fataawa za sharh-us-sunnah ya barbahaariy - ´allaamah al-fawzaan

82
1 Mkusanyiko Wa Fataawa Za Sharh-us-Sunnah Lil-Barbahaariy Abu Muhammad bin ´Aliy bin Khalaf al-Barbahaariy ´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan Mfasiri: Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush ©

Upload: wanachuoni

Post on 14-Apr-2015

313 views

Category:

Documents


15 download

DESCRIPTION

Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

TRANSCRIPT

Page 1: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

1

Mkusanyiko Wa Fataawa Za

Sharh-us-Sunnah Lil-Barbahaariy

Abu Muhammad bin ´Aliy bin

Khalaf al-Barbahaariy

´Allaamah Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

Mfasiri:

Abu Bakr Khatwiyb al-Atrush

©

Page 2: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

2

Dibaji

Bismillaah, Alhamdulillaah. Swalah na salaam zimwendee Mtume wetu

Muhammad na ahli zake na Maswahabah zake (Radhiya Allaahu ´anhum

ajma´iyn) mpaka siku ya mwisho. Amma ba´ad:

Himidi zote ni Zake Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) Aliyeniwezesha

kukusanya Fataawa hizi. Hizi ni Fataawa zilizokusanywa baada ya Duruus

zote alizotoa Shaykh al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah) akisherehesha kitabu

cha Imaam al-Barbahaariy (Rahimahullaah) mmoja wa wanachuoni wakubwa

maarufu, kitabu ni cha ´Aqiydah kinaitwa “Sharh-us-Sunnah Lil

Barbahaariy.”

Fataawa nyingi ni kuhusiana na masuala ya ´Aqiydah kwani kitabu chenyewe

ni cha ´Aqiydah. Kuna baadhi ya Fataawa pia kuhusiana na ´Aqiydah na

masuala ya Fiqh na mengineyo ila si nyingi.

Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) kijitabu hichi kilichokusanya

Fataawa muhimu ziweze kutunufaisha sisi na nyinyi na kuleta faida kubwa

katika Ummah wetu wa Kiislamu. Tunamuomba Allaah Atuwafikishe sote

kwa Ayapendayo na Kuyaridhia.

Tanbihi: Fataawa zote hizi tumezifasiri kwa njia ya Video na zinapatikana

Youtube waweza kusoma na huku wasikiliza. Kwa mwenye kutaka hizo

Fataawa za Video aende Alhidaaya au Youtube kwa juu sehemu ya kutafuta

aandike au kukopi kichwa cha habari cha Fatwa (kama ilivyo hapo chini kwa

kila Fatwa ina kichwa chake cha habari) na atafute itajitokeza In Shaa Allaah.

Jazaakumu Allaahu Khayra

Swalla Allaahu ´alaa Muhammad, wa ´alaa aalihi wa Aswhaabihi wa sallam.

Page 3: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

3

Fataawa zilizomo: 1. Masuala Ya ´Amali Ni Katika Imani Yana Khilafu? 2. Tofauti Ya ´Arshi Na Kursiyy 3. Aadam (´alayhis-Salaam) Ni Mtume Au Nabii? 4. Kafanya Zinaa Na Aliwahi Kuoa, Apigwe Mawe Au Fimbo? 5. Mwenye Kusema Ya Kwamba Aadam Alifanya Makosa Mawili 6. Suufiyyah Wanaochukulia Anashiyd Ni Kumdhukuru Allaah 7. Bid´ah Ya Kilugha 8. Dalili Ipi Ya Kwamba Maneno Ya Allaah Ni Kwa Herufi Na Sauti? 9. Du´aa Na Kuunga Udugu Kunarudisha Qadar? 10. Fitina Ya Shubuha Na Fitina Ya Kufuata Matamanio 11. Msingi Wa ´Aqiydah Ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah Kwa Maswahabah 12. Hadiyth "Allaah Kamuumba Aadam Kwa Sura Yake" 13. Ni Watu Gani Hawa? 14. Si Sharti Kwa Mlinganiaji Awe Hana Makosa 15. Hukumu Ya Aliyekufa Kabla Ya Kuja Mtume Muhammad (´alayhis-Salaam) 16. Hukumu Ya Kufa Na Mtu Hakumpa Mkono Wa Utiifu Kiongozi Wa Kiislamu 17. Kutamani Mtu Laiti Angelikuwa Pamoja Na Maswahabah 18. Hukumu Ya Mtu Ambaye Anategemea Qur-aan Tu Na Kupinga Sunnah 19. Mwenye Kumtukana Abu Bakr, ´Umar Na´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anhum) 20. Hukumu Ya Wendawazimu Aakhirah 21. Ibaadhi (Maibaadhi) Wasemao Kuwa Qur-aan Imeumbwa 22. Watu Wanaotahadharisha Madhehebu Ya Salaf 23. Baadhi Ya Fadhila Za Mu´aawiyah (Radhiya Allaahu ´anhu) 24. Imani Kwa Mujibu Wa Jahmiyyah 25. Imani Ya Kwamba Qur-aan Imeumbwa Ni Ukafiri 26. Jahmiyyah Wapo Leo? 27. Nani Kasema Kwamba Kutofautiana Ni Rahmah? 28. Kusoma Elimu Ya Falsafa, Mantiki, Na Mfano Wa Hizo 29. Mtume Na Imaam Ahmad Kumuona Allaah Usingizi 30. Kwenda Kaburini Kumzuru Maiti Wako Ila Hujui Mahali Alipo 31. Kafiri Akinipa Salaam Kamili, Je Nami Nimpe Kamili? 32. Madu´aat Wanaodai Wanalingania Katika Haki Za Mwanamke 33. Kuwalea Watoto Kwa Filamu Za Katuni 34. Kauli Inayosema Jahannam (Moto) Utaisha 35. Kazi Hii Ni Maalum Kwa Wanachuoni 36. Kipi Kilichoumbwa Kabla, ´Arshi Au Kalamu? 37. Shaykh Fawzaan Kuhusu Kitabu Cha Ibn-ul-Qayyim "ar-Ruuh" 38. Kuashiria Kwa Mkono Wakati Wa Kutaja Sifa Za Allaah (´Azza wa Jalla) 39. Kuchukua Elimu Kwa Watu Wanaokhalifu Manhaj Ya Salaf 40. Kuwa Na Nia Nzuri Haitakasi Kosa La Mtu 41. Maulidi Yana Bid´ah Na Shirki 42. Mwenye Kuifanyia Mzaha Sunnah Ya Mtume (´alayhis-Salaam) Ni Kafiri 43. Kumfuata Mwanachuoni Katika Kitu Kipya Cha Fiqh 44. Kumkufurisha Mshirikina Kwa Kitendo Chake Cha Dhahiri 45. Kukataza Uovu Kwa Kumpa Mtu Mkanda 46. Mume Anaweza Kumrejea Mke Wake Bila Ya Mashahidi? 47. Kufuru Ndogo Ya Kumwingilia Mke Kwa Nyuma 48. Kumvalisha Hijaab Binti Wa Miaka Saba

Page 4: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

4 49. Inajuzu Kunyoa Kipara? 50. Inajuzu Kuoa Wasichana Wa Nje Ya Ndoa? 51. Kuomba "Ee Allaah Usinikadirie Kadha Na Kadha" 52. Kwanini Ahl-us-Sunnah Wanawakufurisha Jahmiyyah? 53. Ni Kweli Watu Wa Makaburini Hutembeleana Kila Siku Ya Ijumaa? 54. Watoto Wa Shaykh Katika Kitabu "ad-Durur as-Sania" 55. Makafiri Wanaposilimu Watoto Wao Huzingatiwa Kuwa Ni Wa Zinaa? 56. Dalili Ya Mafungu Matatu Ya Tawhiyd Katika Qur-aan 57. Watu Wa Mantiki, Wanafalsafa Na Wanatheolojia 58. Wanaosema Watawala Ni Ma´ulamaa Na Sio Viongozi Waasi Na Madhalimu 59. Tafsiri Ya Neno "adh-Dhikra", Katika Suurat 16; Aayah Ya 44 60. Radd Kwa Mwenye Kutatiza Watu Na Kitabu Na "Sharh as-Sunnah” Cha al-Barbahaariy 61. Bid´ah Zinazoenezwa Na Kuchukua Elimu Kwa Njia Ya Simu 62. Mtu Yuko Huru Katika Uislamu Katika Mipaka Ya Kishari´ah 63. Sifa Ya Kundi Lililookoka 64. Ahl-ul-Takfiyr Ni Katika Ahl-ul-Bid´ah Wabaya Zaidi 65. Kuwatakia Swalah Na Salaam Kwa Wasiokuwa Mitume 66. Kumuuliza Muislamu Katika Mji Wa Kiislamu "Wewe Ni Muumini"? 67. Kumkuta Imamu Katika Takbiyrah Ya Tatu Katika Swalah Ya Janaza 68. Mwanaume Kuswali Na Suruwali 69. Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) Waliwahi Kumuona Masiyh ad-Dajjaal? 70. Mtu Akimuona Allaah Usingizini Kamuona Kweli? 71. Je, Sunnah Inaweza Kufuta Qur-aan? 72. Sisi Tunalingania Katika Umoja Wa Waislamu 73. Kufuata Kauli Za Wanachuoni Kwa Matamanio 74. Kuna Tofauti Kati Ya Mashia Na Raafidhwah? 75. Kuoa Kwa Nia Ya Talaka Ni Kumhadaa Mwanamke 76. Salaf Walikuwa Hawajui ´Ilm-ul-Kalaam 77. Sababu Ya Khawaarij Kupigwa Vita 78. Roho Hukutana Na Kuongea Ndani Ya Kaburi? 80. Qur-aan Lazima Iendane Sambamba Na Sunnah 81. ´Adhaab Na Qiswaas 82. Nishikamane Na Jamaa´ah Ipi Katika Miji Ya Kikafiri? 83. Kisichokuwa Na Asli Katika Dini Ndio Bid´ah 84. Sababu 4 Za Kukufanya Upate Unyenyekevu Wakati Wa Kusoma Qur-aan 85. Waliopewa Mtihani Wa Kupenda Picha 86. Mtu Anamtii Mtawala Ambaye Yuko Chini Ya Uongozi Wake 87. Ninapoulizwa Swali Ilihali Najua Jibu, Naweza Kulijibia? 88. Lini Mji Unakuwa Wa Kiislamu Na WaKikafiri? 89. Nini Maana Ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah? 90. Ipi Dini Sahihi Kabla Ya Mtume (´alayhis-Salaam) Kuja Na Uislamu? 91. Hadiyth "Kutofautiana Kwa Ummah Wangu Ni Rahmah" Ni Dhaifu 92. Nani Bora Zaidi; "Mu´aawiyah" Au "´Umar bin ´Abdil-´Aziyz"? 93. Uwajibu Wa Msomi Kuthibitisha Sifa Za Allaah 94. Kumtanguliza ´Aliy Juu Ya ´Uthmaan Kwa Fadhila Au Uongozi 95. Ipi Hukumu Ya Mwenye Kusema Uhuru Ni Bora Kuliko Shari´ah? 96. Je, Kutukana Maswahabah Ni Kumtukana Mtume (´alayhis-Salaam)? 97. Mwenye Kumtukana Mtume (´alayhis-Salaam) Ana Tawbah? 98. Mtu Anayemponda Mu´aawiyah Na ´Amr bin ´Aasw 99. "Hatutegemi Sunnah, Qur-aan Yatosha" 100. Anayekufa Kwa Saratani Na Kuunguwa Kwa Moto, Wamekufa Mashahidi?

Page 5: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

5 101. Anayeacha Swalah Akianza Ni Wajibu Kukoga Na Kutoa Shahaadah Upya? 102. Mwenye Deni Lake Kafa, Pesa Hizi Nizifanye Nini? 103. Kuacha Swalah Ya Witr Na Sunnah YaKabla Ya Fajr Daima 104. Mwanachuoni Kuwa Na Baadhi Ya Makosa Katika Masuala Ya ´Aqiydah 105. "al-Mustwafah" Ni Jina La Mtume(´alayhis-Salaam)? 106. Jahmiyyah Ndio Pote Baya Zaidi Katika Murji-ah 107. Inajuzu Kwangu Kuhudhuria Na Kusimamia Jeneza Na Mzazi Wangu Kafiri? 108. Mu´tazilah, Ashaa´irah Na Maaturidiyyah Ni Wanafunzi Wa Jahmiyyah 109. Mtume Ana Orodha Ya Majina Ya WatuWa Peponi Na Motoni? 110. Usiku Wa Mi´raaj, Mtume Alisikia Maneno Ya Allaah Moja Kwa Moja? 111. Msimamo Wa Imaam al-Bukhaariy Juu Ya Qur-aan 112. Wanaokufa Kwa Ajali Ya Ndege Hupatwa Na Maumivu Ya Kutokwa Na Roho? 113. Watu Wa Sasa Walioathirika Na Suufiyyah Na Qubuuriyyah 114. Chuo Kikuu Cha Mchanganyiko Wa Wanaume Na Wanawake 115. Majini Pia Watamuona Allaah Aakhirah Peponi? 116. Mwenye Kusema Mikono Miwili Ya Allaah Katika Qur-aan Ni Majaaz 117. Maiti Naweza Kumwambia Khabari Za Familia Yake? 118. Suufiyyah Ni Wajinga 119. Maana Ya "Hayaat al-Barzakhiyyah" 120. Tafsiri Ya Kauli Ya Allaah "Hapana Kulazimisha Katika Dini" 121. Mtu Kama Huyu Ndie Mwenye Udhuru 122. Kwanini Raafidhwah WanawatukanaMaswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) 123. Kuziwekea Hadiyth Sahihi Majaaz 124. Mwenye Kuwatukana Wake Wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) 125. Kuwasikiliza Wapiga Visa 126. Kuanza Kuwalingania Ma´ulamaa Wapotofu Ni Bora Zaidi Kuliko Kuanza Na `Awwaam Wao 127. Kuuliza Daraja Ya Hadiyth 128. Asiyemuombea Du´aa Mtawala Wa Waislamu Ni Mtu Wa Bid´ah 129. Kutoka Siku 40 Ni Katika Bid´ah Za Suufiyyah 130. Hadiyth Hii Inajuzisha Kutoka Na Jamaa´at-ut-Tabliygh? 131. Kwenda Na Jamaa´at-ut-Tabliygh KufanyaDa´wah Katika Miji Ya Makafiri 132. Nikiingia Nyumba Na Hakuna Mtu Nitoe Salaam? 133. Radd Kwa Madu´aat Wanaojuzisha Kutibu Uchawi Kwa Uchawi 134. Kuswali Nyuma Ya Qubuuriyyuun 135. Kusoma Siyrah Ya Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) 136. Kusikiliza Visa Vya Tofauti Za Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) 137. "Shikamaneni Na ´Atiyq, Na Tahadharini Na Mambo Ya Kuzua" 138. Kusema Neno "Sayyidna" Abu Bakr (Radhiya Allaahu ´anhu) Inajuzu? 139. Kushahidilia Swahabah Fulani Kuwa Peponi Pasina Ushahidi 140. Kusema Kuwa Pepo Au Moto Utaisha 141. Kusema Kafiri Fulani Kafa Katika Ukafiri Na Ni Wa Motoni 142. Kusema Fulani Kafa Shahidi 143. Ashaa´irah Ni Katika Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah? 144. Tunapenda Haki Zaidi Kuliko Fulani 145. Kuridhia Qadhwaa Na Qadar Ni Wajibu 146. Uwajibu Wa Kujirejea Unapokosea 147. Kuongea Ni Katika Sifa Ya Allaah Ya Kimatendo 148. Madu´aat Wasiolingania Katika Tawhiyd Wala Hawaonyi Dhidi Ya Mubtadi´ah Na Bid´ah

Page 6: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

6

بسم اهلل الرحمن الرحيم 1. Masuala Ya ´Amali Ni Katika Imani Yana Khilafu?

Swali:

Imeenea katika mji wetu wanaosema ya kwamba yule mwenye kuacha ´amali

za mwili ni masuala yana khilafu baina ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Je,

kauli hii ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Muongo huyu. Hakuna khilafu baina ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ya

kwamba ´amali ni katika Imani. Wala haisihi Imani bila ya ´amali, kama jinsi

haisihi ´amali bila ya Imani. Ni mambo mawili yanayoenda sambamba. Hii

ndio kauli ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah ya kwamba Imani ni:

"Kauli kwa ulimi, na kuamini moyoni na ´amali za mwili. Inazidi kwa utiifu

na kupungua kwa maasi."

Na lau ikikadiriwa ya kwamba kuna khilafu kwa baadhi ya Ahl-us-Sunnah,

ibra ni kwa yale yaliyosimama juu ya dalili na Jamhuri ya Ahl-us-Sunnah. Na

huchukuliwa hii ni kauli mbovu inayokhalifu isiyotegemewa.

2. Tofauti Ya ´Arshi Na Kursiyy

Swali:

Ipi tofauti kati ya ´Arshi na Kursiyy?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 7: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

7

´Arshi sio Kursiyy. ´Arshi ndio kiumbe kilicho juu kabisa katika viumbe, na

ndio [kiumbe] kikubwa katika viumbe. Na Allaah (Subhaanahu) Kastawaa1

juu yake. Ama Kursiyy iko chini ya ´Arshi. Imethibiti katika Hadiyth ya

kwamba ndio mahali pa Miguu [ya Allaah]. Iko chini ya ´Arshi, na ni ndogo

kuliko ´Arshi na ni kubwa kuliko mbingu na ardhi.

3. Aadam (´alayhis-Salaam) Ni Mtume Au Nabii?

Swali:

Aadam alikuwa ni Nabii au Mtume?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni Nabii. Ni Nabii Aliyeongeleshwa kama ilivyo katika Hadiyth.

Aliongeleshwa na Allaah.

4. Kafanya Zinaa Na Aliwahi Kuoa, Apigwe Mawe Au Fimbo?

Swali:

Kuna mtu alioa kisha akataliki na hakuoa tena, kisha akaanguka kwa

mwanamke ambaye si Halali kwake. Katika hali hii, je apewe adhabu ya

kupigwa mawe?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Maadamu hilo limetokea baada ya kufanya ndoa sahihi, hata kama

[alioa] katika miaka ya mwanzoni na akazini katika [miaka] ya mwishoni,

apigwe mawe. Kwa kuwa katangulia kufanya ndoa iliyokuwa ya sahihi.

1 Kalingana sawa

Page 8: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

8

5. Mwenye Kusema Ya Kwamba Aadam Alifanya Makosa Mawili

Swali:

Imethibiti katika baadhi ya Hadiyth ya kwamba Aadam (´alayhis-Salaam)

alifanya makosa mawili. Kosa la kwanza aliomba...

´Allaamah al-Fawzaan:

Ewe ndugu! Msimseme vibaya Aadam. Aadam ni Nabii katika Manabii wa

Allaah. Ni Nabii Aliyeongeleshwa. Isitoshe, ni baba yenu. Hata baba yenu

mwamsema hivyo? Acheni maneno kama haya.

6. Suufiyyah Wanaochukulia Anashiyd Ni Kumdhukuru Allaah

Swali:

Tumekusikia ukisema ya kwamba anayesikiliza Anashiyd2 za Kiislamu ni

katika Suufiyyah3 na ni katika Hawaa. Je, tutahadharishe kukaa na watu

wake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Wapi mmesikia maneno haya ya kwamba anayezisikiliza ni katika Suufiyyah?

Mimi sikumbuki kama nilisema hivyo. Lakini mimi nilisema hizi Anashid

ambazo wanaziita ni za Kiislamu, ni Anashiyd za Suufiyyah. Kwa kuwa

Suufiyyah wanachukulia ya kwamba Anashidy ni Dhikr liLlaah kumdhukuru

Allaah. Wanachukulia ni za Kiislamu. Kumdhukuru Allaah. Hivi ndio

nilisema. Ama kusema ya kwamba mwenye kuzisikiliza anakuwa Suufiy, si

sahihi. 2 Qaswiydah 3 Masufi

Page 9: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

9

7. Bid´ah Ya Kilugha

Swali:

Ni yapi makusudio ya Bid´ah al-Lughawiyyah Bid´ah ya kilugha?

´Allaamah al-Fawzaan:

Bid´ah ya kilugha ni kwa mfano wa hii gari yako. Gari yako hii ni Bid´ah

lakini ni Bid´ah ya kilugha. Kwa kuwa ni kitu kipya ambacho hakikuwepo,

mwanzoni watu walikuwa wakipanda punda na mipando mingine. Kukaja

badala yavyo gari n.k. Hii ndio Bid´ah ya kilugha.

8. Dalili Ipi Ya Kwamba Maneno Ya Allaah Ni Kwa Herufi Na Sauti?

Swali:

Tunajua ya kwamba katika Itikadi ya Ahl-us-Sunnah ni kuwa Maneno ya

Allaah ni kwa herufi na sauti. Ipi dalili ya kwamba ni kwa herufi na kwa

sauti?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kwa kuwa ni Maneno yanayosikika na ni wito. "Akamnadi Mola Wake",

"Tukamnadi". Na wito lazima uwe kwa herufi na sauti.

9. Du´aa Na Kuunga Udugu Kunarudisha Qadar?

Swali:

Page 10: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

10

Je Du´aa, na kuunga udugu na kuwatendea wema kunarudisha Qadar?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni sababu. Havirudishi Qadar, kwa kuwa Allaah Kakadiria ya kwamba

utaunga udugu. Ni Qadar. Kakadiria ya kwamba utaswali, utatoa Swadaaqah.

Ni katika Qadar ya Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala).

10. Fitina Ya Shubuha Na Fitina Ya Kufuata Matamanio

Swali:

Mtu ambaye katumbukia katika kitu katika maasi huzingatiwa ni katika Ahl-

ul-Ahwaa? Na ni ipi tofauti baina yake na baina ya Swaahib-ul-Hawaa

Mubtadi´?4

´Allaamah al-Fawzaan:

Sivyo hivyo. Sio kila mwenye kutumbukia katika maasi anakuwa ni katika

Ahl-ul-Ahwaa. Huyu ni katika Ahl-ul-Shahawaat5. Kwa kuwa fitina

imegawanyika sehemu mbili:

1. Fitina ya kufuata matamanio; kama Zinaa, kuiba, kunywa pombe na kula

Ribaa.

2. Na fitina ya shubuha - na Allaah Atukinge nayo. Hii ndio baya zaidi. Nayo

ni ile inayokuwa katika ´Aqiydah. Na hii ndio fitina ya Ahl-ul-Ahwaa. Fitina

ya Ahl-ul-Ahwaa inakuwa katika shubuha. Hii ndio baya zaidi.

11. Msingi Wa ´Aqiydah Ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah Kwa Maswahabah

4 Mtu wa Bid´ah 5 Wanaofuata mtamanio yao

Page 11: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

11

Swali:

Yapi maoni yako kwa mwenye kusema:

"Yule ambaye alisimama katika fitina iliyotokea baina ya ´Aliy na Mu´aawiyah

(Radhiya Allaahu ´anhumaa) ni bora kuliko yule ambaye alishiriki katikafitina

hii."?

´Allaamah al-Fawzaan:

Sisi tuko na "Qaa´iydah" msingi, nao ni kwamba hatuingilii yaliyopitika baina

ya Maswahabah, na wala hatusemi kamwe yeyote katika wao alikosea.

Hatuingilii yaliyopitika baina yao. Bali tunawatakia radhi na kuwachukuliwa

ni katika karne bora. Huu ndio msingi na ni katika Usuul (msingi) wa

´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah.

12. Hadiyth "Allaah Kamuumba Aadam Kwa Sura Yake"

Swali:

Wamesema baadhi ya wanachuoni kuhusu Hadiyth:

"Kwa hakika Allaah Kamuumba Aadam kwa sura Yake."

Wakasema ya kwamba dhamiri inamrudilia Aadam. Je, ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hadiyth itakuwa na faida gani? Ikifasiriwa ya kwamba dhamiri inamrudilia

Aadam Hadiyth itakuwa haina faida.

"Kwa hakika Allaah Kamuumba Aadam kwa sura Yake."

Hili halina shaka. Hili ni jambo la kwanza. Jambo la pili ni kwamba, imekuja

katika Riwaayah nyingine inayofasiri hii:

Page 12: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

12

"... kwa sura ya Ar-Rahmaan."

Namna hii. Wala isikutatize [Hadiyth] hii. Kwa kuwa baadhi ya watu

wameingiza akili zao ndani ya masuala haya. Allaah Hakukukalifisha hili.

Thibitisha yaliyokuja na kuthibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam), kama yalivyokuja. Ikiwa hukubainikiwa na kitu, tawaqqaf

(usiseme kitu) kwa hili na waulize wanachuoni. Ama kuyaingilia sana ndani,

haijuzu.

13. Ni Watu Gani Hawa?

Swali:

Imethiti katika Hadiyth ya kwamba kuna watu watakaozuiwa [kunywa]

katika hodhi, aseme Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): "Ni watu

wangu, ni watu wangu." Aambiwe: "Wewe hujui waliozusha baada yako." Ni

watu gani hawa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Watu hawa ni wale walioritadi na wanafiki waliodhihirisha Uislamu nao

wako juu ya unafiki.

14. Si Sharti Kwa Mlinganiaji Awe Hana Makosa

Swali:

Je, Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) anaweza kujaalia Uongofu wa kuonesha na

kuelekeza kupitia mikono ya muumini mwenye Imani pungufu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 13: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

13

Ndio. Mwenye kulingania kwa Allaah anaongoza. Anaongoza kwa Allaah,

kwa maana ya kwamba anabainisha na kuelekeza. "Hidaayat ad-Dalaalah"

maana yake ni kwamba anabainisha na kuelekeza. Na hili hupitika kwa kila

mlinganiaji. Na wala si sharti kwa mlinganiaji awe mkamilifu, si sharti kwa

mlinganiaji awe mkamilifu asiwe na makosa. Yanayoshurutishwa kwake ni

yeye kuwa na Imani, elimu na ´Aqiydah sahihi na Manhaj safi hata kama

atakuwa na baadhi ya vijikosa khafifu.

15. Hukumu Ya Aliyekufa Kabla Ya Kuja Mtume Muhammad (´alayhis-Salaam)

Swali:

Aliyekufa kabla ya kutumwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Je,

ataitwa Muislamu au kafiri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ataitwa ni katika Ahl-ul-Fatrah. Na hukumu yake ni kwa Allaah (Subhaanahu

wa Ta´ala).

16. Hukumu Ya Kufa Na Mtu Hakumpa Mkono Wa Utiifu Kiongozi Wa Kiislamu

Swali:

Kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa aliyekufa na

hakumpa mkono wa utiifu kiongozi(mtawala) yeyote ya kwamba kafa kifo

cha ki-Jaahiliyyah. Atakuwa kafanya dhambi kubwa katika madhambi

makubwa akawa ni Faasiq au katika katika Uislamu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 14: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

14

Atakuwa ni Faasiq. Na kafanya dhambi kubwa katika madhambi makubwa.

Lakini hatoki katika Uislam.

17. Kutamani Mtu Laiti Angelikuwa Pamoja Na Maswahabah

Swali:

Tunaposoma fadhila za Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum), kupigana

kwao Jihaad na Zuhd yao na nguvu ya Imani yao tunasema "laiti tungelikuwa

nao au laiti tungelipigana Jihaad pamoja nao tukiwa na Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam)." Je, kauli hii ni sahihi na kutamani huku

kunajuzu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haifai kufanya hivi, haifai kwako kutamani ungekuwa nao. Kwa kuwa

waweza kuwa nao na ukakosa kustahamili, hujui huenda usingelistahamili.

Kuna watu hawakustahamili, walikuwa pamoja nao na hawakuweza

kustahamili, wakapoteana kufanya unafiki - Allaah Atukinge. Hujui.

Yatosheleza kwako wewe kuwapenda, kuwatakia radhi, kuwaombea

msamaha, uwafuate na utetee heshima zao. Haya yanatosheleza kwako katika

haki yao.

18. Hukumu Ya Mtu Ambaye Anategemea Qur-aan Tu Na Kupinga Sunnah

Swali:

Nilimuona mtu ambaye kwa uinje anaonekana ni mwema na kahifadhi Qur-

aan, na pindi nilipomueleza Sunnah na Hadiyth akanambia mimi ni mtu wa

Qur-aaniy na anategemea Aayah za Qur-aan tu. Je, huyu ni katika watu

waliopinda ambao hawategemi Sunnah?

Page 15: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

15

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu ni baina ya mambo mawili, ima ni mjinga kapandikizwa fikra hizi

kutoka kwa wengine akidhani ya kwamba ni sahihi. Huyu anapewa udhuru

mpaka abainishiwe. Akiendelea anahukumiwa kuwa ni kafiri, kwa kuwa

anamkadhibisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Au kakusudia

kitu hichi, kakusudia kusema hivi na anajua ya kwamba ni upotofu na

kwamba ni makosa, huyu anakufuru bila ya shaka. Kwa kuwa kakusudia

kuziponda Hadiyth za Mtume na kumkadhibisha (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam).

19. Mwenye Kumtukana Abu Bakr, ´Umar Na´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anhum)

Swali:

Mwenye kumtukana Abu Bakr, ´Umar na ´Uthmaan (Radhiya Allaahu

´anhum) na kuwaponda na wala hakubali ukhalifa wao. Je, mtu anaweza

kusema ya kwamba ni Waislamu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Ikiwa anajua dalili ya hilo na akazikataa, huyu anakufuru. Ama

ikiwa anafuata kichwa mchunga au ni mjinga, huyu anapewa udhuru mpaka

abainishiwe haki. Akiendelea [baada ya kubainishiwa haki], anahukumiwa

kuwa ni kafiri.

20. Hukumu Ya Wendawazimu Aakhirah

Swali:

Hukumu ya wendawazimu siku ya Qiyaamah yaani mafikio yao?

Page 16: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

16

´Allaamah al-Fawzaan:

Mafikio yao ni kwa Allaah ambaye Kawaumba. Mimi sijui.

21. Ibaadhi (Maibaadhi) Wasemao Kuwa Qur-aan Imeumbwa

Swali:

Ni kipote kipi cha tatu ambacho kinasema ya kwamba Qur-aan imeumbwa

mbali na Jahmiyyah na Mu´tazilah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Nimewaambia ya kwamba ni Ashaa´irah, ndio wanasema kuwa maana

haikuumbwa, ama lafdhi imeumbwa. Wanasema hii ambayo imeandikwa

katika sahifu imeumbwa, kwa kuwa ni lafdhi na herufi.

Muulizaji:

Vipi kuhusu Ibaadhi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Ibaadhi ni pamoja na Jahmiyyah. Nao wanasema kwamba

imeumbwa.

22. Watu Wanaotahadharisha Madhehebu Ya Salaf

Swali:

Page 17: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

17

Ni watu gani ambao wanalingania katika kutahadharisha madhehebu ya Salaf

ambao uliwataja?

´Allaamah al-Fawzaan:

Wako wengi ewe ndugu katika waandishi leo. Wanasema sio lazima kwetu

kuwarejelea Salaf na kurejelea kauli za wanachuoni, ambao wanasema hili ni

Haramu na hili ni Halali.

23. Baadhi Ya Fadhila Za Mu´aawiyah (Radhiya Allaahu ´anhu)

Swali:

Je, yamethibiti matamshi haya kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam):

"Mfalme bora ni Mu´aawiyah."?

´Allaamah al-Fawzaan:

Allaah Anajua zaidi. Sujui. Mu´aawiyah yatosheleza ya kwamba ni Swahaabiy

katika Maswahabah wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Na ni shemeji ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Dada yake

Ummu Habiybah ni mke wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam), na ni mwandishi wa Wahyi pia. Anamwandikia Wahyi Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Na ana fadhila kubwa (Radhiya Allaahu

´anhu).

24. Imani Kwa Mujibu Wa Jahmiyyah

Swali:

Page 18: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

18

Ni ipi Imani kwa Jahmiyyah? Na yapi madhehebu yao kwa Imani katika

Swalah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Nimeshakariri hili mara nyingi na kusema ya kwamba madhehebu katika

Imani ni maarifa (ujuzu) tu moyoni, hata kama mtu hakufanya ´amali yoyote,

hata kama mtu hakutamka Shahadatayn huchukuliwa ni muumini kwao. Kwa

kuwa anajua moyoni mwake.

25. Imani Ya Kwamba Qur-aan Imeumbwa Ni Ukafiri

Swali:

Umesema ya kwamba Jahmiyyah wamekufuru kwa mambo yote haya

wanayoamini. Je, tufahamu kwa hili ya kwamba hakufuru katika wao

isipokuwa yule ambaye yamemkusanyikia mambo yote haya?

´Allaamah al-Fawzaan:

Akiwa na baadhi yake, haambiwi kuwa ni Jahmiy, anaambiwa yuko na kitu

katika Tajahhum na Jahmiyyah. Ikiwa kitu hichi anachokiamini kinakufurisha,

anakufurishwa hata kama ni baadhi yake. Ni kama mfano wa Imani ya

kwamba Qur-aan imeumbwa, hii ni kufuru. Maneno ya Jahmiyyah kuko

ambayo ni kufuru ya wazi na kuko ambayo ni chini ya kufuru. Hivyo si kila

ambaye ana kitu katika madhehebu ya Jahmiyyah anakuwa kafiri, isipokuwa

tu ikiwa kitu hicho alichonacho kinakufurisha. Hapo ndipo anakufurishwa.

Lakini ambaye imemkusanyikiwa Imani yote ya Jahmiyyah, huyu hakuna

shaka ya kufuru yake.

26. Jahmiyyah Wapo Leo?

Page 19: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

19

Swali:

Wanasema baadhi ya watu ya kwamba madhehebu ya Jahmiyyah yamepotea

na hakupatikani katika zama hizi hata mmoja. Je, kauli hii ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Anajuaje kama Jahmiyyah wamepotea? Je, yeye anajua Jahmiyyah na anajua

madhehebu yao mpaka aseme kuwa yamepotea? Jahmiyyah wapo na vitabu

vyao vipo na wafuasi wake wapo.

27. Nani Kasema Kwamba Kutofautiana Ni Rahmah?

Swali:

Je, kutofautiana ni Rahmah kama tunavyosikia?

´Allaamah al-Fawzaan:

Nani kasema kuwa ni Rahmah?Allaah (Jalla wa ´Alaa) Anasema:

حم ربك ول يزالون مختلفينإلا من را

"Na hawatoacha kukhitilafiana. Isipokuwa yule Aliyemrehemu Mola wako."

(11:118-119)

Kamtofautisha Aliyerehemu Mola wako katika waliyotofautiana. Ni dalili

ioneshayo ya kwamba Rahmah ni katika Umoja. Rahmah inapatikan katika

Umoja na si kutofautiana.

حم ربك ول يزالون مختلفينإلا من را

"Na hawatoacha kukhitilafiana. Isipokuwa yule Aliyemrehemu Mola wako."

(11:118-119)

28. Kusoma Elimu Ya Falsafa, Mantiki, Na Mfano Wa Hizo

Page 20: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

20

Swali:

Je, inajuzu kusoma elimu ya mantiki? Na ni ipi tofauti kati ya elimu ya

mantiki na elimu ya falsafa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Falsafa sio katika mantiki, inaingia mantiki na nyinginezo. Allaah

Katutosheleza kwa Kitabu na Sunnah. Soma Kitabu na Sunnah, na

usijishughulishe na mantiki na falsafa.

29. Mtume Na Imaam Ahmad Kumuona Allaah Usingizi

Swali:

Je, imethibiti kwa Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) ya kwamba alimuona

Allaah usingizini? Na je, inawezekana kumuona Allaah duniani katika

usingizi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, yasemekana hili ya kwamba Imaam Ahmad alimuona Allaah usingizini.

Yasemekana na Allaah Anajua zaidi. Kumuona Allaah usingizini ni jambo

linawezekana bila ya shaka. Alimuona Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) usingizini.

30. Kwenda Kaburini Kumzuru Maiti Wako Ila Hujui Mahali Alipo

Swali:

Page 21: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

21

Nikienda kaburini kumzuru maiti mmoja na wala sijui mahali kaburi lake

lilipo, nikamtolea Salaam. Je, hujua kama nimeenda kumtembelea?

´Allaamah al-Fawzaan:

Allaah Anajua zaidi. Mimi sijui. Haya ni mambo yasiyojua yeyote ila Allaah

(Subhaanahu wa Ta´ala). Wewe watolee Salaam maiti na muombee maiti

wako. Na Allaah Hapotekewi na kitu (Subhaanahu wa Ta´ala).

31. Kafiri Akinipa Salaam Kamili, Je Nami Nimpe Kamili?

Swali:

Kafiri akikupa Salaam ya sahihi ya wazi kwa kusema: "as-Salaam ´alaykum

war-Rahmatullaahi wa Barakatuh", je nimrudishie kwa mfano wake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Mrudishie kwa kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Wanapokusalimieni Ahl-ul-Kitaab waambieni "wa ´alaykum" (Nanyi pia)."

Usizidishie zaidi ya "wa ´alaykum". Hii inakuwa inaendana na Kauli Yake

(Ta´ala):

وها وا بأحسن منها أو رد ة فحي يتم بتحيا إذا حي

"Na mtapoamkiwa kwa maamkizi yoyote, basi itikieni kwa yaliyo bora kuliko

hayo au yarudisheni hayo hayo (kama mlivyoamkiwa)." (04:86)

Hadiyth inaendana sawa na Aayah.

32. Madu´aat Wanaodai Wanalingania Katika Haki Za Mwanamke

Page 22: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

22

Swali:

Tunasikia na kusoma siku hizi watu wengi ambao wanalingania katika yale

yanayoitwa "haki za mwanamke" na wanaita katika kujuzisha mchanganyiko

sokoni, [mwanamke] kuendesha gari na mengineyo. Upi wajibu wetu kwa

hilo? Na je, hawa ndio wale walinganiaji wanaolingania katika milango ya

Motoni tutahadhari nao?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni kama nilivyosema hivi karibu, ikiwa wewe uko na elimu kwa makosa ya

watu hawa wapige Radd, ni juu yako uwatwange Radd sawa sawa kwa fikra

zao. Katika Khutbah za Ijumaa, mihadhara na makala zinazoandikwa na

kusambazwa, na katika kitabu ikiwa uko na uwezo. Ama ikiwa huna elimu, ni

juu yako uwafikishie wanachuoni wanayoyasema.

33. Kuwalea Watoto Kwa Filamu Za Katuni

Swali:

Umeongelea kuhusu uumbaji na picha. Ni nini hukumu ya filamu za katuni

ambazo wanadai kuwa zinawalea watoto?

´Allaamah al-Fawzaan:

Picha zote [ni Haramu], sawa ikiwa ni filamu za katuni au nyinginezo. Ni

picha. Kila utachoona kuwa ni picha. Bali hizi ni aina baya zaidi ya picha, kwa

kuwa zinafanya harakati, zinasema, zinacheka n.k. Hizi ni baya zaidi kuliko

picha za kutundikwa, picha za kichwa tu na mwili usiofanya harakati. Ni baya

zaidi. Na wala tusiwalee watoto wetu katika maasi ya picha. Hili ndio

wanataka kwetu makafiri. Wanataka tuwalee watoto wetu kwa kwenda

kinyume na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

Page 23: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

23

34. Kauli Inayosema Jahannam (Moto) Utaisha

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kusema ya kwamba Moto utaisha? Na je, achukuliwe

kuwa ni mpotofu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Achukuliwe kuwa kakosea kwa hilo. Wananasibisha hili kwa Shaykh-ul-

Islaam bin Taymiyyah, lakini halikuthibiti kutoka kwake uthibitisho wa wazi.

Na lau imethibiti ni kosa.

35. Kazi Hii Ni Maalum Kwa Wanachuoni

Swali:

Ni nani mwenye haki ya kutafsiki watu na kuwakufurisha?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili ni kwa wanachuoni na watu wa Baswiyrah wajuao ni nani anayestahiki

Kufuru, Fisq na Bid´ah. Hili ni maalum kwa wanachuoni.

36. Kipi Kilichoumbwa Kabla, ´Arshi Au Kalamu?

Swali:

Tofauti ya kipi kilichoumbwa kwanza, ni ´Arshi au ni kalamu. Hii ni tofauti

iliotokea baina ya Salaf au ni baina ya waliokuja mwisho?

Page 24: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

24

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili kalisema Ibn-ul-Qayyim kwa waliokuwa kabla yake, lilitokea wakati wa

Salaf kwa kuchukua nususi. Kipi kinachotangulizwa, ´Arshi ndio iliumbwa

kabla au kalamu? Sahihi ni kwamba ´Arshi ndio iliumbwa kabla kama

inavyoonesha dalili Hadiyth. Na jambo hili ni sahali. Mwenye kusema kalamu

ndio ya kwanza au ´Arshi ndio ya kwanza, ni jambo la sahali halina utatizi.

37. Shaykh Fawzaan Kuhusu Kitabu Cha Ibn-ul-Qayyim "ar-Ruuh"

Swali:

Mtu huyu anauliza kuhusu Kitaab "ar-Ruuh cha Ibn-ul-Qayyim na kama kuna

makosa na anayeanza hafai kukisoma?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Kina faida kubwa na utafiti. Na pia kina mambo ambayo yanatakiwa

kutazamwa. Mwanafunzi anayeanza asikisome. Ambaye anaweza kukisoma

ni yule aliye thabiti na achukue ya faida humo na aache ambayo yanatakiwa

kutazawa. Yasemekana ya kwamba ndio kitabu cha kwanza alichoandika Ibn-

ul-Qayyim kabla ya kukutana na Shaykh wake [Ibn Taymiyyah]. Yasemwa

hivi na Allaah Anajua zaidi.

38. Kuashiria Kwa Mkono Wakati Wa Kutaja Sifa Za Allaah (´Azza wa Jalla)

Swali:

Inajuzu kuashiria kwa mkono wakati wa kutaja Hadiyth za Sifa za Allaah

(´Azza wa Jalla)?

Page 25: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

25

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Usiashirie kwa mkono.

39. Kuchukua Elimu Kwa Watu Wanaokhalifu Manhaj Ya Salaf

Swali:

Ni upi msimamo wetu kwa Madu´aat6 wanaokwenda kinyume na Manhaj ya

Salaf? Je, ichukuliwe elimu yao au iachwe? Na je, inajuzu kusoma baadhi ya

vitabu vyao vya faida?

´Allaamah al-Fawzaan:

Allaah Amewatajirisha (tosheleza) kwa watu hawa. Chukueni elimu kwa

watu wake waliyonyooka na vitabu vyenye manufaa vya faida. Na hakuna

haja ya vitabu vya watu hawa.

40. Kuwa Na Nia Nzuri Haitakasi Kosa La Mtu

Swali:

Baadhi ya watu wanafanya maasi na mambo ya Haramu na

tunapowabainishia wanasema "nia yangu ni nzuri, na mimi nataka kheri na

napenda kheri na watu wake, lakini mimi nachukia maasi haya." Vipi kumpa

nasaha mtu kama huyu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haya ni maneno yasiyofidisha. Anasema "mimi nia yangu ni nzuri",

kinachoongelewa si nia yako bali ni kitendo chako. Maadamu kitendo chako

6 Walinganiaji, wahubiri

Page 26: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

26

ni cha makosa, ni wajibu kwako kuleta Tawbah na kujirejea. Na nia nzuri

haitakasi kosa kamwe, kama tulivyosema. Ni juu ya aliyekosea arudi katika

usawa na hana udhuru ya kusema "nia yangu ni nzuri na akaendelea kwenye

kosa." Haijuzu kwake hili. Itapobainika kwake usawa ajirudi.

41. Maulidi Yana Bid´ah Na Shirki

Swali:

Je, Bid´ah ya kusherehekea Maulidi ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) ni Bid´ah khafifu inayotujuzishia kukaa na wanayoifanya au hapana?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kusherehekea Maulidi ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Bid´ah

bila ya shaka. Kwa kuwa ni kitendo ambacho hakikufanya Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam), Khalifah wake waongofu wala karne bora. Wala

hayakuzushwa isipokuwa baada ya karne ya nne, wakati utawala wa

Faatwimiyyuun, ambao ni Mashia wanaotoka magharibi. Wao ndio walikuja

na Bid´ah ya Maulidi. Hivyo ni Bid´ah bila ya shaka. Isitoshe, yanaingia kitu

katika Shirki, nayo ni kumuomba msaada Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam), kuomba atatue haja na kumshtakia kwa mambo yaliowasibu

Waislamu. Wanamshtakia Mtume na wala hawamshtakii Allaah (Jalla ´Alaa).

Na wala hawamuombi msaada Allaah, wanamuomba msaada Mtume katika

mnasaba huu. Na wao wanajua ya kwamba hutokea kitu katika haya. Hivyo

yamejumuisha baina ya Bid´ah na baina ya Shirki.

42. Mwenye Kuifanyia Mzaha Sunnah Ya Mtume (´alayhis-Salaam) Ni Kafiri

Swali:

Page 27: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

27

Kumedhihiri zama hizi wanaoifanyia mzaha Sunnah ya Mtume wa Allaah

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Je, kuifanyia mzaha Sunnah ni katika

Kufuru?

´Allaamah al-Fawzaan:

Una shaka juu ya hili? Mwenye kuifanyia mzaha Sunnah ya Mtume, hakuna

shaka ya ukafiriwake. Kwa kuwa anamkadhibisha Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) na kumponda.

43. Kumfuata Mwanachuoni Katika Kitu Kipya Cha Fiqh

Swali:

Akijitahidi mwanachuoni na kusema katika masuala ya Fiqh jambo ambalo

halikusema yeyote katika Salaf. Je, inajuzu kumfuata kipofu kwa hilo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kwa kiasi cha dalili. Ikiwa yuko na dalili, ndio inachukuliwa kauli yake. Ama

ikiwa hana dalili hapana. Hata Salaf, ikiwa mtu hana dalili inaachwa kauli

yake. Sisi tunafuata dalili.

44. Kumkufurisha Mshirikina Kwa Kitendo Chake Cha Dhahiri

Swali:

Je, tumkufurishe anayesujudia sanamu au kuchinjia sanamu au tusubiri

mpaka kwanza tumsimamishie hoja?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 28: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

28

Yeye anakufuru kwa hili. Unaweza kuhukumu kitendo chake kuwa ni kufuru

na ukamkufurisha kwa dhahiri [wa uliyoyaona]. Kisha baada ya hapo

ukamnasihi. Akitubu [sawa], la sivyo anachukuliwa kuwa ni kafiri kwa

dhahiri na kwa ndani.

45. Kukataza Uovu Kwa Kumpa Mtu Mkanda

Swali:

Mwenye kuona maovu akampa aliyeyafanya mkanda. Je, huchukuliwa huku

ni katika kukataza maovu kwa ulimi? Na dhimma itakuwa imenitoka kwa

kufanya hivi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Huenda asijui ni mkanda gani. Ni lazima umbainishie. Umwambie ewe

ndugu unaona kuwa huku ni kwenda kinyume na hivyo nakupa mkanda

usikilize ili ustafidi. Ama kumpa mkanda na kunyama, huenda akauunguza

mkanda au asifaidiki nao au asiupe umuhimu. Lakini ukimbainishia pale

unapompa na mkanda ili astafidi kutoka kwenye mkanda huo, ni jambo zuri

hili.

46. Mume Anaweza Kumrejea Mke Wake Bila Ya Mashahidi?

Swali:

Je, ni wajibu kushahidisha katika kumrejea mke?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili ni jambo limependekezwa na sio la wajibu. Lau atamrejea bila ya

mashahidi ni sahihi.

Page 29: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

29

47. Kufuru Ndogo Ya Kumwingilia Mke Kwa Nyuma

Swali:

Ni aina ipi ya kufuru iliokuja katika kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam):

"Mwenye kumwendea mke wake kwa nyuma amekufuru."?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hii ni kufuru ndogo. Haimtoi mtu katika Uislamu. Ni kama mfano wa [kauli

yake Mtume]:

"Kumtusi muumini ni ufasiki, na kumuua ni kufuru."

Yaani ni kufuru chini ya kufuru [kubwa]. Hii ni katika kufuru ndogo. Hatoki

katika Uislamu yule ambaye kamwendea mke wake nyuma. Bali anakuwa

kafanya dhambi kubwa katika madhambi makubwa. Imesifiwa kuwa ni

kufuru kwa ajili ya watu waigope.

48. Kumvalisha Hijaab Binti Wa Miaka Saba

Swali:

Binti mwenye miaka saba avikwe Hijaab?

´Allaamah al-Fawzaan:

Azoweshwe Hijaab. Kama jinsi anavyozoweshwa Swalah, Wudhuu, Swawm.

Azoweshwe hili na kukuzwa juu ya hilo.

Page 30: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

30

49. Inajuzu Kunyoa Kipara?

Swali:

Ipi hukumu ya kunyoa kichwa bila ya sababu? Je, ni kujifananisha na

Khawaarij?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakuna neno. Kunyoa kichwa hakuna neno na wala hakuna neno kukiacha.

Ni wajibu kunyoa au kupunguza wakati wa Hajj na ´Umrah, nje ya hapo

wewe ni mwenye khiyari. Ukitaka utakinyoa na ukitaka utakiacha. Lakini mtu

akiamini kuwa kukinyoa ni katika Dini na kadhalika, utakuwa ni katika

Khawaarij. Akiamini ya kwamba kukinyoa ni mubaha [imeruhusiwa] na wala

haina neno, hakuna ubaya kufanya hivyo.

50. Inajuzu Kuoa Wasichana Wa Nje Ya Ndoa?

Swali:

Inajuzu kuoa watoto wa Zinaa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Wakiwa ni wema, makatazo yako wapi? Wakiwa ni wema, hakuna makatazo.

Lakini bora mtu kujiepusha, pengine akawa na kitu katika tabia ya mama yake

au wamama zake. Pengine wakawa wamerithi. Mtu ajiepushe. Ama kusihi

inasihi. Wakiwa ni wema inasihi.

51. Kuomba "Ee Allaah Usinikadirie Kadha Na Kadha"

Page 31: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

31

Swali:

Je, inajuzu kusema:

"Ee Allaah Usinikadirie wala usiniandikie kadha na kadha."?

´Allaamah al-Fawzaan:

Sema badala yake "Ee Allaah usinikadirie! Ee Allaah nakuomba upole,

Rahmah na urahisi!, na mfano wa haya."

52. Kwanini Ahl-us-Sunnah Wanawakufurisha Jahmiyyah?

Swali:

Vipi Jahmiyyah wanakufurishwa na Ahl-us-Sunnah pamoja na kwamba

Jahmiyyah wanamjua Allaah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Tunasema makusudio sio kumjua tu kwani hata Iblisi anamjua Allaah.

قال رب بما أغويتني

"(Ibliys) Akasema: “Mola wangu! Kwa vile Umenitia makosani." (15:39)

Iblisi anamjua Allaah, Fir´awn anamjua Allaah. Hakutoshelezi kujua tu.

"Imani ni kutamka kwa ulimi, kuamini moyoni na matendo ya viungo; inazidi

kwa utiifu na kupungua kwa maasi." Hii ndio Imani.

53. Ni Kweli Watu Wa Makaburini Hutembeleana Kila Siku Ya Ijumaa?

Swali:

Page 32: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

32

Je, ni sahihi watu wa makaburini wanatembeleana makaburini mwao yao kila

siku ya Ijumaa na khaswa waumini?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kwa kweli hatujui, haya ni mambo ya Aakhirah hatuthibitishi kitu isipokuwa

kwa dalili. Anayesema kwamba wanatembeleana atuletee dalili ya kwamba

wanatembeleana. Ama maneno ya watu ni mengi, lakini kinachozingatiwa ni

dalili. Iko wapi dalili? Kuna mwenye kuwaona wakitembeleana,

akawashuhudia mwenyewe wakikusanyika na kadhalika? Kuna dalili katika

Shari´ah mpaka aseme dalili ni namna hii? Hana dalili.

54. Watoto Wa Shaykh Katika Kitabu "ad-Durur as-Sania"

Swali:

Katika Kitaab "al-Durur as-Sania" wakati mwingine kunasemwa: "Waliulizwa

watoto wa Shaykh". Ni yapi makusudio watoto wa Shaykh?

´Allaamah al-Fawzaan:

Watoto wa Shaykh ni Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab; ´Abdullaah, ´Aliy,

Ibraahiym, Hasan na Husayn. Na mkubwa wao ni ´Aliy kwa kuwa anaitwa

Abu ´Aliy. Hawa ndio watoto wa Shaykh.

55. Makafiri Wanaposilimu Watoto Wao Huzingatiwa Kuwa Ni Wa Zinaa?

Swali:

Je, watoto wa makafiri huzingatiwa ni watoto wa Zinaa kwa vile wazazi wao

hawakufunga ndoa sahihi?

Page 33: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

33

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Adhabu huchukuliwa ni ya kwao [wa zazi] na watoto wao ni wa

Kishari´ah. Na kwa sababu hii ndio maana mwenye kusilimu katika makafiri,

hakuwaamrisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kufunga ndoa

upya na wala hakuwanyanganya watoto wao kutoka kwao.

56. Dalili Ya Mafungu Matatu Ya Tawhiyd Katika Qur-aan

Swali:

Ipi hukumu kwa mwenye kupinga kugawa Tawhiyd mafungu matatu;

Rubuubiyyah, Uluuhiyyah na al-Asmaa´ was-Swifaat na anasema haya ni

katika mambo yaliyozushwa ambayo hayakuwepo wakati wa Mtume

(´alayhis-Salaam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mimi nimekwishawaambia ya kwamba watu hawa wanajaribu

kuiharibu´Aqiydah. Mara utawasikia wanasema hakuna neno "´Aqiydah"

wala "at-Tawhiyd" katika Qur-aan na Sunnah. Na mara wanasema kuigawa

Tawhiyd mafungu matatu ni Bid´ah. Wanataka kutatiza watu katika jambo

hili. Neno ´Aqiydah lipo katika Qur-aan na Sunnah, bali ni jina lililotolewa

katika Qur-aan na Sunnah, jina la ´Aqiydah na Tawhiyd. Hata kama si kwa

andiko la moja kwa moja, lakini lipo kimaana. Ama mafungu ya Tawhiyd ni

jambo lipo katika Qur-aan. Bali Qur-aan yote ni Tawhiyd kama alivyosema

hilo Ibn-ul-Qayyim. Yanayozungumzia Rubuubiyyah (Ubwana) wa Allaah,

Ufalme Wake, Uwezo Wake na Matakwa Yake; haya ni katika Tawhiyd

Rubuubiyyah. Yanayozungumzia Majina na Sifa za Allaah ni katika Tawhiyd

al-Asmaa´ was-Swifaat. Yanayozungumzia kumuabudu Allaah Mmoja

Asiyekuwa na mshirika na kuacha ´Ibaadah (kuabudu) asiyekuwa Yeye, ni

katika Taawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Yote yanapatikana katika Qur-aan. Mafungu

ya Tawhiyd matatu yanapatikana kuanzia Suurat ya kwanza al-Faatihah.

Page 34: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

34

ه رب العالمين الحمد للـا

"Alhamduli-Llaah (Himdi zote) Anastahiki Allaah Mola wa walimwengu."

Hii ni Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah. "Mola wa walimwengu."

ين حيم مالك يوم الد ن الرا ـ حم الرا

"Ar-Rahmaanir-Rahiym (Mwingi wa Rahmah-Mwenye Kurehemu). Maalik

(Mfalme) wa siku ya malipo."

Hii ni Tawhiyd al-Asmaa´ was-Swifaat.

اك نستعين اك نعبد وإيا إيا

"Wewe Pekee tunakuabudu na Wewe Pekee tunakuomba msaada."

Hii ni Tawhiyd ipi? Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah.

Katika Suurat ya mwisho ya Qur-aan; Suurat "an-Naas".

قل أعوذ برب النااس

"Sema: “Najikinga na Mola wa watu."

Hii ni Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah.

"Ilaah wa watu." Hii ni Tawhiyd ipi? Tawhiyd-u-Uluuhiyyah.

ملك النااس

“Maliki (Mfalme) wa watu."

Hii ni Tawhiyd ipi? al-Asmaa´ was-Swifaat.

Lakini watu hawa ima ni wajinga wasiojua chochote. Na asiyejua vipi atataka

naye kukataza asiyoyajua? Au ima ni wapotofu wanaotaka kuiharibu

´Aqiydah na mara nyingi huwa hivi kwao.

57. Watu Wa Mantiki, Wanafalsafa Na Wanatheolojia

Swali:

Page 35: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

35

Ipi tofauti kati ya al-Manaatwiqah (watu wa mantiki), al-Falaasifah

(wanafalsafa) na Ahl-ul-Kalaam (wanatheolojia)?

´Allaamah al-Fawzaan:

al-Manaatwiqah ndio Ahl-ul-Kalaam. Ama Falaasifah ni wale wanaodai wana

hekima na mara nyingi huwa katika makafiri. Ama ´ulamaa al-Kalaam na

´ulamaa al-Mantwiq ni katika vipote vya Kiislamu; kama Mu´tazilah na

waliofuata elimu yao ya mantiki na akategemea dalili yao au hoja yao katika

´Aqiydah. Watu hawa ni vipote katika vipote vya Waislamu. Lakini miongoni

mwao kuko ambao wametoka katika Uislamu na miongoni mwao kuko

ambao wamepotea na hawakutoka katika Uislamu kiasi cha daraja yao. Ama

Falaasifah wengi wao huwa makafiri.

58. Wanaosema Watawala Ni Ma´ulamaa Na Sio Viongozi Waasi Na Madhalimu

Swali:

Katika zama zetu hizi kuna Waislamu wanaosema ya kwamba watawala ni

wanachuoni na sio raisi wa dola kutokana na kasoro alizonazo. Ipi hukumu ya

kauli hii na ipi nasaha yako?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haya ni madhehebu ya Khawaarij na Allaah Atukinge. Katika Maswahabah

kulikuwepo wanachuoni na walikuwa wakimtii Abu Bakr, ´Umar, ´Uthmaan

na ´Aliy na wala hawakusema Imaam [kiongozi] wetu ni mwanachuoni fulani.

Na wala hakuna Muislamu yeyote aliyesema kwamba mtawala wetu ni

mwanachuoni fulani. Wanasema ni kiongozi wetu katika elimu, ama kusema

ni kiongozi wetu katika usikivu na utiifu hakuna hata mmoja aliyesema hivi

katika Waislamu. Hakuna asemae hivi isipokuwa mtu ambaye ni mpumbavu

asiyekuwa na akili au asiyekuwa na Dini kabisa.

Page 36: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

36

59. Tafsiri Ya Neno "adh-Dhikra", Katika Suurat 16; Aayah Ya 44

Swali:

كر رون وأنزلنا إليك الذ ل إليهم ولعلاهم يتفكا لتبين للنااس ما نز

"Na Tumekuteremshia Adh-Dhikra (Qur-aan ee Muhammad عليه وآله صلى هللا

ili uwabainishie watu (kwa Sunnah) yaliyotere-mshwa kwao na huenda (وسلم

wakapata kutafakari.” (16:44)

Je, ni Qur-aan au Sunnah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni vyote viwili. Lakini asli ni Qur-aan, na kunaingia humo Sunnah.

60. Radd Kwa Mwenye Kutatiza Watu Na Kitabu Na "Sharh as-Sunnah” Cha al-Barbahaariy

Swali:

Kuna mtu kanitatiza kwa kitabu hichi "Sharh as-Sunnah" cha Imaam al-

Barbahaariy na kwamba hakikuthibiti kwake kihistoria. Je, maneno yake ni

sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Lipi ajualo kuhusiana na historia? Huyu ni mjinga asiyejijua. Yaani yeye

haamini wanachuoni ambao wamekithibitisha kitabu hichi? Na wala

hamuamini Shaykh-ul-Islaam bin Taymiyyah ambaye kanukuu kutoka katika

Risaalah hii [ya Barbahaariy] katika Fataawa zake? Yaani tukadhibishe

wanachuoni na tumsadikishe yeye? Lipi ajualo katika historia na maisha ya

wanachuoni? Huyu ni mjinga asiyejijua. Na pengine kaguswa katika nafsi

yake na kitu kwa ´Aqiydah hii, hivyo anataka kutatiza watu kwacho. Watu

Page 37: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

37

wamesema hata kuwa Qur-aan sio Maneno ya Allaah. Mnastaajabu? Je,

hakuna watu ambao wanasema Qur-aan sio Maneno ya Allaah? Ajitokeze mtu

aseme Risaalah hii sio maneno ya al-Barbahaariy. Hili halistaajabishi.

61. Bid´ah Zinazoenezwa Na Kuchukua Elimu Kwa Njia Ya Simu

Swali:

Tunasikia siku hizi ya kwamba kuna mtu katolewa katika kaburi lake na uso

wake umeungua na haya yameenea kwa njia za simu. Je, tusadikishe khabari

hizi au ni katika mambo ya Ghayb?

´Allaamah al-Fawzaan:

Msisadikishe simu kamwe katika mambo haya. Kwa kuwa nyuma ya siku

hizo kuna watu wapotofu ambao wanataka kueneza Bid´ah na kuharibu

´Aqiydah za Waislamu. Hivyo tahadharini sana. Wala msichukue elimu

kwenye simu.

62. Mtu Yuko Huru Katika Uislamu Katika Mipaka Ya Kishari´ah

Swali:

Anayesema katika al-Mufakkiruun ya kwamba yeye ni ´Ilmaaniy au

Libraaliy...

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni nini maana ya Libraaliy? Uhuru? Uhuru wa kinyama au uhuru wa

Kishari´ah? Ikiwa ni uhuru wa kinyama ni kufuru, ama ikiwa anamaanisha

yuko huru kwa mipaka ya Kishari´ah, haina neno. Watu wako huru -

Alhamdulillaah - katika mambo yao katika mipaka ya Kishari´ah. Wako huru

Page 38: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

38

katika mali zao, katika mipaka ya Kishari´ah. Uhuru sio moja kwa moja,

uhuru umedhibitiwa kwa dhawabiti za Kishari´ah.

63. Sifa Ya Kundi Lililookoka

Swali:

Je, kuna tofauti kati ya at-Twaaifah al-Mansuurah kundi lililonusuriwa na al-

Firqah an-Naajiyah pote lililookoka?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haliwezi kunusuriwa isipokuwa ni lazima liwe lililookoka, na haliwezi kuwa

ni lililookoka isipokuwa ni lazima liwe ni lililonusuriwa. Sifa zote hizi ni za

kundi hili. Ni pote lililonusuriwa, lililookoka, Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah.

Sifa zote hizi ni zake. Anayetofautisha baina ya hayo, huyu hana dalili ya

kufanya kwake hivi.

64. Ahl-ul-Takfiyr Ni Katika Ahl-ul-Bid´ah Wabaya Zaidi

Swali:

Ahl-ul-Takfiyr wanaowakufurisha Waislamu ni katika Ahl-ul-Bid´ah?7 Na

nikikaa nao kwa makusudio ya kuwabadili ikiwa wako katika makosa, je

itakuwa kikao hichi ni chenye kulaumiwa?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ahl-ul-Takfiyr ni katika Ahl-ul-Bid´ah wabaya zaidi. Wanaowakufurisha

Waislamu ni katika Bid´ah baya zaidi. Ama kukaa nao, ni kama tulivyosema

mwanzo. Ikiwa uko na uwezo wa kukaa nao na kujadiliana nao na kuradi 7 Watu wa Bid´ah

Page 39: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

39

shubuha zao, hili ni jambo la wajibu. Kwa kuwa hili ni katika kulingania kwa

Allaah.

"Lau Allaah Atamuongoza mtu mmoja kupitia mikono yako, ni kheri kwako

kuliko zizi la minyama."

65. Kuwatakia Swalah Na Salaam Kwa Wasiokuwa Mitume

Swali:

Kulipokuja jina la Mahdiy ulisema (´alayhis-Salaam). Je, anazingatiwa ni

katika manzilah ya Mitume au huku ni kwa ajili ya heshima tu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Inajuzu kuwatakia Salaam kwa wasiokuwa Mitume na kusema "Swalah na

salaam ziwe juu yao." Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema:

"Allaahumma swalliy ´alaa Aali Abiy ´Awfah (اللهم صل على آل أبي عوفة)". Inajuzu

kuwatakia Swalah na Salaam kwa wasiokuwa Mitume, lakini mtu asidumu

kwa kufanya hivyo kama mtu anavyodumu kuwatakia Swalah na Salaam

Mitume. Ikisemwa baadhi ya nyakati hakuna neno.

66. Kumuuliza Muislamu Katika Mji Wa Kiislamu "Wewe Ni Muumini"?

Swali:

Akiniuliza mtu: "Je, wewe ni muumini?" Je, naweza kusema: "Ndio, mimi ni

muumini na ninakusudia namwamini Allaah, Malaika Wake, vitabu Vyake na

Mitume Wake, siku ya Mwisho na Qadar; kheri na shari yake?".

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 40: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

40

Yaani wewe uko katika mji wa kikafiri na hajui ya kwamba wewe ni muumini

muislamu mpaka akuulize? Kusema "mimi ni muislamu hakuna neno".

Usiseme "mimi ni muumini", sema "mimi ni muislamu" ikiwa uko katika mji

wa kikafiri. Ama ukiwa katika mji wa Kiislamu, hakuna haja ya maswali kama

haya.

67. Kumkuta Imamu Katika Takbiyrah Ya Tatu Katika Swalah Ya Janaza

Swali:

Nikiingia katika Swalah ya Janaza katika Takbiyrah ya tatu. Vipi ntatimiza

Swalah yangu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kabiri na Imamu zilizobaki, na pindi Imamu atapotoa Salaam kamilisha

Takbiyrah zilizobaki. Ni kama uliyepitwa katika Swalah ya faradhi, sawa

sawa. Kamilisha na toa Salaam baada ya kukamilisha.

68. Mwanaume Kuswali Na Suruwali

Swali:

Kuna mnasaba upi wa kutajwa suruwali katika kitabu hichi (Sharh as-Sunnah

lil-Barbahaariy) pamoja na kuwa ni kitabu cha ´Aqiydah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kama nilivyowaambia, kunatajwa masuala ya Fiqh wakati fulani ili

kuwakhalifu Mubtadi´ah.8 Kwa kuwa kuko wanaopinga kuswali na suruwali.

Suruwali ikisitiri ´Awrah, mtu anaswali nayo. Muhimu ni kusitiri ´Awrah, hii 8 Watu wa Bid´ah

Page 41: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

41

ni sharti moja wapo ya kusihi kwa Swalah. Kusitiri ´Awrah. Kwa nisba ya

mwanaume ni baina ya kitovu mpaka kwenye magoti. Kwa nisba ya

mwanamke, mwili wake wote ni ´Awrah ndani ya Swalah.

69. Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) Waliwahi Kumuona Masiyh ad-Dajjaal? Swali:

Je, Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) walimuona Masiyh ad-Dajjaal na

mnyama?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hakukuthibiti kitu katika hili. Yasemekana ni Ibn Sayyaad ndio Masiyh ad-

Dajjaal. Lakini haikuthibiti ya kwamba ndio Dajjaal. Ibn Sayyaad alikuwepo,

lakini haikuthibiti ya kwamba yeye ndio Dajjaal.

70. Mtu Akimuona Allaah Usingizini Kamuona Kweli?

Swali:

Mtu akimuona Mola Wake usingizini. Sura ya Allaah (Jalla wa ´Alaa) ni ya

uhakika kama atavyomuona mwenye kuota usingizini?

´Allaamah al-Fawzaan:

Enyi ndugu! Mimi siingii ndani ya jambo hili. Ni nani ana uwezo wa kusema

namjua Allaah ukweli wa kumjua na nimemuona Allaah kwa Sura Yake ya

hakika (Subhaanahu wa Ta´ala)? Unaweza kujiwa na Shaytwaan na kusema

"mimi ndio Allaah au mimi ndio mola wako" au akasema "mimi ndio Mtume

wa Allaah." Utamuona mtu anaingia katika jambo na pengine asitoke humo.

Page 42: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

42

Aache jambo hili. Kumuona Allaah usingizini kunahitajia nguvu ya Imani na

mtu awe anamjua Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) na nguvu ya elimu.

71. Je, Sunnah Inaweza Kufuta Qur-aan?

Swali:

Tumejua ya kwamba Sunnah inafasiri Qur-aan. Je, Sunnah inaweza kufuta

kitu katika Qur-aan?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, inawezekana. Usuuliyyuun wanasema kwamba Qur-aan inafuta

Sunnah na Sunnah inafuta Qur-aan. Na Qur-aan inafuta Qur-aan na Sunnah

inafuta Sunnah.

72. Sisi Tunalingania Katika Umoja Wa Waislamu

Swali:

Yapi maoni yako kwa mwenye kusema:

"Msiwafarikanishe Waislamu na wala msitahadharishe Raafidhwah kwa

kuwa ni Waislamu"?

´Allaamah al-Fawzaan:

Sisi hatuwafarikanishi Waislamu, bali tunalingania katika Umoja wa

Waislamu. Lakini Waislamu wasiokuwa na moja ya jambo katika mambo

yanayovunja Uislamu wa mtu, Waislamu sahihi sisi tunalingania wawe na

Umoja. Ama mwenye moja katika mambo yanayomtoa mtu katika Uislamu,

hawa sio Waislamu.

Page 43: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

43

73. Kufuata Kauli Za Wanachuoni Kwa Matamanio

Swali:

Ipi maana ya kauli ya Salaf (Rahimahumu Allaah):

"Anayefuata [mambo ya] rukhusa amefanya Uzanaadiqah."?

Ina maana anakuwa mnafiki?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, kwa kuwa anafuata hawaa (matamanio) yake. Huyu ni mbaya kuliko

mnafiki. Kwa kuwa mtu huyu anatoka katika Dini. Itafikia awe ni mwenye

kuchukua kila rukhusa iliyosema mwanachuoni na akaacha kauli sahihi

[yenye nguvu] mpaka anakuwa mnafiki.

74. Kuna Tofauti Kati Ya Mashia Na Raafidhwah?

Swali:

Ipi tofauti kati ya Mashia na Raafidhwah? Na ni zipi aina zao?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mashia wako aina mbali mbali, sio kundi moja. Kuna Mashia khafifu, Mashia

wenye kuchupa mipaka, Mashia al-Baatwiniyyah na kadhalika. Mashia wako

makundi mengi. Raafidhwah ni kundi katika Mashia; Zayniyyah,

Raafidhwah, al-Baatwiniyyah n.k. Yote haya ni katika makundi ya Mashia.

Page 44: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

44

75. Kuoa Kwa Nia Ya Talaka Ni Kumhadaa Mwanamke

Swali:

Ipi hukumu ya kuoa kwa nia ya Talaka. Na je, ni kama Mut´ah?9

´Allaamah al-Fawzaan:

Kuoa kwa nia ya Talaka sio kama Mut´ah, kuna tofauti. Lakini kauli ya sahihi

ni kwamba haijuzu. Kwa kuwa ni kumhadaa mwanamke, [haikukatazwa]

kwa sababu ni kama Mut´ah ila ni kwa sababu ni kumhadaa mwanamke na

walii wake. Kwa kuwa umemuoa kwa nia ya kubaki naye na wewe unaficha

ndani ya nafsi yako nia ya [... sauti imepotea... ]. Ni Mut´ah ndogo na sio

Mut´ah [...]. [...] kwa nisba ya mwenye kunuia [...], mke, walii. Hii haiitwi

Mut´ah ya kihakika.

76. Salaf Walikuwa Hawajui ´Ilm-ul-Kalaam

Swali:

Imesihi kwa mmoja katika wanachuoni wa Salaf ya kwamba aliita elimu ya

´Aqiydah ´Ilm-ul-Kalaam (elimu ya kimantiki)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Salaf hapakupatikana katika wakati wao ´Ilm-ul-Kalaam, ilipatikana katika

zama za mwisho baada ya karne bora. Ikaenea baada ya karne bora.

Walikuwa hawajui ´Ilm-ul-Kalaam.

77. Sababu Ya Khawaarij Kupigwa Vita

9 Ndoa ya muda; ambayo hukumu yake ni haramu

Page 45: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

45

Swali:

Katika wanachuoni kuko waliowakufurisha Khawaarij na kutumia dalili ya

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Nitawaua kama walivyouawa kina ´Aad."

Na kuna ambao hawakuwakufurisha kwa kutumia dalili ya ´Aliy (Radhiya

Allaahu ´anhu) alipoulizwa kama wao ni makafiri:

"Hapana. Wameikimbia kufuru."

Ipi kauli yenye nguvu katika kauli hizi mbili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Wametofautiana wanachuoni katika kuwakufurisha Khawaarij, na

wengi wao wanaona kuwa sio makafiri bali ni wapotofu. Kule ´Aliy (Radhiya

Allaahu ´anhu) kuwaua na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

kaamrisha kuwapiga vita, sio kwa sababu ya kufuru yao. Yule ambaye

anawafarakanisha Waislamu na kuhalalisha damu ya Waislamu anapigwa

vita hata kama ni Muislamu. Kupigwa vita haina maana kwamba ni makafiri.

Kila anayejiingiza kwa Waislamu na anataka kuwafarakanisha au kuhalalisha

damu yao, apigwe vita hata kama ni Muislamu.

78. Roho Hukutana Na Kuongea Ndani Ya Kaburi?

Swali:

Roho ndani ya kaburi zinaonana na kuongea?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ewe ndugu hatujui yaliyomo ndani ya kaburi. Haya ni katika mambo ya

Ghayb. Hakuongelewi khabari ya makaburini isipokuwa kwa dalili. Sisi

hatuingii katika mambo haya.

Page 46: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

46

79. Sauti Ni Ya Msomaji, Maneno Ni YaAllaah

Swali:

Kauli hii ilithibiti kutoka kwa Salaf:

"Maneno ya ni Maneno ya Al-Baariy (Allaah) na sauti ni sauti ya msomaji?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, yamesihi. Maneno ni Maneno ya Al-Baariy na sauti pindi mtu

anaposoma [Qur-aan] ni maneno ya msomaji. Hii ndio maana ya kauli ya Ahl-

us-Sunnah wal-Jamaa´ah. Yanayosomwa ni Maneno ya Allaah, na lafdhi hichi

ni kitendo cha kiumbe.

80. Qur-aan Lazima Iendane Sambamba Na Sunnah

Swali:

Je, ni sahihi kusema "Qur-aan inaihitajia Sunnah zaidi kuliko jinsi Sunnah

inavyoihitajia Qur-aan"?.

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Qur-aan pamoja na Sunnah. Haitoshelezi moja wapo yenyewe

isipokuwa pamoja na nyenzake. Ikichukuliwa Qur-aan pasina Sunnah, itabaki

Qur-aan bila ya Tafsiyr sehemu kubwa na bila ya bayana.

81. ´Adhaab Na Qiswaas

Page 47: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

47

Swali:

Ipi tofauti baina ya Qiswaas10 na baina ya ´Adhaab?

´Allaamah al-Fawzaan:

´Adhaab ni natija ya Qiswaas.

82. Nishikamane Na Jamaa´ah Ipi Katika Miji Ya Kikafiri?

Swali:

Tumejua uwajibu wa kushikamana na Jamaa´ah na mimi niko katika mji moja

wapo ambayo inahukumu kinyume na Shari´ah ya Allaah. Ni Jamaa´ah ipi

ambayo ni wajibu kwangu kujiunga nayo?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ambao wako katika madhehebu ya haki; katika ´Aqiydah, ´Ibaadah,

wamesalimika na Shirki na Bid´ah na wako madhubuti katika kushikamana

na dalili. Hawa ndio Jamaa´ah.

83. Kisichokuwa Na Asli Katika Dini Ndio Bid´ah

Swali:

Tumesikia baadhi ya wanachuoni wakisema : "Hii ni Bid´ah", na wakati

mwingine wanasema: "Jambo hili halina asli". Vipi kujumuisha baina ya lafdhi

hizi mbili?

10 Kisasi

Page 48: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

48

´Allaamah al-Fawzaan:

Haya yanagongana. Jambo lisilokuwa na asli yaani ni Bid´ah. Kwa kuwa

Bid´ah ni yasiyokuwa na asli katika Kitabu na Sunnah. Hii ndio Bid´ah.

84. Sababu 4 Za Kukufanya Upate Unyenyekevu Wakati Wa Kusoma Qur-aan

Swali:

Mimi nina matatizo, nayo ni wakati ninaposoma Qur-aan siogopi na wala

sifahamu chochote kana kuwa sisomi maneno ya kiarabu. Bali wakati

mwingine nafikiria kitu na huku nasoma Qur-aan kwa masikitiko makubwa.

Ipi sababu ya hili kwa vile mwanzoni nilikuwa tofauti na hivi ninaposoma

Qur-aan?

´Allaamah al-Fawzaan:

Pengine uko na mukhalafaat na maasi na umeshikamana na dunia. Ni juu

yako uihesabu nafsi yako juu ya jambo hili. Na unyenyekevu ni kitu kinatoka

kwa Allaah (Subhaanahu Ta´ala), lakini wewe fanya sababu za kukufanya

upateunyenyekevu.

Na katika sababu za kukufanya uwe na unyenyekevu: a) Omba kinga kwa

Allaah kutokana na Shaytwaan aliyelaaniwa mwanzoni mwa kisomo, b)

usome kwa moyo uliyohudhuria, c) uzingatie Aayah unazosoma kwa

kuzifikiri na maana yake na d) na usome katika wakati mzuri usiokuwa na

vishawishi. Hizi ni sababu.

85. Waliopewa Mtihani Wa Kupenda Picha

Swali:

Page 49: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

49

Nimepewa mtihani wa kupenda picha na ninazitundika [... sauti imepotea... ]

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni juu yako kutubu kwa Allaah na kujiweka mbali na jambo hilo.

86. Mtu Anamtii Mtawala Ambaye Yuko Chini Ya Uongozi Wake

Swali:

Mimi naishi katika mji huu Saudi Arabia lakini si mtu mwenye asli ya hapa.

Ni mtawala gani ambaye ni wajibu kwangu kumtii na ambaye juu ya shingo

langu kuna bay´ah, ni mtawala wa mji huu au mtawala wa mji wangu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni mtawala ambaye wewe uko chini ya uongozi wake. Wewe uko katika mji

huu, ni wajibu kwako kumtii mtawala wa mji huu. Na utapoenda katika mji

wako, wewe utambay´ah mtawala wa mji huo.

87. Ninapoulizwa Swali Ilihali Najua Jibu, Naweza Kulijibia?

Swali:

Ataponiuliza mtu usahihi wa Hadiyth au udhaifu wake, je nijibu ikiwa najua

jibu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 50: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

50

Ikiwa unajua jibu kutoka kwenye kitabu kiaminifu, mjibu. Mwambie: "kasema

fulani kadha na kadha, kuhusiana na Hadiyth hii", muelekezo katika

maregeleo ikiwa ni kitabu cha kuaminika. Ama ikiwa kitabu hakiaminiki au

mwandishi wake hajulikani, wewe nyamaza na kusema: "mimi sijui kitu

kuhusiana na hili. Waulize wanachuoni na wenye fani ya Hadiyth."

88. Lini Mji Unakuwa Wa Kiislamu Na WaKikafiri?

Swali:

Lini mji unahukumiwa ya kuwa ni mji wa Kiislamu au mji wa kufuru?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa unahukumu kwa Uislamu, ni mji wa Kiislamu. Na ikiwa unahukumu

kwa kufuru, basi ni mji wa kikafiri. Kinachotazamwa ni inavyohukumu.

89. Nini Maana Ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah?

Swali:

Ni nini maana ya Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah na lini Muislamu anakuwa

katika Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Yaa Subhaana Allaah! Hili tumelirudi mara nyingi katika darsa. Ahl-us-

Sunnah ni wale walioshikamana kwa yale aliyokuwemo Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) na Maswahabah wake. Makusudio ya "as-Sunnah"

ni njia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hii ndio Sunnah. "al-

Jamaa´ah" ni wale waliomo juu ya haki hata kama watakuwa wadogo. Yule

Page 51: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

51

ambaye atakuwa juu ya haki, hata kama atakuwa mmoja au wadogo basi yeye

ni "al-Jamaa´ah".

90. Ipi Dini Sahihi Kabla Ya Mtume (´alayhis-Salaam) Kuja Na Uislamu?

Swali:

Je, Dini sahihi kabla ya kutumwa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi

wa sallam) ni Haniyfiyyah Mila (Dini) ya Ibraahiym au ni Shari´ah ya ´Iysa

(´alayhis-Salaam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kwa nisba ya waarabu Aal Ismaa´iyl, Dini waliokuwemo ni Dini ya

Ibraahiym. Dini ya baba yake na Ismaa´iyl ni Dini ya Ibraahiym (´alayhis-

Salaam). Ama kwa nisba ya mayahudi na manaswara walikuwa katika Dini ya

Muusa na ´Iysa (´alayhimus-Salaam). Na kuko katika waarabu walioathirika

na uyahudi na unaswara, na wakaacha Dini ya Ibraahiym.

91. Hadiyth "Kutofautiana Kwa Ummah Wangu Ni Rahmah" Ni Dhaifu

Swali:

Kuna ambao wanatumia kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):

"Kutofautiana kwa Ummah wangu ni Rahmah." katika masuala ya tofauti,

ni halali au haramu. Hili ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Hili ni kosa. Yaani akisema hivyo, kinachofahamika ni kwamba

wakiwa wamoja ni adhabu? Ikiwa kutofautiana kwao ni Rahmah

kinachofahamika ni kwamba wakiwa wamoja itakuwa ni adhabu. Na hili

Page 52: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

52

hakuna aliyelisema. Bali ni kinyume chake. Kuwa kwao wamoja ndio Rahmah

na kutofautiana kwao ni adhabu. Hili ndo sahihi bali ndo sawa. Kasema

Allaah (Ta´ala):

حم ربك ول يزالون مختلفينإلا من را

"Na hawatoacha kukhitilafiana. Isipokuwa yule Aliyemrehemu Mola wako."

(11:118-119)

Kawatoa katika waliotofautiana wale Aliowarehemu Allaah.

Hawakutofautiana. Na Hadiyth isemayo:

"Kutofautiana kwa Ummah wangu ni Rahmah."

Haikuthibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

92. Nani Bora Zaidi; "Mu´aawiyah" Au "´Umar bin ´Abdil-´Aziyz"?

Swali:

Inajuzu kumfadhilisha ´Umar bin ´Abdul-´Aziyz juu ya Mu´aawiyah (Radhiya

Allaahu ´anhu)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Halijuzu hili. Hakuna yeyote anayefadhilishwa juu ya Swahabah

kamwe. Hili halijuzu. Si ´Umar bin ´Abdul-´Aziyz wala mwengine yeyote.

´Umar bin ´Abdul-´Aziyz (Radhiya Allaahu ´anhu) ana fadhila zake, manzilah

yake, elimu na ni katika Mujaddidiyn katika Uislamu. Lakini hawekwi sawa

wala kuwekwa karibu na mmoja katika Maswahabah, si Mu´aawiyah wala

mwengine yeyote.

93. Uwajibu Wa Msomi Kuthibitisha Sifa Za Allaah

Swali:

Page 53: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

53

Ipi hukumu ya mwenye kuulizwa baadhi ya Sifa za Allaah anasema "sijui".

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa hajajifunza kweli, aseme "sijui". Ama ikiwa ni mjuzi na amesoma

´Aqiydah, ni wajibu kubainisha elimu aliyonayo.

94. Kumtanguliza ´Aliy Juu Ya ´Uthmaan Kwa Fadhila Au Uongozi

Swali:

Anayemfadhilisha ´Aliy juu ya ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anhumaa), je

huchukuliwa ni Raafidhwiy au Shi´iy?11

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Hachukuliwi ni Raafidhwiy wala Shi´iy. Kufadhilishwa ´Aliy juu ya

´Uthmaan ni masuala yana tofauti kwa baadhi ya Maswahabah na

wanachuoni. Hatozingatiwa mtu huyu kuwa na kitu katika ushia. Isipokuwa

tu, yule ambaye anamtanguliza ´Aliy juu ya ´Uthmaan katika uongozi, au juu

ya Abu Bakr na ´Umar huyo ndo atakuwa ni Raafidhwiy. Uongozi ni tofauti

na fadhila.

95. Ipi Hukumu Ya Mwenye Kusema Uhuru Ni Bora Kuliko Shari´ah?

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kusema ya kwamba uhuru ni bora kuliko Shari´ah?

´Allaamah al-Fawzaan: 11 Mshia

Page 54: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

54

Huyu mna shaka ya kwamba ni kafiri? Anasema kwamba uhuru ni bora

kuliko Shari´ah, huyu ni kafiri mwenye ukafiri mbaya. Allaah Atukinge.

96. Je, Kutukana Maswahabah Ni Kumtukana Mtume (´alayhis-Salaam)?

Swali:

Anayewatukana Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) anakuwa

kamtukana Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili halina shaka. Kwa kuwa ni Mtume ndo kawafanya kuwa waadilifu,

kawasifia na kakataza kuwatukana. Kwa hivyo, yule anayewatukana

Maswahabah anakuwa kamtukana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam). Kwa kuwa ni Mtume ndo kawafanya kuwa waadilifu, na huyu

anawakadhibisha. Huyu anakwenda kinyume na Mtume na anapingana na

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuona kwake kuwa Maswahabah

ni waadiliifu.

97. Mwenye Kumtukana Mtume (´alayhis-Salaam) Ana Tawbah?

Swali:

Katika ´Aqiydah ya Ahl-us-Sunnah ni kwamba hakuna dhambi ila mja yuko

na Tawbah, je huingia humo mwenye kutubia kwa kumtukana Mtume

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Page 55: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

55

Ndio. Kila mwenye kutubia. Lakini anayemtukana Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) hatoacha kupewa adhabu, ama Tawbah - ikiwa ni mkweli

baina yeye na Allaah - Allaah Atamkubalia. Lakini hatoacha kupewa adhabu.

98. Mtu Anayemponda Mu´aawiyah Na ´Amr bin ´Aasw

Swali:

Ipi hukumu ya anayewaponda Maswahabah kama mfano waMu´aawiyah na

Amr bin ´Aasw (Radhiya Allaahu ´anhumaa) katika baadhi ya waandishi na

al-Mufakkiriyn?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hawa ni Maswahabah watukufu. Mu´aawiyah (Radhiya Allaahu ´anhu) ni

Swahabah mtukufu na ni mwandishi wa Wahyi. Ni katika waandishi wa

Wahyi wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na ni

kiongozi wa Waislamu baada ya ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anhumaa). Allaah

Aliwakusanya Waislamu na akawafanya kuwa na Umoja kupitia mikono

yake. Ana fadhila nyingi (Radhiya Allaahu ´anhu). ´Amr bin ´Aasw pia ana

fadhila nyingi na ni Mujaahid katika njia ya Allaah (Radhiya Allaahu ´anhu).

Ana manzilah katika Uislamu. Hakuna anayewaponda isipokuwa ima ni

mjinga au ni mdanganyifu au kaathirika na Itikadi ya Shi´ah ambao

wanamtukana Mu´aawiyah, ´Amr bin ´Aasw na al-Mughiyrah bin Shu´bah.

99. "Hatutegemi Sunnah, Qur-aan Yatosha"

Swali:

Kauli ya mwandishi [al-Barbahaariy] (Rahimahu Allaah):

"Na utaposikia mtu hataki Athaar (Sunnah) na badala yake anataka Qur-aan

tu, basi usishuku ya kwamba ni mtu yuko na Zandaqah."

Page 56: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

56

Je, ina maana ni kafiri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Ni kafiri. Akikataa Sunnah, kuna nini ikiwa hii sio kufuru? Hii ni

kufuru ya wazi. Akisema "hatutegemei Sunnah kamwe, bali tunategemea

Qur-aan tu", hii ni kufuru.

100. Anayekufa Kwa Saratani Na Kuunguwa Kwa Moto, Wamekufa Mashahidi?

Swali:

Anayekufa kwa kuunguwa au kwa saratani, je wanaitwa kuwa ni mashahidi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kutokana na Hadiyth, wanaitwa ni mashahidi. Lakini ni mashahidi Aakhirah

na si duniani. Shahidi wa duniani ni yule wa vitani. Ama shahidi wa Aakhirah

ni shahidi ambaye si wa vitani; kama kuunguwa kwa moto, kuuawa kwa

dhuluma na kadhalika, hawa wanatarajiwa Shahaadah.

101. Anayeacha Swalah Akianza Ni Wajibu Kukoga Na Kutoa Shahaadah Upya?

Swali:

Ni jambo lenye kujulikana ya kwamba mwenye kuacha Swalah kwa uvivu na

kuzembea anakuwa kafiri. Akiacha Swalah kama Swalah ya Dhuhr kwa

kukusudia mpaka ukatoka wakati wake, je ni wajibu akoge kisha atoe

Shahaadah upya kwa kuwa nitakuwa nimetoka katika Uislamu na kuwa

kafiri?

Page 57: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

57

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, ukikusudia hili ni juu yako Tawbah na kuingia katika Uislamu upya.

Kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

"Ahadi iliopo baina yetu sisi na wao [makafiri] ni Swalah, atakayeiacha basi

amekufuru."

"Baina ya mja na kufuru, ni kuacha Swalah."

Kuna [ushahidi] ulio wazi zaidi kuliko huu?

Hali kadhalika Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kaamrisha kulipa

Swalah kwa yule mwenye kupitikiwa na usingizi au kusahau, ni dalili

ioneshayo ya kwamba mwenye kukusudia si sahihi na haimfai kwake kulipa.

102. Mwenye Deni Lake Kafa, Pesa Hizi Nizifanye Nini?

Swali:

Mtu ambaye alikuwa na deni la mtu na wala hawezi kumrudishia kwa sababu

ya kukosekana mwenye deni lake, lipi la wajibu juu yake katika hali hii?

´Allaamah al-Fawzaan:

Warithi wake. Akifa mtu wa deni, ana warithi. Awape warithi wake.

103. Kuacha Swalah Ya Witr Na Sunnah YaKabla Ya Fajr Daima

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kuacha Swalah ya Witr na kadumu kwa kuacha

Sunnah ya Swalah ya Subh?

Page 58: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

58

´Allaamah al-Fawzaan:

Huyu kapindukia. Bali Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) imepokelewa

kutoka kwake ya kwamba kasema:

"Mwenye kudumu kwa kuacha Witr, usikubaliwe ushahidi wake, kwa kuwa

ni mtu muovu."

Na Imaam Abu Haniyfah anaonelea ya kwamba Witr ni wajibu na si Sunnah,

bali ni wajibu kwa Abu Haniyfah. Witr imesisitizwa.

Ama Rakaa mbili za kabla ya Fajr, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

alikuwa haziachi sawa akiwa mkazi au msafiri. Ni dalili ioneshayo ya

kwamba ni Sunnah iliyosisitizwa. Haijuzu, au haitakikani kwa mtu kuziacha

kwa kuwa ni Sunnah zilizosisitizwa. Akiziacha basi ni mwenye mapungufu

na kapindukia.

104. Mwanachuoni Kuwa Na Baadhi Ya Makosa Katika Masuala Ya ´Aqiydah

Swali:

Kauli ya al-Barbahaariy (Rahimahu Allaah):

"Haambiwi mtu kuwa ni "Swaahibu as-Sunnah" (mtu wa Sunnah) mpaka

Sunnah yote imkusanyikie."

Mwenye kukosea katika wanachuoni katika baadhi ya masuala ya ´Aqiydah

kwa Ijtihaad, kama mwenye kuharibu sifa moja au mbili na mengine yote

anaafikiana na Ahl-us-Sunnah, je huzingatiwa ni katika Ahl-us-Sunnah au

aitweje?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, huzingatiwa ni katika Ahl-us-Sunnah kwa mengi yanayoonekana

kwake. Ama kukosea kosa moja mbili au kitu kidogo, hii huchukuliwa ni

Page 59: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

59

kasoro kwake lakini haimtoi katika Ahl-us-Sunnah. Ama makosa yakiwa

mengi, anatoka katika Ahl-us-Sunnah.

105. "al-Mustwafah" Ni Jina La Mtume(´alayhis-Salaam)?

Swali:

Katika majina ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni pamoja na "al-

Mustwafaa" (aliyechaguliwa) au hii ni sifa yake tu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni jina na sifa. Ambaye anataka kujizidishia [elimu] kuhusiana na masuala

haya, arejelee [kitabu] "Jalaail al-Afhaam was-Swalaat was-Salaam ´alaa

khayr-il-Anaam" cha Imaam Ibn-ul-Qayyim. Kataja majina ya Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) na kasherehekesha kila jina.

106. Jahmiyyah Ndio Pote Baya Zaidi Katika Murji-ah

Swali:

Je, Murji-ah wanaingia katika Jahmiyyah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Jahmiyyah ni pote katika Murji-ah. Lakini ndio baya zaidi, baya zaidi katika

mapote ya Murji-ah ni Jahmiyyah.

107. Inajuzu Kwangu Kuhudhuria Na Kusimamia Jeneza Na Mzazi Wangu Kafiri?

Page 60: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

60

Swali:

Je, inajuzu kwa Muislamu kuhudhuria jeneza la wazazi wake wawili na wote

wawili sio Waislamu kwa kuwa kutohudhuria kwake kutasababisha matatizo

baina yake yeye na ndugu na jamaa zake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Kafiri anasimamiwa na makafiri, na Muislamu hasimamii jeneza la

kafiri hata kama itakuwa ni katika watoto wake. Isipokuwa tu ikiwa hakuna

wakumzika, hivyo atamzika. Kwa kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) alimuamrisha ´Aliy kumzika Abu Twaalib, amfukie. Kwa hivyo,

kukiwa hakuna yeyote atakayemsimamia katika makafiri, Waislamu

hawatomuacha juu ya ardhi, bali watamzika. Lakini hawatomzika katika

makaburi ya Waislamu.

108. Mu´tazilah, Ashaa´irah Na Maaturidiyyah Ni Wanafunzi Wa Jahmiyyah

Swali:

Je, Mu´tazilah ni Jahmiyyah katika Majina na Sifa za Allaah, Khawaarij katika

Imani na uongozi na Qadariyyah katika Qadar?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kwa kiasi wa waliyo nayo. Wako na Tajahhum, Qadar n.k. Kwa kiasi wa

waliyo nayo. Ni katika wanafunzi wa Jahmiyyah, Mu´tazilah ni katika

wanafunzi wa Jahmiyyah. Hali kadhalika, Ashaa´irah na Maaturidiyyah wako

na kitu katika madhehebu ya Jahmiyyah, sawa kiwe ni kidogo au kikubwa.

Lakini asli katika upotofu ni madhehebu ya Jahmiyyah. Wamerithi mambo

haya.

Page 61: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

61

109. Mtume Ana Orodha Ya Majina Ya Watu Wa Peponi Na Motoni?

Swali:

Je, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anajua majina ya watu wa

Peponi na majina ya watu wa Motoni?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mtume hajui isipokuwa yale Aliyomfunza Allaah (´Azza wa Jalla) na wala

hajui majina ya watu wa Peponi na majina ya watu wa Motoni. Hajui hili.

Yeye hajui isipokuwa yale Aliyomfunza Allaah (´Azza wa Jalla).

110. Usiku Wa Mi´raaj, Mtume Alisikia Maneno Ya Allaah Moja Kwa Moja?

Swali:

Je, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisikia Maneno ya Allaah

(´Azza wa Jalla) moja kwa moja usiku wa Mi´raaj au alisikia kwa mkaakati?

´Allaamah al-Fawzaan:

Alisikia moja kwa moja bila ya mkaakati. Alisikia Maneno ya Allaah bila ya

mkaakati. Ni katika usiku huu tu. Ama siku zingine zote, Wahyi ulikuwa

ukimteremkia kwa kuletewa na Jibriyl (´alayhis-Salaam).

111. Msimamo Wa Imaam al-Bukhaariy Juu Ya Qur-aan

Swali:

Page 62: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

62

Upi usahihi wa maneno ya mwenye kusema "kwa hakika al-Bukhaariy

(Rahimahu Allaah) alichagua kunyamaza katika masuala ya kusema kuwa

Qur-aan imeumbwa."?

´Allaamah al-Fawzaan:

Huu ni uongo. al-Bukhaariy alipewa mtihani katika jambo hili, pindi

aliposema kama alivyosema Imaam Ahmad [ya kwamba Qur-aan ni Maneno

ya Allaah na Hayakuumbwa] alipewa mtihani baadhi ya watu wa wakati

wake na wakamhama. Alifikwa na yakufikwa. Kama inavyojulikana katika

Historia na Siyrah yake (Rahimahu Allaah).

112. Wanaokufa Kwa Ajali Ya Ndege Hupatwa Na Maumivu Ya Kutokwa Na Roho?

Swali:

Vipi kujumuisha baina ya maumivu ya kutokwa na roho [wakati wa mauti] na

baina ya wanaokufa kwa ajali ya ndege katika makafiri na Waislamu na wala

hawapati maumivu ya mauti?

´Allaamah al-Fawzaan:

Wewe umejuaje kuwa hawahisi maumivu ya mauti? Hakuna yeyote

anayekufa bila ya kuhisi maumivu ya mauti. Huku ni kupinga bila ya dalili.

113. Watu Wa Sasa Walioathirika Na Suufiyyah Na Qubuuriyyah

Swali:

Kunapatikana katika baadhi ya vitabu vya madhehebu manne baadhi ya

mambo ya ´Aqiydah yanayokwenda kinyume na waliyokuwemo Salaf; kama

Page 63: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

63

Tawassul kwa viumbe, Du´aa kwa jaha n.k. Je, mwenye kuyachukua na

kuyaeneza katika duruus akatazwe au hapana?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haya sio katika maneno ya Salaf. Haya ni katika vitabu vya waliokuja

baadaye, walioathirika na Suufiyyah na Qubuuriyyah. Ni katika vitabu vya

waliokujabaadaye. Ama vitabu vya Salaf, maimamu wanne, na waliokuwa

kabla yao, katikati yao na zama zao huwezi kukuta mambo kama haya,

vimesalimika na mambo haya. Na mimi nimewaambia, wananasibishiwa

maimamu wanne wa Fiqh mambo ya ´Aqiydah yasiyokuwa katika

madhehebu yao.

114. Chuo Kikuu Cha Mchanganyiko Wa Wanaume Na Wanawake

Swali:

Ipi hukumu ya kusoma katika chuo kikuu cha mchanganyiko, sawa ikiwa ni

kwa wanaume au wanawake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haijuzu kusoma katika chuo kikuu cha mchanganyiko, kutokana na maovu

yanayopatikana na fitina. Ama kusoma, atapata masomo yasiyokuwa na

mchanganyiko na asome.

115. Majini Pia Watamuona Allaah Aakhirah Peponi?

Swali:

Je, Allaah Ataonekana Peponi hususan na wanaadabu au pamoja na Majini

pia?

Page 64: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

64

´Allaamah al-Fawzaan:

Haya hatuyajui ewe ndugu. Ambayo hatukujiwa na dalili yake hatuyatafuti.

116. Mwenye Kusema Mikono Miwili Ya Allaah Katika Qur-aan Ni Majaaz

Swali:

Ipi Radd kwa mwenye kusema:

"Mikono miwili iliotajwa ya Allaah (´Azza wa Jalla) katika Qur-aan ya

kwamba ni majaaz."?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili ni batili. Yaani sio ya ukweli, majaaz maana yake ni kwamba sio Mikono

miwili ya uhakika. Haya ndio madhehebu ya Jahmiyyah. Allaah Atukinge.

117. Maiti Naweza Kumwambia Khabari Za Familia Yake?

Swali:

Inaruhusiwa kumueleza maiti hali za familia yake?

´Allaamah al-Fawzaan:

Nini? Nani kakwambia haya ya kumueleza maiti hali ya familia yake? Je,

wewe unaweza ukawafikia ili uweze kuwafikishia khabari hizo? Maneno yote

haya ni ya kipuuzi. Msalimie maiti na umuombee kisha uondoke.

Page 65: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

65

118. Suufiyyah Ni Wajinga

Swali:

Suufiyyah wamechukua ´Aqiydah yao kutoka kwa Jahmiyyah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Suufiyyah wamechukua ´Aqiydah yao... Asli ni kwamba Taswawwuf

maana yake ni kujitahidi katika ´Ibaadah, na Tashaddud [kukazia] katika

´Ibaadah. Ilianza namna hii. Kisha ikakua, kukaingia humo Malaahidah

mpaka ikafikiakatika Wahdat-ul-Wujuud. Na sababu ya hili ni ujinga, ya

kwamba ni wajinga. Kwa kuwa Suufiyyah kama mnavyojua, hawaonelei mtu

kutafuta elimu. Wanasema msisome kwa kuwa kutafuta elimu

kutawashughulisha na ´Ibaadah na kumdhukuru Allaah. Fanyeni ´Ibaadah na

Dhikr, elimu itawajia kutoka kwa Allaah (Jalla wa ´Alaa). Shaytwaan ndio

anawaambia hivi. Ndio maana wanatumbukia katika waliyotumbukia.

119. Maana Ya "Hayaat al-Barzakhiyyah"

Swali:

Nini makusudio ya uhai wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

kaburini mwake ni "Hayaat al-Barzakhiyyah"?12

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni kama mashahidi wengine. Hayaat al-Barzakhiyyah maana yake ni kwamba

ni katika mambo ya Aakhirah na sio kama uhai wake wa duniani. Na kwa ajili

hiyo, Maswahabah hawakuwa wakienda katika kaburi lake na kusema Mtume

yuko hai, wakimuuliza na kumuomba. Hawakuwa wakifanya hivi. Japokuwa

12 Maisha ya ndani ya kaburi

Page 66: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

66

yuko hai, lakini ni "Hayaat al-Barzakhiyyah", ni uhai hususan wa Aakhirah.

Mfano wa uhai wake huu sio kama uhai wake wa duniani. Kuna tofauti.

120. Tafsiri Ya Kauli Ya Allaah "Hapana Kulazimisha Katika Dini"

Swali:

Kauli ya Allaah Ta´ala:

ين ل إكراه في الد

"Hapana kulazimisha katika Dini (kuingiza iymaan katika moyo wa mtu)"

(02:256)

Kuna ambao wanaitumia kama dalili na kusema ya kwamba mtu ana uhuru

wa moja kwa moja katika Dini yake. Maneno haya ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Lau yangekuwa ni sahihi kusingelikuwa na haja ya kutuma Mitume na

kuteremsha vitabu na kuwekwa Jihaad katika njia ya Allaah. Kila mmoja

angelikuwa huru na kila mmoja anaabudu atakacho. Na wala kusingelikuwa

haja ya kitu. Haya maneno ni batili. "Hapana kulazimisha katika Dini" hakuna

yeyote awezae kuiingiza Dini kwenye moyo wa yeyote au kumfanya mtu

akaipenda Dini isipokuwa Allaah (Jalla wa ´Alaa). Hakuna yeyote anayemiliki

moyoni na kuiendesha. Hii ndio maana ya:

"Hapana kulazimisha katika Dini."

121. Mtu Kama Huyu Ndie Mwenye Udhuru

Swali:

Lini hupewa mjinga udhuru kwa ujinga wake katika masuala ya ´Aqiydah?

Page 67: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

67

´Allaamah al-Fawzaan:

Atapokuwa hana mtu yeyote wa kumfunza. Hapati mtu wa kumfunza,

kumuuliza, atapewa udhuru mpaka atapopata wa kumfunza na kumuelekeza.

Na je, leo masuala ya ´Aqiydah yamefichikana ilihali yanafunzwa na

kuenezwa? Katika vyombo vya khabari mashariki na magharibi na yanasikia

watu wote. Allaah (Jalla wa ´Alaa) kutokana na Hekima Yake Kaweka vitu

hivi ili kufikisha Dini hii. Ilipokuwa Dini hii imetumilizwa kwa wanaadamu

wote, Akaweka vya kuifikisha, kwanza kwa Jihaad. Ilipokuwa Jihaad

haiwezekani, kukaja vyombo vya khabari hivi vinavyowafikishia Dini watu

wote sawa wa mashariki na magharibi. Alhamduli Allaah. Hakuna yeyote

mwenye udhuru leo.

122. Kwanini Raafidhwah Wanawatukana Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum)

Swali:

Ipi sababu ya Raafidhwah13 kuwatukana Maswahabah (Radhiya Allaahu

´anhum)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mmesikia. Ni kwa sababu wanachukia Uislamu, na Maswahabah wao ndio

waliosimamisha Uislamu. Waliusimamisha katika uhai wa Mtume (Swalla

Allaahu ´alayhi wa sallam) na baada ya kufa kwa Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam). Kwa ajili hiyo, ndio maana wakawa wenye kuwaponda

wapokezi na wabebaji wake. Walioufikisha katika Ummah. Hawakuwatukana

kwa jengine ila ni kwa sababu hii. Ni kwa ajili ya nini? Isipokuwa ni kwa

sababu ni wao ndio waliisimamisha Dini hii na kuifikisha.

13 Raafidhwah au Rawaafidhw ni kundi katika Mashia, na ndio kundi ovu zaidi.

Page 68: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

68

123. Kuziwekea Hadiyth Sahihi Majaaz

Swali:

Mwenye kuziwekea Hadiyth zilizothibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu

´alayhi wa sallam) majaaz14 kwa ajili ya taawili ya kiakili, huzingatiwa ni

katika Ahl-ul-Ahwaa15?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Ikiwa anaziwekea majaaz ili kubadili maana yake ya sahihi, ni katika

Ahl-ul-Ahwaa.

124. Mwenye Kuwatukana Wake Wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)

Swali:

Anayewaponda wake wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa

kuwatukana na Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum),anakufuru na kwa

nini?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Kwa kuwa anaewatukana wake wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) anamtukana Allaah (´Azza wa Jalla). Kwa kuwa Allaah ndio ambaye

Kamchagulia wake hawa Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

14 Kuziwekea mafumbo; yaani kwa mfano badala ya kuthibitisha Sifa Tukufu za Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) kama ya Mikoni, Mguu na nyinginezo wao watu wa Bid´ah wanasema “neema”, “amri Yake” na taawili kama hizo. 15 Watu wanaofuata matamanio; yaani watu wa Bid´ah

Page 69: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

69

Na vipi Allaah Atamchagulia Mtume Wake wake wenye kutukanywa? Hali

kadhalika anamtukana Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Vipi

atakuwa mke wa Mtume ambaye ni mama wa waumini juu yao kuna aibu au

kasoro? Na anakuwa katukana Ijmaa´ ya Ummah ambayo imekubaliana

fadhila za mama wa waumini, na kwamba wao ndio mama wa waumini, na

wake zake ni mama zao - hili lipo katika Qur-aan. Je, hivi kweli wewe

unaridhia mtu kumtukana mama yako? Mama yako wa nasaba huwezi

kuridhia mtu kumtukana, tusemeje mama yako katika Dini ambaye ni wake

wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)? Vipi utaridhie mtu

kumtukana? Mama yako wa Dini ni mkubwa kuliko mama yako wa nasaba na

hili halina shaka. Hakuna shaka ya kuwa, mwenye kukusudia kuwatukana

wake wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) - mwenye kukusudia hili

- basi huyo ni kafiri.

Hali kadhalika Maswahabah, mwenye kukusudia kuwaponda huyo ni kafiri.

Kwa kuwa Allaah (Jalla wa ´Alaa) Anasema:

ليغيظ بهم الكفاار

"Ili liwaghadhibishe makafiri." (48:29)

125. Kuwasikiliza Wapiga Visa

Swali:

Ipi hukumu ya kusikiliza wapiga visa kwa ajili ya kutengenemaa kwa kuwa

mimi siwezi kukaa kwenye duruus za elimu kwa Wanachuoni. Sifahamu

mustwalaha wa kielimu ya Kishari´ah ambao wanausema?

´Allaamah al-Fawzaan:

Usikae na wapiga visa. Salaf walikuwa wakihadhari dhidi ya wapiga visa

ambao wanajishughulisha sana na hadithi hata kama itakuwa ni uongo. Na

wanatumia nguvu nyingi kwa kupiga visa ambavyo wanadai vinaathiri watu.

Wala hawatumii nguvu zao katika Qur-aan na Sunnah. Msingi wao

umejengeka juu ya kupiga visa na hadithi. Salaf walikuwa wakihadhari watu

Page 70: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

70

kama hawa na kuwasikiliza.

126. Kuanza Kuwalingania Ma´ulamaa Wapotofu Ni Bora Zaidi Kuliko Kuanza Na `Awwaam Wao

Swali:

Je, wanalinganiwa ma´ulamaa wapotofu kama wanavyolinganiwa

´Awwaam16 wao katika Rawaafidhw na Qubuuriyyuun?

´Allaamah al-Fawzaan:

Bila shaka. Da´wah ni wajibu sawa kwa ma´ulamaa wao na ´Awwaam wao.

Da´wah ni wajibu. Na lau wataongoka ma´ulamaa wao pia ´Awwaam wao

wataongoka, huenda wakatubu baadhi yao ikawa ni sababu ya kuongoka

wengi katika wafuasi wao. Kuanza kwa ma´ulamaa wao, bila ya shaka hili ni

bora kuliko kuanza kwa ´Awwaam wao.

127. Kuuliza Daraja Ya Hadiyth

Swali:

Mwenye kuuliza usahihi wa Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa

sallam) huchuliwa ni mwenye shaka na Hadiyth yake (´alayhis-Salaam)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hapana. Anayeuliza daraja ya Hadiyth, huyu ni kwa ajili anataka

kuhakikisha. Na hili ni wajibu kwake kuuliza na kujua usahihi wa Hadiyth

kama ni dhaifu, au ni maudhu´ah n.k. Huku ni kuhakikisha na si kuwekea

16 Watu wa kawaida wasiokuwa na elimu

Page 71: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

71

shaka. Kuwekea shaka ni pale ambapo Hadiyth itasihi kisha akawa na shaka

maana yake na kuifanyia kazi. Akasema haifai Hadiyth hii katika wakati huu,

huyu ndiye mwenye kuwekea shaka na mpotofu. Allaah Atukinge. Ama

kutafuta daraja ya Hadiyth ili ahakikishe, hakuna ubaya wa hilo.

128. Asiyemuombea Du´aa Mtawala Wa Waislamu Ni Mtu Wa Bid´ah

Swali:

Je, ni sahihi yaliyosemwa na baadhi ya wanachuoni ya kwamba:

"Asiyemuombea Du´aa mtawala, hakika huyo ni mtu wa Bid´ah"?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Hili limethibiti kutoka kwa Salaf. Wamesema ukimuona mtu

hamuombei Du´aa mtawala, basi mtuhumu katika Dini yake. Nadhani hata

katika kitabu hichi [Sharh-us-Sunnah Lil-Barbahaariy] yamo tutayapitia.

129. Kutoka Siku 40 Ni Katika Bid´ah Za Suufiyyah

Swali:

Je, kuwalazimisha watu kutoka kwa ajili ya Da´wah siku 40, mwezi na miezi

40 ni katika kujikalifisha kunakolaumiwa au ni katika juhudi katika kheri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hili ni katika Bid´ah. Haliwezi kuitwa kuwa ni kujikalifisha kunakolaumiwa

tu, bali tendo hili huitwa kuwa ni Bid´ah. Hizi ni katika Bid´ah za Suufiyyah.

Na hakuna katika Da´wah kutoka masiku, miezi 40 au kadha na kadha. Yote

haya ni katika Bid´ah ambayo Allaah Hakuteremsha chochote kuhusiana na

hilo.

Page 72: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

72

130. Hadiyth Hii Inajuzisha Kutoka Na Jamaa´at-ut-Tabliygh?

Swali:

Wanatumia baadhi yao [Jamaa´at-ut-Tabliygh] kwa Hadiyth Swahiyh

isemayo:

"Kwa hakika huu ni mji muovu, akaenda katika mji mwingine ambapo

Anatiiwa Allaah"

Kujuzisha kutoka na Jamaa´at-ut-Tabliygh. Dalili hii ni sahihi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mashaa Allaah!! Hadiyth hii iko wapi na Jamaa´at-ut-Tabliygh? Hii ni katika

Hijrah, hii ni safari ya Hijrah ewe ndugu. Na sio safari ya [... sauti haiko wazi...

], hii ni safari ya Hijrah. Katoka kama Muhaajir.

131. Kwenda Na Jamaa´at-ut-Tabliygh KufanyaDa´wah Katika Miji Ya Makafiri

Swali:

Ipi hukumu ya kutoka na Jamaa´at-ud-Da´wah17 kwenda kulingania katika

miji ya makafiri?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mwenye kutaka kufanya Da´wah atapata nafasi na alinganie kwa Allaah

sehemu yoyote bila yayeye kujiunga na kundi au chama. Ikiwa yuko na elimu,

alinganie kwa Allaah yeye mwenyewe bila ya kujiunga na makundi na

vyama, kwa kuwa mambo haya ndani yake kunaingia baadhi ya vitu, baadhi

ya mifumo - kama mnavyojua - alinganie kwa Allaah na wala asiwe

17 Jamaa´at-ut-Tabliygh

Page 73: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

73

amejiunga na yeyote. Na wala hahitajii kutoka wala kuingia. Alinganie kwa

Allaah sehemu yoyote atapopata fursa.

132. Nikiingia Nyumba Na Hakuna Mtu Nitoe Salaam?

Swali:

Muislamu atoe Salaam atapoingia nyumba isiyokuwa na mtu hata mmoja?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio, toa Salaam.

فإذا دخلتم بيوتا فسلموا على أنفسكم

"Mtakapoingia majumbani toleaneni salamu." (24:61)

Hii ni kwa jumla. Na nyumba haikosi Malaika, majini Waislamu n.k.

133. Radd Kwa Madu´aat Wanaojuzisha Kutibu Uchawi Kwa Uchawi

Swali:

Nataka bayana na kuwekewa wazi katika masuala ya hukumu ya kutibu

uchawi kwa kutumia uchawi mfano wake, kwa kuwa tumesikia baadhi ya

wanaodai wana elimu wakisema ya kwamba hilo linajuzu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Kutibu uchawi kwa kutumia uchawi mfano wake haijuzu. Na ni kufuru. Kwa

kuwa uchawi ni kufuru sawa kujifunza nao na kuufunza na kuutumia. Sawa

autumia ili kutibu uchawi au kautumia ili kuwadhuru watu. Anasema

(Ta´ala):

Page 74: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

74

حر وما أنزل على الملكين ببابل هاروت ياطين كفروا يعلمون النااس الس كنا الشا ـ ن من أحد وماروت وما يعلماول

ما نحن فتنة فل تكفر ى يقول إنا حتا

"Lakini shayaatwiyn ndio waliokufuru; wanafundisha watu uchawi na

yaliyoteremshwa kwa Malaika wawili (katika mji wa) Baabil Haaruwt na

Maaruwt. Na (hao Malaika wawili) hawamfundishi yeyote mpaka

wamueleze: “Hakika sisi ni fitnah (mtihani), basi usikufuru (kufanya

uchawi)".” (02:102)

Yaani msijifunze uchawi. Ni dalili ioneshayo ya kwamba uchawi ni kufuru.

Mwisho wa Aayah Anasema:

من خلق اشتراه ما له في الخرة ولقد علموا لمن

"Na kwa hakika walielewa kwamba atakayenunua (atayefanya biashara ya

uchawi) hatopata katika Aakhirah fungu lolote." (02:102)

Yaani hana katika Pepo fungu. Na hili haliwi isipokuwa kwa kafiri. Allaah

Atukinge. Vipi atajitokeza mwenye kusema ya kwamba inajuzu kutumia

uchawi? Yaani mtu ajitibu kwa kufuru?

Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema:

"Msijitibu kwa haramu."

Na uchawi ni haramu kubwa.

Na Ibn Mas´uud (Radhiya Allaahu ´anhu) anasema - kama ilivyo katika

Swahiyh al-Bukhaariy:

"Kwa hakika Allaah Hakufanya dawa yenu katika yale Aliyowaharamishia."

Na uchawi ni haramu kwetu.

"Allaah Hakuteremsha ugonjwa ila Kateremsha dawa yake."

Uchawi una dawa isiyokuwa kufuru na uchawi. Maneno haya hafikirii [uzito

ulionayo] mwenye nayo, na lau angelifikiria sidhani kama angelijuzisha kwa

kukimbilia kutoa Fatwa kama hii. Tunamuomba kwa Allaah uongofu, al-

Baswiyrah, kurejea katika haki. Isitoshe, tukifungua mlango kujuzisha

wachawi kuwatibu watu tutabaki nao katika mji na uchawi ukaenea katika mji

kwa hoja ya kwamba mtu huyu anawatibu watu. Yaa Subhaana Allaah!

Page 75: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

75

Hafikirii huyu matukio yake? Hivi kweli hamuogopi na kumcha Allaah

(Ta´aal) kwa kuwadanganya kwake watu kwa udanganyifu kama huu?

134. Kuswali Nyuma Ya Qubuuriyyuun18

Swali:

Inasihi kuswali nyuma ya waabudu wa makaburi kwa kuwa wanasema "Laa

ilaaha illa Allaah, Muhammad Rasuulu Allaah"?

´Allaamah al-Fawzaan:

Haisihi. Kwa kuwa kuabudu kwao makaburi kunavunja kauli yao "Laa ilaaha

illa Allaah, Muhammad Rasuulu Allaah." Hivyo, si kila mwenye kusema Laa

ilaaha illa Allaah Muhammad Rasuulu Allaah anakuwa Muislamu isipokuwa

mpaka aifanyie kazi na ajitenge na yanayoivunja.

135. Kusoma Siyrah19 Ya Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum)

Swali:

Kusoma Siyrah ya Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) na kujua

walivyokuwa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) huchukuliwa ni

katika ukaribisho unaomkurubisha mtu kwa Allaah (´Azza wa Jalla)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ndio. Ni katika kujikurubisha na ni katika ´Aqiydah pia. Hili ni katika

´Aqiydah kwa kuwa katika misingi ya ´Aqiydah ni kuwapenda Maswahabah

18 Waabudu makaburi 19 Historia

Page 76: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

76

wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Na huwezi kujua

fadhilah zao na manzilah yao isipokuwa ukisoma Siyrah yao na hali zao.

136. Kusikiliza Visa Vya Tofauti Za Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum)

Swali:

Ipi hukumu ya kusikiliza visa kwa yaliyopitika baina ya Maswahabah

(Radhiya Allaahu ´anhum)?

´Allaamah al-Fawzaan:

Usisikilize, kwa kuwa huenda ukaingiwa katika nafsi yako [na shubuha].

Usisikilize mikanda hii au ukasoma vitabu hivi. Jiweke navyo mbali. Ila tu

kwa yule mwenye elimu ya sawa sawa na anataka kuvipiga Radd, atavipitia

kwa dharurah au akasikiliza [mikanda] hiyo kwa dharurah ili aipige Radd.

137. "Shikamaneni Na ´Atiyq, Na Tahadharini Na Mambo Ya Kuzua"

Swali:

Yapi maoni yako kwa andiko hili:

"Shikamaneni na ´Atiyq, na tahadharini na mambo ya kuzusha."?

´Allaamah al-Fawzaan:

´Atiyq yaani waliokuwemo Salaf. Maana yake ni sahihi. ´Atiyq yaani ya

zamani waliokuwemo Salaf-us-Swaalih.

Page 77: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

77

138. Kusema Neno "Sayyidna" Abu Bakr (Radhiya Allaahu ´anhu) Inajuzu?

Swali:

Kusema "Sayyidna" (bwana wetu) kwa Abu Bakr na Maswahabah wengine

waliobaki (Radhiya Allaahu ´anhum) inajuzu? Na je, kumekuja Hadiyth

kutokakwa Mtume (´alayhis-Salaam) inayosema: "Msiniite bwana katika

Swalah"?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ama kuhusiana na Hadiyth hiyo, mimi sijui. Ama kusema Sayyidna Abu

Hurayrah, Sayyidna Abu Bakr na kadhalika huku ni kuwatukuza na

kuwaheshimu. Halina ubaya In Shaa Allaah.

139. Kushahidilia Swahabah Fulani Kuwa Peponi Pasina Ushahidi

Swali:

Ikiwa tunashahidilia Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) wote wako

Peponi, wamekufa waumini, Allaah Kawaridhia nao wamemridhia, kwa nini

tusimshahidilie mmoja wao binafsi ya kuwa yuko Peponi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Hatushahidilii ila kwa dalili. Lakini tunasema kwa ujumla ya kwamba

Maswahabah wote wako Peponi, kwa ushahidi wa Allaah na Mtume Wake

(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Ambaye kafa katika Uislamu, ama

aliyeritadi ni katika watu wa Motoni.

140. Kusema Kuwa Pepo Au Moto Utaisha

Page 78: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

78

Swali:

Anakufuru anayesema Pepo na Moto vitakwisha, au Pepo tu au Moto tu?

´Allaamah al-Fawzaan:

Enyi ndugu! Mimi ninawanasihi kutoingia katika masuala haya. Ikiwa kuna

mwanachuoni yeyote aliyekosea na akaingia humo, usifuate jambo hili. Sisi

tunaamini Pepo na Moto, na kwamba vimeumbwa, na kwamba Pepo ni

nyumba ya wachaji Allaah na Moto ni nyumba ya makafiri. Ipi faida ya

kwamba vitaisha au havitosha? Hatuingii katika hili na wala hakuna faida

nyuma ya hili. Ikiwa kuna yeyote katika wanachuoni aliyekosea, sisi

tunamtakia Rahmah, kumuombea maghfirah na tunaacha maudhui haya na

wala hatuyaenezi kwa watu.

141. Kusema Kafiri Fulani Kafa Katika Ukafiri Na Ni Wa Motoni

Swali:

Swali hili limekariri. Akifa mtu na tunajua ya kwamba kafa kafiri, tushahidilie

kwa binafsi yake ya kwamba ni katika watu wa Motoni?

´Allaamah al-Fawzaan:

Unajuaje kuwa kafa kafiri? Unajua Ghayb? Pengine katubu na wewe hujui?

Unatakiwa kusema, yadhihirika kwangu ya kwamba kafa katika ukafiri,

yadhihirika kwangu kadha na ninakhofia kuwa kafa kafiri. Ama kuhusisha

kwa kusema kafa katika ukafiri, huku ni katika kudai kujua elimu ya Ghayb.

142. Kusema Fulani Kafa Shahidi

Swali:

Page 79: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

79

Ipi kauli sahihi kwa kusema kwetu ya kwamba fulani ni shahidi? Kumekithiri

siku hizi kusema neno hili.

´Allaamah al-Fawzaan:

Hali kadhalika, hatuhukumu ya kwamba fulani ni shahidi ila yenye kuonesha

dalili. Ama wengine, sisi tunatarajia kwao Shahaadah. Tunatarajia na wala

hatusemi "ni shahidi", bali tunasema tunatarajia kwake Shahaadah. Kwa kuwa

kuhukumu ya kwamba ni shahidi, hili linahitajia kujua makusudio yake [ya

moyoni]. Je, anapigana kulinua Neno la Allaah? Vita hivi vinajuzu au hapana?

Si kila mwenye kupigana anaambiwa kuwa ni shahidi.

143. Ashaa´irah Ni Katika Ahl-us-Sunnah wal-Jamaa´ah?

Swali:

Je, al-Ashaa´irah na Maaturidiyyah ni katika Ahl-us-Sunnah?

´Allaamah al-Fawzaan:

Mwenye kwenda kinyume na Ahl-us-Sunnah sio katika wao. Na al-

Ashaa´irah wanategemea ´Ilm-ul-Mantwiq na ´Ilm-ul-Kalaam katika

´Aqiydah. Wanachukua ´Aqiydah yao katika ´Ilm-ul-Mantwiq, vipi watakuwa

ni katika Ahl-us-Sunnah? Upokeaji (utegemezi) wao sio kama Ahl-us-Sunnah.

144. Tunapenda Haki Zaidi Kuliko Fulani

Swali:

Page 80: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

80

Je, inatakikana kwa wanafunzi kusambaza Radd ya mwanachuoni kwa yule

aliyemradi?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ikiwa hili lina maslahi, ndio. Ikiwa kuisambaza hiyo Radd kuna maslahi ya

kutahadharisha madhehebu haya, au kauli hii, hilo halina shaka. Tunaipenda

haki zaidi kuliko fulani. Hatumlindi fulani au karama za fulani, kama

wanavyosema na kuiacha haki.

145. Kuridhia Qadhwaa20 Na Qadar21 Ni Wajibu

Swali:

Kuridhia Qadhwaa na Qadar ni wajibu au amustahaba22?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni wajibu. Kuridhia Qadhwaa na Qadar, ina maana kuviamini na kuviitakidi.

Ama kuridhia maradhi na kadhalika, hili si lazima ya wewe kuridhia maradhi.

Lakini unalazimika kusubiria hilo, ama kuridhia hilo hili halikulazimi. Lakini

subiria hilo na usikasirike na kulalamika.

146. Uwajibu Wa Kujirejea Unapokosea

Swali:

Ipi hukumu ya mwenye kufasiri kitu kwa kutegemea dalili kisha ikambainikia

ya kwamba tafsiri yake ni ya makosa. Lipi lililo la wajibu kwake?

20 Aliyopanga Allaah 21 Aliyokadiria Allaah 22 Jambo linalopendekezwa

Page 81: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

81

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni wajibu kwake kurejea kosa lake. Na ikiwa kosa hili lilienea kwa watu,

inampasa kuwabainishia hili watu na kwamba amejirejea.

147. Kuongea Ni Katika Sifa Ya Allaah Ya Kimatendo

Swali:

Sifa ya kuongea kwa Allaah ni ya kidhati au kimatendo au ni yote mawili?

´Allaamah al-Fawzaan:

Ni kujikalifisha kulikoje huku? Inatosha kwako kusema, Maneno ya Allaah

(Subhaanahu wa Ta´ala) ni katika Sifa za matendo yake. Maneno ni katika Sifa

za matendo, aifanyayo wakati Atakapo (Subhaanahu wa Ta´ala) na kwa

namna Atakayo. Na wala hatuingii katika kupindukia kama huku.

148. Madu´aat Wasiolingania Katika Tawhiyd Wala Hawaonyi Dhidi Ya

Mubtadi´ah Na Bid´ah

Swali:

Muulizaji anauliza, jee dhawabiti hii ni sahihi:

"Yule ambaye halinganii katika Tawhiyd na wala haonyi dhidi ya Shirki,

Bid´ah na Ahl-ul-Bid´ah, (mtu huyo) ni Mubtadiy´23 na yule asiyembadiy´24 na

yeye ni Mubtadiy´ kama yeye"?

23 Mtu wa Bid´ah 24 Asiyemtia katika Bid´ah

Page 82: Fataawa Za Sharh-Us-Sunnah Ya Barbahaariy - ´Allaamah al-Fawzaan

82

´Allaamah al-Fawzaan:

Mtu huyu ikiwa anajinasibisha na Da´wah katika Dini ya Allaah na wala hajali

Tawhiydi na wala hajali Shirki na haonyi dhidi yake na kuhamasisha

kushikamana na Sunnah, huyu anakwenda kinyume na Manhaj ya Mitume

(´alayhis-Swalaat was-Salaam). Ni mbaya zaidi kuliko hata Mubtadiy´. Huyu

anakwenda kinyume na Manhaj ya Mitume (´alayhimus-Salaam). Kwa kuwa

Mitume walikuwa wakiijali ´Aqiydah na wakiibainisha na kuonya dhidi ya

Shirki. Wakabainisha hukumu za Kishari´ah na kuziweka wazi. Hii ndio

Manhaj ya Mitume na wafuasi wa Mitume (´alayhimus-Salaam).

Chanzo: http://www.alfawzan.af.org.sa/alldroos?tid_1=164

Swalla Allaahu ´alaa Muhammad, wa ´alaa aalihi wa Aswhaabihi wa sallam.