annuur 1095

12
ISSN 0856 - 3861 Na. 1095 DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA , OKTOBA 18 - 24, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/= Sauti ya Waislamu www.annuurpapers.co.tz Ansaar Sunnah wasokotewa kitanzi Waingizwa katika ‘buku jeusi’ la UN Watabiriwa mauwaji ‘staili’ ya Rogo Sikiliza ‘UCHURO’ wa CNN, Standard “Leahy Amendment” ifanye kazi agizo la Bunge litimie SHEIKH Salim Adib. AL-MARHUUM Sheikh Aboud Rogo. Sheikh Salim hatunaye Innalillah wainna ilayhir Rajiuun. Sheikh Salim Ali Mohamed (48) amefariki Jumatatu tarehe 07/10/2013 majira ya saa tatu asubuhi. Habari Uk. 4 Innalillah Wainna illahr Rajiuun USTADHI Ramadhani Mohammed Mbulu (43), ambaye ni miongoni mwa Mtuhumiwa kesi ya Kanisa afariki akiwa na pingu mguuni Mahakama yawaachia wenzake huru Na Bakari Mwakangwale Waislamu 10 waliokuwa wakituhumiwa kuiba na kuharibu mali za Kanisa la Kilutheri Mbagala Jijini Dar Inaendelea Uk. 4 AL-MARHUUM Ustadh Ramadhani Mbulu. NAIBU Amiri wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar JUMIKI, Sheikh Azzan Khalid Hamdan, ambaye ni mmoja wa viongozi wa wa Kiislamu walioko kizuizini Zanzibar kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, hivi sasa yuko nchini India na amenza Sheikh Azzan aanza matibabu India Na Mwandishi Wetu SHEIKH Azzan Khalid Hamdan Inaendelea Uk. 2 KATIKA jumla ya mambo ambayo Dr. Mohamed Elbaradei anasema ni ya kuigwa na kupigiwa mfano, kutoka kwa Watu wa Marekani, ni sheria, sera, kanuni na msimamo wake wa kujali, kulinda na kuheshimu utu, uhuru na haki za binadamu. Anasema, kwa hilo anaona fahari kubwa kuwa amekuwa ni mwanafunzi aliyenolewa na kulelewa katika vyuo vikuu vya New York. Hilo linaelezwa pia na Inaendelea Uk. 2

Upload: annurtanzania

Post on 29-Nov-2015

864 views

Category:

Documents


12 download

TRANSCRIPT

ISSN 0856 - 3861 Na. 1095 DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA , OKTOBA 18 - 24, 2013 BEI TShs 500/=, Kshs 50/=

Sauti ya Waislamuwww.annuurpapers.co.tz

Ansaar Sunnah wasokotewa kitanzi

Waingizwa katika ‘buku jeusi’ la UNWatabiriwa mauwaji ‘staili’ ya RogoSikiliza ‘UCHURO’ wa CNN, Standard

“Leahy Amendment” ifanye kazi agizo la Bunge litimie

SHEIKH Salim Adib.

AL-MARHUUM Sheikh Aboud Rogo.

Sheikh Salim hatunaye

Innalillah wainna ilayhir Rajiuun.Sheikh Salim Ali Mohamed (48) amefariki Jumatatu tarehe 07/10/2013 majira ya saa tatu asubuhi. Habari Uk. 4

Innalillah Wainna illahr RajiuunU S TA D H I R a m a d h a n i Mohammed Mbulu (43), ambaye ni miongoni mwa

Mtuhumiwa kesi ya Kanisa afariki akiwa na pingu mguuni

Mahakama yawaachia wenzake huru Na Bakari Mwakangwale Waislamu 10 waliokuwa

wakituhumiwa kuiba na kuharibu mali za Kanisa la Kilutheri Mbagala Jijini Dar

Inaendelea Uk. 4AL-MARHUUM Ustadh

Ramadhani Mbulu.

NAIBU Amiri wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar JUMIKI, Sheikh Azzan Khalid Hamdan, ambaye ni mmoja wa viongozi wa wa Kiislamu walioko kizuizini Zanzibar kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, hivi sasa yuko nchini India na amenza

Sheikh Azzan aanzamatibabu India

Na Mwandishi Wetu

SHEIKH Azzan Khalid HamdanInaendelea Uk. 2

KATIKA jumla ya mambo ambayo Dr. Mohamed Elbaradei anasema ni ya kuigwa na kupigiwa m f a n o , k u t o k a k wa Watu wa Marekani, ni sheria, sera, kanuni na msimamo wake wa kujali, kulinda na kuheshimu

utu, uhuru na haki za binadamu. Anasema, kwa hilo anaona fahari kubwa kuwa amekuwa ni mwanafunzi aliyenolewa na kulelewa katika vyuo vikuu vya New York.

Hilo linaelezwa pia na Inaendelea Uk. 2

2 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 2013

AN-NUUR S.L.P. 55105, Simu: +022 2400786

Cel: 0784 370 208, 0713 110 148, 0755 260 087 , DSM. www.annuurpapers.co.tz E-mail: [email protected]

Ofisi zetu zipo: Manzese Tip TopUsangi House (Jengo dogo), barabara ya Morogoro, D'Salaam

Tahariri/Habari

“Leahy Amendment” ifanye kazi agizo la Bunge litimiewale waliopata bahati ya kuitembelea nchi hiyo kupitia program maalum zinazoandaliwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi hiyo.

Ni kutokana na historia na rekodi yake h iyo inayojidhihirisha kutokana na kauli za waasisi wa taifa hilo, katiba na sheria zake za kujali haki za binadamu, uhuru na utu wa kila mtu, Serikali ya Marekani pamoja na kuwa kinara katika vita ya kupambana na ugadi ambapo imekuwa ikitoa misaada ya namna mbalimbli kwa nchi za Afrika Mashariki, bado imekuwa ikiweka taratibu kuhakikisha kuwa haki za binadamu hazivunjwi katika kutekeleza vita hiyo.

Katika taarifa yake “Counter ing Terror ism in East Africa: The U.S. Response (November 3, 2010), baada ya kuelezwa kwa urefu jinsi Serikali ya Marekani inavyotoa misaada na kushirikiana na nchi za Afrika Mashariki kukabiliana na kitisho cha ugaidi, taarifa imegusia pia kile kilichoitwa “Human Rights Concerns.”

Kat ika taar i fa hiyo i l iyotokana na utafit i uliofanywa na Kitengo chs Utafiti cha Bunge la Congress (Congressional Research Service) ikaelezwa kuwa kumekuwa na taarifa za uvunjifu wa haki za binadamu katika baadhi ya nchi zinazopokea misaada k u t o k a M a r e k a n i ya kupambana na ugaidi (U.S. counterterrorism assistance).

.Wizara ya Mambo ya Nje ikasema kuwa miongoni m wa m a m b o m a o v u yanayofanyika ni mauwaji (unlawful killings), utesaji, na utumiaji mkubwa wa nguvu unaofanywa na vyombo vya usalama.

N c h i z i l i z o t a j w a kuhusika na v i tendo hivyo viovu na haramu vya utesaji na mauwaji ni Burundi, Ethiopia, Kenya, Sudan, na Uganda.

Kwa nchi za Afrika

Inatoka Uk. 1 Mashariki, ripoti hiyo ya Bunge la Marekani ( C o n g r e s s ) i n a s e m a kuwa baadhi ya Serikali zimekuwa zikifumbia m a c h o n a k u b a r i k i uovu unaofanywa na vikosi vya kupambana na ugaidi (anti-terrorism security forces.) Kwamba vikosi hivyo vimekuwa vikionea watu na kufanya uhalifu unaovunja haki za binadamu kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi.

“State Department cited reports of unlawful killings, torture, abuse, and excessive force by security forces in Burundi, Ethiopia, Kenya, Sudan, and Uganda. …In some East African countries, there are allegations that governments have condoned abuses by anti-terrorism security forces or violated citizen rights under the pretext of countering terrorism.”

Sehemu ya ripoti hiyo inasema na kuongeza k u w a U g a n d a - J o i n t Anti-Terrorism Task Force ( JATT) na Kenya’s Anti-Terror Police Unit (ATPU) zimekuwa zikishutumiwa kwa mauwaji (unlawful killings), kupotea watu na mateso.

Ripoti ikataja kuwa makundi ya Waislamu wa Kenya, yamekuwa yakiishutumu Serikali ya nchi hiyo kwa kutumia sheria ya kupambana na ugaidi kuwahujumu Waislamu.

Madai ya Waislamu Kenya yameungwa mkono pia na ripoti ya Shirika la Kutetea Wafungwa-Amnesty Internat iona l (2008) ambayo i l i ta ja vitendo vya kukamatwa Waislamu na kupelekwa Ethiopia , Somal ia na M a r e k a n i a m b a p o wanateswa au kufungwa bila ya kufikishwa katika taratibu za kawaida za kimahakama.

Ni kutokana na historia na rekodi hiyo katika sheria za Marekani ya kujali utu, heshma na uhuru wa binadamu, t aar i fa ina fahamisha kuwa Bunge la Congress l imekuwa l ik ip i t i sha sheria kuzuiya misaada ya

kiusalama na kijeshi (U.S. security assistance) isitolewe kwa vikosi vya usalama ambavyo vimekuwa na rekodi ya kutuhumiwa kufanya utesaji na kuvunja haki za binadamu.

Moja ya Sheria hizo za Congress ni ile maarufu kwa jina la “Leahy Amendment” ambayo huzuiya misaada inayotolewa chini ya m p a n g o w a F o r e i g n Ass i s t ance Ac t (FAA) pamoja na ile ya Arms Export Control Act (AECA).

“In addition to the Leahy Amendment, Congress has introduced other legislative provisions that restrict assistance to foreign forces, including several in East Africa, that have demonstrated a lack of respect for human rights, rule of law, or civilian control.”

Kwa kuwa na mpango h u u n a i k i z i n g a t i wa kuwa Marekani ndio mshir ika na mfadhil i mkuu wa mipango yote ya kupambana na ugaidi duniani, ndio tunasema hatuna budi kuthamini nia njema na msimamo wa Serikali hiyo. Tunasema hivyo kwa sababu, kama sheria hizo zitasimamiwa na kutekelezwa pamoja na taratibu nyingine, hapana shaka haitegemewi kutokea mauwaji holela, utesaji na uvunjifu wa haki za binadamu kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi.

Kwa hivi sasa Serikali ya Kenya kupitia kikosi chake maalum cha kupambana na ugaidi- Anti-Terror P o l i c e U n i t ( AT P U ) , kinashutumiwa kuhusika na mauwaj i ya watu kadhaa, utesaji na wengine kupotea. Taarifa maaalum ya Congress tunayoinukuu katika maoni yetu haya, inazungumzia tatizo hili pale inaposema:

“Human rights reports

suggest that corruption a n d i m p u n i t y r e m a i n significant problems within the country’s police force, and there have been credible allegations of serious abuses, including extrajudic ia l executions. Some reports also suggest that the police, including the U.S.-trained Anti-Terrorism Police Unit, have reportedly mishandled critical evidence.”

(Tazama pia: U.N. Special Rapporteur on Extrajudicial Executions Philip Alston, “ S t a t e m e n t o n F a c t -Finding Mission to Kenya,” February 25, 2010; and U.S. Department of State, 2009 Country Reports on Human Rights, op. cit.

See: “Kenya: Police Lose Vital Files on Al-Qaeda,” Nairobi Star, July 20, 2009.)

Ukija kwenye ile ripoti maalum ya ‘Monitoring Group’ nayo inazungumzia tatizo hilo hilo. Inasema ule mpango na mkakati wa kupambana na Al Shabaab Afrika Mashariki, (Al-Shabaab/East Africa Al-Qaida Disruption Initiative), umekuwa ukishutumiwa kuwa ndio unahusika katika mauwaji yaliyo kinyume cha sheria ya Masheikh wa Kenya.

Kwa maneno yake taarifa hiyo iliyowasilishwa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa inasema:

"The initiative has targeted Al Hijra and been responsible for "unexplained killings, disappearances, continuous 'catch and release' arrest raids and operational disruptions"

Sasa kama huu ndio ukweli matarajio ni kuona ile sheria ya Congress, yaani “Leahy Amendment” ikifanya kazi yake kwa Kenya. Na kwa hakika kama ikitekelezwa, hapana shaka matukio kama haya ya mauwaji (Extrajudicial Executions) yangekoma. Ambalo pengine ni ombi k wa h a wa wa n a o t o a mafunzo kwa vikosi kama

hiki cha Kenya, ATPU, kwanza wange ing iza somo la sheria na haki za binadamu katika mtaala wao. Lakini muhimu zaidi, wangesimamia utekelezaji wa sheria zao wenyewe.

Tunayasema haya kwa sababu litakuwa si jambo la kueleweka na kwa hakika la kuchanganya, iwapo ripoti ya Lauren Pl o c h , i t a z u n g u m z i a juu ya mauwaji, utesaji na uvunjifu wa haki za binadamu unaofanywa na ATPU, wanaopewa mafunzo na kila aina ya misaada kutoka Marekani, lakini ripoti hiyo hiyo inasema kuwa Kenya ndiyo nchi inayopokea misaada mikubwa zaidi ya shughuli za kiulinzi, kupambana na ugaidi pamoja na ile ya kijeshi, kuliko nchi yoyote Afrika Kusini mwa Sahara.

Katika sura hii mtu atajiuliza kulikoni i le “Leahy Amendment”?

Iwapo “the U.S.-trained A n t i - Te r r o r i s m P o l i c e Unit (ATPU) wa Kenya wanashutumiwa kwa mauwaji, utesaji na utekaji watu wakapotea, mtu atashawishika kuhoji , ni mtaala wa aina gani unaotoa polisi wa sampuli hii?

H a p a n a s h a k a inawezekana kukawa na tatizo kwa wakufunzi na mtaala wanaotumia. Kwa hiyo hili nalo ni la kuangalia.

Hoja ya msingi hapa ni kama ilivyoelezwa vizuri katika ripoti ya Congress ya Marekani.

K w a m b a j a p o tunapambana na ugaidi, lakini watu wasitumie kisingizio cha kupambana na ugaidi kuuwa watu ovyo (Extrajudicial Executions), kutesa watu, kuhujumu utu wao, heshima zao na ubinadamu wao.

Sheikh Azzan aanza matibabu IndiaInatoka Uk. 2kupatiwa matibabu.

Matibabu hayo yamenza baada ya serikali kutoa k i b a l i n a Wa i s l a m u kuchaingia gharama za matibabu yake, baada ya afya yake kuzorota alipokuwa kizuizini miezi kadhaa iliyopita, ambapo aliishiwa nguvu na kuzimia mara kadhaa.

K u f u a t i a h a l i h i y o Sheikh Azzan alipelekwa katika Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar, ambapo b a a d a ya m a d a k t a r i kumfanyia uchunguzi, walibaini kuwa maradhi

yanayomsibu hayawezi kutibiwa hospitalini hapo, hivyo walishauri Sheikh Azzan apelekwe nje ya nchi kwa matibabu zaidi.

Hata hivyo urasimu ilisababisha uwezekano wa kuwahishwa katika matibabu, lakini hatimaye Wizara ya Afya ilifanikisha kupatikana kibali na Sheikh Azzan kusafirishwa India kwa matibabu mwishoni mwa wiki iliyopita.

Habari kutika India zinasema kuwa Sheikh Azzan mara baada ya kuwas i l i hosp i ta l in i , alipokelewa na madaktari na mara moja alifanyiwa

uchunguzi na kubainika kuwa figo zake zina vijiwe.

I m e e l e z w a k u w a t a y a r i m a d a k t a r i wamesghamfanyia upasiaji wa figo ya kushotio na b a a d a ya w i k i m o j a atafanyiwa katika figo ya upande wa pili.

Aidha Sheikh Azzan akiwa hospitalini hapo, atafanyiwa vipimo vya kichwani kufuatia tatizo l a k u k o s a u s i n g i z i lililomkabili alipokuwa kizuizini.

Sheikh Azan amefuatana na mkewe pamoja na Dk.Rashid Ahmed kutoka hospitali ya Mnazi Mmoja.

3 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 2013Habari

Ansaar Sunnah wasokotewa kitanziHUENDA si muda mrefu hali yaweza isiwe shwari tena Tanzania-(Mungu aepushie mbali).

Wanaotabiriwa kuwa katika orodha ya mwanzo kufikwa na ‘majanga’, ni Masheikh wa Ansaar Sunna.

A n s a a r wa m e t a j wa katika ripoti maarufu (The Monitoring Group) ya Umoja wa Mataifa ambayo imenukuliwa sana na vyombo vya habari vya Kenya katika kuelezea tukio la kuuliwa Sheikh Aboud Rogo na h iv i karibuni Sheikh Ibrahim Ismail Omar.

Sheikh Rogo anatajwa kuwa mmoja wa viongozi wa kundi linalojulikana k a m a A l H i j r a linalotuhumiwa kuwa na siasa kali na linalofanya kazi ya kutoa mafunzo kwa vijana wanaokwenda kujiunga na Al Shabaab, Somalia.

K a t i k a r i p o t i h i y o inadaiwa kuwa awali A l - H i j a w a l i k u w a wakijulikana kwa jina la The Muslim Youth Centre.

Kwa mujibu wa taarifa ya The Monitoring Group, ambayo imewasilishwa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, kama ilivyonukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari vya Kenya na vya kimataifa, Al-Hijra wametangaza vita ndani ya Kenya kwa niaba ya Al Shabaab na kwa lengo la kuiunga mkono Al Shabaab.

Na kwamba kat ika kufanya hivyo linatafuta kuungwa mkono katika Tanzania na watu wa mwanzo kuf ik iwa n i Ansar Muslim Youth Centre, Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la Daily Nation (Jumanne, Julai 23, 2013, Ripoti ya ‘Monitoing Group’ (UN) katika Somalia na Eritrea, imeonya kuwa Al Shabaab inapanga kuwatumia Muslim Youth Centre (MYC).kufanya shambulio kubwa ndani ya Kenya.

Sasa baada ya kufanyika shambulio la Westgate, m w a n d i s h i T h o m a s Joscelyn anasema kuwa Umoja wa Mataifa ulionya juu ya shambulio kubwa ndani ya Kenya likifanywa na mshirika mkubwa wa Al Shabaab.

“Just over two months prior to the Westgate Mall siege in Nairobi, the UN warned that Shabaab's main ally in Kenya was planning "to conduct new and more

Na Mwandishi Maalum

complex operations." A n a s e m a T h o m a s

na kisha kumtaja huyo “mshirika mkubwa (main ally) kuwa ni Al Hijra, awali akijulikana kama Muslim Youth Centre.

Katika habari/makala yake ya Septemba 25, 2013 Thomas Joscelyn anasema kuwa onyo la Umoja wa Mataifa , l inapatikana katika repoti yake ya Julai 12 kama ilivyotolewa na kuchapishwa na UN's Monitoring Group on Somalia and Eritrea.

K i s h a a n a n u k u u sehemu ya ripoti hiyo inayowahusisha Ansaar Suna Tanzania akisema:

“The report contains many details about Shabaab's operations in Somalia and throughout the region. Shabaab, an al Qaeda affiliate, "expected to exploit its strong ties with extremist groups in Kenya and the United Republic of Tanzania to facilitate its external operations.”

CNN nayo haikuachwa nyuma katika kuwasokotea kamba Ansaar, inasema:

“Probably owing to its limited success and the rather kinetic approach to counter-terrorism taken by the Kenyan security services, Al Hijra, in partnership with the Ansar Muslim Youth Centre in the United Republic of Tanzania, has sought operat ional direction and guidance since the latter part of 2012 from individuals with former ties to Al-Qaida in East Africa and self-styled Al-Qaida affiliates.”

Na mahali pengine CNN inasema: “It is important to recall that al-Shabaab is part of the al-Qaeda movement,

with strong links to al-Qaeda in the Arabian peninsular, the Magreb and other groups like Boko-Haram in Nigeria, as well as Kenyan groups like al-Hijra and the Tanzanian Ansar Muslim Youth Centre as well as al-Shabaab affiliates in Rwanda and Burundi.”

CNN ikitumia taarifa ya Monitoing Group ya UN, inatoa uchambuzi u n a o e l e k e z a k u w a walioshambulia Westgate ni hawa Al-Hijra/Tanzania Ansar Muslim Youth.

Ripoti hiyo inafafanua kuwa kukamatwa kwa mji wa Kismayu na jeshi la AMISOM, kumeidhoofisha sana Al Shabaab pamoja na Al Hijira.

L a k i n i p a m o j a n a udhaifu huo, bado Al-Hijra, imedhamiria kuwa kitisho kwa amani na usalama ndani na nje ya Somalia.

Na ndio maana inataka kuongeza nguvu kwa kumpata mshirika ambaye ni “Ansar Muslim Youth Centre in Tanzania”.

Labda ili kuona uzito w a m a d a i h a y a n a k u u n g a n i s h wa h u k o w a n a k o u n g a n i s h w a ‘Ansar’ wa Tanzania, rejea taarifa za vyombo vya habari vya Kenya na Reuters ambavyo vimeunganisha kuuliwa Sheikh Ibarahim Omar na shambulio la Westgate Mall ambapo inadaiwa kuwa waliuliwa watu takribani 70.

“At least four people were dead in the riots that ensued after an Islamic cleric was killed, two weeks after Islamic militants killed at least 67 people in a Nairobi shopping mall.”

Gazeti lingine likasema:

“The shooting of Sheikh I b rah im Omar ign i t ed religious tensions in the commercial and tourism hub, two weeks after Islamist militants killed at least 67 people in a raid on a Nairobi shopping mall.”

H i y o n i t a a r i f a ya magazeti kwamba watu wanne waliuliwa kufuatia vurugu zilizoibuka baada ya kuuliwa Sheikh Ibrahim Omar.

Habar i haz ikuishia hapo, zinamuunganisha Sheikh Ibrahim na kuuliwa watu 67 pale Westgate mall, Nairobi.

“Islamic cleric was killed, two weeks after Islamic militants killed at least 67 people in a Nairobi shopping mall.”

Kinachosemwa hapa ni kuwa watu 67 waliuliwa na Waislamu ( Is lamic militants).

Na hivyo kuuliwa Sheikh Ibrahim wiki mbili baada ya Waislamu kuuwa watu 67, watu wanalipa kisasi.

N i k a n a k w a m b a unasema ni haki kuuliwa Sheikh Ibrahim, kama yeye (Waislamu) walivyouwa watu 67!

Swali la msingi ni je, ni Waislamu (Islamic militants) waliovamia Westgate Mall na kuuwa watu 67?

Lakini taarifa hizi za Thomas Joscelyn zinakupa mwanga ni kwa nini magazeti hapa nchini yalikuwa yaking’ang’ania kusema kuwa magaidi w a l i k u w a w a m e v a a vitambaa vilivyoandikwa Qur’an huku mengine yakidai kuwa magaidi walitoa test kabla ya kuuwa.

U n a u l i z w a u s o m e

aya ya Qur’an na kutaja jina la Mama wa Mtume M u h a m m a d , k i s h a unaachiwa. Wanaoshindwa ndio Wakristo, wanauliwa!

Unapata picha pia ni kwa nini baadhi ya magazeti yalikuwa yaking’ang’ania kuwa Samantha kakimbilia Tanzania (kuwafuta Ansar, washirika wa Al Hijra).

Nini kinafuata baada ya habari/propaganda hii? Ansaar na Waislamu wa Tanzania kwa ujumla watarajie nini?

S i k i l i z a t a a r i f a ya ‘Monitoring Group’, ya Thomas Joscelyn pamoja na yale yaliyoandikwa na gazeti la Standard.

Mwandishi Thomas a n a s e m a k u w a u p o mpango wa kupambana na watuhumiwa wa ugaidi ambao hujulikana kwa jina la "Al-Shabaab/East Africa Al-Qaida Disruption I n i t i a t i v e , " a m b a o unafadhiliwa na Marekani.

Huu ni mpango na mkakati katika jitihada za kuzisaidia nchi za Afrika Mashariki kupambana na magaidi.

Sasa msikilize vizuri: Anasema: "The initiative has targeted Al Hijra and been responsible for "unexplained killings, disappearances, continuous 'catch and release' arrest raids and operational disruptions"

Anasisi t iza Thomas kuwa hasemi hayo kwa kudhani bali ni kwa mujibu wa taarifa ya Umoja wa Mataifa iliyochapishwa na Monitoring Group.

Anaongeza akisema, “UN. report identifies several Al Hijra leaders who have been killed or disappeared as part of the initiative, including Sheikh Aboud Rogo Mohammed, Al Hijra's "ideological leader," who was "inexplicably killed in Mombasa, Kenya" on Aug. 27, 2012. Rogo was designated a terrorist by the US government and the UN the previous month, on July 5, 2012. The Treasury Department said Rogo played a key role in recruiting Kenyans for Shabaab, among other nefarious activities.”

Wanaotajwa na ripoti ya “Monitoring Group” kwamba wametoweka k a t i k a m a z i n g i r a ya kutatanisha ni Sylvester Opiyo alias Musa Osodo, Jeremiah Onyango Okumu, Steven Mwanzia Osaka aka Duda Black na Duda Brown.

K wa u p a n d e wa k e gazeti la Standard la Kenya likieleza juu ya mauwaji na upoteaji huo wa watu linasema kuwa kwa mujibu

Inaendelea Uk. 4

SHEIKH Salim Adib aliyenusurika katika mauaji ya Sheikh Ibrahim 'Rogo'.

4 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 2013Habari

Ansaar Sunnah wasokotewa kitanziInatoka Uk. 3

wa vyanzo vya habari kutoka ndani ya Idara ya Usalama ya Kenya, wahusika ni Usalama, Kenya, na hasa kikosi maalum cha kupambana na ugaidi (ATPU).

Standard la Jumamosi iliyopita linasema kuwa vyanzo vya habari kutoka Idara ya Usalama (Kenya) vinasema kuwa Sheikh Ibrahim Ismail Omar-alias Rogo, aliuliwa ili kuzuiya shambul io kubwa la kigaidi alilohisiwa kutaka kutekeleza mwisho wa wiki iliyopita katika mji wa Mombasa.

“Intelligence sources told The Standard On Saturday that Sheikh Ibrahim — alias Rogo alias Amour — was killed “in order to disrupt a major terrorist attack in Mombasa this weekend.”

K w a u p a n d e mwingine, gazeti hilo la Standard likasema kuwa kulikuwa na ripoti kuwa pol is i wangeendesha kamatakamata wakivamia makazi ya watu usiku (night raids) na Misikitini katika maeneo ya Kisauni, Likoni, Changamwe na Misikiti kadhaa katika Mombasa.

K w a m u j i b u w a sheria ya kupambana na ugadi, polisi wakiuwa mtuhumiwa wa ugaidi wapo ndani ya sheria. Sio kosa. Hakuna jinai katika kuuwa kwa lengo hilo hata kama utakosea katika kumtuhumu mtu.

Kwa hiyo kama taarifa za

Standard ni za kweli, kuwa Sheikh Ibrahim kauliwa ili kuzuiya shambulio la kigaidi, hakutakuwa na mtuhumiwa wa mauwaji hayo atakayekamatwa.

H a t a a k i k a m a t wa , hakuna kesi, ili mradi tu polisi atadai kuwa a l i y e u l i wa n i g a i d i mtarajiwa.

Kwa muunganiko huo wa CNN na taarifa ya Bwana Thomas Joscelyn j u u y a A n s a r S u n a Tanzania, kinachotafutwa n i m a u w a j i k a m a ya l i y o wa f i k a S h e i k h Aboud Rogo na Ibrahim Ismail.

L a k i n i l i n g i n e l a kuzingatia na kuchukua t a h a d h a r i k u b wa n i kuwa, tunaambiwa kuwa shambulio la Westgate Kenya limekuja kiasi miezi miwili baada ya kutolewa tahadhari kuwa Kenya kuna Al Hijra wenye uwezo wa kufanya shambulio kubwa la kigaidi.

Sasa maadhali CNN na akina Thomas wanadai kuwa Tanzanian Ansar Muslim Youth Centre, nao ni ‘al-Shabaab like group’, huu ni uchuro.

Ni bundi kalia mchana kweupe juu ya paa la nyumba.

Tumuombe Mungu, u z a l e n d o n a b u s a r a itawale kwa viongozi wetu wa Serikali pamoja na kwa polisi na makachero wetu walio katika hiyo "Al-Shabaab/East Africa Al-Qaida Disruption Initiative."

Innalillah wainna ilayhir Rajiuun.

Sheikh Salim Ali Mohamed (48) amefariki Jumatatu tarehe 07/10/2013 majira ya saa tatu asubuhi.

Kifo chake kilitokana na ajali baada ya kugongwa na gari akiwa anaendesha pikipiki (vespa) katika eneo la Mavambaruku lililoko kati ya Chake Mjini na Machomane.

Mazishi yalifanyika siku hiyo hiyo ya Jumatatu baada ya swala ya adhuhuri maeneo ya Chambani kitongoji cha Tondooni wilaya ya Mkoani ambako ndiko alikozaliwa.

Marehemu Sheikh Salim katika uhai wake alikuwa Mwalimu Mkuu Msaidizi wa skuli ya sekondari ya Wawi.

Pia amekuwa kiongozi wa harakati mbalimbali za Kiislamu kisiwani Pemba.

Sheikh Salim hatunayeNa Mwandishi Wetu, Pemba

A l i k u wa K a t i b u wa Jumuiya ya Maimam wilaya ya Chake, Amir wa kwanza wa UKUEM katika wilaya ya Chake, mjumbe wa Shura ya maadili Chake, Amir Kamati ya Walimu Waislamu kisiwa cha Pemba na Katibu wa Msikiti wa Madungu ulio jirani na anapoishi.

Marehemu alikuwa pia Naibu Amiri wa Kamati ya Kuendeleza Uislamu Kisiwa cha Pemba na ndiye aliyekuwa muwasilishaji wa ripoti ya harakati za kisiwa cha Pemba katika semina za viongozi na matamasha ya kitaifa yanayofanyika katika maeneo mbalimbali Tanzania Bara na Visiwani.

Kwa mara ya mwisho amewasilisha ripoti ya kisiwa cha Pemba katika Tamasha

la k i ta i fa l i l i lo fanyika Shengejuu Pemba mwezi June/Julai, 2013.

Marehemu Sheikh Salim Anakumbukwa kuwa ndiye katika watu wa mwanzo waliopokea fikra za harakati za kuanzisha vituo kwa kila mkoa, ambapo fikra hiyo aliipata kutokana na maazimio ya kujenga vituo vya elimu kwa kila mkoa yal iyopat ikana kwenye semina iliyofanyika Kirinjiko mwaka 2003 ambapo naye alikuwa miongoni mwa washiriki.

A l i s h i r i k i k a t i k a m a t a m a s h a ya k i t a i f a Nyasaka Islamic High School - Mwanza mwaka 2004, Mkuzo Islamic High shool –Songea, 2009 na Kirinjiko Islamic Centre.

Sheikh Salim ameshiriki m a r a n y i n g i k a t i k a matamasha ya Kanda na Kitaifa pamoja na semina za viongozi.

Katika kuyafanyia kazi hayo aliweza kuhamasisha jamii suala la ujenzi wa shule na kufanikiwa kuanzisha shule ya msingi ya Kiislamu Kijangwani mwaka 2005.

M p a k a s a s a K i s i wa cha Pemba kina shule za Kiislamu tatu zilizoanzishwa kwa mtindo wa kuhamasisha jamii.

Kwa upande mwingine S h e i k h S a l i m a l i k u wa akipokea wageni kutoka maeneo mbalimbali kwa ajili ya kufanya Daawah kisiwani humo.

H a k i k a k i f o c h a k e kimeacha pengo kubwa

na ili kumuenzi Waislamu wanatakiwa kuiga juhudi zake katika harakati za kuupeleka mbele Uislamu.

Pa m o j a n a k wa m b a alikuwa mfanya kazi wa Ser ika l i ya Mapinduzi Zanzibar, bado alitumia muda wake mwingi katika harakati za kuupeleka mbele Uislamu.

Harakati zake za mwisho zilizopelekea kukutwa na ajali, alikuwa akitokea ofisi za UKUEM, Chake mjini a k i e l e k e a M a c h o m a n e kukusanya michango kwa ajili ya matibabu ya Sheikh Azan.

Marehemu Sheikh Salim ameacha wajane wawili na watoto 14, ambapo watoto 8 ni wa kiume na 6 wa kike.

Allah amfanyie wepesi katika safari yake. Amsamehe madhambi yake na ampe jaza njema na kumzidishia katika mema yake.

Inaendelea Uk. 7

W a k a t i n i k i w a mwanafunzi siku moja nilikuwa naongea na Profesa mmoja kutoka Sweden akaniambia kuwa sisi Waafrika tuna bahati sana lakini hatujitambui. Nilipomuliza ni kwa nini anasema hivyo akaniambia kuwa bahati tuliyokuwa nayo ni ile ya kuwa ‘pamoja’ katika mambo yetu mengi , k i t u a m b a c h o h u k o kwao uzunguni kwa kiasi kikubwa kilikuwa kimetoweka.

“ N i l i p o f i k a h a p a kwa mara ya kwanza n i l i s h a n g a a s a n a . Mnakutana barabarani wawili – hamkuwa na miadi (appointment) wala nini – lakini mnapoteza dakika mbili tatu kupeana salamu na kuulizana h a b a r i ! U n a m u u l i z a mtu njia, anaona kuwa kukue lekeza tu kwa mdomo haitoshi, anaamua k u a c h a a l i c h o k u w a a n a f a n ya a k u p e l e k e huko unakotaka kwenda kabisa kabisa! Baada ya kukaa kwa siku chache hii hali iliniathiri na kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nikajiona kama naishi katika jamii ya wanadamu! Ni kweli Wa a f r i k a m n a h i t a j i kuongeza ufanisi katika shughuli zenu, lakini

Nguvu ya ibada katika kulinda siha njema - connection ya familia

Na Juma Kilaghai ufanis i wenyewe s io wa kutuiga s is i . S is i t u m e s h a h a r i b i k i w a vibaya!”

H a y a n i m a n e n o al iyoyatumia Profesa Aeglifeat, kama sijasahu, n a d h a n i h i l o n d i l o lililokuwa jina lake, ingawa nina hisia nzito kuwa tahajia (spelling) ya jina lake nitakuwa nimeikosea.

Nilipomuuliza kuwa kwani kule kwao hali ilikuwaje hadi yeye kufikia kusema hivyo alijibu.

“Kabla sijaondoka kule Sweden kuja huku, serikali ilifanya utafiti kuhusu matatizo ya kiafya ya wazee ambayo yalikuwa ya n a i g h a r i m u f e d h a nyingi sana! Ilichogundua ni kwamba wazee wengi hawakuwa na maradhi halisi , bali walikuwa wanaugua upweke! Sasa upweke unatibiwaje? Baada ya tafakuri serikali ikagundua suluhisho la tatizo hilo. Suluhisho l e n ye we l i l i k u wa n i kuwatafuta watoto wa wazee hao popote walipo waingie makubaliano na serikali kulipwa kiasi fulani cha posho, ili katika nyakati fulani fulani wakawazuru wazee wao. Kwa hesabu za serikali mkakati huu ulikuwa na gharama nafuu zaidi kuliko gharama ya dawa ambayo serikali ilikuwa inalazimika kuingia kwa

niaba ya wazee hao! Sasa kama huku siyo kuharibikiwa ni nini? Hebu fikiria, ulipwe ndiyo ukamtembelee mzazi wako?!”

W a a n d i s h i P t a k n a D u n c a n ( 2 0 0 1 ) w a n a u l e l e z e a upweke kuwa ni hali inayoambatana na msongo mkali inayotokana na k u w e k w a p e m b e n i kimaono (emotionally) au ki jamii (social ly) . Wanaendelea kuelezea kuwa kuwa mpweke au kutokuwa mpweke siyo suala la kuzungukwa na watu karibu; bali ni suala la ubora wa mahusiano b a i n a y a k o n a h a o wanaokuzunguka.

“Uchungu wa mwana aujua mzazi!’ ni msemo ambao ni kielelezo halisi cha hal i hi i . Hakuna a w e z a y e k u c h u k u a n a f a s i ya m z a z i , n a wala hakuna awezaye kuchukua nafasi ya mtoto wa kuzaa. Muunganiko wa kibaiolojia wa hawa watu wawili una nguvu mno. Mzazi wa mwenzako hata ungemtendea wema wa aina gani, pamoja na kukushukuru kwa dhati, bado atatamani kama wema huo angekuwa anatendewa na mwanae wa kuzaa, na vivyo hivyo kwa mtoto. Mtoto yatima, haijalishi atalelewa kwa

5 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 2013Habari za Kimataifa

WA Z I R I wa U t u m i s h i na Uhamiaji wa Misri amesema kuwa, misaada ya Marekani kwa nchi hiyo katika kipindi cha miaka 40 iliyopita, haikuwa na msaada wowote kwa wananchi bali imewaongezea umasikini, dhiki, ukosefu wa ajira na balaa la njaa.

Wa z i r i K a m a l a b u A' twiyyah, ameyasema hayo baada ya kuulizwa na waandishi wa habari juu ya athari zitakazoikumba Misri, iwapo Washington itaamua kukata baadhi ya misaada yake kwa taifa la Misri.

Waziri abu Atwiyyah alisisit iza kuwa, katika kipindi chote cha miaka 40

NYARAKA mpya zilizovuja zinaonyesha kuwa maafisa wa kijeshi wa Marekani walitumia kisirisiri mbinu z a k i k a t i l i z a u t e s a j i dhidi ya wafungwa wa jela ya Guantanamo, ili kuwalazimisha waache mgomo wao wa kutokula chakula.

Mawakili wanaowatetea wafungwa hao wamefichua m a d h i l a h a y o , b a a d a ya kuf ichua baadhi ya mahojiano waliyofanya na wafungwa waliogoma katika jela ya Guantanamo.

M a s h a m b u l i z i yanayofanywa usiku katika jela hiyo dhidi ya wafungwa na kubadili kiwango cha joto cha vyumba vya jela hiyo, ni miongoni mwa mbinu za kikatili zilizotumiwa na wanajeshi wa Marekani ili kusitisha mgomo wa kula chakula wa wafungwa wa Guantanamo.

Z a i d i ya wa f u n g wa wanaume 100 kati ya 164 wa jela hiyo, walianza kugoma kula chakula mwezi Februari mwaka huu wakilalamikia mazingira ya mateso na vifungo visivyo na mwisho dhidi yao.

Inakumbukwa kwamba wakati Rais Barack Obama wa M a r e k a n i , wa k a t i anawania urais na hata baada ya kushindwa uchaguzi mkuu katika awamu yake ya kwanza, alitangaza rasmi kwamba moja ya hatua za awali atakazochukua baada ya kuingia ikulu ya White House ni kulifunga gereza hilo maarufu kwa utesaji la Guantanamo.

K w a m b a w a f u n g w a wanaoshikiliwa katika gareza hilo, kesi zao zitahamishiwa k a t i k a m a h a k a m a z a Marekani kwa ajili ya hatua za kisheria, badala ya wafungwa

SERIKALI ya Ugiriki imekataa pendekezo lililotolewa na serikali ya Uturuki la kufunguliwa Chuo cha kidini cha Halki cha wafuasi wa dini ya Kikr is to ya Madhehebu ya Orthodox kwenye kisiwa kimoja kinachomil ikiwa na Uturuki, lakini sambamba na kufunguliwa Misikiti miwili ya kihistoria iliyopo jijini Athens, mji mkuu wa nchi hiyo.

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ugiriki Evangelos Venizelos, ameyasema hayo saa chache baada ya matamshi

Ugiriki yakataa kufungua Misikiti ya kaleal iyoyatowa bungeni Waziri Mkuu wa Uturuki Racep Tayyip Erdogan, kwamba Ankara iko tayari kuifungua taasisi hiyo kwa sharti kwamba Athens nayo ifungue Misikiti hiyo miwili ya kale nchini humo.

E r d o g a n a m e s e m a kuwa, Misikiti hiyo ya kihistoria ni urithi wa zama za Othmaniya (Ottoman Empire). Moja ya Misikiti hiyo ni Masjidul Fat-hiya, ambao ulijengwa yapata miaka 100 baada ya Ugiriki kukombolewa kutoka mikononi mwa dola la Othmaniya.

Athens ndio mji mkuu p e k e e b a r a n i U l a ya ambao hadi sasa hakuna h a t a m s i k i t i m m o j a unaotumiwa kwa ibada. Imeelezwa kuwa, idadi ya Waislamu nchini Ugiriki inafikia laki tatu na serikali ya nchi hiyo imekubali matakwa ya Waislamu ya kujengwa Msikit i , katika eneo ambalo awali kulikuwa na kambi ya kijeshi ya nchi hiyo, hatua ambayo imepingwa vikali na chama cha kihafidhina cha Golden Dawn, chenye ushawishi mkubwa nchini humo. (irib.ir)

Obama aliongopa kuifunga QuantanamoWafungwa wazidi kuteswa

hao kuendelea kutumikia vifungo bila kushtakiwa mahakamani, huku gereza hilo likiwa limekidhiri kwa utesaji.

Wachunguzi wa masuala ya haki wanaiona Jela ya Guantanamo kuwa ni ishara ya Marekani kukanyaga haki za binadamu kwa makusudi.

Mgomo wa kula chakula wa muda mrefu unaofanywa na wafungwa wa jela ya Guantanamo na ambao umehatarisha maisha ya wafungwa hao, kwa mara nyingine umezivutia hisia za walimwengu kufuatia kupea kiwango cha uvunjwaji wa h a k i z a b i n a d a m u unaofanywa na Washington katika jela hiyo.

Mwezi Mei katika tahariri ya gazeti la Kiingereza la The Guardian, imebainishwa Marekani kuwatia mbaroni watu wasio na hatia huko Guantanamo ambapo ilieleza kuwa, kitendo cha kutiwa mbaroni kwa muda mrefu watu wasio na hatia yoyote, kwa hakika kunahesabika kuwa fedheha kwa Marekani kutokana na kukanyaga kwake haki za binadamu.

Aidha kuhus iana na hilo, mmoja wa mawakili wa wafungwa wa jela ya Guantanamo Cindy Ponchu, amenukuliwa akiiambia t e l e v i s h e n i ya R u s s i a Today kwamba, kutokana na wafungwa wa jela hiyo k u g o m a k u l a c h a k u l a kwa muda mrefu, sasa wanakabiliwa na hali mbaya sana na tayari, wamedhoofika kiafya huku kukiwa hakuna mtu wa kuwajali.

Ponchu ameongeza kuwa, hivi sasa kunashuhudiwa hali mbaya na yenye kutisha katika jela hiyo.

Msemaji wa jela hiyo, Luteni Kanali Samuel House

wa jeshi la Marekani, aliwahi kunukuliwa akisema kuwa karibu nusu ya wafungwa kati ya 166 wanaoshikiliwa katika jela hiyo, wamegoma kula chakula cha aina yoyote ile na hivi sasa wanalishwa kwa nguvu na kwa kutumia mipira ya kupitia puani, huku watano wakiwa wamelazwa hospitalini.

Wafungwa 166 waliopo katika jela hiyo ya kutisha, w a l i a n z a m g o m o w a kutokula chakula tangu mwezi Februari mwaka huu wakilalamikia hali mbaya ya jela hiyo, kuporwa v i t u v y a o z i k i w e m o barua, kuwadhalilishwa na kuyavunjia heshima matukufu ya Kiislamu, hususan nakala za Qur’ani Tukufu.

Licha ya kutoka hali hiyo, mamlaka ya Washington wanatumia nguvu na ukatili katika kuzima mgomo huo.

K a t i k a k a m p e n i z a uchaguzi mkuu wa Marekani mwaka 2008, Rais Barack Obama Obama aliitaja hali

ya jela hiyo kuwa yenye kuwalea magaidi.

Siku ya pili ya kuingia White House, rais huyo a l isa ini sher ia ambayo ilitaka kufungwa jela ya Guantanamo kufikia mwaka 2010.

Hadi sasa ni mwaka 2013, bado jela hiyo inaendelea na shughuli zake za utesaji na ukandamizaji wa haki za binadamu. Tayari Wizara ya Ul inzi ya Marekani Pentagon, imeshawasilisha mpango wake wa kutumia dola milioni 50 kwa ajili ya kuikarabati jela hiyo.

Hadi sasa Rais Obama hajatekeleza ahadi yeyote al iyoitoa kuhusiana na kuifunga jela ya Guantanamo, zaidi ya kutoa ruhusa kwa maafisa wanaosimamia usaili wa wafungwa wa jela hiyo, kutumia aina yoyote ya adhabu kandamizi dhidi ya wafungwa hao.

W a f u n g w a h a o wa n a e n d e l e a k u t e s wa wakitumikia vifungo bila kushtakiwa mahakamani na haki ikatendeka.

K a t i k a j a m i i y a

k i d e m o k r a s i a n a i l i y o s t a a r a b i k a , w a t u w a n a o t u h u m i w a k w a makosa au kudaiwa kutenda jinai yeyote wanapaswa kuwekwa kuzuizini kwa kipindi maalumu kwa ajili ya uchunguzi kwa mujibu wa sheria.

K i t e n d o c h a w a t u kuwaweka kizuizini bila hat ia au kuthibi t ishwa tuhuma dhidi yao, huo ni uvunjwaji wa wazi wa haki za binadamu.

Jela ya Guantanamo iligeuzwa na Washington muongo ul iopita kuwa sehemu ya kutekelezwa vitendo vya ukandamizaji wa wazi wa haki za binadamu na sheria za kimataifa. iliasisiwa kwa lengo hilo mwaka 2001 baada ya mashambulizi ya kijeshi ya Marekani nchini A f g h a n i s t a n , a m b a p o wa s h u k i wa wa u g a i d i kutoka sehemu mbalimbali za dunia, hutiwa mbaroni na kupelekwa katika jela hiyo kwa ajili ya kufanyiwa usaili unaoambatana na mateso makali dhidi yao. (irib.ir)

Misaada ya Marekani imeleta umasikini Misri iliyopita wananchi wa Misri

wamekuwa masikini na kukabiliwa na balaa la njaa na wamekuwa hawana ajira.

K w a m u d a m r e f u , Marekani imekuwa ikitoa zana za kijeshi kwa utawala wa Hosni Mubarak, unaofikia dola bilioni moja na milioni mia tatu kwa mwaka na misaada mingine ya kifedha ipatayo dola milioni 250, ikiwa ni ya pili kwa kupata misaada mingi baada ya utawala wa Kizayuni wa Israel.

Hivi karibuni Marekani i l i tangaza nia yake ya kusitisha misaada yake ya kijeshi Misri, kwa madai ya kutoridhishwa na hali inayoendelea nchini humo. (irib.ir)

Mfungwa wa jela ya Guantanamo akiwa katika Machela na pingu gerezani humo.

6 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 2013Makala

Mombasa wananyolewa tutie vichwa vyetu maji

MIAKA kadhaa nyuma wakati wa uhai wa Sheikh Omar el Bashir, palitokea tukio moja ambalo linapasa kuvuta fikra za Waislamu kwa kina sana kwa sasa pengine kuliko hata wakati ule.

Tukio lenyewe ilikuwa hivi: Wakati huo Sheikh O m a r B a s h i r a l i k u wa kakamatwa na kuwekwa rumande. Wakafika vijana nyumbani kwake wakiwa na viroba vya mchele. Vijana hao wal io j i tambul i sha k wa m k e w e k u wa n i ‘Wanaharataki’ wa Kiislamu, walisema mchele huo ni sadaka kwa ajili ya familia ya Sheikh.

Wakasherehesha vya kutosha kwamba ‘Muislamu nduguye Muislamu’ na kwamba Waislamu katika k u p e n d a n a k w a o n a kuhurumiana kwao, ni kama mwili mmoja. Kiungo kimoja kikipata jeraha, basi mwili mzima hutetemeka kwa machungu na homa. K wa h i y o wa k a s e m a , isingewezekana Waislamu wakala na kunywa bila ya kujali familia ya Sheikh ipo katika hali gani. Ndio wameleta sadaka hiyo.

Sadaka ya viroba vya mchele ikapokelewa. Lakini mara tu walipoondoka vijana hao, wakaja askari wakidai kufanya upekuzi. Moja kwa moja wakaviendea vile viroba vya mchele. Kilichofuatia ni sherehe ya habari kwa TV na magazeti. Ikaripotiwa kuwa nyumbani kwa Sheikh Omar El Bashir kumekamatwa milipuko ya kutengezea mabomu iliyokuwa imefichwa katika viroba vya mchele.

Nimekumbuka kisa hiki baada ya kusikia taarifa ya mama mmoja wa Mombasa akihojiwa na BBC akieleza jinsi mumewe alivyopigwa na polisi na akakamatwa na kupelekwa rumande baadae ikaripotiwa kuwa alikutwa na guruneti. Hiyo ilikuwa Ijumaa.

Anasema mama huyo kuwa ghafla polisi walivamia nyumba yao wakaanza kumpiga mumewe huku wakipekuwa kila mahali wakimwambia atoe silaha alizoficha huku wakidai kuwa yeye ni gaidi. Ni Al Shabaab. Kipigo kilikuwa kikali na mara zote mumewe akiwaambia polisi kuwa yeye hana silaha watamuuwa bure. Mkewe aki jar ibu kumtetea kwa kusema kuwa hana silaha naye akaburuzwa vya kutosha.

“Mtaniuwa bure. Sina kitu. Sina silaha.” Alisema mama huyo akimnukuu m u m e w e a k i l i a k w a uchungu kutokana na kipigo cha polisi.

Akisimulia mama huyo anasema, alishangaa kusikia ikidaiwa kuwa mumewe alikamatwa na guruneti.

Na Omar Msangi

Anasema anachokumbuka ni kuwa askari hao walikuja na fuko fulani likionekana kujaa kitu ndani na juu kuwekwa makaratasi. Hakujua lina nini, lakini ndio fuko hilo baadae ilidaiwa kuwa lina guruneti alilokamatwa nalo mumewe. Hadi sasa bwana huyo-Muislamu wa Mombasa yupo ndani akituhumiwa gaidi aliyekutwa na guruneti la kufanyia ugaidi.

Kesi kama hiyo ilimkuta pia Almarhum Sheikh Aboud Rogo. Huyu naye alikamatwa na Polisi kwa tuhuma za kumkuta na silaha kinyume na sheria.

Alipelekwa mbele ya mahakama ya Mombasa Agosti 14 kwa mashitaka ya kupanga mashambulizi katika maeneo ya umma.

Sheikh Rogo aliyakana mashitaka dhidi yake na kuachiwa kwa dhamana hadi Oktoba 15, ambapo kesi yake ilikuwa isikilizwe tena. Lakini akauawa takribani wiki tatu kabla ya tarehe hiyo.

H a b a r i z i l i z o k u w a z i m e s a m b a a M o m b a s a wakati ule ni kuwa Sheikh Rogo al ikuwa amenasa picha za Polisi waliokuwa wa m e p a n d i k i z a s i l a h a nyumbani kwake kisha wakamkamata na kudai ni zake. Lakini kabla Sheikh hajafikisha ushahidi wa picha hizo Mahakamani, ndio akauliwa kabla ya kufika siku ya kesi.

Ukiacha hilo, kumekuwa

na mfululizo wa mauwaji walengwa wakiwa Masheikh. J u z i h a p a wa m e u l i wa Masheikh watatu ikiwa ni pamoja na Sheikh Ibrahim Omari, maarufu Ibrahim R o g o . M a s h e i k h h a o wameuliwa kama alivyouliwa Sheikh Aboud Mohammed Rogo. Gari lao liliminiwa risasi wakitoka Msikitini ambapo wote walikufa papo hapo. Mwenzao mmoja waliyekuwa naye ndiye alinusurika.

Taarifa zinaeleza kwamba Abu Makaburi na Sheikh Ibrahim Omar, kabla ya kukutwa na mauti walikuwa wakipata vitisho vya kuuliwa, ikidaiwa kuwa vitisho hivyo vililenga kuzima vuguvugu la Da'awah ya haki.

Baadhi ya wananchi wa Mombasa wanakituhumu k i k o s i m a a l u m u c h a kupambana na ugaidi kuwa ndicho k i l i choteke leza mauaji hayo.

Baadhi ya taarifa zinadai kuwa pamoja na kuuliwa Sheikh Ibrahim Rogo na wenzake watatu, Masheikh wengine akiwemo Sheikh Abu Bakar Makaburi, nao wanafuatiliwa ikidaiwa kuwa wanahusishwa na vitendo vya kigaidi.

P o l i s i w a m e s e m a k u wa m u h u b i r i h u y o alikuwa amehubiri katika msikiti uliohusishwa na wanamgambo wa Kiisilamu wa Al Shabaab.

Sheikh Ibrahim Rogo, ambaye al ikuwa akitoa mihadhara kwenye Msikiti wa Musa mjini Mombasa,

alituhumiwa na jeshi la polisi kuwa anawachochea vijana wa Kiislamu kujitumbukiza kwenye makundi ya kigaidi.

Kwa mujibu wa taarífa ya Jukwaa la Haki za Binaadamu kwa Waislamu, (kama ilivyoripotiwa katika An nuur ya wiki iliyopita), mnamo mwezi Machi mwaka 2002, mhadhiri mwengine wa Kiislamu, Samir Khan, aliyekuwa pia akikabiliwa na mashitaka ya kuwa na silaha kinyume na sheria na kutoa mafunzo kwa ajili ya al-Shabaab, na rafiki yake Mohammed Qassim, walitolewa kwenye basi mjini Mombasa na watu waliojitambulisha kama polisi.

M w i l i w a K h a n ulikuja kugundulika siku kadhaa baadaye katika mbuga ya Tsavo, ukiwa umekatwakatwa vibaya huku hatima ya Kassim ikiwa hadi sasa haijuilikani.

Kwa mujibu wa Human Rights Watch, mwanzoni Polisi ya Kenya ilikuwa imewaambia waandishi wa habari kuwa Khan alikuwa ameshikiliwa na Kikosi Maalum cha Kupambana na Ugaidi, lakini baadaye wakakana kumshikilia.

H i i n d i y o h a l i inayowakabili Waislamu wa Kenya hivi sasa. Ni hali ya hatari. Ni ishara tosha kwamba maisha ya walinganiaji wa Kiislamu yamo hatarini. Kinachojitokeza ni kuwa kadiri serikali ya Kenya i n a v y o s e m a i n a j i z a t i t i kupambana na ugaidi , ndivyo wanavyoumia zaidi Waislamu.

U k i r e j e a h i s t o r i a ya miaka ya 1960s/70s, ya Amerika ya Kuisni, utaona kuwa mauwaji yaliyokuwa yakifanyika katika nchi hizo yakiwakumba watu wa dini, wanaharakati wa taasisi za kijamii, waandishi wa habari na wengine wengi waliokuwa wakitetea haki za wazalendo wa nchi hizo, sura yake ndiyo kama hii inayoibuka Kenya.

S a s a m a a d h a l i Kenya ni jirani zetu, na m a a d h a l i m a u wa j i n a utesaji unaofanyika huko unanasibishwa na vita dhidi ya ugaidi, na maadhali hapa kwetu napo imepigwa sana propaganda kuwa kuna magaidi, basi tujiandae. Waislamu tukae macho. Ni vigumu kusema ni tahadhari gani zichukuliwe kwa sababu kama inavyosemwa, hasidi hana sababu, lakini yapo mambo ya kuzingatia.

M o j a l a m u h i m u n i

kuielewa hali hiyo. Watu waie lewe h iyo ha l i i l i w a s i b u r u z w e k i j i n g a kutokana na propaganda za vyombo vya habari na baadhi ya wanasiasa na vyombo vya usalama. Kwa maana kuwa, kwanza, wasije wakafanywa washirika wa kuwapiga vita Waslamu wenzao wakiwadhania kuwa ni magaidi.

Pi l i , kuwa macho na ‘wanaharakati’ kama wale ‘wanaharakati viroba vya mchele.’

Tatu, pengine tufanye jitihada kubwa zaidi za kizalendo kuieleimisha jamii ikiwa ni pamoja na vyombo vya habari na hata taasisi za kiserikali kwamba nchi ikishatumbukizwa katika vita hii na kufanywa mshirika muhimu katika kupambana na ugaidi, ndio imeangamia.

H a k u n a n c h i iliyoaminishwa na mabeberu kuwa inakabiliwa na kitisho cha ugaid i , ika fanywa mshirika muhimu katika kupambana na magaidi iliyosalimika.

La kufahamu ni kuwa kadiri unavyosambaziwa taarifa kuwa una magaidi na kupewa mikakati au ukajiwekea mikakati ya kupambana nao na ukaomba m s a a d a k u t o k a k w a unaowadhania kuwa wana utaalamu na uzoefu; ndivyo unavyojisokotea kitanzi madhubuti na cha uhakika cha kuinyonga amani na usalama wa nchi yako.

Uzoefu unaonesha kuwa nchi ikishazama katika vita ya kupambana na magaidi, mauwaji kama haya ya Sheikh Ibrahim yatakuwa ya mara kwa mara.

Maguruneti yataendelea k u v u r u m i s h wa k a t i k a shabaha mbalimbali na kuuwa watu wasio na hatia.

Na hayo yakifanyika, yataendelea kupandisha mori na mdadi wa vikosi maalum vya kupambana na ugaidi na polisi wa kawaida kukamata watuhumiwa.

P e n g i n e b a d a l a y a wananchi kuihimiza Serikali yetu kujizatiti kupambana na magaidi, tungeitaka ifanye juhudi kusoma hii hali katika nchi zilizotutangulia katika mchezo huu.

Akijibu tuhuma kuwa huenda Polisi Kenya ndio wanaopandikiza silaha kisha hukamata Masheikh wa Kiislamu na kuwabambika ugaidi, Kamanda wa Polisi Mombasa alitoa maelezo marefu akidai kuwa wao wanachofanya ni kuhakikisha usalama wa nchi na kwamba usalama ni kwa kila mtu. Kwamba vita dhidi ya ugaidi lazima ipiganwe kwa juhudi kubwa na kwa nguvu zote.

L a k i n i m a s i k i n i alichoghafilika Kamanda huyo (labda naye kutokana na kasumba aliyokwishalishwa) n i k u wa h a k u n a n c h i i t a k a y o s a l i m i k a k w a kuingizwa katika mchezo wa kupambana na magaidi.

Itasalimika kwa kukana k u wa h a i n a m a g a i d i . Kama ingekuwa vikosi vya kupambana na ugaidi vinaipa nchi amani, basi amani na usalama huo ungeonekana hii leo Afghanistan, Pakistan, Yemen, I raq , L ibya na Somalia.

Kupambana na ugaidi ni kufuta usalamaWanaong’ang’ani vita hii wana lao jamboWaseme wanamtumikia nani? Wanapata nini?

Sheikh Ibrahim Omari, maarufu Ibrahim Rogo.

7 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 2013Makala

Inaendelea Uk. 10

Nguvu ya ibada katika kulinda siha njema - connection ya familia

Inatoka Uk. 4upendo kiasi gani, pamoja na kufurahia upendo huo, ndani ya moyo wake bado atatamani sana kuwa huyo anayemlea angekuwa ni mzazi wake wa kumzaa. Na hiki ndicho kilichokuwa kinawaathiri hao wazee we t u wa K i s we d e n . Serikali ilikuwa inajitahidi kuwapa kila kitu, lakini h a i k u t o s h a . M i o y o yao ilikuwa inatamani kuwaona watoto wao, wazungumze nao, japo kwa muda kidogo tu!”

Je, upweke unaathiri v i p i a f ya z a wa t u ? Wataalamu wanasema u p w e k e h u c h o c h e a mwili kuzalisha homoni ( h o r m o n e s ) a m b a z o zinabadilisha mifumo ya mwili katika hali ambayo n i h a s i . Wa a n d i s h i Ptak na Duncan (2001) wanasema miongoni mwa magonjwa yanayotokana na upweke ni vidonda vya tumbo, pumu, kiharusi, mfadhaiko, maumivu mfululuzo ya kichwa, m a g o n j wa ya m o y o , ulevi, hamu ya kujiua, na magonjwa ya mfumo wa kinga za mwili. Aidha wanasema upweke mara nyingi hutuzuia tusipone, au tusipate nafuu katika maradhi yanayotusumbua.

Kutokana na matatizo h a y a y a u p w e k e uliopindukia, leo uzunguni wamebuni utaratibu wa tiba unaotumia wanyama (Animal Assisted Therapy). Baadhi ya v ipengele vya utaratibu huu ni kuwatumia wanyama mbalimbali kuwa karibu n a wa t u mb a l i mb a l i wenye matatizo ya kiafya, kitendo ambacho tafiti z i m e o n y e s h a k u w a kinasaidia sana kutoa ahueni kwa mgonjwa. Kusema ule ukweli huko uzunguni wamefikia hatua hiyo kwa kule kudhani kwao kuwa hawamuhitaji tena Mungu! Mungu amebaki kama kielelezo cha misimu ya sherehe, lakini siyo kwa kutoa miongozo ya jinsi ya kuishi katika hii dunia.

Moja ya ibada kubwa kabisa ni kuwaheshimu w a z a z i w a w i l i , n a k u w a t u m i k i a b i l a k i n y o n g o h a d i p a l e watakapoondoka juu

uso huu wa dunia. Kwa mtizamo huu wa kidini, jukumu la kuwatunza wazazi wazee siyo la jamii bali ni la watoto wao. Kama ambavyo Wasweden wamegundua wakati washachelewa, watoto ni dawa kubwa sana kwa wazazi wao pale wanapokabiliwa na maradhi ya uzee.

Suala la kuwatendea wazazi wema na ihsani ni suala ambalo limesisitizwa sana na dini. Mathalani baadhi ya maelekezo ya Uislamu kuhusu suala hili ni haya yafuatayo:

“Muabuduni Mwenyezi M u n g u n a w a l a msimshirikishe na chochote, na wafanyieni ihsani wazazi wawili, na jamaa na mayatima na maskini.” (Quran 4:36)

“ N a M o l a w a k o a m e h u k u m u k u w a msimuabudu yeyote ila Yeye tu. Na (ameagiza) k u w a f a n y i a w e m a (mkubwa) wazazi. Kama mmoja wao akifikia uzee,

(naye yuko) pamoja nawe, au wote wawili , basi usiwaambie hata “Ah!” wala usiwakemee. Na useme nao kwa msemo wa heshima (kabisa). Na uwainamishie bawa la unyenyekevu (njia ya kuwaonea) huruma (kwa kuwaona wamekuwa wazee). Na useme “Mola wangu! Warehemu (wazee wangu) kama walivyonilea katika utoto” (Quran 17: 23-24)

“Wanakuul iza watoe nini? Sema: “Mali yoyote mtakayotoa (itoeni) muwape wazazi, na ndugu, mayatima, na masikini, na wasafiri ( wa l i o h a r i b i k i wa ) , n a waliokuwa (kama hawa). Na wema wowote mnaofanya Mwenyezi Mungu anajua.” (Quran 2: 215)

“ N a t u m e m u u s i a mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu na akamzaa kwa taabu. Na amebeba mimba yake hadi kumwachisha ziwa ; (uchache

wake) ni miezi thelathini. Na hata anapofikia baleghe yake na akawa mwenye umri wa miaka arobaini (mtoto mwema) husema : “Ewe Mola wangu! Niwezeshe nishukuru neema zako ulizonineemesha mimi na wazazi wangu, na niwezeshe nifanye vitendo v izur i unavyovipenda , na unitengenezee watoto wangu; kwa yakini ninatubu kwako; na hakika mimi ni miongoni mwa waliosilimu (walionyenyekea).” (Quran 46:15)

K w a k u z i n g a t i a maelekezo haya ya Quran tukufu, na bila shaka kwa kuungwa mkono na maelekezo ya vitabu vya dini nyingine ambazo chimbuko lake ni Mungu mmoja, suala la watoto k u w a f a n y i a w a z a z i wao wema na ukarimu ni miongoni mwa ibada k u b wa k a b i s a . K i l a mwenye kutekeleza ibada hii ajue kuwa amempa pia mzazi wake au wazazi wake, dawa kubwa na ya kipekee; ambayo bila ya shaka yoyote itaboresha sana ubora wa maisha kiafya kwa wazazi wake.

M u n g u a k i p e n d a tutaendeleza mada hii wiki ijayo.

(Kwa hisani ya Ukurasa wa Herbal Impact katika Facebook)

T u n a p o z u n g u m z i a lishe, suala la uhalali au uharamu halipimiki kwa kipimo sawa kwa kila mtu. Ni suala linalotegemea zaidi utamaduni wa jamii mbalimbali tofauti, na au imani za dini. Uhalali au uharamu katika lishe unaoegemea kwenye utamaduni fulani, ni tofauti na ule uhalali au uharamu unaoegemea kwenye imani ya dini. Uhalal i au uharamu katika lishe unaoegemea k w e n y e u t a m a d u n i hubadilika kulingana na mabadiliko ya utamaduni husika, tofauti na ule unaoegemea kwenye imani za dini ambao unakuwa ni wa kudumu, ukiwa ni sehemu muhimu ya mafundisho ya dini husika.

Kwa mfano, Wamaasai wa zamani walikuwa h a wa l i s a m a k i wa l a

Nguvu ya ibada katika kulinda siha njemaConnection ya lishe (halali, nzuri na kiasi)

Na Juma Kilaghai kuku. Sehemu kubwa ya utamaduni wa Kimaasai miaka hiyo ulijifunga k w e n y e u f u g a j i w a n g ’ o m b e . C h a k u l a halali kwa Wamaasai wa enzi hizo kilikuwa ni kile kinachotokana na wanyama hao – nyama, maziwa, damu na samli. L e o h i i u t a m a d u n i ulijiofungamanisha na u f u g a j i wa n g ’ o m b e k w a k i a s i k i k u b w a u m e s a m b a r a t i k a . Leo vi jana wengi wa Kimaasai wanakimbilia mijini kufanya kazi za ulinzi, ususi wa rasta za Kimaasai, na uuzaji wa miti shamba. Kutokana na vijana hawa kutokuwa tena na mahusiano ya karibu na ng’ombe, leo wanakula kuku, samaki, na hata nafaka mbalimbali.

Kwa upande wa pili, pamoja na mabadiliko yote yanayotokea katika jamii – kiutamaduni, kielimu, kitekinolojia, nakadhalika

– Wakristo wa madhehebu ya Kisabato hadi leo lishe yao inaamuliwa na maandiko katika vitabu vyao vya dini. Ukimkuta Msabato kwa mfano anakula samaki wasio na magamba, basi ujue kuwa huyo ni asi tu, na wala ulaji wake huo hauwakilishi mabadiliko yoyote ya kilishe katika dhehebu hilo kwa ujumla. Vivo hivyo kwa waumini wa dini ya Kiislamu. Mafundisho ya dini ya Kiislamu yanatakaza ulaji wa vyakula kadhaa, kwa mfano nyama ya nguruwe. Sasa pamoja na kwamba tuko kwenye karne ya ishirini na moja, karne ya sayansi na tekinolojia, tena katika kipindi ambacho upashanaji wa habari kwa kasi (information age) ndio njia kuu ya uchumi, hutamkuta Muislamu akila nguruwe hadharani kwa sababu l imetoka tamko la jumla kutoka

kwa wanazuoni wa dini hiyo kwamba sasa ‘kiti moto’ ni halali. Ukimkuta Muislamu huyo basi ni asi tu, kama ambavyo yule Msabato alaye samaki asiye na magamba alivyo asi kwa dhehebu lake.

Kwa kuwa suala la a f ya n j ema n i su a la linalotegemea, pamoja na mambo mengine , lishe bora na wala siyo utamaduni wala dini ya mtu, hebu suala la uhalali tulijadili, tukiwa tumelifungamanisha na suala la uzuri (ubora). Kwa muktadha huu, chakula kinaweza kikawa ni halali lakini kikawa siyo kizuri (bora). Kwa mfano maziwa ni chakula ambacho ni halali kabisa kwa itikadi ya dini zote, hata Mabaniani. Hata hivyo ubora wa maziwa unategemea kama yamesindikwa ama la. Maziwa yaliyosindikwa kwa nia ya kuyapa uhai wa muda mrefu madukani (long shelf life) siyo chakula bora. Sababu ya kukosa ubora ni kuwa katika

usindakaji huo maumbile ya baadhi ya virutubisho kwenye maziwa hayo hubadilika, na mabadiliko hayo yanawadhuru baadhi ya walaji bila wenyewe kujitambua. Madhara haya mara nyingi yanakuja katika mtindo wa mzio (allerge), na mtumiaji anaweza akahangaika sana kabla ya kugundua kuwa kinachomsumbua ni utumiaji wa maziwa yaliyosindikwa!

Mfano mwingine ni nyama, mathalani ya ng’ombe. Nyama husika inaweza kuwa imepatikana b a a d a y a n g ’ o m b e kuchinjwa kwa taratibu zote za Kiislamu, na kwa maana hiyo ikawa ni halali kuliwa na kila mtu. Sasa mtu akichukua nyama hiyo akaenda kuchoma mishikaki, bila kuchukua tahadhari stahiki, uhalali wa nyama hiyo utabaki pale pale, lakini mishikaki husika haiwezi kuitwa ni chakula kizuri. Hii ni kutokana na ukweli

8 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 2013Makala

WASWAHILI tunajua sote msemo maarufu wa Wimbo Mbaya H a c h o m b e z e w i Mtoto. Kwa mila na utamaduni wetu, mzazi atajiepusha kwa kila hali kuimba wimbo a i n a h i y o a m b a o unaweza kumpeleka au kumuelekeza mtoto pabaya.

Lakini hii haiwazui w a t u w e n g i n e wasimwimbie wimbo mbaya mtoto wako. Na miongoni mwa w a t u w e n g i n e n i pamoja na ndugu zako kama ilivyotokea hivi karibuni kwa magazeti ya Ta n z a n i a B a r a kuchapisha makala yenye kuiimbia nyimbo mbaya sana Zanzibar.

K i s i n g i z i o c h a o cha kuchapisha n i kuwa makala hayo yamepatikana kutoka kwenye mashirika ya habari ya kimataifa, a u y a m e a n d i k w a baada ya uchunguzi wa waandishi wao. Lakini kwa fikra zangu wahariri wanapaswa kuwa na hadhari kuwa makala yatokayo nje yanayoeleza kuwa kuna mvutano na uhasama wa kidini na wenye mnaso wa Ki-Alqa’ida au wa Ki-Al-Shabaab, hayawezi kutumiwa tu hivi hivi.

Kwa itakavyokuwa na kwa kipimo chochote kile, Mhariri wa gazeti lo lo te l i l e l a Bara anapaswa kuwa anaijua Zanzibar. Mbali na hayo alipaswa pia kufanya juhudi kuyatia makala hayo

k a t i k a m i z a n i a na kwa hivyo yawe yametumika pia kwa fa ida ya Zanzibar , ambayo ni sehemu ya taifa hili.

Upotoshaji mkubwa u l i o f a n y wa k a t i k a makala kama hayo, a u h a t a m a o n i ya Wahariri yasiojenga, u n a i d h a l i l i s h a Z a n z i b a r . L a k i n i upotoshwaji mkubwa n i u le wa Mhar i r i kukubali makala hayo yachapishwe katika gazeti lake akijua kuwa yanaukashifu upande mmoja wa Jamhuri

Wimbo mbaya wa magazeti Na Ali Saleh

ya Muungano, yaani Zanzibar.

K w a k u y a k u b a l i makala hayo Mhariri anakuwa anakubali kuwa hali iko mbaya sana Zanzibar kwa sababu ya matukio ya watu kumwagiwa t i n d i k a l i n a k w a sababu za kidini wakati waliotiwa tindikali ni pamoja na Waislamu akiwemo Sheikh Fadhil Soraga.

Na wakati Tanzania Bara nako tindikali inatumika, na ambako pia risasi, mabomu sio vitu vigeni, tena vyereje k wa Z a n z i b a r i we mwao?

Kama hisia za kuwepo kwa mtafaruku wa kidini ni kwa sababu ya kupata nguvu Uamsho, Mhariri wa gazeti anapaswa kujua kuwa jumuiya ya Uamsho imepata nguvu si kwa ajili ya mtizamo wa kidini ila ni kwa sababu ya kudai haki za Wazanzibari. Na haya Bara si mageni pia.

Mhariri anajua hilo kwa sababu Uamsho imesajiliwa, imefanya kazi nyingi za kijamii

lakini jina lake limeingia dosari katika kipindi h ik i cha mchakato wa Katiba kwa kudai Zanzibar ipate haki zake kamili ndani ya Jamhuri ya Muungano. Kamwe U a m s h o h a i j a s e m a kuwa inataka Zanzibar ijitenge wala Zanzibar iwe dola ya Kiislamu.

Kinachonisikitisha zaidi ni kuona Serikali ya Zanzibar imekaa k i m ya , b u r d a n wa sururi, haya yakifanyika n a ya k i f a n y wa n a ndugu zao wa damu. H a i we z e k a n i wa l a haikhalis kabisa kwa Serikali ya Zanzibar kulinyamazia suala kama hil i . Naamini ingekuwa jambo hilo limefanywa na gazeti l a Z a n z i b a r L e o kuchapisha makala yanayoipaka matope Serikali ya Muungano, b a s i S e r i k a l i h i y o ingekuwa imeshafanya v i s h i n d o d h i d i ya Zanzibar.

Kama ningepewa fursa ya kuishauri Serikali ya Zanzibar katika hili, basi inatosha kuwaambia kuwa wawasiliane moja

kwa moja na wenzao wa Tanzania Bara juu ya hujuma hii. Lakini wakati nyimbo mbaya ikiimbwa upande wa pili wa bahari, hata humu ndani pia mwenzetu m m o j a , K a m i s h n a Mussa Ali Mussa, naye amechukua tarumbeta akipaza nyimbo kama hiyo. Anapiga zumari ndani ya nyumba yake.

K a t i k a k i p i n d i h ik i cha mt ik i s iko wa mashambulizi ya tindikali, ambayo wengi tunayalaani kwa nguvu zote kuwa ni ya kinyama n a ya s i o v u m i l i k a , K a m i s h n a M u s s a ametoka hadharani m n a s a b a n a h i l o akisema kuwa kuna wapigana j i wa Al -Shabaab waliokamatwa wanaotaka kwenda k u p i g a n a S o m a l i a . Hili ni suala zito. Sijui kama Kamishna Mussa alitaka kuyaunganisha mashambulizi hayo ya tindikali na kundi hilo, lakini mantiki ya kawaida imekataa kwa sababu mashambulizi hayo hayana mwelekeo wa ki Al-Shabab kwa aina ya silaha na pia kulenga mtu mmoja mmoja, na zaidi pia kulenga Wakristo.

Pil i , nyimbo hiyo mbaya ya Kamishna Mussa ina mwangi mkubwa. Je, alitaka kusema kuna vikundi vya s ir i (cel ls) vya

A l - S h a b a b h a p a Z a n z i b a r n a k a m a vipo waliopatikana ni wachache tu kati yao, na kama wapo wengine kwa nini akatoa taarifa hizo hadharani wakati b a d o h a w a j a t i w a mbaroni?

K u t a n g a z a k a m a Al-Shabaab wamepita tu , maana yake n i k u i o g o p e s h a n a kuipelekea Zanzibar i t e n g w e b i l a s h i . Inafaa na ni muhimu matamshi ya Kamishna Mussa yafafanuliwe na yaelezewe katika usuli mwema la sivyo yanaweza kuwa na hasara kubwa kwa Zanzibar , kwa s i s i wenyewe kuj i imbia nyimbo mbaya kuwa k umb e Al -Shab aab w a m e w e z a k u f i k a Zanzibar.

Ugumu bila ya shaka utakuja tunapotaka kujipapatua kwa sababu ya kauli ambayo pengine ilipaswa kuzuiwa au kufanyiwa utafiti zaidi.

Katika mazingira k a m a h a y o humkumbuka mjomba yangu Faisal Mbamba aliyewahi kuniusia, “Bora kujikwaa dole utatia chokaa, kuliko kujikwaa ulimi.”

Nataraji uungwana wa Kamishna Mussa, pamoja na cheo chake ni muhimu kwa maslahi ya Zanzibar, maana nchi itaendelea kuwepo na kwa vyovyote vile Uislamu hapa kwetu hautaweza kufutika.

(Makala hii ni kwa hisani ya Zanzibar Daima online)

Kamishna Mussa

Inawatangazia Waumini wote kuwa kutakuwa na Ibada ya ITIKAF, itakayofanyika katika Msikiti wa MTAMBANI, Kinondoni.

SIKU: Jumamosi –Oktoba 19, 2013

MUDA: kuanzia saa 3:00-Usiku, Baada ya Sala ya Ishaai.

Inshaa Allah.

Kwa niaba ya Amir

SHURA YA MAIMAM (T)ITIKAF

9 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 2013Habari/Matangazo

Inatangaza nafasi za Masomo kwa wanafunzi wote wanaohitaji kujiunga na Pre- Form One Boarding and Day. Masomo yameanza Tarehe 30/09/2013, Shule ipo Wilaya ya Bagamoyo Mkoa wa Pwani-km 7 kutoka njia Panda ya Chalinze Tanga, Kuelekea Morogoro.

Nafasi za Kidato cha Kwanza mwaka 2014Pia tuna nafasi za kuhamia kwa Kidato cha 2 na 3.

Usaili Kidato cha Kwanza utafanyika Tarehe 16/11/2013, kwa awamu ya kwanza. Awamu ya pili usaili utafanyika Tarehe 30/11/2013 na awamu ya Tatu Tarehe 20/12/2013.

Kwa maelezo zaidi piga simu hizi:-

0762-270 378/ 0659 303 203/ 0784- 323 203. Au E-mail: chalinzecentre@ yahoo.com

MKUU WA SHULE

Chalinze Islamic SeminaryPre-Form One

Al-Masjid Ummu Salama, Sahare Tanga, tunakaribisha mchango toka kwa Waislamu wote kuchangia ujenzi wa Msikiti.

Mwenye mchango anaweza kuwasiliana na Mwenyekiti kupitia namba:- 0713 439 079 au Katibu 0654 486 700.

Wabillah Tawfiiq.

Mchango wa ujenzi wa Msikiti

Mtuhumiwa kesi ya Kanisa Inatoka Uk. 1es Salaam amefariki.

Ust. Mbulu, amefikwa na umauti Jumatatu wiki hii katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, akiwa mikononi mwa Jeshi la Magereza baada ya kuugua na kushindwa kupatiwa matibabu ya kina na kuzikwa siku ya Jumanne huko Kimanzichana, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.

Taarifa kutoka kwa baadhi ya Waislamu na ndugu wa marehemu zimesema kuwa Ust. Mbulu, alizidiwa na maradhi katika Gereza la Segerea Jijini Dar es Salaam na kukimbizwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kupatiwa matibabu ambako mauti yalimkuta.

Imeelezwa kuwa awali Ust. Mbulu, alipelekwa katika Hospitali ya Amana, kwa ajili ya matibabu kufuatia kupatwa na maradhi ya koo akiwa mahabusu katika garaza la Segerea jijini Dar.

Hata hivyo baada ya kufikishwa hospitalini hapo, ilidaiwa kuwa madaktari wal ishauri Ust . Mbulu kupelekwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi na matibabu zaidi. Hata hivyo imedaiwa kuwa badala ya mgonjwa huyo kupelekwa Muhimbili kama ilivyoshauliwa na madaktari wa hospitalini ya Amana, alirejeshwa gerezani Segerea.

Habari zinasema kwamba kitendo cha kumrejesha mtuhumiwa gerezani akiwa mahututi, ilimlazimu Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu (T), Sheikh Ponda Issa Ponda, aliyeko mahabusu gerezani humo, kulalamikia kitendo hicho hali iliyotoa msukumo kwa Ust. Mbulu kupelekwa hospitali ya Muhimbili.

“Walitueleza kuwa humo gerezani Sheikh Ponda, aliongea kwa ukali kuwa inakuwaje mnamtoa hospitali huyu mtu na kumrejesha gerezani hali ya kuwa mnaona hali yake ni mbaya, hivi nia yenu ni kumuua?”, Mke wa marehemu Mbulu, Bi. Sheynazi Athumani Mnete, alisema akinukuu maelezo aliyodai kuwa aliyatoa Sheikh Ponda gerezani humo.

Bi. Sheynazi alifafanua k w a m b a t a a r i f a h i z o walizipata kutoka gerezani kupit ia kwa mahabusu walioonana nao gerezani hapo, baada ya kurejeshwa Ust. Mbulu gerezani humo akiwa mahututi ambapo habari hizo zilimfikia Sheikh Ponda.

Imeelezwa kuwa baada ya malalamiko ya Sheikh Ponda, baadae marehemu alipelekwa Muhimbili ambapo siku ya Jumamosi (iliyopita), ndugu wa marehemu walilazimika k w e n d a k u f u a t a t i l i a hospitalini hapo.

Mke huyo wa marehemu alisema kuwa walifanikiwa kumkuta mumewe akiwa wodini, hali yake ikiwa hairidhishi kabisa huku akiwa na pingu mguuni.

A w a l i a k i o n g e a n a mwandishi wa habari hizi juu ya mkasa huo, mke huyo wa marehemu alisema alikuwa akifahamu kwamba mumewe alikuwa ni mgonjwa tangu mwanzoni mwa mwezi wa tisa mwaka huu.

Alisema alipokwenda kumtembelea gerezani k a b l a ya k u z i d i wa n a kupelekwa hospita l ini , mumewe alimwambia kuwa anasumbuliwa na matezi ya shingo, maradhi ambayo yalimuanza akiwa gerezani humo.

“ N i l i p o k w e n d a kumuona mwezi wa tisa mwanzoni, nilikuta ndio tezi zimemuanza. Nilimuuliza m b o n a u m e b a d i l i k a sana, alisema anaumwa, n i k a m u l i z a u n a u m w a nini, akasema amevimba shingoni…”. alieleza mke wa marehemu.

H a t a h i v y o a l i s e m a marehemu al imwambia kwamba anaendelea na dozi ya sindano za saa humo gerezani na kuomba kupelekewa shuka kutokana na hali ya baridi kuwa kali, jambo ambalo lilitekelezwa.

A l i s e m a a l i e n d e l e a kumtembelea mumewe mwezi huo wa tisa, lakini alibaini hali yake inazidi kudhoofu na hata alikuwa akiongea kwa taabu kutokana na maumivu.

Bi. Sheynazi alisema, a l i p o m u u l i z a k u h u s u utaratibu wa kupelekwa h o s p i t a l i n i , m u m e w e alimweleza kuwa hapakuwa na gari la kumpeleka kupata matibabu hospitalini.

Alisema wiki iliyofuatia alirudi tena gerezani lakini h a l i a l i y o m k u t a n a y o mumewe ilikuwa ni mbaya zaidi kuliko awali, jambo ambalo lilimfanya alie kwa uchungu.

“Alikuja askari mmoja a l iyekuwa pembeni na kuniambia nimshauri mume wangu, amwombe daktari amwandikie kibali cha kupata matibabu ya nje, baadae ndipo alipopelekwa katika Hospitali ya Amana, Ilala kwa ajili ya matibabu, lakini wao wakiwa hawafahamu kinachoendelea.

Alisema baada ya wiki moja alipokea simu kutoka kwa mmoja wa askari Magereza aliyekuwa akimlinda na kumtaka aende gerezani. Alifanya hivyo akiongozana na baba wa marehemu.

A l i s e m a wa l i p o f i k a gerezani Segerea walielezwa k w a m b a n d u g u y a o amelazwa katika hospitali ya Amana kutokana na hali yake kiafya kuzidi kuwa mbaya.

Bi. Sheynazi alisema baada ya taarifa hiyo, siku hiyo hiyo ya Oktoba 5, waliondoka gerezani hapo moja kwa moja kuelekea Hospitali ya Amana, wakiwa na kibali maalum kutoka gerezani

hapo.Wa l i f i k a wa l i m k u t a

mumewe akiwa kat ika hali mbaya zaidi ya kuliko waliyomkuta nayo gerezani walipomtembelea Wodi namba tatu, hospitalini hapo akiwa na pingu mguuni.

Alisema wakiwa pale walidhani kuwa Magereza inashughulikia matibabu y a k e , l a k i n i a l i d a i walimfikisha pale hospitali na kumbwaga tu, hawakumjali kwa matibabu yake kwa ujumla.

“ Wa o k u we p o k wa o pale ni kumlinda yule bwana as inyanyuke na kukimbia, maana pamoja na hali aliyokuwa nayo ya kutojiweza bado alikuwa na pingu mguuni”. Alisema mjane huyo.

Siku iliyofuata mkewe aliwahi kufika Hospitalini na kujaribu kuongea naye, kujua zaidi kama kuna matibabu ya aina yoyote anayopata kulingana na mardhi yake.

“A l i n i a m b i a p a l e anapata huduma kutoka kwa Waislamu wa kikundi cha Jawra, ambao ndio pia wanaonunua dawa na pengine za kutuliza maumivu tu kwa sababu hakuna kipimo alichopata” Alibainisha.

Siku iliyofuata mkewe huyo alionana na viongozi hao wa Jawra, wanaoshughulikia wagonjwa kisha aliwaeleza kuwa mgonjwa wake si mfungwa wala mtuhumiwa wa kosa lingine, bali ni mmoja wa waathitika wa kadhia ya kukojolewa Qur’ an Mbagala.

“Yule Ustadhi baada kumfafanulia, alitoka nje na kurejea na wenzake wengine watatu, kisha walifanya shura huku wakiongea na mgonjwa, alikuwa akiongea kwa shida kutokana na hali yake kuwa mbaya.” Alisema.

Alisema siku iliyofuata alipigiwa simu na viongozi wa S h u r a ya M a i m a m ambao walimweleza kuwa watamshughulikia mgonjwa huyo na mara moja vipimo vilianza kwa mgonjwa huyo.

“Kwanza alipigwa picha ya X-rays, alichukuliwa damu na majibu ya madaktari yalisema kuwa apelekwe M u h i m b i l i k wa k u wa matibabu yake pale Amana hakuna.” Alisema mke huyo wa Marehemu.

Baada ya taarifa hiyo ya Amana, ilielezwa kuwa Alhamisi ya wiki iliyopita, lilifika gari la Magereza hospi ta l in i hapo kisha walimchukua na kumrejesha g e r e z a n i n a h a l i ya k e mahututi licha ya madaktari kutaka apelekwe Muhimbili.

“Hatua hiyo iliwashtua sana wanafamilia, lakini zaidi ni jinsi walivyomwondoa pale wodini, walimrusha katika gari kama vile ni jambazi muuaji wakaondoka naye.” Alisema.

M k e w a m a r e h e m u anaeleza kuwa alilazimika kumfahamisha mjomba wa marehemu, ili aweze kumfatilia Segerea siku ya Ijumaa (iliyopita), lakini alidai alipofika huko pamoja na kujieleza alikataliwa kabisa kuingia hata kupewa taarifa yoyote ya marehemu.

Alisema walipofuatilia zaidi, ndipo walipoambiwa k u w a m g o n j w a w a o amepelekwa Hospitali ya Muhimbili na baada ya muda mfupi alifariki.

Alisema kuwa baada ya kufariki, askari Magereza aliyekuwepo pale Muhimbili a l i w a e l e z a k w a m b a wafuatilie kibali Segerea, alipokuwa akishikiliwa.

Mbali na kufikwa na umauti, marehemu katika siku za mwanzoni akiwa mahabusu, alikuwa anauguza mguu wake aliovunjwa kwa kipigo cha Polisi katika harakati za Jeshi la polisi

kuwakamata Waislamu.Marehemu Ramadhani

M o h a m m e d M b u l u amaeacha wake wawili na watoto watatu.

Marehemu Mbulu pamoja na wenzake tisa, walikuwa wakituhumiwa kuvunja na kupora katika Kanisa la KKT Mbagala.

Siku chache baada ya kifo cha Ust. Mbulu Jumatatu wiki hii , Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Jijini Dar es Salaam jana Alhamis imewaachia huru watuhumiwa wengine tisa waliokuwa wakituhumiwa pamoja na marekemu baada ya kukutwa kuwa hawana hatia.

W a t u h u m i w a h a o wamekaa rumande kwa m w a k a m z i m a t a n g u walipokamatwa Oktoba 12, 2012, baada ya serikali kuzuia dhamana zao kufuatia ghasia zilizozuka mwezi Oktoba mwaka jana, baada ya kijana mmoja kukojolea Qur’an huko Mbagala.

Ilidaiwa kuwa baada ya tukio hilo, watuhumiwa

10 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 2013SHAIRI/HABARI

TUSOMENI AN-NUURMhariri muadhamu, nipokee hodi hodiJanibu japo nikumu, ya gazetilo suudiNdaniye abra nikimu, nitoe wito saidiKwa habari za yakini, tusomeni AN-NUUR.

Naibtadi nudhumu, kwa Allah kumhimidiThuma swala na salamu, kwa rasuli Muhammadi Kadhalika taadhimu, kwa swahaba murshidiKwa habari za yakini, tusomeni AN-NUUR.

Baada ya taadhimu, sina budi kulinadiGazeti letu adhimu, ndani lenye irishadiKadhalika taalimu, na mzomzo suudiKwa habari za yakini, tusomeni AN-NUUR.

Limesimama kawimu, pamwe na kutabaradiLengole hasa ikumu, ya Ilahi TauhidiNa zende zote kuzimu, za rajimu itikadiKwa habari za yakini, tusomeni AN-NUUR.

Kwa makalaze adhimu, za kisomi na weledi Latujaza ufahamu, wa mengi yaso idadiKwa habari na elimu, kwalo tunastafidiKwa habari za yakini, tusomeni AN-NUUR.

Latetea madhulumu, kwa uvumba na kwa udi, Ukweli laudhimu, na urongo kuurudiKwa yake mastakimu, kulisoma yatubidi,Kwa habari za yakini, tusomeni AN-NUUR.

Daima dumu dawamu, kwalo nyuma tusirudiIJUMAA 'napotimu, sote tufanze juhudiNakalaye tujihimu, japo moja kwa nakidiKwa habari za yakini, tusomeni AN-NUUR.

Kaditamati nudhumu, sitozidisha idadi Thamaniya zimetimu, za wito bila inadiChini naweka kalamu, AN-NUUR "Tuliridi" Tusomeni AN-NUUR, kwa habari za yakini.

ABUU NYAMKOMOGIMWANZA

Inanichoma sanaNi mshairi asili, niloitopea kaziLeo meguswa na hili, wacha niliweke waziLini huu udhalili, utaisha viongozi?Ngoja niwape kauli, jitmai langu choziInanichoma sana.

Inanichoma sana, kauli mbiu ya moyoHadi ninapata homa, juu haya nisemayo,Kitu gani mwaegema, kujivina mfanyayoKuwa kimya twatazama, mwatuona mapoyoyoInanichoma sana.

Mlianza ukoloni, kutunyima hivyo vyeoHamsomi visirani, kuatibu kimbilioTumesoma na bungeni, mwakerwa wetu ujioFileari jicho fini, tukinena dafraoInanichoma sana.

Maafa ya Mwembechai, mkavuruga amani,Athari zipo hai, kwake Chuki AthumaniMwachangia vurumai, hata haya hamuoniKwa bezo na kujidai, mwashutumu yetu diniInanichoma sana.

OIC na Kadhi, tumehoji kwa ghilibuTibuni haya maradhi, taifa lapata taabuMaamuzi m’mehodhi, yakini mwatusulubuKatiba haijakidhi, takwa la hii adhabuInanichoma sana.

Metuona wenu punda, mwatuendesha kwa fimboKione anawaponda, mkampiga kikumboRisasi kwa Sheikh Ponda, mlichofanya utumboKwa kututona kidonda, yenu yataenda komboInanichoma sana.

Japo na Jeraha lake, gerezani akatiwaNafasi wakili wake, kunena hakupatiwaKuhusu shtaka lake, eti Tume taundiwaNi ipi faida yake, Tume inomilikiwa?Inanichoma sana.

Na Nasri [email protected]

No: 0759202192

Nguvu ya ibada katika kulinda siha njemaInatoka Uk. 7

kuwa uchomaji wa mishikaki ni aina ya upishi ambao unahitaji tahadhari nyama isije ikaungua n a k u f a n y a m k a a . M a e n e o yaliyofanya mkaa ni maeneo ambayo ya m e t e n g e n e z a s u m u m b a y a zinazodhuru afya. Sumu hizi zinaitwa ‘ H e t e r o C y c l i c Amines ’ . Sumu hizi zinatajwa kuwa ni miongoni mwa vichocheo vikubwa vya ugonjwa wa saratani. Wataalamu wanaeleza kuwa kuipaka nyama husika vioungo k a m a m a n j a n o ( t u r m e r i c ) n a m a j a n i y a rosemary husaidia kupunguza athari hizo.

Mfano mwingine ni unga wa sembe. Unga wa sembe ni halali, na tena u n a p e n d e z a m a c h o n i . H a t a hivyo unga huo ni chakula kisicho na ubora wowote; sana sana ni chakula chenye muelekeo m k u b w a w a kukuletea maradhi. N i c h a k u l a ambacho nyuzi-lishe pamoja na viini lishe vingine v i m e o n d o l e w a na kubakiwa na w a n g a m t u p u . Wanga huu mtupu unapoingia mwilini bila kuambatana n a v i i n i l i s h e vilivyoondolewa h u s a b a b i s h a k inga za mwil i kuhisi kuwa mwili umevamiwa; na kuanza kujipanga k u t o a u l i n z i . K i t e n d o h i k i husababisha seli z o t e z a m w i l i k u v a m i w a n a u v i m b e m wa k o ( inf lammat ion) , hali ambayo iwapo itadumu kwa muda mrefu, ina madhara m a k u b wa s a n a kiafya mwilini.

Mifano ni mingi mno ya vyakula halali lakini visivyo na ubora. Watu wa n a c h o t a k i wa k u z i n g a t i a n i k wa m b a d h a n a hizi mbili ni lazima z iende pamoja . D h a n a ya t a t u inayoambatana na dhana hizi pacha, ni kanuni ya ‘kiasi’. Chakula kinaweza kikawa ni halali na chenye ubora unaotakiwa, lakini kikawa na madhara m a k u b w a k w a mtumiaji kutokana na kutokuzingatia kanuni hii ya ‘kiasi’ wakati wa kukila. Kanuni ya kiasi inatuhita j i kula kiasi cha chakula na kuacha sehemu nyingine ya tumbo ikiwa wazi kwa ajili ya maji na hewa. Ukweli wa kanuni hii unadhihiri pale unapomkuta mtu amekula vyakula vingi na vya aina tofauti tofauti kwa wa k a t i m m o j a , hadi akashiba sana. Kinachofuata hapa n i k u v i m b i w a . U n a f u u utapatikana tu pale ambapo mhusika atatapika. Kitendo cha kutapika ni ujumbe unaoletwa na tumbo kwamba ‘ Umenijaza sana nashindwa kufanya kazi!’

Kula kiasi kuna umuhimu mkubwa sana kiafya. Hii ni kutokana na ukweli kuwa seli zako za mwili zinahitaj i kiasi fualani tu cha virutubisho ili ziweze kufanya kazi zake kwa ufanisi. Ziada yoyote au itageuzwa kuwa mafuta yahifadhiwe m w i l i n i ( k a m a hiyo ziada inatoka kwenye wanga), au itageuka kuwa s u m u m b a y a m w i l i n i n a k u k u s a b a b i s h i a madhara mengi, kama hiyo ziada inatoka kwenye

prot in i . Mafuta yanapohifadhiwa mwilini kwa wingi h u z a a u n e n e uliopindukia, na unene uliopindukia huzaa magonjwa mengi ya kimfumo; ikiwa ni pamoja na sh in ik izo la damu, k i sukar i c h a u k u b wa n i , ugonjwa wa moyo, nakadhalika.

K w a u p a n d e wa p i l i , m w i l i u n a p o k u w a umezidiwa na sumu zinazotokana na mabaki ya protini hupelekea mwili huo kujaa tindikali; tindikali ambayo hujenga mazingira bora ya kustawisha k u z a l i a n a k w a wingi kwa vijidudu vinavyoambukiza maradhi, na pia kuzichochea seli za mwili kujibadili na kuwa seli za saratani!

K u l a v ya k u l a halali, vizuri, na kwa kiasi ndiyo pia maagizo ya Mungu Muumba. Na huu ndio msingi wa kusema ibada i n a l i n d a s i h a , kwani ibada n i kufuata maagizo ya Mwenyezi Mungu.

Katika Uislamu kuna mafundisho y a f u a t a y o yanayohusiana na l i she kul ingana n a m a e l e z o tuliyoyatanguliza:

“Enyi mlioamini! Kuleni vizuri na halali tulivyokuruzukuni, na Mumshukuru Mwenyezi Mungu, i k i w a n i k w e l i m n a m u a b u d u ” (Quran 2:172)

“ E n y i w a t u ! Kuleni vi l ivyomo katika ardhi, halali na vizuri, wala msifuate nyayo za shetani. Bila ya shaka yeye kwenu ni adui aliye dhahiri” (Quran 2: 168)

“ Y e y e amekuharamishieni m z o g a t u , n a damu, na nyama ya

nguruwe, na nyama ya mnyama ambaye wakati wa kuchinjwa kwake hakutajiwa jina la Mwenyezi Mungu pekee. Lakini aliyefikwa na dharura (ya kula vitu hivi) bila kutamani wala kupita kiasi, yeye hana dhambi. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwingi wa kusamehe ( n a ) m w i n g i wa kurehemu.” (Quran 2:173)

“Enyi wanaadamu! Chukueni mapambo yenu wakati wa kila sala; na kuleni (vizuri) na kunyweni (vizuri). Lakini msipite kiasi t u . H a k i k a ye ye (Mwenyezi Mungu ) hawapendi wapitao kiasi.” (Quran 7:31)

Katika kusisitiza umuhimu wa kula kiasi tu, Mtume Muhammad (SAW) amesema:

“ U d h a i f u m k u b w a w a mwanadamu n i katika tumbo lake. Kama ni lazima ule, basi gawanya tumbo lako katika sehemu tatu. Tumia sehemu moja kwa chakula, na bakiza s e h e m u m b i l i zilizobaki kwa ajili ya maji na hewa”

Na katika hadithi nyingine, bwana M t u m e ( S AW ) a m e n u k u l i w a akisema:

“ T u m b o n i tangi la mwili na mishipa mbalimbali ya damu huelekea h u k o . T u m b o linapokuwa na siha mishipa ya damu hutoka huko ikiwa na afya njema, lakini tumbo linapokuwa na maradhi mishipa hiyo hutoka huko i k i w a i m e b e b a magonjwa”

Mungu akipenda tutaendeleza mada hii juma lijalo. (Kwa hisani ya Ukurasa wa Herbal I m p a c t k a t i k a Facebook.)

11 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 11-17, 2013Makala

NIMEHUZUNISHWA kwa kiasi kikubwa na mauaji ya kikatili ya Waislamu wanne yaliyotokea usiku wa Septemba 03, mwaka huu mjini Mombasa, Kenya. Mauaji haya ni ya kinyama na yanapaswa kulaaniwa na wapenda amani wote duniani.

Wa u a j i w a S h e i k h Ibrahim Rogo na wenzake, wa m e d h i h i r i s h a k u wa ni waoga na waliofilisika kifikra. Ningependa kutoa rambirambi zangu kwa familia za Waislamu hawa na kumuomba Mwenyezi M u n g u a wa p e s u b i r a katika kipindi hiki kigumu. Na Mwenyez i Mungu, I n s h a a l l a h , a wa i n g i z e k w e n y e r e h e m a z a k e marehemu hawa.

M a u a j i y a S h e i k h Ibrahim Rogo na wenzake yamefungua jeraha lingine kwa Waislamu wa Kenya, baada ya mauaj i kama hayo ya wahubiri kadhaa wa Kiislamu nchini humo mwaka jana. Tunaziomba

Mauaji ya Sheikh Ibrahim RogoNa Said Rajab

Taasisi za kutetea Haki za Binadamu duniani kusimama na kupinga dhulma hizi.

Kwa hakika, huku ni kuwanyima haki Waislamu wa Kenya, lakini kuwanyima zaidi ni hatua ya serikali ya nchi hiyo, kuwahadaa kwamba inafanya uchunguzi wa mauaji hayo kwa kuunda Tume! Kama kawaida , Serikali ya Kenya inawajua waliomuua Sheikh Ibrahim Rogo. Inachofanya sasa ni kukimbia tu kivuli chake, kwa kuwapiga Waislamu wa nchi hiyo changa la macho.

Hatua ya kuuawa kinyama kwa Sheikh Ibrahim Rogo na wenzake watatu, inaonyesha wazi kwamba Serikali ya Kenya haijali kabisa usalama wa Waislamu nchini humo, na kwamba maisha ya wahubiri wa Kiislamu nchini humo yako hatarini.

Ni ukweli ulio wazi kabisa kwamba mauaji haya ya kishenzi, yana uhusiano

wa moja kwa moja na "vita dhidi ya ugaidi", ambayo imeletwa nchini Kenya kwa chokochoko za Marekani. Wananchi wa Kenya, kama ilivyo Watanzania, kimsingi hawana vita dhidi ya ugaidi. Kuna watu hapa nchini wanatamani Watanzania wabebe gharama kubwa ya vita isiyokuwa yao.

Kwa sababu Itikadi ya Kikomunisti haina nafasi tena ya kurejea duniani, hofu kubwa ya Marekani ni kurejea kwa Uislamu kuongoza dunia. Hii ndiyo sababu Marekani imeanzisha vita dhidi ya Uislamu na Waislamu duniani, ambapo wamewabandika Waislamu jina la 'magaidi' na 'siasa kali'.

Kwa hakika, Uislamu hauko hivyo na wala hauna m a j i n a m a b a y a k a m a M a r e k a n i i n a v y o t a k a . Uislamu umeletwa duniani kama rehema kwa wanadamu wote. Mwenyezi Mungu

Mtukufu anasema:"Nasi hatukukutuma ila

uwe rehema kwa walimwengu wote" Qur(21:107).

K w a Wa i s l a m u w a Kenya na ndugu zao wa Tanzania, mauaji ya kinyama ya Sheikh Ibrahim Rogo ni funzo kubwa kwetu. Kwanza yanaandaliwa mazingira ya kuwatia watu ujinga wa hatari ya "magaidi"; wananchi wakishalewa bangi hilo la ugaidi, Waislamu wakweli wanaokemea dhulma bila hofu kwa kuwanyooshea kidole madhalimu wanaanza kuuawa au kukamatwa.

Miezi michache iliyopita, Sheikh Ponda Issa Ponda alipigwa risasi na polisi mkoani Morogoro, katika m a z i n g i r a k a m a y a l e aliyouawa Ibrahim Rogo mjini Mombasa. Polisi walitaka kumuua Sheikh Ponda!

Kwanini?Amesimama kidete kutetea haki za Waislamu z i n a z o k a n d a m i z wa n a amekataa kabisa kufungwa mdomo na madhalimu.

Niwakumbushe ndugu zangu katika imani wa Kenya na Tanzania, wakati mitihani mizito kama hii inapotufika, basi tusipotoshe wito wa Uislamu kwa sababu ya woga, au kutaka kujikomba kwa madhalimu. Tunapaswa kumuiga

Mtume wa Mwenyezi Mungu jinsi alivyoendesha harakati zake kitaalamu na kwa ujasiri mkubwa pale Makkah. Aliikosoa vikali itikadi potofu ya kijahili na akaonyesha fikra sahihi ya Uislamu.

Mtume wa Mwenyezi Mungu alifichua mbinu na hila za watawala waovu na akapinga kwa uwazi uovu wao. Licha ya kupata misukosuko mingi kutoka kwa watawala wa Makkah, Mtume hakusalimu amri na akaendeleza harakati zake mpaka Uislamu ukasimama.

V I T A v y a k i s a s a vinapiganwa katika viwanja mbalimbali , vikiwemo v y o m b o v y a h a b a r i . Tumeshuhudia vyombo vya habari vikiendelea kushupalia uongo ulio dhahiri, vikipindisha ukweli ulio wazi, vikirudiarudia taarifa potofu na kuchezesha maoni ya umma, ili kuunga mkono malengo yao maovu.

Taarifa za vyombo vya habari na uwasilishaji wake wa matukio kwenye maeneo ya migogoro, kama vile Iraq, Palestina, Afghanistan, Misri, Somalia na kwengineko, ni za upande mmoja na zinawekwa katika namna ambayo, mtu hupati picha halisi ya kile kinachoendelea.

Waandishi wa habari wanaotumika kuficha uovu n a d h u l m a , h a wa we z i kuandika kiuadilifu upande wa pili wa vita, hata kama wanaujua ukweli. Wao na vyombo vyao ni sehemu ya mapambano dhidi ya wale wanaotakiwa kuangamizwa - Waislamu.

Angalia jinsi tukio la ' m a g a i d i ' wa M t wa r a lilivyokuzwa bila sababu, na vyombo vya habari vinavyoongozwa na watu wanaojiita ni wanataaluma. Unajiuliza watu hawa ni waandishi wa habari au waandikaji wa habari?

Badala ya kuongozwa na misingi ya taaluma ya Uandishi wa Habari, baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari hapa nchini, wanaongozwa na chuki za kidini. Hawawezi kuandika mema ya Waislamu, hata kama wanayaona! Kweli kabisa, magazeti mengine y a n a s t a h i l i k u i t w a v i p e p e r u s h i . K u y a i t a magazet i n i ku ivun j ia heshima tasnia nzima ya habari!

Ndugu zangu Waislamu, habari nyingi tunazopokea kupitia vyombo vya habari

Vyombo vya habari ni uwanja wa mapambano!Na Said Rajab wala si habari. Habari za

kweli zipo, lakini zinafichwa na vyombo hivyo.Vyombo vya habari vya ulimwengu vinadhibitiwa na mataifa makubwa ya Magharibi, yakiongozwa na Marekani. Maslahi ya mataifa hayo ndiyo yanayolindwa zaidi katika utoaji wa habari.

K u k u z a m a m b o , k u p i n d i s h a u k we l i n a kuzungusha uongo, ndiyo tunayoyashuhudia kila siku kwenye vyombo vya habari vya ul imwengu. Mawe yanayorushwa na vijana wadogo wa Kipalestina, kama hatua ya kujihami dhidi ya askari wa Israeli, walio ndani ya vifaru na magari ya kivita, yanaitwa mashambulizi hatari ya kigaidi!

L a k i n i m a u a j i y a Wapalestina 107, wakiwemo wa n a wa k e , wa t o t o n a vikongwe mwaka 1948, yaliyofanywa na Menachem Begin, aliyekuwa Waziri Mkuu wa Israel na aliyeshinda "Tuzo ya Amani ya Nobel", kwenye vijiji vya Deir Yassin, nchini Palestina siyo vitendo vya kigaidi!

Mauaj i ya maelfu ya Wapalestina kwenye kambi za wakimbizi za Sabra na Shatila yaliyotekelezwa na Jenerali Ariel Sharon, mwaka 1982 , ambaye baadaye alikuwa Waziri Mkuu wa Israeli, aliyeitwa - "the man of peace", siyo vitendo vya kigaidi! Kwa mtu mwenye akili zilizofunga barabara, lazima atashangazwa na taarifa hizi! Maana atajiuliza sasa hapa gaidi nani? Na jawabu sahihi atalipata yeye mwenyewe.

Lakini wale wenye akili tepetepe, wanaotegemea zaidi vyombo vya habari vifikiri kwa niaba yao, ndiyo wanaoweza kuamini upuuzi kama ule wa Mtwara.

Nchini Iraq, watu ambao ndiyo waliokuwa wakitajwa na vyombo vya habari , kama waathirika wa ukatili

wa Saddam Hussein, sasa ndiyo wanaoangushiwa mabomu mazito ya 'cluster' na 'depleted uranium' ili kutekeleza "demokrasia" nchini humo. Ni a jabu kuona majeshi ya Marekani nchini Iraq, yanaitumia Abu Ghraib ile ile iliyojengwa na dikteta Saddam Hussein, kupandikiza demokrasia!

M a k u n d i y o t e yanayopigana dhidi ya u va m i z i wa m a b e b e r u katika nchi zao, wanaitwa magaidi na vyombo vya habari. Vyombo hivi katika uchambuzi wake wa habari, vinasema; "Magaidi hawa wanaongozwa na malipo, ambayo Mwenyezi Mungu atawapa peponi".

Hii maana yake ni kwamba hawapigani na wavamizi, wala wale wanaokalia nchi zao kimabavu, isipokuwa wanataka malipo ya peponi tu, na wako tayari hata kujitoa muhanga kwa ajili hiyo! Huo ndiyo mtazamo unaojengwa na vyombo vya habari kwa umma.

Uislamu unawasilishwa kama "ugaidi", lengo likiwa kusukuma mbele ajenda ya kibeberu ya mataifa ya magharibi, yanayozivamia nchi za Waislamu na kupora rasil imali . Ukweli huu, ambao ndiyo chimbuko la mgogoro, unaofichwa na vyombo vya habari.

Huu ndiyo msiba wa ulimwengu wa leo, ambao watu wengi hawaujui au wanaupuuza kwa makusudi. Hivi watu wangapi, kwa mfano, wanajua ukweli ufuatao kuhusu Iraq:

Zaidi ya wanawake milioni moja wa Iraq wamekuwa wajane. Waume zao, ni kati ya Wairaq milioni 1.2 na milioni 1.3 waliouawa na majeshi ya kigeni yanayoikal ia kimabavu nchi hiyo. Milioni moja wengine wamepotea kusikojulikana, na wengine laki nne wako magerezani wakiteseka.

Watoto milioni tano wa Iraq wamepoteza wazazi wao na kuwa mayatima. Aidha,

wazazi wao wameuawa, "wamepotea", wamefungwa au wamelazimika kuikimbia nchi na kuacha kila kitu nyuma. Ni miongoni mwa wakimbizi milioni saba wa Iraq.

Hivi sasa, kuna wafungwa wanawake wa Iraq elfu kumi. Asilimia 95 yao wanafanyiwa u n ya n ya s a j i m k u b wa , okiwemo kubakwa. Habari kama hizi haziandikwi wala kutangazwa kwenye vyombo vya habari vikubwa.

Wa n a c h o t a n g a z a n i mashambulizi ya kujitoa muhanga dhidi ya raia yaliyofanywa na wapiganaji wa Kiislamu, wakati ukweli n i kwamba wao ndiyo wanaofanya mashambulizi h a y o n a k u wa s i n g i z i a Waislamu.

Ndugu zangu, wenzetu wa Iraq, Afghanistan,Yemen na Palestina wanaangamizwa vibaya sana, chini ya uongo mkubwa na uliopangiliwa vyema wa vyombo vya habari. Watu wengi sana duniani, w a k i w e m o Wa i s l a m u wenyewe, hawajui hilo. Hawajui unafiki, ubalakala wala uadui wa vyombo vya habari.

Mtume wetu Muhammad, Rehema na Amani ziwe juu yake, alituonya kuhusu zama zetu hizi. Alisema:

"Wakati wa Dajjal utakuwa ni miaka ya kuchanganyikiwa. Watu watamuamini muongo na kutomuamini anayesema kweli. Watu hawatamuamini muadilifu, na watamuamini a s i y e m u a d i l i f u ; n a ruwaybidha watakuwa na kauli".

Mtu mmoja akauliza: "Ni akina nani hao?" Mtume alijibu: "Wale wanaomuasi Mwenyezi Mungu watakuwa na kauli katika uendeshaji wa mambo."

Kwa hiyo wale Waislamu wenye uwezo wa kutafsiri maandiko ya kidini kwa usahihi, wanajua kwamba hizi ni dalili muhimu sana za nyakat i za mwisho,

a m b a p o m i f u m o y a kitwaghuti na upotofu ndiyo inayoendesha mambo, kama ilivyobashiriwa kwenye hadithi hiyo.

Saa hiyo itakapokaribia, rehema itagubikwa na ukatili, ukweli utafunikwa kwa uongo, uwazi utafichwa na vinyago, na dunia itaonekana kusahau haki maana yake nini hasa! Katika mazingira kama haya, inakuwa ni muhimu kwa Waislamu kushikamana kikamilifu na mafundisho ya dini yao.

Wais lamu wasiogope propaganda, uongo, fitna, uzandiki na unafiki wa vyombo vya habari, na badala yake wafuate njia ile ile waliyopita Simba wa Uislamu duniani, Mujahidina. Bila shaka, Mwenyezi Mungu ataleta ukweli wa kufutilia mbali uongo wa mabeberu unaosambazwa na vyombo hivyo:

"Na sema: "Ukweli umefika; na uongo umetoweka. Na uongo (mwishowe) huwa ndiyo wenye kutoweka" Qur(17:81).

Ni jambo la wazi kabisa kwamba wale wanaotenda uhalifu juu ya uhalifu, hawataki kuitwa wahalifu, wakati Waislamu ambao wamepachikwa jina la ugaidi, nao hawawezi kukubali kuitwa majina mabaya na kusingiziwa uhalifu. Kwa hiyo vita kwenye vyombo vya habari, kati ya kambi hizo mbili itaendelea tu.

Jambo la kushangaza ni kwamba Waislamu wengi sana duniani, hawajui kama wapo kwenye uwanja wa mapambano wa vyombo vya habari. Wanapigana vita upande wa pili dhidi yao wenyewe bila kutambua. Lakini wale Waislamu wenye kujitambua wanabaki moja kwa moja kwenye misingi ya dini yao, ambayo wanaiona kama mbadala wa kiitikadi, kiakili na kisiasa kwa mfumo unaotawala dunia leo, ambao umeonyesha dalili zote za kusambaratika.

12 AN-NUURDHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 201312 MAKALA

Gazeti hili hutolewa na Islamic Propagation Centre S.L.P. 55105 na kupigwa chapa na Business Printers Limited, S.L.P. 78495 Dar es Salaam.

AN-NUUR12 DHUL-HIJJA 1434, IJUMAA OKTOBA 18 - 24, 2013

SERIKALI imeanza kukusanya maoni ya wadau wa elimu nchini kuhusu upangaji wa viwango vya alama (Grade Ranges) katika mitihani ya kuhitimu kidato cha Nne na cha Sita.

K wa m u j i b u wa Dodoso za kukusanya maoni zilizo sambazwa k w a w a k u u w a shule mbalimbali za Sekondari Jijini Dar es Salaam kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, zimesema hali hiyo itasaidia kuwa na namna bora ya upangaji viwango vya alama utakaoanza kutumika sasa.

Hatua hiyo ya Serikali inaonyesha kuyafanyia kazi malalamiko ya Wa i s l a m u k u p i t i a Baraza la Wakuu wa Shule za Ki i s lamu nchini kufuatia barua yao kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, ambayo pamoja na mambo m e n g i n e , wa l i h o j i uadilifu na usiri usio na sababu na kutumika kanuni zisizokubalika kitaaluma ndani ya Baraza la Mit ihani T a n z a n i a k a t i k a k u p a n g a m a t o k e o NECTA.

Katika sehemu ya barua yao ya mapema mwezi Machi mwaka huu, Baraza hilo la Wakuu wa Shule za Ki i s lamu l i l i e l eza , “Mhe. Waziri Mkuu, kwa kuzingatia yote tuliyoyasema hapo juu ndiyo maana tunasema tatizo lililopo linaweza k u t a t u l i wa , i k i wa utaamua kuwataka viongozi waandamizi wa NECTA na wale wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi

Serikali yaanza kukusanya maoni kuhusu NECTANa Bakari Mwakangwale kuweka hadharani

a lama za mi t ihani walizo pata wanafunzi wa kidato cha nne baada ya zoezi la usahihishaji kukamilika …” .

D o d o s o h i l o ( n a k a l a t u n a y o ) k a t i k a u t a n g u l i z i wake limeeleza kuwa, Serikali imedhamiria kufanya luinganishi (harmonization) wa m a s u a l a ya a l a m a kat ika mit ihani ya kidato cha nne na sita, i l i kupata muundo mmoja utakaokuwa wa wazi kwa wadau wote wa elimu ya sekondari.

“Kwa kuwa wewe n i m i o n g o n i m wa wadau muhimu wa el imu, maoni yako yanahitajika sana ili tuweze kupata picha ya ujumla katika maeneo mawili, upangaji wa viwango vya alama na matumizi ya alama za tathimini endelevu ya mwanafunzi.

“ M a o n i y a k o yatasaidia katika kutoa uamuzi wa kitaifa wa namna bora zaidi ya u p a n g a j i v i wa n g o vya alama kwa ajili ya watahin iwa wa kidato cha nne na sita utakaoanza kutumika sasa na miaka ijayo…” Imesema sehemu ya dodosa hilo, likifuatiwa n a m a s w a l i y a mapendekezo.

Kupitia Dodoso hilo, pia Serikali inakusanya maoni kuhusu matumizi ya alama endelevu y a m w a n a f u n z i ( C o n t i n u o u s A s s e s s m e n t [ C A ] ), jambo ambalo pia Baraza la Wakuu wa Shule za Ki i s lamu walililamikia.

Katika utetezi wake kupitia Dodoso hilo, Serikali imedai kuwa imeamua kukusanya

maoni hayo kwa kuwa muda mrefu upangaji wa viwango vya alama vinavyotumika katika mitihani ya kuhitimu kidato cha nne na sita havifanani, pamoja na kwamba mitihani yote hiyo ni ya elimu ya sekondari.

K u t o k a n a n a m k a n g a n y i k o h u o bas i , huenda ndio sababu Baraza hilo

katika barua yao ya kutaka marekebisho, l ikamueleza Waziri Mkuu kwamba,

“ N i u k w e l i u s i o p i n g i k a k u wa wadau wote wa Baraza la Mitihani tukiwemo sisi wenyewe, tunakabiliwa na changamoto ya usiri mkubwa wa uendeshaji wa shughuli za NECTA.

Hatujui mchango wa mazoezi ya kila siku

I m e e l e z w a k u w a M o h a m m a d M o r s i , Rais a l iyeondolewa madarakani nchini Misri ambaye yuko kizuizini, ana hali mbaya kiafya kwa muda wa wiki mbili sasa.

Habari zinasema kuwa, madaktari wamekuwa wa k i e n d a k u m p a t i a m a t i b a b u M o r s i hukohuko kizuizini, lakini serikali ya mpito imekataa

(CA) katika alama za mwisho anazopewa mwanafunzi, hatujui pass mark wala grade ranges zinazotumiwa na Baraza la Mitihani kwa sasa”. ilifafanua barua ya Wakuu wa Shule za Kiislamu kwa Waziri Mkuu.

B a r u a h i y o y a Wakuu wa Shule za Kiislamu kwa Waziri Pinda, ilieleza kwamba Baraza la Mit ihani haliko tayari kufanya mambo kuwa wazi kwa wadau wake, licha ya utafiti wa serikali na ule wa Kamati ya Mlama, kuitaka NECTA kufanya hivyo.

Barua hiyo ilijenga hoja na kuonyesha kuwa, kumekuwa na ushahidi mwingi wa kimazingira na wa wazi kutokana na tafiti mbalimbali na kwamba, i n a k u w a v i g u m u kwa sasa kuaminika matokeo yanayotolewa na Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).

Hiyo ni kutokana na kukithiri kwa usiri us io na sababu na kanuni zisizo kubalika kitaaluma katika kutoa madaraja ya mwisho ambayo mara nyingi yanazua maswali yasiyo na majibu.

Hali ya afya ya Morsi si nzurikumhamishia hospitalini kwa uchunguzi zaidi wa kiafya.

Hata hivyo mmoja wa watu wa familia ya kiongozi huyo wa zamani wa Misri amesisitiza kuwa, Morsi ameapa kuendelea kupigania haki zake za kisheria hadi mwisho wa uhai wake.

Usama Morsi, mtoto wa Mohammad Morsi ameikosoa vikali serikali ya mpito kwa kuendelea

kusikiliza kesi za viongozi wa harakati ya Ikhwaanul Muslimin, wakati huu wa kusherehekea sikukuu ya Idul Adh’ha na kusisitiza kuwa k i tendo h icho kinakinzana kikamilifu na katiba ya nchi hiyo.

Jumapi l i i l iyopi ta , Mwendesha Mashtaka wa Misri alisema kuwa, Morsi ataendelea kubaki k izuiz ini kwa muda mwezi mmoja zaidi.

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda.

Soma Gazeti la AN-NNUR

kila Ijumaa