mofolojia ya kiswahili · web viewkatika lugha ya kiswahili viambishi ni vingi. na kama...

75
Mofolojia ya Kiswahili 2018 OSW 233 MOFOLOJIA YA KISWAHILI (NUKUU) MUHADHARA WA KWANZA 1: MOFOLOJIA Fasili ya Mofolojia Mofolojia ni taaluma ya isimu inayoshughuliki muundo wa maneno. Ni taaluma inayoshughulikia vipashio vya lugha na mpangilio wake katika uundaji wa maneno. Mofolojia : ni utanzu mmojawapo katika tanzu za isimu Tanzu hizo za isimu ni: 1.Mofolojia 2.Fonolojia 3.Sintaksia 4. Semantiki na 5.Pragmatiki Uhusiano wa Mofolojia na matawi mengine ya isimu Mofolojia na fonolojia Vipashio vya kifonolojia (fonimu) ndivyo vitumikavyo kuunda vipashio vya kimofolojia (mofimu). Mfano soda limeundwa kwa fonimu /s/, /o/, /d/, /a/ na bibi limeundwa kwa fonimu /b/, /i/, /b/, /i/ Kanuni za kifonolojia huweza kutumika kuelezea maumbo ya kimofolojia ambayo yanaathiriana. Mfano: mofimu ya umoja katika ngeli ya kwanza inajitokeza kama m- ikifuatiwa na konsonanti ila hujitokeza kama mw- ikifuatiwa na irabu (m + ti = mti, mu + eupe = mweupe). Mofolojia na sintaksia Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 1

Upload: others

Post on 07-Feb-2020

93 views

Category:

Documents


5 download

TRANSCRIPT

Page 1: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

OSW 233 MOFOLOJIA YA KISWAHILI (NUKUU)

MUHADHARA WA KWANZA 1: MOFOLOJIA

Fasili ya MofolojiaMofolojia ni taaluma ya isimu inayoshughuliki muundo wa maneno. Ni taaluma inayoshughulikia vipashio vya lugha na mpangilio wake katika uundaji wa maneno.

Mofolojia : ni utanzu mmojawapo katika tanzu za isimu

Tanzu hizo za isimu ni:

1. Mofolojia2. Fonolojia3. Sintaksia4. Semantiki na5. Pragmatiki

Uhusiano wa Mofolojia na matawi mengine ya isimu Mofolojia na fonolojia

Vipashio vya kifonolojia (fonimu) ndivyo vitumikavyo kuunda vipashio vya kimofolojia (mofimu). Mfano soda limeundwa kwa fonimu /s/, /o/, /d/, /a/ na bibi limeundwa kwa fonimu /b/, /i/, /b/, /i/

Kanuni za kifonolojia huweza kutumika kuelezea maumbo ya kimofolojia ambayo yanaathiriana. Mfano: mofimu ya umoja katika ngeli ya kwanza inajitokeza kama m- ikifuatiwa na konsonanti ila hujitokeza kama mw- ikifuatiwa na irabu (m + ti = mti, mu + eupe = mweupe).

Mofolojia na sintaksia

Vipashio vya kimofolojia (mofimu/neno) huunda daraja ya sintaksia. Mfano: sentensi walitusafirisha imeundwa na mofimu wa-li-tu-safiri-sh-a

Mabadiliko ya umbo la mofimu/neno huathiri muundo wa sentensi nzima (mf. umoja na wingi).

(i) Mtoto mefu mweusi anakuja(ii)Watoto warefu weusi wanakuja

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 1

Page 2: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Mofolojia na semantiki

Semantiki ni taaluma ya maana. Mofimu ni kipashio cha lugha chenye maana mfano; neno kisu lina mofimu mbili ambazo ni ki- umoja na – su ya mzizi. Ukizigawanya zaidi mofimu hizi utapata k-i-s-u; ambazo ni sauti/herufi zisizo na maana na si mofimu. Hivyo mofimu si umbo ni maana – ikiwa ni ya kisarufi au ya kileksika.

Mofolojia hujishughulisha na uundaji wa maneno katika lugha husika; msingi wa neno ni maana. Hivyo mpangilio wa mofimu usioleta maana katika lugha husika hauwezi kutambuliwa kama neno. Mfano. palingunywi ni mfuatano wa fonimu uliozingatia taratibu za lugha ya Kiswahili lakini si neno la Kiswahili kwa sababu halina maana katika lugha hiyo.

Mambo ya kuzingatia katika taaluma ya mofolojia

Uundaji wa maneno

Hapa tunaangalia vijenzi vya neno husika. Kwa mfano neno limeundwa na mofimu huru pekee kama papai, mofimu huru na mofimu tegemezi kama mpapai (m + papai) au mofimu tegemezi tupu kama mtu (m + tu).

Katika uundaji wa maneno tunaangalia vilevile njia mbalimbali za uundaji wa maneno katika lugha ya Kiswahili kama vile kutohoa, uambatishaji, urudufu, uhulutishaji, uambishaji, n.k.

NJIA ZA UUNDAJI WA MANENO /ISTILAHI/ MSAMIATIUundaji wa maneno ni mchakato unaowezesha lugha kujiongezea msamiati ili kukidhi haja ya mawasiliano na kuendana na mabadiliko yanayotokea kila siku.

Maneno ya lugha ya Kiswahili hayaundwi kiholela bali hufuata taratibu na kanuni zinazokubalika kitaalamu.

Njia zitumikazo kuunda maneno ni kama zifuatazo:

Unyambuaji

Njia hii inatumia mzizi mmoja wa neno na kuzalisha maneno mapya kwa kupachika viambishi nyambuaji.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 2

Page 3: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Mfano

soma

Somo

Kisomo

Msomi

Msomaji

lima

Mkulima

Kilimo

Mlimaji

Uambatishaji/mwambatano

Hii ni njia ya kuunda maneno mapya kwa kuambatanisha maneno mawili.

Mfano

Mwana+chama - Mwanachama

Askari+kanzu – Askarikanzu Bwana+shamba - Bwanashamba

Urudufishaji / Uradidi

Hii ni mbinu ya kurudiarudia neno au sehemu ya neno na kuunda neno jipya ambalo huwa na maana tofauti na maneno yanayorudiwarudiwa.

Mfano

(a) Pole : polepole

(b) Sawa : sawasawa

(c) Haraka : harakaharaka

Akronimu/ufupishajiMaeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 3

Page 4: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Ufupishaji ni njia mojawapo ya kuunda maneno mapya, ufupishaji huweza kufanyika kwa namna mbili ambazo ni.

Kufupisha kwa kuchukua herufi za mwanzo MfanoCWT (Chama cha Walimu Tanzania) VVU (Virusi Vya Ukimwi)

Kufupisha kwa kuchukua silabi za mwanzo za maneno yanayofupishwa

Mfano

BAKITA (Baraza la Kiswahili la Taifa)

TUKI (Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili)

TATAKI (Taasisi ya Taaluma za Kiswahili)

Uhulutishaji

Ni njia ya kuunda maneno mapya kwa kuchukua vijisehemu vya neno pasipo kufuata kanuni yoyote.

Mfano:

Mnyama mfu – nyamafuChakula cha jioni – chajioHati za kukataza – hatazaMtu asiye kwao - msikwao

Utohoaji

Ni uchukuaji wa maneno toka lugha moja na kuyatumia kwenye lugha nyingine baada ya kuyarekebisha kimatamshi na kimaandishi ili yaendane na sarufi ya lugha inayotohoa.

Mfano

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 4

Page 5: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Neno Lugha asilia Kiswahili

Shirt Kiingereza Shati

Schule Kijerumani Shule

Bakura Kiarabu Bakora

Benjera Kireno Bendera

Matching guys Kiingereza Machinga

KuchukuaHii ni mbinu ya kuongenza maneno kwa kuyachukua toka lugha yake ya asili na kuyatumia kama yalivyo katika lugha inayotohoa. Uchukuaji hufanyika kwa lugha zinazoendana kisarufi kama Kiswahili na lugha za kibantu.

MfanoKitivo — kisambaa /kipareIkulu - kinyamweziKigoda - kizaramo

Kubadili mpangilio wa fonimu

Mfano

Lima – mila – imla - mali

Kufananisha umbo /sauti /tabia

MfanoKufananisha umbo Kifaru-(mnyama faru)Mkono wa tembo-(mkonga wa tembo)Kidole tumbo-(umbo la kidole)Kufananisha TabiaUbeberu-(beberu la mbuzi)Ukupe-(mdudu kupe)

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 5

Page 6: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Kufananisha SautiPikipiki (mlio wa pikipiki)Mtutu (mlio wa bunduki)Nyau (mlio wa paka)Kuku - kokoriko (mlio wa kuku)

Njia ya udondoshaji

Mfanomkwe wake - mkwewe mwana wake - mwanawe ndugu yake – nduguye

Kuzingatia matumizi ya kitu

MfanoBanio - (kubana) Chanio - (kuchana) Fyekeo - (kufyeka)Kutarjumi/kutafsiriMfano;Fluid – (ugiligili)Acquired immunal deficiency syndrome - Upungufu wa kinga mwiliniHuman immunal virus – virusi vya ukimwiAnti-rentro-virus - dawa za kufubaza makali ya ukimwi

Makundi na mahusiano ya maneno

Taaluma ya mofolojia inaangalia pia makundi ya aina za maneno kama vile nomino, kitenzi, kivumishi, kielezi, n.k. na wakati huohuo huchunguza uhusiano uliopo baina ya makundi hayo ya maneno. Kwa mfano kuna uhusiano wa moja kwa moja baina ya nomino na kivumishi au baina ya kitenzi na kielezi wakati ambapo hakuna uhusiano huo baina ya kitenzi na kivumishi au baina ya nomino na kielezi. Aidha, hakuna uhusiano wowote wa kisarufi baina ya vihisishi na maneno mengine yaliyomo katika tungo.

Kanuni za uundaji wa maneno

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 6

Page 7: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Uundaji wa maneno hufuata kanuni mbalimbali za kimofolojia na za kimofofonolojia. Miongoni mwa kanuni zinazotawala katika kuunda maneno ni kama vile uyeyushaji, ukaakaishaji, odondoshaji, uingizaji, tangamano la irabu, mvutano wa irabu, n.k.

Hivyo mwanaisimu yeyote anayejishughulisha na uwanja huu wa mofolojia lazima ayajue na kuyazingatia kwa kina mambo haya.

MUHADHARA WA 2 : MOFU NA MOFIMU

MOFU

Fasili ya mofuMofu ni kipashio cha kimofolojia kiwakilishacho mofimu.kutokana na maana hii twaweza kusema mofu ni kiwakilishi na mofimu ndiyo iwakilishwayo na mofu.

Mofu ni umbo linalositiri mofimu. Hivyo mofu ni umbo tu linalodhihirika kimatamshi kama fonimu/sauti na kimaandishi kama herufi.

Aina za mofuMara nyingi mofu huainishwa kwa kutumia vigezo vikuu viwili. Kigezo cha kwanza ni kwa mujibu wa maana iwakilishwayo na mofu na kigezo cha pili ni kwa mujibu wa muundo/mofolojia ya mofu yenyewe. Kwa kutumia kigezo cha maana iwakilishwayo na mofu tunapata mofu huru, mofu funge na mofu tata.

Mofu huruNi yale maumbo yanayobeba maana zinazojitosheleza/kamili. Katika Kiswahili mizizi ya maneno mengi huwa ni mofu huru kwa mfano nomino (baba, kalamu, Magomeni, n.k.), vivumishi (safi, imara, bora, dhaifu, n.k.), viwakilishi (sisi, wewe, wao, n.k.), vielezi (leo, haraka, taratibu, n.k.) viunganishi (na, halafu, lakini).

Mofu Funge/tegemeziNi maumbo ambayo husitiri maana zisizojitosheleza. Mofu funge huhitaji kufungamana na mofu nyengine ili kuzalisha umbo lenye maana kamili. Kwa mfano; maumbo a, li, tu, lish, na a ni maumbo ambayo hatuwezi kujua maana zake hadi pale maumbo hayo yatakapounganishwa na kuwa umbo

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 7

Page 8: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

moja alitulisha. Hapa sasa tunaweza kufafanua maana zilizofichwa ndani ya maumbo haya ambazo ni:-

Mofu Maana (mofimu)a- Nafsi (ya tatu)

Idadi (umoja)Neli (ya kwanza A-WA)

-li- MtendaWakati (uliopita)

-tu- Nafsi (ya kwanza)Idadi (wingi)

-l- Mzizi-ish- Usababishi/utendeshi-a Dhamira arifu

Mofu tataNi mofu ambazo hubeba maana zaidi ya moja. Mfano neno ‘atanipikia’ lina mofu sita (a-ta-ni-pik-i-a), mofu i- (ya pili kutoka kulia) inawakilisha mofimu/inabeba maana ya utendea ambayo ndiyo chanzo cha utata; kwani yaweza kueleweka kama:

Kupika kwa niaba yangu Kupika kwa ajili yangu

Kigezo cha mofolojia ya mofu tunapata mofu kapa na mofu changamano.

Mofu kapaNi mofu zisizodhihirika kimatamshi wala kimaandishi ila athari zake zipo na zinaeleweka kwa wamilisi wa lugha husika. Mofu hizi huwakilishwa kwa alama Ɵ. Mfano;Umoja wingiu-funguo ƟfunguoƟjani ma-janiƟsimu Ɵsimu

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 8

Page 9: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Mofu changamanoMofu changamano ni mofu ambazo huundwa kwa kuweka pamoja angalau mofu huru mbili au mofu funge na mofu huru na kuunda neno lenye kuleta maana kamili, kwa mfano:Mofu huru + Mofu huru- {fundi} + {chuma} = fundichuma. - {gari} + {moshi} = garimoshi.

Mofu funge + Mofu huru-{mw} + {ana} + nchi = mwananchi. {ki} + {ona} + mbali = kionambali.

MOFIMUMofimu ni kipashio dhahania cha lugha ambacho husitiriwa na mofu. Hivyo tunapozungumzia mofimu tunaangalia zaidi maana ambayo ni dhahania na siyo umbo. Kwa mantiki hii kigezo kikubwa cha kubainisha/kutambua mofimu ni maana.

Aina za mofimu

Mofimu huruNi mofimu inayojitosheleza kimaana bila ya kuongezwa kiambishi cha aina yoyote. Ina uwezo wa kusimama pekee kama neno. Mfano; Maryam, paka, simu, papai, n.k.

Mofimu tegemeziNi aina ya mofimu ambazo hazijitoshelezi kimaana. Mofimu hizi hukamilika kimaana zinapoongezwa mofimu nyengine. Haziwezi kusimama pekee kama neno. Mfano; ki-tabu, m-tu, mu-ana-funz-i, n.k.

Matatizo ya utengaji/ubainishaji wa mofimu Tatizo la kwanza ni kukosekana kwa umbo dhahiri la mofimu

Mfano: θ+chungwa : ma+chungwa

θ+bega : ma+begaθ+jiwe : ma+we

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 9

Page 10: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

θ+shati : ma+shati

Katika mifano hiyo mofimu za umoja ni //θ// na za wingi ni //ma//

Tatizo la pili ni kukosekana maneno asilia yanayozalisha maneno unde.

Mfano:

Fupi – fupika –fupishaRefu - refuka –refusha

*Kau – kauka – kausha

Mifano hiyo ina maneno asilia na maneno unde. Maneno (fupi na refu) ni maneno asilia ya maneno unde fupisha na refusha. Lakini (kau) sio neno asili la neno (kauka na kausha) kwa sababu neno hilo (kau) halikubaliki kwa maneno ya namna hiyo.

Tatizo la tatu ni ugumu wa kutenganisha mofimu katika maneno mwambatano.

Mfano:

Mwanajeshi

Mu-ana-jeshi

Mw-ana-jeshi

Mw-an-a-jeshi

Mw-anajeshi

Maneno mwambatano yanaundwa kwa mzizi zaidi ya mmoja hivyo huwa ni vigumu kubaini mofimu ni zipi na mizizi ni ipi.

KANUNI ZA KUTENGANISHA MOFIMU

Kanuni ya kwanza; zingatia maumbo yenye maana sawa. Maumbo hayo huweza kufanana au kuhitilafiana kiumbo lakini hutokea katika mazingira yaleyale.

Mfano

a) atakupiga

b) atampiga

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 10

Page 11: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

ata-ku-pig-a

a-ta-m-pig-a

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 11

Page 12: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

c) alikupiga -li-ku-pig-a

d) utanipiga -ta-ni-pig-a

e) utatupiga -ta-tu-pig-a

f) mlijipiga -li-ji-pig-a

Mofimu

1. mofimu nafsi --------- (a)-3-umoja

--------- (u)-2-umoja

---------- (m)-2-wingi

---------- (tu)-1-wingi

2. mofimu njeo ------------- (ta)-ijayo

------------- (li)-iliyopita

-------------- (na)-iliyopo

3. yambwa ---------------- (ku)-wewe

--------- (m)-yeye

---------- (ni)-mimi

----------- (ji)-binafsi

Kanuni ya pili; Hapa kinachozingatiwa ni maumbo yenye maana moja lakini yasiyo na umbo sawa la kimofolojia.

Mfano;

a) mtumwab) mvulanac) mjakazid) mwenzie) mwanadamu

watumwawavulanawajakaziwenziwanadamu

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 12

Page 13: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

mofimumofimu za idadi

//umoja//---------m/-k-------- mw/-i

//wingi//--------- wa/-k---------- w/-I

Kanuni ya tatu; Kanuni hii inadai kuwa alomofu moja au zaidi zimo katika mtawanyo mkamilishano ambapo moja ikitokea basi ya pili haitokei. Yambwa na yambiwa haziwezi kutokea katika mazingira yale yale.

Mfano

Baba alinimpigia mimi simu

Sisi tuliwamuona nyinyi

Yeye alimwakuta wao

(m) na (mu)

(wa) na (w)Zimo katika mtawanyo mkamilishano au mgawanyo wa kiutowano

Kanuni ya nne; Umbo moja na zaidi huweza kuwa katika mpishano huru kama maumbo hayo yana maana moja na yametokea katika mazingira yaleyale.Mfanongombe badala ya ng’ombe khabari badala ya habari lafiki badala ya Rafiki ntoto badala ya mtoto

Kanuni ya tano; inadai kuwa maumbo yenye maana tofauti ni mofimu na maumbo tofauti yenye maana sawa ni alomofu.

MUHADHARA WA 3 : ALOMOFUMaeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 13

Page 14: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Fasili ya alomofu

Alomofu ni maumbo mbalimbali yanayowakilisha dhana moja ya kisarufi. Alomofu ni maumbo mbalimbali ya mofimu moja.

Alomofu hufafanuliwa kama maumbo zaidi ya moja (mbalimbali) ya mofimu moja.

Mazingira ya utokeaji wa alomofu

Alomofu hazitokei kibahati nasibu tu. Mara nyingi utokeaji wa alomofu fulani unategemea kupatikana kwa mazingira mahususi. Mazingira hayo yanaweza kuelezeka kifonolojia, kileksika na kisarufi.

Mazingira ya kifonolojia

Kuna baadhi ya alomofu utokeaji wake hutegemea kuwepo au kutokuwepo kwa sauti/fonimu fulani. Kwa mfano; mofimu iwakilishayo umoja katika ngeli ya KI-VI hujitokeza kwa umbo la ki- ikifuatiwa na konsonanti lakini mofimu hiyo hiyo huwakilishwa na umbo la ch- ikifuatwa na irabu.

Mfano:

Ki +tabu = kitabu, ki+buyu = kibuyu, ki+sima = kisima

Ki+umba = chumba, ki+ama =chama, ki+etu = chetu, ki+ekundu = chekundu

Mazingira ya kileksika (kikamusi/kimaana)

Alomofu pia hujitokeza kutokana na mazingira ya kileksika. Tofauti na mazingira ya kifonolojia ambayo aghalabu hutabirika mazingira ya kileksika hayatabiriki na hutegemea zaidi neno husika.

Mfano:

Mtume ---------mitume

Waziri---------mawaziri

Kiongozi ----viongozi

Malaika --------malaika

Mganga --------waganga

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 14

Page 15: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Kwa kuzingatia mazingira ya kileksika ya mifano hapo juu tunaweza kusema kuwa mofu ya umoja //m// inaweza kujitokeza kama //m//, /θ/ na /ki/ wakati mofu ya wingi //wa// inajitokeza kama //mi//, //ma//, //vi// na // θ //.

Mazingira ya kisarufi

Wakati mwengine alomofu hutokea kwa sababu za kisarufi. Mfano mzuri unapatikana katika mofimu za njeo. Mabadiliko ya wakati unaohusishwa na tendo husababisha kupatikana kwa maumbo mbalimbali yawakilishayo njeo. Angalia mifano ifuatayo:

A B

Anaandika - haandiki

Aliandika - hakuandika

Ataandika - hataandika

Ameandika - hajaandika

Kutokana na mifano hii maumbo yanayowakilisha njeo katika kifungu A ni //na//, /li//, //ta// na //me// yanayoashiria wakati uliopo, wakati uliopita (muda mrefu) na wakati uliopita (muda mfupi) hali yakinishi na katika kifungu B ni //i//, //ku//, //ta// na //ja// yanayowakilisha nyakati hizohizo katika ukanushi.

Aina za alomofu

Alomofu za njeo : ----- -na-, -li-, -me-, -ta-, -ku-, -ja- (anasoma, alisoma, amesoma, atasoma, hakusoma, hajasoma).

Alomofu za nafsi : ni, tu, u, m, a, wa (ninasoma, tunasoma, unasoma, mnasoma, anasoma, wanasoma).

Alomofu za wingi : mi-, vi, wa-, ma-, n.k. (miti, vijiko, watoto, majembe)

Alomofu za umoja : ki-, m-, u-, li-, n.k. (kibanda, mkeka, ukuta, limeoza)

Alomofu za usababishi/utendeshi : ish, esh, z, fy, vy, sh (katisha, somesha, liza, ogofya, levya, safisha)

Alomofu za ukanushi : si, ha, (hu-) (siandiki, haandiki, h(a)uandiki)

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 15

Page 16: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Alomofu za urejeshi : ye, cho, po, vyo, ko, n.k. (aliyeondoka, kilichozama, nilipokosa, ulivyokurupuka, walikokimbilia)

Alomofu za masharti : ki, nge, ngeli, ngali, ngeli, kama, endapo (akija, angekuja, angalikuja, kama atakuja, endapo atakuja)

MUHADHARA WA 4 : KIAMBISHI

Fasili ya kiambishi

Kiambishi ni mofu iongezwayo kwenye mzizi wa neno na kuwakilisha maana ya kisarufi.

Aina za viambishi

Aghalabu viambishi huainishwa kwa kutegemea mahali ambapo viambishi hivyo huwekwa katika neno. Hivyo kwa ujumla tunapata aina kuu tatu za viambishi ambazo ni; viambishi awali, viambishi ndani/kati na viambishi tamati.

Viambishi awaliNi viambishi ambavyo huwekwa kabla ya mzizi wa neno. Mfano; neno tunakuja……tu-na-ku ni viambishi awali vilivyowekwa kabla ya mzizi wa neno –j- . mifano mingine ni hatulimi, wanasoma, n.k.

Viambishi ndani/katiHivi ni viambishi ambavyo huwekwa katikati ya mzizi wa neno. Hakuna mfano wa neno la Kiswahili lenye kiambishi ndani kwa sababu lugha ya Kiswahili haina muundo huo. Mifano tunaweza kuipata katika lugha nyingine kama vile lugha ya Kibari kutoka Sudani ya kusini. Katika lugha hii mofimu ya idadi huoneshwa kwa kutumia viambishi ndani. Mfano;Popon ------------------------ shimo (umoja)Popojin ---------------------- mashimo (wingi) –ji ni kiambishi ndani cha wingi.Bun ----------------------------- kitabu (umoja)Bukan ------------------------ vitabu (wingi) –ka- ni kiambishi ndani cha wingi.

Viambishi tamatiNi aina ya viambishi ambavyo huwekwa baada ya mzizi wa neno. Mfano

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 16

Page 17: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Chumbani ------------------ chumba (mzizi) + -ni (kiambishi tamati)Somo ------------------------som (mzizi) + -o (kiambishi tamati)Pikisha --------------------- pik (mzizi) + ish + -a (viambishi tamati)Kutokana na maelezo na mifano ya hapo juu tunaona kuwa lugha ya Kiswahili ina aina mbili tu za viambishi; viambishi awali na viambishi tamati. Jambo la kuzingatia ni kwamba viambishi vya aina zote huweza kujitokeza katika neno moja la Kiswahili. Kwa mfano hatujawapigisheni- maumbo yaliyokolezwa wino kabla ya mzizi –pig- ni viambishi awali na yale yaliyo baada ya mzizi ni viambishi tamati. Vilevile tunaona kuwa viambishi ni maumbo tegemezi yanayofanya kazi ya kuleta maana yanapounganishwa na mzizi tu. Na pia tumegusia kuwa viambishi huwakilisha maana za kisarufi tu.

Mpangilio wa viambishiKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana fulani ya kisarufi. Hivyo basi ni lazima kuwe na utaratibu maalumu wa kuvipanga viambishi katika mzizi wa neno ili neno litoe maana na taarifa iliyokusudiwa. Katika sehemu hii tutaonesha mpangilio wa viambishi katika maneno ya lugha ya Kiswahili. Tutaangalia zaidi kitenzi na nomino.

Mpangilio wa viambishi awali katika kitenzi Kwa kawaida kitenzi huanza na kiambishi nafsi, mfano a-cheka Kiambishi nafsi hufuatiwa na kiambishi cha wakati mfano alicheka Kiambishi cha wakati hufuatiwa na kiambishi rejeshi mfano

aliyecheka Kiambishi rejeshi hufuatiwa na kiambishi yambwa/yambiwa mfano

aliyemcheka.

Mpangilio wa viambishi tamati katika kitenziKama ilivyoelezwa awali kuwa viambishi tamati ni vile vinavyokaa baada ya mzizi wa neno. Aghalabu viambishi tamati huwa ni vya mnyambuliko na hutokea kimoja tu katika neno. Mfano; Wanapigwa – utendwa.Wanapigana – kutendana

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 17

Page 18: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Wanapigika – kutendekaWanapigisha – kutendeshaWanapigiana – kutendeana, n.k.Hata hivyo, iwapo kitenzi kitakuwa na viambishi tamati zaidi basi mzizi huo huwa ni mzizi wa mnyambuliko na aghalabu unakuwa umeundwa kwa kiini cha neno na mofimu ya kutendana (mf. pigan). Ikiwa mzizi una kiambishi cha kutendana //an//, baadaye huja kiambishi cha kutendesha //sh,ish,esh// n.k. na kisha hufuata kiambishi cha utendeka //ik, ek// au kiambishi cha utendwa //w// (hutegemea na taarifa inayotolewa) na kumalizia na kiambishi –a kinachokamilisha maana. Chunguza utaratibu huu katika maneno yafuatayo:

TuliowapiganishaTumepiganishikaTumepiganishwa

Mifano iliyotolewa hapo juu ni ya vitenzi yakinifu tu. Hata hivyo, ni vyema ieleweke kuwa utaratibu huu hufanya kazi hata katika hali ya ukanushi isipokuwa kiambishi cha ukanushi si, ha (hu) hutokea mwanzoni kabisa kabla ya kile cha nafsi. Mfano.Utapika ---------------- h(a)utapika (wakati ujao)Tumepigana ---------- hatujapigana (wakati uliopita – muda mfupi)Walitufurahisha --------- hawakutufurahisha (wakati uliopita)Hata hivy, hali huwa tofauti kidogo kwa upande wa wakati uliopo kwani kiambishi cha wakati na hudondoshwa na umbo la kitenzi humalisika kwa irabu i badala ya a kama ilivyozoeleka. Kuna wataalamu wanaodai kuwa hii irabu ya mwisho i ndicho kiambishi cha wakati uliopo katika ukanushi.Mfano:

Tunasoma – hatusomi (*hatunasoma)Ninapika – sipiki (*sinapika)

Mpangilio wa viambishi katika nomino

Aghalabu nomino huweza kuandamana na viambishi vya aina tatu tu. Viambishi hivyo ni bya idadi (umoja na wingi), ukubwa na udogo. Mfano;

Mtoto (m ya umoja) kitoto (ki ya udogo) jitoto (ji ya ukubwa) kijitoto (ki ya umoja na udogo na ji ya udogo).

Watoto – vitoto- mitoto – mijitoto – vijitotoMaeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 18

Page 19: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Wakati mwingine hutokea nomino ikabeba viambishi vya aina mbili kwa pamoja. Katika hali hiyo kiambishi cha idadi hutangulia na ndipo kikaja kiambishi cha ukubwa/udogo kama ilivyo katika mifano hapo juu.

Viambishi nominishi: ni vile ambavyo vinapoambikwa katika neno lisilokuwa nomino hulifanya neno hilo kuwa nomino.

Mfano

Ji > mchoraji, mtangazaji, uimbaji, muuaji, upimaji, n.k. Zi> Upekuzi, uchaguzi, ufafanuzi i > Ushindi, uchunguzi, ubishi, msomi O > Somo, upendo, mkopo fu > udanganyifu, usahaulifu, uchangamfu, usumbufu

kama ilivyoelezwa katika mifano hapo juu, utokeaji wa viambishi hivi aghalabu huambatana na utokeaji wa viambishi awali vya nomino vinavyodokeza idadi, udogo au ukubwa wa nomino (m/wa, ki/vi, u, ma, n.k.)

viambishi elezi: ni vile ambavyo vinapoambikwa katika neno lisilokuwa kielezi hulifanya neno hilo kuwa kielezi.

Mfano

ni > sokoni, barabarani, darasani, n.k ki > kijeuri, kiume, kikatili vi > vizuri, vibaya

MUHADHARA WA 5 : MZIZI

Fasili ya mzizi

Mzizi ni neno au sehemu ya neno ambayo hubeba taarifa ya msingi na haibadilikibadiliki.

Sifa bainifu za mzizi

Mzizi hubeba taarifa ya kileksika Mzizi haubadilikibadiliki Mzizi ni mofu muhimu kuliko mofu zote katika neno Mzizi hauwezi kuachwa wakati wote neno linapotumika

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 19

Page 20: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Aina za mzizi

Mzizi huru: ni mzizi usiopokea kiambishi cha aina yoyote. Mfano; mama, sawa, chungwa, n.k.

Mzizi funge: ni mzizi unaoandamana na viambishi ili kukamilisha maana mfano; kisu, mti, n.k. –su na –ti ni mfano wa mizizi ya maneno ambayo maana zake hupatikana baada ya kufungamanishwa na viambishi.

Mzizi asilia: ni mzizi unaotokana na kiini cha neno. Mfano wa mzizi asilia ni andik- katika neno andika, kat- katika neno kata, n.k.

Mzizi wa mnyambuliko: ni mzizi unaotokana na mzizi asilia pamoja na viambishi. Kwa mfano andikish- ni mzizi wa mnyambuliko unaoweza kuzalisha maneno kama andikisha, andikishwa, andikishana, andikishia, n.k. na pigan- ni mzizi wa mnyambuliko unaoweza kuzalisha maneno kama vile pigana, oigania, piganiwa, piganisha, n.k

Miundo ya mzizi

Neno zima: mf. sungura, mbuzi, kopo, bibi Konsonanti pekee: mf. –p- katika nipe, -f- katika kifo Irabu pekee: mf. –u- katika usiniue, o- katika wameoana Silabi moja: mf. –ki katika kiti, to- katika toa, li-katika lia Silabi moja au zaidi pamoja na sehemu tu ya silabi nyingine : mf. som-

katika soma, kat-katika kata, andik-katika andika, tafut-katika tafuta. Silabi zaidi ya moja : mf. kimbi- katika kimbia, fafanu-katika ufafanuzi.

MUHADHARA WA 6 : NENO

Fasili ya neno

Neno ni kipashio cha kiisimu kinachoundwa na mofimu moja au zaidi na kutoa maana fulani katika lugha husika. Maana hiyo yaweza kuwa ya kisarufi au ya kileksika.

Aina za maneno

Maneno hugawanywa katika aina zake kwa vigezo viwili ambavyo ni: kigezo cha muundo na kigezo cha kazi.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 20

Page 21: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Aina za maneno kimuundo

Neno sahili : ni neno linaloundwa kwa mzizi huru mmoja (mf. mama, wewe, maji, hewa, n.k)

Neno ambatani : ni neno linaloundwa kwa mizizi miwili. Yawezekana ikawa ni mzizi funge na mzizi huru au mizizi huru miwili (mf. mwanaanga, mwanahewa, bwanashamba)

Neno changamano : ni neno linaloundwa kwa mzizi funge pamoja na viambishi mbalimbali (mf. mapigo, mwendeshaji, n.k.)

Aina za maneno kikazi/kiuamilifu

Kwa kutumia kigezo cha kazi/uamilifu tunapata aina zifuatazo za maneno:-

Nomino (N) Kiwakilishi (w) Kivumishi (V) Kitenzi (T) Kielezi (E) Kihusishi (H) Kiunganishi (U) Kihisishi/Kiingizi (I)

TAARIFA ZINAZOPATIKANA KATIKA NENO

Taarifa ya kifonolojiaNi kujua fonimu zilizotumika kuunda neno hilo. Mf. neno /paka/ limeundwa na fonimu /p/, /a/ na /k/

Taarifa ya kimofolojiaNi kujua mofimu zinazounda neno hilo. Mf. neno /paka/ limeundwa kwa mofimu moja huru na neno /mtu/ limeundwa na mofimu tegemezi mbili m-na -tu

Taarifa ya kisintaksiaNi kujua aina ya neno kulingana na uamilifu wake katika tungo. Mf;(a) Kitu chema hakidumu (b) chema hakidumu

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 21

Page 22: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Neno chema katika (a) ni kivumishi na neno chema katika (b) ni kiwakilishi. Tunajua aina ya neno kwa kuangalia kazi na nafasi yake katika tungo.

Taarifa ya kisemantikiNi kujua maana ya neno. Ili mkusanyiko wa silabi ukubalike kuwa ni neno lazima uwe na maana katika lugha husika; hivyo mkusanyiko usioleta maana si neno. Mf; paletihoju ni mkusanyiko wa silabi usioleta maana katika lugha ya Kiswahili na hivyo hili si neno la Kiswahili.

Neno na leksimuImeelezwa katika fasili ya neno kwamba neno lazima liwe na maana ya kisarufi au ya kileksika/kikamusi. Neno lenye maana kileksika huweza kusimama peke yake kama kidahizo katika kamusi. Hivyo basi tunaweza kusema leksimu ni kipashio cha kidhahania ambacho ni cha msingi katika msamiati wa lugha na hubeba dhana ya kwanza ya neno. Ni maneno yenye maana za kileksika ambayo huwa vidahizo katika kamusi. Mfano;Doa ji/ma – 1. Alama au tone ambalo lina rangi tofauti na mwili wa kitu 2. Aibu, dosari, ila, kasoro.Maneno yenye maana za kisarufi ambayo hayawezi kutumika kama kidahizo katika kamusi yanabaki kuwa maneno tu lakini si leksimu.NENO NA MOFIMUNeno ni mkusanyiko wa silabi zinazotamkwa au kuandikwa na kuleta maana fulani katika lugha. Mkusanyiko huo wa silabi unaweza kuwa ishara ya maana ya kileksa au maana kisarufi.Mofimu kwa upande mwingine ni kipashio cha kiisimu chenye maana ya kileksika au kisarufi. Maneno huweza kuwa na mofimu moja au zaidi lakini si lazima wakati wote iwe neno.LEKSIMU NA MOFIMULeksimu ni kipashio kidogo cha msamiati kinachoweza kusimama peke yake katika kamusi kama kidahizo. Mofimu inaweza kusimama peke yake hasa ikiwa mofimu huru.

MUHADHARA WA 7: NENO (Aina za Maneno – Nomino)Nomino: ni maneno ambayo hutaja majina ya watu, vitu, mahali, vyeo, dhana na hata tendo.

Aina za nominoNomino za pekee

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 22

Page 23: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Nomino za kawaidaNomino za dhahaniaNomino za jumla

Dhima ya nominoKiima cha sentensi: Juma analimaYambwa : Juma amenunua kitabuYambiwa : Juma amemnunulia Ali kitabuKijalizo : Juma ndiye kiongozi wetu

MUHADHARA WA 8 : NGELI ZA NOMINO (Mkabala wa Kimofolojia)

Fasili ya ngeli

Ni uwekaji wa nomino katika makundi mbalimbali kulingana na vigezo maalumu. Vigezo hivyo vyaweza kuwa vya kimofolojia, kisintaksia n.k. kutokana na vigezo hivyo ndipo tunapopata migawanyo tofauti ya ngeli; kama mgawanyo wa ngeli kimapokeo na mgawanyo wa ngeli kimamboleo/kisasa.

Mgawanyo wa ngeli za nomino kimapokeo

Huu ni uainishaji wa ngeli kwa kutumia kigezo cha mofolojia ya nomino. Tunapotumia kigezo hiki kugawa nomino za Kiswahili katika ngeli tunazingatia zaidi viambishi awali vya idadi – umoja na wingi ambavyo ni vya kawaida katika nomino hizo – si viambishi vyenye kuonesha dhana ya ukubwa na udogo. Kwa kigezo hiki tunapata makundi yafuatayo ya ngeli:-

a) Ngeli ya M(U) – WA (Mtu-watu, mtoto-watoto)b) Ngeli ya M-Mi (mti-miti, mkono-mikono)c) Ngeli ya JI-MA (jicho-macho, jiwe-mawe)d) Ngeli ya KI-VI (kinu-vinu, kiwete-viwete)e) Ngeli ya U-N (ulimi-ndimi, ufa-nyufa)f) Ngeli ya U-MA (uamuzi-maamuzi, upishi-mapishi)g) Ngeli ya U-Ɵ (upawa- Ɵpawa, ukucha- Ɵkucha)h) Ngeli ya Ɵ-MA (Ɵchungwa-machungwa, Ɵjani-majani)i) Ngeli ya Ɵ- Ɵ (Ɵnyumba- Ɵnyumba, Ɵnguo- Ɵnguo)

UBORA WA KIGEZO CHA KIMOFOLOJIA

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 23

Page 24: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

a) Uwezekano wa kuzigawa nomino nyingi za Kiswahili ni mkubwa kwa kuwa nyingi zimegawanyika katika maumbo hayo ya umoja na wingi.

b) Ni kigezo muhimu kwani kinajikita zaidi katika nomino na kivumishi chake peke yake hakigusi aina nyingine ya neno tofauti na kigezo cha kisintaksia ambacho hugusa hadi kitenzi.

c) Huwasaidia wanasarufi linganishi kuonesha uhusiano wa lugha za kikoa kimoja.

d) Kilisaidia kuondokana na uainishaji ngeli kwa kutegemea tofauti za kibayolojia.

e) Kinasaidia kutambua mofolojia ya nomino kama ni huru au changamano.

UDHAIFU WA KIGEZO CHA KIMOFOLOJIA

a) Kuna viambishi katika ngeli tofauti vinavyofanana. Mfano Kiambishi M- kinajitokeza katika ngeli ya 1 na 3 na MA- inajitokeza katika ngeli ya 8 na 13.

b) Kuna nomino nyingine ambazo hazijidhihirishi katika umoja na wingi. Mfano ngeli ya 8 na 9.

c) Nomino zenye hadhi tofauti kuwekwa kwenye ngeli moja mf. (kiwete,kinu), (sikio,tawi).

d) Kuna matumizi ya vigezo viwili kwa pamoja, kigezo cha maumbo ya idadi na kigezo cha sifa za nomino.

e) Idadi ya ngeli ni kubwa na hivyo humfanya msomaji kupata tabu ya kuzikariri.

f) Wanamapokeo wamegawanyika pasipo sababu za msingi, kuna wenye ngeli 18, 16 na 9.

MUHADHARA WA 9 : MGAWANYO WA NGELI ZA NOMINO KIMAMBOLEO

Huu ni uainishaji wa ngeli kwa kutumia kigezo cha sintaksia ya nomino. Uainishaji huu huzingatia uhusiano wa nomino na maneno mengine katika tungo kwa kuangalia viambishi vya upatanishi wa kisarufi vinavyojitokeza mwanzoni mwa maneno yanayoandamana na nomino katika tungo. Viambishi hivyo huathiriwa na umbo la nomino inayozungumzwa katika tungo husika. Kwa kutumia kigezo hiki tunapata makundi yafuatayo ya ngeli:-

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 24

Page 25: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

a) Ngeli ya YU-A/WA: mtoto yuasoma/mtoto anasoma-watoto wanasoma

b) Ngeli ya U-I: mkoba umechanika-mikoba imechanika

c) Ngali ya LI-YA: debe linauzwa-madebe yanauzwa

d) Ngeli ya KI-VI: kiatu kimetupwa-viatu vimetupwa

e) Ngeli ya I-ZI: ndizi imeiva-ndizi zimeiva

f) Ngeli ya U: ushawishi umemponza-ufisadi umekithiri

g) Ngeli ya U-YA: ugonjwa umetukatisha tamaa-magonjwa yametukatisha tamaa

h) Ngeli ya U-ZI: ungo umeharibika-nyungo zimeharibika

i) Ngeli ya YA: maji yanamwagika, mafuta yamekwisha

j) Ngeli ya I: chai imenywewa

k) Ngeli ya KU: kulima kunakondesha, kula kwake kutamdhuru

l) Ngeli ya PA-MU-KU: kiwanjani petu panafaa, nyumba munagiza, kule kunatisha

UBORA WA MTAZAMO WA KISASA

Kigezo cha kisintaksia kinachotumiwa katika mtazamo wa kisasa kugawa ngeli kwa kuzingatia upatanisho wa kisarufi kina ubora wake kama ifuatavyo:

Kimepunguza makundi mengi ya ngeli za nomino

Ni rahisi kuzikariri kwani ni chache.

Kila nomino huweza kuingia katika ngeli yake kwa kuzingatia upatanisho wa kisarufi.

Nomino hupangwa katika ngeli zake kulingana na sifa na hadhi yake.

Husaidia kubaini umoja na wingi wa nomino zisizo na maumbo dhahiri ya idadi.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 25

Page 26: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Kigezo hiki kimepunguza kujirudiarudia kwa ngeli.

Husaidia kubainisha uhusiano wa nomino na maneno mengine katika tungo.

Husaidia kuonesha urejeshi wa vitenzi na nomino zake.

UDHAIFU WA MTAZAMO WA KISASA

Bado kuna ngeli za nomino zinazojirudia mf. Ngeli ya 2,6 na 7 umoja zinatumia u.

Ngeli ya kwanza umoja ina viambishi viwili (Yu/A)

Bado kuna nomino zenye kuleta mgogoro katika ngeli mf. Makala, Jambazi, marashi.

Pamoja na umoja na wingi kutawala, kigezo cha sifa ya nomino hujitokeza ili kuepuka kuchanganya majina yenye sifa na hadhi tofauti mf. Kinyonga hukubali zaidi ngeli ya (KI-VI) lakini huwekwa katika ngeli ya kwanza kwa sifa ya kiumbe hai.

Kigezo hiki hakijaweza kuonesha mofolojia ya nomino.

MUHADHARA WA 10: VIWAKILISHI

Fasili ya viwakilishi

Viwakilishi ni maneno yanayosimama badala ya nomino au kikundi nomino.

Muundo wa viwakilishi

Kwa ujumla viwakilishi hujitokeza katika miundo miwili. Kiwakilishi huweza kuwa huru au kiambata. Kiwakilishi huru ni kile kinachosimama pekee kikiwa neno kamili kama vile mimi, yeye, nani, nini, n.k. kwa upande wa kiwakilishi kiambata ni kiwakilishi ambacho huambatanishwa mwanzoni mwa kitenzi.

Aina za viwakilishi

1. Viwaklishi vya sifa : kizuri chajiuza, kibaya chajitembeza

2. Viwakilishi vya idadi: wawil wameokolewa, mmoja hajulikani alipo.

3. Viwakilishi vioneshi: yule habebeki, huyu nampenda

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 26

Page 27: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

4. Viwakilishi viulizi: ipi unaitaka? Lipi limekuudhi?

5. Viwakilishi vimilikishi: wangu ni mweusi, wao amezidi mno

6. Viwakilishi nafsi: mimi sijali, nyinyi mnacheza

Nafasi ya kiwakilishi: kiwakilishi hutokea badala ya nomino/huchukua nafasi ya nomino pale ambapo nomino haipo.

MUHADHARA WA 11 : VIVUMISHI

Fasili ya kivumishi

Vivumishi ni maneno ambayo huandamana na nomino ili kuongeza sifa au taarifa muhimu kwa nomino (huifanya nomino ivume).

Muundo wa vivumishi

Kwa kutumia kigezo cha kimuundo kuna aina mbili za vivumishi ambazo ni:

Vivumishi vinavyoambishwa mf; dogo, refu, chungu, zuri, n.k

Vivumishi vinaweza kuambishwa kulingana na upatanishi wa kisarufi wa nomino inayovumishwa. Hivyo tunaweza kupata tungo kama ki+dogo, wa+refu, m+chungu, vi+zuri, n.k

Vivumishi visivyoambishwa-aghalabu vivumishi vya aina hii hutokana na maneno yenye asili ya lugha ya Kiarabu mf; Jamali,dhaifu,n.k

Aina za vivumishi

Vivumishi vya sifa: hivi ni aina ya vivumishi vinavyotoa sifa ya nomino. Mfano kitambaa kizuri, mti mrefu, mwanafunzi mvivu, mtandio mweupe. Jambo la kuzingatia hapa si lazima ile sifa iwe njema hata sifa mbaya pia ni kivumishi.

Vivumishi vya idadi: hivi ni vivumishi vinavyoonesha idadi ya vitu mbalimbali. Mfano watoto wawili, nyumba moja.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 27

Page 28: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Vivumishi vya idadi vinaweza kujitokeza katika aina tatu ndogondogo.

- Vivumihi vya aina hii hutoa taarifa kuhusu idadi ya nomino ambazo kiwango chake kimetajwa.

- Vivumishi vya idadi vinavyoweza kuvumisha nomino kwa kutaja idadi ya nomino hizo kiujumla jumla bila kudhihirisha idadi halisi.

- Vivumishi vya idadi ambavyo huonesha nafasi iliyochukuliwa na nomino fulani katika orodha.

Vivumishi vya kuonesha:vivumishi vya aina hii huonesha mahali au upande kitu kilipo. Vivumishi vya aina hii hujengwa na mzizi {h} kwa vitu vilivyopo karibu na mzizi {le} kwa vitu vilivyo mbali. mfano kijana huyu, kuku wale

Vivumishi vya pekee: vivumishi hivi huitwa vya pekee kwa sababu kila kimojwapo huwa na maana maalumu. Pia kila kimojawapo huchukua upatanisho wake wa kisarufi kulingana na ngeli ya nomino ambayo kinaivumisha. Mizizi ya vivumishi hivi ni ote, o-ote, enye, enyewe, ingine, ingineo. Mfano chakula chochote, wakati wowote

Vivumishi viulizi: hivi ni vivumishi ambavyo hufafanua nomino kwa kuuliza habari zake. Mfano nguo ipi? Msichana yupi?watu wangapi?

Vivumishi vya jina kwa jina: ni vivumishi ambavyo jina huvumisha jina lililotangulia katika mfuatano. mfano mwalimu Majaliwa, Mzee kipofu

Vivumishi vimilikishi: ni vivumishi vinavyoonesha kuwa kitu fulani kina milikiwa na mtu au kitu kingine mfano: mali yangu, paka wako, nchi yetu

MODULI 4: VITENZI, VIELIZI NA VIUNGANISHI

VITENZI (T)

Vitenzi ni maneno yanayosimamia kitendo. Kila kitenzi huwa na shina la kitenzi (sehemu ndogo zaidi ya kitenzi ambayo ndiyo huwakilisha tendo hilo). Shina la kitenzi huambatanishwa na viambishi ili kutoa maana iliyokusudiwa

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 28

Page 29: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

kama vile mtendaji, mtendewa, wakati kitendo kinafanyika na pia kauli ya kitenzi hicho.

Aina za Vitenzi

Vitenzi Halisi

Vitenzi Visaidizi + Vitenzi Vikuu

Vitenzi Vishirikishi

Vitenzi Sambamba

Vitenzi Halisi

Hivi ni vitenzi vinavyorejelea kitendo moja kwa moja. Vitenzi halisi vinapoambatanishwa na vitenzi vidogo katika sentensi, huitwa vitenzi vikuu.

k.m: soma, kula, sikiza

Waziri Mwasimba aliwasili jana kutoka ng'ambo.

Kawia atapikia wageni.

Funga mlango wa dirisha.

Vitenzi Visaidizi

Vitenzi visaidizi hutangulia vitenzi halisi (vitenzi vikuu) katika sentensi ili kuleta maana inayokusudiwa kulingana na wakati au hali.

k.m: -kuwa, -ngali,

Jua lilikuwa limewaka sana.

Bi Safina angali analala

Vitenzi Vishirikishi

Vitenzi vishirikishi hutumika kuelezea hali iliyopo au mazingira. Kuna aina mbili za vitenzi vishirikishi:

a) Vitenzi Vishirikishi Vipungufu - havichukua viambishi vyovyote.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 29

Page 30: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

k.m: ni, si, yu

Kaka yako ni mjanja sana.

Huyo si mtoto wangu!

Paka wake yu hapa.

b) Vitenzi Vishirikishi Vikamilifu - huchukua viambishi vya nafsi au ngeli. Vitenzi hivi vinaweza kusimama peke yake au vinaweza kufuatiliwa na vitenzi vikuu.

k.m: ndiye, ndio, ndipo

Sanita ndiye mkurugenzi wa kampuni

Huku ndiko kulikoibiwa

Muundo wa Vitenzi

Kwa kuzingatia muundo wa vitenzi, tunaweza kuweka vitenzi katika aina zifuatazo:

1. Vitenzi vya Silabi Moja

2. Vitenzi vya Kigeni

3. Vitenzi vya Kibantu

Vitenzi vya Silabi Moja

Hivi ni vitenzi vyenye silabi moja pekee. Ili kuleta maana kamili, vitenzi hivi huambatanishwa na kiungo KU- katika kauli ya kutenda. Kama vitenzi vingine, vitenzi vya silabi moja vinaweza kunyambuliwa.

k.m: soma, kula, sikiza

1. -cha - kucha - jua linapochomoza asubuhi k.m kumekucha

2. -fa - kufa - kuacha kupumua, kupoteza uhai k.m amekufa

3. -ja- kuja - fika mahali hapa k.m nimekuja

4. -la- kula - kutia chakula mdomoni k.m anakulaMaeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 30

Page 31: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

5. -nya- kunya - kutoa mabaki ya chakula toka tumboni k.m mtoto amekunya

6. -nywa- kunywa - kutia kinywaji kama vile maji au maziwa mdomoni k.m ninakunywa uji

7. -pa- kupa - kumkabithi/kumpatia mtu kitu k.m amenipa pesa

8. -pwa- kupwa - kujaa hadi pomoni - k.m kisima kimekupwa maji

9. -twa- kutwa - jua linapozama magharibi na usiku kuingia k.m kumekutwa

10.-wa- kuwa - kutokea katika hali au mahali fulani k.m alikuwa

Vitenzi vya Kigeni

Hivi ni vitenzi vyenye asili kutoka kwa lugha nyingine badala ya Kibantu. Baadhi ya lugha hizo ni Kiarabu, Kizungu, Kireno, Kihispania n.k. Vitenzi hivi havifuatilii muundo wa kawaida wa vitenzi vya Kiswahili ambavyo huishia kwa sauti -a. Badala yake, vitenzi hivi huishia kwa sauti nyingine kama vile -e, i, -o, na u

k.m: haribu, tubu, shukuru, salimu, thamini, amini, samehe, baleghe

Vitenzi vya Kibantu

Hivi ni vitenzi vyenye asili ya Kibantu na ambavyo huishia kwa sauti -a. Kitengo hiki hujumuisha asilimia kubwa zaidi ya vitenzi vya Kiswahili

k.m: simama, shika, tembea, beba, soma, lia

VIELEZI (E)

Vielezi ni maneno yanayotoa habari zaidi kuhusu kitendo kilivyofanyika. Pia vielezi hutoa habari zaidi kuhusu hali, vivumishi au vielezi vingine.

Aina za Vielezi

Vielezi vya Mahali

Vielezi vya mahali hutoa habari kuhusu mahali ambapo kitendo kilifanyika. Aghalabu vielezi hivi huundwa kwa kutumia jina la mahali au kwa kuongeza kiungo -NI mwishoni mwa neno linaloashiria mahali.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 31

Page 32: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

k.m: nyumbani, kazini, shuleni

Mtoto huyo hajatulia nyumbani tangu alipotoka Mombasa.

Msipitie sokoni mkienda kanisani.

Vielezi vya Wakati

Huelezea zaidi kuhusu wakati kitendo kipofanyika

k.m: jioni, jana, asubuhi, saa saba, mwaka juzi

Mzee Kasorogani amesema kwamba ataoga mwaka ujao

Musa alilazimishwa kuchimba mtaro saa sita usiku

Kisaka na Musa watakutana kesho

Vielezi vya Idadi

Vielezi vya idadi hutulezea kitendo kilifanyika mara ngapi

a) Idadi Kamili

Vielezi vya Idadi Kamili hutaja idadi kamili ya mara ngapi kitendo kilifanyika.

k.m: mara mbili, siku mbili kwa juma, mara kumi

Gibi alimzaba kofi mara tatu na kisha akakimbia.

Daktari alimwagiza mama huyo achukue dawa mara tatu kwa siku na arudi hospitalini siku mbili kwa mwezi

b) Idadi Isiyodhihirika

Vielezi vya Idadi Isiyodhirika huelezea kiasi ambacho kitendo kilifanyika bila kutaja kiasi kamili

k.m: chache, nyingi, kadhaa, kidogo, wastani

Mwizi wa kuku alipigwa mara kadhaa kabla ya kuokolewa na polisi.

Yeye hunipigia simu mara kwa mara

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 32

Page 33: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

VIelezi Vya Namna

Huelezea jinsi au namna kitendo kinavyofanyika. Kitendo kinaweza kufanyika kwa namna mbalimbali. Hivyo basi kuna aina mbalimbali za vielezi vya namna:

a) Vielezi vya Namna Halisi

Hutufahamisha jinsi kitendo kinavyofanyika kwa kutumia maneno halisi (bila kuambatanishwa na maneno mengine au viambishi vingine).

k.m: vizuri, ovyo, haraka

Kioo cha bibi harusi kilianguka na kuharibika vibaya

Mama alipika chakula upesi

Amepigwa kalamu kwa kufanya kazi kiholela

b) Vielezi vya Namna Hali

Hutufahamisha hali ambayo kitendo kilifanyika. Vielezi hivi hujihusisha na tabia ya kitu/mtendaji wa kitendo

k.m: kwa furaha, kwa makini,

Bibi harusi aliingia kanisani kwa madaha

Mtoto alilia kwa maumivu mengi

c) Vielezi vya Namna Kitumizi/Ala

Hutoa habari kuhusu kifaa, ala au mbinu iliyotumiwa kufanya kitendo fulani

k.m: kwa kisu, kwa jembe, kwa meno, kwa moto, kwa maji

Mkulima aliangusha mti mkubwa kwa shoka

Mzee huyo alimpiga mke wake kwa bakora kabla ya kuchoma nguo zake kwa makaa

d) Vielezi Vikariri

Husisitiza kitendo kinavyofanyika kwa kutaja kielezi kinachorejelewa mara mbili mfululizo.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 33

Page 34: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

k.m: haraka haraka, ovyo ovyo, juu juu

Polisi walipoingia, wezi walitawanyika haraka haraka.

Wanafunzi wengi hufanya kazi yao ovyo ovyo

e) Vielezi vya Ki-Mfanano

Vielezi mfanano hutumia KI-mfanano kuelezea kitendo kinavyofanyika kwa kulinganisha.

k.m: kitoto, kiungwana,

Babake huongea kiungwana.

Harida hutembea kijeshi

f) Vielezi Viigizi

Vielezi hivi huigiza sauti au mlio wa kitu, kitendo kitendo kilipofanyika kwa kutumia tanakali za sauti

k.m: tuli, chubwi, tifu, chururu

Mwanafunzi alitulia tuli mwalimu alipomzaba kofi pa!

Kaswimu aliangusha simu changaraweni tifu na kujitumbukiza majini chubwi

g) Vielezi vya Vielezi

Vielezi hivi hutumika kuelezea kielezi kingine. Hivyo basi, hutanguliwa na kielezi badala ya kitendo

k.m: sana, kabisa, hasa, mno

Mamake Kajino alitembea polepole sana.

Chungu kilivunjika vibaya kabisa

h) Vielezi vya Vivumishi

Hutoa habari zaidi kuhusu kivumishi

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 34

Page 35: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

k.m: sana, kabisa, hasa, mno

Yeye ni mrefu sana

Mtoto wake ana tabia nzuri mno

VIUNGANISHI (U)

Viunganishi ni maneno yanayoutumika kuunganisha, kulinganisha au kuonesha uhusiano wa dhana mbili au zaidi.

Aina za Viunganishi

Zifuatazo ni aina mbalimbali za viunganishi kulingana na matumizi yake

Kuonesha Umilikaji

A-Unganifu Kiatu cha Mzee Sakarani kimepasuka.

KWA (umilikaji wa mahali)

Mbinguni kwa kuna makao mengi.

Kujumuisha

na Baba, mama na watoto huunda familia kamili.

pamoja na Mwizi aliiba runinga pamoja na redio

fauka ya, licha ya

Fauka ya mapigo yote, Kafa alikatakatwa kwa kisu.

zaidi ya, juu ya

Unataka nini tena zaidi ya mema yote niliyokutendea?

pia, vilevile Alimpiga mkewe na bintiye vilevile

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 35

Page 36: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

mbali na Mbali na hayo nitakujengea nyumba ya kifahari.

aidha Keti akitoka shuleni atapika. Aidha atampelekea nyanya sukuma wiki.

wala (kukanusha)

Kutofautisha

lakini, ila Ongea nayeilausimwambie mipango yetu.

bila Tasha aliondoka bila kusema lolote.

bali Sitawaacha kama mayatima bali nitawatumia msaidizi.

kinyume na, tofauti na

Jana kulinyesha kinyume na utabiri wa hali ya hewa.

ingawa, ingawaje

Nitamtembelea ingawa sijui nitamwambia nini.

japo, ijapokuwa Nakuomba upokee nilichokileta japo ni kidogo sana.

ilhali Fungo zimepotea ilhali zilikuwa zimewekwa vizuri.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 36

Page 37: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

minghairi ya Waliendelea kutenda dhambi minghairi ya kuhubiriwa kanisani.

dhidi ya Vita dhidi ya gonjwa hilo vingali vinaendelea.

Kuonesha Sababu

ili Hanna aliumizwa ili asikumbuke aliyoyaona.

kwa, kwa vile

Emili alinyamaza kwa vile kugombana na rafikize.

kwa maana, kwa kuwa

Aria alipigwa na butwaa kwa maana mpenzi wake aligeuka kuwa mwalimu wake.

kwani Melisa alijificha kwani hakutaka kuonekana na Spensa.

kwa minanjili ya

Chali alitembea mwendo huo wote kwa minanjili ya   kuongea na Katosha.

maadam Wanawake katika familia hiyo hawali maini maadam mama mkongwe alilaani maini katika familia hiyo.

madhali Madhali sote tuko hapa, tunaweza kuanzisha mkutano mapema

Kuonesha Matokeo

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 37

Page 38: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

basi, hivyo basi

Umekula ng'ombe mzima, hivyo basi huna budi kumalizia mkia.

kwa hivyo Alipatikana na makosa ya kumnajisi bintiye, kwa hivyo akahukumiwa miaka kumi gerezani.

ndiposa Mama Kelele alipenda kuongea sana, ndiposa wakamkata midomo.

Kulinganisha

kama, sawa na

Kunywa pombe ni kama kujichimbia kaburi mwenyewe.

kulingana na Mwalimu Makunza hafanyi kazi kulingana na maadili ya shuleni.

kuliko, zaidi ya

Talia ni mfupi kuliko Nuru

vile Mganga Daimoni hutibu vile alivyofunzwa na Mganga Kuzimu.

Kuonesha Kitu kimoja kama sehemu ya kingine

kati ya Vitatu kati ya vitabu hivi vimepigwa marufuku.

miongoni mwa

Miongoni mwa walioachiliwa, ni Ngiri na Mende.

baadhi ya Baadhi ya wasichana kutoka Vikwazoni

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 38

Page 39: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

hawaheshimu miili yao.

mojawapo Mojawapo ya   maembe uliyochuma yameoza.

Kuonesha Kitu kufanyika baada ya kingine

kisha Soma mfano huu kisha usome sentensi ifuatayo.

halafu Alichukua kisu halafu akatokomea gizani.

Kuonesha Kitu kufanyika badala ya kingine

badala ya Mapepo yalimchukua Shakawa badala ya bintiye

kwa niaba ya Mama Roga alitoa hotuba kwa niaba ya mumewe.

Kuonesha Uwezekano

labda, pengine Sina pesa leo, labda uje kesho.

ama, au Ama Anita au Katosha anaweza kuja.

huenda Huenda kesho ikifika, Mungu atende miujiza.

Kuonesha Masharti

bora, muradi Sitakuuliza bora tu usichelewe.

ikiwa, iwapo Ikiwa huna jambo muhimu la kusema, nyamaza.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 39

Page 40: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

VIHISISHI, VIHUSISHI NA NJIA ZA KUUNDA MANENO

Vihisishi: ni sauti, neno au kikundi cha maneno kinachotamkwa na mwanadamu kuashiria hisia tofauti kama vie furaha, huzuni, mshituko, n.k. mfano wa vihisishi ni kama Mungu wangu!, mama wee! Mtume simama!

Kwa kawaida vihisishi ni maneno ambayo huwa hayana uhusiano wa kisarufi na aina nyingine za maneno katika tungo. Hivyo vihisishi hujitegemea na kujitosheleza.

Kimuundo vihisishi haviambishwi na wala havina kanuni maalumu ya mfuatano.

Vilevile kwa vihisishi vyenye muundo wa kikundi hauwezi kubadilisha neno moja kwa lingine hata kama yana hadhi sawa.

Kwa mfano hatuwezi kusema

*miungu yangu! (badala ya Mungu wangu!)

*baba wee! (badala ya mama wee!)

Aina za vihisishi/viingizi

Viingizi vinaweza kugawanywa kwa kutumia vigezo vya kisemantiki.

Mkabala huu unatumika kugawa viingizi kulingana na maana zinazowakilishwa na viingizi vyenyewe.

Maana hizo ni hisia zinazobebwa na viingizi hivyo. Kutokana na hisia hizo tunaweza kuvigawanya katika makundi ya maana zinazohusiana kwa karibu. Kwa mtazamo huo, viingizi vinaweza kugawanywa katika makundi matatu makuu ambayo ni:

(a) Viingizi vinavyoonesha mhemko au hisia kali:

Viingizi hivi ni vile vinavyowakilisha hisia tofauti anazokuwa nazo mzungumzaji ambazo zinaweza kuwa nzuri au mbaya. Kundi hili la kwanza linaweza kugawanywa katika sehemu ndogo nne kutokana na hisia mbalimbali alizonazo mzungumzaji zinazowakilishwa na aina hii ya viingizi ni kama ifuatavyo:

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 40

Page 41: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

(i) Viingizi vya furaha – hivi ni vile vinavyoonesha hali ya furaha aliyonayo mzungumzaji, kwa mfano, oyaa!, oyee!, huree!, n.k.

(ii)Viingizi vya huzuni – hivi ni vile vinavyoonesha hali ya masikitiko au huzuni iliyompata mzungumzaji, kwa mfano, pole!, maskini! Jamani!, n.k.

(iii)Viingizi vya mshangao – hivi ni vile vinavyoonesha hali ya mshangao uliompata mzungumzaji, kama vile. Eti!, salale!, ajabu!, kumbe!, n.k.

(iv) Viingizi vya mshituko – hivi ni vile vinavyoonesha hali ya mshituko uliompata mzungumzaji, kwa mfano loo!, amaa!, aisee!, n.k

(b)Viingizi vya maamrisho au msisitizo wa jambo au tukio:

Viingizi vya namna hii huonesha amri anayotoa mzungumzaji, kama vile haraka!, hima!, njoo!, nenda!, n.k.

(c) Viingizi vya maadili : hivi ni vile vinavyoonesha hisia zinazohusiana na maadili mbalimbali, yawe mema au mabaya. Aina hii ya viingizi inaweza kugawanywa katika makundi yafuatayo:

(i) Viingizi vya mwitiko – hivi ni vile ambavyo vinaonesha hisia za mwitiko anaokuwa nao mzungumzaji akiwa ameitwa au anapokabiliana na jambo katika mazungumzo, kwa mfano abee!, bee!, rabeka!, naam!, n.k.

(ii)Viingizi vya ombi – hivi ni vile ambavyo vinaonesha hisia za ombi kwa mfano, aha!, enhe!, simile!, astaghafirullah!, hodi!, n.k.

(iii)Viingizi vya bezo – hivi ni vile ambavyo vinaonesha hisia za bezo na dharau ya mzungumzaji, kwa mfano aka!, zii!, sasa!, n.k.

(iv) Viingizi vya kutakia heri – hivi ni vile vinavyowasilisha hisia za mzungumzaji za kutakia heri na kupongezana, kama vile: inshaallah!, ahsante!, hongera!, n.k.

(v)Viingizi vya kukiri jambo – hivi ni vile vinavyowasilisha hisia za kukiri, kwa mfano; laity! Haya! Taib!, n.k.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 41

Page 42: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

(vi) Viingizi vya kiapo – hivi ni vile ambavyo vinaonesha hisia za kuapa ili kuonesha mzungumzaji wa jambo fulani atalitenda au kukana kutenda jambo, kwa mfano; wallah!

(vii) Viingizi vya salamu – hivi ni vile vinavyotumika kutoa salamu za mzungumzaji kwa mtu mwingine wanapokutana watu wawili au zaidi, kwa mfano; shikamoo! Marhaba! Hujambo!, n.k.

Kwa kawaida viingizi havina uhusiano wa kimuundo na maneno mengine katika sentensi.

Huweza kuondolewa katika sentensi bila ya kuathiri muundo wa sentensi husika. Hata hivyo, viingizi huipa sentensi dhamira/hali fulani.

VIHUSISHI

Ni maneno yanayojitokeza baada ya nomino na kufanya kazi ya kuhusisha dhana tofauti. Umbo kuu/muhimu la kihusishi ni a-unganifu. Imeitwa a-unganifu kutokana na namna maumbile yake ya utendaji kazi yalivyo – kwamba ni lazima iunganishwe na mofu zinazowakilisha aina ya ngeli inayohusika mfano;

- Mtoto wa mama – wa-inahusisha mtoto na mama (ngei ya A-WA)

- Kiti cha mbao – cha – inahusisha kiti na mbao (ngeli ya KI-VI)

- Jiko la umeme – la – inahusisha jiko na umeme (ngeli ya (LI-YA)

Vilevile, kuna umbo na na kwa ambayo pia hutumika kama vihusishi ingawa yapo pia katika kundi la viunganishi mfano;

- Ameondoka na mkoba wako

- Ameangukiwa na jiwe

- Amejikata kwa kisu

- Tutasafiri kwa ndege, n.k.

Katika kujifunza aina za maneno ni muhimu kuelewa kuwa umbo la neno halitoshi kutambulisha aina ya neno. Unaweza ukagundua kuwa neno moja linajitokeza katika makundi tofauti; kwa mfano neno vizuri linaweza kuwa kiwakilishi, kivumishi au kielezi pia, neno kulala linaweza kuwa nomino au kitenzi.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 42

Page 43: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Halikadhalika neno Juma linaweza kuwa nomino au kivumishi. Hivyo ambo la msingi ni kuangalia kazi na nafasi ambayo neno hilo huchukua katika tungo.

UUNDAJI WA MANENO (NJIA ZA UUNDAJI WA MANENO)

Uundaji wa maneno ni mchakato unaowezesha lugha kujiongezea msamiati ili kukidhi haja ya mawasiliano na kuendana na mabadiliko yanayotokea kila siku.

Maneno ya lugha ya Kiswahili hayaundwi kiholela bali hufuata taratibu na kanuni zinazokubalika kitaalamu.

Njia zitumikazo kuunda maneno ni kama zifuatazo:

Unyambuaji

Njia hii inatumia mzizi mmoja wa neno na kuzalisha maneno mapya kwa kupachika viambishi nyambuaji

Mfano

Soma

Somo

Kisomo

Msomi

Msomaji

Lima

Mkulima

Kilimo

Mlimaji

Uambatishaji/mwambatano

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 43

Page 44: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Hii ni njia ya kuunda maneno mapya kwa kuambatanisha maneno mawili.

Mfano

Mwana+chama - Mwanachama

Askari+kanzu - Askarikanzu

Bwana+shamba – Bwanashamba

Urudufishaji / Uradidi

Hii ni mbinu ya kurudiarudia neno au sehemu ya neno na kuunda neno jipya ambalo huwa na maana tofauti na maneno yanayorudiwarudiwa.

Mfano

(d) Pole : polepole

(e) Sawa : sawasawa

(f) Haraka : harakaharaka

Akronimu/ufupishaji

Ufupishaji ni njia mojawapo ya kuundia maneno mapya,ufupishaji huweza kufanyika kwa namna mbili ambazo ni.

Kufupisha kwa kuchukua herufi za mwanzo Mfano

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 44

Page 45: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

CWT (Chama cha Walimu Tanzania) VVU (Virusi Vya Ukimwi)

Kufupisha kwa kuchukua silabi za mwanzo za maneno yanayo fupishwa

Mfano

BAKITA (Baraza la Kiswahili la Taifa)

TUKI (Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili)

TATAKI (Taasisi ya Taaluma za Kiswahili)

Uhulutishaji

Ni njia ya kuunda maneno mapya kwa kuchukua vijisehemu vya neno pasipo kufuata kanuni yoyote.

Mfano

Mnyama mfu – nyamafu

chakula cha jioni – chajio

hati za kukataza – hataza

Mtu asiye kwao - msikwao

Utohoaji

Ni uchukuaji wa maneno toka lugha moja na kuyatumia kwenye lugha nyingine baada ya kuyarekebisha kimatamshi na kimaandishi ili yaendane na sarufi ya lugha inayotohoa.

Mfano

Neno Lugha asilia Kiswahili

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 45

Page 46: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Shirt Kiingereza Shati

Schule Kijerumani Shule

Bakura Kiarabu Bakora

Benjera Kireno Bendera

Matching Kiingereza machinga

guys

Kuchukua

Hii ni mbinu ya kuongenza maneno kwa kuyachukua toka lugha yake na kuyatumia kama yalivyo. Uchukuaji hufanyika kwa lugha zinazoendana kisarufi kama Kiswahili na lugha za kibantu.

Mfano

Kitivo — kisambaa /kipare

Ikulu - kinyamwezi

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 46

Page 47: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Kigoda - kizaramo

Kubadili mpangilio wa fonimu

Mfano

Lima – mila – imla - mali

Kufananisha umbo /sauti /tabia

Mfano

Kufananisha umbo

- kifaru-(mnyama faru)

- mkono wa tembo-(mkonga wa tembo)

- kidole tumbo-(umbo la kidole)

Kufananisha Tabia

Ubeberu-(beberu la mbuzi)

Ukupe-(mdudu kupe)

Kufananisha Sauti

Pikipiki (mlio wa pikipiki)

Mtutu (mlio wa bunduki)

Nyau (mlio wa paka)

Kuku - kokoriko (mlio wa kuku)

Njia ya udondoshaji

Mfano

mkwe wake - mkwewe Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 47

Page 48: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

mwana wake - mwanawe

ndugu yake – nduguye

Kuzingatia matumizi ya kitu

Mfano

Banio - (kubana)

Chanio - (kuchana)

Fyekeo - (kufyeka)

Kutarjumi/kutafsiri

Mfano;

Fluid – (ugiligili)

Acquired immunal deficiency syndrome (Upungufu wa kinga mwilini)

Human immunal virus – (virusi vya ukimwi)

Anti-rentro-virus - (dawa za kufubaza makali ya ukimwi)

DHANA YA MOFOFONOLOJIA NA MOFOSINTAKSIA

Maana ya Mofofonolojia

Ni taaluma inayoshughulikia uchanganuzi na uainishaji wa vipengele vya kifonolojia vinavyoathiri maumbo ya mofimu katika mfuatano wake.

Mofofonolojia huzalisha kanuni ambazo zinaelezea mazingira ya utokeaji wa mofu na alomofu zake.

Kanuni hizi huelezea maathiriano ya kifonolojia yanayoathiri mofolojia ya maneno na jinsi badiliko la kimofofonolojia la neno linavyoelezeka kikanuni.

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 48

Page 49: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Kanuni hizi husaidia kujua jinsi maneno yanavyobadilika toka muundo ndani wa neno hadi muundo nje wa neno.

Kanuni za kimofofonolojia hutawaliwa na sifa zifuatazo

1. Kanuni za kifonolojia hazina vighairi mfano; hakuna vighairi katika kanuni ya kifonolojia isemayo mkazo katika Kiswahili huwekwa silabi ya pili kutoka mwishoni mwa neno.

2. Kanuni za kimofofonolojia huwa na vighairi vingi; Kanuni hii huhusu lugha mahususi na hutumika katika baadhi ya mofimu tu kwa mfano katika mofu ya utendea.

mfano

piga> pigia

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 49

Page 50: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

panga> pangia

funga> fungia

tenga> tengea

choma> chomea

//utendea//----->i/-mz+[a,i,u]

------->e/-mz+[e,o]

AINA ZA KANUNI ZA KIMOFOFONOLOJIA

1.Kanuni ya usilimisho

Kanuni hii inahusu maathiriano ya mofimu zinazofuatana. Maathiriano hayo huzifanya mofimu zifanane zaidi kuliko zikiwa pekee.

Mfano(1)

a) n+goma----->{ngoma}

b) n+dizi------>{ndizi}

c) n+buzi----->{mbuzi}Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 50

Page 51: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

d) n+bingu----->{mbingu}

n------>m/-k

Huu ni usilimisho wa nazali inayofuatwa na konsonanti

a) n+refu----->{ndefu}

b) n+limi---->{ndimi}

r------>d/n-

l------->d/n-

Huo ni usilimisho wa konsonanti inayotanguliwa na nazali(N)

2.Ukaakaishaji

Haya ni maathiriano ambayo sauti isiyo ya kaakaa gumu hulazimishwa kuwa sauti ya kaakaa gumu.

Mfano

a) ki+ama------->chama

b) ki+ombo------->chombo

c) ki+uma-------->chuma

d) ki+eo------>cheo

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 51

Page 52: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

3. Udondoshaji

Mofimu hudondoshwa kutokana na mfuatano wa mofimu unaoleta maathiriano Mfano

a) wanasoma –hawasomi

b) anasoma-hasomi

c) nilikunywa-sikunywa //njeo// -------> θ/-ukanushi

4. Tangamano la irabu

Ni utaratibu wa irabu moja kukubali kuandamana na irabu nyingine katika mazingira maalumu. Kwa kawaida irabu iliyo katika mzizi huathiri utokeaji wa irabu ya mnyambuliko. Hivyo ikiwa irabu ya mzizi ni a,i au u irabu ya mnyambuliko huwa i na ikiwa irabu ya mzizi ni e au o basi irabu ya mnyambuliko huwa e.

Mfano

Panga ----- pangia

Funga …. Fungia

Piga ……pigia

Choma …..chomea

Sema …… semea

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 52

Page 53: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

5. Mvutano wa irabu

Ni hali inayojitokeza wakati irabu ya juu na irabu ya chini zinapofuatana katika neno. Irabu hizo huvutana na kusababisha kutokea kwa irabu isiyo ya juu wala chini. Mfano,

ma+ino = meno

wa+ingi = wengi

ma+ingine = mengine

6. Uyeyushaji

Ni kitendo cha kubadili irabu kuwa nusu –irabu au kiyeyusho. Hali hii hutokea wakati irabu mbili zinapokutana mfano; irabu – u hubadilika na kuwa kiyeyusho /w/ inapokaribiana na a au i (mu+alimu=mwalimu, mu+imbaji = mwimbaji) na irabu -i- hubadilika na kuwa kiyeyusho /y/ inapokaribiana na irabu a, o au u (vi+ama= vyama, vi+ombo = vyombo, vi+uma = vyuma)

7. Vighairi

Ni mofimu au maneno yanayokiuka kanuni za kawaida za lugha husika. Mfano;

Kiatu………… viatu

Kisu……………visu

Choo ………….vyoo

Chama ………..vyama

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 53

Page 54: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

Nomino choo, vyoo, chama, vyama ni vighairi kwa sababu yanaingia ngeli ya KI-VI lakini hayabebi viambishi husika mwanzoni.

D11/9/2018HANA YA MOFOSINTAKSIA

Ni taaluma inayoshughulikia uchanganuzi na uainishaji wa vipengele vya kisintaksia vinavyoathiri maumbo ya mofimu katika mfuatano wake.

Vipengele vya kisintaksia vinavyoathiri mofolojia ni:

(a) Umoja na wingi: maneno mengi ya Kiswahili huwa na maumbo tofauti yanapokuwa katika hali ya umoja na yanapokuwa katika hali ya wingi.

Mfano

Umoja Wingi

Kidole vidole

Ungo nyungo

Jicho macho

Kwa kuangalia mifano ya hapo juu tunaona kuwa wingi wa kitu kinachotajwa ni kilekile, mabadiliko ya maumbo hutokea kuingana na idadi ya kitajwa. Maneno mengi tu ya Kiswahili huwa na tabia hii lakini sio yote. Hii ina maana kwamba baadhi ya maneno hubaki kama yalivyo (hayabadiliki) ikiwa yapo katika umoja au katika wingi. Mfano wa maneno hayo ni sabuni, njia, nguo, nyumba, zawadi, n.k.

(b)Njeo: katika Kiswahili kuna viambishi mbalimbali vinavyotumiwa kuwakilisha njeo. Hivyo basi, kadiri mzungumzaji anavyofikiria dhana

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 54

Page 55: Mofolojia ya Kiswahili · Web viewKatika lugha ya Kiswahili viambishi ni vingi. Na kama ilivyogusiwa hapo juu kuwa vinaweza kujitokeza kwa pamoja katika neno moja ili kutoa maana

Mofolojia ya Kiswahili 2018

ya wakati fulani katika mazungumzo yake ndipo umbo la neno linapobadilika kulingana na wakati huo. Mfano; analima,atalima,amelima,alilima (na – wakati uliopo, ta – wakati ujao, me – wakati uliopita timilifu, li – wakati uliopita)

(c) Ukanushi : dhana ingine ya kisintaksia inayosababisha umbo la neno kubadilika ni ukanushi. Angalia mifano ifuatayo:

A B

Uyakinishi Ukanushi

Anapika ……………. hapiki

Amepika …………… hajapika

Alipika …………….. hakupika

Atapika …………….. hatapika

Mifano hiyo inaonesha kwamba kutokana na kuwepo kwa mofimu ha ya ukanushi katika maneno ya jozi B maumbo yanayowakilisha wakati yamebadilika. Umbo na la wakati uliopo halionekani katika nafasi yake badala yake kuna umbo i mwishoni mwa kitenzi, wakati uliopita (muda mfupi) unawakilishwa na ja badala ya me na wakati uliopita unawakilishwa na ku badala ya li. Umbo linalowakilisha wakati ujao pekee ndilo lisiloathiriwa na mabadiliko haya.

(d)

Maeda, T.S 0717104507 www.mwalimuwakiswahili.co.tz Uk 55