi za ukaguzi

    (uchunguzi wa fedha na matumizi yake). Katika hali hii, kama Wajumbe hawa wa Kamati,

    hawasomeshwa vizuri masuala ya fedha na wakayafahamu, kazi tunayowapa ya kudhibiti fedha

    za Serikali haitafanyika kabisa ama haitatekelezwa kwa ufanisi. Hili linahitaji kwanza kuijengea

    uwezo wa kifedha na kitaalamu Afisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu, ili nayo iweze

    kuiwezesha Kamati ya P.A.C kutekeleza majukumu yake, kitaaluma na kitaalamu.

    Hili na lifanyike pia kwa kuongeza utaalamu kwa Sekretarieti ya Kamati, ambayo ndio roho,

    macho na masikio ya Kamati, lakini pia kwa kuongeza bajeti ya Afisi ya Mdhibiti, ili fursa zaidi

    za masomo kwa Wajumbe, Sekretarieti ya Kamati pamoja na Watendaji wote wa Afisi ya

    Mdhibiti ziweze kuongezeka.